18 Sept 2010


Tunasikitiza kutangaza kifo cha Pr. Joseph Shem Onyango (pichani akiwa na mkewe na wajukuu) Kilichotokea jana mchana Kihonda, Morogoro kutokana na ajali ya barabarani. Mchungaji alikuwa akielekea kwenye kituo cha basi tayari kwa safari ya kwenda dar kushiriki katika sabato ya wageni jumamosi tarehe 18.9.10 kwenye kanisa la Tegeta. Marehemu alizaliwa 1936 na amekuwa akililitumika kanisa la waadeventista wasabato kwa zaidi ya miaka 40, Pr. atakumbukwa sana na watu wengi africa mashariki kutokana na huduma zake kwenye kanisa za kaya na familia pamoja na sera za ndoa.

Mazishi yanategemewa kufanyika alhamisi mji wa morogoro.

Asanteni

Frank Eyembe
Urban Pulse Creative

BLOGU HII INATOA SALAMU ZA POLE KWA WAFIWA.BWANA AMETOA BWANA AMETWAA,JINA LAKE LIHIMIDIWE MILELE


Sijaitunga mimi,nimeipokea tu,nikasioma na kuisambaza

Ee KIKWETE Uliye tufilisi, 
Jina lako USANII MTUPU, 
utakalo lifanyike BAGAMOYO TU,
utupe leo mabilioni yetu ya EPA, uwapeleke MAFISADI wote Mahakamani, 
uwape WASTAAFU pesa zao, 
uwasamehe wafungwa hasa BABU SEYA kama ulivyomsamehe LOWASA, 
Usitutie katika mikataba FEKI,
 kwa kuwa UFISADI ni fani yako na uwongo hata milele, 
na Uanguke kwenye uchaguzi ujao kama unavyoanguka hovyo jukwaani, AMINA 


UPDATE: Nimetumiwa Sala nyingine,hii inamhusu Dokta Slaa,nimeisoma na kuisambaza



""IMANI YA CHADEMA""
Namwamin Dk.WILBROAD, mwana wa SLAA, Ndugu Yetu, aliyepitia vikwazo vingi kwa hujuma za CCM. Akateswa kwa kashfa za Ndoa, Akadhihakiwa, Akapingwa, Akaonyesha msimamo; Siku ya siku akasimama kwa kishindo; Akapaza sauti, Ameketi mkono wa kuume kutetea haki za Watanzania; Kutoka huko atakuja kuwahukumu mafisadi.

16 Sept 2010




Zambian First Lady Dragged to Court

Zambian First Lady has been dragged to court for “unconstitutionally” using public resources to campaign for President Rupiah Banda's re-election bid in the 2011 General Election.

According to a statement of claim filed in the Lusaka High Court, the plaintiffs - Evelyn Kangwa and Marjorie Nakaponda - contended that Ms Thandiwe Banda has been using public funds, helicopters and vehicles to tour the country when in fact she was not entitled to the same in the constitution.

They stated that in August 2010 alone, the president's wife visited seven districts in Northern and Luapula provinces using two Zambia Air Force (ZAF) helicopters.

In the said districts, the duo said that Ms Banda visited traditional rulers and women clubs, and gave out money without disclosing the source of the same.

Ms Nakaponda and Ms Kangwa added that during Ms Banda’s visit to Chiengi District, she urged the residents to vote for Mr Banda in the 2011 presidential elections.
Source of money

They added that during the First Lady's visit to Mpulungu and Isoka districts, she was involved in the distribution of the ruling Movement for Multiparty Democracy (MMD) hammer mills and bicycles that were all transported in government vehicles.

The matter will come up before Lusaka High Court judge Phillip Musonda on September 24, 2010.

Zambia’s main opposition leader Michael Sata wrote to President Banda demanding to know the source of the money his wife was “generously giving out” to various women’s clubs countrywide, including Mpulungu constituency, which is due to hold parliamentary by-elections next month.
In addition, a local lobby group, the Anti Voter Apathy Project (AVAP), said Ms Banda had been distributing campaign materials bearing the portrait of President Banda.

Zambia’s ruling party spokesperson Dora Siliya defended Ms Banda, arguing that the First Lady was doing what every other previous First Lady had done in the country.

According Zambian Constitution, a First Lady has no immunity from prosecution. Further, the national budget does not provide funds for her as an individual.

News article sent by Mwl Nkuzi Mhango


NAPENDA KUWAPA TAARIFA WADAU WOTE WA CHEKA UPASUKE KUA, PAMOJA NA KUCHEKA PAKA KUPASUKA SASA WATAWEZA ANGALIA FILAMU BILA CHENGA FILAMU MPYA TOKA NJE NA ZENGINE KIBAO KILA SIKU, MTAPATA VINJALI NA KUTAZAMA MKIWA HAPA CHEKA UPASUKE. FILAMU ZOTE NI SALAMA HIVYO BASI KATIKA KUZIDI KUENDELEZA BURUDANI ZAIDI KWA WADAU WA CHEKA UPASUKE NAWASIHI TENA KUENDELEA KUWEPO ENEO HILI MAANA MAMBO ZAIDI PAMBA MOTO BILA KUSAHAU VICHEKESHO BADO VIPO KILA SIKU KAMA KAWAIDA PIA KATUNI.SHUKRANI KWENU WOTE KUENDELEA KUA PAMOJA KATIKA KUSOGEZA GURUDUMU. ASANTENI SANA.

15 Sept 2010



A retired doctor held a slave in her suburban home for four years, a court was told yesterday. Saeeda Khan, 68, is accused of making Mwanahanisi Mruke work up to 24 hours a day cleaning, cooking and gardening. She fed her scraps of bread and made her sleep on a thin mattress on the kitchen floor with only a sheet for warmth, it was alleged.

 Khan and her late husband, who was also a doctor, allegedly paid Miss Mruke just £10 a month – a low salary even in Tanzania, the African country they brought her to Britain from in 2006. Miss Mruke, 46, had all her calls monitored and was not allowed to leave the £500,000 home in Harrow, North West London, without Khan, Westminster magistrates heard. ‘She lived in extremely poor conditions for a number of years,’ prosecutor Malachy Pakenham told the hearing. Additional payments of £40 a month were meant to go to a bank in Tanzania to pay for Miss Mruke’s daughter’s education, but much of this was never received, the court heard.

Khan, a British citizen who has lived in the UK for 30 years, is believed to be the first person charged with modern slavery. Scotland Yard detectives started investigating the case in February following a tip-off. Officers from the Human Exploitation and Organised Crime Command, known as SCD9, were involved. Khan did not have to sit in the dock during the ten-minute hearing because she suffers from arthritis and has recently had an operation on her knees.

She pleaded not guilty to a charge of arranging and facilitating the arrival of a foreign national with the intention of exploitation in the UK and elsewhere. The charge carries a maximum sentence of ten years in jail. Khan was bailed to appear before the court next month. Before she came to the UK, Miss Mruke worked in a hospital run by Khan’s late husband in Dar es Salaam, the capital of Tanzania. Khan is alleged to have kept her slave in her three-bedroom bungalow in Harrow which she shared with her 40-year-old son, who has mental health problems. Khan’s daughter, who also has learning difficulties, lived in the property too but has since moved out. Neighbours said Khan spent tens of thousands of pounds renovating the property when she moved in about a decade ago. Two cars, including a new Volvo estate, are usually seen parked in the driveway.

James Carpenter, who lives next door, said he often saw Miss Mruke going for walks with Khan’s son. He said: ‘She would follow him up and down the street, normally about ten yards behind him. ‘She only spoke the East African language of Swahili, so we couldn’t communicate with her and she couldn’t really speak to anyone. ‘Sometimes, we would wave and nod at her just to be polite. She would normally wave back. ‘She wore normal, western clothing. I had no reason to suspect anything untoward was going on. ‘But it’s a very quiet area and nobody round here really knows their neighbours very well.’

Slave trading has been outlawed in Britain since the 19th century. However, the UK remains a major destination for trafficked women. Human rights organisations claim up to 1,000 people are made to work as slaves.


Dharau inayoonyeshwa na mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kuendelea kutoa ahadi zaidi ilhali nyingi ya alizotoa mwaka 2005 hazijatimizwa,sasa imehamia kwa mkewe.Katika ukurasa wake wa Twitter (@salmakikwete),mke huyo wa Rais ameandika "“Tuwasikilize,tupembue chuya zikae upande wake,chenga upande wake na mchele ukae upande wake,tuseme lililo lililo la kweli,kama serikali haitatoza kodi,itaendeshaje shughuli zake?” Kauli hiyo pia inapatikana kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Kwanza,pamoja na kumheshimu kama First Lady lakini ilipaswa huyu mama akae kimya.Anatumia raslimali za taifa kumkapeni mumewe wakati anafahamu fika yeye (Salma) si mgombea.Huu ujasiri wa kinafiki wa kutetea kodi sijui unatoka wapi kwa vile tatizo letu kama taifa sio tu kwenye uzembe katika ukusanyaji kodi bali pia matumizi mabaya ya hata hiyo kodi ndogo inayokusanywa baada marafiki wa watawala kupewa misamaha ya kido kifisadi.

Hivi huyu mama anafahamu kuwa mumewe alipofanya ziara ya ghafla Bandari ya Dar es Salaam alitamka waziwazi kuwa anawafahamu watu wanaofanya ufisadi bandarini hapo?Na miongoni mwa ufisadi mkubwa sehemu hiyo ni dili za kukwepa kodi.

Sasa kama kweli ana uchungu na mapato ya serikali kwanini asimkumbushe mumewe kuhusu majina ya mafisadi wa Bandari ambao hadi dakika hii hajawataja au kuwasilisha majina yao kwa wahusika?

Kama unadhani namsingizi Kikwete hebu soma habari ifuatayoiliyochapishwa na gazeti la Nipashe la Machi 3 mwaka huu

Nawajua wanaosaidia kukwepa kodi TRA- Kikwete
2009-03-03 10:59:53
Na Joseph Mwendapole
Rais Jakaya Kikwete amesema ana orodha ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) wasio waaminifu ambao wanashirikiana na wafanyabiashara kukwepa kodi kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Alisema anaifanyia kazi orodha hiyo na akishamalizana nayo atamkabidhi Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya, ili achunguze na kuwafukuza kazi wafanyakazi watakaothibitika kujihusisha na vitendo hivyo.
Aliyasema hayo jana wakati akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari (TPA) na wadau wa bandari Tanzania alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni ufuatiliaji wa agizo alilotoa mwezi uliopita kupunguza msongamano wa makontena.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia watu wanaoikosesha mapato.
Akitoa mfano namna wizi huo unavyofanywa, Rais Kikwete alisema wanaweza kuendesha zoezi hilo kwa simu ambapo mtu aliyeko Dubai anapewa maelezo namna atakavyojaza fomu ili mzigo wake usipite kwenye scanner, hali inayoweza kupitisha mizigo haramu kama dawa za kulevya.
Alisema wafanyakazi na wafanyabiashara hao wanatumia udanganyifu kuwa kontena hizo zimebeba mitumba, kumbe ndani ya mitumba hiyo wakati mwingine inatumika kufunika magari.
``Ninayo orodha ndefu na nitaikabidhi kwa Kamishna Mkuu wa TRA, Kitilya ili awafuatilie na ahakikishe anawatimua kazi mara moja wale watakaobainika wanahusika na mchezo huo ili tuanze upya,`` alisema.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia kuwa na wafanyakazi wanaokula njama za kuipotezea mapato.
Kikwete alisema bandarini kuna uzembe mkubwa ambao hauvumiliki na aliuagiza uongozi kuondoa matatizo yaliyopo badala ya kukaa na kunung`unika.
Alisema msongamano wa makontena umekuwa ukiisababishia serikali kukosa mapato mengi na alisisitiza kuwa bandari ni sehemu muhimu ambayo serikali haiwezi kuiacha iwe ya hovyo.
Akiwa katika kitengo cha kuchunguza bidhaa katika kontena, Tiscan, Rais Kikwete alisema maelezo aliyopewa na TPA yanatofautiana na yale aliyopewa na viongozi wa Tiscan.
``Hapa mbona mimi sielewi naomba mnieleweshe, hawa Tiscan wanasema wana uwezo wa kuchunguza hata makontena 200 kwa siku ila wanasema tatizo ni nyinyi hamleti kontena za kutosha... Jamani fanyeni kazi na muachane na visingizio na malalamiko,`` alisema Kikwete.
Aliagiza mamlaka hiyo impe taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa upunguzaji wa makontena ndani ya wiki mbili zijazo na aliahidi kutembelea tena bandari hiyo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Forodha, Otieno Igogo, alimweleza Rais Kikwete kuwa wadau wa Bandari ya Dar es Salaam walikubaliana kulipa dola 30 ikiwa ni gharama za kuhamishia kontena moja katika bandari kavu.
Igogo alimweleza Rais kuwa ingawa wadau wote wamekuwa wakichangia, Kampuni ya Kimataifa ya Kupakua Kontena Bandarini (TICTS), imegoma kutoa fedha hizo.
Alisema dola 30 ambazo TICTS walipaswa kulipa kwa kila kontena linalohamishiwa bandari kavu kama wanavyolipa wadau wengine, zimekuwa zikitolewa na TPA.
Baada ya kauli hiyo ya Igogo, Rais alisema anashangaa kuona jeuri hiyo ya TICTS na kusema kuwa TPA ina mamlaka, lakini haitaki kuyatumia.
Kikwete alisema TPA imefanya vizuri kulipa gharama ambazo TICTS imekataa kuzilipa, lakini aliagiza mamlaka hiyo ihakikishe TICTS inazirudisha mara moja.
``Nyinyi mnashangaza sana, mna mamlaka, lakini hamyatumii... Sasa hizi gharama lazima walipe na wakiwashinda mwelezeni waziri na waziri akishindwa niambieni mimi,`` alisema.
Wakati huo huo, Kikwete alikataa maelezo marefu ambayo Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraem Mgawe, alitaka kuyasoma mbele yake na badala yake akamtaka amweleze sababu za msongamano kutoma lizika.
Baada ya kuelezwa hivyo, Mgawe alimweleza Rais Kikwete kuwa kikosi kazi kilichoundwa kufuatia agizo lake kinaendelea kujitahidi kuondoa msongamano uliopo.
Alisema Mamlaka inatarajia kuwa utekelezaji wa mikakati iliyowekwa itafanikisha kupunguza hali ya msongamano mwezi Machi mwaka huu.
Mgawe alisema katika kipindi cha mwaka 2007/08, TPA ilihudumia tani milioni 6.239, ambalo ni ongezeko la tani 227,222 au asilimia 3.8 ikilinganishwa na tani milioni 6.003 zilizohudumiwa mwaka 2006/07.
Alisema katika kipindi hicho mamlaka ilipata ziada ya Sh. bilioni 37.879 kutokana na mapato ya Sh. bilioni 168.789 na matumizi ya Sh. bilioni 133.909.
SOURCE: NIPASHE

Wito wangu kwa Salma Kikwete ni simple: kama alikuwa anataka kugombea uongozi angegombea lakini sio kuendelea kutumia raslimali za taifa kumkampenia mumewe.Anapaswa kutambua kuwa raslimali hizo zinagharamiwa na walipa kodi ambapo wengi wao si wana-CCM (takwimu za karibuni zinaonyesha wanachama wa CCM ni takriban milioni 5 tu kati ya Watanzania takriban milioni 45).

Tunatambua kuwa Salma anataka kuendelea kuwa First Lady lakini asifanye hivyo kwa kuwabebesha gharama Watanzania wote hata wasio wana-CCM.Anaweza kuitumia WAMA kumfanyia kampeni mumewe lakini Watanzania hawataki kuona ufisadi wa mchana mweupe unaofanywa kwa misingi ya kifamilia.

Naamini mwanamama huyu anafuatilia habari za kimataifa,na hivyo amesikia yaliyomkumba Vera Chiluba,mke wa aliyekuwa Rais wa zamani wa Zambia,Frederick Chiluba,aliyehukumiwa kwenda jela kwa ufisadi.

Ni vema Salma akasoma alama za nyakati ili pindi mumewe atakapokabidhi madaraka kwa Dokta Wilbroad Slaa hapo Novemba familia ya Kikwete isianze "kutafutana".

Na hiyo "tweet" yake ya kuchambua pumba na mchele nadhani ni vema akiielekeza kwa mumewe ambaye so far anaonekana kunogewa na "ugonjwa" wa kutoa ahadi.Mara uwanja wa ndege Kigoma,mara kuboresha kilimo cha kakao,mara atawapatia akinamama chanjo ya cervical cancer,mara vijiji 11 vya Mkinga vitapatiwa maji,mara hili mara lile alimradi ni "vurugu mechi ya ahadi".Kwani Rais wa Tanzania 2005-hadi sasa alikuwa nani kama sio Jakaya Mrisho Kikwete?Kwanini hayo anayoahidi sasa hakuyatekeleza katika awamu yake ya sasa?Na kwani tuamini kuwa atayatekeleza katika awamu yake ya mwisho-kipindi atakachokuwa bize kujitengenezea mazingira ya "kumpumzika kwa amani" kama Mkapa?

Blogu hii inawakumbusha tena wapiga kura kwamba Kikwete hayuko serious ndio maana ameamua kurejea nyingi ya ahadi zake za 2005 bila aibu wala kuwaomba msamaha Watanzania kwa kutozitekeleza.Kumrejesha tena Ikulu itakuwa ni kosa kubwa kupita kiasi kwani katika awamu yake ya mwisho atairejesha nchi yetu kwenye zama za mawe.

TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA
TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA
TANZANIA BILA KIKWETE,SIO TU INAWEZEKANA,BALI NI MUHIMU LAZIMA KWA USTAWI WA TAIFA LETU.
CHAGUA DOKTA SLAA KWA UKOMBOZI NA "UHURU WA PILI",CHAGUA CHADEMA KWA TANZANIA YENYE NEEMA.


Dharau inayoonyeshwa na mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kuendelea kutoa ahadi zaidi ilhali nyingi ya alizotoa mwaka 2005 hazijatimizwa,sasa imehamia kwa mkewe.Katika ukurasa wake wa Twitter (@salmakikwete),mke huyo wa Rais ameandika "“Tuwasikilize,tupembue chuya zikae upande wake,chenga upande wake na mchele ukae upande wake,tuseme lililo lililo la kweli,kama serikali haitatoza kodi,itaendeshaje shughuli zake?” Kauli hiyo pia inapatikana kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Kwanza,pamoja na kumheshimu kama First Lady lakini ilipaswa huyu mama akae kimya.Anatumia raslimali za taifa kumkapeni mumewe wakati anafahamu fika yeye (Salma) si mgombea.Huu ujasiri wa kinafiki wa kutetea kodi sijui unatoka wapi kwa vile tatizo letu kama taifa sio tu kwenye uzembe katika ukusanyaji kodi bali pia matumizi mabaya ya hata hiyo kodi ndogo inayokusanywa baada marafiki wa watawala kupewa misamaha ya kido kifisadi.

Hivi huyu mama anafahamu kuwa mumewe alipofanya ziara ya ghafla Bandari ya Dar es Salaam alitamka waziwazi kuwa anawafahamu watu wanaofanya ufisadi bandarini hapo?Na miongoni mwa ufisadi mkubwa sehemu hiyo ni dili za kukwepa kodi.

Sasa kama kweli ana uchungu na mapato ya serikali kwanini asimkumbushe mumewe kuhusu majina ya mafisadi wa Bandari ambao hadi dakika hii hajawataja au kuwasilisha majina yao kwa wahusika?

Kama unadhani namsingizi Kikwete hebu soma habari ifuatayoiliyochapishwa na gazeti la Nipashe la Machi 3 mwaka huu

Nawajua wanaosaidia kukwepa kodi TRA- Kikwete
2009-03-03 10:59:53
Na Joseph Mwendapole
Rais Jakaya Kikwete amesema ana orodha ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) wasio waaminifu ambao wanashirikiana na wafanyabiashara kukwepa kodi kwenye Bandari ya Dar es Salaam.
Alisema anaifanyia kazi orodha hiyo na akishamalizana nayo atamkabidhi Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya, ili achunguze na kuwafukuza kazi wafanyakazi watakaothibitika kujihusisha na vitendo hivyo.
Aliyasema hayo jana wakati akizungumza na viongozi wa Mamlaka ya Bandari (TPA) na wadau wa bandari Tanzania alipotembelea Bandari ya Dar es Salaam ikiwa ni ufuatiliaji wa agizo alilotoa mwezi uliopita kupunguza msongamano wa makontena.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia watu wanaoikosesha mapato.
Akitoa mfano namna wizi huo unavyofanywa, Rais Kikwete alisema wanaweza kuendesha zoezi hilo kwa simu ambapo mtu aliyeko Dubai anapewa maelezo namna atakavyojaza fomu ili mzigo wake usipite kwenye scanner, hali inayoweza kupitisha mizigo haramu kama dawa za kulevya.
Alisema wafanyakazi na wafanyabiashara hao wanatumia udanganyifu kuwa kontena hizo zimebeba mitumba, kumbe ndani ya mitumba hiyo wakati mwingine inatumika kufunika magari.
``Ninayo orodha ndefu na nitaikabidhi kwa Kamishna Mkuu wa TRA, Kitilya ili awafuatilie na ahakikishe anawatimua kazi mara moja wale watakaobainika wanahusika na mchezo huo ili tuanze upya,`` alisema.
Alisema serikali haiwezi kuvumilia kuwa na wafanyakazi wanaokula njama za kuipotezea mapato.
Kikwete alisema bandarini kuna uzembe mkubwa ambao hauvumiliki na aliuagiza uongozi kuondoa matatizo yaliyopo badala ya kukaa na kunung`unika.
Alisema msongamano wa makontena umekuwa ukiisababishia serikali kukosa mapato mengi na alisisitiza kuwa bandari ni sehemu muhimu ambayo serikali haiwezi kuiacha iwe ya hovyo.
Akiwa katika kitengo cha kuchunguza bidhaa katika kontena, Tiscan, Rais Kikwete alisema maelezo aliyopewa na TPA yanatofautiana na yale aliyopewa na viongozi wa Tiscan.
``Hapa mbona mimi sielewi naomba mnieleweshe, hawa Tiscan wanasema wana uwezo wa kuchunguza hata makontena 200 kwa siku ila wanasema tatizo ni nyinyi hamleti kontena za kutosha... Jamani fanyeni kazi na muachane na visingizio na malalamiko,`` alisema Kikwete.
Aliagiza mamlaka hiyo impe taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa upunguzaji wa makontena ndani ya wiki mbili zijazo na aliahidi kutembelea tena bandari hiyo.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wakala wa Forodha, Otieno Igogo, alimweleza Rais Kikwete kuwa wadau wa Bandari ya Dar es Salaam walikubaliana kulipa dola 30 ikiwa ni gharama za kuhamishia kontena moja katika bandari kavu.
Igogo alimweleza Rais kuwa ingawa wadau wote wamekuwa wakichangia, Kampuni ya Kimataifa ya Kupakua Kontena Bandarini (TICTS), imegoma kutoa fedha hizo.
Alisema dola 30 ambazo TICTS walipaswa kulipa kwa kila kontena linalohamishiwa bandari kavu kama wanavyolipa wadau wengine, zimekuwa zikitolewa na TPA.
Baada ya kauli hiyo ya Igogo, Rais alisema anashangaa kuona jeuri hiyo ya TICTS na kusema kuwa TPA ina mamlaka, lakini haitaki kuyatumia.
Kikwete alisema TPA imefanya vizuri kulipa gharama ambazo TICTS imekataa kuzilipa, lakini aliagiza mamlaka hiyo ihakikishe TICTS inazirudisha mara moja.
``Nyinyi mnashangaza sana, mna mamlaka, lakini hamyatumii... Sasa hizi gharama lazima walipe na wakiwashinda mwelezeni waziri na waziri akishindwa niambieni mimi,`` alisema.
Wakati huo huo, Kikwete alikataa maelezo marefu ambayo Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraem Mgawe, alitaka kuyasoma mbele yake na badala yake akamtaka amweleze sababu za msongamano kutoma lizika.
Baada ya kuelezwa hivyo, Mgawe alimweleza Rais Kikwete kuwa kikosi kazi kilichoundwa kufuatia agizo lake kinaendelea kujitahidi kuondoa msongamano uliopo.
Alisema Mamlaka inatarajia kuwa utekelezaji wa mikakati iliyowekwa itafanikisha kupunguza hali ya msongamano mwezi Machi mwaka huu.
Mgawe alisema katika kipindi cha mwaka 2007/08, TPA ilihudumia tani milioni 6.239, ambalo ni ongezeko la tani 227,222 au asilimia 3.8 ikilinganishwa na tani milioni 6.003 zilizohudumiwa mwaka 2006/07.
Alisema katika kipindi hicho mamlaka ilipata ziada ya Sh. bilioni 37.879 kutokana na mapato ya Sh. bilioni 168.789 na matumizi ya Sh. bilioni 133.909.
SOURCE: NIPASHE

Wito wangu kwa Salma Kikwete ni simple: kama alikuwa anataka kugombea uongozi angegombea lakini sio kuendelea kutumia raslimali za taifa kumkampenia mumewe.Anapaswa kutambua kuwa raslimali hizo zinagharamiwa na walipa kodi ambapo wengi wao si wana-CCM (takwimu za karibuni zinaonyesha wanachama wa CCM ni takriban milioni 5 tu kati ya Watanzania takriban milioni 45).

Tunatambua kuwa Salma anataka kuendelea kuwa First Lady lakini asifanye hivyo kwa kuwabebesha gharama Watanzania wote hata wasio wana-CCM.Anaweza kuitumia WAMA kumfanyia kampeni mumewe lakini Watanzania hawataki kuona ufisadi wa mchana mweupe unaofanywa kwa misingi ya kifamilia.

Naamini mwanamama huyu anafuatilia habari za kimataifa,na hivyo amesikia yaliyomkumba Vera Chiluba,mke wa aliyekuwa Rais wa zamani wa Zambia,Frederick Chiluba,aliyehukumiwa kwenda jela kwa ufisadi.

Ni vema Salma akasoma alama za nyakati ili pindi mumewe atakapokabidhi madaraka kwa Dokta Wilbroad Slaa hapo Novemba familia ya Kikwete isianze "kutafutana".

Na hiyo "tweet" yake ya kuchambua pumba na mchele nadhani ni vema akiielekeza kwa mumewe ambaye so far anaonekana kunogewa na "ugonjwa" wa kutoa ahadi.Mara uwanja wa ndege Kigoma,mara kuboresha kilimo cha kakao,mara atawapatia akinamama chanjo ya cervical cancer,mara vijiji 11 vya Mkinga vitapatiwa maji,mara hili mara lile alimradi ni "vurugu mechi ya ahadi".Kwani Rais wa Tanzania 2005-hadi sasa alikuwa nani kama sio Jakaya Mrisho Kikwete?Kwanini hayo anayoahidi sasa hakuyatekeleza katika awamu yake ya sasa?Na kwani tuamini kuwa atayatekeleza katika awamu yake ya mwisho-kipindi atakachokuwa bize kujitengenezea mazingira ya "kumpumzika kwa amani" kama Mkapa?

Blogu hii inawakumbusha tena wapiga kura kwamba Kikwete hayuko serious ndio maana ameamua kurejea nyingi ya ahadi zake za 2005 bila aibu wala kuwaomba msamaha Watanzania kwa kutozitekeleza.Kumrejesha tena Ikulu itakuwa ni kosa kubwa kupita kiasi kwani katika awamu yake ya mwisho atairejesha nchi yetu kwenye zama za mawe.

TANZANIA BILA UFISADI INAWEZEKANA
TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA
TANZANIA BILA KIKWETE,SIO TU INAWEZEKANA,BALI NI MUHIMU LAZIMA KWA USTAWI WA TAIFA LETU.
CHAGUA DOKTA SLAA KWA UKOMBOZI NA "UHURU WA PILI",CHAGUA CHADEMA KWA TANZANIA YENYE NEEMA.




13 Sept 2010



Hii ndiyo Bunda ya Dk. Slaa

Leo tuko Bunda. Acha picha hizi ziseme zenyewe. Maelezo mengine
baadaye. Itoshe tu kusema kwamba miongoni mwa maelfu ya wana Bunda waliofurika kumsikiliza Dk. Slaa katika viwanja vya Sabasaba ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Francis Isack. Alikaa jukwaa moja na Dk. Slaa, naye alimsifu kwa ukomavu wa kisiasa, lakini akamuonya kwamba kama alikuwa amekwenda pale kwa nia tofauti, atazame umma, apime nguvu yake na apeleke taarifa za kile anachosikia na kuona. Alimsimamisha DC huyo akawasalimia wananchi kwa kunyosha mikono juu.

Picha na Habari kwa Hisani ya NGURUMO

Je wajua kuwa licha ya mgombea wa CCM Jakaya Kikwete kukacha mdahalo na wagombea wa vyama vingine anapatikana kirahisi mtandaoni ambapo "anauza" sera zake na "mafanikio" yake?Kama ulikuwa hufahamu basi nenda Twitter kisha tafuta @Kikwete2010 au nenda Facebook kisha tafuta Jakaya Kikwete.

I know siasa za chama kimoja zimeacha kasumba ya kufurahia kugusana mabega na watawala.No wonder kuna wenzetu muda huu wanakenua meno yote thelathini na kitu kwa vile wamepokea ujumbe kama huu "Kikwete2010 is following you..." au "Salma Kikwete is Following you..." 

Si ajabu kuna wenzetu wamefotokopi meseji za aina hiyo wakiamini kuwa Kikwete na mkewe Salma wanawajali saaaana hadi wameamua kuwa-follow up huko Twitter au kuungana nao hapo Facebook.KALAGABAHO!Kwanini hujiulizi WHY NOW?Kikwete na mkewe walikuwa Ikulu tangu Desemba 2005 na HAWAKUKUTAFUTA.Hushangai kwanini leo wanataka urafiki nawe?Well,sio kosa kuwa rafiki na rais au mkewe lakini urafiki huu hauna tofauti na ule wa mtenda tendo la ndoa na kondomu.Zana hiyo (kondom) huwa na umuhimu wa kipekee (kwa wale wanaojali) kabla na wakati wa tendo la ndoa,lakini pindi shughuli ikimalizika kondom huwa ni uchafu usiovumilika.ANGALIA,usijetumika kama kondomu: Kikwete akuone muhimu sasa kwa vile anahitaji kura lakini akakusahau (kama alivyokusahau 2005-till now) baada ya kurejea Ikulu.

Badala ya ku-retweet kila anachoandika,tumia haki yako kama Mtanzania kuhoji masuala mbalimbali yanayolikabili taifa.Twende mbali zaidi ya kupongeza na kuona sifa "kugusana mabega" na watawala.Sio kosa kushabikia lakini ushabiki wenye maana ni ule unaombatana na matumizi sahihi ya akili.

Now you-in case you didn't.Muulize Kikwete,je ile kauli aliyotoa mwaka 2006 kuwa anawafahamu wala rushwa kwa majina ila anawapa muda wa kujirekebisha imefikia wapi?Je wameshajirekebisha?Je anaweza kututajia majina ya waliojirekebisha na waliogoma kufuata ombi hilo la kichovu?

Muulize pia kwamba kabla ya sakata la Richmond aliahidi kuwa tatizo la umeme lingebaki kuwa historia.A few months later,matapeli wa Richmond wakaingia kwenye picha.Today,tatizo la umeme ni as sugu as ufisadi.Mkalie kooni na kumhoji,kama huko nyuma alitoa ahadi ya kutupatia ufumbuzi wa umeme na hakutimiza,kwanini tumwamini sasa?

Muulizie pia kama bado anaamini kuwa mimba za wanafunzi wa kike zinasababishwa na kimbelembele chao.Yah,muulize swali hilo kwa vile hadi sasa bado hajakanusha au kuwaomba msamaha Watanzania kwa kauli hiyo ya kizembe.

Usikose kumuuliza pia kama hadi sasa hajui sababu zinazoifanya Tanzania kuwa masikini maana alinukuliwa akijiuliza swali hilo.Nenda mbali kidogo na kumhoji kama alikuwa hajua kwanini Tanzania ni masikini sasa anafanya nini hapo Ikulu?

Sasa hivi amenzisha hash tag #Mafanikio huko Twitter.Hapo utapata nafasi nzuri ya kujionea waziwazi namna Awamu ya Nne ya Kikwete ilivyoshindwa kuikomboa Tanzania kutoka kwenye umasikini licha ya raslimali lukuki tulizonazo.Hapo Kikwete na wapambe wake wanataja mapato yaliyotokana na utalii na madini.Mkalie kooni na kumhoji kama mapato ndio hayo,kwanini sie bado masikini?Fedha hizo zimeenda wapi kama sio kwenye akaunti za mafisadi?Na kwenye utalii muulize pia kuhusu meno ya tembo yaliyokamatwa huko Hong Kong yakitokea Tanzania.

Kumbuka,usikubali kutumika kwa maslahi ya mtu mwingine.Kumhoji mwanasiasa anayeomba kukuongoza ni haki yako.Usiichezee.Badala ya kujipendekeza kwa RT (Retweets za Kikwete2010) tumia fursa hiyo kumuuliza maswali ya msingi yanayohitaji majibu ya haraka.

PAMOJA TUNAWEZA

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.