4 Aug 2011


Tanzania yetu sijui inaelekea wapi!Yaani ufisadi unasambaa kila kona.Wengi mnakumbuka usanii waliofanya kampuni ya utafiti ya Synovate wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.Kwa kifupi,waliamua kuweka kando professionalism na hadhi ya kampuni yao ili wawaridhishe watu wa CCM.Nilikerwa sana na uhuni wao hadi nikafikia hatua ya kumwandikia bosi wao.Kama ilivyo kawaida ya wababaishaji,aliruka kimanga na kudai hawapendelei chama chochote.

Sasa leo nimekumbana na habari iliyonikera kupita maelezo.Eti kampuni hiyo imefanya utafiti wa kura ya maoni kuhusu nafasi ya urais.Hadi hapo hakuna tatizo kwani tunashuhudia takriban kila wiki taasisi za kura za maoni kama Gallup zikiendesha kura za maoni kupima utendaji kazi wa Rais Obama,Congress,nk.Tatizo la kura ya maoni ya Synovate lipo kwenye ukweli kwamba wamekwepa kumweka Rais Jakaya Kikwete kwenye opinion poll hiyo,na badala yake wameweka wanasiasa wengine,ambapo Dkt Willibroad Slaa ameibuka kidedea.

Synovate wamefanya makusudi kukwepa kupima utendaji kazi wa Kikwete.Wangeweza kabisa kuangalia approval rating yake pasipo kumpambanisha na Dkt Slaa.Lakini wamekwepa kwa vile wanajua bayana kuwa  wengi wa Watanzania wenye akili timamu wamechoshwa na ubabaishaji wa rais wao.

Lakini hata kama Synovate wameamua kuendelea kujipendekeza kwa Kikwete na CCM,hiyo haitoondoa ukweli kuwa wengi wa Watanzania wamemchoka Kikwete,na kwa hakika wanasubiri kwa hamu afungashe virago vyake hapo 2015 (huku kukiwa na hofu kuwa by then nchi itakuwa imeharibika beyond repair).

Sidhani kama Synovate wangeamua kuchapisha approval rating ya Kikwete wangelazimishwa kuondoka Tanzania.Lakini naamini kabisa kuwa kampuni hii inafahamu fika kuwa kuficha kukubalika/kuchukiwa kwa Kikwete hakumsaidii kiongozi huyo dhaifu.Ni sawa na mgonjwa wa ukimwi kufichwa matokeo ya vipimo vya damu yake.Kamwe virusi vya ugonjwa huo havitoondoka mwilini kwa vile tu mwathirika hajajulishwa.

Anyway,habari husia ni hii hapa chini
Dk Slaa ang’ara urais 
Wednesday, 03 August 2011 23:11
0
digg

NI IWAPO UCHAGUZI MKUU UNGEFANYIKA SASA ANGESHINDA.

Leon Bahati
MATOKEO ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya Synovate yanaonyesha kwamba iwapo Rais Jakaya Kikwete angeamua kujiweka kando na ukaitishwa Uchaguzi Mkuu sasa, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa angeibuka mshindi wa nafasi hiyo.Ripoti ya Synovate iliyotolewa jijini Dar es Salaam jana ambayo inawapa wapinzani fursa ya ushindi kwa mara ya kwanza, wagombea kutoka vyama vya upinzani wana uwezo wa kupata asilimia 67 iwapo uchaguzi ungefanyika sasa.

Dk Slaa anaongoza kwa kupata asilimia 42, akifuatiwa na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (asilimia 14), Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (asilimia 12) na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe asilimia tisa.

Synovate inaeleza kwenye ripoti hiyo kwamba matokeo ya utafiti huo yanatokana na watu mbalimbali wenye umri zaidi ya kuanzia miaka 18 walioulizwa maswali ya ana kwa ana vijijini na mijini.

Katika kupata maoni juu ya mtu ambaye wangependa awe rais waliuliza: “Mbali na Rais Jakaya Kiwete, ni mtu gani ungeweza kumchagua kuwa Rais iwapo atakuwa miongoni mwa wagombea?”
Kwa mujibu wa matokeo hayo, iwapo uchaguzi ungefanyika sasa, Pinda angeambulia nafasi ya tatu licha ya kwamba CCM ndicho chama kinachoongoza kwa kuaminika mbele ya umma ikilinganishwa na vyama vingine vya siasa.Katika utafiti wake huo uliofanywa kati ya Mei 2 hadi 29, mwaka huu, jumla ya watu 1,994 walihojiwa.

CCM wamtaka Dk Slaa
Utafiti huo unaonyesha kuwa wanachama wengi wa CCM walionyesha kuvutiwa na Dk Slaa ikilinganishwa na viongozi wengine ndani ya chama hicho tawala.Hii inatokana na takwimu kuonyesha kuwa kati ya waliohojiwa katika utafiti huo, wengi wanatokana na CCM, lakini wakamchagua Dk Slaa.

Takwimu za ripoti hiyo zinaonyesha kuwa kati ya waliohojiwa, walipoulizwa kuhusu vyama vyao asilimia 51 walisema ni CCM, asilimia 35 wakasema Chadema, 10, CUF na TLP asilimia moja.

Mbali na Dk Slaa, Profesa Lipumba, Pinda na Zitto wanasiasa wengine wanne wanaofuatia ambao asilimia walizopata zimo kwenye mabano ni Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli (4), Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (2) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (2).

Kadhalika, vigogo tisa waliofungana kwa kupata asilimia moja ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo ni Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal, Spika wa Bunge, Anne Makinda, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe na Waziri wa Maji, Profesa Mark Mwandosya.

Katika utafiti huo, Synovate iliegemea nyanja tatu za utafiti ambazo ni siasa, uchumi na masuala ya kijamii na utamaduni.

Mgombea urais CCM 2015
Ndani ya CCM, anayepewa nafasi ya kwanza kuwa mgombea urais kwa mwaka 2015 ni Pinda aliyepata asilimia 35 akifuatiwa na Dk Magufuli asilimia 14.

Wanaofuatia kwa mvuto pamoja na asilimia walizopata kwenye mabano ni Membe (8), Sitta (3), Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye (3), Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa (3) na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi (2).

Vigogo tisa ndani ya CCM walifungana kwa kupata asilimia moja nao ni Makinda, Dk Mwakyembe, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Magembe na Waziri Mkuu wa zamani, Dk Salim Ahmed Salim.
Wengine ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk Asha-Rose Migiro, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba.

Uvuaji gamba CCM
Utafiti huo wa Synovate unaonyesha kuwa Watanzania wengi wanatofautiana juu ya uelewa wa mpango wa CCM wa kujivua gamba.

Katika mpango huo ripoti hiyo inasema asilimia 41 walisema ni mpango wa kuwataka watu kujiuzulu kwenye uongozi wakati asilimia 29 walisema ni mpango wa kutaka kukisafisha chama.

Inaonyesha kuwa asilimia 15 ya waliohojiwa walielezea kujivua gamba kuwa ni mabadiliko ya uongozi kwa kuondoa viongozi wabovu na asilimia tano wakasema ni mpango wa kuondoa viongozi wote watuhumiwa wa ufisadi.

Asilimia mbili walisema ni mpango wa kukifanya chama hicho cha siasa kiwe na mfumo wa wazi na unaoeleweka wakati asilimia moja walisema ni suala la kujizuzulu, kutafuta viongozi wachapakazi na wenye tija. Kuna wanaouchukulia kuwa ni mkakati wa kisanii wa kuwadanganya wananchi.

Kwa ujumla, taarifa hiyo ilisema ni asilimia 45 tu ambao wana taarifa kuwa kuna Sekretarieti ya CCM ilijiuzulu na Mwenyekiti wake, Rais Kikwete amekwishateua wengine kushika nafasi hizo.

Kero kubwa nchini
Asilimia 56 walisema tatizo kubwa linalowakumba ni kupanda kwa bei ya vyakula, gharama za maisha na umaskini na asilimia 46 walisema njaa na tatizo kwenye kilimo.Tatizo la ufisadi nchini lilichukua nafasi ya tatu kwa kupata asilimia 36, ukosefu wa ajira (31), tatizo la nyumba, barabara na umeme (27), elimu (23), afya (21), maji (16), uharibifu wa mazingira (12), taasisi za siasa (10), haki za binadamu, uhalifu (6) ubeberu na usafirishaji wa dawa za kulevya (3).

Katiba Mpya
Miongoni mwa mambo ambayo yanatajwa kuwa ni vikwazo kwa Tanzania kupata Katiba Mpya ni rushwa (26), kukosekana kwa umoja (19), maslahi ya kisiasa (18), ufahamu mdogo (11) na kukosekana kwa msukumo wa kisiasa (9).

Hata hivyo, asilimia 78 walisema wanataka yawepo mabadiliko ya katiba nchini wakati asilimia 21 hawaoni umuhimu wake.Lakini asilimia 42 walisema wana uhakika kwamba mpango wa Katiba Mpya utafanikiwa.
Lakini pia makosa ya Katiba iliyopo yalielezwa kuwa ni kupitwa na wakati, kuandikwa kwa Kiingereza zaidi kuliko Kiswahili, kukosekana kwa utawala bora, kutokuwepo kwa sheria za haki za binadamu na uhuru wa vyombo vya habari.

CHANZO: Mwananchi

3 Aug 2011

Chuwit kama kuwadi kubwa lao (master pimp)

Wanaposema siasa ni mchezo mchafu hawaongopi: Bango la  Chuwit wakati wa kampeni za uchaguzi

Pengine ushasikia msemo wa Kiingereza usemao "in the long run it is experience that counts." Kwa tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili ni kwamba uzoefu unalipa.Kadhalika,naamini utakuwa umeshasikia matukio ambapo mwizi mstaafu anatumika kukamata wezi waliopo.Hii ni moja ya mbinu muhimu sana kwa polisi na watumishi wengine wa taasisi za usalama.

Lakini ishu hii imechukua sura mpya huko Thailand baada ya tajiri mstaafu wa biashara za umalaya,Chuwit Kamolvisit,kujiingiza kwenye siasa na hatimaye kufanikiwa kuwa mbunge.Mbunge huyo ambaye anadai angependa zaidi kuitwa kuwadi (pimp)kuliko mwanasiasa ameingia kwa kasi ya kipekee kwenye siasa akidhamiria kupambana na tatizo la rushwa katika nchi hiyo inayosifika kwa utalii wa ngono (sex tourism).

Chuwit alikuwa tajiri anayemiliki massage parlour (sijui neno la Kiswahili ni lipi) na vyombo kadhaa vya habari vinamtaja kama kuwadi kubwa lao (super pimp) mstaafu.Anadai kuwa ili kumudu biashara chafu kama yake ilimlazimu kuwahonga polisi mara kwa mara kwa minajili ya kukwepa mkono mrefu wa sheria (si mrefu kihivyo,anyway).Sasa baada ya kuingia kwenye siasa anataka kutumia uzoefu huo wa kukwepa sheria kwa kutumia rushwa kupambana na rushwa.

Awali,mwanasiasa huyo alichapisha kitabu alichokipa jina lenye utata la Dogstyle Politics (yaani,ashakum si matusi,"Siasa za Chuma Mboga".Katika kitabu hicho,Chuwit anatoa mwanga kuhusu mwenendo wa siasa za nchi hiyo kulingana na uzoefu alioupta wakati wa uchaguzi,Anazilinganisha tabia za wanasiasa na mbwa.Lakini anadai baadhi ya vyama vya siasa vinapaswa kufananishwa na nyoka mwenye sumu kali Cobra,kwani havina itikali wala msimamo na ni hatari zaidi ya mbwa.Katika kitabu hicho,mwanasiasa huyo mwenye vituko ameandika shairi lisemalo, "Kuna tofauti gani kati ya binadamu na mbwa?Hawezi kuongea-mbwa hadanganyi,na mapenzi ya kweli ya mbwa ni kwa mmiliki wake"

Binafsi nadhani watu kama Chuwit wanahitajika sana katika Tanzania yetu iliyogubikwa na ufisadi.Hebu pata picha mtu kama Rostam Aziz aamue kwa dhati kuanzisha vita dhidi ya mafisadi.Kwa mfano aanze na namna mtandao uliomwingiza madarakani Rais Jakaya Kikwete ulivyoundwa,fitna walizofanya kusafisha njia ya Ikulu,madili kama ya EPA,Richmond na Dowans yalivyofanikishwa na michezo mingine michafu inayoipa uhai CCM na serikali yake!

Au chukulia mfano Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge aamue "liwalo na liwe" na kumwaga "chenga hadharani" kwa kuufahamisha umma jinsi mikataba ya kijambazi inavyofanikishwa na kurutubisha ufisadi.Au pengine Edward Lowassa baada ya kuona "anazinguliwa" aamue kuwa "bora tufe wote" na kuweka hadharani kila baya analojua linalosababisha Tanzania kuendelea kuwa kichaka cha ufisadi huku maisha ya Mtanzania wa kawaida yakizidi kuwa duni tofauti na danganya toto za Kikwete za "maishabora kwa kila Mtanzania (nadhani alimaanisha 'kwa kila fisadi')

1 Aug 2011


Show ya "Growing Up African" inayo onesha familia kutoka Tanzania na maisha yao Marekani imeanza kutoa video online. Kutoka mwezi wa tatu hadi saa hivi show ilikua inayonekana East Africa TV. Kwenye mwezi huu wa August kila Episode ya Season ya Kwanza itakua kwenye website yao. Kwenye hizi episodes utakutana na ndugu wote kwenye familia kutoka kwa Bea, Eliza, Jesca, Johnson hadi Andrew ambapo huwa maisha yao ni tufauti kwa kila mtu. Episode zitakuwa na familia nzima ambao utaona hile "family dynamic" ya ndungu. Hii show kwanza, niyasisi Watanzania na tunabidi tuwasikie mnavyosema kabla ya kuwa kwenye International Spotlight na kuja na Season ya pili September. Watu hizo episode wanaweza kwenda kwenye youtube.com, au kwenye website www.growingupafrican.com kuona hayo mambo. Website saa hivi hiko tayari na yenyewe ina mambo mengi kama mawazo ya familia kwenye issues kama musiki, fashion, urembo, na vinginevyo vingi kwenye blog zao.

Asanteni Sana, na ninaomba ushauri na mawazo kutoka kwenu kama watanzania wenzetu.

"Growing Up African" since it's inception through our supportive blogs in October 2010 has grown to become a household name in the East African Community. Currently the show is available only on East Africa TV that broadcasts to Uganda, Burundi, Kenya, Rwanda and lastly Tanzania. It is our deep honor to present the first Season of the show to those viewers outside the viewing area of these five countries. We have received numerous requests through mail and phone calls to let people from abroad into this well formed hype machine. In it's first Season, we did experience several setbacks but like any successful business development comes with time. The show is now available on our website at WWW.GROWINGUPAFRICAN.com and Youtube Channel at 

As we prepare to launch the Second Season in September on East Africa Television, we would like to give an opportunity to everyone to catch up on the show.










Qatar-based broadcaster has struck a deal with US network Time Warner Cable, taking it to around 2m homes in the region

The English-language arm of Arabic news channel Al Jazeera has launched on a US cable network in New York.

At midnight last night, Al Jazeera English (AJE) began broadcasting on US network Time Warner Cable, taking it to around 2 million homes in the region.

Six months on from the eruption of widespread protest across the Middle East, the agreement follows the most high-profile period in the history of the Qatar-based news channel.

In the immediate aftermath of the uprisings, some US media commentators – including Jeff Jarvis – called for US cable networks to add Al Jazeera, claiming that it was "downright un-American not to". AJE was at that point only available online to viewers in the US.

AJE's Arabic sister channel has been viewed with suspicion by the US, and was criticised by George Bush during his presidency after airing video messages from Osama Bin Laden. Its newsrooms were also bombed by the US in both Afghanistan and Iraq, although US authorities claimed the strikes were mistakes.

AJE, on the other hand, won praise from the US administration for its coverage of the uprisings in the Arab world, with secretary of state Hilary Clinton saying that the channel was airing "real news".

"Viewership of Al Jazeera is going up in the United States because it's real news. You may not agree with it, but you feel like you're getting real news around the clock instead of a million commercials and arguments between talking heads and the kind of stuff that we do on our news, which is not particularly informative to us, let alone foreigners."

Al Anstey, managing director of AJE, told the New York Times that early meetings with US networks had been about trying to correct "myths and misconceptions" about the AJE, but that now they don't come up.

Anstey added that the channel, which receives some funding from the Qatari finance ministry, will not be seeking the per-subscriber fee common to most US cable channels. "Revenue is not our priority," he said. "It’s being seen."

SOURCE:Journalism.co.uk


Familia yenye furaha: Kushoto ni Baba mtoto Jordan (15),akifuatiwa na  mama mtoto Tia (14) na kichanga  Gracie,na nyuma ni babu kijana  Shem (29) na kulia ni bibi kijana  Kelly (30)

Kwa namna ilivyozoeleka,unaposikia "babu" au "bibi" unadhani pasi wasi kuwa mtajwa ni aliyekula chumvi nyingi,na huenda umri wake upo kwenye miaka ya 50 na kuendelea.Na sia ajbu ana mvi lukuki.

Hali si hivyo kwa Shem Davies,kijana mwenye umri wa miaka 29 ambaye wiki hii amekuwa "Babu Kijana Zaidi nchini Uingereza."Davies,ambaye hana kazi (unemployed),amefanikiwa kupata mjukuu baada ya bintiye wa kike aitwaye Tia (umri miaka 14!!) kujifungua mtoto aitwaye Gracie.
Baba na mwana:  Shem na mwanaye Tia na kijukuu Gracie

Kuzaliwa kwa Tia (miaka 14 iliyopita) ni matokeo ya uhusiano wa kimapenzi kati ya Shem na mwandani wake wa zamani aitwaye Kelly John mwenye umri wa miaka 30 sasa.

Kuchanganya madawa zaidi,kijana aliyezaa na Tia (mama mtoto mwenye miaka 14) naye ni serengeri boy wa miaka 15 tu!Kwa jina anaitwa Jordan Williams (pichani chini akiwa na mzazi mwenzie na kichanga chao)

Kwahiyo mjukuu amepatikana kwa mama mwenye miaka 14 na baba mwenye miaka 15,na ana babu wa miaka 29 na bibi wa miaka 30!

Lakini ukiangalia kwenye picha zinazoambatana na habari hii itakuwia vigumu kutambua umri wa wahusika wa Isidingo hii.Tatizo ni kwamba ni vigumu sana kukadiria umri wa hawa "wazungu."

Uingereza ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa mabinti wanaojifungua kabla ya kutimiza miaka 18.

CHANZO: Daily Mail


Rushwa Inavyoua Elimu ya Watoto Wetu

CHANZO: Haki Elimu


MAPENDEKEZO YA MASHIRIKA YA KIRAIA JUU YA MUSWADA WA SHERIA YA MAPITIO YA KATIBA, 2011.

The Biggest Spending Tanzanian Embassies 

- Budget 2011/12

A Rapid Analysis of the biggest spending Tanzanian Embassies - Budget 2011/12
Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation Budget 2011/12
  • UN Missions alone to spend 5,051,259,000/-
  • Missions in Europe and Moscow to spend 12,481,913,000/-
  • Embassies in four EA capitals allocated 3,746,956,000/- 
  • The Africa allocation is 10,945,095,000/-
  • Administration costs nearly half of ministerial vote
  • Salaries for London mission the highest (Pensionable posts & non-pensionable) at 868,142,918/- and Kigali the lowest at 80,201,559/-

Programme 20 - Diplomatic MissionsTshs
Permanent Mission to the UN - New York2,882,502,000
Permanent Mission to the UN - Geneva2,168,757,000
Embassy of Tanzania - Paris2,133,493,000
Embassy of Tanzania - London2,009,942,000
Embassy of Tanzania - Moscow1,907,166,000
Embassy of Tanzania - Rome1,891,547,000
Embassy of Tanzania - Berlin1,776,946,000
Embassy of Tanzania - Washington DC1,714,958,000
Embassy of Tanzania - Abu Dhabi1,710,597,000
Embassy of Tanzania - Tokyo1,662,626,000
Embassy of Tanzania - Nairobi1,625,277,000
Embassy of Tanzania - Brasilia1,532,748,000
Embassy of Tanzania - Brussels1,465,353,000
Embassy of Tanzania - Ottawa1,367,032,000
Embassy of Tanzania - Beijing1,352,422,000
Embassy of Tanzania - Stockholm1,297,466,000
Embassy of Tanzania - Pretoria1,269,178,000
Embassy of Tanzania - New Delhi1,215,144,000
Embassy of Tanzania - Kuala Lumpur1,160,872,000
Embassy of Tanzania - Riyadh1,156,879,000
Embassy of Tanzania - Addis Ababa892,277,000
Embassy of Tanzania - Maputo873,151,000
Embassy of Tanzania - Kampala822,513,000
Embassy of Tanzania - Kinshasa797,422,000
Embassy of Tanzania - Abuja778,726,000
Embassy of Tanzania - Muscat765,066,000
Embassy of Tanzania - Harare722,034,000
Embassy of Tanzania - Lusaka692,592,000
Embassy of Tanzania - Bujumbura659,258,000
Embassy of Tanzania - Kigali639,908,000
Embassy of Tanzania - Cairo595,191,000
Embassy of Tanzania - Lilongwe577,568,000
TOTAL Programme42,116,611,000
Administration Programme 1038,486,246,000
Total of Vote 34 80,602,857,000
Less Retention Scheme funds14,872,492,146
Net total of vote65,730,364,854
 


Idd Simba aitabiria kifo CCM

• AKERWA NA MALUMBANO NDANI YA BUNGE

na Waandishi wetu

MWANASIASA mkongwe nchini, Idd Simba, amekitabiria kifo Chama cha Mapinduzi (CCM) endapo hakitachukua hatua za haraka kudhibiti makundi yaliyo ndani yake ambayo mengi yanatokana na baadhi wanachama kuanza mapema mbio za kukimbilia Ikulu wakitaka urais.

Idd Simba, mwenyekiti wa baraza la wazee wa mkoa wa Dar es Salaam alisema hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kufungua semina ya maimamu na wanazuoni wa Kiislamu, iliyofanyika katika hoteli ya Starlight, Dar es Salaam.

Alisema makundi yaliyojengeka ndani ya CCM yamesababisha chama hicho kupoteza kuaminika na wananchi hali ambayo inahatarisha amani nchini.

Alisema kutokana na hali hiyo moja ya mkakati wa kwanza wa baraza la wazee wa mkoa wa Dar es Salaam ni kuhakikisha linadhibiti hali hiyo ili kuweka mazingira mazuri ndani ya CCM katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Pamoja na mambo mengine, aliwaonya wanachama wanaojiundia makundi ya mtandao kwa kuelekeza nguvu zao za kuelekea Ikulu badala ya kukisaidia chama kuwa imara mbele ya wananchi.

“Kupoteza mwelekeo kwa chama chetu kunatokana na makundi ya watu ambao wana nia ya kukimbilia Ikulu na hali hii sisi wazee wa mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na wenzetu nchi nzima tumejipanga kuthibiti hali hii.

“Kila anayesema hivi sasa anamtolea mfano Mwalimu Nyerere, sasa hayupo nani anayeendeleza na kukienzi chama kama ilivyokuwa wakati wake? Ili kuondokana na tabaka hili sisi wazee tunajipanga kukishauri chama kama kunatokea matatizo kama ilivyo sasa wazee tuweze kushauri kwa maslahi ya chama na wanachama kwa ujumla pamoja na kujenga misingi imara ya uzalendo na siasa zilizotukuka ndani na nje ya CCM,” alisema Simba ambaye amepata kuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu.

Alisema ili kujenga misingi imara lazima siasa ndani ya CCM, zijengwe na watu hasa kwa kuongozwa na itikadi kama aliivyokuwa ikisimamiwa na Mwalimu Nyerere na wasaidizi wake.

“Sisi wazee na wanachama wote wa CCM tusiposimama imara kuna hatari ya chama kupoteza mwekelekeo; sasa juhudi zinazofanywa za kurudisha misingi ya chama na mwenyekiti wa taifa, Rais Jakaya Kikwete, na sekretarieti tunahitaji kusimamia na kukomesha makundi yanayokitafuna chama ndani,” alisema Simba.

Hali ya kisiasa nchini

Akizungumzia mwenendo wa kisiasa alisema hivi sasa amani imekuwa ikivurugwa na vyama vya siasa kutokana na kila chama kutanguliza utashi na maslahi ya chma husika kuliko wananchi na taifa kwa ujumla.

Alisema malumbano yanayotokea mara kwa mara bungeni, siku moja yanaweza kuwaingiza wananchi barabarani kwa kuhisi wawakilishi waliowachagua hawana tija kwao.

“Haya yanayoendelea hivi sasa bungeni ni ya kusikitisha sana kwani hivi sasa muhimili muhimu wa Bunge unayumba na hata kukosa mwelekeo kutokana na baadhi ya wabunge kuona pale ni jukwaa la kisiasa.

“Huwezi ukawa na wabunge wenye kuonyesha ufundi wa kuzungumza na kila mara mwongozo wa Spika au taarifa wakati hivi sasa Watanzania wanahitaji kutatuliwa matatizo yao na watunga sheria hao,” alisema mwenyekiti huyo wa wazee wa mkoa wa Dar es Salaam.

Amani ya nchi

Kuhusu suala hilo, Simba ambaye alikuwa waziri katika utawala wa awamu ya tatu kisha baadaye kuwa mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi Taifa, alisema hivi sasa amani ya nchi iko shakani kutokana na kauli za viongozi wa vyama vya siasa wanazozitoa katika Bunge na mikutano yao ya kisiasa.

“Kila mbunge au kiongozi ametanguliza maslahi yake binafsi kwa kugombea vyeo vya uwakilishi na kulumbana kupitia Bunge kuliko watu waliomchagua huku akisahau lilolompeleka pale, kwa hatua hii kuna kila dalili za kuchafua amani yetu,” alisema Simba.

CCK yasikitishwa na Bunge

Katika hatua nyingine, Chama cha Kijamii (CCK), kimesema Bunge limepoteza heshima kutokana na wabunge kusimama kutetea maslahi ya vyama vyao na kusahau wananchi ambao walichagua serikali yao kukaa madarakani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa CCK, Renatus Muabhi, alisema kuwa kupoteza heshima kwa Bunge kumetokana na wabunge kuwakilisha vyama na kuacha wananchi wakiwa hawana imani na serikali yao katika kupata maisha bora.

Alilaani wabunge kutohudhuria kwa wingi bungeni hali inayosababisha wabunge wanaopitisha bajeti kuwa wachache hivyo kuwafanya wananchi wengi kukosa kuwakilishwa ipasavyo.

Dowuta yatoa tamko

Wakati huo huo, Chama cha Wafanyakazi wa Shughuli za Meli na Bandari (DOWUTA) kimesema Buge la sasa limekosa dira na kutokana na hali hiyo kuna haja ya kuwepo kwa chuo kinachofundisha uongozi kabla ya watu hao kuteuliwa katika nafasi za uongozi.

Akizungumza na Tanzania Daima, ofisini kwake mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu wa Dowuta, Abdallah Kibunda, alisema Bunge la sasa linatia aibu machoni mwa jamii hivyo kulifanya kukosa dira.

“Bunge la sasa ni la ghasia tu, wabunge wamejisahau kwani badala ya kujadili masuala ya maendeleo wanalumbana bila mpango wakati malumbano yalishaisha wakati wa kampeni
“Hao ni wawakilishi wa wananchi hivyo hawana budi kujirekebisha. Hata hivyo suala la uongozi linahitaji taaluma na kungekuwa na chuo ambacho moja ya sifa ni viongozi wakiwemo mawaziri, wabunge, wakuu wa mikoa na wengine kupitia huko kabla hawajateuliwa ingekuwa vizuri,” alisema Kibunda.

Alisema malumbano hayo hayawanufaishi wapigakura kwani asilimia kubwa ya wapigakura si wanachama wa CCM, CHADEMA, CUF wala TLP bali waliwapigia kura wabunge hao kutokana na kunadi sera zao kwao wakitegemea watapata maendeleo lakini kinyume chake wabunge hao wamekuwa wakilumbana siku hadi siku badala ya kupaza sauti zao bungeni kusaidia kuondoa kero za wananchi.

Alisema kwa hali hiyo wabunge hawana budi kurekebisha mara moja tabia hiyo kabla haijaleta athari zaidi.

Kwa mujibu wa katibu huyo, mkutano huo wa Bunge ni muhimu kwa sababu unajadili maendeleo ya taifa yakiwemo ya wafanyakazi katika kukuza uchumi wa taifa ili kukuza uchumi.

Alisema badala ya wabunge hao kujadili matatizo ya wafanyakazi kama vile mazingira mabovu ya kazi waliyonayo, kukatwa kodi na mengine badala yake kila mtu anafanya jambo analojisikia.

Alitoa rai kwa wabunge kufanya kazi kwa hekima, umakini na busara wawapo bungeni kwa maslai ya taifa.



يجوز للشهر الكريم من وحي القرآن الحاجب عليكم السلام والسعادة والازدهار

30 Jul 2011


Mitandao ya jamii ya Facebook na Twitter imetengeneza kizazi kinachoendekeza umimi kupita kiasi kiasi kwamba watu hawajali masuala mengine huku wakiwa na tamaa kama watoto wadogo kuona watu wanasema mazuri kuhusu wao,picha zao,wanayoandika kwenye mitandao hiyo,nk.

Kuendelea kuwepo kwenye mitandao hiyo kwa muda mrefu kunamwacha mtumiaji akiwa na mgogoro wa kujitambua (identity crisis),tamaa ya kutambulika katika namna ileile mtoto mdogo anamwambia mzazi wake, "Mama,nimefanya hivi."

Baroness Greenfield,profesa wa taaluma ya madawa (pharmacology) katika Chuo Kikuu cha Oxford,anaamini kuwa kukua kwa urafiki wa mtandaoni-sambamba na matumizi makubwa ya michezo ya kompyuta-vinaweza kupelekea kuuchanganya ubongo.

Hii inaweza kusababisha upungufu kwenye kukazani mambo ya muhimu,hitaji la kutamani kusifiwa na uwezo mdogo wa mawasiliano yasiyohitaji kutumia maneno (non-verbal communication) kwa mfano kumwangalia mtu usoni wakati wa maongezi.

Zaidi ya watu milini 750 duniani wanatumia mtandao wa Facebook kuonyeshana picha na video na mara kwa mara hubandika maelezo kuhusu mienendo na mawazo yao.

Mamilioni pia wamejiunga na mtandao wa Twitter ambao huwawezesha watumiaji kusambaza ujumbe mfupi na picha kuhusu wao wenyewe.

Baroness Greenfield,mkurugenzi wa zamani wa taasisi ya utafiti ya Royal Institution alisema, "kinachonipa wasiwasi ni ile hali ambapo unaweza kutarajia mtu atawaza au kusema nini ambayo ni hali ya kawaida huko Twitter."

"Kwanini mtu ahitaji kujua umekula nini wakati wa kifungua kinywa?Inanikumbusha jinsi mtoto mdogo anavyosema, 'mama angalia ninachofanya' "

"Ni kama mgogoro wa kujitambua.Kimsingi,hali hii inaufunga ubongo kwenye kuhusisha wakati/muda"

Mwanataaluma huyo alidai kuwa baadhi ya watumiaji wa Facebook wanajisikia wanapaswa kuwa "watu maarufu wadogo wadogo" (mini celebrities) ambao wanaangaliwa na kunyenyekewa na watu wengine kila siku.

"Wanafanya vitu vinavyoendana na Facebook kwani njia pekee wanayoweza kutumia kujitambulisha kwa umma ni kwa kuwafahamisha watu wengine kuhusu kinachoendelea kwenye maisha yao."

"Ni kana kwamba watu wanaishi katika dunia isiyo halisi bali dunia ambayo kinachomata ni nini watu wanafikiria kuhusu wewe au kama wanaweza kubonyeza kwenye picha au ulichoandika," alisema Profesa huyo.

"Fikiria kuhusu madhara kwa jamii ikiwa watu wanajali zaidi kuhusu nini watu wengine wanafikiria kuhusu wao kuliko nini wanachofokiria kuhusu wao wenyewe."

Mawazo ya mwanazuoni huyo yaliungwa mkono na Sue Palmer,mtaalam wa fasihi andishi na mtunzi wa vitabu,ambaye alisema kuwa wasichana hususan wanaamini wao ni bidhaa ambayo lazima iuzwe kwenye Facebook.

Alisema: 'Watu walizowea kuwa na picha ya kuchora (zinazowaonyesha wao) lakini sasa tunaweza kujichora wenyewe mtandaoni.Ni kama kuwa mshiriki kwenye shoo yako mwenyewe ya TV ambayo umeiunda na kuiweka hadharani kwa dunia kuiona.'

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Mail




50 Cent - From hip-hop to Hollywood
Curtis Jackson, aka 50 Cent, is moving into movies. He tells Kaleem Aftab about his next lead role and his $200m production company
Friday, 29 July 2011 
Well, it's a pretty fair exchange: in exchange for not being able to walk around in the mall, you can buy everything in it." Curtis Jackson, aka 50 Cent, is fairly relaxed about the price of fame. Nor does he have to worry about heeding the mantra of his first album Get Rich or Die Tryin'. Album sales galore, a burgeoning film and writing career and several sound investments – including a multi-million dollar payday when the vitamin water company he had shares in sold to Coca-Cola – have seen the latest estimates of his wealth hit half a billion dollars. 
Eight years after his debut album turned the former New York drugs-runner into an international superstar, the 36-year old proffers the following assessment of his wealth and success: "I see money as a facilitator," he elaborates. "If airlines don't have a plane that goes to where you want to go, a private jet will. If a studio doesn't go after a project and think it's the right project for right now, I can go and get it made. I think that to some people I may appear a little off, but they're just not on the same page as me."
His back story has been told many times, most notably on that best-selling debut album, which in turn inspired Jim Sheridan's 2005 movie, starring Jackson, and in his autobiography From Pieces to Weight: Once Upon a Time in Southside Queens. Briefly, Jackson grew up in Queens, New York. His drug-dealing mother died when he was aged eight, he was bought up by his grandmother, and started dealing crack at the age of 12. Then, just days before he was about to film his first music video, the rapper was shot multiple times in front of his grandmother's house. 
It was his musical hero Tupac who made the "thug life" tag a badge of honour for rappers and to start with 50 Cent tried hard to live up to the stereotype: "My first CD contained all of the dysfunctional behaviour that was affecting me. And you become your music to the general public, so I became exactly what the CD was in their eyes. Having it go on to be the widest-selling hip-hop album and sell 12 million CDs worldwide made it intense. So people have a perception of me that's going to be like that until I continue to be successful in other fields. Eventually that will open people's minds up so they think in different ways about me." 
One of the ways he's trying to change those perceptions is through film. I meet him after the international premiere of his new film, Things Fall Apart, in Aruba. He wrote, produced and stars in the film, all under his real name Curtis Jackson, distancing himself from his musician persona. "Growing up, I had to be two people anyway," he says. "I had to be aggressive enough to get by in the environment that I grew up in, and I had to be my grandmother's baby in the house. You wouldn't believe it, but I wasn't allowed to curse in the house at all." 
I admit that I have quite a fondness for his third cognomen "Fiddy" but apparently only close friends or Robert De Niro get to call him that. Jackson met De Niro and Al Pacino when he appeared with them in Righteous Kill in 2008. "It's interesting being around them, because when you are around someone that has that much aura, and so much attention focused on them, I get a chance to be a regular guy on the side, so it's kind of cool to hang out with them." 
Try as he might, Jackson has so far failed to find that breakout role that will make people see him as something other than a rapper-turned-actor. In his only major starring role, Get Rich... he pretty much played himself, in the newsroom comedy Morning Glory he did play himself, Righteous Kill saw him play a drug dealer who meets with an untimely death, and Joel Schumacher's lamentable Twelve found him selling drugs once again. 
So it's no surprise that he had to write and produce himself to land a lead role. Things Fall Apart is another tale from Jackson's childhood in which he plays a promising young American footballer whose chances of a professional career are dashed when he is diagnosed with an aggressive form of cancer. "Charles Pringle was my best friend growing up," explains Jackson. "Some of the dialogue in the film is close to what he actually said to me. Over 12 million people will die this year from cancer and hopefully this film will help us to become more conscious of it. 
But I don't want to become a spokesperson for cancer. I could have done that without making this film. I thought to be part of a project that has some personal value was interesting. I try to be part of projects that have some sort of artistic integrity. It was a passion project and that helped me to have the discipline to make the physical transformation." 
Indeed, the most remarkable moment of Things Fall Apart comes after a time lapse when Jackson goes from bodybuilder physique to gaunt and skinny. The actor lost 60lbs in three months, citing Tom Hanks in Philadelphia, Robert De Niro in Raging Bull and Christian Bale in The Machinist as inspirations. In difficult dieting moments, he would find solace by reading interviews online in which the actors talked about how tough it was to lose weight. 
A keen sports fan – he follows only basketball star Carmelo Anthony and his best friend, the boxer Floyd "Money" Mayweather, on Twitter, though he has 4.7million followers – Jackson is now back to his physical peak. When we meet, he's wearing a natty suit and sunglasses adorned with gold cheetahs for arms. This is dressing "business", he says, and in keeping with that mode he wants to talk about the $200 million (£120m) he has raised for his company Cheetah Vision to make 10 films, in the action genre and in which he will appear: "The first of the 10 is Setup, which stars myself, Bruce Willis and Ryan Phillippe. My character has a revenge plot. And then there is Freelancers with Robert De Niro and Forest Whitaker in which I play a rookie police officer." Also upcoming is Vengeance with Danny Trejo. 
Jackson feels strongly that he's capable of transcending artistic fields: "When you make it in one portion of art, people doubt you in others. I don't take it personally," he says. "I think it's a reflection of how they feel about themselves. They doubt themselves in different areas and they just reflect that off on you. When I'm passionate about something I pretty much get to it. People say, 'He's a rapper, he can't act'. I guess they forgot about Will Smith, right? And they forgot about Mark Wahlberg, and they forgot about Queen Latifah. They forgot about a lot of people."
Jackson has also turned to books and next year will publish Playground a tale of a 13-year-old facing up to the consequences of his actions, aimed at teenagers who have been bullied in school. 
Mall boast aside, he feels that emotional well being cannot be sated by mere untold riches: "When you grow up without money, money feels like it's the answer to all your problems, because every problem in front of you is financial. But when you acquire money, you realise that it just creates other problems, and they have nothing to do with money." 
His major problems at the moment seem to be largely music related. His fourth album, Before I Self Destruct, flopped in 2009. That album was attached to a film that 50 Cent wrote and directed, which in turn flopped. His fifth album, inspired by his experiences listening to dance music in UK clubs, has been continually delayed. "That album", he says. "Will only play in the comfort of my own home". Recently he announced that he expects his next record to drop in November – and he's feeling the weight of expectation: "I've got a lot of pressure on me releasing the next record. I'm still trying to top my first album. I don't think I can match the actual sales on that record, but I can match the energy." 
'Things Fall Apart', 'Vengeance' and 'Setup' are released later this year


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.