12 Nov 2008


Serikali imewataka wanafunzi wote wa vyuo vya elimu ya juu nchini kuingia madarasani mara moja ifikapo saa moja asubuhi leo. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Jumanne Maghembe alisema sera ya uchangiaji huduma za jamii ikiwamo elimu, halikwepeki katika mazingira haya ya kiuchumi. 

“Sera yoyote ile haiwezi kubadilishwa mara moja bila ya majadiliano ya kina yanahusisha wadau wote,” alisisitiza Profesa Maghembe, katika kujibu madai ya wanafunzi hao wanaopinga sera ya uchangiaji elimu ya juu hasa suala la mikopo wakitaka kulipwa asilimia 100. 

Waziri huyo wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi alisema matatizo yote ya kiutendaji katika utekelezaji wa sera ya elimu yatatafutiwa ufumbuzi. “Itaundwa kamati itakayowashirikisha wadau wote mkiwamo wanafunzi,” alisema Profesa Maghembe, ingawa hakufafanua hatua zitakazochukuliwa endapo wanafunzi watakataa kutii agizo hilo la kurejea madarasani leo. 

Akiahirisha Bunge mjini Dodoma Ijumaa iliyopita, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema hivi sasa serikali inabeba gharama za kuchangia elimu ya juu, na haitawezekana kutoa mikopo kwa asilimia 100. “Kwa hali ya kawaida, hii mikopo ilitakiwa ilipiwe riba kwa wanafunzi, lakini kwa sasa serikali inabeba mzigo huo. 

Hatuna uchaguzi mwingine, bali kuendelea kuchangia gharama za elimu ili wanafunzi wengi zaidi wapate elimu ya juu,” alisema Pinda bungeni na kuongeza: “Napenda nirudie kusema kwamba serikali wakati wote itakuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanafunzi wanapata kile wanachostahili kujiendeleza kielimu. 

Naomba nitamke kuwa wanafunzi wale wanaotaka wanafunzi wote kupewa mikopo asilimia 100 haiwezekani.” Awali, jana wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani wameendelea kusisitiza kuendelea na mgomo leo baada ya Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutotokea chuoni hapo. 

Akihutubia wanafunzi waliokusanyika kwa shauku katika Ukumbi wa Nkrumah kusubiri tamko la serikali, Rais wa Serikali ya Wanafunzi (DARUSO), Anthony Machibya alidai amepata taarifa kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mkurugenzi wa Elimu ya Juu, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu pamoja na wasaidizi wake waliitwa Ikulu na Rais kwenda kujadili matatizo yao. 

“Profesa Mukandala ameondoka kimya kimya na wasaidizi wake wameenda Ikulu kujadili mgomo wetu, nimepigiwa simu na Karani wake, kwa hiyo tusikate tamaa tuendelee na msimamo wetu mpaka tuone hatima yetu,” alisema Machibya na kuongeza kuwa mgomo utaendelea kama kawaida hawatarudi nyuma. Aidha, magari matatu yakiwa na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), yalikuwa yakirandaranda katika maeneo ya chuo hicho tangu juzi na jana kuhakikisha usalama wa mali na watu unakuwapo.

CHANZO: Habari Leo


VIONGOZI wa Nchi za Maziwa Makuu wamesema ipo haja ya kupeleka majeshi kwa ajili ya kurejesha amani eneo la Kivu lililopo Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambako kwa sasa hali ya usalama si shwari kutokana na mapigano yanayoendelea. 

Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe ambaye alisema uamuzi huo ulitolewa na viongozi wa nchi hizo na kuungwa mkono na wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika. 

Alisema hatua hiyo inatokana na hali ya siasa ilivyo Kaskazini Mashariki mwa DRC kuwa mbaya kufuatia mashambulizi yaliyoanzishwa na kundi la waasin wanaoongozwa na Bw. Laurent Nkunda. 

"Mashambulizi hayo yamesababisha athari kubwa kwa wananchi, kiasi cha watu wengi kukimbia makazi yao hivi karibuni. Pamoja na kuwepo makubaliano mengi ya awali, Laurent Nkunda na kundi lake bado hawaheshimu makubaliano hayo," alisema Bw.Membe. 

Alisisitiza kuwa kwa hali ilivyo sasa nchini DRC viongozi wa Umoja wa Afrika (AU) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja huo, Rais Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na viongozi wengine kadhaa wamekuwa wamekifanya mikutano ya dharura ili kuona jinsi gani wanaweza kumaliza mapigano yanayoendelea na kurejesha amani. 

Pia alisema maamuzi mengine yaliyotolewa na viongozi hao ni SADC kupeleka haraka wataalamu wa jeshi kusaidia kuangalia mipaka ya DRC na nchi jirani. 

Vile vile SADC iwe na ujumbe katika timu ya upatanishi iliyoanzishwa na wakuu wa nchi za Maziwa Makuu ambapo Rais Mstaafu wa Naijeria, Jenerali Olesegun Obassanjo na Rais Mstaafu wa Tanzania, Bw. Benjamin Mkapa wa Tanzania wamechaguliwa kuwa wajumbe wa timu hiyo. 

Alipoulizwa kuna tofauti gani kati ya Bw. Nkunda na aliyekuwa muasi wa Komoro, Kanali Mohamed Bakar, Bw. Membe alisema hawana tofauti kwa sababu wote ni waasi. 

"Hakuna tofauti kati ya hawa wawili kwani Kanali Bakari aliiasi Serikali yake Nkunda naye ni muasi ndio maana tunamtaka asitishe mapigano na tunakoelekea akiendelea kukaidi kuna hatari ya AU kupeleka majeshi ya kumdhibiti," aliongeza. 

Kuhusu hali ya kiasa nchini Zimbabwe, Bw.Membe alisema bado juhudi za kutafuta suluhu kuhusiana na muskabali wa nchi hiyo unaendelea.

CHANZO: Majira

NI WAKATI WA VITENDO ZAIDI KULIKO MANENO.

11 Nov 2008

The startling case of an AIDS patient who underwent a bone marrow transplant to treat leukemia is stirring new hope that gene-therapy strategies on the far edges of AIDS research might someday cure the disease.

The patient, a 42-year-old American living in Berlin, is still recovering from his leukemia therapy, but he appears to have won his battle with AIDS. Doctors have not been able to detect the virus in his blood for more than 600 days, despite his having ceased all conventional AIDS medication. Normally when a patient stops taking AIDS drugs, the virus stampedes through the body within weeks, or days.

"I was very surprised," said the doctor, Gero Hütter.

The breakthrough appears to be that Dr. Hütter, a soft-spoken hematologist who isn't an AIDS specialist, deliberately replaced the patient's bone marrow cells with those from a donor who has a naturally occurring genetic mutation that renders his cells immune to almost all strains of HIV, the virus that causes AIDS.

The development suggests a potential new therapeutic avenue and comes as the search for a cure has adopted new urgency. Many fear that current AIDS drugs aren't sustainable. Known as antiretrovirals, the medications prevent the virus from replicating but must be taken every day for life and are expensive for poor countries where the disease runs rampant. Last year, AIDS killed two million people; 2.7 million more contracted the virus, so treatment costs will keep ballooning.

While cautioning that the Berlin case could be a fluke, David Baltimore, who won a Nobel prize for his research on tumor viruses, deemed it "a very good sign" and a virtual "proof of principle" for gene-therapy approaches. Dr. Baltimore and his colleague, University of California at Los Angeles researcher Irvin Chen, have developed a gene therapy strategy against HIV that works in a similar way to the Berlin case. Drs. Baltimore and Chen have formed a private company to develop the therapy.

Back in 1996, when "cocktails" of antiretroviral drugs were proved effective, some researchers proposed that all cells harboring HIV might eventually die off, leading to eradication of HIV from the body -- in short, a cure. Those hopes foundered on the discovery that HIV, which integrates itself into a patient's own DNA, hides in so-called "sanctuary cells," where it lies dormant yet remains capable of reigniting an infection.

But that same year, researchers discovered that some gay men astonishingly remained uninfected despite engaging in very risky sex with as many as hundreds of partners. These men had inherited a mutation from both their parents that made them virtually immune to HIV.

The mutation prevents a molecule called CCR5 from appearing on the surface of cells. CCR5 acts as a kind of door for the virus. Since most HIV strains must bind to CCR5 to enter cells, the mutation bars the virus from entering. A new AIDS drug, Selzentry, made by Pfizer Inc., doesn't attack HIV itself but works by blocking CCR5.

About 1% of Europeans, and even more in northern Europe, inherit the CCR5 mutation from both parents. People of African, Asian and South American descent almost never carry it.

Dr. Hütter, 39, remembered this research when his American leukemia patient failed first-line chemotherapy in 2006. He was treating the patient at Berlin's Charité Medical University, the same institution where German physician Robert Koch performed some of his groundbreaking research on infectious diseases in the 19th century. Dr. Hütter scoured research on CCR5 and consulted with his superiors.

Finally, he recommended standard second-line treatment: a bone marrow transplant -- but from a donor who had inherited the CCR5 mutation from both parents. Bone marrow is where immune-system cells are generated, so transplanting mutant bone-marrow cells would render the patient immune to HIV into perpetuity, at least in theory.

There were a total of 80 compatible blood donors living in Germany. Luckily, on the 61st sample he tested, Dr. Hütter's colleague Daniel Nowak found one with the mutation from both parents.

To prepare for the transplant, Dr. Hütter first administered a standard regimen of powerful drugs and radiation to kill the patient's own bone marrow cells and many immune-system cells. This procedure, lethal to many cells that harbor HIV, may have helped the treatment succeed.

The transplant specialists ordered the patient to stop taking his AIDS drugs when they transfused the donor cells, because they feared the powerful drugs might undermine the cells' ability to survive in their new host. They planned to resume the drugs once HIV re-emerged in the blood.

But it never did. Nearly two years later, standard tests haven't detected virus in his blood, or in the brain and rectal tissues where it often hides.

The case was presented to scientists earlier this year at the Conference on Retroviruses and Opportunistic Infections. In September, the nonprofit Foundation for AIDS Research, or amFAR, convened a small scientific meeting on the case. Most researchers there believed some HIV still lurks in the patient but that it can't ignite a raging infection, most likely because its target cells are invulnerable mutants. The scientists agreed that the patient is "functionally cured."

Caveats are legion. If enough time passes, the extraordinarily protean HIV might evolve to overcome the mutant cells' invulnerability. Blocking CCR5 might have side effects: A study suggests that people with the mutation are more likely to die from West Nile virus. Most worrisome: The transplant treatment itself, given only to late-stage cancer patients, kills up to 30% of patients. While scientists are drawing up research protocols to try this approach on other leukemia and lymphoma patients, they know it will never be widely used to treat AIDS because of the mortality risk.

There is a potentially safer alternative: Re-engineering a patient's own cells through gene therapy. Due to some disastrous failures, gene therapy now "has a bad name," says Dr. Baltimore. In 1999, an 18-year-old patient died in a gene therapy trial. Even one of gene therapy's greatest successes -- curing children of the inherited "bubble boy" disease -- came at the high price of causing some patients to develop leukemia.

Gene therapy also faces daunting technical challenges. For example, the therapeutic genes are carried to cells by re-engineered viruses, and they must be made perfectly safe. Also, most gene therapy currently works by removing cells, genetically modifying them out of the body, then transfusing them back in -- a complicated procedure that would prove too expensive for the developing world. Dr. Baltimore and others are working on therapeutic viruses they could inject into a patient as easily as a flu vaccine. But, he says, "we're a long way from that."

Expecting that gene therapy will eventually play a major role in medicine, several research groups are testing different approaches for AIDS. At City of Hope cancer center in Duarte, Calif., John Rossi and colleagues actually use HIV itself, genetically engineered to be harmless, to deliver to patients' white blood cells three genes: one that inactivates CCR5 and two others that disable HIV. He has already completed the procedure on four patients and may perform it on another.

One big hurdle: doctors can't yet genetically modify all target cells. In theory, HIV would kill off the susceptible ones and, a victim of its own grim success, be left only with the genetically engineered cells that it can't infect. But so far that's just theory. All Dr. Rossi's patients remain on standard AIDS drugs, so it isn't yet known what would happen if they stopped taking them.

In 1989, Dr. Rossi had a case eerily similar to the one in Berlin. A 41-year-old patient with AIDS and lymphoma underwent radiation and drug therapy to ablate his bone marrow and received new cells from a donor. It is not known if those cells had the protective CCR5 mutation, because its relation to HIV hadn't been discovered yet. But after the transplant, HIV disappeared from the patient's blood. The patient died of his cancer 47 days after the procedure. Autopsy tests from eight organs and the tumor revealed no HIV.








Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Mohamed maarufu kama TID, amekata rufaa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kupinga adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja jela alichohukumiwa mwaka huu. 

Rufani hiyo ya msanii huyo ambaye tangu ahukumiwe kifungo hicho amekwishatumikia adhabu hiyo kwa miezi minne, itaanza kusikilizwa leo na Jaji Robert Makaramba; kwa mujibu wa habari zilizotolewa na ofisa mmoja wa mahakama hiyo. 

TID alihukumiwa kwenda jela mwaka mmoja kutokana na kutiwa hatiani kwa kosa la kushambulia na kumjeruhi kichwani na mkononi kijana aliyefahamika kwa jina la Ben Mashibe. Msanii huyo alimjeruhi Mashibe kichwani na mkononi kwa kutumia chombo cha kuwekea majivu ya sigara ‘ash tray’ na alisomewa mashtaka hayo mara ya kwanza Julai 10, mwaka huu mbele ya Hakimu Hamisa Kalombola wa Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni. 

Mwendesha Mashtaka wa kesi hiyo, Inspekta Nyagabona alidai TID alitenda kosa hilo Julai 2, mwaka jana saa sita na nusu usiku katika Hoteli ya Slipway iliyopo Msasani Dar es Salaam. TID mwenye umri wa miaka 26, alitiwa hatiani na Hakimu Kalombola baada ya hakimu huyo kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi wanne walioletwa mahakamani na upande wa mashitaka

10 Nov 2008

Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

MKURUGENZI wa kampuni ya Shivacom Tanzania, Bw. Tamir Sonaiya ametoa jumla ya sh. milioni 400 kwa Umoja wa Vijana ya CCM (UVCCM) kwa ajili ya kugharamia Mkutano Mkuu wa Umoja huo unaotarajiwa kufanyika kabla ya Desemba 15, mwaka huu. 

Kati ya fedha hizo sh. milioni 150 zitakuwa ni posho za wajumbe 1,000 wa mkutano huo ambapo kila mmoja atalipwa sh. 50,000 na kiasi cha milioni 250,000 zimetumika katika kutengenezea fulana, mikoba, kofia na bendera za chama kwa ajili ya mkutano huo. 

Fedha hizo zilikabidhiwa jana makao makuu ya CCM mjini hapa mbele ya Rais Jakaya Kikwete. 

Akikabidhi fedha hizo, Bw. Sonaiya alisema kuwa ameamua kujitolea kusaidia chama chake kwa kuwa yeye ni kada mwaminifu wa CCM na vifaa vyote alivyotoa vimetengenezwa kutoka katika kiwanda chake. 

Kwa upande wa Rais Kikwete alimpongeza Mkurugenzi huyo kwa kujitolea fedha hizo na kuwataka makada wengine wa CCM wenye uwezo kusaidia chama hasa kwa wakati huu wa kuelekea uchaguzi Mkuu ambapo fedha nyingi huhitajika ili kugharamia maandalizi ya mikutano hiyo. 

“Kinachosumbua sana kwenye mikutano ni namna ya kupata fedha za kuhudumia mikutano hiyo hivyo kwa hatua iliyofanywa na Umoja wa Vijana itasaidia kuondokana na tatizo la fedha lililokuwa likiwakabili katika maandalizi ya mkutano wao,” alisema Rais Kikwete. 

Fedha hizo zimepatikana kupitia uhamasishaji uliofanywa na kamati iliyoteuliwa na Baraza Kuu la Umoja huo kwa ajili ya kufanya maandalizi ya mkutano huo ikiwa chini ya Waziri wa Nishati na Madini, Bw. Willium Ngeleja, Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Laurence Masha na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Willium Lukuvi.

CHANZO: Majira













MVUTANO mkali uliibuka jana katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa NEC- CCM kuhusu mwenendo wa baadhi ya wabunge wa chama katika mambo mbalimbali yaliyolihusu taifa na chama hicho. Tanzania Daima Jumapili imedokezwa.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho vililieleza gazeti hili kuwa mvutano huo uliibuka baada ya baadhi ya wajumbe wa kikao hicho ambao si wabunge kuwashangaa wenzao ambao wamekuwa wakiibua hoja zenye mwelekeo wa kuishambulia serikali na wale wanaoendeleza hoja zenye mwelekeo wa kuchochea udini.

Habari hizo zilieleza kuwa wajumbe wa kikao ambao si wabunge walionyesha dhahiri kuchukizwa na hatua ya baadhi ya wajumbe ambao ni wabunge ya kuanza kuwachimba viongozi wa kitaifa wa chama hicho kwamba inahatarisha umoja wa chama hicho.

Sambamba na taarifa za kuwepo mjadala mkali kuhusu hoja hizo, taarifa nyingine zilizolifikia gazeti hili zilieleza kuwa wakakti Bunge likisubiri hatua zitakazochukuliwa na serikali dhidi ya gazeti lake la Habari Leo, baada ya kufichua njama za kundi dogo la wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kusuka zengwe la kumpinga hadharani Mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete, kuhusu hatua alizozichukua dhidi ya wezi wa EPA, chama hicho kimeanzisha uchunguzi wa kuwabaini wabunge waliodaiwa kuhusika katika mpango huo.

Vyanzo vya habari vya kuaminika kutoka ndani ya chama hicho, vimedokeza zaidi kuwa hatua hiyo ina nia ya kutaka kuthibitisha kilichoandikwa na gazeti hilo la serikali kama ni kweli au ni uongo na uchochezi, kama ilivyodaiwa juzi bungeni na Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka.

Sendeka, mmoja wa wabunge machachari ndani ya CCM, juzi akitumia kanuni ya Bunge namba 68, alieleza masikitiko yake kuhusu habari iliyoandikwa katika ukurasa wa kwanza wa gazeti la Habari Leo kuwa ilikuwa ya uchochezi na kuitaka serikali ichukue hatua kama ilizochukua kwa gazeti la MwanaHalisi, ambalo limefungiwa miezi mitatu, kwa madai ya kuchapisha habari ya uchochezi kuhusu kuwepo mpango wa kumng’oa madarakani Rais Kikwete, ifikapo mwaka 2010.

Habari iliyochapishwa na Habari Leo ilieleza kuwa kuna kundi la wabunge ambalo kwa makusudi lilikusudia kuwasilisha hoja hiyo bungeni, lakini mkakati huo ulizimwa na habari iliyochapishwa na gazeti hilo kabla ya kundi hilo kuwasilisha linachokiamini kuwa Rais Kikwete hajachukua hatua stahiki katika kulishughulikia suala la wezi wa EPA.

“CCM imeshitushwa na hoja hiyo kuletwa bungeni, kuomba serikali ichukue hatua dhidi ya gazeti la Habari Leo wakati taarifa hiyo inaelezwa na walioitoa kuwa ni kweli tupu. Sasa chama kimeamua kufanya uchuguzi ili kije na majina ya wabunge waliokuwa na mpango huo na mahala walipoendeshea vikao hivyo ili kuuthibitishia ulimwengu kwamba habari hiyo ni sahihi na kwamba kuna wabunge waliopanga kumdhalilisha rais,” kilisema chanzo chetu hicho cha habari.

Juzi Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Serikali ya Daily News na Habari Leo, Isaac Mruma, alikaririwa akieleza kuwa habari iliyoandikwa na gazeti analolisimamia ni sahihi na ya kweli.

“Kwanza napenda kusema kuwa tuna uhakika na tulichokiandika kuwa ni kweli, kwani chanzo chetu cha habari ni cha kuaminika,” alisema Mruma.

Alipoulizwa ni kwanini walichapisha habari hiyo upande mmoja bila kupata maelezo ya upande wa pili, yaani bungeni au kwa wabunge waliotuhumiwa, Mruma alisema taarifa hiyo waliipata usiku, hivyo walishindwa kuwatafuta wahusika, licha ya kwamba waliwajua kupitia chanzo chao cha habari.

Alisema kutokana na hali hiyo, waliamua kuyaondoa majina ya wabunge wote waliokuwa wakitajwa kuhusika katika mpango huo wa kumpinga Rais Kikwete, kuhusu namna alivyoeleza jinsi suala la EPA litakavyoshughulikiwa, wakati akilihutubia taifa hivi karibuni.

Mruma aliwataka wabunge kutambua kwamba gazeti la Habari Leo ni chombo cha serikali na lina dhamana ya kuchukua tahadhari kwa kuandika jambo lolote linaloonekana kwa namna moja ama nyingine kujaribu kuiyumbisha serikali au rais aliye madarakani.

Habari zaidi kutoka mjini hapa ambapo kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kinaendelea, zilieleza kuwa huenda suala la habari hiyo likaibua mjadala mzito katika kikao cha NEC kinachoendelea leo mjini hapa.

Akiwasilisha maelezo yake juzi bungeni, Sendeka alisema habari hiyo iliyokuwa na kichwa kisemacho ‘Kundi la wabunge CCM lasuka zengwe la EPA, ilikuwa na lengo la kuleta mtafaruku na uchochezi kati ya wabunge wa CCM na serikali.

Hoja ya Sendeka iliungwa mkono na Spika Samuel Sitta, ambaye alieleza kushangazwa kwake na habari hiyo kutoa maelekezo kwa serikali kufuatilia suala hilo na kupelekewa taarifa.

Kwa upande wake serikali, ilisema tayari ilishaanza kulishughulikia suala hilo kwa kuwahoji wahusika.

CHANZO: Tanzania Daima

9 Nov 2008


UTATA umegubika mchakato wa zabuni nyeti ya matengenezo ya mfumo wa usalama ndani ya Benki Kuu Tanzania (BoT), ambayo imetolewa kwa Kampuni ya Siemens ya Afrika Kusini.

Kuibuka kwa utata huo kumekuja wakati Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu akiwa katika mipango ya kuisafisha benki hiyo na tuhuma mbalimbali, ikiwemo ya ufisadi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Nyaraka ambazo gazeti hili inazo, zinaonyesha utata huo umeibuka kutokana na malalamiko kutoka kwa Kampuni ya ESS ya Afrika Kusini, ambayo haijaridhishwa na taratibu za mchakato zilivyofanyika.

Kwa mujibu wa nyaraka hizo, ESS inaonekana kulalamikia hatua ambayo imeita kuwa ni kuwepo mawasiliano kabla, kati ya watendaji wa Siemens na baadhi ya watu ndani ya Bodi ya Zabuni ya BoT.

Mawasiliano hayo yalinaswa katika barua pepe kati ya mwakilishi wa Simens nchini Julai 29,2008, akifahamisha viongozi wake kufanya mawasiliano na mtu mmoja muhimu ndani ya BoT.

Sehemu ya barua hiyo inasomeka, " Nimeweza kuzungumza na mtu mmoja wa kuaminika ndani ya BoT, na amesema zipo zabuni mbili tofauti, ila sisi tutapatiwa moja tu ya utengenezaji mfumo wa usalama."

Barua hiyo, iliandikwa Julai wakati mshindi wa zabuni alipatikana Oktoba 28, ambapo ESS kama mmoja wa washiriki, alifahamishwa.

Utata mwingine katika zabuni hiyo unatokana na kile kinachoelezwa kwamba, Siemens ilishiriki katika uwekaji mfumo huo katika ujenzi wa jengo la ghorofa 18 maarufu kama Twin Towers na lile la Gulioni Zanzibar, ambayo yanachunguzwa.

"Sasa ikitokea ukaguzi wa Twin Towers umeonyesha kulitumika mabilioni bila kuangalia Value for money (thamani ya pesa kwa kitu), itakuaje?" kilihoji chanzo kimoja.

Siemens katika mkataba huo wa miaka miwili iliomba zabuni kwa sh 3.4 bilioni, hata hivyo, makampuni mengine kwa mujibu wa nyaraka za BoT yako juu zaidi.

Hata hivyo, akizungumzia utata huo ofisini kwake jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, Gavana Ndulu, alisema hadi sasa ana imani kwamba, mchakato wa zabuni hiyo ulifuata taratibu husika.

Kwa mujibu wa Profesa Ndulu iwapo atabaini kuna tatizo lolote ikiwemo ukiukwaji wa mkataba huo hatasita kuisitisha.

Profesa Ndulu alisema dai la kwamba Siemens ilijenga Twin Towers ni kweli, lakini akabainisha kuwa hata kampuni nyingine ambayo ni pamoja na ESS na Group 5, pia zilishiriki katika ujenzi huo na pia ziliomba zabuni hiyo.

Profesa Ndulu alisema kabla ya kushirikisha kampuni hizo tatu ambazo zote zilishiriki katika uwekaji wa mfumo wa usalama kwa ngazi tofauti, ilibidi bodi itafute mwongozo kutoka Mamlaka ya Zabuni (PPRA), ambayo ilithibitisha hakuna tatizo.

Mwananchi Jumapili ilifanikiwa kuona nakala ya baraka za PPRA kwa BoT, ikieleza kuwa hakuna matatizo kwa makampuni hayo kushiriki ili mradi vigezo vizingatiwe.

"Najibu moja baada ya jingine, unanijua sifichi kitu na sipendi kupindisha mambo, kuhusu Siemens kushiriki katika Twin Towers, ni kweli, lakini hata ESS na Group 5 walishiriki kwa ngazi tofauti, Group 5 ndiyo wanaojenga jengo hilo, lakini pia wameshiriki," alisema Profesa Ndulu na kuongeza;

"Kama ni kigezo hicho, tusingeruhusu hata ESS na Group 5, kampuni hizi mbili na Siemens zote zimeshiriki katika Twin Towers, ndiyo maana kabla ya zabuni tukaenda PPRA kupata ufafanuzi, wakaruhusu," alisema.

Akifafanua kuwepo mawasiliano kati ya watu ndani ya bodi na Siemens, alisema hadi sasa hajaona tatizo kwani ni kweli zabuni zilikuwa mbili, lakini BoT ikaamua yenyewe kuchukua kazi moja ya kushughulikia uendeshaji wa mambo mbalimbali na kuacha hilo la ukaratabati mfumo wa usalama.

"Ni kweli, zabuni zilikuwa mbili, tulipoona wenyewe tunayo idara ya kuangalia mambo mbalimbali ikiwemo usafi na ununuzi wa vifaa, tukaamua tuipunguzie gharama kwa benki kwa kuipa zabuni kampuni moja, lakini pia si kwamba tunamwachia peke yake, wapo vijana wetu mahiri wanashirikiana nao," alifafanua.

Profesa Ndulu alisema hajaona tatizo katika hatua hiyo kwani zabuni ilitangazwa Juni na mawasiliano yamefanyika Julai, huo ni utaratibu wa kawaida kwa sababu kuna vitu ambavyo kampuni zote zinapaswa kuelezwa baada ya zabuni kufunguliwa.

"Sasa kusema kwamba zabuni ambayo itatolewa kwa ajili ya kugombaniwa ni ya usalama si uendeshaji, si tatizo ndicho tulichoeleza kwa kampuni zote," alifafanua.

Profesa Ndulu alisema ingawa haingii wala kuruhusiwa kuingilia mambo ya zabuni, lakini amekuwa akiuliza na kupatiwa taarifa za mara kwa mara kwa lengo la kuangalia utaratibu wa kutekelezwa kwa kuzingatia taratibu za kisheria.

"Mimi sitaki watu wapindishe mambo hata kidogo, nitasimamia sheria na kanuni, ndiyo maana huwa wakati mwingine nataka ufafanuzi wa mambo mbalimbali," alisisitiza Gavana Ndulu.

BoT katika kipindi cha kuanzia mwaka 2000 imekuwa na matatizo mbalimbali, ambayo hata hivyo, chini ya uongozi wa Profesa Ndulu amekuwa akijaribu kuisafisha na tuhuma hizo.

Baadhi ya mambo aliyoahidi kuyashughulikia ni kuchunguza mchakato wa ujenzi wa majengo pacha ya benki hiyo jijini Dar es Salaam na lililoko Zanzibar, kupitia ajira za watumishi wa BoT ambaye ametekeleza kwa kiasi kikubwa.

CHANZO: Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.