Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida mahiri la Raia Mwema inazungumzia changamoto zinazoikabili Idara yetu ya Usalama wa Taifa (TISS).BONYEZA HAPA kuisoma pamoja na habari na makala nyingine moto moto ndani ya jarida hili makini kwa habari na uchambuzi.
31 Mar 2011
26 Mar 2011
Habari na picha hii zimetumwa na mdau wa Mbeya yetu,nami naiwasilisha kama ilivyo...with no comment!
Mganga mwingine wa tiba za magonjwa Sugu aliyefahamika kwa jina la Jafar Welino(17) mkazi wa mtaa wa Mianzini Kitongoji cha Mabatini jijini Mbeya ameibuka na kutoa tiba kwa mamia ya wakazi wa jiji la Mbeya na viotongoji vyake.
Umati wa watu ulionekana katika nyumba anayoishi kijana huyo wakisubiri kupatiwa tiba hiyo huku wakiwa na vikombe vyao mikononi. Baadhi ya wananchi waliofika eneo hilo walidai kuwa wamefika hapo kutokana na taarifa za kuwa kijana huyo anatibu magonjwa Sugu bure kama vile ambavyo anatibu Mchungaji mstaafu wa Loliondo Mzee Ambilikile Mwasapila.
Akizungumza kwa niaba ya kijana huyo mama mkubwa wa mganga huyo aliyejitambulisha kwa jina la Edina Sanga alisema kuwa kijana huyo alianza tiba hiyo wiki mbili zilizopita ambapo kabla ya kuanza kutibu alimueleza mama yake huyo kuwa alitokewa na mama yake mzazi a,mbaye kwa sasa ni marehemu akimuelekeza kurithi mikoba yake.
Bi.Sanga alisema kuwa mama yake kijana huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa ni mtu mwenye maruhani ambapo kwa kutumia maruhani hayo alikuwa akitoa tiba kwa wakazi mbalimbali mjini Mbeya.Alisema kijana huyo ambaye wamezaliwa mapacha na dada yake aliyemtambulisha kwa jina la Hadija Welino kwamba yeye anasoma kidato cha Nne katika shule ya sekondari Itende.
Hata hivyo Bi.Sanga alisema kuwa kijana huyo aliitwa katika ofisi ya Ofisa Mtendaji ili kutoa maelezo ya namna ambavyo anaendesha tiba hiyo na kuwa hata hivyo anaendelea kutoa tiba kwa watu kwa kunywa vikombe viwili kwa muda wa siku mbili. Alisema kuwa dawa hiyo aliifuata katika kijiji cha Iyula kilichopo wilayani Mbozi na kuwa mara alipofika alianza kuichemsha na kuwagawia wananchi wanaosumbuliwa na maradhi sugu. Aidha umati wa watu walikuwa wamejipanga katika mistari kusubiri tiba hiyo ambapo
Mwenyekiti wa mtaa wa Mianzini Bi.Elizabethy Mwakabungu aliweka utaratibu wa wananchi kupata tiba ikiwa ni pamoja na kuchangia fedha kidogo kwa ajili ya kununulia kuni za kuchemshia dawa hiyo.Akizungumza na umati wa watu waliokuja kujipatia tiba hiyo Mwenyekiti huyo wa mtaa alisema kuwa kila ambaye atapata kikombe kimoja cha dawa anatakiwa kupata kikombe cha pili siku inayofuata.
‘’Mganga katuagiza kuwa kila anayekunywa kikombe kimoja anatakiwa kunywa kikombe cha pili siku inayofuata…yeyote atakayekunywa hatakiwi kunywa pombe kwa muda wa siku saba,’’alisema Bi. Mwakabungu
Wakipata kikombe
maelekezo ya kufika eneo hilo
Pamoja tunaendeleza kupashana Habari
HABARI NA PICHA: Mbeya Yetu
Mganga mwingine wa tiba za magonjwa Sugu aliyefahamika kwa jina la Jafar Welino(17) mkazi wa mtaa wa Mianzini Kitongoji cha Mabatini jijini Mbeya ameibuka na kutoa tiba kwa mamia ya wakazi wa jiji la Mbeya na viotongoji vyake.
Umati wa watu ulionekana katika nyumba anayoishi kijana huyo wakisubiri kupatiwa tiba hiyo huku wakiwa na vikombe vyao mikononi. Baadhi ya wananchi waliofika eneo hilo walidai kuwa wamefika hapo kutokana na taarifa za kuwa kijana huyo anatibu magonjwa Sugu bure kama vile ambavyo anatibu Mchungaji mstaafu wa Loliondo Mzee Ambilikile Mwasapila.
Akizungumza kwa niaba ya kijana huyo mama mkubwa wa mganga huyo aliyejitambulisha kwa jina la Edina Sanga alisema kuwa kijana huyo alianza tiba hiyo wiki mbili zilizopita ambapo kabla ya kuanza kutibu alimueleza mama yake huyo kuwa alitokewa na mama yake mzazi a,mbaye kwa sasa ni marehemu akimuelekeza kurithi mikoba yake.
Bi.Sanga alisema kuwa mama yake kijana huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alikuwa ni mtu mwenye maruhani ambapo kwa kutumia maruhani hayo alikuwa akitoa tiba kwa wakazi mbalimbali mjini Mbeya.Alisema kijana huyo ambaye wamezaliwa mapacha na dada yake aliyemtambulisha kwa jina la Hadija Welino kwamba yeye anasoma kidato cha Nne katika shule ya sekondari Itende.
Hata hivyo Bi.Sanga alisema kuwa kijana huyo aliitwa katika ofisi ya Ofisa Mtendaji ili kutoa maelezo ya namna ambavyo anaendesha tiba hiyo na kuwa hata hivyo anaendelea kutoa tiba kwa watu kwa kunywa vikombe viwili kwa muda wa siku mbili. Alisema kuwa dawa hiyo aliifuata katika kijiji cha Iyula kilichopo wilayani Mbozi na kuwa mara alipofika alianza kuichemsha na kuwagawia wananchi wanaosumbuliwa na maradhi sugu. Aidha umati wa watu walikuwa wamejipanga katika mistari kusubiri tiba hiyo ambapo
Mwenyekiti wa mtaa wa Mianzini Bi.Elizabethy Mwakabungu aliweka utaratibu wa wananchi kupata tiba ikiwa ni pamoja na kuchangia fedha kidogo kwa ajili ya kununulia kuni za kuchemshia dawa hiyo.Akizungumza na umati wa watu waliokuja kujipatia tiba hiyo Mwenyekiti huyo wa mtaa alisema kuwa kila ambaye atapata kikombe kimoja cha dawa anatakiwa kupata kikombe cha pili siku inayofuata.
‘’Mganga katuagiza kuwa kila anayekunywa kikombe kimoja anatakiwa kunywa kikombe cha pili siku inayofuata…yeyote atakayekunywa hatakiwi kunywa pombe kwa muda wa siku saba,’’alisema Bi. Mwakabungu
Wakipata kikombe
maelekezo ya kufika eneo hilo
Pamoja tunaendeleza kupashana Habari
HABARI NA PICHA: Mbeya Yetu
26.3.11
Evarist Chahali
Summer Time
No comments
Kwa kumbukumbu tu,kwa hapa Uingereza msimu wa majira ya joto (summer) unaanza hapo saa 7 usiku.Kama ilivyo ada,inalazimu kusogeza muda kwa saa moja.
Tovuti hii inawatakia nyote Summer Time njema
26.3.11
Evarist Chahali
Maandamano
No comments
Picha zote mbili zinahusu MAANDAMANO.Picha ya kwanza juu inahusu maandamano yanayotarajiwa kufanyika leo jijini London,na kushirikisha vyama mbalimbali vya wafanyakazi,lengo likiwa kuibana serikali ya hapa Uingereza kuhusu hatua zake za kubana matumizi (spending cuts).
Picha ya pili inaonyesha kikundi kidogo cha waandamanaji eneo la Kinondoni Mtambani wakiandamana kulaani mashambulizi ya Wamarekani,Waingereza,Wafaransa,na washirika wao dhidi ya majeshi ya serikali ya kidikteta ya Kanali Muamar Gaddafi.
Charity begins at home.Hivi wenzetu hawa walioandamana kumtetea Gaddafi hawaelewi kuwa hata huko Libya kuna maandamano ya kumng'oa dikteta huyo?Lakini, la muhimu zaidi,kama ni mdadi wa maandamano,kwanini basi waungwana hawa wasingeandamana kudai maisha bora....
Aliyesema "akili ni nywele kila mtu ana zake" wala hakukosea
24 Mar 2011
24.3.11
Evarist Chahali
RAIA MWEMA
No comments
Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema inazungumzia namna watawala wetu wanavyoendekeza matumizi ya anasa huku wananchi wa kawaida wakizidi kuwa masikini.Bonyeza HAPA kusoma makala hiyo pamoja na habari na makala nyingine maridhawa katika jarida hili maridhawa la RAIA MWEMA.
20 Mar 2011
20.3.11
Evarist Chahali
Gaddafi, MAFISADI
2 comments
Pichani ni hekalu linalomilikiwa na Dikteta Muamar Gaddafi.Jumba hilo la kifahari (thamani yake ni takriban shilingi bilioni 27)lipo jijini London lakini kwa sasa limepata "wamiliki" wapya...watu wasio na makazi maalumu (squatters) wameamua kuchukua sheria mkononi na kuhamia hapo.Nani asiyetaka kuishi kwenye hekalu?Na hasa pale mmiliki wa hekalu hilo maji hana hakika kama kesho atakuwa madarakani!!!
Je mafisadi wanapoona picha kama hii viroho haviwadundi japo kidogo?Good news is,hata wasipokumbwa na kimbembe kama hiki cha Gaddafi,siku moja wataitwa mbele ya haki na Mwenyezi Mungu...na hayo mabilioni wanayotudhulumu,kutunyang'anya,kutuibia,kutupora,nk WATAYAACHA HAPA HAPA DUNIANI.
18 Mar 2011
18.3.11
Evarist Chahali
Babu, UKIMWI
1 comment
Mwaka huu mbona mambo!!!Baada ya stori inayokamata chati kwa sasa-ya "Babu" anayedaiwa kuwa na uwezo wa kutibu maradhi kadhaa ikiwa pamoja na ukimwi (na Watanzania wamesahau kabisa habari za akina Adawi na Dowans yake)-sasa ameibuka "Babu" mwingine huko Rombo.
Hebu soma kwanza mkasa huu
Rombo kama LoliondoThursday, 17 March 2011 20:25
Daniel Mjema, Moshi
Ni siku za mwisho? Hili ndilo swali lililoanza kuumiza vichwa vya watu baada ya kijana mmoja kuibuka wilayani Rombo, mkoani Kilimanjaro na kudai ameoteshwa dawa ya ajabu na Bikira Maria inayotibu magonjwa sugu ukiwamo Ukimwi.Kama ilivyo kwa mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambikile Mwasapile wa Loliondo ambaye amejizolea umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi, kijana huyo naye amekuwa akitoa tiba kwa sh500.
Kwa imani ya waumini wa Kanisa Katoliki Duniani, Bikira Maria ni mama wa Yesu ambaye anaaminiwa na waumini wa Kanisa hilo na hata katika sala jina lake ndilo linalotumika zaidi huku wakiamini kuwa Yesu ni mtoto wa Mungu.Habari za uhakika kutoka eneo la Customs katika mji mdogo wa Tarakea, mpakani mwa Kenya na Tanzania, zilimtaja kijana huyo ambaye sasa anajiita Nabii, kuwa ni Hilary James Kitwai (28), kutoka wilayani Babati.
Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu kutoka Tarakea, Kitwai alisisitiza kuwa dawa hiyo ameoteshwa na Bikira Maria na Yesu na kwamba inatibu Ukimwi, Saratani, Kisukari, Shinikizo la Damu, Figo, Pumu na maradhi ya maumivu.
"Walinitokea kwenye ndoto wakanionyesha huo mti na waliniambia kwa sasa tuko wawili tu Tanzania, lakini huyo mwenzangu simfahamu. Mimi natoza Sh500 lakini katika hiyo pesa yangu na familia yangu ni Sh300 tu,"alidai.
Kitwai ambaye amekuwa gumzo katika mji wa Tarakea, alisema anakabiliwa na changamoto kubwa katika kuwahudumia wenye mahitaji kwa kuwa hana msaada na kuomba serikali imsaidie kumpatia wahudumu.
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari kutoka wilayani Rombo, tayari vyombo vya ulinzi na usalama vimemzuia kwa muda, kijana huyo kutoa tiba inayofanana na ya mchungaji Mwasapile na kuitisha sampuli za mizizi anayoitumia.
Kijana huyo ambaye ni fundi baiskeli kwa miaka mingi katika eneo hilo, aliibuka Jumatatu wiki hii na kuanza kutoa tiba kwa kutumia kikombe na tayari watu takribani 100 kutoka Kenya na Tanzania wamekunywa dawa yake.
"Anadai kuwa ameoteshwa na Bikira Maria na alielekezwa huo mti ambao una utomvu na kuanzia juzi (Jumatatu),watu kama 100 hivi walishakunywa dawa hiyo ambayo wenyeji wanadai mti wake ni sumu,"kilidai chanzo chetu.Ofisa Mtendaji wa Kata ya Tarakea, Motamburu, Kimario, alilithibitishia Mwananchi kuwapo kwa kijana huyo.
Kimario alisema yeye binafsi, Ofisa Afya na Ofisa Usalama wa Taifa, walifika nyumbani kwa kijana huyo juzi na kumfanyia mahojiano."Tulimhoji akasema alitokewa na Bikira Maria na Yesu ambao walimwonyesha mti huo ambao upo katika Mto Tarakea na walimwambia yupo mmoja tayari anayetibu maradhi sugu na kwamba yeye atakuwa wa pili,"alisema mtendaji.
Kwa mujibu wa mtendaji huyo, kijana huyo aliwaeleza kuwa baada ya Babu wa Loliondo na Yeye, bado atatokea mtu wa tatu ambaye naye ataoteshwa dawa za kutibu maradhi hayo na baada ya hapo Yesu mwenyewe atakuja duniani.
"Tulimuuliza kama ameshatoa dawa hiyo kwa watu mbalimbali akasema alianza kutoa Jumapili na watu kama 20 hivi walikunywa na alitupa vipande vya miti viwili vya dawa hiyo na tumevikabidhi kwa uongozi wa juu,"alisema Kimario.
Kwa mujibu wa Kimario aliyekuwa akimkariri kijana huyo, alisema 'nabii' huyo ameamua kutoendelea kutoa tiba hiyo hadi hapo serikali itakaporidhia na kwamba kwa sasa anamuomba Mungu ampe maono zaidi juu ya dawa hiyo.
Wananchi walioongea na Mwananchi baada ya kuzagaa kwa taarifa hizo, wameitahadharisha serikali kuwa makini na watu wanaojiita ni manabii vinginevyo wananchi wanaweza kukumbwa na maafa ya kunywa sumu bila kujua.
Wananchi hao wameitaka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kuwajibika kikamilifu kwa kuzuia matumizi ya dawa ambazo hazijathibitishwa kutokuwa na madhara.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, Anthony Tesha ambaye pamoja na kukiri kusikia habari hizo lakini alisema anaviachia vyombo husika kufuatilia jambo hilo.
CHANZO: Mwananchi
18.3.11
Evarist Chahali
Ndoto za JK
2 comments
Ama kweli ndoto zimepata muotaji.Yaani ukisikia baadhi ya ndoto za mtu aliyekabidhiwa kuongoza Watanzania zaidi ya milioni 40-namaanisha Rais Jakaya Kikwete-unaweza kuugua ghafla.Ukiweka kando rekodi yake ya kusafiri mno nje ya nchi,Kikwete anaweza kuweka rekodi nyingine ya kuwa kiongozi wa nchi aliyewahi kutoa ahadi nyingi zaidi kuliko yeyote yule duniani.Na rekodi hiyo inaweza kupata ushindani kutoka kwa nyingine ya "Mwanasiasa aliyetoa ahadi hewa nyingi zaidi kuliko yeyote yule.
Sasa amekuja na ahadi mpya ya kuwaunganisha wanafunzi mpango maalumu wa kutumia mkongo wa mawasiliano, ili kukabiliana na upungufu wa walimu katika shule za sekondari nchini.Katika kufanikisha "mpango huo kabambe", shule zote za sekondari zitaunganishwa katika mtandao huo ambao utawawezesha mwalimu mmoja kufundisha shule hizo wakati mmoja.
Wazo zuri lakini ni la kidanganyifu.Kama serikali ya Kikwete inasuasua kumudu ujenzi wa vyoo katika shule,achilia mbali madawati,madarasa na nyumba za walimu,hizo ndoto za kuwezesha teknolojia ya kisasa anayoizungumzia inatoka wapi?
Na kwa mgao huu wa umeme unaosababishwa na ufisadi ulioshamiri kweye sekta ya nishati,hiyo teknolojia ya mkongo itatumia nishati ya kuni,maji au majini ya Sheikh Yahya (kama bado hayaja-expire)?
Hivi nani amemwambia Kikwete kuwa akikaa kimya-badala ya kutoa ahadi zinazotokana na ndoto za mchana-urais wake utakuwa mashakani?
Hebu jisomee mwenyewe uzushi huu
JK: Tutatumia mkongo kufundishia wanafunziThursday, 17 March 2011 20:27
Fredy AzzahRAIS Jakaya Kikwete, amesema serikali imebuni mpango maalumu wa kutumia mkongo wa mawasiliano, ili kukabiliana na upungufu wa walimu katika shule za sekondari nchini.Katika kufanikisha jambo hilo, shule zote za sekondari zitaunganishwa katika mtandao huo ambao utawawezesha mwalimu mmoja kufundisha shule hizo wakati mmoja.Alisema hayo jana jijini Dar es Salaam alipotembelea Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kukagua utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Januari mwaka 2006 na kutoa maagizo ya kuboresha elimu kwa miaka mitano ijayo.
"Pamoja na kuwa tuna tatizo la upungufu wa walimu kwa jumla, hali ni mbaya sana kwa walimu wa sayansi, mpaka sasa kuna upungufu wa walimu 34,000 na sisi kwa mwaka uwezo wetu ni kuzalisha walimu 10,000," alisema Rais Kikwete.
Alisema ili kukabiliana na tatizo hilo, serikali itaziunganisha shule za serikali katika mkonga wa taifa wakati ikiendelea pia kuzalisha walimu kadri itakavyoweza."Kutokana na idadi ya walimu wanaosoma, tatizo la walimu litaweza kwisha baada ya miaka mitatu, lakini sasa pamoja na walimu 10,000 kumaliza masomo yao kwa mwaka, unaweza kukuta bado tuna upungufu wa walimu 40,0000 kwa mwaka," alisema
"Tukiziunganisha shule zetu kwenye mkongo wa taifa ambao mpaka kufikia Juni mwaka huu utakuwa umekamilika, mwalimu mmoja akiwa hapa, anaweza kufundisha wanafunzi wa kemia nchi nzima kwa wakati mmoja." alisisitiza.
Alisema mpango huo ukifanikiwa mwalimu atakaye kuwa yupo kwenye darasa la shule husika, kazi yake itakuwa ni kusimamia wanafunzi kufanya mazoezi na yatakayotolewa na mwalimu aliyekuwa akifundisha kwa njia ya mtandano na kusahihisha kazi zao.
Alieleza kuwa, tayari serikali imeshafanya mazungumzo na kampuni moja ya Kimarekani ambayo itasaidia katika teknolojia hiyo."Wameshanionyesha jinsi tutakavyofanya kwenye maeneo ambayo yana umeme na hata yale yasiyokuwa na umeme," alisema Rais Rais pia aliitaka wizara kuweka bayana mipango yake kuhusu namna ya kuinua ubora wa elimu.
17 Mar 2011
"Tiba ya Babu" imeibua kila aina ya vimbwanga.Nikianza kuviorodhesha vimbwanga hivyo basi tutakesha kwani kila kukicha kuna mapya.Mara tusikie wagonjwa waliotoroka mahospitalini "wamefumaniana" na madaktari waliotorokwa na wagonjwa hao,huku wote-wagonjwa na madaktari wakiwa kwenye foleni kusbiri "tiba ya Babu"
Lakini siui kama msomaji mpendwa umebaini "mpasuko wa kimtizamo" kati ya maswahiba wawili maarufu,Rostam Aziz na Edward Lowassa.Wakati Rostam alinukuliwa akiiponda "tiba" hiyo,swahiba wake-Lowassa-sio tu alitinga kwa "Babu kupata kikombe" bali pia inaelezwa amewalipia wapiga kura wake gharama za usafiri kwenda kupata "tiba" hiyo.
Je hii ni dalili ya mwanzo ya mpasuko kati ya wanasiasa hawa ambao majina yao ni kama synonymous na ufisadi?Au wanatuzuga tu mind games?You decide
Lakini siui kama msomaji mpendwa umebaini "mpasuko wa kimtizamo" kati ya maswahiba wawili maarufu,Rostam Aziz na Edward Lowassa.Wakati Rostam alinukuliwa akiiponda "tiba" hiyo,swahiba wake-Lowassa-sio tu alitinga kwa "Babu kupata kikombe" bali pia inaelezwa amewalipia wapiga kura wake gharama za usafiri kwenda kupata "tiba" hiyo.
Je hii ni dalili ya mwanzo ya mpasuko kati ya wanasiasa hawa ambao majina yao ni kama synonymous na ufisadi?Au wanatuzuga tu mind games?You decide
Rostam aponda tiba ya Mchungaji Loliondo
Tuesday, 15 March 2011 21:22
Shija Felician, Igunga
WAKATI Watanzania wengi wakimiminika kwenda wilayani Loliondo, mkoani Arusha kupata dawa inayodaiwa kutibu magonjwa sugu, Mbunge wa Igunga (CCM), Rostam Aziz ameibuka na kusema tiba hiyo haina lolote akidai kwamba ndugu zake watano wameitumia lakini hawajapona.
Akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara wa kuwashukuru wapigakura uliofanyika kwenye Viwanja vya CCM wilayani Igunga, Tabora mbunge huyo alisema haiamini dawa hiyo kwa kuwa ana ushahidi kwa ndugu zake hao ambao anadai kwamba wanaendelea kuugua kisukari licha ya kutumia dawa hiyo siku saba zilizopita.
Aliwataka wale watakaokwenda Loliondo ambao wanatumia dawa za hospitalini kuendelea kuzitumia badala ya kuzipuuza na kuzitupa... “Ndugu zangu wananchi wa Igunga, mimi mjomba wangu Hassan mnamfahamu karibu wote hapa mjini ni mgonjwa wa siku nyingi wa kisukari. Ameshakunywa dawa hiyo lakini mpaka sasa ni mgonjwa kama mnavyomuona sasa hiyo dawa inaponyesha nani?”
Hata hivyo, aliwataka wananchi wote wenye imani juu ya dawa hiyo waende huku akiwasisitizia kutopuuza ushauri wa madaktari kwani.
Wakati Rostam akipinga dawa hiyo, wilayani Kahama, mamia ya wafanyabiashara wamefunga shughuli zao na kukimbilia Loliondo kwa Mchungaji Mwasapile kunywa dawa hiyo huku baadhi ya waliorejea baada ya kuinywa wakidai kuwa hali zao sasa ni nzuri.
Wafanyabiashara hao wengi wao wanaondoka kwa siri wakidai wanakwenda Dar es Salaam katika shughuli zao, lakini siri imefichuka baada ya baadhi yao kuoneka katika runinga wakiwa katika foleni wakisubiri kupatiwa huduma hiyo.
Mbali ya kuzungumzia suala hilo la tiba ambalo limegusa hisia za wananchi wengi wa Afrika Mashariki, mbunge huyo aliwapa pole wananchi wa Igunga ambao nyumba zao zimeezuliwa na upepo uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha wiki iliyopita ambazo ziliathiri kaya 19. Aitoa msaada wa Sh500,000 kwa kila kaya iliyokumbwa na maafa hayo.
Lowassa apata kikombe Loliondo
Tuesday, 15 March 2011 23:47
Waandishi Wetu
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa juzi alipata tiba ya magonjwa sugu inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapile katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale, Loliondo, mkoani Arusha.Lowassa alifika katika eneo hilo mchana akiwa na viongozi kadhaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro na Serikali kisha kupata kikombe kimoja chenye dawa kinachotolewa na mchungaji huyo kwa ajili ya tiba.
Tofauti na viongozi wengine, Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli (CCM), Jimbo linalopakana na Kijiji cha Samunge, alikwenda huko akiwa na viongozi mbalimbali wakiwamo viongozi wa dini na baadhi ya wapigakura wake.
Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana, Lowassa alithibitisha kwenda Loliondo na kuwataja viongozi wa dini alioambatana nao katika msafara wake kuwa ni Askofu Msaidizi wa KKKT, Dayosisi ya Kaskazini, Dk Frederick Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Dayosisi ya Kaskazini Kati (Arusha), Mchungaji John Nangole.
Katika ramani ya utendaji kazi ya KKKT, Jimbo la Masai Kaskazini ndipo kilipo Kijiji cha Samunge ambako ni makazi ya Mchungaji Mwasapile.“Ni kweli, nimekwenda pale na wapigakura wangu pamoja na viongozi wa dini, Msaidizi wa Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini, Dk Shoo na Mkuu wa Jimbo la Masai Kaskazini, Mchungaji Nangole,” alisema Lowassa na kuuliza: “Kwani hiyo nayo ni habari jamani?”
Baada ya Lowassa kufika katika kijiji hicho akiwa na ujumbe wake, aliongoza moja kwa moja hadi kwa Mchungaji Mwasapile na kuzungumza naye kisha akapata kikombe cha tiba na kuondoka.
Kabla ya Lowassa kwenda kupata tiba, amekuwa akitoa msaada wa nauli kwa wagonjwa mbalimbali wa jimbo lake kwenda kwa mchungaji huyo ambaye dawa yake inadaiwa kutibu magonjwa ya saratani, kisukari, pumu, shinikizo la damu na Ukimwi.Lowassa ni miongoni mwa wanasiasa maarufu nchini ambao wameshafika kwa mchungaji huyo kupata tiba hiyo wakiwamo mawaziri, naibu mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wilaya.
16 Mar 2011
16.3.11
Evarist Chahali
NATE DOGG
1 comment
American singer Nate Dogg, real name Nathaniel Dwayne Hale, has died at the age of 41.The cause of death has not yet been confirmed but in December 2007 the singer was left paralysed on one side of his body after a massive stroke and was struck by a second one in September 2008.
Subscribe to:
Comments (Atom)












