3 Nov 2008

Obama's grandmother, Madelyn Dunham,RIGHT,and grandfather, Stanley Dunham.CLICK HERE  for more about her death.

Nyumbani kwa Obama kijijini Kogelo,Kenya.

Kwa mujibu wa ripota wa CNN aliyeko kijiji cha Kogelo huko Kenya,ambacho kinahusiana kwa karibu sana na asili ya Barack Obama,kuna kundi la viumbe-hai wanaoombea mgombea wa urais huyo asishinde kesho ili viumbe hao wasalimike.Hao ni ng'ombe ambao wanaandaliwa kwa ajili ya sherehe kubwa pindi Obama atapotangazwa mshindi.Ni dhahiri kwamba asiposhinda,ng'ombe hao nao watasalimika.Who would you  have felt more sorry for?

Wakati ng'ombe hao wakisubiri hatima yao,sangoma mmoja kijijini hapo ametabiri kuwa Obama atashinda uchaguzi huo wa kesho.Of course,sangoma huyo-John Radima-sio pundit wa major TV networks au pollster kutoka Gallup,lakini ameweza kukamata attention ya vyombo vya habari vya kimataifa.

Kwa upande wa grandmother wa Obama,yeye anasema hawezi ku-take things for granted hadi hapo mshindi atapotangazwa,na anafuatilia kwa karibu maendeleo ya mjukuu wake kwenye runinga inayotumia solar power kwa vile hakuna umeme katika makazi yake.Sarah Onyango Obama,wenye miaka 86,anasema kwamba katika soka huwezi kutabiri ushindi mpaka goli lipatikane.Wakati bibi Sarah (pichani chini) akisubiria kwa hamu matokeo ya kesho,upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kisumu umewafanya baadhi ya watu kutania kwamba huenda ni maandalizi ya ujio wa Air Force One ikiwa na Obama.



Kizitto Noya, Kilwa Masoko
WAKATI baadhi ya watu wakiamini kuwa serikali ilitumia busara kuhakikisha fedha zilizochotwa kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), zinarejeshwa kabla ya wezi kufikishwa mahakamani, katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad haamini kama fedha hizo zimerejeshwa.

Na badala yake waziri huyo kiongozi wa zamani wa Zanzibar anasema madai ya kurejeshwa kwa Sh69 bilioni kati ya Sh133 ni mwendelezo wa usanii wa chama na serikali yake.

Maalim Seif alisema hayo mwishoni wa wiki alipokuwa akihutubia maelfu ya wakazi wa Mkoa wa Lindi kwenye Uwanja wa Kilwa Masoko, baada ya kupokea maandamano ya CUF ya kupinga ufisadi na kushinikiza wezi hao wa fedha za EPA wafikishwe mahakamani.

Alisema hawezi kuamini kwamba mafisadi hao wamerudisha fedha mpaka aone kwamba wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili za kuiba Sh133bilioni.

"Mimi naamini kwamba, hakuna hata mtuhumiwa mmoja wa ufisadi wa EPA aliyerudisha fedha na kauli ya Rais (Jakaya) Kikwete ni mwendelezo wa usanii wa serikali ya CCM kuwalaghai Watanzania ili waamini kuwa kazi imefanyika," alisema.

Alisema yeye kama Watanzania wengine wenye akili timamu, hataamini kwamba kuna fedha iliyorudishwa na mafisadi wa EPA na kwamba atafanya hivyo ikiwa ataona mafisadi hao wanafunguliwa kesi mahakamani.

Kauli ya Maalim Seif ilifuatia maswali ya waandamanaji hao kumtaka aeleze msimamo wa CUF kuhusu ufisadi wa EPA na mazungumzo ya mwafaka baina ya chama chake na CCM.

Alisema CUF hairidhishwi na namna serikali inavyoshughulikia suala la EPA na ndio maana viongozi wake wakuu wanazunguka nchi nzima kufanya maandamano ya amani kupinga ufisadi huo na kuishinikiza serikali iwafikishe mahakamani.

Rais Kikwete alitaka wezi hao warejeshe fedha kabla ya Oktoba 31 na kwamba wale ambao watashindwa kuzirejesha, wafikishwe mahakamani ifikapo Novemba mosi.

Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi aliyoitoa Oktoba 31, Rais Kikwete alisema jumla ya Sh69 bilioni zimesharejeshwa na kwamba, ametoa ruhusa kwa watuhumiwa kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo, hadi jana Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), alikuwa bado hajawasimamisha watuhumiwa hao mahakamani.

Kuhusu mwafaka, Maalim Seif alisema CCM ilianza kutumia nguvu ya ulaghai katika suala hilo kwa kujifanya inataka kumaliza mgogoro wa mpasuko wa Zanzibar wakati ikijua kuwa haina nia hiyo.

Alisema: "CUF tumegundua ulaghai huo na sasa tumewaambia kwamba haturudi tena kwenye mikutano ya mwafaka. Tunataka kama wana nia njema na mwafaka, wasaini makubaliano yaliyofikiwa," alisema.

Alisema CUF pia imefunga mjadala na vikao vya mwafaka baina yake na CCM baada ya kuona kuwa wenzao wa CCM wanawarubuni na kuwahadaa.

Kuhusu nguvu ya utajiri wa kifisadi, Maalim Seif alisema CCM inatumia fedha nyingi kuwarubuni wananchi kwa zawadi ili waendelee kuiamini na kuwachagua, fedha ambazo baadaye wanazirudisha kwa wizi wa mali za umma na ufisadi.

"Pia CCM wanatumia ya nguvu dola kuwatisha wananchi na kuwapiga wananchi ili wasiwe huru kuwachagua vingozi wanaowapenda," alisema.

CHANZO: Mwananchi

PENGINE HOFU YA AINA HII INATOKANA NA UKWELI KWAMBA HAO WANAODAIWA KUREJESHA MABILIONI HAYO WAMEENDELEA KUWA ANONYMOUS.IWAPO MAJORITY YA WATOA SADAKA MAKANISANI NA ZAKA MISIKITINI (SUALA AMBALO NI LA HIARI NA SI LA KISHERIA HUJIWEKA WAZI) HOW COME THEN WADAIWA (SUALA LA KISHERIA) WAHIFADHIWE?NI SIMPLE LOGIC:KAMA MDAIWA NI ANONYMOUS,ITAPOELEZWA KUWA AMELIPA DENI NA KUENDELEA KUBAKIA ANYNYMOUS BASI LAZIMA KUTAKUWA NA STRONG SUSPICION KAMA DENI HILO LIMELIPWA KWELI.

MSIMU WA MVUA,BARABARA YA KWENDA KWETU IFAKARA NI MITHILI YA SWIMMING POOL YA MATOPE.SIJUI NA HII NAYO WAWEKEZAJI WATATAKA IBINAFSISHWE.HOFU YANGU WANAWEZA WAKAICHUKUA KISHA WAKAIGEUZA SHAMBA LA MPUNGA,SASA SIJUI AKINA SIE TUTAENDA HUKO KWA UNGO...

Kwa jinsi baadhi ya wawekezaji wetu huko nyumbani walivyo wasanii (inasemekana wengi wao huja na empty briefs case na vi-credit cards vyenye dola chache tu lakini huondoka na mamilioni ya dola) si ajabu mpango huu wa kubinafsisha baadhi ya barabara za jiji la Dar unaweza kutufikisha mahala tukakuta daraja la Salender limevunjwa na kugeuzwa kibangaluu cha mwekezaji flani!Sijui njia ya mkato itakuwa baharini au vipi!Nina wasiwasi zaidi na eneo la Victoria kwani kutokana na majimaji ya eneo lile si ajabu mwekezaji akaamua kufunga barabara na kuanzisha shamba la maua.Sounds like a joke,doesnt it?Lakini ukisoma habari hii hapa chini unaweza kupata picha kama hiyo inayonijia mie

Dar es Salaam city authority`s $3bn transport crisis rescue plan, which will involve private individuals funding the multibillion-project, has elicited strong resentment from the public. 

A cross-section of motorists and city residents interviewed on Friday said they were completely opposed to the idea terming it as misplaced. Any attempt to carry on with the plan would only show how things have gone awry for the government.

``No, it can`t be! It can�t just happen! That would be completely outrageous! It will be like selling off this country,`` a visibly surprised and thoroughly agitated Rajabu Hassan Mambo, a taxi driver at Mwenge in Dar es Salaam, said.

He was reacting to the recent mooted plan, which aims to revamp the city`s road transport network through private funding that will see individuals own public utility roads.

Mambo likened the idea to giving out one`s plot to a private developer, and then upon assuming residence on the same plot, you go on to pay rent for the rest of your life.

Overwhelmed by ceaseless traffic snarl-ups on most roads heading to, and from the city centre, city authorities have embarked on an expensive and overly ambitious Dar es Salaam Transport Policy and System Development Master Plan to remedy the situation by 2030. Under the arrangement, private individuals are invited to invest in the reconstruction of sections of some roads and widening of the main highways within the city.

According to the Dar es Salaam city mayor Adam Kimbisa, any prospective private investor will be apportioned a section of the road to finance its refurbishment, and then collect toll from motorists to recover expenses incurred.

Mayor Kimbisa justified the plan, stating that it has successfully been carried out in Malaysia`s capital city, Kuala Lumpur.

Several interviewed by The Guardian on Sunday said they were disappointed with the country`s leadership.

Jankar Mbungo for example faulted the government for remaining out of touch with real issues affecting Tanzanians.

``We, ordinary citizens, are burdened with taxes already. Prices of commodities are all time high, and instead of the government making policies that will solve the country`s problems it`s making life more difficult for us.`` Mr Mbungo stated.
SOURCE: Sunday Observer


(MY APOLOGIES FOR THE GRAPHIC IMAGE BUT I HOPE THIS SENDS A STRONG MESSAGE TO THOSE WHO WANT TO DRAG OUR COUNTRY INTO THIS SORT OF CRUELTY)
Mogadishu, Somalia - A 13-year-old girl who said she had been raped was stoned to death in Somalia after being accused of adultery by Islamic militants, a human-rights group said.
Dozens of men stoned Aisha Ibrahim Duhulow to death Oct. 27 in a stadium packed with 1,000 spectators in the southern port city of Kismayo, Amnesty International and Somali media reported, citing witnesses. The Islamic militia in charge of Kismayo had accused her of adultery after she reported that three men had raped her, the rights group said.

Initial local media reports said Duhulow was 23, but her father told Amnesty International she was 13. Some of the Somali journalists who first reported the killing later told Amnesty International that they had reported she was 23 based upon her physical appearance.

Calls to Somali government officials and the local administration in Kismayo rang unanswered Saturday.

"This child suffered a horrendous death at the behest of the armed opposition groups who currently control Kismayo," David Copeman, Amnesty International's Somalia campaigner, said in a statement Friday.

Somalia is among the world's most violent and impoverished countries. The nation of some 8 million people has not had a functioning government since warlords overthrew a dictator in 1991 then turned on each other.

A quarter of Somali children die before age 5; nearly every public institution has collapsed. Fighting is a daily occurrence, with violent deaths reported nearly every day.

SOURCE:AP

Mitambo ya Richmond ikiwasili kwa mbwembwe.Kampuni hiyo ya kitapeli imerithiwa na Dowans.Picha kwa hisani ya MICHUZI

Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd imetangaza rasmi zabuni ya kuuza mitambo yake ya kuzalisha umeme ikiwa ni miezi mitatu baada ya serikali kusitisha mkataba wake na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco). 

Dowans Tanzania Limited ilirithi mkataba wa kuiuzia umeme wa megawati 120 Tanesco kutoka kwa Kampuni ya Richmond Development LLC ambayo baadaye iligundulika kuwa ni kampuni hewa. Serikali ilifikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo Agosti mosi mwaka huu baada ya kuridhika kuwa mkataba huo haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria. 

Serikali pia ilisema ilibaini iwapo mkataba husika ungekuwa halali, uhamishaji wa mkataba kutoka RDVCO badala ya Richmond Development LLC kwenda Dowans Tanzania Ltd, haukufuata msingi wa mkataba.“Hivyo uhamishaji haukuwa halali na ifahamike kwamba mkataba ulikuwa baina ya Richmond Development Company LLC na Tanesco na siyo na REDVCO na Tanesco,” alisema. 

Tangazo ambalo limetolewa na kampuni hiyo leo kwa vyombo vya habari, limesema watu au kampuni makini ambazo zitakuwa na nia ya kununua mitambo hiyo wanakaribishwa kuinunua. Kutolewa kwa tangazo hilo la kuuza mitambo yake, huenda ikawa ni ishara ya kampuni hiyo kufungasha virago baada ya kimya kingi tangu mkataba huo usitishwe. 

Baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, Tanesco imekuwa ikitumia pamoja na vyanzo vingine vya umeme, mitambo yake ya megawati 100 iliyojengwa na Kampuni ya Watsilla ya Finland ili kufidia upungufu uliotokana na kuondoka Dowans. Tanesco pia imekuwa ikinunua umeme kutoka kwa kampuni za Songas na IPTL. 

Siku chache baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, mmoja wa maofisa wa Dowans aliiambia HabariLeo kuwa walikuwa na njia nyingi za kufanya na mitambo hiyo ikiwa kuikodisha au kuiuza kwa watu wengine. “Kukatishwa kwa mkataba haina maana hatuwezi endelea na kazi, tutatafuta wateja wengine kama kampuni za migodi na kuwauzia umeme au tunaweza kukodisha mitambo yenyewe,” alisema ofisa huyo. 

Kwa mujibu wa tangazo hilo, mitambo hiyo ina mashine tano za uzalishaji wa umeme ambazo mnunuzi atazinunua kwa bei ya hali yake ilivyo kwa wakati wa kununua. “Vifaa vyote ikiwa pamoja na vipuri na vifaa vingine vya pembeni vipo na vitauzwa kwa pamoja kama bidhaa moja,” lilisema tangazo hilo. 

Mkataba kati ya Tanesco na kampuni ya Richmond Development LLC umekuwa ni mmoja wa mikataba ambayo ilivuta hisia za watu wengi kitu ambacho kilisababisha kuundwa kwa Kamati iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), ambako kutokana na ripoti hiyo, aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa alijiuzulu. 

Wengine waliojiuzulu ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa Waziri wa Wizara hiyo na kabla ya kuhamishiwa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kutokana na mapendekezo ya ripoti hiyo, serikali iliahidi kuyafanyia kazi mapendekezo ya ripoti hiyo, ambapo moja ya hatua iliyochukuliwa ni kusitisha mkataba na Dowans.

 CHANZO : HabariLeo

I SMELL SOMETHING FISHY HERE.HII TENDA YA KUTANGAZWA KWA PRESS RELEASE INAZIDISHA SUSPICION YANGU.KWANINI ISIWE TANGAZO LA ZABUNI GAZETINI BADALA YA KU-SEEK ATTENTION KWENYE MAGAZETI,AMBAYO MENGI YAO HUWA HAYANA MUDA WA KU-READ BETWEEN LINES YANAPOPATA STORIES?I SUSPECT KUNA DILI INATAKA KUCHEZWA HAPA.POTENTIAL BUYER WA MITAMBO HIYO ATAKUWA TANESCO (CLICK HAPA NA HAPA KUPATA HINT). ITANUNULIWA KWA UTARATIBU UNAOONEKANA TRANSPARENT (HIVI TRANSPARENCY INA UMUHIMUWOWOTE  KATIKA KUNUNUA BIDHAA BOMU?) KISHA MITAMBO HIYO (AMBAYO "WAMBEA" WANADAI NI INJINI MBOVU ZA NDEGE) ITAISHIA "KUBUMA".DOWANS WAKATI HUO ISHAKUWA KAMPUNI MFU,KAMA MZAZI WAKE RICHMOND.LET'S WAIT AND SEE!

2 Nov 2008

Lewis Hamiliton made history,a few minutes ago,after becoming the first Black and the youngest  winner of Formula One Championship.And another history could be written day after tomorrow if Obama wins in the U.S. Presidential Election.Where is James Watson?

Pakistani police break up marriage between 4-year-old girl and 7-year-old boy

Mohammad Ismil (C) holds his 7-year old son Mohammad Waseem (R) and his son's 4-year old "bride" Nisha (L) at a police station in Karachi, Pakistan

Pakistani police raided a child marriage ceremony in the city of Karachi and arrested a cleric who was presiding over the wedding of a 4-year-old girl and a 7-year-old boy.

Pakistani law says people must be 18 to marry but some Islamic laws allow girls to marry after puberty.

Yet despite the laws, young girls are often given away in marriage to settle disputes or pay off debts.

Police said they raided a house on Thursday evening following complaints from residents, including a former district government official, who said the girl was being married off by her father for about 500,000 rupees (£3,750).

The official told Reuters: 'We had noticed some gatherings at this house for a couple of days.

'Last night I went there and saw that the little girl was actually getting married. So we called the police.'

Some other residents said the marriage was taking place to resolve a long-standing family dispute. Police said they had arrested the boy's father but the girl's father had run away.

SOURCE: Dailymail



Comedians flani wamemuingiza mkenge Gavana Sarah Palin kumuaminisha kuwa anaongea na Rais wa Ufaransa Nicholas Sarkozy.Sikiliza kichekesho hicho kwa ku-click link ifuatayo hapa chini:


Talking of Gov Palin,kituko kingine ni kwamba katika mkutano wake wa kampeni huko Polk City,Florida jina la mgombea mwenza wake,John McCain,was surprisingly missing kama inavyoonekana katika picha ifuatayo hapo chini.Au ndio ameshaanza kampeni za 2012?


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.