8 Jul 2015

Ufuatao ni waraka kutoka kwa Chama cha DP kinachoongozwa na Mchungaji Christopher Mtikila kumpiga mwania nia ya Urais Edward Lowassa

KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU
TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA
Edward Lowasa ni balaa kwa Taifa!

Democratic Party (DP) inatarajia kufikisha Mahakamani chama cha
CCM pamoja na wanachama wake sita, Edward Lowasa na wengine,
kwa mujibu wa Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, kwa kosa kubwa sana la kuvunja Katiba na Sheria za Nchi kwa kuanza kampeni ya Uchaguzi kabla ya wakati unaopasa kwa mujibu wa Sheria.

1. Tunao ushahidi mzito unaothibitisha kwamba Edward Lowasa na
wenzake walianza kampeni ya urais ndani ya chama chao kabla ya
wakati, na kwamba chama chao kiliwapa adhabu ya kutofanya siasa
kwa miezi 12. Lakini safari hii Lowasa ameanza kampeni ya urais
Arusha kwa mkutano mkubwa sana wa hadhara wa kampeni haramu
na kumwaga rushwa ya kutisha!

2. Kama ni wadhamini alipaswa kuwapata katika ofisi za chama chake, katika mikoa nane (8) tu Tanganyika na mikoa miwili tu Unguja na Pemba, wadhamini 45 tu katika kila mkoa. Lakini Edward Lowasa amefanya mikutano nchi nzima, ya kuwaahidi maelfu ya wananchi katika kila mkutano wa hadhara, mambo atakayofanya kama wakimpa kura zao awe Rais! Hii ndiyo kampeni halisi, ambayo ni ukiukaji wa Katiba na Sheria za Nchi! Uchaguzi Mkuu unaendeshwa na Sheria, hivyo ni lazima Sheria ichukue mkondo wake dhidi yake kwa kuivunja.

3. Edward Lowasa amevunja Katiba ya Nchi na Sheria ya kiwango cha
fedha kinachoruhusiwa kutumika katika shughuli halali za Uchaguzi,
kiasi kwamba CCM na Taasisi zote za uchunguzi wa kifedha nchini,
upelelezi wa Jinai na Usalama wa Taifa ni mlazima wanayo kazi muhimu sana ya kupata ukweli kuhusu haya mabilioni ya fedha yanayomwagwa nchini na fisadi Edward Lowasa, ameyapata wapi na kwa namna gani, kumehusika ‘’Money laundering’ au la, kama mapato ya mapesa hayo yote ni halali, na kama mapato hayo yote yalilipiwa kodi inayopasa kwa ajili ya Taifa.

Ni marufuku kabisa tena ni makufuru Edward Lowasa kuruhusiwa
kugombea urais, kwa sababu amevunja Katiba ya Nchi na Sheria na
Kanuni za Uchaguzi. Sifa mojawapo ya kustahili kugombea uongozi wa nchi yoyote ni maadili mema na uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na
taratibu za Utawala wa Sheria
4. Edward Lowasa, kwa kujimilikisha maeneo nchi nzima kwa kutumia kifisadi Uwaziri wake wa Ardhi, ameliweka Taifa katika hatari kubwa ya mmwagiko wa damu baina ya wakulima na wafugaji, baada ya kueneza nchi nzima makundi ya ng’ombe wake, na kusababisha mapigano makali ya mara kwa mara kila mahali nchini kati ya wafugaji wake na wakulima. Kwa sababu ya uovu huu hata katika kampeni yake haramu Lowasa ameshindwa kusema lolote juu ya kilimo, ingawa ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu na ndiyo shughuli inayotunza uhai wa asilimia 95 ya wananchi!

Kwa kuwaingilia wakulima katika ardhi yao, kuwaua ovyo, kuwaonea
kiasi cha kufisha matumaini yao katika kilimo, kumeifanya kauli mbiu ya “Kilimo kwanza” kuwa porojo tu ya kisanii!

5. Edward Lowasa ni mwiko kabisa kupewa kugombea urais, kwa
sababu siyo tu aliutumia kifisadi Uwaziri wa Ardhi akajitajirisha na
kujipatia maeneo makubwa ya ardhi nchini kote, bali alitumia kifisadi
zaidi uwaziri wa nchi katika ofisi ya Waziri Mkuu, katika uagizaji wa
mashangingi ya Wabunge, mawaziri, wakuu wa Mikoa na Wilaya.

6. Edward Lowasa alikemewa mnamo mwaka 1995 na Mwalimu Nyerere anayeenziwa na CCM lama “Baba” yao, alipotaka kugombea urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, wala hakuweza kujitetea kwavile utapeli wote aliojitajirishia ulikuwa mezani. Leo baada ya mabiashara haramu mengi na kulipora sana Taifa kukiwa ni pamoja na utapeli wa “kununua mvua Thailand” na kuliibia Taifa mabilioni ya fedha kwa kutumia kampuni hewa ya RICHMOND, huyu ni fisadi-nyangumi. Ni mlemavu wa rushwa tu wa kununuliwa na mapesa machafu anayomwaga Lowasa, anayeweza kumruhusu fisadi Edward Lowasa agombee urais.

Sifa za mtu wa kukugombea Urais zimeelezwa bayana na Mwenyezi
Mungu katika Kumbukumbu la Torati 17:15-20, ambazo Edward
Lowasa hana hata mojawapo! Lowasa awali alikemewa na Mwalimu
Nyerere ambaye CCM wanamuenzi kama “Baba” yao, kuwa hafai kabisa kuwania urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, kama alivyomtangaza hata Reginald Mengi pale alipolazimika kujiuzulu Uwaziri Mkuu kwa ajili ya wizi kwa kampuni hewa ya Richmond, lakini leo akiwa fisadi la kutisha zaidi kuliko papa eti anataka urais!
Si ajabu kwamba magabacholi yalioipora vibaya sana Nchi hii kama Sigh Setti na hata Nazir Karamagi wote wamo katika genge la Edward
Lowasa! Si ajabu hata fisadi Reginald Mengi leo kuungana na fisadi
Lowasa yakizingatiwa machafu yake yeye mwenyewe, na kuhusika kwa Mengi na mauaji ya Chacha Wangwe, pamoja na mpango wa Chadema
wa kumwua Mchungaji Mtikila, waraka feki wa kujaribu kuupotosha
ukweli ukatangazwa kwa ITV yake.

Katika uwaziri wake katika ofisi ya Waziri Mkuu, na katika Uwaziri wakewa Ardhi na Uwaziri Mkuu, Lowasa alifanya ufisadi ambao katika nchi kama China zenye uchungu na maslahi ya mataifa yao angekuwa wa kupigwa risasi hadharani, lakini katika nchi yetu anatafuta urais!

7. Edward Lowasa AFYA yake imempiga marufuku kugombea Urais!
Kwa ajili ya kila ajira duniasni kote, moja ya mashart makuu ni lazima mwombaji awe na afya iliyo bora, ndiyo sababu ni lazima ajira ya kila mwombaji itegemee taarifa ya kitaalamu ya madaktari, inayothibitisha kwamba hana dosari kiafya. Sharti hili ni la lazima kwa sababu:
a. Majukumu yote atakayopewa mwajiriwa atayatekeleza kikamilifu
kwa kutumia viungo vya mwili wake, kwahiyo viungo vyake vyote
ni lazima viwe katika hali iliyo imara kwa ajili ya kazi.

b. Hata kama kwa uthibitisho wa kitaalamu wa madaktari mwajiriwa
anazo akili nzuri kichwani mwake, akiwa na hitilafu katika viungo
vingine vya mwili wake huathiri afya ya akili zake na uwezo wa
utendaji wa akili zake.

c. Kazi ya Rais ni ngumu sana, kwa sababu ni pamoja na kusimamia
shughuli zote za maendeleo ya nchi nzima, na matatizo yote
yanayowatokea wananchi wote kila walipo, na kusimamia
utekelezaji wa majukumu yote ya watendaji wote katika Taifa,
hivyo kwamba maamuzi sahihi yanatokana na afya bora yenye
kuhakikisha uwezo unaopasa wa kiakili wakati wote

d. Hitilafu katika afya hudhoofisha uwezo wa kifikira na kusababisha
maamuzi mabovu, ambayo huleta athari mbaya sana kwa Taifa. Na
udhaifu huo huathiri mpaka maadili na hata uzalendo wa huyo
kiongozi mdhaifu. Kwa mfano akipatikana Rais anayeishi kwa
matumaini, kwa hofu ya kupoteza uhai kabla hajaweka sawa
mambo yake na ya familia na jamii yake atatumikia maslahi yake
zaidi kuliko Taifa, tatizo hilo la afya likawa limelikosesha Taifa
kipaumbele, na kuliangamiza kimaendeleo!
e. Wanaowania kugombea urais ni lazima wachunguzwe kwa makini
sana afya zao, kwa sababu kukifanyika makosa akatawazwa
mwenye hitilafu za kiafya, atakwenda kuwa mzigo mzito sana kwa
Taifa, hususan ugharamiaji wa utunzaji wa uhai wake ndani na nje
ya nchi, kukosekana na umakini anaopasa kuwa nao kwa ajili ya
dhamana kubwa aliyopewa n.k.

Kutokana na AFYA yake kuwa dhaifu sana hata kwa kumwona kwa
macho tu, kabla ya uchunguzi wa kitaalamu ni kwamba Edward Lowasa hawezi kabisa kugombea Urais. Kwani amekosa sifa muhimu sana ya afya bora, ambayo ni ya lazima kwa mtu yeyote anayestahili kupewa dhamana kubwa sana ya kuliongoza Taifa. Pengine hata kugombea urais kwenyewe anatafuta kutokana na hitilafu ya kiafya, iliyosababisha udhaifu katika kufanya maamuzi, hivyo amejikuta kwa bahati mbaya anagombea asichokiweza kabisa.

Ni lazima wagombea wote wa Urais, wa Ubunge na hata wa Udiwani
wachunguzwe kwa makini afya zao kabla ya kupewa kugombea, na hata kuchunguzwa tena katikati ya muhula wa utumishi wao, kama kweli tunalithamini na kuliheshimu Taifa.

Sifa za urais ni wito au uhanga kwa ajili ya Nchi ambao ni zaidi ya
maadili ya kizalendo, maono, vipawa na AFYA BORA. Ni dhana potofu
sana kwamba sifa ya urais ni kushabikiwa na umati wa watu! Kwa
sababu wengi hufuata mapesa na husombwa hata na magari ili umati
wa kishabiki tu upatikane. Lakini kumpenda mtu huwa lazima kuwe na sababu, wakati ushabiki ni pepo mchafu au ‘psychological deficiency’.





4 Jul 2015

Kwa niaba ya familia ya Mzee Philemon Chahali, ninaomba kuwashukuru nyote mnaoungana nasi kumwombea dua/sala ili apone. Hatuna cha kuwalipa bali kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu awabariki kwa upendo wenu. Pia kwa vile hali ya baba bado si ya kuridhisha, tunawaomba tuendelee na dua/sala zaidi. Wanasema 'penye wengi Mungu yupo' basi ni matumaini yetu kuwa ushirikiano huu katika sala/dua utapelekea kupona kwa Mzee Chahali. Again, asanteni sana, na Mungu awabariki sana.

Tangu nipate taarifa za kuumwa kwa baba, nimepunguza kujishughulisha na 'kelele' zangu kuhusu masuala mbalimbali yanayoikabili Tanzania yetu. Sijafanya hivyo kwa maana ya kupuuzia masuala hayo bali kichwa changu kimetawaliwa na suala la afya ya baba yangu kwani ndo mzazi pekee niliyebakiwa naye baada ya kufiwa na mama mwaka 2008.

Hata hivyo, leo nimelazimika kuandika makala hii baada ya kufanya maongezi na jamaa yangu mmoja huko Tanzania ambaye katika nafasi yake kikazi, anafahamu mambo mengi yanayojiri 'nyuma ya pazia.'

Alichoniambia kimenishtua sana. Ni kuhusu kampeni zinazoendelea mtandaoni zinazomhusisha mtoto mdogo anayejiita DOGO JEMBE. Pia kampeni hizo zinatumia hashtag #IkuluSio.

Huyo jamaa yangu, pengine kutokana na majukumu yake kikazi au ufuatiliaji tu, amenionyesha ushahidi unaothibitisha kuwa kampeni hiyo inaendeshwa na mtangaza nia mmoja wa CCM. Kwahiyo tofauti na picha inayojengwa na DOGO JEMBE kuwa yupo upande wa maslahi ya Watanzania, kimsingi mtoto huyo anatumiwa tu na mwanasiasa huyo anayetaka urais. 

Kwa mujibu wa jamaa yangu huyo anayefanya kazi katika taasisi moja 'nyeti' huko nyumbani, kosa la msingi lililofanywa na waandaaji wa kampeni hiyo ni kwenye kitu kinachofahamika kama IP Address ambayo kwa lugha nyepesi ni anwani ya mlolongo wa namba zinazotenganishwa na nukta ambao unaitambua kompyuta katika mtandao. 'Mtaalam' huyo amefanikiwa kubaini kuwa posts za kampeni hiyo zinatoka kwa IP address ya mdogo wa mwania nia fulani. Amenitumia screenshots zenye uthibitisho kuhusu suala hilo.

Amenijulisha pia kuwa taasisi anayoitumikia inafahamu bayana kuhusu 'uhuni' huo, na hii unaisoma hapa kwa mara ya kwanza, usishangae ukikutana na breaking news hii katika vyombo vya habari katika siku chache zijazo. Inaelekea kuna 'wakubwa' hawajapendezwa na mbinu hiyo ya kuwahadaa Watanzania kwa kisingizio cha kumsaka Rais bora.

Kilichomkera, kinachonikera, na ambacho pengine nawe Mtanzania kitakukera ni kitendo cha mwania huyo kuwafanya Watanzania wapumbavu. Kwanini nasema hivyo? Kwanza ni 'kosa' la kumtumia mtoto mdogo kuvuta hisia za watu, kuwaaminisha kuwa lengo ni kupigania maslahi ya taifa kwa kuamsha tafakuri ya nani hasa anatufaa kuwa Rais wetu ajaye, ilhali ukweli ni kwamba kampeni hiyo ina lengo la kumpigia debe mwania nia huyo.

Kumtumia mtoto huyo mdogo kwa minajili ya kisiasa hakuna tofauti na kile kinachoitwa CHILD LABOUR, yaani kuwatumikisha watoto. Sasa hapo tu yatupasa kutambua kuwa child labour ni ukiukwaji wa haki za binadamu, na kwa minajili hiyo, mwania nia anayesaka urais kwa kukumbatia ukiukwaji wa haki za watoto/binadamu HAFAI.

Pili, hadaa, usanii, na uhuni mwingine wa kisiasa ndivyo miongoni mwa vitu vilivyotufikisha hapa. Sasa kama katika hatua hizi za awali tu za kuwania kupitishwa na chama kuwania urais mwanasiasa anaanza kukumbatia vitu kama hivyo, huhitaji kuwa mwenye uelewa mkubwa wa kisiasa kubaini kuwa mwania nia huyo hafai hata ujumbe wa nyumba kumi, achilia mbali urais.

Tatu, japo watoto wana haki ya kikatiba na kidemokrasia kuzungumzia kuhusu hatma ya taifa letu ikiwa ni pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao, hiyo sio excuse kwa wamasiasa yeyote yule kutumia haki hiyo ya watoto kwa manufaa yake binafsi. Angekuwa jasiri, angejitokeza mwenyewe hadharani badala ya kujikampenia kwa kutumia child labour.

Kwa mujibu wa jamaa yangu huyo ambaye kwa ninavyomfahamu hana kambi yoyote hasa kwa vile majukumu yake kikazi yanamzuwia kujihusisha na siasa, kuna data nyingine ambazo zinaihusisha moja kwa moja kampeni hiyo na mwania nia huyo.

Japo nipo katika wakati mgumu kutokana na kuzorota kwa afya ya Mzee Chahali lakini afya ya Tanzania yetu ni muhimu pia kama afya ya mzazi wangu, na nimeshindwa kukaa kimya baada ya kuletewa ushahidi kuhusu 'uhuni' huu. 

Amenieleza kuwa kauli ya Dogo Jembe kuwa 'Ikulu sio ya baba yako' ilimlenga Makongoro Nyerere kwa vile yeye ni mtoto wa Nyerere, na kauli kuwa 'Ikulu sio hospitali' illimlenga Lowassa kwa vile mwania nia huyo amedaiwa kuwa afya yake sio nzuri japo haijathibitishwa. 


Lakini pengine hata bila kupata 'ufunuo' huu, ilipaswa tujiulize NANI ANAYEFADHILI KAMPENI HII YA KISASA KABISA?

Kwa mtizamo wa jamaa yangu huyo, kosa jingine la kampeni hiyo ni kwamba imejitengenezea 'ufupi wa maisha' kwa maana kwamba ipo siku Dogo Jembe atalazimika kuwashawishi tena Watanzania kuwa 'mtaka nia flani ana sifa za dogo jembe, na ndio anafaa kuwa Rais,' na hapo all hell will break loose kwa sababu kila mwenye akili timamu atabaini nani alikuwa behind kampeni hiyo.

Anyway, ningetamani kuandika kwa kirefu lakini wito wangu kwa Watanzania wenzangu ni mdogo tu: AKILI ZA KUAMBIWA, CHANGANYA NA ZA KWAKO. Tumeshwahi kuhadaiwa huko nyuma, tumeshaona matokeo ya hadaa hizo, chonde chonde, tusirejee tena makosa hayo. Kama katika kuwania tu kupitishwa na CCM, mwanasiasa yupo radhi kutumia mtoto mdogo kuwahadaa Watanzania, je akifanikiwa kuingia Ikulu itakuwaje? Ni muhimu pia kutambua kuwa mwanasiasa ambaye yupo desperate mno kuingia Ikulu lazima atakuwa na ajenda zake binafsi,

Nimalizie kwa kuwashukuru tena nyote mnaojumuika nasi kumfanyia dua/sala Mzee Chahali, na ninawashukuru sana, na kuwaombea Mungu awabariki sana. 



25 Jun 2015

NIANZE makala hii kwa kuomba radhi kutokana na kushindwa kuwaletea makala katika toleo lililopita. Hiyo ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu. Ninaomba pia kutumia fursa hii kuwatakia ndugu zangu Waislamu mfungo mwema wa mwezi Mtukukufu wa Ramadhani.
Katika makala ya hii nitaendelea kuzungumzia kinyang’anyiro cha Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu. Na zaidi nitaelemea katika nafasi ya urais, hususan mchakato unaoendelea ndani ya chama tawala, CCM, ambapo hadi wakati ninaandaa makala hii, makada 37 wa chama hicho wameshajitokeza kuomba ridhaa ya chama hicho kuwapitisha kuwania nafasi hiyo.
Lakini kabda sijaingia kwa undani, pengine ni muhimu tukumbushane kuwa wakati idadi ya makada 37 (ambayo huenda ikaongezeka) ni ya kihistoria, suala la kushtua zaidi ni ukweli kwamba miongoni mwao ni pamoja na Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na mawaziri kamili saba, bila kujumuisha manaibu waziri.
Nimekumbushia suala hili kwa sababu ni vigumu kufahamu serikali yetu muda huu inaendeshwaje, hasa ikizingatiwa kuwa Rais Jakaya Kikwete nae amekuwa katika safari za mara kwa mara nje ya nchi (wakati ninaandika makala hii yupo nchini India).
Ukiondoa Makamu wa Rais, ambaye anakuwa kaimu Rais wakati Rais anapokuwa nje, licha ya majukumu ya kiwaziri, Waziri Mkuu na hao mawaziri wengine pia ni wabunge. Katika hili ni vigumu kufahamu wanamudu vipi kugawa muda wao kwa majukumu yao ya kiserikali, kiubunge na hayo ya kuwania kuteuliwa kuwania nafasi ya Urais.
Hata hivyo, si vigumu kudhani kwamba kwa muda huu, akili na nguvu kubwa kwa makada wote waliotangaza nia zitakuwa zimeelekezwa kwenye kinyang’anyiro cha Urais. Kwa kiasi gani hilo linaathiri utumishi wao kwa umma, ni vigumu kwa sisi wengine kufahamu.
Nikirejea kwenye suala la makada wa CCM kutangaza nia zao kuwania urais, jina lililosikika zaidi wiki iliyopita lilikuwa la Jaji Mkuu wa zamani, Augustino Ramadhan. Japo jina lake lilishawahi kutajwa huko nyuma kama mmoja wa watu ‘wanaoweza kuokoa jahazi,’ lakini kwa kiasi kikubwa habari zilizosikika huko nyuma zilionekana kama tetesi tu pasi uthibitisho.
Angalau mara mbili, gazeti hili la Raia Mwema lilibeba habari zilizohusu uwezekano wa Jaji Ramadhani kugombea urais kwa tiketi ya CCM.

Binafsi, kwanza ninaheshimu uamuzi wa Jaji Ramadhani kwani ni haki yake ya Kikatiba kuchukua uamuzi huo. Hata hivyo, tayari kuna baadhi ya wananchi walioshtushwa kumsikia Jaji huyo akielezea kuwa amekuwa mwanachama wa CCM tangu miaka ya sitini.
Kwanza ninadhani alipitwa tu kutoa kauli hiyo kwa sababu CCM iliundwa mwaka 1977 baada ya TANU na ASP kuungana. Kwahiyo, hakukuwa na CCM miaka ya sitini.
Jaji huyo alieleza kuwa alijiondoa CCM mwaka 1992 kufuatia mabadiliko ya sheria, ambapo mfumo wa vyama vingi uliruhusiwa na hiyo kupelekea watumishi wa umma kutoruhusiwa kuwa wanachama wa vyama vya siasa.
Japo Jaji Ramadhan anasema alijiondoa CCM wakati huo, kuna wanaokwenda mbali zaidi na kutaka uthibitisho katika suala hilo. Sote tunaijua Tanzania yetu, na kwa hakika tunawafahamu vema viongozi na wanasiasa wetu. Ni kwa mantiki hiyo, kuna wanaotaka uthibitisho kuwa kweli Jaji huyo alijiondoa CCM na kutokuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa katika utumishi wake, ikiwa ni pamoja na Ujaji Mkuu.
Na kauli hiyo ya uana-CCM wake, kwa namna flani, imerejesha tena suala la hukumu iliyotolewa na Jaji huyo kwa kushirikiana na majiji wengine dhidi ya kesi ya Mchungaji Christopher Mtikila aliyetaka mahakama itamke kuwa sheria inayozuwia mgombea binafsi ni kinyume cha Katiba.
Pasi kuingiza kiundani katika kesi na hukumu hiyo, binafsi ninaichukulia hukumu hiyo kuwa moja ya hiba (legacies) kuu za utumishi wa Jaji Ramadhani.
Kwa baadhi yetu tunadhani Jaji huyo angebaki shujaa kwa demokrasia kwa sababu mfumo wa sasa unaolazimisha wawania nafasi mbalimbali za uongozi ikiwa pamoja na urais kuwa wanachama wa vyama vya siasa unatupunja fursa ya kupata viongozi wa kisiasa wazalendo lakini wasiotaka kujihusisha na vyama vya siasa.
Hata hivyo, ili kumtendea haki, ni muhimu kutambua kuwa hukumu hiyo haikuwa maamuzi binafsi ya Jaji Ramadhani bali licha ya kuwahusisha majaji wengine pia, ilikuwa ni ya kisheria na sio hisia binafsi.
Lakini kwangu, licha ya dalili zinazoonekana wazi kuwa kana kwamba CCM imeshapata mgombea wake urais kufuatia uamuzi wa Jaji Ramdhan kutangaza nia, nina wasiwasi kidogo kuhusu ufanisi wake.
Kubwa zaidi ni ukweli kwamba Idara ya Mahakama, ambayo licha ya Jaji Ramadhan kuitumikia muda mrefu bali pia aliwahi kuwa mkuu wake kwa maana ya ujaji mkuu, imeendelea kuwa moja ya taasisi sugu kwa rushwa. Takribani kila ripoti inayotolewa kuhusu tatizo la rushwa katika taasisi mbalimbali za serikali nchini mwetu, Idara ya Mahakama haikosekani, na tena ikishika nafasi za juu.
Mara baada ya kuchukua fomu kuomba CCM imteue kuwania Urais, Jaji Ramadhan aliwaambia waandishi wa habari kuwa atatumia uzefu wake kupambana na ufisadi. Swali la msingi: uzoefu upi? Huohuo ulioshindwa ukiondoa Idara ya Mahakama katika orodha ya taasisi zinazoongoza kwa rushwa?
Kwa upande mwingine, Jaji Ramadhan alikuwa mjumbe wa ‘Tume ya Warioba’ iliyokusanya maoni kuhusu mabadiliko ya Katiba. Sote twakumbuka yaliyomsibu Jaji Joseph Warioba na baadhi ya wasaidizi wake kupigania sio tu kazi nzuri iliyofanywa na tume yao bali pia mustakabali wa Katiba mpya.
Kwanini Jaji Ramadhani amekuwa kimya sana katika suala hilo? Je ukimya wake ulitokana na kufahamu kuwa siku moja angeomba kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM?
Na katika hilohilo, kwa vile mapendekezo ya Tume hiyo iliyomshirikisha Jaji Ramadhani yalikuwa muungano wenye muundo wa serikali tatu, je kwa vile CCM ambayo jaji huyo anaiomba ridhaa ya kumteua awe mgombea wake ina msimamo wa serikali mbili kama ilivyo sasa, hilo si tatizo angalau kimsimamo na kimtizamo?
Hadi muda huu, Jaji Ramadhani ni Rais wa Mahakama ya Afrika kuhusu haki za binadamu. Sihitaji kuorodhesha matukio lukuki ya ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Tanzania lakini miongoni mwa matukio makubwa ni pamoja na ukatili unaofanywa na Jeshi la Polisi na rushwa (naam, rushwa sio tu adui wa haki bali pia inachangia ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu).
Je Jaji Ramadhani amekuwa wapi wakati ukiukwaji wa haki za binadamu ukiendelea kushamiri na kuwa kama umehalalishwa na Katiba yetu? Ni nani anaweza kusimama hadharani na kuwaambia Watanzania kuwa ‘Urais wa Jaji Ramdhani katika Mahakama ya Haki za Binadamu Afrika umechangia hili na lile katika kutetea au kudumisha haki za binadamu nchini Tanzania’?
Niwe mkweli, binafsi ninamwona Jaji Ramadhani kama Rais Kikwete alipojitambulisha mwaka 2005 kuwania urais na hatimaye kushindwa nafasi hiyo.
Alionekana mtu mwadilifu, aliyeitumikia nchi kwa muda mrefu, na pengine kubwa zaidi, msafi (asiye na kashfa). Sifa hizo zinalingana na tunazosikia kuhusu Jaji Ramadhan. Je, kwa mfano, kuwa msafi ni sawa na kuwa na uwezo wa kuongoza nchi?
Lakini la mwisho kuhusu kada huyo ni taarifa za awali kuwa amekuwa akiombwa na baadhi ya wana-CCM kuwania nafasi ya urais (kuna wanaodai kuwa ndio mtu pekee anayeweza kumudu ‘kumzuia’ Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa asiingie Ikulu, na wengine wanasema Jaji huyo ndio ‘msafi zaidi’ kuliko makada wengine wanazowania nafasi hiyo).
Swali la msingi: je hao waliomwomba (kama ni kweli) hawafanyi hivyo kwa maslahi yao binafsi? Na je, kumwomba huko (kama ni kweli) hakutopelekea urais wa Jaji Ramadhan (iwapo atashinda) ukaishia kuwa kama ‘deni la kwa wanamtandao’ lilivyouandama utawala wa Rais Kikwete?

Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha tena Watanzania wenzangu kuwa ni muhimu tujiulize na kuwauliza wawania urais maswali magumu ili tusije kuishia kujiulaumu huko mbeleni.
Nchi yetu ipo katika wakati mgumu; umasini wa kupindukia huku ufisadi ukizidi kuimarika, uhaba mkubwa wa uzalendo, utovu mkubwa wa maadili ya uongozi ikiwa na pamoja na uhuni katika matumizi ya fedha za umma, shilingi inayporomoka kama ipo kwenye mashindano ya marathoni na kadhalika.
Tunahitaji rais ambaye si tu anajua matatizo yetu bali pia ana uzalendo na uwezo wa kukabiliana nayo. Hatuhitaji Rais msafi lakini mwoga wa kupambana na maharamia wanaoibomoa nchi yetu kila kukicha.
Hatuhitaji mtu anayeahidi kupambana na rushwa ilhali hana mfano japo mmoja wa jinsi alivyowahi kupambana na rushwa.

-

24 Jun 2015






IT'S SPORAH CUSTOM HANDMADE WIGS... Finest Quality Handmade Custom Made Wig In Any Shade Or Length To Suit Your Style. 

Add caption

Meet the host at the Sporah Treasure Launch, Award winning Voxafrica UK Sports 360 Presenter Mr. Adesope Olajide
Meet the Co-Host, The Former model Irene Major and the wife of Canadian oil tycoon Sam Mail. 

Irene Major and Vox Africa TV presenter Adesope ready for the day.

WELCOMING THE GUESTS!








INTRODUCING LIVE PERFORMANCE
Add caption
Add caption
Add caption
Chipper Inter Performing LIVE at The Sporah Treasure Launch. 

Team Sporah making sure  that everyone is taken care.of







WELCOMING SPORAH 




And Irene Major had a question for Sporah "WHY HAIR? Why she decided to branch into hair business as a talk show queen.

Sporah talking about the Drive behind SPORAH TREASURE.




Kwa picha zaidi BONYEZA HAPA

23 Jun 2015

Polisi jijini London hapa Uingereza wamemkamata Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa ya Rwanda, Jenerali Karenzi Karake, kutokana na maombi ya Hispania ambako anahitajika kwa makosa ya uhalifu wa kivita.

Jenerali Karake, Mkurugenzi Mkuu wa National Intelligence and Security Services alikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Heathrow, Jumamosi iliyopita, kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na polisi wa hapa jana.

"Karenzi Karake, mwenye umri wa miaka 54, raia wa Rwanda, alifikishwa mbele ya mahakama ya Westminster, (jijini London)...baada ya kukamatwa kwa kutumia hati ya Ulaya ya kusaka watuhumiwa (European Arrest Warrant) kwa niaba ya mamlaka za Hispania, ambako anatafutwa kuhusiana na uhalifu wa kivita dhidi ya raia," ilieleza taarifa iliyotolewa kwa barua-pepe.

Jenerali huyo alirudishwa rumande hadi Alhamisi.

Haikuwezekana mara moja kuwasiliana na familia ya mkuu huyu wa ushushushu au mwanasheria wake nje wa muda wa kazi jijini London. Ubalozi wa Rwanda hapa Uingereza nao haujatoa maelezo yoyote.

Mwaka 2008, jaji wa mahakama kuu ya Hisania, Fernando Andreu, aliwatuhumu viongozi 40 wa kijeshi na kisiasa wa Rwanda, ikiwa ni pamoja na Jenerali Karake, kujihusisha na mauaji ya kisasi kufuatia mauaji ya kimbari yaliyoikumba nchi hiyo mwaka 1994.

Jaji huyo aliwaona watuhumiwa hao na hatia ya mauaji ya kimbari, ualifu dhidi ya binadamu na ugaidi, makosa yaliyopelekea vifo vya mamia ya maelfu ya watu ikiwa ni pamoja na Wahispania.

CHANZO: imetafsiriwa kutoka Matthewaid.com


21 Jun 2015

Ni kitu gani?

Summer Solstice, kwa lugha nyepesi, ni siku yenye mchana mrefu zaidi kuliko zote katika mwaka. Neno 'mchana' hapa linamaanisha muda wa mwanga wa jua. Ni siku mbapo baadhi ya sehemu, kama hapa Uingereza, zina masaa mengi zaidi ya mchana (mwanga wa jua) kuliko usiku (muda wa kiza).
Pengine ni muhimu kufahamu kwamba kwa hapa Uingereza, kwa mfano, maana ya mchana na usiku ni tofauti na huko nyumbani, kwa kiasi flani. Kwa mfano, Ukikutana na mtu saa 6 alfajiri, salamu huwa 'Good morning' kwani kwa wenzetu hawa, asubuhi inaanza rasmi saa 6 kamili 'usiku.' (0000 midnight). Vilevile, katika msimu wa baridi ambapo jua huzama mapema na kuchelewa kuchomoza, si ajabu ukiagwa kwa 'Good night' saa 11 jioni, kwa sababu muda huo tayari jua limeshazama.
Neno 'Solstice' linatokana na neno la Kilatini  'solstitium' linalomaanisha meaning ‘jua kusimama’.

Kwanini inatokea?

Kwa wenye kumbukumbu ya somo la Jiografia, Summer Solstice hutokea pale mhimili wa sayari yetu 'unapoegemea' zaidi kuelekea kwenye jua.
Kinyume cha tukio hili,  Winter Solstice, hutokea pale mhimili wa dunia 'unapoelemea' mbali zaidi na jua, na kusababisha muda mfupi zaidi wa jua katika siku, yaani mchana - kwa maana ya mwanga wa jua- unakuwa mfupi mno kuliko usiku.

Inatokea lini?

Summer solstice hutokea kati ya Juni 20 na 22.
Kwa mwaka huu ni leo Jumapili Juni 21.
Kwa hapa Glasgow, jua litachomoza saa 10 na dakika 31 asubuni (takkriban saa moja tangu muda huu ninapoandika makala hii) na kuzama  saa 4 na dakika 6 usiku


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.