4 Jul 2009



3 Jul 2009


Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mufti Issa bin Shaaban Simba, amekasilishwa na uamuzi wa serikali kuhusu Mahakama ya Kadhi.

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.

Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.

Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.

Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka .


CHANZO: Mwananchi


KWA MWENENDO HUU SI AJABU KUSIKIA HATA WATANZANIA WALIOAHIDIWA MAISHA BORA NAO WAKAJITOKEZA KUDAI HAWAITAKI CCM....HOJA IKIWA MAISHA BORA YALIYOAHIDIWA YAMEISHIA KWA KUNDI DOGO LA MAFISADI PEKEE!



In a recent interview with MTV News, The Game relayed Michael Jackson’s attempts to end the beef between him and 50 Cent. Although the rappers eventually laid the feud to rest (without Jackson’s help) the tension between the two still remained.However, The Game has finally taken it upon himself to give a formal apology, not just to 50, but to the whole Interscope label.“For 50, I’m just gonna apologize to him, just as a man,” he told MTV. “It has nothing to do with music, or beef, or nothing like that. It ain’t about being the bigger man. He can take it and say, ‘Game is apologizing,’ ‘Game’s a sucka, he’s apologizing.’ I’m apologizing for me to him, to [Dr.] Dre, to Jimmy Iovine, to Eminem, to all the fans. Because if you think about what Interscope was when we were gellin’, man we were it. We were an unstoppable force.”

He explained that while he was a member of G-Unit, there were some things he needed to do “for my career to have longevity, and for me to survive in Hip Hop music,” and this may have played a part in the dissolving relationship between himself and 50 Cent. He also expressed some regret that G-Unit and the Interscope label did not get to experience the success that it could have had, potentially.

“Now, four albums in, I can say as a man that G-Unit, Game, Aftermath, Black Wall Street, Interscope, Geffen, Eminem, Shady, from [Lloyd] Banks to [Young] Buck to [Tony] Yayo to Dre to whoever; If it woulda kept going: endless paper. Millions of albums sold. Because we were great together.”

The Game also expressed his strong belief that, had he and G-Unit (and perhaps Young Buck) not parted ways, many things would have been different.

“Me and Fif’s chemistry is what Method Man was to Redman when they get in. Red ain’t from Wu-Tang but you know when Meth gets wit' Redman it’s goin’ down… [Me and 50’s] biggest records were together. Whether I was on them or I wasn’t on them. Whether he was on them or he wasn’t on them. When we were in gellin’ writing together as a family, we had it man. If we never would have [broken] up, I think Detox would have been out and we all would have been selling millions from Banks to Buck, and Tony Yayo. I’m going to apologize for my role.”

50 Cent and the Aftermath camp have not yet issued a response.

SOURCE: Hiphopdx.com


1 Jul 2009


CCM wafanya mkutano kanisani, wampiga kiongozi wa kigango

Na Frederick Katulanda, Biharamulo

WAFUASI wa CCM juzi walivamia Kanisa Katoliki, Kigango cha Nyantakara kilicho Kata ya Lusahunga na kufanya mkutano wao, huku wakimshambulia na kumjeruhi katibu wa kanisa hilo baada ya kuwaamuru watoke.

Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 3:00 asubuhi wakati wafuasi hao wa wanawake wa CCM, wakiongozwa na mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la John, walipoingia kanisani humo kwa madhumuni ya kuchukua viti kwa ajili ya mkutano wao. Badala ya kuchukua viti, waliamua kutotoka na kufanyia mkutano huo kanisani.

Akizungunza na Mwananchi katekista wa kigango hicho ambacho kipo katika parokia ya Kaniha, jimbo la Kahama, Faustine Damas alisema wafuasi hao wa CCM waliingia kanisani na kuchukua meza ya kuendeshea ibada na kuigeuza kuwa meza ya wageni wao na baadaye kuendesha mkutano wao.

Alieleza kuwa alipofika kanisani alistaajabu kusikia nyimbo wa 'Tieni, tieni' ukiimbwa na baada ya kuingia ndani alikuta wakiwa wanaendelea na mkutano wao huku wakitumia meza kuu ya ibada, jambo ambalo lilimfanya ampigie simu katibu wa kigango hicho, Festus Masumbuko ambaye baada ya kuwaomba waondoke na kuwanyang'anya meza hiyo ya ibada, wafuasi hao wa CCM walianza kumpiga.

"Waliamua kugoma kuondoka na ndipo alipowanyang'anya meza ya ibada, lakini wakamvamia na kumpiga mateke na ngumi. Wamemjeruhi vibaya na pia wamemchania shati," alieleza katekista huyo.

Alisema kutokana na hali hiyo alilazimika kupiga kelele na ndipo wananchi walipofika na kumwokoa. Lakini wakati hali hiyo ikiendelea, mfuasi mmoja wa CCM alipiga simu polisi na kuwaeleza kuwa walikuwa wakifanyiwa vurugu na ndipo polisi walipoenda eneo hilo na kuwakamata wananchi waliokuwa wanataka kumuokoa katibu.

Wananchi hao wanashikiliwa na polisi kwa kufanya vurugu katika mkutano huku wana CCM wakiachiwa huru na kuondoka zao.

Kutokana na hali hiyo paroko wa parokia ya Kaniha, Padri Isaya Bahati ambaye pia ni msaidizi wa askofu wa jimbo la Kahama, alisema muda mfupi baadaye akiwa polisi kuwa amesikitishwa na vurugu hizo na kusisitiza kuwa kanisa kama nyumba ya ibada inapaswa kuheshimika kwa vile si uwanja wala ukumbi wa mikutano.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, naibu katibu mkuu wa CCM, George Mkuchika alisema hana taarifa ya vurugu za wafuasi wake kanisani na kwamba kwa kuwa amepokea taarifa hizo, atazifuatilia kwa kina.

“Ngoja nifuatilie kwa kina kujua ni nini kimetokea,” alieleza Mkuchika.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Henry Salewi alisema kuwa hakuwa kwenye eneo la uchaguzi na kumtaka mwandishi awasiliane na kamishina Telesphol Anaclet ambaye ndiye amekuwa akishughulikia masuala hayo. Hata hivyo, kamishna huyo alisema jeshi la polisi linaendelea na masuala yake hivyo lipewe nafasi ya kufanya kazi.

“Naomba mtuache tufanye kazi yetu sina cha kukueleza kwa sasa,” alisema kamishina huyo wa oparesheni maalumu ya uchaguzi na akakata simu.

Waliokamatwa na jeshi hilo la polisi wametajwa kuwa ni Evarist Dotto, Semen Elias, Mosha Makoye, Batista na Timetheo ambao walitambulika kwa jina moja.

CHANZO: Mwananchi

HITIMISHO LISILOHITAJI TAFAKURI YA KINA NI KWAMBA CCM IMEFILISIKA KISIASA,NA KATIKA KUTAPATAPA KWAKE IKO TAYARI HATA KUWEKA REHANI AMANI NA UTULIVU WA TAIFA LETU.

NA KWA JINSI ILIVYOSHINDWA KUJINASUA NA TUHUMA KWAMBA INAKUMBATIA UFISADI NA MAFISADI,NI DHAHIRI KAMPENI ZA 2010 ZITASHUHUDIA MAZINGAOMBWE,UHUNI NA UPUUZI ZAIDI YA HUU.DINI NI KITU HATARI KINAPOTUMIWA KWA MINAJILI YA UBINAFSI WA KISIASA JAPO BINAFSI SINA KIPINGAMIZI NA KUCHANGANYA DINI NA SIASA ALIMRADI WAHUSIKA WAWE MAKINI KUTENGANISHA LIPI LA KAIZARI NA LIPI LA KIROHO.

30 Jun 2009





Kifo cha mtu maarufu huambatana na kila aina ya tetesi.Na kifo cha Michael Jackson is no exception.Ukisikiliza,kuona au kusoma kuhusu kifo cha mfalme huyo wa Pop,unaweza kumhukumu kirahisi tu kuwa alikuwa mithili ya mfu aliye hai (dead man walking).Baadhi ya vyombo vya habari vinadai Michael alikuwa akibwia madawa lukuki ya kumudu maumivu ya mwili.Mengine yanadai alikuwa amekongoroka kupita kiasi.Gazeti moja limekwenda mbali zaidi na kudai kwamba eti miezi michache iliyopita,ilibainika wazi kuwa Michael alikuwa na miezi si zaidi ya sita ya kuishi.Lakini picha hizi zilizopigwa wakati wa rehersal zake zilizopangwa kufanyika O2 Arena mwezi ujao,zinatoa taswira tofauti kabisa.


29 Jun 2009

Bwana Mapesa,John Momose Cheyo,Mbunge wa Bariadi kwa tiketi ya UDP akitoka nje ya jengo la bunge baada ya kukumbana na makali ya viwango na spidi vya Mheshimiwa Spika Samuel Sitta.Ironically,Cheyo ni mwandishi-mwenza (co-author) wa kitabu BUNGE LENYE MENO.

CHANZO: Jamii Forums




NI PIGO KUBWA KWA TAIFA NA PENGO LISILOZIBIKA.


KWA MARA NYINGINE,TANZANIA IMEPOTEZA MSOMI MAHIRI WA KIMATAIFA.

NI PIGO KUBWA HASA KWA VILE TAIFA BADO LINA MAPENGO YALIYOACHWA NA WASOMI WENGINE MAHIRI WALIOTANGULIA KWA MUUMBA,KAMA PROFESA CURTHBERT OMARI NA PROFESA CHACHAGE S. CHACHAGE.

MUNGU ILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI,AMEEN

28 Jun 2009


L’Oréal, the French cosmetics giant, whose advertising campaigns proclaim “because you’re worth it”, was found guilty of racial discrimination for considering black, Arab and Asian women unworthy of selling its shampoo.

France’s highest court was told that the group had sought an all-white team of sales staff to promote Fructis Style, a haircare product made by Garnier, L’Oréal’s beauty division.

The word went out that Garnier’s hostesses should be BBR — “bleu, blanc, rouge” — the colours of the French flag. The expression is widely recognised in the French recruitment world as a code for white French people born to white French parents, a court was told, in effect excluding the four million or so members of ethnic minorities in France.

La Cour de Cassation, the equivalent of the US Supreme Court, said that the policy was illegal under French employment law, upholding a ruling given by the Paris Appeal Court in 2007.

The judgment was a significant blow to the image of the world’s biggest cosmetics group, which has spent millions of dollars in global advertising campaigns featuring stars such as Andie MacDowell, Eva Longoria, Penélope Cruz and Claudia Schiffer.

That image already suffered a battering when L’Oréal executives were forced to deny claims that they had lightened the singer Beyoncé Knowles’s skin for a campaign last year. The ruling also hinted at widespread prejudice among French shoppers since L’Oréal believed that they were more likely to buy shampoo from white sales staff, the court was told.

The ruling will fuel anger among black and Arab French people, who complain that they face widespread discrimination when seeking employment.

The court ruled that Adecco, the temporary recruitment agency whose Districom division hired the hostesses, was also guilty of racial discrimination. The Paris Appeal Court had fined both L’Oréal and Adecco €30,000 (£25,500) and ordered them to pay a further €30,000 each in damages to SOS Racisme, the anti-racist campaign group, which brought the case. The court upheld the fines but told the appeal court judges to reconsider the damages.

L’Oréal expressed “disappointment” at the judgment, which ends three years of legal wrangling over the discrimination claims. Adecco declined to comment.

Samuel Thomas, the vice-chairman of SOS Racisme, described the ruling as a “very great victory”. He said: “Whatever the size of the company, none is able to escape prosecution.”

The court was told that a Districom executive had sent a fax to its headquarters in 2000 saying that Garnier’s hostesses should be aged 18 to 22, wear size 38 to 42 clothes (British sizes 8 to 12) and be “BBR”.

Prosecutors said that Garnier wanted to exclude members of the ethnic minorities on the ground that they would be less likely to sell its shampoo in French shops. The court was told that only 4.65 per cent of the hostesses hired for Garnier’s campaign were black, Asian or Arab.

Before the BBR fax went out, the agency had been offering a pool of candidates in which 38.7 per cent were from ethnic minorities, suggesting that they had been blocked during the final stages of recruitment.

Districom employees said that they were given oral instructions to favour white sales staff. But Thérèse Coulange, the deputy managing director of Districom, who sent the fax, said that she had merely wanted hostesses able to “express themselves correctly in French”. She said that the fax had been a personal initiative and not the implementation of company policy.

Laurent Dubois, Garnier’s former managing director, told a lower court that he had “never given the slightest order to discriminate against anyone” and described racial prejudice as “foreign to L’Oréal’s genes”.
SOURCE: The Times

27 Jun 2009


Kifo!

Yaani,licha ya kumaanisha mwisho wa safari ya uhai wa binadamu,kifo huambatana na matukio ya ajabu kabisa ambayo pengine yangepelekea tifu laiti marehemu angeweza kuyasemea.Nikupe mfano hai.Kabla ya kukutana na mauti,marehemu mama yangu aliugua kwa takriban miaka mitatu.Japo kwenye mambo ya imani za kidini tunaambiwa uzima na uhai ni mipango ya Mungu,mara kadhaa mikono ya binadamu wenzetu huhusika kuharibu au kutokomeza kabisa uhai wa binadamu wenzao.Maelezo ya kitabibu yalitufahamisha kuwa marehemu mama alifariki kutokana na sehemu kubwa ya ubongo wake kuathiriwa na mishtuko ya moyo (strokes) miwili aliyopata wakati wa uhai wake.

Mshtuko wa kwanza ulichangiwa na kitendo cha mtu wa karibu na marehemu.Alimfanyia tendo ambalo lilimwacha marehemu akisononeka hadi anaingia kaburini.Ni hadithi ndefu,na kwa vile pengine hapa si mahala mwafaka kuweka kila jambo wazi,nachoweza kukielezea ni namna mhusika huyo (alomtenda ubaya mama hadi akaishia kupata mshtuko wa kwanza wa moyo) "alivyojibaraguza" wakati wa mazishi ya mama Juni 2,2008.

Kuna takriban nyakati tatu hivi katika msiba ambazo kwa hakika zinatia uchungu usioelezeka.Kwangu,kwanza ilikuwa ni wakati wa taarifa kuwa "mama yako amefariki".Kwanza unaona kama ni utani,kisha inakuwa kama ndoto,lakini pindi akili inapofunguka na kugundua si utani wala ndoto,hapo ni bwawa la machozi,sambamba na mayowe ya kilio,na wengine huishia kumfuata wanayemlilia (kifo kinazaa kifo kingine).Pili ni wakati wa kuona maiti,aidha mortuary au wakati wa kuaga maiti kabla ya mazishi.Yaani hapo kumbukumbu zote za uhai wa marehemu zinakurejea.Tatu ni wakati wa kutumbukiza jeneza kaburini na kisha kufukia kaburi.Maneno "wewe xxx (jina la marehemu) mavumbini ulitoka,na mavumbini utarejea" (kwa sie Wakristo) ni machungu na yanaumiza mno!

Nirejee kwenye matukio ya siku ya mazishi ambayo laiti marehemu angeweza kusema lolote muda huo...!Tukiwa makaburini,yule kiumbe niliyemtaja awali kuwa alimtendea mama kitu kibaya kilichopelekea stroke alikuwa ameshikiliwa na watu wawili wakimdhibiti asijitumbukize kaburini!Yaani ungedhani ndio mtu mwenye uchungu mkuuuubwa kuliko hata sie wengine tuliokuwa tunajitahidi kujikaza japo kwa shida.Kwa sekunde kadhaa nilibaki nimeduwaa nikishangaa usanii wa mnafiki huyo.Huyu ni mtu aliyemchukia marehemu mama hadi siku anafariki,sasa iweje leo apandwe na uchungu kiasi cha kutaka kuingia na mama yangu kaburini?Laiti ningekuwa na bastola muda huo pengine saa hizi ningekuwa jela!

Hilo ni tukio la kweli.Ukitaka kushuhudia unafiki wa daraja la kwanza,nenda msibani.Sio kila chozi linalotiririka na yowe linalopigwa ni matendo ya dhati.Kuna wanaolia kutimiza wajibu na wengine "kuua soo".Utamliliaje mtu ulokuwa unamchukia wakati wa uhai wake?How come mauti yawe na thamani zaidi ya uhai?Au hayo yanafanyika kwa vile marehemu hawezi kuamka na kumsuta mtu?

Twende kwenye kifo cha Michael Jackson.Moja ya mambo yatakayokumbukwa zaidi kuhusu msanii huyu ni kipaji chake cha muziki kilichopelekea kupachika "cheo" cha mfalme wa pop duniani.Lakini ni jambo lisilofichika kwamba kwa miaka kadhaa kabla ya kifo chake hapo juzi,Michael alikuwa maarufu zaidi kwa vituko kuliko muziki wake.

Marehemu huwa hasemwi vibaya,na hiyo ni sehemu ya unafiki wa wanadamu wengi.Yayumkinika kusema kwamba Michael,kabla ya kesi ya udhalilishaji wa watoto,aliwapa kisogo watu weusi.Alitumia sehemu kubwa ya maisha yake kutafuta "uzungu" (kuwa mtu mweupe zaidi ya rangi ya mwili).Alipokumbwa na kesi hiyo,sapoti kubwa haikutoka kwa Weupe wenzake" bali Weusi ambao walifumbia macho dharau ya mfalme huyo wa pop dhidi ya asili yake.

Wapo wanaoona kifo cha msanii huyo mahiri kilikuwa kikijijenga kadri siku zinavyokwenda mbele.Hauhitaji kuwa mtaalam wa mwili wa binadamu kugundua kuwa transformation ya Michael kutoka mtu mweusi kuwa mweupe zaidi ya weupe wa kawaida ingeweza kuhatarisha afya yake.
Kulikuwa na tetesi kuwa alikuwa na kansa ya ngozi,just like tetesi kwamba kuna wakati pua yake "iling'oka"!Ukichanganya na vituko kama kumning'iniza mwanae katika dirisha la chumba kilicho juu ghorofani,kuficha sura yake na masks za ajabu ajabu,nk ni dhahiri kuwa alikuwa anajitengenezea njia ya mkato ya kumrejea Muumba.


Hata hivyo,ni muhimu kutambua kuwa kuna watu waliomfikisha Michael hapo alipofia.Inaelezwa kuwa mwanamuziki huyo alikuwa mhanga wa manyanyaso dhidi ya watoto yaliyokuwa yakifanywa na baba yake mzazi.Japo mzee huyo,Joe Jackson, alionekana kuwa bega kwa bega na mwanae wakati wa kesi yake (Michael) lakini hiyo haikusaidia kukwepa hisia za baadhi ya wachambuzi wa tabia waliokuwa wakimtuhumu kuwa ndio chanzo cha "kuharibika" kwa mwanae.

Yote katika yote,kwa vile wengi wetu tumemfahamu Michael kutokana na kipaji chake cha muziki,huku tukielezwa kwamba huenda kifo chake kimetokana na overdose ya painkillers alizokuwa akitumia ili arejee jukwaani kutuburudisha,ni dhahiri kwamba historia itamtendea haki ya kuendelea kumheshimu kama MFALME WA POP!Na katika hilo,kuna kila dalili kwamba atarejea kwenye chati za muziki duniani kutokana na kupanda kwa mauzo ya albamu zake kama sehemu ya kumbukumbu.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.