20 Sept 2011


Kama ilivyozoeleka,blogu hii inaelemea zaidi katika masuala ya siasa.Lakini kuna nyakati ninajaribu kuangalia nyanja nyingine za maisha katika jamii.Na kwa bahati nzuri kabla ya kuzamia kwenye Siasa kitaaluma nilikuwa mwanafunzi wa Sosholojia (ndio mchepuo niliosoma katika Shahada ya Kwanza hapo Mlimani).

Ninajaribu kuanzisha utaratibu ambapo angalau mara moja kwa wiki nitajadili mada ya kijamii,hususan masuala ambayo ni ya kibinafsi zaidi kama vile mahusiano,mapenzi,nk.Nakaribisha michango na maoni kutoka kwa wasomaji.

Leo ninaanza na jinsi mwanaume anavyoweza kukabiliana na kuvunjika kwa uhusiano kati yake na mwanamke.Karibu sana.

JINSI YA MWANAUME KUDILI NA KUVUNJIKA KWA UHUSIANO NA MWANAMKE

Pointi tatu muhimu za kuzingatia:

  • Kwanza unapaswa kufuta kumbukumbu zote za uhusiano uliovunjika
  • Jaribu kutumia muda mwingi kuwa karibu na watu 'uliowapuuza' wakati ukiwa 'bize' na mwandani wako.Watu hao wanaweza kuwa familia yako,ndugu zako au marafiki zako
  • Kisasi kikubwa dhidi ya aliyekubwaga ni mafanikio.Kwahiyo hamasika kupata mafaniko ili 'ulipe kisasi.'
Hakuna anayeweza kubisha kwamba moja ya mambo magumu kwa manaume yoyote yule (na kwa wanawake pia) ni pale uhusiano na mwenza wako unapovunjika.Mara nyingi wanaume wengi wanapokumbwa na tatizo hilo hujipa matumaini potofu kwamba maisha yataendelea kama kawaida licha ya ukweli kwamba mioyoni mwao wanaumia vya kutosha.Wengi huendelea kujifariji na matumaini 'feki' kuwa wenza waliowabwaga watarejea.

Matokeo ya matumaini hayo 'feki' ni mithili ya mkuki wa kukataliwa wenye makali pande zote (double edged sword of rejection).Kwanza ni maumivu yanayotokana na ukweli kwamba umebwagwa,na kisha ukweli mwingine unaofuatia baadaye kuwa matarajio feki kuwa mwenza atarejea,well,yalikuwa feki.Mwenza wako ndio ameondoka moja kwa moja,na hatorejea (hapa tunazungumzia kubwagana ambako hakuna dalili wala uwezekano wa suluhu).

Lakini maumivu haya yanaweza kufupishwa kwa aliyebwagwa kutambua kuwa hali ndio hiyo-ameshabwagwa na hakuna uwezekano wa kurejea katika hali ilivyokuwa awali.Kuendelea kusubiri na kutarajia miujiza ni sawa na kujifungia kwenye mzunguko wa mateso usio na mwisho (endless circle of turture).

Kwahiyo ili kumudu kuendelea na maisha yako ya kawaida baada ya kubwagwa (au hata kubwagana) jaribu kufuata njia zifuatazo:

ACHA KUJILAUMU

Mara nyingi sie wanaume tumejenga tabia ya kuwa mithili ya watoto wakubwa (big babies) ambapo hatuachi kujilaumu.Kubwagwa ni kama kunaongeza ukubwa wa tabia hii.Kuna wanaochukulia kubwagwa kama mwisho wa dunia,yaani kana kwamba kuondoka kwa mwenza wako maishani mwako ni kama ameondoka na sababu ya wewe kuendelea kuishi.

Lakini ukijaribu kidogo tu kujiuliza "Niliishije kabla sijakutana na huyu aliyenibwaga?" utagundua kuwa ulikuwa ukiishi kama kawaida,na kama binadamu wengine.Kwahiyo,huu ni ushaidi tosha kuwa kama uliwahi kuweza kuishi bila mwenza aliyekubwaga ni dhahiri unaweza kuishi pia baada ya mwenza huyo kuondoka maishani mwako.Acha kujilaumu,jipange upya,na endelea kuishi.

FUTA KUMBUKUMBU

Kama nilivyoandika hapo juu,wengi wa wanaume wanaobwagwa huendelea kuwa na matumaini 'feki' kuwa mwenza aliyeamua kuondoka atarejea.Kwamba labda ni tisha toto tu,au anatikisha kiberiti tu.Mara nyingi wanaume tunapobwagwa hatupendi kukiri hadharani kuwa inatuuma.Wengi wetu hujifanya jasiri mbele ya 'washkaji' zetu tukijigamba kuwa 'ahh yule demu anadhani mimi nitababaika kwa vile tumeachana' (actually huwa tunakwepa kutumia neno 'kanibwaga').

Kiasili,katika mahusiano wanaume wengi wanapenda kuwa ndio walioshika usukani.Kwahiyo hata wanapobwagwa bado watajaribu kudanganya umma kuwa wao ndio waliokuwa wa kwanza kubwaga.Lakini kimsingi huko ni kujidanganya kwa sababu hao unaojaribu kuwaaminisha ujasiri wao hawajali sana (na pengine nao wana ishu zao binafsi zinazowanyima nafasi ya kujihangaisha na ishu zako).

Penigne una picha za mwenza aliyekubwaga,au zawadi mbalimbali alizokupatia wakati wa uhusiano wenu.Licha ya kubwagwa,unaweza kuogopa kuzitupa kwa hofu kuwa labda atarejea na akikuta azawadi alizokupatia hazipo atakasirika na kuondoka tena.Tumia akili yako vizuri.Ameondoka jumla,hatorudi.Usijaze bure nafasi kwenye albamu yako au kwenye sehemu unapoweka zawadi/kumbukumbu zako kwa matarajio hewa.

Uwepo wa kumbukumbu hizo (picha, zawadi,nk) ni sawa na uwepo wa mwenza aliyekubwaga kiroho japo si kimwili.Kila utakapoziona utaendelea kumkumbuka na kutamani awepo au arejee maishani mwako.Ukweli ni kwamba hatorejea.Cha kufanya basi ni kuteketeza kila kumbukumbu ya huyo aliyekubwaga.Hufanyi hivyo kwa ajili ya hasira bali ni kujipa nafasi ya kuendelea na maisha yako kama yalivyokuwa kabla hujakutana naye.Kumbuka,utakapopata mwenza mwingine hutazihitaji kumbukumbu hizo,sio tu kwa vile tayari una mwingine lakini pia itamsaidia mwenza wako mpya kupata uhakika kuwa wewe ni wake peke yake.

JIREJESHE KWA ULIOWATELEKEZA

Wengi wetu tunafahamu jinsi mapenzi motomoto yanavyoweza kutuweka mbali na watu wetu wengine wa karibu.Si kwamba tukiwa kwenye mapenzi tunawasahau watu hao lakini mara nyingi ni maotkeo ya kuweka akili na nguvu zaidi kwenye mahusiano yetu na wenza wetu,na hivyo kupata fursa finyu ya kuwa karibu na watu wetu wa karibu (kwa mfano wanafamilia wenzetu,ndugu,jamaa na marafiki).

Kufanya kosa si kosa bali kurejea kosa.Na alimradi wakati uko na mwenza wako hukuwafanyia dharau watu wako wa karibu basi ni dhahiri utakaporejea kwao (na pengine kuwafahamisha bayana kuwa umebwagwa) watakuwa radhi kukupokea.Kuwa karibu na watu wako wa karibu kutakusaidia sana kukarabati maisha yako,hasa kwa vile walikuwa nawe hata kabla hujakutana na huyo aliyekubwaga.

Kumbuka,mara nyingi hawa ni watu wanaokupenda kwa dhati- aidha kwa vile ninyi ni damu moja au ni watu uliopitia nao kwenye milima na mabonde.Kwa wanafamailia na ndugu,hawa kiasili ni watu ambao tunapaswa kuwa nao kwa vile tofauti na uchaguzi tunaokuwa nao kudeti mtu fulani au la,sheria za kibinadamu hazitupi fursa ya kuchagua nani tuzaliwe naye au atuzae.Ukaribu na watu wako wa karibu utasaidia kukukumbusha nani mwenye umuhimu wa kweli katika maisha yako.

USIKURUPUKE 

Hapa unaonywa usikurupuke kutaka kuanzisha uhusiano mwingine kuziba pengo la yule aliyekubwaga.Uzoefu unaonyesha kuwa mara nyingi jitihada za haraka haraka kutaka kuziba pengo hilo huishi kwenye maumivu/majonzi zaidi kuliko mafanikio.Tatizo kubwa hapa ni kwamba katika papara ya kutaka kuziba pengo hilo,unaweza kukosa muda wa kumwelewa vyema huyo 'unayemfukuzia.' Mara nyingi jitihada hizo huelemea zaidi kwenye kupata 'demu bomba zaidi ya yule aliyenizingua.' Lakini kama wasemavyo waswahili,usione vyaelea vimeundwa.Huyo 'demu bomba' anaweza kuwa na mwenza wake au ana 'pozi nyiiingi' ambazo sana sana zitaishi kukuumiza tu.

Suluhisho ni 'kutuliza boli.' Vuta pumzi.Angalia sababu zilizopelekea ukabwagwa au mkabwagana na mwenza aliyetangulia.Ukishaelewa chanzo/sababu itakupatia nafasi nzuri ya sio tu kuepuka kurejea makosa ya awali bali pia kujenga uwezekano wa kupata mtu aliye bora zaidi ya aliyetangulia.

JIHAMASISHE

Wengi wetu tunapobwagwa tunakuwa mateka wa hasira.Na katika hasira hizo baadhi yetu hujikuta tukifanya vitu vya kitoto,kijinga na visivyo na maana kabisa.Si ajabu kuona mtu akibwagwa akakimbilia kwenye waal ya Facebook profile ya aliyembwaga na kutundika 'madudu' yenye lengo la aidha kumuumiza mhusika au kujaribu kumshawishi arejee.Unaweza kukidhi mahitaji yako kwa dakika au siku chahe lakini mara nyngi matokeo ya 'upuuzi' wa aina hiyo huwa sio mazuri hasa pale utakapobaini kuwa 'kujigonga' kwako hakujafanikiwa kubadili msimamo wake.

Kumbuka,aliyekubwaga anaweza kuwa anafuatilia kwa karibu namna unavyodili na uamuzi wake.Matarajio ya wengi wanaobwaga wenza wao ni kuwa aliyebwagwa ataumia,atakonda,atateseka au,kwa hakika,ataaanza kubembeleza.Hiyo ni attention seeking.Na hakuna dawa mwafaka kwa attention seekers kama kuwapuuza.Kuendelea na maisha yako kana kwamba hakuna lililotokea sio tu itakuwa kama kumwadhibu attention seeker aliyekubwaga (ie kuvunja matumaini yake kuwa amekuumiza na labda utambembeleza) bali pia utakuwa unajisaidia wewe mwenyewe kuendelea na maisha yako kama kawaida.

Kisasi kikubwa kabisa kwa aliyekubwaga ni kwa wewe kupata mafanikio.Yaani badala ya wewe kuonekana umekondeana kwa mawazo ya kubwagwa,siku ya siku unakutana na aliyekubwaga na kukuona ukiwa mwenye furaha na mafanikio.Na kwa vile 'what goes around always comes around' si ajabu aliyekubwaga kwa wakati ho atakuwa anajutia kwanini alichukua uamuzi huo-lakini hawezi kukubembeleza mrejeane kwa sababu yeye ndiye aliyeamua bila kulazimishwa kuwa mwachane.

Pata picha,baada ya kubwaga unaelekeza nguvu zako kwenye kujiendeleza kimaisha (kitaaluma au kikazi),unatumia muda wako kujenga mwili wako kwa mazoezi, na kwa vile Mungu humjalia kila anayejituma,unafikia mafanikio yanayoweza kugeuza shingo za watu (ya kutamanisha).Mafanikio ni sawa na sumaku,lazima yatakusaidia kuongeza nafasi zako za kupata mwenza bora,pengine bora zaidi ya yule aliyekubwaga.Sasa siki ua siku,mwenyewe umenawiri vyema kutokana na kazi inayolipa vyema,na pembeni una mwenza bora,kisha unakutana na aliyekubwaga awali akiwa kachoka kimaisha na pengine akiwa na mwenza wa ovyo ovyo.Anashindwa kujizuia na kujikuta anakuuliza "hey fulani uko wapi siku hizi...naona mambo si mabaya..."Usiwe na haraka ya kujibu bali jitahidi kadri uwezavyo kuachia kicheko cha dharau....na badala ya kujibu swali lake mkebehi kwa kurejea swali lilelile na pigiria msumari kwa "hata wewe naona mambo si mabaya"...na kicheko kingine..Hiyo inaitwa kushinda vita bila kwenda vitani.

AMKA NA ENDELEA NA SAFARI

Vyovyote utakavyofanya huwezi kumzuia mwenza aliyedhamiria kukubwaga.Pengine amepata mtu aliye bora zaidi yako,pengine ameamua tu.Kama binti anatamani kuwa na mtu mwenye uwezo mkubwa kifedha kuliko wewe,kuendelea kumbembeleza mwendelee kuwa pamoja kutakuingiza kwenye vishawishi vya ufisadi,au matendo mengine mabaya ambayo si ajabu badala ya kukusaidia kumridhisha mwenza wako yakaishia kukupeleka jela.Naamini umeshaona au kuskia stori kibao za watu waliolazimika kujiingiza kwenye uhalifu ili kupata fedha za kuwaridhisha wenza wao.

Of course,mwenza wako ana haki ya kutaka kilicho bora.Lakini hiyo sio sababu ya kutaka uurefushe mkono wako zaidi ya uwezo wake.Mwneza wako ana haki ya kukupa changamoto za koboresha maisha yako/yenu lakini sio kwa namna ya kukusukuma uhatarishe maisha yako kwa ajili yake.Kumbuka,kama maisha yake ni muhimu,yako ni muhimu pia.Kama anakupenda kwa dhati atakubaliana na hali yako alimradi isiwe hali yako ni matokeo ya uvivu au uzembe wako au uoga wako kijituma.

Kwa hiyo badala ya kuendelea kuifanya hali ngumu (kubwagwa) kuwa ngumu zaidi,futa machoz yako,amka na endelea na maisha yako.Katika saikolojia kuna imani kwamba mengi ya tunayoyaita matatizo ni matokeo ya fikra zetu tu.Njaa,kwa mfano,si lazima imaanishe mahitaji ya mwili (tumbo) bali ni fikra kuwa tumbo linahitaji kitu fulani.Tamaa ni hali ya kutamani usichokuwa nacho hata kama si cha muhimu.Badala ya kujipa moyo kuwa mwenza wako atarudi aua atajilaumu kukubwaga,kwanini usielekeze fikra zako kwenye masuala mengine ya muhimu katika maisha yako?Kumbuka wewe ndiye nahodha ya maisha yako,kumkabidhi mtu mwingine jukumu hilo sio tu kunaondoka uhuru wako wa kukufikisha unakotaka kwenda bali pia kuna hatari ya kupotezwa.

Kwa leo inatosha!

MAKALA HII IMEANDALIWA KUTOKANA NA VYANZO MBALIMBALI MTANDAONI HUSUSAN MTANDAO WA AskMen 

MAKALA IJAYO ITAZUNGUMZIA IMANI ILIYOJENGEKA MIONGONI MWA MABINTI/WANAWAKE WENGI WA KITANZANIA KUWA WANAUME WA KITANZANIA NI MAHIRI KWA KU-CHEAT,AU KUNUKUU KIUSAHIHI, "OVYO KABISA", "BURE KABISA", "CHU*I MKONONI", NA KAULI KAMA HIZO.KICHANGAMSHA UBONGO: JE TABIA YA MWANAUME (AU MWANAMKE) INA MAHUSIANO YOYOTE NA URAIA WAKE?

HADI MUDA HUO,NAKUTAKIA SIKU NJEMA




Mdau mmoja mkubwa wa blogu hii amenitumia ujumbe ufuatao,nami naomba niuwasilishe kama ulivyo 


20/09/2011 09:00 kaka chahali.....naheshimu sana kazi zako za uandishi....ila kwahili nahisi umekosea

nikweli magamba wanafanya kila wawezalo huko igunga ila kutumia picha isiyo na uhalisia juu ya tukio hilo ni jambo la kudhalilisha taaluma yako ya uandishi.....

Picha ya kwanza ni imepigwa morogoro na si igunga na tena ilikuwa ni mashindano ya kula .....verify it here http://issamichuzi.blogspot.com/2011/07/mashindano-ya-kula-yafana-sana-mkoani.html

chonde ni heri kutoa habari bila picha kuliko kucopy and paste picha za matukio mawili tofauti....

ningefurahi kama utalitolea ufafanuzi jambo hili....

Regards,KM
mdau ninayefatilia kazizako twitter,facebook na kwenye hii blog yetu tuk


Baada ya kufuatilia kiungo (link) kilichobainishwa na mdau huyo nimegundua kuwa chanzo cha picha husika (ambacho ni jukwaa la mtandaoni la Jamii Forums) hakikuwasilisha picha husika kwa usahihi.

Naomba kutumia fursa hii kuomba radhi kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wote walioguswa na picha husika.Kuna nyakati waandishi hujikuta katika wakati mgumu kuthibitisha uhalisia wa kila habari,picha au chanzo cha habari/picha husika.

Lakini ni matumaini yangu makubwa kuwa kila msomaji wa blogu hii ataiga mfano wa mdau MK pindi kunapojitokeza mapungufu au makosa ya aina yoyote ile.Kwangu,kukosolewa ni miongoni mwa njia za kujifunza na kujirekebisha.Naomba kumshukuru sana mdau MK kwa ujumbe wake,na ninatumini tutazidi kushirikiana.


Kikwete mtegoni tena
• Asaini tangazo la serikali lililochakachuliwa

na Waandishi wetu

RAIS Jakaya Kikwete amedanganywa tena na baadhi ya watendaji wake, akasaini tangazo lililochakachuliwa.

Septemba 5 mwaka huu, Kikwete alisaini tangazo la kusudio la uanzishaji wa wilaya mpya ya Butiama, lakini katika namna ya kushangaza, sasa inaonekana eneo la wilaya mpya ni Nyamisisi.

Hali hiyo inayotia fedheha kwa Rais wa nchi, imebainika juzi wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipofika Butiama kuzuru kaburi la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Pinda alilazimika kuwatuliza wakazi wa eneo hili waliotaka kujua sababu za msingi za Rais kubadili msimamo wake na kuhamishia makao mapya yaliyotakiwa kuwa Butiama na kuyapeleka Nyamisisi.

Pinda alikiri bayana kuwa Rais alisaini tangazo hilo akijua kuwa kilichoandikwa ni makao makuu kuwa Butiama bila kujua eneo lililoandikwa ni Nyamisisi.

“Hata kama kuna mtu alitaka makao makuu yawe Nyamisisi, kwa kweli haikupaswa hiyo Nyamisisi kuchomekwa hivyo. Hata mngeniuliza mimi makao makuu yawe wapi, ningesema lazima yawe Butiama tu,” alisema Pinda na kushangiliwa.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema tangazo hilo lilikuwa na makosa kutokana na kutaja eneo la makao makuu tofauti na lile lililopendekezwa.

Pinda alisema mpango wa serikali ulikuwa ni makao makuu ya wilaya hiyo yawe katika kijiji cha Butiama ili kumuenzi Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Akijibu malalamiko ya wakazi wa Butiama, walioingia katika eneo la nyumba hiyo, wakimtaka atamke kuwa makao makuu yatakuwa Butiama, Pinda alisema:

“Hili la Butiama kwa kweli linaleta manenomaneno. Sisi serikalini tulidhani ukiwa na wilaya ya Butiama na makao makuu ni lazima yawe Butiama, ili tumuenzi Baba wa Taifa.

Hata hivyo, alisema pamoja na tangazo hilo kuchomekwa neno Nyamisisi, bado mtu aliyefanya hivyo hajafanikiwa, kwani tangazo hilo sio uamuzi wa mwisho wa kuhusu suala hilo.

Aliwataka wananchi wa Butiama kulichukulia tangazo hilo kuwa ni pendekezo tu ambalo wanapaswa kulitolea maoni yao kuhusu kulikubali au kulikataa na kwamba maamuzi ya mwisho kuhusu wapi yawe makao makuu ya wilaya hiyo yatatokana na maoni ya wananchi wenyewe.

Alisisitiza kuwa Butiama ikiwa wilaya sio tu huduma za msingi zitaboreshwa na kuwapa watu sababu ya kwenda wilayani hapo, bali pia itawapa sababu ya kwenda kuzuru nyumbani kwa Hayati Baba wa Taifa.

Pinda pia alimpa fursa mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere, kutoa kauli yake kuhusu suala hilo, ambaye alisema yeye asingependa kuliingilia suala hilo.

“Hili suala halina tatizo, ninyi na wananchi wote mtakavyoamua ndivyo iwe hivyohivyo,” alisema Mama Maria.

Maswa watishia kuandamana

Katika hatua nyingine, hatua ya Rais Kikwete kuunda mikoa mipya, imezua balaa baada ya mamia ya wananchi wa wilaya ya Maswa, mkoa wa Shinyanga kuandaa maandamano iwapo serikali itaamua kuyaweka makao makuu ya mkoa mpya wa Simiyu katika wilaya ya Bariadi.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana katika Uwanja wa Nguzo Nane na kuhudhuriwa na mamia ya wakazi wa wilaya hiyo, wananchi hao wamedai kuwa hawako tayari kutendewa hivyo na wataandamana hata ikilazimu kupigwa risasi.

Katika mkutano huo ulioitishwa kwa ajili ya kutoa maoni ya mapendekezo juu ya nia ya serikali ya kupeleka makao makuu ya mkoa mpya wa Simiyu mjini Bariadi, wananchi hao wamesema uamuzi huo ni dharau kwao na unataka kufanywa kwa ajili ya manufaa ya viongozi wachache.

“Sisi wana Maswa tutaandamana bila kujali itikadi za vyama kama hatutasikilizwa na tuko tayari kupigwa risasi. Hatuwezi kunyang’anywa haki yetu kwa ajili ya ubinafsi wa viongozi wachache,” alisema mkazi mmoja wa Maswa, Thomas Nkola, na kushangiliwa na umati wa wananchi.

Walisema kuwa viongozi wa mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Bariadi wamekuwa na desturi ya ubinafsi katika masuala yenye maslahi ya umma kitendo kilichodhihirika katika ujenzi wa barabara ya lami ya Mwigumbi –Maswa-Lamadi.

“Viongozi wetu wa mkoa wa Shinyanga na wa Bariadi wametuona sisi wa Maswa watulivu sana hivyo wanatumia mwanya huo kutuchezea.

“Mfano ujenzi wa barabara ya lami ya Mwigumbi-Maswa-Lamadi ilitakiwa ianzie Mwigumbi kuja Maswa lakini kutokana na ubinafsi wao imeanzia Bariadi kwenda Lamadi,” alisema mwananchi mwingine, Samwel Kidima.

Walisema licha ya mapenzi mema aliyonayo Rais Jakaya Kikwete ya kuanzisha mkoa huo, ni vizuri mchakato wa kupata makao makuu yake ukaanza upya kwani wa awali haukupitia katika vikao halali kama vile baraza la madiwani na kamati za ushauri za wilaya (DCC) hali ambayo imezua mgogoro mkubwa na kufanya kutokuwepo kwa mahusiano mazuri kati ya wananchi wa wilaya hizo.

“Rais Kikwete alipoamua kuanzisha mikoa na wilaya mpya alikuwa na nia nzuri sana lakini jambo la kushangaza mchakato wa kutoa mapendekezo ya makao makuu ya mkoa wa Simiyu hayakufuata utaratibu kwani ilitakiwa uanzie katika vikao vya baraza la madiwani na kamati za ushauri za wilaya ndiyo maana jambo hili limezua mgogoro mkubwa na sasa mahusiano kati ya wananchi wa wilaya ya Maswa na Bariadi si mazuri hivyo mchakato uanze upya,” alisema Edward Bunyongoli.

Walisema iwapo serikali itabaki na msimamo wake huo basi wao wataendelea kubaki katika mkoa wa Shinyanga lakini hawako tayari kukubaliana na uamuzi huo uliofanywa kwa ajili ya maslahi ya watu wachache wabinafsi.

“Kama serikali itabaki na msimamo kuwa Bariadi ndiyo makao makuu ya mkoa wa Simiyu sisi tutabaki katika mkoa wa Shinyanga kwani hatuko tayari kukubali uamuzi huo uliotawaliwa na vitendo vya kifisadi,” alisema Kulwa Nangale.

Hii si mara ya kwanza kudanganywa kwa Rais kwani ameshadanganywa zaidi ya mara 12 miongoni mwa mambo aliyodanganywa ni pamoja na ile ya kuzindua mradi wa Bwawa la Manchira lililoko wilayani Serengeti wakati tayari wananchi wamekwishafungua kesi Mahakama Kuu ya Mwanza wakidai fidia.

Kesi hiyo iliyofunguliwa ni matokeo ya viongozi wa serikali wilayani humo kuhusika kuwalipa fidia watu wasiohusika na kuwaacha walengwa waliofanyiwa tathmini.

Pia aliwahi kudanganywa kwamba daraja la Mkenda lililoko Ruvuma ambalo ni njia muhimu kuelekea Msumbiji, lilikuwa limekamilika.

Katika tukio jingine, Rais aliwahi kupewa taarifa zisizo sahihi kuhusu tuhuma za rushwa zilizokuwa zikimkababili Anatory Choya kisha akamteua kuwa mkuu wa wilaya, lakini siku siku chache baadaye akafunguliwa mashtaka na TAKUKURU.

Mwaka juzi, akiwa ziarani Mbeya msafara wa Rais ulishambuliwa kwa mawe na watu, lakini wasaidizi wake wakaja kutoa taarifa kwamba watu hao walikuwa ni wahuni na walikuwa wakimsubiri Rais kwa muda mrefu bila mafinikio.

Hata hivyo, baadaye uchunguzi huru ulibainisha kwamba tukio hilo lilikuwa na mafungamano ya kisiasa na makovu ya mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM kwa mwaka 2005.

Mlolongo huo mrefu wa upotoshaji taarifa kwa Rais uliibuka tena katika utoaji wa magari ya misaada ambapo badala ya kupewa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Longido alipewa wa Ngorongoro.

Tukio hilo lilimfanya mkuu huyo wa nchi kukasirika na kumzodoa mkurugenzi huyo, lakini baadaye ikabainika mkurugenzi huyo alikwenda kutokana na makosa ya maafisa wa Ikulu.

Katika mlolongo huo, tukio kubwa kabisa ni Rais kutia saini kwa mbwembwe Sheria ya Gharama za Fedha za Uchaguzi ambayo ilichomekwa vipengele nje ya Bunge kitu ambacho ni kinyume cha sheria.

Tukio hilo ambalo ni la uvunjifu wa Katiba, liliibuliwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, ambaye awali, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fedrerick Werema, alikanusha.

Hata hivyo, baadaye sheria hiyo ilirudishwa bungeni na kukarabatiwa kwa mgongo wa mabadiliko ya sheria mbalimbali.

Mei mwaka jana, Rais alipewa taarifa za upotoshaji kuhusu mazungumzo ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) na serikali, kwa kuelezwa shirikisho hilo halikuhudhuria mkutano wa saa 4:00 asubuhi kama ilivyopangwa.

Hata hivyo, TUCTA wakatoa ushahidi wa barua za mwaliko wa mkutano huo wa Aprili 22 mwaka jana, ambazo zilikuwa mbili, moja ikionyesha walitakiwa kufika katika mazungumzo Hazina saa 4:00 asubuhi na nyingine saa 8:00 mchana.

Katika kuonyesha upotoshaji kwa Rais, wasaidizi hao walimpa barua iliyokuwa ikionyesha walipaswa kukutana saa 4:00 asubuhi huku ile ya saa 8:00 wakawa wameificha.

Rais akizungumza na wazee wa mkoa wa Dares Salaam aliwashambulia viongozi wa TUCTA hasa Naibu Katibu Mkuu, Nicolas Mgaya, akimwita mnafiki, mzandiki, na mchochezi.

19 Sept 2011

 
SALAM,
Habari zenu wadau wote popote Duniani Tunapenda kuwasalimu wakubwa Shikamoo na tulio Umri sawa Mambo zenu!, Baada ya salamu hizi tunapenda kuwaletea habari njema sana kwa wazazi na wanafunzi ambao walikuwa wamefanya mtihani kidato cha sita lakini hawakufanikiwa kuyaona majina yao wakati wa Selection ya kwanza, Lakini muda sio mrefu sana yametoka majina mapya ya Second Selection ambapo utaweza Bahatika kuliona jina lako, la ndugu yako, rafiki ama mwanao. Tunawaomba mkipata taarifa hii muwape na wengine pia ili wapate kutazama majina hayo. mwisho tunawapa hongera sana wale walio chaguliwa kwa mala ya kwanza na hawa ambao mmechaguliwa kwa mala ya pili. Web site ya Matukio na wanavyuo itaendelea kuwaletea habari zaidi za vyuo mbali mbali Tanzania. 

Nyongeza: Tunaomba sana ushirikiano wenu uongozi wa vyuo mbali mbali Tanzania, ikiwa ni kututumia matukio mbali mbali ambayo yanatokea katika vyuo vyenu, mfano mikutano,mahafari na mambo kama hayo, pia kama mna applications za kutaka wanafunzi wajiunge na vyuo vyenu pia tunakaribisha sana na matangazo mengine. Kwa wanafunzi wa vyuo mbali mbali Tanzania pia tunawaomba ushirikiono wenu wa ukaribu wa kututumia matukio mbali mbali sisi ni wasimamizi tuu wa kupost habari lakini mshiriki mkuu ni wewe msomaji na mtumaji wa matukio. Lengo ni kuwaunganisha wanafunzi wote wa vyuo Tanzania. Pamoja tunaweza 

Matukio yote ama kitu chochote tutumieni kupitia Barua pepe: [email protected]
Asanteni sana
Matukio na wanavyuo Crew


BOFYA HAPA CHINI KUONA MAJINA HAYO
 

BEFFTA Founder Pauline Long with Frank from Urban Pulse
Beutiful ladies in the house
Dj Abbas with Miss Jestina George
Live perfomance
 
 
Urban Pulse and Miss Jestina George who's blog www.missjestinageorge.blogspot.com has been nominated as Blog of the Year, had the pleasure of attending the 3rd BEFFTA AWARDS nomination party at the London Hilton on Park Lane on Friday 16 September 2011.
URBAN PULSE CREW with Entrepreneurs
 
The party was awesome full glamour and excitements with Celebrities guests, Enterpreneurs, Shakers & Movers in showbiz.
Sola Oyebade from MAHOGANY PRODUCTION adressing to the invited guests during the launch party at Hilton Park lane Hotel, London
 
BEFFTA Awards is a distinctly special awards ceremony honouring the best showbiz and entertainment personalities in the black and ethnic communities in the UK, USA and globally. BEFFTA Awards is the first of its kind rewarding under one roof outstanding achievements and contributions from Africans, Caribbeans and Asians in entertainment, film, fashion, television and arts. This international prestigious ceremony celebrates an all round accomplishments of a hard working community within entertainment and showbiz especially the unknown talent that need exposure. The awards ceremony founded by Pauline Long also aims to inspire black and ethnic personalities worldwide to achieve at the highest levels.
 
The nomination categories were as follows:
 
MusicDance
Comedy
Radio
Newspapers
Magazines
Blogs
Events
DJ
Photographers
Fashion Category:
Fashion Designers
Stylists
Make-up Artists
Fashion Choreographers
Models
Beauty Pageants
Film Category
TV Category
ART Category
 
 
BEFFTA  Awards – Black Entertainment Film Fashion Television and Arts will be on the 22.10.2011
Thanks,
 

One of this year's BEFTA Award nominee Jestina George from Miss Jestina George Blog posing for the camera during the lauch party

URBAN PULSE CREATIVE In Association with MISS JESTINA BLOG

18 Sept 2011

Umoja Wa Bloggers Wa Kitanzania
September 17, 2011

Dear Tanzanian Bloggers,

Do you guys have a union? Why don't you create a Tanzania bloggers union? Haya ni maswali nimekua nikiulizwa na watu mara kwa mara…Kila muda kidogo huwa napokea email inayohusu hili jambo. Nimejitahidi sana kukaa mbali na hii topic lakini kila ninavyofunga macho ndio emails zinazidi kuuliza lini umoja utaanzwisha? Je upo umoja wa watanzania.

Mimi kukaa mbali na hili suala na kuwajibu watu ni kuwa mimi naamini umoja wa kitu chochote unaanzishwa na watu kwa mapenzi yao. Na umoja huo ni lazima uwe na malengo na faida za kuwa mwanachama katika umoja huo. Bila hilo kutakua hakuna maana ya kuwa na umoja au hata ukiwepo hautadumu. Halafu lingine lililokua linanifanya mimi niwe mbali na hii issue ni kuwa mimi sina blog. Ni hivi karibuni tu ndio nimefufua blog yangu ambayo nilikua nayo zamani lakini sikuiendelezaga baada ya kupokea email ya kijana wa miaka 14 akiniambia huwa anafuatilia sana Tanzanian blog awards site na ameona kuwa ninahamasisha sana watu wawe na moyo wa kupenda kuwa na blogs lakini hajaona blog yangu. Hiyo ndio ilikua aha moment yangu. Nikakumbuka ule msemo unaosema “Talk the talk and walk the walk.”.

Anyway baada ya kufikiri sana nimeona kwa vile sasa hivi technology inaweza kuwakutanisha watu kwa urahisi kutoka pande zote za ulimwengu hivyo inaweza kuwa rahisi kwa wale watakaopenda kujiunga kuweza kuwasiliana na kujadili mambo yao kwa urahisi. Na kwa vile kama tunavyofahamu muda sio mrefu Google+ itakua inapatikana kwa kila mtu na itakua inaweza kuwaunganisha watu 10 kwa wakati mmoja hivyo nikafikiria labda kwa kutumia technology hii kuna kitu cha maana kinaweza kufanyika.

Kwa muda huu mfupi nimepata experience kubwa sana kuhusu blogs za watanzania walioko ndani na nje ya Tanzania. Kuna baadhi ya bloggers nimeweza kufahamiana nao katika personal level. Ila baada ya kuongea na wengi ni kuwa sasa hivi nikiwa nasoma blog yeyote ambapo mwandishi wake yupo Tanzania nasoma na kuiangalia tofauti na kama nilivyokua naangalia hapo nyuma. Well, blog yeyote ni lazima kuipa heshima kwa blogger anayeiandika bila kujali yupo wapi lakini baada ya kuongea na bloggers wengi nimegundua mazingira na vitendea kazi wanavyotumia kuili kuweza kufanya blog zao ziwe nzrui ni taabu sana. Blogs nyingi ni nzuri na zina idea nzuir lakini hao bloggers wakiulelezea jinsi wanavyofanya kuweza kupost chochote unakaa chini na kujiuliza WHY and always don't take things for granted.

Hivi mnafahamu kuna bloggers wengine mpaka leo wanatumia internet cafés kumaintain blogs zao. Just imagine mtu anaacha kuingia kwenye internet café ajisomee kwenye net mambo anayotaka anakalia kuweka blog ili mimi na wewe tusome yale anayoyapost. Kuna watu wengine bado wanatumia computers za kazini kublog na watu hao wameniambia kuwa huwa wanawahi kazini mapema ili watumie computer za kazi kabla muda wa kazi haujaanza. Wengine wanaskip lunch breaks zao ili watumie huo muda kublog. Na kuna baadhi wameniambia wao wanaruhusiwa kwenda na nyumbani na laptop za kazini lakini huyo mmoja alinichekesha…It is not a a laughable issue lakini alisema laptop battery charge yake ni ndogo sana sometimes akiwa kwenye daladala anatumia kidogo by the time akifika nyumbani battery imeisha na nyumbani hakuna umeme. Hivyo anakua yupo na laptop lakini hawezi kufanya chochote nayo.

Yaani kuna mambo mengi sana ambayo nimekaa nikajiuliza how can we help? Ndio nikasema once tukishajua watu wangapi wanapenda au watajiunga then agenda inayofuata ni kuweka fundraising. Siku hizi kuna online fundraising sites nyingi tu ambazo huwa tunaweza kuanzisha na zinaonyesha how much watu wamecontribute na baada ya hapo…Kuna off lease laptop very reasonable price zinaweza kupatikana na kusaidia bloggers wa kitanzania who are really in need. Kuna mambo mengi sana kama sio hawa bloggers wa kawaida kuweka wengine wetu wala tusingeweza kuona wala kufahamu. Sasa what is our appreciation? Kama tusipotafuta njia ya kusaidiana nani atakuja kutusaidia? Hata tukiweza kukusanya na kununua moja ni better than nothing. Ni bora kulikokukaa tu na kusema kila mtu atajisaidia mwenyewe.

That is why I am presenting this to you guys …Email me for any suggestions and how we can do and then we will start from there….

Mimi nilichokua nafikiria kwa kuanza kila bara atokee mtu mmoja takayependa kuwa mwenyekiti wa bloggers walioko huko..Hao watu watawasiliana ana kuchagua mwenzyekiti wa wate..Na kama watu watakua wengi basi kuwe na msaidizi na katibu katika kila bara..Kama ni wachache basi itajulikana baadaye jinsi ya kufanya. I don't think kutahitajika cashier mpaka huko mbele kukishaundwa kitu cha maana. Na nadahani itakua fair hao viongozi wawe at least wamekua na blog kwa zaidi ya miaka miwili.

Mimi nipo willing to organise and help to put together this baada ya hapo nitawaachia wanaochagulia na kubakia as a just mwanachama. Hivyo nimeweka hiyo form hapo ili nione ni watu wanagapi wanataka kujiunga. Kwa sababau hatakwenye hii newsletter kuna mambo naona hayanihusu mimi kuyatuma na hayo mambo yangekua vizuri yakitumwa kwa bloggers kma wangekua na umoja.

Na labda niweke clear kama watu wakipatikana huo umoja sio lazima Kwa kila blogger kujiunga. Na pia kujiunga au kutojiunga haitasababisha mtu kuingia katika mashindano yetu au la. This will be two separate things as I said before nikishaweza kusaidia kuput together kama kuna vitu vya kuforward kwa viongozi I will do that and step aside.

Kuna vitu vingi vitaweza kufanyika kwa bloggers vikiwa under umoja wa bloggers.

Okay nasubiri kusikia kutoka kwenu.. Na form ya kutaka kufahamu ni watu wangapi watapenda kujiunga nimeiweka kwenye hiyo site...

Pauline
Founder, Tanzanian Blogs Awards



PRESS RELEASE
BEN TELEVISION
25 ASHLEY ROAD
TOTTENHAM
LONDON, N17 9LJ

09/Sept/2011

RE: PRESS RELEASE
RE: BEN TV DIPLOMATIC AWARDS 2011
This to announce that The Tanzania , Uganda and Kenya High commissions in London have been nominated to receive awards in the following categories:

· Diaspora growth, development and involvement

· Good customer service at the High commission/embassy

· Positive projection of country’s image abroad

· Economic and Cultural diplomacy

· Country’s Human Development


Other categories to be awarded are:
Diplomat of the year from Africa, Caribbean and Pacific 2011
Diplomat of the Year from the Americas
Deputy Head of mission of the year
Distinguished contribution to diplomacy

The night will recognise and celebrate the diplomatic achievements made within the African, Caribbean and Pacific regions on the 4th November 2011 at the Hilton park lane Hotel

Which category do you think fits your High commission? Please send your entries, comments and nominations to [email protected], or [email protected]

The BEN TV DIPLOMATIC AWARDS will be adding glamour to Africa’s Golden Jubilee celebrations with:

* Top Nollywood stars & the best of African film stars
* UK celebrities and crème de la crème
* Diplomats and professionals


For further information: email [email protected],newdealafrica.co.uk

Signed.
Ayoub mzee
Public/current Affairs Desk
BEN TV SKY 184
TEL + 44 7960811614/+442088088800

Notes
Africa is truly a great nation with great people. We celebrate Africa at 52. We celebrate you and other great people like you as an inspiration to the next generation of leaders.

BEN TV is a Black and ethnic oriented ,urban , diverse and cosmopolitan Family channel ,established to provide a whole some mix of entertainment ,educative and informational programmes suitable for family viewing .It also includes a range of cultured programming to empower ,transform and challenge the conventional perception of Africa, Caribbean and African Diaspora


Ajali Ya Boat Ya Zanzibar

Kama wote tunavyofahamu taifa limepatwa na msiba mkubwa sana kutokana na ajali ya boat iliyotokea huko Zanzibar. Tunaomba Mwenyenzi Mungu awape faraja wale wote waliopoteza ndugu, jamaa au marafiki katika ajali hii na pia tunaomba Mwenyenzi Mungu awaweke mahali pema wale wote waliopoteza maisha yao katika ajali hii. Katika kipindi hiki kigumu tumeweza kuona kwa mara nyingine tena jinsi social medias zilivyo na mchango mkubwa katika jamii zetu. Kwa vile ajali hii ilitokea mwisho wa week blogs zilisaidia sana kutoa habari kwa haraka sana kuhusu ajali hii kuliko hata vyombo vya habari. Watu wengi waliweza kufuatilia na kuelewa mambo mengi kuhusu ajali hii kwa urahisi kuliko kusubiri vyombo vya habari kutangaza au kuchapisha katika magazeti. Mchango wa bloggers ni mkubwa sana katika jamii zetu hasa kama nchi yetu ambazo hazina centralized alert system. Tunawashukuru sana wale wote waliojitahidi kutupatia updates za habari hii kila mara..


Campaign Ya Kupunguza Ajali Nchini
Kuna watu wameniandikia na kuniuliza ni nini kinaweza kufanyika ili tuanzishe campaign ya kuwapa watu awareness ya kusaidia kupunguza ajali Tanzania? NImefurahishwa na moyo wa watu hawa kwa vile baadhi yao sio watanzania lakini wameweza kufuatilia habari za ajalii hii na kugundua kuwa ajali ni tatizo sugu nchini Tanzania. Bado nina brainstorming vitu ambavyo vinaweza kuanzishwa katika campain hii lakini kama kuna watu wana ideas please naomba mzitume ili tuangalie ni zipi zitaweza kufanyika na kuwafikia watu wengi na kwa budget gani. Ili tuangalie jinsi tutakavyoanza kufanya fundraising ya kusupport campain hiyo. Tukumbuke leo kwa mwenzio kesho kwako. Hizi ajali hazichagui jinsia, umri, kisomo wala kipato. Zinakuja kutoka kila pande. Tusipojisaidia wenyewe nani atakuja kutusaidia?

Campain itahusika na:-
1. Kuhamasisha madereva kujifunza sheria za barabarani
2. Kuhamasisha madereva kupima macho mara kwa mara.
3. Kuhamasisha watu wawe responsible kwa maisha yako eg don't drink and drive, follow the speed limit, wear seat belt, wear a helmet etc.
4. Kuhamasisha watu kwa wale wanaotumia public transportation kufuata sheria za usalama.

Kama mtu ana idea yeyote basi msisiste kututumia.



follow on Twitter | friend on Facebook | forward to a friend
Copyright © 2011 Tanzanian Blog Awards, All rights reserved.
You are receiving this email because you are in our Tanzanian bloggers' list ...If you wish to be removed from our list please email us...
Our mailing address is:

Tanzanian Blog Awards
122 Laurel Ave Suite 3
Maplewood, NJ 07040

15 Sept 2011

EMPOWER | EDUCATE | ENTERPRISE women in TANZANIA 
 

TWENDE

Copyright © 2011 Tanzania Women Entreprenuers Network & Development Exposition, All rights reserved.
You are receiving this email because we Believe in Empowering, Educating and Enterprising Women. Together We Can.
Our mailing address is:
Tanzania Women Entreprenuers Network & Development Exposition
105 Kilimani road
Dar Es Salaam 10684



Raia Mwema Ughaibuni
Rais Kikwete na ‘usanii’ wa Mahakama ya Kadhi!
Evarist Chahali
Uskochi
14 Sep 2011
Toleo na 203
NIANZE makala hii kwa kutoa salamu zangu za rambirambi kwa wafiwa waliopoteza ndugu na/au jamaa zao katika ajali ya boti ilivyotokea usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita kwenye Bahari ya Hindi kati ya Nungwi na Pemba.
Kwa mara nyingine tena Watanzania tunashuhudia wenzetu wakipoteza maisha katika ajali ambayo, kwa namna moja au nyingine, ingeweza kuepukika.
Japo hadi wakati naandaa makala hii hakujatolewa taarifa rasmi ya chanzo cha ajali hiyo, lakini kwa mujibu wa abiria walionusurika katika ajali hiyo inadaiwa kuwa chanzo inaweza kuwa boti husika kuelemewa na wingi wa abiria na mizigo.
Kwa nini ninasema ajali hiyo ingeweza kuepukika? Ni wazi kuwa laiti mamlaka zinazohusika zingeweka mbele uhai wa abiria na kuzingatia sheria zinazotawala usafiri wa majini, ni wazi kuwa chombo hicho cha usafiri kisingezidisha shehena zaidi ya uwezo wake.
Lakini kwa kuwa kipindi hiki ni cha maombolezo, naomba nisiingie kiundani zaidi kuhusu namna taifa linavyoweza kuepusha matukio ya kusikitisha kama hili kutokea tena. Kwa sasa tuelekeze nguvu zetu katika kuwasaidia majeruhi na kuwafariji wafiwa.
Nielekee kwenye dhima ya makala hii. Katika maadhimisho ya hivi karibuni ya sherehe za Idd, Rais Jakaya Kikwete alitoa hotuba iliyoelekea kuwagusa wengi ambapo, pamoja na mengine, alizungumzia suala la kurejesha (na si kuanzisha) Mahakama ya Kadhi.
Nasema kurejesha kwa vile mahakama hiyo ilikuwepo huko nyuma kabla ya kufutwa.Kwahiyo,iwapo itafanikiwa kuwepo tena itakuwa si kwa mara ya kwanza; bali mwendelezo tu wa ile iliyokuwepo awali.
Bila kuuma maneno, napenda kumwaga shutuma kwa Rais Kikwete mwenyewe kama sehemu ya tatizo la uanzishwaji wa mahakama hiyo. Ikumbukwe kuwa Chama cha Mapinduzi katika Ilani yake ya Uchaguzi ya mwaka 2005 kiliahidi kushughulikia uanzishwaji wa mahakama hiyo.
Kimsingi, hakukuwa na shinikizo lolote kwa chama hicho kuja na ahadi hiyo hewa, lakini baadaye kukatokea kurushiana mpira kati ya watendaji wa serikali na wale wa CCM.
Kama ambavyo Watanzania wengine ‘walivyoingizwa mkenge’ na ahadi hewa za kuletewa maisha bora (na badala yake kuishia kushuhudia maisha bora kwa mfisadi pekee),CCM ilitumia ahadi hiyo ya kurejesha Mahakama ya Kadhi kwa minajili tu ya kupata kura za Waislam.
Kwa bahati mbaya,Waislam hawakuibana CCM wakati huo kuhoji kwa undani namna ahadi hiyo ingetekelezwa. Kwa mfano, hawakujihangaisha kukibana chama hicho kiwape ratiba kamili ya utekelezaji wa ahadi hiyo.
Lakini haikuwachukua muda mrefu kubaini kuwa ahadi hiyo ilikuwa ni ‘changa la macho’ na ya kisiasa zaidi kuliko yenye nia ya kusikiliza kilio chao cha muda mrefu.
Binafsi, licha ya kuwa Mkristo, sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama hiyo alimradi sheria na taratibu zikizingatiwa. Msimamo wangu huo unatokana na ukweli kwamba kihistoria huko nyuma hakukuwa na tatizo lolote lililotokana na uwepo wa mahakama hiyo.
Ni muhimu kwetu kutambua kuwa, kwa muda mrefu tofauti zetu za kidini zimefunikwa na Utanzania wetu; japokuwa baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakifanya kila wawezalo kupanda mbegu za udini kwa maslahi yao binafsi.
Siamini kabisa kuwa iwapo Mahakama ya Kadhi ikirejeshwa itawaathiri wasio Waislam kwa vile lengo kuu la chombo hicho ni kuwahudumiwa Waislam pekee.
Na jingine zuri ni kwamba mahakama hiyo inaweza kusaidia kupambana na maovu katika jamii; hususan suala la ufisadi.
Kwa nini ninamlaumu Kikwete kuhusu sakata hilo la Mahakama ya Kadhi? Licha ya utetezi wake wakati fulani kuwa si yeye aliyeandika Ilani ya Uchaguzi ya chama chake mwaka 2005, ukweli ni kwamba aliitumia ilani hiyo kugombea kura takriban nchi nzima.
Ni wazi kuwa aliona mahala fulani kwenye ilani hiyo ikieleza kwamba chama anachokitumikia na kukitumia kugombea urais kimeahidi jambo ambalo, kimsingi, yeye mwenyewe linamgusa (kwa maana naye ni Muislam).
Lakini katika ubabaishaji uliozoeleka wa wanasiasa wetu, ‘maji yalipozidi unga’, Kikwete alifikia hatua ya kudai aliyeanzisha wazo la kurejeshwa Mahakama ya Kadhi ni Augustine Mrema, na sio yeye (Kikwete).
Huku ni kukwepa wajibu; kwani hata kama wazo hilo lingekuwa kweli limeanzishwa na Mrema, lakini lina umuhimu kwa sehemu fulani ya jamii, basi, la msingi sio aliyenazisha wazo; bali kulitekeleza katika namna inayostahili.
Katika hotuba hiyo,Kikwete alizungumzia pia suala la udini na kuonya viongozi wa dini kutotumia nafasi zao kuchochea chokochoko za kidini.
Ninaamini wakati Kikwete anazungumza hayo, alikuwa anafahamu fika kuwa siasa sio jambo haramu kuingizwa kwenye dini; hasa ikizingatiwa michango ya dini katika harakati za uhuru wa nchi yetu.
Kauli za kuhamasisha kutenganisha dini na siasa hazina mashiko makubwa kwa vile hazina tofauti na kauli zilizokuwa zikitolewa na mkoloni kwa minajili ya kukwaza jitihada zetu za kupata uhuru.
Kwa wanaofahamu historia za mapambano ya ukombozi wetu kutoka himaya ya mkoloni, watakumbuka fika namna misikiti ilivyokuwa sehemu muhimu ya harakati hizo.
Mkoloni alijaribu kuharamisha dini kwenye siasa kwa vile alifahamu kuwa dini inagusa imani na inawaunganisha wanajamii/waumini kirahisi zaidi kufikia lengo wanalokusudia.
Wanasiasa wa zama za Kikwete wanarejea kauli kama hizo za mkoloni si kwa minajili ya hofu ya vurugu; bali kwa vile wanafahamu kuwa pindi wananchi watakapounganishwa na imani zao kupambana na siasa za kibabaishaji, basi, watawala watakuwa katika nafasi ileile iliyomkuta mkoloni enzi za kupigani uhuru.
Katika hotuba hiyo, Kikwete aliwataka viongozi wa dini kuhubiri amani ili kuepusha waumini wao kujihusisha na mambo yasiyokubalika. Kwa maana nyingine, alikuwa anawahamasisha kuhubiri dhidi ya maovu kama ufisadi na mengine yanayoshabihiana nayo.
Sasa, watumishi wa Mungu watawezaje kuepuka kuzungumzia siasa iwapo baadhi (kama si wengi) ya mafisadi, ni wanasiasa?
Naomba unielewe hapo.Utawezaje kuzungumzia mwanasoka, kwa mfano, pasipo kuzungumzia soka?
Kimsingi, Kikwete na wanasiasa wengi wa Tanzania wanapaswa kuwashukuru sana viongozi wa dini; kwani viongozi hao wamechangia sana kuwawezesha wanasiasa wasiofaa kuchaguliwa au kuendelea kuwepo madarakani.
Ni wazi Rais anakumbuka kuwa wakati anagombea urais kwa mara ya kwanza, baadhi ya viongozi wa dini walimtakasa na kudai yeye ni ‘chaguo la Mungu.’
Kwa nini basi hakuwakemea wakati huo kuwa wanachanganya dini na siasa? Lakini kibaya zaidi ni namna baadhi ya watu wa karibu wa timu ya kampeni ya Kikwete kwenye uchaguzi mkuu uliopita walivyofanya kila waliloweza kupandikiza mbegu za udini.
Kila aliyefuatilia kampeni hizo kwa makini atakumbuka namna mgombea wa tiketi ya urais kupitia CHADEMA, Dkt Willibrod Slaa ‘alivyochorwa’ taswira ya ‘mgombea wa Kanisa Katoliki’ huku baadhi ya vyombo vya habari vinavyomilikiwa na serikali vikidiriki kumwita padre licha ya ukweli kuwa Dk. Slaa hakuwa padre wakati huo.
Pamoja na lawama hizo kwa Kikwete, naungana naye mkono katika maelezo yake kwa Waislam kuwa adui wao katika azma yao ya kurejeshewa Mahakama ya Kadhi si kanisa au maaskofu.
Ni kweli kwamba kanisa na maaskofu wameonyesha hofu yao (si upinzani) pengine kwa kuwa kumekuwa na jitihada duni kwa Waislam wenyewe kukazani kwenye elimu ya uraia (kwa Waislam na wasio Waislam) kuhusu namna mahakama hiyo zitakavyofanya kazi.
Kama alivyosema Kikwete, Mahakama ya Kadhi haitashughulikia kesi za jinai, na hivyo wanaohofia adhabu za kukatwa mikono au kuuawa kwa mawe hawapaswi kuwa na hofu hiyo. Kinachohitajika hapo ni elimu ya kutosha kwa umma.
Nimalizie kwa kurejesha lawama tena kwa Kikwete; kwani japo aliwahakikishia Waislam kuwa kikwazo cha urejeshwaji wa Mahakama ya kadhi si Kanisa au maaskofu, hakuwaeleza ukweli kwamba kikwazo kikubwa ni walaghai wa CCM ambao mwaka 2005 walitoa ahadi hiyo kwa minajili ya kupata kura za Waislam pasipo dhamira ya dhati ya kushughulikia suala hilo.
Kabla ya kuahidi kuwa suala hilo linashughulikiwa, Kikwete alipaswa kuwaomba radhi Waislam kwa ‘usanii uliofanywa na CCM kuingiza hoja hiyo kwenye ilani yake ya uchaguzi mwaka 2005’ lakini hadi sasa imeendelea kuwa ahadi tu - kama zilivyo ahadi nyingine lukuki zinazoendelea kutolewa kila kukicha.

Wasomaji

200
Wasiliana


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.