25 Jun 2009


Breaking News hii ni kwa mujibu wa TMZ.COM ambapo wanaeleza
Michael Jackson Dies

Posted Jun 25th 2009 5:20PM by
TMZ Staff

We've just learned Michael Jackson has died. He was 50.
Michael suffered a cardiac arrest earlier this afternoon at his Holmby Hills home and paramedics were unable to revive him. We're told when paramedics arrived Jackson had no pulse and they never got a pulse back.

A source tells us Jackson was dead when paramedics arrived. A cardiologist at UCLA tells TMZ Jackson died of cardiac arrest.

Once at the hospital, the staff tried to resuscitate him but he was completely unresponsive.
We're told one of the staff members at Jackson's home called 911.La Toya ran in the hospital sobbing after Jackson was pronounced dead.Michael is survived by three children: Michael Joseph Jackson, Jr., Paris Michael Katherine Jackson and Prince "Blanket" Michael Jackson II.

Story developing...

24 Jun 2009

Pichani,Berlusconi akijifuta jasho baada ya kutwanga swali kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga kuhusu tuhuma zinazoweza kuotesha nyasi ndoa yake na mkewe anayeonyeshwa kwenye background.

Waziri Mkuu wa Italia,Silvio Berlusconi,amekanusha madai kwamba alinunua huduma ya tendo la ndoa kwa changudoa mmoja,Patrizia D'Addario.Kiongozi huyo machachari na mwingi wa vituko,anakabiliwa na shinikizo la kisiasa kufuatia madai hayo ya kujimwayamwaya na kimada aliyekuwa miongoni mwa waliohudhuria pati iliyoandaliwa na Berlusconi.

Hadhi ya mwanasiasa huyo tajiri imekumbwa na migogoro lukuki,na hivi karibuni alikuwa na tuhuma za kuvunja amri ya sita na binti wa miaka 18,Noemi Letizia (pichani chini)


Kwa jeuri,Berlusconi amekanusha madai ya kununua ngono huku akikisitiza kwamba "Sijawahi kuona raha ya kununua ngono badala ya ujasiri wa kutongoza".
Vyama vya upinzani pamoja na Kanisa Katoliki wanamtaka Berlusconi kujieleza kuhusiana na skandali hiyo iliyoibuliwa na tume moja ya kuchunguza rushwa huko Italia ya kusini,ambapo inaelezwa kwamba kimada mhusika (kushoto,pichani chini) aliieleza tume hiyo kuwa alilipwa na Berlusconi ili kumpa huduma ya ngono na ana mkanda uliorekodi tukio hilo.

Yote haya yanajiri wakati mke wa Waziri Mkuu huyo akiwa kwenye taratibu za kuomba talaka huku akimtuhumu mumewe kwamba anapendelea sana dogodogo.

CHANZO: itn

Na sie tungekuwa na uhuru wa kuweka ishu kama hizi hadharani,sijui nani angesalimika among vingunge wetu!

Kontebo wa Polisi,Tariq Dost (pichani juu) amefungua mashtaka dhidi ya mwajiri wake na Mamlaka ya Polisi ya eneo la Midlands,hapa Uingereza, kutokana na matamshi ya mwaka 2007 kwamba anafanana na gaidi nambari wani Osama bin Laden (pichani chini).Nadhani kisa ni huo "mzuzu".Je wanafanana?
CHANZO: The Daily Mail


Slaa up in arms on 'silencing' in House
By Faraja Jube Dodoma

Karatu MP Willibrod Slaa has threatened to "go public" with what he said were issues of national interest the Parliament blocked him from tabling in the august House on Monday.

Some MPs heckled the firebrand opposition leader as he stood up in parliament on Monday to give a speech on the Prime Minister's Office 2009/10 Budget.

Dr Slaa had reportedly prepared a vitriolic attack on former President Benjamin Mkapa and the Government over alleged mismanagement of funds.

Before giving his speech, the Chadema leader was reminded to respect the Parliamentary Standing Orders and warned not to breach the law in his presentation.

But in an interview with The Citizen yesterday, Dr Slaa said the National Assembly Speaker, Mr Samwel Sitta, had no right to block debate on sensitive public issues.

He said: "I have written to the Speaker asking him why unnecessary restrictions are being imposed on MPs who want to discuss matters of public interest in parliament."

He threatened to go public with the same issues he was barred from presenting in parliament saying he had the right to let people know about matters that affected them.

"If they don't want us to speak in parliament, it will reach a point where the only reasonable thing to do is table the agenda to the people," said Dr Slaa.

CCM MPs accused the opposition legislator of attempting to use the platform to launch a verbal attack against Mr Mkapa.

Mr Mudhihir Mudhihir (Mchinga-CCM) defended the former president saying he had done "a lot of good things but people want to see the negative only".

"It was under his leadership that this country recorded significant increases in Government revenue," the MP said, praising Mr Mkapa's administration for containing inflation and opening a number of trade opportunities.

Another CCM legislator, Dr Chrisant Mzindakaya (Kwela), tried to have Dr Slaa blocked from presenting his speech at all.

But even when he finally gave his speech, the opposition leader was forced to skip tabling his prepared questions on controversial deals the Mkapa administration allegedly signed.

And in an apparent reference to Dr Slaa, Dr Mzindakaya lashed out at "jealousy hypocrites and good-for-nothing crusaders against corruption".

"Those who criticise Mr Mkapa are agents of the Devil and loafers who have done nothing in life, but are motivated by jealousy and hatred. They are themselves corrupt people," he said.

But Dr Slaa insisted he would not relent on the issues he was barred from talking about saying the Constitution and Parliamentary Immunities and Privileges Act guarantee MPs the freedom to challenge the Government in the parliament.

"I will not accept such moves by anyone any more. This is all compromising principles. But I will stand up for my principles and for justice. We all have the right voice our concerns," he said.

Dr Slaa, who had prepared his disputed speech as a shadow minister, said the Government was obliged to respond to all queries raised by MPs in parliament.

"Even if the issues are sensitive, this is the whole purpose of raising them so that people can know and be informed about what is going on," he said.

"But there has been a tendency to block all sensitive issues from being discussed in parliament," he added.

Before he gave his controversial speech, Mr Sitta told the opposition MP he had read the speech and warned him against making statements that breached parliamentary regulations.

The Speaker had also ordered Dr Slaa not to use abusive language against a former president or discuss issues that had been lined for debate during the session.

Earlier, the chairman of the Parliamentary Committee on Justice, Constitutional Affairs and Governance, Mr George Lubeleje, a CCM MP, had tabled the committee's position against Dr Slaa's speech.

However, the opposition leader retorted: "Why must I have any confidence in the committee or Speaker's office if they insist on imposing on us?"

He questioned the Speaker's application of the Parliamentary Standing Orders to the contentious issues of Meremeta, Tangold, Mwananchi and Deep Green Finance companies.

Last Friday, Dr Slaa asked the Government to respond to allegations of funds mismanagement involving the four companies that have become subjects of public debate.

"I was just questioning the Government over the embezzlement of Sh155 billion in Meremeta and not about the issues pertaining to national security," he said.

Mr Sitta postponed the debate to this Monday saying the Government should be given time to prepare its response.

But Dr Slaa also questioned the Parliament barred debate on the CAG report. "Where does the Speaker obtain the directive to block the debate?"

On the PMO's 2009/10 Budget estimates, the Chadema leader queried the allocation of billions of shillings to entertainment and hospitality, which he said had nothing to do the welfare of people.

He had to put up with sporadic interventions, mainly from Mr Philip Marmo, the minister of State in the President's Office (Good Governance), who also serves as coordinator of parliamentary activities.

Mr Marmo wanted, among other things, the Speaker to reprimand Dr Slaa for his reference to the amount of funds set aside for particular votes in the Government's Budget.

However, Mr Sitta said there was nothing wrong with the MP debating the Government's budget priorities.


SOURCE: The Citizen


Kama hujawahi kuhudhuria matamasha au maonyesho ya wasanii wetu huko Bongo,wala usidhani ume-miss raha pekee.Kuna karaha pia,hususan ile inayotokana na mastaa wetu kudekezwa kupita kiasi na vyombo vya dola.Kwa kifupi,huko ni bangi nje nje,wasanii hugeuka madikteta wanaoweza kufanya lolote lile hadharani ikiwa pamoja na unyanyasaji wa waziwazi dhidi ya dada zetu.Na baada ya "unga" kugeuka "kilevi cha kawaida",wengi wa wasanii hao hujitundika madawa hayo vya kutosha pasipo hofu ya kuchukuliwa hatua na vyombo vya dola.

Nadhani wapo wanaokumbuka msanii mmoja wa bongefleava aliyekamatwa na bangi katika mkoa mmoja wa nyanda za juu kusini.Ni Daz Baba wa kundi lililokuwa likijulikana kama Daz Nundaz.Iliishia kuwa amekamatwa tu,wala hakukuwa na taarifa za msanii hiyo kufikishwa mahakamani au hata kupewa onyo (si lazima kila kosa limaanishe kifungo).

Twende kwa baadhi ya marapa maarufu Msafiri Diouf na Banza Stone.
Haihitaji upelelezi kujua kuwa wanatumia kilevi haramu,lakini dola haijihangaishi kuwachukulia hatua ambazo licha ya kuwaadhibu zingesaidia pia kuokoa maisha yao kwani ni dhahiri kwamba mwisho wao sio mzuri.

Kuna msanii anaitwa Chid Benz.

Licha ya sifa yake ya kufanya vizuri zaidi anaposhirikishwa kwenye nyimbo za wasanii wengine (wanaita "kolabo" as corruption ya neno collaboration) zaidi ya nyimbo zake mwenyewe,mwanabongofleva huyo ni maarufu pia kwa vurugu na vipigo kwa wasanii wenzie.Dola imeendelea kumwangalia tu,hali inayoweza kupelekea Chid Benz kuamini kuwa yuko juu ya sheria kutoa kipondo kwa yeyote yule anapojiskia kufanya hivyo.

Leo,kwenye tovuti ya Global Publishers kuna habari kwamba msaanii Khaleed Mohammed,almaaruf T.I.D,amemjeruhi mwanafunzi mmoja wa kike baada ya kumshushia kipigo cha nguvu.Kwa mujibu wa tovuti hiyo,T.I.D nasakwa na polisi na "hajulikani alipo".Nisingependa kutoa hukumu kwa vile mie si mahakama,lakini napenda kukiri kwamba nilishangazwa na habari kwamba msanii huyo alikuwa miongoni mwa waliopewa msamaha na Rais katika maadhimisho ya siku flani ya kitaifa.

Sikushangaa kwa vile aliyesamehewa ni T.I.D,bali vigezo vilivyotumika kumpa msamaha huo.Kwa tunaofahamu ukweli kuhusu kesi hiyo,yayumkinika kuwa maombi ya msahama ya mtenda kosa kwa waliotendewa kosa yalisikilizwa,na kwa vile waliotendewa kosa ni "wenye kuwezesha jua liwake au lisiwake",yaani "the powers-that-be",msanii huyo akajumuishwa kwenye msamaha wa Rais.

Tukio hili la sasa ambapo T.I.D amerejea kosa lilelile lililompeleka jela in the first place,sio tu linazidisha hisia kuwa wengi wa wasanii na mastaa wetu wanaringia ugoigoi wa wanadola wetu katika kuchukua hatua inapostahili,bali pia ni fedheha na aibu kwa suala zima la msamaha wa rais.Navyofahamu,msamaha huo huzingatia tabia ya mfungwa,afya yake,idadi ya siku zilizosalia katika kifungo chake,na pengine kikubwa zaidi,mwenendo wake pindi akipewa msamaha huo.

Ni dhahiri kwamba jinsi jeshi la Magereza "lilivyojichokea" si rahisi kwake kukamilisha vigezo hivyo vyote.Na katika jamii ambayo mwenye fedha ni mithili ya mungu-mtu huku ufisadi ukishamiri kila kukicha,yayumkinika kuamini iwamba misamaha ya rais imekuwa ikitumika ndivyo sivyo.

Hivi tunajenga jamii ya aina gani?Wkati wenzetu katika nchi zilzoendelea wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa kudhibiti uvutaji wa sigara katika maoneo ya mikusanyiko,sie tunaelekea kuruhusu uvutaji wa bangi kana kwamba ni kitu halali.Nilisoma mahala flani kwamba msanii mmoja wa filamu za kibongo alichomoa bastola hadharani kisa wapita njia walimlalamikia kwa kupaki gari lake barabarani.

Jeuri hii wanaipata wapi?

Hypothesis yangu ni hii: itikadi ya ujamaa iliifanya sehemu kubwa ya Watanzania kuwa wanyonge wasio na stahili ya kuwa karibu na makundi yenye nguvu au mvuto kwenye jamii hiyo e.g. wanasiasa,wasanii,nk.Japo tunadai kuwa ujamaa umekufa,mentality ya itikadi hiyo bado iko hai na inatuathiri katika namna tunavyodili na watu hao walio kwenye "makundi maalumu" kwa mfano "mastaa wetu".Polisi wa trafiki anajiuliza mara mbilimbili "kuipiga mkono" Benz au Vogue,kwa vile akilini mwake,dereva wa gari hilo ola thamani anaweza "kuhatarisha ajira yake".Mtaani,msanii anageuka "mungu-mtu",wananchi wanatamani kuwa karibu nae,angalau kugusana mabega nae,wanadola wanachelea kumchukulia hatua (pengine kwa kudhani kuwa kwa vyovyote vile msanii hiyo atakuwa na connection na mtoto wa kigogo flani),na upuuzi mwingine kama huo.

Sio kwamba ujamaa ni mbaya per se.Kuna mazuri flani,ila hapa nimezungumzia legacy ya itikadi ya ujamaa katika upande hasi.Pengine kunahitajika mjadala wa kitaifa kutafakari mambo kama haya.

UNAONAJE?

23 Jun 2009

Pichani,Mwanasoshojia akimuaga Mzaa chema.

BLOGU HII INATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUTOKANA NA KIFO CHA MAMA MZAZI WA BLOGA MWANASOSHOLOJIA.HAKUNA MANENO MWAFAKA YANAYOWEZA KUKULIWAZA WEWE BINAFSI NA FAMILIA YENU KWA UJUMLA,LAKINI TUAMINI KUWA MUNGU AMEMPENDA MAREHEMU ZAIDI YETU,NA NDIO MAANA AMEMCHUKUA.NA KWA VILE MUNGU NI WA UPENDO,BASI TUNA HAKIKA ATAMPATIA MAREHEMU PUMZIKO LA AMANI NA RAHA YA MILELE.

POLE SANA,MWANASOSHOLOJIA.

Dunia haina dogo.Kuna wambeya wanaodai eti huyo "nzi" alikuwa ni skadi lililotumwa na Dick Cheney kwa Obama.Kuna wengine wanadai huyo wala hakuwa "nzi" bali roboti lilotengenezwa na majasusi wa Kimarekani kupeleka ujumbe kwa Kim Jong Ill na mikwara yake ya nyuklia.Wapo wanaomhusisha "nzi" huyo na uchaguzi wa Irani..... Alimradi burudani!

ELEKEZO: Neno "nzi" limetumika kama tafsiri isiyo rasmi ya "fly" (BAKITA mko wapi?)


Inakera ati!hususan kwa simu vimeo zinazokula chaji kama hazina akili nzuri.Wajuzi wa simu wanadai kwamba baadhi ya simu "zina allergy na full charge",yaani chaji haidumu.

Taarifa zinaeleza kwamba maabara ya Kampuni ya Nokia hapo Cambridge wanatafiti ujio wa simu itakayokuwa ikijichaji yenyewe.Badala ya kutumia chaja za kawaida,simu hiyo itakuwa ikijichaji kwa kugema nishati kutoka kwa mawimbi ya radio (radio waves) yanayotoka kwenye antena,milingoti ya televisheni,Wi-Fi transmitters,nk.

CHANZO: The Guardian


The British National Party could face legal action over its 'whites only' membership policy, a watchdog said yesterday.The party could be taken to court for three counts of discriminating on grounds of colour, the Equalities and Human Rights Commission said.

If the BNP refuses to allow non-whites to join the party, it could face heavy fines, or its assets could be seized - making it almost impossible for them to fight elections effectively.

Senior party members, such as leader Nick Griffin, could even be imprisoned, if the courts so decided. The move comes two weeks after the BNP won its first seats in the European Parliament following a collapse in Labour support. The party has around 60 councillors across the country.

Their constitution says only those with 'indigenous Caucasian' racial backgrounds can become members of the party. It is believed to be the first time that race watchdogs have threatened a political party with legal action.

The commission said the party appeared to be guilty of three breaches of the Race Relations Act: not allowing non-whites to join the party, not allowing them to take jobs at the party, and not providing equal services to constituents based on the colour of their skin.

They said this amounted to discrimination on the grounds of race and colour, which is banned under the act.The EHRC called on the BNP to provide written undertakings by 20 July that it will make the required changes or it could face a legal injunction. If not they could bring a civil action against them at the High Court.
If the party still did not comply, judges could find it guilty of contempt of court, which could lead to fines or even jail for BNP leaders.

A spokesman for the watchdog said: 'This exclusion is contrary to the Race Relations Act which the party is legally obliged to comply with. The commission therefore thinks that the BNP may have acted, and be acting, illegally.

'The commission has required the BNP to provide a written undertaking that it will not discriminate contrary to the Race Relations Act in its employment and recruitment policies, procedures and practices.'

The commission said it was also concerned that the BNP's elected representatives may not intend to offer or provide services on an equal basis to all their constituents and members of the public irrespective of race or colour.

John Wadham, the Commission's legal director, said: 'The legal advice we have received indicates that the British National Party's constitution and membership criteria, employment practices and provision of services to constituents and the public may breach discrimination laws which all political parties are legally obliged to uphold.

'We await a response from the BNP to our letter before deciding what further action we may take. Litigation or enforcement action can be avoided by the BNP giving a satisfactory response to our letter.'
The commission has received around 50 calls from members of the public recently about the BNP's membership policy, although it is believed that officials were already looking into the issue.

But last night BNP leader Nick Griffin, who was elected as an MEP for the north west of England earlier this month, said the party's rules were 'entirely legal', adding: 'We are not discriminating on the grounds of colour'.

He claimed the party was an exempted organisation under the Race Relations Act, which protected organisations which represented minority groups.Mr Griffin said this meant 'ethnic groups who need special protection such as the English in their own country, who are now second class citizens' were 'entitled to discriminate on that basis and not on the grounds of colour'.

A spokesman for the BNP said: 'We are not going to respond to threats like this. We will look at it, but it is an entirely politically-motivated attack. 'I don't think we should be bullied by outside forces. They are asking us to change our whole political ideology.'




Pengine siendi na wakati.Pengine mgumu wa kuelewa.Pengine....well,pengine sina hoja bali naibua tu cha kuropoka.All in all,mie ni miongoni mwa sijui wengi au wachache ambao hizi SIKU MAALUM hazina umuhimu kihivyo.Tuanze na siku ya kuzaliwa (BIRTHDAY).Mie nilizaliwa tarehe inayofanana na siku ya Uhuru na Jamhuri,yaani 9 Desemba (mwaka sabini na kitu).Excuse yangu kubwa ya "kuipuuza" birthday yangu huwa "tayari taifa linasherehekea pamoja nami".Si unajua 9 Desemba huwa ni mapumziko huko home?Halafu maswala ya gwaride na vikorombwezo vingine.Well,inatosha kuwa kiji-excuse cha namna flani.La muhimu kwangu katika kila 9 Desemba ni kumshukuru Mungu kwa kunifikisha siku hiyo,kisha kuongea na wazazi.Baba na marehemu mama walijenga utaratibu wa kutuimbia wimbo wa hepi bethdei to yuuu...That's it.Sala,wimbo na dua za wazazi,siku imekamilika.Hizo habari za birthday parties ni msamiati ambao haujaingia kwenye kamusi yangu.


Kuna kitu inaitwa MAHAFALI.Well,sikumbuki vyema kuhusu mahafali ya kumaliza darasa la saba lakini natambua kuwa ilikuwa mbinde hapo Ifakara.Uchumi wa familia haukuruhusu anasa zisizo na msingi,na wakati huo (1985) taifa nalo lilikuwa katika wakati mgumu vilevile.Si zamani kihivyo.lakini mengi ya yanayoonekana leo hayakuwepo zama hizo.

Nadhani kitu pekee nachokumbuka kuhusu mahafali ya kumaliza kidato cha nne ni uamuzi nilokuja kuujutia baadaye wa kuonja kilevi cha kiwandani.Nilijaribu bia aina ya Safari Lager kwa mara ya kwanza maishani.Of course,kabla ya hapo nilishawahi kujaribu kilevi cha asili cha pombe ya mpunga.Ili nisije sahau,ni vema nikujulishe kidogo kuhusu pombe hii inayonukia kama wali.Kwa kifupi,ukiinywa saa 10 jioni basi inakuwa kichwani hadi kesho saa 10 jioni.Well,at least kwa "vichwa panzi" kama nilivyokuwa siku hizo.

Basi hiyo Safari Lager ilinipelekesha kupita maelezo.Nadhani nilifanya vituko kadhaa lakini kumbukumbu zaidi niliyonayo ni kuugua kwa takriban wiki hivi.Ungetegemea kuwa hiyo ndio ingekuwa mara yangu ya kwanza na ya mwisho kugusa kilauri.Wapi!Ukiniuliza namna gani niliweza kuji-transform kutoa mnywaji anayeugua wiki nzima baada ya kunywa bia moja hadi kufikia hatua kummudu John Mtembezi (John Walker),sidhani kama nitakuwa na jibu sahihi.

Anyway,mahafali ya kidato cha sita hata sikumbuki yalikuwaje.Shule yenyewe ilikuwa ya kijeshi (Tabora Boys) halafu nilikuwa miles away from home.Mahafali kwa maana ya mahafali yalikuwa ya kuhitimu Mlimani (UDSM).Kuna waungwana walishauri nitengeneze kadi za mchango wa sherehe ya mahafali.Well,it worked.Watu wakapiga donation,likapatikana fungu la kufanya sherehe ya maana mtaa wa Isisi,Kinondoni.Na kuna mahala flani walinisaidia bia za bei nafuu.

Hapa Aberdeen nilijichukulia tu vyeti vyangu hapo 2003 na 2004.Ila nikikamilisha libeneke hili la sasa,huenda nikajumuika na watu wawili watatu maana hii ya sasaa ni shughuli nzito kwa kiasi kikubwa.

Back to the topic.Sijui Father's Day ni leo au kesho au ishapita.Honestly,muda huu naoandika post hii sina hakika,na sitaki kuhakikisha kwa ku-google.Kwangu,siku ya Baba yangu (na kama ilivyokuwa kwa Mama yangu) ni kila siku.Najua kwanini kuna siku moja maalumu,lakini kwa mie kila siku ni maalum.Yaleyale ya siku ya Wapendanao.Nikimpenda mwandani wangu basi ni suala la kila siku na Ferbuari 14 inakuwa siku kama siku nyingine tu.Of course,nimeshawahi kuonekana kichekesho huko nyuma lakini hainisumbui.

Vipi,huu mtazamo wangu unaouonaje?Ukale,uzembe wa kwenda na wakati,sahihi au you dont even care?

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.