9 Aug 2011









































CHANZO: Daily Mail

8 Aug 2011


Screen shot 2011-08-07 at 2.34.44 PM

Antwan "Big Boi" Patton was arrested in Miami on Sunday afternoon on drug possession charges.
Patton, half of the platinum-selling, Grammy-winning group Outkast, was charged with three counts of possession of a controlled substance and one count of possession of drug paraphernalia — all felony charges, according to the Miami-Dade County Corrections Department website.
The 36-year-old was caught by drug-sniffing dogs while getting off a cruise ship.
Patton was carrying Viagra, which he didn’t have a prescription for, Ecstasy pills and MDMA powder, the main ingredient in Ecstasy. 
"While Big Boi was traveling with his group and friends, a small amount of contraband was found in the collective luggage," the rapper's attorney Daniel Kane said in a statement. "I am confident when the entire facts are aired Big Boi will be completely exonerated."

He's being held on a $16,000 bond at the Pre-Trial Detention Center in Miami. 


SOURCE: Los Angeles Times



EMPOWER | EDUCATE | ENTERPRISE.
Is this email not displaying correctly?
View it in your browser.

TWENDE

 follow on Twitter | friend on Facebook | forward to a friend 
Copyright © 2011 Tanzania Women Entreprenuers Network Development Exposition, All rights reserved.
You are receiving this email because you gave us your email address during one of the activities and events related to our company.
Our mailing address is:
Tanzania Women Entreprenuers Network Development Exposition
105 Kilimani Road
Dar Es Salaam 10684


Mauaji ya Mark Duggan,Mwingereza Mweusi,yaliyotokana na kupigwa risasi na polis hapo Alhamisi iliyopita ndio yamepelekea vurugu kubwa zinazoendelea katika kitongoji cha Tottenham,Kaskazini mwa jiji la London kama picha zifuatazo zinavyoonyesha






















CHANZO: Daily Mail

7 Aug 2011

Picha kwa hisani ya Je Unajua Hii

Masaburi awatusi wabunge

• ATISHIA KULIPUA UFISADI WAO HADHARANI

na Ramadhani Siwayombe, Arusha

MEYA wa jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi, ambaye ametakiwa na wabunge wa jiji la Dar es Salaam kujiuzulu kupisha uchunguzi kutokana na kashfa ya uuzaji kifisadi Shirika la Usafirishaji Dar es Salaam (UDA), amewajibu wabunge hao na kusema kuwa kuna baadhi yao wanashindwa kufikiri kwa kutumia vichwa na badala yake wanafikiri kwa kutumia 'makalio'.

Masaburi alitoa kauli hiyo nzito jana mjini hapa alipozungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Naura Spring ambapo anahudhuria mkutano wa pamoja wa kamati za uongozi za serikali za mitaa za nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EACLAT).

Alisema wabunge katika kuchangia hoja ya suala la UDA wamegawanyika katika mafungu matatu ambao alisema katika mafungu hayo moja halijui lolote kuhusiana na sakata hilo na limedandia tu hoja na kuwataja miongoni mwao ni mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi, na mbunge wa Mafia, Abdukarim Shah.

Alitaja kundi la pili kuwa ni la wabunge wa jiji la Dar es Salaam ambao ni mbunge wa Ubungo, John Mnyika, na mbunge wa Kawe, Halima Mdee, ambao alisema wanatafuta umaarufu wa kisiasa kupitia sakata la UDA.

Alisema Mnyika aliweza kuhoji hata katika vikao rasmi, lakini Mdee hajui chochote kwa kuwa hajawahi kuhudhuria vikao vya jiji mpaka sasa.

Aidha, kundi la tatu ambalo ndilo alilituhumu zaidi kufikiri kwa kutumia makalio badala ya kichwa ni la wabunge Abasi Mtemvu (Temeke), Musa Azzan 'Zungu'(Ilala) na Makongoro Mahanga (Segerea) ambao alidai kuwa wanajua ukweli wa jambo hilo lakini wanapotosha ili kuficha madhambi yao ambayo alisema yataibuliwa muda si mrefu ya ufisadi ndani ya jiji hilo.

"Hawa wabunge ambao wana nyadhifa toka kipindi kilichopita ndio wanaohusika na kulifilisi shirika hilo na mashirika mengine ya jiji kwa kuwa mchakato wa kuuzwa kwa shirika hilo ulianza toka mwaka 2008 ambapo mimi nilikuwa hata sijawa diwani," alisema Masaburi.

Alieleza kuwa toka kipindi hicho kwa mujibu wa madokezo yaliyopo kuhusiana na uuzwaji wa shirika hilo, yanaonyesha maamuzi yalipitishwa na vikao halali hadi kuuzwa kwake mapema mwaka huu ambapo yeye hajashiriki kwa lolote mpaka wanauziana.

"Mimi ndiye niliyeibua hii tuhuma ya kuuzwa kwa UDA wakati nikihoji mali zinazomilikiwa na jiji na kuambiwa UDA imeishauzwa; nilipofuatilia nikakuta imeuzwa shilingi milioni 285! Nilipofuatilia hizo fedha kama zipo nikakuta milioni 200 zimeshaliwa; nikaamua kumsimamisha meneja wa shirika hilo na mhasibu. Sasa leo nageuziwa kibao kuwa mimi ndiye nimeuza inashangaza sana!" alisema Masaburi.

Aliendelea kusema wabunge hao wanang'ang'ania ajiuzulu kutokana na hofu iliyotanda baada ya kuanza kazi ya kuibua ufisadi ndani ya jiji hilo kwa kuanzia na UDA.

"Baada ya kuibua ufisadi UDA sasa nimepanga nihamie shirika la DDC ambako Mtemvu ni mwenyekiti wa bodi; shirika ambalo nalo kuna ufisadi mkubwa umefanyika ikiwemo kuuza mashamba ya shirika hilo na baadhi ya nyumba," alisema.

Alisema akimaliza suala hilo atahamia kuhakiki matumizi ya ujenzi wa Machinga Complex ambapo alidai inashangaza kusikia zimetumika bilioni 1.2 kujenga zile nyavu za vizimba ambavyo alifananisha na nyumba za wanyama wafugwao.

Alisema kutokana na mkakati wake huo anaomba wabunge wampe muda wa kutekeleza hayo.

Masaburi alisema hawezi kujiuzulu kwa shinikizo la mafisadi na kudai endapo akifuatilia mashirika yote hayo na kubaini yapo sahihi yuko radhi kujiuzulu kama itahitajika.

"Naomba wanipe muda kidogo nisafishe ufisadi ndani ya jiji la Dar es Salaam kutokana na mikataba ya ajabu iliyoingiwa baina ya viongozi waliokuwepo madarakani kipindi cha nyuma wakishirikiana na wabunge na kulitia umaskini jiji ili kama kuna hoja za msingi wabunge wapate hoja za kujadili bungeni," alijinasibu Masaburi.

Alifafanua kuwa kuhusu suala la malipo ya mwenyekiti wa bodi ya shirika hilo, Iddi Simba, kutoka kwa wanunuzi wa shirika hilo yeye hatambui kwa kuwa hakuna risiti yoyote ya UDA inayoonyesha malipo hayo.

Aliongeza kuwa hata baada ya yeye kupata barua za kuwepo kwa malipo ya sh milioni 320 zilizofanywa kupitia akaunti ya Iddi Simba alimfuata mwenyekiti huyo na kuhojiana naye na alikiri kupokea malipo hayo, lakini alisema hayahusiani na mauzo ya UDA na kusema yanahusiana na biashara zao binafsi.

Alisema kutokana na majibu hayo ya Iddi Simba hakuwa na mamlaka ya kung'ang'ania kuwa malipo hayo ni sehemu ya malipo ya UDA hivyo vyombo kama Takukuru ndio nafasi yao ya kuchunguza suala hilo.

Akizungumzia tamko la Waziri Mkuu kuviagiza vyombo vya Takukuru, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na ofisi ya DCI kushughulikia suala hilo, aliunga mkono uamuzi huo kwani ndio utabainisha wazi wote waliohusika katika kuliuza shirika hilo.

Sakata la kuuzwa kwa UDA lilichukua nafasi katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Uchukuzi ambapo ilifikia wakati wabunge kutishia kutoipitisha bajeti hiyo na kutaka wote waliohusika katika uuzaji wa shirika hilo wawajibishwe ikiwemo Masaburi kwamba ajiuzulu kabla ya Waziri Mkuu kuingilia kati na kuunda tume kuchunguza suala hilo.

CHANZO: Tanzania Daima

6 Aug 2011


Nimekutana nayo huko Jamii Forums.Habari hii imenikumbusha mbinu iliyotumiwa na utawala wa mkoloni kuendeleza utawala wake dhalimu.Wakoloni walitugawanya kwa misingi mbalimbali,hususan rangi,na kwa kiasi kikubwa walifanikiwa kuchelewesha jithada za ukombozi wetu.Lakini kama zilivyo mbinu nyingine za ujanja ujanja,mbinu hiyo haikuweza kudumu milele.Kwa hakika hakuna mbinu yoyote inayoweza kuzuwia kiu ya mwanadamu kuleta mabadiliko bora kwake.

Kinachonisikitisha katika habari hii ni namna baadhi ya wanablogu wenzetu wanavyokubali kuuza utu wao (na kuwasaliti mamilioni ya walalahoi) kwa ajili tu ya maslahi binafsi.Wosia wangu kwao ni mwepesi tu: waangalie namna CCM ilivyowatumia wanahabari katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010,na mara baada ya Wanamtandao kufanikiwa kumwingiza Kikwete Ikulu wakawatosa wengi wa wanahabari hao.Kuna wanahabari walibembelezwa kuacha vibarua vyao nje ya nchi,wakawatumikia wanamtandao na baada ya umuhimu wao kwisha,wakatoswa.Ni vema mabloga walioingia mkenge huu wakatambua kuwa nafasi yao walionayo ni mhimili wa nne wa dola.Lakini la muhimu zaidi,wakae wakielewa kuwa,ashakum si matusi watatumika kama kondomu: MUHIMU SANA KABLA NA WAKATI WA TENDO LA NDOA LAKINI HUONEKANA UCHAFU USIOVUMILIKA BAADA YA TENDO HILO.

You have been warned.

Soma habari husika hapa chini


CCM yaanzisha Mtandao wa Friendly Media to CCM

Wana Jf

Nimesoma habari ambayo imenistua na imenibidi niongee na Mhariri wa Gazeti la Mtanzani Ndg Jacton Manyerere na amenithibitishia kuwa habari aliyoandika ni ya uhakika.

Idara ya Uenezi na Itikadi ya CCM ambayo ipo Chini ya Ndg Nape imeanzisha Mtandao wa Vyombo vya Habari na wana Habari Rafiki na Bloggers na amekuwa akikutana nao Mara kwa Mara.

Kutokana Taarifa za Gazeti la Mtanzania (Media House ambao si Rafiki na CCM kwa Sasa), media ambazo hazitahudhuria ktk mkutano wa Tar 13 na 14 mwezi huu utakaofanyika Morogoro ni Mwananchi Communication, New Habari, Hali Halisi na Free Media. Vyombo hivi si Rafiki wa CCM.

Na Bwana Jacton ansema doc ya FCCM inaonyesha uwepo wa Mpango Mkakati wa Kuanzisha FORUM itakayoitwa KWETUFORUM na pia utaanzishwa mpango halisi wa kuimaliza Jamii Forums.

Pamoja na mpango huu awali walikua wakutane Dodoma wakati wa kamati kuu na mnamo mwezi wa Tano Nape alifanya kikao makao makuu ya CCM na akakutana Bloggers na kuwaahidi kuwasaidia lakini waisaidie CCM ktk Mkutano huo alikuwepo Blogger mmoja wa Jinsia ya Kike... kutokana na mahudhurio ya kikao hicho.

Kilichonishangaza ni baada ya kusoma Agenda za Mkutano ktk Gazeti la Mtanzania leo nimeshangaa katibu wa mpango huu ni dada ambaye sisi hapa Nipashe alikuwa haheshimiki na alisimamishwa kazi.

Binafsi hii ninailaani kwakua inaleta Taswira Mbaya na ninatarajia kuona Editors Forum wanalifanyia kazi kama CCM inatugawa wana Habari ktk Makundi ya Rafiki na Adui ni jambo baya kufanywa na chama kikongwe kama Hiki. Nadhani huyu dogo Nape amechanganyikiwa kabisa.

Nimeona niilete hapa Jamvini Tulijadili.

Story ipo ukurasa wa kwanza ktk Gazeti la Mtanzania na inaendelea ukurusa wa nane

CHANZO: Jamii Forums




JK: Nawajua wala rushwa kwa majina
By Richard Williams | Published  02/22/2006 | Habari za Kitaifa |Rating:
.Asema tabasamu lake lisipotoshe watu
.Maamuzi yake si nguvu ya soda




RAIS Jakaya Mrisho Kikwete amesema anawajua kwa majina wala rushwa katika wizara na kwamba nguvu anayokwenda nayo siyo ya soda.

Alikuwa akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika jana katika uwanja wa michezo wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga, mkutano ambao lengo lake lilikuwa ni kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa ushindi wa kishindo waliompatia yeye na Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu wa Desemba 14, mwaka jana.

Rais Kikwete ambaye mkoa wa Rukwa ulikuwa ni wa nne katika ziara zake za kuwashukuru wananchi, amesisitiza kwamba kauli mbalimbali ambazo amekuwa akizitoa katika ziara zake za kutembelea wizara mbalimbali na idara za serikali ni kauli ambazo hazitoi kwa kutania, bali ni kauli za mambo anayoyafahamu vyema na kwamba mengine ameyaweka akiba. 

"Sizungumzi kwa utani nayajua ninayoyasema. Nilichoweka akiba ni kuwataja watu kwa majina, wasidhani nikienda wizarani nikasema watu hawa wanakula rushwa wasidhani siwajui kwa majina, ninawajua, bali kwa sasa ninatoa muda kwa watu hao wajisahihishe. Mwenye masikio nadhani atakuwa amesikia," alisisitiza.

Katika mazungumzo yake na wananchi hao ambayo mara kwa mara yalikuwa yakikatishwa na vigelegele na nderemo; Rais alirudia tena kauli yake kwamba Mwenyezi Mungu amemuumba akiwa na sura ya tabasamu jambo alilosema kuwa hawezi kulibadili, lakini tabasamu hilo lisiwapotoshe watu, kwani yanapokuja mambo ya msingi huwa hana mchezo na mtu. 

Alisisitiza kuwa kila kiongozi katika nafasi wajibu wake ni kuwatumikia wananchi na kwamba wananchi wanayo haki ya kupata huduma kutoka kwa kiongozi huyo. 

"Ikifika mahali Mtanzania akitaka huduma kutoka kwa mtumishi wa serikali anayelipwa mshahara, basi ni lazima kwanza kabla ya kupewa huduma hiyo, amlipe mtumishi yule, tukifika huko basi huo ni ukiukwaji wa maadili ya kazi na mtu kama huyo hastahili kuwa mtumishi wa umma.

"Tumejipanga vizuri ndani ya serikali katika kuwatumikia wananchi, na hii siyo nguvu ya soda, ukisimama mbele yetu utasukumwa," alisema na kushangiliwa na wananchi.

Rais amebainisha kuwa wale watumishi ambao wamekuwa wakidhani kuwa kutokana na unyeti wa taaluma zao basi hata wakinyanyasa wananchi hawataondolewa katika nafasi zao, wakidhani hivyo wanajidangaya.

"Anayedhani kuwa ataendelea kuharibu kwa sababu katika taaluma yake itachukua muda kuwafundisha watu wengine, anajidanyaganya, tuko tayari kuanza upya. Bora tabu kuliko kuwa na mtu wa aina hiyo ambaye badala ya kuwatumikia wananchi yeye anawatesa," alisema.


Alisema maamuzi mbalimbali ambayo serikali inayachukua hivi sasa na hapo baadaye yanalenga katika kuurejesha utumishi wa umma katika mstari ulionyooka na kwa sababu hiyo amewataka watumishi wa serikali kuu na serikali za mitaa kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia maadili ya kazi na viapo walivyokula



Alisema mfanyakazi atakayetekeleza kazi zake kwa kuzingatia maadili ya kazi yake, hata nishani anaweze kupewa na serikali, lakini kwa yule ambaye atafanya kinyume chake serikali haitakuwa na muda naye.



"Hatuna ugomvi na mtu wala hatuna chuki na mtu, tunachotaka kutoka kwako ni utumishi wako uliotukuka kama ulivyoapa kufanya kazi kwa kuzingiatia maadili," alisisitiza Rais na kuufanya umati wa wananchi wa Sumbawanga kumshangilia.



Alisema kuwa anachotoa ni ilani na kukumbushana kama gari lilikuwa linapita kwenye majani, basi sasa lirejee barabarani ili kule lilikokuwa linapita lisije kuwakanyaga watu.



Kikwete alisema uwajibikaji huo wa watumishi wa serikali kuu na mitaa unawahusu vilevile wakuu wa mikoa ambao tayari alishazungumza nao, na atarudia tena kwa wakuu wa wilaya na wakuregenzi wakati atakapokutana nao mara baada ya kukamilisha kazi ya kuwateua.



Akiwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kumpatia ushindi wa asilimia 86, Rais alisema kuwa ahadi ya serikali ya kuwajengea barabara ya lami kutoka Sumbawanga hadi Tunduma, iko palepale na kwamba kazi ya uchoraji imekwisha kamilika na zabuni za kutafuta kandarasi ili kazi ianze inaendelea. 



Kuhusu mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa huo, Rais amewaomba wananchi hao kuzitumia vizuri ili waweze kuzalisha chakula cha kuwatosha wao na ziada itumike kuwalisha Watanzania wengine ambao mikoa yao imekosa mvua.



Rais Kikwete alishindwa kuhutubia jana mjini Iringa kwa sababu ya mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na radi na hivyo atahutubia leo na baadaye atakwenda kutembelea mabwawa yanayotoa umeme ya Kihansi na Mtera.



Mikoa ya Rukwa na Mbeya ambayo hivi sasa mvua zinanyesha, ingawa zilichelewa kuanza, hali ya mashamba na mazao ni ya kuridhisha hali inayoashiria kuwa kama mvua hizo zinataendelea basi kuna uhakika wa kupata chakula kwa wingi.



Mkoa wa Rukwa hauna matatizo ya njaa isipokuwa katika wilaya ya Mpanda ambako bei ya mahindi imepanda hadi kufikia sh. 10,000 kwa debe, kupanda kwa bei huko kumetoka na wananchi wa maeneo hayo kuuza kwa wingi mahindi yao za ziada 
katika nchi jirani ambako kuna njaa.



Mkoa huo wa Rukwa unatarajia kuzalisha tani milioni 1.2 za mahindi wakati mahitaji halisi ya mkoa ni tani 500,000.


Kutoka gazeti la Uhuru
ISSN 0876-3896 NA.19240
Na Maura Mwingira, Sumbawanga

HABARI HII ILICHAPIHSWA KWENYE MTANDAO WA HABARI TANZANIA


Kwanza nitoe ufafanuzi wa neno "Dola ya Kiusalama", ambalo ni tafsiri yangu isiyo rasmi ya security state.Kwa kifupi,dola ya kiusalama inaruhusu bughudha na unyanyasaji kwa wananchi wasio na hatia kwa kisingizio cha maslahi ya usalama wa taifa.

Kwa makusudi,Tanzania yetu inaelekea kurejeshwa kwenye zama hizo za wanausalama kupewa ruhusa ya kumbughudhi mwananchi yoyote yule kwa kisingizio cha "kusaka taarifa za kiusalama." Of course,sheria za nchi zinavipatia mamlaka vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wao katika namna inavyoweza kutafsiriwa kama unyanyasaji wa wananchi,lakini hilo si tatizo kubwa iwapo uchunguzi huo unafanyika kwa maslahi ya umma.

Taarifa nilizonazo ni kwamba wanausalama wetu wameanza kuwasumbua baadhi ya wananchi wasio na hatia wakishinikiza kufahamu "chanzo cha tetesi za ufisadi mkubwa huko JWTZ".Usidhani kuwa wanasaka chanzo hicho kwa minajili ya kusaidiana nacho katika uchunguzi wa suala hilo (kama upo).Wanataka kumfunga mdogo.

Huu ni uhuni wa kitaaluma.Kama huyo anayetuhumiwa kukibwa fedha za umma anaona amekashifiwa,kwanini asiende mahakamani?Nini kinafichwa katika suala hili?Natambua kuna wanaodai kuwa suala hili ni nyeti sana na linaweza kupelekea uasi huko jeshini (ambapo asilimia kubwa ya askari wanaishi maisha magumu kulinganisha na makamanda wao).Lakini hoja hiyo haina uzito kushinda ukweli kwamba fisadi ni fisadi,awe raia au kamanda wa jeshi,na hatua za kisheria lazima zichukuliwe dhidi yake.

Watawala wanataka kulificha suala hili chini ya zulia.Lakini itambulikwe kuwa tunaishi zama tofauti na huko nyuma.Iwapo suala hili halitashughulikiwa kikamilifu na kiuadilifu,basi wahusika wakae wakijua kuwa kuna siku litalipuka upya.

Na nyie mnaojaribu kunyanyasa wananchi kuwashinikiza wawaambie vyanzo vya tetesi za ufisadi jeshini ACHENI MARA MOJA.Hatupendi kuharibu hadhi ya nchi yetu kwa nchi na taasisi wafadhili lakini mkiendeleza uhuni huu tutashawishika kuweka hadharani jinsi mnavyojaribu kufunika ufisadi kwa kuwanyanyasa wanaoibua taarifa hizo.

Nimechukua hatua zaidi kwa kum-tweet Rais Jakaya Kikwete (@jmkikwete) kama invyoonekana mwanzoni mwa makala hii.



Juu ni taswira mbali mbali zinazo onesha jinsi ujenzi wa soko kuu la Mwanjelwa ulivyo simama, ulianza kwa kasi lakini kwa sasa hakuna kinacho endelea na miezi kadhaa iliyo pita jengo hilo lilibomoka wakati wanaendelea na ujenzi. Tutaendelea kuwafahamisha zaidi juu ya swala hili 

HUU NDIO UBUNIFU WA DARAJA LA JUU KWA WATEMBEA KWA MIGUU WA JIJI LA MBEYA ENEO LA MWANJELWA MIAKA MIWILI IJAYO KAMA ULIVYOBUNIWA NA TAASISI YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA MBEYA

Taswira ya karibu inayo onesha Soko la Mwanjelwa jijini Mbeya 

SWALI NI JE ITAWEZEKANA? IKIWA SOKO TUU LINASUA SUA NA LIPO BARABARANI ENEO WANALO TAKA KUWEKA KIVUKO HICHO.

Imetumwa na Mbeya Yetu Blog

5 Aug 2011


4 Aug 2011





Raia Mwema Ughaibuni
Spika wetu na wauchapao usingizi bungeni!
Evarist Chahali
Uskochi
3 Aug 2011
Toleo na 197
MATUKIO ya kutia aibu yanayozidi kutokea katika kikao kinachoendelea cha Bunge la Bajeti huko Dodoma yanatoa picha moja ya msingi kuwa Spika Anne Makinda anaelekea kushindwa kumudu wajibu wake.
Haihitaji kuwa mchambuzi mahiri wa siasa kutambua hilo. Japo tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi Bunge letu limeshindwa kumudu uwepo wa wabunge wa vyama vya Upinzani, lakini kwa jinsi hali ilivyo sasa; chombo hicho muhimu kwa taifa kimegeuka kuwa uwanja wa vurugu.
Ninamshutumu Spika Makinda kwa sababu tangu apate wadhifa huo, amekuwa akijitahidi kadri awezavyo kuendesha Bunge kibabe; huku akitaka kuuthibitishia umma kuwa anakimudu kiti cha uspika ipaswavyo.
Lakini inawezekana kabisa kuwa chanzo cha matatizo yanayozidi kushamiri Bungeni ni madaraka makubwa anayopewa Spika dhidi ya wabunge. Sio siri kwamba madaraka ya Spika yanampa nguvu kubwa mno ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria; huku kukiwa hakuna namna nzuri ya mwafaka ya kumdhibiti.
Kibaya zaidi, kwa makusudi, chama tawala kimeshikilia msimamo wa kuwa na Spika anayetoka moja ya vyama vyenye wabunge bungeni. Busara nyepesi tu inaweza kueleza kuwa katika mazingira ya uchanga wetu kwenye siasa za vyama vingi, Spika lazima atapendelea chama anachotoka.
Tukubali tusikubali, upendeleo ni moja ya vikwazo vikubwa vya maendeleo sio ya Tanzania pekee; bali sehemu kubwa ya nchi za Dunia ya Tatu. Ukimpa mtu madaraka pasipo kutengeneza mazingira bora ya kumdhibiti kuyatumia madaraka hayo isivyofaa, moja ya mambo ya mwanzo kabisa yanayoweza kutokea ni upendeleo.
Na laiti mtu huyo akitambua kuwa ana uhuru wa kufanya apendavyo, basi, atafanya upendeleo wa waziwazi akijua fika kuwa kufanya hivyo hakutoathiri nafasi yake.
Ni rahisi kuhitimisha kuwa Spika Makinda kazi inamshinda iwapo hatutorejea nyuma kidogo na kuangalia utendaji kazi wa waliomtangulia. Lakini kumbukumbu ndogo tu inaweza kutupa mwanga kuwa vitendo vya maspika wote baada ya kuruhusiwa mfumo wa vyama vingi, vimekuwa sio tu vya kidikteta dhidi ya wabunge wa vyama vya Upinzani; bali pia vinaweza kabisa kutafsiriwa kuwa matumizi mabaya ya nafasi hiyo muhimu.
Jingine ambalo linaweza kupoteza kabisa sio tu heshima ya nafasi ya cheo cha Spika bali pia umuhimu mzima wa kuwa na Bunge, ni mtindo wa ku-kasimu madaraka ya kuongoza vikao vya bunge kwa wabunge mbalimbali.
Hilo lisingekuwa tatizo laiti wabunge wote tulionao wangekuwa wa ina moja; yaani wanatambua kwa nini wanalipwa mamilioni ya shilingi kila mwezi kuwatumikia Watanzania.
Lakini sote tunajua kwamba asilimia kubwa tu ya wabunge wetu ni watu wasiojali kabisa jukumu la kuwatumikia wananchi waliowachagua kuwa wabunge, na badala yake wanaendekeza maslahi binafsi; huku picha zikiwaonyesha baadhi yao wakichapa usingizi kwenye vikao.
Na suala hilo la wabunge kulala linaweza kuibua mjadala mwingine kwenye maeneo mawili ya msingi. Kwanza, hivi ni haki kweli kwa mbunge kulipwa mamilioni ya shilingi kama posho; kisha akaishia kulala bungeni? Hivi huo kama sio ukupe ni nini?
Huo si uungwana hata kidogo, kwa sababu wakati mbunge anakoroma bungeni na kulipwa fedha kibao, walalahoi huko mitaani wanadamka alfajiri kusaka fedha ambazo kila kukicha zinazidi kuwa ngumu kupatikana kutokana na hali ngumu ya maisha.
Pili, kama maamuzi ya kuwatimua wabunge yanazingatia haki, kwanini basi wabunge wanaolala bungeni nao wasikumbane na “hasira za Spika” kwa kutolewa nje? Japo kusinzia au kulala si kosa, lakini katika mazingira ya kawaida tu mtumishi anayelala kazini anapaswa kuadhibiwa.
Jingine ambalo mara nyingi hujitokeza nje ya bunge, ni tabia za baadhi ya wabunge baada ya vikao vya chombo hicho kinachopaswa kuwa kitukufu kutokana na dhamana yake kwa umma.
Unaweza kudhani huu ni uzushi kwa vile hakuna chombo cha habari kinachoweza kuthubutu kuripoti hili, lakini ukweli ni kwamba tabia za baadhi ya wabunge wetu nyakati za jioni au wakati wa mapumziko ya mwisho wa wiki sio tu hayaendani na nyadhifa zao; bali pia zinakinzana na wajibu walionao kwenye familia zao.
Sote tunafahamu kwanini akina dada wanaofanya biashara za kuuza miili yao hukimbilia Dodoma kila kunapokuwa na vikao vya bunge. Jibu ni kwamba huo ni msimu wa ‘kuchuma’. Hivi kweli tunawalipa watu hawa mamilioni ya shilingi kwa ajili ya kufanya mambo kinyume na maadili?
Unaweza kutetea kuwa hiyo ni tabia ya mtu binafsi, lakini hoja hiyo inakosa uzito kutokana na ukweli kwamba, kwanza watu hao binafsi wanatumia fedha za walipakodi kufanya anasa zisizostahili, na pili, anasa hizo zinaweza kabisa kuathiri uwezo wao wa kutumikia umma kwa uadilifu.
Unadhani Mheshimiwa mbunge mwenye miadi na “dada poa” anaweza kweli kuelekeza akili yake kutuliza maswali ya msingi kuhusu matatizo yanayowakabili wapigakura wake?
Hili linaweza kuonekana kama tatizo dogo, lakini lina uzito mkubwa; kwani mtu asiye mwadilifu kwa familia yake hawezi kuwa mwadilifu kwa wapiga kura wake au taifa kwa ujumla.
Uhuni wa baadhi ya wabunge wetu umevuka mipaka hadi kufikia hatua ya kumfanya Waziri Mkuu kama mtu wa kumtania. Sikuamini macho yangu niliposoma habari kwamba baadhi ya wabunge wanafoji sahihi ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuandika vimemo feki kwamba mbunge fulani anahitajiwa kukutana na Pinda wakati si kweli.
Taarifa zilizopo ni kwamba mmoja wa wabunge wenye tabia hiyo ya kitoto ameshafahamika, lakini katika kuashiria kuwa bunge hili limekithiri mizaha, hakuna hatua itakayochukuliwa dhidi ya mbunge huyo. Kwa lugha nyingine ni sawa na kuhalalisha upuuzi aliofanya mbunge huyo.
Kuna picha kubwa zaidi kuhusu mapungufu ya bunge letu ambalo katika msimu uliopita lilipata kujigamba na kutunga kitabu chenye jina “Bunge Lenye Meno” (nami nikaandika makala bloguni kwangu nikaliita “Bunge Lenye Meno ya Plastiki”).
Wingi wa wabunge wa CCM ndani ya Bunge hilo umeshindwa kabisa kumsaidia Mtanzania wa kawaida, kwa sababu, kwa CCM na viongozi wake (pamoja na wabunge), maslahi ya chama yana umuhimu mkubwa zaidi kuliko maslahi ya nchi.
Kila mara tunashuhudia wingi wa wabunge wa CCM unavyosababisha sheria mbovu kupita baada ya wabunge hao “kupewa somo la kuwekana sawa.”
Japo tunaweza kujidanganya kuwa demokrasia inakua kutokana na kuongezeka kwa idadi ya wabunge wa vyama vya Upinzani, ukweli unabaki kuwa tangu vyama vingi viruhusiwe; bunge letu limeendelea kuwa la chama kimoja. Hapa ninamaanisha kuwa wingi wa wabunge wa chama tawala unafunika kabisa uwezekano wa uwepo wa wapinzani kuleta mabadiliko yanayotarajiwa.
Kulaumu tu bila kutoa ushauri hakuwezi kusaidia kutatua tatizo lililopo. Spika Makinda na wasaidizi wake wanapaswa kutambua kuwa kuwatimua nje ya bunge wabunge wa CHADEMA na wengine wa vyama vya Upinzani pekee kunatoa picha moja tu ya uonevu kwa upande mmoja na upendeleo kwa upande mwingine.
Lakini hilo si la msingi zaidi kulinganisha na ukweli kwamba kuwatimua wabunge kwa “makosa” yanayoweza kurekebishika kwa maonyo tu kuna madhara makubwa kwa wapigakura wanaowakilishwa na wabunge hao.
Adhabu kwa mbunge ni adhabu kwa maelfu kama sio malaki ya wapiga kura wanaowakilishwa na mbunge husika. Spika anaweza kujitetea kwamba hawezi kulea tabia mbovu bungeni. Sasa iweje tabia hiyo mbaya iwe ni kwa wabunge wa Upinzani pekee?
Vipi kuhusu baadhi ya wabunge wa CCM tunaowaona kwenye picha wakiwa wamelala; huku bunge linaendelea? Na vipi kuhusu baadhi ya wabunge watoro wasiohudhuria vikao wakati tayari wameshachota malipo ya posho zao?
Nimalizie kwa kusisitiza kuwa Tanzania yetu ni muhimu kuliko maslahi ya mtu au chama binafsi. Kila mbunge, ikiwa ni pamoja na Spika, ni waajiriwa wa Watanzania. Wananchi ndio wanaowalipa mishahara yao monono na posho zao zisizoendana kabisa na umasikini wetu. Ni dhahiri wananchi hawaridhishwi na mwenendo huu wa sasa wa bunge letu.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.