12 Jul 2009


Kizitto Noya na Habel Chidawali, Dodoma

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Shamsa Mwangunga, amekiri kukithiri wizi wa nyara za serikali hasa pembe za ndovu na kueleza kuwa sio rahisi kudhibiti vitendo hivyo kwa kuwa vinafanywa na mtandao wa watu wenye fedha nyingi.

Mwangunga alisema hayo bungeni jana alipokuwa akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake mjini na kufafanua wizi wa makontena mawili ya pembe za ndovu yaliyokamatwa Machi, mwaka huu nchini Vietnam.

“Kukithiri kwa wizi huo kumetokana na Wizara ya Maliasili na Utalii kutohusishwa na ukaguzi wa mizigo bandarini na soko kubwa la nyara hizo liko katika nchi za Asia. Mtandao wa watu wenye fedha nyingi ndio unaendesha biashara hiyo kwa kushirikiana na maafisa wa bandari,” alisema Mwangunga.

“Ninasema maafisa wa bandari wanahusika kwa sababu bandarini ndiko kwenye lango la kupitisha nyara hizo na maafisa wake ni miongoni mwa watuhumiwa katika matukio hayo.”

Mwangunga alikuwa akijibu hoja ya mbunge wa Same Mashariki Anne Kilango Malecela ambaye juzi alitishia kutoa hoja binafsi kutaka iundwe Kamati teule ya Bunge kuchunguza wizi wa makontena hayo yaliyokamatwa Machi 25, mwaka huu nchini Vietnam.

Mbunge huyo alitaka kamati hiyo ichunguze jinsi makontena hayo yalivyopita kwenye bandari za hapa nchini baada ya kukaguliwa na mamlaka husika na kufika Vietnam bila kujulikana kuwa yalibeba pembe za ndovu.

"Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie kuhusu jambo ambalo kwa kweli limenisikitisha sana ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii ambao ni wizi wa nyara; wizi wa pembe za ndovu. Wizi huu Mheshimiwa Spika, unafanyika kama vile nchi yetu hakuna ulinzi," alilaumu Kilango na kuongeza:

"Nimefanya utafiti nina faili zima; Mheshimiwa Spika nilikwenda kufanya utafiti, baada ya kusoma kwenye magazeti kuhusu makontena mawili yaliyokamatwa Vietnam, nikaona nisiishie hapo niende ndani mpaka nipate faili zima.

"Nasikitika sana. Nilikwenda kuhoji; nikaelezwa; nikapewa na faili; nikasoma kontena zile mbili zilipitia bandari yetu kama kawaida".

Kilango aliomba atumie kanuni ya 117 ya Bunge kuwasilisha hoja binafsi kutaka iundwe kamati teule kwa ajili ya kuchunguza jambo hilo.

Hata hivyo, jana Spika wa Bunge Samuel Sitta ambaye juzi aliahidi kufanyia kazi suala hilo, alitupa hoja hiyo baada ya Kilango kushindwa kuwasilisha kusudio lake hilo kwa maandishi kwa wakati.

”Kulikuwa na hoja ya kuundwa kamati teule jana, lakini niseme kwamba, hoja hiyo sijaipata hapa kwa maandishi, nimwombe Katibu aendelee na shughuli za leo,” alisema Sitta muda mfupi kabla ya bunge kukaa kama kamati.

Kabla ya Sitta kusema hivyo, aliingia bungeni akikimbia akiwa ameshika bahasha ya kaki ambayo ilisemekana kuwa ilikuwa na hoja yake hiyo kimaandishi ambayo alitarajia kuiwasilisha.

”Naona kuna kitu kinataka kunifikia sijui kama ndio hiyo hoja, ah, lakini kwa mujibu wa kanuni za Bunge siwezi kuipokea hoja hiyo na kusema kweli itakuwa ndiyo basi, sitaipokea tena hivyo tunaendelea waheshimiwa,” alisema Sitta.

Akizungumza na gazeti hili katika viwanja vya Bunge jana, Kilango alisema alichelewesha kupeleka hoja yake baada ya awali kushauriwa na Spika kuwa suala hilo liachwe liendelee kushughulikiwa na Polisi wa Interpol chini ya makubaliano ya Lusaka (Lusaka Agreement).

”Mimi hoja nilishaandaa, lakini Spika alinishauri kuwa kwa vile suala hilo linashughulikiwa na Interpol, tuache kwanza.

Lakini hii haina maana kwamba, hoja imekufa. Nitaiibua tena wakati wowote baada ya interpol kumaliza kazi yake,” alisema.

Awali akizungumzia wizi huo Mwangunga alisema ulitokea Machi 25 mwaka huu na tayari watu tisa wamekamatwa na kuhojiwa.

”Kati yao, watu wanne wamefunguliwa kesi mahakamani mkoani Tanga,” alisema Mwangunga na kutaja majina ya watuhumiwa hao.

Alisema mbali na tukio hilo, kontena lingine lilikamatwa Machi Mosi, mwaka huu katika Bandari ya Manila Ufilipino ambako pembe za ndovu zenye uzito wa tani tano lilikamatwa.

Siku nne baadaye maafisa Forodha wa Vietnam walikamata kontena lingine namba ESU 1174 lililokuwa na tani 6.2 za pembe za ndovu.

Hata hivyo, Mwangunga alishindwa kusema pembe hizo za ndovu zilitoka wapi kama alivyotakiwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe.

Kabwe alitaka waziri huyo aeleze endapo shehena hiyo ni ndovu wanaoendelea kuuawa au zimekwapuliwa kutoka kwenye ghala la serikali.

”Siwezi kusema kuwa zilitoka wapi kwani katika ghala za serikali hakuna wizi uliotokea na namna zilivyopangwa na kama ingechukuliwa hata moja ni rahisi sana kujua, hivyo inawezekana zilitoka katika maeneo yetu au hata nchi jirani waliamua kusafirisha kwa kupitia bandari zetu kutokana na udhaifu uliopo katika bandari za hapa nchini,” alisema Mwangunga.

CHANZO: Mwananchi

INA MAANA WIZARA INGEWEZA KUWADHIBITI MAFISADI HAO LAITI MTANDAO WAO UNGEKUWA NA FEDHA KIDOGO AU HOHEHAHE?HII WIZARA IMEKUWA KICHAKA CHA MAFISADI MIAKA NENDA MIAKA RUDI.BY THE WAY,KAMA MAFISADI WANAWEZA KUTUIBIA BENKI KUU (THRU EPA,etc) AMBAPO KUNA ULINZI WA HALI YA JUU,TUTEGEMEE NINI HUKO MBUNGANI?TUTAJUA MENGI PINDI IKIFANYIKA "SENSA" YA RASLIMALI ZETU HUKO MBUGANI.HOPEFULLY,BY THEN MAFISADI HAWA HAWATAKUWA WAMEKOMBA KILA KITU!


<

11 Jul 2009


Pamoja na sifa zake nyingi ikiwa ni pamoja na kuwa jiji la tatu kwa ukubwa (kwa idadi ya watu idadi ya watu,nyuma ya London na Birmingham) hapa UK,Glasgow,unabeba historia ya "Simba na Yanga" za Scotland,yaani klabu mbili za soka zenye upinzani wa kupindukia:Glasgow Rangers (almaaruf RANGERS) na Celtic.Tofauti na upinzani wa Simba na Yanga,au Manchester City na Manchester United,au kwingineko kwenye "mafahali wawili wanaopigania ubabe kwenye mji mmoja",upinzani kati ya Celtic na Rangers umevuka mipaka ya soka.Wakati Celtic ni,generally speaking,Wakatoliki,Rangers ni Waanglikana.Zamani hizi,ilikuwa jambo lisilowezekana kabisa kwa mchezaji Mkatoliki kusajiliwa na Rangers,au Muanglikana kusajiliwa na Celtic.

Sasa,moja ya tahadhari wanazopewa wageni katika jiji la Glasgow ni rangi za timu hizo mbili.Ukirogwa kuvaa "jezi" za Rangers kwenye maeneo ya wapenzi wa Celtic,au kutinga rangi za Celtic kwenye maeneo ya kujidai ya Rangers,tarajia yasiyotarajiwa.






In his first visit to Africa since taking office, Barack Obama said today that the continent of his ancestors must overcome tyranny and corruption if it is to flourish.

Speaking in Ghana's parliament, Obama said the key to Africa's future prosperity was democratic and accountable government.

"Development depends upon good governance. That is the ingredient which has been missing in far too many places, for far too long. That is the change that can unlock Africa's potential," he said.

In an tough speech aimed at politicians across the continent, he gave an unsentimental account of squandered opportunities since the end of colonial rule. "No country is going to create wealth if its leaders exploit the economy to enrich themselves, or police can be bought off by drug traffickers," he said.

"No business wants to invest in a place where the government skims 20% off the top ... No person wants to live in a society where the rule of law gives way to the rule of brutality and bribery. That is not democracy, that is tyranny, and now is the time for it to end.

"Africa doesn't need strongmen, it needs strong institutions."

Obama conceded that colonialism had left a legacy of conflicts and arbitrary borders. "But the west is not to blame for the destruction of the Zimbabwean economy over the last decade, or wars in which children are enlisted as combatants.

"Africa is not the crude caricature of a continent at war," he said. "But for far too many Africans conflict is a part of life, as constant as the sun. There are wars over land and wars over resources. And it is still far too easy for those without conscience to manipulate whole communities into fighting among faiths and tribes."

Earlier, after meeting Ghana's president, John Atta Mills, Obama praised the country's record of democracy and economic growth as a rare success in a continent beset by corruption and poor governance.

"We think that Ghana can be an extraordinary model for success throughout the continent."

This morning, Obama was given a hero's welcome in the country's capital, Accra. Thousands of people wearing Obama T-shirts thronged the streets, cheering and waving as his motorcade swept past.

Walls and utility poles were plastered with posters of Obama and Mills, as well as the word "change" – the mantra of Obama's presidential election campaign. Other posters showed the president and his wife, Michelle, with the greeting "Ghana loves you".

Obama and his family arrived late last night from the G8 summit in Italy, where the world's richest nations agreed on a $20bn (£12.4bn) food security plan to help poor nations feed themselves during the global recession.

Speaking in Italy before he left, Obama said: "There is no reason why Africa cannot be self-sufficient when it comes to food."


The Obamas will visit Gold Coast Castle, a former British slave trading post. Michelle Obama is a great-great granddaughter of slaves.

The visit comes as the US plans a much more assertive policy in Africa, using both diplomacy and the threat of force to end the protracted conflicts in Democratic Republic of the Congo and Nigeria, which are seen as two of the main obstacles to the continent's progress.

"This is both a special and an important visit for him personally as president, but also for our country to articulate a vision for Africa," said Robert Gibbs, the White House spokesman.

Despite the enthusiastic reception from ordinary Ghanians, no major public events have been planned during Obama's 21-hour visit, for fear it could cause a celebratory stampede, as almost happened during a 1998 stop by Bill Clinton.


SOURCE: The Guardian

10 Jul 2009

Rais Barack Obama anaonekana kama "analipiga jicho" bunda (makalio) la binti wa Kibrazili,Mayara Tavarez,huku Rais Nicholas Sarkozy akishika tama!Yes,He can!


9 Jul 2009


A British diplomat in Russia, James Hudson, has quit after being filmed having sex with two blonde prostitutes.Hudson, 37, resigned from his posting to the Urals over the video, which is thought to have been secretly shot by Russian spies.

The footage apparently shows Mr Hudson, wearing a dressing gown, kissing the two semi-naked girls while drinking champagne in a brothel
...CONTINUES



8 Jul 2009


Neo-Nazis are plotting a 'spectacular' terrorist attack on Britain to fuel racial tension, Scotland Yard's counter-terrorism officers fear.

Senior officers have increased their surveillance of suspects to monitor their ability to carry out a deadly attack aimed at causing a 'breakdown in community cohesion'.

The chilling warning comes after last month's startling gains by the BNP in the local and European elections which many fear may 'embolden' violent Far-Right extremists.

Commander Shaun Sawyer, from the Met's specialist operations wing told a meeting of British Muslims last night: 'I fear that they will have a spectacular ...

'They will carry out an attack that will lead to a loss of life or injury to a community somewhere. They're not choosy about which community.'

His comments came after Commissioner Sir Paul Stephenson asked officers to examine what effect the recession could have on far-right violence.

And the news mirrors similar warnings of the threat from far-right sympathisers issued in America in recent months.

While countering a threat from Islamic extremists remains the priority many officers now believe that funds need to be funnelled towards preventing a possible strike by the Far-Right.

Threat level in the UK may be downgraded, says terror chief

Despite the warning, Assistant Commissioner John Yates today warned that counter terrorism police face budget cuts.

He admitted savings must be made in two years time despite the risks posed by the looming London 2012 Olympic Games.

The senior officer, who took control of Scotland Yard's specialist operations wing three months ago, said it would be "naive" to think counter terrorism work would escape the recession.

Last weekend it was revealed that a network of suspected extremists with access to 300 weapons and 80 bombs has been uncovered by counter- terrorism detectives.

Thirty-two people were questioned by police and 22 properties were raided over an alleged plot to bomb mosques.

It was the biggest terrorist arms haul since the IRA mainland bombings in the 1990s.

Sir Norman Bettison, the chief constable of West Yorkshire, said: 'The big bad wolf is still the Al-Qaeda threat.

'But my people are knocking over right-wing extremists quite regularly. We are interdicting it so that it doesn't first emerge into the public eye out of a critical incident like an explosion.'

It is more than 10 years since neo-Nazi nail bomber David Copeland attacked three targets in London in 1999.

Three people died at the Admiral Duncan gay pub in Soho.

Copeland also targeted the Muslim community in Brick Lane, east London, and a supermarket in Brixton, south London.

Abdurahman Jafar of the Muslim Safety Forum, where the concerns were raised, said:

'Muslims are the first line of victims in the extreme right's campaign of hate and division and they make no secret about that.

'Statistics show a strong correlation between the rise of racist and Islamophobic hate crime and the ascendancy of the BNP.'

Mark Gardner, of the Community Security Trust, which monitors violence against Jews, said there has been a surge in right-wing incidents.

He said: 'Ten years after the Nazi nail bombings in London, we are seeing increasing numbers of neo-Nazis being arrested in their attempts to start some kind of so-called race war.

'It is the Muslim community that appears to be most targeted, but all of society is at risk, and we are in regular discussion with police about the problem.

'Worse still, the recent electoral successes for the BNP may cause some would-be terrorists to be further emboldened in their actions.'

Last year neo-Nazi Martyn Gilleard, 31, was convicted of three terrorism offences and jailed for 16 years.

Gilleard idolised Adolf Hitler and urged sympathisers to act to preserve the 'purity of the white race'.

When police raided his flat they found bullets, swords, knives and four nail bombs under a bed used by his five-year-old child.

Officers also found DIY bomb manuals, a guide on making a sub-machine gun and internet instructions on carrying out assassinations by poison.

A speech he had recorded in a notebook mentioned 'killing Muslims, blowing up mosques and fighting back'.

No one at the Muslim Safety Forum was available for comment. The Metropolitan Police declined to comment.

Last month a white supremacist with links to the BNP shot dead a security guard at Washington's Holocaust Museum in a racially-motivated killing.

Before launching the attack, 88-year-old James von Brunn sent out an email claiming: 'It's time to kill all the Jews.'

Von Brunn was shot and wounded by museum security officers after he walked into the packed tourist attraction and began firing indiscriminately.

4 Jul 2009



KWANZA Merged

Picha kwa hisani ya KENNEDY

Wanasema siasa ni mchazo mchafu.Lakini siasa katika bara letu la Afrika ni zaidi ya mchezo mchafu.Ni mchanganyiko wa kanyaboya,songombingo,mbinde,usanii,ufisadi na what have you.Hiyo sio kumaanisha kuwa siasa katika maeneo mengine,kama Ulaya na kwingineko ni safi kihivyo.Lakini angalau hawa wenzetu check-and-balance mechanism zinafanya kazi kwa kiasi kikubwa.Sie tunazo lakini aidha wenye majukumu ya kuzitumia wako bize sana na posho au nyumba ndogo au hawajui kwa nini wapo mahala panapopaswa kufanya hiyo check na balance.

Hivi CCM walikuwa wanafikiri nini mwaka 2005 kuahidi kuwa wangeshughulikia uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi?Binafsi sina tatizo na uanzishwaji wa mahakama hiyo as long as suala hilo linafanywa kwa uangalifu.Sio priority kwa sasa lakini kwa vile ni haki kwa Waislamu,then hakuna budi kuangalia uwezekano huo.Kwahiyo,CCM hawakufanya kosa "kukubali" kuanzisha Mahakama ya aina hiyo baada ya uchaguzi mkuu wa 2005.Hawakufanya kosa kwa vile wazo hilo sio baya au la hatari kama baadhi ya watu wanavyofikiria.Nitatafuta wasaa mwafaka siku nyingine kuelezea kwanini Waislam wako sahihi kudai mahakama hiyo na kwanini uanzishwaji wake hauna madhara kwa wasio waislam.In fact,suala sio "kuanzisha" bali "kurejesha" kwa vile mahakama za aina hiyo zilikuwepo wakati wa ukoloni na muda mfupi baada ya uhuru.

Kosa la jinai (yes,ni jinai) la CCM ni kutoa ahadi nyeti kama hiyo wakati inafahamu fika kwamba haina muda wa kuishughulikia.Ni kosa pia kwa vile pamoja na ahadi hiyo ya kuanzisha mahakama ya kadhi tayari chama hicho kilikuwa kimeshatoa ahadi nyingine lukuki kana kwamba kinaomba kutawala kwa miaka 100 na sio mitano (2005-2010)!Kulikuwa na ahadi za kuwakalia kooni wala rushwa,kushughulikia kero za Muungano,kuboresha maisha ya Watanzania,na ahadi nyingine kedekede.Si tu kwamba wakati tunaelekea mwishoni mwa miaka hiyo mitano rushwa imeshamiri na ku-mutate into ufisadi (kumbuka,neno hili limejitokeza katika kipindi hiki),kero za Muungano sio tu kuwa bado zipo ila tumeshuhudia "kibiriti kikitikiswa mpaka kinataka kulipuka",na hayo maisha bora kwa kila Mtanzania sanasana yamewezekana kwa mafisadi na washirika zao....

Hili la kuahidi kushughulikia masuala yanayogusa imani (ya kiroho) ilhali hakuna dhamira au uwezo wa kufanya hivyo ni jambo hatari mno.Dini ni hatari zaidi ya ukabila kwani inahusisha uhai na kifo (mtu akifa kwa ajili ya dini ni martyr,at least dini nyingi zinaamini hivyo).

Kauli za viongozi kuhusu suala hili sio tu zimekuwa za kujichanganya bali zimechangia kukuza tatizo hilo.Mara mchakato unaendelea,mara sheria za kiislam zitaingizwa kwenye sheria za mahakama za sasa (hicho tayari kinafanyika),mara hili,mara lile.Kama kawaida,wahusika wanasubiri lilipuke ndio watafute chanzo cha mlipuko.Unfortunately,milipuko mingine ikianza hata huo muda wa kutafuta chanzo hautokuwepo.Waulize Nigeria!

Tuiombee nchi yetu.












Michael Jackson mithili ya chura!?The Jacko mithili ya Bikira Maria!?Ukishangaa yanayohusu maisha na kifo cha the King of Pop basi hujakutana na "kazi za sanaa" zinazomhusu the Jacko.Picha za juu ni baadhi tu ya "kazi" hizo.Unajua,fani yenyewe ya sanaa imetawaliwa na ujanja ujanja wa namna flani.Kwa mfano nenda maeneo ya Msasani kwa wauza vinyago wa Kimakonde.Utakutana na kinyago cha Nyerere,kwa mfano,lakini zaidi ya ukweli kuwa kinyago hicho ni cha mpingo (kama alivyodai mchonga kinyago),the rest havifanani kabisa na Nyerere,unless uwe hujawahi kuona sura ya Baba wa Taifa.Pita pita mitaani,utakutana na wasanii wanaodai wanaweza kukuchora na wakikamilisha mchoro utadhani unajiangalia kwenye kioo.Of course,wapo wenye vipaji vya namna hiyo.Lakini kuna " wasanii" pia.Atakuchora,kisha akikupatia "picha yako" unaweza kuishia kutamani kumkaba loba (kabali) ya mbao!

Na kifo cha Michael kinaelekea kuwa dili la nguvu kwa WASANII kwa maana ya ARTISTS na WASANII kwa maana ya CONFIDENCE ARTISTS (con artists).Ama kweli kufa kufaana!



3 Jul 2009


Mufti Simba aagiza Waislamu waikatae CCM

Mufti Issa bin Shaaban Simba, amekasilishwa na uamuzi wa serikali kuhusu Mahakama ya Kadhi.

Na Ummy Muya

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limesema kutokana na serikali kutupilia mbali ombi la kunzisha Mahakama ya Kadhi, Waislamu hawataipigia kura CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Katika taarifa yake, Bakwata ilifikia hatua ya kusema Waislamu wasimchague Rais Jakaya Kikwete iwapo atasimamishwa na CCM kugombea urais, ikiwa ni pamoja na wabunge na madiwani watakaosimamishwa na chama hicho tawala kutokana na kitendo cha serikali kutupilia mbali hoja ya Mahakama ya Kadhi.

Kauli hiyo imetolewa jana wakati Mufti Issa bin Shaaban Simba alipokuwa akitoa tamko kupinga uamuzi wa serikali kutaka kutumia sheria za dini ya Kiislamu katika mahakama za kawaida badala ya kuanzisha Mahakama ya Kadhi, kitu ambacho alisema anaamini kitawanyima haki Waislamu.

Alisema serikali imedhihirisha kuwa inaendeshwa na Wakristo na si kweli kama serikali haina dini na akamtaka Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kubatilisha kauli hiyo kwa kuwa inamchafua Rais Jakaya Kikwete mbele ya umma wa Waislamu.

Waziri ametuthibitishia kama Rais Kikwete alikuwa akitulaghai ili tumpigie kura kwa kigezo kuwa suala hilo litashughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi na sio kuchanganywa kama ilivyokuwa mwaka 1970 katika Sheria ya Ndoa na kuwanyima haki Waislamu,alisema.

Alisema kwa muda mrefu sana Waislamu wamekuwa kimya wakitumia hekima na busara kudai haki zao, lakini katika hatua hii ambayo serikali imefikia hawapo tayari kuendelea kudhalilishwa na kuwa kitendo hicho ni dhalimu.

Mufti alisema wamekuwa wakiiomba Mahakama ya Kadhi kwa zaidi ya miaka 20 na hivyo hawezi kuendelea kuwa kimya na kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa kwa kuwa mahakama hiyo ni haki yao.

Alisema kauli ya Waziri Chikawe imedhihirisha kuwa serikali ina wenyewe na Waislamu wamewekwa katika tabaka la pili pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwatuliza kwa ahadi kuwa watalipatia ufumbuzi suala hilo.

Natoa wito kwa Masheikh wote nchini na Waislamu wa madhehebu yote kupinga vikali kauli iliyotolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na kwamba Waislamu waige mfano wa Waislamu wa Afrika Kusini,alisema Mufti na kuhoji:

Kwa nini iwe Afrika ya Kusini na isiwe Zanzibar, Uganda na Kenya ambazo zipo ndani ya Afrika Mashariki? Kwa niaba ya Waislamu nasema serikali haikututendea haki na imetuchukiza sana,alisema.

Alisema lengo la kuomba mahakama hiyo ni kuhakikisha Waislamu wanashughulikia masuala yao ya ndoa na mirathi na si vinginevyo, hivyo waziri asipotoshe jamii kwa kutumia mifano ambayo haiko sahihi.

Mahakama hii haitawakata wezi mikono kwa kuwa nchi hii ina katiba na sheria na sisi tutazirudisha kesi zote za jinai mikononi mwa serikali. Sifahamu hiyo kamati ambayo waziri alisema alikuwa amekaa na kutoa tamko hilo ilikuwa na watu gani,alihoji.

Aliongeza kuwa kutokana na mapungufu hayo waziri arudi tena na kukutana na masheikh ili apate muongozo wa nini Waislamu wanahitaji na sio kuzungumza bila kuwa na usahihi wa kile anachosema.

Wakizungumza na waandishi wa habari baada ya tamko la Bakwata, masheikh walikuwa na mitazamo tofauti. Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Salum Mussa alisema wapo baadhi ya Waislamu ambao watakubali kutokana na ufinyu wao wa elimu ya dini.

Mussa alisema haoni sababu ya serikali kufanya njia ya mkato katika suala hilo kwani Waislamu wanahitaji Mahakama ya Kadhi kama ilivyo kwa wafanyabiashara ambao wana mahakama yao.

Hukumu inayotolewa katika Mahakama ya Kadhi ni ibada kwa mujibu wa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) hivyo ni lazima kwa atakayetoa hukumu hiyo awe Muislamu na si vinginevyo,alisema.

Namshanga waziri anapotaka sheria hizi zitumiwe katika mahakama za kawaida. Aliona wapi John akawa imamu,alihoji sheikh huyo wa mkoa wa Dar es Salaam.

Naye katibu wa Bakwata wilayani Ilala, Sheikh Issa Ausi alisema historia iko wazi. Waasisi na wanaharakati ambao waliitoa Tanganyika mikononi mwa wakoloni walikuwa Waislamu, na akahoji sababu za serikali kuwa mstari wa mbele kuwafunga midomo leo.

Bakwata imezinduka sasa Waislamu wote tumeungana katika kupigania haki zetu na kutetea maslahi yetu na serikali itambue kuwa Bakwata iko hai hao Wakristo walikuwa wapi wakati sisi tukipigania uhuru,alihoji.

Wakati huohuo, Sheikh Salum Rwambo alisema anawashangaa wabunge Waislamu ambao baadhi ni mahajat na malhaj wanakaa kimya na kushindwa kutetea hoja za msingi na kudai kuwa huo sasa ndio mwisho wao wa kuwaita masheikh na kutaka waombewe dua ili wasipate wepesi katika kampeni zao.

Sheikh Rwambo pia alimsifia mbunge wa Nzega Lucas Selelii kwamba ni miongoni mwa wabunge katika Bunge hilo wanaozungumza ukweli na kwa kujiamini tofauti na wengine ambao wanaenda kukaa bila kufanya kazi zilizowapeleka .


CHANZO: Mwananchi


KWA MWENENDO HUU SI AJABU KUSIKIA HATA WATANZANIA WALIOAHIDIWA MAISHA BORA NAO WAKAJITOKEZA KUDAI HAWAITAKI CCM....HOJA IKIWA MAISHA BORA YALIYOAHIDIWA YAMEISHIA KWA KUNDI DOGO LA MAFISADI PEKEE!

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.