HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WATANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE,KWA WANANCHI KUHUSU HALI YA UCHUMI NCHINI NA MCHAKATO WA KATIBA MPYA, TAREHE 17 NOVEMBA, 2011
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,Mstahiki Meya,Viongozi wa Serikali,Wazee wangu,Ndugu Wananchi,
Nakushukuru Mkuu wa Mkoa na viongozi wenzako wa Jiji la Dar es Salaam kwa kuniandalia fursa hii ya kukutana na Wazee wa Dar es Salaam. Nawashukuru sana wazee wangu kwa kuitikia wito wangu huu wa kukutana nanyi. Nimefarijika sana kwa mahudhurio yenu makubwa pamoja na taarifa kuwa ya muda mfupi.Nimewaiteni wazee wangu nizungumze nanyi na kupitia kwenu nizungumze na wananchi wote wa Tanzania. Mwisho wa mwezi uliopita sikuweza kufanya hivyo kupitia utaratibu wetu wa kawaida kwa sababu nilikuwa kwenye Mkutano wa Jumuiya ya Madola nchini Australia. Mwisho wa Mwezi huu nitakuwa Bujumbura kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, hivyo sitaweza kuongea na wananchi wakati huo. Lakini, yapo masuala kadhaa ambayo ni muhimu watu kupata ufafanuzi kutoka kwangu. Kwa ajili hiyo nimeona nitumie fursa hii kuzungumza nanyi siku ya leo. Leo nataka kuzungumzia hali ya uchumi na mchakato wa kupata Katiba Mpya.
Hali ya UchumiNdugu Wananchi;Katika kuelezea hali uchumi nchini, naomba nianze kwa kuelezea hali ya uchumi duniani kwani yanayotokea nchini yana uhusiano mkubwa na yanayotokea duniani. Hali ya uchumi duniani siyo shwari. Ukweli ni kwamba hali katika uchumi wa mataifa ya Marekani, Ulaya Magharibi na Japan haijatengemaa kufuatia machafuko ya masoko ya fedha na mdororo wa uchumi wa miaka miwili iliyopita. Hivi sasa uchumi wa mataifa tajiri ya Ulaya , wanachama wa Umoja wa Ulaya na hasa wanachama wa Umoja wa Sarafu ya Euro unapita katika kipindi kigumu na mashaka. Thamani ya sarafu hiyo inashuka na hata kuaminika kwake ni kwa mashaka. Mfumuko wa bei umepanda, ukosefu wa ajira umeongezeka na ipo hofu kubwa ya uchumi wa nchi hizo kudorora tena. Lakini nchi hizi ndiyo masoko makubwa ya bidhaa zetu, watalii na bidhaa za viwandani. Hivyo, athari zao zinatugusa na sisi. Kuongezeka kwa mfumuko wa bei kunaongeza bei ya bidhaa tunazonunua kutoka kwao. Aidha, kutetereka kwa uchumi wao nako kumepunguza masoko ya bidhaa zetu.Lakini kulegalega kwa sarafu ya Euro kumesaidia kuimarika kwa sarafu ya dola ambayo kabla ya hapo ilikuwa imepungua nguvu. Kwa sababu hiyo thamani ya sarafu ya dola imepanda duniani ikilinganishwa karibu na sarafu nyingine zote pamoja na yetu. Wakati huo huo bei ya mafuta imeendelea kupanda duniani kutoka dola 76.1 kwa pipa Septemba,, 2010 hadi dola 100.5 Septemba, 2011. Jumla ya yote haya ni kuongezeka kwa mfumuko wa bei kutoka asilimia 4.2 Oktoba, 2010 hadi asilimia 17.9 Oktoba, 2011.Ndugu Wananchi;Serikali na vyombo husika vimekuwa vinachukua hatua mbalimbali kukabiliana na matatizo ya kushuka kwa thamani ya shilingi, bei ya mafuta, bei ya sukari na matatizo ya umeme. Kuhusu kushuka kwa thamani ya shilingi Benki Kuu imeendelea kuchukua hatua zilizopo ndani ya mamlaka yake hususan kubana ulanguzi wa fedha za kigeni, kudhibiti matumizi ya fedha kigeni kufanyia malipo hapa nchini na kuongeza fedha za kigeni katika masoko ya fedha. Kwa kweli uwezo wao una ukomo. Jawabu la uhakika lipo kwenye uchumi wa mataifa makubwa kuchukua hatua thabiti kuimarisha uchumi wao ili thamani ya dola irejee mahali pake stahiki na bidhaa zetu zipate masoko ya uhakika na bei nzuri ili mapato yetu ya fedha za kigeni yaongezeke.Kwa upande wa mfumuko wa bei, ni vyema tukatambua kuwa Asilimia 75 ya ongezeko hili imetokana na kupanda kwa bei ya chakula na mafuta. Asilimia 25 iliyobaki imechangiwa na sera za fedha. Kwa upande wa mafuta, tunaamini utaratibu wa kuagiza mafuta kwa pamoja utasaidia kudhibiti bei za ndani za bidhaa hiyo. Aidha, itsaidia kupunguza makali ya athari ya bei za dunia zinazopanda. Kwa upande wa bei za vyakula, tatizo kubwa ni uhaba wa chakula katika nchi jirani unaosababisha wote kututegema sisi na hivyo kupandisha bei nchini. Tunaendelea kudhibiti magendo ya chakula na wakati huo kutengeneza taratibu rasmi za kuziuzia chakula nchi jirani.Kwa upande wa sukari tumeamua kuruhusu tani 120,000 ziagizwe ili kupunguza uhaba wa bidhaa hiyo na kushusha bei yake.
Hatuko Peke Yetu
Ndugu Wananchi;Ni vizuri tukafahamu kuwa, matatizo ya mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya fedha yetu siyo yetu peke yetu. Nchi zote za Afrika Mashariki zinakabiliana na matatizo haya. Kwa mfano, mfumuko wa bei kwetu ni asilimia 17.9, Kenya wako asilimia 18.9 na Uganda asilimia 30.5. Wakati mwaka wa jana sote tulikuwa kwa watani karibu asilimia 5. Kwa upande wa kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya dola sote tumeathirika. Shilingi ya Tanzania imeshuka kwa asilimia 9.4, Kenya kwa asilimia 6.8 na Uganda kwa asilimia 17.4. Randi ya Afrika Kusini kwa asilimia 18.7, Rupia ya India kwa asilimia 9.8, Pauni ya Uingereza kwa asilimia 6.6. na Euro kwa asilimia 9.7.Ndugu Wananchi;Katika kukabiliana na tatizo la umeme, Serikali inaendelea kutekeleza mpango wa dharura wa kuongeza uzalishaji wa umeme. Serikali imewawezesha TANESCO kukodi mitambo ya kuzalisha umeme kutoka kwenye makampuni ya Symbion (112 MW) na Aggreko (100 MW) na kununua mafuta ya kuendeshea mitambo ya IPTL (100 MW).Napenda niwahakikishie wananchi kuwa, ifikapo Desemba, 2011 hali ya upatikanaji wa umeme itakuwa nzuri na mgao utapungua sana baada ya kufunga mitambo mingine mipya ya kuzalisha umeme ya TANESCO (160 MW) na Symbion (60 MW). Mikakati tuliyonayo ya muda mrefu ni kuongeza mitambo zaidi na kuongeza upatikanaji wa gesi ya kuendeshea mitambo kwa kujenga bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam.Mchakato wa KatibaNdugu Wananchi;Kama mtakavyokumbuka tarehe 31 Desemba 2010 katika hotuba yangu ya kuuaga mwaka 2010 na kuukaribisha mwaka 2011 nilizungumzia maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika ambayo sasa ni Tanzania Bara tarehe 9 Desemba, 2011. Miongoni mwa mambo ambayo niliyataja kuwa tutayafanya katika kusherehekea siku hiyo adhimu ilikuwa ni kuanzisha mchakato wa kuitazama upya Katiba ya nchi yetu kwa nia ya kuihuisha ili hatimaye tuwe na Katiba mpya.Nilifafanua siku ile kwamba tunataka kufanya hivyo si kwa sababu Katiba yetu ya sasa ni mbaya, la hasha! Nilieleza kwamba Katiba yetu ya sasa ni nzuri na imelilea vyema taifa letu. Tuna nchi yenye amani, utulivu na umoja pamoja na watu wake kuwa wa rangi, makabila, dini na itikadi mbalimbali za kisiasa. Tunayo nchi ambayo imepiga hatua kubwa sana ya maendeleo ukilinganisha na ilivyokuwa miaka 50 iliyopita. Pamoja na hayo tunataka kuihuisha Katiba yetu ili tuwe na Katiba inayoendana na Tanzania ya miaka 50 baada ya Uhuru wa Tanzania Bara, Tanzania ya miaka 47 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na Tanzania ya miaka 47 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.Kwa ajili hiyo nilielezea dhamira yangu ya kuunda Tume Maalum ya Katiba yaani Constitutional Review Commissionitakayojumuisha Watanzania wa makundi mbalimbali katika jamii yetu na kutoka pande zetu mbili za Muungano. Aidha, nilifafanua kuwa jukumu la msingi la Tume hiyo litakuwa ni kuongoza na kuratibu mchakato wa kupata maoni ya Watanzania kuhusu nini wanachokitaka kiwemo katika Katiba yao.Tume itasikiliza maoni hayo na baadaye kutengeneza rasimu ya Katiba mpya ambayo baada ya kukubaliwa na Bunge itafikishwa kwa wananchi kutoa ridhaa yao kwa kupiga kura. Nilisisitiza kuwa mchakato huo utawahusisha Watanzania wote wa ngazi zote na popote walipo mijini na vijijini. Hapatakuwa na aina yoyote ya kuwabagua watu kwa itikadi zao za siasa, shughuli wazifanyazo, dini zao, rangi zao au jinsia zao.Ndugu Wananchi;Nilifarijika sana na kauli za pongezi kwangu na kwa Serikali kwa uamuzi wa kuanzisha mchakato wa kupata Katiba mpya. Miongoni mwa waliotoa pongezi alikuwa Ndugu Freeman Mbowe, Mbunge wa Hai na Mwenyekiti wa CHADEMA ambaye wakati akichangia hotuba yangu ya kufungua Bunge Jipya, tarehe 11 Februari, 2011; nanukuu Hansad ya Bunge aliposema “Mheshimiwa Spika, ninapenda kwenye hili, nimpongeze Rais kwa kuwa msikivu, na Rais anapofanya jema tutampongeza, Serikali yake inapofanya jema tutaipongeza na Chama chochote kitakapofanya jambo jema kwa Taifa letu, tutakipongeza. Napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa sababu moja ya msingi sana, kuridhia mabadiliko au kuitafuta upya Katiba ya nchi yetu.” mwisho wa kunukuu. Lakini siku chache baadaye Chama chake kikaja na msimamo tofauti, wakawa wanalalamikia kunyang’anywa hoja yao na kukataa Rais asiunde Tume ya Katiba na wala asihusike kabisa na mchakato huu. Tangu wakati huo wameendesha kampeni kubwa ya kutaka Rais asihusishwe kwenye mchakato wa kubadili KatibaKwa kweli watu wengi wanaoitakia mema nchi yetu walishangazwa na madai hayo na vitendo vya ndugu zetu hao. Hii si mara ya kwanza kwa nchi yetu kufanya zoezi la marekebisho ya Katiba au hata kuandika upya Katiba tangu Uhuru na Muungano. Mara zote hizo iliundwa Tume ya kukusanya maoni ya wananchi ambayo iliundwa na Rais. Ndivyo ilivyokuwa wakati wa Rais wa Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere, Rais wa Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Rais wa tatu Mzee Benjamin Mkapa. Mwalimu Julius Nyerere alifanya hivyo mara tatu. Mara ya kwanza mwaka 1963 wakati wa kubadilisha mfumo wa vyama vingi kwenda Chama kimoja, Rais aliunda Tume ya Mheshimiwa Rashid Kawawa, Amon Nsekela. Mara ya pili wakati wa kutengeneza Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 aliunda Tume ya Mzee Sheikh Thabit Kombo.Mwaka 1984 Mabadiliko ya Katiba ya 1977 yaliyoweka ukomo wa Urais na kuingiza katika Katiba Haki za Binadamu, yaliyotokana na mchakato uliokuwa ni wa Kichama, ambapo CCM ilikusanya maoni kupitia mtandao wa kichama kuanzia Matawi hadi kufikia Makao Makuu. Wakati wa Rais Ali Hassan Mwinyi wa Awamu ya Pili, kulikuwa na Tume ya Jaji Mkuu Francis Nyalali iliyotuletea mabadiliko ya nane ya Katiba yaliyoruhusu vyama vingi vya siasa. Wakati wa Rais wa Awamu ya Tatu, mzee Benjamin Mkapa kuliundwa Tume ya Jaji Kisanga iliyoleta mabadiliko ya 13 na 14 ya Katiba ya nchi.Hivyo la ajabu lipi kwa Rais wa sasa kuunda Tume ya Katiba? Amepungukiwa nini Kikatiba na Kisheria ambacho Marais wenzake walikuwa nacho katika madaraka yao? Hakipo hata kimoja! Madaraka waliyokuwa nayo Marais waliomtangulia ndiyo aliyonayo Rais wa sasa. Hajapungukiwa chochote kwa mujibu wa Katiba na Sheria za nchi. Kwa kweli hakuna hoja yoyote ya msingi ya kumuengua Rais katika mchakato wa kutengeneza Katiba ya nchi. Haipo hoja ya Kikatiba wala ya Kisheria. Hivi Rais asipounda Tume, nani aiunde Tume hiyo? Na huyo atakayeunda atapatikanaje?Juzi Bungeni msemaji wa kambi ya upinzani, katika mjadala wa Muswada wa Kuunda Tume ya Kukusanya Maonialisema Rais ni dikteta. Ama kweli “akutukanae hakuchagulii tusi” kama ulivyo msemo wa Kiswahili. Hivi mimi kweli ni dikteta? Kwa jambo lipi? Hivi ndugu zangu Rais dikteta anatoa uhuru mkubwa kama uliopo sasa wa vyombo vya habari na wa watu kutoa maoni yao? Kama mimi ningekuwa dikteta kweli nina hakika hata yeye asingethubutu kusema hivyo na kama angethubutu basi mpaka sasa asingekuwa anatembea kwa uhuru. Mimi ninachofahamu ni kuwa nasemwa kwa kuwapa watu, vyama vya siasa na vyombo vya habari uhuru mkubwa mno ambao watu wanaona unatumika vibaya kusema maneno yasiyokuwa na staha au hata matusi, fitina na kupandikiza chuki katika jamii. Labda, nijaribu kuwa dikteta kidogo watu waone tofauti yake. Naamini kungekuwa na malalamiko makubwa zaidi ya haya.Ndugu Wananchi;Mimi na wenzangu Serikalini tumefanya yote ambayo Katiba ya nchi na Sheria vinaruhusu. Ndivyo Marais walionitangulia na Serikali zao walivyofanya tena sisi tumefanya zaidi ya wao. Wote waliunda Tume za kukusanya maoni ya Katiba na wakati wa Mwalimu Julius Nyerere liliundwa Bunge Maalum la Katiba lililojumuisha Wabunge na wananchi wengine kama tulivyoamua kufanya sisi. Ilifanyika hivyo wakati wa kutengeneza Katiba ya Tanganyika kuwa Jamhuri na Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977. Sisi tulichofanya cha ziada ni kulihusisha Bunge kutunga Sheria ya Kuunda Tume ya kusimamia mchakato wa Katiba mpya na vile vile kuwapa wananchi wote ridhaa ya kuamua kwa kuipigia kura Katiba inayopendekezwa. Ni kutokana na nyongeza hii ndipo tukaona busara ya kuwepo kwa Sheria maalum ya kuongoza mchakato wa kupata Katiba mpya. Tumepanua demokrasia na kuwahusisha wananchi wenyewe siyo tu katika kutoa maoni bali pia kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu Katiba ya nchi yao, badala ya kuwaachia Wabunge na viongozi wengine Serikalini peke yao. Kwa kweli tunastahili pongezi badala ya shutuma na lawama zisizokuwa na msingi.Pia inasikitisha kuona au kuwasikia watu wanaojua wakijifanya ukweli huu hawaoni au hawajui. Baya zaidi ni pale wanapojihusisha na kupotosha ukweli na kuipaka sura isiyokuwa ya kweli kuhusu kinachofanywa na Serikali. Mimi hujiuliza kwa nini wanafanya hivi. Kwa nini wanafanya hiyana ya upotoshaji wote huu? Kwa kweli sipati majibu ya uhakika. Labda ndiyo ile dhamira ya kutaka nchi isitawalike. Au ndiyo pengine ni ile nia ya kutaka kwenda Ikulu kwa njia ya mkato. Ati kwa kutumia nguvu ya umma. Basi hata hiyo nguvu unaitumia bila ya kuwa na hoja za kweli?Ndugu Wananchi;Nayasema haya kwa sababu kumekuwepo na upotoshaji mkubwa wa jambo hili tangu baada ya hotuba yangu ya tarehe 31 Desemba, 2010 mpaka wakati wa kuwasilishwa kwa Muswada wa Sheria wa Kuunda Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliomalizika leo Bungeni. Upotoshaji wa kwanza ulikuwa ni ule wa kujenga dhana kana kwamba Serikali imewasilisha Muswada wenyewe wa Katiba mpya. Wapo watu wamefanywa waamini hivyo wakati si kweli hata kidogo. Huu ni Muswada ambao ukipitishwa, itaundwa Tume ya kukusanya maoni ya wananchi kuhusu nini wanachokitaka kijumuishwe katika Katiba yao mpya. Kwa maneno mengine, maoni yenu mtakayoyatoa wananchi kwa Tume ndiyo yatakayotumika kutengeneza Katiba mpya.
Ndugu Wananchi;Katika Muswada huu kuna mambo tuliyotaja kuwa ni ya msingi ambayo yamewekewa wigo wa kuhakikisha yanalindwa. Mambo hayo ni yale ambayo yanalitambulisha taifa letu na tunu zake kuu. Mambo yenyewe ni haya yafuatayo: Kuwepo kwa nchi yetu na mipaka yake; kuwepo kwa Serikali, Bunge na Mahakama; kuwepo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; kuwepo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar; umoja wetu, mshikamano wetu na usalama wetu; Mfumo wa uchaguzi kwa kura unaotoa fursa kwa wote; Hifadhi ya haki za Binadamu; Haki za watu; Usawa mbele ya sheria na haki; Uhuru wa kuabudu na kuvumiliana kwa imani zetu.Kumekuwepo na upotoshaji ati huko ni kuwaziba watu midomo. Siyo hivyo hata kidogo. Mambo hayo yanajadiliwa, lakini siyo kwa nia ya kuyaondoa bali kuboresha. Kwa mfano, kuhusu Muungano, tunachosema ni kwamba hatujadili kuwepo au kutokuwepo kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bali namna bora ya kuendesha shughuli za Muungano wetu. Lakini, tulichokifanya siyo kitu kigeni, hata Rais wa kwanza alifanya hivyo mwaka 1963 alipounda Tume ya Mfumo wa Chama Kimoja cha Siasa iliyoongozwa na Mheshimiwa Rashid Kawawa. Alitoa mwongozo na aliyataja mambo ya kulinda. Sisi tulichokifanya ni kuyataja kwenye sheria badala ya kuwa Mwongozo wa Rais.Ndugu Zangu, Watanzania Wenzangu;Kwani Katiba ya Nchi ni kitu gani. Katiba hutaja nchi na mipaka yake. Kwetu sisi nchi yenyewe ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotokana na kuungana kwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika. Pili, Katiba inaelezea jinsi nchi hiyo itakavyoendeshwa kwa maana ya mihimili mikuu mitatu ya dola ya Utawala/Serikali, Bunge na Mahakama. Katiba inafafanua jinsi Serikali inavyopatikana, muundo wake na inavyofanya kazi.Aidha, inaeleza jinsi Bunge linavyopatikana, jinsi linavyofanya kazi ya kutunga sheria na mahusiano yake na mihimili mingine. Vile vile, Katiba inaeleza jinsi Mahakama inavyofanya kazi ya kutoa haki, muundo wake na jinsi Majaji na Mahakimu wanavyofanya kazi. Kwa kweli mchakato wote huu unahusu hayo. Tunatakiwa kutoa maoni juu ya namna gani bora zaidi na ikiwezekana namna mpya ya kuendesha shughuli za Muungano wetu na jinsi mihimili yetu inavyopatikana na kufanya shughuli zake.Ndugu Wananchi;Jambo lingine lililopotoshwa ni dhana ya muswada kusomwa mara ya kwanza. Kwa mujibu wa utaratibu wa kutunga sheria, Miswada, husomwa mara tatu Bungeni. Muswada kusomwa mara ya kwanza ni pale unapogawiwa kwa Wabunge baada ya kuchapishwa katika gazeti la Serikali siku 21 kabla ya kuwasilishwa Bungeni. Baada ya kuchapishwa, hugawiwa kwa Wabunge. Muswada husomwa mara ya kwanza Bungeni ili kutoa fursa kwa Mheshimiwa Spika kuwasilisha Muswada huo kwenye Kamati iuchunguze na kuutolea maoni. Mheshimiwa Spika anaweza pia kuielekeza Kamati kutafuta maoni ya wananchi.Baada ya Kamati kukamilisha kazi yake, Muswada husomwa mara ya pilli ambapo Muwasilishaji atatoa hoja kwamba Bunge liujadili Muswada pamoja na kutoa maelezo ya Muswada. Mjadala huanza kwa Kamati ya Bunge kutoa maoni yake ikifuatiwa na maoni ya Kambi ya Upinzani. Wakati Kamati ya Bunge inapojadili Muswada, Waziri mhusika huwepo na mara nyingi maoni ya Kamati ya Wabunge na wadau hujumuishwa wakati Waziri anapowasilisha hoja Bungeni ya Muswada unaposomwa mara ya pili. Baada ya mjadala, Bunge hukaa kama Kamati ya Bunge zima ambapo hupitia Muswada kifungu kwa kifungu.Katika hatua hii Wabunge huweza kupendekeza mabadiliko mahsusi kwenye kila kifungu. Aidha, Waziri nae anaweza kutetea marekebisho ya Muswada. Baadaye Bunge hurejea, taarifa ya Kamati ya Bunge zima hutolewa kwamba Muswada umepitiwa kifungu kwa kifungu na kukubaliwa. Kisha Muswada husomwa mara ya tatu kuashiria kwamba Muswada umepitishwa. Mara nyingi Muswada hutokana na majadiliano katika hatua hizi zote, mabadiliko hufanywa na wakati mwingine mabadiliko huwa makubwa kiasi kwamba kufanya Muswada uliochapishwa na kusomwa mara ya kwanza na ule uliokubaliwa mwishoni uwe tofauti kabisa.Ndugu Wananchi;Muswada huu ulisomwa mara ya kwanza mwezi Aprili na kupelekwa kwenye Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala mwezi Aprili, 2011. Tangu wakati huo Kamati imekuwa ikiufanyia uchunguzi Muswada huo na kukusanya maoni ya wadau. Walisikiliza wadau Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar pamoja na kufuatilia maoni ya makongamano, magazetini na kwenye mitandao. Kisha Kamati ikayajadili na kutoa mapendekezo yake ambayo Serikali iliyasikiliza na kuyajumuisha wakati uliposomwa mara ya pili. Muswada huu haukuwahi kuondolewa Bungeni. Kwa sababu hiyo, hakuna sababu ya kurudia kusomwa mara ya kwanza kwa mujibu wa taratibu za kuendesha Bunge.Tukumbuke kwamba baadhi yao waliahidi kwamba wangetoa Katiba Mpya katika siku mia moja tu. Serikali imechukua miezi kumi na mmoja na wanalaumu kwamba eti inawahisha mchakato!! Hiyo Katiba ya siku mia moja sijui wangeipataje bila kuwashirikisha wananchi?Ndugu Wananchi;Ni kutokana na hoja hizo Spika akaamua Muswada uendelee kujadiliwa na Bunge na leo Bunge limeupitisha Muswada huo. Baadae Muswada utaletwa kwangu kwa ajili ya kutiwa saini uwe Sheria. Baada ya hapo itabakia kazi yangu na Rais wa Zanzibar kuunda hiyo Tume ili mapema mwakani kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ianze. Lengo letu ni kuwa ifikapo mwaka 2014 zoezi zima liwe limekamilika ili mwaka 2015 tufanye uchaguzi tukiwa na Katiba mpya. Itapendeza tukisherehekea miaka 50 ya Muungano na Katiba mpya. Ni matumaini yangu kwamba wananchi wote watashiriki kwa ukamilifu kutoa maoni yao kwa Tume hiyo.
Ndugu Wananchi;Nimechukua muda wenu mwingi kuyafafanua masuala haya kwa umuhimu wake. Nia ni kutaka watu waelewe maoni ya upande wa Serikali. Matatizo ya kiuchumi yanayotukabili tunaendelea kuyashughulikia. Yale yaliyo kwenye uwezo wetu tutayamaliza na yale yaliyo nje ya uwezo wetu tutaendelea kuchukua hatua za kupunguza makali. Aidha, tutaendelea kutoa wito kwa mataifa husika kuchukua hatua thabiti kutatua matatizo yao kwani tunaoumia ni wengi.Ndugu Wananchi;Kwa upande wa mchakato wa kupata Katiba mpya nawasihi Watanzania tujiandae kwa maoni ya kutoa kwenye Tume ya Katiba mara itakapoanza kazi. Kwa wale ambao hawatapata walichokitaka nawaomba warudi kundini, sote tuungane kwa hatua inayofuata. Najua wanayo maoni mengi mazuri wayatayarishe na kuyawasilisha kwa Tume itakayoundwa. Njia ya maandamano na vurugu si ya busara kufuata. Haijengi bali inabomoa, haina faida bali hasara nyingi, haina faraja bali machungu kwa pande zote. Busara ituongoze sote kuchagua njia inayojenga, yenye faida, furaha na faraja kwa wote. Tutofautiane bila kupigana. Serikali itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani na utulivu.
Mwisho
Ndugu Wananchi,Naomba nimalizie kwa kuwashukuru wananchi kwa kuwa na subira kwa kipindi chote hiki toka tutangaze nia yetu ya kuanza mchakato wa kupata Katiba mpya. Kwa mara nyingine tena nawaomba mjiandae kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata Katiba mpya mara utakapoanza ili tuendelee kuijenga na kuiendeleza nchi yetu na vile vile tuendelee kuithamini na kuitunza amani ya nchi yetu.
Mungu Ibariki Afrika!Mungu Ibariki Tanzania!Asanteni sana kwa kunisikiliza!
27 Nov 2011
26 Nov 2011
26.11.11
Evarist Chahali
EDWARD LOWASSA, Nova Kambota
2 comments
MKUU NIMEFURAHISHWA NA LOWASSA KUANZA KUANIKA UKWELI KUHUSU RICHMOND KWA KWELI NAONA ANAFANYA KILE NILICHOWAHI KUTABIRI KWENYE MAKALA YANGU YA "LOWASSA SEMA NENO MOJA TU" SASA KWA KULIONA HILO NIMEAMUA KUMTUNGIA SHAIRI HILO HAPO CHINI NAOMBA LITUNDIKE KWENYE BLOG YAKO WADAU WALISOME......
Kalamu yangu nashika, shairi nakutungia
Kamanda umeongea, kiwingu umeondoa
Hukutaka kusinzia,makosa kuyarudia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Mwananchi nimesoma, la jana nilinunua
Machoya yakatuama, dukuduku umetoa
Uliyosema Dodoma, Kwakweli yanavutia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Richmond kupasua, mapema uligundua
Kikwete ukamwambia, mkataba kuondoa
Rais akakataa, nini alitegemea?
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Nape akashikilia, lile asilolijua
Mikoani kaambaa, uzushi kang’ang’ania
Jinalo kulichafua, wewe ukavumilia
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Mapema nilitabiri, falsafa nikapinga
Magamba sikukariri, kuvuana sikuunga
Ukweli niliukiri, mantiki iso kunga
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa
Beti sita nakomea, kalamu naweka chini
Mengi nimeongelea, soma tena kwa makini
Yatazidi kutokea,kusini kaskazini
Jibu umetupatia, viva kamanda Lowassa.
Shairi limetungwa na Nova Kambota Mwanaharakati,
+255717 709618
Tanzania, East Africa
Jumamosi, November 26, 2011
25 Nov 2011
25.11.11
Evarist Chahali
TWANGA PEPETA
No comments
![]() |
| Bendi ya Twanga Pepeta wakijiandaa kuingia kwenye Pipa |
![]() |
| Chalz baba akiwa tayari kuingia kwenye Pipa |
![]() |
| Full Mzuka |
![]() |
| kikosi cha Twanga kikijiaandaa kuingia Katika Uwanja wa Julius Nyerere |
![]() |
| Kutoka Kulia Amigolous akiwapa Mikoba Jojoo, Jumanne, Baby Tall na Luiza |
![]() |
| kutoka kushoto Shalapova, Charles Baba na Shakashia |
![]() |
| Maria Soloma akiwaaga mashabiki wake Nyumbani |
![]() |
| Victor Mkambi mpiga kinanda wa Twanga akiwa na Maria Soloma ambae ni dancer wa twanga |
Twanga Pepeta ''KISIMA CHA BURUDANI'' wameondoka leo asubuhi kutoka uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere kuelekea kuvinjari katika Jiji la London ili kusugua kisigino na wapenzi wao walioko nchini Uingereza na nchi jirani ikiwa ni katika kusherehekea maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania. Kundi hilo lililokamilika katika safu zake za waimbaji, wapiga vyombo na wacheza show linatarajiwa kuwasha moto wa burudani yao siku ya Jumamosi, tarehe 26 Novemba 2011 katika Ukumbi wa Club 2000 Savoir Banqueting Suite, Popin Building Southway, Wembley HA9 0HB kuanzia saa Tatu Kamili Usiku mpaka alfajiri (9pm til late).
Mheshimiwa Balozi Peter Kalaghe atakuwa mgeni rasmi. CD za album mpya na za zamani zitauzwa na vinywaji pamoja na vyakula vya kitanzania vitakuwepo vya kumwaga. Viingilio vitakuwa £20 (singles) na £35 (couples) kabla ya saa sita (mid night) na £25 (singles) na £40 (couples) baada ya saa sita usiku.
Njoo tujumuike, njoo usugue kisigino, njoo usherehekee uhuru wa nchi yako, njoo ule na kunywa kitanzania. Burudani ni watu na watu ni pamoja na wewe. Tanzania itajengwa na watu wenye moyo kama wewe. Karibuni sana.
Shughuli hii imeandaliwa na Urban Pulse Creative wakishirikiana na Miss Jestina Blog, chini ya maelekezo thabiti ya Ubalozi wa Tanzania, London.
Tumethubutu, Tumeweza na Tunaendelea Mbele
25.11.11
Evarist Chahali
Burudani, Jose Chameleone, Picha
No comments

Mwana muziki wa kizazi kimpya ndani ya Washington DC, AJ Ubao wa kwanza (kushoto) pamoja mzee wa kuwachanganya Dmk global Dickson Mkama. wa kwanza( kulia) wakiwanyumba ya jukwa na mwana muzingi aliekuwa anasubiriwa kwa hamu siku ya jana Jumatano Nov23, 2011 katika sherehe za Thanksgiving Muimba Jose Chameleone katikatia, akisubiriwa kwa hamu na wapenzi wake 
Nyuma ya jukwa mwana dada Luren akipata flash ya pikee kabla ya unyesho kuanzaa 
Muimbaji Ana Lov akipata flash ya pamoja na rafiki yake kwenye onesho hilo la Mwanamuziki wa Uganda Jose Chameleone. 
Cheif wa swahilivilla Abou Shatry akipata picha ya pamoja na kundi zima la muimbaji kutoka Uganda Jose Chameleone. 
Aj Ubao alikuwa ni mumbaji wa pili kuimba katika onyesho hilo waliosherikiana na mwanamuziki wa kutoka Uganda Jose Chameleone, wakiwa nyuma ya jukwa akipata flash ya pamoja na mdhamin wake wapendo 
Wapenzi wa tazamaji wakisubiri kwa hamu onyesho hilo kuazarasmi ndani ya ukumbi wa Rendezvous mitaa ya Parklawn Dr, Rockville Maryland U.S 
Mwana muziki wa kizazi kimpya kwa muziki wa R&B ndani ya Washington DC, AJ Ubao akiwarusha vibaya sana wapenzi wa muziki wa nyumbani wanaoishi hapa DMV Jana jumatano Nov 23, 2011 Nchini Marekani.

Wapenzi wa muziki wakinyumbani wakiwa wanamshangaa Msanii wa hapa Washington DC, AJ Ubao 
Mwanamuziki wa Uganda Jose Chameleone akifanya vituz vyake ndani ya Rendezvous Hall mitaa ya Parklawn Dr, Rockville Maryland U.S 
Mamia ya watu jana walifurika kuja kumuangali Msanii kutoka Nchini Uganda kwa jina maarufu la Jose Chameleone, ana nyimba zake, ikiwemo mama roda, Jamalila analia, na nyingi nyenginezo. 
Mamia ya warembo waliohudhuria kwenye Show hiyo ya Mwanamuziki wa Uganda Jose Chameleone
Warembo mikono juu wakiwa wamevudiwa na uwimbaji wa mwanamuziki huyo ndani ya ukumbi uliofurika warembo wa Kiafrica. 
Juu na chini full warembo wakipata hisia za muziki wa muimbaji maarefu kutoka nchini Uganda Jose Chameleone.

Sauti ya muimbaji Jose Chameleone inayofurahisha warembo wamuziki wa kinyumbani 
Kama kawaida yake akiwa na kundizima ndani ya Washington DC Jana Jumatano Nov 23,2011 
Wakati mwengine warembo hupandwa na jazbaba wale wanaposhindwa kujizuwia na kuomba mic ili kuchombeza wimbo uliokuwa unaimbwa hewani wa kipepo

Mambo ya jana hayo cheza ni kucheze ndani ya Rendezvous Hall 
Mapozi na wewe: mrembo akipata picha kutoka kwa mpiga picha wetu 
Hivyo ndiovyo ilivyoo hakuna fitina 
Cheza nikucheze juu na chini warembo wa Kiganda ndani ya Nyumba 
Mrembo aleehudhuria ndani ya unyesho hilo kabambe la Muimbaji Kutoka Nchini Uganda Jose Chameleone 
Kwakweli ilikuwa sho ya aina yake wapenzi wengi ambao ni Waganda aliofurika na kumuunga mkono jamaa yao 
Mwana mitindo wa Uganda jina lake hatujaweza kulipata vyema lakini ni Mwanamitindo wa Uganda! 
Cheza ni kuche hiyo huku warembo wakipata flashi ya pamoja kwenye show hiyo ya Mwanamuziki wa Uganda Jose Chameleone Alivyo warusha Wakaazi wa DMV Jana Nov 23, 2011 kwenye siku kuu ya Thanksgiving Nchini Marekani.
Picha zote na http://swahilivilla.blogspot.com/
25.11.11
Evarist Chahali
Habari
No comments
![]() |
| William John |
![]() |
| Joseph Kaniki |
Wachezaji wawili wa kitanzania, Joseph Kaniki (Golota) na William John wamefanikiwa kujiunga na timu ya ligi daraja la pili KonyaSpor (KIF) nchini Sweden, baada ya kufanikiwa kupita katika majaribio( Trials). Majaribio hayo yalijumuisha wachezaji zaidi ya thelathini ambapo wachezaji watano walichaguliwa kujiunga na klabu hiyo ya ligi daraja la pili KonyaSpor (KIF)
Habari hii imeletwa kwenu na:http://www.africa4life.com/
25.11.11
Evarist Chahali
RAIA MWEMA
1 comment
Uskochi
NIANZE makala hii kwa kutoa pongezi za dhati kwa mmoja wa watoto wa Rais Jakaya Kikwete, Miraj, kwa kauli yake kuhusu vurugu zilizotokea hivi karibuni katika baadhi ya maeneo nchini.
Gazeti moja huko nyumbani lilinukuu kauli ya Miraj kwenye ukurasa wake wa mtandao wa jamii wa Facebook akisema kwamba ni makosa kukihusisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na vurugu hizo.
Kwa mujibu wa gazeti hilo, mtoto huyo wa Rais alieleza kwamba CHADEMA si nchi bali ni chama cha siasa na si wanachama wa chama hicho pekee wenye shida na matatizo bali ni Watanzania wote.
Nimelazimika kutoa pongezi hizi kwa sababu kwa kiasi kikubwa siasa za vyama vingi zimezua mazingira ya uadui na uhasama kwa misingi ya kiitikadi. Na katika hili, chama tawala CCM ambacho wengi wetu tunakiangalia kama kiongozi kwenye ulingo wa siasa, si tu kwa vile kimekuwa madarakani kwa muda mrefu bali pia ndicho kilichoridhia mageuzi ya kisiasa nchini, kimekuwa kinara wa siasa za chuki.
Miraji si mwanasiasa, lakini si tu ni mtoto wa Rais ambaye ametokana na CCM bali pia baba yake ni Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho tawala. Na japo Kikwete mwenyewe si mahiri sana kwenye siasa za uhasama kati ya CCM na vyama vya upinzani, ukimya wake pindi baadhi ya viongozi wenzie wanaofanya kila jitihada kujenga picha kuwa vyama vya upinzani havina tofauti na wahaini unaweza kuashiria kuwa naye ni muumini wa siasa za aina hiyo.
Mtoto huyo wa Rais alinukuliwa akitukumbusha kuwa, “Tofauti ni harakati na sera... tupendane Watanzania, tutafika mbali kwa umoja na mshikamano wetu na wala si kwa kejeli na matusi…, wenye haki tuwasimamie wote na penye haki tusimame sote.” Sote tunatambua kuwa tofauti zetu za kiitikadi haziongezi au kupunguza Utanzania wetu.
Japo habari hiyo haikuvuma sana lakini uzito wake unaweza kuwa na umuhimu mkubwa kwa mustakabali wa taifa letu. Wiki iliyopita tumeshuhudia jinsi baadhi ya mawaziri na wabunge wa CCM, wakiongozwa na Spika Anne Makinda, wakiwakebehi wabunge wa CHADEMA na NCCR-Mageuzi kama vile uamuzi wao wa kutoka nje ya Bunge kupinga uendeshaji wa mjadala wa mabadiliko ya Katika ni uhayawani.
Hivi kuna ugumu gani kuendesha mijadala muhimu kwa taifa kwa kutumia hoja za kiutu-uzima na mantiki badala ya vijembe na kebehi ambazo hazisaidii lolote? Hivi kama mtoto wa Rais ambaye ni kijana wa umri wa kati tu anaweza kuwa na busara za kuweka mbele maslahi ya taifa badala ya unazi wa kisiasa, inakuwaje vigumu kwa wanasiasa watu wazima ambao baadhi yao wamekuwa kwenye fani hiyo miaka nenda miaka rudi?
Baada ya pongezi hizo na mafunzo kwa wanasiasa wanaoendekeza siasa za uhasama, nigeukie kwa ufupi kuhusu mjadala wa Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba. Sitajadili kwa undani sana kwa sababu ubabe uliofanywa na CCM kuilazimisha hoja ambayo kimsingi haikuwa yao, umeikoroga akili yangu kiasi kwamba siwezi kujadili suala hili kwa ufasaha.
Lakini kwa kifupi tu, ninapenda kuwakumbusha CCM kwamba wanaweza kutumia ubabe kulazimisha matakwa yao pasipo kujali athari za ubabe huo kwa umma lakini kwa hakika ipo siku watajutia kufanya hivyo.
Kimsingi, moja ya mambo yanayolalamikiwa sana na wapinzani, wanaharakati na baadhi ya wananchi kuhusu muswada huo ni madaraka makubwa ya Rais. Nashukuru angalau, suala la Rais kupewa madaraka ya kuandaa hadidu za rejea limeondolewa kutoka mikononi mwake, katika mjadala uliopitishwa na Bunge wiki iliyopita.
Kuna mambo makubwa mawili yanayowasukuma CCM kutaka mwendelezo wa Katiba mithili ya hii inayolalamikiwa. Kwanza, Katiba hiyo imekisaidia sana chama hicho kushinda chaguzi mbalimbali na hivyo kuendelea kuwa madarakani. Chama hicho tawala kinafahamu kuwa Katiba inayokidhi mahitaji ya demokrasia ya kweli ni sawa na kitanzi kwake.
Lakini la pili ni ukweli kwamba kwa wana-CCM wengi wazo kwamba kuna siku chama hicho kinaweza kung’olewa madarakani na kuwa chama cha upinzani ni ndoto ambayo kamwe haitotimia. Maana laiti wangeamini kuwa hilo linawezekana basi wangekuwa makini kubariki muswada wenye mwelekeo wa kuzaa Katiba inayompa Rais madaraka makubwa kupita kiasi. Wangefanya hivyo kwa kuelewa kuwa laiti wakiingia kuwa chama cha upinzani, madaraka hayo yanaweza kabisa kutumika kuwakandamiza.
Na mjadala huo wa muswada wa mabadiliko ya Katiba unatoa picha ya changamoto kubwa zinazovikabili vyama vya upinzani kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao hapo mwaka 2015. Tulichojifunza katika sokomoko hilo ni kwamba chama tawala kipo tayari kufanya lolote lile kuhakikisha kinaendelea kuwa madarakani.
Japo sijapata fursa mwafaka ya mwendelezo wa makala zangu kuhusu changamoto mbalimbali kwa vyama vya upinzani katika uchaguzi huo, kilicho wazi ni ukweli kuwa kikwazo kikubwa cha demokrasia ya kweli nchini ni CCM - chama ambacho kinapenda kutuaminisha kuwa kiliridhia mageuzi ya kisiasa pasi na hofu wala kinyongo.
Vyama vya upinzani vinaweza kabisa kufanikiwa kuuza sera zao vizuri na vikafanikiwa pia kuwashawishi Watanzania watoe ridhaa kwao kuirithi CCM. Lakini kwa mwenendo huu wa siasa za kibabe ambao unarutubishwa na wingi wa wabunge wa CCM bungeni itakuwa vigumu sana kwa vyama hivyo kufanikiwa.
Na hapa tunazungumzia utaratibu wa kisiasa ambao kila mwenye macho anaouna na mwenye masikio anausikia (nikimaanisha kuwa jitihada za CCM kukwaza upatikanaji wa Katiba “safi” zimeshuhudiwa bayana). Sasa kama chama hicho tawala kinaweza kufanya mambo haya hadharani hali ikoje kwa mambo yasiyoonekana hadharani?
Kama ambavyo nimekuwa nikibainisha mara kadhaa, tatizo si CCM kuendelea kuwa madarakani. Laiti chama hicho kingeendelea kuwa cha wakulima na wafanyakazi (na si cha kulea mafisadi wanaofanya alama za jembe na nyundo zionekane kama kijiko na bunduki-kuashiria ulaji na ufisadi), basi tungekesha tukiomba kiendelee kututawala milele.
Lakini kwa vile ni wazi kuwa CCM si tu kimeshindwa kukidhi matarajio ya Watanzania bali pia kimeishiwa mbinu bora zaidi za uongozi wa taifa, kuna kila sababu ya kutoa fursa kwa wengine kutuongoza na kutukomboa kutoka katika lindi la umasikini linaloigubika nchi yetu.
Ukisoma ripoti ya Bunge kuhusu sakata linalomhusu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Davidi Jairo (na swahiba wake Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, sambamba na Waziri na Naibu wake, William Ngeleja na Adam Malima, pamoja na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Ludovick Utoh) unawezakujiuliza tena; “kama ufisadi mmoja uliowekwa hadharani uko hivi, mambo yakoje kwingineko ambako yanayoendelea huko hayajawekwa hadharani?”
Ni matukio ya ufisadi kama huo yanayowatia wasiwasi CCM kuwapa Watanzania Katiba inavyoweza kabisa kukiweka chama kingine madarakani. Wanafahamu kuwa laiti wakiondolewa kwenye utawala kwa njia halali za kidemokrasia, madudu mengine chungo mbovu ambayo yayumkinika kuamini kuwa yanaendelea hadi muda huu, yatawekwa hadharani.
Si kama nimekata tamaa lakini kuna kila dalili kwamba kutarajia kwamba CCM watajenga mazingira ambayo yanaweza kuwa chanzo chama hicho kung’oka madarakani ni ndoto ya mchana. Kila mpenda demokrasia angetamani kuona tunakuwa na chaguzi huru na haki lakini hilo ni vigumu kutokea kwa mwenendo huu.
Wakati naandaa makala hii, CCM walikuwa wanakutana huko Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine wanatarajiwa “kukaliana kooni” kuhusu suala la “kuvuana magamba.” Japo pengine si njia mwafaka, lakini misukosuko inayokikabili chama hicho inaweza kuwa ndio njia pekee inavyoweza kukisambaratisha na hatimaye kutoa fursa isiyotarajiwa kwa wazalendo wengine kuongoza taifa letu.
Sikiombei mabaya chama hicho tawala lakini kama njia za kistaarabu za kutaka mazingira mwafaka ya kidemokrasia yanayoruhusu mabadiliko zinakwamishwa na chama hicho hicho basi sioni ubaya kutamani mpasuko mkubwa utakaofanya kiishiwe pumzi ya kubaki madarakani au kuhujumu chaguzi zijazo.
20 Nov 2011
20.11.11
Evarist Chahali
TAARIFA YA MSIBA
No comments
KWA NIABA YA WASOMAJI WA BLOGU HII NINATOA POLE NYINGI KWA BLOGA MWENZETU DINAHICIOUS KWA MSIBA MKUBWA WA KIFO CHA BABA YAKE MZAZI.
KAMA MTU NILIYEKWISHAPOTEZA MZAZI,NINAFAHAMU KIBINAFSI MAJONZI NA UCHUNGU VINAVYOAMBATANA NA KUPOTEZA MZAZI.KIFO NI KIFO LAKINI CHA MZAZI KINAGUSA SANA.KWA BAHATI MBAYA,HAKUNA MANENO YANAYOJITOSHELEZA KUMFARIJI MFIWA ZAIDI YA KUUNGANA NAYE KWA SALA KUMWOMBEA MAREHEMU APATE PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE,APUMZIKE KWA AMANI.
HATA HIVYO,NILIPOFIWA NA MAMA MZAZI MWAKA 2008,PADRE ALIYEONGOZA IBADA YA MAZISHI ALISEMA HAYA: "SOTE TUMELETWA DUNIANI NA MUNGU KWA UPENDO WAKE USIOMITHILIKA.KAMA WANADAMU,TUNAPENDA TUWE PAMOJA SIKU ZOTE.LAKINI BABA YETU ALIYETULETA DUNIANI ANATUPENDA ZAIDI,NA HIVYO ANAWEZA KUTUCHUKUA WAKATI WOWOTE UKE.PAMOJA NA UCHUNGU TUNAOKUWA NAO TUNAPOONDOKEWA NA TUMPENDAYE,NI VEMA KUFAHAMU KUWA JAPO SIE TULIMPENDA MAREHEMU LAKINI BABA YETU (MUNGU) ALIMPENDA ZAIDI NA HIVYO AMEAMUA KUMCHUKUA.NA KWA VILE TUNAJUA ANA UPENDO MKUBWA BASI NA TUPATE FARAJA KUWA HUKO AENDAKO ATAPUMZISHWA KWA AMANI NA UPENDO."
NATAMBUA MANENO HAYA YANAWEZA YASISAIDIE KUPUNGUZA MAJONZI LAKINI YANAWEZA KULETA FARAJA KATIKA KIPINDI CHA MAJONZI YA MSIBA.
POLE SANA DINA,TUPO PAMOJA KATIKA SALA.
PUMZIKO LA MILELE UMPE EE BWANA NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE APUMZIKE KWA AMANI AMEN
19 Nov 2011
19.11.11
Evarist Chahali
TANZANIA DAIMA
2 comments
Kupitiwa, Uzembe au Ufisadi wa Kitaaluma (ya uandishi wa habari)?Leo ni Jumamosi ya tarehe 19 Novemba 2011 lakini tovuti ya Tanzania Daima ina habari za Jumatatu ya tarehe 11 April 2011,zaidi ya miezi saba iliyopita.Hii ni aibu kubwa kwa gazeti ambalo limejipatia umaarufu kwa kukemea ubabaishaji,uzembe na ufisadi...
HOVYOO!!!
18 Nov 2011
18.11.11
Evarist Chahali
JAKAYA KIKWETE
1 comment
Subscribe to:
Posts (Atom)















