8 Oct 2008

Hawa TANESCO vipi?Kwanza walitangaza mgao wa umeme wa takriban masaa matano kwa siku kabla ya kuongeza muda na kuwa takriban masaa kumi kwa siku.Siku chache baadaye wakatangaza kuisha kwa mgao huo,lakini kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima,mgao umerejea tena.Ubabaishaji wa aina hii utaendelea hadi lini?


Inapotokea pundits wa Fox News,Mort Condracke,Bill Kristal,Nina Easton na Fred Barnes, wanakubaliana kitu kimoja "kummaliza" John McCain basi hapo huhitaji kwenda mbali kuhitimisha kwamba mgombea huyo kachemsha.And that's exactly what happened mara baada ya mdahalo kati ya Obama na McCain ambao ulichukua format ya town hall meeting.Kadhalika,mtizamo wa undecided voters kwa mujibu wa Frank Luntz ni kwamba Obama ameshinda tena mdahalo huo ambao ni wa pili kati ya midahalo mitatu iliyokubaliwa na wagombea hao.

Kwa mujibu wa wachambuzi wa uchaguzi huo,McCain alihitaji a kcock-out punch,yaani ilikuwa ni lazima afanye vizuri katika mdahalo huo ili kujiweka vizuri katika jitihada zake za kushinda uchaguzi hapo Novemba 4.Kura nyingi za maoni zinaonyesha mgombea huyo wa Republican akiwa nyuma ya Obama,na ilitarajiwa kwamba kufanya kwake vizuri katika mdahalo huo kungemsaidia kupunguza gap hiyo.Kilichokuwa kinawapa matumaini wafuasi wa McCain ni uzoefu wake katika town hall meetings.Hata hivyo,uzoefu huo unaonekana kutomsaidia mgombea huyo,na pengine fursa yake pekee ni aidha kitoke kitu kisichotarajiwa (hata kama hakihusiani na uchaguzi huo) ambacho kitabadili kabisa landscape ya uchaguzi huo au afanye vizuri kupita kiasi katika mdahalo wa mwisho (na wakati huohuo Obama afanye vibaya).

Moja ya kauli ambazo zinaweza kumgharimu McCain ni ile ya kumuita Obama "that one",na kinyume na mdahalo uliopita ambapo wagombea hao walishikana mikono kabla na baada,safari hii hilo halikutokea baada ya shughuli hiyo pevu ambapo McCain alikuwa wa kwanza kuondoka kitini (pengine kukwepa handshake na Obama).

Kwa uchambuzi na habari zaidi bofya HAPA na HAPA na HAPA




Mitihani zaidi kidato cha nne yavuja Necta iko njia panda
BARAZA la Mitihani Tanzania (Necta) bado liko njia panda kuhusu hatua za kuchukua baada ya mtihani mwingine wa kuhitimu kidato cha nne mwaka huu kuthibitika kuwa umevuja.

Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi kwa siku kadhaa sasa unaonyesha kwamba, wanafunzi wa kidato cha nne tayari walishakuwa na mitihani hiyo, hivyo wamekuwa wakijibu maswali katika maeneo mbalimbali ya nchi kabla ya kuingia kwenye chumba cha mtihani.

Juzi Baraza lilitangaza kuufuta mtihani wa somo la Hisabati ambao ulikuwa uanze kufanywa kwa kile kilichoelezwa kuwa umevuja na kwamba, vyombo vya usalama vinafanya uchunguzi zaidi kwa mitihani mingine ya Kiswahili, Kiingereza, Fizikia na Uraia inayodaiwa kuvuja.

Lakini jana Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova aliwaambia waandishi wa habari kuwa jeshi lake linawashikilia wanafunzi wawili kutoka kituo cha Perfect Vision, mmoja kwa tuhuma za kukutwa na majibu ya mtihani wa somo la Civics (Uraia) na mwingine kwa kumfanyia mwenzake.

Kamanda Kova alisema watuhumiwa hao, walikamatwa juzi saa 11:00 jioni wakiwa katika kituo hicho kilichopo maeneo ya Ubungo karibu na nyumba za Shirika la Nyumba nchini.

Kwa mujibu wa Kamanda Kova, mwanafunzi wa kwanza kukamatwa ni mtahiniwa wa kujitegemea Rhoda Juma Mombora (37) ambaye alikamatwa na majibu ya mtihani wa somo hilo uliofanywa juzi mchana. Mtuhumiwa wa pili, Clara Haule (20) mkazi wa Makumbusho alikamatwa akimfanyia mtihani Anjela Maganga mwenye namba P1475/0023.

Kova alisema watuhumiwa hao, wanashikiliwa na polisi na uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili. Idadi ya watuhumiwa inafikiriwa kuongezeka.

Japokuwa ni watahiniwa hao tu walionaswa, wanafunzi mbalimbali waliozungumza na Mwananchi katika maeneo mbalimbali nchini na jijini Dar es Salaam walidai kuwa wana mitihani yote na kwamba hata waliyofanya juzi walikuwa nayo. Walisema baada ya kuingia katika chumba cha mtihani walibaini kuwa ndiyo yenyewe.

"Mitihani yote tunayo hata ule wa jana (juzi) wa somo la Uraia (Civics), tulikuwa nao na baada ya kuingia katika chumba cha mtihani tulibaini kuwa ndiyo wenyewe, swali mpaka swali," alidai mwanafunzi mmoja wa jijini Dar es Salaam (jina tunalo).

Mwanafunzi huyo alidai kuwa walipata mitihani hiyo kutoka kwa watu walio karibu na Baraza baada ya kuchanga fedha na kuwapatia watu hao.

Mazingira ya kuvuja kwa mitihani hiyo yanaonyesha kuwa iliibwa kutokana na mpango wa ndani uliosukwa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu kwa lengo la kujipatia kipato.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo baada ya kupata mitihani wanafunzi hao wamekuwa wakitumia simu za mikononi kupeana maswali au majibu kabla ya kuingia katika chumba cha mitihani.

Katika hatua nyingine Umoja wa Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya juu nchini (Tahliso) umetaka mtihani wote wa kidato cha nne ufutwe na kisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe na watendaji wakuu wa Baraza kujiuzulu kutokana na kashfa hiyo ambayo mara ya mwisho ilitokea mwaka 1998.

Katibu Mkuu wa Tahliso, Mtatiro Julius alisema jana jijini kuwa, kashfa ya kuvuja kwa mitihani hiyo inawahusu viongozi hao moja kwa moja na hivyo hawapaswi kukwepa kuwajibika.

"Waziri anapaswa kuwajibika mwenyewe kwa kulinda heshima yake, lakini zaidi kwa manufaa ya umma kwani ameshindwa kuwasimamia vema watendaji wa chini yake," alisema Mtatiro na kuongeza:

"Kitendo cha mitihani kuvuja na serikali kuufuta mmoja na kuacha mingine iendelee kitazalisha wasomi wasiokuwa na uwezo,".

Kwa mujibu wa Mtatiro, inasikitisha kuona serikali inakiri kuvuja kwa mtihani wa Hisabati kwani kauli hii inaleta uwezekano wa mitihani yote kuwa imevuja kwa kuwa mitihani hiyo iliandaliwa pamoja na kusambazwa pamoja.

"Hali ya kuvuja kwa mitihani nchini imekuwa ya kawaida sana ingawa miaka mingine serikali inakanusha tuhuma hizo. Katika hili la mwaka huu, ni lazima Rais Jakaya Kikwete atumie nafasi yake kuwawajibisha watendaji wake," alisema.

Mtatiro alibainisha kuwa tatizo la kuvuja kwa mitihani nchini linatokana pamoja na mambo mengine tamaa ya fedha na walimu kutolipwa mishahara mizuri.

Aliitaja sababu nyingine ya kuvuja kwa mitihani kuwa ni ubinafsi na uzembe unaofanywa na baadhi ya watendaji wakuu katika kusimamia mitihani na upole wa Rais Kikwete katika kuwachukulia hatua watendaji wake wanaoboronga kazini.

"Upole wa Rais Kikwete ndiyo unaosababisha watendaji wa chini wajione kuwa wako huru na hakuna wa kuwawajibisha," alisema.

Juzi Baraza lilifuta mtihani wa Hisabati baada ya kubainika umevuja. Hata hivyo Baraza halikuwa tayari kutaja sehemu wala watu waliokamatwa na mtihani ambao sasa utatungwa mwingine na kufanywa Oktoba 27, mwaka huu.

Mwaka 1998, Baraza hilo lilifuta mitihani yote baada ya kubaini kuwa mingi ilivuja na hivyo kulazimika kusogeza mbele tarehe ya kuanza kwa mitihani na hali inaonekana inaweza kujirudia mwaka huu kutokana na mitihani hiyo kuzagaa kama njugu.

Awali Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania, Dk Joyce Ndalichako alisema baraza hilo limeanza kufanya uchunguzi wa uvujaji wa mitihani mingine nchi nzima baada ya kupata taarifa juu ya kuwepo kwa mitihani zaidi kwenye mikono ya watahiniwa ikiwemo Kingereza, Kiswahili, Fizikia na Uraia.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi kuhusu kuvuja kwa mitihani, Dk Ndalichako alisema vyombo vya usalama vimekamata mitihani ya Kiswahili, Kiingereza, Uraia, Fizikia pamoja na Historia na kwamba, uchunguzi zaidi unafanyika, lakini hakutaja sehemu ambazo mitihani hiyo ilikamatwa kwa kile alichoeleza kuhofia kuharibu uchunguzi unaoendelea.

Kashfa ya kuvuja kwa mitihani ni mwendelezo wa kashfa mbalimbali zinazoendelea kulikumba Baraza hilo baada ya hivi karibuni kuripotiwa kuibwa vyeti 4,000 vikiwa na namba bila ya majina.

SOURCE: Mwananchi

MBONA HII INATOKEA KILA MWAKA LABDA TATIZO KWA MITIHANI YA MWAKA HUU NI HIYO MEDIA ATTENTION.KUNA WATU WENYE JUKUMU LA KUHAKIKISHA MITIHANI HAIVUJI,NA WANALIPWA KWA KAZI HIYO LAKINI MWAKA HADI MWAKA MAMBO YANAENDELEA KUWA YALEYALE.NA SIJUI KWANINI HADI MUDA HUU UONGOZI WA NECTA HAUJAWAJIBIKA.ANYWAY,WANAJUA KWA UTAMADUNI WETU KUBORONGA SIO SABABU TOSHA YA KUJIUZULU MAJUKUMU WALIYOKABIDHIWA.


7 Oct 2008

Mwaka:1992
Mahala: Ruvu JKT
Miss Independent: Binti mrembo wa haja.Lakini kikwazo ni kwamba ni mtoto wa Mkuu wa Kikosi (CO).Na kwa wale ambao hawakuwahi kukanyaga JKT,CO ni Mungu-mtu wa Kikosi.You can imagine what would be the consequence ya "kuziingiza" kwa Miss Independent ambaye ni Mkuu wa Kikosi.

Mwaka: 1995
Mahala: Chuo flani (location withheld)
Miss Independent: Mmoja wa mabosi wa chuo hicho.Unajua kuna warembo ambao nadhani Mola alitumia siku nzima kuwa-design na siku nyingine nzima kuwaumba.Sheria za mahala hapo ziko wazi: speak to the boss only when they speak to you.

Mwaka: 2008
Mahala:Dar es Salaam.
Miss Independent: Kumwita huyu binti mrembo ni kutomtendea haki.Angeweza kuonewa donge hata na malaika.Hakuna neno linaloweza kuelezea urembo wake.Kikwazo ni kwamba anatoka familia yenye kujiweza mno.Hapo mahala pake pa kazi alikuwa anaondoka na tips za haja nyingi zikiwa in foreign currencies,achilia mbali fedha zisizohesabika alizokuwa akipewa na wale wanaoamini kuwa dawa ya kumpata mrembo yeyote ni fedha.Lakini they say when all luck is gone miracles happen in strangest form.This episode had a happy ending just like Ne-yo couldnt believe his ears when Miss Independent,Gabriele Union,apologized and....see the clip below





A French scientist awarded the Nobel Prize for discovering the Aids virus has  predicted there would be a 'therapeutic vaccine' for the disease within four years.

Luc Montagnier and his team discovered HIV at the French Pasteur Institute in Paris 25 years ago, and have been awarded the prestigious prize along with other scientists who worked on discovering the root of the virus.

Montagnier, 76, said a treatment could be possible in the future with a 'therapeutic' rather than preventive vaccine for which results might be published in three or four years if financial backing is forthcoming.

'I think it will be possible with a therapeutic vaccine rather than preventative vaccinations. We would give it to people who are already infected.

A therapeutic vaccine prevents disease from flourishing after it has taken hold.

The Nobel Assembly of Sweden's Karolinska Institute praised their work, saying: 'The discovery was one prerequisite for the current understanding of the biology of the disease and its antiretroviral treatment.'

The other half of the Nobel prize was awarded for the German scientist's research that 'went against current dogma' by setting forth that oncogenic human papilloma virus (HPV) caused cervical cancer, the second most common cancer among women.

Medicine is traditionally the first of the Nobel prizes awarded each year.

The prizes for achievement in science, literature and peace were first awarded in 1901 in accordance with the will of dynamite inventor and businessman Alfred Nobel.

The economics prize is a later addition, established by the Swedish Riksbank in 1968.

The Nobel laureate for physics will be announced tomorrow, followed by the chemistry Nobel on Wednesday, literature on Thursday and the Nobel Peace Prize on Friday in Oslo.

SOURCE: Daily Mail


6 Oct 2008



CLICK HERE to read the story.


Here's a summary of the smartest new political analysis on the Web: by Gerald F. Seib and Sara Murray 

It's been a bad stretch for Sen. John McCain, but few have been willing to go this far: Former Hillary Clinton spokesman Howard Wolfson, now writing for The New Republic, declares flatly "The race is over." Sen. Barack Obama will win, he says. 

"John McCain's candidacy is as much a casualty of Wall Street as Lehman or Merrill. Like those once vibrant institutions, McCain's collapse was stunning and quick. One minute you are a well-respected brand. The next you are yelling at the messengers of your demise as all around you the numbers start blinking red and stop adding up." Before the Wall Street collapse, Wolfson writes, "Senator McCain was ahead." But today, "an election dominated at its inception by the war in Iraq is now overwhelmingly focused on the economy. More than half of voters in polls say that the economy is their top concern and Senator Obama enjoys double digit leads among voters asked who can better fix our economic mess. Put simply, there is no way Senator McCain can win if he continues to trail Senator Obama by double digits on the top concern of more than half of voters."

But the Obama campaign isn't taking any chances. Politico's Mike Allen reports that his campaign "on Monday is launching a multimedia campaign to draw attention to the involvement of Sen. John McCain (R-Ariz.) in the ‘Keating Five' savings-and-loan scandal of 1989-91, which blemished McCain's public image and set him on his course as a self-styled reformer." The move is a reaction to the McCain camp's new efforts to tie Sen. Obama to 1960s radical William Ayers and scandal-plagued Chicago businessman Tony Rezko. Overnight, Allen says, the Obama campaign "began e-mailing millions of supporters a link to a website, KeatingEconomics.com, which will have a 13-minute documentary on the scandal beginning at noon Eastern time on Monday. The e-mails urge recipients to pass the link on to friends. The Obama campaign, including its surrogates appearing on radio and television, will argue that the deregulatory fervor that caused massive, cascading savings-and-loan collapses in the late ‘80s was pursued by McCain throughout his career, and helped cause the current credit crisis."

The Huffington Post's Thomas B. Edsall writes that "At a time of extreme economic crisis at home and two wars abroad, John McCain is gambling that an attack mounted by Sarah Palin on Barack Obama's tangential ties to 1970s radical bomber Bill Ayers will reverse the Arizona Senator's steadily diminishing prospect of victory on November 4. This strategy carries high risks. First and foremost, a number of experts in the field doubt that when the economy has been on the brink of collapse, when the situation in Afghanistan is worsening, and the debate over the US war in Iraq has intensified, negative campaigning is an effective political tool." 

It's also naive to expect that Obama won't fight back. Plus, negative campaigning tends to damage both candidates. Edsall quotes polling expert Nate Silver as saying "It may be quite difficult for McCain to attack Obama in this fashion without significantly damaging his own brand. What's interesting is that, with the exception of the past couple of weeks, McCain's and Obama's ratings have been fairly strongly correlated, tending to rise and fall together. This is not to say that negative campaigning doesn't work - it sometimes does - but it works at diminished efficiency, because you may be giving back 50 cents on the dollar by harming your own approval scores."

Now onto battleground states. Washingtonpost.com's Chris Cillizza has updated his electoral map, which puts Obama above the 300 mark. "The movement is most noticeable in states - particularly in the Industrial Midwest - where the economy has been a front-burner issue for years...With that in mind, we have moved Ohio from McCain's column to Obama's - amid polling including a new Columbus Dispatch survey that shows the Illinois senator with an edge. The other major change in this week's Fix map is Virginia, which we are moving from McCain to Obama. Electoral history in the state is daunting for Obama - the last Democrat to carry the state at the presidential level was Lyndon Johnson way back in 1964 - but the Democratic candidate is lavishing time and money on the Commonwealth. And, even top Virginia Republicans are starting to express their concern publicly about McCain's dimming prospects there

SOURCE: Wall Street Journal



With 30 days until Nov. 4, Karl Rove projects that Sen. Barack Obama (D-Ill.) would get at least 273 electoral votes – three more than are needed to win – if the presidential election were held today.

But Rove warns that this race is “susceptible to rapid changes,” so no definite prediction is possible.

The remarkable forecast from the architect of the last two nationwide political victories underscores the straits that have rapidly enveloped Sen. John McCain (R-Ariz.) as the banking and credit crisis spread.

Rove writes on Rove.com: “39 new state polls released in the first three days of October have given Barack Obama his first lead over the magic number of 270 since mid-July. Minnesota (10 EV) and New Hampshire (4 EV) both moved from toss-up to Obama, giving him 273 electoral votes to McCain’s 163, with 102 votes remaining as a toss-up.

“If the election were held today, Obama would win every state John Kerry won in 2004, while adding New Mexico (5 EV), Iowa (7 EV), and Colorado (9 EV) to his coalition. Remember, though, that these state polls are a lagging indicator and most do not include any surveying done after the vice-presidential debate on Thursday night.”

Rove cautioned on “Fox News Sunday”: “Remember, the campaign ebbs and flows. What we're seeing here is a result of the focus of the American people, voters, on the economic problems that have dominated the news the last several weeks. What's happened then is a shift to Obama.

“Just remember, 17 days ago in the electoral college, McCain led 227 to 216. Fifteen days ago, on the eve of the news on the bailout, he led 216-215.This race is susceptible to rapid changes and we're likely to see, in the remaining four weeks, more changes.”

On “Meet the Press” on Sunday, NBC News Political Director Chuck Todd said Obama is still one state away from solidifying the 270 electoral votes he needs to win the White House. Colorado, Virginia or Florida would put it away for Obama if the election were held today, Todd said.

“Even if it’s Nevada [making the total] 269, it sends it to the House, where Democrats have an advantage,” Todd said. “As it stands today, John McCain would have to run the table. Now, good news for him: They’re all states that voted Republican four years ago.

“However, he’s behind right now a little bit in Ohio. There’s a dispute of who’s ahead or who’s behind in Florida but it feel as if Obama’s a little bit ahead in Florida. Obama’s a little bit ahead in Colorado. And it’s a dead even race in Virginia. Dead even in Nevada. And even Missouri, which we almost put in tossup this week, is getting very close, where McCain just has a very narrow lead.”

Todd said a landslide could be 364 electoral votes – “the high-water mark.” In 1980, Ronald Reagan got 489. In 1988, George H.W. Bush got 426. “The McCain folks now have to hold everything … to keep this thing competitive,” Todd said.


Mike Murphy, a Republican strategist who was the architect of McCain’s 2000 campaign said on “Meet the Press”: “It’s McCain’s barn that’s on fire. … Thirty days out, I think McCain can win. But the fact is, [if the] election were held today, he’d lose. And I think he’s on a losing path.

“I think the McCain campaign has to look in the mirror now and decide, do we need to change up the strategy? They’ve been running the grinding campaign on Obama. There’s a lot of good things to attack Obama about – people have a lot of doubts about Obama. But they’ve got to fix McCain. McCain has to connect with voters on the economy. He’s got to get ticket-splitters. Get out of base Republican issues and get people who are worried about the economy and health care over. Or in this anti-Republican environment, this trend line is very, very bad.”

Appearing with Murphy, Democratic consultant Paul Begala, who helped mastermind Bill Clinton’s 1992 win, said he had talked to the Obama high command. “They’re flooding the zone,” Begala said. “They’re going into places where Democrats used to never dare go. Indiana! I cannot believe we’re sitting here 30 days before an election, talking about Indiana, a potential tossup state. Or North Carolina and Virginia.

“Barack Obama would be the first non-Southerner from my party to carry a Southern state since JFK – before I was born, before Barack was born. This is an incredible map.

Source: POLITICO



AND FINNALY (This is not a Classic,and it's not from the US of A.Just listen to the message)

REMINISCING THE DAYS WHEN I JUST LANDED INTO THE UK
AND THIS REMINDS OF THE OLD JKT DAYZ
AND FINALLY,I JUST HOPE SOMEONE IS READING BETWEEN THE LINES WHEN WATCHING THIS CLIP BELOW


5 Oct 2008


JAJI Kiongozi, Salum Massati, amesema kuanzia sasa madereva watakaosababisha vifo katika ajali za barabarani watanyang’anywa leseni na hata kufungwa miaka miwili jela ili kupunguza matukio hayo.

Akizungumza mjini hapa, Jaji Massati alisema ili kufanikisha mkakati huo, Mahakama ya Tanzania imewaagiza mahakimu wake kutafsiri vizuri na kwa usahihi sheria ya makosa ya barabarani ili kuwabana madereva wazembe. 

Agizo hilo lilitolewa alipokuwa akizungumza na watumishi wa mahakama hiyo Kanda ya Iringa. 

Alisema kwa kipindi kirefu madereva wanaopatikana na hatia za kuua kutokana na makosa ya barabarani wamekuwa wakipata adhabu ndogo, jambo linalolalamikiwa kuchochea matukio ya ajali. 

“Hivi sasa mahakama zimebebeshwa mzigo huu wa lawama kana kwamba sisi ndio chanzo cha kuendelea kwa ajali nyingi barabarani kwa kuwa adhabu tunazotoa haziwiani na makosa yanayofanywa yakiwamo ya kusababisha vifo,” alisema. 

“Sheria inataka anayesababisha kifo kwa makosa ya barabarani ahukumiwe miaka miwili jela na anyang’anywe leseni yake, lakini mahakimu wetu hawatoi hukumu hiyo,” alisema. 

Alisema badala yake madereva wengi wanaokutwa na hatia za makosa hayo hupigwa faini ndogo na kuachiwa. 

Jaji Massati alisema mianya iliyopo katika sheria ya Usalama Barabarani imesababisha wakati mwingine dereva aliyesababisha ajali ambayo hata kama imeua watu 20 apigwe faini na kurudishiwa leseni yake. 

“Pale Kibaha, Pwani aliwahi kukamatwa dereva mwenye leseni feki aliyesababisha ajali na kuua, hata hivyo alipofikishwa mahakamani alihukumiwa kwa faini ya Sh 10,000 na kurudishiwa leseni yake. 

“Sidhani kama hukumu hiyo ilikuwa sahihi na inatoa fundisho kwa madereva wengine kuzingatia sheria zote za barabarani,” alitoa mfano.


Kwa mujibu wa sheria,kila mvunja sheria anapaswa kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria (kifungo ikiwa ni mojawapo ya adhabu hizo).Ajali za barabarani zinapoteza maisha ya Watanzania wenzetu kila kukicha,lakini ufisadi nao unaathiri (na pengine hata kupoteza) maisha ya mamilioni ya Watanzania kila dakika.Madereva wanaosababisha ajali na mafisadi wote ni wavunja sheria na wanapaswa kudhibitiwa kwa kuchukuliwa hatua kali ili,kwa upande mmoja,iwe fundisho kwa wengine,na kwa upande mwingine,wavunja sheria wavune wanachopanda.

Lakini pamoja na kuunga mkono mtazamo wa Jaji Kiongozi,nadhani kuna umuhimu wa kwenda mbali zaidi kuangalia vyanzo vya ajali mbali ya uzembe wa madereva.Tuchukulie madereva wa daladala kwa mfano.Mazingira yao ya kazi yanafanywa kuwa magumu na wamiliki wa daladala wenye uchu wa faida pasipo kujali sana mazingira ya kazi ya wanaowaletea faida hiyo.Na hapo tumewaweka kando askari trafiki wenye kudai rushwa waziwazi kana kwamba ni haki yao.

Hivi anayeamua kuweka chasis ya lori kwenye basi la abiria ni dereva au mmiliki wa basi hilo?Je linapopata ajali kutokana na mechanical corruption hiyo wa kulaumiwa ni dereva au mmiliki wa basi hilo?Na vipi kuhusu trafiki wanaokagua mabasi ya abiria?Au vipi kuhusu wiki ya usalama barabarani ambayo inaadhimishwa kila mwaka?Kwa mmiliki wa basi bovu kulikabidhi kwa dereva kwa ajili ya biashara inamaanisha kwamba ametoa baraka kwa lolote litakalotokea,ikiwa ni pamoja na ajali.Same could be concluded about mamlaka zinazoruhusu gari bovu kuwepo barabarani.

Hapa tunarudi kwenye tatizo lilelile la kila mara la kuangalia matokeo badala ya chanzo.Au kwa mtazamo mpana zaidi,kuhukumu vidagaa badala ya papa.Madereva wengi wa mabasi ya abiria wanalazimika kuyakubali mazingira magumu ya kazi hiyo sio kwa vile wanaipenda sana bali kutokana na tatizo zima la ajira huko nyumbani.Hakuna mtu mwenye akili timamu aliye tayari kuendesha "jeneza linalotembea" (a walking coffin),yaani magari ambayo yako barabarani kwa kudra za Mwenyezi Mungu pekee.

Sawa,madereva wanaosababisha ajali wanapaswa kuchukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kifungo.Lakini pasipo kukomesha tatizo la kuwepo kwa magari mabovu barabarani,vifungo vitaendelea na ajali zitaendelea pia.By the way,kama vifungo pekee vingekuwa kizuizi cha kuvunja sheria,idadi ya wafungwa waliopo magerezani (na mazingira ya kutisha wanayoishi huko) ingetosha kukomesha uvunjifu wa sheria unaoweza kupelekea mtu kwenda gerezani.Pasipo kuangalia upande wa pili wa tatizo,yaani wamiliki wa vyombo vya usafiri wanaoweka mbele faida kuliko uhai wa abiria wao,na trafiki wanaothamini rushwa kuliko maisha ya Watanzania wenzao,basi ajali zitaendelea hata kama adhabu kwa kosa la kusababisha ajali itakuwa hukumu ya kifo.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.