8 Mar 2014

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

7 Mar 2014


I wish you luck, happiness and riches today, tomorrow and beyond.
As you look back on yesterday, may your memories be warm ones. As you celebrate today, may your heart be filled with happiness and joy. As you look ahead to tomorrow, may your deepest hopes and dreams come true for you!
I wish you to celebrate all the wonderful things that make you so special, not just on your special day, but on every day of the year!
I wish that for every extra candle on your cake, you receive an extra reason to smile. 
Happy Birthday to you!
happy birthday wishes pictures


MWISHONI mwa wiki iliyopita kulijitokeza malumbano makali, hususan katika mtandao wa kijamii wa Twitter, kuhusu suala la ushoga.
Sina hakika mjadala huo ulianza vipi lakini ninadhani kwa upande mmoja ulichochewa na sakata linaloendelea kati ya serikali ya Uganda na baadhi ya nchi za Magharibi baada ya Rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni, kusaini muswada unaopiga marufuku ushoga kuwa sheria inayoambatana na adhabu kali. Kwa upande mwingine, nahisi mjadala huo ulichangiwa na majadiliano yanayoendelea katika Bunge la Katiba huko Dodoma, ambapo suala la haki za mashoga limejichomoza.
Kwa upande wa Bunge la Katiba, kuna tuhuma kuwa ‘ajenda ya ushoga’ imeletwa makusudi kwa minajili ya kuepesha (divert) mtizamo wa Watanzania katika ‘masuala ya msingi zaidi’ yanayopaswa kujadiliwa katika Bunge hilo maalumu.
Lakini pengine kabla sijaingia kiundani katika mada hii ni vema nikaweka bayana msimamo wangu kuhusu suala hili la ushoga. Huko nyuma niliwahi kuandika makala iliyozungumzia mjadala wa ushoga, makala iliyobeba kichwa cha habari “Tatizo ni unafiki wetu, sio ushoga.”
Hoja kubwa ya ‘wapinzani wa haki za mashoga’ ni kwamba suala hilo haliendani na mila na desturi zetu. Lakini kabla ya kwenda mbali, hivi hizo mila na desturi zetu ni zipi hasa? Mara kadhaa tumekuwa tukiwalaumu ‘wazungu’ kwa kuiangalia au kuizungumzia Afrika kana kwamba ni kijiji kimoja kikubwa kinachoundwa na familia moja kubwa. Wengi wetu tumekuwa mahiri kuwakumbusha ‘wazungu’ kwamba Afrika ni mkusanyiko wa mataifa zaidi ya 50, na ndani ya mataifa hayo kuna makabila lukuki yenye mila na desturi tofauti.
Sasa tukirejea kwa Tanzania yetu, hivi ‘mila na desturi za Kitanzania’ ni zipi hasa? Naomba ieleweke kwamba sikatai kwamba tuna mila na desturi bali ninapata shida kuelewa hizo ‘mila na desturi za jumla’ zinazofuatwa na kila Mtanzania.
Kuna hoja nyingine inahusu imani za kidini, kwamba “katika dini zote, ushoga ni haramu.” Tunarejea palepale. Kwa sababu dini fulani zinasema kitu hiki ni haramu haina maana basi kila mtu (asiye muumini au hata muumini wa dini hiyo) lazima aafiki mtizamo huo. Tukumbuke kuwa dini ni imani, na imani hailazimishwi. Sasa kwa vile Tanzania yetu si nchi ya kidini, japo wengi wa Watanzania wana dini, kinachotakwa haramu katika dini fulani si sheria inayopaswa kufuatwa na kila Mtanzania.
Maana kama kila matakwa ya dini lazima yafuatwe kama sheria ya nchi, hali itakuwaje katika suala kama la ulaji wa nyama ya nguruwe ambayo ni ruhusa kwa Wakristo lakini ni haramu kwa Waislamu? Tupige marufuku ulaji wa nyama ya nguruwe kwa vile ni haramu kwa Waislamu au turuhusu kwa vile ni halali kwa Wakristo? Usuluhishi unapatikana katika busara za kutambua haki na wajibu: uhalali usikwaze haramu na haramu isikwaze halali.
Wakati mjadala huo wa ushoga unaendelea huko Twitter, muungwana moja alinihoji iwapo msimamo wangu kuhusu haki za mashoga unatokana na uwepo wangu huku Uingereza. Nikamjibu kuwa mie ni muumini wa haki za binadamu, na haki hizo ni pamoja na za mashoga.
Mwingine akaenda mbali na kuhoji iwapo nami ni shoga eti kwa sababu ninawatetea sana. Nilimuuliza, hivi tunavyopambana dhidi ya ujangili na kupigania haki za uhai wa tembo wetu, kwa mfano, basi nasi ni tembo?  Kuna vijana wanaopigania haki za wazee, wasio na ulemavu wanaopigania haki za walemavu, na wanaume wanaopigania haki za wanawake. Ni suala la imani.
Ninaendelea kuamini kuwa kwa mtu ambaye si shoga, sioni kwanini asumbuliwe na haki za mashoga. Ni haki za mashoga, sio za wewe usiye shoga. Kwanini basi zikusumbue? Oh dini yako inakataza. Sawa, lakini dini fulani inakataza kula nguruwe lakini yako inaruhusu. Oh mila na desturi zinakataza, vipi kwa asiyehusika na mila na desturi hizo?
Waingereza wana msemo ‘two wrongs don’t make a right’ ambao kwa tafsiri isiyo rasmi ni unamaanisha ‘kwa vile kosa la kwanza limeachwa kama si kosa, haimaanishi kosa la pili nalo liachwe pia.’  Msemo huu unatumika sana dhidi ya wanaohoji “kwanini hizo mila na desturi zikumbukwe kwenye suala la ushoga pekee na sio dhidi ya ufisadi, biashara ya dawa za kulevya, ukahaba na mengine kama hayo?”
Wapinzani wa haki za mashoga wanadai “kwa vile hatutilii mkazo kuhusu imani za dini zetu na mila na desturi zetu kupambana na maovu mbalimbali katika jamii, haimaanishi tusikemee ushoga.” Sawa, lakini haki za mashoga zinachangia vipi uwepo wa mgawo wa umeme usiokwisha? Au mashoga wanachangiaje kushamiri kwa biashara ya dawa za kulevya? Na ni kwa vipi mashoga wanahusika na kuzaliana kwa kasi kwa matapeli wa kisiasa katika mfumo wa siasa wa nchi yetu?
Ninatambua kuwa msimamo wangu katika suala hili sio popular (unaoafikiwa na wengi). Ninatambua pia kuwa kuna wasomaji watakaoniona mtu wa ajabu kabisa kwa kutetea haki za mashoga. Ninahisi pia kuna watakaodhani kuwa labda ‘nimechanganyikiwa.’ Sina tatizo na mtizamo huo kwa sababu ni matumizi ya haki na uhuru wao. Na ndio moja ya faida kubwa za haki na uhuru: kufanya hata kile ambacho mtu mwingine hakiafiki. Sasa, kama sio tu tunapenda haki na uhuru, kwanini tuchukie vitu hivyo hivyo kwa wenzetu?
Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha Watanzania wenzangu kuhusu ukweli huu ambao pengine ni mchungu kwa wapinzani wa haki za mashoga: Sio tu kwamba Tanzania yetu ina mashoga bali pia kasi ya kukua kwa ushoga ni kubwa. Na hata miongoni mwa wapinzani wa ushoga kuna mashoga pia lakini wanaotumia fursa hiyo ya kupinga ushoga kwa minajili ya kuficha ‘siri’ yao. Tunaweza kuendelea kudai ‘ushoga ni haramu...mila na desturi zetu zinapinga ushoga...” lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa ushoga upo na mashoga wapo.
Wito wangu kwa ‘wapinzani’ wa ushoga sio wabadili mtizamo wao bali kama kweli wanaoongozwa na dini au mila na desturi kupinga ‘laana’ ya ushoga, basi ni vema pia wakielekeza hasira zao dhidi ya majanga ya kitaifa kama vile ufisadi na biashara ya madawa ya kulevya, sambamba na usaliti katika uhusiano au ndoa (suala maarufu la ‘nyumba ndogo’ na ‘mambo mengine yasiyofaa.’

- See more at: http://www.raiamwema.co.tz/uhalali-usikwaze-haramu-na-haramu-isikwaze-halali#sthash.tuSqf3kJ.dpuf

6 Mar 2014

Wakati haijafahamika nani aliyelipwa mabilioni ya shilingi yaliyokuwa kwenye akaunti ya Escrow katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kutokana na mvutano baina ya Tanesco na Kampuni ya IPTL, imebainika kuwa Bunge liliwahi kuagiza fedha hizo zisichukuliwe mpaka mitambo ya IPTL itakapokuwa chini ya Tanesco mwakani.
Hiyo imo katika taarifa ya iliyokuwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2007.
Hata hivyo, Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu alithibitisha jana kuchotwa kwa Dola za Marekani 122 Milioni (Sh195.2 bilioni) katika akaunti hiyo, lakini akakataa kutaja nani hasa aliyelipwa.
Mkataba wa miaka 20 baina ya IPTL na Tanesco ulisainiwa mwaka 1995 na ulitakiwa kuisha 2015 na mitambo hiyo kuwa mali ya Tanesco.
Hata hivyo, ukiwa umebaki mwaka mmoja kumalizika, imebainika kuwa mitambo hiyo imeuzwa kwa Kampuni ya Pan African Power, ambayo inatarajiwa kuingia mkataba mwingine na Tanesco ili iwauzie umeme.
Ndulu alisema fedha zilizokuwa kwenye akaunti hiyo ni Dola za Marekani 22 milioni na Sh161 bilioni za Tanzania ambazo zote kwa pamoja ndizo zilizofikisha jumla ya Sh195.2 bilioni.
Vyanzo vingine vilitoa takwimu mbili tofauti, kimoja kikisema kiasi cha fedha hizo kilifikia Dola za Marekani 270 milioni na kingine Dola 250 milioni. Kuhusu nani mwenye mamlaka ya kutoa fedha hizo, Profesa Ndulu alisema kwa mujibu wa mkataba wa kufunguliwa kwa akaunti ya fedha hizo, ni Wizara ya Nishati na Madini pamoja na IPTL.
“Hakuna mtu mwingine anayeweza kuidhinisha kutolewa kwa fedha hizo zaidi ya hao, kwa hiyo hao ndiyo waliosaini kutolewa kwa hizo fedha na taratibu zote zilifuatwa,” alisema Profesa Ndulu.
Alipoulizwa ni nani aliyelipwa fedha hizo, Profesa Ndulu alisema IPTL ndiyo iliyokuwa na mamlaka ya kusema ni nani alipwe na ilifanya hivyo.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alipoulizwa juu ya fedha hizo alisema: “Kwa kawaida huwa nina majibu mafupi sana, lakini kwa kuwa mmeamua kuandika uongo, endeleeni, siwezi kukujibu chochote wasiliana na hao IPTL wakujibu.”
Hata hivyo, haikuwa rahisi kumpata kiongozi wa IPTL kuzungumzia suala hilo kwa kuwa tayari kampuni hiyo ni mufilisi.
Msimamo wa Bunge
Ripoti ya POAC inasema Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) aliorodhesha matatizo ya mkataba kati ya Tanesco na IPTL na kuangalia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mipango ya kununua mitambo hiyo na kuibadilisha iwe inatumia gesi badala ya mafuta mazito.
“Mgogoro uliopo hivi sasa kati ya Tanesco na IPTL unahusu kiwango cha malipo ya uwekezaji yaani capacity charges ambacho IPTL walikuwa wanalipwa na Tanesco. Kwa mujibu wa mkataba huo, capacity charge inapaswa kukokotolewa kwa kuzingatia mtaji wa asilimia 30 na mkopo wa asilimia 22.31.
Baada ya uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa, ilikubalika kuwa mtaji uliowekezwa uwe ni Dola za Marekani 36 milioni.
Hata hivyo, baada ya uchunguzi wa Tanesco iligundulika kuwa IPTL haikuwekeza fedha hizo, bali Sh50,000,” inasema ripoti hiyo.
Ilisema kuwa, mpaka kufikia Mei 2008, Tanesco ilikuwa imeilipa IPTL Sh221 bilioni tangu ilipoanza uzalishaji umeme Januari 2002.
Kamati iliagiza: “Wanasheria wa Tanesco na Serikali watumie ushahidi wote uliopo kuhakikisha kuwa kiwango cha fedha kilichopo kwenye akaunti maalumu (Escrow) ndicho hichohicho kitumike kumaliza madeni yaliyopo na vilevile kufanyia marekebisho mitambo hiyo ili itumie gesi,” inasema taarifa hiyo.
Pendekezo hilo lilipitishwa na Bunge huku POAC ikitoa maelekezo kwa Gavana Ndulu kuwa fedha zilizopo Escrow zisitumike kwa namna yoyote ile bila mitambo ya IPTL kuwa ya umma na kubadilishwa na kutumia gesi asilia.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa POAC, ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe alisema ameshtushwa na taarifa za kutolewa kwa fedha hizo kinyemela.
“Tunaitaka Serikali kutoa taarifa kama kweli hizo fedha zimetolewa, kwa sasa siwezi kutoa msimamo wetu kwa kuwa hatujakaa kama kamati, tunatarajia kuitisha kikao cha dharura Dodoma kuzungumzia suala hili,” alisema Zitto.
 CHANZO: Mwananchi




 
Mshindi wa kura za maoni za kugombea ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete amesema siasa anazofanya sasa hazina uhusiano wala ubia na baba yake.
Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kutangazwa kwa matokeo ya kura za maoni za chama hicho katika jimbo hilo kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Msata alisema anafanya siasa kwa maisha yake na si kwa mgongo wa baba yake kwani aliingia katika siasa akiwa na umri wa miaka mitano na hakuwahi kufanya hivyo kwa sababu ya baba yake.
“Siasa ninayofanya haina uhusiano na baba yangu, nafanya siasa kwa maisha yangu na sina ubia na baba yangu katika hili” alisema mtoto huyo wa Rais Jakaya Kikwete.
Akijibu swali la kwa nini amejiingiza katika siasa tofauti na maneno yake aliyowahi kutamka mwaka 2010 kuwa hawezi kushiriki katika kinyang’anyiro cha ubunge katika jimbo hilo, Ridhiwani alisema wakati huo hakuwa tayari.
“Kwenye siasa usiwe muwazi katika kila kitu, ukiwa hivyo unawapa nafasi maadui kukushambulia, mimi hapa Chalinze ni kwetu, kwa wazazi wangu na kule Bagamoyo tunakwenda tu kikazi na ndiyo maana nikaamua kurudi nyumbani kuomba ridhaa. Nashukuru kuongoza katika kura za maoni ninaona ni kiasi gani ninaungwa mkono,” alisema.
Katika kura hizo za maoni Ridhiwani alibuka mshindi kwa kura 758, akifuatiwa na Imani Madega aliyepata kura 335, Ramadhan Maneno (206) na Mkwazu Changwa (17).
Kamati Kuu ya CCM (CC), inatarajiwa kukutana Machi 8, mwaka huu kupitisha jina mgombea wake wa ubunge katika jimbo hilo nafasi ambayo iliachwa wazi na Said Bwanamdogo aliyefariki dunia Januari 22, mwaka huu.

 
Wanasayansi wanadai kuwa wamefanikiwa kuwadunga waathirika 12 wa Ukimwi viini vya kinga ambavyo vina uwezo wa kuzuwia virusi vya ugonjwa huo. Watafiti wanadai kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kuelekea kwenye matibabu kamili ya Ukimwi, ugonjwa unaomlazimu mwathirika kutumia vidonge vya kupunguza makali kwa muda wote wa uhai wake.

"Hii inaimarisha imani yetu kwamba viini vya aina ya T (T cells) vilivyorekebishwa ni ufunguo muhimu katika kuondoa haja ya mwathirika wa Ukimwi kuhitaji dawa kwa muda wote wa uhai wake..." alieleza Dkt Carl H. June, Profesa wa Richard W. Vague katika tiba za kinga katika Idara Tiba na Matibabu na Dawa za Maabara , Shule ya Madawa ya Penn's Perelman huko Philadelphia nchini Marekani.

Watafiti walitumia teknolojia inayojulikana kama "zinc finger nuclease" (ZFN)- waliyoielezea kama 'mkasi wa kimolekyuli kurekebisha viini vya T katika mfumo wa kinga mwilini ili kuiga kuongezeka kwa CCR-5-delta-32, viini vinayofahamika kwa kuwafanya baadhi ya watu wasipate Ukimwi.

Soma habari kamili HAPA (na usisite kuwasiliana nami iwapo utahitaji tasfiri)

5 Mar 2014

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
mg23-w480-h580
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.