22 Jul 2011

Samuel Sitta mwenyewe anayepigwa mkwara na Guninita yupo hoi kwa usingizi.Labda hapo anaota yeye bado Spika

Guninita ‘amvaa’ Sitta
Posted By admin On July 22, 2011 @ 7:59 am In Habari kuu,Mtanzania |

• Adai ni mzigo, anawadanganya na kuwapotosha wananchi
• Asisitiza ni sehemu ya tatizo la mgawo wa umeme
• Asema si mgeni serikalini, ni mchochezi, mnafiki na mfitini
• Aonya anaigawa, anaitumbukiza CCM kwenye shimo
• Asema mambo yakiendelea hicho mwaka 2015 CCM itaambulia patupu

Na Habakuki Urio

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita amemlaumu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta akidai ni mnafiki na mchochezi anayetumika kuigawa CCM na kukitumbukiza chama hicho kwenye shimo.

“Sitta ni sehemu ya serikali na si mgeni serikalini. Alikuwapo tangu kipindi cha Mwalimu Nyerere, na pia alikuwa Spika wa Bunge. Kwa nafasi hizi yeye ni sehemu ya tatizo na siyo kuwadanganya wananchi na kuwapotosha kwa kuirushia serikali lawama.

‘Anaudanganya umma. Anataka kujenga umaarufu ambao siyo wa kwake. Kama ni kuharibu waliharibu wote na siyo kusema tatizo ni la serikali.
‘Sitta amekuwa mchawi wa CCM… chama kinajimaliza chenyewe tena kwa kutumia viongozi wa nafasi za juu.,” alisema Guninita.

Guninita alikuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara Mbezi na Mbezi kwa Msigani katika jana, katika ziara ya kutekeleza agizo la Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete la kuleta mageuzi ndani ya chama hicho na ‘kujivua gamba’.

Alisema hali ya siasa ndani ya chama hicho si shwari kutokana na mgawanyiko mkubwa wa baadhi ya viongozi ambao wanazungumza wanavyojisikia bila kujali maslahi na ukweli ndani ya Chama hicho.

“Kilichotufikisha hapa tulipo leo ni unafiki na fitina za viongozi kama Sitta ambao hawaeleweki wanafanya nini ndani ya chama chetu. Ndiyo maana viongozi wanajiuzulu ovyo, kitu ambacho siyo sahihi, chama kinapoteza makada muhimu na kuwaacha watu mizigo na wafitini.

“Namshangaa Waziri Sitta, ana uwezo wa kwenda kwa Rais muda anaojisikia na pia alikuwa na nafasi ya kuyasema mambo yale katika vikao vya chana “party caucus”, na pia kwenye vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) lakini anaropoka mambo kama hayo mbele ya umma wa watanzania na kuwapa umaarufu wapinzani.

“Amekosa busara kwa kuwa amekiuka maagizo ya Rais. Tunajua hakutumwa na Rais, bali alikurupuka tu, na bila kujijua anaiponda Ilani ya Uchaguzi ya CCM ambayo ndiyo muongozo wa kutekeleza majukumu yetu.
‘Mawaziri na wabunge wanasema tofauti na Rais anavyosema kuhusu matatizo ya umeme kwa sasa,” alisema Guninita

Alisema kauli mbovu za baadhi ya viongozi ambazo hazina ukweli zinabomoa chama, na kama CCM haitakauwa makini na kuwaonya wapotoshaji hao katika uchaguzi mkuu wa 2015 chama hicho kitaambulia patupu.

“Upinzani wanajipanga vizuri katika kuhakikisha mwaka 2015 wanachukua nchi, na kwa hali hii tulio nayo … kwa kauli za akina Sitta watafanikiwa kwa kuwa chama kitakuwa kimeyumba na kukosa imani kwa wapigakura wake.

“Haya siyo maneno ya Waziri, huyu jamaa ana mambo yake anayotekeleza… haiwezekani Sitta leo kuyasema haya, labda ana hasira za kukosa Uspika wakati yalikuwa makubaliano ya CCM kumuondoa kwa mafanikio ya chama na kutimiza sera ya 50 kwa 50.

‘Nilimsikia akisema kuwa atatembea mikoa yote kulisema hilo, lakini nawahakikishia kuwa hatafika Dar es Salaam labda aje na barua ya Mwenyekiti au Katibu Mkuu wa CCM kuwa wamemruhusu kupotosha jamii. Nasema kuwa hatutakubaliana na uongo wake,” alisisitiza Guninita.

Hivi karibuni, katika mkutano wa hadharani mjini Mbeya, Sitta pamoja na mambo mengine, alikaririwa akishauri serikali iwaombe radhi wananchi kutokana na tatizo la mgawo wa umeme unaoendelea nchini hivi sasa.

Guninita alisema mkutano wa jana ni matunda ya makubaliano ya kujivua gamba kama alivyoagiza Mwenyekiti Kikwete na kuwataka viongozi wote wa CCM kutembelea matawi na mashina katika maeneo yao kuyajua matatizo ya wapiga kura wao na kuimarisha mizizi ya chama ambayo ipo katika mashina na matawi.


 
Who Needs Humans?
As if American workers don’t have it rough enough, with unemployment skyrocketing and jobs moving overseas, now there’s another threat: robots.
by Daniel Lyons, July 18, 2011
Amid all the job losses of the Great Recession, there is one category of worker that the economic disruption has been good for: nonhumans.
From self-service checkout lines at the supermarket to industrial robots armed with saws and taught to carve up animal carcasses in slaughter-houses, these ever-more-intelligent machines are now not just assisting workers but actually kicking them out of their jobs.
Automation isn’t just affecting factory workers, either. Some law firms now use artificial intelligence software to scan and read mountains of legal documents, work that previously was performed by highly paid human lawyers.
“Robots continue to have an impact on blue-collar jobs, and white-collar jobs are under attack by microprocessors,” says Edward Leamer, an economics professor at UCLA’s Anderson School of Management and director of the UCLA Anderson Forecast, a survey of the U.S. and California economies. Leamer says the recession permanently wiped out 2.5 million jobs. U.S. gross domestic product has climbed back to pre-recession levels, meaning we’re producing as much as before, only with 6 percent fewer workers. To be sure, robotics are not the only job killers out there, with outsourcing stealing far more gigs than automation.
Jeff Burnstein, president of the Robotics Industry Association, a trade group in Ann Arbor, Mich., argues that robots actually save U.S. jobs. His logic: companies that embrace automation might use fewer workers, but that’s still better than firing everyone and moving the work overseas.
It’s not that robots are cheaper than humans, though often they are. It’s that they are better. “In some cases the quality requirements are so stringent that even if you wanted to have a human do the job, you couldn’t,” Burnstein says. He cites General Motors, which uses robots to lay a bead of sealant on windshields, because humans can’t do the job as precisely.
Same goes for surgeons, who are using robotic systems to perform an ever-growing list of operations—not because the machines save money but because, thanks to the greater precision of robots, the patients recover in less time and have fewer complications, says Dr. Myriam Curet, chief medical adviser at Intuitive Surgical in Sunnyvale, Calif. The surgery bots don’t replace surgeons—you still need a surgeon to drive the robot. And they’re not cheap. Prices go as high as $2.2 million. Nevertheless, Intuitive sold 400 of them just last year. If you’ve had a prostatectomy recently, chances are a robot was involved.

Surgeons may survive the robot invasion, but others at the hospital might not be so lucky, as iRobot, maker of the Roomba, a robot vacuum cleaner, has been showing off Ava, a three-foot-tall droid on wheels that carries a tablet computer. iRobot reckons Ava could be used as a courier in a hospital. And once you’re home, recovering, Ava could let you talk to your doctor, so there’s no need to send someone to your house. That “mobile telepresence” could be useful at the office. If you’re away on a trip, you can still attend a meeting. Just connect via videoconferencing software, so your face appears on Ava’s screen.

Is any job safe? I was hoping to say “journalist,” but researchers are already developing algorithms that can gather facts and write a news story. Which means that a few years from now, a robot could be writing this column. And who will read it? Well, there might be a lot of us hanging around with lots of free time on our hands.

SOURCE: Newsweek 


















Picha zote hizo kwa hisani ya gazeti la Daily Mail zilidakwa na kamera dakika ambapo waogeleaji (pichani) walipokuwa wanajirusha kutoka jukwaani.Ashakum si matusi,hutolaumiwa ukidhani baadhi yao wanajikakamua msalani kushusha "kubwa".

Appeal for Support How to Register


Moja ya matatizo mengi yanayomkabili mtu tuliyemchagua kuwa Rais wetu,Jakaya Kikwete,ni kutokuwa serious.Yeye ni mwepesi wa kuchekacheka hata kwenye mambo yanayohitaji kuwa serious.Anyway,kwanini nimesema hatuna rais?Sio siri,nimepatwa na kichwa kuuma baada ya kusoma mahojiano yafuatayo kati ya Kikwete na mwandishi wa BBC.Angalia majibu yake,angalia vicheko vyake...na kwa hakika unaweza kuafikiana nami kuwa huyu mtu sio tu mbabaishaji bali yawezekana hajui kwanini ni Rais wetu.Anyway,soma mwenyewe

BBC: Suala la Umeme Mheshimiwa Rais Kikwete ungependa kulizungumzia nini?

Rais Kikwete: Tatizo la umeme kimsingi ni suala la ukame tu. Kwa sababu mabwawa yetu ya kuzalisha umeme yanayotoa umeme karibu MW600 sasa hivi yanatoa umeme kidogo sana. Maji pungufu ndio maana kuna tatizo hilo.

BBC:Mheshimiwa, hili suala si la leo wala si la jana limekuwepo kwa muda mrefu, kwanini serikali haina njia mbadala ya kuweza kutatua suala hili? Tanzania ina raslimali nyingi mheshimiwa Kikwete!

Rais Kikwete: Kwanza serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe, unajua unajua hivyo, Kwa sababu (kicheko) ingekuwa na uwezo wa kufanya mvua inyeshe mabwawa yale yangejaa. Ni kweli kuwa Tanzania inazo raslimali za kutosha na katika kipindi hiki - toka wakati ule - sisi tulipoingia tumekuta suala la Ukame na mwaka 2007 tukapata matatizo ya kwanza.

Baada ya pale tukafanya uamuzi kwamba sasa tuanze kuwekeza katika vyanzo vingine; tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vyanzo vingine. Tuongeze uzalishaji wa umeme kutoka vya vya kutumia gesi asilia twende kwenye makaa ya mawe. Kutoka vyanzo vya gesi asilia tayari tuna mtambo pale Ubungo, na toka mwaka 2009 mpaka sasa tumeshaongeza MW145, itakapofika Disemba tutakuwa tumeongeza MW160 nyingine. Tutakuwa tumeongeza MW300 siyo kidogo.

BBC: Mhe. Kikwete Mmoja katika wabunge Bw. John Mnyika ambaye ni Mbunge wa upinzani ambaye ni Waziri Kivuli wa Nishati amekuwa akilalamika na kwamba amewahi kusema kwamba hili tatizo ni tatizo linalowahusu Watanzania wote na amesema mje pamoja na kuona vipi mtakavyotatua tatizo hili. Na sasa hivi Bungeni wamesimamisha mswada, wa kutoa bajeti ya nishati ya Tanzania. Wewe unachukulia vipi matamshi kama haya kutoka kwa Wabunge?

Rais Kikwete: Mimi nasema hivi yeye si Mbunge atoe maarifa yake tu; anayo maarifa gani na anapendekeza kitu gani. Kwa sababu toka Uhuru mabwawa tuliyotengeneza ni Kidatu MW200, Mtera MW80, Kihansi MW 165 mimi nilipokuwa Waziri wa Nishati, pale Pangani tumeongeza.

Sasa ufikirie kwamba toka Uhuru tumeweza kuzalisha umeme wa MW600, lakini toka 2009 mpaka Disemba mwaka huu tutakuwa tumeongeza MW300! Ni jitihada kubwa. Mimi nasema kwamba usipozitambua hizo ni kwamba wewe mwenyewe siyo mkweli.

Sasa ni hivi, unajua hii mitambo ya umeme si mitambo unaenda kununua kama unavyonunua jaketi lako hili. Ni kwamba ukitaka mitambo ya umeme, lazima uweke order wakutengenezee. Huu mtambo unaofika mwaka huu Disemba order tuliweka mwezi wa Juni mwaka jana. Inachukua muda huo kutengeneza. Sasa ingekuwa mnaenda kutafuta mitumba, mitumba ya mitambo tu ya kununua iko mingi kweli. Tukasema hatuwezi kufanya hivyo.

Mimi nasema hivi, kitu kikubwa ni kuwa na subira. Tumefanya jitihada kubwa. Ni lazima watu watambue kuwa tumefanya jitihada kubwa katika miaka hii toka 2009 mpaka sasa hivi 2011 Disemba tutakuwa tumeongeza MW300 kulinganisha na MW600 ambazo tumeziongeza katika miaka yote hii. Nasema ni lazima watu watambue hivi. Sasa kama kuna mtu ana maarifa ya haraka zaidi nasema mtu atoe maarifa hayo na sisi kama yapo tutayafanyia kazi.

BBC: Kuna njia kama umeme wa jua, umeme wa kutokea ardhini wa mvuke, kwanini serikali haitafuti njia mbadala kuzalisha umeme kwa njia hizo?

Rais Kikwete: Nasema hivi, hata umeme wa jua lazima ujenge, umeme wa mvuke lazima ujenge, si kitu cha mwezi mmoja. Nasema huo ndio ukweli wenyewe na wakati mwingine na nyinyi mjifunze hayo mambo ya kitaalamu kulikoni kuuliza tu hivi hivi. Unajua ungekuwa na wewe unauliza kwa hoja - “unajua kwamba hiki kitu hiki ingekuwa umeme wa jua miezi miwili tu upo” - tungeweza kufanya hivyo.

Sisi sasa hivi kwa mfano tunajiandaa kuzalisha umeme wa kutumia Upepo, pale Singida. Tuna mwaka wa tatu sasa tuna mipango na Wakorea wa Kusini, umeme haujakuwepo. Kwa hiyo nasema hayo ni maelezo rahisi. Wanasema “mbona jua lipo?” katengeneze umeme wa jua kama jua lipo! (kicheko).

BBC: Watanzania wamekuwa wakisema (mwisho kabisa) kwamba Tanesco ingebinafsishwa ili waweze kupata makampuni kufanya kazi hiyo ya umeme?

Rais Kikwete: Aah! Kwani ukitaifisha kesho ndio utapata mitambo kesho? Nasema hivi ni vizuri kuelewa tu - kwanza tatizo la msingi - ni maji kukauka kwenye mabwawa. Maji yasingekauka kwenye mabwawa tatizo hili halipo. Maji yamekauka kwenye mabwawa kwa sababu ya ukame. Hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuia ukame usiwepo. Sasa hiki ndicho kiini cha tatizo. Sasa nasema sisi jitihada ambayo tumeifanya ni kupunguza sasa kutegemea umeme unaotakana na nguvu ya maji.

Toka mwaka 2009 tumewekeza adi Disemba 2011 tutakuwa tumeongeza MW 310, yenyewe hiyo ni hitihada kubwa, ni vizuri ukaitambua jitihada hiyo. Kulikoni kusema kitu tu nasema hata kama huna majawabu rahisi utuambie tu.

MSIKILIZE HAPA


Usanii wa Wachina katika kufoji umekwenda hatua ya juu zaidi baada ya bloga mmoja kugundua maduka makubwa (malls) matatu ya bidhaa za kampuni ya Apple (inayotengeneza iPhone,iPads,nk).Kichekesho ni kwamba maduka hayo ni feki kwa vile hayana kibali cha kampuni ya Apple.Lakini to make matter even worse,biahdaa zote za Apple zinazouzwa kwenye maduka hayo nazo ni feki pia.Kama hiyo haitoshi,hata wafanyakazi wa maduka hayo nao "waliingizwa mjini" kwani siku zote walikuwa wanaamini kuwa wao ni waajiriwa wa Apple ya Marekani.

Halafu hawa ndio watu tunaowaamini kama mapatna wetu wa maendeleo katika jitihada zetu za kujiweka mbali na "Wazungu"!! Angalia picha hizi na video








Mwanamama mmoja na mumewe huko Aberdeen,Scotland walikumbwa na kiwewe baada ya kukumbana na bonge la dude kwenye ufukwe wa Bahari ya Kaskazini.Well,dude hilo halikuwa hai bali kiufasaha ni masalia ya "sea monster" (sijaui tafsiri yake kwa Kiswahili ni ipi)?Pata picha ndio ungekuwa wewe peke yako...Hadi sasa haijafahamiaka masalia hayo ni ya kiumbe gani wa baharini lakini wataalam wanabashiri kuwa inawezekana ni ya papa muuaji (killer whale) au papa rubani (pilot whale)

Papa muuaji  

Papa rubani

20 Jul 2011



Majaribio yameanza ya kinga inayotokana na mimea kutumika kama kinga dhidi ya virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga ya mwili (UKIMWI).Kinga hiyo inatengenezwa kwa kutumia majani ya tumbaku iliyozalishwa maabara,ikitarajiwa kuwa ufanisi wake utapunguza gharama ya dawa za kurefusha maisha ya waathirika wa ugonjwa huo,na kwa muda mrefu kupata tiba ya kudumu ya ugonjwa huo.

Vidonge vilivyotengenzwa kutokana na mimea vinafanyiwa majaribio kwa kundi la wanawake hapa Uingereza,hasa kuangalia ufanisi wake.Watengenezaji wa vidonge hivyo wanategemea vitasaidia kupatikana kwa kinga dhidi ya maambukizo ya virusi vinavyosababisha ukimwi lakini mafanikio makubwa yanatarajiwa kwenye ukweli kwamba molekyuli zinazotarajiwa kuwa na ufanisi ni nafuu zaidi kwa minajili ya gharama.

Majaribio hayo katika miili ya binadamu yameidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Madawa na Huduma za Afya ya hapa Uingereza,na inafanyika huko Guildford katika taasisi ya utafiti wa afya ya Chuo Kikuu cha Surrey.

"Pharma-Plant" ni mradi ulioanzishwa miaka saba iliyopita ukiwa na lengo la kutumia mimea iliyozalishwa maabara kupunguza gharama ya uzalishaji wa vidonge kwa ajili ya tiba mbalimbali.Wanasayansi wanadhamiria kutengenza madawa yenye ufanisi lakini kwa gharama nafuu,na kuzisaidia nchi masikini duniani.

Habari hii imetafsiriwa kutoka katika gazeti la Guardian.Kwa habari kamili soma HAPA

19 Jul 2011


Rais Kikwete kutembelea Afrika Kusini 
Monday, 18 July 2011 21:28

Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete, jana alianza ziara ya kihistoria ya kidola nchini Afrika Kusini, ikiwa ni ziara ya kwanza ya aina yake, kufanywa na Rais wa Tanzania katika nchi hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Rais Kikwete anafanya ziara hiyo kwa mwaliko wa Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye utawala wake umekuwa uhusiano wa karibu na Tanzania, tangu aliposhika madaraka ya kuongoza taifa hilo kubwa kiuchumi kuliko mengine, katika Afrika.

Rais Kikwete na ujumbe wake unaojumshia pia mkewe, Mama Salma Kikwete, uliondoka nchini jana mchana kwenda Pretoria, kwa ziara hiyo ya siku nne.Pamoja na kwamba marais wa Tanzania waliomtangulia Rais Kikwete wametembelea Afrika Kusini mara nyingi kwa shughuli mbalimbali, lakini hakuna kiongozi aliyepata kualikwa kufanya ziara rasmi, ya kiserikali ama ya Kidola, tangu nchi hiyo ilipoingia katika mfumo wa demokrasia mwaka 1994.

Kwa mujibu wa ratiba ya ziara hiyo, Rais Kikwete na ujumbe wake, watapokelewa rasmi leo asubuhi katika Jumba la Serikali, mjini Pretoria.Tayari Rais Zuma na mkewe walikwishajipanga kwa sherehe za makaribisho zitakazofuatiwa na mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati ya Tanzania na Afrika Kusini.

Mazungumzo hayo, yatafuatiwa na utiaji saini wa mikataba na makubaliano katika nyanja mbalimbali kati ya nchi hizo mbili.Baadaye, viongozi hao wawili watahutubia mkutano wa waandishi wa habari na baada ya hapo, Rais Kikwete atatembelea Uwanja wa Uhuru akiandamana na Rais Zuma.

Mchana viongozi hao watahudhuria chakula cha mchana kikiwashirikisha pia wafanyabiashara wa Tanzania na Afrika Kusini ambao watazungumza na kuelezea umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.Jioni, Rais Zuma ataandaa dhifa ya kitaifa kwa ajili ya Rais Kikwete na ujumbe wake .

Keshokutwa, Rais Kikwete na ujumbe wake watakwenda Cape Town, ambako miongoni mwa mambo mengine ujumbe huo utatembelea Kisiwa cha Robben ambako wapigania uhuru maarufu wa Afrika Kusini, akiwamo Rais Mstaafu Nelson Mandela, walifungwa kwa miaka mingi na makaburu. Rais Kikwete atarejea nyumbani keshokutwa asubuhi.

CHANZO: Mwananchi 

LABDA AKIREJEA KUZURURA TATIZO LA UMEME LITAKUWA LIMEPATA UFUMBUZI. 




Kama kuna kosa ambalo Watanzania watalijutia kwa muda mrefu sana ni lile walilofanya mwaka 2005 na kisha kulirudia mwaka jana kumchagua Jakaya Kikwete kuwa Rais wa nne wa Tanzania.Tusiume maneno,mengi ya matatizo yanayoikabili nchi yetu kwa sasa ymesababisha,yanasababishwa au yamechangiwa au yanachangiwa na ubabaishaji wa Kikwete.

Ni nani mwenye akili timamu asiyefahamu kuwa wakati kelele dhidi ya ufisadi zinaelekezwa kwa "mapacha watatu" waliobaki wawili (ie Lowassa na Chenge,na Ristam aliyejiuzulu),Kikwete ni sehemu muhimu kabisa ya tuhuma zinazoelekezwa kwa wanasiasa hao.Hapa simaanishi kuwatetea mafisadi hao bali ninachojaribu kupigia mstari ni ukweli kwamba Kikwete hana tofauti na Lowassa,Chenge au Rostam.Na hilo halihitaji ufafanuzi.Yeye anajua,mapacha watuatu waliobaki wawili wanajua,na kila Mtanzania mwenye akili tiammu anajua.Kwanini hadi leo Kikwete bado ni Rais wetu ni swali gumu kulijibu just like lile la kwanini alichaguliwa mara ya kwanza mwaka 2005 na baadaye 2010 ilhali wanamjua walikuwa wanatambua bayana kuwa hana sifa za kushika wadhifa huo mkubwa kabisa katika nchi yetu.

Anyway,lengo la makala hii sio kujadili ubabaishaji wa Kikwete katika utendaji kazi wake bali lengo ni kukemea kwa nguvu kubwa uhuni uliofanywa na Kikwete wa kufanya harusi ya mdogo wake kwenye Ikulu ndogo ya Bagamoyo.Hivi kwa kuwa Rais,Kikwete anadhani kuwa Watanzania wametoa urais kwa ukoo wake mzima?Kwanini asikodi ukumbi kwa fedha zake kisha akamfanyia sherehe mdogo wake?

Kama huelewi kwanini ninalamika,Ikulu iwe ile ya Magogoni au hizo ndogo za wilayani na mikoani ni mahala patakatifu-kama alivyowahi kusema Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.Si mahala ambapo kila Tom,Harry and Dick anaweza kufanya atakalo.Lakini licha ya utakatifu huo wa Ikulu,ifahamike kuwa mahala hapo panaendeshwa kwa fedha za walipakodi.Kwa mantiki hiyo,kufanyia sherehe mahala hapo ni sawa na kuwabebesha gharama Watanzania kwa ajili ya harusi ya ndugu wa Kikwete.Sidhani hata waliompigia kura mwaka jana au 2005 walitamani kuona kura waliyompigia Jakaya inageuzwa kuwa mithili ya kuupigia kura ukoo wake mzima.

Huu ni uhuni unaopaswa kukemewa vikali.Rais anaweza kuzurura nje ya nchi atakavyo (inaelekea kama hakuna namna ya kumwelewesha kuwa safari zake za mara kwa mara nje ya nchi ni mzigo mkubwa kwa Watanzania) lakini kamwe tusiruhusu nafasi ya Urais ikageuzwa kuwa kama cheo cha kifamilia.

Madhara ya kumwacha Kikwete aendelee na madudu yake ni kwamba anaweza kumaliza muda wake hapo 2015 na kuiacha Tanzania ikiwa jina tu-haina maadili,haina raslimali,na kibaya zaidi,nafasi ya urais ikaishia kuwa na heshima ndogo kuliko ya mwenyekiti wa serikali ya mtaa.

PICHA: Kwa hisani ya Global Publishers

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.