(Katuni kwa hisani ya FEDE)
Si maneno yangu,bali nimenukuu kutoka gazeti la Mwananchi
Jamani wapiga kura,huyu mtu kachoka na anastahili apumzishwe.Yawezekana kabisa kuwa udhaifu katika uongozi wake unachangiwa na uchovu huo ambao chanzo chake kimeendelea kuwa muujiza kama ulivyo muujiza wa nani anamiliki kampuni ya kifisadi ya Kagoda.
Na ukichanganya na utitiri huu wa ahadi za kuchakachua.....
(Katuni kwa hisani ya FEDE)
Si maneno yangu,bali nimenukuu kutoka gazeti la Mwananchi
...Kikwete aliyeonyesha uchovu katika mkutano huo alishuka ghafla jukwaani na kuondoka baada ya kuwatambulisha wagombea ubunge, akiwaacha wananchi wakimsubiri...Hata hivyo, kuteremka ghafla jukwaani kwa Kikwete kulimaliza mkutano huo bila kufungwa rasmi huku wananchi wakibaki na maswali juu ya mustakabali wa mkutano huo uliofunguliwa na mwenyekiti wa CCM wilaya.Marwa Mwita, mkazi wa Mugumu, alisema bado anajiuliza ilikuwaje mgombea huyo akaondoka bila ya kuaga.
"Hilo ni jambo la kujiuliza, lakini huenda amechoka na anasahau alitakiwa kufanya nini. Kwanza amechelewa kufika, hakuomba radhi, kahutubia mambo yale yale ya kila mwaka".
Jamani wapiga kura,huyu mtu kachoka na anastahili apumzishwe.Yawezekana kabisa kuwa udhaifu katika uongozi wake unachangiwa na uchovu huo ambao chanzo chake kimeendelea kuwa muujiza kama ulivyo muujiza wa nani anamiliki kampuni ya kifisadi ya Kagoda.
Na ukichanganya na utitiri huu wa ahadi za kuchakachua.....
(Katuni kwa hisani ya FEDE)






















