15 Mar 2011


Kuna kila dalili kuwa chama tawala CCM sasa kinajiendesha kwa mtindo wa bora liende.Asubuhi utasikia huyu karopoka hili,mchana utamsikia mwingine karopoka lile,alimradi ni vurugu mechi kila siku.

UVCCM hawana mamlaka kutung'oa-Chiligati
*Makamba asema hayo ni maoni ya vijana
*Lowassa ahoji nani asiyeona uchumi ulivyo?

Na John Daniel
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Maponduzi (NEC) Itikadi na Uenezi, Bw. John Chiligati amesema licha ya Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) kuwa na haki ya kutoa maoni, lakini hawana mamlaka ya kuiondoa sekretarieti madarakani.

Wakati Bw. Chiligati akitoa kauli hiyo, wajumbe wenzake wa sekretarieti waliotakiwa kuachia ngazi kwa kushindwa kutimiza wajibu wao wa 'kumsaidia' mwenyekiti wametofautina kuhusu kauli hiyo huku wakishindwa kuzungumzia kwa uwazi wito huo wa vijana.

Jana gazeti hili liliwakaririwa vuoa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) ukiitaka sekretarieti ya chama hicho kujizulu kabla umoja huo haujachukua hatua za kuwaondoa kwa kuwa imeshindwa kumsaidia Rais Jakaya Kikwete.

Kauli hiyo ilitolewa na Makamu Mwenyekiti wa umoja huo wa mkoani Pwani, Bw. Abdallah Ulega wakati akifungua Baraza la Umoja wa Vijana Mkoa humo, huku akisisitiza kuwa sekretaeti hiyo haifai kwa kuwa ilisababisha chama hicho kushinda kwa taabu katika uchaguzi mkuu uliopita, na kuwa ndiyo imekuwa ikitoa siri kwa chama cha upinzani cha CHADEMA.

Secreterieti inayoongozwa na Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuf Makamba, inajumuisha Manaibu Katibu Wakuu Bara, Kapteni George Mkuchika na Salehe Ramadhani Ferouz (Zanzibar), Katibu wa Itikadi na Uenenezi, Kapteni John Chiligati, Katibu wa Idara ya Uchumi na Fedha, Bw. Amos Makala na Katibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard Membe.

Akizungumza na Majira jana Bw. Chiligati alisema kimsingi vijana hao wametumia uhuru wao ndani ya chama kutoa maoni yao na kwamba haoni sababu ya hatua hiyo kusumbua vichwa vya watu kwa kuwa ni jambo la kawaida kikatiba.

"Ni haki yao kutoa maoni, sioni cha ajabu hapo, vijana wana haki ya kuzungumza na kutoa maoni yao kwa uhuru kabisa.

"Lakini Secretarieti inachaguliwa na NEC na tunawajibika kwa NEC kupitia Kamati Kuu, hao waliotuchagua ndio wana mamlaka ya kutuondoa, lakini hilo haliwakatazi vijana kutoa maoni," alisema Bw. Chiligati.

Alipoulizwa changamoto waliyopata na iwapo wanajiandaa kuwasilisha mapendekezo yao kwenye vikao vya juu kutokana na wito wa UVCCM hakuwa tayari kutoa majibu ya moja kwa moja badala yake alisisitiza kuwa hayo ni maoni ya vijana.

"Nimesema hayo ni maoni ya vijana na wana haki ya kuyatoa," alisistiza Bw. Chiligati bila kufafanua.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuf Makamba alisema licha ya kuheshimu uhuru wa kutoa maoni lakini haamini kama yaliyoandikwa katika vyombo vya habari ndiyo yaliyozungumzwa na UVCCM mkoa wa Pwani.

"Hayo ndio maoni ya vijana, wamekaa kwenye baraza lao na wakaona hivyo. Hayo ndio maoni yao mimi sina cha kusema," alisema Bw. Makamba.

Alipotakiwa kujibu iwapo katiba, kanuni na taratibu za CCM zinatoa nafasi kwa umoja huo kuondoa secretarieti iwapo imeshindwa kutimiza wajibu wake alisema;

"Ni maoni yao, lakini pia sina hakika kama yaliyoandikwa yako sawa sawa," alisema Bw. Makamba bila kutoa ufafanuzi wa kina.

Alipoulizwa hatua atakazochukua kama Mtendaji Mkuu wa CCM kuhusu wito huo wa UVCCM alisema yeye hawezi kujitetea kupitia magazeti na kusisitiza kuwa hayo ni maoni ya vijana.

"Siwezi kufanya kazi ya kujitetea kwenye magazeti, wao ni vijana wa CCM, wamekaa kwenye baraza lao wakasema, sasa unataka nisema nini? alihoji Bw. Makamba na kuongeza, "Nasema hivyo ndivyo walivyoona. wajumbe wengine wa sekretarieti hiyo hawakupatikana kutoa maoni yao kwa simu zao zilikuwa zinaita bila majibu.

Mbali na sekretarieti, vijana hao waliwashambulia mawaziri wakuu wastaafu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye wakisema kauli zao za kukikosoa chama hazina lengo zuri bali ni njia tu ya kutafuta urais 2015

Akizungumzia suala hilo, Bw. Lowassa ambaye pia alionywa na vijana hao kutoa maoni nje ya vikao wakati anayo nafasi ya kukutana na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM Rais Jakaya Kikwete, alisema maoni yake kuhusu uchumi hayana sababu ya kusubiri vikao.

"Nilikuwa vijijini kwenye ziara sijasoma magazeti, lakini wewe nikikuuliza hali ya uchumi utasema kuwa ni nzuri?Nani asiyejua kuwa kuna hali ngumu ya uchumi! Hata bei ya nyanya imependa hilo nalo tusubiri vikao? alihoji Bw. Lowassa.

Alisema kama mtu anataka kuwania urais mwaka 2015 hawezi kuanza kampeni kwa sasa kwa kuwa kufanya hivyo ni kutoa nafasi ya kushughulikiwa na kuchafuliwa na maadui. Bw. Sumaye hakupatikana jana kwenye simu yake.

Majira ilipomtafuta Makamu Mwenyekiti Taifa wa CCM, Bw. Pius Msekwa ili kuzungumzia wito huo wa UVCCM, alisema hawezi kusema lolote kwa kuwa hayo ni maoni ya vijana na kila mmoja anayo haki ya kutoa maoni yake.

"Hayo ni maoni ya vijana, sasa unataka nitoe maoni gani?" alihoji Bw. Msekwa. 

CHANZO: Majira

14 Mar 2011


TIBA inayotolewa na Mchungaji Mstaafu wa KKKT (Babu), Ambilikile Mwasapile katika kijiji cha Samunge, Loliondo, imeendelea kuonyesha maajabu yake baada ya wagonjwa kadhaa wa hospitali mbili kubwa nchini kukutana na madaktari wao kwenye foleni, kila mmmoja akitafuta uponyaji.
.

Wakati hayo yakiendelea, Mbunge wa Kilindi mkoani Tanga, Bi. Beatrice Shellukindo ametoa ushuhuda tiba hiyo ya Babu si jambo la mzaha bali inaponya, yeye amenufaika nayo, pamoja na ndugu zake 18 alioongozana nao.

Wakizungumza na majira kwa nyakati tofauti siku chache baada ya kurudi walikokwenda kufuatilia tiba hiyo, baadhi ya wanachi walithibitisha wagonjwa hao kupigana vikumbo na madaktari wao kwenye foleni kila mtu akijaribu kutatua tatizo lake.

“Sisi tulikwenda baada ya kushauriwa na daktari wa Hospitali ya Rufaa ya KCMC ambaye anamtibu ndugu yangu. alitwambiwa moja kwa moja ya kwamba tumpeleke mgonjwa wetu kwa Babu,” alisema Timothy Ndalichako, mkazi wa Njoro, mjini Moshi.

Alisema siku chache baada ya kupewa ushauri huo ambao ulitiwa chumvi na kuenea kwa taarifa za huduma ya Babu, walitafuta taratibu za kumpeleka ndugu mgonjwa huyo Loliondo na kufanikiwa kuipata baada ya siku mbili kwa kuwa wakati huo msongamano ulikuwa haujawa mkubwa.

“Tukiwa kwenye foleni siku ya pili, ndipo tukamuona daktari aliyetushauri akiwa ameandamana na wenzake kwenye gari, nao wakiwa wanaingia eneo la tiba Loliondo,” alisema.

Aidha alisema alichogunduwa ni kwamba madaktari wengine kutoka hospitali hiyo maarufu hapa nchini na nje ya nchi pamoja na wale wa hospitali nyingine za mjini Moshi, walishafika na wengine walikuwa wakiendelea kufika eneo hilo kufuatia tiba hiyo mbadala.

Kwa upande wake, Bw. Manase Kiara, alidai kukutana na daktari bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, aliyekwenda Loliondo kufuatia tiba hiyo.

“Niliondoka na wenzangu baada ya kujipanga kwenda kupata tiba baada ya kuhangaikia kwa muda mrefu Muhimbili. Kufika huko mimi na wenzangu tulikutana na dokta wetu ambaye baada ya kusalimiana naye tu alituambia mpeni Mungu yaliyo yake Mungu na ya Kaisari mpeni Kaisari,” alisema.

Wakati huo huo baadhi ya wananchi wa mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro wameipongeza serikali kwa tamko lake kuwa haijazuia huduma ya tiba inayotolewa Mchungaji Mwasapile kwa miezi kadhaa sasa.

Shellukindo atoa ushuhuda wa tiba

Mbunge wa Jimbo la Kilindi mkoani Tanga, Bi. Beatrice Shelukindo amesema akiwa na ndugu zake 18 wakiwa na matatizo mbalimbali ya kiafya ikiwemo yeye mwenyewe kusumbuliwa na magonjwa mbalimbali kwa muda mrefu, wamefika kwa Babu na kupata tiba.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu akiwa Arusha jana baada ya safari iliyomchukua wiki nzima, Bi. Beatrice alisema sio jambo la mzaha, dawa ya Babu inaponya.

Bi. Shelukindo alisema walifika katika Kijiji cha Samunge wilayani Ngorongoro Machi 7, mwaka huu, lakini kutokana na wingi wa wagonjwa walipata tiba Machi 11 yeye na ndugu zake, na baada ya hapo kila mtu akajisikia amepona, wakiwemo waliokuwa wanasumbuliwa na saratani.

"Mimi mwenyewe nilikuwa nasumbuliwa na presha na vidonda vya tumbo kwa muda mrefu, lakini baada ya kunywa kikombe kile cha dawa nilipona, tangu Ijumaa sijagusa kabisa kidonge cha aina yeyote, iwe kwa ajili ya vidonda vya tumbo au presha.

"Lakini maajabu yapo kwa mtoto wangu wa kike, akiwa na miaka 37 tulimpeleka hajiwezi na hajaweza kula wala kusema kwa miezi sita, zaidi ya kunywa uji tu kwa vile alikuwa anasumbuliwa na kansa, lakini baada ya kutoka hapo, kwanza tulishangaa baada ya kutaka tumpe chakula.

"Na kutokana na shida ya safari, wakati wa kurudi tulimuandalia ndege ya kurudi Dar es Salaam alikataa na jana Jumamosi (Machi) amerudi kwa basi. Mwingine ni mama mdogo alikuwa anasumbuliwa na presha mbaya, lakini ghafla amepona," alisema Bi. Shelukindo.

Bi. Shelukindo alisema pia alikwenda na ndugu yake mwanaume, yeye alikuwa anaumwa macho kiasi ambacho moja lilipasuka, lakini alipofika kwa Babu na kunywa dawa amepona, na ndugu zake wote aliokwenda nao wanaendelea vizuri.

"Yusuph (mwandishi) nakusihi sana uende kwa yule mchungaji. Sio vitu vya kubuni, dawa yake inaponya. Hakika ndugu zangu wote wamepona. Ni kweli imani pia ni muhimu katika kutumia dawa hiyo, lakini yenyewe bado inaponya, na inaanza kufanya kazi siku moja mpaka saba tangu unywe dawa hiyo," alimaliza kwa kutoa ushuhuda huo Bi. Shelukindo.


Mazingira yaanza kuwekwa sawa

Hofu ya usalama ilikuwa imetanda kwenye Kijiji cha Samunge imeanza kuondoka baada ya serikali wilayani Ngorongoro
imesema kuanza uboresha wa miundombinu, usafi wa mazingira na kuweka utaratibu mzuri wa wagonjwa kupata tiba.

Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Elias Wawa Lali alisema jana kuwa
siku chache tu zijazo wananchi watapata tiba hiyo kwa muda mfupi na katika mazingira safi na salama kwa kuwa tayari wameanza jitihada za kukamilisha mpango huo kwa kushirikiana na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati.

Kwa mujibu wa DC huyo kanisa hilo limesema kuwa watahakikisha wananchi hawapati tena taabu walizokuwa wakizipata siku kadhaa zilizopita za kukaa siku zaidi ya tano bila tiba huku wakitishiwa na hatari ya kimazingira kwa afya zao.

“Kila mmoja anazungumza habari ya Loliondo hata yule ambaye hana taarifa sahihi za huko, lakini uhakika ni kwamba tayari mipango yetu inakwenda vizuri tunachozubiri na
wataalamu hao wa ujenzi kutuletea tathimini nzima ya kinachohitajika huko,” alisisitiza DC.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Askofu Thomas Laiser alisema kanisa hilo katika kuhakikisha azma yao inatimia linatarajia kutumia zaidi ya sh milioni 75
katika kuboresha mazingira ya tiba hiyo.

Fedha hizo ni kwa ajili ya kujenga majengo maalumu yenye uwezo wa kuhudumia watu zaidi ya 600 kwa wakati moja, huku kukiwa na huduma bora za matundu ya vyoo na maji safi na salama ya kutosha.

Aliongeza wachoraji na wasanifu wa majengo wakiongozwa na Katibu Mkuu wa KKKT Dayosisi hiyo, Bw. Ezrael Kariyongi hivi sasa wapo kijijini Samunge wakifanya tathimini ya mradi huo.

Alisema kuwa hata hivyo bajeti hiyo itategemea taarifa ya mchanganuo wa ujenzi huo ambapo utekelezaji wake utafanyika ndani ya wiki mbili zijazo ambapo mchungaji huyo ataendelea na tiba hiyo.

Imeandaliwa na Yusuph Mussa, Korogwe; na Heckton Chuwa,
Moshi; na Said Njuki, Arusha

CHANZO: Majira


MWENYEKITI wa TLP, Augustine Mrema, ametinga Loliondo kwa Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Ambilikile Mwasapile kunywa dawa na kutamba ni kwa ajili ya kuongeza nguvu ya mwili kupambana na ufisadi

Mrema, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), alisema jukumu alilokabidhiwa kuzunguka nchi nzima ni kubwa linalohitaji kuimarisha afya yake.

“Kazi niliyokabidhiwa ni kubwa, kuzunguka nchi nzima kupambana na ufisadi kunahitaji kuimarisha afya yangu,” alisema Mrema na kuongeza:

“Bila kuimarisha afya huwezi kufanya kazi hii niliyokabidhiwa, waeleze Watanzania kuwa nimeimarisha afya sasa nikupambana na mafisadi kwenye halmashauri nchini kwa kwenda mbele.”

Alisema Watanzania wanatakiwa kumshukuru Mungu kwa ‘kuwashushia’ Mchungaji mstaafu Ambilikile Mwasapile (76), kwa sababu hawatumii gharama kubwa zaidi ya 500.

“Kama angekuwa Marekani tungeenda kwa Sh500? dawa yake haina kuchakachua unakunywa. Dawa nimekunywa na nimerudi na picha nimepiga naye ” alisema Mrema kwa kujiamini.

Hata hivyo, Mrema hakubainisha magonjwa yanayomsumbua hadi kwenda kwa Mchungaji Mwasapile, ingawa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu. Siku za hivi karibuni vigogo wengi wa Serikali na CCM wamekuwa wakienda Loliondo kwa ajili ya tiba.

CHANZO:Mwananchi

13 Mar 2011


With nearly half a billion dollars in the bank Sean Combs, aka 'Diddy' has beaten rap colleague Jay-Z to the top of Forbes magazine's list of Hip-Hop's Wealthiest Artists..

The Bad Boy Records founder has an estimated wealth of $475 million, which he has acquired from his clothing line Sean John, his record label, and several product endorsements.

Jay-Z, meanwhile, closely follows with $450 million.

The Forbes list was put together by taking into consideration the artists' current holdings and past earnings.

Only performers were included on the list, which is why hip-hop tycoon Russell Simmons didn't place.

Following Diddy and Jay-Z is Dr. Dre with $125 million, 50 Cent and Birdman are tied at fourth place with $100 million.

In Pictures: Hip-Hop’s Wealthiest Artists

1. P.DIDDY


Sean "Diddy" Combs Worth: $475 million Fast Facts: Artist formerly known as Puff Daddy built fortune chiefly through clothing line Sean John, record label Bad Boy and Ciroc vodka. Acting gigs, television shows and guest appearances add to coffers. Told Forbes in 1999: "I'm gonna be bigger than David Geffen." Not there yet


2. JAY-Z



Shawn "Jay-Z" Carter Worth: $450 million Fast Facts: Beyonce's husband sold Rocawear clothing label for $204 million in 2007; signed 10-year $150 million Live Nation deal in 2008. Holds stakes in New Jersey Nets, 40/40 Club chain, ad firm Translation, other businesses. Lyrical boasts appear accurate: "I'm like really half a billie . . . you got baby money."


3. DR DRE




Andre "Dr. Dre" Young Worth: $125 million Fast Facts: Superproducer/rapper helped launch careers of Snoop Dogg, Eminem, 50 Cent. Expanded wealth with Aftermath record label, Beats headphones and HP laptop line. Likens himself to world's first billionaire: "Young black Rockefeller ... gettin' money like a bank teller."


4. BIRDMAN




Bryan "Birdman" Williams Worth: $100 million Fast Facts: Cofounded Cash Money Records with brother Ronald and inked $30 million distribution deal with Universal in 1998; affiliated Young Money lineup now includes rappers Lil Wayne and Nicki Minaj. Lyrical boasts ("Richer than the richest!") are simply not true.


5. 50 CENT



Curtis "50 Cent" Jackson Worth: $100 million Fast Facts: Received nine figures for Vitaminwater stake in 2007; spent freely on cars, renovations to mansion formerly owned by Mike Tyson. Cushion remains from catalog, acting gigs and 50 Cent-themed videogames, books, clothes and headphones. Future billionaire? Told Forbes in 2008: "It's probably going to take me 10 years."

SOURCE: Forbes.com

11 Mar 2011


Hivi kwanini watawala wetu wanaogopa sana maandamano?Wakati mchecheto ulioikumba Serikali ya Rais Jakaya Kikwete na CCM yake (kutokana na maandamano ya amani ya Chadema) haujaisha,gazeti la Mwananchi linaripoti kuwa askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) wamezuia maandamano ya wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari jijini Dar es Salaam

Soma habari kamili hapa chini:

KIKOSI cha Kutuliza Ghasia cha Jeshi la Polisi (FFU) jana kilitawanya maandamano ya wanafunzi wa baadhi ya shule za msingi na sekondari za Mkoa wa Dar es Salaam waliokuwa wakielekea Ikulu kupinga ongezeko jipya la nauli za daladala.

Kundi la kwanza la wanafunzi hao lilijikusanya katika Viwanja vya Mnazi Mmoja majira ya mchana na kuanza maandamano hayo yaliyokuwa na lengo la kumfikishia ujumbe Rais Jakaya Kikwete wa kutoridhishwa na ongezeko hilo la nauli. Kundi jingine la wanafunzi lilianzia maandamano hayo katika Uwanja wa Karume.

Mwandishi wa habari hii alipofika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja aliwakuta wanafunzi hao wakijipanga kuanza maandamano hayo huku wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali. Baadhi ya mabango hayo yalisomeka: ‘Kama ni maji ya pilipili, hayawezi kuwa suluhisho la migomo.’

Baadhi ya wanafunzi walisema wameamua kupinga nauli hiyo mpya kwa maandamano ili kuishinikiza serikali iifute wakitaka kurejeshwa kwa ile ya zamani ya Sh100 ili kuwapunguzia mzigo wazazi wao kuwasomesha.
“Sisi wengine kwa siku tunapanda magari matatu hadi kufika shule na hapo bado hujala. Sasa kwa hali hii kweli tutasoma?" Alihoji mmoja wa wanafunzi hao.

Mwanafunzi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Habib Juma alisema nauli ya Sh150 kwa mwanafunzi ni kubwa mno kuimudu akisema kipato cha wazazi wengi ni duni na baadhi yao wanashindwa hata kutoa michango mbalimbali ya shule.

Hata hivyo, jitihada za wanafunzi hao kufikisha ujumbe wao Ikulu ziligonga mwamba baada ya kudhibitiwa na FFU muda mfupi tu baada ya kuingia barabarani.Askari hao waliokuwa na pikipiki walitanda barabarani na kuwatawanya wanafunzi hao na baadaye waliwashikilia wanafunzi wawili wa kiume baada ya wenzao kukimbia. Wanafunzi hao walipakiwa kwenye gari la polisi na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Msimbazi.

Nauli hizo mpya za daladala zilizotangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), wiki iliyopita zilianza kutumika rasmi jana.Ofisa Mfawidhi wa Sumatra katika Kanda ya Dar es Salaam, Conrad Shio alisema nauli hizo zimegawanywa katika makundi matatu kwamba wanafunzi watatozwa Sh150 kwa safari, kundi la pili ni njia zenye nauli moja ya Sh300 na la tatu ni la njia zenye nauli zaidi ya moja na kwamba nauli hizo zimeongezeka kwa Sh50 katika nauli za awali, katika kila safari moja.

Shio alitoa mfano akisema kwa njia ambayo abiria wake walikuwa wanatozwa nauli ya Sh250 kwa safari, sasa watatozwa Sh300.Alisema katika Kanda ya Mashariki nauli ya juu zaidi itakuwa Sh1,700 kwa safari kati ya Kigamboni na Pembamnazi, eneo ambalo awali nauli yake ilikuwa Sh1,300.

Sumatra imeongeza nauli hizo baada ya kupokea maombi ya wamiliki wa mabasi mwishoni mwa mwaka jana wakilalamikia kupanda kwa gharama za uendeshaji.

ANGALIZO: Ubabe huzaa ubabe.Kama watawala wetu wanadiriki kutumia ubabe hadi kwa wanafunzi wa shule za msingi na serikali,basi tukae tukijua kuwa tulipo na tuendako si salama.Maandamano ni haki ya msingi ya kila mwananchi alimradi hayahatarishi amani.Hivi kuna ugumu gani kwa askari kutoa escort kwa waandamanaji hadi watapowasilisha ujumbe wao kunakohusika na kisha kuwasihi warejee makwao kwa amani?

Hizi ni dalili za wazi za udikteta kwa kisingizio cha kulinda amani na utulivu.

10 Mar 2011

Katika makala yangu ndani ya jarida mahiri la Raia Mwema toleo la wiki hii nimechambua hotuba ya Rais Kikwete ya mwisho wa mwezi Machi.Lakini pamoja na makala hiyo na nyinginezo zilizoandikwa na magwiji wa uchambuzi,pia kuna habari mbalimbali zinazohusu kila kada ya jamii

BONYEZA HAPA kusoma makala hiyo.

7 Mar 2011


On behalf of my readers I would like to wish a very happy birthday to a fellow blogger,Faith Charles Hillary a.k.a Candy.She is just one of those people you feel quite privileged to have known.She might be in her early 20s but her knowledge and blogging skills are supremely amazing.


Here is a little "gift" for you.

.


Kwa siku kadhaa sasa kumekuwa na taarifa kuwa Mchungaji mmoja mstaafu huko Monduli,mkoani Arusha anatoa tiba ya Ukimwi kwa gharama nafuu ya shilingi 500.Inaelezwa kuwa maelfu kwa maelfu ya watu wamekuwa wakimiminika kwa Mchungaji huyo Ambilikile Mwasakile kujipatia tiba ya gonjwa hilo hatari .

Japo kwa kiasi kikubwa ugonjwa wa Ukimwi unadhibitika kwa sasa kutokana na uvumbuzi wa dawa zenye ufanisi zaidi katika kudhibiti athari za ugonjwa huo,tiba rasmi haijapatikana.Hata hivyo,ukweli huu haumaanishi kuwa tiba ya Mchungaji Mwasakile ni feki kwa vile hadi sasa hakuna mtu au taasisi iliyopinga madai yake.

Pia,huwezi kuwashangaa maelfu ya watu wanaofurika kwa Mchungaji huyo kusaka tiba.Kama malaria tu inawafanya watu wakimbilie mahospitalini,sembuse waathirika wa Ukimwi!

Lakini kama kichwa cha habari kinavyohoji,ukimya wa Wizara ya Afya na serikali kwa ujumla kuhusu madai hayo unaweza kuzua zahma kama ile ya upatu maarufu wa DECI.Katika sakata hilo la "kupanda mbegu",watumishi kadhaa wa Mungu walifanikiwa kuhamasisha maelfu kwa maelfu ya Watanzania "kupanda mbegu" zao kwa matarajio ya kuvuna mamilioni.Sote tunajua kilichofuata.

Serikali ilikuwa ikifahamu uwepo wa DECI lakini haikuchukua hatua stahili (kuruhusu au kuharamisha) hadi pale ilipozinduka na kupiga marufuku upatu huo,hatua iliyowaacha wananchi lukuki wakiwa wamepoteza fedha zao "za ngama".

Sasa japo katika suala hili la tiba ya ukimwi,malipo ni shilingi 500 tu,unyeti wa suala hilo na faida au athari zake unalazimisha serikali kutoa kauli rasmi.Tunafahamu ombwe kubwa la uongozi linaloikabili serikali yetu lakini si kwa kiwango cha kushindwa kusema lolote kuhusu suala hili "dogo" japo linaloweza kuwa na athari kubwa kwa jamii.

Hivi kwa mfano tiba ya Mchungaji huyo ni feki,je hiyo haitoathiri watu wanaoweza kusitisha matibabu ya dawa za kudhibiti virusi vya Ukimwi (ARVs?Serikali yoyote yenye kujali watu wake inapaswa kutoa kauli ya mwongozo kwa wananchi wake kuhusu ukweli au uongo wa madai hayo ya kupatikana kwa tiba ya ukimwi.

Japo kujaribu kuhalalisha au kupinga madai hayo si kazi nyepesi,mazingira yafuatayo yanaweza kutoa mwanga japo kidogo:

Kwanza,katika imani za kidini,kuna uwezekano kwa binadamu kujaliwa karama za kufanya miujiza.Nadhani baadhi ya wasomaji wanafahamu kazi za watu kama Father Nkwera na yule mama wa Mikocheni (anadhani alikuwa anaitwa Esther kama sikosei).Kadhalika,wengi wetu tumesikia miujiza ya Sheikh Shariff.

Pili,kuna watu wanaoaminika kuwa na uwezo wa kutibu maradhi mbalimbali kwa kutumia tiba za asili.Katika ukoo wetu,kuna ndugu yangu mmoja ambaye amekuwa akitoa tiba za asili katika eneo la Kiberege huko Morogoro.Kila nilipokuwa namtembelea nilikuwa nashuhudia namna anavyotibu watu wenye matatizo mbalimbali,ya kiafya na kimaisha.Hata hivyo,hapo kwenye "zahanati" yake kuna tangazo kuwa yeye hana uwezo wa kutibu ukimwi.

Tatu,ni rahisi kuzusha jambo na likaaminika miongoni mwa wengi.Na kama jambo lenyewe ni habari njema basi si ajabu "waaminifu" wa awali wakasambaza habari hizo "njema" na kupelekea tetesi zisizo na ukweli kupata uaminifu.Waingereza wana msemo kwamba uongo usipokemea unaishia kupata hadhi ya kuwa ukweli.Sasa ikitokea kuwa madai ya Mchungaji huyo si ya kweli,lakini hakuna anayekanusha,basi madai hayo yanaweza kuchukua hadhi ya "ukweli".

Kinachonipa wasiwasi ni kauli ya Mchungaji Mwasakile kuwa alianza kutoa matibabu hayo mwezi Agosti mwaka jana baada ya kuoteshwa na Mungu.Kwa maana hiyo,kuna watu kadhaa ambao wanaweza kuwa mashuhuda wa ufanisi wa dawa anazotoa kwa wagonjwa wake.Kwanini habari hizo hazikufahamika hadi majuzi,inabaki kuwa muujiza kama habari yenyewe ya tiba.

Pengine unaweza kusema si rahisi mtu kutapeli kwa kutoza shilingi 500 tu.Lakini ukifanya hesabu za chap chap utagundua kuwa laiti wagonjwa 2000 tu wakilipa kiwango hicho,Mchungaji atakuwa ametengeneza shilingi milioni moja.Na kwa mujibu wa taarifa za idadi ya watu wanaoelekea kwa Mchungaji huyo,yawezekana ameshachuma shilingi milioni kadhaa hadi sasa.


Ni mapema mno kubaishiri lolote kuhusu madai hayo.Kwa upande mmoja tiba kwa nguvu za kiroho au dawa asilia inawezekana,japo sina hakika kama ukimwi nao unatibika kwa njia hizo.Lakini,again,katika Mungu yote yanawezekana.

Serikali inaweza kuwasaidia Watanzania kwa kutoa tamko rahisi kuhusu madai hayo.Na licha ya ombwe la uongozi linaloikabili serikali yetu,suala hili linaweza kuwa rahisi zaidi hasa kwa vile taarifa zinaeleza kuwa vigogo kadhaa wameonekana wakielekea kwa Mchungaji huyo kwenda kujipatia tiba.Hawa wanaweza kuwa mashuhuda wazuri katika suala hilo.


Wakati jamii inasubiri uthibitisho wa madai ya Mchungaji huyo ni vema kubaki na msimamo rasmi wa kitabibu kuwa ukimwi hauna tiba.Na kwa waliokwishapewa "tiba" ya Mchungaji huyo,ni muhimu kwao kufanya vipimo vya kitaalamu kuthibitisha kama kweli wamepona.Na kama wakipona basi iwe fundisho kwao badala ya "kurejesha libeneke kwa kasi mpya,nguvu mpya na ari mpya"

Picha zote kwa hisani ya Michuzi

Kwa habari na picha zaidi soma hapa kwa Miss Jestina

5 Mar 2011


Tunaposema kuna ombwe la uongozi kwenye Serikali ya Rais Jakaya Kikwete baadhi ya vichwa panzi wanatuita wachochezi.Sasa unapoona Waziri anauchapa usingizi kwenye mkutano wa kimataifa,huku bosi wake akiwa kando,basi sijui tusemeje!!!

Na tunaposema Kikwete ni kiongozi dhaifu sio kama ni uchochezi,majungu au chuki binafsi.Hivi kama Rais anashindwa kumkemea Waziri wake kwa kulala kwenye mkutano tunaoambiwa una umuhimu mkubwa kwa nchi yetu (hadi imelazimu mkuu wa nchi aende mwenyewe badala ya kuwakilishwa na Makamu wake,Waziri Mkuu au Waziri wa Nishati na Madini)atamudu vipi kukemea wabaka uchumi ambao baadhi yao ni watu wake wa karibu waliochangia harakati zake za kuukwaa Urais?

Na kuna umuhimu gani kwa fedha ya walipa kodi kugharamia safari ya Ngeleja ambaye anaishia kulala mkutanoni badala ya kutuwakilisha?Au Kikwete amelazimika kwenda mwenyewe badala ya kumwacha Ngeleja pekee kwa vile alijua kuwa waziri wake huyo ataishia kuuchapa usingizi mkutanoni?

Kutegemea watu wa aina hii wanaweza kumsaidia Mtanzania kuondokana na umasikini wa kutupa ni sawa na kutegemea kugema damu kwenye jiwe.Na ukiona waziri mzima pasi haya anachapa usingizi huku Rais wake akiwa kando basi ujue wazi kuwa si akina Richmond na Dowans tu waliomudu kutuingiza mkenge bali tutarajie mengi zaidi.Unadhani kama Ngeleja anathubutu kuuchapa usingizi katika mkutano wa kimataifa unaouhusu maslahi ya nchi,hali inakuwaje wakati anashughulikia maslahi ya nchi ofisini mwake?Sintoshangaa kusikia kuna mikataba ya kuhamisha madini yetu ikisainiwa huku waziri yuko fofofo usingizini

Au Ngeleja ameanzisha mashindano ya kuchapa usingizi dhidi ya Mbunge wa CCM Kapteni John Komba,ambaye kama inavyoonekana pichani chini,alifumwa akiwakilisha wapiga kura wa jimbo lake kwa kuchapa usingizi Bungeni Dodoma



Picha kwa hisani ya Jamii Forums


JINA LA BLOG: MBEYA YETU
Tunapenda kulitambulisha wadau wote libeneke jipya la Mbeya Yetu ambapo nia na malengo ni kuwaletea habari mbali mbali kutoka Jijini Mbeya, Tanzania na Duniani kwa Ujumla ikiwa unatukio la aina lolote usisite kututumia kupitia [email protected] . karibuni nyote na asanteni kwa kututembelea.

Kwa pamoja tunaweza.
.

Karibuni sana wadau.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.