5 Sept 2011










Kuna wagombea watatu wenye kuchuana vikali Igunga; Dr Peter Kafumu ( CCM), Leopard Mahona ( CUF) na Joseph Kashindye ( CHADEMA). Blogu yako ya Jamii Shirikishwa, Mjengwablog, imekuandalia Pima- Maji ili utoe maoni yako kwa kupiga kura.  Zimebaki siku sita za kupiga kura. Swali ni hili; Je, ni nani ataibuka kidedea Igunga? Piga kura juu kulia kwenye http://mjengwa.blogspot.com

4 Sept 2011






Kwa sasa nitaiwasilisha kama ilivyo lakini naahidi kuifanyia tafsiri ya Kiswahili baadaye leo.

Viewing cable 06DARESSALAAM277, KIKWETE CORRUPTION TIDBIT

If you are new to these pages, please read an introduction on the structure of a cable as well as how to discuss them with others. See also the FAQs



This record is a partial extract of the original cable. The full text of the original cable is not available.

C O N F I D E N T I A L DAR ES SALAAM 000277 SIPDIS DEPT FOR INR, R.EHRENREICH E.O. 12958: DECL: 02/13/2016 TAGS:

PGOVPRELTZSUBJECT: KIKWETE CORRUPTION TIDBIT Classified By: Ambassador Michael Retzer, Reason 1.5 (d) 1. (C) President Kikwete has accepted gifts (bribes) from the owner of the Kempinski Hotel chain,s Tanzanian properties, a citizen of the United Arab Emirates. 2.

(C) In a conversation with the manager and the publicity director of Dar Es Salaam,s Kilimanjaro-Kempinski Hotel hours after accompanying A/S Frazer to her October 18, 2005 meeting with then-Foreign Minister Kikwete,
I commented on Kikwete's flashy attire, asking "Who dresses him?" "We do," they responded. Initially thinking this meant Kikwete frequented a men,s shop in the hotel, I learned later in the evening from hotel publicity director Lisa Pile (protect) that the hotel owner*UAE citizen Ali Albwardy*had recently flown Kikwete to London for a subsidized shopping expedition.Among other things, on that trip Ali Albwardy bought Kikwete five Saville Row suits. He had also recently made a $1 million cash contribution to the CCM (which is a legal contribution under current Tanzanian law). 3.

(C) Pile told me the Kempinski Hotel chain is greatly expanding its presence in Tanzania. She said that in December it would open "the best hotel in Zanzibar." Her prediction was a little off; the new Kempinski hotel, located on the beach on Zanzibar,s east coast, opened January 5. I attended the opening ceremony along with Zanzibari President Karume, who was asked publicly by Ali Albwardy for a site in Stone Town to build a new hotel. Later that day, Pile revealed that the Zanzibar government had already earmarked for Ali Albwardy a hotel site in Stone Town.
4.

(C) Pile also said in the October 18 conversation that Ali Abwardy was about to receive the rights to construct two new hotels on the mainland: one on the edge of Ngorongoro Crater and another on the Serengeti plain overlooking the main animal migration routes. Stringent conservation rules currently ban the construction of permanent structures inside national parks*including in the crater and on the Serengeti plain*but Pile said that in November legislation would be introduced to parliament to authorize the new hotels.

(Comment: We have received no reports on new legislation, but the Dar Es Salaam Daily News on January 15 reported that the Tanzania National Parks Authority had approved construction of a five star hotel on the Serengeti plain.)
4.

(C) Later on October 18, over dinner, an Indian/South Asian man described as a business associate of Ali Albwardy briefly took Pile from the table for a conversation in Kiswahili. I am not sure what was said, but Kikwete's name came up several times and
he passed her an envelope. Pile told me the envelope was stuffed with 1 million shillings ( $1,000) and was to pay for a Kikwete meeting at the Kilmanjaro-Kempinski later that month. Apparently Kikwete is a regular customer, but no name ever appears on the hotel registry when a government bigshot has an "event" in one of the guest rooms. 5.

(C) Bio Note: Lisa Pile, an Australian citizen, has lived in Dar working for Kempinski Hotels since early 2004. Before that she had served in a similar capacity with the Kempinski chain in China. Her family in Australia is prominent in Australia's Liberal Party (the center-right party of Prime Minister John Howard).
6.

(C) Comment: What does it all mean? I don,t know, but my guess is that the investor Ali Albwardy has access to oil money out of the UAE.
I suspect giving free clothes and the campaign donation is just the way these people do business. 7.

(C) For his part, Kikwete probably thinks having all these five star hotels around is a good idea for the country,and I agree with him. His new minister of Natural Resources and Tourism, Anthony Diallo, says he wants to double tourism,s contribution to the national economy in ten year,s time.
Kikwete probably believes there is no harm in taking these "little gifts" to do what he would have been inclined to do anyway. That said, they are what they are: bribes.

2 Sept 2011

Mawaziri wa kiume nchini Zimbabwe wapo mbioni kutahiriwa kama sehemu ya mkakati wa serikali ya nchi hiyo kuhamasisha njia hiyo inayoaminika kupunguza maambukizi ya Ukimwi.

Tafiti zinaonyesha kuwa tohara kwa wanaume inasaidia kupunguza uwezekano wa maambukizi ya Ukimwi (wakati wa tendo la ndoa) kwa takriban asilimia 60.Hata hivyo,wataalamu wa tiba wanaonya kuwa tohara hiyo sio njia mbadala ya hatua nyingine za kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.

Zimbabwe ilianzisha kampeni kubwa mwaka juzi ikiwalenga angalau wanaume milioni 1.2 katika jitihada za kupambana na maambukizi mapya ya ugonjwa huo.

Vituo vinavyoendesha zoezi hilo vimeeleza kuwa watu wengi wamekuwa wakijitokeza na wanaonyesha kukubaliana na hatua hiyo.

Lakini sasa kuna mpango wa kuwalenga wanasiasa wa ngazi za juu ikiwamo mawaziri,wabunge na madiwani ili nao watahiriwe.

Naibu Waziri Mkuu Thokozani Khupe ameeleza kuwa hatua hiyo inaendana na mkakati wa serikali kupambana na Ukimwi.

"Utafiti umeonyesha kuwa wanaume waliotahiriwa wana nafuu  ya maambukizi ya Ukimwi pungufu kwa mara nane,na kama viongozi serikalini tunapaswa kuongoza kwa kuonyesha mfano ili tunaowaongoza watambua umuhimu na faida ya tohara," Khupe alilieleza gazeti la Sunday News la Bulawayo.

"Lengo letu ni kuwa na vifo sifuri kutokana na Ukimwi.Tunaweza tu kufanikiwa iwapo viongozi wataonyesha mfano.Watu wanapaswa kuelewa kuwa Ukimwi upo na haipaswi kudhani kwamba kuzungumzia tohara ni mwiko."

Zimbabwe ni moja ya nchi zilizoathiriwa vibaya sana na janga la Ukimwi huku kiwango cha maambukizi kikiwa miongoni mwa vikubwa zaidi duniani.

Hata hivyo,kiwango cha maambukizi kimepungua kwa kasi,takriban kwa nusu kutoka asilimia 29 ya Wazimbabwe wote mwaka 1997 hadi kufikia asilimia 16 mwaka 2007.

Watafiti wanaeleza kuwa wananchi wameanza kukubali kubadili tabia za ngono kutokana na kukua kwa uelewa kuhusu vifo vinavyotokana na Ukimwi na hofu ya kuambukizwa virusi vya ugonjwa huo.

"Nchi chache sana duniani zimeshuhudia kupungua kwa maambukizi,na katika Afrika,Zimbabwe ilionekana kama sio rahisi kumudu kupunguza maambukizi," Simon Grason wa chuo cha Imperial jijini London alieleza katika ripoti ya hivi karibuni.

CHANZO: Nimetafsiri habari hii kutoka gazeti la New Zimbabwean (bonyeza kiungo kuisoma katika lugha ya Kiingereza)


Kocha wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila (Super D) kushoto akitangazwa mshindi zida ya bondia Safari Berdard kipindi hicho

Super D Boxing Coach kushoto Akipambana na Rashidi Ali

Super D Boxing Coach kulia akipambana na Ajibu Salumu
Salam alykum kaka kwenye maktaba yangu ya picha nimekutana na picha hizo kaka si vibaya ukawakumbusha bondia machachari aliekuwa anasimamisha mashabiki vitini awapo ulingoni asante kwa ushirkiano wako tupo pamoja
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania




--
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times
Mob;+255787 406930
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

 
  • superd vs ajibu.JPG
  • super d vs rashid ali.JPG
  • super d ushindi.JPG


Na Nova Kambota,
Namkumbuka mwanamuziki wa kizazi kipya Seleman Msindi maarufu kama Afande sele na kile kibao chake cha “Darubini kali” anapohoji “kama unapenda pepo kwanini uogope kifo?”
Tungo hii kwa namna ya pekee inamgusa waziri mkuu wa Tanzania Mh Mizengo Pinda maarufu kama “mtoto wa mkulima” ndiyo namuuliza Pinda ataonaje pepo pasipo kufa kwanza?
Tangu kuteuliwa kwake mara baada ya Edward Lowassa kujiuzulu, Kwa wale wanaomjua Pinda walishasema kuwa “Pinda atapwaya sana”, sasa ikiwa ni takribani miaka mitatu na nusu tayari mambo hadharani kuwa Pinda “kashindwa kazi”
Kwa wasiomjua Mizengo Pinda tafuteni ukweli mtamjua tu, ni Mizengo Pinda huyu amebaki kuwa mshauri wa Kikwete badala ya waziri mkuu kufikia hatua ya kutamka bungeni kuwa hana mamlaka, ni Pinda huyu asiye na makundi lakini anakubali kumezwa na mitandao na makundi ya CCM na bosi wake Kikwete na sasa nimeanza kusikia watu wakimwita ni “mtoto wa mkulima anayeishi kibilionea”
Hakuna ubishi kuwa hata watetezi wachache wa Pinda waliobaki sasa wamefadhaishwa na udhaifu wake kama sio uwoga wa kupindukia, “jeuri” ya Luhanjo na sakata la Jairo limemwaka njia panda Mizengo Pinda, amebaki kujiumauma na kutapatapa tu, kadhalilishwa lakini hataki kuchukua hatua, katukanwa lakini anachekelea! Huyu ndiye Mizengo Pinda.
Waziri mkuu Pinda akiongelea sakata la Jairo akajiapiza kuwa angekuwa na mamlaka angemfukuza kazi Jairo kwa maana nyingine Pinda amekiri kuwa Jairo anastahili adhabu na serikali haikutaka kumwangusha waziri mkuu “ikamtwanga likizo ya malipo” Bw Jairo lakini ghafla katibu mkuu kiongozi anaibuka na kumdhalilisha waziri mkuu eti Jairo hana kosa arudi kazini, wakati Pinda akisita kuchukua hatua wabunge kwa umoja wao wameamua kumtetea waziri mkuu kwa kudhalilishwa sasa Bunge limeunda kamati.
Hivi katika mduara huu wa “kudhalilishana na kushushiana heshima” ipi nafasi ya Pinda? Yapi maamuzi ya Pinda? Kichekesho ni kuwa Pinda “yupoyupo tu” hajachukua uamuzi na dalili zinaonyesha kuwa kwa mara nyingine tena Pinda amekubali kupiga magoti na kujishusha sehemu aliyotakiwa apigiwe  magoti yeye huyu ndiye Pinda ambaye bilashaka hata “ukimpiga ngumi” yeye wakati wa kukurudishia lazima atavaa gloves ili asikuumize.
Pinda anataka pepo? Anataka watanzania tumkumbuke kuwa ni kiongozi jasiri? Basi hana budi kufa ili aione hiyo pepo! Naam amedhalilishwa sana, ameshushiwa hadhi yake, na sasa ni wakati wayeye kufikiria kujiuzulu.
Haiwezekani Luhanjo na Pinda waendelee kuitumikia serikali moja, hiki kitakuwa ni kiinimacho , ni lazima mmoja wao atoke, na kwa vile wote tunakubaliana Pinda anaitamani pepo, anataka kukumbukwa mioyoni mwa watanzania, lazima aachane na serikali hii ya akina Luhanjo na Jairo, hana budi kumwachia Kikwete ateue waziri mkuu mwingine ambaye atakubali kuvunjiwa heshima, Naam! Pepo haiji hivihivi, ni lazima Pinda afe leo ili aione pepo kesho!

Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
Tanzania, East Africa,
Alhamisi, September 1, 2011.


Here is the beginning of my post. Endelea.

1 Sept 2011


Natumai Muwazima wa Afya Njema na Happy Eid kwa Ndugu zetu waislam wote hapo kazini, Samahanini sana kwa usumbufu tunaomba Msaada wenu mtusaidie kutoa taarifa hiyo hapo chini ya juu ya mabadiriko ya jina la website yetu na pia jina la Radio. Natanguliza Shukkrani zangu. Kazi Njema.

TAARIFA YA MABADILIKO YA JINA NA LINK YA TONE INTERNET RADIO KWENDA TONE ONLINE RADIO
Tone Multimedia Company Limited inapenda kuwapa taarifa wananchi wote popote Duniani kuwa tumefanya mabadiliko ya jina la Radio pia jina la Tovuti ambapo mala ya kwanza ilikuwa inaitwa Tone Internet radio na Jina la Tovuti lilikuwa ni www.toneinternetradio. blogspot.com, Kutokana na Sababu za kimsingi za kuingiliana kwa mtandao na Radio moja iliyopo USA inakwenda kwa jina la Tune Internet Radio ndio sababu iliyo tupelekea kubadilisha  jina na kuzaliwa kwa jina jipya la Tone Online Radio ambapo tovuti yake sasa itakuwa ni www.toneonlineradio.blogspot. com na ikumbukwe pia Tone Online Radio ni Radio inayo tumia internet Pekee hatuna Frequency za aina yoyote. asanteni sana atakae pata link hii ampatie na mwenzake. Kwa pamoja tunaendelea kuleta maendeleo ya mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia.
Natanguliza Shukrani kwa niaba ya Uongozi,
Imetolewa na,
Joseph Mwaisango
Mkurugenzi wa Mawasiliano
Tone Multimedia Company Limited.

KUSIKILIZA TONE ONLINE RADIO BOFYA HAPA:  www.toneonlineradio.blogspot. com

30 Aug 2011



Raymond Kaminyoge
MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imeshusha bei ya mafuta kuanzia leo.Kwa hatua hiyo, bei ya ukomo ya petroli kwa Mkoa wa Dar es Salaam sasa itakuwa Sh2,070, huku dizeli ikiwa Sh1,999 na mafuta ya taa Sh1,980. Bei ya ukomo wa bidhaa hiyo itatofautiana kulingana na umbali wa maeneo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu alisema hiyo ni kutokana na kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo katika soko la dunia.Alisema ikilinganishwa na bei ya zamani, petroli imeshuka kwa Sh44.55 sawa na asilimia 2.11 huku dizeli ikishuka kwa Sh31.99 sawa na asilimia 1.57 na mafuta ya taa yakishuka kwa Sh25.62 sawa na asilimia 1.28.Mnamo Agosti 2, Ewura, ilishusha bei ya mafuta.

ZAIDI SOMA HAPA
Petroli ilishuka kwa Sh202.37 kwa lita ambayo ilikuwa ni sawa na asimilia 9.17, dizeli kwa Sh173.49 sawa na asilimia 8.32 na mafuta ya taa kwa 181.37, sawa na asilimia 8.70 hali iliyosababisha vurugu na uhaba wa bidhaa hiyo.

Lakini, siku 11 baada ya kushusha bei hiyo, Ewura ilipandisha tena bei ya mafuta kutokana na kile ilichodai kuwa ni kupanda bei katika soko la dunia na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania na kusababisha Bodi ya mamlaka hiyo kubanwa na Baraza la Mawaziri.

26 Aug 2011






BY COSMAS MLEKANI

Chama cha Madaktari nchini (MAT) kimesema tiba inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwasapila, kwa njia ya kikombe kwa ajili ya kutibu magonjwa sugu, imeleta maafa makubwa kwa wagonjwa.

Makamu wa Rais wa MAT, Dk. Primus Saidia, alitoa tamko hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana suala zima la magonjwa yasiyoambukiza na tiba mbadala.

Alisema kuwa wagonjwa wengi baada ya kunywa kikombe cha Babu waliacha kunywa dawa za magonjwa yaliyokuwa yakiwasumbua na kusababisha wengi wao kupooza, kufa na wengine hali zao kuzidi kuwa mbaya.

“Ni vyema wananchi walio wagonjwa wa shinikizo la damu, kisukari, anemia na magonjwa mengine wakafuata ushauri wa madaktari badala ya kulaghaiwa na wachache,” alisema Dk. Saidia bila kufafanua zaidi.

Alisema umma wa Watanzania umekuwa ukilaghaiwa kwa tiba mbadala na kuacha kutumia dawa za hospitali hivyo kuongeza ukubwa wa tatizo na wanapokimbilia hospitali tayari hali zao zinakuwa mbaya.

Dk. Saidia alisema ili dawa iweze kutumika hufanyiwa utafiti kwa kati ya miaka 10 hadi 15.

Naye Katibu Mkuu wa MAT, Dk. Richard Kabangira, ambaye ni daktari bingwa ya tiba wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando, alisema: “Serikali yetu haisikilizi wana taaluma, mfano Babu wa Loliondo utafiti uliofanyika pale ni wa dawa kutokuwa na madhara kwa binadamu na sio kutibu magonjwa.” alisema Dk. Kabangila na kuongeza:

“Hospitali ya Rufaa ya Bugando ilipokea wagonjwa wengi wa kisukari baada ya kutoka Loliondo kufuatia wagonjwa hao kuacha kunywa dawa walizopewa hospitalini.”

Alisema waliwasiliana na wanachama wao nchini kote kufuatilia hali za wagonjwa waliokuwa wamekwenda kwa Babu kupata kikombe na waligundua kwamba waliokuwa wanatumia dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi (ARV), shinikizo la damu, kisukari na hata saratani waliacha dawa baada ya kunywa kikombe cha Babu.

Alisema pamoja na watu kadhaa kutoa ushahidi kuwa wamepona kwa dawa hiyo, utafiti uliofanywa na MAT, umegundua kuwa hakuna hata mtu mmoja aliyepona baada ya kunywa dawa ya Babu.

Alisema watumiaji wa ARV walipungua kama ilivyo kwa hao wengine, lakini baada ya muda hali zao zilikuwa mbaya wengine walikimbilia hospitalini lakini kwa kuwa walikuwa wamevuruga mtiririko wa tiba, walipata madhara makubwa.

Dk. Kabangira alisema MAT ilimwandikia barua Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii juu ya hatari ya tiba ya Babu, na kutoa ushauri wao, lakini ulipuuzwa kwa sababu za kisiasa.

Kufuatia hali hiyo, MAT imetoa wito kwa Serikali na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuwaeleza wananchi ukweli ili wasiangamie huku wakieleza kusikitishwa kwao kutokana na tiba hiyo kutumika kisiasa.

Mchungaji Mwasapila alianza kutoa tiba hiyo mapema mwaka huu na kusababisha maelfu ya wananchi kutoka pembe zote za nchi na nje ya nchi kukimbilia nyumbani kwake katika kijiji cha Samunge, Loliondo katika Wilaya ya Ngorongoro, mkoani Arusha kupata tiba hiyo dhidi ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya kisukari, Ukimwi, saratani na shinikizo la damu.

Viongozi mbalimbali wa madheheu ya dini nao walikuwa miongoni mwa maelfu waliokwenda Samunge na kupata kikombe huku wakitoa ushuhuda kwamba wamepona kwa dawa ya Mchungaji Mwasapila maarufu kwa jina la Babu.

Safari ya kwenda Samunge ilikumbana na changamoto ya barabara mbovu zilizosababisha misongamano na kuilazimisha serikali kuingilia kati kupanga utaratibu pamoja na kusaidia kuboresha miundombinu.

Chama hicho leo kinafanya mkutano wao mjini Mwanza, suala la tiba ya Babu linatarajiwa kuibuka katika mkutano huo unaowakutanisha wanachama wake. SOURCE: NIPASHE

25 Aug 2011




Sharing this story may save some life,may touch someone's life in a similar related problem,may bring hope to hopeless situation.Yawezakua si wewe na unaweza kuchukulia just simple.ila yaweza kumgusa mwenzio na kupelekea ku save maisha yake..
tumekua tukiamka kila leo na kutembea , unaweza kujiona una nguvu na afya tele bila ya kujijua kuwa kuna ugongwa unakula ndani kwa ndani,
au unaweza kutokewa na hali isiyoya kawaida ya hafla ila ukapuuzia na kuipa kisogo,waweza kugundua tatizo kwa mtoto wako ndugu yako,jirani yako au mtu yeyote 
yule wa karibu bali ukajenga woga au  ukazarau na kutokutilia manane hali yake,bila ya kujua kuwa ukimya wako unazidi kuhatarisha maisha ya mwenzako huyo.

Kila kiungo kina u.muhimu katika mwili wa binaadamu ila siku ya leo napenda kugusia zaidi kwenye  Macho.
CONE SHAPE YA CORNEA

KERATOSCONUS 
 Ni jina kutoka Greek na ni  miongoni mwa magojwa ya macho.na naweza kuitafsiri kama hali ya kuendelea ambayo inafanya muundo wa kawaida wa cornea ambao ni curve kwenda kwenye muundo wa cone.

 Ukijiuliza chanzo au sababu ya maradhi haya jibu ni kuwa hakijulikani ingawa wana sayansi wamejaribu kuleta vyanzo tofauti.
Wapo wanaosema ni urithi na mazingira yanachangia.Keratoconus huathiri mtu mmoja kwenye watu zaidi ya 2000.ingawa kwa hivi sasa maradhi haya yanakua zaidi.

Back to my story nilipokua na umri wa miaka 4 nilianza kupata tatizo la macho na baada ya kupelekwa hospital nilishauriwa kuanza kutumia miwani

Jambo hili halikuungwa mkono na mama angu na ikambidi ajaribu kutafuta njia na ushauri kutoka kwa madaktari mbalimbali..na ndipo aliposhauri badala ya kuvaa miwani nijaribu kutumia tiba mbalimbali na vyakula vitakavyonisaidi hadi umri wangu utakaposogea mbele
nilipofika std 5 hakukuwa na jinsi tena bali ni kurudi hospital na kuanza kuvaa miwani kwani tayari macho yangu yalishaanza kupoteza uwezo wa kuona bila ya masaada huo.

Sikuwa napenda kuvaa miwani kwani yalikua yakinikosesha raha na kunizuia kushiriki katika michezo mbalimbali shuleni na badala ya takecare of myself inanibidi ni takecare of my glasses,haikua rahisi.


ASANTE REA KWA MAKALA HII NZURI.KWA NIABA YA WASOMAJI WA KULIKONI UGAHIBUNI TUNAKUTAKIA HERI NYINGI KATIKA SIKU HII UNAYOSHEREHEKEA KUZALIWA KWAKO.MWENYEZI MUNGU AKUZIDISHIE KILA LILILO JEMA NA PIA TUNAKUTAKIA SWAUM NJEMA.

24 Aug 2011



PICHA ZOTE HIZI ZIMEPIGWA KATIKA KIKAO CHA BUNGE KINACHOENDELEA HUKO DODOMA.HIVI WAZIRI MZEMBE KAMA HUYU ANAYEDIRIKI KULALA OVYO OVYO HADHARANI  (BUNGENI) AKIWA OFISINI KWAKE SI NDIO ANAJIFUNIKA NA SHUKA KABISA.JE CHANZO CHA KULALA LALA OVYO KAMA TEJA NI UCHOVU NYAKATI ZA USIKU (ATUELEZE ANAKESHA AKIFANYA NINI),MARADHI KAMA SLEEPING SICKNESS AU "TEJA"?

JE INAWEZEKANA WASSIRA ALIKWENDA KWA BABU WA LOLIONDO KUSAKA TIBA YA SLEEPING SICKNESS?


KIONGOZI MCHOVU KAMA HUYU ANAPASWA KUSTAAFISHWA KWA MANUFAA YA UMMA.LAKINI INAELEKE KULALA HADHARANI NI TATIZO LINALOANZIA NGAZI ZA JUU KABISA

 NA LIMESAMBAA MIONGONI MWA VIGOGO,KAMA PICHA ZIFUATAZO ZINAVYOONYESHA (MAJI HUFUATA MKONDO)








ENEWEI,HEBU PATA UHONDOMWINGINE WA WACHAPA USINGIZI HAWA.WANASEMA RAHA YA USINGIZI IPATE MLALAJI









22 Aug 2011


Imetumwa na mdau Kato Lukaija

Wapo watu wanoamini kwamba pakipatikana suluhisho la matatizo ya biashara na uchumi kati ya bara na Zanzibar, basi kero za muungano zitakua zimekwisha. Hawa wanafanana na viongozi wetu wanaoamini kwamba muungano wa kiuchumi wa Afrika mashariki ni atua itakayotosheleza kuleta muungano wa kisiasa na kiutamaduni .Kwa mtazamo huu, uchumi ndio msingi wa kila jambo, liwe la kitamaduni,kisiasa au kitaifa. Na ndio maana nguvu zinaelekezwa zaidi kwenye diplomasia ya uchumi.

Lakini Muungano wetu,pamoja na kuunganisha uchumi wetu kwa matumizi ya sarafu moja,bado umegubikwa na hali ya kutosikilizana.Hali imekua hivyo kwa muda mrefu. Kwa hiyo kero zake,kama mijadala mingi inavyoonesha,haisababishwi na matatizo ya uchumi peke yake. Kuna tatizo la utata wa historia yenyewe ya muungano.

Kuna historia mbili za Muungano. Watu wa bara wanaona Muungano ni matokeo ya Mapinduzi ya Zanzibar yalioundoa utawala wa kitumwa wa Waarabu. Lakini nje ya madarasa rasmi ya historia hiyo,wapo vijana wanaharakati wa Zanzibar, kama Harith Ghasany,mwandishi wa KWAHERI UKOLONI,KWA HERI UHURU. Wanaharakati hawa wanadai kwamba Mapinduzi ya Zanzibar ni tunda la usuda ya Nyerere na kanisa dhidi ya waislamu na waarabu wa Zanzibar.Hivyo Muungano unaonekana kama ukoloni.

Hali hii inahitaji Wazee wakae na kukubaliana kuandika historia moja.  Wafanye kama Rais Kagame. Pamoja na kuangaikia uchumi,Kagame amehakikisha kwamba historia ya kweli ya mauaji ya 1994 ndio inayofundishwa na watu wote.Kagame anajua kwamba mtu haishi kwa mkate tu,ila kwa kila neno litokalo kwa bwana. Kwa hiyo vijana tunaomba wazee waandike historia moja tu. Wazee  wakisimamia historia moja tu, Muungano wetu utapona.

                             ------Kato Lukaija,  P.O.BOX 10351, DAR ES SALAAM.
                                         



Taarifa ifuatayo imetumwa na mwananchi aliyejitambulisha kama Msemakweli.Naiwasilisha kama ilivyo:
 Uvamizi wa wanajeshi dhidi ya wanakijiji Kimbiji ! Polisi kigamboni wamekua BUBU!hawajakubali kupokea malalamiko ya wanakijiji ! nani ? wa  kumfunga simba kengele? 
MALI NA MAKAZI YA WANAKIJIJI WAPATAO 200 Kimbiji zimeharibiwa.
 Uvamizi uliofanyika 16.08.2011 jumatano saa 4.00 hasubui wakazi kijiji cha Kimbiji,nje kidogo ya jiji la Dar,wamekuwa na mashaka ya maisha baada ya makazi na mazao yao kuharibiwavibaya na wanajeshi (JWTZ) ambao walivamia kijiji hiko na kuvunja vunja makazi ya raia..kinyume cha sheria. 
Hata hivyo baadhi ya wanakijiji walipereka taarifa katika vya  vituo vya polisi vya Kigamboni na mji mwema,havijakubali kupokea malalamiko ya wanachi walioharibiwa mali zao na kutishiwa usalama wao,hadi sasa inaonekana kuwa wanachi wa Kimbiji hawana wa kuwalinda wao na mali zao,kama inavyoeleza katiba ya nchi kuwa kila raia ana haki ya kupewa ulinzi wa maisha yake na mali zake! 
Katika Sakata hili la wanajeshi (JWTZ) kuvamia makazi ya raia na kuharibu mali za raiabado lina utata  wa nani ? kumfunga kengengele simba?


AFISA UBALOZI "USTAADH" IDRISA ZAHARANI AKIKARIBISHA WAGENI


Add caption






Salam,

Ubalozi wa Tanzania Hapa London Leo uliwaalika watanzania wote kutoka madhehebu na dini mbalimbali kuja kupata futari ya pamoja walioandaa ikiwa ni ishara njema ya kuonyesha amani,upendo, ukarimu kwa watanzania wote. Vyakula vya aina mbalimbali viliandaliwa  na vilipikwa katika hadhi ya kitanzania. Naibu Balozi Mh Chabaka aliwashuru wadau wote ambao waliweza kuja na kujumuika na kufuturu kwa pamoja. Aidha Mh Balozi aliahidi kushirikiana na watanzania kwa ukaribu zaidi katika hali na mali pia kuwaomba kutoa ushirikiano wao na ubalozi katika kuboresha mawasiliano na utendaji wa kazi ili kusukuma mbele gurudumu la maendeleo. Aliendelea kwa kusema Ubalozi upo kwa ajili yetu hivyo tuutumie ipasavyo.

Kwa niaba ya URBAN PULSE CREATIVE Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa ubalozi wetu kwa namna walivyojitolea kutengeneza futari na kuwakaribisha wadau kuja kufuturu.

Asanteni Sana,

MUNGU IBARIKI AFRICA, MUNGU IBARIKI TANZANIA

URBAN PULSE CREATIVE



BENDI ya mziki ya msondo ngoma imepata TUZO ya the Best Rhumba Group katika East Africa Music Awards mashindano yariyofanyika Nairobi Kenya na kukusanyika kwa bendi za Afrika Mashariki na bendi ya msondo kuibuka Kidedea katika mashindano hayo akisibitisha ushindi uho meneja wa bendi Saidi KIbiriti alipokuwa akiongea na Msemaji wa Bendi hiyo, Rajabu Mhamila , Super D (pichani)

Alisema wameshinda tuzo hiyo na watahakikisha wanaionesha kwa mashabiki wa bendi hiyo ili kudhirisha kuwa bendi ipo ng'ang'ari popote duniani mana bendi imekamilika kila idara alisema Super D
(pichani)

Bendi hiyo itanza mazoezi siku ya jumatatu kwa ajili ya kujiandaa na sikukuu ya Iddi inayotarajia kufanyika wiki ijayo ambapo wanaingia kambini kusuka vibao vipya ikiwemo na kuvifanyia kazi vile vya Zamani

Super D alisema bendi hiyo siku ya Iddi Mosi itapiga katika viwanja vya TTC Chang'ombe ambapo mashabiki watapata kuona tuzo hiyo ya Afrika Mashariki walioitwaa hivi karibuni na kupata fursa ya kupiga nayo picha katika viwanja hivyo

Bendi hiyo inayotamba na vibao vyake vipya vya Suluu uliotungwa na Shabani Dede na Nadhili ya Mapenzi uliotungwa na Juma Katundu

Rajabu Mhamila 'Super D'
Photojournalist at Majira, Business Times [email protected] www.burudan.blogspot.com
 Mob;+255787 406930
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania




Bondia YOhana Robart wa kambi ya Ilala akioneshana ufundi wa kutupa masumbwi na mtoto, Zainabu MHamila 'IKOTA' wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi hiyo juzi.(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com )

kondo

Kocha wa mchezo wa ngumi kondo Nassoro (kulia) akimwelekeza mtoto Zainabu Mhamila 'IKOTA' jinsi ya kutupa masumbwi wakati wa mazoezi ya kambi ya Ilala yanayoendelea katika ukumbi wa Amana CCM Dar es salaam.(Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com )
--
Super D Boxing Coach
Photojournalist at Majira, Business Times [email protected] www.burudan.blogspot.com
 Mob;+255787 406930
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.