17 May 2010



Picha zaidi kuhusu ajali ya jana.



Jana majira ya saa 2 usiku nilishuhudia mzinga huu katika barabara ya Cumbernauld hapa Glasgow.

16 May 2010



It's been quite a while since our Dear leader Jakaya Mrisho Kikwete last visited the United Kingdom.As a seasoned world traveller,and in the spirit of the Anglo-Tanzania friendship,I suspect JK will be here sooner than later.And in an effort to maintain his record as the first African president to meet Barack Obama,he certainly could be here in a matter of weeks if not days.

Just because you poor souls can't afford to visit other areas in Tanzania either because the fares are too dear,or your intended destinations are inaccesible due to TRL taking a long break from serving walalahoi,or simply because you're scared of dying after looking closely at the growing figures of road accidents (and subsequent deaths) doesn't mean our Dear leader,God's choice,JK should not continue to 'accumulate his international air miles'.

Yes,as Basil Pesambili Mramba once said,a president cannot travel on top of a camel.Of course,he was not really defending that infamous decision to buy a rarely used Presidential jet but rather the dough on its way to his own bank account.

Satiric or not,truth remains that our leaders are so distant from the led that they hardly understand why people keep on complaining about one thing or another.It goes without saying that if Dr Shukuru Kawambwa were to be stranded at a train station for just a couple of hours due to the TRL bullshit,he surely would understand how it affects walalahoi.And if JK trips were to rely on ATC,he certainly would have thought the importance of having a 'living' national carrier (ATC is long dead except for the name and the likes of Mustafa Nyang'anyi who make most of what's left of the corporation).

It's down to such distance that,for instance,our God-sent president came to the decision to order DCs to carry out house house-to-house searches to 'catch' kids who didn't up to schools despite having been selected to join secondary education.Assuming the searches pay dividents,would the militias acting on powers invested to them by the DCs be turning up at the 'truant' kids' homes day in day out to force them to go to schools?Did His Excellency Jakaya do any brainstorming as to why these kids chose to abscond school in the first place?They certainly are not allergic to education,or are they?Would it still chasing these kids deemed necessary had the much-hyped 'secondary school in every ward' corresponded with number of desks for students,housing and salary on time for teachers,and such logistical considerations?Although I truly understand the importance of education,I think this misguided directive should rather target owners of Kagoda and their fellow mafisadi than our innocent kids.

I know the privileged fews whose hands are superglued to the national cake would regard this article as being seditious.Whatever!That's all I can tell them.

15 May 2010

Kwa hakika baadhi ya kauli za Rais wetu Jakaya Kikwete zinachanganya kupita kiasi.Juzijuzi tu alisaini kwa mbwembwe sheria tuliyoambiwa imelenga kudhibiti rushwa katika chaguzi.Tukiweka kando suala la wasaidizi wake kumwingiza mkenge kwa kuchomekea vipengele kinyemela,sambamba na mapungufu lukuki katika utekelezaji wa sheria hiyo (kubwa likiwa uswahiba kati ya CCM ya Kikwete huyohuyo na mafisadi),uamuzi wa kuwa na sheria hiyo ulileta faraja kidogo kwamba angalau mkuu wa nchi sasa anaanza kuikabili rushwa kwa vitendo badala ya maneno na ahadi tupu.

Sasa kabla hata sheria hiyo haijapata nafasi ya kutumika ipasavyo,JK kaja na hadithi mpya.Kwa mujibu wa vyombo vya habari,Rais amewaeleza viongozi wa dini kuwa suala la takrima kwenye chaguzi ni gumu kulidhibiti.Kama huelewi vizuri maana ya takrima basi naomba nikugamishe kuwa hiyo ni jina la kistaarabu (polite name) la rushwa au hongo wanayotoa wagombea kwa kisingizio cha 'ukarimu'.
Kinachonifanya nishindwe kumuelewa JK ni hiki: ina maana wakati anaipigia chapio sheria anayoamini itadhibiti rushwa kwenye chaguzi alikuwa hafahamu kuwa takrima (ambayo ni rushwa) ni ngumu kudhibitiwa? Au tuseme JK haamini kuwa takrima ni rushwa na ndio maana iliharamishwa?Na je kama takrima ni ngumu kudhibitiwa kwahiyo inakuwa halali?Je kiongozi wetu huyu haoni kuwa mkanganyiko anaozua unaweza kupelekea mvurugano baada ya uchaguzi ambapo wagombea watakaoshindwa kutokana na uwezo wao duni kumudu kutoa takrima wakikimbilia mahakamani,watoa rushwa (takrima) watatumia kauli ya JK kuhalalisha kuwa walichofanya ni sehemu ya utamaduni wetu wa ukarimu ("kama alivyobainisha Rais tarehe 14/05/2010)?

Habari kamili kuhusu kauli hiyo ya JK soma HAPA na HAPA.

14 May 2010

Labda na watawala wetu watakuwa na la kujifunza.

Habari kamili bonyeza HAPA.

Picha kwa Hisani ya SARAH wa Angalia Bongo.

Bila shaka ushaskia msemo wa Kiswahili 'Kufa Kufaana'.Nadhani kwa kimombo ndio tunachoita 'blessing in disguise'.Na ndivyo inavyoelekea kutokea katika sakata la 'ugomvi' kati ya msanii T.I.D na supastaa wa mpira wa kikapu,Mtanzania Hasheem Thabit,anayechezea timu ya Memphis Grizzliers kwenye ligi maarufu ya NBA huko Marekani.Katika pitapita yangu mtandaoni nimekuta habari hiyo imeshadakwa na vyombo vya habari vya kimataifa.Why not wakati Hasheem ni jina kubwa huko Marekani?

Sasa yayumkinika kusema kuwa sakata hilo limemnufaisha T.I.D 'kiaina' kwa vile katika kuripoti habari hiyo jina lake pia limekuwa likitajwa kama inavyoonekana katika habari ifuatayo kwenye mtandao wa kituo cha runinga cha FOX MEMPHIS cha huko Marekani:

MEMPHIS, Tenn. - The agent for Memphis Grizzlies center Hasheem Thabeet has told the team that an alleged incident involving Thabeet and R&B singer T.I.D never took place.


FOX13 Sports Director Matt Stark spoke with Ugo Udezue, Thabeet's agent, by phone Tuesday night, and Mr. Udezue said the allegations that Hasheem had knocked out the singer were completely false.


Udezue acknowledged that Thabeet was in a nightclub last weekend when an altercation broke out, but that the Grizzlies center was in a private section of the club and being protected by three bodyguards at the time, which is the norm for Thabeet when staying in Tanzania. Udezue says his client was immediately removed from the club, and was stunned later to hear the allegations that he had been involved.


Udezue said he believes the singer made the story up as a publicity stunt, and to get his music played on the radio.


Habari hiyo imekamata kasi kwenye mtandao kama inavyoonyesha HAPA.Japo natambua kuwa msanii T.I.D  'ana jina' kiasi chake katika anga za kimataifa,lakini ni dhahiri tukio hili linaweza kuwa limemtangaza zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

I just hope ugomvi huo haukuwa publicity stunt na publicity iliyojitokeza kwa T.I.D ni coincidental tu.Otherwise,mastaa wa kimataifa wataendelea kukutana na zahma kama hizo kwani zinaelekea kuwa na manufaa kwa upande mmoja wa wahusika wa tukio.

Ama kweli kufa kufaana!

Kuna wakati najiuliza kwanini sie masikini wa kutupwa ni hodari sana kwenye matumizi ya ovyo ovyo.Moja ya kumbukumbu za serikali ya awamu ya nne ilikuwa kuongeza mishahara ya wabunge licha ya hali yetu mbovu kabisa ya uchumi.Sambamba na hilo ni utitiri wa magari ya kifahari ambayo kimsingi si miongoni mwa vipaumbele kwa taifa masikini kama letu.

Wakati sie tunaendeleza matumizi ya kutapanya huku tukitembeza bakuli kwa wafadhili,serikali mpya ya hapa Uingereza chini ya David Cameron imetangaza kuwa mishahara ya mawaziri itapunguzwa kwa asilimia 5 na hakutakuwa na nyongeza katika mishahara hiyo (pay freeze) kwa miaka mitano.Mshahara wa sasa wa Waziri Mkuu Cameron utakuwa pungufu ukilinganisha na mishahara wanayolipwa meya wa manispaa mbalimbali 61 (kila manispaa hapa inajipangia kiwango cha mishahara ya viongozi wao kulingana na uwezo wa manispaa husika.Kukupa picha nzuri,alichofanya Cameron ni kama JK angeamua alipwe mshahara pungufu kulinganisha na meya wa manispaa ya Temeke au Kinondoni...ah,naota tu.Afanye hivyo achekwe!!!?)



Yah,unaweza kusema hizi ni mbwembwe tu za serikali mpya,au manjonjo tu,lakini ukweli ni kwamba serikali makini ni ile inayoonyesha kwa vitendo kuwa inatambua hali inayolikabili taifa.Cameron ameingia madarakani wakati Uingereza ikiwa kwenye msukosuko wa uchumi,na moja ya vipaumbele vya serikali yake ni kurekebisha uchumi mapema iwezekanavyo.

Kwa mujibu wa gazeti la The Sun la hapa,mshahara wa Waziri Mkuu Cameron umepunguzwa kwa pauni 7,500 na kubaki pauni 142,500.Mishahara ya Naibu Waziri Mkuu Nick Clegg na mawaziri wengine waandamizi itakatwa pauni 7,082 na kubaki pauni 134,565 huku mawaziri wa kawaida wakikatwa pauni 5,197 na kubaki pauni 98,740.Mishahara ya mawaziri 'wadogo' itakatwa pauni 4,707 na kubaki 89,435.Hatua hiyo ya kukata mishahara kwa asilimia 5 itaokoa pauni milioni 3.

Wakati hayo yanatokea,gazeti la Mwananchi lina habari kuwa nchi wahisani wanaochangia bajeti ya serikali yetu wameamua kuunguza mchango wao kwenye bajeti ya serikali kwa mwaka 2010/2011 kwa sababu mbalimbali, ikiwamo ni pamoja na kasi ndogo ya serikali katika kutekeleza mageuzi kwenye sekta za umma.

Taarifa ya wahisani hao iliyotolewa jijini Dar es Salaam juzi, inaeleza kuwa mwaka huo wa fedha, watatoa dola za Marekani 534 milioni sawa na Sh721bilioni, ambazo ni pungufu kwa Dola za Marekani 220 milioni sawa na Sh297 bilioni walizotoa mwaka 2009/2010.

Wahisani wa bajeti ya serikali ni Benki ya Maendeleo Afrika (ADB), Canada, Denmark, Jumuiya ya Ulaya (EU), Finland, Ujerumani, Ireland, Japan, Uholanzi, Norway, Sweden, Uswisi, Uingereza na Benki ya Dunia (WB) mwaka jana walichangia Sh1.9 trilioni katika bajeti ya serikali kupitia miradi ya maendeleo na mifuko ya kisekta.

Taarifa hiyo ilitaja maeneo ambayo serikali ilishindwa kufikia malengo kuwa ni mabadiliko ya haraka katika menejimenti ya sekta ya fedha za umma, mategemeo ya kuboreka kwa hali ya mazingira ya uwekezaji na uboreshaji wa huduma kwa kutoka sekta za umma.

Hii ni mara ya nne kwa wahisani hao kuiwekea ngumu serikali katika kuchangia bajeti yake kila inapofikia mwisho wa mwaka, kwa kushindwa kutekeleza mambo wanayofikiria wao kuwa ni muhimu zaidi katika maendeleo ya nchi.

Mwaka juzi wahisani hao waligoma kutoa fedha baada ya serikali kusuasua kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi wakiwemo wa fedha za EPA mpaka zilipofunguliwa kesi kadhaa ambazo mpaka sasa zinanguruma mahakamani.

Tatizo la viongozi wetu sie ni porojo nyingi na ulaghai mwingi wa kisiasa.Majukwaani wanahubiri kama watu wenye uchungu kweli na nchi yetu,lakini matendo yao tofauti kama kiza na mwanga.Tunapenda kuishi kifahari wakati uwezo wetu ni duni kabisa.Yani kuna wakati naangalia msafara wa Waziri Mkuu hapa,kisha nikikumbuka misafara ya viongozi wetu wakuu nabaki na maswali mengi kuliko majibu.Hebu angalia video hii hapo chini inayoonyesha msafara wa Gordon Brown siku alipokwenda makazi ya Malkia Elizabeth (Buckingham Palace) kuwasilisha ombi lake la kujiuzulu.

13 May 2010

Ndoa ya Mkeka.Haya ni mambo ya pwani zaidi kuliko 'bara'.Kule kwetu Ifakara hakuna vitu kama hivyo,lakini maeneo kama Tanga,Dar,Bagamoyo,nk ndoa za mkeka 'zinakula sahani moja' kwa umaarufu kama ndoa 'za kawaida'.Actually,ilikuwa almanusra 'nipigwe ndoa ya mkeka' wakati nilipoishi Tanga kwa takriban miaka 15 ilopita.Unajua tena mambo ya ujana...ukiyaangalia wakati huu wa utu uzima inabaki kichekesho.Anyway,kwa kifupi ndoa ya mkeka ni mithili ya fumanizi kati ya wanaovunja amri ya sita pasipo minajili ya kuwa wanandoa,na 'katika kuwapa one-stop fundisho na ufumbuzi' wanafungishwa ndoa ya chap-chap.It's like "si mnapenda kuvunja amri ya sita kisirisiri?Okay,sasa tunawahalalishia mtende manyotenda for the rest of your lives"...lol!Tatizo ni kwamba ni nadra kwa ndoa za mkeka kudumu kwa vile huwa ni'za kulazimisha'.Yani hazina tofauti na stori kama binti 'anayejiachia' na kupata ujauzito ili aolewe na mpenziwe.It rarely works!


Well,makala hii inazungumzia 'ndoa ya mkeka ya kisiasa' kati ya chama cha wahafidhina (Conservatives) na kile cha Waliberali (Liberal Democrats) ambao kwa pamoja wameunda serikali ya mseto hapa Uingereza. 

Uamuzi wa kiongozi wa Conservatives kuunda serikali ya mseto na Liberal Democrats umepokelewa kwa hisia tofauti huku watu wengi wakitabiri kuwa mseto huo hauna maisha marefu.Kikubwa kinachopelekea utabiri huo ni itikadi za vyama husika sambamba na tofauti zao katika sera zao.Japo tumeambiwa kuwa moja ya sababu zilizopelekea kufanikiwa kwa mseto huo ni kwa kila chama "kukubali matokeo" kwa aidha kuelegeza au kuachana kabisa na baadhi ya misimamo yao,hiyo haimaanishi kuwa misimamo hiyo imepotea 'vichwani' mwa wafuasi wa vyama hivyo.

Wakati wahafidhina wanafahamika kwa mrengo wao wa kulia na kati-kulia (right wing or centre-right politics) waliberali ni maarufu zaidi kwa mrengo wa kushoto na kidogo kati-kushoto (left wing or centre-left politics).Pengine hili sio rahisi sana kueleweka kama tukichukulia siasa zetu huko nyumbani kama mfano,kwani nadhani tunaweza kukubaliana kwamba nafasi ya mrengo katika siasa zetu huko Afrika ni ndogo sana.Yayumkinika kabisa kusema kuwa fedha za kukiwezesha chama au mgombea kununua kura ni muhimu zaidi kwenye siasa zetu kuliko mrengo wa chama au mgombea husika.Na hili ni tatizo kwa vile chama (au mgombea) kisicho na mrengo (au msimamo) ni sawa na bendera inayoweza kuelekea upande wowote ule kulingana na mvumo wa upepo.

Wenye hofu kuhusu 'ndoa ya mkeka' kati ya wahafidhina na waliberali wana sababu za msingi kwa vile mseto kati ya siasa za mrengo wa kulia na zile za mrengo wa kushoto hauko mbali sana na jitihada za kuchanganya maji na mafuta.Wakati chama cha Conservatives kinafahamika zaidi kwa siasa zake za kuwakumbatia matajiri huku zikiwakalia kooni 'walalahoi' kwa kudi kubwa (tayari kuna taarifa za 'kiama' cha kodi) waliberali wanafahamika zaidi kwa siasa za kuwa karibu na jamii huku vitu kama haki za binadamu,uvumulivu na ushirikiano vikiwa na umuhimu mkubwa.

Wakati Liberal Democrats walikuwa na sera ya msamaha (amnesty) kwa wahamiaji 'haramu' (illegal immigrants) huku wakisisitiza kuwa hatua kali dhidi ya wahamiaji hao si ufumbuzi kwa vile 'zinazidi kuwaficha msituni',chama cha Conservative kiliweka bayana msimamo wake wa kupunguza idadi ya wahamiaji kwa kuweka ukomo (cap) katika idadi ya wanaoingia/kuhamia Uingereza,sambamba na sheria kali za uhamiaji.Na katika hatua inayoweza kuwagharimu Liberal Democrats,chama hicho kimekubali kuachana na sera yake ya msamaha kwa 'wahamiaji haramu' na badala yake kimeafiki hatua ya Conservatives kuweka ukomo kwenye idadi ya wahamiaji wanaoingia nchini hapa.

Kuna tofauti ya kimtizamo kuhusu umoja na ushirikiano wa Ulaya.Wahafidhina wanasifika kwa upinzani wao dhidi ya suala hilo huku waliberali wakipendelea kuona ushirikiano huo ukisambaa zaidi ikiwa ni pamoja na wazo la Uingereza kutumia sarafu ya Euro badala ya Pound Sterling.Katika kufanikisha 'ndoa' yao,Liberal Democrats wamekubali kusitisha mipango yao kuhusu kukuza ushiriakiano wa Ulaya,jambo linaloweza kuwaudhi waumini wa siasa za chama hicho.

Lakini tayari kuna dalili za mpasuko kwenye 'ndoa hiyo ya mkeka' baada ya taarifa kwenye baadhi ya magazeti ya hapa kwamba 'Waziri' mpya wa fedha ((Kansela) George Osborne (wa Conservatives) amepinga vikali wazo kwamba 'Waziri' wa biashara (Business Secretary) Vince Cable (wa chama cha Liberal Democrats) ndiye atakayekuwa na dhamana ya kufanya mabadiiko kwenye mfumo wa mabenki (kwa minajili ya kudhibiti na kuzuwia uwezekano wa mtikisiko wa kifedha/kiuchumi kutokana na 'uzembe' wa mabenki katika utekelezaji wa sheria za fedha).Badala yake,hazina chini ya Osborne ndio itakayoshikilia dhamana ya utekelezaji wa sera ya mabenki na sekta ya fedha kwa ujumla.


Taarifa zaidi zinaeleza kuwa kuna hofu kuwa chama cha Liberal Democrats kitakimbiwa na idadi kubwa tu ya wafuasi wake kufuatia uamuzi wake wa kushirikiana na Conservatives.Hali hiyo sio tofauti sana kwa upande wa wahafidhina kwani kuna idadi kubwa tu miongoni mwao wanaoona 'ndoa hiyo ya mkeka' kuwa jambo lisilofaa.Pengine tatizo kubwa kwa vyama vyote viwili ni wale walio 'mwisho wa upande' wa mrengo wa vyama hivyo,yaani wenye mrengo wa kulia kabisa kwa upande wa Conservatives na wa mrengo wa kushoto kabisa kwa upande wa waliberali.Hawa ni watu wanaoongozwa na imani na itikadi,na haiwaingii akilini kuona mambo hayo ya msingi yakiwekwa rehani kwa minajili tu ya kuunda serikali.

Lakini kuna wanaoona kuwa 'ndoa hii ya mkeka' kati ya David Cameron na Nick Clegg inaweza kudumu kwa vile kimsingi viongozi hao wawili wana mambo kadhaa yanayoshabihiana.Wote walisoma shule 'za bei mbaya',wanatoka familia zenye uwezo mkubwa kifedha na,kimsingi, wanaishi katika tabaka tawala.Kwa minajili hii,baadhi ya wachambuzi wanatabiri kuwa mfanano wa haiba za Cameron na Clegg,na sio tofauti katika itikadi zao,utafanikisha kudumu kwa serikali hiyo ya 'ajabu' kati chama chenye siasa za mrengo wa kulia (conservatives) na kile cha mrengo wa kushoto (Liberal Democrats).

Pamoja na yote hayo,siasa ni mchezo usiotabirika.Siku chache zilizopita ingekuwa jambo lisilofikirika kwa wahafidhana na waliberali kushirikiana katika uongozi wa serikali,lakini leo hii 'habari ndio hiyo'.Basi kwa minajili hiyohiyo,haitokuwa ajabu kwa 'ndoa hii ya mkeka' kudumu muda mrefu kuliko inavyotarajiwa.

Muda utatanabaisha (time will tell).

11 May 2010




Gordon Brown has just announced on live tv that he is stepping down as the Prime Minister.It's now clear that the next PM shall be David Cameron.

. http://goo.gl/5bKK.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.