11 Apr 2009

MAELEZO YA PICHA KUTOKA KATIKA GAZETI LA HABARI LEO YANASOMEKA:

Behewa la mafuta la TRL liliacha njia eneo la Kurasini, Dar es Salaam na kuanguka.Wafanyakazi wa kampuni hiyo walikutwa wakikinga mafuta hayo ili kuyahifadhi katika mapipa chini ya ulinzi mkali wa polisi. (Picha na Yusuf Badi).
NADHANI MWENZANGU PIA UKIANGALIA PICHA HIYO KWA MAKINI UTABAKI UNAJIULIZA KWAMBA HAO WAHINDI WA TRL NI WAWEKEZAJI KWELI AU VIINIMACHO?TALKING OF VIINIMACHO,YAYUMKINIKA KUJIULIZA IWAPO HAWA JAMAA HAWAJAWAROGA HAO WANAONG'ANG'ANIA KUENDELEZA MKATABA WA KIMAZINGAOMBWE NA TRL.KAMA ILIVYO DESTURI YETU YA ZIMAMOTO,TUNASUBIRI WALIKOROGE KWANZA,KISHA WAINGIE MITINI HALAFU KUNYWA TULINYWE SIE!NA HAPA NENO "KULIKOROGA" LINAMAANISHA KU-MESS UP NA MAISHA YA ABIRIA WANAOTEGEMEA USAFIRI WA RELI YA KATI.

ASEMA WACHACHE WALIOTHUBUTU WAACHIWE WAPIGE VITA UFISADI

Salim Said


MBUNGE wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela amesema viongozi wa chama tawala (CCM) wanaogopa kupambana na ufisadi kwa kuwa wanaopambana nao ni viongozi au wabunge wenzao na hivyo kutaka wale wachache waliothubutu kuendeleza vita hiyo waachiwe.

Mama huyo, ambaye amekuwa mmoja wa watu wenye uwezo wa kujenga hoja bungeni wakati wa kuzungumzia ufisadi, alisema anashangaa jinsi viongozi wanavyoshindwa kupambana na ufisadi kama unavyoelezwa kwenye sura ya nane ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM inayozungumzia vita dhidi ya uovu huo.

Bila ya kutoa mifano bayana, mama huyo amesema ni wabunge wachache wanaoweza kusimama kidete kutetea kipengele hicho, akiwemo yeye; na kwamba kama vita ya ufisadi itafanyiwa kazi ipasavyo, nchi yote itakuwa na utulivu na amani, vitu ambavyo alisema vinahitajiwa na kila Mtanzania.

Akizungumza katika kipindi cha Tuongee Asubuhi kinachorushwa hewani na kituo cha televisheni cha Star Tv, Kilango alisema ugumu wa kipengele hicho ni kwamba, wanapambana na wabunge, viongozi na wanachama wenzao wa CCM.

"Ugumu wa sura ya nane ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ni kwamba unapambana na mwanachama mwenzako, mbunge na hata kiongozi mwenzako. Na hii ndio inawafanya watu wengi kushindwa, isipokuwa wachache kama mimi ambao tumethubutu," alisema Kilango.

"Unaposimama imara kutaka kufanya mabadiliko, kutetea haki na kupinga ubatili, unapaswa kutegemea mengi na mimi niliyategemea na ndio maana sipati tabu katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi."

Kilango alisema viongozi na wananchi wa Tanzania wanapaswa kuwa wa kweli na wawazi katika kupinga rushwa kama wanavyofanya watu wa Marekani.

"Nchini Marekani mtu aliyetaka kurithi nafasi ya useneta wa Obama alitanguliza rushwa ili kuwashawishi wajumbe, jambo ambalo liliwafanya Wamarekani kusimama imara na kuzungumza ukweli kuhusu kashfa hiyo," alisema.

Kilango, ambaye alipata tuzo ya 'Mwanamke Jasiri' aliyopewa na serikali ya Marekani hivi karibuni, alisema jamii inapaswa kuwaunga mkono kwa nguvu zote wachache waliothubutu kuikemea rushwa nchini.

"Kuna watu wachache ambao walijiona wana haki ya kula mali za umma, lazima tuwanyoshee vidole na jamii ituunge mkono katika hili," alisema Kilango.

"Tunawaomba wengi wasiothubutu kusema, watuachie tulioweza... wasitubughudhi, wasitunyamazishe na wala wasiwe na nia ya kutaka kutumaliza kwa kuwa hawatafanikiwa kamwe. Sisi tutaendelea hadi awamu ijayo."

Katika kashfa nyingi za ufisadi, viongozi na wabunge wa CCM ndio wamekuwa wakituhumiwa kuhusika na miongoni mwa waliofikishwa mahakamani ni viongozi wa zamani katika serikali ya CCM, huku moto dhidi ya wabunge wa sasa ukizidi kuwaka katika kashfa za miradi mikubwa.

Miongoni mwa miradi hiyo ni ununuzi wa rada, ambao umeelezwa kuwa ulifanywa kwa kuongeza bei ili iwe juu kwa lengo la kujipatia kamisheni nzuri, mradi wa uzalishaji umeme wa dharura uliosababisha mawaziri kujiuzulu baada ya kutajwa kwenye ripoti ya kamati teule ya bunge na mradi wa uzalishaji umeme kwa kutumia makaa ya mawe wa Kiwira.

Pia kashfa nyingine iliyohusisha wanachama na viongozi wa CCM ni wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), kashfa ambayo inahusisha majina vigogo wanaohusishwa na kampuni zilizochota fedha nyingi lakini imekuwa ni vigumu kuwataja.

Kashfa hizo zimekuwa zikisababisha malumbano baina ya wanachama wa CCM.

Lakini Kilango hakutaja majina ya watu wanaojaribu kuwazuia au kuwamaliza, bali aliapa kuendelea na vita hiyo kwa kuwa hayo ni maumbile yake.

"Mimi ndivyo nilivyozaliwa na ni maumbile yangu kuzungumza ukweli. Rangi nyekundu nitaisema kuwa ni nyekundu na bluu pia, wala hakuna mtu atakayeweza kuninyamazisha ili niseme kuwa ni nyeupe, kibaiolojia siku zote naweza," alisema na kuongeza:

"Wapo wapole, waoga ambao hata chumbani kulala peke yao wanaogopa, lakini pia wako majasiri wanaothubutu."

Alisema Watanzania walishachoshwa na rushwa na walifikia hatua ya kujenga imani kuwa wabunge wa CCM wapo kwa ajili ya kuilinda serikali yao na wanaoweza kuikosoa ni wabunge wa upinzani tu.

"Sasa wananchi wa Tanzania wanapaswa kuondoa imani hiyo na sisi tupo kwa ajili ya wananchi na msimamo wangu mimi chama hakiwezi kupendwa kama hakikosolewi. Tukikosoa ndio tunakipa afya na si kukidhoofisha kama wanavyodhani baadhi ya watu," alisema.

Alifafanua kuwa, vita dhidi ya rushwa ni kama mashindano ya riadha kwani kuna wanaoanza, wanaoshindwa katikati, wanaomaliza na pia kuna wasiothubutu kuanza.

Kilango alikataa kuwataja wale wanaompiga vita, lakini alisema anaposimama bungeni kuzungumza anafahamu kuwa anazungumza na dunia, hivyo hategemei kupigiwa makofi na wote au kapingwa na wote.

"Wanaopiga makofi nafurahi, pia kuna wale ninaogusa masilahi yao waache wachukie. Lakini mimi nimeamua kuwa kiongozi, hivyo sitishwi na sitatingishwa na watu wenye mitazamo tofauti na mimi. Dhamira yangu ya kuwatumikia Watanzania ipo palepale," alisisitiza
Kilango.

CHANZO: Mwananchi

BRAVO MHESHIMIWA KILANGO,IT'S HIGH TIME SOMEONE CALLS A SPADE A SPADE.WHEN YOU MAKE ENEMIES,THAT MEANS YOU'VE STOOD UP FOR SOMETHING YOU BELIEVE IN.IT IS IN PEOPLE LIKE YOU,MHESHIMIWA KILANGO,THAT MANY OF WAZALENDO AND WALALAHOI FIND A GLIME OF HOPE FOR TANZANIA.SILENCE IS NOT AN OPTION AS IT MIGHT BE TRANSLATED BY MAFISADI AS INSTITUTIONALISING THEIR SABOTAGE OF OUR ECONOMY AND PLUNDER OF WHATEVER IS LEFT OF OUR NATURAL RESOURCES.

10 Apr 2009

NAOMBA USOME HABARI IFUATAYO KISHA TUSHIRIKIANE KUFANYA TAFAKURI KATIKA MASWALI YANAYOJITOKEZA (katika maneno yenye rangi nyekundu).
Na Salim Said

KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa imekikataa kwa mara ya pili kitabu cha hesabu za mapato na matumizi ya Halmashauri ya Wilaya ya Monduli, mkoani Arusha baada ya kubaini mapungufu, ikiwa ni pamoja na udanganyifu.

Kamati hiyo pia imewapa adhabu ya kukatwa asilimia 15 ya mishahara ya watendaji sita wa halmashauri hiyo kwa kosa la kuidanganya kamati hiyo ilipowatembelea Januari mwaka huu.

Kamati hiyo ilianza kupitia taarifa za mapato na matumizi ya serikali za mitaa kuanzia Jumatatu wiki hii na imeshapitia hesabu za halmashauri za mkoa wa Dodoma na jana ilipitia halmashauri za mkoa wa Arusha.

Awali kabla ya kukataliwa kwa kitabu hicho, mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Cyprian Oyier alionekana kushindwa kutoa maelezo ya kutosha kwa wabunge kuhusu makosa waliyofanya na mapungufu yaliyojitokeza katika kitabu chao.

Oyier alikiri mbele ya wajumbe wa kamati hiyo na wageni waalikwa kuwa waliidanganya kamati ilipoenda kuwatembelea wilayani kwao kwa kuwaeleza kuwa halmashauri ilijenga nyumba ya walimu kwa Sh30 milioni, jambo ambalo halikuwa la kweli.

Nyumba hiyo iliyogharimu zaidi ya Sh 30 milioni ilibainika kuwa imejengwa na Shirika la Hifadhi ya Taifa (Tanapa) na wao kukabidhiwa funguo tu baada ya wajumbe kufanya ziara shuleni hapo.

Baada ya kukitaa kitabu hicho, wakuu wa halmashauri hiyo na waandishi, walitakiwa kutoka nje kwa muda, ili kuwapa nafasi wabunge kupanga adhabu. Baada ya dakika 20, kaimu mwenyekiti wa kamati hiyo, Samuel Chitalilo alisema kuidanganya kamati ni kosa la jinai, lakini kamati imewaonea huruma.

Alisema wangeweza kuwataka kurudi tena mbele ya kamati, lakini wanawasamehe kwa kuwakata asilimia 15 mishahara yao ya mwezi wa tano mwaka huu. “Tunawarudisha mkaandae tena kitabu chenu... hiki tunakikataa kwa mara ya pili. Angalieni wenzenu wa Same walivyoandaa vizuri ili mkija tena tusije kukikataa tena,” alisema Chitalilo na kuongeza:

Mmeidanganya kamati na mmekiri kosa, hili ni kosa la jinai, lakini kamati imewaonea huruma kwa kuwapa adhabu ya kujifunza na ili iwe fundisho kwa wengine”.

“Mkurugenzi wa halmashauri, mhandisi, ofisa mipango, mkaguzi wa ndani, mweka hazina na ofisa elimu aliyekuwapo wakati huo tutawakata asilimia 15 ya mishahara yenu ya Mei.”

Naye mbunge wa Kinondoni na mjumbe wa kamati hiyo, Idd Azzan alisema halmashauri hiyo ilitoa taarifa za uongo kwa kamati na kwamba walipokwenda kuitembelea shule hiyo walipewa taarifa tofauti kutoka kwa mkuu wa shule hiyo.

Alifafanua kwamba wanatoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwa halmashauri zinazotoa taarifa za uongo. “Adhabu hii tunataka iwe fundisho kwa wengine, kwa kuwa fedha za serikali hazitumiki ipasavyo katika ngazi za halmashauri, zinatumika kwa safari na posho za viongozi jambo ambalo ni kinyume na malengo ya fedha hizo,” alisema Azzan.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo alikataa kuzungumza na Mwananchi baada ya kupewa adhabu hiyo, huku mwenyekiti wa halmashauri hiyo, David Pelo akisema kuwa hiyo ni bahati mbaya na hakuna aliyekusudia kutoa taarifa za uongo.

“Tutajitahidi kufuata maelekezo yenu, tunawashukuru kwa kutoturudisha tena katika kamati kwa kuwa fedha za halmashauri zingetumika pia kwa usafiri,” alisema Pelo.

Haya ni ya kawaida na yanaweza kutokea kwa halmashauri yoyote, pia tutarudia kuandika kitabu kama tulivyoelekezwa na tutaenda kwa wenzetu wa Same kwa kuwa wao wamefanya vizuri.”

Kamati mbalimbali za bunge zinaendelea na vikao vyake kwenye ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam kuanzia Jumatatu wiki hii.

CHANZO: Mwananchi

TAFAKURI:

KITABU CHA MAHESABU KILIPOKUTWA NA MAKOSA MARA YA KWANZA,WAHESHIMIWA WABUNGE WAKAAMUA KUKITAA ILI KIFANYIWE MAREKEBISHO.KILIPOLETWA MARA YA PILI,WAHUSIKA WAKAAMUA LIWALO NA LIWE,WAKAKIRI KUWA WALIDANGANYA.HIVI TUJIULIZE,WAHESHIMIWA WABUNGE WALIPOTAKA MAREKEBISHO HAWAKUWA WANAKARIBISHA USANII KUTOKA KWA WATENDAJI HAO WA HALMASHAURI?HAIHITAJI ELIMU YOYOTE KUTAMBUA KWAMBA MAHESABU YA TAASISI YA UMMA YANAPOKUWA NA KASORO INAASHIRIA UFISADI WA NAMNA FLANI,HIVYO KUWATAKA WAHUSIKA WAREKEBISHE NI MITHILI YA KUWAPA MUDA WA KUFUNIKA UFISADI HUO.

JAPO NAAFIKIANA NA MANTIKI YA KUWAADHIBU WATENDAJI WASIOTEKELEZA MAJUKUMU YAO IPASAVYO,NAPATWA NA WASIWASI NA NAMNA KAMATI HIYO YA BUNGE ILIVYOJIPA MAJUKUMU YA MAHAKAMA NA KUAMUA KUKATA ASILIMIA 15 YA MISHAHARA YA WATENDAJI HUSIKA.HUU NI UKIUKWAJI WA UTAWALA WA SHERIA KWA VILE KAMA ILIBAINIKA KUWAPO KWA UBADHIRIFU WA FEDHA ZA UMAA,MAHALA MWAFAKA PA KUSHUGULIKIA SUALA HILO NI POLISI NA MAHAKAMA.

NA JINGINE LA KUJIULIZA NI NAMNA MAKATO HAYO YATAVYOWEZA KUFIDIA FEDHA ZILIZOIBIWA NA USIMAMIZI WA KUHAKIKISHA KUWA MAKATO HAYO HAYAISHII MFUKONI MWA MAFISADI WENGINE.

MHESHIMIWA CHITALILO (rejea HAPA na HAPA) ANATAMKA BAYANA KWAMBA WATENDAJI HAO WAMETENDA KOSA LA JINAI,LAKINI CHA KUSHANGAZA ANADAI ETI KAMATI IMEWASAMEHE NA BADALA YAKE KUWAAMURU WAKWATWE ASILIMIA HIZO 15 ZA MISHAHARA YAO.HIVI INGEKUWA NI FEDHA ZAKE BINAFSI NDIO ZIMEIBIWA ANGEWEZA KUTOA MAAMUZI YA KUSTAAJABISHA NAMNA HIYO?

HIVI KWA UTARATIBU HUU WA KULEA UZEMBE,UBADHIRIFU,UJAMBAZI NA UFISADI KUNA UWEZEKANO WOWOTE WA KUFIKIA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA?

TUTAFAKARI!


BLOGU HII INAKUTAKIA WEWE MSOMAJI MPENDWA IJUMAA KUU NJEMA.KAMA AMBAVYO BWANA WETU YESU KRISTO ALIVYOWEZA KUVUMILIA MATESO NA HATIMAYE KIFO MSALABANI ILI KUTOKOMBOA SISI WANADAMU,KILA MMOJA WETU KATIKA NAFASI YAKE ANAWEZA KUJINYIMA KUWASAIDIA WALE WANAOHITAJI MSAADA WETU KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE.

My Lord,
your son has suffered so much, shed so much blood.
I was born with so many faults
and my nature is so full of weakness,
and yet your son Jesus has died on the cross.
For me.
I know your grace has the power
to cleanse me of my many sins
and to make me more like your Son.
Thank you for your goodness and love for me.
I ask you, Father, to watch over me - always.

May the Lord bless us,
protect us from all evil
and bring us to everlasting life.
Amen.



9 Apr 2009

Twelve men have been arrested during a major anti-terror operation which was triggered by a top police officer's security blunder. Skip related content

Eight addresses in Liverpool, Lancashire and Greater Manchester were raided by counter-terrorism police in connection with a suspected al-Qaeda plot.

One man was held at Liverpool John Moores University while four others were arrested in the Toxteth and Wavertree areas of the city during the operation by officers from the North West Counter-Terrorism Unit, Merseyside Police, Greater Manchester Police and Lancashire Constabulary.

In Greater Manchester, two men were held at an internet cafe in Cheetham Hill Road and two others were arrested at an address in Galsworthy Road while another man was detained on the M602.

In Clitheroe, Lancashire, two security guards were reportedly arrested at a Homebase store.

It has emerged that the raids had to be brought forward after Metropolitan Police Assistant Commissioner Bob Quick was earlier photographed walking into 19 Downing Street carrying sensitive documents, some of which could be read.

One of the papers, which was clearly marked "secret", is said to have carried an outline briefing of an ongoing counter-terrorism operation and reportedly included the names of several senior officers, locations and details about the nature of the threat.

Mr Quick, the UK's most senior anti-terror officer, had been due to meet Prime Minister Gordon Brown and Home Secretary Jacqui Smith. He has apologised to Metropolitan Police Commissioner Sir Paul Stephenson, saying he "deeply regretted" the incident.

At the Liverpool university, terrified students were held inside the main library on Maryland Street for up to 30 minutes as two Asian men in their mid to late 20s were searched by police.

Craig Ahmed, 24, a business student from Maghull, Merseyside, said: "Suddenly there was all shouting and commotion outside so I went to the window and saw about eight police officers.

"One of them was armed and was pointing his gun at two men who were ordered to lie face down on the ground. For about half an hour they held the men on the floor. The police were shouting things at them but I couldn't hear what was being said."

Elsewhere, there were multiple arrests as armed police raided an internet cafe and other addresses in Cheetham Hill in Manchester.

Police also sealed off a terrace of properties in Earle Road in the Wavertree area of Liverpool while arrests were made at a Homebase store in Clitheroe, Lancashire.

Meanwhile, Whitehall officials are said to be furious about the security breach.

But it is not the first time Mr Quick, who returned to the Met last year from Surrey where he was chief constable, has become embroiled in controversy. Last December he apologised for an outburst in which he accused senior Conservatives of leaking a story about his wife's business interests.

Mr Quick faced unwanted newspaper headlines after it emerged his wife Judith was running a luxury car hire firm from their home and details of their address were published on a website.

The stories followed hot on the heels of his involvement in overseeing the arrest of shadow immigration minister Damian Green as part of a Whitehall leak inquiry.

Speaking at his home, Mr Quick told a reporter his wife and children were forced to move out because of security concerns sparked by the public furore. The comments were an unusual response from a man who regularly meets members of the global intelligence community and whose role thrives on discretion.
SOURCE: ITN



CAUTION:CONTAINS EXPLICIT MATERIAL)

7 Apr 2009


Development Entrepreneurship for Community Initiative (Deci) Tanzania, which is operating a pyramid scheme, has no bank account, investigations have established.

Meanwhile, BoT and other regulatory agencies came under the spotlight yesterday, with some Deci members and other stakeholders querying why it had taken them "so long" to establish irregularities in Deci's operations.

A source in the team that investigated Deci's operations told The Citizen yesterday that tens of millions of shillings collected from members were actually deposited in personal bank accounts operated by Deci officials.

"We wanted to know whether Deci had a company account, and who were their bankers, and they told us that the company did not have a bank account opened in its name," said the source, who did not want to be named because he was not authorised to reveal the probe team's findings to the media.

He added that Deci officials told investigators that money collected from members was kept in their (officials) personal accounts.

The probe team comprised officials from the Directorate of Criminal Investigations, Financial Intelligence Unit (FIU) of the Finance and Economic Affairs ministry, Tanzania Intelligence and Security Services, Bank of Tanzania (BoT) and Capital Markets and Securities Authority (CMSA).

It was also established that Deci was using a letter from BoT to gain the trust of people who wanted to join its pyramid scheme, and convince them that the company was operating legally.

The source said the letter was in response to Deci's application for a licence, adding that the central bank directed the firm to seek registration from the Industries and Commerce ministry.

BoT's director of banking supervision, Mr Joseph Massawe, said yesterday that Deci sent an application to the central bank two years ago seeking registration as an institution that would be issuing loans without taking deposits.

He said BoT advised Deci officials to seek registration from the relevant ministry.

"They have been misusing our letter of no objection. This matter is now in police hands. We have given them all the details on Deci's operations," Mr Massawe said.

Meanwhile, there was tension at Deci's headquarters in Mabibo, Dar es Salaam, following reports that many people who had invested in the pyramid scheme could lose their money.

People could be seen standing in groups discussing the latest developments in low tones.

However, some were hopeful, maintaining that Tanzanians were being deliberately misled into believing that Deci was a criminal outfit.

Others queried why it had taken BoT three years to realise that Deci was operating illegally.

Mr Eliseus Losulie described Deci as a saviour of poor people "who have for many years been exploited by other financial institutions, including banks".

"We reject BoT's announcement made through the media, we have already invested a lot of money here...where were they since 2007? They are liars," he said.

Another member said there was a need conduct a public awareness campaign to make those who were "demonising" Deci understand its operations.

"May be we should raise money and pay for airtime at a television station so that our leaders can explain what Deci is all about," he suggested.

Long queues could be seen outside the Deci offices at Mabibo yesterday as people waited to deposit money.

A man came out of the offices, displaying two receipts, and declaring that there was no one to stop Deci operations except God.

"Here are my receipts, I have just deposited my money. I don't care what BoT says, "we are tired of these politics which will not take us anywhere," he said.

Efforts by The Citizen to reach Deci officials failed as their mobile phones went unanswered.

At its Mabibo headquarters in Dar es Salaam, the company is said to be receiving deposits from an estimated 3,000 people every day.

Deci officials told The Citizen last week that they had paid out over Sh35 billion in "profits" and registered more than 500,000 members since last year when their operations began picking up.

They dismissed reports that the firm was running an illegal scheme as "unfounded and witch-hunting", but could not explain where the money to pay the huge interests came from.


SOURCE: The Citizen

I CAN'T HELP ECHOING SAME QUESTION AS ASKED BY MANY "WHERE HAVE THEY BEEN (relevant authorities) SINCE 2007?"I JUST HOPE IT'S NOT CONFLICT OF INTERESTS THAT HAS ALL THE SUDDEN MADE DECI OPERATIONS ILLEGAL.
THOUGH I AM IN NO WAY CONDONING FRAUD OR "DAYLIGHT ROBBERIES",THE POOR ARE LIKELY TURN TO SUCH GET-RICH-QUICK SCHEMES WHEN THEY ARE BEING NEGLECTED OR UNDER-SERVED BY FORMAL FINANCIAL SECTOR.




BoT now pegs growth at between 5 and 6pc
By The Citizen Reporter

Tanzania's economy will grow by between 5 to 6.1 per cent this year, according to a top BoT official.

BoT director of policy Joseph Massawe said projections by the IMF were "ill advised".

Dr Massawe said Tanzania's economy had not been much affected by the global financial crisis, adding that the effects could be more pronounced in the coming months.

Some economists have also disputed the Bretton Woods institution's forecasts, saying they are too pessimistic and give the wrong impression of the country's economic outlook.

An IMF delegation said early last week the country's economy would grow by between four and five per cent this year due to the global downturn.

But commenting on the sidelines of the annual poverty alleviation meeting in Dar es Salaam recently, local economists said the projections had missed the point since the fundamentals of the country's economy remain sound.

An economic analyst, Prof Haidari Amani of the Economic and Social Research Foundation, said the global financier�s figures were questionable because the economic crisis had no direct impact on the country's economy.

What factors have the IMF used to make their projections because Tanzania's economy depends mostly on agriculture. The four per cent growth can only be possible if agricultural production falls,"he said.

Prof Amani said there were indications that most troubled Western economies, especially the US and in West Europe, would stabilise by end of year, 'making it impossible for Tanzania to get worse.'

Last December, the Government projected a 7.1 per cent economic growth for 2009, which Finance and Economic Affairs minister Mustafa Mkulo last week revised down to 6.5 per cent.

Other economic analysts have also disputed the IMF figures saying Tanzania's economic outlook seemed strong enough to survive the recession this year.

BoT said recently banks in the country were well capitalised and although interest rates have edged up marginally, there has not been any dramatic disruptions witnessed in the country.

And on the sidelines of the Research on Poverty Alleviation (Repoa) annual meeting in Dar es Salaam, local economists said the global crisis has had a
minimal effect on the country.


SOURCE: The Citizen


WHO CARES?THEY COULD AS WELL FORECAST THE ECONOMY WILL GROW AT A RATE OF 50%....THESE "IMPRESSIVE" STATISTICS WOULD ONLY MAKE SENSE WHEN THEY TRANSLATE INTO A COMMON MAN ON THE STREET IS CERTAIN OF HAVING THEIR NEXT MEAL.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.