15 Sept 2010



A retired doctor held a slave in her suburban home for four years, a court was told yesterday. Saeeda Khan, 68, is accused of making Mwanahanisi Mruke work up to 24 hours a day cleaning, cooking and gardening. She fed her scraps of bread and made her sleep on a thin mattress on the kitchen floor with only a sheet for warmth, it was alleged.

 Khan and her late husband, who was also a doctor, allegedly paid Miss Mruke just £10 a month – a low salary even in Tanzania, the African country they brought her to Britain from in 2006. Miss Mruke, 46, had all her calls monitored and was not allowed to leave the £500,000 home in Harrow, North West London, without Khan, Westminster magistrates heard. ‘She lived in extremely poor conditions for a number of years,’ prosecutor Malachy Pakenham told the hearing. Additional payments of £40 a month were meant to go to a bank in Tanzania to pay for Miss Mruke’s daughter’s education, but much of this was never received, the court heard.

Khan, a British citizen who has lived in the UK for 30 years, is believed to be the first person charged with modern slavery. Scotland Yard detectives started investigating the case in February following a tip-off. Officers from the Human Exploitation and Organised Crime Command, known as SCD9, were involved. Khan did not have to sit in the dock during the ten-minute hearing because she suffers from arthritis and has recently had an operation on her knees.

She pleaded not guilty to a charge of arranging and facilitating the arrival of a foreign national with the intention of exploitation in the UK and elsewhere. The charge carries a maximum sentence of ten years in jail. Khan was bailed to appear before the court next month. Before she came to the UK, Miss Mruke worked in a hospital run by Khan’s late husband in Dar es Salaam, the capital of Tanzania. Khan is alleged to have kept her slave in her three-bedroom bungalow in Harrow which she shared with her 40-year-old son, who has mental health problems. Khan’s daughter, who also has learning difficulties, lived in the property too but has since moved out. Neighbours said Khan spent tens of thousands of pounds renovating the property when she moved in about a decade ago. Two cars, including a new Volvo estate, are usually seen parked in the driveway.

James Carpenter, who lives next door, said he often saw Miss Mruke going for walks with Khan’s son. He said: ‘She would follow him up and down the street, normally about ten yards behind him. ‘She only spoke the East African language of Swahili, so we couldn’t communicate with her and she couldn’t really speak to anyone. ‘Sometimes, we would wave and nod at her just to be polite. She would normally wave back. ‘She wore normal, western clothing. I had no reason to suspect anything untoward was going on. ‘But it’s a very quiet area and nobody round here really knows their neighbours very well.’

Slave trading has been outlawed in Britain since the 19th century. However, the UK remains a major destination for trafficked women. Human rights organisations claim up to 1,000 people are made to work as slaves.


Dharau inayoonyeshwa na mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kuendelea kutoa ahadi zaidi ilhali nyingi ya alizotoa mwaka 2005 hazijatimizwa,sasa imehamia kwa mkewe.Katika ukurasa wake wa Twitter (@salmakikwete),mke huyo wa Rais ameandika "“Tuwasikilize,tupembue chuya zikae upande wake,chenga upande wake na mchele ukae upande wake,tuseme lililo lililo la kweli,kama serikali haitatoza kodi,itaendeshaje shughuli zake?” Kauli hiyo pia inapatikana kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Kwanza,pamoja na kumheshimu kama First Lady lakini ilipaswa huyu mama akae kimya.Anatumia raslimali za taifa kumkapeni mumewe wakati anafahamu fika yeye (Salma) si mgombea.Huu ujasiri wa kinafiki wa kutetea kodi sijui unatoka wapi kwa vile tatizo letu kama taifa sio tu kwenye uzembe katika ukusanyaji kodi bali pia matumizi mabaya ya hata hiyo kodi ndogo inayokusanywa baada marafiki wa watawala kupewa misamaha ya kido kifisadi.

Hivi huyu mama anafahamu kuwa mumewe alipofanya ziara ya ghafla Bandari ya Dar es Salaam alitamka waziwazi kuwa anawafahamu watu wanaofanya ufisadi bandarini hapo?Na miongoni mwa ufisadi mkubwa sehemu hiyo ni dili za kukwepa kodi.

Sasa kama kweli ana uchungu na mapato ya serikali kwanini asimkumbushe mumewe kuhusu majina ya mafisadi wa Bandari ambao hadi dakika hii hajawataja au kuwasilisha majina yao kwa wahusika?

Kama unadhani namsingizi Kikwete hebu soma habari ifuatayoiliyochapishwa na gazeti la Nipashe la Machi 3 mwaka huu

Nawajua wanaosaidia kukwepa kodi TRA- Kikwete
2009-03-03 10:59:53
Na Joseph Mwendapole
Rais Jakaya Kikwete amesema ana orodha ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) wasio waaminifu ambao wanashirikiana na wafanyabiashara kukwepa kodi kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Alisema anaifanyia kazi orodha hiyo na akishamalizana nayo atamkabidhi Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya, ili achunguze na kuwafukuza kazi wafanyakazi watakaothibitika kujihusisha na vitendo hivyo.
Aliyasema hayo jana wakati akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari (TPA) na wadau wa bandari Tanzania alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni ufuatiliaji wa agizo alilotoa mwezi uliopita kupunguza msongamano wa makontena.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia watu wanaoikosesha mapato.
Akitoa mfano namna wizi huo unavyofanywa, Rais Kikwete alisema wanaweza kuendesha zoezi hilo kwa simu ambapo mtu aliyeko Dubai anapewa maelezo namna atakavyojaza fomu ili mzigo wake usipite kwenye scanner, hali inayoweza kupitisha mizigo haramu kama dawa za kulevya.
Alisema wafanyakazi na wafanyabiashara hao wanatumia udanganyifu kuwa kontena hizo zimebeba mitumba, kumbe ndani ya mitumba hiyo wakati mwingine inatumika kufunika magari.
``Ninayo orodha ndefu na nitaikabidhi kwa Kamishna Mkuu wa TRA, Kitilya ili awafuatilie na ahakikishe anawatimua kazi mara moja wale watakaobainika wanahusika na mchezo huo ili tuanze upya,`` alisema.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia kuwa na wafanyakazi wanaokula njama za kuipotezea mapato.
Kikwete alisema bandarini kuna uzembe mkubwa ambao hauvumiliki na aliuagiza uongozi kuondoa matatizo yaliyopo badala ya kukaa na kunung`unika.
Alisema msongamano wa makontena umekuwa ukiisababishia serikali kukosa mapato mengi na alisisitiza kuwa bandari ni sehemu muhimu ambayo serikali haiwezi kuiacha iwe ya hovyo.
Akiwa katika kitengo cha kuchunguza bidhaa katika kontena, Tiscan, Rais Kikwete alisema maelezo aliyopewa na TPA yanatofautiana na yale aliyopewa na viongozi wa Tiscan.
``Hapa mbona mimi sielewi naomba mnieleweshe, hawa Tiscan wanasema wana uwezo wa kuchunguza hata makontena 200 kwa siku ila wanasema tatizo ni nyinyi hamleti kontena za kutosha... Jamani fanyeni kazi na muachane na visingizio na malalamiko,`` alisema Kikwete.
Aliagiza mamlaka hiyo impe taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa upunguzaji wa makontena ndani ya wiki mbili zijazo na aliahidi kutembelea tena bandari hiyo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Forodha, Otieno Igogo, alimweleza Rais Kikwete kuwa wadau wa Bandari ya Dar es Salaam walikubaliana kulipa dola 30 ikiwa ni gharama za kuhamishia kontena moja katika bandari kavu.
Igogo alimweleza Rais kuwa ingawa wadau wote wamekuwa wakichangia, Kampuni ya Kimataifa ya Kupakua Kontena Bandarini (TICTS), imegoma kutoa fedha hizo.
Alisema dola 30 ambazo TICTS walipaswa kulipa kwa kila kontena linalohamishiwa bandari kavu kama wanavyolipa wadau wengine, zimekuwa zikitolewa na TPA.
Baada ya kauli hiyo ya Igogo, Rais alisema anashangaa kuona jeuri hiyo ya TICTS na kusema kuwa TPA ina mamlaka, lakini haitaki kuyatumia.
Kikwete alisema TPA imefanya vizuri kulipa gharama ambazo TICTS imekataa kuzilipa, lakini aliagiza mamlaka hiyo ihakikishe TICTS inazirudisha mara moja.
``Nyinyi mnashangaza sana, mna mamlaka, lakini hamyatumii... Sasa hizi gharama lazima walipe na wakiwashinda mwelezeni waziri na waziri akishindwa niambieni mimi,`` alisema.
Wakati huo huo, Kikwete alikataa maelezo marefu ambayo Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraem Mgawe, alitaka kuyasoma mbele yake na badala yake akamtaka amweleze sababu za msongamano kutoma lizika.
Baada ya kuelezwa hivyo, Mgawe alimweleza Rais Kikwete kuwa kikosi kazi kilichoundwa kufuatia agizo lake kinaendelea kujitahidi kuondoa msongamano uliopo.
Alisema Mamlaka inatarajia kuwa utekelezaji wa mikakati iliyowekwa itafanikisha kupunguza hali ya msongamano mwezi Machi mwaka huu.
Mgawe alisema katika kipindi cha mwaka 2007/08, TPA ilihudumia tani milioni 6.239, ambalo ni ongezeko la tani 227,222 au asilimia 3.8 ikilinganishwa na tani milioni 6.003 zilizohudumiwa mwaka 2006/07.
Alisema katika kipindi hicho mamlaka ilipata ziada ya Sh. bilioni 37.879 kutokana na mapato ya Sh. bilioni 168.789 na matumizi ya Sh. bilioni 133.909.
SOURCE: NIPASHE

Wito wangu kwa Salma Kikwete ni simple: kama alikuwa anataka kugombea uongozi angegombea lakini sio kuendelea kutumia raslimali za taifa kumkampenia mumewe.Anapaswa kutambua kuwa raslimali hizo zinagharamiwa na walipa kodi ambapo wengi wao si wana-CCM (takwimu za karibuni zinaonyesha wanachama wa CCM ni takriban milioni 5 tu kati ya Watanzania takriban milioni 45).

Tunatambua kuwa Salma anataka kuendelea kuwa First Lady lakini asifanye hivyo kwa kuwabebesha gharama Watanzania wote hata wasio wana-CCM.Anaweza kuitumia WAMA kumfanyia kampeni mumewe lakini Watanzania hawataki kuona ufisadi wa mchana mweupe unaofanywa kwa misingi ya kifamilia.

Naamini mwanamama huyu anafuatilia habari za kimataifa,na hivyo amesikia yaliyomkumba Vera Chiluba,mke wa aliyekuwa Rais wa zamani wa Zambia,Frederick Chiluba,aliyehukumiwa kwenda jela kwa ufisadi.

Ni vema Salma akasoma alama za nyakati ili pindi mumewe atakapokabidhi madaraka kwa Dokta Wilbroad Slaa hapo Novemba familia ya Kikwete isianze "kutafutana".

Na hiyo "tweet" yake ya kuchambua pumba na mchele nadhani ni vema akiielekeza kwa mumewe ambaye so far anaonekana kunogewa na "ugonjwa" wa kutoa ahadi.Mara uwanja wa ndege Kigoma,mara kuboresha kilimo cha kakao,mara atawapatia akinamama chanjo ya cervical cancer,mara vijiji 11 vya Mkinga vitapatiwa maji,mara hili mara lile alimradi ni "vurugu mechi ya ahadi".Kwani Rais wa Tanzania 2005-hadi sasa alikuwa nani kama sio Jakaya Mrisho Kikwete?Kwanini hayo anayoahidi sasa hakuyatekeleza katika awamu yake ya sasa?Na kwani tuamini kuwa atayatekeleza katika awamu yake ya mwisho-kipindi atakachokuwa bize kujitengenezea mazingira ya "kumpumzika kwa amani" kama Mkapa?

Blogu hii inawakumbusha tena wapiga kura kwamba Kikwete hayuko serious ndio maana ameamua kurejea nyingi ya ahadi zake za 2005 bila aibu wala kuwaomba msamaha Watanzania kwa kutozitekeleza.Kumrejesha tena Ikulu itakuwa ni kosa kubwa kupita kiasi kwani katika awamu yake ya mwisho atairejesha nchi yetu kwenye zama za mawe.

TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA
TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA
TANZANIA BILA KIKWETE,SIO TU INAWEZEKANA,BALI NI MUHIMU LAZIMA KWA USTAWI WA TAIFA LETU.
CHAGUA DOKTA SLAA KWA UKOMBOZI NA "UHURU WA PILI",CHAGUA CHADEMA KWA TANZANIA YENYE NEEMA.


Dharau inayoonyeshwa na mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kuendelea kutoa ahadi zaidi ilhali nyingi ya alizotoa mwaka 2005 hazijatimizwa,sasa imehamia kwa mkewe.Katika ukurasa wake wa Twitter (@salmakikwete),mke huyo wa Rais ameandika "“Tuwasikilize,tupembue chuya zikae upande wake,chenga upande wake na mchele ukae upande wake,tuseme lililo lililo la kweli,kama serikali haitatoza kodi,itaendeshaje shughuli zake?” Kauli hiyo pia inapatikana kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Kwanza,pamoja na kumheshimu kama First Lady lakini ilipaswa huyu mama akae kimya.Anatumia raslimali za taifa kumkapeni mumewe wakati anafahamu fika yeye (Salma) si mgombea.Huu ujasiri wa kinafiki wa kutetea kodi sijui unatoka wapi kwa vile tatizo letu kama taifa sio tu kwenye uzembe katika ukusanyaji kodi bali pia matumizi mabaya ya hata hiyo kodi ndogo inayokusanywa baada marafiki wa watawala kupewa misamaha ya kido kifisadi.

Hivi huyu mama anafahamu kuwa mumewe alipofanya ziara ya ghafla Bandari ya Dar es Salaam alitamka waziwazi kuwa anawafahamu watu wanaofanya ufisadi bandarini hapo?Na miongoni mwa ufisadi mkubwa sehemu hiyo ni dili za kukwepa kodi.

Sasa kama kweli ana uchungu na mapato ya serikali kwanini asimkumbushe mumewe kuhusu majina ya mafisadi wa Bandari ambao hadi dakika hii hajawataja au kuwasilisha majina yao kwa wahusika?

Kama unadhani namsingizi Kikwete hebu soma habari ifuatayoiliyochapishwa na gazeti la Nipashe la Machi 3 mwaka huu

Nawajua wanaosaidia kukwepa kodi TRA- Kikwete
2009-03-03 10:59:53
Na Joseph Mwendapole
Rais Jakaya Kikwete amesema ana orodha ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) wasio waaminifu ambao wanashirikiana na wafanyabiashara kukwepa kodi kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Alisema anaifanyia kazi orodha hiyo na akishamalizana nayo atamkabidhi Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya, ili achunguze na kuwafukuza kazi wafanyakazi watakaothibitika kujihusisha na vitendo hivyo.
Aliyasema hayo jana wakati akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari (TPA) na wadau wa bandari Tanzania alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni ufuatiliaji wa agizo alilotoa mwezi uliopita kupunguza msongamano wa makontena.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia watu wanaoikosesha mapato.
Akitoa mfano namna wizi huo unavyofanywa, Rais Kikwete alisema wanaweza kuendesha zoezi hilo kwa simu ambapo mtu aliyeko Dubai anapewa maelezo namna atakavyojaza fomu ili mzigo wake usipite kwenye scanner, hali inayoweza kupitisha mizigo haramu kama dawa za kulevya.
Alisema wafanyakazi na wafanyabiashara hao wanatumia udanganyifu kuwa kontena hizo zimebeba mitumba, kumbe ndani ya mitumba hiyo wakati mwingine inatumika kufunika magari.
``Ninayo orodha ndefu na nitaikabidhi kwa Kamishna Mkuu wa TRA, Kitilya ili awafuatilie na ahakikishe anawatimua kazi mara moja wale watakaobainika wanahusika na mchezo huo ili tuanze upya,`` alisema.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia kuwa na wafanyakazi wanaokula njama za kuipotezea mapato.
Kikwete alisema bandarini kuna uzembe mkubwa ambao hauvumiliki na aliuagiza uongozi kuondoa matatizo yaliyopo badala ya kukaa na kunung`unika.
Alisema msongamano wa makontena umekuwa ukiisababishia serikali kukosa mapato mengi na alisisitiza kuwa bandari ni sehemu muhimu ambayo serikali haiwezi kuiacha iwe ya hovyo.
Akiwa katika kitengo cha kuchunguza bidhaa katika kontena, Tiscan, Rais Kikwete alisema maelezo aliyopewa na TPA yanatofautiana na yale aliyopewa na viongozi wa Tiscan.
``Hapa mbona mimi sielewi naomba mnieleweshe, hawa Tiscan wanasema wana uwezo wa kuchunguza hata makontena 200 kwa siku ila wanasema tatizo ni nyinyi hamleti kontena za kutosha... Jamani fanyeni kazi na muachane na visingizio na malalamiko,`` alisema Kikwete.
Aliagiza mamlaka hiyo impe taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa upunguzaji wa makontena ndani ya wiki mbili zijazo na aliahidi kutembelea tena bandari hiyo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Forodha, Otieno Igogo, alimweleza Rais Kikwete kuwa wadau wa Bandari ya Dar es Salaam walikubaliana kulipa dola 30 ikiwa ni gharama za kuhamishia kontena moja katika bandari kavu.
Igogo alimweleza Rais kuwa ingawa wadau wote wamekuwa wakichangia, Kampuni ya Kimataifa ya Kupakua Kontena Bandarini (TICTS), imegoma kutoa fedha hizo.
Alisema dola 30 ambazo TICTS walipaswa kulipa kwa kila kontena linalohamishiwa bandari kavu kama wanavyolipa wadau wengine, zimekuwa zikitolewa na TPA.
Baada ya kauli hiyo ya Igogo, Rais alisema anashangaa kuona jeuri hiyo ya TICTS na kusema kuwa TPA ina mamlaka, lakini haitaki kuyatumia.
Kikwete alisema TPA imefanya vizuri kulipa gharama ambazo TICTS imekataa kuzilipa, lakini aliagiza mamlaka hiyo ihakikishe TICTS inazirudisha mara moja.
``Nyinyi mnashangaza sana, mna mamlaka, lakini hamyatumii... Sasa hizi gharama lazima walipe na wakiwashinda mwelezeni waziri na waziri akishindwa niambieni mimi,`` alisema.
Wakati huo huo, Kikwete alikataa maelezo marefu ambayo Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraem Mgawe, alitaka kuyasoma mbele yake na badala yake akamtaka amweleze sababu za msongamano kutoma lizika.
Baada ya kuelezwa hivyo, Mgawe alimweleza Rais Kikwete kuwa kikosi kazi kilichoundwa kufuatia agizo lake kinaendelea kujitahidi kuondoa msongamano uliopo.
Alisema Mamlaka inatarajia kuwa utekelezaji wa mikakati iliyowekwa itafanikisha kupunguza hali ya msongamano mwezi Machi mwaka huu.
Mgawe alisema katika kipindi cha mwaka 2007/08, TPA ilihudumia tani milioni 6.239, ambalo ni ongezeko la tani 227,222 au asilimia 3.8 ikilinganishwa na tani milioni 6.003 zilizohudumiwa mwaka 2006/07.
Alisema katika kipindi hicho mamlaka ilipata ziada ya Sh. bilioni 37.879 kutokana na mapato ya Sh. bilioni 168.789 na matumizi ya Sh. bilioni 133.909.
SOURCE: NIPASHE

Wito wangu kwa Salma Kikwete ni simple: kama alikuwa anataka kugombea uongozi angegombea lakini sio kuendelea kutumia raslimali za taifa kumkampenia mumewe.Anapaswa kutambua kuwa raslimali hizo zinagharamiwa na walipa kodi ambapo wengi wao si wana-CCM (takwimu za karibuni zinaonyesha wanachama wa CCM ni takriban milioni 5 tu kati ya Watanzania takriban milioni 45).

Tunatambua kuwa Salma anataka kuendelea kuwa First Lady lakini asifanye hivyo kwa kuwabebesha gharama Watanzania wote hata wasio wana-CCM.Anaweza kuitumia WAMA kumfanyia kampeni mumewe lakini Watanzania hawataki kuona ufisadi wa mchana mweupe unaofanywa kwa misingi ya kifamilia.

Naamini mwanamama huyu anafuatilia habari za kimataifa,na hivyo amesikia yaliyomkumba Vera Chiluba,mke wa aliyekuwa Rais wa zamani wa Zambia,Frederick Chiluba,aliyehukumiwa kwenda jela kwa ufisadi.

Ni vema Salma akasoma alama za nyakati ili pindi mumewe atakapokabidhi madaraka kwa Dokta Wilbroad Slaa hapo Novemba familia ya Kikwete isianze "kutafutana".

Na hiyo "tweet" yake ya kuchambua pumba na mchele nadhani ni vema akiielekeza kwa mumewe ambaye so far anaonekana kunogewa na "ugonjwa" wa kutoa ahadi.Mara uwanja wa ndege Kigoma,mara kuboresha kilimo cha kakao,mara atawapatia akinamama chanjo ya cervical cancer,mara vijiji 11 vya Mkinga vitapatiwa maji,mara hili mara lile alimradi ni "vurugu mechi ya ahadi".Kwani Rais wa Tanzania 2005-hadi sasa alikuwa nani kama sio Jakaya Mrisho Kikwete?Kwanini hayo anayoahidi sasa hakuyatekeleza katika awamu yake ya sasa?Na kwani tuamini kuwa atayatekeleza katika awamu yake ya mwisho-kipindi atakachokuwa bize kujitengenezea mazingira ya "kumpumzika kwa amani" kama Mkapa?

Blogu hii inawakumbusha tena wapiga kura kwamba Kikwete hayuko serious ndio maana ameamua kurejea nyingi ya ahadi zake za 2005 bila aibu wala kuwaomba msamaha Watanzania kwa kutozitekeleza.Kumrejesha tena Ikulu itakuwa ni kosa kubwa kupita kiasi kwani katika awamu yake ya mwisho atairejesha nchi yetu kwenye zama za mawe.

TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA
TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA
TANZANIA BILA KIKWETE,SIO TU INAWEZEKANA,BALI NI MUHIMU LAZIMA KWA USTAWI WA TAIFA LETU.
CHAGUA DOKTA SLAA KWA UKOMBOZI NA "UHURU WA PILI",CHAGUA CHADEMA KWA TANZANIA YENYE NEEMA.




13 Sept 2010



Hii ndiyo Bunda ya Dk. Slaa

Leo tuko Bunda. Acha picha hizi ziseme zenyewe. Maelezo mengine
baadaye. Itoshe tu kusema kwamba miongoni mwa maelfu ya wana Bunda waliofurika kumsikiliza Dk. Slaa katika viwanja vya Sabasaba ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Francis Isack. Alikaa jukwaa moja na Dk. Slaa, naye alimsifu kwa ukomavu wa kisiasa, lakini akamuonya kwamba kama alikuwa amekwenda pale kwa nia tofauti, atazame umma, apime nguvu yake na apeleke taarifa za kile anachosikia na kuona. Alimsimamisha DC huyo akawasalimia wananchi kwa kunyosha mikono juu.

Picha na Habari kwa Hisani ya NGURUMO

Je wajua kuwa licha ya mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kukacha mdahalo na wagombea wa vyama vingine anapatikana kirahisi mtandaoni ambapo "anauza" sera zake na "mafanikio" yake?Kama ulikuwa hufahamu basi nenda Twitter kisha tafuta @Kikwete2010 au nenda Facebook kisha tafuta Jakaya Kikwete.

I know siasa za chama kimoja zimeacha kasumba ya kufurahia kugusana mabega na watawala.No wonder kuna wenzetu muda huu wanakenua meno yote thelathini na kitu kwa vile wamepokea ujumbe kama huu "Kikwete2010 is following you..." au "Salma Kikwete is Following you..." 

Si ajabu kuna wenzetu wamefotokopi meseji za aina hiyo wakiamini kuwa Kikwete na mkewe Salma wanawajali saaaana hadi wameamua kuwa-follow up huko Twitter au kuungana nao hapo Facebook.KALAGABAHO!Kwanini hujiulizi WHY NOW?Kikwete na mkewe walikuwa Ikulu tangu Desemba 2005 na HAWAKUKUTAFUTA.Hushangai kwanini leo wanataka urafiki nawe?Well,sio kosa kuwa rafiki na rais au mkewe lakini urafiki huu hauna tofauti na ule wa mtenda tendo la ndoa na kondomu.Zana hiyo (kondom) huwa na umuhimu wa kipekee (kwa wale wanaojali) kabla na wakati wa tendo la ndoa,lakini pindi shughuli ikimalizika kondom huwa ni uchafu usiovumilika.ANGALIA,usijetumika kama kondomu: Kikwete akuone muhimu sasa kwa vile anahitaji kura lakini akakusahau (kama alivyokusahau 2005-till now) baada ya kurejea Ikulu.

Badala ya ku-retweet kila anachoandika,tumia haki yako kama Mtanzania kuhoji masuala mbalimbali yanayolikabili taifa.Twende mbali zaidi ya kupongeza na kuona sifa "kugusana mabega" na watawala.Sio kosa kushabikia lakini ushabiki wenye maana ni ule unaombatana na matumizi sahihi ya akili.

Now you-in case you didn't.Muulize Kikwete,je ile kauli aliyotoa mwaka 2006 kuwa anawafahamu wala rushwa kwa majina ila anawapa muda wa kujirekebisha imefikia wapi?Je wameshajirekebisha?Je anaweza kututajia majina ya waliojirekebisha na waliogoma kufuata ombi hilo la kichovu?

Muulize pia kwamba kabla ya sakata la Richmond aliahidi kuwa tatizo la umeme lingebaki kuwa historia.A few months later,matapeli wa Richmond wakaingia kwenye picha.Today,tatizo la umeme ni as sugu as ufisadi.Mkalie kooni na kumhoji,kama huko nyuma alitoa ahadi ya kutupatia ufumbuzi wa umeme na hakutimiza,kwanini tumwamini sasa?

Muulizie pia kama bado anaamini kuwa mimba za wanafunzi wa kike zinasababishwa na kimbelembele chao.Yah,muulize swali hilo kwa vile hadi sasa bado hajakanusha au kuwaomba msamaha Watanzania kwa kauli hiyo ya kizembe.

Usikose kumuuliza pia kama hadi sasa hajui sababu zinazoifanya Tanzania kuwa masikini maana alinukuliwa akijiuliza swali hilo.Nenda mbali kidogo na kumhoji kama alikuwa hajua kwanini Tanzania ni masikini sasa anafanya nini hapo Ikulu?

Sasa hivi amenzisha hash tag #Mafanikio huko Twitter.Hapo utapata nafasi nzuri ya kujionea waziwazi namna Awamu ya Nne ya Kikwete ilivyoshindwa kuikomboa Tanzania kutoka kwenye umasikini licha ya raslimali lukuki tulizonazo.Hapo Kikwete na wapambe wake wanataja mapato yaliyotokana na utalii na madini.Mkalie kooni na kumhoji kama mapato ndio hayo,kwanini sie bado masikini?Fedha hizo zimeenda wapi kama sio kwenye akaunti za mafisadi?Na kwenye utalii muulize pia kuhusu meno ya tembo yaliyokamatwa huko Hong Kong yakitokea Tanzania.

Kumbuka,usikubali kutumika kwa maslahi ya mtu mwingine.Kumhoji mwanasiasa anayeomba kukuongoza ni haki yako.Usiichezee.Badala ya kujipendekeza kwa RT (Retweets za Kikwete2010) tumia fursa hiyo kumuuliza maswali ya msingi yanayohitaji majibu ya haraka.

PAMOJA TUNAWEZA

12 Sept 2010












Sijui ndio dalili kuwa mwenendo wa kampeni unakwenda ovyo au ni ubabaishaji tu,lakini "mkwara" uliochimbwa na mnajimu mahiri,Sheikh Yahya Hussein,kwamba anampatia Rais Jakaya Kikwete ulinzi wa majini ni suala linalopaswa kukemewa kwa nguvu zote.Na ukweli kwamba mtajwa-i.e. Kikwete- amekaa kimya ni ushahidi tosha kuwa ananufaishwa na majini hayo.

Kwa baadhi yetu tunaofahamu yanayofanyika "nyuma ya pazia" (behind the scene) hatushtushwi kihivyo na habari hizo kwa vile siasa za Tanzania na ushirikina ni kama samaki na maji.Hakuna msimu mzuri kwa waganga wa kienyeji kama huu wa uchaguzi ambapo wanasiasa wababaishaji wanajaribu kupata msaada wa nguvu za giza ili wapate ushindi.

Awali,Sheikh Yahya alitoa tishio kuwa atakayejitokeza kuwania nafasi ya urais na Kikwete atakutwa na mauti.Well,so far tukio pekee la kutishia uhai wa mwanasiasa katika harakati za uchaguzi wa mwaka huu ni kudondoka jukwaani kwa Kikwete wakati anazindua kampeni zake kwenye viwanja vya Jangwani.Whether majini yaligoma kutumikishwa au Kikwete alikiuka masharti ya mganga wake Sheikh Yahya leaves a lot to be desired.

Binafsi natafsiri tishio hili jipya la Sheikh Yahya kama mkakati mufilisi wa Kikwete na CCM yake kuwatisha wapiga kura.Yea,kwani kama si hivyo kwanini basi mhusika asikanushe hadharani na kusema "ulinzi pekee nilionao ni huu unaotolewa na Idara ya Usalama wa Taifa".Hawa ni wataalam wa ulinzi wa viongozi na wanalipwa kwa ajili ya kazi hiyo.Sasa kama kuna ulinzi mwingine wa nguvu za giza,na ambao Kikwete anauamini,basi pengine ni muhimu kuokoa fedha za walipa kodi kwa kusitisha ulinzi anapotatiwa na "walinzi binadamu" na abaki na hayo majini ya Sheikh Yahya.

Samahani kama nitakuudhi lakini nashawishika kueleza kuwa napatab tabu sana kuelewa kwani pamoja na madudu yote haya-from sera to ushirikina,from afya mgogoro to kurudia ahadi za 2005 as if hii ndio mara ya kwanza kwa JK kuwania urais-bado kuna Watanzania wenzetu wanatamani mwanasiasa huyu na chama chake warejee madarakani.Jamani,hivi Kikwete na CCM wafanye nini zaidi ili mfikie hatua ya kusema "aah sasa basi,just go away!"?

Hivi mkiweka kando ushabiki,hizi "ahadi za fotokopi" anazotoa Kikwete zilishindikana vipi kutekelezwa katika miaka yake mitano aliyokuwa madarakani?Hata kama angejitetea kuwa muda mwingi alikuwa nje ya nchi kutalii bado alikuwa na baraza kubwa la mawaziri ambalo lingeweza kabisa kutekeleza maagizo yake.

Kama mnampenda kwa dhati basi bora msimpe kura ili aweze kupumzika kwa amani kwani kumrejesha tena Ikulu hapo Oktoba ni kumbebesha mzigo ule ule uliomshinda katika miaka mitano tunayomaliza.Hii ni kwa faida yake na yenu.Na anazidi kuwaonyesha kuwa badala ya kutegemea mambo halisi kufikia malengo yaliyokusudiwa,sasa kageukia majini.Nchi haiwezi kuongozwa kwa msaada wa majini.Na kamwe Tanzania haiwezi kupiga hatua kama miongoni mwa wasaidizi wa Rais ni majini.

MPIGA KURA,SHEIKH YAHYA AMEKUPA SABABU NYINGINE KATI YA NYINGI ZILIZOPO ZA KUMNYIMA KURA YAKO KIKWETE.KURA KWA KIKWETE ITAKUGHARIMU MIAKA MITANO IJAYO AMBAPO LICHA YA UFISADI,FEDHA ZA WALIPAKODI ZITATUMIKA KULIPA FADHILA KWA MAJINI WANAOMPATIA ULINZI WAKATI HUU WA KAMPENI.

KUMBUKA JINI LIKITOKA KWENYE CHUPA HALIRUDI.IN CASE YOU FORGET,VIDEO IFUATAYO ITAKUKUMBUSHA(GENIE IN A BOTTLE)




Yesterday,the world joined Americans in remembering the 9/11 terrorist attacks which left scores dead and many others injured.The aftermath of the attacks has completely transformed global politics and rekindled hostile relations between the West and the Muslim world.Is the US,and the world in general,safer from further terrorist attacks?Is there a possibility of another 9/11 in the future (God forbid)?

Despite varying opinions on the subject,it is fair to conclude that terrorism remains the main threat to mankind to-date.Unfortunately,some of the actions taken by the Americans after the 9/11 attacks have somehow served as recruitment tools for future terrorists.The Iraq invasion,for instance,had little to do with 9/11 although George Bush and his fellow neo-cons tried their best to sell the idea,and eventually failed.Of course,it was necessary to bring an end to Saddam Hussein's evil rule,but, arguarbly,not at the cost the world is likely to pay.The invasion has most likely acted as a huge recruitment tool for terrorist in the Gulf region.Presence of the US troops in the country became an instant pull factor for terrorists from different parts of the world.

Although the US invasion of Afghanistan could be justified,mainly due to the fact that the Taliban offered a safe haven for Osama bin Laden,the alleged mastermind of the 9/11 attacks,there are growing signs that the war would ultimately be concluded without a clear victory,just as the case has been in Iraq.Worse still,Osama is still at large,and his capture-if it ever happens-would probably be by sheer luck than the US military and intelligence might.

The 9/11 terrorist attacks escalated the West-Muslim world relations, already uneasy,to  more confrontational stance.The US and other Western countries were willing to sacrifice civil liberties in the name of national security.As a result,the minority Muslim population in these countries became even more alienated as they became the prime targets of some draconian anti-terror legislations.Scores have since then been arrested and put into detention with most denied access to legal representation.The mere existence of the Guantanamo facility is a clear evidence as to how a nation many tend to turn to for global  leadership of the free world is in fact abusing civil liberties.

However,intelligence and security matters are quite complex.Actually,speaking from a professional point of view,the fact that there has never been another terrorist attack in the US should certainly be perceived as quite a success for the various organisations entrusted by the Americans to keep them safe.While such organisations are required to be vigilant 24/7,a terrorist needs only a minute if not seconds to succeed in their evil mission.

All in all,for the world to be such a nice place to live,the threat from terrorism needs to be eliminated at least to a maximum level.Unfortunately,the future does not look so promising.In some way,the West is still not doing enough to address what some objective observers regards to be the pull factors in Islamic radicalisation.I will mention a few with Tanzania being a specific case.

Many studies on Islamic radicalism have shown that poverty plays a crucial role in attracting secular Muslims to turn into Islamic extremists.My own research has so far pointed out that one of the major factor for the rise of Islamism in Tanzania is,putting it bluntly,poverty.During my fieldwork,some respondents who supported the Islamist cause in the country confirmed that their participation in various Islamist groups in Tanzania was a way to protest against the State.Such groups offered them a platform to address social and economic problems facing the country.

Tanzania has emerged as "darling of the West" despite rampant corruption and inherent social injustices.The current regime under President Jakaya Kikwete who is vying for a second term in the coming elections in October has wrecked the fragile economy while trading in dangerous grounds by promising unrealistic solutions to the grievances by the disgruntled Muslim population e.g. promising re-establishing Kadhi courts and joining the OIC.Five years later,such promises which were given during the 2005 General Election campaigns are yet to be realised,putting the country in a compromising position for possible troubles in the future.

Ironically,Kikwete has been showered with praises for his leadership,with the latest coming from the UN Secretary General,Ban Ki-Moon wishing him victory in the forthcoming election.He was also the first leader from Africa to meet President Barack Obama since he got into the White House.It is widely known in the security circles that the American interest on Tanzania is in their effort to contain a growing terrorist threats posed by various Islamist groups in Somalia.The West has turned a blind eye to what is currently happening in Tanzania just because their strategic interest in the country are far more important than the welfare of the majority of Tanzanians.Undoubtedly,Kikwete and his party will portray themselves to voters as being trusted by the West,and therefore try to win some cheap votes.

It is fair to say that the huge share of Africa's stolen wealth is in some Western financial institutions.It also makes no sense at all to see the West pouring aid to African countries when some part of such aid is either used to oppress democracy at a local level or strengthening corrupt regimes such as Tanzania's.As a result,the majority poor would readily fall victim to religious fanatics who promise heaven to them while doing their best to fill the vacuum caused by the State in provision of basic social and economic needs.

I am not calling for suspension of aid but what Africans need is transparent and responsible aid.For such aid to be effective,donor countries have to make sure that the money they offer benefit the whole population and not just a clique of corrupt politicians.The same strictness that some Western governments have shown towards recipients of stimulus packages in their countries should be applied to recipients of their aid.

Finally,as this year's 9/11 commemoration was overshadowed by  the crazy threat  by a Florida-based "twisted pastor" Terry Jones that he would burn the Holy Koran,it is worth reminding all peace-loving people of the world that replicating what the terrorists are doing will only give them further excuses to continue with their evil acts.A blank hate towards all Muslims would only encourage even those who are totally opposed to religious extremism to join forces with terrorists.

Let's work together,regardless of our faiths, to keep the world a better place to live.

9 Sept 2010

Image and video hosting by TinyPic
Waandishi Wetu
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewazuia wagombea wake wa ubunge kushiriki katika mdahalo unaoendeshwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa kuhusisha wagombea wa vyama vyote katika kila jimbo.
Kipindi hicho kinarushwa kila Jumanne kupitia Kituo cha Televisheni cha TBC1 kwa lengo la kuwasikiliza wagombea wakijinadi pamoja na kunadi sera za vyama vyao.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana zimeeleza kuwa wagombea wa CCM wamezuiwa kushiriki mdahalo huo kwa barua iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa chama hicho,Yusuf Makamba kwenda kwa makatibu wa chama wa wilaya na mikoa yote nchini.

"Ninawaandikia kuwajulisha kwamba, wagombea wetu wasishiriki katika aina hiyo ya mdahalo, mpaka hapo mtakapoelezwa vinginevyo.” imesema sehemu ya barua hiyo ambayo nakala yake imepelekwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania, TBC.

Hata hivyo tayari wagombea kadhaa wa ubunge wa CCM wameshiriki kipindi hicho kilichoanza kurushwa hewani mbili zilizopita kwa kuwakutanisha wagombea ubunge wa vyama mbalimbali vya siasa nchini.

Baadhi ya wagombea ubunge wa CCM waliokwisha shiriki mdahalo huo ni pamoja na Hawa Ngh’umbi wa Jimbo la Ubungo na Chrispin Meela anayegombea ubunge katika jimbo la Vunjo.
"Kipindi hicho kimerushwa hewani kwa mara ya kwanza katika Jimbo la Ubungo Dar es Salaam na mgombea wa CCM alishiriki, sijui kwa maelekezo ya nani. Sina tatizo na kipindi. Nina tatizo na ushiriki wetu," ainasema sehemu ya barua hiyo ya Katibu Mkuu.

Katika kipindi hicho wagombea ubunge wa vyama mbalimbali huulizwa maswali na wasikilizaji na watazamaji wanahudhuria katika mdahalo huo.

Kipindi hicho kiliporushwa kwa mara ya kwanza katika Jimbo la Ubungo, mgombea wa CCM (Hawa Ngh’umbi )alipata wakati mgumu kujibu maswali ya watazamaji wa kipindi hicho na kuishia kupandwa na jazba nakutishia kumshitaki, mtu aliyemuliza swali gumu.

Katika barua yake hiyo ya Agosti 31, mwaka huu, Makamba licha ya kukitilia mashaka kipindi hicho na alihoji mgombea wao wa Ubungo alishiriki kwenye mdhahalo huo kwa maelekezo ya nani.
Katika kile kinachoweza kutafsiriwa kwamba agizo hilo la Makamba limeanza kutekelezwa, juzi mgombea ubunge wa CCM katika Jimbo la Arusha Mjini, Batilda Buriania hakushiriki kipindi hicho.

Hata hivyo, Batilda alisema hakuhudhuria mdahalo wa Arusha kutokana na chama chake kutopewa taarifa na yeye ni mgombea wa CCM sio mgombea binafsi.


“Nimekuwa nikitumiwa ujumbe wa simu kuwa nimeingia mitini katika mdahalo…mimi siwezi kuingia mitini nimedhuria midahalo mikubwa tena ya kimataifa ndani na nje ya nchi siwezi kukimbia hivi sasa,”alisema Dk Batilda.

Barua hiyo yenye kumbukumbu namba CCM/OND/SG/194/9 ya Agosti 31 ambayo Mwananchi imefanikiwa kuiona, Makamba aliwaambia makatibu hao wa CCM kuwa wagombea wote wa chama hich wasishiriki kipindi hicho hadi CCM itakapotafakari kwa kina manufaa itakayopata kwa kushiriki kwao
Alisisitiza kuwa CCM ina utaratibu wake wa kujinadi na kunadi sera zake kwa wananchi ambao anaamini kuwa bado unakidhi haja.

“Tuna utaratibu mzuri wa kijinadi na kunadi sera zetu kwa wananchi; utaratibu wa mikutano ya hadhara na mikutano ya ndani. Utaratibu huo bado unakidhi haja. Tunaendelea nao,” alisema Makamba.

Akizungumza na gazeti hili jana, Makamba alisisitiza akisema: "Hatutaki. Tumekataa ndio. Sisi yetu ni mikutamo ya hadhara. Tutaeleza huko malengo, ilani yetu na sera zetu kwa wananchi. Hatuoni sababu ya kukaa katika chumba kidogo na kuwapa nafasi ya ushiriki watu wachache."

Aliendelea: "Hatuoni sababu ya kwenda kwenye huo mjadala kwa kuwa mikutano yetu ya hadhara inajitosheleza."

Alipotakiwa kueleza kama chama kitawachukulia hatua wagombea wake waliokwishashiriki kipindi hicho, Makamba alijibu: "Hakuna adhabu watakayochukuliwa kwa sababu chama kilikuwa hakijatoa maagizo."

Taarifa zilizopatikana baadaye jana zilieleza kwamba, agizo hilo la Makamba pia limepokelewa katika jimboni Karatu ambako mgombea ubunge wa CCM aliamua kujitoa kwenye mdahalo huo juzi.

Mdahalo wa wagombea wa jimbo hilo, ulipangwa kufanyika juzi katika ukumbi wa maendeleo Karatu, lakini wakati wagombea wengine wakiwa wanajiandaa, taarifa zilitolewa kuwa mgombea wa CCM, Dk Wilbard Lorry hawezi kuhudhuria.

Viongozi wa vyama vya Chadema na CUF, katika wilaya hiyo, walilalamikia kuahirishwa ghafla kwa mdahalo huo wakati walikuwa wamesitisha kampeni vijijini na kurudi Karatu.

Katibu wa CUF Wilaya ya Karatu, Stivin Siay alisema chama chao kilikuwa kimemwandaa mgombea wake kwa mdahalo huo.

“Tunashangaa kujiondoa kwa CCM katika mdahalo huu kumesababisha mdahalo kuahirishwa…,” alisema Siay.

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya ya Karatu, Moshi Darabe alisema walipata taarifa za kuahirishwa mdahalo huo dakika za mwisho kwa maelezo kuwa mgombea wa CCM hatahudhuria.

Alisema taarifa hizo kwanza zilipatikana ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, ambao ndio awali walitoa taarifa za kuwepo maombi ya TBC kuandaa mdahalo huo.

Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Karatu, Clemence Berege akizungumzia kuahirishwa kwa mdahalo huo alisema kwamba, ofisi yake haihusiki kwani waliotaka kuendesha mdahalo huo ni TBC.

Habari hii imeandaliwa na Mussa Juma, Arusha na Exuper Kachenje

Chanzo: Mwananchi


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.