29 Aug 2014


Ninaandika makala hii nikitambua bayana kuwa itamuudhi kila mtu anayeingia mtandaoni kwa minajili ya kuwanyanyasa watu wengine. Lakini siku zote ninaamini katika busara hii: kuuchukia ukweli hakuufanyi kuwa uongo. Ukweli ni ukweli na uongo ni uongo. Ukweli hauwezi kuwa uongo, na kadhalika uongo hauwezi kuwa ukweli. Kamwe asilani.

Wakati tunaomboleza kifo cha ndugu yetu Betty Ndejembi hatuwezi kukwepa ukweli kwamba siku chache kabla ya kifo chake binti huyo alinynyaswa mno kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter. Japo hadi muda huu hatuwezi kuhusisha moja kwa moja uhusiano kati ya unyanyasaji huo na kifo cha binti huyo, ukweli tu kwamba mtu akinyanyaswa masaa kadhaa kabla ya kifo chake, waweza kujenga picha flani.

Naomba ieleweke kuwa simlaumu mtu kwa sababu sina mamlaka ya kufanya hivyo bali dhima ya makala hii ni rambirambi zangu na kuzungumzia tatizo la unyanyasaji mtandaoni, sambamba na suala zima la unafiki kila kinapojiri kifo hususan cha mtu maarufu.

Tuna tatizo kubwa huko mitandaoni. Tumefika hatua ya kuwapa umaarufu watu wenye matusi ya nguoni, wazushi, wambeya, wanafiki, wanaharamu na kila aina ya binaadamu wanaostahili laana lakini twaishia kuwatukuza. Kwa Twitter, matusi imekuwa ni njia ya mkato ya kupata umaarufu. Kuna wenzetu wengi tu wenye 'umaarufu' huko Twitter, na ukidadisi chanzo cha 'umaarufu' huo, utaambiwa 'ah huyu ana matusi si mchezo!'

Kuna watu wazima na akili zao wanatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii aidha kunyanyasa wenzao kama si kusherehesha unyanyasaji huo. Marehemu aliitwa majina kadhaa ya kumdhihaki kabla ya kukutana na mauti. Japo sijui chanzo cha 'ugomvi na aliogombana nao' (na ndio maana sikujihusisha nao kwani haukunihusu), kuna wanafiki wengi tu waliokuwa katika nafasi nzuri ya kuzima moto huo hasa kwa vile baadhi yao walikuwa wakizifahamu pande zote mbili za 'ugomvi' husika.


La kukera zaidi ambalo ni wazi litajichomoza wakati wa maombolezo haya ni unafiki: baadhi ya watu walewale waliodiriki kumwandama marehemu wakati wa uhai wake watageuka kuwa wenye uchungu mkubwa baada ya kifo chake. Hii inanikumbusha suala ambalo nimeshawahi kulizungumzia mara kadhaa, katika hali ya utani japo wenye uweli, kwamba 'wakati mwafaka kabisa wa kutafuta vipaji vya uigizaji ni kwenye misiba: watu walewale waliokuwa wakikuchukia kwa nguvu zote watageuka wenye uchungu mkubwa kwa kifo chako.

Ukiangalia baadhi ya tweets za mwisho za marehemu ni wazi kuwa binti huyo alikuwa anahitaji msaada kutoka kwa wanaomjali




Hata pasi uelewa wa taaluma ya saikolojia, tweets za aina hii zinaashiria tatizo, na laiti 'wenye upendo wa dhati' wangeingilia kati muda huo, huenda muda huu Betty asingekuwa marehemu. 


Na hizo tweets mbili ambazo ni miongoni mwa za mwisho kabisa za marehemu ni ushuhuda tosha wa jinsi alivyokuwa akisumbuliwa na wanyanyasaji dhidi yake mtandaoni. Ndio pengine kilichomuua ni maradhi ya kawaida ya kibinadamu lakini kila mwenye ubinadamu hatoshindwa kuhusisha unyanyasaji huu na hali mbaya ya afya aliyokuwa nayo hadi anafariki.

Kuna watakaolaumu kuwa ninatumia kifo cha binti huyo kwa 'maslahi binafsi.' Hapana, sina maslahi yoyote binafsi hasa ikizingatiwa kuwa sikuwa nikifahamiana na marehemu. Hakuna anani-follow na mie sikuwa nam-follow. Labda maslahi pekee niliyonayo ni upinzani wangu mkali dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni. Vyovyote ilivyo, marehemu alikuwa bullied kabla hajafariki na atakayetaka kukataa ukweli huo na akatae lakini utabaki kuwa ukweli usioweza kugeuka uongo. Na kwa hakika, kila aliyeshiriki kumnyanyasa binti huyo atakuwa anasutwa na nafsi yake, hata kama atatafuta hifadhi kwenye 'huu sio wakati wa kulaumiana' au 'we failed you Betty.' 

Mara nyingi nimekuwa nikiwalaumu watu wanaodai 'Instagram imekuwa mbaya' au Twitter imeharibika siku hizi' ambapo mara zote nimewakumbusha wahusika kuwa katika hii mitandao ya kijamii, ni muhimu kuwa makini katika nani wa kum-follow. Maana yangu ni kwamba ukim-follow mtu mwenye matusi, utashuhudia matusi katika anachoandika. Ukim-follow mtu wa busara, utashuhudia busara.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni kumeibuka kundi kubwa tu la watu wenye busara na elimu zao lakini wepesi wa kuvutiwa na vitu vya 'kipuuzi' - umbeya, matusi, majungu, na upuuzi mwingine, na hawasiti kushea na wanaowa-follow. Ni hivi, mtu akitweet tusi, kisha ukali-retweet, utambue kuwa unalikuza (amplify) tusi hilo. Na kimsingi, kwa kiasi kikubwa, tuna-RT vitu tunavyoviunga mkono. Uki-RT tusi maana yake unaliunga mkono. Na ni wazi mwenye kujiheshimu, na kuheshimu 'watu wa maana' wanaom-follow hawezi ku-RT upuuzi.

Tatizo kubwa sasa ni kwamba waweza kuamua kuwa-follow watu unaodhani wana busara au akili za kutosha lakini ukaishia kusoma vitu vya ajabu ajabu kwenye timeline yako kutokana na haya 'mahaba' ya ku-RT vitu vya kipuuzi. 

Binafsi, nadhani chanzo kikubwa cha mitandao ya kijamii kuwa 'sehemu za kukera, kuogopesha, kunyanyasana, nk' ni ile hali ya baadhi ya wenzetu kutokuwa na vitu muhimu vya kufanya katika maisha yao. Ni wazi kwamba ukiwa busy na maisha yako hutokuwa na muda wa kubughudhi wenzako. 

Kingine kinachopelekea social media kuwa 'dunia uwanja wa fujo' ni ugonjwa mkubwa unawasumbua baadhi ya wenzetu: kusaka sifa wasizostahili. Wanasema,. ashakum si matusi, 'lugha ya mpumbavu ni matusi,' na ndo maana baadhi ya wenzetu wasio na cha maana cha kuongea katika hadhara hukimbili matusi, unyanyasaji, maneno macha

Nitamke bayana kuwa siandiki makala hii nikitegemea kuungwa mkono na wahusika wa unyanyasaji mtandaoni. Na kwa hakika kuna uwezekano mkubwa wa makala hii kuzua 'kampeni ya chuki' dhidi yangu kutokana na makala hii. Tatizo kubwa la wenzetu hawa ni kutotaka kuambiwa kuwa 'Hapana, hili ni kosa. Na kosa ni kosa, haliwezi kuwa sahihi.' Lakini pamoja na uwezekano wa 'kuwashiwa moto' kutokana na makala hii, wito wangu kwa kila mwenye busara na akili ni kuliangalia tukio hili la kusikitisha kama 'wake up call.' Tujifunze, tujisahihishe. Tuache kusherehesha vitu vya kipuuzi mtandaoni.

Ifike mahala, ukishindwa kumkemea mtu mwenye tabia mbaya mtandaoni basi chukua option  rahisi ya kum-unfollow au ikibidi kum-block. Na ifike mahala kuwafahamisha watu wanaoendekeza utoto, majungu, umbeya, unyanyasaji na upuuzi mwingine kuwa kama hawana kitu cha maana cha kufanya katika maisha yao basi isiwe sababu ya kuwasumbua wenzao wenye majukumu katika maisha yao.

Tukemee maovu badala ya kutarajia yataondoka yenyewe tu. Tuomboleze kifo cha Betty kwa kusema 'NO' kwa cyberbullies (wanyanyasaji wa mtandaoni). Tufike sehemu tuache kuwasujudia wahuni wanaodhani matusi ni sehemu ya wimbo wa taifa. Tuwakwepe waendekeza majungu, wanyanyasaji, wataka sifa za kipuuzi, na watu wasiofaa katik maisha yetu.


Wakati 'tunatafuta haki kwa marehemu Betty kutokana na unyama aliofanyiwa,' suala ambalo ni la kisheria, kilicho ndani ya uwezo wetu ni kukemea unyanyasaji mtandaoni (cyber bullying). Wakati hadi muda huu hatuwajui waliomfanyia marehemu unyama huo, takriban sote twawajua vema wanyanyasaji wa mtandaoni. Tuanze na hawa, kwani leo wamefanya kwa kwa marehemu Betty kesho itakuwa kwako.

Mwisho kabisa, ni muhimu kwetu sote kutambua kuwa tulitoka kwa udongo na tutarudi kwa udongo. Kifo ni hatma ya kila mmoja wetu.Betty ametutoka lakini nasi twaelekea huko. Visa, chuki, kunyanyasana, na vitu vingine visivyopendeza japo ni kama sehemu ya maisha yetu havipaswi kupewa nafasi katika maisha yetu haya ambayo hakuna mmoja wetu mwenye japo 'lue' ya lini yatafikia kikomo. TUPENDANE na TUHESHIMIANE.

Kwako marehemu Betty, hakuna tunaloweza kusema au kufanya sasa kurejesha uhai wako. Na hakuna neno sahihi la kuonyesha jinsi gani kifo chako kimewagusa wengi. Kubwa tunaloweza kufanya ni kukuombea kwa Mwenyezi Mungu akupatie pumziko la milele na mwanga wa milele akuangazie upumzike kwa amani. Amina.




28 Aug 2014

Kabla ya kukuletea 'darasa' hili ni vema nikakufahamisha kitu kimoja: 'tabia' iliyozoeleka miongoni mwa Wamarekani wengi kudhani kuwa 'dunia' inaishia kwenye mipaka ya nchi hiyo tu. Kuna idadi kubwa tu ya Wamarekani wasio na habari na 'dunia nje ya Marekani,' na pengine ndo maana si ajabu kukutana na 'Kombe la Dunia' la mchezo flani nchi humo linalohusisha timu za Marekani pekee...kwa vile kwa mtizamo wa wengi, Marekani ndio dunia.

Twende kwenye mada husika. Pengine kutokana na mtizamo huo fyongo, baadhi ya watengenezaji apps za simu 'hujisahau' na kudhani wamiliki pekee wa simu wapo Marekani hivyo apps zao zikiwekwa Google Play, kwa mfano, zinaweza kutumika nchini humo tu. Na hii ni moja ya sababu za kukutana na ujumbe "This app is not available in your country."

Lakini next time ukikutana na ujumbe huo usipaniki, kwani darasa lifuatalo linakueleza kiufasaha jinsi unavyoweza 'kuizunguka amri hiyo,' na kufanikiwa ku-download app yoyote ile katika simu yako, alimradi iwe 'compatible.'

Fuatilia video ifuatayo, lakini kama utakwama mahali flani basi usisite kuwasiliana nami kwa ufafanuzi zaidi.



Kwa habari zaidi za teknolojia, endelea kutembelea blogu hii, na rahisisha zoezi hilo kwa kubonyeza menu ya TEKNOLOJIA hapo juu. Karibuni sana.

26 Aug 2014


debate pair
The poll followed an ill-tempered referendum debate in which Salmond forced Darling onto the back foot.
Alistair Darling defeated by a 71% to 29% margin, according to Guardian/ICM poll of Scots who watched the debate





Alex Salmond emerged as the clear winner of the second Scottish independence debate, besting Alistair Darling by a 71% to 29% margin, according to an instant Guardian/ICM poll of Scots who had watched the debate.
Salmond will be delighted to decisively overturn the verdict in the first round, in which a similar ICM poll found Alistair Darling had won by 56% to 44%.
The poll followed an ill-tempered referendum debate in which Salmond forced Darling onto the back foot on the currency, the NHS and Labour's decision to partner with the Conservatives in the Better Together campaign against independence.
The headline figures exclude viewers who say they don't know who won the debate – with these included the figures are 65% for Salmond, 26% for Darling, and 9% who were not sure.
As in the first debate, Alex Salmond was deemed to have the "more appealing personality", this time enjoying an 54% to 32% advantage on this count. But the difference this time came on the question of who had the best arguments. While Darling had the advantage last time around, this time Salmond leapt ahead to take a commanding 56% to 36% lead.

Morale in the yes camp will be boosted by the extraordinarily emphatic win that Salmond notched up among those who had gone into the evening planning to vote for independence – 98% of those expressing a view gave it to the first minister, and only 2% to Darling. In contrast, things were much more balanced among no voters – 59% gave Darling the edge, but a substantial 41% felt Salmond had the better night.
ICM weighted the sample to representative of the Scotland population by age, gender, region and previous voting behaviour (reported 2011 vote for the Holyrood election). But it is important to bear in mind that this is a survey of voters who actually watched the debate, as opposed to the electorate as a whole. Going in to the debate, this sample was more pro-independence than most polls of voters as a whole have suggested – splitting 44% yes to 46% no with 10% not sure. Over the course of the debate, there was little change in this balance. The don't knows dropped back two percentage points to eight, while both yes and no edged up one each to 45% and 47% respectively as a fraction of viewers made up their mind.
ICM pre-recruited a sample of 1,155 people who said they would be watching the debate live and who agreed to complete the survey immediately afterwards, which they were duly sent. All participants were recruited from ICM's own online panel plus those of two of the biggest suppliers of Scottish panel in the market research industry. The post-debate survey data is based on 505 completed interviews. ICM is a member of the British Polling Council and abides by its rules.
SOURCE: The Guardian

25 Aug 2014



 


Mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola hadi hivi karibuni ulikuwa katika baadhi ya nchi za Afrika Magharibi pekee: Sierra Leone,Liberia, Nigeria, na Guinea. Sasa nchi ya tano imeingia kundini,imeripotiwa kuwa watu wawili wamefariki kwa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC)- zamani Zaire- nchi iliyopo Afrika ya Kati.

Waziri wa Afya wa DRC, Dr Felix Kabange Numbi, ameeleza kuwa watu wawili wamefariki kwa Ebola, Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.Kwa mujibu wa ripoti, tayari kuna vifo 13 vilivyosababishwa na ugonjwa huo hatari. Awali, Shirika la Afya Duniani (WHO) lilidhani vifo hivyo havihusiani na Ebola hadi ilipothibitishwa na DRC kuwa vimetokana na Ebola.

Uhusino kati ya Ebola DRC na mlipiko katika nchi za Afrika Magharibi hauko bayana, huku WHO ikieleza kuwa bado inaendelea na uchunguzi, hasa kubaini iwapo dalili za 'Ebola ya DRC' ni sawa au tofauti na ile ya Afrika Magharibi.

Hadi mwaka huu, milipuko iliyopita ya Ebola ilikuwa Afrika ya Kati, huku DRC ikiwa mhanga wa mara kwa mara. Kwa mara ya kwanza, Ebola iligundulika eneo hilo mwaka 1976

Je Ebola itaibukia wapi kwingine?

Hadi sasa kumekuwa na matukio yanayohusishwa na Ebola katika bara la Ulaya, Asia na Amerika ya Kaskazini, lakini katika matukio yote, wagonjwa walipimwa na kugundulika hawajaambukizwa ugonjwa huo. Wataalam wa afya hawana hofu ya Ebola kusambaa katika nchi zilizoendelea, kwa sababu milipuko ya ugonjwa huo hujitokeza zaidi katika nchi zenye maji yasiyo salama na zisizo na raslimali za kupambana nao, na sio mataifa tajiri kama Marekani.

Kwa sasa, uwezekano mkubwa wa kusambaa kwa Ebola katika maeneo ambayo hayajaathiriwa ni watu wanaosafiri kutoka eneo moja hadi jingine.Kwa kiwango cha nchi, uwezekano mkubwa wa kusambaa kwa ugonjwa huo ni kwa safari za ndege.

Hadi kufikia Agosti 22  mwaka huu kuna matukio 1082 ya Ebola na vifo 624 vilivyoripotiwa kutokana na ugonjwa huo hatari 

Imetafsiriwa kutoka tovuti ya kituo cha runinga cha VOX

24 Aug 2014

Leaving: Brown is seen walking to his Lamborghini after the drama at 1Oak in Los Angeles
Chris Brown akielekea kwenye Lamborghini lake kuondoka katika klabu ya usiku palipotokea shambulio la risasi
Prodyuza Marion Suge Knight (pichani chini) amejeruhiwa kwa risasi amejeruhiwa kwa risasi katika shambuli lililotokea katika pati iliyokuwa ikiendeshwa na msanii Chris Brown.
Music producer Suge Knight has been injured during a shooting at an awards show party at a Los Angeles nightclub hosted by singer Chris Brown, it has been reported
Mashuhuda wanaeleza kuwa msanii huyo ambaye bado yupo katika msamaha wa uchungu (parole) baada ya kutoka jela hivi karibuni ndiye alikuwa mlengwa wa shambulio hilo, ambapo alikuwa MC wa pati ya utangulizi wa Tuzo za Video za Muziki (MVA) zitakazofanyika leo usiku (kwa saa za Marekani).
OK now: Brown smiled as he left the nightclub where he was reportedly targeted by a gunman
Inadhaniwa kuwa Chris hakuumia katika shambulio hilo, lakini watu wengine watatu, akiwemo Suge Knight, mwanzilishi wa lebo ya muziki ya Death Row Records iliyokuwa ikitumiwa na msanii mwingine maarufu wa nchi hiyo, Marehemu Tupac Shakur, walijeruhiwa na kupelekwa hospitali ya Cedar's Sinai. Inaelezwa kuwa mmoja wa majeruhi hao yupo taabani.
Witnesses: Partygoers talk to emergency personnel after the shooting 
Mwanamitindo na mcheza filamu Tyson Beckford na memba wa kundi la Black Eyees Peas Apple De Ap walikuwa miongoni mwa waliohudhuria pati hiyo, na walieleza kuwa walisikia sauti nne za risasi mida ya saa 7.30 alfajiri ya kuamkia leo.
Treatment: Another victim is fitted with a neck brace following the dramatic shooting
Majeruhi akitibiwa
Suge Knight ambaye kwa sasa anamiliki kampuni ya muziki ya Black Kapital Records alionekana na polisi  nje ya ukumbi baada ya shambulio hilo na akachukuliwa katika gari la kubeba wagonjwa. Inaelezwa kuwa alipigwa risasi mbili, na kujeruhiwa tumboni na mkononi na sasa anafanyiwa upasuaji.
Host: Brown enjoys the party before the alleged shooting took place
Chris Brown 'akijirusha' kabla ya shambulio
Waliofanya shambulio hilo walikamatwa na polisi ambao sasa wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Mastaa wengine waliokuwa kwenye pati hiyo ni pamoja na Justin Beiber na rapa The Game.
Guests: Justin Bieber (right) was among the guests at the VMA Pre-Party hosted by  Brown
Justin Beiber alikuwa miongoni mwa waliohudhuria pati hiyo, kama ilivyokuwa kwa rapa The Game (pichani chini)

Jayceon Terrell Taylor, aka The Game attends a VMA Pre-Party hosted by Chris Brown and Pia Mia
Iliposikika milio ya risasi hizo, Chris Brown alionekana akiruka kuelekea kwenye eneo la baa katika klabu hiyo ya usiku (nightclub), huku kwa hasira akiwaagiza watu wengine kujikinga.
Aftermath: Brown jumped on a table after the shooting, apparently furious at what had taken place
Chrsi Brown akiruka kuelekea eneo la baa baada ya milio ya risasi
Saa 12 kasorobo asubuhi ya leo, msanii huyo alitwiti


Akimaanisha 'Jamii haiwezi kustarehe au kuburudika pasipo mikwaruzo.'
Injured: Another victim is transferred into an ambulance in a stretcher
Majeruhi wakiingizwa kwenye gari la kubebea wagonjwa
Angry: Brown at first appeared to still be furious when he made his way from the West Hollywood club
Chris Brown akiwa ametahayari baada ya shambulio hilo



CHANZO : The Mail Online




Smart mannequins that ¿talk¿ to shoppers through their smartphones will go live today in branches of House of Fraser, Hawes & Curtis and the Bentalls department store

Tafsiri: 1. Duka la nguo linaingiza mtandaoni taarifa kuhusu bidhaa husika.

2. Mteja anapaswa ku-download app iitwayo Icneme katika simu yake ili kuwezesha connection ya Bluetooth.

3. Mteja akipita futi 150 karibu ya duka husika, anapata ujumbe katika simu yake, na sasa anaweza kupata taarifa kamili ya nguo husika ilivyovaliwa na mdoli (mannequin) wa maonyesho ya nguo dukani.

4. App iliyomo kwenye simu ya mteja itamwonyesha malili ilipo nguo husika ndani ya duka husika. Pia itampa kiungo (link) ya tovuti ya duka hilo kumwezesha kuinunua nguo hiyo katika muda wowote ule, iwe mchana au usiku.


Kaleem, a keen cricketer, said the teachers at his school have told him other children are 'scared' of his hands

Doctors in India have been left baffled by his growing hands and many are at a loss as to what the condition is

The youngster has difficulty eating, tying his shoelaces and carrying out other basic tasks due to his  hands

Kaleem's father Shamim, 45, (pictured together above) is worried his son will never become independent

Kaleem, from India, was born with hands twice the size of an average baby and they have continued to grow

Mtoto wa miaka minne nchini India, Kaleem (pichani) amewachanganya madaktari kufuatia mikono yake kuvimba kupita kiasi na sasa imefikia uzito wa kilo 12. Mtoto huyo kwa sasa anashindwa kutekeleza japo majukumu madogo tu kama kufunga 'kamba' (laces) za viatu vyake baada ya kuzaliwa akiwa na mikono mikubwa mno.

Kaleem anadai amekuwa akibughudhiwa mno na watoto wenzie wanaomcheka kutokana na maumbile hayo ya ajabu. "Napata mguu kuvaa nguo zangu, kufunga vifungo hata kuvaa nguo ya ndani, anasema mtoto huyo ambaye mama yake alibaini maradhi yake tangu akiwa mdogo lakini hakuwa na cha kufanya kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha. Wazazi wa Kaleem wana kipato kisichozidi Paundi za Kiingereza 15 (takriban Tsh 42,000) kwa mwezi.

Baba yake, Shamim, anahofu mwanae hatoweza kujitegemea maishani, na anajilaumu kwa kushindwa kumhudumia kutokana na uwezo duni wa kifedha. Dr Ratani, mkurugenzi wa kituo cha afya kilichomfanyia uchunguzi mtoto huyo anakiri kuwa maradhi hayo ni ya ajabu na magumu kutibika. 

CHANZO: The Mail Online



 Only men who suffered impotence as a side effect of illness or those evaluated by a specialist could be given the pills on the NHS
Mamia kwa maelfu ya wanaume hapa Uingereza wanatarajiwa kunufaika na uamuzi wa Taasisi ya Huduma za Afya (NHS) kulegeza masharti ya upatikanaji wa vidonge vya kuboresha nguvu za kiume, Viagra.

Hadi mwezi huu, watu pekee walioruhusiwa kupewa Viagra hospitalini ni wale ambao pungufu wa nguvu zao za kiume ulitokana na athari za matibabu ya maradhi mengine (side effects).

Lakini tangu taratibu za usajili na upatikanaji (patent) ya Viagra ilipoisha muda wake mwaka jana, bei ya vidonge hivyo imeshuka kwa asilimia 93 kwa vile makampuni mengine ya madawa yameruhusiwa kutengeneza aina zisizo asili (generic) za vidonge hivyo.

Kutokana na hali hiyo, NHS imeeleza kuwa watu wote wenye matatizo ya nguvu za kiume wanaruhusiwa kupata Viagra. Madaktari wengi wamefurahishwa na uamuzi huo wakiamini kuwa utasaidia kuboresha mahusiano ya kinyumba na hata kuokoa ndoa.

Hadi 'patent' ya Viagra inakwisha muda wake, Viagra ilikuwa ikiuzwa kwa Paundi za Kiingereza 21.27 (Tsh 58,567.39) kwa pakti ya vidonge vinne lakini bei hiyo sasa imeshuka hadi Paundi .1.45 (Tsh 3,992.61)kwa pakti moja ya vidonge vinne.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.