17 Mar 2010


KLABU ya soka ya Real Madrid ya nchini Hispania jana imemkabidhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete tuzo ya Jezi ya kiungo mshambuliaji wa timu hiyo Critiano Ronaldo. Akizungumza katika hafura hiyo iliyofanyika Ikuru jana Meya wa jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa ambaye alimukabidhi Rais jezi hiyo kwa niaba ya viongozi wa klabu ya Real Madrid kutokana kutambua mchango wake katika mchezo wa soka.

"Kwa heshima hiyo Klabu hiyo imetoa tuzo Jezi namba tisa inayovaliwa na mchezaji mahiri wa timu hiyo Cristano Ronado," alisema Kimbisa.

Naye Rais Kikweta mara baada ya kupokea tuzo hiyo ameshukuru klabu hiyo ya Real Madrid kwa zawadi hiyo ambayo alisema kuwa ni hesima kubwa kwa Watanzania.

"Nashukuru sana kwa zawadi hii, Madrid ni timu kubwa duniani kutukumbuka sisi Watanzania ni faraja kubwa kwetu.

"Itabidi tutafute sababu mpya ya kuwaalika upya kuja hapa nchini kufutia ili ya awali kushindikana, ni matumani yetu pia tutapata watu ambao watatusaidia kuwaleta," alisema.

Klabu hiyo ya Real Madrid itarajia kufanya ziara yake hapa nchini kwa ajili ya uzinduzi wa Uwanja wa Taifa mwanzoni mwa mwaka juzi lakini kutokana kuchelewa kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo timu hiyo hakuweza kufanya hivyo.

CHANZO: Mwananchi.

16 Mar 2010


RAIS Jakaya Kikwete ameweka hadharani mambo yanayomchefua katika utendaji wake kuwa ni viongozi wa mashirika ya umma na taasisi zilizo katika hali mbaya kifedha, kumghilibu ili awaongezee mitaji wakati historia inaonyesha kuwa kufilisika kwa mashirika hayo kumetokana na utendaji mbovu.

Rais Kikwete alisema anajisikia vizuri na hata moyo wa kuongeza msukumo katika kuitaka serikali itoe fedha kwa taasisi zinazojiendesha kwa faida ili ziendelee kufanya vizuri kuliko taasisi hizo zinazofilisika.

Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akibadilishana mawazo na watendaji wakuu wa tume mpya ya mipango mara baada ya kuwaapisha Ikulu jana.

. Utakuta shirika lilikuwa na ndege tisa. Sasa lina ndege mbili. Anakuja mtu anasema, Mheshimiwa tungeweza kufanya vizuri iwapo tungeongezewa ndege saba,? alisema Rais Kikwete wakati akipata kinywaji na watendaji hao watano, akiwemo Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

?Ebu fikiria, walikuwa na ndege tisa sasa zimepungua hadi mbili, lakini wao wanaona sasa waongezewe nyingine. Hii inaingia akilini!

?Ingekuwa sasa wanazo 13 halafu wakaja na maelezo kwamba wangefanya vizuri zaidi iwapo wangeongezewa, hapo inaweza kuingia akilini.?

Rais Kikwete aliwaonya watendaji hao wakuu wa chombo hicho ambacho kitategemewa kufanya mapinduzi ya kiuchumi nchini kwamba viongozi wa mashirika na taasisi wa namna hiyo watafika kwao, hivyo wawe makini katika kuamua kulingana na matakwa yao.

Ingawa Rais Kikwete alionekana kueleza hilo kama mfano tu, mazingira yalionyesha kuwa ni moja ya mambo makuu aliyotaka kuwausia katika utendaji wao, kwenye majukumu waliyopewa watekeleze.

Hali hiyo alidhihirisha kutokana na kurudia mara tatu, kusisitiza juu ya ghiliba za viongozi hao wabovu aliosema kuwa licha ya kufanya vibaya kiutendaji, huishawishi serikali izidi kutoa fedha.

Ingawa Rais Kikwete hakutaja shirika lenye tabia hiyo, kauli yake inaweza kuhusishwa na kuyumba kwa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) ambalo hivi sasa limebakiwa na ndege mbili tu baada ya kuyumba kiutendaji.

ATCL, ambayo ilikuwa ikitamba katika miaka ya themanini kutokana na kuwa na ukiritimba katika usafiri wa anga, iliingia mkataba na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) kwa ajili ya kuboresha huduma zake, lakini likajikuta likiporomoka zaidi hadi mkataba ulipovunjwa mwaka 2006.

Mwaka jana, shirika hilo lilizuiwa kufanya safari za anga baada ya kunyang'anywa leseni ya kupaa angani, hatua ambayo ililidhoofisha zaidi shirika hilo. Baada ya kurejeshewa leseni hiyo, bado ATCL imeshindwa kurudi katika hali yake ya kawaida licha ya serikali kutumbukiza fedha nyingi kujaribu kulinasua.

Takribani wiki mbili zilizopita, ndege ya ATCL ilipata hitilafu wakati ikitua mkoani Mwanza na kusababisha shirika hilo kusimamisha tena huduma zake kutokana na kukwama kwa ndege hiyo.

Awali kabla ya mazungumzo hayo ya chai, Rais Kikwete alimwapisha Dk Philipo Mpango kuwa katibu mtendaji wa Tume ya Mipango, akisaidiwa na manaibu katibu wanne; Maduka Kessy, Happiness Mgalula, Florence Mwandri na Cliphod Tandale.

Tume hiyo ya Mipango imeundwa ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Kikwete baada ya kuivunja iliyokuwa Wizara ya Mipango na Uchumi, alipokuwa anaunda baraza jipya la mawaziri mwaka 2007.

Mara baada ya kuvunja wizara hiyo, idara ya uchumi iliunganishwa na iliyokuwa Wizara ya Fedha na kuifanya iwe na jina jipya la Wizara ya Fedha na Uchumi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dk Mpango alisema tume hiyo itakuwa chombo muhimu cha serikali katika kuweka mipango yenye tija kiuchumi kwa taifa.

Lakini alisema kwamba anakabiliwa na changamoto kubwa ya kupanga mipango mizuri ya nchi ambayo itasababisha mapinduzi ya kiuchumi, hasa ikizingatiwa kwamba kwa kipindi kirefu mikakati imekuwa ikiwekwa lakini bado Tanzania inaendelea kuorodheshwa kwenye nchi maskini.

?Kinachoniumiza ni kuona taifa linaendelea kuwa maskini hata baada ya miaka 40 ya uhuru,? alieleza Dk Mpango.

Miongoni mwa mambo ambayo yamekuwa yakikwamisha nchi kuendelea, alisema, ni taifa kuwa na vipaumbele vingi kuliko rasilimali yake ya kiuchumi.

Katika mazingira hayo, alisema mikakati mingi imekuwa haikamiliki kutokana na kile kidogo kinachopatikana.

Dk Mpango akasema pamoja na kwamba mawazo ya tume yake yatatokana na ushauri wa wataalamu wake, binafsi anaona watatilia mkazo vipaumbele vichache ili suala la maendeleo liwe la hatua kwa hatua.

Alitoa mfano wa Bandari ya Dar es Salaam kwamba inaweza kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo nchini iwapo itaimarishwa pamoja na miundombinu ya reli ili nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), zitegemee kupitisha bidhaa zake Tanzania.

CHANZO:Mwananchi.


Bananas may hold the key to powerful new treatments that protect against the Aids virus.In laboratory tests, scientists found that a banana ingredient called BanLec was as potent as two existing anti-HIV drugs.

They believe cheap therapies based on BanLec have the potential to save millions of lives. The ingredient is a lectin, a naturally occurring chemical in plants which fights infection.

Researchers in the US found that the lectin found in bananas can inhibit HIV infection by blocking the virus's entry into the body. BanLec acts on the protein "envelope" that encloses HIV's genetic material.

Lead author Michael Swanson, from the University of Michigan, said: "The problem with some HIV drugs is that the virus can mutate and become resistant, but that's much harder to do in the presence of lectins.

"Lectins can bind to the sugars found on different spots of the HIV-1 envelope, and presumably it will take multiple mutations for the virus to get around them."

The research is reported in the Journal of Biological Chemistry.
SOURCE: Yahoo! News

14 Mar 2010


Wana-Msimbazi mmeweka rekodi nzuri na inayostahili pongezi.Tunataraji mtatafsiri rekodi hiyo kwa kufanya vema katika michuano ya kimataifa.Penye nia pana njia.
POINTI za Simba sasa zimetosha na imeibuka bingwa wa soka Ligi Kuu Tanzania Bara kwa mwaka 2009/2010, lakini ikiwa ni mara ya 17 kwa klabu hiyo kutwaa ubingwa huo.

Hatua hiyo inatokana na ushindi wa mabao 2-0 iliyoupata jana dhidi ya Azam kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam katika mchezo wa ligi hiyo uliokuwa mkali na wa kusisimua ambao ni wa raundi ya 20.

Kutokana na matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 56 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote katika ligi hiyo, ambapo Yanga iliyofikisha pointi 45 ikishika nafasi ya pili ikishinda michezo yake mitatu iliyosalia itafikisha pointi 54.

Chereko, nderemo na vifijo vya mashabiki wa Simba vilitawala Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam mara baada ya filimbi ya mwisho ya mwamuzi Ibrahim Kidiwa ambayo iliashiria mwisho wa mechi kati yao na Azam.

Baada ya mpira kumalizika wachezaji wa Simba walizunguka uwanja wakiwapungia mikono mashabiki wao, ambao wengi wao walikuwa wamevalia fulana zenye maneno Simba Bingwa 2009/2011, huku wakiwa wanaonekana wenye furaha isiyo kifani baada ya kutwaa ubingwa huo, huku wakiwa na rekodi safi ya kutopeza mechi yoyote kwenye ligi hiyo na ikiwa imetoka sare mara mbili tu kati ya mechi 20 ilizocheza.

Mabao mawili yaliyofungwa moja katika kila kipindi na mshambuliaji Mkenya wa timu hiyo, Mike Barasa ndio yaliyoiwezesha Simba kuwavua rasmi ubingwa watani zao wa jadi, Yanga, huku ikiwa imesaliwa na mechi mbili mkononi ikiwemo ile dhidi ya watani zao hao itakayochezwa Aprili 11 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Bao la kwanza la Simba lilifungwa dakika ya saba kwa kichwa na Barasa ambaye aliunganisha krosi ya Mkenya mwenzie Hillary Echesa na kuwafanya mashabiki wa Simba kushangilia baada ya kuenea kwa maneno ya uzushi kuwa mnajimu mmoja alitabiri Simba ingepoteza mchezo na isingeweza kutwaa ubingwa.

Baada ya bao hilo Simba ambao walionekana kupania, walilisakama lango la Azam na dakika mbili baada ya bao hilo, Ulimboka Mwakingwe alipiga krosi ndani ya eneo la hatari lakini Musa Hassan ‘Mgosi’ akiwa katika nafasi nzuri ya kufunga alishindwa kumiliki mpira huo, hivyo kupoteza nafasi hiyo. Huku Simba wakionekana kutandaza kandanda safi na kufanya washangiliwe na mashabiki wao waliofurika uwanjani hapo kushuhudia timu yao ikitwaa ubingwa baada ya kuukosa kwa takribani miaka mitatu, walianza kupooza mashambulizi na hivyo kuanza kutoa nafasi kwa Azam ambao walionekana kutawala sehemu ya kiungo kipindi cha kwanza.

Kutokana na udhaifu huo Azam walipeleka mashambulizi kadhaa, langoni mwa Simba na katika dakika 35 washambuliaji John Bocco, Danny Wagaluka walishindwa kupachika bao kufuatia krosi ya Malika Ndeule, baada ya Bocco kuikosa na kipa Juma Kaseja kuuwahi kabla ya kumfikia Wagaluka.

Bocco alikosa bao pale shuti lake alilopiga akiwa kwenye ukingo wa eneo la hatari na kudakwa na Kaseja, dakika mbili baadaye mshambuliaji huyo alijaribu tena shuti kali ambalo lilimtoka Kaseja kabla hajaliwahi na kulidaka tena.

Kipindi cha pili kilianza kwa Azam kufanya mabadiliko ya kuwaingiza Ally Manzi na Mau Ally badala ya Said Sued na Wagaluka.

Mabadiliko ambayo yalionekana kuongeza uhai katika safu ya ushambuliaji ya Azam na kuleta sekeseke kadhaa kwenye safu ya ulinzi ya Simba ambayo ilikuwa ikiongozwa na Kelvin Yondani na Juma Nyosso, kwani Manzi alionekana kumsumbua beki wa kushoto, Juma Jabu.

Simba ilifanya mabadiliko yake ya kwanza dakika ya 55 kwa kumtoa Ulimboka Mwakingwe na nafasi yake kuchukuliwa na Uhuru Selemani na dakika ya 57 nusura Mohamed Banka apachike bao la pili baada ya kupiga shuti kali la adhabu ambalo liligonga mwamba wa juu na kurejea uwanjani huku, kipa Vladimir Niyonkuru akiwa ameshapoteza hesabu, lakini walinzi wake waliokoa.

Dakika ya 60 Azam walijibu shambulio hilo pale Manzi alipomtoka Jabu na kupiga krosi safi ambayo Bocco alichelewa kuinganisha wavuni, dakika mbili baada ya Azam kukosa bao hilo, Uhuru Seleman alitoa pasi ya kubetua kwa Barasa aliyekuwa kwenye eneo la hatari ambaye bila ajizi aliukwamisha mpira wavuni na kuipatia Simba bao la pili.

Yanga iliyokuwa ikitetea ubingwa huo, yenyewe imetwaa kombe hilo mara 21.

CHANZO: Habari Leo.


COMPUTER hackers linked to the Russian mafia robbed Royal Bank of Scotland customers of £6million in 12 hours.The crooks pulled off the massive sting by dispatching an army of thieves using cloned debit cards to blitz more than 2000 cash machines in 280 cities worldwide.

Stunned bosses at the Edinburgh bank were helpless to stop £6million of cash being plundered from the ATMs in Scotland's biggest bank heist.. But, we can reveal gang leader Viktor Pleshchuk, 28, has been snared in the Russian city of St Petersburg following a massive FBI investigation.

Acting US Attorney Sally Quillian Yates described the heist as "perhaps the most sophisticated and organised computer fraud attack ever conducted".The plot was hatched by Oleg Covelin, 28, in Moldova, who discovered a flaw in the bank's computer system.He contacted Sergei Tsurikov, 25, in Tallin, Estonia, who joined forces with Pleshchuk to orchestrate the electronic heist.

The gang hacked into the bank's system to clone 44 debit cards and discover their PIN numbers.They electronically hiked the available balances and deleted withdrawal limits on each card before distributing them to a network of foot soldiers, known as "cashers".At the stroke of midnight US time, the cashers drained ATMs using the cloned cards.

They struck at machines in Britain, the US, Russia, Ukraine, Estonia, Italy, Hong Kong, Japan and Canada.
During the 12-hour robbery, Pleshchuk and Tsurikov hacked back into the bank's system to see the transactions taking place on their computer screens.They obtained just under $9.5million - around £6.3million - between midnight and noon.FBI Agent Ross Rice said: "We've seen similar attempts to defraud a bank through ATM machines but not anywhere near the scale we have here."

The hackers then deactivated the cards and attempted to destroy electronic records of their crime within the bank's system.The cashers were allowed to keep 30 to 50 per cent of the cash with the rest being sent electronically back to the hackers.The three suspects have all been extradited to the US where they are to stand trial accused of the attack on the RBS WorldPay division in Atlanta.

Former hacker Kevin Mitnick, who now works as a computer security consultant, said: "It was so well co-ordinated. These guys hacked into RBS WorldPay, they took control of their servers and reverse engineered the encryption so they could get the debit card PINs.

"They then distributed the account numbers and PINs to a network of cashers - criminals who will withdraw funds from ATMs.

"They co-ordinated this attack so the cashers would cash out in a 12-hour period and stole $9.5million. That's an incredibly sophisticated attack."

The gang targeted the bank at the height of the global financial crisis in November 2008, striking just three weeks after shamed RBS chief Sir Fred Goodwin was forced to quit.

At that time, the bank was only saved from collapse by an emergency £20billion injection of public cash and is now 84 per cent owned by British taxpayers.

Angry US customers whose cards were cloned by the gang are suing RBS in a $5million class action lawsuit.
The action by Keith Irwin, of Pennsylvania, accuses the bank of negligence and breach of contract.

Michael McCoy, of the Identity Theft Institute, received a warning letter from RBS telling him that his personal details may have been stolen by the gang.

But he hit out as the bank only offered a 12-month free credit rating - while warning customers to be vigilant for 24 months.

He said: "It's an insult to me and any other consumer.

"Come on, a one-year subscription, what's that going to do?

"Any intelligent thief understands these letters are going out so why won't they use it in the 13th month?"

"On the back of this letter they encourage you to remain vigilant for 12 to 24 months but they're only going to offer me a product for 12 months. It boggles my mind."

Customers are also angry at the fact the bank "identified the breach" on November 10, 2008, but kept it secret for 43 days.

They eventually issued a press release in the US about the fraud two days before Christmas in what furious victims claim was a deliberate ruse to avoid publicity.

The press release said fraud had only been committed on 100 cards - giving no hint of the financial scale of the attack.

A fourth unnamed hacker is also facing criminal charges. He is believed to have fully co-operated with the FBI.

In the dock with the four hackers are four other Estonians. Tsurikov is accused of distributing cards and PINs to Igor Grudjev in Estonia.

Grudjev then distributed them to Ronald Tsoi, Evelin Tsoi and Mihhail Jegenvov, who withdrew £191,000 from ATMs in Tallin during the 12-hour period.

The cloned cards belonged to US workers whose wages are paid directly into their bank accounts.
The RBS WorldPay website states: "From face-to-face transactions to online and phone transactions, we provide an effective, secure service."

At the time, Ben Barone, president and CEO of RBS WorldPay, said: "We have taken important, immediate steps to mitigate risk and none of the affected cardholders will be responsible for unauthorised activity on their account resulting from this situation."

RBS declined to comment because of the ongoing legal proceedings.

Raid was planned like terror operation

Experts claim preparation for the worldwide bank scam was on a similar scale to an al-Qaeda terrorist operation.

Uri Rivner, of RSA Identity Protection & Verification, said: "The technical aspects in this case were not that impressive but the level of co-ordination was staggering.

"Managing time zone issues and co-ordinating cashers in nine nations - all required to hit as many ATMs as possible within 12 hours - makes me think of an al-Qaeda type of strategy of multiple attacks in a single day.
"A lot of planning and a very high degree of international co-operation went into this."

The four hackers in the dock are all in their 20s, from Russia and other former Soviet states. The FBI are in no doubt that they worked for the Russian mafia. Once they had identified a way into the RBS internal network, they spent months plotting on private internet forums.

They began looking for "jackpot servers" using free scanning software to locate valuable, protected data.
Experts reckon they stumbled on the details of the 44 cards before artificially hiking the balances and abolishing the daily withdrawal limits.

SOURCE:The Daily Record.


It's like you were gone yesterday.I just can't believe that you're gone.On this day,I'd be calling you and daddy to say how much I love you,mamma.But you're not there.The only comfort I have is the strong belief that you're resting in peace.And though you're not with us on this Mother's Day,you remain the best thing God could give any son.Rest in peace,mamma.You'll always be missed and remembered!Oh! My mama, happy mother’s day
You are the greatest mother I have ever had
You are my mother today
You will be my mother tomorrow
You are always my mother
You will forever be my mother

Thank you my mother for bringing me into this world
Thank you my mother for taking care of me in your womb
Thank you my mother caring for me as a toddler
Thank you my mother for feeding me since I was a baby
Thank you my mother for all the clothes you bought for me
Thank you my mother for teaching me good manners at home

Thank you my mother for sending me to school
Thank you my mother for supervising my homework
Thank you my mother for ensuring I eat before going to school
Thank you my mother for all the regular pocket money
Thank you my mother for liking my friends
Thank you my mother for all the everyday advices

My mother always remind me that fingers are not equal
As I grow up, I have seen the correlation of this analogy
To many human beings, neighbors, societies and nationalities
Oh! My mama, thank you for your words of wisdom
My mother taught me many things that I have never read in books
Thank you my mother for all your guiding philosophies

Oh! My mama, I sincerely wish everyday could be Mother’s Day
One day in a year is not enough to thank my wonderful mother
Oh! My mama, I will forever be your child
Oh! My mama, you will eternally be my mother
Thank you my mother for being my best friend
Thank you my mother for being my trusted adviser
I honestly wish you HAPPY MOTHER’S DAY!
.Rest in Eternal Peace,mamma!

13 Mar 2010


Wiki hii tumeadimisha siku ya wanawake duniani.Na kesho ni siku ya mama zetu.Ni kipindi mwafaka cha kungalia mchango wa jinsia ya kike katika ngazi ya familia hadi taifa.Tukubali tusikubali,dunia imeendelea kutawaliwa na mfumo dume.Na bara letu la Afrika (na pengine sehemu kubwa ya Dunia ya Tatu) haki za akinamama na mchango wa jinsia ya kike vimeendelea kupuuzwa.Kwa bahati nzuri kwangu,kabla wiki hii muhimu haijamalizika nilipata wasaa wa kuongea na bloga maarufu wa Kitanzania,Sarah Peter,mmiliki wa blogu ijulikanayo kama ANGALIA BONGO. Sihitaji kumpamba kwani ukitembelea blogu hiyo utaafikiana nami kuwa binti huyu licha ya udogo wake wa umri ana kipaji cha hali ya juu katika kuwasilisha ujumbe wake kwa wasomaji wa blog yake na jamii kwa ujumlaNimejijengea mazingira ya kutembelea takriban blogu zote za Watanzania wenzangu kila siku,au angalau mara kadhaa kwa wiki.Licha ya idadi kubwa ya blogu hizo kuwa kwenye blogroll yangu,nina orodha kubwa ya subscription kwenye Google reader,na inanisaidia sana kufahamu kinachoendelea kwenye blogsphere.



Back to Sarah.Nilianza kublog mwaka 2006 na tangu wakati huo blogging imekuwa sehemu muhimu ya maisha yangu.Lakini hadi jana nilikuwa sijakutana na bloga ambaye ndani ya dakika chache alinifumbua macho kwa kiwango kikubwa as to wapi panahitaji marekebisho bloguni mwangu na namna nyingine za kunoresha uwanja huu.Lakini ukidhani hilo ni kubwa zaidi,basi tembelea kwanza hiyo blog ya ANGALIA BONGO kisha utapata picha nzuri zaidi ya nachokieleza.



Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kuhusu blog hiyo hasa kiu yangu ya kumfahamu vema mmiliki wake.Awali nilidhani kuwa Sarah ni 'mtu mzima' (kiumri) kwani nyingi ya posts zake zimesheheni upeo unaoendana na utu uzima.Tofauti na dhana hiyo,kumbe Sarah ni binti aliyezaliwa miaka ya 80 hivyo ana miaka ishirini na kitu (lakini haifiki 25).Kwa kifupi,ni binti mdogo mwenye akili kubwa na kipaji cha hali ya juu.Na siandiki hivi kwa minajili ya 'kumpa ujiko' (hata ningekuwa nafanya hivyo ingekuwa kazi bure kwani tayari ana 'ujiko' wa kutosha)bali ni katika kutambua mchango wa jinsia ya kike katika fani ya habari hususan kwenye matumizi ya vipasha habari vya jamii (social media) kama blogu.



Hata hivyo,pamoja na mwonekano maridhwawa wa blogu ya ANGALIA BONGO na habari zenye kila ishara kuwa aliyeandika anajua vema anachofanya,kumwelewa vema Sarah kunahitaji uongee nae kama ilivyotokea kwangu jana.Alinipa darasa la chapchap kuhusu mambo mbalimbali ya maana.Na mie ni mwanafunzi mzuri napokutana na mwalimu mzuri.Na haikuchukua muda kwangu kabaini kwamba binti huyu ana akiba kubwa ya akili na kipaji,na hadi sasa kinachotumika ni kiasi kidogo tu cha kipaji na akili hiyo.Sasa kama kiasi kidogo ndio mambo makubwa namna hiyo,ni dhahiri kuwa bloga huyu atakuwa mbali sana akiamua kutumia uwezo wake wote(na anasema atafanya hivyo mbeleni).



Ukiangalia picha zake,unaweza kumhukumu isivyo.Ana mwonekano wa 'kisistaduu' (sina tafsiri sahihi ya neno hili) na ni rahisi kudhani ana 'pozi' (maringo).Lakini hata kama angekuwa hivyo (i.e. sistaduu mwenye pozi),which she is not,character hizo zingefunikwa na kipaji na upeo wake.Sarah anaeleza kwamba yuko into many stuffs japo amebobea zaidi kwenye mambo ya burudani (entertainment).Licha ya background yake kama journalist na radio producer,uwezo wake wa kufikiri na kuandika haraka unachangia sana kuifanya blog yake kuwa mahala pa kumridhisha kila msomaji anayepatembelea.Lakini kingine kinachopendeza katika wasifu wa binti huyu ni imani yake ya kiroho.Anasema kuwa dini ni kitu muhimu sana katika maisha yake,na kwa kuthibiths ahilo ameandika I...always believe in Jesus, Remember İm a pure Christian.Imani thabiti katika dini inasaidia sana kuimarisha vipaji na kutanua upeo,na ni ishara ya karama za Muumba.



Ni dhahiri kuwa bloga huyu ana nafasi ya kufanya mambo makubwa huko mbeleni,na ni matarajio yangu kuwa siku moja Sarah ataitangaza nchi yetu si tu kupitia blog yake bali pia katika fani flani muhimu.Nilimtania kuwa this time in 2012 or so natarajia kumuona akiwa katika delegation ya Mama Asha Rose Migiro,sio kwa vile ni Mtanzania mwenzake bali akiwajibika katika wadhifa flani.Na kama si hilo,basi sintoshangaa akija na chapisho kama Ebony au The Source ya kitanzania.

Kila la heri Sarah!


Moja ya maeneo yeynye kuhitaji mtazamo mpya katika Tanzania ni haki za raia.Ni ukweli usipingika kwamba nchi yetu ina haki za aina mbili: kwa wenye nacho/vigogo na kwa walalahoi.Kuna mifano mingi ya kuthibitisha hilo lakini hapa nitaonyesha mifano michache kuokoa muda.Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge alipopata ajali iliyopelekea vifo vya watu wawili,jeshi la polisi lilikurupuka kuunda tume ya kuchunguza ajali hiyo.Baada ya ajali hiyo,zimetokea ajali nyingine kadhaa zilizopelekea vifo vya watu kadhaa lakini hatujasikia jeshi la polisi likiunda tume kuchunguza ajali hizo.Jibu jepesi ni kwamba waliopoteza maisha kwenye ajali hizo si vigogo hivyo 'hakukuwa na umuhimu kwa kuundwa tume za uchunguzi'.Mfano mwingine ni kauli ya Rais Mstaafu Ben Mkapa kwamba wanaoajiri mahauziboi na mahazigeli wanapaswa kuwa na mafaili ya waajiriwa wao ili pindi likitokea tatizo wapatikane kirahisi.Mkapa aliyasema hayo alipoenda kumpa pole Balozi Andrew Daraja kufuatia mauaji ya mkewe ambayou yanadaiwa kufanywa na hauziboi wa balozi huyo. Kwanza,tukio zima la kifo cha mke wa Balozi linatengeneza mazingira ya ukiukwaji haki za hauziboi husika.Ieleweke kuwa nami nimeguswa na mauaji hayo ya kinyama lakini hiyo haiwezi kuhalalisha jamii kujichukulia sheria mkononi na kumhukumu hauziboi huyo.Jeshi la polisi ndilo lenye mamlaka ya kuchunguza mauaji hayo na kisha kuiachia mahakama itoe hukumu.

Twende kwenye ushauri wa Mkapa.Kwa mawazo ya Rais huyo mstaafu,kuwa na mafaili yenye taarifa za mahauziboi na mahauzigeli kutasaidia kuwapata kirahisi pindi wakihusishwa na vitendo visivyofaa.Mkapa anaelekea kuthamini zaidi haki za vigogo wenzie wanaoajiri mahauziboi na mahazigeli huku wakilipwa mishahara kiduchu na kutumikishwa kama watumwa,ilhali anapuuza haki za waajiriwa hao ambao ni adimu kwao kuwa na mikataba ya ajira huku ajira zenyewe zikiwa mithili ya maandishi ya chaki ubaoni (blackboard).Ukijisugua tu na ubao,yanafutika.

Japo wazo la Mkapa sio baya kihivyo,lakini kwanini lije wakati huu ambapo hauziboi anahusishwa na mauaji ya mke wa mwanadiplomasia Daraja?Ni hadithi zilezile za barabara kukarabatiwa kukiwa na ziara za viongozi wakati zimesahauliwa miaka nenda miaka rudi kwa vile tu watumiaji wa barabara hizo si vigogo.Kama kulikuwa na umuhimu wa kuwepo mafaili yenye taarifa za watumishi wa ndani basi isingehitaji kusubiri hadi hauziboi atuhumiwe kumuua mke wa balozi.

Na ni kwa vile walalahoi hawana uwezo wa kumudu kuajiri wanasheria wazuri lakini kwa namna 'jamii ilivyokwishatoa hukumu dhidi ya hauziboi wa Balozi Daraja' ni dhahiri kesi yake mahakamani ingestahili kufutwa kwani 'ameshahukumiwa uraiani'.Mkapa alipaswa kutambua kuwa kauli yake kama Rais Mstaafu inaweza kabisa kutafsiriwa kuwa nae amefuata mkumbo wa kuamini kuwa 'ukiwa mlalahoi na ukatuhumiwa,basi unabaki mkosaji hadi itakapothibitika vinginevyo' (guilty until proven innocent).

Mlalahoi Jerry Muro alipotuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa mtuhumiwa wa rushwa (funny,isn't it?),kamanda Kova na vijana wake wakakurupuka chap chap kutujulisha kuwa jeshi lake lina teknolojia za kisasa za kufuatilia wala rushwa (sijui kwanini hawajashea ujuzi huo na TAKUKURU).Lakini wakati Kova akituaminisha mazingaombwe hayo,tunabaki na maswali kwamba kama vyombo vyetu vya dola viko makini kiasi hicho ilikuwaje basi wale majambazi wa EPA walimudu kutuibia mabilioni yetu pale Benki Kuu,mahala paliposheheni mitambo ya kisasa ya ulinzi?Au kwani teknolojia iliyotumika kumnasa Muro haikutumika kuwabaini majambazi wa Richmond?Na kwanini isitumike kumfahamu Kagoda ni mdudu wa aina gani?

Jibu rahisi ni kwamba Muro aligusa maslahi ya wakubwa (na vijana wao in the name of Jeshi la Polisi) na wakaamua kumpa 'jambajamba' (excuse my language) ili 'atulie'.Chenge ameendelea 'kutanua' licha ya tuhuma za vijisenti vyake vyenye thamani ya bilioni huko visiwani Jersey.Na bado teknolojia ya jeshi la polisi iliyomnasa Muro haijafanikiwa kuona kama Chenge anastahili kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.Jawabu la utata huo ni jepesi: Chenge ni kigogo,na Muro ni mlalahoi.

Magereza yetu yamesheheni wezi wa kuku na vibaka wengineo huku majambazi halisi wa uchumi wetu wanaendelea kutudhihaki mitaani wakiwa kwenye ma-vogue yao ya bei mbaya.Tanzania yetu imefika mahala ukijaribu kukemea uovu unaohusisha vigogo unaonekana kama mhaini,na utaandamwa zaidi ya Wamarekani wanavyomtafuta Osama bin Laden.Na kwa huko mtaani,ukiwa na bahati mbaya ya kuwa na mke/mpenzi mzuri anayetamaniwa na kigogo,andika umeumia.Nakumbuka hadithi ya jamaa mmoja aliyepewa kitengo nje ya nchi ili kigogo aliyekuwa anatoka na mkewe apate wasaa mzuri wa kufaidi 'haki za vigogo zilizoangukia kwa bahati mbaya kwa mlalahoi'.

Ni katika mazingira hayo ndio maana baadhi ya watu wanadiriki kuamini kwamba laiti Babu Seya na wanae 'wasingegusa haki za vigogo' angeendelea kuwa uraiani akitumbuiza na bakulutu zake.Siungi mkono ulawiti lakini wajuzi wa kona za Dar es Salaam wataafikiana nami nikisema kuwa kuna vigogo wengi tu wanaofanya michezo michafu kwa vibinti vidogodogo mitaani lakini wadhifa wao unawalinda,na wanaishia kuitwa 'viwembe' badala ya kuwa jela kama Babu Seya.Again,mwanamuziki huyo na mwanae Papii Kocha wako 'mbele ya sheria' kwa vile ni walalahoi na si uzito wa makosa yao.Nithibitishie kuwa siko sahihi (prove me wrong).

Wito wangu kwa walalahoi wenzangu ni huu: kaa ukitambua kuwa sheria na haki nchini mwetu zina sura mbili: upofu kwa makosa ya vigogo na macho makali (hata kwenye giza) kwa walalahoi.Fanya manjonjo yako ukitambua ukweli huo mchngu,ukigusa 'haki' za vigogo,andika umeumia.Tambua kwamba wanywa gongo huko Uwanja wa fisi wanapokamatwa na vyombo vya dola (mara nyingi hawanywi pombe hiyo hatari kwa vile hawajali afya zao bali uchumi mbovu) tunaambiwa kosa lao ni kutumia kinywaji hicho haramu lakini ikitokea vigogo na watoto wao wakajihusisha na kuuza na kutumia madawa ya kulevya,hawagusiw kwa vile 'ni haki yao kujistarehesha' (ndio maana ile orodha ya wauza unga ambayo ex-minister Mwapachu aliikabidhi kwa JK haijafanyiwa kazi hadi kesho).

Ni ukweli mchungu na unaoumiza lakini ubaki ukweli na hali halisi.By the way,Waingereza wanasema TRUTH HURTS!

12 Mar 2010

 Habari zilizotawala vyombo vya habari vya hapa Uingereza ni kufikishwa mahakamani kwa wabunge watatu wa chama tawala (Labour) na mbunge wa bunge la mabwanyenye kutoka chama cha Conservatives.Kwa pamoja wabunge hao wanatuhumiwa kufuja fedha .Wabunge hao, Elliot Morley, David Chaytor na Jim Devine wa Labour na Lord Hanningfield wa Conservatives wanashtakiwa kwa ubadhirifu wa jumla ya takriban pauni 60,000 za mafao ya wabunge.Wakati hayo yakitokea hapa katika nchi ambayo ni wafadhili wetu wakubwa,hadi muda huu sie tumeendelea kuwekwa kizani kuhusu mdudu aitwaye Kagoda,huku mtuhumiwa wa ufisadi wa rada na wale wa ujambazi wa Richmond wakiendelea "kupeta". Ni dhahiri kwamba watawala wetu hawako serious na mapambano dhidi ya uhalifu wa vigogo.Hebu angalia mfano mwepesi wa ishu ya mtangazaji wa TBC,Jerry Muro.Japo blogu hii si mahakama ya kuamua kama mtangazaji huyo hana hatia au,kasi ya vyombo vya dola katika kushughulikia 'tuhuma' dhidi yake zilikuwa kubwa sana tofauti na namna vyombo vya dola vinavyojiumauma hadi leo kuhusu majambazi wa kampuni ya Kagoda waliokwiba shilingi bilioni 40 katika utapeli wa EPA.Watawala wetu wameendelea kuweka pamba masikioni na kupuuza kilio cha umma kuhusu haja ya angalau kutajiwa wamiliki wa kampuni hiyo ya kijambazi.

Ndio maana blogu hii imeendelea kuiona sheria mpya ya kudhibiti rushwa katika chaguzi kuwa ni mwendelezo wa ahadi lukuki za kunoresha ustawi wa taifa letu lakini ahadi hizo zimeendelea kuwa viinimacho visivyotekelezeka.Sheria hii inaweza kupelekea waheshimiwa wawili watatu kutiwa nguvuni (kama TAKUKURU watashikiwa silaha kuwezesha hilo), vichwa vya habari vitasomeka kwa herufi kubwa kwamba sheria imeanza kufanya kazi.Lakini kana kwamba wana ugonjwa wa kusahau historia,baadhi ya wanahabari wetu watazembea kurejea matukio ya nyuma ambapo kesi kama za akini Profesa Mahalu,na hizi za karibuni za Mramba na Yona zinaendelea kusuasua mahakamani pasipo dalili za haki kutendeka-kwa watuhumiwa na walipakodi wa Tanzania.

Watakaonaswa baada ya sheria hiyo 'kuanza kutumika' watakuwa mithili ya 'muzi wa kafara',na 'changa la macho' kuonyesha umma kuwa sheria inafanya kazi lakini mwisho wa siku itaishia kuwa 'flani kafikishwa mahakamani',and that's it.Suala sio kumfikisha mtuhumiwa mahakamani bali haki itendeke,na sio itendeke tu bali ionekane imetendeka.

Yayumkinika kusema kuwa kesi za EPA zinazoendelea kwa mwendo wa kinyonga hazikidhi haja ya umma hasa kwa vile japo wote ni watuhumiwa lakini wale wa Kagoda waliiba fedha nyingi zaidi.Cha kushangaza ni kwamba hadi leo wameendelea kuhifadhiwa.Sasa tukisema ufisadi ni sera ya CCM tutaambiwa tumekosa nidhamu?

Tukio la kufikishwa mahakamani kwa wabunge hawa wa Uingereza kunapaswa kutufumbua macho kwa vile kama nchi inayotufadhili iko hailei wabadhirifu iweje sie tunaotegemea misaada tunakuwa na 'sintofahamu' katika kuwachukulia hatua mafisadi?Hivi kuna sababu za msingi kwanini hadi leo Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge hajafikishwa mahakamani kuhusu vijibilioni vyake huko visiwani Jersey?Basi hata kama wanamwonea aibu,yaani CCM wanashindwa hata kuona haya kwa mtuhumiwa huyo kuwa mwenyekiti wa kamati yake ya maadili?Au ufisadi ni sehemu ya maadili katika chama hicho?

Wakati tukiendelea kuaminishwa kuwa sheria hiyo ya kudhibiti rushwa kwenye chaguzi itakuwa 'kiboko' ya rushwa,toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema lina habari kuwa rushwa inamwagwa katika majimbo kadhaa kama wahusika hawana akili nzuri.Sijui huko ni kumkejeli Rais Kikwete aliyetamka bayana kuwa atasaini sheria hiyo kwa mbwembwe au ni kuujulisha umma kuwa CCM na rushwa ni damu damu!Kilicho wazi ni kuwa hakuna mgombea wa CCM atakayefanikiwa kupitishwa na chama hicho pasipo kutoa rushwa.Hilo halihitaji mjadala.Na kama Rais Kikwete anaamini kuwa sheria anayoipigia jaramba itakomesha rushwa kwenye chaguzi,basi ni vema naye akatafakari upya kama kuna umuhimu wa kuendelea kuwa kiongozi wa watu wasioafikiana na mtizamo wake.

Kinachosikitisha zaidi ni namna jamii isivyoonekana kukoseshwa usingizi na namna nchi yetu inavyozidi kutafunwa na mafisadi.Angalia mwitikio wa wananchi kuhusu 'makamanda wa vijana' wa CCM.Hivi watu hawajiulizi hawa makamanda walikuwa wapi siku zote kiasi cha kukurupuka ghafla kufishana makoti na joto lote hilo kwa kifuniko cha 'ukamanda wa vijana'?Na huo ukamanda unawasaidiaje vijana husika?Kwanini makamanda hao wasielekeze nguvu zao katika kupambana na ufisadi? Kwa asiyefahamu 'siri ya ukamanda wa vijana' basi aelewe kuwa kila anayevikwa wadhifa huo ni 'mgombea mtarajiwa'.Ni namna ya kujiweka karibu na wapiga kura.

Lakini sina tatizo sana na makamanda hao bali hao wanaoaminishwa kuwa ili waendelee wanahitaji makamanda wa vijana.Mie ni muumini mkubwa wa wazo kwamba UFISADI ni kikwazo nambari wani cha maendeleo yetu,au sababu kubwa ya kwanini tumeendelea kuwa masikini wa kutupwa licha ya utajiri lukuki wa maliasili tulionao.Logic yangu ni simple.Huwezi kujaza maji kwenye ndoo yenye matobo au kujaza upepo kwenye mpira uliotoboka.Paipo kudhibiti ufisadi na mafisadi,maendeleo yataendelea kuwa ndoto inayogeuka ukweli mchungu kila kukicha.

Na tukitegemea kwamba wanufaika wa ufisadi watajumuika nasi katika kukomesha kilekile kinachowawezesha 'kutanua' na ma-vogue,mahekalu ya bei mbaya na nyumba ndogo zisizohesabika basi tutaendelea kusubiri milele,au kwa lugha nyingine,TUANDIKE TUMEUMIA.

FUNGUKA MACHO,WAKATI NI SASA!.

10 Mar 2010

TAkukuru
Katika toleo jana la gazeti la Mwananchi kuna habari kwamba Mbunge wa Nyang’hwale,James Musalika, alilazimika ‘kuingia mitini’ kuwakwepa makachero wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) waliokwenda katika ‘hafla’ kati ya mbunge huyo na wapiga kura.Kwa mujibu wa Mwananchi,hatua hiyo ya wanadola wa TAKUKURU ni katika utekelezaji wa ‘ruhusa’ waliyopewa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete ‘kudhibiti wanasiasa wanaotoa rushwa kwenye chaguzi’.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.