15 Aug 2014

 Kunywa maji ya kutosha 

  1. Increase Your Ejaculate Step 1 Version 2.jpg


  1. Epuka joto kwa sehemu zako za siri
    Increase Your Ejaculate Step 2 Version 2.jpg

  2. ee
  3. Epuka 'nguo za ndani' za kubana
    Increase Your Ejaculate Step 3 Version 2.jpg


  4. Epuka 'kupinda nne'
    Increase Your Ejaculate Step 4 Version 2.jpg

    .


  5. Punguza tendo la ndoa kwa muda ile kurejesha mbegu za kiume 'zilizopotea'
    Increase Your Ejaculate Step 5 Version 2.jpg
    Add caption
  1. Tumia vitamini vya Zinc na Folic Acid
    Increase Your Ejaculate Step 6.jpg


  2. Punguza kunywa soda
    Increase Your Ejaculate Step 7.jpg


  3.  Meza vitamini vya Amino Acid vya aina hizi: L-Arginine, L-Lysine na L-Carnitin Increase Your Ejaculate Step 8.jpg

  4. Jaribu 'vidonge vya asili' viitavyo Horny Goat Weed
    Increase Your Ejaculate Step 9.jpg


  5. Kula matunda na mbogamboga (hasa maharage mekundu, maji ya nazi, apples, wild blueberries, blackberry, cranberry)
    Increase Your Ejaculate Step 10.jpg


    Chua misuli ya 'sehemu yako ya siri' pasipo kufikia 'kileleni'

    1. Increase Your Ejaculate Step 11.jpg

    2. Punguza na hatimaye acha kuvuta sigara (na bangi ni adui mkubwa wa mbegu za kiume)
      Increase Your Ejaculate Step 12.jpg

      • Punguza msongo wa mawazo (stress)
        Increase Your Ejaculate Step 13.jpg

        • Fanya mazoezi mara kwa mara
          Increase Your Ejaculate Step 14.jpg

        • Zingatia ngono salama (maradhi ya zinaa yanaathiri vibaya uzalishaji mbegu za kiume)
          Increase Your Ejaculate Step 15.jpg

          CHANZO: WikiHow

        12 Aug 2014


        Hali nchini Iraki ni tete kufuatia uamuzi wa Rais wa nchi hiyo Fouadi Masoum (I guess wewe kame mie tulikuwa hatumfahamu mtu huyu wala kujua kama Iraki ina rais) 'kumtimua' Waziri Mkuu Nuri al-Maliki, aliyekuwa madarakani kwa miaka minane, na kumteua Haidar al-Abadi kuchukua wadhifa huo.

        Hata hivyo, Maliki sio tu  amegoma kuondoka madarakani bali pia amemwaga wanamgambo na vikosi maalum vya jeshi (special forces) mitaani, na kupelekea kizaazaa cha aina yake.

        Marekani, ambayo ilisaidia kumweka madarakani Maliki mwaka 2003 imempongeza Waziri Mkuu mpya al-Abadi, msaidizi wa zamani wa Maliki, kuashiria kuunga mkono mabadiliko hayo.

        Akihutubia kwa njia ya televisheni (naam, pamoja na vurugu zote nchini Iraki bado televisheni zinafanya kazi) amesema hatua ya Rais kufanya mabadiliko hayo ni ukiukwaji hatari wa Katiba, huku akiambatana na 'wapambe' wake, ameahidi kutatua 'kero' hiyo.

        Mkwe wake, Hussein al-Maliki, ameyaelezea mabadiliko hayo kuwa ni kinyume cha sheria, na kudai yatabadilishwa kortini. "Hatutokaa kimya," alidai.

        Hata hivyo, Marekani imemwonya Maliki kutotumia nguvu za dola kung'ang'ania madaraka.

        Mwislamu wa madehebu ya Shia, Maliki analaumiwa na washirika wake wa zamani huko Marekani na Iran kwa kuwasukuma waumini wa madhehebu ya SUnni katika mapambano yaliyopelekea 'sintofahamu' inayoendelea sasa kwa kikundi cha Sunni cha ISIS kudhamiria kuigeuza nchi hiyo kuwa taifa la Kiislam. Viongozi wengi wa ki-Sunni na Kikurdi wamekuwa wakipiga kelele kuwa Maliki anastahili kuachia ngazi, huku hata baadhi ya viongozi wenzake wa ki-shia wakiwa na msimamo kama huo.

        CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka vyanzo mbalimbali mtandaoni

        11 Aug 2014


        Vacancy
        Governance Advisor
        Irish Aid is the Government of Ireland’s programme of assistance to developing countries operating under the Embassy of Ireland in Tanzania.  The programme focuses on Health, Nutrition and Agriculture, with a strong governance component supporting the achievement of results across the programme.
           
        The Embassy is seeking to recruit a highly motivated and experienced Governance Advisor to join its Development Team.  Reporting to the Senior Governance Adviser and working with the Governance Team and across the other teams at the Embassy, the successful candidate will be expected to contribute to the delivery of a high quality programme.  He/she will have responsibility for management of a number of the governance programme components as well as the provision of strategic input and advice on governance across the Embassy.  The Advisor also will provide support to the team on mainstreaming governance within their areas of responsibility.  

        Candidates applying for the position are expected to have: (i) a post graduate degree in governance,  politics, law, international development, social sciences or other relevant disciplines; (ii) a minimum of four years relevant work experience as well as (iii) knowledge and understanding of the political economy  and governance environment  in Tanzania .  A detailed job description is available on the Embassy of Ireland website www.embassyofireland.or.tz .
        Interested candidates should forward a cover letter together with their most recent Curriculum Vitae and contact details to:[email protected] by 14 August 2014.

                           
        Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba nusura wapigane baada ya kupishana kauli wakati wa mjadala wa ndani ya Kamati Namba Sita inayoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira.
        Habari kutoka ndani ya kamati hiyo inayofanyia vikao vyake katika moja ya kumbi za Dodoma Hoteli zinasema, mvutano huo ulitokea Alhamisi iliyopita na kusababisha Wassira kusitisha kwa muda kikao hicho, kisha kwenda kuwasuluhisha.
        Jana, Wassira licha ya kukiri kutokea kwa mvutano huo, alikanusha taarifa kwamba aliahirisha kikao hicho kwa ajili ya kuwasuluhisha.
        “Kupishana katika masuala haya makubwa ni jambo la kawaida, hivyo mimi sidhani kama ni jambo linalopaswa kwenda mpaka kwenye magazeti maana kila wakati hutokea tofauti hizi na ndiyo maana sisi wenyeviti tupo ili kusimamia mijadala,” alisema Wassira na kuongeza:
        “Lakini kwamba eti hilo jambo lilisababisha kikao kuahirishwa au kusitishwa hapana, kikao kiliendelea na kazi yake baada ya hilo lililoleta na ubishani kumalizwa”.
        Habari zilizolifikia gazeti hili zinasema mvutano huo ulitokea wakati kamati hiyo ilipokuwa ikijadili Sura ya Nne na Tano, hususan suala la uraia wa nchi mbili. Sura ya tano ndiyo inayozungumzia masuala ya uraia.
        “Sophia Simba yeye anataka uraia wa nchi mbili wakati Werema alikuwa akisema hilo jambo haliwezekani kutokea kwa sasa,” kilisema chanzo chetu.
        Kwa mujibu wa taarifa hizo, mvutano huo uliendelea baina ya viongozi hao na ndipo Jaji Werema aliposimama katika mchango wake na kuhoji elimu ya Simba, hivyo kuamsha hasira za waziri huyo ambaye pia alijibu mapigo.
        “AG alipopewa nafasi ya kuzungumzia baada ya mabishano ya muda alihoji shule (elimu) ya Simba kwamba amesoma shule gani akimaanisha kwamba ni mgumu kuelewa, kwa hiyo waziri alikasirika na yeye alianza kujibu mapigo,” kiliongeza chanzo hicho.
        Baada ya kutokea mvutano huo, baadhi ya wajumbe waliingilia kati kusitisha mzozo huo, ndipo Mwenyekiti Wassira alipositisha kikao hicho kwa muda kisha kuwasuluhisha wahusika.
        Walipotafutwa jana kwa nyakati tofauti kuzungumzia mzozo wao, Werema na Simba hawakuwa tayari kubainisha kilichotokea.


        Werema alitaka aachwe apumzike na kwamba mambo ya kamati yaachwe kwenye kamati.
        “Jamani hamtuachi hata tupumzike Jumapili yote hii? Tafadhali bwana niache nipumzike, hayo mambo kama ni ya kamati, yaachwe kwenye kamati,” alisema Werema na kukata simu.
        Simba baada ya kuulizwa alisema: “Heeeee hayo makubwa… I have no comment (sina cha kusema”), kisha alikata simu.
        Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alisema ofisi yake haikuwa imepata taarifa kuhusu mzozo huo na kwamba angefuatilia ili aweze kufahamu kuhusu kilichojiri.
        “Nina maofisa wa kutosha katika kila kamati, sasa nashangaa kwamba jambo kubwa kama hilo litokee halafu nisipate taarifa, lakini ngoja nifuatilie lakini kwa sasa sina taarifa yoyote,” alisema Hamad.
        Werema
        Juni mwaka huu, Jaji Werema alitaka kumtia adabu Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila bungeni Dodoma baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu kuahirisha kikao cha Bunge, ikiwa ni muda mfupi baada ya Werema na Kafulila kurushiana maneno bungeni.
        Jaji Werema alichukia baada ya Kafulila kumwita mwizi, akijibu mapigo baada ya mbunge huyo kuitwa tumbili na mwanasheria huyo.
        Hali hiyo ilijitokeza baada ya kutofautiana kauli kuhusu mgogoro wa fedha za akaunti ya Escrow kulipwa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL.
        CHANZO: Mwananchi 
        ANGALIZO: Picha ni kielelezo tu 

        Tuwe wakweli, japo matumizi ya emoji yanaweza kufanya ulichoandika kionekane sio serious lakini kwa hakika emoji zinasaidia kuonyesha mood yako. Sasa sote twafahamu kuwa emoji hutumika zaidi kwenye simu, hasa za kisasa. Je wafanyaje ukitaka kuzitumia mtandaoni, kwenye Twitter au kwingineko?

        Tembelea tovuti hii na utakuta lundo la emoji. Ukishaiona unayotaka, i-copy kisha i-paste kwenye sentensi yako...there you go!

        Endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali ikiwa ni pamoja na za teknolojia. Bonyeza TEKNOLOJIA hapo kwenye main menu utakutana na mengi ya muhimu katika eneo hilo. Karibuni sana


        WIKIENDI iliyopita haikuwa njema kwa mtangazaji Ephraim Kibonde baada ya kutupwa nyuma ya nondo katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar kwa msala wa kudaiwa kugonga gari na kutoa lugha ya matusi, Ijumaa Wikienda lina full stori.
        Mtangazaji Ephraim Kibonde akidhibitiwa na Polisi wa usalama barabarani maeneo ya Mwenge.
        Kwa mujibu wa chanzo chetu makini cha habari ambacho kimeshuhudia sakata hilo mwanzo mwisho, ishu nzima ilianzia maeneo ya Makumbusho ambapo gari alilokuwa akilitumia Kibonde, liligonga kwa nyuma gari jingine na kisha kukimbia.
        “Baada ya kugonga, Kibonde alirudi nyuma kisha kuanza kukimbia ambapo trafiki alitumia gari lililogongwa na Kibonde kumkimbiza,” kilimwaga data chanzo hicho.Chanzo hicho kilifafanua kuwa baada ya polisi kumkimbiza kwa saa kadhaa, walifanikiwa kumkamata maeneo ya Mwenge ambapo trafiki alipanda kwenye gari la Kibonde na kumuamuru arudi eneo la tukio lakini Kibonde hakuwa tayari kurudi ndipo alipoanza kukimbia tena, huku askari aliyemkamata akiwa ndani ya gari.
        Ephraim Kibonde akiwa nyuma ya nondo katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar es Salaam.
        “Inaonekana kulitokea kutoelewana kati ya askari na Kibonde ndipo askari huyo alipowasiliana na wenzie kwa njia ya radio call ili wambananishe na alipofika Ubungo kwenye mataa wakamtaiti na kumpeleka kituoni, Oysterbay,” kilihitimisha chanzo chetu.
        Baada ya kupata maelezo hayo, kachero wa Ijumaa Wikienda alitia timu katika kituo cha Oysterbay ili kutaka kujua mustakabali mzima wa ishu hiyo ambapo alimshuhudia Kibonde akiwa amesimama nyuma ya nondo huku akiwa anaimba ‘nyimbo’ anazozijua mwenyewe.
        Mtangazaji huyo amefunguliwa kesi iliyopewa RB namba OB/RB/13806/20014 KUGONGA NA   LUGHA YA MATUSI.


        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .
        .


        Jasusi ChatBot

        Categories

        Blog Archive

        © Evarist Chahali 2006-2022

        Search Engine Optimization SEO

        Powered by Blogger.