26 Jun 2010

Sijui ni ukosefu wa mawasiliano au uzembe tu,au pengine ni mkakati wa makusudi wa kutoa kauli zinazotofautiana ili baadaye iwe rahisi "kuziruka kimanga",lakini ni dhahiri kuwa mmoja kati ya viongozi hawa anatudanganya.Wakati Waziri wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe akirejea ahadi kama ya mwaka 2005 (wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu) kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi,Makamu Mwenyekiti wa CCM Pius Msekwa anasema bayana kuwa suala hilo halipo (labda Waislamu wenyewe walishughulikie "kivyao").Hebu soma kwanza hapa chini

Kwa mujibu wa Gazeti la Tanzania Daima: SERIKALI imesema Mahakama ya Kadhi itaanza katika mwaka wa fedha 2010/11 baada ya jopo la wanazuoni wa Kiislamu wanaoziangalia na kuzihuisha sheria za Kiislamu kukamilisha kazi hiyo.

Jambo hilo lilibainishwa jana bungeni na Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe wakati akisoma hotuba ya makadirio ya matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2010/2011 ambapo ameliomba Bunge limuidhinishie kiasi cha sh bilioni 116.8

Alisema kuwa jopo hilo linaziangalia na kuzihuisha sheria za Kiislamu zinazohusiana na ndoa, mirathi na urithi kwa madhumini ya kuziorodhesha ili zitambuliwe chini ya sheria za dini ya Kiislamu (Islamic Law resstatment act).

Aliongeza kuwa jopo hilo lilianza kazi hiyo baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kukutana na Mufti, Sheikh Mkuu, Issa Bin Shaaban Simba, na kukubaliana kuwa waanzishe mchakato wa Mahakama ya Kadhi.

Lakini Gazeti la Majira linaripoti kwamba:

Katika hatua nyingine, Bw. Msekwa amefafanua sababu za ilani ya CCM mwaka huu kutohusisha kipengele cha uanzishwaji wa Mahakam ya Kadhi kama ilivyokuwa mwaka 2005.

Alisema kuwa ahadi hiyo iliyotolewa 2005 tayari utekelezaji wake umekamilika.

Katika ilani hiyo, kifungu namba 108(b) CCM iliahidi kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa mahakama ya kadhi Tanzania bara, ambalo limekamilika kwa kukabidhi wenye dini yenyewe wahusike katika uanzishwaji wa mahakama hiyo, kwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siyo ya kidini.

"Serikali inaweza kukubali au kukataa, ndiyo maana ya kulipatia ufumbuzi lakini watu wanalitafsiri vibaya kuwa
serikali kupitia kifungu hicho imekubali kuanzishwa kwa mahakama hiyo wakati sivyo," alisema Bw. Msekwa.

Alibanisha kuwa serikali ilifanyia kazi kupitia Tume ya Kurekebisha sheria ambayo ilishauri kwamba haitakuwa sahihi kwa mahakama ya kadhi kuundwa na serikali kwa kuwa ni suala linalohusu taratibu za dini ya kiislamu.

Aliongeza kuwa baada ya serikali kupata ushauri huo ilifanya uamuzi kwamba haitaunda mahakama ya kadhi lakini kwa kuwa suala hilo linahusu taratibu za dini la kiislamu, waislamu wapo huru kuunda mahakama hiyo ndani ya taratibu za dini yao.

21 Jun 2010

Zaidi ya shilingi bilioni 150 zimefisadiwa kutoka katika Mfuko wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi,na hiyo ni kwa mwaka juzi (2008) pekee. Kiasi hicho kinajumuisha shilingi bilioni 71.2 zilizotengwa katika mwaka wa fedha 2007/8 lakini hazifika mahala zilipokusudiwa.Utafiti unachofuatilia mwenendo wa matumizi ya fedha za umma-PETS (Public Expenditure Tracking Survey)kinaonyesha kuwa takriban shilingi bilioni 47 zinatafunwa kila mwaka kwa udanganyifu wa malipo hewa katika sekta ya elimu.


Ripoti inayoonyesha ufisadi huo,ambayo ni ya kina zaidi kuliko zilizotangulia,ilikabidhiwa kwa serikali tangu mwezi April mwaka jana.

Gazeti la Citizen limepata nakala ya ripoti hiyo ambayo inaonyesha kwa kiasi gani udhibiti hafifu wa mifumo ya fedha za umma unavyochangia kushuka kwa kiwango cha elimu nchini.

Serikali iliamua kuagiza utafiti huo kwa shule za msingi na sekondari Tanzania Bara ili kubaini kama kutanuka kwa miundombinu ya elimu na kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na shule kunaendana na kuongezeka kwa raslimali zinazotengwa.

Kadhalika,ilitaka kufahamu kama raslimali zinafika kwa watoa huduma,hususan shule, na kwa kiwango gani mipango ya utanuzi imetekelezwa pasipo kuathiri kiwango cha ubora wa elimu kwa kuzingatia kipimo cha matokeo ya wanafunzi.

Taasisi zilizoshirikishwa katika kipimo hicho ni pamoja na Wizara za Elimu na Mafunzo,Fedha na Mipango ya Uchumi,Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa),Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto,na Shirika la Taifa la Takwimu (TBS).Kadhalika,wawakilishi wa vikundi vya kiraia na wahisani walihusishwa.

Kwa majibu wa matokeo ya utafiti huo,wakati kwa miaka kadhaa sasa serikali imekuwa ikiongeza bajeti ya elimu kutoka shilingi bilioni 701.1 mwaka 2005/6 hadi kufikia shilingi trilioni 1.43 mwaka 2008/9 na shilingi trilioni 2.045 kwa mwaka 2010/11,raslimali kwa elimu ya msingi zimekuwa zikishuka kutoka asilimia 55.8 zilizotengwa miaka mitano iliyopita hadi asilimia 46.6 mwaka juzi.

Fedha kwa ajili ya ujezi wa madarasa,nyumba za walimu,vyoo na miundombinu mingine pia zimekuwa zikishuka kwa kasi.Wakati wastani wa fedha zilizotengwa zilikuwa wastani wa shilingi bilioni 109 katika awamu ya kwanza ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (PEPD)kutoka mwaka 2002 hadi 2006,kiwango hicho katika mwaka wa fedha 2010/11 kimeshuka hadi kufikia shilingi bilioni 14 tu katika awamu ya pili ya PEPD kuanzia mwaka 2007 hadi 2011.

Na athari ni za hapo kwa hapo na za kina.Kwa mujibu wa takwimu,wakati madarasa 10,771 yalijengwa miaka saba iliyopita,idadi hiyo imepungua hadi kufikia 1,263 katika mwaka 2008.Hiyo ni mbali ya ukweli kwamba uwiano kati ya wanafunzi na uwezo wa darasa ulikuwa 1:78 kwa mwaka huo ni takrban maradufu ya uwiano stahili wa darasa moja kwa wanafunzi 40 (1:40)

Pia Utafiti huo ulibaini kuwa wakati shilingi bilioni 544.2 zilitolewa kwa manispaa kama mtaji na misaada ya kawaida kwa sekta ya elimu katika mwaka wa fedha 2008,kiwango halisi kilichopokelewa kilikuwa shilingi bilioni 473 na kuacha pengo la shilingi bilioni 71.2

Kadhalika,utafiti huo unaonyesha kuwa mamlaka 66 kati ya 131 zilizohusishwa katika utafiti huo zilielekeza shilingi bilioni 28.9 kwenye matumizi mengineyo badala ya minajili ya elimu kama ilivyokusudiwa.

Mwaka 2008,serikali iliwapangia vituo walimu wapya 1271 katika maeneo ya vijijini lakini ni asilimia 35 tu (walimu 444) walioripoti maeneo hayo.Lakini,wakati jiji la Dar es Salaam lilipangiwa walimu 182 tu,mamlaka husika ziliajiri walimu 441.

Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la The Citizen



20 Jun 2010

RAIS Jakaya Kikwete ameliponda Shirika la Haki Elimu kwa kusema ni waongo, wazushi na wanafiki.

“ Ukweli siku zote hujitenga na uongo Haki Elimu ni waongo, wazushi na wanafiki wanapodiriki kuwatangazia umma wa watanzania eti kuna uhaba wa nyumba za walimu zipatazo 22,000 nchini na kwamba Serikali ya Nne kwa kipindi chote cha utawala wake kimemudu kujenga idadi ya nyumba za walimu zipatazo 300 tu haya ni matusi kwetu….kweli akutukanae hakuchagulii tusi…..watu wazima ovyoo” amesema Rais

---------------------------------------------------------------------------------------------------------
RAIS Jakaya Kikwete amesema Serikali ya Awamu ya Nne imetekeleza kwa vitendo ahadi zote za uchaguzi ilizowaahidi wananchi ukiwamo ujenzi wa miradi mikubwa mitatu ya barabara kuu za mkoa wa Rukwa zenye urefu wa kilometa 657.5 kwa kiwango cha lami.

“Tuliyowaahidi wananchi tumeyatekeleza kwa hakika tumefanikiwa vizuri sana katika ujenzi wa barabara, elimu na afya,”

Alisema hayo juzi wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kiwanja cha michezo cha Nelson Mandela mjini hapa, huku akishangaa wanaobeza safari zake za nje ya nchi.

Alisema watu hao hawamnyimi usingizi hata kidogo na alihoji kama asingekwenda Marekani kuonana na Rais George Bush (mstaafu) nani angefadhili ujenzi wa mradi mkubwa wa barabara ya Tunduma – Laela – Sumbawanga yenye urefu wa kilometa 224.5 kwa kiwango cha lami.

LAKINI NI MAJUZI TU GAZETI LA HABARI LEO LILIMNUKUU RAIS AKISEMA YAFUATAYO

AHADI ambazo hazijatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Nne zitatekelezwa katika Bajeti hii ya mwaka 2010/11, imeelezwa.

Akizungumza jana mjini hapa katika kikao cha kazi na wakuu wa mikoa na wa wilaya pamoja na makatibu tawala wa mikoa yote Tanzania Bara, Rais Jakaya Kikwete aliwataka viongozi hao kusimamia shughuli za Serikali kikamilifu.

Aliwataka kutokwenda likizo katika kipidi hiki cha kuelekea uchaguzi na wasimamie kazi kama wanavyofanya wakati wote.
Rais Kikwete alisema katika kipindi cha miaka mitano tangu Serikali yake iingie madarakani mengi waliyoahidi yametekelezwa.

“Juzi kabla ya Bajeti hata kwenye Baraza la Mawaziri, tulizungumzia ahadi zetu na nyingi tumeshazitekeleza, lakini zilizobaki na majukumu tuliyojipangia kwa miaka yote hii tutatekeleza katika Bajeti hii … tulipoingia mwaka wa kwanza, tulitekeleza ya Awamu ya Mzee Mkapa (Rais mstaafu Benjamin) sasa tunaendelea na kutekeleza yetu,” alisema.

SASA KAMA AHADI ZOTE ZIMESHATEKELEZWA,HIZO ZINAZODAIWA KUTEKELEZWA KATIKA BAJETI HII YA 2010/11 NI AHADI ZIPI TENA?

NA SOTE TUNAKUMBUKA THE MOTHER OF ALL PROMISES,ILE YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.HIVI KWELI RAIS KIKWETE ANATAKA KUTUAMBIA KUWA KILA MTANZANIA HIVI SASA ANA MAISHA BORA?

KADHALIKA JK ALITAMKA BAYANA KUWA ANAWAFAHAMU WALA RUSHWA KWA MAJINA NA KUSEMA ANAWAPA MUDA WAJIREKEBISHE VINGINEVYO ANGEWACHUKULIA HATUA.JE RAIS ANAPOTUAMBIA KUWA AHADI ZOTE ZIMESHATEKELEZWA ANAMAANISHA TATIZO LA RUSHWA NALO LIMEKWISHA?AU ANAMAANISHA WALA RUSHWA ALOSEMA ANAWAFAHAMU KWA MAJINA WAMEAMUA KUJIREKEBISHA?

-----------------------------------------------------------------------------------------------
RAIS Jakaya Kikwete amewataka wanaume wasiwe 'mafataki', wawaache watoto wa kike wasome.

Kikwete amesema, wanaume wanapaswa kuwafuata wanawake wakubwa wenzao na si watoto, na kwamba, wanawake wapo wengi.

“Ninachowaomba wanafunzi wa kike washuhulike na masomo, mambo ya mimba yaacheni… kina baba waacheni watoto wa shule kina mama watu wazima wamejaa tele acheni kupiga ufataki” Rais Kikwete ameyasema hayo wakati anajibu swali la mtoto Rehema Abbas wa Dar es Salaam.

HAYA NI MAENDELEO MAPYA BAADA YA KIKWETE HUYUHUYU KUSEMA YAFUATAYO HIVI KARIBUNI

JK: Mimba kwa wanafunzi ni kiherehere chao

Monday, 07 June 2010 07:33
Rais Jakaya Kikwete amesema matukio ya mimba kwa wanafunzi wa kike nchini yanasababishwa na viherehere vya wanafunzi wenyewe.

Aidha, Rais Kikwete amekiri kwamba matukio ya mauaji ya vikongwe pamoja na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), yanalidhalilisha taifa.

Rais Kikwete alitoa kauli hizo katika kijiji cha Kisesa wilayani Magu jana wakati akihutubia wananchi kwenye ufunguzi wa mashindano ya ngoma kwa kabila la Wasukuma; ngoma ambazo zinajulikana kama 'Bulabo'.

" Kila anayepata Ukimwi anaufuata mwenyewe na wengine ni viherehere vyao; kwa mfano watoto wa shule," alisema Rais Kikwete wakati akijibu risala ya Mkurugenzi wa Makumbusho ya Bujola, Fadha Frasince Sandhu, ambaye alisema ujumbe wa mashindano hayo mwaka huu ni vita dhidi ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Kwa mujibu wa Rais Kikwete, suala la zinaa kwa bianadamu, siyo la lazima hivyo binadamu anaweza kujizuia ama kujikinga kwa kutumia kondomu.
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Instead of counting candles,
Or tallying the years,
Contemplate your blessings now,
As your birthday nears.
Consider special people
Who love you, and who care,
And others who’ve enriched your life
Just by being there.
Think about the memories
Passing years can never mar,
Experiences great and small
That have made you who you are.
Another year is a happy gift,
So cut your cake, and say,
"Instead of counting birthdays,
 Count blessings every day!"

18 Jun 2010

ZIARA ya Rais Jakaya Kikwete mkoani Kigoma jana ilipata mushkeli baada ya gari moja kupinduka wakati msafari wake ukitokea Kibondo kuelekea Kigoma Mjini.

Rais Kikwete, ambaye msafara wake umekuwa ukikumbwa na matukio ya hatari katika muda wa wiki tatiu, alikuwa anaenda Kigoma Mjini kuhitimisha ziara yake hiyo ya siku tatu mkoani hapa.

Awali matukio mawili yaliyoukumba msafara wake yaliyuhusu magari ya Ikulu, likiwemo gari alilopanda wakati akiwa ziara ya wiki moja jijini Dar es salaam ambalo lilichomoka tairi muda mfupi baada ya kushuka, lakini ajali ya jana ilihusu gari la CCM mkoani Kigoma.
. Soma habari kamili HAPA.

17 Jun 2010

Desemba 9 mwakani,Tanzania yetu itatimiza miaka 50 tangu ipate uhuru.Pengine tarakimu 50 inapunguza uzito,kwahiyo ni vema kubainisha kuwa umri huo ni sawa na NUSU KARNE (herufi kubwa kuonyesha msisitizo).Wakati umri huo wa mtu mzima ungepaswa kuwa habari njema,hali ni tofauti kwetu.Tulowakabidhi dhamana ya kutuongoza wanakurupuka na mambo ya ajabu ajabu kana kwamba wako ndotoni au wako kwenye mchezo wa kuigiza usio na ujumbe wowote.

Ngoja niende moja kwa moja kwenye pointi.Hivi Mtanzania mwenzangu inakuingia akilini kweli kusikia kauli kwamba jengo la Bunge letu tukufu "litafanyiwa ukarabati wa kufa mtu" unaotarajiwa kugharimu shilingi bilioni 30.9 "ili kuwawezesha waheshimiwa sana waendane na teknolojia ya kisasa wanapokuwa Bungeni"!!!?Kwa mujibu wa Spika Samuel Sitta mchakato wa ukarabati huo umeshakamilika na unatarajiwa kuanza mara moja,ambapo utapokamilika kila kiti cha mbunge kitakuwa na runinga pamoja na mawasilino ya kisasa ya kompyuta.

Ofkozi,ni muhimu kwenda na wakati katika suala zima la teknolojia lakini pamoja na umuhimu huo shilingi bilioni 30 na ushee ni nyingi mno na tunazihitaji kwenye maeneo mengine yaliyo hio bin taaban kama vile miundombinu,huduma za afya,maji,nk.Hivi kweli runinga kwenye kiti cha mbunge ni muhimu kuliko madawati au nyumba za walimu?Je hizo bilioni 30 zingeweza kujenga zahanati ngapi au visima vingapi vya kuwapatia walalahoi huduma ya maji ya uhakika?

Lakini kabla sijatuliza hasira zangu kutokana na kauli hiyo ya Spika Sitta,JK nae amekuja na mpya akidai kwamba katika miaka mitano ijayo kila mwalimu atakuwa na laptop.Namheshimu sana Rais wangu lakini baadhi ya kauli zake zinanitatiza sana.Hivi kipaumbele katika elimu yetu ya kusuasua ni laptop kwa walimu au makazi bora kwa walimu hao sambamba na kuboreshewa maslahi yao na mazingira yao ya kazi?Mwalimu mwenye laptop anafundishaje wanafunzi waliokaa chini ya mti?Na wakati JK anatoa mpya hiyo hajatuambia umeme wa kuziwezesha laptop hizo utakuwa wa nguvu za jua au zitatumia mafuta ya taa kwani sote tunafahamu uhuni wa TANESCO.


Sijui ni uzembe wa watawala wetu kuelewa matatizo yetu na vipaumbele vyetu kama taifa au ni makusudi tu lakini kwa mwenendo huu itatuwia vigumu kutembea vifua mbele hapo mwakani tutaposherehekea nusu karne tangu tupate uhuru. 

Enewei,hebu soma mazingaombwe hayo HAPA na HAPA.

16 Jun 2010

Having lived in Scotland for nearly a decade,I quite understand why a Scottish football legend is not happy with the inclusion of foreign born players in national teams.The Scots are so proud of their identity that some of their sentiments could easily be mistaken for racism.However,although one could finds racists almost throughout the world,Scotland is generally a very welcoming countries to foreigners.

Hendry was quoted in the Daily Record stating categorically that he would rather see Scotland not reach another World Cup final than "play a fraud like Cacau".He was referring to a Brazilian-born German striker,Claudemir Jeronimo Barretto,commonly known as Cacau,who qualified to play for the Germans because their rules allow for naturalisation after two years' residence in the country.

The Scottish legend who captained Hendry, who captained Scotland at France '98, would "rather go down in history with the distinction of being the last man to do that than see his homeland become a haven for uncapped players".

"Every time I went out on the park to play for Scotland I regarded it as going to war for my country", said Hendry and made it clear that the sight of a German team with one Brazilian and three other players who were born in Poland beating Australia was unappealing to him.

I am certainly sure that even after the Swiss victory over Spain with their sole goal coming from a Cape Verde-born Gelson Fernandes,Hendry, with his Scottish Highland upbringing, which represents tradition, heritage and refusal to make nationality an administrative matter,would change his opinion on the the inclusion of foreign born players in national teams.

In my opinion,however,Scots might as well continue to face humiliation in international football should mentality such as Hendry's continue to dominate.I understand the importance of national integrity and identity when it comes to national teams but in football,like in many other sports,winning is everything.It is a result driven business,and when a team wins,identities of those who made such a victory possible is obviously immaterial.

With globalisation bringing people of different background even closer,it is quite hard to pretend that foreign born citizens have a lesser status and role to play in their current nationalities.Why should the issue of national identity be confined to football when we see how many foreign born GPs saving lives in hospitals?If Hendry is comfortable to be served by a foreign born doctor or nurse,why would he feel that a foreign born German player is "a fraud"?

It's important to embrace our diversity and integration by allowing the few who were not born in Scotland to give something to this country they now call home.It would not in any way whatsoever make "a pure Scots" like Hendry less Scottish,just like the goals scored by the likes of Hendrik Larson didn't make Celtic less Scottish.

And HERE is the Daily Record article in question.

15 Jun 2010

Wakati Waingereza wanasubiri Bajeti ya Dharura ya Serikali mpya iliyoingia madarakani hivi karibuni,watawala hapa wameweka bayana kuwa baadhi ya hatua zitakazochukuliwa kurekebisha uchumi zitapelekea machungu kwa wananchi wengi.Hakuna haja ya kudanganyana kwa vile hata wangeficha ukweli huo,muda wa makali hayo ukifika watawala wangeumbuka.Na ni vema pia kuwatayarisha wananchi ili pindi hali itapokwenda mrama wawe katika tahadhari na wamejiandaa vya kutosha.

Lakini kwa watawala wetu,kusema ukweli ni kama kujivunjia heshima.Na si kwa wao tu,bali hata wananchi wanapoamua kuweka bayana hisia zao kuwa nchi yetu inapelekwa pabaya,watawala wanaona kama wanakosewa heshima.Kilichopelekea niandike makala hii ni kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa ahadi ambazo hazijatekelezwa katika miaka minne iliyopita zitatekelezwa katika bajeti hii.Sijui ni ushauri mbovu wa washauri wake,sijui ndio kampeni,au sijui ni kuwafanya Watanzania mabwege sana,lakini kwa kila anayefahamu hali ya uchumi wetu na wingi wa ahadi zilizokwishatolewa ni dhahiri kuwa kauli hiyo sio ya kweli.

Kikwete anapaswa kurejea ahadi alizotoa wakati wa kampeni zake mwaka 2005,na alizoendelea kutoa katika miaka minne iliyopita,kisha angejaribu kuangalia nini kimekwaza ahadi hizo.Hebu kwa minajili ya makala hii tuangalie baadhi ya ahadi hizo na kutathmini kama kweli bajeti hii ya kutegemea hisani za wafadhili itaweza kutimiza ahadi hizo.JK alinukuliwa mwezi August 2008 akisema tatizo la umeme lingepatiwa ufumbuzi wa kudumu.Miezi michache baadaye ufumbuzi ukapatikana,si kwa wananchi bali kwa akaunti za matapeli wa Richmond.Je ni kweli kuwa bajeti hii itaweza kutimiza ahadi hiyo ya JK kuhusu tatizo la umeme?Na mbona hatuelezi utatuzi huo utakuwaje?

Twende kwenye suala la rushwa na ufisadi.JK alitamka bayana kuwa watu wasitafsiri vibaya tabasamu lake kwani hatakuwa na huruma kwa fisadi yoyote yule.Akaenda mbele zaidi kutanabaisha kuwa anawafahamu wala rushwa na anawapa muda wa kujirekebisha.Sote tunajua kinachoendelea katika Awamu hii ya Nne chini ya JK.Ufisadi umeota mizizi kupita kiasi huku mafisadi wakiendelea kulindwa,na wanaojiuzulu wanafarijiwa kuwa "kuna siku watarejea serikalini".Hivi ni kweli kuwa bajeti hii itawezesha utekelezaji wa ahadi hiyo ya JK kupambana na mafisadi?Kilichomshinda katika miaka minne iliyopita kitawezekanaje miezi hii michache kabla ya uchaguzi?Na je inahitaji bajeti moja kabla ya uchaguzi kumwezesha kuwadhibiti mafisadi?


Anyway,hebu soma kauli zake katika habari ifuatayo kisha ufanye tafakuri jadidi 



Ahadi za JK kukamilika Bajeti hii
Imeandikwa na Na Maulid Ahmed, Dodoma; Tarehe: 12th June 2010 @ 23:52

Ahadi ambazo hazijatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Nne zitatekelezwa katika Bajeti hii ya mwaka 2010/11, imeelezwa.

Akizungumza jana mjini hapa katika kikao cha kazi na wakuu wa mikoa na wa wilaya pamoja na makatibu tawala wa mikoa yote Tanzania Bara, Rais Jakaya Kikwete aliwataka viongozi hao kusimamia shughuli za Serikali kikamilifu.

Aliwataka kutokwenda likizo katika kipidi hiki cha kuelekea uchaguzi na wasimamie kazi kama wanavyofanya wakati wote.
Rais Kikwete alisema katika kipindi cha miaka mitano tangu Serikali yake iingie madarakani mengi waliyoahidi yametekelezwa.

“Juzi kabla ya Bajeti hata kwenye Baraza la Mawaziri, tulizungumzia ahadi zetu na nyingi tumeshazitekeleza, lakini zilizobaki na majukumu tuliyojipangia kwa miaka yote hii tutatekeleza katika Bajeti hii … tulipoingia mwaka wa kwanza, tulitekeleza ya Awamu ya Mzee Mkapa (Rais mstaafu Benjamin) sasa tunaendelea na kutekeleza yetu,” alisema.

Akizungumzia uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu, alisema “tunakwenda kwenye uchaguzi na michakato imeshaanza, lakini Serikali haiendi likizo, usione uchaguzi nawe ukaenda likizo, fanya shughuli za maendeleo kwa kuzisimamia kama mnavyofanya wakati wote”.

Alisema hataki kuona uchaguzi unaharibikia mikononi mwa viongozi hao na kuwataka kuhakikisha wagombea hawanyimwi haki ya kumwaga sera zao majukwaani, kura zinapigwa kwa amani na kunakuwa na utulivu wakati wote, kuanzia mchakato wa wagombea hadi uchaguzi.

Rais Kikwete aliyehutubia viongozi hao kwa dakika 10, alitaja baadhi ya mafanikio ya Serikali yake, kuwa ni kuendelea na ujenzi wa barabara za lami, watoto kusoma elimu ya msingi na sekondari, upanuzi wa elimu ya juu na huduma bora za afya kupatikana...

CHANZO: Habari Leo

Japo mie si mchambuzi mzuri wa soka lakini naamini utaafikiana nami kuwa Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini zimeendelea "kuboa" wapenzi wa soka.Majuzi tumeshuhudia Waingereza walivyopelekeshwa na vijana wa Obama,huku kipa wao akiingia kwenye vitabu vya historia kama kituko cha mwaka.Kati ya wawakilishi wetu sita wa Bara la Afrika,ni Ghana tu waliotupa raha japo kwa ushindi kiduchu.Wenyeji South Afrika walilazimishwa sare (huku wakionyesha bayana kuwa ni wasindikizaji tu),Nigeria wakatutia machungu zaidi kwa kuonyesha kiwango duni dhidi ya Argentina (ambao nao hawakuonyesha kiwango kilichotarajiwa),Cameroon ndio wakatukata maini kwa kiwango cha chini kabisa cha soka huku Algeria wakifanya kilichotarajiwa (wasindikizaji).Matumaini ya Afrika sasa yamebaki kwa Ivory Coast wanaoingia dimbani mchana huu (kwa mida ya hapa Uingereza).


JapoUjerumani na Uholanzi, vigogo wengine wanaotarajiwa kufanya vizuri kwenye michuano hiyo,wameshaonyesha makali yao huku tukisubiria kuwaona Brazil,Uhispania na Ureno,sare ya Italia kwa Paraguay imeacha maswali kama Wataliano ni tishio kweli kama ilivyotarajiwa,japo wanafahamika kwa tabia yao ya kubadilika kadri michuano inavysonga mbele.

Kwahiyo,kwa kifupi hadi sasa Fainali hizo zinaweza kuelezwa kama "zinaboa" kwa kiasi flani japo ni mapema mno kufikia hitimisho hilo.By the way,hii ni wiki ya kwanza tu na kuna timu kadhaa ambazo hazijaingia dimbani.Yote katika yote,mshindi bayana katika kinyang'anyiro hicho ni VUVUZELA,matarumbeta yanayoendelea kutawala vichwa vya habari kuhusiana na michuano hiyo.

Wakati kuna "kelele" (mithili ya hizo za Vuvuzela) kwamba matarumbeta hayo yanakera huku wengine wakitaka yazuiliwe,Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) na waandaaji wa michuano hiyo wameweka bayana msimamo wao kuwa Vuvuzela ni sehemu muhimu katika michuano hiyo.Ni utamaduni wa wenyeji,na kama tunavyofahamu "ukienda kwa Warumi inabidi uishi kama Warumi".Hata hivyo,tayari hatua kadhaa zimeanza kuchukuliwa dhidi ya kelele za Vuvuzela.Kituo cha runinga cha BBC kinachoonyesha michuano hiyo kwa hapa Uingereza (wakipokezana na ITV ya hapa) kina mpango wa kuwezesha watazamaji kubonyeza kitufe chekundu kwenye runinga zao ili "kuondokana na kelele za Vuvuzela" baada ya kupokea malalamiko 545 kutoka kwa watazamaji wanaodai kuwa matarumbeta hayo "yanawazingua".

Kadhalika,kampuni inayotengeneza Vuvuzela imetangaza aina mpya ya matarumbeta hayo ambayo itakuwa na "kelele pungufu",hatua inayotarajiwa kupunguza malalamiko zaidi.Jana,mchezaji Robin van Persie wa Uholanzi alionekana akilalamika kwa refarii kuwa hakusikia firimbi kuwa ameotea kutokana na kelele za Vuvuzela.Kadhalika,kipa wa timu ya Denmark Thomas Sorensen alieleza kuwa angetumia lugha za alama (sign language) kuwasiliana na wachezaji wenzie kwa vile Vuvuzela "zilikuwa zikimeza sauti yake".Mwanasoka wa Ureno,Christiano ametamka bayana kuwa angependa kuona Vuvuzela zikipigwa stop katika michuano hiyo.


Na kama wasemavyo Waswahili kuwa "kufa kufaana",tayari kuna "wajanja" wameibuka kutengeneza faida kutoka kwa wanaokerwa na kelele za Vuvuzela.Kampuni moja ya Ujerumani inaripoti kuwa imevumbua "teknolojia ya kuchuja kelele za Vuvuzela"ambapo mtazamaji akichomeka kidude kiitwachoSurfpoeten kwenye runinga yake,basi makelele ya Vuvuzela yanakuwa kwishne (angalia picha ifuatayo).
Lakini wakati hayo yakitokea,umaarufu wa Vuvuzela unazidi kupaa kiasi cha baadhi ya watu kuhisi kuwa bila kujali yeyote atakayetwaa ubingwa katika Fainali hizo,mshindi halisi atabaki kuwa Vuvuzela.Inaripotiwa kuwa supamaketi maarufu hapa Uingereza,Sainsbury,imeshauza Vuvuzela 22,000 katika masaa 12 ya mwanzo wa mashindano hayo na mchezaji wa Timu ya Taifa ya Uingereza Jamie Carragher ameshanunua Vuvuzela mbili kwa ajili ya wanawe.Kadhalika,inatarajiwa kuwa msimu ujao wa Ligi Kuu ya hapa utashuhudia Vuvuzela kadhaa kwenye mechi mbalimbali.Wachezesha kamari wa Paddy Power wanaendesha kamari ya kubashiri timu gani itakuwa ya kwanza kuuza matarumbeta hayo kwa mashabiki wake huku Manchester United wakiongoza kwa turufu ya 4/1.

Na katika kuthibitisha kuwa Vuvuzela imejichukulia umaarufu mkubwa,tayari kuna app ya Vuvuzela kwenye simu ya kisasa ya iPhone.Well,kama kuwepo kwa app hiyo hakujakuonyesha umaarufu wa Vuvuzela,idadi ya dowloads yaweza kukushawishi kwani tayari apps 750,000 (yaani robo tatu ya milioni) za Vuvuzela zimeshakuwa downloaded tangu ilipozinduliwa.Inatarajiwa kuwa Vuvuzela app (angalia picha yake hapo chini) itaweza kutumika kwenye iPad na iPod.


Mwisho,kama kuna watu wananufaika vya kutosha na vuguvugu la Kombe la Dunia basi ni Rais wa TFF Leodgar Tenga na wababaishaji wenzake waliojiingiza mkenge kuialika Brazil kisha kuambulia kipigo cha magoli matano na hasara ya bilioni kadhaa.Hata hivyo,licha ya usahaulifu wa kawaida wa Watanzania,michuano hiyo inawasaidia sana akina Tenga kwa vile macho ya mashabiki wengi wa soka wa Tanzania yameelekezwa huko Afrika Kusini na hivyo kusahau kuhusu deni walilobebeshwa na akina Tenga.Ni dhahiri kuwa michano hiyo itapomalizika mwezi ujao,habari ya hasara na deni hilo itakuwa imezikwa na kusahaulika kabisa.

13 Jun 2010


Picha na Habari (bonyeza hapa uisome) kwa Hisani ya MICHUZI

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.