26 Apr 2011


Wait a minute!Hivi jina "Mzee wa Kijiko" si lilikuwa la mwanamuziki wa dansi Ally Choki

Well,mazingaombwe ya kuibuka kwa watu wanaodai kupewa nguvu na Mungu kuponyesha magonjwa sugu yanaendelea baada ya mkazi mmoaj kuibuka na kudai anatibu kwa kijiko.Hebu soma mwenyewe habari kamili hapa chini

Fatuma Maumba, Mtwara

BAADA ya Mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapila kuanza kutoa dawa ya kikombe katika Kijiji cha Samunge, kilichopo Loliondo Mkoa wa Arusha, mkoani Mtwara ameibuka mtu mmoja anayetibu kwa kutoa dawa ya kijiko.

Kutokana na kuwapo kwa mtu huyo, Ahmad Linangwa maarufu kama Mzee wa Kijiko, wananchi wengi wamekuwa wakifurika katika Kijiji cha Moma Wilaya ya Mtwara Vijijini, Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kupata dawa ya kijiko.

Akizungumza na MTANZANIA nyumbani kwake kijijini hapo juzi, Linangwa alisema kabla ya kuanza kutoa dawa hiyo inayotibu magonjwa sugu ukiwamo ukimwi, awali aliota na kupewa maelekezo na Mwenyezi Mungu namna ya kuchanganya miti ya aina tatu kwa ajili ya kupata dawa hiyo.

“Pamoja na kupewa maelekezo hayo Aprili 18 mwaka huu, pia niliambiwa baada ya kuchanganya miti hiyo, nivilige kitu kama goroli kisha nichanganye na maji pori ambayo nitayagema kwenye mti unaoitwa Mtamba.

“Nikishafanya hivyo, maji hayo niwape wagonjwa nao watapona magonjwa yanayowasumbua,” alisema Linangwa.

Kwa mujibu wa Lingangwa, kabla ya kuanza kuwapa wagonjwa dawa hiyo, alianza kuinywa yeye wakati alipokuwa porini akiiandaa.

“Nilianza kuinywa nikiwa kule porini, nilipomaliza kuinywa, nilikimbilia nyumbani haraka ili kama ni sumu iniue wakati nimeshafika nyumbani lakini sikufa.

“Kwa hiyo watu waje watumie dawa hii, haina masharti yoyote kwani kama mtu anatumia dawa za hospitali anaweza kuendelea na dawa hizo bila wasiwasi, kama unakunywa pombe, au unavuta sigara, dawa yangu haina matatizo,” alisema Mzee wa Kijiko.

Kutokana na kuwapo kwa matibabu hayo, nauli kwa pikipiki na bajaji zimepanda kutoka Mtwara Mjini hadi kijijini Moma.

CHANZO: New Habari

23 Apr 2011



Ningetamani kuitasiri ripoti hii kutoka kimombo kwenda lugha ya taifa Kiswahili lakini ni ndefu (kurasa zaidi ya 20).Tovuti hii ipo tayari kutoa msaada wa bure kwa yeyote atakayeshindwa kuielewa katika "Lgha hii ya Malkia Elizabeti".

Loliondo Technical Report

CHANZO: Jamii Forums


Nimekutana nayo huko Jamii Forums:

Kichuguu;

Mimi kama mmoja wa wanachama waandamizi wa Jamii Forums ambapo nimekuwa mwanchama kwa karibu miaka mitano sasa tangu ikiwa Jambo Forums kabla ya kubadili jina na kuwa Jamiiforums nimekerwa sana na matamshi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM kuwa forums hii ni ya vijana wa CHADEMA. Naona kuwa amenivunjia sana heshima yangu mbele ya wenzangu kwa kunipa image ya kuwa mimi ni mpiga propaganda wa CHADEMA.

Baada ya kutafakari kwa kina matamshi ya Pius Msekwa na jinsi yalivyoathiri image yangu kama mwanachama wa JamiiForums, nimeamua kumfungulia mashtaka ya defamation kwenye mahakama ya Douglas County hapa Omaha Nebraska nchini Marekani. Nimejadiliana na mwanasheria wangu ambaye amenipatia kifungu cha sheria kinachoniruhusu kumshitaki raia wa nchi ya nje kwenye mahakama hii, iwapo marekani ina uhusiano wa kibalozi na nchi ya mshitakiwa. Sasa hivi tuko katika hatua za mwisho mwisho za kukusanya ushahidi imara.

Nimeshapata nakala za magazeti ya kiswahili na kiingereza ila nimekuwa natafuta video clip yenye kumwonyesha Msekwa akiwa anasema maneno hayo. Vile vile bado tunashauriana kiwango cha malipo ya Punitive Damages na Compensatory Damages; mwanasheria anashauri kuwa viwango hivyo vipimiwe zaidi kwa kuangalia jinsi gani Msekwa binafsi na chama chake walivyofaidika au watakavyofaidika kutokana na matamshi yake hayo, na kwa kiasi kidogo jinsi gani yalivyoathiri image yangu binafsi kama mwanachama mwanadamizi ambaye hujitambulisha kwa wenzagu wote kuwa mimi ni Premium Member wa JamiiForums.

Tukikamailisha taratibu zote, nitawaarifuni au mtasikia kwenye vyombo vya habari Msekwa akiwa subpoenaed kwenye kesi hii ambayo pamoja na mambo mengine ninataka kuwadhibiti wanasiasa wasiwe wanaropoka mambo bila kuwa na uhakika nayo.

Ngoma inogile


TUHUMA za ufisadi ambazo Dk. Willibrod Slaa amemshushia Rais Jakaya Kikwete, zimezima mbwembwe na majigambo ya “mapambano dhidi ya ufisadi” ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

Mwishoni mwa wiki, ikiwa ni wiki moja tangu CCM itangaze “kujivua gamba” la ufisadi, Dk. Slaa amemtuhumu Rais Kikwete kushindwa kusimamia rasilimali za taifa kwa kuruhusu au kunyamazia wizi wa Sh. 249 bilioni.

Fedha hizi ni zile za mfuko wa madeni ya taifa.

Aidha, Dk. Slaa amesema Rais Kikwete ameshindwa pia kusimamia matumizi ya Sh. 70 bilioni zinazodaiwa kurejeshwa na wezi waliokiri kuiba kutoka akaunti ya EPA “ambazo hadi sasa hazijulikani matumizi yake.”

“Udhaifu huu wa Kikwete na serikali yake umechangia ufisadi wa kiwango cha juu katika matumizi ya fedha za umma,” ameeleza Dk. Slaa.

Kwa mujibu wa nyaraka za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambazo Dk. Slaa amenukuu, Sh. 70 bilioni zilidaiwa kuingizwa katika Benki ya Rasilimali (TIB) na baadaye zikadaiwa kuwa zilitolewa ili kuanzisha benki ya wakulima ambayo haijaanzishwa.

Dk. Slaa alidondosha makombora hayo kwenye mkutano mkubwa wa hadhara katika uwanja wa Chipukizi mkoani Tabora, Jumamosi alasiri.

Kwenye mkutano huo, Dk. Slaa aliwataja pia rais mstaafu Benjamin Mkapa, makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM John Malecela, katibu mkuu mstaafu wa CCM, Philip Mangula, waziri wa ujenzi, John Magufuli na ofisa wa ngazi ya juu wa mamlaka ya mapato ya taifa (TRA), Placidius Luoga kuwa wameshiriki ufisadi.

“Hawa, kwa njia mbalimbali, ama wameruhusu au wameidhinisha au wamenyamazia ufujaji wa raslimali za taifa,” Dk. Slaa aliuambia mkutano wa hadhara uliohudhuria na umati wa wananchi.

Hii ni mara ya pili kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuanika majina ya wale kinaowaita “vigogo wala nchi” kwa kuwahusisha na ufujaji wa fedha na raslimali za taifa.

Akiwa na wanasheria wa chama hicho, Mabere Marando na Profesa Abdallah Safari, Dk. Slaa alisoma jina moja baada ya jingine na kutoa maelezo juu ya ushiriki wa kila mmoja katika alichoita kufisidi taifa.

Tayari kishindo cha CHADEMA mjini Tabora kimeleta kizaazaa ndani ya CCM na kufanya nderemo za juu ya kujivua gamba kuonekana kama tamthiliya.

Haya yanatokea wakati katibu mkuu mpya Wilson Mukama anasema atapambana na “mafisadi” na kwamba atawaandikia barua kuwataka wajiondoe kwenye chama.

Naye katibu mwenezi mpya, Nape Nnauye, akinusa kishindo cha Tabora, amejiingiza katika malumbano na CHADEMA. Jumapili mjini Zanzibar, alidai kuwa CHADEMA kinatumiwa na “mafisadi” ili kumchafua Rais Kikwete na mtoto wake Ridhiwani.

Lakini kwenye mkutano wa Tabora, hakuna kiongozi yeyote wa CHADEMA aliyetaja jina la Ridhiwan, jambo ambalo limetafsiriwa kuwa Nnauye alitarajia kuona jina la mtoto huyo wa rais katika orodha ya watuhumiwa.

Wakionekana wamejipanga na kufanya kile walichokiamini, Dk. Slaa na timu yake walianza kueleza kile walichoita, “wizi mkubwa usioweza kuvumilika” uliofanywa na viongozi wa CCM na watendaji serikalini.

Alikuwa Profesa Safari aliyeanza kumtuhumu Mkapa kuwa ameingiza nchi katika matatizo makubwa kwa kuruhusu uuzaji holela wa nyumba za serikali. Alisema nyumba hizo ni sharti zirejeshwe serikalini na bila masharti.

“Tunataka nyumba hizo zirejeshwe mara moja. Iwapo hilo halikufanyika, tutatumia nguvu ya umma kuzirejesha,” alieleza Prof. Safari huku akishangiliwa.

Naye Marando alisema hakuna kiongozi yeyote ndani ya CCM, akiwamo Rais Kikwete, anayeweza kujinasua katika tuhuma za wizi wa mabilioni ya shilingi za EPA zilizokwapuliwa ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Akiongea huku akiwa na nyaraka kadhaa mkononi alizodai zilitumika kukwapulia mamilioni hayo, Marando alisema katika wizi huo, Mkapa ndiye kinara mkuu.

Aliwataja wengine waliohusika na wizi huo kuwa ni Rais Kikwete, Rostam Aziz na Edward Lowassa. Marando aliituhumu serikali kwa kushindwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wakuu wa wizi wa EPA, badala yake imeshitaki “vidagaa.”

“Mimi nimepata nyaraka zinazoonyesha kuwa John Kato, ndiye William Kemhondo na Francis William ni Barack Goda. Wote hawa wawili ni wafanyakazi wa kampuni ya Caspian Limited, inayomilikiwa na Rostam Aziz.

Akasema yuko tayari kuendesha kesi dhidi ya Kagoda bure na kuahidi kuwa haitafika mwaka 2015 kabla hajawatia gerezani watuhumiwa wote.

Ndipo ikafuata zamu ya Dk. Slaa. Akaanza kueleza wizi ulivyotokea na akasoma tuhuma ya kila mmoja. Akasema orodha yake ya sasa, itaongezeka kwa kadri nyaraka na ushahidi unavyokusanywa na kupitiwa na timu ya wanasheria wa chama chake.

Akiongea kwa staili ileile ya Mwembeyanga, ambako alitangaza orodha ya kwanza ya watuhumiwa 11 wa ufisadi, miaka mitatu iliyopita, Dk. Slaa alisema, “Kuna watu wananituhumu kwamba mimi namsakama Kikwete kwa kuwa ni muislamu. Mimi siangalii dini ya mtu, kabila lake wala sura yake.”

Akivuta pumzi, Dk. Slaa alisema, “Ninachoangalia ni nchi yangu. Ndiyo maana huko nyuma niliwahi kumkemea Sumaye (Fredrick Sumaye) ambaye ni ndugu yangu, kabila langu na dini moja. Lakini pale serikali ilipolegalega katika kusimamia rasilimali za taifa, nilimkemea bila woga.” Ndipo alianza:

Jakaya Kikwete: Huyu ameshindwa kusimamia rasilimali za taifa kwa kuruhusu au kunyamazia wizi wa Sh. 249 bilioni pamoja na Sh. 70 bilioni zilizorejeshwa na wanaodaiwa kuwa wezi wa EPA. Fedha hizo, kwa mujibu wa nyaraka za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), zilidaiwa kuingizwa katika Benki ya Rasilimali (TIB) na baadaye zikadaiwa kuwa zilitolewa ili kuanzisha benki ya wakulima.

Nyaraka zinaonyesha kuwa pamoja na fedha hizo kutolewa TIB, hadi sasa kinachoitwa benki ya wakulima hakijaanzishwa. Alitoa siku 90 kwa Kikwete kueleza mahali ziliko fedha hizo, vingevyo yeye na chama chake wataamini kuwa fedha hizo zilitumiwa na CCM katika uchaguzi mkuu uliopita.

“Huyu Kikwete amefadhiliwa na wezi, ndiyo maana ameshindwa kuchukua hatua kwa wezi hao,” alieleza.

Dk. Slaa amesema anatoa siku 90 kwa serikali kueleza zilipo fedha za DECI, Sh. 70 bilioni za EPA, Sh. 249 bilioni kutoka deni la taifa na mabilioni mengine ambayo yamegunduliwa na mkaguzi wa hesabu za serikali.

Katika tuhuma za Mwembeyanga, CHADEMA walimtuhumu Kikwete, kwa wadhifa wake wakati huo, kusaini “mikataba mibovu” ya madini na makampuni ya kimataifa, iliyosababisha upotevu wa utajiri mkubwa na kuifanya serikali ishindwe kuhudumia vizuri wananchi wake.

Inadaiwa Kikwete alisaini mkataba na kampuni ya SAMAX Limited iliyopewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora, mradi ulioleta mateso kwa maelfu ya wachimbaji wadogo baada ya kuondolewa kwenye makazi yao kwa nguvu.

SAMAX iliuza mradi wake kwa Ashanti Goldfields ya Ghana kwa kiasi cha dola za Marekani 253 milioni. Nao Ashanti waliuza mgodi huo kwa kampuni ya Resolute Limited ambao ndio wanamiliki mgodi wa Golden Pride ulioko Lusu, Nzega uliofunguliwa Novemba 1998.

Kikwete anadaiwa pia kusaini mkataba na kampuni ya Kahama Mining Corporation Ltd (KMCL) ambayo ni kampuni tanzu ya Sutton Resources ya Canada.

Mara zote wananchi waliswagwa nje ya makazi yao ya miaka mingi ili kupisha wawekezaji na hawakulipwa fidia kwa mali zao. Takriban wananchi 400,000 waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo la Bulyanhulu, Kahama waliachwa bila makazi.

Baadaye Sutton iliuza KMCL na Bulyanhulu kwa kampuni ya dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada kwa dola 280 milioni. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.

Benjamin Mkapa: Anatuhumiwa kushiriki au kubariki, au kunyamazia ukwapuaji wa fedha za EPA na kubariki uuzaji wa nyumba za serikali.

Kwa mujibu wa upinzani, ufisadi mkubwa ulitendeka chini ya utawala wa Mkapa.

Aidha, Mkapa anatuhumiwa kushiriki, moja kwa moja au kwa kutumia ndugu na/au washirika wa karibu wa familia yake, kumilikisha asilimia 85 ya hisa za kampuni ya Kiwira Coal Mines Ltd., inayochimba mkaa wa mawe huko Kiwira, Mkoani Mbeya kwa kampuni ya Tanpower Resources Limited inayomilikiwa na baadhi ya watu wa familia yake.

John Malecela: Ametuhumiwa kusaidia baadhi ya watuhumiwa waliokwapua mabilioni ya shilingi katika akaunti ya EPA. Upinzani ulionyesha hata baadhi ya vimemo vya Malecela vinavyodaiwa kutumika katika kufanikisha wizi.

Dk. Slaa amesema nyaraka ambazo Marando amemkabidhi zinaonyesha kuwa Malecela alisaidia wizi kufanyika.

Philiph Mangula: Ametuhumiwa kusaidia wizi wa EPA kwa maslahi ya chama chake na wao binafsi. Dk. Slaa alisema vimemo alivyoandika Mangula vilikuwa vya kumwelekeza gavana wa benki kuu wakati huo, Daudi Balali.

John Magufuli: Ametuhumiwa kutumia madaraka ya umma kwa maslahi binafsi. Magufuli ametajwa kuwa ndiye aliyepeleka katika baraza la mawaziri waraka uliotaka serikali iuze nyumba za umma na kutumia ruhusa hiyo kujimilikisha moja ya nyumba hizo.

Mbali na yeye kujiuzia nyumba hizo, Magufuli akagawa baadhi ya nyumba za serikali kwa ndugu na jamaa zake; hata mtu mmoja “chini ya mwaka miaka 18.”

Placidius Luoga: Anatajwa kwa kuingizia serikali hasara ya Sh. 800 bilioni kwa hatua yake ya kuzuia magari ya kampuni ya Tango Transport ya mjini Dar es Salaam, kwa miaka 10 kwa kisingizio cha kutolipa kodi.

Dk. Slaa amesema hatua hiyo ilisababisha mhusika kwenda mahakamani na sasa serikali imeamriwa kumlipa mlalamikaji kiasi hicho cha fedha. Dk. Slaa ameeleza kuwa serikali imeanza kulipa na tayari imetoa Sh. 500 milioni.

Pamoja na kuingiza hasara kiasi hicho kwa serikali, Luoga bado ni mwajiriwa TRA.

Katika orodha ya Mwembeyanga iliyotaja watuhumiwa 11, Edward Lowassa alituhumiwa kuhusika na kashfa ya kampuni ya City Water iliyopewa uendeshaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) mwaka 2002.

Mwanasheria Tundu Lissu aliyefafanua dai hilo alisema, anajua kilichomo katika mkataba huo ndiyo maana anamtuhumu Lowassa kuwa mhusika katika kadhia hiyo.

Lissu ni mmoja wa mawakili wa serikali katika shauri la City Water kwenye Mahakama ya Kimataifa nchini Uholanzi ambayo inashughulikia usuluhishi wa mgogoro unaotokana na kukatishwa kwa mkataba wa City Water.

Kabla ya kukatishwa mkataba, Citywater walikwishasababisha hasara ya dola 12.5 milioni, hivyo kuthibitisha onyo lililotolewa na Benki ya Dunia mapema juu ya uwezo duni wa kampuni hizo.

Lowassa anatajwa pia kwa kuhusika kwake na kashfa ya kampuni ya Richmond Development Corporation (RDC) iliyopewa zabuni ya kuzalisha megawati 100 za umeme wa dharura mwaka 2006.

Miongoni mwa watuhumiwa ufisadi katika orodha ya mwaka 2007, ni pamoja na Nazir Karamagi, Daudi Balali, Nimrod Mkono, Rostam Aziz, Patrick Rutabanzibwa, Gray Mgonja, Basil Mramba na Andrew Chenge.

Karamagi anatuhumiwa kukaidi maoni ya Kamati ya Ushauri ya Madini ambayo ilimtaka asisaini mkataba wa Buzwagi hadi hapo serikali itakaporekebisha sheria na sera ili ipate mapato zaidi.

Gavana Balali alituhumiwa mambo mengi ikiwa ni pamoja na kufumbia macho ufujaji wa mali za umma unaofikia Sh. 522, 459,255,000 kupitia mradi wa ujenzi wa majengo pacha ya BoT jijini Dar es Salaam na Gulioni huko Zanzibar; na hongo ya dola 5 milioni kutoka kampuni ya Skanska Jensen ya Sweden ambayo ilipigwa marufuku kushiriki zabuni ya ujenzi wa majengo ya BoT.

Balali alituhumiwa pia kuidhinisha malipo ya dola za Marekani 118,396,460.36 kwa kampuni muflisi ya Meremeta Ltd., kupitia benki ya nchini Afrika Kusini. Meremeta ilikuwa ikichimba dhahabu Buhemba, wilayani Musoma.

Gavana alituhumiwa pia kudhinisha malipo ya dola za Marekani 13,736,628.73 kwa kampuni ya Tangold Ltd., kwa madai kuwa ni ugharimiaji wa “mali na madeni ya Meremeta Ltd yaliyohamishiwa kwenye kampuni mpya ya Tangold ambayo inamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100.”

Hata hivyo, iligundulika kuwa Tangold Limited ni kampuni ya kigeni iliyosajiliwa kwa mara ya kwanza nchini Jamhuri ya Mauritius na baadaye kuandikishwa nchini Tanzania kama tawi la kampuni ya kigeni.”

Wakurugenzi wa Tangold Limited, kwa mujibu wa taarifa zilizoko BRELA, ni pamoja na Daudi Balali. Gray S. Mgonja, Andrew J. Chenge, Patrick W.R. Rutabanzibwa na Vicent F. Mrisho.

Andrew Chenge alituhumiwa, miongoni mwa mengine mengi, kuishauri vibaya serikali na kuwa mkurugenzi katika kampuni ya kigeni ya Tangold Limited iliyoshiriki na/au kufaidika na malipo haramu ya dola 13,736,628.73.

Basil Mramba alituhumiwa, pamoja na mambo mengine, kushinikiza kampuni ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Washington DC, Marekani, kupewa kazi ya kukagua hesabu za makampuni ya uchimbaji dhahabu nchini.

Rostam Aziz alituhumiwa kushiriki katika ukwapuzi wa mamilioni ya shilingi kutoka BoT uliofanywa na kampuni ya Kagoda Agriuculture Limited.

Nimrod Mkono alitajwa kutokana na barua ya CAG iliyobainisha kuwa Benki Kuu ilikuwa ikilipa kampuni yake ya Mkono & Co. Advocates, malipo makubwa zaidi, kuhusiana na kesi ya Valambhia, ambamo BoT inadaiwa jumla ya Sh. 60 bilioni

CHANZO: Mwanahalisi

22 Apr 2011


Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida mahiri la Raia Mwema inazungumzia suala lililokamata hisia za Watanzania wengi kwa sasa la CCM kujivua magamba.Makala hiyo inachambua chanzo cha magamba hayo na namna inavyomwia vigumu Mwenyekiti wa CCM,Rais Kikwete kufanikisha azma yake ya kukisafisha chama hicho (if at all ana azma hiyo).

Jarida hilo pia limesheni makala nyingine moto moto,sambamba na habari za uhakika ikiwa ni pamoja na zile zinazohusu ufisadi mpya wa "Stimulus Package".Zaidi,BONYEZA HAPA KUSOMA MAKALA HIYO na HAPA kusoma jarida zima.


Nina miaka kadhaa sijawahi kwenda kanisani.Sijisifu wala kujisikia vizuri.Kila mara ninapoongea na Baba huwa nalazimika kumdanganya kuwa siku hizi nakwenda kanisani.Ninatoka familia ya kidini hasa,na huenda leo hii ningekuwa padre kama nisingeamini kuwa sina wito.Hata hivyo,familia yetu imemtoa mmoja wetu kwa Bwana,na sasa yeye ni sista.
Mdogo wangu mpendwa,Sista Maria-Solana Chahali

Leo ni Ijumaa Kuu,siku ambayo Bwana wetu Yesu Kristo alikufa msalabani kwa ajili yetu.Nimesema sijatia mguu kanisani kwa miaka kdhaa lakini najitahidi kadri ninavyoweza kuishi kulingana na matakwa ya Bwana.Sio kwenda kanisani au kuimba mapambio kutakompatia mwanadamu uzima wa milele bali matendo.Japo ni muhimu kujumuika na waumimni wenzetu makanisani,la muhimu zaidi ni kuishi kwa mfano wa Bwana Yesu ambaye licha ya upendo wake usiomithilika alikuwa tayari kufa msalabani kwa dhambi zetu ili atuletee ukombozi.

Wakati tovuti hii inakutakia wewe msomaji mpenda Ijumaa Kuu njema,siku hii inaweza kuadhimishwa ipasavyo kwa kutafakari kuhusu upendo wa Bwana,kujitoa kwake kwa jili yetu na upeno kwa ujumla.Kama humpendi jirani yako unayemwona kila siku utakuwa mnafiki kudai unampenda Bwana mbaye hujawahi kumwona.Yesu ni upendo na amani.


Jarida la kimataifa la TIME la nchini Marekani limechapisha orodha yake ya kila mwka ya watu wenye ushawishi mkubwa zaidi duniani (the Time 100 Most Influential People in the World).

Kinarani katika orodha hiyo ni Wael Ghonim,mwanaharakati aliyahamasisha mageuzi ya kidemokrasia nchini Misri kwa kutumia vyombo vya habari vya jamii (social media) na hatimaye kupelekea kuanguka kwa utawala wa kidikteta wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo,Hosni Mubarak.


BONYEZA PICHA IFUATAYO kusoma orodha kamili



19 Apr 2011


Mara kwa mara nimekuwa ninasumbuliwa na watu wanaodhani jina langu la Evarist lina mahusiano na Mlima Everest.Hata hivyo,kwa upole kabisa,huwa ninawaelimisha kuwa jina hilo ni Kitatoliki na nimelirithi kutoka kwa Mtakatifu Evaristus,aliyekuwa Baba Mtakatifu (Pope) kati ya mwaka 99 hadi 108.

Lakini ukilinganisha jina langu na majina mengine,kwa mfano ya kijiji kimoja huko Wales,hapa Uningereza,basi mie sipaswi hata kunung'unika.Kijiji hicho kinaitwa Llanfairpwllgwyngyllgogerychwyrndrobwllllantysiliogogogoch.Kurahisisha ugumu na urefu wa jina hilo,kijiji hicho pia hujulikana kama Llanfairpwllgwyngyll, au spelled Llanfair Pwllgwyngyll.Kurahisisha zaidi,hujulikana kwa kifupi kama Llanfair PG or Llanfairpwll.

Unaweza kudhani hilo ndio jina refu zaidi duniani.Hapana.Kuna mengine kadhaa,kama ambavyo nimeorodhesha hapa:

Jina kamili:
Taumatawhakatangihangakoauauotamateaturipukakapikimaungahoronukupokaiwhenuakitanatahu (herufi 85)
Kifupisho: Taumatawhakatangihangakoauauotamateapokaiwhenuakitanatahu (herufi 57)
Mahali: North Island, New Zealand
Lugha: Māori
Sehemu hii inashilikia rekodi katika Guinness World Records kama jina la sehemu lililo refu zaidi kuliko yote.

Jina kamili: Llanfairpwllgwyngyllgogerychwyrndrobwllllantysiliogogogoch (herufi 58)
Kifupi: Llanfairpwllgwyngyll (herufi 20)
Mahali: Anglesey, Wales, Uingereza
Lugha: Ki-Welshi

Jina kamili: Chargoggagoggmanchauggagoggchaubunagungamaugg (herufi 45)
Kifupi: Ziwa Chaubunagungamaug (herufi 17)
Mahali: Ziwa huko Massachusetts,Marekani.
Language: Nipmuc

Jina kamili: Tweebuffelsmeteenskootmorsdoodgeskietfontein (herufi 44)
Mahali: Afrika Kusini
Lugha: Afrikaans

Jina kamili: Äteritsiputeritsipuolilautatsijänkä (herufi 35)
Mahali: Lapland, Finland

Jina kamili: Pekwachnamaykoskwaskwaypinwanik (herufi 31)
Mahali: ziwa huko Manitoba na Nunavut,Kanada
LUGHA: Inuktitut

Jina kamili: Venkatanarasimharajuvaripeta (herufi 28)
Mahali: kijiji huko Andhra Pradesh, India

Jina kamili: Mamungkukumpurangkuntjunya (herufi 26)
Mahali: Australia Kusini
Lugha: Pitjantjatjara

Jina kamili: Bullaunancheathrairaluinn (herufi 25)
Mahali: County Galway, Ireland

Jina kamili: Gasselterboerveenschemond (herufi 25)
Mahali: Drenthe, Uholanzi
Lugha: Kidachi

Jina kamili: Kuchistiniwamiskahikan (herufi 22)
Mahali: kisiwa huko Quebec, Canada

Jina kamili: Parangaricutirimicuaro (herufi 22)
Mahali: mji huko Michoacán, Mexico
Lugha: P'urhepecha

Jina kamili: Drehideenglashanatooha (herufi 22 letters)
Mahali: daraja huko County Tipperary, Ireland

Jina kamili: Siemieniakowszczyzna (herufi 20)
Mahali:kijiji huko Hajnówka County, Poland
Lugha: Kipolishi

Jina kamili: Newtownmountkennedy (herufi 19)
Mahali: kijiji huko County Wicklow, Ireland
Lugha: Kiingereza

Jina kamili: Thiruvananthapuram (herufi 18)
Mahali: mji huko Kerala, India
Lugha: Malayalam

Jina kamili: Torreblascopedro (herufi 16)
Mahali: Kijiji huko Andalucía,Hispania.

Jina kamili: Hostotipaquillo (herufi 15)
Mahali: mji huko Jalisco, Mexico
Lugha: Nahuatl

VYANZO: Wikipedia

18 Apr 2011


1. Poveglia
Where is it? The Venetian lagoon, Italy
Why can’t I visit?: Because it’s haunted! According to legend it was used to isolate plague victims during Roman times, and then as a giant Black Death grave in the Middle Ages. As if that wasn’t scary enough, it’s also home to spooky abandoned building – complete with bell tower naturally – that was apparently a mental hospital. These days it’s off-limits to visitors unless you bribe a gondolier to take you there.

2. Area 51
Where is it? Nevada, USA
Why can’t I visit?: It’s a top secret military testing base, protected by armed private security teams patrolling in jeeps who are authorised to use deadly force to deal with intruders. Whether or not you believe UFOs have crashed landed there, the ridiculously strict security around the base means you’re never going to find out for sure.

3. Le Cercle Munster
Where is it? Luxembourg
Why can’t I visit?: It’s an exclusive private members club that’s extremely selective about adding new members. Want to join? You must be backed by two sponsors and be approved by a selection committee made up of bigwigs from the finance world. Unless you’re an incredibly rich banker, businessman or equity trader, you’ll never see the sumptuous insides of the club, take part in the ‘Programme culturel’ or eat the delicious food at the in-house restaurant. Damn!

4. Church of Our Lady Mary of Zion
Where is it? Axum, Ethiopia
Why can’t I visit?: Because it’s no ordinary church. According to legend it's home to one of the most important biblical artefacts ever – the Ark of the Covenant (and we thought Indiana Jones left it in a warehouse). Only a specially chosen monk is allowed to guard the ‘Ark’. No-one else is allowed to lay eyes on it or even get close, in case they melt presumably (see Indiana Jones again). Of course, some claim this secrecy means the Ethiopian church is telling porkies…

5. Most of Niihau Island
Where is it? The Hawaiian Islands, USA
Why can’t I visit?: Super-rich family the Robinsons (they’re not Swiss) bought Niihau in 1915 and closed it off to preserve its indigenous culture and wildlife. The 200-or-so natives who live there lead a blissful existence free of electricity, burger joints and, for the most part, tourists. There are very rare helicopter tours to the isle where you can wander along one of the beaches, but getting anywhere near the locals is strictly forbidden; hence its nickname, the, er, ‘Forbidden Island’.

6. Bohemian Grove
Where is it? California, USA
Why can’t I visit?: It’s an extremely secretive men-only club whose members include artists, musicians, businessmen politicians… and the odd president (Nixon was a member). Once a year they all gather for a two-week long festival where (allegedly) rituals such as the ‘Cremation of Care’ - a wicker-man-style faux-pagan rite - and the ‘Grove Play’ - a large-scale musical theatre production - are performed by members. It sounds like fun to us, but somehow I don’t think we’ll get an invite…

7. Lechiguilla Cave
Where is it? New Mexico, USA
Why can’t I visit?: It’s perhaps the most beautiful cave on the planet and frankly, the authorities don’t want you ruining it. Discovered in 1986 by miners, the sprawling underground complex is home to stunning speleothems, gypsum chandeliers and hydromagnesite balloons. We don’t know what any of these are, but they sound impressive. Sadly, unless you’re an extremely experienced caver you’ll never get a permit to see them.

8. Jiangsu National Security Education museum
Where is it? Nanjing, China
Why can’t I visit?: Anyone is allowed in… as long as they are Chinese. There’s a big sign outside the front of this very unusual museum stating that only Chinese citizens are allowed inside. The unusual entry requirements are because the museum documents the history of Chinese espionage, and the state doesn’t want us foreigners finding out their spying secrets.

9. Ilha de Queimada Grande
Where is it? Off the shore of Brazil
Why can’t I visit?: Basically, because it’s full of snakes – hence the nickname: ‘Snake Island’. Local legend states there’s between one and five snakes per square metre on the island. And not just any old snakes, most of ‘em are golden lanceheads – noted for their extremely potent venom. Because of this, understandably, the Brazilian Navy forbids tourists from stepping foot on the island.

10. The peak of Mount Kailash
Where is it? The Himalayas, Tibet
Why can’t I visit?: Because it's home to a Hindu god. Lord Shiva, to be precise, who resides at the summit in a state of perpetual meditation. Sounds like bliss to us, which is appropriate, as Buddhists also believe the peak is home to the Buddha Demchok, who represents supreme bliss. Because of this religious significance the peak was always considered off-limits by most climbers, before this Chinese government issued an official ban in 2001

SOURCE: Yahoo!Travel UK


Mkutano mwingine wa wawekezaji umeanza leo jijini Dar es Salaam.Mkutano huo ni mwendelezo wa mikutano mingine inayopigiwa debe kwa nguvu kuhusiana na umuhimu wa wawekezaji kwa uchumi wetu.

Naamini wengi wet bado tunakumbuka vuguvugu la Mkutano wa Sullivan.Baadaye ukafuatiwa na mkutano mkubwa wa mambo ya uchumi (economic forum).So far,hayo yamebaki kuwa matukio tu ambayo kwa upande mmoja yamewaachia baadhi ya wajanja utajiri wa kutosha baada ya kupewa tenda za chakula,malazi,vifaa,nk huku Watanzania wakiendelea kubaki masikini (na hapo tukiweka kando adha ya usafiri kutokana na barabara kufungwa kwa ajili ya misafara ya waheshimiwa).

Wakati viongozi wetu wakituhadaa na mikutano ya kila mwaka ya wawekezaji,kuna umuhimu wa kufanya uchambuzi wa kina kuhusu suala zima la uwekezaji.Kama uwekezaji mkubwa uliopo hadi sasa hauna manufaa kwa Mtanzania wa kawaida,ni miujiza gani itapelekea wawekezaji wapya walete mabadiliko?

Suala moja la msingi linalopuuzwa na watawala wetu ni ukweli kwamba wawekezaji sio taasisi za hiari za kutuletea maendeleo yetu.Hawa ni wafanyabiashara ambao miaka michache tu iliyopita tuliwaita kila aina ya majina-from watangulizi wa ukoloni to mabeberu.Of course dunian imebadilika,lakini mabadiliko hayo sio yawe at expense of wazawa au wenye nchi.

Tunaingia gharama kubwa kuvutia watu wa aina ya Richmond,Dowans,wezi wa madini huko migodini,na wababaishaji wengine.Wengi wa wanaoitwa wawekezaji wanakuja na briefcase tupu zikiwa na mikataba tupu lakini ikishasainiwa,na baada ya miaka michache wanaondoka wakiwa na mamilioni kwenye akaunti zao-huku wakiacha,kwa upande mmoja, mafisadi wameongeza idadi ya nyumba ndogo zao,mahekalu yao na magari yao ya kifisadi,na upande mwingine walalahoi wakikodolea ardhi yao iliyoachwa mashimo matupu baada ya raslimali yote kuibiwa.

Tunakaribishaje wawekzaji kabla ya kutengeneza sera na sheria mwafaka za kutuwezesha kunufaika na ujio wa wawekezaji hao?Na uwekezaji wa aina ya "kupangisha nyumba kisha mwenye nyumba kulala mtaani" ni uhayawani usiopaswa kuendelea.

Tunafahamishwa wizi unaofanywa na baadhi ya makampuni ya simu ambayo kila baada ya muda flani yanabadili majina ilhali huduma zao mbovu zikiendelea kuwa zile zile za kuchefua.

Tunakaribisha wawekezaji wakati baadhi ya hao waliopo wanapata hadi jeuri ya kuchoma moto wazawa (rejea tukio la Kigamboni)lakini vyombo vya dola vinachelea kuchukua hatua zinazostahili.

Viongozi wetu wanapaswa kuwa makini na kurejea yaliyotokea nchini Afrika Kusini hivi karibuni ambapo wazawa waliamua kuelekeza hasira zao kwa wageni wakiamini kuwa ndio chanzo cha matatizo yao ya kila siku japo ukweli ni kwamba chanzo cha tatizo ni uongozi mbovu wa watawala wa nchi hiyo.

Tumeshuhudia jana baadhi ya wakazi wa Kigamboni wakiamua kupambana na wawekezaji japo kama ilivyo kawaida waliishia kudhibitiwa na polis,na huenda wakafunguliwa mashtaka huku mwekezaji aliyeua akiachwa "anakula kuku kwa mrija".

Nikirejea tukio hilo la Kigamboni,nilifadhaika kusoma tweet ya Mbunge wa jimbo hilo akieleza bila aibu kuwa "maandamano yamekuwa SUPPRESSED na CULPRITS watachukuliwa hatua za kisheria".Huyu ni mwakilishi wa watu haohao waliompoteza mwenzao kwa kuchomwa moto na mwekezaji!

Anyway,ujio wa wawekezaji ni habari njema kwa mafisadi kwani unapanua fursa za kupata teni pasenti na vijizawadi vya likizo huko ughaibuni,huku the so called wawekezaji wakigeuza nchi yetu kuwa shamba la bibi.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.