Showing posts with label IDARA YA USALAMA WA TAIFA. Show all posts
Showing posts with label IDARA YA USALAMA WA TAIFA. Show all posts

10 Feb 2017


Kwamba Idara yetu ya Usalama wa Taifa imekuwa ikibebeshwa lawama mbalimbali kwa takriban 'kila baya' linaloihusu Tanzania yetu, sio siri. Ni kitu cha wazi ambacho ninaamini hata wana-Usalama wetu pia wanakifahamu.

Hata hivyo, kwa kiasi kikubwa lawama hizo huchangiwa na uelewa mdogo au usiopo kabisa kuhusu dhamana muhimu ya taasisi za usalama wa taifa kwa nchi husika, na jinsi taasisi hizo zinavyofanya kazi muda wote kuhakikisha usalama wa nchi husika.

Lakini pengine kabla ya kuingia kiundani kuhusu mada yangu, nigusie maongezi yangu na jamaa yangu mmoja, shushushu mstaafu kutoka nchi moja ya Afrika Magharibi. Jana aliamua 'kunifungukia,' kwanini mtu mwenye umri wa kati kama yeye ni 'shushushu mstaafu' (tumezowea kuona wastaafu wakiwa watu wenye miaka 50 na kuendelea, lakini huyo bwana ni wa umri wa miaka thelathini na kitu tu).

Alinidokeza kwa kifupi kuwa alilazimika 'kutoroka' nchini kwake baada ya kufeli kwa jaribio la mapinduzi katika taifa analotoka ambalo huko nyuma lilikuwa kama linapendelea zaidi mapinduzi kuliko chaguzi.  Alidai kuwa "mapinduzi hayo yalikuwa ni kwa minajili ya kuikwamua nchi hiyo kutoka katika nira ya utawala wa kidikteta wa kijeshi."

Hadi kufikia hatua hiyo ya maongezi hayo, ilitokana na huyo jamaa kuwa alitembelea kwenye ukurasa wangu wa Facebook, na kuona matangazo ya kitabu changu kuhusu taaluma ya Uafisa Usalama wa Taifa (USHUSHUSHU). Awali hakuelewa kitabu kinahusu nini kwa sababu maelezo yote kuhusu kitabu hicho yapo kwa Kiswahili, na yeye haielewi lugha hiyo. Alichofanya ni "kuomba msaada wa Google Translate," na akaweza kufahamu kitabu hicho kinahusu nini.

Akanambia kuwa amevutiwa sana na kitabu hicho kwa sababu kwa Bara la Afrika lina uhaba mkubwa mno wa katika fasihi simulizi kuhusu taaluma ya Uafisa Usalama wa Taifa. Na akanishauri nianze haraka iwezekanavyo kukitafsiri kitabu hicho kwa lugha ya Kiingereza ili kiweze kuwafikia wana-Usalama wengi zaidi katika nchi mbalimbali zenye uhaba mkubwa wa maandiko ya wazi kuhusu taaluma yao.

Japo sijawahi kuliongelea hili hadharani, moja ya mafanikio mkaubwa mno ya kitabu hiki yamekuwa katika wananchi wa kawaida kuielewa Idara ya Usalama wa Taifa kwa mtazamo chanya zaidi, hasa kutokana na maelezo ya kina ya kazi za taasisi hiyo muhimu kabisa kwa ustawi na uhai wa taifa lolote lile.

Angalia pongezi za msomaji mmoja wa kitabu hicho


Na kwa hakika, licha ya kuandika kitabu hicho kwa ajili ya jamii kwa ujumla, walengwa wakuu pia ni maafisa usalama wa taifa popote pale walipo. Kwa umahiri mkubwa, kitabu kimeepuka 'kuandika yasiyopaswa kuandikwa,' na kuwekea mkazo katika maoeneo ambayo licha ya kujenga ufahamu, yanasaidia kuwaelimisha raia kuwa Idara za Usalama wa Taifa ni kama roho na pumzi za taifa lolote lile. 


Naomba kutumia fursa hii kuwakaribisha ndugu zangu wa Idara ya Usalama wa Taifa kukinunua kitabu hiki kwa minajili ya kujielimisha, sambamba na kupata mtazamo wa 'akina sie' ambao ni wadau wa sekta ya Usalama wa Taifa. 

Kadhalika, kitabu hiki ni dedicated kwa Maafisa wa Usalama wa Taifa popote pale walipo, hasa kwa kutambua safari ndefu na ngumu waliyopitia hadi kufika walipo sasa, na "kuwa kwao macho masaa 24 ya siku 365 za mwaka" kwa minajili ya usalama wa mataifa yao. 


Kwa walio nje ya Tanzania, kitabu kinapatikana www.chahalibooks.com na AMAZON 

Kwa Tanzania, kitabu kinapatikana katika maduka ya vitabu yafuatayo


DAR ES SALAAM:

TPH BOOKSHOP, 24 Samora Street jirani na Sapna (Simu 0687-238-126/ 0759-390-082);
GENERAL BOOKSELLERS, Mtaa wa Mkwepu (Simu MAMA MEENA 0784-887-871)
DAR ES SALAAM BOOSHOP, Mtaa wa Makunganya (Simu MR MPONDA 0657-827-172)
MLIMANI BOOKSHOP, Kariakoo (Simu 0754-269-042)
ZAI BOOKSHOP, Kariakoo (Simu0754-292-532)
ELITE BOOKSTORE, Mbezi Beach Tangi Bovu karibu na Goba Road (Simu 0754-767-336)

MOSHI: APE BOOK, Rindi Lane, Opoosite I&M Bank (Simu 0754767336)

ARUSHA: KASE BOOKSTORE, ELCT Building, Joel Maeda Street

TANGA: HAFAT BOOKSHOP, Barabara ya Saba (Simu HASSAN SHEDAFA 0767-216-403)

MWANZA:
GUNDA BOOKSHOP Karibu na NHC Regional Office Bantu Street/Kemondo (Simu 0753-969-421)
VICTORIA BOOKSHOP, along Bantu Street, Kemondo (Simu 0755-375-034)

MUSOMA: NYAMBUSI BOOKSHOP, Opposite NMB Bank Main Branch (0767-578-565)

IRINGA: LUTENGANO INVESTMENT (Bakwata House), Miomboni St mkabala na Akiba House (Simu 0763-751-978)

KIGOMA: NDAMEZYE ENTERPRISES, Mkabala na NBC Bank (0713534116)

MBEYA VOLILE BOOKSHOP, Mount Loleza, mkabala na TRA (Simu SANGA 0754412075)

MOROGORO: Wasiliana na Marcelino kwa simu 0767612566 ; 0621081500; 0655612566. 






27 Aug 2016

Tarehe 24 mwezi huu, Rais Dokta John Magufuli alimteua Dokta Modestus Kipilimba kuwa Mkurugenzi Mkuu (DGIS) wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS). Uteuzi huo umefanyika kufuatia kustaafu kwa mkurugenzi aliyemaliza muda wake, Othman Rashid.

Makala hii inajikita katika uchambuzi wa uteuzi huo kwa kuangalia changamoto na fursa zinazomkabili kiongozi huyo mkuu wa taasisi hiyo nyeti kabisa. Kwa mtizamo wangu, kama kuna kitu ambacho kinaweza kuzua maswali kuhusu uteuzi huo basi ni wadhifa wa Director of Risk Management alioshikilia Dokta Kipilimba huko nyuma alipokuwa mtumishi wa Benki Kuu ya Tanzania.

Sote twafahamu jinsi Benki Kuu yetu imekuwa ikiandamwa na matukio mfululizo ya ufisadi, kuanzia EPA hadi Tegeta Escrow. Kwa wadhifa wake katika taasisi hiyo, kuna uwezekano wa bosi huyo mpya wa mashushushu kuonekana ‘sehemu ya mfumo ulioshindwa kudhibiti ufisadi.’ Hata hivyo, utetezi unaweza kuwa huenda yeye alitekeleza majukumu yake vema lakini walio juu yake hawakuchukua hatua stahili.

Kadhalika, huko mtandaoni kuna ‘tuhuma’ kadhaa kuhusu Dokta Kipilimba, lakini itakuwa sio kumtendea haki yeye, blogu hii na mie mwenyewe kujadili tuhuma ambazo hazina ushahidi wowote. Ni muhimu kutambua kuwa Tanzania yetu licha ya kuwa kisiwa cha amani pia ni kisiwa cha majungu, uzandiki, fitna, umbeya na uzushi.

Changamoto kubwa kwa Dokta Kipilimba ni pamoja na kurejesha hadhi na heshima ya Idara ya Usalama wa Taifa. Katika miaka ya hivi karibuni, taasisi hiyo muhimu kabisa imekuwa ikishutumiwa kuwa inachangia ustawi wa ufisadi, ujangili, biashara ya madawa ya kulevya, nk.

Wanaoilaumu taasisi hiyo hawamaanishi kuwa watumishi wake wanahusika katika matukio hayo ya kihalifu as such bali kushindwa kwa Idara hiyo kukabiliana na kushamiri kwa matendo hayo ya kihalifu, ambayo kimsingi ni matishio kwa usalama wa taifa, na kazi kuu ya Idara hiyo ni kukabiliana na matishio kwa usalama wa taifa la Tanzania.

Ninaamini kuwa Dokta Kipilimba anafahamu kanuni muhimu kuhusu ufanisi au mapungufu ya idara ya usalama wa taifa popote pale duniani, kwamba “kushamiri kwa vitendo vinavyotishia usalama wa taifa lolote lile ni kiashiria cha mapungufu ya idara ya usalama wa taifa ya nchi husika, na kudhibitiwa kwa vitendo vinavyotishia usalama wa taifa popote pale duniani ni kiashiria cha uimara wa idara ya usalama wa taifa ya nchi husika.”

Kwahiyo, kwa kuzingatia kanuni hiyo, kushamiri kwa biashara ya madawa ya kulevya, ujangili, rushwa, na ufisadi mwingine ni viashiria vya mapungufu ya Idara yetu ya Usalama wa Taifa.

Changamoto nyingine kwa Dokta Kipilimba ni tuhuma za mara kwa mara dhidi taasisi hiyo muhimu kabisa kuwa katika utendaji kazi wake imegeuka kuwa kama ‘kitengo cha usalama cha chama tawala CCM.’ Idara hiyo imekuwa ikituhumiwa kuwa kwa kiasi kikubwa imeweka kando taaluma ya ushushushu (tradecraft) na kutekeleza majukumu yake kisiasa.

Madhara ya muda mfupi ya kasoro hiyo ni taasisi hiyo kujenga uhasama na vyama vya upinzani na kwa namna flani kupoteza heshima na uhalali wake. Lakini la kuogofya zaidi ni madhara ya muda mrefu, ambapo watu wanaoweza kuwa ni matishio kwa usalama wa taifa letu wanaweza kutumia ‘urafiki’ unaodaiwa kuwepo kati ya Idara ya Usalama wa Taifa na CCM, wakitambua bayana kuwa ‘Idara haina muda na makada wa chama tawala,’ na hatimaye kufanikiwa kutimiza azma zao ovu.

Baadhi ya watumishi wa zamani wa taasisi hiyo walijikuta matatizoni kwa vile tu walitekeleza majukumu yao dhidi ya wanasiasa wa chama tawala, na wakaishia kuonekana kama wahaini.

Changamoto nyingine kwa Dokta Kipilimba ni tuhuma zinazoikabili taasisi hiyo kuhusu mfumo wa ajira ambapo inadaiwa kuwa zimekuwa zikitolewa kwa upendeleo kwa ndugu na jamaa za ‘vigogo.’ Tatizo kubwa hapa ni kwamba utiifu wa ‘ndugu na jamaa hao wa vigogo’ haupo kwa taifa bali kwa vigogo hao waliowaingiza Idarani. Pengine sio vibaya kufikiria ‘utaratibu wa wazi’ katika ‘recruitment’ kama inavyofanywa na wenzetu wa CIA, NSA, MI5, MI6, HGCQ, nk wanaotangaza nafasi za ajira kwenye vyombo vya habari.

Pia kuna tatizo la baadhi ya maafisa usalama wa taifa ‘kujiumbua’ kwa makusudi kwa sababu wanazojua wao wenyewe, kubwa ikiwa kutaka sifa tu, au waogopwe ‘mtaani.’ Hii inaathiri sana ufanisi wa maafisa wa aina hiyo kwani ni vigumu kutekeleza majukumu yao ipasavyo pasi usiri.

Sambamba na hilo ni kasumba ya muda mrefu ambapo baadhi ya maafisa wa Idara hiyo waliopo kwenye vitengo mbalimbali kuwepo huko kwa muda mrefu mno kiasi cha kuathiri utendaji wao. Miongoni mwa maeneo hayo ni pamoja na ‘vituo muhimu’ na kwenye ofisi za balozi zetu nje ya nchi. Ikumbukwe kuwa unless afisa ametengeneza deep cover, uwepo wake kwa muda mrefu katika sehemu aliyokuwa ‘penetrated’ au kituo chake cha kazi kwingineko (mfano ubalozini) unaweza kupelekea ‘akaungua’ (burned).

Changamoto nyingine kubwa ni uwepo wa majasusi kibao nchini mwetu, hususan kutoka nchi moja jirani, huku wengi wa majasusi hao wakiwa wameajiriwa katika taasisi za umma na binafsi. Hili ni tishio kubwa kwa usalama wa taifa wa Tanzania yetu.

Kwa upande fursa kwa Dokta Kipilimba, licha ya kuwa ‘mwenyeji’ katika taasisi hiyo muhimu, wasifu wake kitaaluma unamweka katika nafasi nzuri sana kukabiliana na changamoto za karne ya 21 ambayo imetawaliwa zaidi na teknolojia ya kisasa.

Dokta Kipilimba ni msomi aliyebobea kwenye teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) na yayumkinika kuamini kuwa anaweza kutumia usomi wake kuibadilisha Idara yetu ya Usalama wa Taifa kwenda na wakati, kufanya kazi kama taasisi ya kishushushu ya karne ya 21, ambayo licha ya kutegemea HUMINT inaweza pia kutumia njia nyingine za kukusanya taarifa za kiusalama kwa kutumia teknolojia (GEOINT, MASINT, SIGINT, CYBINT, FININT na TECHINT kwa ujumla)

Na katika kwenda na teknolojia ya kisasa, basi pengine si vibaya iwapo Idara yetu ikafikiria haja ya uwepo wake kwenye mtandao, kwa kuwa na tovuti yake kamili na pia kufungua akaunti kwenye mitandao ya kijamii, hususan Twitter na Facebook. Hii sio tu inaweza kusaidia kutengeneza "human face" ya intel service bali pia yatoa fursa nzuri katika OSINT.

Fursa nyingine kwa Dokta Kipilimba ni matarajio ya sapoti ya kutosha kutoka kwa Rais Dokta Magufuli ambaye kama alivyoahidi wakati wa kampeni za kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka jana, mapambano dhidi ya ufisadi yamepewa kipaumbe cha hali ya juu kabisa. Kama ‘sponsor’ na ‘consumer’ wa taarifa za kila siku usalama, inatarajiwa kuwa Dokta Magufuli atatekeleza ushauri wa Idara katika kukabiliana na matishio mbalimbali ya usalama wa taifa letu.

Dokta Kipilimba ana fursa ya kuleta mageuzi kwa Idara ya Usalama wa Taifa kwa kuangalia uwezekano wa kuwafikia watu walio nje ya taasisi hiyo, hasa pale uwezo wa Idara yetu unapokuwa limited. Nitoe mfano. Katika kupata taarifa mwafaka wa kudumu kuhusu, kwa mfano, mgogoro wa kisiasa huko Zanzibar, Idara inaweza ku-reach out wanazuoni wa historia ya taifa letu walipo ndani na nje ya nchi yetu.

Ikumbukwe kuwa sio rahisi kwa taasisi hiyo kuwa na maafisa au watoa habari katika kila eneo. Wenzetu wa nchi za Magharibi wamekuwa wakikabiliana na hali hiyo kwa kufanya kazi na ‘makandarasi’ (contractors), ambao of course, wamekidhi taratibu kama vile vetting.

Sambamba na hilo ni Idara hiyo kuangalia uwezekano wa kutumia hazina kubwa tu ya maafisa wake wa zamani, hususan wastaafu. Ikumbukwe kuwa wengi wao ni watu wanaowindwa na ‘subjects’ mbalimbali wanaolenga kulihujumu taifa letu.

Nimalizie makala hii kwa kutoa pongezi za dhati kwa Dokta Kipilimba na Naibu wake (DDGIS) Robert Msalika, sambamba na kumtakia mapumziko mema Mkurugenzi mstaafu Othman, na kumkaribisha ‘uraiani.’

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI IDARA YETU YA USALAMA WA TAIFA




21 Jul 2015




Juzi nilipatiwa uthibitisho wa kitu nilichokwishaambiwa awali: Idara yetu ya Usalama wa Taifa iliandaa operesheni dhidi ya mtu aliyepaswa kuja Tanzania kumzika baba yake. 

Nilipata taarifa kuhusu kinachoendelea katika Idara hiyo masaa kadhaa baada ya kutangaza kuwa baba yangu, Mzee Chahali amefariki. Afisa mmoja wa Idara hiyo alinipa ushauri kuwa nisije huko nyumbani kwa sababu kuna hujuma dhidi yangu. Kuthibitisha kuwa taasisi hiyo ni ya kibabaishaji, nilipata taarifa hizo muda mfupi tu baada ya maandalizi ya operesheni hiyo, and guess what, mie nipo Uingereza. Sasa kama mie nisiye na hatia yoyote na masikini nisiye na fedha za kuhonga, jiulize, ni wauza unga wangapi wenye mamilioni ya kuhonga  wanaopewa taarifa huko nyumbani kutoka katika Idara hiyo na taasisi nyingine za dola.

Sijawahi kuficha kuwa nilikuwa mtumishi wa taasisi hiyo. Nilikuwa mtumishi mwaminifu kwa takriban miaka 15 hadi mwaka 2008 nilipoamua kuachana nayo. Sijawahi kutamka nini kilichonifanya kuchukua uamuzi huo, lakini kwa kifupi maisha yangu yalikuwa hatarini baada ya kuzushiwa kosa ambalo ni sawa na uhaini. Kwa kifupi, ukiwa mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa ya nchi yeyote ile, kosa la 'kutumikia Idara ya Usalama wa Taifa ya nchi nyingine' ni kile kwa kimombo kinaitwa 'treasonable offence,' yaani kosa la kihaini. Kwanini nilizushiwa hilo, hiyo ni hadithi nyingine, ila sijawahi kuitumikia taasisi nyingine ya Usalama wa Taifa  zaidi ya hiyo ya nchi yangu.

Mwaka 2002, Idara hiyo ilinipatia skolashipu ya kuja kusoma shahada ya uzamili (Masters) huku Uingereza. Baada ya kumaliza shahada hiyo, niliomba ruhusa ya kusoma shahada ya uzamifu (PhD). Lakini kwa vile shahada ya uzamili niliyosoma haikuwa ya kiutafiti (research-based), ilinilazimu kusoma shahada nyingine ya uzamili (MRes) ambayo ni ya kiutafiti, na nilipomaliza nilijiunga na shahada ya uzamifu. Hayo yote yalifanyika kwa ruhusa ya taasisi hiyo.

Matatizo yangu na Idara hiyo yalianza Oktoba mwaka 2006, baada ya mie kuchapisha makala iliyokuwa ikimkemea aliyekuwa Waziri Mkuu wakati huo, Edward Lowassa, kuhusu taarifa za vyombo vya habari vya huko nyumbani kuwa alikuwa akijaribu kuzima mjadala wa skandali ya Richmond. Mmoja wa Wakurugenzi katika Idara hiyo alinipigia simu ya vitisho akinituhumu kuwa 'ninawasidia wapinzani,' 'ninaikosoa serikali ilhali mie ni mtumishi wake (kwa wakati huo),' na kubwa zaidi, kuhoji iwapo ninaitumikia Idara ya Usalama wa Taifa ya nchi nyinyingine. Kadhalika, press secretary wa Lowassa alisambaza makala kali kunikemea

Walinileta huku kusoma stadi za siasa, sasa mie kupevuka kifikra kuhusu vikwazo vya siasa yetu katika maendeleo ya taifa letu ikawa kosa. Uzalendo ulinishinda, ndio maana ikanilazimu kukosoa maovu mbalimbali yaliyokuwa yanawaumiza walalahoi wa Tanzania. Kichekesho ni kwamba kile nilichoandika 2006 na kushambuliwa vikali, ndicho kilichotokea miaka miwili baadaye, na kulazimisha Lowassa kujiuzulu. Na hakuna aliyenipongeza.

Mwaka 2008 nilikuja huko nyumbani kwa miezi kadhaa kumuuguza marehemu mama yangu. Nikidhani kuwa watumishi wenzangu katika Idara hiyo walikuwa wakielewa kilichokuwa kikinisibu wakati huo, wakanisumbua vya kutosha, na hatimaye njia pekee niliyobakiwa nao ilikuwa kuondoka huko nyumbani - japo baba alikuwa taabani kutokana na kifo cha mkewe aliyedumu nae kwenye ndoa kwa miaka 53. Na niliporudi huku, usumbufu ukaendelea: vitisho na upuuzi mwingine. Kwa ushauri wa taasisi za hapa, na kwa kuzingatia kuwa maisha yangu yalikuwa hatarini, nikaamua kuachana na taasisi hiyo. So ukiangalia hadi hapo, sikuwa nimefanya kosa lolote la kustahili kusumbuliwa kiasi hiki.

Kuhusu tukio la majuzi, masaa kadhaa baada ya kutangaza kuwa baba yangu amefariki, nililetewa taarifa ya uwepo wa operesheni maalum dhidi yangu, na aliyenipa taarifa hiyo alinisihi nisije huko nyumbani. Nimeambiwa kuwa Idara hiyo iliweka maofisa wake airport ili 'kunipokea.' Lakini baada ya kutoniona, walituma maafisa watatu, wawili wanaume na mmoja mwanamke, kwenda Ifakara 'kushirikiana nasi kwenye mazishi.' Wahuni hawa hata hawana ubinadamu.

Sijui wametumia kiasi gani cha fedha za walipakodi kukesha macho airport kunisubiri, na sijui hadi sasa washatumia kiasi gani huko Ifakara kuendeleza operesheni yao fyongo. Hawa wahuni hawataki kujifunza. Mwaka juzi, mwezi Februari, walituma watu kuja kunidhuru hapa Uingereza. Kwa vile Idara hiyo inaiendeshwa kishkaji, nadhani walituma wababaishaji walioishia kudakwa na mashushushu wa hapa Uingereza, ambao baadaye waliwafahamisha Polisi hapa Glasgow kuwa nichukue tahadhari muhimu. Na tangu wakati huo nimekuwa nikiishi na uelewa kuwa kuna mtu flani, siku flani atajaribu kunidhuru. Sio rahisi kuishi namna hiyo lakini sio impossible.Na hili tukio la majuzi limekuwa kama 'wake-up call' kwamba hujuma hizo dhidi yangu bado zipo hai.

Nilipokuwa mtumishi wa taasisi hiyo, niliitumikia kwa uadilifu mkubwa, na nilifanya kazi katika vitengo mbalimbali.Lakini kubwa zaidi, hadi ninaondoka huko nyumbani kuja huko kimasomo, nilikuwa Mkuu wa Kanda ya Kiintelijensia katika moja ya kanda zake jijini Dar. Huo si wadhifa mdogo, na ninakumbuka nilipowaambia maafisa wangu kuwa nakwenda Uingereza kimasomo, wapo walioniuliza 'sasa bosi unataka nini zaidi ya hiki ulichonacho sasa?' Japo wakati huo nilikuwa na shahada moja kutoka UDSM, dhamira yangu siku zote ilikuwa kukamata udaktari wa kitaaluma, na nilipopewa skolashipu kuja huku kimasomo, sikufikiria mara mbili.

Enough about that. Laiti Idara yetu ya Usalama ingekuwa na vipaumbele mwafaka basi ingehangaika na wahalifu waliokimbilia kwenye siasa na kuwadhibiti au ingehangaika na tishio la usalama wa taifa letu katika biashara ya madawa ya kulevya. Wanazidi kujaza mafaili kwenye masjala yao yenye majina ya wauza unga lakini wapo bize na watu kama sie tusio na hatia.

Wengi wenu mnanifahamu kama 'mropokaji' lakini kwa vile nilikula kiapo cha utiifu, hata siku moja sijawahi kuropoka kuhusu mambo mbalimbali niliyoshuhudia au kushiriki wakati nikiwa mtumishi wa taasisi hiyo. Sasa kwanini niendelee kuonekana adui? 

Hiyo operesheni fyongo ya mwaka juzi ilinishtua, lakini hii ya majuzi imenichukiza. Ushauri wangu pekee kwa Idara hiyo ni wa aina mbili: kwanza, fedha za Watanzania zinazopotezwa kufuatilia watu wasio na makosa zielekezwe katika kuimarisha uwezo wa Idara hiyo kupambana na wahalifu halisi wanaotishia usalama wa taifa letu, eg mafisadi , wauza unga, majangili, nk. Lakini pili, nimewashauri pia kwamba fedha zinazotumika kutufutilia akina sie' zielekezwe kwenye mafunzo ya maofisa wanaokabidhiwa majukumu ya aina hiyo. Walijaribu kuja kunidhuru hapa UK wakaishia kuumbuka. Na sasa wamejaribu kunishughulikia huko nyumbani, wameishia kupata hasara ya bure. Lakini wahuni hawa hawana uchungu na fedha wanazotumia kwa operesheni fyongo kwa vile hazitoki mfukoni mwao.

Sikupenda kzungumzia suala hili hadharani lakini imenilazimu kufanya hivyo hasa baada ya kufahamishwa kuwa familia yangu huko Tanzania inaishi kwa hofu baada ya kufahamishwa kuwa kuna watu wapo Ifakara kwa 'nia mbaya' dhidi yangu. Ninatambua hii ni vita ya sisimizi (mie) na tembo (Idara hiyo) lakini cha kutia matumaini ni vitu viwili: siku zote Mungu husimama na wanaonyanyaswa, na pili, mafunzo aliyopitia tembo ndio aliyopitia sisimizi. Hapa ni suala la akili ya nani iko mbele ya mwenzie, na ninaamini kuwa kamwe operesheni hizo fyongo hazitofanikiwa. Mlinifunza 'constant vigilance of an officer.' For your information, kwa hakika ninaitumia vizuri sana. This is a battle of wits...and sadly for you, I am still winning.

Sijaandika haya kusaka huruma ya mtu flani au taasisi hiyo. Nimeamua tu kuweka rekodi bayana. 

Asanteni kwa kuchukua muda wenu kunisoma

MESSAGE SENT AND DELIVERED.

4 Apr 2015


Kabla ya kuingia kwa undani kuhusu mada hii, ni muhimu kutanabaisha kuwa uchambuzi huu wa kitaalam (kiintelijensia) unatokana na mchanganyiko wa hisia na facts.Lakini pengine ni muhimu pia kueleza kuhusu nilivyofikia hitimisho lililopelekea kichwa cha habari hapo juu.

Tabia nzuri: Miaka kadhaa wakati nikiwa mtumishi katika taasisi flani huko Tanzania, mkuu wangu wa kazi ambaye pia alikuwa mmoja wa viongozi wakuu wa taasisi hiyo alivutiwa sana na mtizamo wangu wa kutilia mashaka kila jambo. Sio tu kwa vile mtizamo huo uliendana na mafunzo yanayohusu kazi hiyo bali pia ulikuwa na mafanikio. Moja ya kanuni kuu za kazi hiyo ni 'usiamini kitu chochote' sambamba na 'kumini vitu kwaweza kukuletea matatizo au hata kuuawa.' Kwahiyo, kila jambo liliangaliwa kwa pande mbili, huku swali kubwa likiwa 'what if.' Kwa kifupi, mtizamo huo ulisaidia sana kutambua 'ubaya uliojificha katika uzuri.'

Tabia mbaya: Wanasema ukishakuwa mwalimu unabaki mwalimu milele. Nami kwa kiasi kikubwa nimejikuta katika hali hiyo. Uzoefu na ujuzi nilioupata katika kazi hiyo umenifanya niwe mtu wa kutoamini vitu kirahisi, na hata nikiamini bado ninakuwa na wasiwasi flani. Kwa 'maisha ya mtaani,' tabia hiyo ina madhara yake. Kwa mfano, inaathiri relationships kwa kiasi flani maana ili uhusiano uwe imara sharti kuwa na kuaminiana. Kadhalika, jamii inaweza kuniona kama prophet of doom, yaani mtu anayehubiri majanga. Ni rahisi pia kulaumiwa kuwa ni 'mtu wa kuongelea mabaya tu' pale ambapo wengi wanadhani panastahili sifa.

Bottom line: Kinachohitajika ni uwiano kati ya kuamini vitu/watu kwa kuzingatia facts na hisia, kwa uande mmoja, na kutilia shaka vitu/watu kwa kuzingatia facts na hisia. Hili ni rahisi kuliongea lakini pengine ni guu kulitenda hasa kama hisia zinatawala zaidi ya facts, hususan kama hisia zenyewe ni zile zinazofahamika kitaalam kama 'hisia ya sita' (6th sense, yaani zisizotumia kuona, kusikia,kugusa,kulamba,kunusa na kuona)

Baada ya utangulizi huo, tuingie kwenye mada husika. Kuna sababu kadhaa za kimazingira zinazonipa wasiwasi kwamba Tanzania yetu inaweza kukumbwa na shambulio la kigaidi, wakati huu wa sikukuu ya Pasaka au huko mbeleni. Hapa chini, ninabainisha sababu hizo.

Tukio la ugaidi Garisa, nchini Kenya:

Juzi, magaidi wa Al-Shabaab walifanya shambulio kubwa la ugaidi katika mji wa Garisa, uliopo mpakani mwa Kenya na Somalia.Shambulio hilo limepelekea vifo vya watu takriban 150 huku taarifa mbalimbali zikionyesha uwezekano wa kuwepo idadi kubwa zaidi ya waliouawa. 

Awali, nilikuwa upande wa watetezi wa serikali ya Kenya na vyombo vya usalama vya nchi hiyo katika lawama kwamba walizembea kuchukua tahadhari. Hoja yangu kuu ilikuwa kwamba kupewa taarifa kuhusu ugaidi ni kitu kimoja, kuweza kuzifanyia kazi taarifa hizo na kuweza kuzuwia ugaidi ni kitu kingine kabisa. Hata hivyo, utetezi huo umepungua baada ya kupatikana taarifa mbalimbali zinazoashiria mapungufu makubwa ya serikali ya Kenya na taasisi za Usalama nchini humo kukabiliana na tetesi walizopewa kuhusu uwezekano wa shambulio hilo la kigaidi.

Tukiweka kando kilichojiri nchini Kenya lakini tukitilia maanani ukweli kuwa nchi hiyo ilitahadharishwa kabla ya tukio hilo, kwa Tanzania hali ni tofauti. Hadi sasa hakuna taarifa rasmi ya uwezekano wa kutokea shambulio la ugaidi.

Hata hivyo, ni muhimu kutambua kuwa Kenya ina ushairikiano mkubwa zaidi na taasisi za kiusalama za mataifa makubwa zaidi ya Tanzania, hasa ikizingatiwa kuwa Marekani, kwa mfano, ina 'base' yake ya kijeshi nchini humo (Manda Bay


Kwa maana hiyo, tahadharani ya Wamarekani kwa Kenya sio tu kwa maslahi ya Kenya bali ya Wamarekani pia. 

Hitimisho: Kwa kufanikiwa kufanya shambulio kubwa kabisa nchi Kenya, ikiwa ni takriban mwaka na nusu baada ya kufanya shambuli jingine la ugaidi kwenye supamaketi ya Westgate jijini Nairobi, magaidi wa Al-Qaeda wanaweza kushawishika kupanua kampeni yao ya uharamia hadi Uganda (ambako tayari kuna tishio kama ninavyoeleza hapo chini) na hata Tanzania (kwa sababu nitazobainisha mbeleni katika makala hii)

Uwezekano wa shambulio la kigaidi Uganda:

Machi 25 mwaka huu, Marekani ilitoa tahadhari kwa Uganda kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi nchini humo. Kama ilivyo kwa Kenya, Marekani ina maslahi yake nchini Uganda ambako  inarusha ndege zake za upelelezi (PC 12) kutoka Entebbe, Kwahiyo usalama kwa Uganda una maslahi kwa Marekani pia.

Hitimisho: Iwapo Al-Shabaab watafanikiwa kutimiza uovu wao kuishambulia Uganda (Mungu aepushe hili), wanaweza kupata motisho wa kutanua zaidi kampeni yao hadi Tanzania hasa kwa kuzingatia kuwa kundi hilo la kigaidi linaziona nchi hizi tatu kama kikwazo kikubwa kwa uhai wake. 

Shaka ya ugaidi nchini Tanzania:

Moja ya matatizo makubwa ya kufahamu ukubwa au udogo wa tishio la ugaidi nchini Tanznaia ni siasa. Kwa muda mrefu, chama tawala CCM kimekuwa kikiutumia ugaidi kama kisingizio cha kudhibiti vyama vya upinzani na baadhi ya viongozi wake. Kwa minajili hiyo, hata serikali ikitoa taarifa sahihi kuhusu uwezekano wa tishio la ugaidi, kuna uwezekano wa wananchi wengi kudhani hiyo ni siasa tu.

Kana kwamba hiyo haitoshi, mwaka huu Tanzania itafanya uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge hapo Oktoba. Japo haijazoeleka sana, historia inaonyesha kuwa angalau katika uchaguzi mkuu mmoja uliopita zilisikika taarifa za 'tishio la usalama' kutoka kwa nchi jirani. Mbinu hii hutumiwa na vyama tawala kujenga hofu ya kiusalama kwa wapigakura, na kuwaunganisha chini ya mwavuli wa chama kilichopo madarakani. Kwa mantiki hiyo, iwapo kutakuwa na taarifa za tishio la ugaidi, yayumkinika kuhisi baadhi ya wananchi wakatafrisi kuwa ni mbinu tu ya CCM kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.

Lakini tatizo kubwa zaidi kwa sasa ni imani ndogo ya wananchi kwa serikali ya Rais Jakaya Kikwete na nyingi ya taasisi za serikali yake. Uhaba huo wa imani unatokana na mchanganyiko wa hisia za ushahidi wa matukio yaliyopita. Kutokana na kuandamwa mno na kashfa za ufisadi, kumeanza kujengeka imani miongoni mwa Watanzania kuwa serikali yao ni ya kifisadi pia.

Matumizi mabaya ya 'taarifa za kiintelijensia' yamewafanya Watanzania wengi kuwa na hisia kuwa 'taarifa za intelijensia' ni mbinu ya serikali kuwadhibiti. Mara kadhaa,Jeshi la Polisi nchini humo limekuwa likipiga marufuku maandamano ya kisiasa au kijamii kwa kisingizio cha 'taarifa za kiintelijensia.' Hivi karibuni, zilipatikana taarifa za mapigano makali kati ya jeshi la polisi wakishirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) dhidi ya 'magaidi' kwenye mapango ya Amboni mjini Tanga. Mchanganyiko wa taarifa za kukanganya na imani haba ya wananchi kwa jeshi hilo vilipelekea tukio hilo kuonekana kama 'mchezo wa kuigiza.'


Lakini licha ya kasoro hizo zinazoihusu serikali na taasisi zake, kuna tatizo jingine linalohusu vyombo vya habari vya nchi hiyo. Utiriri wa magazeti ya udaku na uhaba wa uandishi wa kiuchunguzi katika 'magazeti makini' umekuwa ukichangia mkanganyiko katika kubaini ukweli na porojo. Mfano mzuri ni tukio hilo la Amboni ambalo kwa kiasi flani liligeuka kama mfululizo 'series' ya mchezo wa kuigiza, huku magazeti ya udaku yakiwa na 'habari' nyingi zaidi ya 'magazeti makini.'

Hali hiyo yaweza kuwa inachangiwa na mahusiano hafifu kati ya taasisi za dola na vyombo vya habari, sambamba na mazowea ya taasisi hizo kutoa tu taarifa pasipo kurhusu maswali kutoka kwa wanahabari. Ukosefu wa taarifa sahihi, sambamba na ugumu wa kupata taarifa hizo huchangia 'udaku' kuziba ombwe husika.

Tukiweka kando kasoro hizo hapo juu, hadi sasa kuna mabo yafuatayo ambayo yanaweza kuwashawishi magaidi kuvamia Tanzania.

1. Mgogoro wa muda mrefu kuhusu uanzishwaji wa mahakama ya kadhi: Japo hadi muda huu suala hili limeendelea kuwagawa Watanzania kwa njia za mijadala na kwa amani, yayumkinika kuhisi kuwa magaidi wanaweza kulitumia kama kisingizio cha kuishambulia Tanzania. Cha kutia hofu ni ukweli kwamba sio tu suala hili limedumua kwa muda mrefu, hasa baada ya chama tawala CCM kuahidi katika Ilani yake ya Uchaguzi Mkuu mwaka 2005 kuwa itaanzisha mahakama hiyo lakini imeshindwa kufanya hivyo hadi leo, bali pia uamuzi usio wa busara wa kuupeleka Bungeni  Muswada wa Uanzishwaji Mahakama ya Kadhi kisha kuuondoa. Kana kwamba hiyo haitoshi, majuzi Rais Kikwete alikaririwa akidai kuwa serikali haina mpango wa kuanzisha mahakama hiyo, na badala yake jukumu hilo linabaki kwa Waislamu wenyewe. Haihitaji uelewa wa sheria kujiuliza kwamba kama suala hilo lilikuwa la Waislamu wenyewe, lilipelekwa Bungeni kwa minajili gani?

Licha ya mjadala huo wa uanzishwaji wa mahakama ya kadhi kuendelea kwa amani, mjadala kuhusu suala hilo umewagawa viongozi wa dini (Wakristo na Waislamu) na kwa kiasi flani umerejesha mgogoro kati ya baadhi ya viongozi wa Kiislam na serikali, sambamba na kuleta sintofahamu miongoni mwa baadhi ya wanasiasa.

2. Vitisho bayana kutoka kwa watu wanaodai ni magaidi.

Hivi karibuni ilipatikana video nchini Tanzania ambapo mtu mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Kaisi Bin Abdallah alidai kuwa kundi lao limekuwa na mafanikio katika ugaidi wa kudhuru polisi na vituo vya polisi. Video hii chini inajieleza yenyewe.



Licha ya 'mapungufu kadhaa' katika video hiyo, ambayo yanaweza kutupa imani kuwa ni porojo tu, kwa kuzingatia nilichokitanabaisha mwanzoni mwa makala hii, yawezekana tishio lililo kwenye video hiyo ni la kweli. Na hili ni moja ya matatizo ya kukabiliana na tishio la ugaidi: kuchukulia taarifa kuwa ni serious au kuzipuuza.

Hofu kuhusu uwezekano wa matukio ya ugaidi nchini Tanzania ilithibitishwa na kauli ya hivi karibuni ya Rais Kikwete kuwa mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya vituo vya polisi katika maeneo mbalimbali nchini humo yana uhusiano wa ugaidi, japo hakubainisha iwapo kuna uhusika wa makundi ya kigaidi ya kimataifa au la.

3. Taarifa za kimataifa:

Hadi muda huu hakuna taarifa za moja kwa moja zinazoashiria uwezekano wa tukio la ugaidi nchini Tanzania. Hata hivyo, bado kuna hali ya tahadhari wa wastani kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi. Wakati serikali ya Canada inaeleza kuwa haina 'ushauri unaohusu taifa (Tanzania) zima, inawashauri raia wake kuchukua tahadhari kubwa kuhusiana na ugaidi. Kwa upande wake, Serikali ya Uingereza inatoa angalizo la jumla tu japo inatahadharisha kuhusu tishio la ugaidi wa Al-Shabaab kwa eneo  la Afrika Mashariki (ikiwa ni pamoja na Tanzania). Serikali ya Marekani inatoa ushauri wa jumla tu kwa kurejea matukio ya uvunjiafu wa amani huko nyuma.

Hata hivyo, ripoti iliyotolewa LEO na taasisi ya HTH Worldwide kuhusu risks zinazoikabili Tanzania, ugaidi unatajwa kuwa ni tishio la kuamika, japo uwezekano wa kutokea shambulizi la ugaidi ni wa wastani.

Pengine taarifa ya kuogofya zaidi ni ile iliyobainisha uwepo wa jitihada za kundi la kigaidi la ISIS kutaka kujiimarisha katika eneo la Afrika Mashariki, ikiwa ni pamoja na Tanzania. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ISIS inajaribu kujenga ushirikiano na Al-Shabaab kwa minajili ya kuwa na infulence katika eneo la Afrika Mashariki.

Kadhalika, majuzi zimepatikana taarifa kutoka Kenya kuhusu mwanamke mmoja wa Kitanzania aliyekamatwa na wenzie wawili Wakenya wakijaribu kwenda Somalia kuwa wenza wa magaidi wa Al-Shabaab.


 Tukio hilo linaakisi kinachotokea katika nchi mbalimbali za huku Magharibi ambapo mabinti kadhaa wamekuwa wakitorokea Syria kwenda kuwa 'wenza' wa magaidi wa ISIS.

Hitimisho:

Ni vigumu kwa kuwa na hakika ya asilimia 100 iwapo magaidi watafanya shambulio au la. Kwa upande mmoja, magaidi wana muda wote wanaohitaji kabla ya kutimiza azma yao, yaani wanaweza kusubiri kwa muda mrefu, ilhali vyombo vya dola havina faida hiyo kwani vinatakiwa kuwa makini muda wote.

Kuna msemo maarufu kuhusu ugaidi, kwamba wakati magaidi wanahitaji DAKIKA MOJA TU kutimiza uovu wao, vyombo vya usalama vinahitaji KILA SEKUNDE YA DAKIKA kuwazuwia magaidi husika.

Na japo uwepo wa taarifa za uhakika kuhusu uwezekano wa shambulio la kigaidi unaweza kusaidia jitihada za kukabiliana na magaidi husika, ukweli mchungu ni kwamba, kuwa na taarifa ni kitu kimoja, uwezo wa kuzitumia taarifa hizo ni kitu kingine.

Wakati huu tunaungana na wenzetu wa Kenya kulaani unyama wa Al-Shabaab, ni muhimu kuchukua tahadhari mahususi ili kuweza kukabiliana na uwezekano wa magaidi hao kushambulia Tanzania. La muhimu zaidi ni umoja na mshikamano, ambao kwa hakika unapotea kwa kasi, na haja ya haraka kwa Serikali kurejejesha imani ya wananchi kwake. Kingine ni umuhimu wa kuweka kando siasa katika masuala nyeti kama haya..

Kubwa zaidi ya yote ni la kitaalamu zaidi. Wakati serikali ya Tanzania imekuwa ikitegemea zaidi msaada wa kimataifa katika kuiimarisha kiuwezo Idara ya Usalama wa Taifa, ni muhimu jitihada za ndani pia zielekezwe katika kuijengea uwezo wa kukabiliana na matishio mbalimbali ya usalama wa taifa, ikiwa ni pamoja na ugaidi. Kwa uelewa wangu, uwezo wa vitengo vya kuzuwia ugaidi na kitengo cha kupambana na ujasusi unaathiriwa na mapungufu ya kimfumo na kisera, sambamba na nafasi ya maafisa wa Idara hiyo kwenye balozi za Tanzania nje ya nchi 'kubweteka' na teuzi zinazodaiwa kufanywa kwa misingi ya undugu,urafiki au kujuana.

Mwisho, tishio la ugaidi sio la kufikirika. Lipo, na kwa bahati mbaya, mazingira ya kulirutubisha tishio hilo yapo pia. 

23 Oct 2014

Makala yangu hii ilichapishwa katika jarifa la RAIA MWEMA Toleo la wiki iliyopita lakini 'nilizembea' kui-post hapa bloguni. Endelea kuisoma:

NIANZE kwa kuelezea matukio mawili, moja linaihusu Marekani na jingine laihusu Israel. 
Tukio la kwanza linahusu kujiuzulu kwa aliyekuwa mkuu wa moja ya idara za usalama za Marekani (zipo nyingi) ambayo ina dhamana ya ulinzi na usalama wa viongozi wakuu wa taifa hilo na familia zao, US Secret Service. 
Mkuu huyo, mwanamama Julia Piersons, alilazimika kujiuzulu baada ya tukio la hivi karibuni la kuhatarisha usalama wa Rais Barack Obama, kutokana na mtu mmoja, Omar Gonzalez, kuruka uzio wa Ikulu ya nchi hiyo akiwa na kisu, kabla hajadhibitiwa na maafisa wa Secret Service. 
Hatimaye tukio hilo lililotawala sana katika vyombo vya habari vya Marekani lilimfanya mwanamama huyo, shushushu mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 30, kuitwa na kuhojiwa na kamati moja ya Bunge la Congress, na mwishowe alitangaza kujiuzulu. 
Licha ya ukweli kwamba mkuu huyo wa mashushushu hakuwa eneo la tukio, dhamira ilimtuma kuwa kama kiongozi wa taasisi yenye dhamana ya ulinzi wa viongozi wakuu wa nchi hiyo, anawajibika kwa uzembe au makosa ya watendaji wake. 
Piersons alikuwa kwenye wadhifa huo kwa takriban miezi 18 tu baada ya mtangulizi wake, Mark Sullivan, kulazimika kujiuzulu baada ya kashfa iliyohusisha baadhi ya maafisa wa Secret Service ‘kufumwa’ wakiwa na makahaba katika ‘msafara wa utangulizi’ (advance party) kabla ya ziara ya Rais Obama nchini Colombia, mwaka juzi. 
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya ushushushu wanamuona Piersons kama mhanga tu wa mapungufu ya kimfumo na kiutendaji yanayoikabili taasisi aliyokuwa akiongoza. 
Wanadai kuwa alikuwa akikabiliwa na jukumu gumu la kuleta mabadiliko ndani ya taasisi hiyo, na wadhifa wake ulikuwa sawa na ‘jukumu lisilowezekana.’ Hata hivyo wanampongeza kwa ‘kubeba mzigo wa lawama’ kwa niaba ya watendaji wake. 
Tukio la pili linahusu filamu ya maelezo (documentary) iitwayo The Gatekeepers, iliyoonyeshwa kwenye kituo cha runinga cha BBC2 mwishoni mwa wiki. 
Filamu hiyo ni ya mahojiano na wakuu sita wa zamani wa Idara ya Usalama wa Ndani wa Israeli, Shin Bet (au 'Shabak' kama inavyojulikana kwa Kiyahudi). 
Filamu hiyo iliyotengenezwa mwaka juzi na kuteuliwa kuwania tuzo za Oscars, imeendelea kuwa na mvuto mkubwa kutokana na ukweli kuwa ni vigumu mno, hasa kwa ‘nchi ya kiusalama’ kama Israeli, kupata fursa ya kufanya mahojiano na wakuu wa taasisi za usalama. 
Katika filamu hiyo inayoelezea kwa undani utendaji kazi wa Shin Bet, idara ya ushushushu yenye ufanisi mkubwa duniani, ikiwa ni pamoja na operesheni mbalimbali za Shin Bet dhidi ya ‘magaidi’ wa Palestina, wakuu hao – Avraham Shalom (1980-1986), Yaakov Peri (1988-1994), Carmi Gillon (1994-1996), Avi Dichter (2000-2005) na Yuval Diskin (2005-2011)- wanatanabahisha jinsi wanasiasa na Wayahudi wenye msimamo mkali walivyo vikwazo kwa jitihada za kutafuta amani ya kudumu katika mgogoro wa muda mrefu wa Israeli na Palestina. 

Kwa ujumla, wote wanahitimisha kuwa licha ya umuhimu kwa serikali ya Israeli na taasisi zake za ulinzi na usalama kutumia nguvu dhidi ya ‘ugaidi wa Wapalestina,’ ukweli mchungu ni kuwa matumizi hayo ya nguvu si tu yanachochea ‘ugaidi’ zaidi bali pia yanakwaza uwezekano wa kupatikana amani ya kudumu. 

Filamu hiyo ilisababisha wakuu hao kushutumiwa na Waisraeli wengi, wakilaumiwa kwa msimamo wao uliotafsiriwa kama kuhalalisha ‘ugaidi’ wa Wapalestina, huku wengine wakiwashutumu kuwa ‘waliongea walichoongea baada ya kustaafu badala ya kubainisha mitizamo yao wakiwa madarakani.’ 
Kwa hakika filamu hiyo (unayoweza kuiangalia hapa http://goo.gl/gY4K6O) si tu inaeleza kwa undani operesheni hatari na za ‘ufanisi wa hali ya juu’ zilizofanywa na Shin Bet chini ya uongozi wa mashushushu hao lakini pia inamsaidia anayeiangalia kufahamu kwa undani mchanganyiko wa siasa na dini na mwingiliano wake katika utendaji kazi wa taasisi za kiusalama za Israeli, na kubwa zaidi ni maelezo ya kina kuhusu mgogoro kati ya nchi hiyo na Palestina. 
Lengo la makala hii si kujadili matukio hayo mawili bali kuyatumia kama ‘darasa la bure’ kwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa. Binafsi, nimekuwa moja ya sauti chache kuhusu haja ya mageuzi ya kimfumo na kiutendaji kwa taasisi hiyo muhimu. 
Kwa bahati mbaya – au makusudi- utendaji kazi na ufanisi wa Idara hiyo haukuguswa kwa kiwango kinachohitajika katika kikao cha Bunge la Katiba na hatimaye Katiba pendekezwa. 
Idara hiyo inakabiliwa na matatizo makubwa japo aidha hayafahamiki sana au yanapuuzwa, na huo ndio msingi wa ushauri wangu kuwa kuna haja ya mageuzi ya haraka. 
Tukijifunza katika kujiuzulu kwa mkuu wa Secret Service, twaweza kujiuliza, hivi kwanini hakuna anayewajibishwa licha ya Idara yetu ya Usalama wa Taifa kuboronga mara kwa mara? 
Pengine kuna watakaojiuliza 'imeboronga lini na katika nini?’ Jibu rahisi ni kwamba, kwa mujibu wa ‘kanuni za taaluma ya usalama wa taifa,’ kushamiri kwa vitendo vinavyotishia usalama wa nchi ni dalili ya wazi ya udhaifu wa idara ya usalama wa taifa ya nchi husika. 
Kwa maana hiyo, kushamiri kwa ufisadi, kwa mfano mmoja tu, ni dalili kwamba taasisi hiyo imeshindwa kazi yake. Kadhalika, Idara hiyo kufanya kazi zake kama ‘kitengo cha usalama cha CCM’ si tu kunaipunguzia kuaminika kwake kwa umma bali pia kunaathiri uwezo wake katika kukabiliana na matishio kwa usalama wa Taifa. 
Majuzi, aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo, Jack Zoka, ‘alizawadiwa’ ubalozi wa nchi yetu huko Canada. Sihitaji kuingia kwa undani kuhusu utendaji kazi wa shushushu huyo lakini atakumbukwa sana na vyama vya upinzani, hasa CHADEMA, sambamba na wengi wa waliojitoa mhanga kuwa sauti ya wanyonge, kwa jinsi alivyowadhibiti. Pengine kabla ya kupewa ubalozi baada ya kustaafu utumishi wa umma, ahojiwe kuhusu mchango wake katika ‘ufanisi’ au udhaifu wa Idara hiyo. 


 
Ni mwendelezo wa kasumba inayolikwaza Taifa katika nyanja mbalimbali: mtu anaboronga pale, anahamishiwa kule. Kwanini watendaji wengine wahofie kuboronga katika majukumu yao ilhali wenzao ‘wanazawadiwa’ badala ya kuwajibishwa? 
Somo kutoka kwa wakuu sita wa zamani wa Shin Bet katika filamu ya The Gatekeeper ni kubwa zaidi. Ukiondoa ‘sauti ndogo’ ya Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Idara yetu ya Usalama wa Taifa, Hans Kitine, takriban viongozi wote wastaafu wa Idara hiyo wamekuwa hawana mchango wa maana katika kuiboresha na hata kuisadia isimame katika upande stahili. 
Ni kweli Tanzania si Israeli, lakini wengi wa wastaafu wa taasisi hiyo, kama ilivyo kwenye taasisi nyingine, ni watu wenye ushawishi mkubwa na wanaheshimika vya kutosha, lakini ukimya wao wakati mambo yanakwenda kombo ni doa. 
Mashushushu hao sita wa Israeli walipokubali kushiriki kwenye filamu hiyo walikuwa wanatambua bayana athari zake, kubwa ikiwa ni uwezekano wa kuonekana wasaliti. Lakini ujasiri ni pamoja na kusema yasiyosemeka. 
Na kwa vile, kimsingi, ukiwa shushushu unabaki kuwa shushushu milele, na kwa sababu ni watu wachache katika jamii wenye uelewa kuhusu utendaji kazi wa taasisi za kiusalama, wastaafu au watumishi wa zamani ndio watu pekee wenye fursa ya ‘kuokoa jahazi.’ 
Nihitimishe makala hii kwa kutaja kwa kifupi maeneo yanayohitaji mageuzi (reforms) kuhusiana na Idara yetu ya Usalama wa Taifa. La kwanza ni umuhimu wa uwazi zaidi katika teuzi za viongozi wakuu wa Idara hiyo, hususan Mkurugenzi Mkuu. 
Ni muhimu kutengeneza mazingira yatakayoepusha uwezekano wa Rais ‘kumteua mtu wake au rafiki yake’ kuongoza taasisi hiyo. Madhara ya uswahiba katika uteuzi kuongoza taasisi nyeti kama hiyo ni pamoja na mteuliwa kujiona ana ‘deni la fadhila’ kwa aliyemteua. 
Kuna haja ya, kwa mfano, uteuzi wa viongozi wa juu wa taasisi hiyo kuidhinishwa na Bunge. 
Pili, ni ulazima wa taasisi hiyo kuwajibika kwa umma kupitia taasisi kama Bunge. Hapa ninamaanisha haja ya viongozi wa taasisi hiyo kuitwa katika kamati husika za Bunge, kwa mfano, kuwaeleza Watanzania ‘kwanini ufisadi unazidi kushamiri ilhali taasisi hiyo haipo likizo?’ 
Tatu ni mabadiliko ya kiutendaji ambapo Idara hiyo iwezeshwe kuufanya ushauri wake utekelezwe, badala ya mazingira yaliyopo ambapo kwa kiasi kikubwa suala hilo linabaki kuwa ridhaa ya Rais ambaye ndiye ‘consumer’ wa taarifa za kiusalama anazopatiwa na Idara. 
Hivi inakuwaje pale Idara hiyo inaposhauri kuhusu suala linalohatarisha usalama wa taifa lakini Rais akalipuuza? 
Mwisho, lengo la makala hii ni jema: kuiboresha Idara yetu ya Usalama wa Taifa (ambayo licha ya mapungufu yake lukuki, binafsi nina imani kuwa inaweza ‘kujikwamua’ kama si kukwamuliwa) kwa maslahi na mustakabali wa Taifa. 
Tanzania ni yetu sote na si kwa ajili ya kikundi kidogo kinachojiendeshea mambo kitakavyo.Penye nia pana njia.





22 Mar 2013

Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Rashid Othman
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Othman Rashid

Julai 11, mwaka jana niliandika makala ifuatayo kwenye jarida la Raia Mwema, ikibeba kichwa "Ni Vigumu Kuiamini Serikali kwa Dkt Ulimboka." Ninakusihi uisome kisha nitaeleza kwanini nimeirejea katika post hii
"KWA mara nyingine, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa tuhuma nzito dhidi ya Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), safari hii ikidaiwa kuwa baadhi ya viongozi wa taasisi hiyo nyeti wana mpango wa kuwaua baadhi ya viongozi wa CHADEMA.
Itakumbukwa kuwa wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu uliopita, CHADEMA kiliituhumu Idara hiyo kuwa ilikuwa inakihujumu chama hicho, tuhuma ambazo zilifanya Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TISS, Jack Zoka (pichani chini), kuzikanusha vikali.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa  Jack Zoka
Tuhuma hizi za CHADEMA zimekuja siku chache baada ya tukio la kusikitisha na la kinyama lililomkuta kiongozi wa jumuiya ya madaktari Dk. Steven Ulimboka ambaye alitekwa na hatimaye kuteswa na watu 'wasiojulikana.'
Katika tukio la Dk. Ulimboka, Serikali imejikuta ikinyooshewa vidole kuwa inahusika, hali iliyomfanya Rais Jakaya Kikwete kulizungumzia suala hilo katika hotuba yake kwa Taifa hivi karibuni.
Lakini takriban kila anayefuatilia kwa ukaribu suala hilo anaweza kuungana nami kutanabahisha ya kuwa japo hotuba ya Rais Kikwete imesaidia kwa namna fulani kuonyesha kuwa Serikali yake imeguswa (kwa maana ya kusikitishwa) na tukio hilo, kwa kiwango kikubwa haijasaidia kuondoa fikra kuwa kuna mkono wa Serikali.
Binafsi, nimelichambua kwa kirefu tukio hilo la kutekwa na kuteswa kwa Dk. Ulimboka katika mfululizo wa makala zangu za sauti (podcasts). Makala husika yenye kichwa cha habari “Nani aliyemteka na kumtesa Dk. Ulimboka?”
Kwa kifupi, katika makala hiyo nimezungumzia dhana tatu kuhusiana na tukio la Dk. Ulimboka. Ya kwanza ni hiyo inayogusa hisia za wengi kuwa Serikali inahusika na tukio hilo. Katika makala hiyo, nimeungana kimtizamo na kauli ya Rais Kikwete kuwa “Serikali imteke na kumtesa Dk. Ulimboka ili iweje.”
Kadhalika, nimeeleza kuwa japo kuna nyakati Serikali kwa kutumia vyombo vya dola inaweza kutumia vitisho na hata nguvu ikibidi ili kuzima upinzani dhidi yake, katika mazingira ya kawaida ni vigumu kuamini kuwa Serikali ya Rais Kikwete ingekuwa tayari kujiingiza matatizoni kwa kumteka na kumtesa kiongozi wa madaktari ili tu iwatishe madaktari wanaogoma.
Nimebainisha hivyo kwa vile ninaamini kuwa Serikali inafahamu fika kuwa kumnyamazisha Dk. Ulimboka hakuwezi kuwanyamazisha madaktari wote nchini.
Dhana ya pili ni ile ya hujuma dhidi ya Serikali. Kimsingi dhana hiyo inabashiri kuwa pengine kuna ‘watu wenye nguvu na jeuri ya fedha’ ambao wamefanya unyama huo dhidi ya Dk. Ulimboka kwa minajili ya 'kuikoroga' Serikali. Takriban kila anayefuatilia mwenendo wa siasa ndani ya chama tawala CCM atakuwa anafahamu kuwa kuna mtifuano mkubwa (japo usiosikika sana waziwazi) unaoendelea ndani ya chama hicho, hususan kuhusiana na kinyang’anyiro cha urais mwaka 2015.
Kwamba kuna mafisadi wanaoweza kumwaga fedha aidha kwa ‘majasusi binafsi’ au ‘majasusi rasmi’ ni jambo linalowezekana. Kinachonifanya niipe uzito mdogo dhana hii ni uchambuzi wa hasara na faida za tendo husika (cost and benefit analysis).
Hivi, kama mafisadi wakimteka na kumtesa Dk. Ulimboka, kisha Serikali ya Kikwete ikaandamwa, mafisadi hao watanufaikaje (zaidi ya kufurahia kuona Serikali inabebeshwa lawama isizostahili)?
Dhana ya tatu, na ambayo binafsi ninaipa uzito mkubwa, ni uwepo wa kile kinachofahamika katika lugha ya Kiingereza kama ‘rogue elements of the state apparatus’ (yaani ‘watendaji katika taasisi za dola ambao wanatenda kazi zao kinyume na taratibu na sheria,’ kwa tafsiri isiyo rasmi).
Dhana hii ya mwisho inaweza kushabihiana na ya pili kwa maana ya hicho nilichoita ‘majasusi rasmi,’ yaani watumishi wa vyombo vya dola ambao wanatumia ujuzi wao kutekeleza matakwa, si ya mwajiri wao, bali ya mafisadi waliowapa fedha kwa ‘kazi maalumu.’
Katika makala hiyo ya sauti nimeeleza kuwa ni wazi vyombo vya dola vilikuwa vikimfuatilia Dk. Ulimboka na waratibu wengine wa mgomo wa madaktari. Hilo si la kuhoji kwani ni utaratibu ‘wa kawaida’ kwa wana usalama. Iwe ni taasisi ya mashushushu wa ndani wa Marekani (FBI), au wenzao wa Uingereza (MI5), au TISShuko nyumbani, kila mtu au kikundi kinachotazamwa kama tishio kiusalama hufuatiliwa kwa karibu.
Sasa basi, kwa kuzingatia dhana hiyo ya ‘rogue elements,’ inawezekana watendaji waliokabidhiwa jukumu hilo waliamua kutumia njia za ‘liwalo na liwe’ (hapana, si kama ile ya tamko la Waziri Mkuu Mizengo Pinda) baada ya ‘njia za kistaarabu’ kumlazimisha Dk. Ulimboka awaeleze ‘nani anayewachochea madaktari kugoma’ kutozaa matunda.
Yaani baada ya diplomasia kushindwa, wakaamua kutumia mateso ya hali ya juu (kwa lugha ya kisheria ‘third degree torture’ na kitaalamu ‘fifth degree torture’).
Kwa nini ninashawishika kuamini kuhusu rogue elements? Tumeshuhudia matukio kadhaa huko nyuma. Naamini wengi wa wasomaji mtakuwa bado mnakumbuka tukio la mwandishi wa habari mahiri na mhariri  wa gazeti la Mwanahalisi, Said Kubenea, kumwagiwa tindikali usoni. Kibaya zaidi katika tukio hilo, mmoja wa wahusika alitajwa kuwa ni mwajiriwa wa TISS.
Sijui kesi hiyo iliishaje lakini la msingi hapa ni kuwa iliacha doa la aina fulani kwa taasisi hiyo hasa kwa vile haikuwahi kumkana afisa huyo (kwa maana ya kusema hakutumwa kiofisi bali alikuwa ‘rogue officer’ tu).
Itakumbukwa pia kuwa Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe aliwahi kueleza kuwa Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa na mpango wa kumuua. Kama ilivyokuwa kwa tukio la Kubenea lililomhusisha mtu aliyatajwa kuwa ni Afisa Usalama wa Taifa, Idara hiyo haikuwahi kukanusha tuhuma hizo.
Tukirejea kwenye tuhuma za CHADEMA dhidi ya TISS, binafsi nashawishika kuamini kuwa kama kuna ukweli katika tuhuma hizo basi itakuwa ni zilezile ‘rogue elements’ ambazo ninaamini zipo ndani ya taasisi hiyo nyeti.
Najua hili halitowapendeza wahusika, lakini kuna hisia kwamba ukiweka kando taasisi hiyo kuendeshwa kama kitengo cha usalama cha CCM moja ya sababu nyingine kubwa ya matatizo yanayoikabili taasisi hiyo ni ajira zilizotolewa pasipo kuzingatia ‘wito’ na ‘kipaji’ cha kuwa Afisa Usalama.
Popote duniani, maafisa usalama wanapaswa kuwa ‘watu zaidi ya watu wa kawaida’ kwa maana ya kuwa na upeo na uwezo wa hali ya juu katika takriban kila nyanja ya akili zao:  na huo ndio msingi wa neno INTELLIGENCE kwa kimombo.
Sasa tunaporuhusu watoto zetu, ndugu au jamaa zetu kuingizwa kwenye taasisi nyeti kama hiyo kwa vile tu ‘kuna maslahi manono’ tunaiweka rehani nchi yetu.
Naomba niwe mkweli. Madudu mengi yanayoendelea katika Tanzania yetu kwa sasa yanachangiwa na ubabaishaji unaoendelea ndani ya idara hiyo muhimu kwa ustawi na maendeleo ya taifa lolote lile duniani. Wao wanafahamu kanuni hii: uimara au kuyumba kwa nchi ni kielelezo cha uimara au udhaifu wa Idara ya Usalama ya nchi husika.
Sasa kama tuna maofisa usalama huko Benki Kuu (BoT) lakini bado ufisadi wa EPA ukafanikiwa, na kama TISS ipo kazini saa 24 lakini bado kuna majambazi wamemudu kutorosha mabilioni ya dola na kuzificha nchini Uswisi basi ni wazi Idara hiyo ni dhaifu.
Na kama tunakubaliana kuwa kuna udhaifu mkubwa katika taasisi hiyo, kwa nini basi CHADEMA wasiamini taarifa kuwa Idara hiyo ina mpango wa kuwadhuru? Sitaki kuamini kuwa, iwapo taarifa hizo ni kweli, basi ni za ki-Idara bali ninaendelea kuhisi kuwa ni matokeo ya kulea ‘rogue elements’ ndani ya chombo hicho muhimu.
Unajua, inapofika mahala Afisa Usalama wa Taifa anaona sifa kutangaza wadhifa wake baa ili vimwana watambue kuwa yeye ni shushushu, au kiongozi mwandamizi wa taasisi hiyo nyeti anapoweza kufanya ‘madudu’ hadi sisi tulio nje ya nchi tukafahamu, basi ni wazi kunahitajika kazi ya ziada kurekebisha mwenendo wa chombo hicho nyeti.
Ninatambua kuwa kuna watakaokerwa (na pengine kushauri hatua ‘mwafaka dhidi ya mtizamo wangu’) lakini ninaamini kuwa kila Afisa Usalama wa Taifa mzalendo na aliyekula kiapo cha utii kwa Taifa anakerwa kuona nchi yetu ikienda kwa mwendo wa bora liende huku rasilimali zetu zikiporwa kwa mtindo wa ‘bandika bandua.’
Pasipo mageuzi ya haraka ndani ya taasisi hiyo si tu itaendelea kutuhumiwa na CHADEMA lakini mwishowe walipa kodi wanaowezesha maslahi manono kwa wanausalama wetu watasema ‘imetosha.’
Watanzania wanaweza kufika mahala wakahoji umuhimu wa kuwa na taasisi ya ‘kufikirika’ ambayo licha ya kuogopwa na wengi (nikiamini bado kuna wanaoiogopa) inashindwa kudhibiti uharamia lukuki unaofanywa dhidi ya nchi yetu na Watanzania wenzetu kwa kutumia madaraka yao.
Nimalizie makala hii kwa kutoa tahadhari kwa Idara hiyo kwamba maswali magumu hayajibiwi kwa majibu mepesi. Mmoja wa viongozi wa ngazi za juu za taasisi hiyo amejibu tuhuma zilizotolewa na CHADEMA kwa namna ileile alivyojibu mwaka 2010 pale Idara hiyo ilipotuhumiwa kuihujumu CHADEMA kwenye kinyang’anyiro cha Uchaguzi Mkuu. Tatizo la kiongozi huyo, na pengine Idara hiyo kwa ujumla ni uzembe wa kusoma alama za nyakati.
Na kila mzalendo-awe ndani ya taasisi hiyo au mwananchi wa kawaida-anapaswa kupinga kwa nguvu zote dalili za kutaka kuigeuza nchi yetu kuwa ‘Mafia State’ (yaani dola ambayo kila TomDick na Harry anaweza kuteka na kutesa au kupanga kuuwa wale  wanaopigania haki za wanyonge kama hao viongozi wa CHADEMA wanaodai kutishiwa kuuawa kwa ‘kosa la kuwakalia kooni wabaka uchumi wetu.’
Biblia inasema mwenye haki ataanguka saba mara sabini lakini atasimama. Na kila mzalendo atakwazwa vya kutosha lakini, inshallah, Tanzania tunayoistahili itafikiwa."
Rais Kikwete (kushoto) akiongea na Othman (katikati) na Mkuu wa  JWTZ  Jenerali Davis Mwamunyange
Juzi, gazeti la Mtanzania limechapisha habari ya kiuchunguzi ambayo kwa kiasi kikubwa imeakisi hicho nilichobashiri katika makala yangu hapo juu.Labda kabla ya kuendelea ninukuu paragrafu zifuatazo kabla hatujaendelea zaidi na mada hii 
"...mgawanyiko kwa wafanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa, ambako uchunguzi unaonyesha kuwa baadhi yao wameasi na kuamua kufanya kazi kwa karibu na makundi yanayowania urais, badala ya ile ya kusimamia maslahi ya taifa.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya makundi hayo, vinaeleza kuwa matukio ya sasa ya kudhuru watu maarufu yanadaiwa kufanywa na watumishi wenye mafunzo ya kutesa na kuua walio ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa kwa malengo yenye maslahi fulani fulani.

Mmoja wa wanasiasa maarufu hapa nchini ambaye amepata kushika nyadhifa mbalimbali serikalini, amelieleza MTANZANIA Jumatano kuwa vitendo vya kushambulia na kudhuru raia vinafanywa na watumishi wa Idara ya Usalama walioviasisi kwa madhumuni ya kuwachonganisha wananchi na serikali yao, ili wazidi kujenga chuki na watawala.

Anaeleza zaidi kuwa wanausalama wanaodaiwa kuasi kutokana na kukatishwa tamaa na mwenendo wa uendeshaji serikali sasa wamejipenyeza na kuwa wakala wa moja ya kundi la wanaCCM linalopambana na makundi mengine ya ndani ya chama hicho kushika ukuu wa dola na wapo pia wanaodaiwa kujipenyeza katika vyama vya upinzani, hususani Chadema na kushiriki harakati za kuiondoa CCM madarakani..."
Ukirejea nilichoandika katika makala yangu utabaini kuwa taarifa hiyo ya kiuchunguzi ni kama imekithibitisha.Siandiki post hii kwa minajili ya kupongezwa au kusifiwa bali kupigia mstari umuhimu wa Idara ya Usalama wa Taifa kufanyiwa marekebisho makubwa haraka iwezekanavyo.
Tunapokuwa na chombo nyeti kama hicho kikiwa kimegawanyika mapande mapande, huku baadhi ya maafisa wake wakijichukulia sheria mkononi, basi ni wazi kuwa nchi inaelekea kubaya.
Najua haya ninayoandikwa yatapuuzwa na Serikali ya Rais Kikwete lakini madhara ya kupuuza huko yanaweza kuwa makubwa kuliko inavyofikiriwa sasa. Ni muhimu kwa Rais Kikwete kutambua kuwa usalama wake binafsi na wa viongozi wengine wakuu wa serikali upo mikononi wa Idara ya Usalama wa Taifa. Hivi katika hali ya kufikirika tu, haiyumkiniki kuhisi kuwa ipo siku baadhi ya maafisa wa Idara hiyo (ambayo ni wazi inaonekana kukosa mwelekeo na mwongozo) wakaishia kumdhuru kiongozi kwa namna moja au nyingine?
Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa wakimsaidia Rais Kikwete alipoanguka jukwaani wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. Picha hii inaonyesha jinsi wanausalama hao walivyo karibu na viongozi wakuu wa kitaifa
Natambua kuwa Rais Kikwete anaweza kuwa anaelewa kinachoendelea ndani ya Idara hiyo lakini kama ilivyo kwenye maeneo mengine, Rais wetu ni mgumu wa maamuzi.Lakini pengine kitakachomkwaza zaidi kushughulikia tatizo hili ni makosa aliyofanya huko nyuma katika uteuzi wa uongozi wa Idara hiyo ambao ulizngatia zaidi 'ushkaji' badala ya 'uwezo wa kiutendaji kazi.'
Rais Kikwete (katikati) akiomba dua na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Othman Rashid (kushoto) na Makamu wa Rais Dkt Gharib Bilal. Kikwete na Othman ni marafiki wa muda mrefu
I just hoipe hakuna baya litakalojitokeza huko mbeleni lakini hisia yangu ya sita inakinzana na imani hiyo.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.