13 Mar 2010


Wiki hii tumeadimisha siku ya wanawake duniani.Na kesho ni siku ya mama zetu.Ni kipindi mwafaka cha kungalia mchango wa jinsia ya kike katika ngazi ya familia hadi taifa.Tukubali tusikubali,dunia imeendelea kutawaliwa na mfumo dume.Na bara letu la Afrika (na pengine sehemu kubwa ya Dunia ya Tatu) haki za akinamama na mchango wa jinsia ya kike vimeendelea kupuuzwa.Kwa bahati nzuri kwangu,kabla wiki hii muhimu haijamalizika nilipata wasaa wa kuongea na bloga maarufu wa Kitanzania,Sarah Peter,mmiliki wa blogu ijulikanayo kama ANGALIA BONGO. Sihitaji kumpamba kwani ukitembelea blogu hiyo utaafikiana nami kuwa binti huyu licha ya udogo wake wa umri ana kipaji cha hali ya juu katika kuwasilisha ujumbe wake kwa wasomaji wa blog yake na jamii kwa ujumlaNimejijengea mazingira ya kutembelea takriban blogu zote za Watanzania wenzangu kila siku,au angalau mara kadhaa kwa wiki.Licha ya idadi kubwa ya blogu hizo kuwa kwenye blogroll yangu,nina orodha kubwa ya subscription kwenye Google reader,na inanisaidia sana kufahamu kinachoendelea kwenye blogsphere.



Back to Sarah.Nilianza kublog mwaka 2006 na tangu wakati huo blogging imekuwa sehemu muhimu ya maisha yangu.Lakini hadi jana nilikuwa sijakutana na bloga ambaye ndani ya dakika chache alinifumbua macho kwa kiwango kikubwa as to wapi panahitaji marekebisho bloguni mwangu na namna nyingine za kunoresha uwanja huu.Lakini ukidhani hilo ni kubwa zaidi,basi tembelea kwanza hiyo blog ya ANGALIA BONGO kisha utapata picha nzuri zaidi ya nachokieleza.



Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kuhusu blog hiyo hasa kiu yangu ya kumfahamu vema mmiliki wake.Awali nilidhani kuwa Sarah ni 'mtu mzima' (kiumri) kwani nyingi ya posts zake zimesheheni upeo unaoendana na utu uzima.Tofauti na dhana hiyo,kumbe Sarah ni binti aliyezaliwa miaka ya 80 hivyo ana miaka ishirini na kitu (lakini haifiki 25).Kwa kifupi,ni binti mdogo mwenye akili kubwa na kipaji cha hali ya juu.Na siandiki hivi kwa minajili ya 'kumpa ujiko' (hata ningekuwa nafanya hivyo ingekuwa kazi bure kwani tayari ana 'ujiko' wa kutosha)bali ni katika kutambua mchango wa jinsia ya kike katika fani ya habari hususan kwenye matumizi ya vipasha habari vya jamii (social media) kama blogu.



Hata hivyo,pamoja na mwonekano maridhwawa wa blogu ya ANGALIA BONGO na habari zenye kila ishara kuwa aliyeandika anajua vema anachofanya,kumwelewa vema Sarah kunahitaji uongee nae kama ilivyotokea kwangu jana.Alinipa darasa la chapchap kuhusu mambo mbalimbali ya maana.Na mie ni mwanafunzi mzuri napokutana na mwalimu mzuri.Na haikuchukua muda kwangu kabaini kwamba binti huyu ana akiba kubwa ya akili na kipaji,na hadi sasa kinachotumika ni kiasi kidogo tu cha kipaji na akili hiyo.Sasa kama kiasi kidogo ndio mambo makubwa namna hiyo,ni dhahiri kuwa bloga huyu atakuwa mbali sana akiamua kutumia uwezo wake wote(na anasema atafanya hivyo mbeleni).



Ukiangalia picha zake,unaweza kumhukumu isivyo.Ana mwonekano wa 'kisistaduu' (sina tafsiri sahihi ya neno hili) na ni rahisi kudhani ana 'pozi' (maringo).Lakini hata kama angekuwa hivyo (i.e. sistaduu mwenye pozi),which she is not,character hizo zingefunikwa na kipaji na upeo wake.Sarah anaeleza kwamba yuko into many stuffs japo amebobea zaidi kwenye mambo ya burudani (entertainment).Licha ya background yake kama journalist na radio producer,uwezo wake wa kufikiri na kuandika haraka unachangia sana kuifanya blog yake kuwa mahala pa kumridhisha kila msomaji anayepatembelea.Lakini kingine kinachopendeza katika wasifu wa binti huyu ni imani yake ya kiroho.Anasema kuwa dini ni kitu muhimu sana katika maisha yake,na kwa kuthibiths ahilo ameandika I...always believe in Jesus, Remember İm a pure Christian.Imani thabiti katika dini inasaidia sana kuimarisha vipaji na kutanua upeo,na ni ishara ya karama za Muumba.



Ni dhahiri kuwa bloga huyu ana nafasi ya kufanya mambo makubwa huko mbeleni,na ni matarajio yangu kuwa siku moja Sarah ataitangaza nchi yetu si tu kupitia blog yake bali pia katika fani flani muhimu.Nilimtania kuwa this time in 2012 or so natarajia kumuona akiwa katika delegation ya Mama Asha Rose Migiro,sio kwa vile ni Mtanzania mwenzake bali akiwajibika katika wadhifa flani.Na kama si hilo,basi sintoshangaa akija na chapisho kama Ebony au The Source ya kitanzania.

Kila la heri Sarah!


Moja ya maeneo yeynye kuhitaji mtazamo mpya katika Tanzania ni haki za raia.Ni ukweli usipingika kwamba nchi yetu ina haki za aina mbili: kwa wenye nacho/vigogo na kwa walalahoi.Kuna mifano mingi ya kuthibitisha hilo lakini hapa nitaonyesha mifano michache kuokoa muda.Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge alipopata ajali iliyopelekea vifo vya watu wawili,jeshi la polisi lilikurupuka kuunda tume ya kuchunguza ajali hiyo.Baada ya ajali hiyo,zimetokea ajali nyingine kadhaa zilizopelekea vifo vya watu kadhaa lakini hatujasikia jeshi la polisi likiunda tume kuchunguza ajali hizo.Jibu jepesi ni kwamba waliopoteza maisha kwenye ajali hizo si vigogo hivyo 'hakukuwa na umuhimu kwa kuundwa tume za uchunguzi'.Mfano mwingine ni kauli ya Rais Mstaafu Ben Mkapa kwamba wanaoajiri mahauziboi na mahazigeli wanapaswa kuwa na mafaili ya waajiriwa wao ili pindi likitokea tatizo wapatikane kirahisi.Mkapa aliyasema hayo alipoenda kumpa pole Balozi Andrew Daraja kufuatia mauaji ya mkewe ambayou yanadaiwa kufanywa na hauziboi wa balozi huyo. Kwanza,tukio zima la kifo cha mke wa Balozi linatengeneza mazingira ya ukiukwaji haki za hauziboi husika.Ieleweke kuwa nami nimeguswa na mauaji hayo ya kinyama lakini hiyo haiwezi kuhalalisha jamii kujichukulia sheria mkononi na kumhukumu hauziboi huyo.Jeshi la polisi ndilo lenye mamlaka ya kuchunguza mauaji hayo na kisha kuiachia mahakama itoe hukumu.

Twende kwenye ushauri wa Mkapa.Kwa mawazo ya Rais huyo mstaafu,kuwa na mafaili yenye taarifa za mahauziboi na mahauzigeli kutasaidia kuwapata kirahisi pindi wakihusishwa na vitendo visivyofaa.Mkapa anaelekea kuthamini zaidi haki za vigogo wenzie wanaoajiri mahauziboi na mahazigeli huku wakilipwa mishahara kiduchu na kutumikishwa kama watumwa,ilhali anapuuza haki za waajiriwa hao ambao ni adimu kwao kuwa na mikataba ya ajira huku ajira zenyewe zikiwa mithili ya maandishi ya chaki ubaoni (blackboard).Ukijisugua tu na ubao,yanafutika.

Japo wazo la Mkapa sio baya kihivyo,lakini kwanini lije wakati huu ambapo hauziboi anahusishwa na mauaji ya mke wa mwanadiplomasia Daraja?Ni hadithi zilezile za barabara kukarabatiwa kukiwa na ziara za viongozi wakati zimesahauliwa miaka nenda miaka rudi kwa vile tu watumiaji wa barabara hizo si vigogo.Kama kulikuwa na umuhimu wa kuwepo mafaili yenye taarifa za watumishi wa ndani basi isingehitaji kusubiri hadi hauziboi atuhumiwe kumuua mke wa balozi.

Na ni kwa vile walalahoi hawana uwezo wa kumudu kuajiri wanasheria wazuri lakini kwa namna 'jamii ilivyokwishatoa hukumu dhidi ya hauziboi wa Balozi Daraja' ni dhahiri kesi yake mahakamani ingestahili kufutwa kwani 'ameshahukumiwa uraiani'.Mkapa alipaswa kutambua kuwa kauli yake kama Rais Mstaafu inaweza kabisa kutafsiriwa kuwa nae amefuata mkumbo wa kuamini kuwa 'ukiwa mlalahoi na ukatuhumiwa,basi unabaki mkosaji hadi itakapothibitika vinginevyo' (guilty until proven innocent).

Mlalahoi Jerry Muro alipotuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa mtuhumiwa wa rushwa (funny,isn't it?),kamanda Kova na vijana wake wakakurupuka chap chap kutujulisha kuwa jeshi lake lina teknolojia za kisasa za kufuatilia wala rushwa (sijui kwanini hawajashea ujuzi huo na TAKUKURU).Lakini wakati Kova akituaminisha mazingaombwe hayo,tunabaki na maswali kwamba kama vyombo vyetu vya dola viko makini kiasi hicho ilikuwaje basi wale majambazi wa EPA walimudu kutuibia mabilioni yetu pale Benki Kuu,mahala paliposheheni mitambo ya kisasa ya ulinzi?Au kwani teknolojia iliyotumika kumnasa Muro haikutumika kuwabaini majambazi wa Richmond?Na kwanini isitumike kumfahamu Kagoda ni mdudu wa aina gani?

Jibu rahisi ni kwamba Muro aligusa maslahi ya wakubwa (na vijana wao in the name of Jeshi la Polisi) na wakaamua kumpa 'jambajamba' (excuse my language) ili 'atulie'.Chenge ameendelea 'kutanua' licha ya tuhuma za vijisenti vyake vyenye thamani ya bilioni huko visiwani Jersey.Na bado teknolojia ya jeshi la polisi iliyomnasa Muro haijafanikiwa kuona kama Chenge anastahili kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.Jawabu la utata huo ni jepesi: Chenge ni kigogo,na Muro ni mlalahoi.

Magereza yetu yamesheheni wezi wa kuku na vibaka wengineo huku majambazi halisi wa uchumi wetu wanaendelea kutudhihaki mitaani wakiwa kwenye ma-vogue yao ya bei mbaya.Tanzania yetu imefika mahala ukijaribu kukemea uovu unaohusisha vigogo unaonekana kama mhaini,na utaandamwa zaidi ya Wamarekani wanavyomtafuta Osama bin Laden.Na kwa huko mtaani,ukiwa na bahati mbaya ya kuwa na mke/mpenzi mzuri anayetamaniwa na kigogo,andika umeumia.Nakumbuka hadithi ya jamaa mmoja aliyepewa kitengo nje ya nchi ili kigogo aliyekuwa anatoka na mkewe apate wasaa mzuri wa kufaidi 'haki za vigogo zilizoangukia kwa bahati mbaya kwa mlalahoi'.

Ni katika mazingira hayo ndio maana baadhi ya watu wanadiriki kuamini kwamba laiti Babu Seya na wanae 'wasingegusa haki za vigogo' angeendelea kuwa uraiani akitumbuiza na bakulutu zake.Siungi mkono ulawiti lakini wajuzi wa kona za Dar es Salaam wataafikiana nami nikisema kuwa kuna vigogo wengi tu wanaofanya michezo michafu kwa vibinti vidogodogo mitaani lakini wadhifa wao unawalinda,na wanaishia kuitwa 'viwembe' badala ya kuwa jela kama Babu Seya.Again,mwanamuziki huyo na mwanae Papii Kocha wako 'mbele ya sheria' kwa vile ni walalahoi na si uzito wa makosa yao.Nithibitishie kuwa siko sahihi (prove me wrong).

Wito wangu kwa walalahoi wenzangu ni huu: kaa ukitambua kuwa sheria na haki nchini mwetu zina sura mbili: upofu kwa makosa ya vigogo na macho makali (hata kwenye giza) kwa walalahoi.Fanya manjonjo yako ukitambua ukweli huo mchngu,ukigusa 'haki' za vigogo,andika umeumia.Tambua kwamba wanywa gongo huko Uwanja wa fisi wanapokamatwa na vyombo vya dola (mara nyingi hawanywi pombe hiyo hatari kwa vile hawajali afya zao bali uchumi mbovu) tunaambiwa kosa lao ni kutumia kinywaji hicho haramu lakini ikitokea vigogo na watoto wao wakajihusisha na kuuza na kutumia madawa ya kulevya,hawagusiw kwa vile 'ni haki yao kujistarehesha' (ndio maana ile orodha ya wauza unga ambayo ex-minister Mwapachu aliikabidhi kwa JK haijafanyiwa kazi hadi kesho).

Ni ukweli mchungu na unaoumiza lakini ubaki ukweli na hali halisi.By the way,Waingereza wanasema TRUTH HURTS!

12 Mar 2010

 Habari zilizotawala vyombo vya habari vya hapa Uingereza ni kufikishwa mahakamani kwa wabunge watatu wa chama tawala (Labour) na mbunge wa bunge la mabwanyenye kutoka chama cha Conservatives.Kwa pamoja wabunge hao wanatuhumiwa kufuja fedha .Wabunge hao, Elliot Morley, David Chaytor na Jim Devine wa Labour na Lord Hanningfield wa Conservatives wanashtakiwa kwa ubadhirifu wa jumla ya takriban pauni 60,000 za mafao ya wabunge.Wakati hayo yakitokea hapa katika nchi ambayo ni wafadhili wetu wakubwa,hadi muda huu sie tumeendelea kuwekwa kizani kuhusu mdudu aitwaye Kagoda,huku mtuhumiwa wa ufisadi wa rada na wale wa ujambazi wa Richmond wakiendelea "kupeta". Ni dhahiri kwamba watawala wetu hawako serious na mapambano dhidi ya uhalifu wa vigogo.Hebu angalia mfano mwepesi wa ishu ya mtangazaji wa TBC,Jerry Muro.Japo blogu hii si mahakama ya kuamua kama mtangazaji huyo hana hatia au,kasi ya vyombo vya dola katika kushughulikia 'tuhuma' dhidi yake zilikuwa kubwa sana tofauti na namna vyombo vya dola vinavyojiumauma hadi leo kuhusu majambazi wa kampuni ya Kagoda waliokwiba shilingi bilioni 40 katika utapeli wa EPA.Watawala wetu wameendelea kuweka pamba masikioni na kupuuza kilio cha umma kuhusu haja ya angalau kutajiwa wamiliki wa kampuni hiyo ya kijambazi.

Ndio maana blogu hii imeendelea kuiona sheria mpya ya kudhibiti rushwa katika chaguzi kuwa ni mwendelezo wa ahadi lukuki za kunoresha ustawi wa taifa letu lakini ahadi hizo zimeendelea kuwa viinimacho visivyotekelezeka.Sheria hii inaweza kupelekea waheshimiwa wawili watatu kutiwa nguvuni (kama TAKUKURU watashikiwa silaha kuwezesha hilo), vichwa vya habari vitasomeka kwa herufi kubwa kwamba sheria imeanza kufanya kazi.Lakini kana kwamba wana ugonjwa wa kusahau historia,baadhi ya wanahabari wetu watazembea kurejea matukio ya nyuma ambapo kesi kama za akini Profesa Mahalu,na hizi za karibuni za Mramba na Yona zinaendelea kusuasua mahakamani pasipo dalili za haki kutendeka-kwa watuhumiwa na walipakodi wa Tanzania.

Watakaonaswa baada ya sheria hiyo 'kuanza kutumika' watakuwa mithili ya 'muzi wa kafara',na 'changa la macho' kuonyesha umma kuwa sheria inafanya kazi lakini mwisho wa siku itaishia kuwa 'flani kafikishwa mahakamani',and that's it.Suala sio kumfikisha mtuhumiwa mahakamani bali haki itendeke,na sio itendeke tu bali ionekane imetendeka.

Yayumkinika kusema kuwa kesi za EPA zinazoendelea kwa mwendo wa kinyonga hazikidhi haja ya umma hasa kwa vile japo wote ni watuhumiwa lakini wale wa Kagoda waliiba fedha nyingi zaidi.Cha kushangaza ni kwamba hadi leo wameendelea kuhifadhiwa.Sasa tukisema ufisadi ni sera ya CCM tutaambiwa tumekosa nidhamu?

Tukio la kufikishwa mahakamani kwa wabunge hawa wa Uingereza kunapaswa kutufumbua macho kwa vile kama nchi inayotufadhili iko hailei wabadhirifu iweje sie tunaotegemea misaada tunakuwa na 'sintofahamu' katika kuwachukulia hatua mafisadi?Hivi kuna sababu za msingi kwanini hadi leo Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge hajafikishwa mahakamani kuhusu vijibilioni vyake huko visiwani Jersey?Basi hata kama wanamwonea aibu,yaani CCM wanashindwa hata kuona haya kwa mtuhumiwa huyo kuwa mwenyekiti wa kamati yake ya maadili?Au ufisadi ni sehemu ya maadili katika chama hicho?

Wakati tukiendelea kuaminishwa kuwa sheria hiyo ya kudhibiti rushwa kwenye chaguzi itakuwa 'kiboko' ya rushwa,toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema lina habari kuwa rushwa inamwagwa katika majimbo kadhaa kama wahusika hawana akili nzuri.Sijui huko ni kumkejeli Rais Kikwete aliyetamka bayana kuwa atasaini sheria hiyo kwa mbwembwe au ni kuujulisha umma kuwa CCM na rushwa ni damu damu!Kilicho wazi ni kuwa hakuna mgombea wa CCM atakayefanikiwa kupitishwa na chama hicho pasipo kutoa rushwa.Hilo halihitaji mjadala.Na kama Rais Kikwete anaamini kuwa sheria anayoipigia jaramba itakomesha rushwa kwenye chaguzi,basi ni vema naye akatafakari upya kama kuna umuhimu wa kuendelea kuwa kiongozi wa watu wasioafikiana na mtizamo wake.

Kinachosikitisha zaidi ni namna jamii isivyoonekana kukoseshwa usingizi na namna nchi yetu inavyozidi kutafunwa na mafisadi.Angalia mwitikio wa wananchi kuhusu 'makamanda wa vijana' wa CCM.Hivi watu hawajiulizi hawa makamanda walikuwa wapi siku zote kiasi cha kukurupuka ghafla kufishana makoti na joto lote hilo kwa kifuniko cha 'ukamanda wa vijana'?Na huo ukamanda unawasaidiaje vijana husika?Kwanini makamanda hao wasielekeze nguvu zao katika kupambana na ufisadi? Kwa asiyefahamu 'siri ya ukamanda wa vijana' basi aelewe kuwa kila anayevikwa wadhifa huo ni 'mgombea mtarajiwa'.Ni namna ya kujiweka karibu na wapiga kura.

Lakini sina tatizo sana na makamanda hao bali hao wanaoaminishwa kuwa ili waendelee wanahitaji makamanda wa vijana.Mie ni muumini mkubwa wa wazo kwamba UFISADI ni kikwazo nambari wani cha maendeleo yetu,au sababu kubwa ya kwanini tumeendelea kuwa masikini wa kutupwa licha ya utajiri lukuki wa maliasili tulionao.Logic yangu ni simple.Huwezi kujaza maji kwenye ndoo yenye matobo au kujaza upepo kwenye mpira uliotoboka.Paipo kudhibiti ufisadi na mafisadi,maendeleo yataendelea kuwa ndoto inayogeuka ukweli mchungu kila kukicha.

Na tukitegemea kwamba wanufaika wa ufisadi watajumuika nasi katika kukomesha kilekile kinachowawezesha 'kutanua' na ma-vogue,mahekalu ya bei mbaya na nyumba ndogo zisizohesabika basi tutaendelea kusubiri milele,au kwa lugha nyingine,TUANDIKE TUMEUMIA.

FUNGUKA MACHO,WAKATI NI SASA!.

10 Mar 2010

TAkukuru
Katika toleo jana la gazeti la Mwananchi kuna habari kwamba Mbunge wa Nyang’hwale,James Musalika, alilazimika ‘kuingia mitini’ kuwakwepa makachero wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) waliokwenda katika ‘hafla’ kati ya mbunge huyo na wapiga kura.Kwa mujibu wa Mwananchi,hatua hiyo ya wanadola wa TAKUKURU ni katika utekelezaji wa ‘ruhusa’ waliyopewa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete ‘kudhibiti wanasiasa wanaotoa rushwa kwenye chaguzi’.

8 Mar 2010


Blogu yako inaendelea kuja na mabadiliko ya hapa na pale lengo likiwa kukupatia wewe msomaji mpendwa 'ile kitu roho inapenda'.Katika kutekeleza azma hiyo,blogu hii inatarajia kuwaleta mahojiano na watu mbalimbali ambao kwa namna moja au nyingine wana mchango katika kulitangaza jina la nchi yetu. Kadri mambo yatakavyokwenda sawa,walengwa wa mahojiano hayo ni pamoja na wasanii wetu,wanasiasa (hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu),wanamichezo,pamoja na makundi mengine ya kijamii

Kwa vile blogu hii ni yako wewe msomaji mpendwa,na mimi ni mtumishi wako tu,basi nakaribisha maoni ya nani ungependa kuona anafanyiwa mahojiano.Mimi nitajaribu kutuma maombi ya mahojiano hayo,na nikifanikiwa,nitayatundika hapa bloguni.Ili kutoweka ubaguzi wa aina yoyote,blogu hii inakaribisha pia Mtanzania yeyote anayeona kuwa kwa nafasi yake na popote pale alipo anaiwakilisha Tanzania yetu kwa namna moja au nyingine.

Mahojiano hayo yatakuwa katika mfumo wa maandishi japokuwa mipango ya muda mrefu ni kuwa na mahojiano ya sauti pia,na ikiwezekana,mahojiano ya video.Kwa watakaotumiwa maombi ya mahojiano,au kwa wanaotaka kuhojiwa,hii inaweza kuwa fursa nzuri kwao kutangaza vipaji vyao au shughuli zao hususan nje ya Tanzania.Kadhalika,mahojiano hayo yatakuwa aidha kwa Kiswahili au Kiingereza kutegemea maafikiano na mhojiwa.Baadhi ya mahojiano hayo yatafanyika kwa Kiswahili na kutafsiriwa kwa Kiingereza ili kutoa fursa sawa kwa wasomaji wa blogu hii ambao hawafahamu Kiswahili.

Stay tuned, more to come in 2010.


It's nearly less than seven months before Tanzanians go to poll to elect,among others, the 5th phase president,should all go well.However,none of the major opposition parties have so far come up with any names of their potential presidential candidates.Does this imply that they have indirectly endorsed a potential CCM candidate,the incumbent president Jakaya Kikwete?The Swahili word for it is 'kusuasua'.Arguably,that's how one could describe opposition politics in Tanzania.Nearly two decades after Tanzania embarked into multiparty politics,most,if not all,of the country's opposition parties have been a hughe disappointment.It could well be concluded that Tanzanians are yet to benefit from the considerably huge number of opposition parties.They are more popular for their seemingly incessant internal skirmishes than their polices or service to the society.Although the ruling party CCM has frequently been accused of meddling into the Opposition's affairs,the truth remains that they are either too weak or too disorganised to pose any serious challenge to the ruling party.

The first multiparty elections saw the perceived might of NCCR Mageuzi,a party that was seen as a serious contender for the ruling of the country.However,sooner after the party lost miserably to CCM,it embarked into a bitter power struggle that eventually led to its chairman,and one of the four 1995 presidential candidates,Augustine Mrema,to switch sides to join TLP.

The next two elections in 2000 and 2005 continued to be the same sad story as CUF and Chadema succeeded in pulling huge crowds during their campaign rallies but only for them to receive meagre number of votes.

Although Chadema emerged fairly stronger in the elections after winning a substantial number of seats in local elections,and has so far gained considerable support in its outspoken stance against economic sabotage (ufisadi) it has so far failed to project any personality that voters could take as a serious contender against Kikwete.And with election looming,the party seems more concerned with increasing their share of parliamentary votes than winning the presidential seat.

The opposition is well aware of how strong CCM remains despite its poor record in delivering its election promises.While opposition parties have an uphill task of convincing potential members and supporters to join them,the ruling party has a distinct advantage from the pre-political reform era where membership to the party was compulsory.That's on top of the current de-facto single-party political environment in which all the characteristics of a one party state prevail except for the legal and constitutional provisions making it official.

One would have expected that by now the opposition parties should have started the process of nominating their presidential candidates process if their participation in the coming election is to make any difference. Faced with acute financial and logical constraints,and with such limited time left before the election,it's fair to conclude that the opposition parties have 'informally' endorsed a CCM candidate even without making such a stance public.

While this blog has nothing personal against such an 'endorsement',it is disaapointed to see how 18 years of opposition politics have produced so little hope to Tanzanians and therefore leaving them with no other choice than continuing to vote for CCM,a party that is so out of touch with voters.Once they lose the election,which is becoming most likely,they (opposition parties) would certainly repeat same old excuses such as calling for an independent electoral commission and constitutional reforms,all of which would brand CCM as a culprit in sabotaging democratic development in Tanzania.However,unless the opposition parties clean up their act,they are doomed to continue to perform dismally in every election.

6 Mar 2010


CCM kinara wa rushwa

Yahya Charahani

WAKATI vita dhidi ya ufisadi ikionekana kupoteza mwelekeo, Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndicho kinachoongoza kwa rushwa nchini, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Matokeo ya utafiti huo, unaojulikana kama 'Mapambano ya Rushwa kwenye Serikali za Mitaa' ambazo unalenga ngazi za vitongoji, vijiji, mitaa na kata', yalitangazwa jana jijini Dar es Salaam na mtafiti kiongozi wa jopo la utafiti, Profesa Suleyman Ngware wa Taasisi ya Taaluma na Maendeleo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (IDS).

Watafiti wengine waliokuwapo katika jopo hilo ni pamoja na Peter Tumaini-Mungu, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (IDS), Anthony Kiberiti wa Takukuru na Stephen Ndaki wa Takukuru.Kwa mujibu wa utafiti huo, CCM inaongoza katika kujihusisha na vitendo vya rushwa kwenye uchaguzi kwa kuzoa asilimia 49.5, ikifuatiwa na Chadema 7.0, CUF 2.7, NCCR 0.5 na TLP iliyoambulia asilimia 0.5.

Hata hivyo, utafiti huo umeonyesha kuwa CCM, ambayo ilitingishwa na vita dhidi ya ufisadi iliyoendeshwa kijasiri na kikundi cha wabunge kabla ya jitihada hizo kupunguzwa kasi, imetambulika kama chama kilichoamka zaidi katika mapambano na rushwa baada ya kujinyakulia asilimia 45.1, ikifuatiwa na Chadema kilicho na asilimia 16.0 na CUF yenye asilimia 6.8.

Ngware aliwaambia wadau mbalimbali kutoka Tamisemi, baadhi ya wakurugenzi wa miji, manispaa na jiji, mameya, wenyeviti wa halmashauri, Tume ya Uchaguzi ya Taifa, wanaharakati, wanasiasa na wanahabari jana kuwa utafiti huo uliofanyika kwa miezi sita, kati ya Mei na Novemba 2009, ulihusisha katika 41 zilizo kwenye wilaya 11 zilizo ndani ya mikoa saba.

Alisema kuwa jumla ya watu 380 walihojiwa (233 wakiwa wanaume na 167 wanawake) kutoka kada mbalimbali za jamii, wakiwamo wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, maafisa wa Tamisemi, makamanda wa Takukuru, mameya na wenyeviti wa halmashauri za wilaya.

Wengine ni wakurugenzi wa halmashauri, viongozi wa dini, wanasheria, madiwani, viongozi wa vyama, wabunge, wanaharakati, wakuu wa shule na wananchi wa kawaida.

Alitaja mikoa hiyo kuwa ni Arusha, Dar es Salaam, Kilimanjaro, Manyara, Morogoro, Dodoma, na Tanga.

"Utafiti huu tumeufanya katika ngazi ya chini kabisa, ambayo ni pamoja na kata, vijiji na wilaya. Umewajumuisha watu wa rika zote ambao tulikuwa tukiwauliza maswali mbalimbali kuhusu rushwa," alisema Profesa Ngware.

"Lengo la utafiti huu ni kuweka msingi wa majadiliano baina ya wananchi na serikali kwa sababu njia hii pekee ndio inaweza kuleta majadiliano na siku zote majadiliano ni mwanzo wa kutatua matatizo."

Kwa mujibu wa Profesa Ngware, wananchi wanatambua uwapo wa Takukuru na mapambano yake dhidi ya rushwa kwa asilimia 79.5, ikifuatiwa na polisi asilimia 31.1, Tume ya Uchaguzi asilimia 18.6, Mamlaka za mikoa na manispaa asilimia 12.4 na waangalizi wa uchaguzi asilimia 7.5, lakini hawaridhiki na ufanisi wao katika mapambano na rushwa.

Alifafanua kuwa lengo kuu la utafiti huo lilikuwa kujifunza hali ya rushwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2009. Kiwango cha tatizo hilo, mbinu zitumiwazo kutenda kosa hilo, wahusika wakuu, mitazamo ya wananchi kuhusu suala la uongozi na rushwa na mbinu na mikakati inayofaa kutekelezwa kupambana na janga hilo.

Kuhusu swali lililouliza kama uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2004 ulikuwa huru na wa haki, asilimia ya jumla ilionyesha 63 kuwa ulikuwa huru na wa haki huku asilimia nyingine 24.7 zilizosalia zikionyesha kuwa haukuwa huru wala wa hali na asilimia nyingine 11.8 hazikujibiwa.

Hata hivyo kwa mkoa mmoja mmoja, Tanga imeongoza kwa asilimia za kukubali kuwa ulikuwa huru na wa haki kwa asilimia 79.2, Manyara (74.3), Morogoro (73.1), Kilimanjaro (72.4), Dodoma (56.0), Arusha (51.4) na Dar es Salaam ikishika nafasi ya mwisho kwa kupata sifuri.

Kwenye utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na viongozi wa serikali za mitaa katika uchaguzi wa mwaka 2004 maoni ya wananchi kutoka ngazi mbalimbali yalionyesha kuwa asilimia 67.5 hazikutekelezwa na asilimia 32.5 ndiyo waliokubali kuwa ahadi hizo zilitekelezeka.

"Utafiti huu unaonyesha wazi kuwa rushwa bado ipo na imeanzia katika ngazi za chini kabisa. Kutokana na ukweli huo moja ya mapendekezo yetu ni kuitaka serikali kuanzisha kitengo maalumu cha kupambana na rushwa wakati wa uchaguzi," alisema.

Pia alipendekeza kuongezwa nguvu zaidi kwa mapambano ya rushwa na si kutegemea Takukuru peke yao kwani utafiti umeonyesha kuwa uwapo wa sheria pekee siyo suluhisho la mapambano dhidi ya rushwa.

Pia alitaka kuwapo kwa kamati maalumu za vijiji kwa ajili ya kupambana na rushwa na kwamba watu wengi walioulizwa walisema kuwa chanzo cha rushwa ni kutotekelezwa kwa sheria zilizopo.

Alisema kuwa asilimia kubwa ya watu waliokuwa wakiulizwa chanzo cha rushwa katika maeneo yao walieleza kuwa inachangiwa zaidi na ubinafsi na ulafi.

Alisisitiza kuwa moja ya umuhimu wa utafiti huo ni kuwafanya wadau mbalimbali nchini na nje ya nchi kujua nini kinafanyika mara baada ya kutoa misaada kwa ajili ya maendeleo ya sekta mbalimbali.

Alieleza kuwa asilimia 37.6 ya watu waliohojiwa walionyesha kujua maana ya rushwa wakiihusisha na fedha, ngono au chochote kinachowanywa kwa malengo binafsi huku asilimia 24.8 wakiitambua kama utoaji wa vitu vyovyote visivyokuwa halali.

Akizungumza wakati akifungua warsha ya utangazaji wa matokeo ya uchaguzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Dk Edward Hosea alisema wamefanya utafiti huo ili kubaini nini vyanzo vya rushwa na mbinu zitumiwazo kutenda kosa hilo ili iweze kuwasaidia wadau mbalimbali wakiwamo serikali, vyama vya siasa na hata Takukuru kukabiliana nayo.

Pia alisema utafiti huo umefanyika kwa lengo la kuondokana na kufanya kazi kwa hisia na kuondokana na utamaduni wa kulaumu bila ya kuwapo taarifa sahihi ambazo mara nyingi hutokana na utafiti.

CHANZO: Mwananchi


Despite the ever increasing dominance of mobile communication,a fixed line service remains as important as one's home address.In the UK,for instance,and probably in some other countries as well,a landline bill is still accepted as a form of ID.And the cost of calling an international land line is far cheaper than a call to a mobile.

It was therefore great news to hear that ZANTEL,one of the major mobile phone companies in Tanzania,was introducing GUMZO, a new and affordable (so they say)  fixed line service in the country.I came across the news when doing my daily "ritual" of going through countless Tanzanian blogs including those which appear on my blogroll.However,my excitement was short-lived after visiting ZANTEL's website.The first thing you would notice when visiting the company's website is its "amateur" looks.One would have expected a big name such as ZANTEL to have something better than what looks like a personal blog.Arguably,My KULIKONI UGHAIBUNI,especially after the "pimping", looks way cuter than ZANTEL's site.

If the impression of their website isn't something to bother you about,then you certainly would end up being as frustrated as I was when you try to search for more information.It really doesn't make sense for ZANTEL to create such a buzz about their GUMZO service only for them to "forget" to mention anything about it on their website.I suspect that the site has not been updated for sometime.All I wanted was to get more information on how I could subscribe to their fixed line service on behalf of someone in TZ but I left the site with none,zilch,nada!

Perhaps the company is so confident in its local advertisement campaigns that it completely ignores potential foreign-based customers.Or could it be the case of not having competent IT personnels?Or not having an IT department at all?Or just business as usual as bongo ilivyo tambarare?

I completely useless when it comes to such stuffs as marketing or sales.However,one does not need to hold even a short-course certificate is such areas to understand how ZANTEL could attract a pretty good number of foreign based customers who could subscribe to their GUMZO service to slash  the costs of making international calls to mobile numbers in Tanzania.

I am not expecting any apology from ZANTEL, not only because such a culture "is still foreign" among majority of service providers in Tanzania,both public and private,but also because the best they could do is making sure that their website lives up to their reputation.

Generally, for majority of service providers in our beloved country,both public and private, do not seem to care about the likes of Evarist who largely relies on the internet when lit comes to looking for local information about services in Tanzania.Ironically,even our media has a very disappointing presence on the internet.For instance,one of the oldest newspaper in the country,Uhuru,has long disappeared into thin air after months of having a website that had been updated at the mercy of their webmaster.Online versions of most of our newspapers have remained more of a privilege than a necessity.My fellow patriot Said Kubenea must have got tired of my frequent emails to his weekly paper reminding them to update their site on time.

I am sorry but I have to say it.Shame on you ZANTEL and all those who follow your suit when it comes to updating their websites.Your website really sucks.

5 Mar 2010

Msafara wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ukiwa umesheheni "mashangingi".Picha kwa hisani ya Mjengwa

Serikali yakiri kutumia zaidi ya kipato

na Sauli Giliard na Marietha Mkoka

MATUMIZI mabaya ya serikali na kuendelea kupanda kwa mfumuko wa bei za bidhaa kwa zaidi ya mara mbili katika kipindi cha kati ya mwaka 2005 na sasa ni chanzo cha maisha magumu ya wananchi, Tanzania Daima limebaini.

Katika wakati ambapo wananchi wapatao milioni nane wanalala au kushinda njaa kwa sababu ya ugumu wa maisha, serikali jana ilikiri kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Kijjah, imekuwa inatumbua shilingi mbili, wakati ina uwezo wa kukusanya shilingi moja.

Akitoa tathmini ya serikali kuhusu hali ya uchumi kwa kipindi cha miaka minne iliyopita, Kijjah alisema mapato ya serikali kwa mwaka ni sh trilioni tano, lakini matumizi ya serikali ni Sh trilioni 10.

Akijadili tathmini hiyo, mchumi na mwanasiasa, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema matumizi hayo makubwa ya serikali yanaathiri vibaya Watanzania wa kawaida, kwani yanachochea mfumuko wa bei unaosababisha gharama za maisha kuwa za juu.

Wakati Kijjah akikiri kwamba kimsingi, mapato ya serikali yamepanda kutoka Sh trilioni 2.167.6 mwaka 2005/06 hadi Sh trilioni 5.096 mwaka 2009/10, Profesa Lipumba alisema kama serikali ingekuwa makini, kulingana na ulaji mkubwa inaoonyesha, makusanyo ya sasa yangekuwa makubwa zaidi na yangekusanya kwa nidhamu.

Alisema serikali inawaachia watu fulani fulani (hakuwataja) na makampuni makubwa yasilipe kodi.

Kwa sababu hiyo, Profesa Lipumba alisema uchumi wa nchi unayumba na kufanya maisha ya Mtanzania yazidi kudorora.

“Hakuna ukusanyaji mzuri wa kodi; watu wanaachiwa, makampuni yanayochimba madini hayalipi kodi ya kutosha….hilo lina athari,” alisema Profesa Lipumba.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa mwaka 2004/05 wakati utawala wa Rais Benjamin Mkapa ukielekea ukingoni matumizi ya serikali yalipanda kutoka Sh trilioni 2.1 hadi Sh. trilioni 2.7 mwaka 2005/06 wakati Rais Jakaya Kikwete anaingia madaraka.

Mbali ya hilo taarifa hiyo ya Kijjah ilionyesha kwamba mfumuko wa bei umepanda kwa zaidi ya mara mbili katika kipindi cha kati ya mwaka 2005 ulipokuwa ni asilimia 5 hadi kufikia asilimia 12.2 Desemba mwaka jana kabla ya kushuka kidogo na kuwa asilimia 10.9 Januari mwaka huu.

Hata hivyo Kijjah, alisema serikali imechukua hatua ili kukabiliana na matumizi hayo makubwa. Alisema imeongeza idadi ya wahasibu na wakaguzi wa ndani katika ngazi zote kuanzia wizara hadi serikali za mitaa.

“Kuanzishwa kwa kitengo cha ufuatiliaji wa matumizi ya umma (bajeti) katika miradi iliyoidhinishwa: Ofisi ya Mkaguzi Mkuu (CAG) imeongezewa nguvu za kisheria kuweza kufanya kazi zake bila kuingiliwa na taasisi yoyote.”

Katibu mkuu huyo ambaye alikuwa amefuatana na naibu wake, John Haule, aliongeza ili kupunguza matumizi makubwa ya serikali, yanahitajika marekebisho katika Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004 ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa watendaji wake.

“Sera ya mapato ya mwaka 2009/10 inalenga kukusanya mapato ya ndani yasiyopungua sh milioni 5,096,016 sawa na asilimia 16.4 ya pato la taifa,” alisema.

Kuhusu thamani ya fedha, Kijjah alisema, shilingi iliendelea kuporomoka kutoka wastani wa shilingi 1,195.75 kwa dola ya Kimarekani mwaka 2008 hadi kufikia shilingi 1,318.71 mwaka jana.

 (Picha kwa hisani ya Mjengwa.)
MATUMIZI mabaya ya serikali na kuendelea kupanda kwa mfumuko wa bei za bidhaa kwa zaidi ya mara mbili katika kipindi cha kati ya mwaka 2005 na sasa ni chanzo cha maisha magumu ya wananchi, Tanzania Daima limebaini.
Katika wakati ambapo wananchi wapatao milioni nane wanalala au kushinda njaa kwa sababu ya ugumu wa maisha, serikali jana ilikiri kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhan Kijjah, imekuwa inatumbua shilingi mbili, wakati ina uwezo wa kukusanya shilingi moja

Akitoa tathmini ya serikali kuhusu hali ya uchumi kwa kipindi cha miaka minne iliyopita, Kijjah alisema mapato ya serikali kwa mwaka ni sh trilioni tano, lakini matumizi ya serikali ni Sh trilioni 10.

Akijadili tathmini hiyo, mchumi na mwanasiasa, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema matumizi hayo makubwa ya serikali yanaathiri vibaya Watanzania wa kawaida, kwani yanachochea mfumuko wa bei unaosababisha gharama za maisha kuwa za juu.

Wakati Kijjah akikiri kwamba kimsingi, mapato ya serikali yamepanda kutoka Sh trilioni 2.167.6 mwaka 2005/06 hadi Sh trilioni 5.096 mwaka 2009/10, Profesa Lipumba alisema kama serikali ingekuwa makini, kulingana na ulaji mkubwa inaoonyesha, makusanyo ya sasa yangekuwa makubwa zaidi na yangekusanya kwa nidhamu.

Alisema serikali inawaachia watu fulani fulani (hakuwataja) na makampuni makubwa yasilipe kodi.

Kwa sababu hiyo, Profesa Lipumba alisema uchumi wa nchi unayumba na kufanya maisha ya Mtanzania yazidi kudorora.

“Hakuna ukusanyaji mzuri wa kodi; watu wanaachiwa, makampuni yanayochimba madini hayalipi kodi ya kutosha….hilo lina athari,” alisema Profesa Lipumba.

Kumbukumbu zinaonyesha kuwa mwaka 2004/05 wakati utawala wa Rais Benjamin Mkapa ukielekea ukingoni matumizi ya serikali yalipanda kutoka Sh trilioni 2.1 hadi Sh. trilioni 2.7 mwaka 2005/06 wakati Rais Jakaya Kikwete anaingia madaraka.

Mbali ya hilo taarifa hiyo ya Kijjah ilionyesha kwamba mfumuko wa bei umepanda kwa zaidi ya mara mbili katika kipindi cha kati ya mwaka 2005 ulipokuwa ni asilimia 5 hadi kufikia asilimia 12.2 Desemba mwaka jana kabla ya kushuka kidogo na kuwa asilimia 10.9 Januari mwaka huu.

Hata hivyo Kijjah, alisema serikali imechukua hatua ili kukabiliana na matumizi hayo makubwa. Alisema imeongeza idadi ya wahasibu na wakaguzi wa ndani katika ngazi zote kuanzia wizara hadi serikali za mitaa.

“Kuanzishwa kwa kitengo cha ufuatiliaji wa matumizi ya umma (bajeti) katika miradi iliyoidhinishwa: Ofisi ya Mkaguzi Mkuu (CAG) imeongezewa nguvu za kisheria kuweza kufanya kazi zake bila kuingiliwa na taasisi yoyote.”

Katibu mkuu huyo ambaye alikuwa amefuatana na naibu wake, John Haule, aliongeza ili kupunguza matumizi makubwa ya serikali, yanahitajika marekebisho katika Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004 ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa watendaji wake.

“Sera ya mapato ya mwaka 2009/10 inalenga kukusanya mapato ya ndani yasiyopungua sh milioni 5,096,016 sawa na asilimia 16.4 ya pato la taifa,” alisema.

Kuhusu thamani ya fedha, Kijjah alisema, shilingi iliendelea kuporomoka kutoka wastani wa shilingi 1,195.75 kwa dola ya Kimarekani mwaka 2008 hadi kufikia shilingi 1,318.71 mwaka jana.

CHANZO: Tanzania Daima

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.