16 Jun 2009

Miongoni mwa nukuu muhimu kuhusisna na Mwenyekiti Mao wa China ni hii: usiseme kitu kama hujakitafiti (tafsiri yangu isiyo rasmi kwenye usemi no research,no right to speak).Sasa sijui tumweleweje huyu Sekulu MUSTAFA MKULO anapodai kwamba kuna baadhi ya taasisi za dini zimekuwa zikitumia vibaya misamaha ya kodi,lakini hakuweza kutaja angalau jina la taasisi moja.Hizi ni dalili za ubabaishaji na uoga.Uoga huo wa kutaja hadharani watumishi wa Mungu wanaotuhumiwa kuvunja sheria unasababishwa na mtoa tuhuma kutokuwa mkamilifu.Ni mithili ya mama anayechelea kutaja madhambi ya bintie kwa kuwa naye yumo katika mchezo huohuo.



Kama kuna wachunga kondoo wa Bwana walikuwa wakitumia misamaha ya kodi vibaya lakini hawakuchukuliwa hatua,inamaanisha chombo kinachoitwa Mamlaka ya Mapato kiko kwenye usingizi wa pono.Kwanini wahusika hawakuchukuliwa hatua?Au kulikuwa na utatu usio mtakatifu wa vigogo serikalini,wafadhili ughaubuni na watumishi wa Mungu?

Hata kama tukiafikiana na maelezo za Mheshimiwa Mkulo kuhusu hako kamchezo kasikopendeza ,ni dhahiri kwamba vitendo vya watenda dhambi hao wachache havimaanishi kuwa dhehebu lote analotoka mtenda dhambi nalo lina makosa.Kuwepo kwa viongozi kadhaa wa dini ambao wamekuwa wakitumia vibaya misamaha ya kodi hakumaanishi kwamba mantiki nzima ya mpango huo imepoteza maana.


Na lini utaratibu huu wa "akikosea mmoja basi wamekosea wote" ulianza?Mbona hapo Benki Kuu palipozaliwa ufisadi wa EPA na nduguye wa Maghorofa Pacha bado wahusika wameendelea "kupeta"?Kama Ballali ndio kinara cha wizi huo,kwanini basi wasaidizi wake (ikiwa ni pamoja na huyu gavana wa sasa) wameachwa kuendelea na kazi?Je Liyumba anapotuhumiwa kufanya ubadhirifu wa fedha za Maghorofa Pacha,kwanini basi menejimenti yote ya Benki Kuu nayo isipandishwe kizimbani kwa vile,kwamujibu wa Mkulo,akikosea mmoja basi wamekosea wote!Mbona Mattaka kalikoroga ATCL kapelekwa NIC,Peter Noni anahusishwa na EPA kapewa ulaji TIB,Mzee wa Vijisenti na mabilioni yake visiwani Jersey bado yuko kwenye kamati ya maadili ya chama tawala!

Kwa madhambi haya,dnio maana hutosikia yeyote akidiriki kutaja jina la kiongozi wa dini anayetuhumiwa kufuja misamaha ya kodi (kama yupo).Mtu asiye msafi hawezi kuonyesha uchafu wa mwenzie.

Lakini binafsi natafsiri kuwa hatua hii ina ajenda mbalimbali zilizofichika ikiwa ni pamoja na kuonyeshana nani mwenye nguvu zaidi: mamlaka za kidunia au za kiroho.Usisahau kauli za hivi karibuni kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kwamba mafisadi wameteka nchi....na kuandaa mkakati wa kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu wa 2010.



Wizara ya Fedha na Uchumi imesema, siasa za Tanzania ni nzuri na kuna mipango mizuri ya maendeleo ndiyo maana umasikini wa kipato unapungua. Hata hivyo Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Omar Yussuf Mzee amesema, bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watanzania wengi wanaishi kwa kula mlo mmoja. Kiongozi huyo wa Serikali amesema leo kuwa, umasikini ni mchakato, unapungua siku hadi siku.

Mzee ameyasema hayo wakati anajibu maswali ya Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya aliyetaka kufahamu ni kwa nini watanzani wengi bado ni masikini wakati nchi imepata uhuru miaka 48 iliyopita.

Mbunge huyo pia alidai bungeni kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kabisa kwa kuwa hakuna siasa safi, na pia hakuna mipango mizuri ya kuwawezesha wananchi wapate maendeleo.

Naibu Waziri Mzee amewaeleza wabunge kuwa kuna umasikini wa aina tatu ukiwamo wa elimu, afya na kipato.Amesema, kama Tanzania isingekuwa na siasa safi na mipango mizuri ya maendeleo, takwimu zisingeonyesha kupungua kwa umasikini wa kipato nchini.


Amewaeleza wabunge kuwa, mwaka 1991, asilimia 21.6 ya watanzania wote milioni 24.8 walikuwa masikini kabisa. Kwa mujibu wa kiongozi huyo, mwaka 2001, Tanzania ilikuwa na watu milioni 31.9, asilimia 18.7 kati yao walikuwa masikini kabisa, na mwaka 2007, asilimia 16.5 ya watanzania milioni 38.3 walikuwa masikini kabisa.

Mzee amelieza Bunge kuwa, watanzania wengi bado ni masikini kwa kwa wengi wao ni wakulima wanaotumia jembe la mkono, bei za pembejeo za kilimo zimepanda, na pia mabadiliko ya hali ya hewa yanathiri uzalishaji kwa kuwa sehemu kubwa ya kilimo nchini hutegemea mvua. Ametaja sababu nyingine kuwa ni ukuaji mdogo wa sekta ya viwanda, wakulima kukosa mitaji, na pia ukosefu wa ajira.


CHANZO: Habari Leo

Wizi mtupu!


Professor Duncan Rice, Principal and Vice Chancellor of the University of Aberdeen, has been honoured with a Knighthood in the Queen’s Birthday Honours.

Professor Rice has been awarded the honour for services to higher education.

Professor Rice said: "On a personal level this is a wonderful honour, and I'm very proud of it. But I know it's intended to recognise all the University has achieved in the last decade. I am just the vehicle, and the real congratulations go to the whole of our community. It is being transformed by the commitment, quality and vision of all my colleagues, and my knighthood is a way of honouring them."

He added: "By the standards of where we were a decade ago, we have manoeuvred ourselves into being one of the top handful of universities in Scotland. That makes this something of a minor golden age. What we really want to do now is to advance into a real golden age, where we are one of the top handful of universities in the world."



14 Jun 2009


Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu has announced he will back a Palestinian state - but only if it is completely demilitarised.

He said a Palestinian state must have no army, no control of its air space and no way of smuggling in weapons.

And a Palestinian state must recognise Israel as a Jewish nation, he said.

Mr Netanyahu's speech, laying out his plans for regional peace, came a month after US President Barack Obama urged him to accept a two-state solution.

The BBC's Paul Wood says Mr Netanyahu broke ground by accepting the principle of a demilitarised Palestinian state, albeit with conditions, and this will be what the White House is looking for.

But our correspondent says the question is whether this will be enough to make up for the lack of movement on the issue of Jewish settlements in the occupied West Bank.

Mr Obama has stressed that he wants all settlement activity to stop.

But in his speech Mr Netanyahu said settlers were not "enemies of peace" and did not move from his position of backing "natural growth" in existing settlements.

Guarantee needed

The Israeli leader offered to talk to the Palestinians immediately and with "no preconditions".

"We want to live with you in peace as good neighbours," he said.

Mr Netanyahu also said he was willing to go to Damascus, Riyadh and Beirut in pursuit of a Middle East peace deal.

He said Israel would "be prepared for a true peace agreement [and] to reach a solution of a demilitarised Palestinian state alongside the Jewish state".

But only if "we receive this guarantee for demilitarisation and the security arrangements required by Israel, and if the Palestinians recognise Israel as the nation of the Jewish people.


SOURCE: BBC


Majuzi,Watanzania wametahadharishwa kuhusu athari za mdodoro wa uchumi wa dunia na madhara yake kwa nchi yetu.Kadhalika,bajeti ya mwaka ujao wa fedha imeandaliwa kwa kuzingatia tahadhari hiyo huku kukitangazwa mpango wa kuchochea uchumi (economic stimulus plan).

Hata hivyo,kama nilivyojadili HAPA,uwezekano wa bajeti na stimulus plan hiyo kufanikiwa,sambamba na umuhimu wa tahadhari iliyotolewa,utategemea zaidi hatua kali na za makusudi dhidi ya ufisadi na mafisadi.Yayumkinika kubashiri kwamba pamoja na imani kwamba mipango hiyo inalenga kulinusuru taifa,wanaufaika wakubwa wanweza kuwa mafisadi wanaojua vema namna ya kubuni mikakati ya ulaji huku wakiwa hawana hofu ya kuchukuliwa hatua yoyote kutokana na siasa za kulindana na kishkaji.

Hebu soma kwanza habari ifuatayo,kisha tujadili kidogo mwishoni.

Wingu zito fedha za EPA
• Chegeni: Zimekwenda kusikojulikana

na Mwandishi Wetu

UTATA umegubika mahali zilipo na matumizi ya fedha zilizorejeshwa na kampuni zilizoshiriki katika wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), uliofanyika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Rais Jakaya Kikwete alipokuwa akilihutubia Bunge mjini Dodoma Agosti mwaka jana, alibainisha fedha hizo zilizorejeshwa na baadhi ya kampuni si mali ya serikali lakini zitawekwa kwenye akaunti maalumu kabla ya kupelekwa katika Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa ajili ya kufungua dirisha dogo la kuwakopesha wakulima wakati nchi ikielekea katika mchakato wa kuanzisha Benki ya Kilimo.

Ingawa Rais Kikwete na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, kwa nyakati tofauti walieleza kuwapo kwa fedha hizo katika akaunti maalumu, taarifa ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata zinasema hadi sasa fedha hizo hazijaingia katika Benki ya TIB, licha ya kuwapo kwa taarifa kuwa fedha hizo zimetumika kununulia mbolea iliyotolewa kwa mfumo wa vocha kwa baadhi ya wakulima hapa nchini.

Chanzo kimoja cha habari kilichomo ndani ya TIB kimedai fedha hizo wamekuwa wakizisikia kupitia katika vyombo mbalimbali vya habari kutoka kwa wanasiasa, ambao wamekuwa wakijinadi kuwa fedha hizo zitatumika kunyanyua kilimo ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.

Chanzo hicho kilibainisha kuwa hadi sasa dirisha la kilimo lililosemwa bado halijaanza kufanya kazi iliyotarajiwa, ingawa maneno ya watu mbalimbali yamekuwa yakibainisha kuanza kazi kwake ambako kungetarajiwa kuwasaidia wakulima kupata mikopo ya muda mrefu, baada ya kuikosa fursa hiyo kwa kipindi kirefu kutokana na kutokopeshwa na taasisi za fedha za hapa nchini.

“Haya mambo huwa tunayasoma, kuyasikia na kuyaona kwenye hivyo vyombo vyenu vya habari, lakini kwenye makaratasi hali ni tofauti, sasa sijui niseme siasa inatawala au muda bado haujafika,” kilisema chanzo hicho.

Tanzania Daima Jumapili, ilifanya juhudi za kumtafuta Mkurugenzi Mtendaji wa TIB, Peter Noni, ambaye ameteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo na Rais Jakaya Kikwete, lakini Ofisa Mwanadamizi wa Mambo ya Uhusiano wa benki hiyo,Catherine Magambo, alisema mkurugenzi wake hawezi kutoa ufafanuzi hivi sasa, kwa kuwa ameanza kazi siku si nyingi na ni busara akapewa wiki moja ili aweze kujipanga.

Catherine, alipotakiwa kueleza kama ana taarifa zozote za kutokuwapo kwa fedha zilizoahidiwa na rais kupelekwa katika benki hiyo, alisema anachokifahamu ni kile kilichoelezwa wakati fulani na Mkurugenzi aliyestaafu, William Mlaki, kuwa hawajapokea fedha hizo na kama kungekuwa na mabadiliko vyombo vya habari vingejua kama walivyofanya hapo awali.

“Nyinyi Tanzania Daima Jumapili, habari kama hii unayoniuliza au unayotaka mkurugenzi wangu akujibu, najuakwamba hakuna kitu ambacho kimebadilika lakini kama mnataka habari zaidi msubiri mkurugenzi mpya azoee ofisi kwa muda wa wiki, halafu ndipo uje kumuuliza maswali yako,” alisema Magambo.

Pia alibainisha kuwa hajaona mabadiliko yoyote juu ya ahadi iliyotolewa pia na Rais Kikwete ya kutoa kiasi cha sh bilioni 15 kwa ajili ya kuendeleza benki hiyo ili iweze kutoa mikopo kwa wakulima.

“Jamani maswali yenu mbona yamezidi, si nimewaambia hakuna mabadiliko na hayo maswali yenu msubirini mkuu? Mbona mnanibana kwa mambo nisiyo na uwezo wa kutoa majibu? Kwani kila ofisi ina utaratibu wake,” alisema Magambo.

Wakati fedha hizo zikionekana kugubikwa na utata, baadhi ya watu wamekuwa wakiiona hatua ya serikali kutangaza kurejeshwa kwa fedha hizo ni kiini macho au zimetumika katika matumizi mengine badala ya kupelekwa katika kilimo kama ilivyoahidiwa, kwa kuwa viwanda vingi vya mbolea kwa mwaka huuvimejikuta vikishindwa kujiendesha baada ya kuzalisha bidhaa hiyo na kukosa wanunuaji.

Dhana hiyo inachagizwa na baadhi ya wakulima ambao wamekuwa wakilalamikia kutokupata mbolea hiyo, licha ya serikali kutangaza kutenga fungula fedha kwa ajili ya kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima ili kukuza kilimo na kuleta mapinduzi ya kijani.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa na wanasiasa mbalimbali wa hapa nchini walikuwa wakihusisha wizi huo wa fedha na mkakati maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwaagiza baadhi ya makada wake na wanachama wakwapue fedha hizo kwa ajili ya matumizi ya kampeni za uchaguzimkuu wa mwaka 2005 uliokiwezesha chama hicho kuibuka na ushindi wa ‘kishindo.’

Hisia hizo zilipata nguvu baada ya kuwapo tetesi kuwa kampuni iliyochota kiasi cha sh bilioni 40 ya Kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, inadaiwa kumilikiwa na baadhi ya vigogo wa chama hicho, jambo lililochangia ugumu wa kukamatwa kwa wamiliki wa kampuni hiyo ambayo inaaminika ndiyo iliyosuka mpango wa uchotaji wa fedha hizo.

Tuhuma hizo mara kadhaa zimekuwa zikikanushwa na viongozi waandamizi wa chama hicho, akiwamo Katibu Mkuu wake, YusufMakamba, ambaye aliweka bayana kuwa CCM haijamtuma mwanachama wake afanye wizi huo na kama kuna mwanachama amehusika na wizi huo apewe lawama hizo binafsi na si chama.

Naye Mbunge wa Busega, Dk. Raphael Chegeni, katikati ya wiki alinukuliwa na vyombo vya habari mjini Dodoma akisema kuwa fedha za EPA zinaonekana kwenda sehemu zisizoonekana kirahisi kwa wananchi, ingekuwabusara kama zingetumika katika ujenzi wa barabara ambayo ingepewa jina la EPA, ili kila
mwananchi aweze kuamini kinachosemwa na viongozi wa serikali.

Alisema mazingira ya fedha hizo tangu awali yalionyesha utata, hivyo ingekuwa busara hata matumizi yake yakafanyika bila kuwapo kwa usiri, ili kuondoa fikra potofu kuwa hakuna fedha iliyorejeshwa.

“Hizi fedha za EPA mimi nafikiri zingetumika kujengea barabara na tukaziita barabara za EPA, ili yeyote anayetaka kuzusha lake ashindwe kufanya hivyo au tumuonyeshe vithibitisho,” alisema Chegeni.

Alisema sekta ya kilimo ni pana na hata fedha zinazotumbukizwa huko ni lazima ziandaliwe mipango mizuri na mapema ili ziweze kufikia walengwa na zilete tija inayotakiwa kuliko inavyoonekana sasa ambapo serikali inasema imetoa mbolea ya ruzuku kwa wingi, lakini wakulima wanalalamika kutoipata mbolea hiyo kwa kiwango kinachohitajika.

Wizi wa fedha za EPA ulibainika baada ya Kampuni ya ukaguzi ya kimatifa ya Ernst &Young kubaini wizi wa sh bilioni 133, ambapo baada ya uchunguzi huo, Rais Kikwete aliamua kumfukuza kazi aliyekuwa Gavana wa benki hiyo, marehemu Daudi Ballali na kuagiza mamlaka husika kufanya uchunguzi kwa maofisa wa benki hiyo ili kufikishwa mbele ya vyombo vyasheria.


CHANZO: Tanzania Daima.

Katika mazingira kama haya,itakuwa kosa kweli kuyamkinisha kwamba hiyo stimulus plan inaweza kuishia kutengeneza dili ya kuifanya EPA ionekane "cha mtoto"?

Halafu,habari hiyo hapo juu ina kitu kingine cha ziada,nacho ni kuhusu PETER NONI.Huyu jamaa anahusishwa kwa karibu na skandali la EPA.Awali wasiwasi wangu ulikuwa kwenye kuteuliwa kwake kuwa Mkurugenzi wa TIB.Kilichonifumbua macho katika habari hii ni ukweli kwamba marejesho ya fedha za EPA yalipangwa kupelekwa TIB.You see the connection?NONI anahusishwa na ishu ya EPA kwa wadhifa aliokuwa nao BoT.Sasa anapokwenda TIB ambako tunaambiwa ndiko zitakapopelekwa marejesho ya fedha za EPA ni mithili ya "kula denge" kuelekea lilipo fungu hilo.

Ndio Tanzania yetu hiyo!












CHANZO: The Guardian


'I don't hate or have any problem with black people other than I hope very much that they remain black people. Other than I hope their children will look as black as they are and as different and as interesting. And where it doesn't happen: it's not my business. No I haven't got a problem, so where does it come from? I don't really know'. That's NICK GRIFFIN,a racist leader of a Nazi British National Party,in an interview with the Independent On Sunday (CLICK THE LINK FOR A FULL TRANSCRIPT OF THE INTERVIEW)

RELATED STORY: (In the Sunday Times) Profile: Nick Griffin.

Laiti jicho lingekuwa risasi,basi hapa Ferguson angekuwa majeruhi,au zaidi...

Hii inajieleza yenyewe.Kama Ferdinand hatukani kimoyomoyo basi anajikaza kumtoa mtu ngeu.Ni siku Man United waliofungwa na Barca kwenye fainali ya Champions League.

Japo Rooney anafarijiana na Tevez,anaonekana mawazo yake yako zaidi kwa mshambuliaji mwenzie Ronaldo.Wachambuzi wa soka la Uingereza wanadai kwamba mara nyingi Rooney alijitoa mhanga kubadili nafasi uwanjani ili kum-accommodate Ronaldo,ambaye anatuhumiwa kuwa m-binafsi uwanjani.

Ni kama Ronaldo anaona kinachofuata-kupewa medali za ushindi wa pili-ni kuzinguana tu.

Pamoja na umahiri katika kusaka magoli,Barbatov anasifika kwa fegi.Ni mvutaji sigara sugu.Na hapa hilo jicho analompa Ronaldo ni kama la mtu aliyelowesha sigara ya mwisho kwenye pakti katikati ya mbuga ya Mikumi.

Jicho la "baba anayeelekea ukingoni kumrekebisha mwanae".








Yote ni katika kuendeleza mila.Ni katika kabila la wahamaji (nomads) la Vadi katika jimbo la Gujarat nchini India.Kabila hilo lenye takriban watu 600 hivi,lina mila ya kuwapatia watoto mafunzo ya sanaa ya kucheza na nyoka (snake charming).Lakini,hilo sio suala la siku moja,wiki,mwezi au mwaka bali ni muongo mzima (mika 10)!
Watoto huingizwa kwenye mafunzo hayo wanapotimiza miaka miwili tangu wazaliwe.Inatarajiwa kuwa watapofikisha umri wa miaka 12,watoto hao watakuwa wakielewa kila kitu kinachohusiana na nyoka.

13 Jun 2009


AHMADINEJAD AMEKUWA AKISHUTUMIWA KWAMBA AMESHINDWA KUBORESHA UCHUMI WA IRAN

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa ya Iran,Rais Mahmoud Ahmadinejad amefanikiwa kutetea nafasi yake kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo wiki hii.Kwa mujibu wa taarifa hizo,Ahmadinejad amepata asilimia 67 ya kura huku mgombea wa mwenye mrengo wa mageuzi,Waziri Mkuu wa zamani Mir Hossein Mousavi,akiambulia asilimia 30. SURA YA MAGEUZI.UKURASA WA MOUSSAVI KWENYE FACEBOOK.

Hata hivyo,kuna taarifa kwamba Mousavi nae anadai ameshinda uchaguzi huo.Wagombea wengine ni pamoja na mwanazuoni mwanamageuzi Mehdi Karroubi (picha inayofuata chini) na kamanda mhafidhina wa Revolutionary Guard Mohsein Rezaei (picha ya mwisho chini).

VYANZO: Kurasa mbalimbali mtandaoni

12 Jun 2009


Bajeti ndio hiyo ishasomwa.Ila nimeonelea nami niiweke hapa.Isome hapo chini baada ja mjadala huu kiduchuTunaambiwa kuna maeneo takriban sita yaliyopewa kipaumbele katika bajeti hiyo.Naamini hata bajeti ya mwaka jana ilikuwa na vipaumbele vilevile lakini sote tunajua hali ikoje muda huu.Tatizo letu kubwa halipo katika kuainisha vipaumbele.Wala hatuna tatizo kuja na grand schemes zinazoweza kabisa kukuaminisha kuwa huenda sooner or later "maisha bora kwa kila Mtanzania yatakuwa sio tena slogan bali ukweli halisi".Tatizo la msingi ni kuvifanya vipaumbele hivyo viwe na maana,in the sense of kuvitafsiri kwa vitendo na si porojo.Sambamba na hilo ni namna vipaumbele hivyo vitakavyoweza kuruka vihunzi vya mafisadi.

Anyway,hilo sio la muhimu sana kwa sasa kulinganisha na uwezekano wa kufanikiwa kwa hizo tahadhari tunazoelezwa.Kwanza,yote yaliyoelezwa yanawezekana kwa sababu nia ipo,sababu zipo na njia zipo pia.Kinachoweza kukwamisha utekelezaji wa mpango mzima wa kunusuru uchumi ni ufisadi.

Nilitarajia bashasha zilizoambatana na bajeti hii zingegusia ishu ya ufisadi lakini wapi!Tuwe wakweli,hivi kuna uhakika gani kuwa hizo fedha zinazotengwa kwa ajili ya kufidiwa sijui watu gani hazitaishia kwa mafisadi?Ni muhimu kuuliza hilo kwa vile akina Kagoda bado wako huru uraiani na yayumkinika kuamini kuwa watashawishika kuchangamkia tenda hii ya "kunusuriwa na mtikisiko wa uchumi wa dunia."Simple logic ni kwamba kama waliweza kuiba bilioni 40 za EPA na taasisi husika zinaogopa hata kuwataja hadharani,kwanini safari hii wasikwapue tena fedha za umma kwa "njia halali"?

Naomba nitoe mfano hao katika kupigia mstari wasiwasi wangu kuhusu hatma ya hizo tahadhari tulizopewa kuhusu mtikisiko wa uchumi duniani.Hivi karibuni ulifanyika mheshimiwa mmoja aitwaye Peter Noni aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Benki wa Raslimali Tanzania (TIB).Uteuzi huu unaweza kuashiria ni kwa namna gani kelele dhidi ya watu wanaohusishwa kwa namna moja au nyingine na ishu za ufisadi zinavyopuuzwa.Jina la Noni limekuwa likitajwa sana kwa wanaojua undani wa ishu nzima ya EPA.Sasa sijui inamaanisha nini kumpeleka sehemu kama TIB,ambayo kwa hakika itapaswa kuwajibika ipasavyo kama tunataka tahadhari ya bajeti iwe na maana.Hii si ni mithili ya kumpa "teja" usimamizi ya stoo ya madawa?

Pasipo kudhibiti ufisadi na mafisadi,yayumkinika kuamini kuwa jitihada zote hizi zitaishia kunufaisha mafisadi na nyumba ndogo zao.Ni kweli kwamba Watanzania wengi wameonyesha umahiri mkubwa wa kukabiliana na hali ngumu ya uchumi na wameshazowea "kukaza mikanda kila wanapotakiwa kufanya hivyo" lakini hii inapswa iwe kwa Watanzania wote na si walalahoi pekee.Ikumbukwe kuwa mikanda hiyo imekuwa ikikazwa tangu wakati na baada ya Vita vya Kagera,na hatujawahi kusikia tamko kwamba WAKATI UMEFIKA KULEGEZA MIKANDA HIYO.Inwezekana kuwa tamko kama hilo halijatolewa kwa vile wakati huo (wa kulegeza mikanda) bado haujafika lakini inauma kuona kufunga mikanda kwa wengi kunatoa fursa kwa walafi wachache kufumuka vitambi (kiasi cha kushindwa hata kuvaa hiyo mikanda,let alone kuikaza) kwa matendo yao ya ufisadi.

Tuweke ushkaji pembeni,tuweke siasa za 2010 pembeni,tutambue kuwa mtikisiko wa uchumi ulimwengini ni kitu halisi na hata wafadhili wetu wanasumbuliwa nao.Tukiendeleza hadithi nzuri pasipo utekelezaji mzuri,tutajikuta pabaya.Tukumbuke kwamba tulikuwa masikini kabla hata ya huu mtikisiko wa sasa.Kinachotuweka pabaya kwa muda huu ni ukweli kwamba tofauti na huko nyuma,sasa hivi wafadhili wetu nao wana matatizo pia.Na kwa vile hakuna uhakika as to lini mtikisiko huu utapungua makali,ni vema pia tukatambua kuwa wafadhili hao wanaweza kutusahau kabisa ili waweze kumudu matatizo yao binafsi.

Inawezekana,only if kukiwa na dhamira thabiti pamoja na kuweka mbele maslahi ya nchi badala vikundi vya watu wachache.Na katika hilo,tayari kuna ishara isiyopendeza kwani waliofikiriwa katika stimulus plan ni wafanyabiashara (kwa maana ya taasisi na watu binafsi) pekee huku wakulima wakipuuzwa.Yet,tunaambiwa KILIMO KWANZA!I hope sio kilimo cha fedha za walipakodi kitachopelekea mavuno mwanana kwa mafisadi na kampeni zao za 2010!

Mungu ibariki Tanzania,na waadhibu pasipo huruma mafisadi wote.


BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010











Kwa hisani ya The Daily Mail.

10 Jun 2009












"I am proud of being the smallest girl. I love all the attention I get. I'm not scared of being small, and I don't regret being small",says Jyoti Amge,a 1ft 11 tall Indian girl.For more about this smallest girl in the world CLICK HERE.


















Pics from The Daily Mail

9 Jun 2009


Kukua kwa teknolojia kuna faida na hasara zake.Kuna nyakati faida huwa kubwa kuliko hasara,na kinyume chake.Kuna nyakati faida huwa kubwa zaidi kwa eneo au sekta flani na hasara kuwa kubwa zaidi kwenye eneo/sekta nyingine.Na ndivyo ilivyo kwa athari za teknolojia ya intaneti kwa "boksi la uzembe" (runinga au televisheni).

Ni dhahiri kwamba kinachoifanya intaneti "iipige bao" runinga ni nafasi ya mtumiaji katika kutumia chombo husika.Chukua mfano huu: unataka kutafuta nafasi za masomo na/au ufadhili sehemu mbalimbali.Unajua mahala mwafaka pa kwenda ni kwa Da Subi.Unafika hapo,unaambiwa "scholarships zitaletwa kwenu saa 2 kamili usiku"!Mfano huo wa kufikirika unasaidia kuonyesha ni kwa namna gani runinga imeendelea kuhodhi uhuru na wepesi wa kupata na kutafuta habari.Kwa upande mwingine,kwa kutumia mfano huohuo,mtumiaji ana uhuru wa kwenda moja kwa moja kwenye tovuti ya Da Subi,au ku-google maneno kama "nukta 77","Subi","Scholarships",nk.


Kingine kinachoikwaza runinga ni namna watumiaji wanavyoweza "kujichanganya" (sio kuwa confused bali namaanisha interactivity).Japo teknolojia ya runinga inajitahidi kwenda na kasi hiyo ya "kujichanganya",kwa mfano kwa kukaribisha maoni yanayoweza kusomwa "laivu",kupiga kura kwenye vipindi kama Big Borther,American Idol,nk,au kutuma video na picha kama ilivyo kwa i-Report ya CNN,ukweli unabaki kuwa maendeleo hayo ni "cha mtoto" ukilinganisha na internet inavyowezesha mambo kwenye social networks kama facebook,myspace,nk.




Kama hiyo haitoshi,mtumiaji wa intaneti anaweza kuangalia runinga pasipo na matatizo (ali mradi kompyuta yake iwe na vifaa stahili na spidi mwafaka) ilhali ku-access intaneti kwenye televisheni bado ni tatizo japo baadhi ya vinajitahidi kumwezesha msomaji kutembelea kurasa flani flani.Tatizo bado linabaki kuwa kurasa hizo ni chache na zinaamuliwa na kituo husika


Wanaopenda uhuru wa kufanya mambo wanavyo taka wao wanaiona teknolojia ya runinga kama ya "kidikteta" ambapo ushiriki wa mtumiaji ni mdogo zaidi kulinganisha na ule wa kwenye intaneti.Unapoingia mtandaoni,huhitaji kuangalia "ratiba ya vipindi" (kama ilivyo kwenye tv) bali una uhuru wa kuzurura upendavyo.


Kwa mujibu wa kituo cha runinga cha Channel 4 cha hapa Uingereza,idadi ya vijana wanaoangalia televisheni imekuwa ikishuka kwa kasi kubwa kulinganisha na matumizi yao ya intaneti.Na pengine katika kutambua hilo ndio maana hata gwiji la umiliki wa vyombo vya habari,Rupert Murdoch,aliamua kununua tovuti ya "kujichanganya" ya Myspace.Tajiri huyo ni mmiliki wa Fox News,Wall Street Journal,New York Times,Sky na mlolongo wa vyombo vya habari duniani anaamini kuwa future ya sekta ya habari iko kwenye intaneti.

Unaonaje?

8 Jun 2009


WHY SHOULD WE ALWAYS LESS,IF NOT NOTHING AT ALL?HIVI TUNGEKUWA NA WAWEKEZAJI NCHINI INDIA (WANAKOTOKA WABABAISHAJI WA TRL) HALAFU WASHINDWE KUKIDHI MATARAJIO YA WAHINDI,UNADHANI WASINGETIMULIWA?POROJO KWAMBA PASIPO TRL HUDUMA ZA RELI YA KATI NDIO KWISHNE HAZIINGII AKILINI HATA KIDOGO.KAMA TUNAWEZA KUWALIPA WABUNGE WETU MAMILIONI YA SHILINGI KILA MWEZI PASIPO KUHITAJI MSAADA WA WAWEKEZAJI,SIONI KWANINI TUSHINDWE KUMUDU UENDESHAJI WA HUDUMA YA TRENI RELI YA KATI.




Abiria 552 waliotakiwa kusafiri na treni ya kati juzi, wamekwama jijini Dar es Salaam baada ya wafanyakazi wa Kampuni ya ReliTanzania (TRL), kugoma kwa lengo la kushinikiza uongozi wa shirika hilo, kusaini mkataba wa Maisha Bora unaojulikana kwa jina la Mkataba wa Hiyari.

Wakizungumza na 'HabariLeo Jumapili' katika nyakati tofauti, baadhi ya abiria waliokuwa wakitarajia kwenda Tabora, Mwanza na Kigoma, walisema walipaswa kusafiri juzi lakini ilipofika saa mbili usiku, walitangaziwa kuwa safari hiyo haipo na kutakiwa kusubiri hadi kesho yake (jana) kujua hatma ya safari hiyo.

“Kweli tulisubiri na ilipofika leo (jana) saa tano, tulitangaziwa kuwa safari haitakuwapo hivyo tujipange kwenye mstari ili turudishiwe nauli zetu. “Sisi tumefedheheshwa sana na kitendo hiki hivyo tunaiomba serikali ichukue hatua madhubuti ili abiria wanaotegemea usafiri wa treni wasiendelee kuumia,” alisema abiria aliyejitambulisha kwa jina la Masanja Said.

HabariLeo Jumapili imeshuhudia abiria wakiwa katika mistari mirefu wakisubiri kurejeshewa fedha za nauli wakati watoto na wazee walikuwa wamelala sakafuni kwenye jengo la kampuni hiyo. Meneja Uhusiano wa TRL, Midladjy Maez, alisema mgomo huo hautambuliki kisheria kwa kuwa viongozi wa Chama cha Wafanyakazi wa Reli (Trawu) wanasema hawajatangaza mgomo.

“Baada ya wafanyakazi kugoma, uongozi uliwasiliana na viongozi wa Trawu lakini viongozi hao walisema hawajatangaza mgomo kwani kisheria tangazo la mgomo linatolewa saa 48 kabla ya kuanzamgomo. Hata hivyo hakuna tangazo lolote wala kiongozi wa mgomo hajulikani,” alisema Meaz.

Inadaiwa kuwa wafanyakazi hao waligoma baada ya viongozi wa Trawu kuwapatia ripoti kwamba uongozi wa kampuni umegoma kusaini mkataba wahiyari na kwamba uongozi umeondoa kipengele kinachomtaka mwajiri kuwalipa wafanyakazi wanaopunguzwa kazi mishahara ya miezi 20 hadi 40 kama mkono wa heri.

Meaz alisema, uongozi wa TRL uliamua kurejeshea abiria fedha zao baada ya juhudi za kuwataka wafanyakazi hao kusitisha mgomo kutozaa matunda. Alisema uongozi umejaribu kuwasiliana na TRAWU Taifa na kujibiwa kuwa hakuna mgomo ila ni shinikizo.

“Tatizo haijulikani nani kiongozi wa mgomo, kila anayeulizwa anasema hajui lolote. Kisheria hakuna mgomo lakini katika hali halisi wafanyakazi wamegoma na ndio maana abiria wamerudishiwa fedha zao za nauli,” alisema Meaz. Juhudi za kuwapata viongozi wa Trawu haikuzaa matundakwa kuwa ofisi zao zilikuwa zimefungwa pia simu za mkononi zilikuwa zimefungwa.

CHANZO: Habari Leo


Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.