16 Feb 2011



Pichani ni Mbunge John Komba wa CCM 'akiwa makini' kwa kuuchapa usingizi Bungeni Dodoma.Hata huyu naye anastahili 'zawadi' ya milioni 90?

Hivi kweli inaingia akilini kusikia kwamba Serikali ya Kikwete ina mpango wa kuwapatia wabunge shilingi milioni 90 kila mmoja "kwa sababu inazojua yenyewe?Majuzi tu tumesikia habari kwamba Serikali hiyo hiyo inatembeza bakuli kwa wahisani ili wasaidie 'kuokoa jahazi' la hali mbaya ya Bajeti ya 2010/11.

Lakini pia tunakumbuka Kikwete alivyokuwa mkali kwa watumishi wa umma walipotishia kugoma kushinikiza kulipwa mishahara inayoendana na hali halisi ya maisha.Sasa kama ilishindikana kuwalipa wafanyakazi wa umma mishahara bora haya mabilioni ya kuwazawadia wabunge yanatoka wapi?

Naona kuna kila jitiahada za watawala wetu kukaribisha yanayojiri huko Arabia na Mashariki ya Kati.Japo inauma kuona mabilioni ya shilingi yakizawadiwa kwa waheshimiwa kama huyo anayechapa usingizi,lakini hatua hiyo inaweza kuwa blessing in disguise kwa maana kwamba huenda ikawahamasisha Watanzania kuiga mifano ya 'walalawima' wenzao wa Tunisia na Misri,na hatimaye kufanikiwa kuleta 'Uhuru wa Pili' (wa kwanza ulikuwa wa kumwondoa mkoloni.Wa pili ni wa kuwaondoa mafisadi)



My sista Jestina,a top-notch fashion blogger,with her exquisitely beautiful daughter Princess Iman .

.



15 Feb 2011


Hatimaye mmoja wa wanasoka mahiri kabisa duniani,Ronaldo wa Brazili,ameamua kuundika madaluga.Staa huyo mwenye kipaji cha hali ya juu ametangaza kustaafu rasmi soka.

Katika makala hii nawaletea video za kumbukumbu ya nguli huyo wa kandanda.Picha zote hizo ni kwa hisani ya gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza






















14 Feb 2011


Leo ni Siku ya Mtakatifu Valentine,maarufu kama Siku ya Wapendanao,au Valentine's Day kwa kimombo. Pengine ni vema kuadhimisha siku hii kwa kutafakari umuhimu wa upendo.

Binafsi,si muumini mzuri wa siku zinazoambatana na matukio.Kwa mfano,mara nyingi huwa naadhimisha siku yangu ya kuzaliwa kwa sala na tafakuri ya miaka iliyopita na ijayo,Mungu akinijalia.Kwa wengine,siku ya kuzaliwa ni wakati wa kuingia gharama zisizo na umuhimu kwa sherehe kubwa zinazowaacha wakiwa na hali ngumu baadaye.Japo ni muhimu kufanya maadhimisho ya siku muhimu kama ya kuzaliwa lakini kuna umuhimu gani kama siku hiyo inabaki kuwa "siku muhimu" tu pasipo kuangalia wapi umetoka,ulipo na unakoelekea?

Na katika mantiki hiyohiyo,Siku ya Wapendanao inakuwa tu na umuhimu kama upendo utatafsiriwa kwa dhamira na vitendo.Kuna umuhimu gani wa kuadhimisha Siku ya Wapendanao kwa kadi za gharama na vinywaji ilhali umewasahau wanaohitaji upendo wako?

Wengi tunaelewa namna baadhi ya wenzetu wanavyoiogopa siku hii kutokana na kuwa na ma-Valentine wengi.Na miongoni mwa hawa ni wale wanaoadhimisha siku hii na "nyumba ndogo" huku wakiacha visingizio kwa wapenzi wao halisi.Hali hiyo inapoteza maana nzima ya siku hii.Haiwezekani mtu kudai anaadhimisha Siku ya Wapendanao kwa kumsaliti mpenzi wake.

Vinginevyo,nawatakia Siku njema ya Wapendanao nikiamini kuwa maadhimisho ya siku hii yatakuwa ya dhamira zaidi kuliko vitendo pekee.

13 Feb 2011



Kumekuwa na tetesi za muda mrefu kuwa hali ya uchumi wa Tanzania ni mbaya.Hata hivyo,kama ilivyozoeleka,wahusika serikalini wameendelea kuwanyima Watanzania haki yao ya msingi ya kufahamishwa hali ya uchumi wa taifa lao. 

Hivi karibuni Gavana wa Benki Kuu,Profesa Benno Ndulu,alizungumza na waandishi wa habari kuhusu ubora wa noti mpya.Licha ya kuonekana kufahamu kuwa wananchi hawaridhishwi na kiwango duni cha noti hizo,Gavana Ndulu alizitetea kwa nguvu zote.Akemee ili ifahamike kuwa 'zimechakachuliwa'?

Akiichambua hali ya uchumi, gavana huyo alisema kwa sasa hali ya uchumi ni nzuri na kwamba nchi ina uwezo wa kulipa huduma kwa miezi sita bila kutegemea sehemu yoyote.Lakini katika kile kinachoweza kiashirikia kiwa kauli hiyo ilikuwa ya kisiasa zaidi kuliko ya kitaalamu,Gavana alidai kuwa mwenye dhamana ya kueleza athari za mgao wa umeme kwa uchumi ni Waziri wa Nishati na Madini.Huku sio tu kukwepa majukumu bali mwendelezo wa danadana za kibabaishaji zinazoeleka kuunda mfumo wa utendaji wa viongozi wengi wa taasisi za umma.Na kwa vile 'Mteuzi Mkuu' Serikalini,yaani Rais,anaonekana kama yupo usingizini kubaini mapungufu ya baadhi ya watendaji aliowateua,ni dhahiri utendaji kwa mfumo wa 'bora liende' utaendelea kuwepo kwa muda mrefu.

Kwa hapa Uingereza,Benki Kuu imekuwa ikitoa taarifa kuhusu viwango vya riba kila mwezi.Taarifa hiyo huambatana na maelezo ya kutosha kuhusu mwenendo wa uchumi wa nchi hii.Na kila baada ya miezi michache,ofisi ya takwimu nayo hutoa taarifa yenye takwimu zinzoashiria kupanda,kutuama au kushuka kwa uchumi.Kadhalika,vielekezo muhimu kuhusu uchumi wa nchi kama vile idadi ya wasio na ajira,mfumuko wa bei,wastani wa thamani ya sarafu,nk vimekuwa vikiwekwa wazi kwa umma.

Na huko nchini Marekani,Serikali ya Rais Barack Obama,imekuwa ikitoa taarifa za hali ya uchumi wa nchi hiyo mara kwa mara,hata kama kufanya hivyo kufanya hivyo kunaathiri namna wananchi wanavyoridhishwa au kutoridhishwa na serikali hiyo.Huku sio tu kutambua haki ya wananchi kuhabarishwa bali pia kuelewa kuwa kuficha ukweli kuhusu hali ya uchumi hakuwezi kuufanya uchumi husika kuboreka.

Na ndio maana licha ya kuwaficha Watanzania kuhusu hali ya uchumi wa nchi yao,sambamba na kauli mbalimbali za kisiasa kuwa 'hali cha uchumi ni poa' gazeti la Mwananchi katika toleo lake la leo linaripoti kuwa Serikali imelazimika kufumua bajeti yake ya mwaka wa fedha 2010/11 kwa kupunguza matumizi ya Wizara ili kufidia upungufu wa Sh670.4 bilioni zilizotegemewa kupatikana kutokana na makusanyo ya kodi katika mwaka huu wa fedha.

Hata hivyo,gazeti hilo lilipomtaka Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustaffa Mkullo, kuihusina na hali hiyo alisema taarifa ya hali ya uchumi wa nchi alishaitoa hivi karibuni kwenye chombo kimoja nchini, hivyo hahitaji kuitoa tena."Nilitoa taarifa kwa wenzenu wa gazeti (sio Mwananchi) sasa siwezi tena kuirudia," alisema.Ni dhahiri kuwa laiti hali ingekuwa nzuri,Mkulo asingefanya dharau hiyo hasa kwa vile viongozi dhaifu huwa wepesi sana kumwaga hadharani habari njema wakiamini zitawaletea sifa.

Wakati Watanzania wanasubiri 'waletewe' Katiba mpya,ni muhimu kuangalia tatizo hili la ukandamizwaji wa makusudi wa haki ya kuhabarishwa.Nchi mbalimbali zina sheria zinazoilazimisha Serikali na taasisi za umma kutoa au kuruhusu upatikanaji wa taarifa.Japo tunafahamu kuwa taarifa nyingi nchini 'zinachakachuliwa' kwa minajli ya kufisadi,kudanganya wapiga kura,kughilibu wafadhili,au sehemu tu ya utamaduni wa kutowajibika,uwepo wa sheria ya Haki ya Habari (Freedom of Information act) utakomesha tabia kama hiyo ya dharau Waziri Mkulo kupuuza kuwaeleza Watanzania kuhusu hali ya uchumi wa nchi yao

12 Feb 2011

Zoezi la ujenzi wa jarida kamili mtandaoni linaendelea vema.Lakini kama ilivyo pindi mtu anapohama kutoka sehemu moja kwenda nyingine,kuna vitu vinavyochukua muda kuwa timilifu.

Naomba nichukue fursa hii kuwashukuru wanahabari-mtandaoni wenzangu waliokubali ombi langu kwao kunitundikia katika blogu zao tangazo la mabadiliko ya anwani ya mtandao huu.Nawashukuru sana.Na pia nawakaribisha sana kushirikiana nami katika tovuti hii shirikishi.

Kwa wale niliowatumia ombi kama hilo lakini wakapuuza,sina maneno nao as such.Kuna baadhi yao ambao nina uhakika wa asilimia kubwa kuwa hawakuona barua pepe niliyowatumia.Nina uhakika huo kwa vile nawafahamu kuwa si watu wenye tabia ya dharau,jeuri au husda.Labda wako bize sana kiasi hawakuwa na muda hata wa kusoma barua-pepe iliyokuwa na ombi hilo.

Lakini kuna wengine ambao nadhani walikuwa na sababu zao "binafsi".Labda hawakupendezwa na uhamaji huu wa kutoka blogu kuelekea jarida kamili mtandaoni (wanasema ukitaka ufarakane na Waswahili basi piga hatua japo nusu).Au labda wao ni viumbe muhimu kabisa ambao hawakupaswa kubughudhiwa na ombi kama hilo.Na kwa baadhi ya waswahili,wanaamini dharau na maringo ni viungo (recipes) vya "umuhimu" wao katika jamii.

Enewei,natambua wametumia haki yao ya kikatiba na kidemokrasia lakini hio haiondoi ukweli kuwa walichofanya si uungwana.Na kwa vile binafsi naamini kwenye kuelezana ukweli,nimeona ni vema kuwashutumu japo naelewa fika haitobadili chochote.

Mwisho,nakaribisha maoni kuhusu tovuti hii hususan yaliyomo na mwonekano.Pia naomba wanahabari-mtandaoni ambao awali nilijumuisha anwani za blogu zao kwenye blogroll yangu lakini kwa sasa hazipo,wasifikiri nimewatelekeza.Naendelea na zoezi la kukusanya viungo vyote vya awali ambavyo kwa bahati mbaya vilifutika wakati wa uhamaji huu unaoendelea.

Tupo pamoja


Serikali ya Uswisi imetangaza kutaifisha mali zote za Dikteta Hosni Mubarak,ambaye jioni hii ameng'olewa madarakani na nguvu ya umma.Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa,haijafahamika iwapo serikali za Uingereza,Marekani na nchi nyingine za Magharibi ambako Mubarak ana mali zake (na kujichumia utajiri unaokadiriwa kufikiwa dola za Kimarekani Bilioni 70) nazo zitachukua hatua kama hiyo ya Uswisi au la.Je mafisadi wetu huko nyumbani wanajifunza lolote katika sakata hili?
I just hope they do!

11 Feb 2011

Habari zaidi baadaye

10 Feb 2011







BLOGU HII YA Kulikoni Ughaibuni INAPENDA KUWAFAHAMISHA KUWA INAHAMIA KATIKA ANWANI MPYA MTANDAONI.AWALI BLOGU HIYO IMEKUWA IKIPATIKANA KATIKA ANWANI http://chahali.blogspot.com/
 LAKINI SASA INAHAMIA KATIKA ANWANI MPYA YA http://www.blogger.com/goog_939388498
.
http://www.chahali.com

PAMOJA NA MABADILIKO HAYO,AMBAYO NI SEHEMU TU YA MABADILIKO MAKUBWA ZAIDI YA UBORESHAJI NA HATUA YA KUELEKEA KUWA TAASISI KAMILI YA HABARI NA UTAFITI,ANWANI YA AWALI ITAENDELEA KUWA HEWANI KWA MUDA WOTE WA ZOEZI HILI LA UHAMAJI (MIGRATION).SAMAHANI SANA KWA USUMBUFU WOWOTE UTAKAOJITOKEZA

ASANTENI NA KARIBUNI SANA http://www.chahali.com/








Mlolongo wa ushahidi kuwa Kikwete ni sehemu muhimu ya ustawi na mafanikio ya ujambazi wa Dowans,na uthibitisho kuwa nchi imemshinda.

www-freemedia-co-tz

www-mwananchi-co-tz

www-freemedia-co-tz (1)

www-mwananchi-co-tz (1)

www-freemedia-co-tz (2)

Www Uhurupublications Com

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.