9 Feb 2012

Nani anasema ukweli kuhusu posho za wabunge?

WIKI iliyopita inaweza kuingia katika vitabu vya historia ya nchi yetu kufuatia mlolongo wa matukio yanayozidi kuashiria kuwa hali si shwari katika uongozi wa nchi yetu.

Tukio la kwanza lilikuwa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu kukanusha habari kwamba Rais Jakaya Kikwete ameshasaini kuridhia ongezeko la posho za wabunge kutoka shilingi 70,000 kwa siku hadi shilingi 200,000.

Kukanusha huko kulifuatia taarifa kwamba Spika Anne Makinda aliwaambia wandishi wa habari kwamba Rais alikuwa ameridhia posho hizo, na kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwaaambia wabunge kwamba Rais alikubali posho zilipwe.  

Binafsi, nilibahatika kufanya maongezi yasiyo rasmi na Rais Kikwete kwenye mtandao wa  jamii wa Twitter. Kama ilivyoeleza taarifa ya Kurugenzi ya Ikulu, Rais Kikwete alieleza kwamba (namnukuu), “Upo mkanganyiko na upotoshaji mkubwa kuhusu jambo hili. Wengi hawaelewi bado. Litatolewa ufafanuzi kwa kina.

Jibu hilo lilitokana na ombi langu kwa Rais ambapo niliandika (ninajinukuu), “Mheshimiwa Rais, ninakusihi umwajibishe ‘mtoto wa mkulima (Waziri Mkuu Pinda) kwa kukuchonganisha na umma eti umebariki posho...

Kadhalika, Rais alifafanua kwamba (namnukuu) “Nilitoa maelekezo kuhusu suala la posho za wabunge. Maelekezo hayo hayakuwa kuridhia jambo hilo.” Baada ya tweet hiyo Rais aliongeza, “Nilikubali haja ya kuangalia upya posho kwa wabunge na niliwataka wabunge kutumia busara na hekima katika kutafakari hili...Wabunge watumie kikao cha Februari cha Bunge kulizungumzia suala hili. Ni muhimu.

Kabla ya kuendelea na mjadala kuhusu suala hili sina budi kumpongeza Rais, si tu kwa majibu yake ya kistaarabu bali pia kuchukua muda wake kusoma na kujibu tweets mbalimbali zinazoelekezwa kwake.
Kwa tabia ya kimungu-mtu iliyozoeleka miongoni mwa viongozi wetu wengi wa Kiafrika, ni nadra sana kwa Rais kufanya mawasiliano na wananchi wa kawaida hasa katika mitandao ya jamii.

Yawezekana kabisa kuwa maelezo yake hayajakidhi shauku ya Watanzania wengi kufahamu nani anasema ukweli lakini hiyo haiondoi ukweli kwamba kwa kutumia muda wake adimu kulizungumzia suala hilo ‘katika maongezi yasiyo rasmi’ ni jambo linalostahili pongezi.

Lakini pamoja na majibu hayo mazuri ya Rais, wananchi wengi bado wanatatizwa na mkanganyiko wa kauli za viongozi kuhusu posho za wabunge.

Kuna maswali kadhaa ambayo hayana majibu hadi sasa (licha ya ufafanuzi wa Rais).Hivi inawezekana kweli Waziri Mkuu kuzusha kuwa Rais aliridhia ongezeko hilo la posho? Ukisoma maelezo ya Rais ‘kati ya mistari’ (between the lines) unaweza kuhisi kuwa labda Pinda hakuyaelewa vizuri maelekezo ya ‘bosi’ wake. Lakini kama ukweli ndio huo, kwanini basi Makinda aje na maelezo mapya? Na kwanini Pinda amekuwa kimya hadi leo?

Binafsi ninaona kuwa suala hili linaweza kumalizwa na Rais Kikwete kwa kuwakumbusha wabunge kuwa japo maombi ya nyongeza ya posho zao yanaweza kuwa ya msingi, ukweli ni kwamba hayaendani na hali halisi ya uchumi wetu.

Na majuzi Rais Kikwete ameeleza waziwazi kuwa serikali yake inakabiliwa na hali ngumu kifedha alipozungumza katika maadhimisho ya Siku ya Sheria, ambapo miongoni mwa wageni waalikwa alikuwa Spika Makinda. Je, inawezekana Rais alikuwa anafikisha ujumbe ‘kistaarabu’ kwa Spika?
Wito wa safu hii kwa Rais Kikwete ni mwepesi na mfupi: huko nyuma alishaweka bayana kuwa tabasamu lake lisitafsiriwe vibaya, na urais wake hauna mbia. Kutegemea hekima na busara za wabunge kujadili maslahi yao ni sawa kabisa na kuwasihi mafisadi waionee huruma nchi yetu. Wabunge wanaopiga kelele kutaka nyongeza ya posho wapo ‘out of touch’ na hali halisi ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.
Haiwezekani kuwasihi watumie hekima na busara wakati wameshaonyesha tangu mwanzo kuwa wana uhaba wa vitu hivyo linapokuja suala la posho.

Mwanzoni mwa makala hii nimeandika kuwa wiki iliyopita ilikumbwa na mlolongo wa matukio na hadi muda huu nimeongelea tukio moja tu. Kwa kifupi, matukio mengine yanayoweza kuonyesha kuwa ombwe la uongozi wa taifa letu linazidi kuwa kubwa ni pamoja na habari zilizopatikana kutoka bungeni Dodoma kuwa Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo ‘aligoma’ kujibu swali aliloulizwa na Spika. Kichekesho ni kwamba japo Spika Makinda amejijengea umaarufu kwa kuliendesha Bunge kwa ‘mkono wa chuma’ dhidi ya wabunge wa vyama vya upinzani katika tukio hilo hakuchukua hatua yoyote dhidi ya Waziri Mkulo.

Kana kwamba hiyo haikuwa ‘kali kubwa ya wiki,’ taarifa zinaeleza kuwa wabunge wa CCM waligoma kukutana na Rais Kikwete kuzungumzia muswada wa mabadiliko ya Katiba, ambapo inasemekana wabunge hao wamedhamiria kuikwamisha.

Je, wabunge hao wamegoma kwa sababu wamechukizwa na kauli ya Rais kuwa hajaridhia matakwa yao ya nyongeza ya posho? Taarifa zinaeleza kuwa sababu iliyopeleka hatua hiyo ni mtizamo wa wabunge hao kuwa marekebisho yaliyofanywa kwenye muswada huo yatapelekea CCM kuangushwa na CHADEMA. Pia inaelezwa kuwa wabunge hao hawajapendezwa na kitendo cha Rais kukubaliana na mapendekezo ya CHADEMA katika maboresho ya muswada huo.

Japo sisi tusio wana-CCM hatuna haki ya kuingilia mambo ya ndani ya chama hicho, lakini kwa vile ni chama tawala na chochote kinachokihusu kinamgusa takriban kila Mtanzania, ni muhimu kukemea utovu huo wa nidhamu ambao unaweza kutafsiriwa tu kuwa ni njama za wazi za kumkwaza Rais kuleta mwafaka wa kitaifa utakaosaidia kuiongoza nchi yetu katika njia sahihi.

Nimalizie makala hii kwa kumkumbusha Rais Kikwete kuwa licha ya kuwa Mwenyekiti wa taifa wa CCM yeye ni Rais wa Watanzania wote.

Kamwe asiruhusu maslahi ya waroho na walafi wachache yaathiri maslahi ya Watanzania wote pasipo kuangalia itikadi zao za kisiasa.

Kadhalika, ninawasihi wazalendo wote (bila kujali tofauti zetu) kumuunga mkono Rais Kikwete katika masuala yenye maslahi kwa Watanzania wote hata kama yeye mwenyewe amelea matatizo haya na sasa yanataka kutupeleka kubaya.

Lakini ili Rais aweze kupata sapoti hiyo ni muhimu na yeye aamue ‘liwalo na liwe,’ lakini Tanzania kama nchi ni muhimu kuliko mtu binafsi au kikundi cha walafi wachache.

8 Feb 2012


Habari za kazi Wadau, poleni na majukumu ya ujenzi wa Taifa.
Kufuatia tatizo la kiufundi lililojitokeza hapo nyuma blogu yako ya Mamapipiro ilishindwa kuendelea na utendaji wake, nawaomba radhi wadau wangu wote ambao mlikosa kupata matukio muhimu ya michezo na burudani kwa zaidi ya wiki moja,hivyo kwa sasa mambo yamekaa sawa hivyo endeleleeni kuperuzi blogu yenu kwa habari kem kem za michezo na burudani kupitia www.mamapipiro.blogspot.com.
Natanguliza shukrani zangu za dhati!



Huku mgomo wa madaktari ukiendelea kushika kasi,kuna dalili kwamba walimu nao wanaelekea kuchukua hatua hiyo kutokana na taarifa za magazeti ambapo wamekumbushia kilio chao cha muda mrefu kuhusu maslahi yao.

Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima,toleo la leo Jumatano,walimu wametoa wito kwa serikali kutekeleza matakwa yao ya maboresho ya maslahi huku wakitaja viwango wanavyostahili kulipwa.

Habari kamili ni hii hapa chini

Walimu wawasha moto mpya
• WATAKA MISHAHARA YA 900,000/-
na Datus Boniface

WIMBI la wafanyakazi wa umma kudai nyongeza ya mishahara, posho na marupurupu limechukua sura mpya baada ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kupendekeza viwango vipya vya mishahara wanavyopaswa kulipwa walimu. 
CWT kimesema mwaka wa fedha unaoanza Julai mwaka huu kinataka kuwe na ongezeko la asilimia 100 kwa walimu wote kulingana na viwango vya madaraja yao, ambapo wa Cheti (Daraja A), anatakiwa kulipwa sh laki tano, stashahada alipwe sh laki saba na nusu na yule wa shahada alipwe zaidi ya sh laki tisa. 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, kwa niaba ya Rais wa CWT, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Ezekiah Oluoch, alisema ongezeko hilo linatokana na kupanda kwa gharama za maisha. 
“Tumefanya tathmini na kujiridhisha kuwa mapendekezo yetu yanawezekana, serikali inaweza kutulipa fedha hizo kwa sababu ina rasilimali za kutosha,” alisema. 
Oluoch alisema mapendekezo hayo yametokana na kikao cha Baraza la Taifa la chama hicho lenye wajumbe 163 wanaowakilisha walimu katika mikoa 21, kilichoketi Januari 31 hadi Februari mosi mjini Morogoro. 
Alibainisha kuwa baraza la taifa limeagiza kuwa majadiliano kuhusu nyongeza ya mishahara yaanze mara moja na yawe yamekamilika mwishoni mwa Machi mwaka huu. 
Alisema wanataka majadiliano hayo yafanywe mapema ili serikali iyaingize makubaliano kwenye bajeti yake ya mwaka huu. 
Oluoch alisema CWT inaamini kuwa majadiliano ni njia pekee ya kupata mwafaka wa ongezeko hilo la mishahara. 
Malipo ya posho
CWT inahitaji kulipwa kwa posho za kufundishia na za mazingira magumu kwa walimu hao, kwa kuwa muda wa kazi zao ni tofauti na watumishi wengine wa umma. 
Kinataka walimu wote wapewe posho ya asilimia 55 kwa walimu wa masomo ya Sayansi na asilimia 50 wa Sanaa, na posho hizo zianze kulipwa kuanzia Julai. 
CWT kimesema kuwa nyongeza ya posho hizo si ngeni kwani Rais Jakaya Kikwete aliwapa ahadi hiyo Siku ya Walimu Duniani Oktoba 5, mwaka 2010. 
Olouch alisema posho ya mazingira magumu, inatakiwa kulipwa kwa asilimia 70 kwa mwalimu anayefanya kazi maeneo ya vijijini, kama utekelezaji wa ahadi ya Rais Kikwete aliyoitoa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Walimu Duniani Oktoba 2010. 
Madeni yasiyohusiana na mishahara
CWT kimeitaka serikali kuwalipa walimu fedha zao za madeni yasiyohusiana na mishahara kabla ya Februari 15 na iwapo itashindwa kufanya hivyo, chama hicho kitachukua hatua dhidi ya waajiri waliokaidi makubaliano yaliyofikiwa. 
Oluoch aliongeza kuwa awali walikubaliana na serikali kuhusu utaratibu wa kulipa madeni hayo ambayo walihakiki kwa pamoja, wakishirikiana na viongozi wa serikali wa ngazi za wilaya, ambapo sh bilioni 22.5 zilitumwa kwenye halmashauri za wilaya na sh bilioni 3.5 zilitumwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. 
Alibainisha kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha alitoa waraka ambao umetafsiriwa vibaya na baadhi ya watendaji wa serikali. 
Aliongeza kwamba, baadhi ya watendaji wametafsiri kinyume kuwa ni kuhakiki upya madai ya walimu badala ya kujiridhisha kama anayelipwa ndiye aliyehakikiwa. 
Alisema utata huo umechangia halmashauri 50 kutowalipa fedha walimu licha ya kuzipata fedha hizo. 
Kulipwa madeni ya mishahara
CWT kinataka kufanyike marekebisho yote ya mishahara na malipo ya mapunjo yafanyike ndani ya mwezi huu bila kukosa. 
Oluoch alisema CWT ilifanya kikao na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Simfue Ombeni, Januari 13 mwaka huu na serikali ilitoa taarifa ya kulipwa kwa walimu 18,000 kiasi cha sh bilioni 18. 
Aliongeza kuwa CWT kupitia Baraza lake limesikitishwa na kauli ya serikali ya kukosa fomu hizo huku serikali ikificha ukweli, kwani tatizo linafahamika na kwamba walimu wengi hawajarekebishiwa mishahara yao baada ya kupanda madaraja. 
Chama hicho kimetaka kufutwa kwa waraka wa serikali wa kupunguza zoezi la upandishwaji wa madaraja kwa asilimia 50 kutokana na maelezo kuwa serikali haina pesa. 

Kama nilivyoandika kwenye makala yangu katika toleo la wiki iliyopita la jarida la Raia Mwema,moja ya madhara ya muda mrefu ya mgomo wa madaktari ni kutoa hamasa kwa watumishi wengine wa umma kudai haki zao kwa njia ya mgomo.

Kwa upande mmoja,iwapo serikali itasalimu amri na kutekeleza matakwa ya madaktari,kuna uwezekano mkubwa wa watumishi wa umma katika sekta nyingine nao kudai watendewe haki kama madaktari (iwapo madai ya matabibu hao yatatimizwa na serikali).

Kwa upande mwingine,hata kama madai ya madaktari yataendelea kupuuzwa,umoja na mshikamano wa wataalamu hao wa afya za binadamu unaweza kuwafanya watumishi wengine wa umma kujiuliza mara mbili kwanini nao wasifuate mkumbo.

Hakuna anayetaka kuona migomo ikitawala nchi yetu lakini kwa makusudi kabisa serikali imeonyesha wazi kuwa inathamini zaidi matakwa yasiyo ya lazima ya wabunge kuliko watumishi wengine wa umma ambao licha ya kuwa na mishahara midogo wanakabiliwa na matatizo chungu mbovu,kubwa likiwa uhaba wa vitendea kazi na makazi duni.Ikumbukwe kuwa wabunge wanaolipwa mamilioni kwa kupiga porojo bungeni wanapatiwa kila huduma na mazingira yao ya kazi ni mithili katika nchi zilizoendelea.

Sijui hatma ya harakati hizi za watumishi wa umma kudai haki zao itakuwaje lakini ni muhimu kuikumbusha serikali kwamba kuna tawala kadhaa zilizoanguka kutokana na ngumu ya migomo ya wafanyakazi.

7 Feb 2012



WAFANYAKAZI WA HAZINA, TANESCO NA WIZARA YA NISHATI WAHUSIKA, NGELEJA ATHIBITISHA UCHUNGUZI KUFANYWA
Mwandishi Wetu
SERIKALI inawachunguza baadhi ya maofisa wake waandamizi kwa tuhuma za wizi wa dola50 milioni za Marekani sawa na Sh86 bilioni, zilizotengwa kwa ajili ya ununuzi wa mafuta mazito ya kuzalishia umeme kwa Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), katika kipindi hiki nchi inapokabiliana na tatizo la uhaba wa nishati hiyo.

IPTL inayozalisha megawati 100 za umeme iliingia mkataba na Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco), lakini utendaji wake umekuwa na mkanganyiko.Chanzo kutoka serikalini kililiambia gazeti dada la The East African la Februari 12, kwamba kuna ushahidi wa kutosha kwamba baadhi ya maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Hazina na Tanesco, wanahusika katika mpango huo wa wizi.

Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alipoulizwa alijibu, “Ndiyo naweza kuthibitisha upo uchunguzi unaoendelea, lakini ndiyo kwanza upo katika hatua za awali.” Tayari taarifa za awali za ukaguzi kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), zinaonyesha kumekuwa na maelezo yaliyokiuka utaratibu wa fedha zilizolipwa na Serikali kwa ajili ya usambazaji wa mafuta mazito kutoka kampuni za ndani.

Ukosefu wa nishati ya umeme unaoikabili nchi kwa sasa unaifanya Tanesco kulipa IPTL dola12 milioni za Marekani sawa na Sh19.2 bilioni kila mwezi, kwa uzalishaji wa megawati 60 badala ya megawati 100.

Mwaka 1995, Tanesco iliingia mkataba na IPTL, mkataba ambao uliihusisha kampuni ya nchini Malaysia , Mechmar Corporation na wawekezaji wa ndani, na VIP Engineering and Marketing Company kwa ajili ya kuzalisha megawati 100 kwa kutumia mitambo inayotumia dizeli kwa miaka 20.Katika mkataba huo, VIP ina hisa ya asilimia 30 na ile ya Mechmar ya Malaysia ikiwa na hisa ya asilimia 70.Serikali ilikubali kulipa kwa ajili ya uzalishaji huo kwa kuwa haikuwa na njia nyingine.

Mpango wa kuifilisi IPTLTayari hivi karibuni Mahakama iliamua IPTL ifiilisiwe na jukumu hilo lilikabidhiwa kwa Wakala wa Ufilisi, Vizazi na Vifo (Rita).Hata hivyo, baadhi ya benki zinazoidai IPTL ziliweka zuio mahakamani zikitaka kwanza kulipwa fedha zao ambazo kampuni hiyo ilikopa.IPTL inakadiriwa kuwa na Sh200 bilioni zilizopo Benki Kuu (BoT) ambazo kama ikifilisiwa zingeangukia mikononi mwa Serikali. Kampuni hiyo imekuwa ikiitafuna Tanesco mabilioni ya shilingi tangu kuingia mkataba huo ambao umekuwa ukitajwa kama wa kifisadi, kuliko hata wa Richmond.


Wakati fedha za umma zikitafunwa bila huruma,mgomo wa madaktari unaoendelea kwa siku kadhaa sasa umeingia katika hatua mpya baada ya madaktari bingwa nao kujiunga na mgomo huo,kama inavyoripotiwa hapa chini:

Geofrey Nyang’oro na Florence Majani
WAKATI Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii ikianza kazi ya kuzungumza na madaktari walio kwenye mgomo, madaktari bingwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na walio katika Taasisi ya Mifupa (MOI) wamegoma. Mgomo huo wa jana ulihusisha vitengo vyote huku wagonjwa waliokuwa wamelazwa hospitalini hapo wakipewa taarifa za kuondoka katika wodi walimolazwa.

Azimio la mgomo huo lilifikiwa katika kikao cha dharura kilichoitishwa na jopo la madaktari bingwa wakiongozwa na Dk James Rwehabura ambaye ni daktari bingwa wa Kitengo cha Uchunguzi wa Magonjwa ya Binadamu.

Habari za ndani kutoka katika kikao cha dharura cha wanataaluma hao, zilisema uamuzi huo ulifikiwa kwenye kikao cha madaktari hao kilichoanza mapema asubuhi jana na kumalizika saa 6:00 mchana. “Kwa pamoja tumekubaliana kuweka vifaa chini, hii ni kutokana na ukweli kuwa hali ya utoaji huduma katika hospitali hii ni mbaya huku taarifa za Serikali zikiwa siyo za kweli,” alidokeza mmoja wa madaktari bingwa.

Daktari huyo aliyekataa kutaja jina lake, alisema, “Tumekubaliana kugoma hadi hapo Serikali itakapotoa majibu ya madai yote yaliyowasilishwa na jumuiya ya madaktari inayoongozwa na Dk Stephen Ulimboka kwa Serikali.” Jumuiya hiyo iliwasilisha madai mbalimbali likiwamo la kuitaka Serikali kupeleka vifaa na dawa katika hospitali za Serikali ili madaktari hao waweze kutoa huduma bora kwa jamii.

Pia, madaktari hao walitaka kusitisha safari za vigogo kwenda kutibiwa nje kwa magonjwa yanayotibika ndani kwa kile walichodai, hali hiyo inachangia wao kudharauliwa na pia kuzorotesha jitihada za Serikali katika uboreshaji wa mazingira ya kazi kwa madaktari hao.

Kwa nyakati tofauti, madaktari hao walibainisha sababu ya mgomo wao na kudai kuwa, kikubwa ni mazingira magumu ya kazi. Daktari mwingine ambaye hakupenda jina lake kuandikwa gazetini alisema, licha ya mishahara na posho ndogo, lakini mazingira ya kufanyia kazi yamekuwa magumu mno.

“Tumeshaamua , ‘tools down’ hospitali haina kitu, hata ‘mask’ hakuna badala yake tunavaa gozi tunapofanya upasuaji, acha hiyo, hata nyuzi za kushonea wakati wa upasuaji hakuna,” alisema daktari huyo. Daktari huyo alisema, hawawezi kufanya kazi katika mazingira hayo kwa sababu yatawasababisha kuwa na utendaji mbovu na baadaye taifa kuwalalamikia.

Alisema hapa nchini madaktari bingwa ni wachache, kwa hiyo kitendo cha wao kufanya kazi peke yao bila wasaidizi, yaani madaktari wa mafunzo na wale wanaomaliza, wanaelemewa na mzigo wa kazi. Dk Henry Mwakyoma, Mhadhiri Mkuu wa Chuo cha Udaktari Muhimbili, (MUHAS) ambaye hakuwapo katika kikao hicho cha dharura alidai kuwa, yeye kama mhadhiri hajagoma, lakini alikiri kuwapo kwa mazingira magumu ya kazi.

“Mpaka sasa hatujalipwa mishahara ya mwezi uliopita, halafu kazi yetu ndiyo kama hii tunatakiwa tufanye utafiti, unategemea tutafanya kazi kwa umakini kweli? Tutawafundisha madaktari kwa umakini?” alihoji Dk Mwakyoma.

Mwakyoma alisema, Serikali haiwezi kudai kuwa haina fedha za kutosha wakati imetumia mamilioni ya shilingi katika sherehe za miaka 50 ya Uhuru na uchaguzi wa Igunga. Alisema ni vyema Serikali ikajipanga na kuamua kushughulikia masuala ya madaktari kwa hekima kwani kukaa kimya bila kutoa suluhu ni sawa na kufanya ushindani usio na maana.

Hata hivyo, Ofisa Habari Mwandamizi wa MNH Aminael Aligaesha alisema jana jambo hilo lilikuwa likishughulikiwa kwani vipo vikao vinavyoendelea.

Wagonjwa watimuliwa wodini
Wodi mbalimbali hospitalini hapo zilitawaliwa na vilio kutokana na wagonjwa na ndugu za wagonjwa kupewa taarifa za kuondoka katika eneo hilo mara moja, kutokana na mgomo huo wa madaktari. Mmoja wa wagonjwa waliokuwa wamelazwa katika wodi ya Sewahaji, Sadick Dimoso (35) mkazi wa Morogoro alisema hali sasa MNH ni mbaya.

“Tumeambiwa tuondoke wodini bila ya kuruhusiwa na daktari, hii ni hatari tena wanasema tuondoke tukakae huku hadi wiki mbili ndio turudi kuangalia,” alisema Amina Ramadhani, aliyekuwa akisubiri kufanyiwa upasuaji wa jicho. Alisema hatua ya kutakiwa kuondoka hospitalini hapo imekatisha matarajio yao ya kuendelea kuwa hai na kuitaka Serikali kufanyia kazi madai ya madaktari.

Wakati kundi la watu wengine wakililia huduma hosptalini hapo, baadhi ya ndugu za wagonjwa waliingia katika mgogoro na walinzi wa wodi hiyo ya Sewahaji wakitaka waandishi wa habari kuingia wodini.

Vikao vya Kamati Wakati hayo yakijiri, vikao baina ya madaktari na Kamati ya Kudumu ya Huduma za Bunge, viliendelea jana katika ofisi ndogo za Bunge huku taarifa zake zikiwa ni siri.

CHANZO (Habari zote mbili): Mwananchi

6 Feb 2012


Kwa hisani ya King Kinya na Globalpublishers

5 Feb 2012

Viongozi wa Chadema jana tarehe 4 Februari 2012 wamekutana na kufanya Mazungumzo na Watanzania wanaoishi Washington DC . Katika msafara huo ambao umeongozwa na Mwenyekiti wa Chadema Mheshimiwa Freeman Mbowe na Mbunge wa Nyamagana na Waziri kivuli wa Mambo ya nje Mheshimiwa Ezekiel Wenje, wameongelea mambo mbalimbali ikiwemo suala la Mipango ya Maendeleo ya Chama na Mikakati ya kujiandaa na chaguzi zijazo hususani uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Hali kadhalika wakazi hao wa Washington DC wametumia fursa hiyo kumuuliza maswali mbalimbali hususani suala la upatikanaji wa Katiba mpya. Akichangia katika mjadala huo Prof N. Boazi amewakumbusha viongozi hao umuhimu wa kuwa na katiba mpya ambayo itampunguzia madaraka Rais tofauti na sasa inayompa Rais  madaraka  makubwa na kunyima fursa kwa wengine.


Pia wakazi wa Washington DC walimuuliza Mheshimiwa Freeman Mbowe kuhusu suala la mgomo wa madaktari unaoendelea. Akijibu suala hili Mheshimiwa mbowe amesema kuwa alipata nafasi ya kuwasiliana na Viongozi wa mgomo huo lakini walimjibu kwamba hawataki kulifanya suala hilo la Mgomo kuonekana la kisiasa kwa kuwahusisha Chadema.



Mheshimiwa Freeman Mbowe akiwahudubia Watanzania wanaoishi  Washington DC jana jumamosi Feb, 4 2011 Nchini Marekani




 Wakazi wa Washington DC wakimsikiliza Mheshimiwa Freeman Mbowe kwa makini katika mkutano huo.




Mbunge wa Nyamagana na Waziri kivuli wa Mambo ya nje Mheshimiwa Ezekiel Wenje akiongea katika mkutano huo.


Baada ya Mheshimiwa Freeman Mbowe na  Ezekiel Wenje kuongea,  Watanzania waliohudhuria walipata nafasi ya kuliza masuali, na  moja ya maswali aliyoulizwa Mhe Freeman Mbowe ni ile dhana kuwa CHADEMA ni "chama cha waChagga na matajiri". Hapa chini anafafanua dhana zote hizo na ile aliyosema iliwahi kusambaa kuwa ni "chama cha waKristo"


CHANZO: Swahilivilla. Shukrani pia kwa Mzee wa Changamoto Mubelwa Bandio kwa kunitumia kiungo (link)

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-lIy1arJHtwAUTAAj5pOBqt-fJFyaFbH5QMz-50TlnSJbLEk7sR2ONFVoQytRS_UBiVfjczZvIR4a5VyH321UkXGZi4r_644-GuOTqRFLnxn7vcDRhE4fKimVTbaI7JDm4-ULsw/+wa+Wilaya+ya+Ilala%2C+Leonidas+Gama+(kushoto)%2C+akipokea+hundi+ya+Sh.+milioni+moja+na+nusu+kutoka+kwa+Grace+Nicolaus..jpg
Angalia kitambi kilivyoshamiri.Huyu ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh-0e9SqWdmkDfeh9Unt4ndaXf71EE_pmX3GZf_4zX1c0K8l1FfiKYKCmPJsWL_RwnAREpAhlNfEO-BxSuYJrSc5Wtwe6-lBVHDMgdpRcxP-y0KLNzscgaRmVOw0jTRPKoxbcmsOg/s1600/IMG_0417.JPG
VITAMBI OYEE: Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama

http://tanzagiza.com/wp-content/uploads/2011/08/john-komba.jpg
HOI KWA USINGIZI: Mheshimiwa John Komba akitafakari matatizo ya wapigakura wake jimboni Mbinga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjS6w1opIlZQhvRN-h2R8nPQPNzTAacUQHaDXT5Fy6phNV-TIjHi92s-z7Ff4wBO6zIaR12thqkPgZYJmM5YW1drqiHxvqQ4UR20rUzo2u8MHY1DH4g44I0Nnjw3A7oBFydpo_afg/s400/DSC_9178.JPG
Kwanini Kapteni Komba aache kuimba kuisifia CCM iliyomwezesha kuwa na kitambi kikubwa namna hiyo?

http://www.jukwaahuru.com/wp-content/uploads/2011/08/PICS-PG-16-300x280.jpg
KITAMBI: Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Didas Masaburi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjBwff1VFHJvt37MimPFWZNHfhc-aGo49Fj7Y_MPN6QQZarjzVLkhIZJeU7-DvZA7r562QdNX8Yv9wkBh4OdalzIk_9x52BPvoJIDFhOKSif5rSnhZbHOh-E864nwA2tY5tKvL7pA/s320/wassira.jpg
Mtu mzima hovyoo!!!
MHESHIMIWA SAMUEL SITTA: Kamanda wa jeshi la kupambana na mafisadi azidiwa nguvu na usingizi
Mzee wa Kiraracha  AGUSTINE MREMA akibuni mbinu za kuipeleka TLP Ikulu

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnxlmjR8JGjkjkFfAfmXhoszH28cc9C3cgHoOgTfy8irC2sc64A20-PleV-a2f1mHT7WmUk2AhgI0wV9sPATZUy8CmTM_lR5sMPGUPK6Yt-oK7HEtVzcpDx1AZUIcw7W5JfZCl/s400/VitiMaalum-Bungeni_kusinzia-1.jpg
Mbunge anaota posho usingizini

Usalama wa nchi nao ukiwa usingizini.

Waziri Ngeleja akiwajibika kwa kuuchapa usingizi bila kumhofia bosi wake hpo pembeni

Maji hufuata mkondo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhee4SIQj0eDwHu4WbdKbCUfByf6Dtvz89R6e1ZgSQclRw1M3WkiqXVQGbGs9gPqd3dKRJwG91cOHIYj5jf5ZhbYZW2NdKLUp6ZWyGapQJQn5DyP4Q-mISpbhyphenhyphenT3d7o8rX2DTlW/s1600/Wanafunzi+wa+shule+ya+Msingi+Mvumi+-Kilosa+(13).JPG
Watoto wanaketi chini hakuna madawati msitu wa Songea na Mafinga Sao Hill akina Lukuvi wamejipigia ufisadi ambapo serikali ingetengeneza masawati ya kutosha nchi nzima,

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgshMqh7qbevYkWEQb9ioGHTD29lpZRq-WYNBHkl3u_LdFQZNQSr3QpHQsNAMjbkRW11Zsf8QdRZNLLXXuibZ_HCNut38gYWhQ02ySZjgvpWDO4cM65_5e1jSohijFBHZKgzsRhHQ/s1600/shule2.jpg
Watoto wakitoka 'darasani' huku wamenyong'onyea

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg2v8GzJvD6NRruhmkVK3cYW89lFhdTPZ1GCv8NO56HuJdDJXF6wa0-qUTnlnoWlCF788rFssSMfwa1hpn81aPeIPAfq4f5TS47uafr4onzzlcWmq5fQAeGKnTfwqTNO0MWQA0E/s400/Shule2.jpg
Shule ya msingi ambamo wanasoma watoto wa wapiga kura

http://www.wavuti.com/uploads/3/0/7/6/3076464/1156230.jpg?518
Hata kwenye shule za sekondari nako hali mbaya

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxBLkaa0_5fe5AtKh-XD-NmsvlUYHID6Tob_RuCV2Y1jfTBeySY-zZHm-pKflpnwaIi80F6G6Xjnvh82OkeOE6HKJB9mD_68aJznTUgYiSUHEcrW6yKzo9LASKc5byoyxGs_1X/s1600/zahanati_ya_kijiji_kisaki,bwakila_morogoro%5B1%5D.jpg
Hii ni zahanati mpiga kura ndo analalia kitanda hicho wao Muhimbili wanaenda kupumnzika kisha hao India

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijl9W9ZlS8r3PJuEpsjNsqBZW20ojOQS6YMOPIQWCgoa1Wfxs8en6wGzGBmK2cLvuidOLHkv0nh-cWeEb5PZOkMwjfskG8hgV6_lAJ7-NfZ3qlzOtWX00xFolgcjeELTGR3oGmJA/s1600/NESI+ZAHANATI+YA+MAKUYU..JPG
Hii ndo maabara ambapo mpiga kura anakuja kupimwa maradhi yake

http://cache.daylife.com/imageserve/0b2n8dk6Uq6cL/610x.jpg
Wapiga kura wanalala mzungu wa nne kitanda kikiwa full mpiga kura inamlazim adondoshe gari sakafuni anamwachia matumaini Mungu

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhEks1CWqCmVykujhKv0gxqK9TBS2NWAUbF49uDKsE8ikYlFlToma6dE0KV0pEHlH5Jw7S4o4BtutPqgDuxaKbVWlCPu6xr3dc40-WX_sR5aKy3mu1OrqjZnDXGHh0TUsdl1GOCHw/s1600/Upungufu+wa+vitanda+vya+kulala+hospitali+ya+Mwananyamala+7+Oktoba+2008%5B1%5D.JPG
Wapiga kura hawa wasio thaminiwa wakiwa wamerundikana kama wanyama wanapatiwa matibabu

http://www.wavuti.com/uploads/3/0/7/6/3076464/191125944.jpg?665
maji anayo tumia mpiga kura kwa kunywa na kupikia na kufulia 

http://www.wavuti.com/uploads/3/0/7/6/3076464/5235999.jpg?648
Mpiga kura wa hao jamaa walio vimbiana matumbo akikata kiu kwa maji kumbuka hayo maji kayafuata kwa kutembea zaidi kilomita 20.

SHUKRANI KWA NANA KANZAGA WA COVENTRY (UK) KWA PICHA




Mpendwa Chama Cha Mapinduzi (CCM),

Heri kwa siku yako ya kuzaliwa.Nakupongeza sana kwa kutimiza miaka 35.Laiti ungekuwa mwanadamu basi kwa umri huo huenda ungekuwa na mke na mtoto/watoto.Anyway,familia yako ni sie Watanzania ambao wakati unazaliwa (1977) hatukuwa na hiari zaidi ya kukuunga mkono na kukuabudu.

Mpendwa CCM,kinachofanya ionekane unachukiwa na wengi si wewe kama chama bali wengi wa viongozi wako.Kama ilivyokuwa kwa watangulizi wako TANU na ASP,ulipozaliwa ulidhamiria kupigania haki za wanyonge,kupambana na ukandamizaji na kujenga jamii iliyo sawa.Ulifanikiwa sana katika kipindi cha utawala wa Marehemu Baba wa Taifa Julius Nyerere.Lakini pindi alipotoka madarakani zikaanza jitihada za makusudi za kukugeuza kimbilio la maharamia wa kisiasa.

Alipofariki Mwalimu,maharamia hao wakakubadilisha kabisa na sasa unaonekana kama kichaka cha mafisadi.Zama za Mwalimu,ulikuwa mfano wa kuigwa si kwenye siasa tu bali hata katika ngazi ya familia.Uliwajali Watanzania japo baadhi ya sera zako hazikuweza kufanikiwa kwa utimilifu (hususan Ujamaa na Kujitegemea).Kilichokukwamisha zaidi ni maharamia waliojivika ngozi ya kondoo ilhali wao ni mbwa mwitu.Watu walewale waliokuwa wakihubiri usawa na kuwatetea wanyonge leo hii wamegeuka watetezi wakubwa wa mabwanyeye,makabaila na wanyonyaji wengine ambao siku hizi tunawaita mafisadi.

CCM umeporwa na walafi wasio na uchungu na nchi yetu.Wafanyabiashara wa kila aina (pamoja na wenye biashara haramu) wamekimbilia kwako si kwa vile wanakupenda bali wanasaka hifadhi ya kuendeleza uharamia wao.

Kabla ya mwasisi wako kufariki alitabiri uwezekano wa kupata mrithi wako kutokana nawe.Kwa mazingira tuliyonayo hilo ni vigumu kutokea kwani kwa kiasi kikubwa hakuna wa nafuu miongoni mwa vionhozi wako.Na siku yako ya kuzaliwa imeadhimishwa kwa kituko cha wabunge waliopatikana kwa kutumia tiketi yako kugoma kukutana na Mwenyekiti wao.Sijui kama ni hasira za sakata la posho wanazotaka waongezewe au wanachochewa na 'nguvu za giza' zinazotaka Mwenyekiti Kikwete asimalize muhula wake wa pili,au amalize kwa fedheha.

Anyway,natamani ningekuwa na muda wa kutosha kuwasilisha salamu hizi lakini naomba niishie hapa.Afterall,today's your big day na pengine sikutendei haki kwa kujumuisha masimango.

Enjoy your big day dude!

Truly yours,

Evarist Chahali


WAJIPANGA KUKWAMISHA MUSWADA  MABADILIKO YA KATIBA
Midraji Ibrahim, Dodoma
SASA ni dhahiri kuwa wigo wa mpasuko kati ya wabunge wa CCM na Serikali unazidi kupanuka, baada ya wabunge hao kugoma kukutana na Rais Jakaya Kikwete mjini Dodoma.Katika kikao chao kilichofanyika Ijumaa usiku ukumbi wa Pius Msekwa mjini hapa, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliwaomba wabunge hao kukutana na Rais Kikwete ili kuwasilisha malalamiko yao dhidi ya Serikali badala ya kuendelea kuikwamisha bungeni.Wabunge hao wanadaiwa kukataa rai hiyo huku wakimweleza waziwazi Pinda kwamba, itakuwa ni kumkosea heshima na adabu Rais, iwapo watakutana naye halafu wakwamishe marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inayotarajiwa kufikishwa bungeni wiki ijayo.

“Itakuwa siyo heshima kukutana na Rais halafu tukwamishe muswada wa marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, kwa sababu tumejipanga kuhakikisha kwamba haupiti,” vilieleza vyanzo vyetu vya uhakika kutoka ndani ya kikao hicho.

Badala yake, wabunge hao walikubali kuteua miongoni mwao watu watano ambao wataonana na Rais Kikwete leo atakapowasili mjini hapa akitokea Mwanza kwenye Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 34 ya CCM.

Wazungumzaji wakuu kwenye kikao hicho wanadaiwa walikuwa pamoja na,  Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na Mbunge wa Shinyanga, Steven Masele.
 
Marekebisho hayo yalitarajiwa kuwasilishwa kesho, lakini walikataa hadi Ijumaa kwa kile walichodai kuwa, wengi wao watakuwa hawajarejea kutoka Mwanza  kwenye sherehe za maadhimisho ya CCM.

Inadaiwa na wabunge hao wa CCM kuwa, marekebisho hayo yanalenga kukimaliza chama hicho na kukiweka madarakani Chadema baada ya kuondolewa kwa wakuu wa wilaya, kushiriki mchakato wa katiba na kazi hiyo kukabidhiwa wakurugenzi wa halmashauri.

“Hii ni dhahiri kuwa marekebisho haya yanaiumiza CCM na kuisimika Chadema madarakani. Kuwaondoa Ma-DC kwenye mchakato wa katiba na kuweka wakurugenzi wa wilaya ambao wote ni Chadema, hatuwezi kukubali kamwe,” kilieleza chanzo chetu.
Pia, inadaiwa na wabunge hao kuwa marekebisho waliyopewa Dar es Salaam kwenye kamati, ni tofauti na yale yaliyowasilishwa bungeni, huku kukiwa na ongezeko la kurasa nne.

Hata hivyo, inadaiwa baada ya wabunge hao kugoma kukutana na Rais Kikwete, alisimama Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Stephen Wasira, akiwataka kupitisha marekebisho hayo kwa sababu ni agizo la Rais, hali iliyosababisha azomewe huku akitupiwa maneno ya kashfa.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge hao ambao hawakupenda kutajwa majina yao, walisema athari wanayoiona mbele kwa kutopitishwa kwa marekebisho hayo, Chadema watapeleka mashtaka kwa umma kwamba sheria ile ilipitishwa kulinda CCM, hivyo haina manufaa kwa umma.

“Lakini CCM hatujajipanga, kila siku anayesimama jukwaani anazungumzia kujivua gamba, kwa hali hii tusubiri mashambulizi mazito siyo tu kutoka kwa Chadema hata nchi za nje,” kilieleza chanzo chetu.

Pia, wabunge hao wa CCM wanadai kuwa miongoni mwa sababu za kukwamisha marekebisho hayo, ni kile walichodai Rais Kikwete kuwadharau kutokana na wao kupitisha muswada wa sheria hiyo, halafu yeye (Kikwete) anakutana na Chadema dakika chache na kukubaliana na hoja zao.

“Sisi tumekaa hapa (bungeni) kwa zaidi siku mbili na akili zetu timamu, tukapitisha muswada ule, anakutana (Kikwete) na Chadema dakika chache anatuletea marekebisho! Hiyo ni dharau na hatuwezi kukubali,” alilalamika mbunge mmoja.

Kura ya kukosa imani na Rais
Katika kikao cha wabunge hao kilichofanyika Alhamisi wiki hii, baadhi yao walihoji sababu zinazokwamisha masuala mbalimbali serikalini kutopatiwa ufumbuzi, huku Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo, akipendekeza kwamba kama tatizo ni Rais Kikwete, watumie utaratibu wa kumpigia kura ya kutokuwa na imani.

Shelukindo anadaiwa alitaka kujua sababu za masuala mbalimbali kukwama na kutopatiwa ufumbuzi wa haraka na kwamba, iwapo tatizo ni Rais Kikwete, wapo tayari kufuata utaratibu wa kumpigia kura ya kutokuwa na imani.

Hata hivyo, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Olle Sendeka, alisimama na kumtaka mbunge huyo kufuta kauli yake, suala ambalo Shelukindo alikubali.

Pia, katika kikao hicho kiliwataka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda, Naibu wake, Dk Lucy Nkya na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni, kujiuzulu kutokana na kuwa chanzo cha mgomo wa madaktari.

Katika kile kinachoonyesha mpasuko huo kuchukua sura mpya, wabunge hao wamekuwa wakikwamisha miswada ya Serikali, suala ambalo siku zilizopita walikuwa wakiipitisha hata pale yanapokuwepo malalamiko kutokana kwa wananchi, kwa kile kilichokuwa kikielezwa kuwa ni ‘msimamo wa chama.’

CHANZO: Mwananchi

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.