20 Apr 2012


Pinda kumfuata Lowassa

• HATMA YA MAWAZIRI WATANO MIKONONI MWA JK

na Mwandishi wetu

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, sasa yuko katika hatari ya kuondolewa madarakani kwa kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kufuatia tuhuma nzito za ubadhirifu wa fedha za umma unaodaiwa kuwahusisha mawaziri watano wakiongozwa na Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo.

Akiwasilisha majumuisho ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe, aliliambia Bunge kuwa kuanzia leo wataanza kukusanya saini za wabunge wenye nia ya kupiga kura hiyo na kwamba uamuzi wake utawasilishwa bungeni Jumatatu wiki ijayo.

Mwenyekiti huyo alisema ikiwa mawaziri hao ambao hata hivyo hakuwataja majina mmoja baada ya mwingine hawatakuwa wamejiuzulu wenyewe hadi kufikia siku hiyo, basi wabunge watamwondoa Pinda madarakani kwa kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye.

Kwa hali hiyo, Zitto alisema kuwa itakuwa ni jukumu la mawaziri hao kabla ya Jumatatu wiki ijayo kuamua wenyewe kujiuzulu au kumwacha waziri mkuu atimuliwe.

Hatua hiyo ya Zitto ilitokana na hoja iliyokuwa imetolewa mapema na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), ambaye aliwataka wenyeviti wa kamati za Bunge wakati watakapokuwa wanajumuisha hoja zao kupendekeza kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu Pinda ikiwa mawaziri wake hawatakuwa wamejiuzulu wenyewe.

Lissu alisema wakati wa kupiga kelele umekwisha, na sasa wanachotakiwa ni kuchukua hatua, kwani mamlaka hiyo wanayo kwa mujibu wa Katiba.

“Waziri Mkuu wajibika kwa madudu ya serikali. Nitaomba wenyeviti wa kamati hizi wanapomalizia mjadala huu kupendekeza kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kwa kujenga mfumo wa siasa wa udokozi. Tukifanya hivyo wananchi watatuamini. Ninyi chama tawala ndio mnaosababisha haya kama mtatumia wingi wenu sawasawa tutafanikiwa, sisi tupo wachache.

“Badala ya kupiga makofi, chukua hatua kwa uozo huu. Mkifanya hivyo mtaheshimika na msipofanya hivyo mtaingia kwenye vitabu vya historia,” alisema.

Alisema masuala ya ufisadi yamekuwa yakizungumzwa na zaidi ya miaka 10 sasa, lakini hawajawahi kuona serikali ikichukua hatua.

“Wakati kila mwaka CAG anatuletea taarifa za wizi, hatujawahi kuona serikali ikichukua hatua dhidi ya wahusika. Hatujawahi kuona mtendaji amechukuliwa hatua wala waziri kuwajibika katika hili. Watu wanapata kupata nafasi za uwaziri ili kuhujumu nchi,” alisema na kuongeza mfumo uliopo ni wa kulinda wezi.

Tanzania sio ya CCM

Akichangia mjadala huo, asubuhi na pia jioni, Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM) aliwafyatua mawaziri kadhaa akisema kuwa wanaongoza kwa kutafuna pesa za Watanzania na kumtaja Waziri wa Fedha Mustafa Mkullo kuwa kinara wa wizi huo.

Mbunge huyo alisema baadhi ya mawaziri wamegeuka kuwa mchwa wanaotafuta fedha za Watanzania bila woga na kuongeza kuwa sasa umefika wakati kwa wabunge kuweka tofauti za kisiasa pembeni na kuzungumza kwa umoja masuala yanayoliangamiza taifa, na katika hilo akadai kuwa hatakuwa tayari kuwaachia mawaziri wachache waangamize nchi.

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.

“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,” alisema mbunge huyo.

Awali Filikunjombe alisema Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, alikuwa amelidanganya Bunge kwa kudai amefuata maagizo yote ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Alisema kuwa ana ushahidi wa kutosha jinsi mawaziri hao wanavyoitafuna nchi na kuhoji Bunge linachukua hatua gani inapobainika mawaziri wamelidanganya Bunge.

“Waziri Chami amedai kuwa ametekeleza agizo la kamati kuhusu uchunguzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS). Uchunguzi ulifanywa wakati mkurugenzi alikuwa akiendelea na kazi, wakati kamati ilishauri wakati wa uchunguzi mkurugenzi huyo awekwe pembeni,” alisema.

Kutokana na kauli hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa shughuli za serikali bungeni, alimtaka kuthibitisha madai kuwa mawaziri wote ni wezi kwa kukabidhi ushahidi na kama hana uhakika na anachozungumza afute kauli hiyo. Hata hivyo, mbunge huyo alisisitiza kuwa alichosema ni kwamba mawaziri wengi ni wezi na si wote.

Mbunge wa Kasulu, Moses Machari, alisema wabunge wanaotaka mawaziri na wabadhirifu kunyongwa wanafanya hivyo wakiwa na akili timamu kwa sababu wamechoshwa na wizi wa waziwazi unaofanywa na mawaziri na baadhi ya viongozi wa serikali bila kuchukuliwa hatua yoyote.

Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Mjini, Vicent Nyerere (CHADEMA), alitaja waziwazi majina ya vigogo wanaomiliki kampuni za ukaguzi wa magari ambazo zilitajwa bungeni kama ni za nje, hali iliyolifanya Bunge kuzizima kwa muda.

Nyerere alisema kuwa makampuni hayo yalilipwa mamilioni ya dola za Kimarekani kwa udanganyifu, na kibaya zaidi waziri mhusika akalidanganya Bunge akidai kuwa taarifa hizo zilikuwa za uongo. Alionyesha kushangazwa kwake na nguvu kubwa ya kumlinda Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) wakati ukweli wa mambo uko wazi.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, alisema kuwa dhana iliyojengeka kuwa wizara hiyo inaibena TBS na mkurugenzi wake, haina ukweli, kwani taarifa ya kamati ndogo ya uchunguzi wa shirika hilo aliipata jana na ameshaiagiza bodi ya shirika hilo kuifanyia kazi.

Hata hivyo, alisema yuko tayari kuweka rehani uwaziri wake iwapo mbunge huyo atathibitisha kuwa kuna kampuni hewa zinazokagua magari nje ya nchi na iwapo kampuni hizo zina uswahiba naye.

“Nimekosea wapi? Kila nilichoagizwa nimetekeleza. Wizara halindi uozo. Tukilazimishwa kufanya maamuzi bila kufuata taratibu tutakuwa tunakiuka sheria,” alisema.

Ujasiri huo hata hivyo, uliyeyuka kama nta jioni, baada ya Nyerere kumuumbua kwa kutaja majina ya wamiliki wa kampuni hizo, hali iliyompa wakati mgumu waziri huyo.

Mbunge wa Nkasi, Ali Kessy (CCM), alishauri Rais Kikwete kuacha upole na kuwashughulia wote wanaotafuna mali za umma.

“Mawaziri walioshindwa kazi waondolewe na wawekwe wengine. Hakuna aliyesomea uwaziri kila mtu anaweza kuwa waziri. Unakuta kiongozi anatembea na msafara wa magari 40 unamtisha nani. Wakati watu hawana dawa wala chakula,” alisema.

Alisema kutokana na ubadhirifu huo, hata watendaji wa chini wa halmashauri wanakuwa na fedha nyingi kuliko halmashauri yenyewe, hali inayochangia kuiendesha serikali.

“Mafisadi wote tuwanyonge. Tukishanyonga 10 wataogopa. Leteni muswada mtu yeyote mwizi wa mali za umma anyongwe na mali itaifishwe. Tutaokoa nchi yetu. Wabunge tuwe wakali, lisiwe Bunge la mchezo mchezo,” alisema.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Serukamba, alisema kila wizara kuna mambo ya hivyo na kusema kinachoonekana mawziri hawajali suala hilo.

“Wabunge wa CCM twende kwenye Party Cacus tukafanye kazi tuliyotumwa. Kama kuna mtu atatulaumu basi, tuondoe waziri asiyefaa. Mbilinyi, Iddi Simba na Ngasongwa waliondolewa humu ndani. Tufanye kazi ya kibunge jamani. Nawaomba wabunge tufanye jukumu letu na tukifanya hakuna waziri atakayefanya mchezo,” alisema.

Wabunge waridhia vikao bila posho

Kutokana na uzito wa suala hilo, wabunge wameunga mkono hoja ya kuendelea na mjadala huo kwa kuongeza siku mbili zaidi hata kama vikao hivyo havitakuwa na posho.

Hoja hiyo ilitolewa na mbunge wa Buchosa, Dk. Charles Tizeba (CCM), ambaye alisema siku zilizotengwa kwa ajili ya kuchangia mjadala huo ni chache, hivyo wabunge wote walioomba kuchangia wanaweza wasipate nafasi.

“Mjadala huu ni muhimu sana, tunaomba kuongezewa siku mbili au tatu za kujadili suala hili hata kama hakuna posho tutafanya hivyo,” alisema Tizeba na hoja hiyo kuungwa mkono na nusu ya wabunge waliokuwapo ukumbini hapo.

Naibu Spika, Job Ndugai, alieleza kuwa hajawahi kuona hoja iliyoungwa mkono kama hiyo na kusema suala hilo atalifikisha kwa Spika, Anne Makinda, ambaye naye atajadiliana nayo na kamati ya uongozi na ndipo atakapotoa majibu kuhusiana na hoja hiyo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Viti Maalum, Christowaja Mtinda (CHADEMA), alisema suala la mishahara hewa limekuwa sugu katika elimu ya juu na kwamba imefikia hatua jina lake limetumika katika suala hilo.

“Pale Open University kuna mtumishi anaitwa Christowanja Mtinda. Sijawahi kuomba kazi hapo wala kufanya kazi hata siku moja,” alisema.

Aidha, alisema makatibu wakuu hawakai katika nyumba zao zilizoko Dodoma na kusema kuwa wanazitumia wakati wa bikao vya Bunge na kuhoji kwa nini nyumba hizo wasipewe wabunge ambao wanapokuwa wanahudhuria vikao vya Bunge wanapata shida kupata nyumba za kuishi.

Naye Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa, alishauri wabunge wapitishe sheria ya kuwapo kwa kamati kwa ajili mawaziri wanaoshindwa kuwajibika.

“Wenzetu wa Kenya wameanzisha sheria kwa ajili ya mawaziri wanaotoa ahadi zisizotekelezeka. Baada ya miezi miwili anaulizwa ametekeleza ahadi kwa kiwango gani, akishindwa anatimuliwa. Kenya wameshafukuza mawaziri. Tukianzisha hiyo mawaziri watahakikisha ahadi zao zinatekelezeka. Ni lazima tuwe na mahali pa kuanzia,” alisema.

Aidha, alihoji wizara kutumia fedha nyingi katika maonesho mbalimbali kama Sabasaba, Nanenane na utumishi na kuhoji yameleta manufaa gani nchini. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, imetumia sh bilioni 1.9 kwa ajili ya maonesho kama hayo katika kipindi cha mwaka 2009/2010.

Mapema asubuhi, Zitto alikuwa ameliomba Bunge kutoa kumbukumbu za mwaka jana kutokana na Waziri Aggrey Mwanri kuendelea kutoa ahadi bila kuwapo kwa utekelezaji.

“Ukichukua ‘hansard’ ya mwaka jana ukasoma maelezo ya majibu ya hoja hayana tofauti na haya anayotaka kutuaminisha leo. Mheshimiwa Naibu Spika naomba kupata mwongozo wako tupate hansard ya mwaka jana ya maelezo ya Mheshimiwa Waziri ili tulinganishe na maelezo ya sasa na aliyotolewa mwaka jana na tuone kama ametekeleza,” alisema Zitto.

Zitto alitoa kauli hiyo, baada ya Waziri Mwanri kueleza serikali imekuwa ikiingilia kati maeneo ambayo yanaona hayaendi na kusema kuwa watakapoanza kushughulikia masuala yanayolalamikiwa na wabunge wasianze kushikwa mikono.

“Tunaomba wabunge tusaidiane; tuseme hakuna kumhamisha mtumishi yeyote aliyekwenda kinyume na tutamchukulia hatua hapo hapo,” alisema.

Aidha, alisema baraza la madiwani limepewa nguvu kushughulikia matatizo yote ya halmashauri husika na kuongeza kwamba hiyo ni vita iliyopangwa na isiyopangwa.

“Hilo rungu tumeshapewa. Tuachieni. Mrema naomba tuamini. Tukitoka hapa kazi ni moja kashi kashi tu...lugha hii inatokana na mazungumzo ya hapa ndani. Halmashauri zilizopata hati chafu, zimeshakabidhiwa barua, haiwezekani sh bilioni 6 zinaondoka halafu mkurugenzi anaendelea kuwapo,” alisema.

Hatma ya mawaziri kwa JK

HATMA ya mawaziri watano wanaotuhumiwa kwa ubadhirifu wa mali ya umma sasa iko mikononi mwa Rais Jakaya Kikwete, kufuatia hatua ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi kutaka watendaji hao wajiuzulu.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya kikao cha wabunge wa CCM kilichofanyika jana mchana mjini hapa zimesema kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ameamua kulifikisha suala hilo mikononi mwa Rais Kikwete kwa uamuzi zaidi.

Chanzo chetu cha kuaminika kutoka ndani ya kikao hicho, kimewataja wabunge wanaotakiwa kujiuzulu kuwa ni pamoja na waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Cyril Chami, na Naibu wake, Lazaro Nyalandu, Waziri wa Fedha, Waziri Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),George Mkuchika, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu na Waziri wa Afya, Dk. Haji Mponda.

Katika kikao hicho cha dharura kilichokuwa chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu Pinda, wabunge hao walisema mawaziri hao wameiaibisha serikali kwa kiwango kikubwa, hali iliyosababisha wananchi kukosa imani na serikali yao na kuichukia.

Kikao hicho kilichoanza saa 7 mchana na kumalizika saa 11 jioni kilikuwa na mvutano mkali kati ya wabunge hao na mawaziri.


Mtalii akijaribu  souvenir huko Brazil


Nchi yetu inaelekea kubaya japo asilimia kubwa ya Watanzania bado wanalichukulia suala hili kama mzaha.Ukimya,upole na kutochukua hatua madhubuti dhidi ya majambazi wanaofilisi nchi yetu ni kama tumewapa ruhusa ya kufanya wapendavyo.

Moja ya makosa makubwa yaliyofanywa na Watanzania wenzangu ni pale walipoamua kuiweka nchi yetu rehani kwa kumkabidhi urais Jakaya Kikwete.Miaka yake mitano ilitawaliwa na matukio yaliyoashiria bayana kuwa TUMELIWA.Lakini makosa yakarejewa tena mwaka juzi na kwa kumpa dhamana ya 'kumalizia alipoishia.'

Kwanini ninamlaumu Kikwete?Yeye ndiye aliyewateua majambazi hawa wanaotafuna raslimali zetu kana kwamba kuna ligi ya ufisadi.Majuzi,Rais alikabidhiwa Ripoti ya Ukaguzi wa Mahesabu ya Serikali,ambapo ndani ya ripoti hiyo kuna maelezo yanayoweza kukupa ugonjwa wa moyo.Ni wizi wa hali ya juu.Lakini badala ya kuchukua hatua,Kikwete huyooo safarini.Amekwenda Brazil kwa ziara ya siku tano.Mzururaji huyu ni nadra kupitisha mwezi bila kwenda ng'ambo.

sINTOFAHAMU YAKE KATIKA UTEUZI WA MAJAMBAZI NA SINTOFAHAMU YAKE KATIKA KUCHUKUA HATUA KALI DHIDI YA WABABAISHAJI ALIOWAKABIDHI DHAMANA YA KUTUNGOZA NDIO CHANZO KIKUBWA CHA YOTE TUNAYOSHUHUDIA HIVI LEO.

Hebu soma habari ifuatayo ya kuchukiza.
Ufisadi wa mabilioni kila kona



Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo
NI KWENYE MAGARI YA SERIKALI,TANESCO,MALIASILI,MABILIONI YA JK,AFYA NA MISHAHARA HEWA
Daniel Mjema Dodoma na Fidelis Butahe
WABUNGE jana waliijia juu Serikali kwa matumizi mabaya ya fedha za umma na ufisadi ulijitokeza kwenye taasisi zake mbalimbali katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, mwaka jana.

Hasira za wabunge hao zilitokana na ripoti tatu za Kamati za Bunge; Mashirika ya Umma (POAC), Serikali za Mitaa (LAAC) na Hesabu za Serikali Kuu (PAC) kuonyesha upotevu wa mabilioni ya shilingi yaliyotumika katika nyanja mbalimbali ikiwemo mishahara hewa na mikataba mibovu.

Mbunge wa Longido (CCM), Michael Laizer alisema ni aibu kila mwaka kuwa na ripoti za wizi wa mali za umma lakini Serikali inakaa kimya.

Alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Longido, mmoja wa maofisa wake aliidhinisha Sh11 milioni kwa ajili ya matengenezo ya gari. “Labda Serikali imechoka sasa inafanya makusudi fedha za wananchi zinaliwa lakini yenyewe inakaa kimya. Serikali itujibu hizi fedha zinazopitishwa kila mwaka zinakwenda wapi?” alihoji Laizer

Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), Magdalena Sakaya alisema Serikali inapaswa kuona aibu kwa kutekeleza pendekezo moja tu kati ya 12 yaliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Alihoji suala la mishahara hewa kuendelea kujitokeza huku Serikali ikikaa kimya na kila mwaka CAG anatoa ripoti yake… “Kuna vitabu vya halmashauri za wilaya ambavyo CAG hakuvikagua kwa kuwa havikuonekana vilipo, sasa hapo tunakwenda wapi? Kuna Sh8 bilioni hazikufika katika halmashauri husika zimekwenda wapi? Wabunge tunatakiwa kuhoji na kupewa majibu sahihi.”

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari alisema sasa Tanzania imekuwa kama Saccos kwa kuwa fedha za umma zinatafunwa bila utaratibu huku vielelezo vikitoweka kusikojulikana.

“Wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki, mawaziri walijaa bungeni ila sasa tunajadili hatima ya Watanzania hawaonekani. Wabunge tuwe kitu kimoja tuibane Serikali itueleze hizi fedha zimekwenda wapi?” alisema Nassari.

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya alisema chama tawala kisipokuwa makini katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kitahukumiwa na vijana.

“Serikali ndiyo chanzo cha fedha kutafunwa… inakuwaje Naibu Waziri wa Maji anasimama na kuahidi mambo mengi wakati anajua wazi kuwa fedha za kutekeleza miradi hazipo?” alihoji.

Alisema mwaka 2015, utakuwa mgumu kwa CCM kwa kuwa wakati huo vijana watakuwa asilimia 85 na wanaweza kukinyima kura kutokana na Serikali yake kushindwa kusimamia masuala ya msingi ya maendeleo.

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee aliwataka wabunge kuacha kulalamika kwa kuwa wao ndiyo wenye rungu la kuishikisha adabu Serikali: “Tukilalamika wananchi waliotuchagua nao watatushangaa kwa kuwa wametutuma kuwawakilisha na si kulalamika.”

Alisema umefikia wakati wa wabunge kuweka itikadi za vyama vyao pembeni na kuwashughulikia mawaziri wa wizara husika ambazo zinaonekana kuwa tatizo.

Mbunge wa Mwibara (CCM), Alphaxard Lugola alimlipua Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo akisema alihusika katika uuzaji wa mali ya Serikali katika Kiwanja namba 10 Barabara ya Nyerere na kwamba anaingilia utendaji wa mashirika ya Serikali.

Alisema kuwa kiwanja hicho awali, ilikuwa kiuzwe kwa Shirika la Tanzania Motors chini ya Kampuni ya Mashirika Hodhi ya Umma (CHC) kwa Sh1.3 bilioni lakini baadaye Mkurugenzi Mkuu wa CHC alipewa barua kusitisha uuzwaji wa jengo hilo na kumtaka kuitisha mazungumzo upya na Morad Sadik, ambaye alikuwa akitaka kununua eneo hilo awali.

“Inakuwaje wizara inaingia utendaji wa taasisi au kampuni zilizopo chini yake?” alihoji.

Awali, baada ya Kipindi cha Maswali na Majibu, Wenyeviti wa Kamati hizo za Bunge; Zitto Kabwe (POAC), John Cheyo (PAC) na Augustine Mrema (LAAC), waliwasilisha ripoti za kamati zao zinazoonyesha kukithiri kwa vitendo vya ufisadi serikalini na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kamati ya PAC
Cheyo alisema kamati yake imebaini kuwapo kwa matumizi ambayo hayakupitishwa na Bunge na kutaja Maonyesho ya Sabasaba, Nanenane na Utumishi kama sehemu ambako fedha hizo zilitumika.

Alisema mwaka 2009/2010 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ilitumia fedha za matumizi ya jumla ya Sh1.10 bilioni kwa ajili ya Maonyesho ya Nanenane ambazo hazikuwamo kwenye bajeti iliyopitishwa na Bunge.

Alisema hata matumizi ya Sh21.63 bilioni zilizotumika kuendesha Mfuko wa Kukwamua Wananchi kiuchumi maarufu kama ‘mabilioni ya JK’ hazikuwapo katika bajeti iliyopitishwa na Bunge. Alipendekeza kuwa ili kuondoa hali hiyo, mfuko huo unatakiwa kuwa na mtu au taasisi ya kuusimamia badala ya kuachwa bila usimamizi.

Alisema kuwepo kwa udanganyifu na ukwepaji kodi kumeisababishia Serikali hasara ya Sh15.4 bilioni na Dola 2.6 milioni za Marekani.

Alisema Wizara ya Maliasili na Utalii na ilipoteza Sh874,853,564 baada ya kufanya uamuzi wa upendeleo wa kutoa kiwango cha chini cha mrabaha kwa mazao ya misitu.
  
Kuhusu magari ya Serikali, Cheyo alisema kumekuwa na matumizi yasiyo ya lazima katika uendeshaji na ukarabati wa magari hayo. Hadi Juni 30, 2010 Serikali ilikuwa inamiliki magari yenye thamani ya Sh5 trilioni.

Alisema mwendelezo wa ununuzi wa magari unaofanywa na Serikali unaongeza gharama za uendeshaji na kusisitiza kwamba matumizi hayo si ya lazima kwa Serikali yenye uchumi mdogo uliozidiwa na madeni.

Kuhusu ukaguzi wa magari uliofanywa na wakala chini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS), PAC imependekeza kuwajibishwa kwa ofisa masuuli wa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kuisababishia Serikali hasara ya Dola 18,343,540 za Marekani ambazo ni karibu Sh30 bilioni na kusisitiza: “Sh30 bilioni zilitumika kufanyia ukaguzi wa magari ambao haukuwepo.”

Alisema pia wamegundua kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kukodi majengo ya wizara na kusisitiza kuwa moja inaweza kulipa kodi ya Sh485 milioni.

Alisema kuna watumishi hewa takriban 3,000 na kwamba Serikali haifahamu lolote kuhusu hali hiyo… “Kuna Sh1.8 bilioni ambazo hutumiwa na Serikali kwa ajili ya kulipa watumishi hewa. Pia imebainika kuwa Serikali haijui thamani ya majengo yake yaliyopo ndani na nje ya nchi.”

POAC

Zitto kwa upande wake, alielezea maeneo yenye matatizo sugu ya matumizi ya fedha ambayo yanahusisha ukiukwaji mkubwa wa Sheria ya Ununuzi wa Umma na kanuni zake.

Alitola mfano wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), ambalo kwa mwaka mmoja wa fedha linafanya ununuzi wenye thamani ya kati ya Sh300 bilioni hadi Sh600 bilioni.

Alisema kwa mwaka wa fedha 2009/2010, Tanesco  ililitumia Sh1.8 bilioni ukilinganisha na Sh65 milioni zilizokuwa zimepangwa katika bajeti ya ukarabati wa gati mojawapo katika Kituo cha Bwawa la Mtera. 

“Ongezeko hilo la gharama za ununuzi kwa ajili ya ukarabati, ni kiasi kikubwa na Kamati haikuridhika na majibu ya menejimenti hivyo kuagiza uchunguzi wa ndani ili kubaini uhalisia wa ununuzi huo,”alisema na kuongeza:

“Tumependekeza Tanesco ianze kutumia vyanzo vyake vya umeme na iache kununua umeme hasa wa kampuni ya IPTL kwani inatumia Sh62.4 kununua umeme katika kampuni hii kwa mwaka.”
  
Alisema Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa (MUCE) kilishindwa kuthibitisha kwa wakaguzi wa hesabu uwepo wa vifaa vya maabara vilivyonunuliwa ambavyo vina thamani ya Sh267 millioni.

Katika ripoti hiyo, Zitto alisema imebainika pia mkataba kati ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), na Kampuni ya Startimes unatakiwa kupitiwa upya ili uinufaishe TBC.

Pia aliugusia matumizi mabaya ya fedha katika Bodi ya Pamba ambako alisema kuwa kiasi cha Sh2 bilioni zilizotolewa na Serikali hazijulikani zilipo na wala hazikuwafikia wakulima wa zao hilo.

LAAC

Kwa upande wake, Mrema aliitaka Serikali ivunje mtandao wa wezi wa mali za umma na kuhoji inakuwaje inawakumbatia mafisadi?
Alihoji majalada ya watuhumiwa wa ufisadi kukaa zaidi ya miaka 10 katika Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka (DPP) na ile ya Makosa ya Jinai (DCI) wakati kesi za uchaguzi zimewekewa kikomo.

Alisema ripoti ya CAG kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2010, inaonyesha kuwa Sh583.2 milioni zililipwa kama mishahara hewa kiasi ambacho alisema kingetosha kujenga madarasa 194.

Mrema alisema katika ripoti hiyo, imebainika kwamba Sh8 bilioni zilitumika katika ununuzi usiokuwa na nyaraka na ama wenye nyaraka pungufu hali inayoashiria kuwapo kwa wizi.

Aliwataja watumishi wa Halmashauri ya Kishapu akisema ni vinara wa ubadhirifu wa Sh6 bilioni na kudai kuwa walishirikiana na baadhi ya watumishi wa Benki ya NMB Tawi la Manonga, Shinyanga kuiba fedha hizo za umma.

Aliwataja watumishi hao kuwa ni Mweka Hazina, Muhdin Mohamed, Mtunza Fedha wa Halmashauri hiyo, Walugu Mussa, Boniface Nkumiming na Mhandisi wa Halmashauri, Leonard Mashamba.

Alisema fedha hizo zilitafunwa kwa kutumia nyaraka feki, uhamisho wa fedha bila idhini na kuzitumia kinyume cha malengo, uhamisho wa fedha ambao haukufika kwenye akaunti husika na malipo kwa walipaji wasiofahamika.

Mrema aliilaumu Serikali kwa kuwahamisha kutoka halmashauri moja kwenda nyingine na Serikali Kuu, watumishi wanaotuhumiwa kwa ufisadi badala ya kuwachukulia hatua za kisheria.

Kamati hiyo imependekeza Bunge likubali kuitaka Serikali kutoa maelezo ya kuridhisha ni kwa nini ubadhirifu huo umeachwa ukishamiri kwa miaka mitatu mfululizo bila wahusika waliotajwa na CAG kuchukuliwa hatua.

“Shida iliyopo hapa ni Serikali kuonekana inawakumbatia wahusika kwa kisingizio cha uchunguzi unaendelea… nini kinachochunguzwa badala ya kupeleka watu mahakamani na kumuita CAG kama shahidi?”


CHANZO: Mwananchi


CAG na madudu ya taasisi zetu

Raia Mwema Ughaibuni
Uskochi
NIANZE kwa kutoa samahani kutokana na safu hii kutoonekana katika matoleo mawili yaliyopita. Hali hiyo ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo.
Makala ya wiki hii inalenga kuamsha tafakuri kuhusu taifa letu na hatma yake. Na pengine njia mwafaka ya kuanzisha tafakuri hiyo ni kwa ‘mchapo’ ufuatao (ambao nilishawahi kuutumia huko nyuma).
Miaka machache iliyopita nilipokuwa safarini kutoka jijini London kuja huku Uskochi nilipata nafasi ya kuzungumza na babu mmoja wa Kiskochi ambaye aliwahi kuishi huko nyumbani Tanzania pamoja na sehemu nyingine mbalimbali za Bara la Afrika.
Maongezi yetu yalilenga zaidi katika tofauti zilizopo kati ya nchi za Afrika na Ulaya, na hususan kati ya Tanzania na Uingereza. Na moja ya maswali aliyonidadisi babu huyo, na ambalo linaendelea kunigusa hadi leo, ni hili: kwa nini nchi yangu ni masikini licha ya utajiri mkubwa ilionao?
Katika ‘kujitetea’ nilikimbilia hoja ya kuwalaumu wakoloni, nikajitutumua na kudai kwamba laiti mkoloni asingekuja Afrika basi huenda bara hilo lingeweza kuwa na kiwango sawa (au zaidi) cha maendeleo kulinganisha na nchi kama Uingereza.
Lakini ‘utetezi’ wangu haukuwa na uhai mrefu kwani babu huyo alizidi kunitupia maswali yaliyopelekea nikose majibu ya maana. Kwa mfano, alikiri kwamba ni kweli ukoloni ulichangia kudumaza maendeleo ya Afrika lakini kwa nini hoja hiyo iendelee kutumiwa kama kisingizio takriban nusu karne tangu nyingi za nchi za bara hilo zipate uhuru?
Baada ya kuniona ‘ninatapatapa’ na sina majibu ya kueleweka, mzee huyo akaamua kunipa msaada kwa kubadili ‘maswali na majibu’ kuwa mjadala wa pande mbili. Alidai kwamba kwa mtizamo wake, tatizo kubwa linalozikabili nchi nyingi za Kiafrika lipo kwenye uongozi na wanaoongozwa (yaani wananchi).
Alieleza kwamba pengine atakuwa hawatendei haki viongozi wa Afrika kwa kuwalaumu  kwa kudumaa maendeleo ya nchi zao. Hoja yake ilikuwa kwamba wengi wa viongozi hao walifanikiwa kuingia madarakani kwa ridhaa za wananchi.
Kimsingi,  alikuwa anawalaumu wananchi wanaohadaika kuwachagua viongozi wabovu lakini badala ya kuwang’oa madarakani kila zinapojitokeza fursa za kufanya hivyo, wananchi hao wanaendelea kuhadaiwa. Babu huyo alidai kuwa takriban kila Mwafrika anayekutana naye analalamika kuhusu viongozi wa nchi yake, lakini ni nadra kusikia mtu mwenye angalau ufumbuzi wa tatizo la kulalamikia. Alieleza bayana kuwa matatizo ya nchi kama Tanzania hayawezi kuisha kwa lawama.
Akaeleza kuwa Uingereza ‘ya kisasa’ tuliyonayo leo ni matokeo ya jitihada zilizofanyika miaka mingi iliyopita. Mzee huyo akatanabaisha kuwa kwa mtizamo wake anaona nchi nyingi za Kiafrika zinaendeshwa kwa mihula ya utawala wa kiongozi (yaani kwa vipande vya muda) kiasi kwamba ni vigumu kubashiri hali itakuwaje kwa mfano miaka 50 ijayo.
Akanipa mfano wa jinsi mifumo ya reli za ardhini mijini (underground railways) na ule wa reli ya chini ya bahari unaounganisha Uingereza na Bara la Ulaya kupitia Ufaransa (Eurotunnel) ilivyotokana na mtizamo ya kuangalia miaka kadhaa mbele.
Akaeleza kuwa wengi wa Waingereza walioshiriki kubuni na kutekeleza miradi hiyo hawakuwa wakifikiria kizazi chao tu bali vizazi vingi vijavyo mbeleni.
Akaendeleza mjadala kwa kutupa lawama kwa viongozi wengi wa Afrika ambao aliwaita walafi na wasio na chembe ya uzalendo. Alibainisha kuwa ulafi wa viongozi hao huonekana bayana katika maisha yao ya anasa licha ya kuzungukwa na mamilioni ya wananchi ambao ni masikini kupindukia.
Kuhusu kukosa uzalendo alitoa mfano wa rafiki yake mmoja aliyejitolea kupelekea mradi mmoja wa maendeleo barani Afrika lakini serikali ya nchi husika ikamkwamisha kwa vile hakukubali kuwapa rushwa (haingii akilini kudai rushwa ili uruhusu usaidiwe).
Tukiweka kando maongezi yangu na babu huyo wa Kiskochi (ambaye tunaendelea kuwasiliana kujadili masuala mbalimbali ya Afrika, na hususan Tanzania), ni muhimu kwa kila mwenye uchungu na nchi yetu ajaribu kuangalia ni kwa namna gani anaweza kuchangia kubadili mwenendo wa mambo.
Majuzi, Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utouh, aliwasilisha ripoti kwa Rais Jakaya Kikwete, ambapo kama ilivyokuwa huko nyuma, imethibitika kuwa kuna ufisadi wa kutisha unaoendelea huko nyumbani.
Kilichonigusa zaidi ni changamoto aliyotoa Utoh kuhusu deni la Taifa ambalo limepanda kutoka shilingi trilioni 10.5 mwaka wa fedha 2009/10 hadi shilingi trilioni 14.4 kwa mwaka 2010/11, na misamaha ya kodi ambayo imeongezeka kwa takriban asilimia 49.
Ni vema tukafahamishana kuwa deni hilo la Taifa lina madhara kwetu na kwa vizazi vijavyo hasa ikizingatiwa kuwa badala ya kuwekeza nguvu kwenye kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, watawala wetu wanachuana kutuongezea mzigo huo.
Moja ya maeneo yanayoongeza mzigo huo  ni safari za viongozi wetu nje ya nchi. Tusiume maneno, moja ya mizigo mikubwa anayobebeshwa mlipakodi wa Tanzania inachangiwa na hizi safari zisizoisha za viongozi. Haiingii akilini hata kidogo kuona viongozi wa moja ya nchi masikini kabisa duniani wanakuwa ziarani nje ya nchi mara nyingi zaidi ya viongozi wa mataifa tajiri duniani kama Marekani, Uingereza, Ujerumani, Japan.
Hata kwa majirani zetu ambao wanatajwa kama ‘matajiri wanaochipukia Barani Afrika’ yaani nchi kama Rwanda na Msumbiji, viongozi wao hawasafiri mfululizo kama wa kwetu.
 Sawa, hata tukiafiki porojo kuwa inabidi wasafiri kwenda kutembeza bakuli huko nje. Lakini kama hilo ni la muhimu zaidi basi tufunge balozi zetu. Maana hata hizo balozi nazo zinatajwa katika takriban kila Ripoti ya CAG kama vinara wa matumizi yanayokiuka taratibu.
Awali niliposikia kuwa misamaha ya kodi imeongezea takriban mara dufu nikahisi labda ni katika utekelezaji wa sera ya Kilimo Kwanza (ambapo ni muhimu kutoa misamaha kwenye pembejeo zinazoingizwa nchini kuinua sekta ya kilimo) au katikaimports zinazolenga sekta muhimu za elimu, afya, nk. Kinachokera ni ukweli kwamba asilimia kubwa ya misamaha hiyo ilitolewa kwa mawaziri na wabunge.
Jamani, hawa watu wanaopata mishahara minono na posho lukuki wanapewa misamaha hiyo ili iweje? Au ndiyo yale yale ya ‘mwenye nacho ataongezewa na yule asiyenacho ataporwa hata kile kidogo alichonacho’?
Kama ambavyo yule babu wa Kiskochi alivyotahadharisha, tunaweza kukesha tukimlaumu huyu na yule lakini hali yetu inazidi kuwa mbaya huku wenzetu kama Rwanda wanamudu kutoka ‘kwenye majivu’ (mauaji ya kimbari) na kufikia hatua ya kuitwa economic tiger wa Afrika.
Tafakari. Chukua hatua.


13 Apr 2012


Go!go It’s My Birthdayyyy!!!

SISTER Stands For



S stands for sincerity, that your world is filled with,


I stands for innocence, of your mind that makes you so rich. 


S stands for strong, that describes your heart best,


T stands for talented, that makes you stand out from the rest. 

E stands for encouraging, just the way you always do,

R stands for rare, and my dearest sister that's true.

Happy Birthday to you! 





12 Apr 2012

Kisiwani Zanzibar walikusanyika kundi la watu katika baraza la wawakilishi wakitaka kuitishwe kura ya maoni.
Wananchi wa Zanzibar wataka kuitishwe kura ya maoni
Wananchi wa Zanzibar wataka kuitishwe kura ya maoni
Huko Zanzibar Tanzania, kundi la watu walikusanyika leo (11.04.2012) katika viwanja vya baraza la wawakilishi wakidai kuitishwa kura ya maoni kuhusu suala la Muungano kati ya iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar 1964 na kuundwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliopo hii leo.
Mohamed Abdul-rahman alizungumza na Rashid Hadi anayedaiwa kuwa kiongozi wa kikundi hicho na kwanza anaelezea sababu za kukusanyika kwao.
(Sikiliza maogezi hayo hapa chini)


Mwandishi: Mohammed Abdul-Rahman
Mhariri: Daniel Gakuba

11 Apr 2012

8 Apr 2012



Mwasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mzee Edwin Mtei, amezungumzia uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Kuratibu Maoni ya Katiba iliyotangazwa majuzi na Rais Jakaya Kikwete.Katika bandiko lake kwenye mtandao wa jamii wa Jamii Forums,Mzee Mtei amepongeza hatua ya Rais Kikwete kuteua Tume hiyo na hatua nzima ya kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba tuliyonayo sasa.

Hata hivyo,mwanasisasa huyo mstaafu ambaye aliwahi kuwa Gavana wa Benki Kuu katika Serikali ya Awamu ya Kwanza,ameonyesha wasiwasi wake kuhusu muundo wa Tume hiyo huku akitafsiri kuwa muundo wa Tume hiyo unadhihirisha kuwa demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania.

Katika bandiko hilo,Mzee Mtei amehoji mantiki ya kukosekana uwiano halisi kati ya wajumbe wa Tanzania Visiwani na wale wa Bara kwa kuzingatia kigezo cha idadi ya watu,na akagusia pia kukosekana kwa uwiano wa imani ya kidini miongoni mwa wajumbe (yaani Waislam na wasio Waislam).

Tayari kauli hiyo ya Mzee Mtei inaelekea kuzua mjadala hata ndani ya Chadema,ambapo Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia chama hicho, Mheshimiwa Zitto Kabwe, amenukuliwa kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema, "Yeyote anayeangalia #TumeyaKatiba kwa misingi ya #Dini za wajumbe amefilisika kimawazo, ni kirusi dhidi ya Utanzania wetu. Azomewe"


Bandiko halisi la Mzee Mtei ni hili hapa chini (BONYEZA PICHA KULIKUZA)





7 Apr 2012

BREAKING NEWSSSSSSSSSSS: MUIGIZAJI STEVEN KANUMBA AFARIKI DUNIA

Taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya wasanii wenzake wa filamu Steven Kanumba amefariki dunia usiku huu.

Kwa mujibu na hisani ya SHAFFIH DAUDA's BLOG

30 Mar 2012

muamba

Zitto na urais: Haki binafsi isiyokidhi alama za nyakati

Uskochi
Zitto Kabwe
Zitto Kabwe
MAKALA yangu katika gazeti hili toleo la Novemba 2, mwaka jana ilihusu nafasi za vyama vya siasa huko nyumbani, katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Katika makala hiyo nilichambua changamoto zinazoikabili CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao, nikagusia nafasi na vikwazo dhidi ya CHADEMA na CUF ambavyo kimsingi, angalau vina nafasi (hata kama haba) ya kutoa upinzani kwa CCM, na hata kuing’oa madarakani.
Nilihitimisha makala hiyo iliyobeba kichwa ‘CCM dhaifu mtaji imara wa urais CHADEMA, CUF’ kwa ahadi ya kuendeleza uchambuzi huo. Leo nitaitupia jicho CHADEMA.
CHADEMA imekuwa ikipanda chati kwa kasi kiasi cha kuweza kubashiriwa kushika hatamu za uongozi baada ya Uchaguzi Mkuu, 2015.
Lakini, uwezekano wa CHADEMA kuingia Ikulu unategemea mazingira ya ndani na nje ya chama hicho. Tuanze na mazingira ya nje, ambayo pengine ni magumu zaidi si kwa CHADEMA pekee bali chama kingine chochote kile cha upinzani kumudu kuing’oa CCM madarakani.
Ukichambua kwa undani mageuzi ya kisiasa huko nyumbani utabaini bado tuna safari ndefu ya kimfumo na kisaikolojia.
Pamoja na uwepo wa vyama kadhaa vya siasa, mazingira ya kisiasa bado yanashabihiana kwa kiasi kikubwa na yale ya mfumo wa chama kimoja. Na tatizo hili limejikita zaidi kwenye vyombo vya dola. Kama kuna eneo moja ambalo mageuzi ya kisiasa yameshindwa kulibadili ni suala la kuvitenganisha vyombo hivyo na siasa.
Jeshi la Polisi limeendelea kuwa mithili ya kitengo cha usalama cha CCM. Tatizo sugu zaidi katika jeshi hilo linachangiwa na maslahi binafsi ya baadhi ya viongozi wake. Na tatizo hilo halipo Tanzania pekee bali ni mbinu inayopendelewa na watawala wengi wenye dhamira ya kuhodhi madaraka, kukandamiza demokrasia na kujitengenezea kinga dhidi ya maovu yao.
Sasa kwa vile utendaji kazi katika vyombo vya dola unaongozwa na kanuni ya ‘kidikteta’ ya kutekeleza amri bila kuhoji, mtawala akimteua shemeji yake kuongoza taasisi kama Jeshi la Polisi, ni wazi chombo hicho kitafanya kazi bila weledi wa kutosha.
Na japo wahusika watang’aka kwa nguvu zote, Idara yetu ya Usalama wa Taifa imeendelea kuwa nguzo muhimu ya mafanikio ya CCM kwenye chaguzi na hakuna uwezekano kwa chama kukamata uongozi wa nchi iwapo idara ya usalama ya nchi husika ‘haitaki’ (iwe kwa sababu za msingi au za kipuuzi).
Kwa vile utendaji kazi wao ni wa siri, chama kinachohujumiwa huishia kushangaa tu jinsi ‘kura zilivyoyeyuka’ pasipo kuwa na ushahidi wa jinsi hujuma husika ilivyofanyika.
Kwa hiyo-na hapa nisiume maneno- ili CHADEMA iweze kutimiza ndoto zake za kuingia Ikulu ni lazima mashushushu wetu waafiki iwe hivyo. Habari njema kidogo kwa chama hicho ni kwamba sio kwamba haiwezekani kabisa kwa Idara ya Usalama wa Taifa kuamua ‘sanduku la kura liamue mshindi halali wa uchaguzi.’
Tofauti na taasisi nyingine za dola, Idara hiyo haiendeshwi kama jeshi kamili bali ni nusu-jeshi (paramilitary). Hii inaweza kutoa mwanya kwa baadhi ya watendaji wa taasisi kama hiyo ‘kupambana’ na ile kanuni inayowabana polisi ya ‘kutekeleza amri bila kuhoji.’
Katika mazingira ya kinadharia, kama ikionekana ni wazi mwelekeo wa CCM ni tishio kwa usalama wa taifa, baadhi ya wazalendo ndani ya Idara hiyo wanaweza kuhakikisha si tu wanahujumu matakwa ya viongozi wanaotaka kuibeba CCM bali pia wanatumia ‘nguvu za giza kwenye chaguzi’ kukisaidia chama cha upinzani.
Kisaikolojia, vyama vya upinzani vinakabiliwa na vikwazo vikuu vitatu. Kwanza, uoga wa ‘Tanzania haiwezekani bila CCM’ na pili ni hofu ya ‘yale yale tuliyoshuhudia yakitokea Kenya,’ yaani machafuko. Sababu zote hizi ni mtaji mkubwa kwa CCM nyakati za uchaguzi.
Kikwazo cha tatu cha kisaikolojia ni hofu ya ‘je watu hawa ambao kimsingi asili yao ni CCM hiyo hiyo wanayotaka kuing’oa hawawezi kweli kugeuka wakipata madaraka na kuwa sawa au wabaya zaidi ya CCM?’
Ahueni kwa CHADEMA ni kwamba, kama mwelekeo wa wake utaendelea kuleta matumaini kwa Watanzania, na wakati huo huo CCM inazidi kugeuka uwanja wa mapambano ya wenyewe kwa wenyewe, basi wapiga kura wanaweza kuamua kuongozwa na chama tofauti.
Kwa bahati mbaya (au makusudi)-na haya ni mazingira ya ndani ya CHADEMA- tayari zimeanza dalili za mgogoro wa kuwania kuteuliwa kuwa mgombea urais.
Wiki iliyopita, Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia chama hicho, Zitto Kabwe, alitangaza kuwa kuutamani urais. Pengine hoja nzito kabisa katika waraka huo uliobeba kichwa cha habari ‘Ndio, nataka kuwa Rais’ ni kauli ya Zitto kuwa (namnukuu); "Sasa kama wananchi watasema huyu Zitto anapaswa kubeba jukumu hili mwaka 2015 tuache iwe. Kama watasema hapana wewe bado mpaka mwaka 2020 au hata 2025 tuache iwe hivyo. Pia Kama hawataki kabisa tuache iwe hivyo.
Naomba ieleweke kuwa Zitto ana haki si tu kutaka urais, bali pia kutangaza dhamira hiyo katika wakati anaotaka. Lakini kimantiki, kama ambavyo mwanasiasa huyo alivyowahi kulishutumu gazeti moja kwa kuzungumzia ilichokiita ‘zimwi la urais CHADEMA’ wakati inaomboleza kifo cha mbunge wa chama hicho, Regia Mtema, ndivyo inavyoshangaza kwa Zitto kutangaza nia ya urais ilhali chama chake kikiwa katika mapambano makali dhidi ya CCM, Arumeru Mashariki
Japo msiba wa Regia hauwezi kulinganishwa na kampeni hizo za uchaguzi, lakini matarajio ya wengi ni kuona viongozi wote wa chama hicho wakielekeza nguvu zao Arumeru Mashariki ili kushinda kiti cha ubunge. Hoja ya msingi hapa si kauli ya Zitto bali timing yake.
Na japo hakuna dalili kuwa mwanasiasa huyo machachari ‘amesusia’ kampeni za Arumeru Mashariki, uamuzi wake wa wa kutangaza nia ya urais kwa wakati huu sio tu unazua mkanganyiko usiohitajika, lakini pia unaathiri nafasi ya chama hicho kufanya vizuri mwaka 2015, hasa ikizingatiwa kuwa amana kubwa ya chama hicho bado ipo kwa Dk. Willbrod Slaa.
Naishauri CHADEMA kuwekeza nguvu kukabili vikwazo vizito vya nje ya chama hicho, badala ya kuanza ndoto za nani awe mgombea.
Wakati kila mwanachama wa CHADEMA ana haki ya kutaka nafasi yoyote ile ikiwa pamoja na urais, ni muhimu kwa chama hicho kutambua kuwa, baadhi ya Watanzania wanakiangalia kwa umakini iwapo si tu kinaweza kuwa mbadala wa CCM bali kumudu kuwakwamua kutoka lindi la ufisadi, umasikini na kudumaa kwa maendeleo.
Na kama alivyoandika Zitto, sauti ya Watanzania-wana CHADEMA na wasio wanachama wa chama hicho- iwe kigezo muhimu cha kuamua nani apewe dhamana ya kuwa mgombea wake hapo 2015 kwa kuzingatia muda mwafaka, kukubalika kwake kwa umma na uadilifu wake binafsi.


28 Mar 2012

Stylish final journey: The Rolls-Royce hearse is converted from a Phantom for those who want the ultimate send-off

Pricey: The one-off funeral chariot is thought to be worth over £400,000, according to its makers

High-spec: The Rolls-Royce hearse has a 6.75-litre V12 engine developing 453bhp and a suspension designed to be the smoothest and most comfortable on the road

Gari hili la kifahari lina thamani ya zaidi ya pauni laki nne za Kiingereza (zaidi ya shilingi bilioni moja za Kitanzania) lakini cha kuogopesha sio hiyo thamani pekee bali ukweli kwamba NI GARI LA KUBEBEA MAITI...!!!

Humiliation: Jose Gonzales has to stand carrying this sign on a street corner after his father caught him stealing $100 from his cousin
Pengine badala ya kuwabebesha mzigo walipa kodi kwa kuwapeleka gerezani mafisadi (ndoto isiyowezekana)-ambako watakula na kulala bure- adhabu mwafaka kwao ingekuwa kuwatembeza mitaani wakiwa wametundikwa mabango yenye kueleza makosa yao.Na hapa chini tunapewa darasa mwafaka la namna ya kutekeleza adhabu hiyo ya kudhalilisha.

Mzazi mmoja huko Denver nchini Marekani aliamua kumpa mwanae adhabu ya kutembea na bango linalotamka bayana kuwa "Mie ni mwizi, nimeiibia familia yangu." Angalia picha hapo juu pamoja na video hapo chini, kisha bonyeza kiungo kusoma habari kamili



CHANZO na kwa habari kamili: Daily Mail

Historic meeting: Pope Benedict XVI meets Fidel Castro in Havana


The meeting comes towards the end of the Pope's three-day visit to the Communist-run island

History in the making: Cuban leader Castro asked the Pope for a 'few minutes of his time' after he said mass in Havana, Cuba

Animated meeting: Castro is said to have asked the Pope about changes in the liturgy under the second Vatican council and what his role was

SOURCE and for more details: Daily Mail

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.