Showing posts with label EDUCATION IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label EDUCATION IN TANZANIA. Show all posts

23 Oct 2008


Serikali imeionya Taasisi ya HakiElimu kuacha kutumia matangazo yake katika vyombo vya habari, kueneza chuki miongoni mwa watoto na vijana nchini na badala yake ingetumia nafasi iliyonayo katika kuwafundisha utawala bora. 

Aidha, imewatahadharisha wote wanaoanzisha taasisi za elimu kwa minajili ya kupata fedha bila kuchangia lolote katika sekta ya elimu, ikiwa ni pamoja na shule zinazotoza wazazi fedha nyingi ambazo hazilingani na mazingira na kiwango cha elimu kinachotolewa. 

Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii katika ofisi za Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Lucy Nkya, alisema HakiElimu pamoja na kuonywa na kusimamishwa hivi karibuni kutokana na utendaji wake, bado imeendelea kutoa matangazo ambayo yanaeneza chuki kwa vijana. 

Hili tangazo tena linalorushwa hata televisheni ya TBC1 la watoto wa sekondari wanazungumzia EPA, wanafanyiwa hesabu na kisha wanaambiwa waseme hizi hela zingefanyia hili na lile, kumbukeni samaki mkunje angali mbichi, huku ni kueneza chuki kwa watoto hawa,” alisema Dk. Nkya. 

Alisema taasisi hiyo ya HakiElimu inakosea kutumia matangazo hayo kwa upande mmoja tu wa kukosoa. “Mimi nimesomea saikolojia, huu mtindo wa kukosoa serikali kwa namna hii, kunawajengea vijana wetu chuki, badala ya kuwafundisha utawala bora, sasa watoto wanafikiri serikali yote ni mafisadi,” alisema. 

Alisema kutokana na matangazo na vitendo hivyo kwa sasa, hata watoto wa baadhi ya viongozi wamelazimika kuhamishwa katika shule za kawaida na kupelekwa shule nyingine kwa vile wanaitwa watoto wa mafisadi na wenzao. 

Aliitaka taasisi ya TEN/MET kufikisha ujumbe kwa HakiElimu kuwa wanayo nafasi nzuri kuelimisha jamii juu ya masuala ya sekta ya elimu na si kueneza chuki pekee, kwani serikali itafika mahala italazimika kutumia meno yake. 

“Msiisingizie serikali haina demokrasia pindi itakapotumia meno yake, haitokuwa kibogoyo tena,” alionya. Naye Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali wa Zanzibar, Haroun Ali Suleiman, alitaka kufahamu uwezo wa kiutendaji wa mtandao huo wa elimu kwa kuwa haujitangazi, kwani pamoja na yeye kuwa Waziri wa Elimu ndio anausikia. 

Kwa upande wake, Mratibu wa TEN/MET, Joseph Kisanji, alikiri kuwa mtandao huo umejificha na kwamba wanajitahidi kwa sasa kuutangaza kwa kutumia mtindo wao bila kuiga HakiElimu. 

Alisema awali wakati HakiElimu ilipokabiliwa na serikali, takribani asasi nyingi za elimu ziliwatetea ukiwamo mtandao huo. “Hata hivyo, kuna mipaka yake katika kutumia media (vyombo vya habari) kwani zina nguvu na tuliwaambia wenzetu juu ya hilo ila hatuna maamuzi, kazi yetu ni kushauri,” alisema. 

Alisema kama suala la tangazo la EPA limeleta athari hadi kufikia watoto wa viongozi kuhamishwa shule ni jambo hatari, hivyo aliahidi kulifikisha katika Bodi ya Mtandao huo ili walijadili na kulifikisha kwa taasisi hiyo ya HakiElimu. 

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TEN/MET, Antoine Gizenga, alisema watalivalia njuga suala la HakiElimu kwani mtandao wao unaitazama taasisi hiyo kama asasi inayosaidia kuibua yaliyojificha. 

Mwaka jana, Ofisi ya Waziri Mkuu ilipiga marufuku machapisho na matangazo yanayotolewa na HakiElimu kupitia vyombo vya habari na kutishia kulichukulia hatua kali za kisheria iwapo itakiuka amri hiyo.

CHANZO: HabariLeo



15 Oct 2008

WALIMU wa Mkoa wa Dar es Salaam jana walimshambulia kwa kumrushia mawe, chupa za maji, viti na meza, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania nchini (CWT), Gratian Mukoba, kwa madai kuwa amewasaliti kwa kukubali kuahirisha mgomo wao, uliotarajiwa kuanza leo nchi nzima.

Tafrani hiyo ambayo inazidi kuliingiza taifa katika sura mpya ya migomo ya wafanyakazi nchini, ilitokea jana katika Ukumbi wa Diamond Jubilee wakati walimu hao walipokutana kwa ajili ya kufanya maandalizi ya mwisho ya mgomo wao waliodai kuwa usingekuwa na kikomo, wenye lengo la kuishinikiza serikali iwalipe malimbikizo yao, yanayofikia zaidi ya sh bilioni 16.

Kikao hicho kilianza majira ya saa nne asubuhi na kuhudhuriwa na maelfu ya walimu kutoka Mkoa wa Dar es Salaam na wawakilishi wa mikoa ya Shinyanga na Mwanza.

Mwanzoni mwa kikao hicho kilichovunjika kutokana na vurugu hizo, walimu walikuwa watulivu kwenye viti vyao, kusikiliza kauli za viongozi wao, hasa Mukoba aliyekuwa akizungumzia hatima ya mgomo huo.

Ilipofika majira ya saa 6:20 mchana, Mukoba alishika kipaza sauti na kuanza kutoa tamko la chama hicho kwa nchi nzima kwamba mgomo wao ambao ulipangwa kuanza leo, umeahirishwa.

Huku baadhi ya walimu wakianza kunyanyuka kwenye vitu vyao na kutoa kelele za miguno iliyosikika kila kona, Mukoba alisema CWT imelazimika kuahirisha mgomo huo baada ya kushauriana na Mwanasheria wao, Gabriel Mnyele, aliyewataka waahirishe ili wapate nafasi ya kukata rufaa kupinga amri ya Mahakama Kuu, Kitengo cha Kazi, iliyozuia mgomo huo usifanyike leo.

“Kwa tamko hili ninalolisoma hapa mbele yenu, mgomo unaahirishwa kwa nchi nzima, hadi mwanasheria wetu atakapotujibu baadaye kutokana na zuio la mahakama lililotolewa jana (juzi),” alisema Mukoba.

Mara baada ya kutoa kauli, huku akiendelea kusoma maazimio mengine, ghafla umati wa walimu ulisimama kutoka kwenye viti vyao na kuvamia meza kuu, huku baadhi wakiipindua na kusababisha viongozi wa CWT kumwagikiwa maji yaliyokuwa juu za meza yao.

Kama hiyo haitoshi, baadhi ya walimu walianza kurusha chupa za maji na viti kwenye meza kuu, kwa lengo la kuwapiga viongozi wao, hasa Mukoba, aliyeonekana kushambuliwa zaidi.

Tafrani hiyo ilidumu kwa takriban dakika 35 ndani ya ukumbi huo uliokuwa na kelele nyingi za kuzomea, huku maofisa usalama wakilazimika kufanya kazi ya ziada kumwokoa Mukoba na viongozi wenzake, waliotaharuki kutokana na kushambuliwa huko.

Vita ya kurusha makopo, chupa za maji na viti iliposhika kasi, Mukoba na wenzake waliamua kukimbilia kwenye moja ya kona za ukumbi huo kujisalimisha, lakini hali hiyo haikuwasaidia, kwani walizidi kushambuliwa kwa kurushiwa vitu kama vibaka.

Tukio hilo lililoonekana kama filamu, mbali ya kuwapo kwa mashambulizi ya kurusha vitu, pia baadhi ya walimu walitoa lugha chafu kuwatukana viongozi hao na kuwataka wajiuzulu mara moja kwa madai kuwa wamewasaliti.

“Leo hatuwaachii, ama zenu ama zetu, walimu tumeonewa, tumedhalilishwa na kuibiwa vya kutosha na wewe Mukoba funga mdomo wako hapo mbele, tena katisha kusoma hilo tamko lako la kilaghai…sasa leo tutakufunza adabu kwa kukucharaza bakora ili ukome tabia hii ya usaliti.

“Kama ulikuwa unajua unakuja kutusomea hilo tamko la kipuuzi, kwanini usingeenda kwenye vyombo vya habari ukautangazie umma, kuliko kutuita hapa ukumbini kuja kutueleza ujinga kama huu…sasa leo utatujua sisi ni nani,” walisikika baadhi ya walimu wakitoa kauli hiyo.

Wakati vurugu hizo zikiendelea, majira ya saa 7:20 mchana makachero wa Jeshi la Polisi wakiongozwa na Kamanda wa Mkoa wa Ilala, Faustine Shirogile, Kamanda wa Upelelezi Mkoa wa kipolisi Ilala, Mkumbo na makachero zaidi ya 20, wakiwa na gari tatu aina ya Land Rover ‘Defender’, walifika eneo hilo kwa ajili ya kuimarisha ulinzi.

Makachero hao, walifanikiwa kuwatorosha viongozi hao kupitia mlango wa nyuma, huku baadhi ya walimu, nao wakitoka nje, kuangalia mlango uliolengwa kutumika kumtoa Mukoba na wenzake.

Wakiwa wanajipanga kumtorosha Mukoba kupitia mlango wa nyuma na kutaka kumwingiza kwenye gari la Polisi badala ya ‘Shangingi’ alilokuja nalo, walimu walibaini hali hiyo na kuamua kusogea karibu na gari hilo bila kuogopa vitisho vya polisi waliokuwa wakifyatua risasi hewani, kuwatawanya.

Wakati huo walimu wengi walikuwa wameshatoka ndani ya ukumbi kwenda kujipanga kandokando mwa barabara ya kwenda Shule ya Msingi Olympio, kwa lengo la kutaka kuendeleza mashambulizi.

Bila kuogopa risasi, wengine wakiwa na mawe mkononi, walilisogelea gari hilo la Polisi lenye namba za usajili T 220 AMV, huku wakiwakebei polisi kuwa nao wana njaa kama walimu na mishahara yao ni midogo, hivyo hawapaswi kuwazuia.

Ilipofika majira ya saa 7:30, polisi walilazimika kumtoa Mukoba na baadhi ya viongozi wa CWT chini ya ulinzi kwa ajili ya kuwapandisha kwenye gari hilo, lakini walimu nao walivyoona hali hiyo, walirusha mawe na jiwe moja lilimpata Mukoba sehemu ya tumbo na kusababisha aanguke kabla ya kusimama tena na kukimbilia ndani ya ‘Defender’ ya polisi.

Baada ya kuingizwa ndani ya gari hilo, polisi walirusha risasi hewani kabla ya dereva kuliondoa kwa kasi ili kuwatawanya walimu hao ambao walikuwa wakiendelea kulirushia mawe gari hilo.

Baada ya gari hilo kuondoka, hasira za walimu hao ziliishia kwenye kuimba nyimbo za kumsifu Mwalimu Nyerere.

Moja ya nyimbo hizo ni pamoja na ule unaotumika kwenye migomo mingi ya wafanyakazi nchini, ambao wao waliongezea vionjo kwa kusema: “Kama siyo juhudi zako Nyerere; Kikwete, Maghembe, Ghasia wangetoka wapi!”

Pia waliimba wimbo unaodai kuwa CCM ni chama cha mafisadi, huku wakikisifia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kuonyesha alama ya vidole viwili juu, inayotumiwa na chama hicho kusalimiana.

“CHADEMA, CHADEMA, CHADEMA oyeee! Sasa inatulazimu tufanye mapinduzi kama waliyofanya wenzetu wa Tarime kwa kuing’oa serikali ya CCM madarakani kwani inatukandamiza wanyonge na kukumbatia mafisadi,” walisikika wakisema baadhi ya walimu hao.

Hata baada ya Mukoba kuondolewa katika sehemu hiyo na kuliacha gari lake ambalo lilitolewa upepo na walimu hao, bado walimu hao walifunga barabara kuzuia magari yote yaliyokuwa yakipita eneo hilo huku, magari ya kifahari yakipigiwa kelele kuwa ni ya kifisadi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya walimu hao walisema licha ya kuwepo kwa amri ya mahakama kuzuia mgomo huo leo, wataendesha mgomo baridi, kwa kwenda kwenye shule zao, kujiandikisha kwenye vitabu vya mahudhurio, kisha kurejea majumbani mwao.

“Viongozi wa serikali wanajifanya wajanja, sasa sisi ndio walimu, na sisi ndio tunawafundisha watoto mashuleni, tutawafundisha uongo na mzazi mwenye uwezo ni vyema akampeleka mtoto wake shule binafsi,” alisema Mwalimu Lidyia Mhina.

Ilipofika majira ya saa 8:30 mchana, baada ya hali kuwa shwari, walimu walikusanyika nje ya ukumbi huo na Mwalimu Maulid Ng’umbe aliwatangazia walimu hao kuwa kuanzia sasa, CWT haina viongozi.

Juzi, Jaji William Mandia, wa Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi, aliamuru CWT kusitisha mgomo mara moja, kwa kuwa unaweza kuharibu mfumo wa elimu, hasa wanafunzi wa kidato cha nne, ambao wapo katika mitihani.

Mgomo huo ulitarajiwa kuanza leo baada ya CWT kutoa notisi ya siku 60 ambayo imemalizika jana. Walimu wote nchini wanaidai serikali zaidi ya sh bilioni 16, zikiwa na fedha za malimbikizo ya mishahara, likizo na kupandishwa madaraja.


8 Oct 2008




Mitihani zaidi kidato cha nne yavuja Necta iko njia panda
BARAZA la Mitihani Tanzania (Necta) bado liko njia panda kuhusu hatua za kuchukua baada ya mtihani mwingine wa kuhitimu kidato cha nne mwaka huu kuthibitika kuwa umevuja.

Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi kwa siku kadhaa sasa unaonyesha kwamba, wanafunzi wa kidato cha nne tayari walishakuwa na mitihani hiyo, hivyo wamekuwa wakijibu maswali katika maeneo mbalimbali ya nchi kabla ya kuingia kwenye chumba cha mtihani.

Juzi Baraza lilitangaza kuufuta mtihani wa somo la Hisabati ambao ulikuwa uanze kufanywa kwa kile kilichoelezwa kuwa umevuja na kwamba, vyombo vya usalama vinafanya uchunguzi zaidi kwa mitihani mingine ya Kiswahili, Kiingereza, Fizikia na Uraia inayodaiwa kuvuja.

Lakini jana Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova aliwaambia waandishi wa habari kuwa jeshi lake linawashikilia wanafunzi wawili kutoka kituo cha Perfect Vision, mmoja kwa tuhuma za kukutwa na majibu ya mtihani wa somo la Civics (Uraia) na mwingine kwa kumfanyia mwenzake.

Kamanda Kova alisema watuhumiwa hao, walikamatwa juzi saa 11:00 jioni wakiwa katika kituo hicho kilichopo maeneo ya Ubungo karibu na nyumba za Shirika la Nyumba nchini.

Kwa mujibu wa Kamanda Kova, mwanafunzi wa kwanza kukamatwa ni mtahiniwa wa kujitegemea Rhoda Juma Mombora (37) ambaye alikamatwa na majibu ya mtihani wa somo hilo uliofanywa juzi mchana. Mtuhumiwa wa pili, Clara Haule (20) mkazi wa Makumbusho alikamatwa akimfanyia mtihani Anjela Maganga mwenye namba P1475/0023.

Kova alisema watuhumiwa hao, wanashikiliwa na polisi na uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili. Idadi ya watuhumiwa inafikiriwa kuongezeka.

Japokuwa ni watahiniwa hao tu walionaswa, wanafunzi mbalimbali waliozungumza na Mwananchi katika maeneo mbalimbali nchini na jijini Dar es Salaam walidai kuwa wana mitihani yote na kwamba hata waliyofanya juzi walikuwa nayo. Walisema baada ya kuingia katika chumba cha mtihani walibaini kuwa ndiyo yenyewe.

"Mitihani yote tunayo hata ule wa jana (juzi) wa somo la Uraia (Civics), tulikuwa nao na baada ya kuingia katika chumba cha mtihani tulibaini kuwa ndiyo wenyewe, swali mpaka swali," alidai mwanafunzi mmoja wa jijini Dar es Salaam (jina tunalo).

Mwanafunzi huyo alidai kuwa walipata mitihani hiyo kutoka kwa watu walio karibu na Baraza baada ya kuchanga fedha na kuwapatia watu hao.

Mazingira ya kuvuja kwa mitihani hiyo yanaonyesha kuwa iliibwa kutokana na mpango wa ndani uliosukwa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu kwa lengo la kujipatia kipato.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo baada ya kupata mitihani wanafunzi hao wamekuwa wakitumia simu za mikononi kupeana maswali au majibu kabla ya kuingia katika chumba cha mitihani.

Katika hatua nyingine Umoja wa Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya juu nchini (Tahliso) umetaka mtihani wote wa kidato cha nne ufutwe na kisha Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe na watendaji wakuu wa Baraza kujiuzulu kutokana na kashfa hiyo ambayo mara ya mwisho ilitokea mwaka 1998.

Katibu Mkuu wa Tahliso, Mtatiro Julius alisema jana jijini kuwa, kashfa ya kuvuja kwa mitihani hiyo inawahusu viongozi hao moja kwa moja na hivyo hawapaswi kukwepa kuwajibika.

"Waziri anapaswa kuwajibika mwenyewe kwa kulinda heshima yake, lakini zaidi kwa manufaa ya umma kwani ameshindwa kuwasimamia vema watendaji wa chini yake," alisema Mtatiro na kuongeza:

"Kitendo cha mitihani kuvuja na serikali kuufuta mmoja na kuacha mingine iendelee kitazalisha wasomi wasiokuwa na uwezo,".

Kwa mujibu wa Mtatiro, inasikitisha kuona serikali inakiri kuvuja kwa mtihani wa Hisabati kwani kauli hii inaleta uwezekano wa mitihani yote kuwa imevuja kwa kuwa mitihani hiyo iliandaliwa pamoja na kusambazwa pamoja.

"Hali ya kuvuja kwa mitihani nchini imekuwa ya kawaida sana ingawa miaka mingine serikali inakanusha tuhuma hizo. Katika hili la mwaka huu, ni lazima Rais Jakaya Kikwete atumie nafasi yake kuwawajibisha watendaji wake," alisema.

Mtatiro alibainisha kuwa tatizo la kuvuja kwa mitihani nchini linatokana pamoja na mambo mengine tamaa ya fedha na walimu kutolipwa mishahara mizuri.

Aliitaja sababu nyingine ya kuvuja kwa mitihani kuwa ni ubinafsi na uzembe unaofanywa na baadhi ya watendaji wakuu katika kusimamia mitihani na upole wa Rais Kikwete katika kuwachukulia hatua watendaji wake wanaoboronga kazini.

"Upole wa Rais Kikwete ndiyo unaosababisha watendaji wa chini wajione kuwa wako huru na hakuna wa kuwawajibisha," alisema.

Juzi Baraza lilifuta mtihani wa Hisabati baada ya kubainika umevuja. Hata hivyo Baraza halikuwa tayari kutaja sehemu wala watu waliokamatwa na mtihani ambao sasa utatungwa mwingine na kufanywa Oktoba 27, mwaka huu.

Mwaka 1998, Baraza hilo lilifuta mitihani yote baada ya kubaini kuwa mingi ilivuja na hivyo kulazimika kusogeza mbele tarehe ya kuanza kwa mitihani na hali inaonekana inaweza kujirudia mwaka huu kutokana na mitihani hiyo kuzagaa kama njugu.

Awali Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania, Dk Joyce Ndalichako alisema baraza hilo limeanza kufanya uchunguzi wa uvujaji wa mitihani mingine nchi nzima baada ya kupata taarifa juu ya kuwepo kwa mitihani zaidi kwenye mikono ya watahiniwa ikiwemo Kingereza, Kiswahili, Fizikia na Uraia.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi kuhusu kuvuja kwa mitihani, Dk Ndalichako alisema vyombo vya usalama vimekamata mitihani ya Kiswahili, Kiingereza, Uraia, Fizikia pamoja na Historia na kwamba, uchunguzi zaidi unafanyika, lakini hakutaja sehemu ambazo mitihani hiyo ilikamatwa kwa kile alichoeleza kuhofia kuharibu uchunguzi unaoendelea.

Kashfa ya kuvuja kwa mitihani ni mwendelezo wa kashfa mbalimbali zinazoendelea kulikumba Baraza hilo baada ya hivi karibuni kuripotiwa kuibwa vyeti 4,000 vikiwa na namba bila ya majina.

SOURCE: Mwananchi

MBONA HII INATOKEA KILA MWAKA LABDA TATIZO KWA MITIHANI YA MWAKA HUU NI HIYO MEDIA ATTENTION.KUNA WATU WENYE JUKUMU LA KUHAKIKISHA MITIHANI HAIVUJI,NA WANALIPWA KWA KAZI HIYO LAKINI MWAKA HADI MWAKA MAMBO YANAENDELEA KUWA YALEYALE.NA SIJUI KWANINI HADI MUDA HUU UONGOZI WA NECTA HAUJAWAJIBIKA.ANYWAY,WANAJUA KWA UTAMADUNI WETU KUBORONGA SIO SABABU TOSHA YA KUJIUZULU MAJUKUMU WALIYOKABIDHIWA.


17 Sept 2008

Chama cha siasa huzaliwa,hukua na kinaweza kufa pengine hata kabla hakijakua.Tofauti nachama nchi ikishazaliwa ni lazima iishi milele,tena kwa gharama yoyote ile.Lakini kuna wenzetu wengine hawataki kuelewa ukweli huo.Kwao,chama cha siasa ni kila kitu hata kama kinaipeleka nchi ahera.Angalia mfano huu mwepesi: chama kinapewa dhamana ya kuongoza nchi,lakini kinaendesha mambo yake kihuni na kupeleka nchi mrama.Ni dhahiri kwamba chama cha aina hiyo kinaamsha vurugu ambazo zitalekea mmomonyoko wa amani katika nchi husika.Kwa bahati mbaya au makusudi,kuna wenzetu hawataki kuamini kwamba ni vigumu kujenga na kudumisha amani kuliko kuivunja.Sote tunawajibika kuhakikisha nchi yetu haipelekwi kusikofaa badala ya kunyoosheana vidole tunapotofautiana namna ya kuboresha ustawi wa Tanzania yetu.

Katika toleo la wiki hii la gazeti mahiri la Raia Mwema,pamoja na mkusanyiko wa habari na makala motomoto,kuna hababari kuhusu the man of the moment,Nape Nnauye.Kuna wanaodai kuwa huyu jamaa aanashupalia ishu za ufisadi ndani ya UVCCM kwa minajili ya kutafuta umaarufu utakaopelekea apate nafasi ya juu kwenye jumuiya hiyo.Sina uhakika kuhusu hilo lakini binafsi naamini kwamba hata kama malengo yake ya ni kupata umaarufu au uongozi,jitihada zake kuushikia bango ufisadi ndilo lililo muhimu zaidi kuliko motives zake.Na wanaokemea ufisadi,hata kama kwa njia zisizo sahihi,wanapaswa kuungwa mkono badala ya kunyanyaswa.Enewei,habari ya Nape ni hii HAPA na mambo mengine motomoto yanapatikana ndani ya gazeti hili la RAIA MWEMA.


15 Sept 2008

Some political analysts argue that ruling parties in Africa never lose elections,and if they do,which is rarely,it is likely not because they failed to deliver to the people who put the parties in power but rather either due to their internal conflicts or laxity.One could easily blame majority of opposition parties in Africa for their failures in organizing themselves in quest to remove ruling parties from power.But the fact is,in most African countries,the idea of an opposition party coming into power spells inexplicable uncertainty to the rulers,largely due to their "sins" during their terms of leadership.

In Tanzania,opposition parties have consistently cried foul during elections accusing the ruling party,CCM,of sabotaging them by either inciting conflicts in the parties or "bribing" their leaders to defect.CCM has also been accused of reluctance to reform the electoral system,which the opposition parties,see as unfair and biased.

I strongly believe that our nation's interest should come first,mainly because political parties may come and go but the nation should always remain intact,peacefully and flourishing.Had every Tanzanian looked beyond partisan politics,it is fair to conclude that those who criticize the ruling party for its perceived failure to deals with mafisadi (economic saboteurs),for instance,would not be considered as giving ammunitions to opposition parties but instead they would be given enormous support.

A while ago,I came across this story which in my view would stir trouble in Tanzania's opposition politics.
Mtikila atamka mazito kifo cha Wangwe

Na Waandishi Wetu 

WAKATI mazingira ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime marehemu Chacha Wangwe yakiendelea kuwa tete, Mwenyekiti wa Democratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila, ameibuka na kile alichodai, taarifa za mpango kamili hadi mauaji ya mwanasiasa huyo. 

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mchungaji Mtikila alidai mipango ya kumuua marehemu Wangwe ilianza kusukwa mkoani Dodoma na baadaye vikao vya kukamilisha mkakati huo, vilifanyika jijini Dar es Salaam wilayani Kinondoni. 

Aliongeza kuwa wahusika baada ya kukamilisha mpango huo na jinsi utakavyotekelezwa, walikwenda nchini Kenya kukodi watu wawili ambao alidai walilipwa sh. milioni 120 kama ujira wa 'kazi' hiyo. 

Mchungaji Mtikila alidai kuwa wauaji hao, ndio walioshirikiana na Bw.Deus Mallya ambaye anadaiwa wakati huo alikuwa amejenga uhusiano mzuri na marehemu Wangwe. 

Alidai siku ya tukio, marehemu Wangwe hakutaka kusafiri lakini alishinikizwa zaidi ya mara tatu na Bw. Mallya ambaye hadi sasa anashitakiwa kwa kosa la kusababisha ajali na kuendesha gari bila leseni.

"Baada ya kushinikizwa sana, marehemu Wangwe alikubali kuanza safari ambapo Bw. Mallya aliwasiliana na washirika wake ambao muda huo walikuwa eneo la tukio wakiwasubiri," alidai Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa; 

"Wakati huo ilikuwa bado mapema hivyo walimshauri apoteze muda japo wa nusu saa, ndipo alipozusha hitilafu ndani ya gari na kurudi gereji na baada ya muda huo kupita ndipo walianza safari kuelekea jijini Dar es Salaam." 

Huku akidai kuwa ana ushahidi wa tukio hilo na yupo tayari kutoa ushirikiano kwa Rais Jakaya Kikwete, Mchungaji Mtikila alizidi kueleza kuwa Bw. Mallya aliendelea kuwasiliana na washirika wake hadi walipofika eneo Pandambili, wilayani Kongwa na kusimamisha gari. 

"Baada ya kusimamisha gari, washirika wa Mallya walipanda na kumpulizia dawa ya usingizi usoni mara nne na hapo hapo alipoteza fahamu," alieleza Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa baada ya hapo ndipo alipigwa kwa kitu cha ncha kali kisogoni. 

"Kwa kuwa Mungu alimpenda sana hakukata roho, aliendelea kuhema ndipo alipopigwa na nyundo na kummalizia kabisa," alidai. Aliongeza kuwa baada ya kutimiza hilo waliweka jiwe kwenye kiongeza mwendo gari likaondoka kwa kasi na lilipindua ili kuonesha kuwa marehemu alikufa kwa ajali lakini muda huo Mallya alikuwa hayuko kwenye gari," 

Alidai kuwa kabla ya kupindua gari hilo, walimfunga marehemu mkanda na kumwibia sh. milioni tisa alizokuwa nazo pamoja na kompyuta yake ndogo 'Lap top' ambayo ilikuwa na nyaraka zake za siri. 

Alidai kuwa baada ya kufanikisha mauaji hayo, Bw. Mallya alitoa 'line' yake ya simu ambayo alikuwa akiitumia kuwasiliana na washirika wake na kuitupa. Alidai kuwa hadi anakamatwa simu yake haikuwa na 'line' yoyote. 

Kwa mujibu wa Mchungaji Mtikila mauaji hayo yalifanyika kati ya 1.30 hadi saa 2.00 usiku, muda mfupi baada ya kumaliza kuwasiliana na familia yake saa 1.27. 

Huku akijata majina ya watu wanaodaiwa kuhusika kwenye mpango huo, alieleza kuwa kipindi cha mchakato wa mpango wa kumuua, Bw. Wangwe, walikuwa wakisafiri kwenda nchini Kenya kusuka mpango huo. 

Mchungaji Mtikila alielekeza lawama zake kwa askari wote waliohusika na uchunguzi wa mauaji hayo kwa akidai kuwa hawakusema ukweli hivyo nao wanastahili kuunganishwa kwenye kesi hiyo. 

Kutokana na mazingira ya kifo cha marehemu Wangwe kugubikwa na maswali mengi, Mchungaji Mtikila amemuomba Rais Kikwete kuunda tume ya kuchunguza mazingira ya kifo chake kama alivyofanya kwa wafanyabiashara wa madini wa Mahenge, Morogoro ambao wanadaiwa kuuawa na Polisi. 

Alidai kwa wadhifa aliokuwa nao marehemu Wangwe katika jamii akiwa Mbunge wa Tarime, Rais ana nafasi ya kuunda tume. "Naupongeza uamuzi wake wa kuunda tume ya kuchunguza vifo vya wafanyabiashara lakini na kwa hili aunde tume na mimi nitakuwa tayari kutoa ushirikiano,"alisisitiza. 

Aliongeza kuwa kama Rais hatafanya hivyo, yeye ataleta wataalam wake kutoka nje kufanya uchunguzi kwani ameishafanya mazungumzo na ubalozi wa nchi moja ambao hakuutaja. 

Mchungaji Mtikila alidai kuwa atakwenda jimboni Tarime wakati huu wa kampeni ili kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu kifo cha marehemu Wangwe. Alisema amesimamisha mgombea kupitia chama chake, Bw. Benson Makanya, ili apate jukwaa la kueleza ukweli kuhusiana na kifo hicho. 

Marehemu Wangwe alikufa kwa ajali ya gari iliyotokea eneo la Pandambili mkoani Dodoma Julai 28 mwaka huu lakini tangu kifo chake, yameibuka maswali mengi huku baadhi ya watu wakidai kuwa aliuawa. 

Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na madaktari wawili kwa nyakati tofauti ulionesha kuwa hakupigwa risasi bali kifo chake kilisababishwa na ajali ya gari.

According to one local paper,the suspects are Freeman Mbowe,Dr Wilbroad Slaa and Tindu Lissu.This is how I look at the picture:If the accused trio decide to ignore Mtikila,it goes without saying that the public would buy the story,and it could bring their political careers to an abrupt end.Going to the court might be the only option left on their table,but Mtikila has a long history of winning charges brought against him in various courts.It should be all smiles in the ruling party's quarters as a Swahili saying goes "adui yako mwombee mabaya" (wish evil things to your enemy)

13 May 2008

Niliposikia mara ya kwanza nilidhani ni stori tu za mjini.Jana nimesikia tena,na safari hii ni kutoka kwa mwanafunzi aliyehitimu kidato cha sita hivi majuzi.Ishu yenyewe iko hivi:eti wanafunzi wa kidato cha sita waliletewa mashuleni fomu za kuomba udhamini wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.Hadi hapo hakuna tatizo,Bodi inawajali wanafunzi hai inawaletea fomu shuleni.Mgogoro unaanzia kwenye taratibu za kurejesha fomu hizo ambapo kila mwanafunzi alipaswa kulipia shs 10,000/= ambazo ni non-refundable.Mgogoro zaidi ni ukweli kwamba zoezi zima la kujaza na kurejesha fomu hizo lilifanyika hata kabla wanafunzi hao hawajafahamu matokeo yao.Kwa maana hiyo,mwenye kufaulu na kufanikiwa kupata admission ya chuo anakuwa amenufaika lakini kwa aliyepata maksi zisizomruhusu kuendelea na masomo ndio ameliwa.This is what we call daylight robbery.Kwanini wasingechukua hiyo elfu 10 baada ya matokeo ili wale wasio na sifa wasiliwe fedha zao bure?Deadline ya kurejesha fomu hizo ilikuwa tarehe 30/04 na matokeo ndio yametoka majuzi.Sipendi kuona mikopo ya wanafunzi inageuzwa kuwa kama bahati nasibu flani,or to be more precise,ujambazi wa mchana kweupe.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.