25 Feb 2012

24 Feb 2012

First Man of Finland caught gawping at Danish princess's breasts

The husband of Finland's president was caught on camera casting an admiring glance at the cleavage of Princess Mary of Denmark.






Pentti Arajarvi, Finland's "first gentleman", cast a glance as he sat next to the princess during a state dinner hosted by her mother-in-law, Queen Margrethe of Denmark.
As all eyes turned towards one of the evening's many speeches, Mr Arajavi's roamed down the neckline of the 43-year-old princess.
When she turned to face him, his gaze jerked upward and for a few awkward moments he pretended to be admiring the ceiling of the Amalienborg Palace in Copenhagen.
An alarmed Princess Mary raised a protective hand over her neckline as Mr Arajavi, 63, continued to squint upwards.
The incident provoked a scathing reaction in the Danish press and is unlikely to do much for the country's relationship with neighbouring Finland, which is governed by Mr Arajavi's wife, Tarja Halonen.
It carries echoes of the 2009 G8 summit in Italy when Nicolas Sarkozy was accused of leering at the figure of a shapely Brazilian woman.


SOURCE: Daily Telegraph

23 Feb 2012


Tamko la Mbunge wa Ubungo kupitia Chadema,Mheshimiwa John Mnyika kuhusu tatizo za upatikanaji wa maji jijini Dares Salaam na ubabaishaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasco):


THURSDAY, FEBRUARY 23, 2012


DAWASCO imekiuka mikataba; hatua za haraka zinahitajika kuboresha upatikanaji wa maji DSM

Kampuni ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) imekiuka mikataba miwili muhimu inayoongoza kazi zake na kusababisha matatizo ya maji katika Jiji la Dar es Salaam ikiwemo maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo.


Imenibidi nitoe taarifa hii kwa umma kwa nilitumia taratibu za kawaida za kiofisi tarehe 14 Februari 2012 kuiandikia barua DAWASCO kuchukua hatua kuhusu tatizo la kutozingatiwa kwa ratiba ya mgawo wa maji katika Jiji la Dar es salaam hali ambayo imesababisha kero ya maji katika maeneo mbalimbali ya jimbo la Ubungo.


Hata hivyo DAWASCO haikujibu barua husika kueleza hatua ambazo imechukua, hivyo natoa mwito wa wazi wa siku tatu kwa DAWASCO kufanya ukaguzi wa mtandao wa maji na kurekebisha kasoro zilizopo na kutoa taarifa kwa umma kuhusu matitizo ya maji yanayoendelea katika maeneo mengi ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo. 


Kazi ya mbunge kwa mujibu wa katiba ni kuwawakilisha wananchi, kutunga sheria na kuisimamia serikali hivyo nakusudia kuchukua hatua zaidi za kibunge dhidi ya DAWASCO iwapo haitazingatia masharti ya mikataba husika na kushughulikia matatizo ya maji yanayoendelea hivi sasa katika jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo.


Ikumbukwe kuwa DAWASCO ni shirika la umma lililoundwa kwa tangazo la Serikali nambari 139 la tarehe 20 Mei 2005 kwa mujibu wa Sheria ya Mashirika ya Umma ya mwaka 1992.


Tarehe 1 Julai 2005 DAWASCO ilipewa mkataba wa ukodishaji (lease agreement) na DAWASA ambao unaitaka DAWASCO kuendesha miundombinu ya maji na kuhakikisha matengenezo ya mtandao wa maji katika jiji la Dar es salaam.


Aidha, katika kutekeleza mkataba huo DAWASCO inapaswa kuzingatia mkataba wa huduma kwa wateja (Client Service Charter) ambao unaitaka DAWASCO kushughulikia kwa muda maalum malalamiko ya wateja na kutoa taarifa kwa umma kila panapokuwa na matatizo ya maji.


Kwa mujibu wa mkataba wa huduma kwa wateja DAWASCO inapaswa kushughulia malalamiko ya wateja na kuyajibu ndani ya siku tano na iwapo matatizo yaliyopo yanahitaji hatua za kiufundi; DAWASCO inatakiwa kushughulikia matatizo hayo ndani ya siku 30.


Kuanzia mwishoni mwa mwezi Disemba 2011 mara baada ya maafa ya mafuriko katika Mkoa wa Dar es salaam mpaka leo tarehe 22 Februari 2012 nimepokea malalamiko mbalimbali toka kwa wananchi kuwa hali ya upatikanaji wa maji katika kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo sio nzuri kama ilivyokuwa baada ya hatua ambazo tulichukua kwa nyakati mbalimbali kuanzia Januari 2011 mpaka Septemba 2011.


Itakumbukwa kwamba tarehe 5 mwezi Septemba 2011 nilifanya maandamano ya kwenda DAWASCO nikiwa na wawakilishi wa wananchi wa kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo ambapo tulifanya mkutano na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO. 


Kufuatia mkutano huo DAWASCO ilichukua hatua mbalimbali ambazo ziliboresha mgawo wa maji katika maeneo kadhaa ya Jimbo la Ubungo kabla ya ratiba ya mgawo kuvurugika kufuatia mafuriko yaliyokumba mkoa wa Dar es salaam.


Hata hivyo, baada ya mafuriko hayo DAWASCO haikuchukua hatua zinazostahili kwa wakati na kuachia kurejea tena kwa mtandao haramu wa biashara ya maji wenye kuhujumu wananchi hususan wa kipato cha chini katika Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Ubungo.


Hivyo, bodi ya wakurugenzi ya DAWASCO chini ya uenyekiti wa Mhandisi Suleiman Said Suleiman na Mtendaji Mkuu wa kampuni Jackson Midala wanapaswa kurekebisha kwa haraka mfumo mzima wa ufuatiliaji wa DAWASCO kuwezesha ukaguzi wa ufanisi wa mtandao mzima wa maji.


Katika kipindi hiki cha matatizo makubwa ya maji katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katika kata mbalimbali za Jimbo la Ubungo DAWASCO iache kuwatumia wafanyakazi wanaohusika na ukaguzi kufanya kazi tofauti za kusoma mita na kugawa Ankara badala yake wafanyakazi tajwa wafanye ufuatiliaji wa dharura wa ufanisi wa mtandao mzima wa maji katika maeneo mbalimbali.


Baadhi ya maeneo ambayo yanapaswa kutembelewa ni kata za Makuburi, Kimara, Saranga, Mbezi Luis, Msigani, Kwembe, Goba, Kibamba, Sinza, Makurumla, Mabibo, Manzese, Ubungo na Mburahati. 


Kwa upande mwingine, kwa kuwa mkataba wa huduma kwa wateja unatoa haki kwa wateja wa DAWASCO lakini pia unaeleza wajibu; natoa mwito kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam kutimiza wajibu wa kuwaelekeza wakaguzi husika mitaa yenye matatizo katika mtandao wa maji ili hatua ziweze kuchukuliwa.


Mkataba huo unawataka wateja wa DAWASCO kutoa taarifa kuhusu uharibifu wa miundombinu, wizi wa maji na kuhusu matatizo ya maji hivyo wananchi watoe taarifa husika na kufuatilia wakaguzi kufika maeneo yao kwa kupiga nambari ya bure 0225500240 au 0762979627 za DAWASCO makao makuu.


Pia, wananchi wanaweza kuwasilisha kero za maji kwa ofisi ya DAWASCO zilizo katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam na kupitia nambari zifuatazo: Temeke +255 775016184, Ilala +255 775048556, Magomeni +255 775016179, Boko/Tegeta +255 775048553, Tabata +255 775016181, Kawe +255 775016185, Kinondoni +255 775016180 na Kimara +255 775048554. 


Wananchi watumie pia nafasi hii kuwasilisha kwa DAWASCO maelezo na vielelezo kuhusu maeneo ambayo hakuna miundombinu ya maji kabisa au miundombinu iliyopo haijawahi kutoa maji kwa kipindi kirefu kwa ajili ya kutaka hatua za ziada. 


Matatizo ya maji katika maeneo mengi ya jiji la Dar es salaam ikiwemo katika Jimbo la Ubungo yamedumu kwa miaka mingi, wananchi wametupa wajibu wa kuwawakilisha kuisimamia serikali na mamlaka zake kupunguza kero husika kwa haraka hivyo wananchi watarajie vitendo zaidi vya kushinikiza uwajibikaji kwenye sekta ya maji katika kipindi cha karibuni.


Imetolewa tarehe 22 Februari 2011 na:


John Mnyika (Mb) 


DCI Manumba amewasiliana na Wizara ya Afya ya nchi gani?

Sumu ya Dk. Mwakyembe
Mwakyembe, Sitta wajiuzulu kutumikia Serikali wanayoituhumu
MIONGONI mwa matukio ya kukumbukwa ya Bunge lililokuwa chini ya Spika wa zamani, Samuel Sitta ni tuhuma kwamba mmoja wa wabunge alifanya vitendo vya ushirikina.
Japo suala hilo lilimalizwa kimya kimya, ukweli unabaki kuwa lilikuwa ni la kuaibisha na pengine kudhihirisha upungufu mkubwa kwa baadhi ya watu tuliowakabidhi jukumu la kutuongoza.
Na kama ilivyozoeleka kwenye masuala mengi yenye utata, Watanzania hawakuwa na jinsi ya kudai ukweli kuhusu suala hilo. Kwa upande mmoja huwezi kuwalaumu hasa ikizingatiwa kuwa, wengi wao wanahangaika tangu mawio hadi machweo kuhakikisha ‘mkono unakwenda kinywani.’ Kwa upande mwingine, watawala wetu wamejitengenezea mazingira ambayo mwananchi wa kawaida hawawezi kudadisi ‘upuuzi’ wao (kama huo wa madai ya ushirikina bungeni).
Lakini pengine kikubwa zaidi ni ukweli kwamba kama hadi leo hii watawala wetu wamegoma kabisa kutuambia kuhusu wahusika wakuu wa ujambazi wa mchana kweupe (daylight robbery) katika skandali za EPA (hasa nani anayemiliki kampuni iliyoiba fedha nyingi ya Kagoda), Richmond, Meremeta, Tangold na nyinginezo, basi ni dhahiri hawakuona haja ya kujihangaisha na ‘jambo dogo’ kama hilo la tuhuma za ushirikina bungeni .
Busara zinatukumbusha kuwa ‘usipoziba ufa utajenga ukuta.’ Tabia ya kuyapuuza masuala yanayopaswa kushughulikiwa ipasavyo sasa imeanza kuzua sokomoko mpya ambayo imeendelea kutawala vichwa vya habari kwa siku kadhaa sasa. Ninazungumzia sakata linalowahusu Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kwa upande mmoja, na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Robert Manumba, kwa upande mwingine.
Unaweza kulipanua sakata hilo na kumjumuisha Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta (ambaye amejitokeza kuwa mtetezi mkuu wa Mwakyembe) na Jeshi zima la Polisi chini ya uongozi wa IGP, Said Mwema.
Tuhuma kwamba Mwakyembe amenyweshwa sumu zilianza kama mzaha. Kadri siku zilivyozidi kwenda, suala hilo lilianza kupata uzito hasa baada ya tamko la wazi lililodai kwamba Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa na mpango wa kumuua.
Sijui nchi yetu imefika mahali gani kiasi naibu waziri na mbunge anaituhumu taasisi muhimu na nyeti ya dola kuwa ina njama za kuondoa uhai wake lakini wahusika waliipuzia. Lakini kama nilivyobainisha hapo awali kuwa, masuala mengi yenye kugusa hisia za umma yamekuwa yakimalizwa kienyeji, hazikufanyika jitihada zozote aidha kukanusha madai hayo ya Mwakyembe wala hatua madhubuti za kuyachunguza.
Mwananchi wa kawaida anaweza kujiuliza, “Hivi kama mashushushu wanaweza kupanga njama za kumuua kiongozi wa kitaifa anayetoka chama tawala CCM; je, hali ikoje kwa viongozi wa vyama vya upinzani? Na je, kama usalama wa vigogo unatishiwa na chombo kinachopaswa kulinda usalama wa nchi, hivi kuna usalama kweli kwa walalahoi?
Pengine suala hilo lilipuuzwa kwa matarajio lingekufa kifo cha asili na kusahaulika akilini mwa Watanzania. Hali ya Mwakyembe ikazidi kuwa mbaya na swahiba wake, Waziri Sitta, akapita huku na kule kuukumbusha umma kuwa mafisadi wakishirikiana na vyombo vya dola ndio waliomdhuru naibu waziri huyo ambaye pia ni mbunge wa Kyela (CCM).
Kama mchezo wa kuigiza vile, Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, akaingizwa kwenye sakata hilo pale alipomtaka Waziri Sitta kuwasilisha ushahidi wa madai yake kuwa Mwakyembe amenyweshwa sumu.
Lakini katika kile kinachoweza kuashiria kuwa nchi yetu inaendeshwa kwa mtindo wa ‘bora liende,’ Nahodha pia alidai kuwa hajawahi kusikia suala hilo (japo yeye ndiye mwenye dhamana ya jeshi la polisi na usalama wa raia), na kuwataka waandishi wa habari wamuulize Sitta aliyetoa tuhuma hizo.
Hatimaye Sitta naye akamjibu Waziri mwenzake (Nahodha) kwa kubainisha kuwa hatapeleka ushahidi wa madai aliyotoa kuwa Mwakyembe alilishwa sumu kwa kuwa polisi tayari wanao ushahidi.
Awali, Nahodha alidai kuwa “...masuala yote yanayohusu uchunguzi hayawezi kuzungumzwa katika vyombo vya habari...ni mambo ambayo hufanyika kwa umakini mkubwa...” na hatimaye DCI Manumba akathibitisha kauli hiyo ya bosi wake (kufanya mambo kwa umakini) kwa kukurupuka na kudai Mwakyembe hajalishwa sumu. Pia, aliwataka wananchi kupuuza madai ya Sitta, akidai kuwa Jeshi la Polisi liliwasiliana na Wizara ya Afya ambayo ilithibitisha ilitoa taarifa kuwa Mwakyembe hakulishwa sumu.
Kauli hiyo ya Manumba ikawaibua Mwakyembe na Sitta ambao walishusha tuhuma nzito dhidi ya Manumba na Jeshi la Polisi kwa ujumla. Mwakyembe alikwenda mbali zaidi na kudai jeshi hilo lilimtuma ‘askari mtuhumiwa wa dawa za kulevya na ujambazi’ kufuatilia taarifa za (Mwakyembe) kutishiwa maisha yake.
Katika kile kinachoashiria kuwa ‘sinema’ hii inaweza kuendelea kwa muda mrefu, muda mfupi kabla sijaandika makala hii Waziri wa Afya, Dk. Hadji Mponda, ameikana kauli ya Manumba kuwa wizara hiyo ilitoa uthibitisho kwa polisi kuwa, Mwakyembe hajalishwa sumu.
Ni vigumu kuwasilisha sakata hili katika mtiririko unaoleta maana kwa sababu staili inayotumiwa na wahusika ni mithili ya ‘piga nikupige.’ Lakini kilicho wazi ni ombwe kubwa kabisa la uongozi kuanzia kwa Rais Jakaya Kikwete mwenyewe.
Kwa vyovyote vile Kikwete anashuhudia mtifuano huu unaoweza kabisa kupoteza imani ya wananchi kwa Serikali yake na taasisi kama Jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa, lakini amekaa kimya kana kwamba mambo hayo yanatokea Somalia na si Tanzania anayoiongoza.
Yeye ndiye aliyewateua Mwakyembe na Sitta, japo uteuzi huo ulionekana na baadhi ya wachambuzi wa siasa za nchi yetu kama mbinu ya ‘kuwadhibiti wanasiasa hao wanaotajwa kuwa ni makamanda wa vita dhidi ya ufisadi.’ Wanaodai hivyo wanapigia mstari kanuni ya uwajibikaji wa pamoja ambayo kama inazingatiwa, haitarajiwi mawaziri wanaotumikia ‘kabineti’ moja kupingana hadharani.
Kama Mwakyembe aliituhumu Idara ya Usalama wa Taifa kuwa ilikuwa na njama za kumuua, na kimsingi kiongozi mkuu wa taasisi hiyo nyeti (sponsor) ni Rais mwenyewe, hiyo inaweza kuzaa tafsiri kuwa Rais ni sehemu ya njama hizo. Kwa hiyo ni wazi kwamba laiti umakini ungetumika tangu mwanzoni mwa sakata hii, Rais Kikwete angeweza kuchukua hatua za aidha kumwajibisha Mwakyembe (kwa vile haiwezekani waziri anayeituhumu taasisi inayoongozwa na Rais kufanya kazi kwa ufanisi na Rais huyo) au kuitisha uchunguzi wa kina wa ili suala hilo kupatiwa majibu sahihi na hatimaye kulimaliza kabisa.
Lakini kwa upande mwingine, ninashindwa kabisa kuwaelewa Mwakyembe na Sitta. Japo ninaguswa na maradhi yanayomsibu Mwakyembe lakini sielewi kwa nini yeye na Sitta wanaendelea kuitumikia Serikali ambayo kimsingi wanaituhumu kuhusika na suala hilo la kulishwa sumu. Idara ya Usalama na Jeshi la Polisi si tu ni taasisi muhimu za Serikali bali pia zote zipo chini ya Rais ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu.
Na kama Mwakyembe alikuwa na uhakika kwamba Idara ya Usalama ina mpango wa kumuua kwa nini hakumwomba Rais aingilie kati, hasa baada ya kubaini (kwa mujibu wa maelezo yake) kuwa Jeshi la Polisi lilikuwa linachukulia tuhuma zake kama mzaha?
Kwa upande wa Idara ya Usalama wa Taifa, ninaamini ukimya wao unachangia kulikuza suala hili. Tuhuma kutoka kwa naibu waziri kuwa taasisi hiyo ina njama za kumuua si ndogo. Sasa kama walidiriki kukana madai yaliyowahi kutolewa na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa kuwa Idara hiyo ilishiriki kumhujumu katika Uchaguzi Mkuu uliopita, kwa nini ikalie kimya tuhuma kuwa inataka kumuua kiongozi asiye na hatia?
Ikumbukwe kuwa kuna nyakati taasisi za intelijensia katika nchi mbalimbali hulazimika ‘kummaliza mlengwa’ (termination) alimradi kufanya hivyo ni kwa maslahi ya nchi. Hilo lipo ndani ya mamlaka wanayokabidhiwa na taifa husika. Naomba ieleweke kuwa hapa simaanishi kuwa Idara yetu ya Usalama wa Taifa nayo inajihusisha na vitendo vya aina hiyo, lakini kwa vile mbinu hiyo ‘inakubalika katika mazingira ya utendaji kazi wa taasisi za aina hiyo,’ kunyamazia tuhuma za Mwakyembe kunaweza kusababisha hisia kuwa ni za kweli.
Jeshi la Polisi nalo lina maswali kadhaa ya kujibu. Kwanza, lini watatoa matokeo ya uchunguzi wao kuhusu tuhuma za Mwakyembe kuwa Idara ya Usalama ilikuwa na njama za kumuua? Pili, kama jeshi hilo limeshatamka bayana kuwa wananchi wapuuze madai ya Waziri Sitta kuwa Mwakyembe amelishwa sumu, kwa nini halijamchukulia hatua ‘kwa kutoa tuhuma nzito kama hizo’? Na tatu, DCI Manumba alipata taarifa kutoka ‘Wizara ya Afya ya nchi gani kuwa Mwakyembe hajalishwa sumu’ (kwani Waziri Mponda ameshang’aka wizara yake kuhusika na hilo)?
Nimalizie makala hii kwa kutoa hadhari kwamba hiki kinachoonekana kama ‘mchezo wa kuigiza’ kinaweza kuwa na madhara makubwa huko mbele.
Wanaozembea kwa kukaa kimya kwa matarajio kuwa suala hili litapotea tu kama masuala ya Kagoda, Meremeta na Tangold wanajidanganya na hatma yake inaweza kuwa mbaya na isiyoweza kurekebishika.


By Joyce Joliga
The Citizen Correspondent
Songea. Police in Songea allegedly shot dead four civilians yesterday, during a fracas associated with a public demonstration against a reported string of murders over the past four months, that the law enforcement organ is accused of neither curbing nor resolving.In a quick rejoinder, however, Ruvuma Regional Police Commander Michael Kamuhanda put the figure of those who had died at two.  

Several other people were injured when police officers used tear gas and live ammunition to quell angry demonstrators, some of whom had stormed the town’s main police station.The Ruvuma regional hospital chief medical officer, Dr Benedicto Ngaiza, confirmed that the hospital  had received four bodies and about 20 injured persons. 

He said two of the bodies had bullet wounds, and  two of the injured persons had bullet injuries  as well, and were rushed to the theatre for operations. All the bodies were delivered by the police,  he explained, adding that, one of them was that of a motorcyclist who had  accidentally hit a tree while speeding  away from the fracas.
Since November last year, nine people have been murdered in the town – a roughly monthly average of two –  some of whose bodies had been mutilated.

The trend has triggered much panic and anger amongst wananchi, who are in the dark over whether the crime is the work of a serial killer or a gang. Worrisome, too, is that, so  long as  the motives of the murders are not known, anyone was a potential next victim.

Chaos  and confusion reigned in Songea for a couple of hours yesterday, as most of the normal  official, business and social activities came to a standstill, as  much attention was  focused on the drama featuring chanting and stone-throwing demonstrators and law enforces who strived to restrain them.

Government offices,  the regional hospital, shops,  and the main bus stand, were among the  sensitive facilities that were temporarily closed and reopened only after relative calm had been restored.

The closures were  prompted by fears by  many people over  being caught in the cross-fire,  or falling victim to looters and petty thieves, since amongst the presumed demonstrators were  people who wielded crude weapons like iron bars.

Many people scattered in various directions towards safer places away from  the procession route, including crew  and passengers awaiting long distance  bus trips. Guards at the regional hospital closed the gates  of the facility as a precaution, as they couldn’t  establish whether  all the people in the huge crowd  that pleaded to be  allowed in were seeking protective shelter, or whether some  were thugs.

 The procession towards the police station  that started early in the morning, attracted hundreds of people marching on foot as well as motorcyclists in slow motion. The crowd swelled as word spread to various parts of the town and more people joined in.

Reports say that  the police fired live ammunition in the air and lobed teargas canisters into the crowds in a bid to restrain them, but, some amongst them continued pushing relentlessly into the police  station compound.

It was at that juncture that the police fired directly  into the crowd, killing two of the protestors, according to RPC Kamuhanda,  who explained that they had refusing to heed orders aimed at preventing a breach of peace. Mr Kamuhanda said investigations had been launched, but  hinted that initial indications pointed to  superstitious beliefs and politicking as causes of the chaos.

The Ruvuma Regional Commissioner, Mr Said Mwambungu,  expressed  dismay over the incident, and appealed to wananchi to remain calm while the Police was continuing with efforts to track down the  perpetrators  of the murders that had fuelled their anger.

He appealed  to Songea residents to avoid walking alone at night, especially if they didn’t have important engagements  that warranted taking risks.

In the evening, Mr Mwambungu chaired a crisis meeting of the regional peace and security committee, to chart  strategies  for containing the mysterious killings.

SOURCE: The Citizen


Chuck D,mwanzilishi na kiongozi wa lilikouwa kundi maarufu la rap huko Marekani,Public Enemy,aliwahi kusema muziki wa rap ndio CNN ya mtaa.Tangu awali,muziki wa rap umekuwa ukizungumzia masuala mbalimbali yanayoikabbili jamii-kutoka ukimwi,mihadarati,ubaguzi wa rangi hadi sera za ndani na za nje.Na sasa tunashuhudia baadhi ya wasanii wetu wakipata mwamko kama huo wa Public Enemy.Ushuhuda ni huu hapa chini.Sahau kidogo kuhusu video na sikiliza ujumbe kwa makini



CHANZO: Dj Choka's Blog

21 Feb 2012


Kwa maelezo zaidi BONYEZA HAPA


It's your birthday and I can't be there
But I'll send you a special birthday wish and a little prayer
Have a happy birthday
I hope that all of your birthday wishes come true
May you have a great time today and find happiness in everything you do.










CHANZO: Jamii Forums

KWA MWENDENO HUU NDIO MAANA TUNASHUHUDIA "MAFURIKO YA WAWEKEZAJI" WANAOISHIA KUPORA AJIRA ZA WAMACHINA (KWA MFANO WACHINA).UKILINGANISHA FOMU HIYO HAPO JUU NA FOMU ZA KUOMBEA VIZA ZA KUINGIA NCHI KAMA UINGEREZA AU MAREKANI UTABAINI JINSI GANI HATUPO SERIOUS KATIKA MAMBO NYETI.

20 Feb 2012


WAPENDWA WATAZAMAJI WA TMTV.
 
TUNAPENDA KUWATANGAZIA KUWA KUTOKANA NA MATATIZO YA KIUFUNDI.
KUMEKUWA NA TATIZO LA KUINGIA KTK TV KATIKA SIKU CHACHE ZILIZOPITA.TATIZO HILO LINAENDELEA KUFANYIWA KAZI.
KWA SASA UNAWEZAENDELEA KUBURUDIKA NA TMTV KWA LINK HII  http://tmtv.eightzerodigital.com/player.php
TUNAWAAHIDI MAMBO MAZURI YANAKUJA,VIDEO KIBAO MPYA ZITAONGEZEKA KWA RAHA ZAIDI KAMA KAWAIDA 24/7 NON-STOP.


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.