18 Jul 2011


BRILLIANT BUDGET SPEECH, HONGERA SANA! 
Nd. Mnyika,
Nimesoma hotuba yako bungeni hapa chini kwa makini sana na kupata faraja kubwa – hongera nyingi, na kama wasemavyo wataliano – BRAVISSIMO!  Pia nimefurahi zaidi baada ya kuona baadhi ya yale ninayoandika na kushauri, hususan maswala ya urani (uranium), kupewa hisa watanzania, STAMICO na TPDC, maswala ya kulinda na kuhufadhi vizuri mazingira ya nchi wakati wa uchumbaji wa madini, haja ya kuchunguza na kubadilisha mikataba mibovu ya madini ikiwa ni pamoja na ulaghai wa kampuni kama Williamson Diamonds, TanzaniteOne, uzembe uliofanyika kuingia mikataba mibovu ya gesi asilia n.k., haya mambo yote umeyachambua ipasavyo na hata kwenda mbele zaidi kwa kuweka bayana baadhi ya mambo mengine ambayo mimi kama mtaaalamu sikuwa nayafahamu kuwa yanatendeka Tanzania hivyo kuweza kunipa habari ambazo zitanisaidia kuyachambua kitaalamu, tena kwa kina. Nimepaka rangi baadhi ya sehemu kwenye hotuba yako kuonyesha yale ambayo yamenigusa zaidi na mambo ambayo niliwahi kuyakemea na kusisitiza yachunguzwe na kubadilishwa kwa muda mrefu.
Nadhani utakuwa umesoma barua zangu za hivi karibuni zinazohusu maswala ya madini nchini Mongolia na Sudani Kusini – ziko hapa. Ni matumaini yangu mtazichambua barua hizi pamoja na wenzako wa kambi ya upinzani Bungeni na muangalie namna gani mnaweza kuhakikisha yale muhimu kwa taifa letu yanaweza yakatekelezwa Tanzania. Ndani ya barua hizo utaona pia maoni yangu kuhusu mauaji ya Tarime uliyoniuliza hapo awali ingawa msimamo wangu kuhusu hili jambo niliwahi kuzungumzia vikali kwenye baadhi ya barua zangu zikiwezo hizi hapa: 1 (soma kuhusu mamillionea wa kimya kimya - Silent Millionaires – walivyowadanganya watu wetu Bulyanhulu. Baadhi ya hawa mamillionea ni/au walikuwa wafanyakazi wa serikali). Soma pia hapa 2, pamoja na hapa 3.
Pia hapa chini nakutumia tovuti za makala kadhaa ambazo nadhani ni muhimu kuzisoma hasa baada ya kuona kuwa ni mambo ambayo uliyazungumzia kwenye hotuba yako na mimi pia nimekuwa nikisisitiza kwa muda mrefu yafanyiwe kazi na serikali. Ni matumaini yangu utaendela na msimamo wako imara wa kuibana serikali ifanye marekebisho pale ambapo inaonekana kuwa rasilimali za taifa haziwanufaishi watanzania, na wale waliongia nchini kama wawekezaji wa kigeni, na hata raia na makampuni yetu ya Tanzania, wanakiuka na kuvunja sheria za sekta ya madini. Ni muhimu makosa makubwa tunayoyafanya kwenye sekata ya madini, gesi asilia na petroli yarekebishwe, tena haraka sana. Kama ulivyoeleza kwenye hotuba yako, hakuna sababu yeyote ya msingi watanzania waishi kwenye umaskini wa kutupwa huku wakiwa na utajiri mkubwa wa madini kama tulionao, utajiri ambao serikali yetu inautoa, hata niseme, kuutupa kwa wageni – hii si sahihi hata kidogo. Nitashukuru kama utakuwa unaniarifu mara kwa mara maendeleo ya jitihada zenu kufanikisha azma hii.
Ahsante, na pongezi nyingi kwa ujasiri na uimara wako Bungeni.
Shaaban
Moscow, Urusi.     


MNAKARIBISHWA NYOTE KWENYE SABATO YA WAGENI TAREHE 23/07/2011

Kanisa la wasabato ( Angaza Swahil UK)  linapenda kuwakaribisha  watu wote    kutoka sehemu mbali mbali za Uingereza katika sabato ya wageni itakayofanyika tarehe 23/07/2011 kuanzia saa 3.00 asb hadi saa 11.00 jioni.
Siku hiyo itakuwa ya pekee kweli kwani vikundi mbali mbali vya nyimbo vitakaribishwa kuimba kutoka kwenye kila dhehebu  .Pia watoto wataonyesha programme mbali mbali.

 THEME: NJOO UJUE UNA NINI MKONONI MWAKO

Baada ya ibada ya mchana tutakusanyika pamoja kwa ajili ya chakula na vinywaji.Usipange kukosa lete rafiki yako .Kama hauna usafiri i wasiliana nasi.KARIBU NYOTE

ANUANI
St Barnabas C Of E Church
Elm Road, Reading, RG6 5TS


 


16 Jul 2011


School of Public Policy Building Bridges
Tanzanian Student Wins Research Award
Most young people in Tanzania have never heard of the Maryland School of Public Policy. But through the generosity of those who saw the promise in Emmanuel Sulle, he has completed his first year of studies at the School and has also won the Conservation Research in Eastern Africa’s Threatened Ecosystems (CREATE) Research Award from the Frankfurt Zoological Society. Sulle will study the impact of microcredit institutions (in this case Community Conservation Banks) which are in place within the Serengeti ecosystem in Tanzania. Sulle will conduct the field research in Tanzania during the winter break of 2011-2012.
"Emmanuel is a wonderful example of the School's bridge across the oceans--of using the tools of public policy to improve the quality of life and to make a big impact on the world," says MSPP Dean Don Kettl.
Sulle was working as a Research Associate at the Tanzania Natural Resource Forum when he was encouraged by Professor Robert Nelson to apply to the MSPP program. Nelson’s son Fred, who worked 12 years in Tanzania on wildlife conservation, had worked with Sulle on two research studies – most recently the published report on “Biofuels, land access and rural livelihoods in Tanzania”.
“We need more people like Emmanuel,” said Bob Nelson, who also serves as Sulle’s informal mentor.
  “Unfortunately, they are hard to identify.”
Sulle is currently in Tanzania collaborating with the Maliasili Initiatives to undertake two research projects on “Wildlife Management Areas and Pastoralist Livelihoods: An Assessment,” and “Analysis from Northern Tanzania and Community-based Conservation in the Tarangire-Manyara Corridor: An Assessment of Existing Models and Experiences.”
“Emmanuel is in a position to take his MSPP education and make a serious policy impact in Tanzania,” says MSPP Student Affairs Assistant Director, Taryn Faulkner.
Sulle earned his BA in Economics from St. Augustine University of Tanzania (SAUT) in 2008. He has carried out a variety of research projects commissioned by, or in collaboration with MISERIOR-Germany, Fulbright, Tanzania Natural Resource Forum, Sand County Foundation, and Health and Development International Consultants. He has authored and co-authored a number of research reports on tourism revenue transparency, wildlife management areas, as well as biofuels, land access, and rural livelihoods in Tanzania.
“I am interested to see rational use of natural resources as a tool for poverty reduction in developing countries,” Sulle said.

HONGERA SANA,NDUGU EMMANUEL.KILA LA HERI.

12 Jul 2011


Ndugu zangu wapendwa,kwa niaba ya familia ya Chahali naomba kuwasilisha shukrani za dhati kwa wote ambao kwa namna moja au nyingine mmeungana nasi kwa maombi kwa baba Mzee Philemon Chahali ambaye hali yake bado ni mahututi kufuatia ajali ya kugongwa na pikipiki huko Ifakara,Alhamisi iliyopita.

Ningetamani sana kutoa shukrani kwa kutaja jina la kila mmoja wenu lakini naomba nitoe shukrani za jumla.Nawashukuru sana bloggers wenzangu ambao licha ya kunisaidia kuweka tangazo la maombi ya sala kwa baba mmekuwa mkinitumia meseji na barua pepe za kunipa moyo pamoja na sala/dua zenu.Katika kuonyesha upendo wa hali ya juu,dada yangu blogger wa hapa UK Rachel Siwa aliweka maombi kwenye misa ya Jumapili iliyopita huko Coventry.Tunakushukuru sana dada Rachel na Mungu akubariki.Bloga mwenzangu Miss Jestina naye amekuwa akitujulia hali ya Mzee mara kadhaa kwa siku,bila kuwasahau wadogo zangu Jackie Lawrence (La Princessa) na Faith Charles Hillary (Candy1World) ,na Mtakatifu Simon Kitururu,bloga Malkiory  Matiya na Nova Kambota

Huko Twitter nimekuwa nikipata sapoti ya kutosha tangu zilipojiri habari za ajali.Dada zangu Maria Sarungi na Lilly  Melody,pamoja na wasanii wetu mahiri kabisa Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) na Joseph Haule (Profesa Jay) ni miongoni mwa wana-Twitter wenzangu ambao wamekuwa mstari wa mbele kunifariji.

Kwa bahati mbaya,ukweli mchungu kuhusu maisha ni kwamba mpaka upate tatizo ndio unaweza kufahamu upendo wa watu wanaokuzunguka.Kuna watu nilikuwa sifahamiani nao kabisa lakini baada ya kusikia habari za ajali iliyomkumba baba wamekuwa ni nguzo muhimu kutusapoti.Kwa kweli ninawashukuru sana na Mungu awabariki sana kwa upendo wenu.Ni imani ya familia yetu kuwa sala zenu na zetu zitamsaidia Mzee Chahali sio tu kupata nafuu bali kupona kabisa.

Kwa vile inaniwia vigumu kublog kutokana na tatizo linalonikabili,naomba pia kutumia fursa hii kuwashukuru wasomaji wote wa blogu hii na watu wengineo walionipigia kura katika Tuzo la Blogu za Kitanzania (Tanzanian Blog Awards) ambapo japo sikuibuka mshindi lakini nimepata matokeo ya kupigiwa mstari.Kwa kifupi,blogu hii imeshika nafasi ya pili katika categories za Best Inspiration Blog na Best News Blogs na imeshika nafasi ya tatu katika category ya Best Political Blog.Ukiangalia kwenye hizo categories mbili za mwanzo utagundua kuwa aliyeshika nafasi ya kwanza ni bloga ambaye blogu yake imeshatembelewa na wasomaji zaidi ya milioni 12 wakati blogu hii "inasuasua" na wasomaji 424538 hadi dakika hii.Kwangu hayo ni mafanikio makubwa sana lakini si mafanikio yangu pekee bali ya wadau wote wa blogu hii.Namshukuru kila aliyenipigia kura,na japo hatukuibuka washindi wa jumla,kushiriki kwenye tuzo hizo na kukamata nafasi za juu ni tuzo kubwa sana.

Naomba nimalizie kwa kurejea tena shukrani zangu na za familia yangu kwenue nyote mnaoshirikiana nasi kwenye maombi kwa ajili ya Mzee Philemon Chahali.Ni matumaini yetu kuwa Bwana anasikiliza sala/dua zetu na atamjalia baba uponyaji kwa vile Mungu ni mwema na mwenye upendo.

ASANTENI SANA

7 Jul 2011


Nasikitika kuwafahamisha kuwa baba mzazi Mzee Philemon Chahali amepata ajali mbaya asubuhi hii huko Ifakara.Amegongwa na pikipiki ambazo ndio usafiri mkuu wa huko.Kwa mujibu wa habari nilizonazo hadi muda huu,hali yake ni mbaya,ambapo licha ya kuvnjika mguu pia ameumia kichwani.Kibaya zaidi ni kwamba umri wake ni kwenye miaka ya 80 kwa hiyo mshtuko tu wa ajli unaweza kumwathiri sana.

Basi naomba kutumia fursa hii kuomba sala zenu.Sie Wakristo tunaamini kuwa wanapojumuka wengi kufanya sala basi Mungu naye anakuwepo.Natumaini kwa sala zenu na za familia yetu Mungu atamjalia baba apone na kurejea katika hali yake ya kawaida.

Natanguliza shukrani zangu za dhati.Asanteni 


Na Nova Kambota,

Rais wa awamu ya tatu Mzee Benjamin Mkapa aliwahi kusema kuwa maisha bila vipaumbele ni ujinga mtupu, bilashaka hili halina ubishi kabisa taifa lolote linaloishi bila vipaumbele hugeuka taifa la wahuni, waporaji, mafisadi, wajinga,duni na zaidi huwa taifa legelege na dhaifu.

Wageni mbalimbali kutoka Ulaya, Marekani ,Asia na sehemu nyingine za ulimwengu waliowahi kufika nchini huwa wanashangazwa sana na umasikini wa kutisha unaowaandama wananchi wa taifa hili. Wageni wanatushangaa sana na wataendelea kushangaa kuanzia Mlima Kilimanjaro,Mlima Meru, Udzungwa, Usambara, Ziwa Tanganyika, Victoria, Bahari ya Hindi mbuga nzuri za wanyama kama Mikumi na Ngorongoro lakini pia misitu ya kumwaga tu,mito mingi, mabonde ndiyo usiseme na ardhi yenye rutuba na

ya kutosha lakini bado miaka hamsini baada ya uhuru mamilioni ya watanzania bado ni masikini wa kutupwa.

Kwa mtiririko huu wa mantiki hapa ndiyo inaibuka hoja kuwa watanzania hawafanani na nchi yao hata kidogo kwa maana ni watu mafukara waliozungukwa na utajiri wa kutisha , hakika kuna utofauti mkubwa kati ya watanzania na utajiri wa taifa lao, hata ukifika pale mbuga ya Ngorongoro wanyama wanacheza na kufurahi na ndege wanarukaruka kwa furaha kubwa, nenda kandokando ya bahari ya Hindi uone mawimbi yanavyopanda na kushuka kwa furaha kisha angalia samaki walivyo na furaha kisha sasa rudi katika maisha ya walalahoi wa nchi hii, kweli inahuzunisha kuona wanyama wana furaha kushinda watanzania, inauma sana!

Kuna kisa kimoja cha kuhuzunisha sana ambacho nadhani watoto wetu wanapaswa kufundishwa madarasani. Inaelezwa kuwa mwaka jana 2010 wakati wa uchaguzi mkuu mwangalizi mmoja wa kimataifa kutoka nje alitembelea Tunduru akaona watu wanavyoogelea kwenye umasikini wa kutisha kisha akatupa macho kwa mbali akaona misitu mizuri na mto Ruvuma kisha akahoji kuwa inakuwaje watu hao ni masikini sana? Wananchi hawakuwa na la kujibu baadaye mzungu huyo akasema kuwa “siamini kabisa na hainiingii akilini kuwa CCM huwa inashinda kihalali kwa maana haiwezekani watu masikini kama hawa waichague CCM”

Hivi nani atanishawishi kuwa CCM inashinda kihalali? Hapa uhalali unaozungumzwa sio wa kura tu bali hata wa kuwaacha watu huru, kwa maana haiwezekani watu wanakuwa masikini, wanafanywa wajinga na mifumo mibovu kiasi kwamba hawajui umuhimu wa kura halafu wanajiandikisha watu milioni 19 kupiga kura lakini siku ya kupiga kura wanajitokeza milioni 5 na CCM wanashinda! Kisha uniambie hapo kuna ushindi? Ushindi gani? wakati milioni 14 nzima hawajapiga kura? Idadi hii inaweza kubadili matokeo, kwa maana nyingine yule mwangalizi wa kimataifa yupo sahihi kabisa kuwa watanzania hawaichagui CCM badala yake inajichagua yenyewe na kujipa madaraka, ajabu sana!

Watanzania wanalia kwa mengi, heri wote wangekuwa masikini lakini kuna wenzao “wajanja wachache” wanaishi kama wafalme kwa jasho la watanzania. Cha ajabu katika umasikini huu wa kutisha wa watanzania kuna baadhi ya watanzania wachache wamejigeuza “miungu watu” wamejimilikisha utajiri wote huu wakisaidiana na waporaji mabeberu kutoka Ulaya na Marekani, hawa hawajui njaa ni nini? hawafahamu masikini anafananaje? Wenyewe wanajua kuvaa suti na tai na mwisho wa mwaka wanaenda kwenye maduka makubwa ya nguo huko London na Dubai ili kuwafanyia “shopping” wake zao na watoto wao wapendwa.

Nchi imekuwa ya matabaka kiasi kwamba mpaka taifa linayumba . Leo hii imefika mahali kuna watu wana nguvu za kutisha kwenye nchi mpaka mkurugenzi wa TAKUKURU anakiri kwenye mtandao wa Wikileaks kuwa Tanzania kuna “untouchables” hawagusiki hawa. Katika mazingira haya bado CCM inahubiri usawa, usawa gani? hata mtoto mdogo hawezi kushawishika kuwa kuna hata chembe ya huo usawa kwenye nchi hii, labda kidogo CCM waje na hoja ya kuwa na nchi mbili za kimatabaka kwenye taifa moja ndiyo! Kuna Tanzania ya tabaka la juu na Tanzania ya tabaka la chini.

Huu ndiyo ukweli wa mambo , na matabaka haya mwanzo wake ni kuwa kuna wale walioshikilia utajiri wa taifa na wale waliotengwa na utajiri huo. Cha kusikitisha zaidi serikali inapigia chapuo mpasuko huu wa kitabaka kiasi kwamba imejenga shule za kata maalumu kwa masikini ili wakafeli na kuna mashule ya kimataifa yenye ubora haya ni maalumu kwa ajili ya watoto wao na maswahiba zao. Serikali haijaishia hapo tu sasa hivi Tanzania fedha iko juu ya sheria , nani asiyefahamu ukiwa na fedha nchi hii unaweza kupindisha sheria? Zaidi ya yote kuonyesha kuwa serikali yetu ni legelege ni jinsi inavyozitekeleza hospitali za serikali kiasi kwamba ni kama majengo tu bila dawa na ili kuonyesha kweli ubaguzi ni mfumo rasmi kwenye nchii hii hakuna “mkubwa” anaayekwenda kwenye hospitali za serikali huko ni kwa kapuku na walalahoi, ubaguzi wa kutisha!

Viongozi hawaishii hapo tu kwenye juhudi zao za kuwafukarisha wananchi na kuwaibia mali zao, sasa wameanzisha soko huria la kura na wapiga kura na mnada kila baada ya miaka mitano. Hivi kwanini viongozi wasiwaache huru watanzania? Kwanini wasiwaache wakajichagulia watu wanaowaamini ni viongozi bora? Huu kama sio ujambazi wa haki za masikini ni nini? yaani hao walioko madarakani mwaka jana tu walipambana kununua kura kama sio kwenye ngazi ya chama basi kwenye uchaguzi kamili lakini ndiyo hivyo ukweli ni kuwa wamenunua kura kwa pesa nyingi na sasa wapo madarakani wanashindana kupora mali za wavuja jasho.

Taifa limekosa vipaumbele , limehalalisha rushwa, uporaji na ufisadi, taifa linapepesuka kwa uhuni na tamaa za viongozi , dola imedhoofika sana hata kamanda mkuu Rais Jakaya Kikwete analifahamu hili lakini tatizo “kupe” wamejaa kuanzia huko CCM mpaka serikalini. Kile alichokitabiri Mwalimu Nyerere sasa kinatokea kweli, Mwalimu aliwahi kusema “serikali isiyojali wananchi wake haina uhalali hata kama imepigiwa kura” sitaki kuamini kuwa serikali ya CCM haina uhalali ila nashawishika kuwa haijali wala kuthamini wananchi wake hivyo kwa maana nyingine imeanza kupoteza uhalali wake.

Imefika sehemu sasa watanzania wanapaswa kufanana na utajiri wa nchi yao, viongozi inabidi wafahamu kuwa watanzania hawana sababu ya kuwa masikini kama walivyo sasa. Watanzania lazima wafanywe kujivunia utanzania wao tofauti na hivi sasa ambapo kuna watanzania wanajilaani kwa kuwa watanzania yote kwasababu ya ubabaishaji wa viongozi wao ambao badala ya kuwatumikia wananchi wao wako “busy” kutumikia matumbo yao na familia zao.

Lakini kama kawaida ya viongozi wetu wana tabia ya kuweka pamba masikioni hawataki kusikia bilashaka hata hili watapuuzia lakini nawapa angalizo kuwa watanzania wanafahamu kuwa hawakuumbwa walivyo bali umasikini wao umetengenezwa hivyo ni swala la muda tu lakini siku ikifika uvumilivu utakapowashinda basi watawang’oa wababaishaji wote wanaojineemesha na mali zao tena kwa njia yoyote ile, hizi ni zama za ukweli na uwazi ni wakati sahihi wa kuwa na mgawanyo sawa wa keki ya taifa…..Allutacontinua!

Nova Kambota Mwanaharakati,



+255717 709618

Tanzania, East Africa

07/07/2011, Alhamisi

Naomba kura yako kwenye tuzo za blog Tanzania kwenye category ya best collaboration/group blog, best informative political blog na best political blog kunipigia kura nenda http://www.tanzanianblogawards.com/


 

6 Jul 2011


Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalam wa Taifa Rashid Othman (wa tatu kushoto,mwenye shati la kitenge)
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TISS, Jack Zoka

Wabunge walipua Usalama wa Taifa  
Tuesday, 05 July 2011 21:00

Ramadhan Semtawa, Dar
WABUNGE watatu jana waliishambulia Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), bungeni baada ya kueleza kuwa imeshindwa kuzuia uhujumu uchumi na badala yake imejikita kwenye siasa za kukipendelea chama tawala, CCM na kuukandamiza upinzani.

Tuhuma hizo zinakuja wakati tayari nchi imetikiswa na matukio kadhaa ya ufisadi ikiwamo wizi wa zaidi ya Sh133 bilioni katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ununuzi wa rada ya kijeshi na ufisadi unaodaiwa kufanywa katika kampuni za Meremeta, Tangold na Deep Green Finance.

Kwa nyakati tofauti wakichangia Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais (Utumishi, Utawala Bora na Uratibu na Mahusiano ya Jamii), wabunge hao waliirushia makombora idara hiyo na kupendekeza ikajifunze nje jinsi ya kufanya kazi zake.

Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, ndiye alikuwa mwiba zaidi baada ya kuweka bayana kwamba idara hiyo imeshindwa kusaidiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kuzuia rushwa kubwa zinazohujumu uchumi wa nchi.

Mchungaji Msigwa ambaye alizungumza kwa hisia kali, alisema idara hiyo imegeuka chombo cha kulinda maslahi ya kisiasa hasa ya CCM na kukandamiza upinzani huku ikiacha uchumi wa nchi ukiendelea kuhujumiwa.

Kwa mujibu wa Msigwa, endapo Idara ya Usalama wa Taifa, ingetumia nguvu nyingi kuzuia uhujumu uchumi kama inavyotumia kukandamiza upinzani kwa kujihusisha kwenye siasa, nchi ingeweza kupiga hatua kubwa.

Alitaka watendaji wake kwenda kujifunza majukumu yao nje ya nchi badala ya kuendelea kujihusisha na siasa kama wanavyofanya sasa.Mchungaji Msigwa alisema nchi inakabiliwa na maadui ndani na nje hivyo ni vema idara ikajikita katika kuwashughulikia hao kuliko kujiingiza zaidi kwenye siasa na kugeuka idara ya usalama ya CCM.


Takukuru na rushwa
Akizungumzia Takukuru na mapambano dhidi ya rushwa kubwa, Mchungaji Msigwa alimtaka Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Dk Edward Hoseah, kuendeleza mapambano na kama wakubwa wakimwekea kiwingu katika utendaji wake, bora aachie ngazi.

Msigwa alifafanua kwamba, hata katika nchi za Kenya na Uganda, wakuu wa taasisi za kupambana na rushwa walipoona mambo ni magumu kutokana na wakubwa kuwadhibiti, waliamua kuachia nyadhifa zao.

Mnyika naye ashambulia usalama
Mbunge wa Ubungo John Mnyika, naye alitumia mjadala huo kuipa somo TISS akiitaka iachane na siasa za kukandamiza upinzani bali ijikite katika kulinda maslahi ya taifa.

Katibu huyo wa wabunge wote wa Chadema bungeni, alisema kazi kubwa za idara hiyo isiwe kujiingiza kwenye siasa kwa kukandamiza upinzani bali kuangalia mustakabali mzuri wa nchi.

Mnyaa: Idara imejikita Bara
Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Habib Mnyaa, alisema awali Usalama wa Taifa ulikuwa ukijitegemea kwa upande wa Zanzibar na iliyokuwa Tanganyika ambayo kwa sasa inaitambulika kwa mwavuli wa Tanzania Bara.

Hata hivyo, alisema baada ya idara hiyo kuunganishwa miaka ya 1980, idara hiyo inaonekana kujikita zaidi Bara huku Zanzibar ikikosa hata ofisi kubwa ya maana kwa ajili ya operesheni.

Maji Marefu aikingia kifua
Hata hivyo, mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Stephen Ngonyani maarufu kama Profesa Majimarefu, alipinga hoja za wabunge wenzake hao, akisema hawaitendei haki kwani imekuwa ikifanya kazi kubwa kulinda usalama wa taifa.

Kwa mujibu wa Ngonyani, wakosoaji hao wa TISS wanapaswa kuwa mashuhuda kwa kwenda nchi jirani na nyingine za Afrika, ambako usalama wa taifa ni mbaya, huku zikikabiliwa na vitisho vikubwa vya mauaji na vurugu.

Akisisitiza alitoa mfano wa nchi moja (hakuitaja) ambako aliwahi kuingizwa ndani kulala wakati wa mchana kutokana na hali mbaya ya usalama katika taifa na kusisisiza, "ninyi mnaoisema Idara ya Usalama wa Taifa hebu acheni kauli zenu hizo."

"Nendeni nchi jirani au kwingine mkaangalie, mimi niliwahi kuingizwa ndani mchana kwenda kulala kutokana na hali mbaya ya usalama. Hapa kwetu Idara inafanya kazi kubwa, nchi imetulia," alizidi kuikingia kifua na kuwararua wakosoaji.

Katika kuonyesha jinsi idara hiyo inavyofanya kazi kwa ufanisi, Ngonyani alitaka Serikali kuongezea mishahara watumishi wa TISS na kuongeza, "hawa vijana tunashinda nao hapa hadi saa 4:00 usiku wanaangalia usalama halafu tunawasema hawafanyi kazi!"

"Tena nasema waongezewe mishara, vijana wanafanya kazi nzuri na kubwa ya kulinda nchi. Tunapaswa kuwapa nguvu siyo kuwalaumu siyo sahihi hata kidogo," alisisitiza Ngonyani.

Katika miaka ya karibuni hasa baada ya kuongezeka vuguvugu la vyama vingi vya siasa, TISS imekuwa ikikokosolewa na baadhi ya watu kutokana na kuacha baadhi ya misingi yake ya kulinda maslahi ya taifa ikiwamo uchumi, kama ilivyokuwa ikifanya wakati wa Awamu ya Kwanza chini ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

Mwaka jana baada ya matokeo ya Uchaguzi Mkuu, idara hiyo pia ilijikuta katika tuhuma za kile kilichoelezwa na Chadema kwamba, ilitumikia kuchakachua matokeo ya kura za urais, hali iliyomlazimu Naibu Mkirugenzi Mkuu Jack Zoka, kujitokeza hadharani na kufanya mkutano na waandishi wa habari kuondoa hali tete na giza lililokuwa limegubika nchi. Zoka alikanusha tuhuma hizo kwamba Idara ilihusika katika kuchakachukua matokeo ya urais.

CHANZO: Mwananchi

Imetumwa na FRANK EYEMBE wa Urban Pulse

5 Jul 2011




ADAM GOLDMAN and MATT APUZZO   07/ 5/11 12:09 AM ET   AP
React
WASHINGTON -- After Navy SEALs killed Osama bin Laden, the White House released a photo of President Barack Obama and his Cabinet inside the Situation Room, watching the daring raid unfold.
Hidden from view, standing just outside the frame of that now-famous photograph was a career CIA analyst. In the hunt for the world's most-wanted terrorist, there may have been no one more important. His job for nearly a decade was finding the al-Qaida leader.
The analyst was the first to put in writing last summer that the CIA might have a legitimate lead on finding bin Laden. He oversaw the collection of clues that led the agency to a fortified compound in Abbottabad, Pakistan. His was among the most confident voices telling Obama that bin Laden was probably behind those walls.
The CIA will not permit him to speak with reporters. But interviews with former and current U.S. intelligence officials reveal a story of quiet persistence and continuity that led to the greatest counterterrorism success in the history of the CIA. Nearly all the officials insisted on anonymity because they were not authorized to speak to reporters or because they did not want their names linked to the bin Laden operation.
The Associated Press has agreed to the CIA's request not to publish his full name and withhold certain biographical details so that he would not become a target for retribution.
Call him John, his middle name.
John was among the hundreds of people who poured into the CIA's Counterterrorism Center after the Sept. 11 attacks, bringing fresh eyes and energy to the fight.
He had been a standout in the agency's Russian and Balkan departments. When Vladimir Putin was coming to power in Russia, for instance, John pulled together details overlooked by others and wrote what some colleagues considered the definitive profile of Putin. He challenged some of the agency's conventional wisdom about Putin's KGB background and painted a much fuller portrait of the man who would come to dominate Russian politics.
That ability to spot the importance of seemingly insignificant details, to weave disparate strands of information into a meaningful story, gave him a particular knack for hunting terrorists.
"He could always give you the broader implications of all these details we were amassing," said John McLaughlin, who as CIA deputy director was briefed regularly by John in the mornings after the 2001 attacks.
From 2003, when he joined the counterterrorism center, through 2005, John was one of the driving forces behind the most successful string of counterterrorism captures in the fight against terrorism: Abu Zubaydah, Abd al-Nashiri, Khalid Sheik Mohammed, Ramzi bin Alshib, Hambali and Faraj al-Libi.
But there was no greater prize than finding bin Laden.
Bin Laden had slipped away from U.S. forces in the Afghan mountains of Tora Bora in 2001, and the CIA believed he had taken shelter in the lawless tribal areas of Pakistan. In 2006, the agency mounted Operation Cannonball, an effort to establish bases in the tribal regions and find bin Laden. Even with all its money and resources, the CIA could not locate its prime target.
By then, the agency was on its third director since Sept. 11, 2001. John had outlasted many of his direct supervisors who retired or went on to other jobs. The CIA doesn't like to keep its people in one spot for too long. They become jaded. They start missing things.
John didn't want to leave. He'd always been persistent. In college, he walked on to a Division I basketball team and hustled his way into a rotation full of scholarship players.
The CIA offered to promote him and move him somewhere else. John wanted to keep the bin Laden file.
He examined and re-examined every aspect of bin Laden's life. How did he live while hiding in Sudan? With whom did he surround himself while living in Kandahar, Afghanistan? What would a bin Laden hideout look like today?
The CIA had a list of potential leads, associates and family members who might have access to bin Laden.
"Just keep working that list bit by bit," one senior intelligence official recalls John telling his team. "He's there somewhere. We'll get there."
John rose through the ranks of the counterterrorism center, but because of his nearly unrivaled experience, he always had influence beyond his title. One former boss confessed that he didn't know exactly what John's position was.
"I knew he was the guy in the room I always listened to," the official said.
While he was shepherding the hunt for bin Laden, John also was pushing to expand the Predator program, the agency's use of unmanned airplanes to launch missiles at terrorists. The CIA largely confined those strikes to targets along Pakistan's border with Afghanistan. But in late 2007 and early 2008, John said the CIA needed to carry out those attacks deeper inside Pakistan.
It was a risky move. Pakistan was an important but shaky ally. John's analysts saw an increase in the number of Westerners training in Pakistani terrorist camps. John worried that those men would soon start showing up on U.S. soil.
"We've got to act," John said, a former senior intelligence official recalls. "There's no explaining inaction."
John took the analysis to then CIA Director Michael Hayden, who agreed and took the recommendation to President George W. Bush. In the last months of the Bush administration, the CIA began striking deeper inside Pakistan. Obama immediately adopted the same strategy and stepped up the pace. Recent attacks have killed al-Qaida's No. 3 official, Mustafa Abu al-Yazid, and Pakistani Taliban leader Baitullah Mehsud.
All the while, John's team was working the list of bin Laden leads. In 2007, a female colleague whom the AP has also agreed not to identify decided to zero in on a man known as Abu Ahmed al-Kuwaiti, a nom de guerre. Other terrorists had identified al-Kuwaiti as an important courier for al-Qaida's upper echelon, and she believed that finding him might help lead to bin Laden.
"They had their teeth clenched on this and they weren't going to let go," McLaughlin said of John and his team. "This was an obsession."
It took three years, but in August 2010, al-Kuwaiti turned up on a National Security Agency wiretap. The female analyst, who had studied journalism at a Big Ten university, tapped out a memo for John, "Closing in on Bin Laden Courier," saying her team believed al-Kuwaiti was somewhere on the outskirts of Islamabad.
As the CIA homed in on al-Kuwaiti, John's team continually updated the memo with fresh information. Everyone knew that anything with bin Laden's name on it would shoot right to the director's desk and invite scrutiny, so the early drafts played down hopes that the courier would lead to bin Laden. But John saw the bigger picture. The hunt for al-Kuwaiti was effectively the hunt for bin Laden, and he was not afraid to say so.
The revised memo was finished in September 2010. John, by then deputy chief of the Pakistan-Afghanistan Department, emailed it to those who needed to know. The title was "Anatomy of a Lead."
As expected, the memo immediately became a hot topic inside CIA headquarters and Director Leon Panetta wanted to know more. John never overpromised, colleagues recall, but he was unafraid to say there was a good chance this might be the break the agency was looking for.
The CIA tracked al-Kuwaiti to a walled compound in Abbottabad. If bin Laden was hiding there, in a busy suburb not far from Pakistan's military academy, it challenged much of what the agency had assumed about his hideout.
But John said it wasn't that far-fetched. Drawing on what he knew about bin Laden's earlier hideouts, he said it made sense that bin Laden had surrounded himself only with his couriers and family and did not use phones or the Internet. The CIA knew that top al-Qaida operatives had lived in urban areas before.
A cautious Panetta took the information to Obama, but there was much more work to be done.
The government tried everything to figure out who was in that compound.
In a small house nearby, the CIA put people who would fit in and not draw any attention. They watched and waited but turned up nothing definitive. Satellites captured images of a tall man walking the grounds of the compound, but never got a look at his face.
Again and again, John and his team asked themselves who else might be living in that compound. They came up with five or six alternatives; bin Laden was always the best explanation.
This went on for months. By about February, John told his bosses, including Panetta, that the CIA could keep trying, but the information was unlikely to get any better. He told Panetta this might be their best chance to find bin Laden and it would not last forever. Panetta made that same point to the president
Panetta held regular meetings on the hunt, often concluding with an around-the-table poll: How sure are you that this is bin Laden?
John was always bullish, rating his confidence as high as 80 percent.
Others weren't so sure, especially those who had been in the room for operations that went bad. Not two years earlier, the CIA thought it had an informant who could lead him to bin Laden's deputy. That man blew himself up at a base in Khost, Afghanistan, killing seven CIA employees and injuring six others.
That didn't come up in the meetings with Panetta, a senior intelligence official said. But everyone knew the risk the CIA was taking if it told the president that bin Laden was in Abbottabad and was wrong.
"We all knew that if he wasn't there and this was a disaster, certainly there would be consequences," the official recalled.
John was among several CIA officials who repeatedly briefed Obama and others at the White House. Current and former officials involved in the discussions said John had a coolness and a reassuring confidence.
By April, the president had decided to send the Navy SEALs to assault the compound.
Though the plan was in motion, John went back to his team, a senior intelligence official said.
"Right up to the last hour," he told them, "if we get any piece of information that suggests it's not him, somebody has to raise their hand before we risk American lives."
Nobody did. Inside the Situation Room, the analyst who was barely known outside the close-knit intelligence world took his place alongside the nation's top security officials, the household names and well-known faces of Washington.
An agonizing 40 minutes after Navy SEALs stormed the compound, the report came back: Bin Laden was dead.
John and his team had guessed correctly, taking an intellectual risk based on incomplete information. It was a gamble that ended a decade of disappointment. Later, Champagne was uncorked back at the CIA, where those in the Counterterrorism Center who had targeted bin Laden for so long celebrated. John's team reveled in the moment.
Two days after bin Laden's death, John accompanied Panetta to Capitol Hill. The Senate Intelligence Committee wanted a full briefing on the successful mission. At one point in the private session, Panetta turned to the man whose counterterrorism resume spanned four CIA directors.
He began to speak, about the operation and about the years of intelligence it was based on. And as he spoke about the mission that had become his career, the calm, collected analyst paused, and he choked up.

___


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.