30 Oct 2008

IT SHOULD HAVE BEEN  SEN JOHN MCCAIN (R-AZ),AND NOT SEN JOHN MCCAIN (D-AZ) AS SEEN IN THE PHOTO ABOVE, IF YOU HAVENT NOTICED WHT'S WRONG.TRYING TO STEAL OBAMA'S LEAD IN THE POLLS?


Read it HERE

Bosi mmoja wa kampuni ya ujenzi aliamua kutumia nyenzo zake za kazi kulipiza kisasi kwa jamaa aliyempora mpenzi wake.Alipopata nafasi mwafaka ya kulipa kisasi akachukua greda/kijiko na kwenda kupondaponda gari ya "mwizi" wake (hiyo hapo pichani chini).BEWARE!

29 Oct 2008


BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) mkoa wa Dar es Salaam limewaonya maaskofu wa Jumuiya za Kikristo Tanzania (CCT) kutoitisha Serikali katika suala la kujiunga na Jumuiya ya Kiislamu (OIC) na kuanzisha Mahakama ya Kadhi nchini wakitishia kuwa kitendo hicho ni uhafidhina na ugaidi. 

Tamko hilo limetolewa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Mussa Salum kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, mara baada ya kikao cha masheikh na maimamu wa mkoa huo kujadili pamoja na mambo mengine, kauli ya maaskofu hao. 

"Waislamu tunasema suala la Tanzania kujiunga ama kutojiunga ni suala la Serikali ya Tanzania kwa maslahi ya wananchi wote," alisema Sheikh Salum. 

Sheikh Salum aliongeza kuwa suala la Mahakama ya Kadhi ni haki ya Waislamu wa nchini na wala halina mjadala kwa kuwa haliwahusu watu wa dini nyingine na kwamba mifano mingi ipo katika nchi mbalimbali juu ya kuwepo kwa mahakama hizo. 

"Mahakama hizi zilikuwepo tangu ukoloni, hivyo hili siyo suala la kuomba kuanzishwa kwake bali tunaiomba Serikali izirejeshe," alisema. 

Pia masheikh na maimamu hao walihoji uhalali wa kuwepo kwa Balozi wa Vatican hapa nchini kuwa anawakilisha nchi gani na kuliita kuwa suala hilo limegubikwa na udini lakini Waislamu hawakuwa wakihoji. 

"Tunawaonya maaskofu kuacha kuishinikiza Serikali mara kwa mara kuhusu masuala yanayohusu Waislamu na waache kupandikiza chuki kwa waumini wao juu ya suala la OIC na Mahakama ya Kadhi na waumini wa dini ya kiislamu kwa ujumla," alisema. 

Mwishoni mwa wiki iliyopita maaskofu 64 wa makanisa mbalimbali nchini walisaini waraka wa kumpinga Waziri Membe aliyekaririwa awali akiwataka Watanzania kutoogopa kujiunga na OIC kwani ni jumuiya yenye maslahi mazuri ya kiuchumi kwa taifa, akikariri utafiti uliofanywa na Serikali. 

Tayari BAKWATA makao makuu imeshatangaza kuitisha mkutano wa hadhara utakaofanyika kwenye viwanja vya Kidongo Chekundu kesho kueleza msimamo wake kuhusu suala hilo.

CHANZO: Majira

Na Mwandishi Maalum, Tabora
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete ametetea mila ya chagulaga kuwa haisababishi wasichana wengi kupata mimba kabla ya wakati, huku akionya dhidi ya vitendo vya viongozi kugeuza mila za watu kuwa adui, na kuziua kwa kisingizio cha kutatua matatizo.

Chagulaga ni kati ya mila za wenyeji wa mkoa wa Tabora ambayo huhusisha wasichana kujipanga ili kuwapa nafasi wavulana kuwaendea na kuchagua wachumba, lakini mamlaka za mjini hapa zimeichukulia kama moja ya njia zinazoongeza idadi ya wanafunzi wa kike kupata mimba wilayani Uyui.

“Haya ndiyo maisha ya watu hawa miaka yote" alisema Rais Kikwete wakati akipokea taarifa ya utendaji wa serikali wilayani Uyui iliyoonyesha kuwa wanafunzi wengi hupata mimba kabla ya wakati wao na hivyo kujikuta wakipoteza nafasi ya kuendelea mbele kimasomo.

"Tusije kugeuza mila za watu kuwa adui na tukaanza kuua mila hizo kwa kisingizio cha kujaribu kutafuta majawabu ya baadhi ya matatizo yanayotukabili,” Rais aliwaambia viongozi wa wilaya hiyo juzi asubuhi ikiwa ni siku ya tano ya ziara yake mkoani Tabora.

“Haya ndio maisha yao ya miaka yote? Hapa mjini watoto wa kike wa shule wanapata mimba na wala hakuna Chagulaga. Tusije tukageuza mila kuwa ndiyo adui. Inawezekana kuwa mila hiyo inawezesha tatizo hilo, lakini ngoma zimekuwepo miaka na miaka, na tatizo la mimba siyo la miaka mingi kiasi hicho.

“Sote hapa tumecheza ngoma, tena usiku. Ni ngoma tu za kawaida za makabila yetu. Na wale wanaowapa mimba watoto wa shule pengine hata kwenye ngoma hawaji. Inawezekana kabisa kuwa watu wanaowapa mimba watoto hawa ni mizee ambayo hata kwenye ngoma haendi. Na je si kweli kuwa sisi sote tumecheza dansi na disko, na si tulirudi nyumbani salama.”

Rais alisema kuwa ni kweli kwamba tatizo lipo laakini tulichambue zaidi ili kupata kiini chake cha msingi. Tusije tukaua mila za watu kwa visingizio tu. Hata kwetu kule tunayo mila ya kuchengula, na wala haina madhara ya kimaendeleo”.

Rais Kikwete, ambaye anatokea mkoa wa Pwani unaosifika kwa ngoma za sherehe, alisisitiza kuwa kwa jadi ya Waafrika kupata mimba nje ya ndoa ni aibu kubwa kwa familia yoyote na kwamba suala hilo halihusiani na mila yoyote.

"Na wala msije kukimbilia kupiga marufuku ngoma za watu, kwa sababu inawezekana kabisa ukasimamisha ngoma, lakini mimba zikaendelea. Kule Chunya (mkoa wa Mbeya) kuna mimba nyingi sana za watoto wa shule kuliko hata hapa, lakini hakuna Chagulaga,” alisema Rais Kikwete.

Awali, mkuu wa wilaya hiyo, Doreen Semali Kisamo alimwambia Rais Kikwete kuwa mila hiyo ya Chagulaga ni moja ya sababu ya mimba nyingi kwa watoto wa kike katika shule za sekondari wilayani humo.

Lakini alikuwa ameelezwa na viongozi wa wilaya hiyo awali kuwa moja ya sababu za kuwa na idadi kubwa ya wasichana wanaopata mimba ni mila za wakazi wa eneo hilo, hasa vijijini, ikiwamo ile ya Chagulaga.

Akiwa Tabora, Rais Kikwete alisimamisha kwa muda ziara yake Jumapili na kwenda Afrika Kusini kufungua kikao cha 10 cha Bunge la Afrika. Rais alirejea Dar es Salaam Jumatatu jioni na kurudi Tabora juzi asubuhi kuendelea na ziara yake.

Katika miaka miwili iliyopita, kiasi cha wanafunzi 44 wa kike wilayani humo walipata mimba.

Pia Rais Kikwete alishtushwa na ongezeko kubwa la watu wilayani humo na kutaka wahusika wa programu ya uzazi wa mpango, maarufu kama "Nyota ya Kijani" kuitupia macho wilaya hiyo.

Rais alielezwa kuwa ongezeko la watu katika wilaya hiyo kwa njia ya kuzaliana ni wastani wa asilimia 4.8 ikiwa ni kiwango cha juu sana ukilinganisha na cha taifa ambacho ni asilimia 2.8.

“Hizi ni takwimu si za kawaida. Ongezeko la asilimia 4.8 pengine ni kubwa kuliko katika eneo lolote nchini kwa sababu wastani wa taifa ni asilimia 2.8. Hii ni mara mbili ya wastani wa taifa,” alisema Kikwete.

Baada ya maelekezo hayo ya Rais, mzee mmoja kwenye mkutano huo alimweleza Rais Kikwete kuwa wakazi wa Uyui wanazaana sana kwa sababu “tunakula sana, na tunazaana sana, mkuu".

Lakini rais akasema: “Hili siyo jambo jema sana. It is striking (linastua). Wastani wa taifa ni asilimia 2.8. Nyota ya kijani lazima iangaze huku.”

Rais pia alionekana kushtushwa na idadi ya mauaji katika wilaya hiyo baada ya kutaarifiwa kuwa watu 34 wameauwa katika miezi sita iliyopita.

Kwa nini mauaji ni mengi mno kiasi hiki? Watu 34 katika miezi sita ni wengi sana katika wilaya moja. Wilaya nyingine zinakaa mwaka mzima bila hata kuuawa mtu yoyote.”

Jana asubuhi, Rais Kikwete alitembelea kijiji cha Kigwa ambako aliweka jiwe la msingi kwenye soko jipya la kijiji/mji hicho katika shughuli iliyohudhuriwa na mamia ya watu.

Akijibu maombi ya baadhi ya viongozi wa kijiji hicho kumtaka atoe maagizo ili kijiji hicho kiwe na hadhi ya kata, Rais Kikwete alisema:

“Kazi yangu si kugawa kata, na wala kata haigawanywi katikati ya kipindi cha uchaguzi. Kwa sababu tukigawa kata katikati ya kipindi cha uchaguzi ni lazima tufanye uchaguzi mpya wa madiwani. Hata hivyo, kugawa kata siyo tatizo, ili mradi tu mfuate taratibu za ugawaji kata.”

Katika kijiji cha mfano cha Milenia cha Mbola, tarafa ya Ilolangula, Rais alikagua miradi inayofanyika chini ya dhana hiyo mpya ya kuendeleza vijiji na kuzungumza na wananchi.

Rais aliwaambia mamia ya wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji hicho kuwa wakazi wa kijiji Milenia wanaokataa kuchangia magunia mawili ya mahindi kwa ajili ya chakula cha watoto wa shule wa kijiji hicho, wasipewe mbolea ya bure mpaka wametimiza masharti hayo.

“Nasikia baadhi yetu hamjachangia magunia mawili ya mahindi kutokana na mazao yenu kama yanavyosema masharti ya uzalishaji katika kijiji hiki. Sasa wale wanaokataa kuchangia kama ilivyokubaliwa, wanyimwe mbolea ya bure kuanzia sasa,” alisema.

Moja ya masharti ya misaada ya Milenia kwa kijiji hicho ni wakulima kupewa mbolea ya bure. Mradi huo unafadhiliwa na wafadhili mbali mbali.

Rais pia aliwaambia wakazi wa kijiji hicho kuthamini elimu kwa watoto wao. “Halitakuwa jambo linalowezekana kuwarithisha watoto wenu fimbo za kuchungia ng’ombe. Bila elimu watoto wenu watapata taabu sana katika miaka ijayo,” alisema.

Kijiji cha Ilolangula ndiko alikozaliwa mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba.

CHANZO: Mwananchi

Wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Dar es Salaam, wameamua kufunga mageti ya chuo hicho kuzuia uongozi wa chuo kuingia na kutoka baada ya Menejimenti kutotimiza ahadi ya kuongea nao, kutokana na mgogoro wa kufeli kwa wanafunzi wengi katika mitihani yao. 

Akipitisha azimio la kufunga mageti hayo, Rais wa Serikali ya Wanafunzi, Ali Mayay, aliwatangazia wanafunzi kuwa magari ya walimu yaliyoko ndani hayatatoka na yaliyoko nje hayataruhusiwa kuingia hadi uongozi wa chuo uzungumze na wanafunzi. 

Makamu Mkuu wa Chuo aliyetajwa kwa jina la A. Ahamed, ndiye aliyeahidi kukutana na wanafunzi hao saa nane mchana, lakini hakutokea hali iliyowakasirisha wanafunzi hao na kuanza kufanya fujo. Awali, wanafunzi hao ambao wamegoma kuingia madarasani, walidai kuwa kiini cha wanafunzi wengi kufelishwa ni mgogoro uliopo baina ya Mkuu wa Chuo na walimu wa CBE. 

Matokeo ya wanafunzi ambayo yametoka hivi karibuni yanaonyesha kuwa matokeo ni mabaya, hali iliyowashtua wanafunzi wanaotaka kupata maelezo kutoka kwa uongozi wa chuo hicho sababu ya wanafunzi kufeli kiasi hicho. Matokeo hayo ya mitihani yamekuwa mabaya kwa wanafunzi wa jioni waliofanya mitihani ya semista ya tatu pamoja na matokeo ya wanafunzi wanaosoma asubuhi ambao walifanya mitihani ya marudio. 

“Sisi tunaamini kuwa mgogoro uliopo baina ya Mkuu wa Chuo na walimu ndio chanzo cha wanafunzi kufelishwa kiasi hiki na sisi tangu Ijumaa tumeamua kutoingia madarasani hadi tupate maelezo kutoka kwa uongozi wa chuo,” alisema Makamu Rais wa Serikali ya Wanafunzi (Cobeso), Godrey Misso. Alisema hawaingii madarasani hadi watakapopata maelekezo kutoka kwa uongozi wa chuo. 

“Waliahidi kuongea na sisi jana (Jumatatu), lakini ikashindikana, wameahidi leo (jana) tunawasubiri,” alisema. Alisema haijawahi kutokea katika historia ya chuo hicho wanafunzi kufeli kiasi hicho. “Haiwezekani katika darasa la watu 400 wafaulu watu sita, ina maana wanafunzi wengine hawana akili?…hiki ndicho tunachopinga,” alisema. Baadhi ya walimu waliozungumza na gazeti hili, walikiri kuwa Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Wilclif Lugoe tangu ajiunge na chuo hicho miezi 10 iliyopita, amefanya marekebisho ya mfumo wa uendeshaji ambayo yanawaathiri walimu kimapato.

CHANZO: HabariLeo

Aberdeen,yesterday

Aberdeenshire

Stevenage,Hertfordshire

Coventry,yesterday.

28 Oct 2008








Picha zote kutoka Jamiiforums

27 Oct 2008


WASHINGTON — Federal agents have broken up a plot to assassinate Democratic presidential candidate Barack Obama and shoot or decapitate 102 black people in a Tennessee murder spree, the ATF said Monday.

In court records unsealed Monday, federal agents said they disrupted plans to rob a gun store and target a predominantly African-American high school by two neo-Nazi skinheads. Agents said the skinheads did not identify the school by name.

Jim Cavanaugh, special agent in charge of the Nashville field office for the Bureau of Alcohol, Tobacco, Firearms and Explosives, said the two men planned to shoot 88 black people and decapitate another 14. The numbers 88 and 14 are symbolic in the white supremacist community.

The men also sought to go on a national killing spree, with Obama as its final target, Cavanaugh told The Associated Press.

"They said that would be their last, final act _ that they would attempt to kill Sen. Obama," Cavanaugh said. "They didn't believe they would be able to do it, but that they would get killed trying."

SOURCE:Huffington Post

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.