5 Dec 2009


TOFAUTI na alivyojigamba kwamba ni mlipaji mzuri wa madeni anayodaiwa na serikali, Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi anadaiwa Sh. 2,576,583,013 tokea mwaka 1993, MwanaHALISI limegundua.

Alikopeshwa Sh. 2 bilioni (2,025,739,660) mwaka 1993 na 1997 na Mfuko wa Kuwezesha Uagizaji Bidhaa (CIS) uliokuwa ukifadhiliwa na serikali ya Japan na kusimamiwa na Wizara ya Fedha na Uchumi.

Alitumia makampuni ya Africa Tanneries Ltd, Tanzania Leather Industries Ltd na Africa Trade Development.

Fedha nyingine alizokopeshwa ni Sh. 1,516,024,125. Hizi alikopeshwa na serikali ili kuagiza mchele kupitia mpango wa Counterpart Fund. Alitumia Kampuni ya African Trade Development.

Imethibitika kwamba Rostam ameshindwa au hataki kulipa deni hilo lililodumu kwa miaka 16 sasa.

Akizungumza na vyombo vya habari 3 Mei 2009, siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es Salaam, Rostam alitamba kuwa ni mlipaji mzuri wa madeni yake kwa serikali.

Alikuwa akijibu tuhuma mbalimbali za ufisadi anaodaiwa kufanya kwa kutumia makampuni yake mbalimbali. Gazeti hili lina kumbukumbu za jinsi alichukua fedha hizo, zilizokusudiwa kuboresha biashara nchini.

Uchunguzi umebaini kuwa mwaka 1993 alichukua Sh. 280 milioni kupitia Kampuni ya African Tanneries Limited. Mwaka 1997 alitumia Kampuni ya Tanzania Leather Industries Limited kuchukua Sh. 725,943,120.

Mwaka huohuo Rostam alitumia Kampuni yake nyingine ya African Trade Development kubeba Sh. 1,019,796,540 kutoka mfuko huo.

Mwishoni mwa mwaka jana, baada ya ‘mshike mshike nguo kuchanika,’ Rostam alilipa Sh. 500 milioni akikusudia kupunguza deni la “mchele.”

Lakini kutokana na kuwepo deni jingine la zaidi ya Sh. 1bilioni katika mfuko wa CIS, mamlaka husika zikaamua kutumia kiasi hicho kupunguza madeni hayo.

Kwa sasa anadaiwa na mfuko huo Sh. 1.060,558,888. Deni hilo likijumlishwa na deni alilokopa kuagiza mchele, Rostam anadaiwa jumla ya Sh. 2,576,583,013. Katika mazungumzo yake na serikali kwa nyakati tofauti, alikiri na kuahidi kulipa ingawa hadi sasa ameendelea kukaidi kulipa.

MwanaHALISI limebaini kuwa tayari mmoja wa wanasheria jijini Dar es Salaam, anayeshughulikia suala la kukusanya madeni hayo anaandaa taarifa ya kisheria itakayokabidhiwa kwa wadeni sugu wakati wowote kuanzia sasa.

Jukumu jingine analotekeleza mtaalamu huyo wa sheria ni kumshauri Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, kufanya mpango wa kutumia mamlaka ya Kamishna Mkuu wa TRA ili kutekeleza azma ya kufilisi mali za Rostam na vigogo wenzake wanaodaiwa.

Pamoja na Rostam, wadeni sugu wengine ambao walizungumza na serikali, wakakiri kudaiwa na wakaahidi kulipa madeni kwa kadri walivyoomba lakini badala ya kulipa wakaingia ‘mitini’ ni pamoja na Mbunge wa Temeke, Abass Mtemvu (CCM).

Mbunge huyo mwaka 1998 alitumia Kampuni ya A.M. General Agency kukopa Yen 20,000,000 sawa na Sh. 280 milioni. Ingawa alikiri kudaiwa na kuahidi kulipa deni, hadi sasa hajalipa hata shilingi moja.

Aliyewahi kuwa Waziri wa Utumishi na Mbunge wa Mlangege, Zanzibar, Fatma Said Ali (CCM), mwaka 1998 alitumia Kampuni ya Tanzania Save Way Co. Ltd., kukopa Yen 20,000,000 lakini akakopeshwa Yen 10,000,000 sawa na Sh.140 milioni. Aliwahi kupunguza Sh. 23,400,000 tu.

Aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wakati wa serikali ya awamu ya pili na ya tatu, ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Henry Shekiffu, mwaka 2000.

Alitumia kampuni ya Shemshi & Sons Limited kukopa Sh. 399,560,000. Amewahi kupunguza Sh. 65,340,051. Hadi sasa anadaiwa Sh. 279,653,794.

Nicodemas Banduka, mwaka 2000 alitumia kampuni ya Kadolo Investment kukopa Yen 105,210045 sawa na Sh. 147,294,630. Aliwahi kulipa Sh. 22,500,000. Hadi sasa anadaiwa Sh.124,794,630.

Mwingine ambaye arobaini zake zimekaribia ni aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), David Mattaka, aliyetumia kampuni ya Petmon Investment, mwaka 2000. Alikopa Sh. 140 milioni, aliwahi kupunguza Sh. 24,712,200. Hadi sasa anadaiwa Sh. 115.287,800.

Ufuatiliaji unabainisha kuwa idadi kubwa ya makampuni yaliyotumiwa na vigogo hao yalianzishwa kwa lengo la kuchota fedha hizo. Mengi kati ya hayo hayapo tena.

Vigogo wengine waliobainika kukopeshwa na CIS lakini taarifa hazielezi kama mali wanazomiliki pia zitafilisiwa, ni aliyekuwa mbunge wa Sengerema, Dk. William Shija ambaye sasa ni Katibu wa Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola.

Alikopa Sh. 140 milioni kwa kutumia kampuni ya Pyramid Investments Limited, mwaka 2000. Amewahi kupunguza Sh. 22,650,000.

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wassira, naye jina lake limo kwenye orodha ya wanaodaiwa ingawa taarifa muhimu, mathalani alikopa kiasi gani, lini na amelipa au bado hazionyeshwi katika kumbukumbu hizo.

Ingawa serikali inaelezwa kuwa kwenye hatua za kukamilisha mipango ya kufilisi mali za wadeni wake hao na wengine, bado inasuasua.

Mkataba wa kufanikisha mikopo hiyo unaruhusu serikali kupitia kwa Kamishna Mkuu wa TRA kufilisi mali za asiyetekeleza mkataba katika kipengele cha kulipa, tena bila kulazimika kwenda mahakamani. Haijafahamika kwa nini TRA haijachukua hatua hiyo.

Dhana inajengeka kwamba huenda “kigugumizi” hicho katika kukusanya madeni ya walipa kodi wa Tanzania, kinatokana na wadaiwa wengi kuwa vigogo ambao miongoni mwao bado wapo kwenye nyadhifa za juu serikalini.

CIS ilianzishwa kwa nia njema ya kukuza sekta ya biashara nchini, kwa kuwasaidia wafanyabiashara kufanya biashara za kimataifa. Kuagiza bidhaa mbalimbali kutoka nchi tofauti, zilizofadhili mpango huo.

Mpango huo ulikuwa ukitekelezwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na Uchumi. Hata hivyo taarifa zinaonyesha kuwa jumla ya Sh. 44 bilioni zilichotwa na wizara nane katika mazingira ambayo hadi sasa serikali haijafafanua.

CHANZO: Mwanahalisi

INAUDHI,INAUMA NA KUSONONESHA LAKINI IT LOOKS AS IF NCHI HAINA WENYEWE KWANI WALIOIBIWA WAKO KIMYA KANA KWAMBA WAMERIDHIKA.JE TUMEKUBALI UFISADI KUWA SEHEMU YA MAISHA YETU YA KILA SIKU?

3 Dec 2009


Sijui tuiweke CCM katika kundi gani maana kila kukicha ni songombingo moja baada ya nyingine.Of course,migongano ni jambo la kawaida kwani hata ukiweka glasi katika boksi moja zinaweza kugongana kama si kuvunjika kabisa.Ndio maana maboksi yaliyosheheni glasi huwa na tahadhari "handle with care" au "fragile".

Pengine kabla sijaendelea na mada yangu kuhusu utovu wa nidhamu unaoendelea ndani ya chama tawala CCM,huku Katibu Mkuu Yusuph Makamba akitoa kauli zisizoendana na hadhi yake katika jamii,ni vema ukasoma habari ifuatayo kisha tujadili kidogo:

Makamba awatukana wanaoshauri Kikwete asigombee 2010

Rais Kikwete kongamano la Nyerere limemweka katika lawama za kutokuwa na maamuzi na kuwa asipendekezwe kugombea awamu ya pili.

Na Leon Bahati
KATIBU mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ambaye katika miezi ya karibuni amekuwa akihaha kutoa ufafanuzi, kukanusha au kujibu tuhuma mbalimbali dhidi ya chama hicho tawala, jana alikuwa na kazi nyingine ya kumtetea Jakaya Kikwete baada ya waziri katika serikali ya awamu ya tatu kushauri asiteuliwe kugombea urais 2010 iwapo atashindwa kufanya maamuzi magumu dhidi ya mafisadi.

Safari hii, Makamba alitumia maneno makali kumjibu waziri huyo, Matheo Qares akisema watu wenye fikra kwamba CCM inaweza kumtosa mwenyekiti wake kwenye mbio za urais wakati wa uchaguzi mkuu wa mwakani, "ni wehu".

Qares, ambaye aliwahi kushika wadhifa nyeti wa Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma, alitoa rai hiyo juzi kwenye kongamano la kumuenzi muasisi wa taifa la Tanzania aliposema kuwa CCM haina budi kutafuta mwanachama mwingine wa kugombea nafasi ya urais mwaka 2010 iwapo Kikwete atashindwa kufanya maamuzi magumu dhidi ya mafisadi, ambao alisema hawakijui chama na wengine uraia wao una utata.

Lakini jana, Makamba alisema watu wenye fikra hizo ni wehu kwa kuwa uteuzi wa wagombea ndani ya CCM ni mchakato usiotoa ruhusa kwa mawazo binafsi ya watu.

"Mtu mwenye akili nzuri hawezi kusema kwamba Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza wajibu wake. Anayefikiria hivyo, ni mwehu," alisema Makamba alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu kauli hizo.

Alisema ni vyema watu hao wakafahamu kuwa mgombea urais wa CCM anateuliwa kwa mujibu wa taratibu za chama kupitia vikao mbalimbali hivyo, wazo binafsi halina nafasi.

Alipoulizwa kuhusu shutuma zinazoelekezwa kwa Rais Kikwete, Makamba alisema asingependa kujibu hoja zilizotolewa na mjumbe mmoja mmoja kwenye kongamano hilo.

Lakini akaeleza kwamba yupo tayari kutoa maoni yake binafsi baada ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuwasilisha kwake mapendekezo waliyofikia kwenye kongamano hilo.

"Mimi mwenyewe sikuwepo kwenye kongamano hilo. Wala sijui mapendekezo yao. Siwezi nikatolea maoni hoja za mtu mmoja mmoja alizotoa kwenye Kongamano hilo. Nitakapopata mapendekezo ya jumla ya taasisi hiyo, nitakawa katika nafasi nzuri ya kutoa maoni yangu."

Katika kongamano hilo, Rais Kikwete amekuwa akilaumiwa kwa kutochukua hatua dhidi ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wengi wao wakielezwa kuwa ni wafanyabiashara ambao wanatuhumiwa kukiteka chama kwa kutumia nguvu zao za pesa.

Wakati fulani Joseph Butiku, mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere ambayo iliandaa kongamano hilo, alisema Rais Kikwete amezungukwa na mafisadi ambao wanaitafuna nchi.

Akizungumza kwenye kongamano hilo juzi, Qares alisema rais hana budi kufumba macho na kuwashughulikia hao watuhumiwa ambao wanadai Kikwete hakujuana nao barabarani na kama atashindwa basi ashauriwe kuwa miaka yake mitano inamtosha.

Kabla ya Qares, Musa Nkangaa, ambaye aliwahi kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya pili, aliituhumu CCM kuwa imepoteza hadhi na kujikuta ikikumbatia matajiri wachafu.

Kwa mujibu wa Nkangaa, CCM imekuwa si chama cha wakulima na wafanyakazi tena, bali kimebaki kuwa chama cha matajiri.

"Ndiyo maana imekuwa ikiweweseka kuwashughulikia watuhumiwa wa Richmond na Kagoda," alisema akimaanisha kashfa ya utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa Richmond Development Company LLC na tuhuma za wizi wa mabilioni ya fedha kutoka BoT.

CHANZO: Mwananchi

Tatizo kubwa la watawala wetu ni yale mazowea waliyojijengea ya kupigiwa makofi na vigeregere hata wanapoongea pumba.Ni katika mstari huohuo,kauli na mawazo mbadala huchukuliwa kuwa ni mithili ya kosa la uhaini.Sidhani kama kuna ubaya kwa wana-CCM kumpa changamoto mwenyekiti wao kama ambavyo Mtanzania yeyote mwenye mapenzi ya dhati anavyostahili haki ya kukemea mwelekeo mbovu wa nchi yetu.

Japo naafikiana na Makamba anapokumbusha wana-CCM wenzie kwamba chama hicho kikongwe kina utaratibu wake wa kumpata mgombea urais lakini hiyo sio sababu ya kuwaziba midomo wale wanaodhani mwanachama mwenzao waliyempitisha kugombea urais katika uchaguzi uliopita,na kushinda,yaani Jakaya Kikwete,ameshindwa kukidhi matarajio ya wana-CCM hao (kama Matheo Qareshi).Sio tusi kutoa mawazo kuwa flani ameshindwa hasa pale kauli kama hiyo inapoambatana na mifano hai kadhaa.

Sidhani kama Makamba anafanya hivyo kwa ile anaamini kuwa Qaresi ni mwehu (ikumbukwe Mtanzania huyo alishawahi kushika nyadhifa za juu ikiwa ni pamoja na uwaziri katika ofisi ya rais) bali ni muendelezo wa kasumba ya kujikomba.Kwa Makamba kumhukumu Qaresi kuwa ni mwehu amekwepa ujasiri wa kujadili hoja badala ya kumjadili mtu.

Ni muhimu tuwe wakweli na wawazi katika kujadili hatma ya taifa letu.Ni dhahiri kuwa vita dhidi ya ufisadi inakwamishwa na mwenye jukumu la kuchukua hatua.Hatuwezi kufanikiwa katika mapambano dhidi ya rushwa (kama yapo at all) ilhali ilishashauriwa kwamba Mkurugenzi wa TAKUKURU,Edward Hosea,ang'olewe madarakani kutokana na kuhusishwa na utapeli wa Richmond.Ushauri huo ulitolewa pia kuhusa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Johnston Mwanyika.Huwezi kuwalaumu Hosea na Mwanyika kwa vile hawakujiteua kushika nyadhifa hizo.Aliyewateua yupo na amesikia yaliyosemwa dhidi yao lakini kaamua kupuuza.

Kwa hakika kama tunataka kuiona Tanzania ikijikomboa kutoka katika lindi la umasikini unaochangiwa kwa kiasi kikubwa na ufisadi,basi ni dhahiri tunahitaji kuangalia makosa yaliyofanyika mwaka 2005 na kuhakikisha hatuyarudii katika uchaguzi mkuu ujao hapo mwakani.Haya mambo ya kuangalia haiba ya mtu na pasipo kujali kama haiba hiyo inaendana na uwezo wa kazi yameshatufikisha hapa,na tukizubaa yatatupeleka pabaya zaidi,

Kinachisikitisha ni mwamko mdogo mingoni mwa Watanzania wa tabaka la kati (the middle class).Tabaka hili lina nafasi nzuri ya kuunganisha nguvu na tabaka la walalahoi ili kulibana tabaka tawala ambalo so far limeji-identify kama sehemu muhimu ya ustawi wa ufisadi na mafisadi.

Inawezekana kabla hatujachelewa.






Honorable office of Senate
Federal Republic of Nigeria
Senate Building Wuse Abuja


FROM; Senator. David Mark,
Senate President Federal Republic of Nigeria.

Dear Beneficiary,

SENATE COMMITTEE ON OUTSTANDING FOREIGN PAYMENT.

May i use this juncture to notify you that our new Government have Paid the bills
which was the cause of the delay of your Payments, and the Office of presidency in conjuction with Senate Commette on outsatnding Foreign Payment have Concluded arrangement with Central Bank of Nigeria and BCEAO to raise International Certified Bank Draft in the tone of $1,000,000.00 (One Million United Staes Dollars) and send across to you upon receipt of the bellow informations through, there Accredited Attoney.

WARNNING/ADVISE: Please note carefully that any fee of any kind DOCUMENTATIONS, COURIER, BRIBE OR GIFT requested from you by anybody, office,banks or group of people from Africa/Nigeria or any part of the world to receive your payment,Except legal fee of the R.E.D.L of FORCE OF NATURE which is just $150.00. is at your OWN RISK, so stay away from any other office, person or group of people and commence communication with only the Central Bank of Nigeria Carredited Attorney till you receive your Certified Bank Draft Deposit With your Bank and Confirm your part payment within Three Bank Working days.

We are really sorry for all the incoviniences you have suffered in the cost of receiving your funds from our Government. Also we assure you that we are doing everything possible to release the Balance of your payment to you by Janaury 2010. we wish to effect this part payment of $1,000,000.00 through the International Certified Draft system to avoid another stress of K.T.T and so on with our banks.and our Government has mandated and paid the FEDEX COURIER SERVICE for the services of delivery the Draft to you.

Therefore, YOU have to get in touch with Central Bank of Nigeria Acredited Attorney Barr. Mike Obi via email or telephone immediately. Below are his contacts

Contact Attorney In-charge : Barr. Mike Obi Tel: 234-1-7652522 EMAIL:([email protected])

Fill bellow informations and Send back to him with R.E.D.L FORCE OF NATURE fee of $150 only. to enable him proceed with the procument of your R.E.D.L FORCE OF NATURE PERMIT from the Legal Department and submit to the Central Bank of Nigeria for onward issuance of your International Certified Draft.

* Full Names.................
* Address. (not P.O.Box)..............
* City..................
* State.................
* Postal Code...........
* Phone.................
* Fax.......................
* Email................
* Age...................
* Marital Status...............
* Sex...............


CHEERS ,
Senator David Mark
Senate President Federal Republic of Nigeria.

30 Nov 2009


When 50 Cent ended his 2003 relationship with actress Vivica A. Fox, the two exchanged insults so harsh that there was no chance for a reconciliation. Until now!

Six years after they split, 50 Cent confirms their newfound friendship on The Tyra Show Tuesday.

See photos of Hollywood's ugliest splits!

"I called her," the rapper, 34, says.

Tyra Banks admits she was shocked they reconnected.

"I'm confused because you guys had beef. You were saying crazy stuff about her," Banks tells 50 Cent. "She even came on this show, and she was not very happy with you."

Find out which stars fared better after a bad breakup

50 Cent says that he dated Fox, 45, for "about a year," despite reports that it was only a month-long romance.

Check out more couples who had many years between them

"It was like a month, but we were still going back and forth with each other for the rest of the year," he said, adding that after their public blowout, "she was really upset with me."

His olive branch?

"I said, 'You got to stop fighting and be in my video,'" he says of his latest music video, "Do You Think About Me."

He says they are now friends. As for whether they'll ever date again, 50 Cent is not counting on it.

Take a look at stars who did reunite their romance

"The song's about when relationships don't work, and when I explained it to her it kind of intensified what the song was about," he says. "And it's now being a visual with the public sees us as that relationship that didn't work."



(AFP) – 7 hours ago

PORT OF SPAIN — Tanzania has fiercely denied allegations said to come from the United Nations that it has illegally funneled arms to Rwandan Hutu rebels in the Democratic Republic of Congo.

"It is simply not true. It is an outright malicious lie being concocted with the evil intention of tarnishing the good name of Tanzania and our government," Tanzanian Foreign Minister Bernard Membe said in a statement late Saturday.

"Tanzania has never and will not even contemplate to indulge in such despicable, reckless and worthless causes of trafficking in arms which foment violent conflicts against friendly neighbors like Rwanda and the DRC."

Membe, attending a Commonwealth summit in Trinidad, also demanded an apology from the United Nations, saying the allegations were contained in a report for the UN Security Council.

He said the allegations were based on "second hand quotes, hearsay, farfetched assumptions and stretched extrapolations."

In the report, as yet unpublished and seen by AFP, researchers said this year's attempts by Congolese, Rwandan and UN forces to disarm Rwandan Hutu rebels in eastern DR Congo have not succeeded and global action is needed to cut off their funds.

"This report concludes that military operations against the FDLR have failed to dismantle the organization's political and military structures on the ground in eastern DRC," the detailed 93-page document begins.

The report alleges that the FDLR recruits and arms fighters using profits from a corrupt international trade in minerals, and calls on the international community to step up efforts to cut off rebel funds.

The militia sprang up in camps in the east of the Democratic Republic of Congo (DRC) housing mainly ethnic Hutu refugees who fled Rwanda after their leaders launched the 1994 genocide, which left some 800,000 people dead.

The document was researched on the ground in Congo and the region over six months by a five-strong stream of experts hired by UN Secretary General Ban Ki-moon.

It was addressed to the chairman of the UN Security Council committee on September 9. It is not known when it will be published.

29 Nov 2009



In 2002, one in every 109 £1 coins was a fake. Today it's one in 40. A former counterfeiter reveals how to spot the fake in your pocket... and asks the question: bearing in mind you can't swap one for legal tender, would you throw yours in the bin?



28 Nov 2009



KINGSTON, Jamaica

RAIS Jakaya Kikwete ametaka ushirikiano zaidi kati ya Jamaica na Tanzania katika nyanja za muziki na michezo.

"Jamaica ina wanariadha wenye kasi zaidi duniani kwa sasa," alisema kwa kusifia.

Alisema kuwa muziki wa rege ni maarufu zaidi nchini Tanzania, huku akimtaja nyota wa muziki huo, Bob Marley kuwa ni maarufu zaidi nchini mwake.

Kikwete aliiomba Jamaica kuisaidia nchi yake kwa kuwapatia kocha wa ajili ya kuendeleza mchezo wa riadha.

Kiongozi wa Upinzani, Portia Simpson Miller alimweleza Kikwete kuwa wanachama wa chama chake, People's National Party nao wako tayar kushirikiana na Tanzania.

CHANZO: Mwananchi

Alimshauri rais aanzishe ofisi nchini kuratibu shughuli za ushirikiano katika ukanda wa Karibiani.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.