18 Mar 2012


Nimetumiwa hii nami naiwasilisha kama ilivyo:




Ndugu Blogger, 
Husika na Kichwa cha Habari hapo juu, kwa masikitiko makubwa chanzo chetu cha ripoti kimepokea Habari ya kwamba kuna mchakato unafanyika wa kuweka usiku wa Bloggers Tanzania Lakini cha kushangaza sana usiku huo utakuwa ni usiku wa ubaguzi pia kwa maana watakao alikwa ni Bloggers wakubwa tuu wa Tanzania sasa tujiulize kwa umakini sana, Kwanza ni wakina nani hao ambao ndio wanazania kuwa ni bloggers wakubwa Tanzania, Pili tujiulize hao wanaojiita kuwa ni Mabloga wakubwa na maarufu tanzania wamechukua kigezo gani? 

Tufike mahali kwamba nyie mnao jiita bloggers wakubwa hapa nchini msiwadharau na kuwatenga hao mabloga wadogo, inasikitisha sana badala ya kuwasaidia nyie mnawakandamiza. kama mpo juu mpo juu tuu hakuna wa kuwashusha chini basi wasaidieni na hao mabloga wadogo wadogo.

Na mwisho kwa niaba ya Timu nzima inayo endelea kufuatilia kwa umakini mchakato mzima wa umoja wa bloggers Tanzania na kufuatilia kwa ukaribu na umakini vikao vya Siri na vya chini vinavyo endelea kwa ajili ya huo usiku wa bloggers, tunapenda kusema kwamba kama mpo hapa ni bora muwashirikishe na wengine email ndio hizi hizi za bloggers. Tusiwe na roho ya kwanini sote ni watanzania.

Imetolewa na 

Ripota wenu




It's like you were gone yesterday.I just can't believe that you're gone.On this day,I'd be calling you and daddy to say how much I love you,mamma.But you're not there.The only comfort I have is the strong belief that you're resting in peace.And though you're not with us on this Mother's Day,you remain the best thing God could give any son.Rest in peace,mamma.You'll always be missed and remembered!Oh! My mama, happy mother’s day
You are the greatest mother I have ever had
You are my mother today
You will be my mother tomorrow
You are always my mother
You will forever be my mother

Thank you my mother for bringing me into this world
Thank you my mother for taking care of me in your womb
Thank you my mother caring for me as a toddler
Thank you my mother for feeding me since I was a baby
Thank you my mother for all the clothes you bought for me
Thank you my mother for teaching me good manners at home

Thank you my mother for sending me to school
Thank you my mother for supervising my homework
Thank you my mother for ensuring I eat before going to school
Thank you my mother for all the regular pocket money
Thank you my mother for liking my friends
Thank you my mother for all the everyday advices

My mother always remind me that fingers are not equal
As I grow up, I have seen the correlation of this analogy
To many human beings, neighbors, societies and nationalities
Oh! My mama, thank you for your words of wisdom
My mother taught me many things that I have never read in books
Thank you my mother for all your guiding philosophies

Oh! My mama, I sincerely wish everyday could be Mother’s Day
One day in a year is not enough to thank my wonderful mother
Oh! My mama, I will forever be your child
Oh! My mama, you will eternally be my mother
Thank you my mother for being my best friend
Thank you my mother for being my trusted adviser
I honestly wish you HAPPY MOTHER’S DAY!
.Rest in Eternal Peace,mamma!

15 Mar 2012


Baada ya kulainika…Madaktari wamevuna au ‘wameliwa’?

HATIMAYE Rais Jakaya Kikwete amefanikiwa kuleta suluhisho katika mgogoro kati ya Serikali yake na madaktari waliopania kugoma wakidai maslahi bora na mazingira mazuri ya kazi. Kadhalika watoa tiba hao walikuwa wakiitaka Serikali iwawajibishe Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Haji Mponda na Naibu wake, Dk. Lucy Nkya.
Kwa upande mmoja, hatua hiyo ya Rais na madaktari ilikuwa habari njema kwa wanyonge wasio na uwezo wa kwenda India au kwingineko nje ya nchi kutibiwa.
Lakini kwa upande mwingine, habari kwamba madaktari wamesalimu amri baada ya kukutana na Rais, Ikulu, zimepokewa kwa hasira na baadhi ya wananchi ambao waliuona mgomo huo kama adhabu sahihi kwa Serikali yao ambayo kwa kiasi kikubwa inazembea kujali maslahi yao.
Binafsi, japo niliipokea taarifa hiyo ya kumalizwa mgomo kwa furaha, nafsini ninaona kama tatizo hilo limeahirishwa kwa muda tu. Wakati madaktari wanaonekana kuwa na imani kuwa Rais Kikwete atatekeleza ahadi alizowapa (pasipo kutuambia kwa nini wana imani hiyo), rekodi isiyopendeza ya Kikwete na Serikali yake katika utekelezaji wa ahadi ingepaswa kuwafahamisha madaktari hao kuzichukulia ahadi hizo za Rais kwa hadhari.
Kama nilivyowahi kuandika mara kadhaa huko nyuma, tatizo la uongozi wa nchi yetu halijawahi kuwa kwenye kutoa ahadi nzuri na zenye kutia matumaini. Viongozi wetu ni wepesi mno kuahidi mambo yaliyo ndani ya uwezo wao na hata miujiza.
Laiti madaktari wangekuwa makini, wangejiuliza kwa nini ahadi zisizoisha kuhusu utatuzi wa tatizo la mgawo wa umeme zinaendelea kuwa ahadi tu huku mgawo ukigeuka kuwa kama stahili katika maisha ya kila siku ya Mtanzania.
Kama kumbukumbu yangu iko vizuri, nadhani ahadi ya mwisho ya Kikwete kuhusu kupunguza makali ya mgawo wa umeme iliashiria tatizo hilo lingeanza kushughulikiwa Desemba, mwaka jana. Lakini ahadi kubwa zaidi ya Rais ilikuwa ile aliyotoa muda mfupi baada ya kuingia madarakani mara ya kwanza (mwaka 2005) ambayo iliishia kwa Watanzania ‘kuingizwa mkenge’ na kampuni feki ya Richmond.
Na kama Tanzania ni shamba la bibi ambapo kila mtu ana uhuru wa kuvuna asichopanda, kampuni hiyo hewa ‘ilizaa’ kampuni nyingine ya Dowans (katika mazingira yanayoleta maana ndotoni tu na si katika hali halisi). Japo inaleta uchungu mkubwa kuizungumzia Dowans na jinsi watendaji mbalimbali wa Serikali walivyosimama kidete kuitetea ilipwe japo haikutekeleza wajibu wake, sakata hilo linashabihiana na maisha ya kawaida ya Mtanzania kwenye ‘kona za uswahilini’ ambapo si jambo la ajabu kwa vibaka kukupora kisha kukupigia kelele za ‘mwizi….mwizi.’ Kinachofuatia hapo ni ‘maumivu mengine’ ya kipigo kutoka kwa wananchi walioamini hadaa za vibaka hao kuwa wewe uliyeporwa ndiye mwizi uliyewapora vibaka hao.
Waingereza wanasema the end justifies the means, yaani; ‘mwisho (wa jambo) huhalalisha njia (iliyotumika kufikia mwisho huo).’ Kwa mantiki hiyo, jitihada za Kikwete zilizofanikiwa kuwalainisha madaktari kutoendelea na mgomo zinahalalisha hatua hiyo.
Lakini suala la msingi hapa si uhalali wa hatua hiyo ya Kikwete na madaktari kuafikiana nae, au hata suala zima la mgomo. Na katika suala la mgomo ni vigumu kuona uhalali wa hatua ambayo kimsingi ingewaumiza wanyonge ambao hata pale huduma za afya zinapopatikana inawawia vigumu kumudu gharama za kupata huduma hizo.
Katika stadi za mantiki, ili jambo liwe halali ni lazima lionekane kuwa halali. Kwa mgomo huo, japo ilikuwa halali kwa madaktari kudai maslahi na mazingira bora ya kazi lakini uhalali wa njia waliyotumia kudai haki yao uliathiriwa na ukweli kwamba mgomo wao ulikuwa na madhara makubwa zaidi kwa wasiohusika (yaani wananchi wa kawaida ambao kimsingi hawahusiki na sababu za uduni wa maslahi na mazingira ya kazi ya madaktari hao).
Lakini hata tukiweka kando suala la uhalali, bado inanitatiza kuelewa madaktari wamepata nini katika mgomo wao wa kwanza na hatua yao ya majuzi kuamini ahadi za Kikwete.
Japo mgomo wa kwanza ulichangia Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Blandina Nyoni na Mganga Mkuu, Deo Mtasiwa kusimamishwa kazi, sitaki kuamini kuwa harakati hizo zilizogusa hisia na uhai wa kila Mtanzania zililenga tu kuona viongozi hao wawili wakisimamishwa (na si kufukuzwa) kazi.
Tangu mwanzo madaktari hao waliitaka Serikali kuchukua hatua dhidi ya Mponda, Nkya, Nyoni na Mutasiwa lakini hadi sasa inaonekana wazi kuwa Serikali haipo tayari kuwatoa rehani waziri na naibu wake.
Na hili liliwekwa bayana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliyeweka wazi msimamo wa Serikali kuwa “kama kugoma basi (madaktari) tu lakini Serikali haiwezi kushinikizwa kuwafukuza kazi Waziri na Naibu wake kwa mgomo.”
Nimebainisha hapo juu kuwa binafsi nahisi suala hili limeahirishwa tu kwa sababu historia ina muhukumu Kikwete linapokuja suala la utekelezaji ahadi, hata zile anazotoa pasipo haja ya kuzitoa.
Hivi madaktari wamesahau ile kauli maarufu ya Kikwete kuwa; anawafahamu wala rushwa lakini anawapa muda tu wa kujirekebisha, na wasipofanya hivyo watagundua kuwa tabasamu lake halimaanishi huruma kwa wazembe na wababaishaji?
Au madaktari wameshasahau kioja alichotoa Rais Bandari ya Dar es Salaam, alipotamka kuwa anawafahamu kwa majina wanaofanya ufisadi bandarini hapo na angeyawasilisha kwa uongozi ili wachukuliwe hatua, lakini hakufanya hivyo hadi leo.
Waingereza wana busara moja isemayo; “The minute you settle for less than you deserve, you get even less than you settled for,” yaani-kwa tafsiri isiyo rasmi- unapokubali ‘yaishe’ licha ya upungufu, utaishia kupata pungufu zaidi ya kile ulichokubali.
Licha ya ukweli kuwa wao ndio waathirika wakubwa, wananchi wengi walikuwa upande wa madaktari kwa maana ya kuunga mkono hoja zao. Mtego waliojiingiza watoa tiba huo ni huu: wakikurupuka tena kutishia kugoma kwa madai kuwa Rais Kikwete aliwalaghai, wataishia kuonekana wababaishaji wasio na msimamo, na pengine wananchi wataamua kuwapuuza na kuwaona kama ‘kundi linalotaka kuweka rehani uhai wa wanyonge.’
Lakini hata tukiamua kuamini kuwa ahadi za Rais kwa madaktari hao ni za dhati, hizo fedha za kuwatimizia madai yao zitatoka wapi? Hapa sina maana kuwa hakuna njia za kupata fedha za kushughulikia madai hayo, bali ukweli ni kwamba Serikali ya Kikwete ina rekodi nzuri ya matumizi ya anasa yasiyoendana na hali mbaya ya uchumi wetu.
Sidhani kama kuna mtu yeyote (pamoja na madaktari) anayedhani Rais yupo tayari kupunguza safari zake za nje ya nchi ili kuokoa fedha japo kidogo kuanza kushughulikia matatizo ya madaktari hao. Na sitaki kabisa kuamini Serikali ya Kikwete iko radhi kuendesha kampeni za CCM huko Arumeru Mashariki kwa ‘kuuza sera’ pekee bila kumwaga fedha kwa wapiga kura (fedha ambazo zingeweza kuanza kutatua kero za madaktari hao).
Pengine gumu zaidi katika utekelezaji wa ahadi hiyo ya Rais kwa madaktari ni ukweli kuwa, pindi Serikali ikianza kutoa fedha za kutatua matatizo ya madaktari kuna uwezekano mkubwa wa watumishi wa kada nyingine kuanza shinikizo la kudai ‘watendewe haki kama madaktari.’
Kama nilivyobainisha katika makala yangu ya wiki iliyopita, kilio cha madaktari kuhusu maslahi na mazingira bora ya kazi ni kiwakilishi tu cha tatizo linalowakabili watumishi wengine wa umma na wananchi wengi kwa ujumla.
Ni wazi kuwa kama Serikali itaamua kupunguza matumizi ya anasa na kushughulikia madai ya madaktari hao, kuna uwezekano wa watumishi wengine wa umma kupata funzo kutoka katika mgomo wa madaktari kuwa ‘ukigoma utaitwa Ikulu, na Rais atatumia nguvu zake kutatua matatizo husika.’
Mwisho, inakera kuona Serikali iliyojaa mawaziri lukuki (ambao wanaongeza mzigo wa gharama za kuwahudumia) inashindwa kupata ufumbuzi wa kundi moja la watumishi wa umma hadi kulazimu Rais aingilie kati.
Tuna Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, mawaziri na manaibu wao kibao (huwezi kukumbuka majina yao wote pasipo kuwa na orodha yao mkononi), na mlolongo wa makatibu wakuu na wakurugenzi wa wizara lakini inabidi kumsubiri Rais ndipo ufumbuzi wa tatizo upatikane.
Anayestahili lawama kubwa si watendaji hao bali aliyewateua. Sote tunafahamu kuwa Rais hakuwahi kushikiwa mtutu wa bunduki ili ateue watendaji ambao sio tu ni wengi bali wengi wao ni kama bado wapo kwenye sherehe za kujipongeza kwa kuteuliwa kwao na Rais, huku baadhi yao wakiwa kama hawajui kwa nini Rais aliwateua.
Na kwa mazingira haya ya lundo la wasaidizi wasio na msaada wa maana kwa Rais, Serikali na umma kwa ujumla, sio tu tutaendelea kushuhudia madaktari, watumishi wengine na wananchi kwa ujumla wakiingia kwenye mgogoro na Serikali kudai uwajibikaji bali pia tutasikia sana vioja kama hivyo vya Naibu Waziri aliyeibiwa hotelini katika mazingira ya kutatanisha.
Utitiri wa viongozi wasio na cha kufanya unaweza kabisa kusababisha waishie kuwa vituko ili angalau majina yao yasikike na ijulikane kuwa wapo kazini.


13 Mar 2012

Your dad would have  probably sang the following song for you.Now you can sing it for kijana wetu.As Big Will raps,I think sometime you wonder what our dogo will turn out to be when he grows up.."a general,a doctor,or may be an MC (like you his dad)..."

And we all gave some hard time to our moms.It's time to appreciate how they raised us and all the pain we gave them

And these are my special messages for your special day.First,we all have dreams...

And we all know we can be what we gonna be if we work hard at it...

And you know what,the stuff we frequently talk on Twitter makes us like the street radio for unsung heroes..WE DO FOR THE PEOPLE

And although it's hard knock life out there

But hey,it's you big day...we the last ones left...and life should go on

Any birthday is party

And in the evening...enjoy your big day as if it's FIESTA

12 Mar 2012



Time to reap what you didn't sow.Come elections,and had it been a husband,CCM could have easily let other men sleep with his wife simply to get their votes...what a useless party!

11 Mar 2012

The Rajapaksa Brothers

The end of the Sri Lankan civil war in the spring and summer of 2009 included a massive genocide perpetrated by the government. About 200,000 Tamil civilians (along with a small number of Tamil Tiger terrorists) were backed into a plot of land about the size of Central Park with the Indian Ocean on one side and the military on the other. The government won the battle against the terrorists, but they killed as many as 40,000 civilians in the process. The two key leaders of the operation were Sri Lankan President Mahinda Rajapaksa and his brother, defense minister Gotabaya Rajapaksa. There have been no war crimes investigations, no truth commissions, and no reckoning for their heinous crimes. —Mark Leon Goldberg



Nuon Chea

"Brother Number Two" and chief ideologue Chea never achieved the same level of popular infamy as his friend and longtime associate Pol Pot. But as the Khmer Rouge's idea man and chief of the party's security committee, Chea was responsible for many of the offensives during the Cambodian communist revolution that killed more than 2.5 million by mass execution, starvation, and overwork.

Chea oversaw the infamous S-21 torture prison in Phnom Penh, from which only 14 of 14,000 alleged enemies of the administration came out alive. According to journalist Nate Thayer, Chea personally received information on every person who came through S-21, ordering them killed after extracting information from them. Now on trial as part of the lumbering Khmer Rouge War Tribunal, Chea has blamed Vietnam, party infiltrators, and others' mistakes for the bloodshed and misery of the Khmer Rouge era. —Faine Greenwood



Ahmed Haroun

His boss, Sudanese President Omar al-Bashir, takes most of the heat, but Haroun is the guy Bashir turned to when he needed to suppress a revolt in Darfur. As a government minister in charge of the "Darfur Security Desk" in 2003 and 2004, he masterminded a brutally effective effective strategy of counterinsurgency-by-genocide. These days he's the governor of the Sudanese state of South Kordofan. Guess what's happening there? —Mark Leon Goldberg



The Haqqani family

Dubbed the "Sopranos of the Afghanistan war" by The New York Times, the Haqqanis are a terrifying menace to Afghan civilians and aid workers. This hybrid mafia-insurgent group commands thousands of fighters in Afghanistan and Pakistan, controls a vast empire of thriving criminal enterprises, trains children to be suicide bombers, and masterminds many of the country's most appalling crimes against civilians. —Una Moore



Bosco Ntaganda

Ntaganda, a Rwandan Tutsi formerly of the Rwandan Patriotic Army, was chief of military operations for the Union of Congolese Patriots (see first slide) from the late 1990s until 2006, when he became military chief of staff of a different militant group, the National Congress for the Defense of the People. Ntaganda, who is known as "The Terminator," has been wanted by the International Criminal Court since 2006 for crimes committed while a commander in the armed wing of the UPC.




Thomas Lubanga Dyilo

This Congolese militia leader is little-known, but he was the first-ever defendant at the International Criminal Court. He is accused of recruiting an army of child soldiers (sound familiar?), then unleashing them on civilian populations in the Ituri province of Eastern Congo. Video evidence presented in court shows him giving marching orders to kids that appeared to be no older than 13. The ICC is scheduled to hand down his verdict on March 14—he is expected to be convicted, but there's no guarantee due to prosecutorial mishaps in the case. —Mark Leon Goldberg

Source: GOOD: News

10 Mar 2012


FRIDAY, MARCH 9, 2012

Mamlaka ya Urais yawezeshe uwajibikaji kumaliza mgogoro wa Serikali na Madaktari


Jana tarehe 8 Machi 2012 asubuhi nilitoa tamko kwa niaba ya CHADEMA la kutaka kauli ya haraka ya Rais Jakaya Kikwete ya kutengua uteuzi wa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hadji Mponda na Naibu Waziri wa wizara husika Dk. Lucy Nkya kutokana na udhaifu wao mkubwa wa kiongozi waliouonyesha katika kushughulikia mgogoro wa madaktari ambao umedumu kwa muda wa takribani miezi miwili. 

Nilieleza kusitikitishwa na ukweli kwamba Rais Kikwete toka mgogoro utokee hajatumia ipasavyo mamlaka yake ya kikatiba kwa mujibu wa ibara ya 34 na 35 na tarehe 5 Februari 2012 aliahidi kwamba atazungumzia kwa kina suala la mgomo wa madaktari lakini badala yake akalizungumza kwa ufupi tarehe 29 Februari 2012 katika hotuba yake kwa taifa bila kuchukua hatua za msingi hali inayoashiria ombwe la uongozi. 

Nilieleza kuwa iwapo Rais Kikwete haitatoa kauli viongozi wakuu wa CHADEMA wataeleza hatua za ziada ambazo chama kitachukua kuiwajibisha serikali. Jioni Serikali ilieleza kuwa leo Rais angezungumza na wazee wa Dar es salaam, na leo imetolewa taarifa kuwa atazungumza nao kesho.

Jana usiku na leo asubuhi masuala kadhaa yameendelea kuhusu mgogoro huu, mosi; hukumu ya mahakama ya kazi, pili; uamuzi wa serikali na wadau wake kufanya propaganda dhidi ya madaktari tatu; uamuzi wa serikali kufanya mawasiliano na uongozi wa madaktari.

Mkakati wa kufanya propaganda hautaisaidia Serikali badala yake iwekeze katika mawasiliano na uongozi wa madaktari kabla ya Rais kuzungumza ili Rais atoe kauli baada ya kuchukua hatua za msingi ikiwemo za kuwezesha uwajibikaji wa viongozi waliotajwa na pia kuanza kushughulikia madai ya madaktari na yale yanayohitaji kuingizwa kwenye bajeti kuwe na makubaliano ya utekelezaji. 

Izingatiwe kwamba matatizo ya Wizara ya Afya pamoja na udhaifu wa kiutendaji yalichangiwa pia na ufinyu wa bajeti, na bajeti husika iliandaliwa na serikali na kupitia kwenye baraza la mawaziri ambalo Rais ni mwenyekiti wake kabla ya kuletwa bungeni na wengine tuliipinga tukitaka fedha zitoke kwenye matumizi mengine ya anasa na kuelekezwa kwenye huduma muhimu za kijamii. 

Pia; kutokana na matatizo katika serikali kwenye wizara mbalimbali yenye madhara ya kiuchumi, kisiasa na kijamii katika taifa tunasisitiza umuhimu wa Rais Kikwete kulivunja baraza la mawaziri ili kufanya mabadiliko ya kimsingi ya kuongeza uwajibikaji kama ilivyoazimiwa pia na kamati kuu ya CHADEMA katika mkutano wake wa tarehe 3 na 4 Machi 2012.

Tarehe 7 na 8 Machi 2012 Waziri Mkuu Mizengo Pinda kwa mara nyingine tena alitoa taarifa kinyume na kauli za awali za tarehe 9 Februari 2012 ambazo badala ya kushughulikia vyanzo vya mgogoro vimeendeleza mgogoro na kusababisha mgomo mwingine wa madaktari wenye athari kubwa kwa wananchi.

Ndio maana nikatoa kauli ya kumtaka Waziri Mkuu kuweka wazi kwa umma taarifa ya uchunguzi uliofanywa na serikali kuhusu tuhuma dhidi ya viongozi wakuu na watendaji waandamizi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, na kushughulikia madai ya msingi ya madaktari. 

Aidha, pamoja na kuunganisha nguvu za pamoja kuhakikisha mgomo unakwisha ili kuepusha athari zaidi kwa umma, ni muhimu hatimaye tathmini huru ikafanyika kuhusu matokeo ya mgogoro na mgomo toka ulipoanza mpaka sasa ikiwemo kueleza wazi idadi ya vifo vilivyotokea na madhara yaliyojitokeza katika hospitali za umma tofauti na kauli potofu iliyotolewa bungeni tarehe 3 Februari 2012 na Waziri husika.

Rais Kikwete alipaswa kabisa kuchukua hatua kuiongoza serikali kufanya maamuzi ya msingi mara baada ya matokeo ya kikao kati ya ujumbe wa Serikali ulioongozwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda na wanataaluma wa kada ya afya sanjari na mkutano kati ya madaktari na wawakilishi wa kada nyingine za sekta ya afya katika utumishi wa umma vilivyofanyika tarehe 9 Februari 2012; kwa kuzingatia pia ushauri tuliotoa tarehe 10 Februari 2012.

Kwa upande mwingine, jana nilirudia kutoa mwito tuliotoa tarehe 30 Januari 2012 kwa TUGHE, MAT na kamati ya muda ya madaktari kuendelea kutoa ushirikiano unaostahili kwa chama, kambi rasmi ya upinzani na wadau wengine ili kuweza kuunganisha nguvu ya pamoja katika kushughulikia madai ya msingi ya madaktari yenye kuathiri sekta ya afya nchini na maisha ya wananchi kwa ujumla. 

Naendelea kuwashukuru wanaharakati kwa kuunganisha nguvu katika kutaka uwajibikaji wa viongozi wa serikali katika kushughulikia mgogoro na madaktari na kinaitaka Serikali kuacha vitisho na matumizi makubwa ya vyombo vya dola kwa madaktari na makundi mengine katika jamii yanapotumia uhuru wa kikatiba kwa kukusanyika, kujadiliana na kuhoji kuhusu uwajibikaji wa serikali na viongozi wake kwa kuzingatia ibara za 8, 18 na 20 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rais Kikwete anapaswa baada ya mawasiliano yanayoendelea kutoa hotuba yenye kuleta matumaini badala ya kurudia tena maelezo yasiyoridhika kama yale yaliyotolewa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda tarehe 9 Februari 2012 na 7 na 8 Machi 2012 kuhusu namna ambavyo imeshughulikia mgogoro huu na madai ya madaktari, watumishi wengine wa umma katika sekta ya afya nchini pamoja na uboreshaji wa huduma katika hospitali, zahanati na vituo vya afya nchini.

Narudia kutoa rai kwa wananchi kuendelea kuunga mkono madai ya msingi ya madaktari ili kuhakikisha kwamba hospitali za umma nchini zinakuwa mahali salama kwenye huduma bora za kulinda maisha ya wananchi hususan wasio na uwezo wa kudumu gharama za matibabu katika hospitali binafsi za ndani na nje ya nchi. 

Pamoja na madai ya maslahi ya madaktari ambayo ni kwa maslahi ya umma, madaktari wanataka pia serikali ichukue hatua za kuboresha huduma za afya. Serikali inaingia gharama kubwa kupeleka baadhi ya watanzania wengi wao wakiwa viongozi kwenda kutibiwa nje ya nchi huduma katika hospitali za umma zinazidi kuzorota kutokana na ukosefu wa madawa, vifaa tiba na wataalamu wa kutosha katika hospitali za umma. 

Aidha, serikali inashindwa kuipa kipaumbele sekta ya afya kwa kisingizio cha kutokuwa na uwezo wakati ambapo inafanya matumizi mengine ya anasa kwa kiwango kikubwa kama ilivyokuwa katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru. Serikali inachelewa kushughulikia madai ya posho za madaktari kama nyongeza ya posho ya kulala kazini (on call allowance) na posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (risk allowance) wakati huo huo serikali hiyo hiyo inazungumzia nyongeza ya fedha katika matumizi mengine ya serikali yasiyokuwa ya lazima. Serikali ishughulikie vyanzo vya migogoro ya kijamii badala ya matokeo.

MTEMBELEE MHESHIMIWA MNYIKA KATIKA BLOGU YAKE INAYOPATIKANA http://mnyika.blogspoti.com.PIA UNAWEZA KUMFUATA TWITTER www.twitter.com/jjmnyika NA UKURASA WAKE WA FACEBOOK NI http://www.facebook.com/pages/John-Mnyika/113913842009362


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.