9 May 2011


Baada ya kifo cha Osama bin Laden,nani anaweza kuchukua nafasi yake?Tuangalie historia na tabia za warithi watarajiwa wa uongozi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda



big-fat-aman-nb04-inline
AFP-Getty Images
Ayman al-Zawahiri
Cheo: "Naibu" wa Osama
Wasifu: Daktari wa macho
Sifa Maalum: Msemaji mahiri wa Al-Qaeda
Maficho: Mara ya mwisho alionekana Khost, Afghanistan, mwaka 2001
Wasifu: "Kichwa" kilichoandaa Mashambulizi ya September 11,2001 nchini Marekani
Anafahamika zaidi kwa: Ushiriki wake katika mashambulizi ya mabomu kwa balozi za Marekani mwaka 1998
"Nembo" (trademark): Miwani ya njano


big-fat-aladel-nb04-inline
FBI-Getty Images
Saif al-Adel
Cheo: Mwandaaji wa operesheni za kigaidi kimataifa
Asili: Vikosi Maalum (special forces) vya Jeshi la Misri
Sifa maalum: "Bwana mipango"
Maficho: Waziristan, kwa mujibu wa ripoti
Wasifu: Aliwekwa kizuizini kwa miaka minane nchini Iran
Anafahamika kwa: Mashambulizi ya mabomu mwaka 1998
"Nembo": Vijinywele kwenye kidevu


big-fat-nb04-allibi-inline
Intel Center
Abu Yahya al-Libi
Cheo: Mwanateolojia
Asili: Mshairi na mwanazuoni
Sifa Maalum: Mwanapropaganda wa Al Qaeda
Maficho: Afghanistan au Pakistan
Wasifu: Alitoroka jula ya Wamarekani huko Bagram, Afghanistan
Anafahamika kwa: kujaribu kumuua Muammar Gaddafi
"Nembo": Hotuba kali


big-fat-nassar-nb04-inline
Intel Center / Polaris
Nasser al-Wuhayshi
Cheo: Kiongozi Peninsula ya Rabia
Asili: Katibu muhtasi wa Osama
Sifa maalum: Alitoroka gerezani Sanaa, Yemen, mwaka 2006
Maficho: Yemen
Wasifu: Alishirikiana bega kwa bega na Osama katika mapambano huko Tora Bora, Afghanistan
Anafahamika zaidi kwa: Kutoroka jela huko Yemen
"Nembo": "Andunje": ni mfupi wa chini ya futi tano



big-fat-adam-nb04-inline
Intel Center / AFP-Getty Images
Adam Gadahn
Cheo: Msemaji
Asili: Anapenda miziki ya sauti kali  yenye ujumbe wa kifo
Sifa maalum: Anamudu kiingereza vizuri,mjuzi wa teknolojia
Maficho: Alihamia Pakistan mwaka 1998, ameoa mkimbizi wa Kiafghanistani
Wasifu: Aliwahi kufungwa kwa kumpa kipigo mwenyekiti wa msikiti aliokuwa akiswali
Anafahamika zaidi kwa: Kumpa elimu Osama kuhusu mtikisiko kwenye sekta ya dhamana ya majengo (mortgage crisis)
"Nembo": Mjukuu wa mtaalam wa Kiyahudi wa elimu ya mkojo (urology)


big-fat-adnan-nb04-inline
FBI-Getty Images
Adnan el-Shukrijumah
Cheo: Afisa mipango ya nje
Asili: alisoma Kemia
Sifa maalum: Aliishi Marekani kwa miaka 15
Maficho: inadhaniwa kuwa Pakistan
Wasifu: Mrithi wa Khalid Sheikh Mohammed
Anafahamika zaidi kwa: Kupanga shambulio lililofeli la mabomu kwenye mfumo wa reli ya chini ya ardhi nchini Marekani mwaka 2009
"Nembo": Kushirikiana na magenge ya majahili wa Honduras


big-fat-nb04-alquso-inline
Fahd al-Quso
Cheo: Kamanda wa operesheni za mashambulizi
Asili: Mbeba mabegi ya bin Laden
Sifa maalum: Kulala fofofo: "alilewa" usingizi hadi akachelewa kazi ya kurekodi shambulio la kigaidi kwa manowari ya  USS Cole.
Maficho: Kaskazini mwa Waziristan
Wasifu: Kuandaa shambulizi la mabomu kwa manowari ya USS Cole.
Anafahamika zaidi kwa : Aliwatambua kwa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) magaidi wawili waliohusika na mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11,2001 nchini Marekani
"Nembo": Nywele zake kwenye paji lake zimekaa kama herufi V iliyogeuzwa


big-fat-nb04-Droukdel-inline-tease
Sifaouoi Mohamed / SIPA
Abdelmalek Droukdel
Cheo: Kiongozi wa  Islamic Maghreb
Asili: mwanafunzi wa sayansi
Sifa maalum: Mtaalam wa milipuko
Maficho: Aljeria
Wasifu: Idara ya Hazina ya Marekani ilitaifisha mali zake mwaka 2007
Anafahamika zaidi kwa: Kuua watu 70 kwenye kwa shambulizi za bomu jijini Algiers,Aljeria
Trademark: Tambara la kijana kama yale ya mabaniani
Imetafsiriwa (isivyo rasmi) kutoka jarida la Newsweek




Mkutano wa tatu wa Diaspora umemalizika majuzi jijini London huku,kama ilivyokuwa kwa Diapora I na Diaspora II,tumeishia kushuhudia zaidi picha za matukio kuliko maelezo ya mambo muhimu yaliyojiri katika mkutano huo (if there were any).Sina tatizo na watu wanaopenda kupiga picha na viongozi kwani huo ni uhuru wao wa kikatiba.Hata hivyo,nina tatizo kubwa na wale wanaodhani picha na viongozi ni muhimu kuliko kuwabana viongozi hao,hususan wanaposhindwa kutoa maelezo ya kueleweka.

Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe amekuwa sura iliyozoeleka kwenye mikutano hiyo ya Diaspora.Kwa wadhifa wake,ni mtu mwafaka kuiwakilisha serikali,sambamba na kusikia maoni,ushauri,maswali,nk kutoka kwa Watanzania wanaoshi nje ya nchi.Lakini kwa mwenendo wa ushiriki wake kwenye mikutano hiyo,yayumkinika kusema kuwa Membe amekuwa kama mtalii tu wa kutoa porojo moja baada ya nyingine badala ya kuwaeleza washiriki wa Diaspora Forums mafanikio yaliyokwishapatikana kutokana na uwepo wake au umuhimu wa mikutano hiyo (kama upo).

Usanii wa kwanza wa Membe ni katika kauli yake kuwa moja ya changamoto zinazoikabili serikali anayoitumikia ni kujua idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi.Huu ni usanii wa kitoto kwa vile Watanzania hao hajawaanza kuja nje wiki iliyopita,wala balozi za Tanzania nje-ambazo Membe ameziagiza kubuni mikakati ya kuwezesha kupata idadi ya Watanzania wanaoishi nje-hazijafunguliwa mwezi huu.

Badala ya kupachika jina la CHANGAMOTO,Membe alistahili kueleza bayana kuwa kutofahamika kwa idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi ni moja tu ya UZEMBE ULIOZOELEKA kwenye balozi zetu.Ni uzembe kwa vile umuhimu wa kufahamu idadi hiyo ya wana-diaspora umekuwepo tangu zamani hizo na sio mwaka huu tu au kwenye Diaspora Forums pekee.

Laiti washiriki wa Disapora hiyo wangekuwa serious,wangemkalia kooni Membe kumhoji kwanini zoezi hilo la kufahamu Watanzania waliopo nje ya nchi halijafanyika huko nyuma,na kwanini tuamini kuwa sasa litafanyika?Ikumbukwe Membe amekuwa Waziri wa Nje kwa miaka sita sasa,hivyo kukurupuka wiki iliyopita kukumbuka umuhimu wa kuwa na idadi ya Watanzania nje ya nchi ni sehemu tu ya ubabaishaji wake.

Membe anadai kuwa sababu ya yeye kuja London kuhudhuria mkutano huo ni kukusanya hoja kutoka kwa wadau ili ziweze kusaidia tatizo la Diaspora kupelekwa Bungeni na hatimaye kuingizwa kwenye Katiba.Come on,Membe!That's too cheap politicking even in your own standards.Yaani kukusanya hoja za Watanzania wanaoishi ughaibuni ni lazima kufanywe na waziri ilhali tuna balozi zetu na vyama mbalimbali vya Watanzania?

Na hata tukimpa Membe benefit of a doubt,kwanini asituambie namna alivyokwisha shughulikia hoja alizokusanya kwenye Diaspora I na Diaspora II kabla ya kukurupuka na usanii mwingine kwenye Diaspora III?Kama hoja za nyuma hazijafanyiwa kazi,how come hizo mpya au mwendelezo wa zile za zamani zitashughulikiwa sasa?

Japo Membe anastahili lawama,lakini washiriki wa Diapora Forums nao wanapaswa kulaumiwa kwa kuruhusu cheap lies kutoka kwa same crooked politicians year in year out.Yayumkinika kuamini kuwa udhaifu wa wahudhuriaji wa Diaspora Forums kuuliza maswali magumu yanayostahili majibu ya msingi unachangia sana kumfanya Membe awe "MGENI RASMI WA KUDUMU" kwenye mikutano hiyo kwani anajua he would easily get away with usanii wake.Unadhani angejua kuwa atakaliwa kooni kuhusu ubabaishaji wake,kwa mfano kwenye suala la dual nationality,angetia mguu kwenye Diaspora Forum iliyopita majuzi?

Lakini kilichonikera zaidi katika usanii wa Membe ni kauli yake ya kitoto kuwa eti changamoto nyingine inayoikabili Diaspora ni "WATU WENGI HAWAFAHAMU VIZURI MAANA YA DIASPORA".Utterly rubbish!Hivi Membe anaweza kutueleza amejuaje kuwa watu wengi hawafahamu maana ya Diaspora?Au,je anaweza kutuambia kwanini hawafahamu maana ya neno hilo ambalo lipo kwenye kamusi?Ungetarajia waliohudhuria mkutanio huo wamzomee Membe kwa kauli hiyo isiyo na kichwa wala miguu.Na Membe ana lipi la kutuambia katika madai yake kuwa neno Diaspora halifahamiki kwa wengi,i.e. kutofahamu maana ya neno hilo kunakwamishaje maazimio ya Diaspora Forums zilizopita?

Haya ndio matatizo ya kualika wageni rasmi wanaokuja kutalii badala ya kuzungumza mambo ya msingi.Ni dhahiri kuwa laiti waandaaji wa Diaspora Forums wangetaka mkutano huo uwe na maana wangeandaa mazingira ya kuepuka wababaishaji kama Waziri Membe ambao ni mahiri sana katika kutoa hotuba za kuleta matumaini lakini hotuba hizo zinabaki kuwa hotuba tu,na kusahaulika mara baada ya kumalizika kwa shughuli husika.

Kama kupiga konzi kwenye kidonda kibichi,Membe pasi aibu aligusia suala la uraia pacha (dual nationality).Akaanza kwa kueleza umuhimu wa uraia pacha,na kusema kuwa nchi zilizoruhusu uraia pacha zimewafanya watu wao kupata kazi nzuri zenye mishahara mikubwa na hivyo kuwawezesha kutuma fedha nyingi katika nchi wanazotoka.Huu ndio uelewa wa Waziri wa Mambo ya Nje kuhusu umuhimu wa Diaspora!!!

Labda hakupitia speech notes zake vizuri,labda hakufanya brainstorming ya kutosha kabla ya kutoa hotuba yake kwa wana-Diaspora,lakini ni wazi Membe anafahamu fika kuwa umuhimu zaidi wa uraia pacha ni suala la haki za binadamu kuliko mishahara mikubwa au kazi nzuri.Nani aliyemwambia Membe kuwa wana-Diaspora wana kazi za ovyo ovyo zisizolipa mishahara mizuri kwa vile tu hawana uraia pacha?

Kwa hoja hizi mfu,ni wazi kuwa Membe si mwakilishi mzuri wa wana-Diaspora katika kilio chao cha muda mrefu cha uraia pacha.Membe amegeuza Diaspora Forums kuwa sehemu ya kuwapa matumaini kuhusu suala hili ilhali hafanyi jitihada zozote kuhakikisha suala hilo linahama kutoka kuwa ahadi hewa na kuwa sheria kamili inayotekelezeka.

Kuhusu changamoto ya kuwawezesha Watanzania walio nje ya nchi kuchangia maendeleo ya Tanzania,Membe anapswa kufahamu kuwa kila Mtanzania aliye nje ya nchi ana connection na Tanzania.Wengine tuna wazazi,kaka,dada,wadogo,nk huko nyumbani na licha ya nchi yetu kujifanya haitambua umuhimu wa Watanzania walio nje,wameendelea kupunguza makala ya ufisadi kwa ndugu na jamaa zao huko nyumbani kwa kuwatumia fedha za matumizi na misaada mingineyo.

Katika mkutano huo,mmoja wa wajumbe alipendekeza uanzishaji wa kumbukumbu mkeka ya ujuzi na fani wazizonazo Watanzania waishio nje.Wazo zuri lakini nadhani mtoa hoja amesahau umuhimu wa data protection,na namna taarifa hizo binafsi za Watanzania walio nje zinavyoweza kuishia mtaa wa Mkwepu kwa wanaotengeneza vitambulisho feki.I would never trust fisadi awe na taarifa zangu binafsi ilhali nafahamu fika kuwa zitaozea tu kwenye mafaili kama sio kufungiuwa vitumbua na maandazi.

Kama taafira zilizokusanywa kufahamu chanzo cha milipuko ya mabomu huko Mbagala na Gongo la Mboto zimepuuzwa,mtoa hoja anataraji mijuiza gani  kwa taarifa za Watanzania walio nje kutumiwa ipasavyo?Nadhani kuna baadhi ya Watanzania wenzetu walio nje hawajishughulishi kufahamu uharamia,ufisadi,ubabaishaji,uzembe na utapeli wa kisiasa unaendelea huko nyumbani kiasi kwamba wanaweza kupoteza muda wao kuwasikiliza akina Membe "wakiuza sura" kwenye Diaspora Forums.

Unajua kwanini nasema Membe anafanya usanii kwenye suala la uraia pacha?Ameshatoa kauli kadhaa za kibabaishaji kuhusu suala hilo,moja ikiwa aliyoitoa Januari mwaka huu kwenye mkutano wa IOM ambapo alidai kuwa utafiti uliofanyika umehitimisha umuhimu wa uraia pacha,Wizara yake imeanzisha kitengo cha kushughulikia suala la Diaspora,na sheria ipo mbioni kuanzishwa.

Lakini kwenye mkutano wa Diaspora uliomalizika wiki iliyopita,Membe wala hakugusia ni lini sheria hiyo itaanza kufanya kazi.Katika mkutano huohuo wa IOM,Membe aliwazuga wajumbe kwa kuahidi kuwa sheria ya uraia pacha ingekuwa tayari kufikia mwisho wa mwaka jana.Amekuja London miezi mitano baadaye na kuendelea ngonjera hizo hizo.

Hebu sikiliza porojo za Membe kwenye Diaspora Forum II iliyofanyika mwaka jana



Na hapa pamoja na kuongelea mambo mengine,mwishoni mwa clip ifuatayo anajibu swali na Freddy  Macha kwa kuahidi tena "MWISHO WA MWAKA HUU" kama alivyoahidi mwaka jana kuwa "MWISHO WA MWAKA HUO 2010".



Enewei,kulikuwa Diaspora Forum I,ikamalizika na picha tukaona.Ikaja Diaspora Forum II,ikamalizika na picha tukaonyeshwa.Na majuzi imemekuja Diaspora Forum III,imemalizika wiki iliyopita na picha tumeziona.Tusubiri Diaspora Forum IV...bila shaka tutaendelea kushuhudia picha nyingine na usanii mwingine unaohanikizwa na maneno kama "mchakato","changamoto","vipaumbele" na usanii mwingine kama huo.Blogu hii inatoa wito kwa wana-Diaspora kujaribu kuwaonyesha Watanzania wenzatu walio nyumbani kuwa licha ya kutopendezwa na ubabaishaji wa baadhi ya viongozi wetu huko nyumbani,hatuwezi kutoa fursa kwa ubabaishaji huo kuwa exported hadi huku ughaibuni.Ili Diaspora Forums ziwe na manufaa,they need to go beyond being just another photo-ops.

7 May 2011


Nilipofika hapa Uingereza kwa mara ya kwanza,takriban muongo mmoja uliopita,nilishangazwa na jinsi wengi wa watu hawa waliotuletea dini huko nyumbani wakiwa hawana habari kabisa na dini.Ilinishangaza kuona baadhi ya majengo yaliyokuwa yakitumika kama nyumba za ibada huko nyuma yakiwa yamegeuzwa klabu za usiku au baa.

Kwa ujumla,idadi kubwa ya wanaohudhuria makanisani kwa hapa ni raia wa kigeni au wale wenye asili ya nje ya nchi hii.Hata hivyo,kuna idadi ya wastani ya Waingereza wanaojitambulisha kama wenye imani ya kidini japo haimaanishi kuwa wanakwenda makanisani.

Pamoja na kuzorota kwa dini miongoni mwa wengi,kwa kiasi kikubwa wananchi hapa wana uadilifu mkubwa hususan katika kutoa huduma.Unajua,kibarua sio suala la mshahara tu bali pia kujali yule unayemhudumia.Kadhalika,kutoa au kupokea rushwa sio tu suala la kukosekana kwa sheria madhubuti bali pia ni suala la kiroho,namna nafsi inavyomsuta mtu kutoa,kudai au kupokea rushwa.

Binafsi nadhani dini ya kweli ni upendo.Na hata katika Biblia Takatifu tunafundishwa kuwa ni vigumu mtu kumpenda Mungu ambaye hamuoni ilhali anamchukia jirani yake anayemwona kila mara.

Japo ni muhimu kuhudhuria nyumba za ibada,lakini binafsi naona ni bora kuwa mtu asiyekwenda kanisani au msikitini lakini anaishi katika namna anayompendeza Mungu (na wanadamu wenzie) kuliko hao wasiokosekana makanisani au misikitini lakini ndio wanaodumisha uzinzi,ufisadi,unafiki,na kila aina ya baya.Hapa simaanishi kuwa kila aendaye kanisani au msikitini hafanyi anayopaswa kufanya,bali napigia mstari umuhimu wa matendo mema.

Kwa hapa Uingereza kumekuwa na mfumuko mkubwa wa makanisa "mapya" (new Christian movements).Makanisa haya yanazidi kupata waumini wengi na kukua aidha kwa sababu madhehebu makuu (Katoliki,Waluteri,Waanglika,nk) yameshindwa kukidhi matarajio ya waumini hao wanaokimbilia makanisa mapya,au kwa upande mwingine ni ukweli kuwa licha ya majukumu ya kiroho,makanisa hayo ambayo waumini wake wengi ni wageni (hususan Waafrika) yamekuwa kama sehemu ya watu wanaotoka eneo moja kujumuika.Mnaijeria akienda kanisa la Kinaijeria anajikuta kama yupo nyumbani,na hivyo hivyo kwa Mtanzania akienda kanisa linaloendesha ibada kwa kiswahili.

Lakini,baadhi ya makanisa hayo yamekuwa yakishutumiwa kuwa ni miradi ya kitapeli ya wajanja flani.Kwa mfano,kituo cha runinga cha Channel 4 kiliwahi kuonyesha documentary ya namna baadhi ya makanisa ya Waafrika jijini London yalivyokuwa yakisababisha kuvunjika kwa ndoa (kwa mfano pale mchungaji anapomwambia mume kuwa mkewe ana majini) na hata kupelekea vifo,hususan vya watoto wadogo wanaotuhumiwa kuwa wana majini.Kibaya zaidi,baadhi ya maaskofu wa makanisa hayo walidiriki kudanganya mabinti kuwa matatizo waliyokuwa nayo yalihitaji maombi maalumu nyakati za usiku,na hatimaye mabinti hao wakaishi kufanyiwa tendo la ndoa.

Utafiti mdogo tuliofanya mie na wanafunzi wenzangu Faith Msina,Latifa Almasi (Queen Latifa) na Baraka Msemwa,mwaka 1999 (kama sehemu ya kozi ya Mwaka wa Tatu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Sosholojia ya Dini) ulionyesha matokeo kwamba wengi wa watu wanaoamua kujiunga na "madhehebu mapya" ni pamoja na wale wenye matatizo ya kibinadamu ambayo "dini kuu" zimeshindwa kuyatatua.Tulifanya utafiti wetu kwenye Kanisa "la Kakobe" (Full Gospel Bible Fellowship),Mwenge jijini Dar,na asilimia kubwa ya wahojiwa walikiri kuwa kilichowavutia kujiunga na kanisa hilo ni "miujiza" mbalimbali,kwa mfano kwenye uponyaji,ajira,nk.

Lakini jambo la kusikitisha ni tabia inayozidi kushamiri ya matapeli kuanzisha makanisa kama ajira.Hawa ni wajanja wanaofahamu fika kuwa masuala ya imani hayahitaji udadisi,na laiti tapeli husika akifanikiwa kutangaza "miujiza yake",basi muda si mrefu kijikanisa chake kitageuka hekalu kubwa la "maombezi na miujiza".Simaanishi kuwa wote wanaoanzisha makanisa ni matapeli,lakini ni ukweli usiopingika kuwa kuna matapeli kadhaa wanaotumia jina la Bwana kutapeli waumini wenye mahitaji ya kimwili na kiroho.

Ni kwa mantiki hiyo basi,siafikiani na msimamo wa baadhi ya wachunga kondoo wanaopinga dhamira ya serikali kukagua mapato na matumizi yao.Pengine ni kukosa ufahamu tu,uamuzi wa serikali kutotoza kodi au kutoangalia mapato na matumizi ya taasisi za dini ni suala la upendeleo (privilege) zaidi kuliko stahili.Kama waumini wa taasisi hizo za kidini wanawajibika kwa mamlaka za mapato,kwanini isiwe kwa viongozi wa dini na/au taasisi zao?

Je wachunga kondoo hao wa Bwana wanahofia nini kuhusu dhamira hiyo nzuri ya serikali?Ieleweke kuwa kama wana kipato juu ya kiwango cha msamaha wa kodi basi ni lazima walipe kodi.Lakini hata kama suala hapa si ulipaji wa kodi,ni muhimu kwa mamlaka za mapato kufahamu mapato na matumizi ya taasisi hizo kama ilivyo kwa taasisi nyingine za umma na za binafsi.Dini si kigezo cha kutofuata sheria,na hata Maandiko Matakatifu yanakumbusha kuwa "ya Musa apewe Musa,na ya Kaizari apewe Kaizari",or something like that.

Enewei,soma habari husika hapa chini

Maaskofu wapinga serikali kudai taarifa za mapato

na Betty Kangonga

BAADHI ya makanisa ya Kipentekoste yamesema si haki kwa serikali kudai taarifa ya mapato na matumizi ya fedha za makanisa wakati yenyewe haitoi hata ruzuku kwa taasisi hizo za dini.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mchungaji wa Kanisa la Maombezi la Ubungo Kibangu (GRC), maarufu kama Mzee wa Upako, Anthony Lusekelo, wakati wa hafla ya chakula cha usiku kwa wachungaji 100 wa makanisa ya Kipentekoste.

“Huu ni uonevu usio na mfano, wachungaji lazima tusimame imara kuhakikisha tunatetea haki zetu, tena tunatakiwa kuacha woga. Kwa nini serikali inahitaji mapato na matumizi wakati hawajui fedha hiyo tunapopata? Tunahitaji serikali ijenge heshima na kazi inayofanywa na viongozi wa dini ndani ya nchi,” alieleza.

CHANZO:Tanzania Daima

6 May 2011


KESI YA BALOZI MAHALU: Mkapa akunjua makucha

na Happiness Katabazi

HATIMAYE utetezi wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, umetua rasmi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam.

Mkapa ambaye ni shahidi wa pili wa kesi hiyo alitoa utetezi huo ambao unaweza kuandika historia mpya katika mwenendo wa kesi nchini, kupitia kiapo chake ambacho kimewasilishwa mahakamani na wakili wa mshtakiwa huyo, Mabere Marando.

Katika moja ya vipengele 13 vya kiapo hicho, pasipo kutaja jina, maelezo ya kiongozi huyo mstaafu yanamgusa Rais Jakaya Kikwete ambaye wakati Mkapa akiwa madarakani alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Hiyo inakuwa ni mara ya kwanza kwa rais mstaafu, kutoa utetezi mahakamani kwa kesi inayomgusa mmoja wa waliokuwa wateule wake wakati akiwa madarakani.

Kesi hiyo Namba 1/2007 ambayo Mahalu anashtakiwa pamoja na Grace Martin inasikilizwa na Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilivin Mugeta.

Katika kesi hiyo, Mahalu na Martin wanatuhumiwa kwa wizi wa shilingi bilioni tatu katika ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Rome.

Katika hati ya kiapo chake cha Machi 31 mwaka huu, ambayo imeandaliwa kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Nyaraka (The Registration of Documents Act, Cap. 117 of 2002), Mkapa anaeleza kuwa kila kilichofanywa na Mahalu kilikuwa sahihi na kilikuwa na baraka ya serikali aliyokuwa akiingoza toka mwaka 1995-2005.

Ushahidi huo wa rais Mkapa ambao Tanzania Daima inayo nakala yake, umeorodhesha maelezo yake yaliyoainishwa katika vipengele 13.

Mkapa katika utetezi wake huo anadai kuwa mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo la ubalozi lililoko katika mtaa wa Vialle Cortina d’Ampezzo 185 mjini Rome ulizingatia sera ya serikali ya upatikanaji au ujenzi wa majengo ya kudumu ya ofisi na makazi na kwamba ulizingatia maslahi ya taifa.

Hati hiyo ya kiapo ambayo tayari wakili Marando amesema ameishaiwasilisha pia Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Eliezer Feleshi, inaanza kwa kusema, “Mimi Benjamin Mkapa, mtu mzima, Mkristo, mkazi wa Dar es Salaam, ninaapa kama ifuatavyo, ’nilikuwa Rais mtendaji wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vipindi viliwili mwaka 1995-2005 na nina uhakika wa yote haya nitakayosema ndani ya kiapo hiki.’

Katika kiapo hicho Mkapa anadai pia kuwa alifahamishwa na watendaji wa serikali aliyokuwa akiingoza jinsi mchakato uliofanyika na ripoti za uthamini wa serikali zilizotumika katika kufikia hatua ya kununua jengo hilo la ubalozi.

Anadai kuwa tathmini ya jengo hilo ambalo Mahalu anadaiwa kufanya udanganyifu na wizi kwa kulipa fedha kinyume na ilivyotajwa katika mkataba ambayo ilifanywa na serikali ya awamu ya tatu kupitia wizara mbili tofauti, Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Ardhi na Maendeleo Mijini.

Anaendelea kudai kuwa, anatambua kuwa ripoti ya serikali ya uthamini wa jengo hilo iliandaliwa na Wizara ya Ujenzi kwa kiwango cha dola za Marekani milioni tatu na Wizara ya Ardhi kwa thamani ya euro milioni 5.5.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo kupitia mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulikuwa wa aina mbili, mmoja ni rasmi na mwingine wa kibiashara na kuongeza kuwa kwa mujibu wa taratibu ya serikali ya Italia na kuwa hilo lilifanyika kwa baraka za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Utaratibu kama huo wa mikataba miwili ushawahi kufanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pale ambapo ilionekana haja kwa kuzingatia maslahi ya taifa kwanza....na kuwa ni mimi ndiye niliyezindua jengo hilo la ubalozi Februari 23 mwaka 2003,” anadai Mkapa.

Shahidi huyo wa Mahalu anadai pia kuwa kwa mujibu wa kiapo chake anakumbuka vyema taarifa ya serikali iliyotolewa bungeni Agosti 3 mwaka 2004 iliyosema na kuthibitisha kuwa taratibu zote zinazohusiana na manunuzi ya jengo kwa mujibu wa maelekezo ya serikali, zilifuatwa na kwamba muuzaji wa jengo hiilo alilipwa fedha zote.

Kumbukumbu ambazo gazeti hili linazo zinaonyesha kwamba, Agosti 3, 2004, Kikwete alitoa maelezo bungeni kuhusu utata uliokuwapo awali kuhusu ununuzi wa jengo hilo la ubalozi.

Kikwete katika maelezo yake hayo ambayo yako pia katika kumbukumbu rasmi za Bunge (Hansard) anaeleza, “Mheshimiwa Naibu Spika mwaka 2001/02 wizara ilinunua jengo la ubalozi counsel katika ubalozi wa Rome katika jitihada za kuondokana na tatizo la kupanga majumba ya watu huko nje na pia kupunguza gharama za kuendelea kulipa pango la nyumba kila mwaka.

“Ununuzi wa jengo hili ulifuata taratibu zote za manunuzi ya majengo ya serikali kwa kuzishirikisha wizara za ujenzi, ardhi na maendeleo ya makazi pamoja na Wizara ya Fedha.

“...Jengo lilifanyiwa tathmini na wataalamu wetu na kukubaliana na ununuzi wa Euro 3,098,781.40 tarehe 6 Machi 2002 fedha za awamu ya kwanza katika ubalozi wa Rome zilipelekwa nazo zilikuwa shilingi 700,000,000 tarehe 28 Juni 2002 zilipelekwa shilingi 120, 000,000.

“Mwishoni mwa tarehe 26 Agosti mwaka 2002 zilipelekwa shilingi 1,000,000,000 jumla ya fedha zilizokuwa zimepelekwa zikafikia shilingi 2,900,000,000 na baada ya hapo ubalozi wetu ulitekeleza taratibu zote za ununuzi wa jengo na kumlipa mwenye nyuma kiasi hicho cha fedha,” alieleza Kikwete.

Akimwelezea Mahalu katika utetezi wake, Mkapa alidai katika kipindi chote alichokuwa rais wa nchi alifanya kazi na mshtakiwa huyo katika nyadhifa mbalimbali za utumishi wa umma na kwamba mshtakiwa huyo ni mtu wa tabia njema, mkweli, mwaminifu na mchapaji kazi.

Mkapa anahitimisha utetezi wake kwa kueleza kuwa, kutokana na mwenendo huo wa kutukuka, Rais wa Italia alimpatia moja ya tuzo za heshima yenye hadhi ya juu kabisa ya taifa hilo Profesa Mahalu, muda mrefu baada ya balozi huyo kuwa ameshaondoka nchini humo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasilisha mahakamani ushahidi huo wa Mkapa jana, wakili Marando alisema mteja wake anakusudia kupeleka jumla ya mashahidi 10.

Mashahidi hao ni mteja wake (Mahalu), Mkapa, Rais Jakaya Kikwete, kwani wakati akinunua jengo hilo ndiye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye ndiye alimpa mteja wake nguvu ya kisheria ya kuendelea na ununuzi wa jengo hilo, aliyekuwa waziri wa Ujenzi wa John Magufuli na mashahidi wengine na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba ambaye pia anakabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bil. 11.7.

Kuwasilishwa kwa hati ya kiapo cha Mkapa mahakamani hapo, kumekuja baada ya Hakimu Mkuu Mfawidhi Ilvin Mugeta kusema kuwa yeye ndiye amejipangia kusikiliza utetezi wa washtakiwa hao Aprili 28 mwaka huu.

Hatua ya Hakimu Mugeta kusikiliza utetezi huo inakuja baada ya Machi 28 mwaka huu, Jaji Sivangilwa Mwangesi ambaye ndiye aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo tangu awali kujitoa baada ya mawakili wa washtakiwa kuwasilisha sababu sita za kumwomba ajitoe kwa sababu kukosa imani naye Machi 25 mwaka huu.

Mapema mwaka 2007, Jamhuri kupitia mawakili wake toka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ben Lincoln na Ponsian Lukosi iliwafikisha mahakamani hapo kwa mara ya kwanza washtakiwa hao kwa makosa ya uhujumu uchumi, wizi wa zaidi ya euro milioni mbili wakati wakisimamia ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Rome nchini Italia.

CHANZO: Tanzania Daima











CHANZO: Jamii Forums

5 May 2011


Makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida maridhawa la Raia Mwema inafanya uchambuzi linganifu kuhusu,kwa upande mmoja,tuhuma zilizomwandama Rais Obama kuwa sio raia wa Marekani,na hatimaye uamuzi wake kutoa cheti chake cha kuzaliwa,na kwa upande mwingine ni tuhuma za ufisadi zinazomwandama Rais Kikwete,na jinsi kutochukua hatua kadhaa kunazifanya tuhuma hizo kuwa na uzito.

Kadhalika,makala hiyo inawagusa jamaa zangu wa Usalama wa Taifa,kwa kuangalia wnavyofanikisha upatikanaji wa taarifa zinazowahusu wanasiasa wa CCM wanaotajwa kama magamba.Lakini ninaibua maswali kadhaa huku nikiwatahadharisha kuhusu uwezekano wa kuzua skandali kama ile ya Watergate ya nchini Marekani ambapo Rais Nixon,pamoja na mambo mengine alitumia nafasi yake kuamrisha ukusanyaji wa taarifa za kiintelijensia dhidi ya wapinzani wake wa kisiasa.

Pamoja na makala hiyo unayowaza kuisoma kwa KUBONYEZA HAPA,jarida hili la Raia Mwema limesheheni habari na chambuzi za kiwango cha juu kabisa. 


4 May 2011






When Osama bin Laden was killed earlier this week,US officials said DNA testing and facial recognition software proved they had got their man.

However, the lack of actual documentation released to the public (so far), and the fact he was buried at sea so quickly, has predictably seen an explosion of conspiracy theories dreamt up by doubters, or ‘deathers’ – as they’ve have now been dubbed. Here are just a few of them.



SOURCE: Yahoo! News

Osama bin Laden conspiracy theories


1. He must be still alive because there’s no proof

The lack of photos, videos and other evidence, plus inconsistencies in accounts of the raid that killed him, apparently shows the US government made the whole thing up.

Taliban spokesman Zabiullah Mujahid is one doubter. He released a statement to journalists saying: “This news is only coming from one side, from Obama’s office, and America has not shown any evidence or proof to support this claim.” Iranian State television also declared: "the mystery [of his death] has increased”.

Anti-war activist Cindy Sheehan, whose son was killed in the Iraq war, also disputed the news on Facebook. She said: "I am sorry, but if you believe the newest death of OBL, you're stupid. Just think to yourself - they paraded Saddam's dead sons around to prove they were dead - why do you suppose they hastily buried this version of OBL at sea? This lying, murderous Empire can only exist with your brainwashed consent - just put your flags away and THINK!"

Naturally, several other Facebook pages made by skeptics have been set up, while searches for "osama bin laden not dead," "osama bin laden still alive" and "bin laden not dead" on Yahoo! spiked off the charts on Monday.

Our figures show most of the searchers of "bin laden conspiracy" were from the US states of Oregon, Wisconsin, North Carolina, Indiana and New Jersey.

2. He’s already dead

Ever since the September 11 attacks there have been numerous reports of bin Laden’s death. Back in 2001 Fox News reported he’d died of lung complications in Tora Bora. In 2005 Senator Harry Reid suggested bin Laden was killed in the Pakistan earthquake, while in 2007 Benazir Bhutto said the al-Qaeda boss was murdered by Pakistani militant Omar Sheikh.

Conspiracy theorists reckon official news of his death was kept from the public to continue justifying the war on terror, with the US government periodically releasing fake videos of the terror leader to keep the world convinced. The theory is that because the powers that be didn’t need bin Laden as a terrorist ‘boogieman’ anymore, they finally announced his death.

3. He was taken alive

Controversial Fox News talk show host Glenn Beck is famous for his conspiracy theories and gave a couple of suggestions about bin Laden’s death on his radio show. Firstly, he speculated that Obama ‘ghosted out’ the al-Qaeda leader - which means the Navy SEALs made it look like he was killed when actually he was taken alive, presumably to be interrogated.

4. He knew about a nuclear bomb

Beck’s other theory was that bin Laden was captured to stop him revealing the location of al-Qaeda’s nuclear bomb. This is reference to WikiLeaks documents that show US security officials briefed other countries on the possibility the terror group had a dirty bomb. Beck didn’t explain why the US government would do this.

5. He’s been ‘on ice’ for years

Another controversial US radio host Alex Jones said the US concocted the story to justify a security crackdown. He reckons bin Laden was killed back in 2002 and his body has been “literally frozen” to be rolled out at a later date.

6. He was given up by Pakistan

Website Maggie’s Farm quotes ‘speculation’ (though they don’t name sources) that, contrary to the reports the US acted alone, Pakistan actually knew all all about Osama’s location and offered up the al-Qaeda leader as a “sweetener” to speed US withdrawal from Afghanistan.

7. He was killed as a pretext for war in Pakistan

David Icke doesn’t agree though. No round-up of conspiracy theories would be complete without a contribution from Icke, who has written extensively about the event on his website. One of his theories is that the killing was fabricated to give the US a reason to actually invade Pakistan because they were harbouring the terror chief. War with China, he suggests, then Russia, will follow. Let’s hope he’s wrong.

8. He was killed to revive Obama’s poll ratings

Barack Obama’s presidency has been a difficult one. Universal healthcare, the budget deficit, high unemployment and fuel costs have resulted in low poll ratings and defeat for the Democrats at last year’s mid-terms, when the Republicans took the House of Representatives.

What better way then, some bloggers have argued, to get those poll ratings up than by suddenly killing America’s most wanted man? Writing on a Tea Party website, one conspiracy theorist said: "Don't you think Obama needs something to assure his re-election?"

9. He was killed to trump Trump

There’s no love lost between Donald Trump and Obama, with the property tycoon reviving the issue of the president’s birth certificate last week. Obama responded by first mocking Trump at the White House correspondents’ annual dinner. Then, when the time came for the bin Laden announcement, ‘Celebrity Apprentice’ had to be interrupted on NBC. The host? Donald Trump.

10. His killing was delayed for the Royal Wedding

The close proximity of the Royal Wedding and the death of bin Laden inevitably means some conspiracy theorists have linked the two events.

Firstly, a security expert told The Daily Express that the reason Wills and Kate postponed their honeymoon - possibly to Jordan – was because they had a tip-off on Friday about the upcoming events in Pakistan.

There’s also been speculation that the White House, who could have killed bin Laden on Friday, delayed pulling the trigger for two days in order for the two events not to clash.

11. His date of death is spooky

Osama bin Laden’s death was announced exactly eight years after George W Bush made his now infamous ‘Mission Accomplished’ announcement. Even spookier, it happened 66 years and 6 hours after the world learned about the death of Hitler. That’s 666.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.