Showing posts with label MTIKILA. Show all posts
Showing posts with label MTIKILA. Show all posts

10 Oct 2015

HATIMAYE tumebakiwa na takriban wiki mbili tu kabla ya Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika hapo Oktoba 25. Wakati kampeni hizo zikielekea ukingoni, matukio mawili makubwa yamejitokeza Jumapili iliyopita.
Tukio la kwanza ni kifo cha mwanasiasa nguli, Mwenyekiti wa chama cha siasa cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila. Tukio jingine lililotokea siku hiyo hiyo ni uamuzi wa mwanzilishi wa CCM na TANU, na mkongwe wa siasa za Tanzania, Kingunge Ngombale Mwiru. Nimeona ni vema kuyajadili matukio haya kwa sababu yote yanahusiana na Uchaguzi Mkuu, kwa namna moja au nyingine.
Tuanze na hilo la pili. Kwanza, tangazo la Kingunge kujiondoa uanachama wa CCM lilistahili liwe na mvuto mkubwa kama Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alipotangaza kung’atuka. Lakini ukweli ‘mchungu’ ni kwamba tukio hilo limeonekana kama mwanachama wa kawaida tu wa CCM kuamua kujiondoa katika chama hicho.
Lakini, pili, uamuzi wa Kingunge kujiondoa CCM, haukuwa jambo la kushtua, kwa vile kwa muda mrefu sasa, kada huyo, rafiki wa karibu wa Baba wa Taifa, alikwishajitambulisha yupo upande gani katika siasa za uchaguzi. Kingunge, alipigana kwa hali na mali kuhakikisha mgombea ‘ chaguo lake,’ Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, anashinda katika mchujo wa chama hicho tawala kupata mgombea wake.
Niliwahi kuandika huko nyuma kuwa laiti busara ingemwongoza mzee huyo – hasa ikzingatiwa kuwa katika mila zetu za Kiafrika, wazee hutazamwa kama ‘visima’ vya busara na hekima – basi asingejiweka upande wa mgombea fulani au hata kama angefanya hivyo, licha ya kuwa ni haki yake ya kidemokrasia na kikatiba, basi labda angefanya kwa usiri.
 Nilitahadharisha hivyo kwa sababu, kwa kuegemea upande mmoja ilhali kuna pande nyingi katika jambo husika kuna matokeo ya aina mbili, kuwa sahihi au kukosea. Sasa, kama matokeo ya kuwa sahihi ni kudumisha hadhi na kukosea ni kupoteza hadhi, kila mwenye busara anatarajiwa kuwa makini katika jambo hilo.
Kitendo cha Kingunge kumuunga mkono Lowassa katika mchakato wa CCM kumpata mgombea wake, na hatimaye jina la kada huyo kukatwa katika mchujo, ilikuwa na athari kwa hadhi ya Kingunge kama mkongwe wa siasa. Bila kujali kuwa Lowassa alionewa au alistahili kukatwa, ukweli tu kwamba hakupitishwa ni sawa na kufeli kwa waliokuwa wakimuunga mkono, ikiwa ni pamoja na Kingunge.
Niliposoma tamko lake la kujiengua CCM nilibakiwa na maswali kadhaa, kubwa likiwa “...hivi huyu ndiye Kingunge yule yule wa zama za Nyerere au huyu ni toleo jipya? Na pengine bila hata kwenda mbali sana na kurejea zama za Nyerere, Kingunge huyu huyu alikuwa mstari wa mbele katika kampeni zilizomwingiza madarakani Rais Jakaya Kikwete, mwaka 2005. Yeye ni sehemu muhimu ya takriban kila analolaumu kuhusu CCM.
Matarajio ya wengi kwa Kingunge yalikuwa angekuwa mrithi wa Baba wa Taifa, si kwa sababu ya umri wake tu bali uumini wake katika Itikadi ya Ujamaa. Kingunge alikaa kimya wakati nguzo kuu ya itikadi hiyo, Azimio la Arusha ikizikwa katika kile kinachofahamika kama Azimio la Zanzibar. Kada huyo licha ya kuwa kimya katika masuala mbalimbali yanayoifanya CCM kupoteza umaarufu, hususan suala la ufisadi, alijitokeza kuwa mtetezi mkubwa wa watu waliotuhumiwa katika orodha maarufu ya watu waliotuhumiwa na Chadema kuwa ndio ‘mapapa wa ufisadi,’ iliyojulikana kama ‘List of Shame.’
Kimsingi, Kingunge aliwananga Chadema na kuwaita waongo, wazushi na wanafiki, wanaosema uongo na hakuna ushahidi, hakuna kiongozi fisadi. Leo hii, mwanasiasa anayeamini kuwa ndio chaguo sahihi kuingoza Tanzania, yaani Lowassa, kajiunga na waongo, wazushi, na wanafiki hao.
Kingunge ni mwathirika wa makosa yake mwenyewe kimkakati. Alipaswa tangu awali, achague kuwa mtetezi wa wananchi kama Baba wa Taifa, au mtetezi wa tabaka tawala. Japo ninatambua madhara ya kuwa mtetezi wa wananchi, kwa maana ya kutengeneza maadui wengi kisiasa, lakini ukweli usiopingika ni kwamba heshima na hadhi ya mtu wa aina hiyo hudumu milele. Tunawakumbuka akina Nyerere na Sokoine si kwa vile tu walikuwa viongozi wetu bali kwa sababu walisimama upande wa wananchi tulio wengi kuliko kulinda tabaka la watawala walio wachache.
Katika hitimisho langu baada ya kupokea taarifa za Kingunge kujiuzulu uanachama wa CCM, niliandika katika mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Kingunge aliwahi kuwa kama Muhmmad Ali wa siasa za Tanzania. Lakini tangazo lake la kujiuzulu CCM leo ni kama Ali angetangaza sasa kuwa anajiuzulu masumbwi. Alikwikushajiuzulu miaka kadhaa iliyopita. Nilichomaanisha ni kuwa, umuhimu wa mkongwe huyo wa siasa za nchi yetu ulisha- expire (kwisha muda wa matumizi) kitambo, na kubaki au kuondoka kwake CCM hakukuwa na faida kwa yeyote zaidi yake mwenyewe. Ninamsikitikia kwa sababu alipaswa kukumbukwa kwa mazuri mengi ya zama za Nyerere lakini dalili ni kwamba ataishi kukumbukwa zaidi kwa jithada za kumbeba Lowassa kwa gharama ya hadhi yake.
Tukiweka hilo kando, taarifa za kifo cha Mchungaji Mtikila kimeonekana kuwashtua Watanzania wengi. Binafsi, nilipopata taarifa hizo, kwanza nilidhani ni utani tu, lakini nilipogundua kuwa zina ukweli, hisia zangu zikaanza kupatwa na wasiwasi fulani.
Wakati tayari kuna taarifa zisizo rasmi mbalimbali zinazosambaa kwa kasi mtandaoni kuhusu chanzo halisi cha kifo cha Mchungaji Mtikila, licha ya taarifa za polisi kuwa chanzo cha ajali iliyosababisha kifo chake ni mwendo kasi wa gari alilokuwa akitumia huku akiwa hajavaa mkanda wa kiti cha gari, ukweli kwamba mwanasiasa huyo machachari alikuwa na ‘mabomu’ kuhusu mmoja wa wagombea urais, ilitosha kuniongezea wasiwasi huo.
Ni muhimu, katika hatua hii kukumbushia kuwa miongoni mwa sababu za umaarufu wa Mtikila ni kile ambacho wengi walikitafsiri kama ‘conspiracy theories,’ yaani hoja zinazoonyesha kubeba ukweli, zikiambatana na aina fulani ya ushahidi, lakini zinabaki vigumu kuzithibitisha.
Kwa mujibu wa taarifa zinazosambaa mtandaoni, Mtikila alikuwa akijipanga kuzuia ugombea wa mmoja wa wagombea urais, kwa hoja mbalimbali, ikiwa ni pamoja na madai yake kuwa mgombea huyo ni sehemu ya mkakati wa kimataifa kuihujumu nchi yetu. Kadhalika, Mchungaji huyo alinukuliwa akiongea kwenye kituo kimoja cha televisheni huko nyumbani (Tanzania) akisisitiza kwa nini anaamini mgombea huyo ni janga kwa taifa.
Sasa, japo kifo ni mapenzi ya Mola, lakini katika mazingira ya kawaida tu, kama anajitokeza mtu kumpinga mwanasiasa hadharani huku akipania kumwekea vikwazo katika safari yake ya Ikulu, kisha mtu huyo akafariki kwa ajali siku chache kabla ya uchaguzi, hisia za kibinadamu zinaweza kuhisi kuna namna hapo.
Kwa bahati mbaya, au pengine makusudi, jeshi la polisi limeonekana kuwa na haraka mno kutangaza chanzo cha ajali iliyosababisha kifo cha mwanasiasa huyo. Iwapo uchunguzi wa vyanzo vya ajali katika nchi zilizoendelea huchukua siku kadhaa licha ya taasisi zao za uchunguzi kuwa na nyezo za hali ya juu, iweje jeshi letu la polisi linalosifika kwa uchunguzi wa mwendo wa konokono lipate uwezo wa ghafla wa hali ya juu kuweza kutambua chanzo cha ajali hiyo siku moja tu baadaye?
Kwa mtizamo wangu, na ili kuwaridhisha Watanzania kuwa kifo cha mwanasiasa huyo hakina mkono wa mtu, polisi walipaswa kufanya uchunguzi wa kina, ikiwa ni pamoja na kupata taarifa ya uchunguzi wa kitabibu kuhusu chanzo cha ajali kabla ya kukurupuka na sababu ambazo ni rahisi kuhisi kuwa ni za kufikirika.
Kwa bahati mbaya, kifo cha Mtikila kilitokea siku moja na tukio la Kingunge kujivua uanachama wa CCM, suala lililosababisha baadhi ya watu kuyahusisha matukio hayo mawili. Pengine ni ‘coincidence’ tu lakini ni nadra kwa Tanzania yetu kukumbwa na matukio makubwa ya kisiasa ndani ya siku moja.
Nimalizie makala hii kwa kuwasihi Watanzania wenzangu kufanya sala na dua kuombea Uchaguzi Mkuu ufanyike na kuhitimishwa kwa amani na usalama.
Kauli zinazoashiria kuchochea machafuko sio tu ziepukwe bali pia zikemewe vikali. 
Tukumbuke kuwa, wakati uchaguzi utafanyika na kupita, Tanzania yetu ni lazima ibaki kuwa nchi moja na yenye usalama kwa kila raia wake. Waingereza wanasema; there is life after election (maisha yetu yataendelea baada ya uchaguzi), kwa hiyo ni muhimu kutotumia fito za kujengea nchi yetu kuchapana wenyewe.
Mungu ibariki Tanzania

5 Oct 2015



TAHADHARI YA PICHA YA MAITI: Mwili wa marehemu baada ya 'ajali.' Je nani aliyepiga picha hii na kuisambaza? Je lengo lilikuwa 'ushahidi kuwa amekufa kweli?'

Kumepatikana waraka ambao unadaiwa kuwa ndio uliopelekea kifo cha Mchungaji Mtikila. Awali, nilibandika maswali kadhaa kuhusu utata unaozunguka kifo hicho kiasi cha kuhisi huenda si 'Mapenzi ya Mungu' bali ni 'mkono wa mtu.' Katika waraka huo hapa chini, ukurasa wa 2,4 na 6 hazipo (sijui kwa nini)










UPDATE: Nimekutana na clip yenye sehemu ya mahojiano na Mchungaji Mtikila, akibainisha kuhusu tuhuma hizo zilizo kwenye waraka huo hapo juu 






Kwanza ni salamu zangu za rambirambi kwa Mchungaji Christopher Mtikila kama nilivyozi-post katika 'disposable website' (tovuti inayokuwa mtandaoni kwa muda tu) hapa 



Baada ya salamu hizi za rambirambi, tuelekee kwenye mada husika. Kwanza, ninaomba kukiri kwamba mara baada ya kusikia taarifa za ajali iliyopelekea kifo cha Mchungaji Mtikila, hisia yangu ya sita ilihoji 'mbona kama kuna mkono wa mtu?' Ninadhani mnakumbuka niliwahi kuzungumzia huko nyuma kuhusu 'hisia ya sita' (katika ule mfululizo wa makal za ushushushu). Siwezi kwa hakika kueleza kwanini nilipatwa na hisia hiyo lakini ilitokea tu, na imenikaa kichwani tangu muda huo.

Baadaye nikakutana na mabandiko yafuatayo huyo Jamii Forums 



 Maswali tata kifo cha Mchungaji Mtikila1. Gari yake haijaharibika kabisa na tunaaambiwa iliacha njia na kupinduka tunajua sababu kubwa ya magari kuacha njia ni kupasuka kwa matairi lakini hili gari la Mchungaji Mtikila hakuna tairi liliposuka. Sasa tuambiwe sababu ya kuacha njia na kupinduka ni nini? 

2. Mchungaji Mtikila hana alipoumia au kubleed damu.(Labda iwe kafa kwa mshtuko wa moyo au internal wounds. Kwenye picha anaoekana hajaumia hata kidogo hata nguo alivozavaa zikiwa hazijachanika hata kidogo.Sasa tuambiwe sababu gani nyingine iliyopelekea kifo chake? 

3.Tunaambiwa ajali alipata SAA 11 alfajiri Chalinze kwaa asili ya eneo la Chalinze ni eneo bize sana kwanini picha iliyosambaa inaonesha ni asubuhi kabisa kumekucha ina maana ajali yake haikushtukiwa na watumiaji wengine wa Barabara mpaka asubuhi. 

Angalizo sijamlaumu mtu yeyote kwenye hii ajali ila ni maswali ambayo nilikuwa najiulza binafsi sasa nawaomba msichafue hali ya hewa.

Na nyingine inayorandana na hiyo 



Mazingira ya kifo cha Mchungaji Mtikila bado kinatia shaka kuu mbele ya jamii na nachelea kusema huyu Mzee ameuawa na genge la mafisadi ili wafanikiwe kisiasa kwani Mtikila alikuwa ameshakusanya vielelezo vyote vya kuwashughulikia.
1. Jeshi la Polisi Watanzania tunaomba mtusaidie kumuhoji kwa kina huyu mtu anaeitwa Mchungaji Patrick Mgaya. Huyu alikuwa ni mmoja wa waliopata ajali pamoja na marehemu Mtikila. Ikumbukwe kuwa Magaya ni mmoja wa mashabiki muhimu sana wa Mgombea Urais kupitia Ukawa ndg Edward Lowassa.Taarifa za siri zinasema kuwa Mchungaji Mgaya na Mchungaji Mtikila walikutana takribani mwezi mmoja uliopita tu na kwamba kuna wasiwasi kuwa alipewa kazi maaluum ya kuhahakisha amamuua Mtikila.


Taarifa kutoka nyumbani kwa marehemu zinasema kuwa Mchungaji Mtikila akiwa na Mchungaji Patrick Mgaya walianza safari siku ya Ijumaa jioni kwenda mkoani Njombe ambapo waliambatana na madereva wawili ambao Mchungaji Mtikila hakuwafahamu. Aliewafahamu watu hawa wote ni Mchungaji Magaya ambae ndie aliekodisha gari waliokwenda nayo Njombe kupitia kwa Ndg Victor James Manyii ambaye mbali ya kutoa gari aliyokodisha pia alitoa madereva wawili ambao pamoja na Mchungaji Mgaya wao hawakufa isipokuwa Mchungaji Mtikila pekee.


Ajali hii imeacha maswali mengi kuliko majibu. Kwa mfano ukiangalia shingo ya marehemu Mtikila utaona kuna kitu kama kamba ambayo inaweza kuleta tafsiri kuwa ilitumika kumnyonga marehemu. Pili, kwanini mwili wa marehemu hauna hata kovu wala mchirizi wowote wa damu? Je, ni nani alimpiga picha Marehemu Mtikila? Je, Patrick Mgaya ni nani? Kabla kuwa mchungaji alikuwa anafanyakazi gani? Je gari lile lilipinduka lenyewe au liligongwa? Na kama lilipinduka ni kwanini liharibike eneo la mbele pekee?Je Ni chombo gani kilikuwa cha kwanza kumpiga picha na kusambaza kwenye mitandao?
Patrick Mgaya alipopiga simu nyumbani kwa marehemu alisema wamepata ajali na kwamba kulikuwa na majeruhi wengi sana akamaliza kwa kusema mtuombee kisha akakata simu, je, hao majeruhi wengi ni akina nani? Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama muhojini Mchungaji Patrick Mgaya maana zipo dalili kuwa kuna mengi anayoyafahamu kuhusu tukio hili. Pia fuatilieni uhusiano uliopo kati ya Rais Paul Kagame, Patrick Mgaya na EADWARD LOWASSA. Pia nashauri Jeshi la Polisi kumuhoji mtu anaeitwa Dr. Jean Bosco Ngendahimana ambae anaishi nyumbani kwa marehemu pale Mikocheni.
Wale wote wenye misimo thabiti juu ya kuchukia Rushwa na Ufisadi wachukue tahadhari. Nasema hivyo sababu Humphrey Polepole alivamiwa nyumbani kwake Mbezi na Dkt. SLAA anapokea sms za vitisho. Vyombo vya dola viwe macho.


Binafsi ninafanya jitihada za angalau kujiridhisha iwapo ajali hiyo na kifo ni 'kazi ya Mungu' au kuna mkono wa binadamu. Ila ninachofahamu ni kwamba hadi mauti yanamkuta, Mchungaji Mtikila alikuwa na 'mabomu' aliyotaraji 'kuyalipua' ndani ya siku hizi chache zilizosalia kabla ya uchaguzi.

Ukipata taarifa zozote kuhusu suala hili ninaomba uwasiliane nami kwa Twitter @chahali au Facebook facebook.com/evarist.chahali.1


8 Jul 2015

Ufuatao ni waraka kutoka kwa Chama cha DP kinachoongozwa na Mchungaji Christopher Mtikila kumpiga mwania nia ya Urais Edward Lowassa

KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU
TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA
Edward Lowasa ni balaa kwa Taifa!

Democratic Party (DP) inatarajia kufikisha Mahakamani chama cha
CCM pamoja na wanachama wake sita, Edward Lowasa na wengine,
kwa mujibu wa Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, kwa kosa kubwa sana la kuvunja Katiba na Sheria za Nchi kwa kuanza kampeni ya Uchaguzi kabla ya wakati unaopasa kwa mujibu wa Sheria.

1. Tunao ushahidi mzito unaothibitisha kwamba Edward Lowasa na
wenzake walianza kampeni ya urais ndani ya chama chao kabla ya
wakati, na kwamba chama chao kiliwapa adhabu ya kutofanya siasa
kwa miezi 12. Lakini safari hii Lowasa ameanza kampeni ya urais
Arusha kwa mkutano mkubwa sana wa hadhara wa kampeni haramu
na kumwaga rushwa ya kutisha!

2. Kama ni wadhamini alipaswa kuwapata katika ofisi za chama chake, katika mikoa nane (8) tu Tanganyika na mikoa miwili tu Unguja na Pemba, wadhamini 45 tu katika kila mkoa. Lakini Edward Lowasa amefanya mikutano nchi nzima, ya kuwaahidi maelfu ya wananchi katika kila mkutano wa hadhara, mambo atakayofanya kama wakimpa kura zao awe Rais! Hii ndiyo kampeni halisi, ambayo ni ukiukaji wa Katiba na Sheria za Nchi! Uchaguzi Mkuu unaendeshwa na Sheria, hivyo ni lazima Sheria ichukue mkondo wake dhidi yake kwa kuivunja.

3. Edward Lowasa amevunja Katiba ya Nchi na Sheria ya kiwango cha
fedha kinachoruhusiwa kutumika katika shughuli halali za Uchaguzi,
kiasi kwamba CCM na Taasisi zote za uchunguzi wa kifedha nchini,
upelelezi wa Jinai na Usalama wa Taifa ni mlazima wanayo kazi muhimu sana ya kupata ukweli kuhusu haya mabilioni ya fedha yanayomwagwa nchini na fisadi Edward Lowasa, ameyapata wapi na kwa namna gani, kumehusika ‘’Money laundering’ au la, kama mapato ya mapesa hayo yote ni halali, na kama mapato hayo yote yalilipiwa kodi inayopasa kwa ajili ya Taifa.

Ni marufuku kabisa tena ni makufuru Edward Lowasa kuruhusiwa
kugombea urais, kwa sababu amevunja Katiba ya Nchi na Sheria na
Kanuni za Uchaguzi. Sifa mojawapo ya kustahili kugombea uongozi wa nchi yoyote ni maadili mema na uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na
taratibu za Utawala wa Sheria
4. Edward Lowasa, kwa kujimilikisha maeneo nchi nzima kwa kutumia kifisadi Uwaziri wake wa Ardhi, ameliweka Taifa katika hatari kubwa ya mmwagiko wa damu baina ya wakulima na wafugaji, baada ya kueneza nchi nzima makundi ya ng’ombe wake, na kusababisha mapigano makali ya mara kwa mara kila mahali nchini kati ya wafugaji wake na wakulima. Kwa sababu ya uovu huu hata katika kampeni yake haramu Lowasa ameshindwa kusema lolote juu ya kilimo, ingawa ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu na ndiyo shughuli inayotunza uhai wa asilimia 95 ya wananchi!

Kwa kuwaingilia wakulima katika ardhi yao, kuwaua ovyo, kuwaonea
kiasi cha kufisha matumaini yao katika kilimo, kumeifanya kauli mbiu ya “Kilimo kwanza” kuwa porojo tu ya kisanii!

5. Edward Lowasa ni mwiko kabisa kupewa kugombea urais, kwa
sababu siyo tu aliutumia kifisadi Uwaziri wa Ardhi akajitajirisha na
kujipatia maeneo makubwa ya ardhi nchini kote, bali alitumia kifisadi
zaidi uwaziri wa nchi katika ofisi ya Waziri Mkuu, katika uagizaji wa
mashangingi ya Wabunge, mawaziri, wakuu wa Mikoa na Wilaya.

6. Edward Lowasa alikemewa mnamo mwaka 1995 na Mwalimu Nyerere anayeenziwa na CCM lama “Baba” yao, alipotaka kugombea urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, wala hakuweza kujitetea kwavile utapeli wote aliojitajirishia ulikuwa mezani. Leo baada ya mabiashara haramu mengi na kulipora sana Taifa kukiwa ni pamoja na utapeli wa “kununua mvua Thailand” na kuliibia Taifa mabilioni ya fedha kwa kutumia kampuni hewa ya RICHMOND, huyu ni fisadi-nyangumi. Ni mlemavu wa rushwa tu wa kununuliwa na mapesa machafu anayomwaga Lowasa, anayeweza kumruhusu fisadi Edward Lowasa agombee urais.

Sifa za mtu wa kukugombea Urais zimeelezwa bayana na Mwenyezi
Mungu katika Kumbukumbu la Torati 17:15-20, ambazo Edward
Lowasa hana hata mojawapo! Lowasa awali alikemewa na Mwalimu
Nyerere ambaye CCM wanamuenzi kama “Baba” yao, kuwa hafai kabisa kuwania urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, kama alivyomtangaza hata Reginald Mengi pale alipolazimika kujiuzulu Uwaziri Mkuu kwa ajili ya wizi kwa kampuni hewa ya Richmond, lakini leo akiwa fisadi la kutisha zaidi kuliko papa eti anataka urais!
Si ajabu kwamba magabacholi yalioipora vibaya sana Nchi hii kama Sigh Setti na hata Nazir Karamagi wote wamo katika genge la Edward
Lowasa! Si ajabu hata fisadi Reginald Mengi leo kuungana na fisadi
Lowasa yakizingatiwa machafu yake yeye mwenyewe, na kuhusika kwa Mengi na mauaji ya Chacha Wangwe, pamoja na mpango wa Chadema
wa kumwua Mchungaji Mtikila, waraka feki wa kujaribu kuupotosha
ukweli ukatangazwa kwa ITV yake.

Katika uwaziri wake katika ofisi ya Waziri Mkuu, na katika Uwaziri wakewa Ardhi na Uwaziri Mkuu, Lowasa alifanya ufisadi ambao katika nchi kama China zenye uchungu na maslahi ya mataifa yao angekuwa wa kupigwa risasi hadharani, lakini katika nchi yetu anatafuta urais!

7. Edward Lowasa AFYA yake imempiga marufuku kugombea Urais!
Kwa ajili ya kila ajira duniasni kote, moja ya mashart makuu ni lazima mwombaji awe na afya iliyo bora, ndiyo sababu ni lazima ajira ya kila mwombaji itegemee taarifa ya kitaalamu ya madaktari, inayothibitisha kwamba hana dosari kiafya. Sharti hili ni la lazima kwa sababu:
a. Majukumu yote atakayopewa mwajiriwa atayatekeleza kikamilifu
kwa kutumia viungo vya mwili wake, kwahiyo viungo vyake vyote
ni lazima viwe katika hali iliyo imara kwa ajili ya kazi.

b. Hata kama kwa uthibitisho wa kitaalamu wa madaktari mwajiriwa
anazo akili nzuri kichwani mwake, akiwa na hitilafu katika viungo
vingine vya mwili wake huathiri afya ya akili zake na uwezo wa
utendaji wa akili zake.

c. Kazi ya Rais ni ngumu sana, kwa sababu ni pamoja na kusimamia
shughuli zote za maendeleo ya nchi nzima, na matatizo yote
yanayowatokea wananchi wote kila walipo, na kusimamia
utekelezaji wa majukumu yote ya watendaji wote katika Taifa,
hivyo kwamba maamuzi sahihi yanatokana na afya bora yenye
kuhakikisha uwezo unaopasa wa kiakili wakati wote

d. Hitilafu katika afya hudhoofisha uwezo wa kifikira na kusababisha
maamuzi mabovu, ambayo huleta athari mbaya sana kwa Taifa. Na
udhaifu huo huathiri mpaka maadili na hata uzalendo wa huyo
kiongozi mdhaifu. Kwa mfano akipatikana Rais anayeishi kwa
matumaini, kwa hofu ya kupoteza uhai kabla hajaweka sawa
mambo yake na ya familia na jamii yake atatumikia maslahi yake
zaidi kuliko Taifa, tatizo hilo la afya likawa limelikosesha Taifa
kipaumbele, na kuliangamiza kimaendeleo!
e. Wanaowania kugombea urais ni lazima wachunguzwe kwa makini
sana afya zao, kwa sababu kukifanyika makosa akatawazwa
mwenye hitilafu za kiafya, atakwenda kuwa mzigo mzito sana kwa
Taifa, hususan ugharamiaji wa utunzaji wa uhai wake ndani na nje
ya nchi, kukosekana na umakini anaopasa kuwa nao kwa ajili ya
dhamana kubwa aliyopewa n.k.

Kutokana na AFYA yake kuwa dhaifu sana hata kwa kumwona kwa
macho tu, kabla ya uchunguzi wa kitaalamu ni kwamba Edward Lowasa hawezi kabisa kugombea Urais. Kwani amekosa sifa muhimu sana ya afya bora, ambayo ni ya lazima kwa mtu yeyote anayestahili kupewa dhamana kubwa sana ya kuliongoza Taifa. Pengine hata kugombea urais kwenyewe anatafuta kutokana na hitilafu ya kiafya, iliyosababisha udhaifu katika kufanya maamuzi, hivyo amejikuta kwa bahati mbaya anagombea asichokiweza kabisa.

Ni lazima wagombea wote wa Urais, wa Ubunge na hata wa Udiwani
wachunguzwe kwa makini afya zao kabla ya kupewa kugombea, na hata kuchunguzwa tena katikati ya muhula wa utumishi wao, kama kweli tunalithamini na kuliheshimu Taifa.

Sifa za urais ni wito au uhanga kwa ajili ya Nchi ambao ni zaidi ya
maadili ya kizalendo, maono, vipawa na AFYA BORA. Ni dhana potofu
sana kwamba sifa ya urais ni kushabikiwa na umati wa watu! Kwa
sababu wengi hufuata mapesa na husombwa hata na magari ili umati
wa kishabiki tu upatikane. Lakini kumpenda mtu huwa lazima kuwe na sababu, wakati ushabiki ni pepo mchafu au ‘psychological deficiency’.





10 May 2011



Leo ni tarehe 10/05/2011,na deadline aliyotoa Ridhiwani Kikwete,mtoto wa Rais Jakaya Kikwete,kwa Katibu Mkuu wa Chadema,Dkt Willibroad Slaa,na Mwenyekiti wa DP,Mchungaji Christopher Mtikila,imemalizika jana.Ridhiwani alitoa dealine ya siku saba kuwataka Dkt Slaa na Mtikila wamwombe radhi kufuatia tuhuma zao dhidi yake kuwa amekuwa bilionea kwa njia za kutilia shaka.

Ni mapema mno kubashiri chochote lakini habari ifuatayo inaweza kutoa mwangaza kuhusu uwezekano wa Ridhiwani kwenda mahakamani kama livyotishia au kutokwenda (which would imply tuhuma hizo dhidi yake ni za kweli).Soma kwanza habari yenyewe


Mtoto wa Rais Kikwete ang’aka

na Janet Josiah

MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, amesema hataki kufuatiliwa maisha yake na wanasiasa hasa wanaomtuhumu kuwa ni bilionea huku akisisitiza kuwashughulikia waolimchafua.

Ridhiwani, alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima akitakiwa kueleza hatua atakazochukua baada ya muda wa siku saba aliowapa Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willbrod Slaa kupita.

Awali, mtoto huyo wa Rais aliwataka wanasiasa hao wamwombe radhi katika kipindi cha siku saba vinginevyo angewapeleka mahakamani kwa kuwa wamemchafua pamoja na familia yake.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwa njia ya simu, ili kujua lini angekwenda mahakamani kuwafungulia mashtaka viongozi hao, alijibu kwa jazba kwamba jambo hilo linahusu maisha yake hivyo haoni sababu ya kufuatiliwa na vyombo vya habari.

“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

Kwa nyakati tofauti Mchungaji Mtikila na Dk. Slaa, walimtuhumu Ridhiwani kwa ukwasi huku wakiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kumchunguza.



Pasipo nia ya kufanya hitimisho lolote,nashindwa kumwelewa Ridhiwani anaposema "jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lenu..."Hivi sio Ridhiwani huyuhuyu aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari,ambapo pamoja na mambo mengine alikanusha tuhuma zilizotolewa na wanasiasa hao,na akawataka wamwombe rahdi vinginevyom angewafikisha mahakamani?Sasa kama jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lao (wanahabari) kwanini basi aliitisha mkutano nao na kuwaelezea same thing anachodai hakiwahusu?

Waandishi wa habari wana kila sababu ya kumhoji kama atawafikisha Slaa na Mtikila mahakamani au la.Kwanini?Kwa sababu,kwanza,alitamka hayo mbele ya waandishi hao hao wa habari,na pili,yeye ni mtoto wa Rais na ametuhumiwa kuwa bilonea kwa mgongo wa baba yake.Sasa hakuna Mtanzania asiyependa kujua kama madai ya wanasiasa hao ni zushi mtupu au yana ukweli ndani yake.

Wito wangu kwa Ridhiwani ni huu:TIMIZA AHADI YAKO YA KWENDA MAHAKAMANI.Tuhuma za wanasiasa hao dhidi yako si ndogo,kwani licha ya kukugusa wewe binafsi zinamgusa pia baba yako ambaye ni Rais wetu (na ambaye siku za karibuni ametangaza kuwa anadhamiri kuukalia kooni ufisadi).Usipokwenda mahakamani itaonyesha kuwa tuhuma hizo zina ukweli.

And to make matter even worse,Dkt Slaa na Mtikila wanaweza kukufungulia kesi ya kuwakashifu,kwani ulidai ni wazushi tu.Sasa kama sio wazushi then go to the court as you promised,bearing in mind kwamba wewe ni mwanasheria.

Enewei,tunasikiliza WHAT'S NEXT!

Ngoma inogire!

3 May 2011


Sakata linalomhusu Ridhiwani Kikwete,mtoto wa Rais Jakaya Kikwete-kwa upande mmoja,na Katibu Mkuu wa Chadema Dkt Willibroad Slaa na Mwenyekiti wa chama cha DP,Mchungaji Christopher Mtikila-kwa upande mwingine,linaanza kupamba moto baada ya wanasiasa hao kumjibu Ridhiwani.Kimbembe hicho kilianza kwa kauli zilizotolewa na Dkt Slaa na Mtikila ambao katika nyakati tofauti walimtuhumu Ridhiwani kuwa bilionea aliyepata fedha isivyo kihalali akitumia mgongo wa baba yake,Rais Kikwete.

Tuhuma hizo zilipelekea Ridhiwani kuitisha mkutano na waandishi wa habari ambapo licha ya kukanusha kuwa sio bilionea-na kudai kuwa magari ya kifahari anayoonekana akiendesha mara kwa mara ni ya kuazima kutoka kwa marafiki zake-alitoa siku saba kwa Dkt Slaa na Mtikila kuthibitisha madai yake vinginevyo atawafikisha mahakamani.

Sasa,kama habari ifuatayo inavyoonyesha,wanasiasa hao wamemtaka Ridhiwani awahi kwenda huko mahakamani,na wao watatumia fursa hiyo kuthibtisha madai yao.Nisikumalizie uhondo,soma mwenyewe hapa chini

Slaa, Mtikila wamtega mtoto JK

Tuesday, 03 May 2011 21:50
Leon Bahati na Raymond Kaminyoge

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amemtega mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, akisema akifanikiwa kukifikisha chama hicho mahakamani atakuwa amefanikiwa kula mfupa ambao uliwashinda vigogo waliowatangazwa hadharani kuwa ni mafisadi nchini.

Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa msimamo wake kuhusu kauli ya Ridhiwani aliyoitaoa Dar es Salaam juzi, kuwa atamfikisha mahakamani ili kuthibitisha kauli yake kwamba mtoto huyo wa rais ni bilionea aliyepata utajiri wa kutisha kipindi kifupi.

Ridhiwani alimpa siku saba Dk Slaa, kuanzia jana awe amekanusha kauli hiyo ya kumtuhumu kuwa fisadi, vinginevyo atamfikisha mahakamani.
"Sisi tunasema atangulie huko mahakamani sisi tutakuja nyuma," alisema Dk Slaa.

Dk Slaa ambaye katika uchaguzi uliopita aligombea urais na kutoa upinzani mkubwa kwa Rais Kikwete aliyetangazwa kuwa mshindi, alisema kauli za kushtakiwa wanapotangaza taarifa za ufisadi hadharani zimekuwa za kawaida.

Alisema wengi waliwahi kutoa kauli kama hiyo kupitia vyombo vya habari baada ya kuwatuhumu hadharani kuwa ni mafisadi, lakini wakashindwa kwenda mahakamani.

"Chadema tuna uzoefu tulipotaja orodha ya mafisadi walitutishia kuwa watatushtaki mahakamani tukawaambia watangulie sisi tutakuja nyuma, lakini walishindwa kutekeleza ahadi yao," alisema Dk Slaa na kuongeza kuwa, iwapo Ridhiwani atafanya hivyo atakuwa amevunja rekodi ambayo imewashinda watu wazito.

Katibu huyo ambaye umaarufu wake ulikuja kwa kasi kipindi cha miaka 15 aliyokuwa Mbunge wa Karatu, Arusha, alijigamba kuwa hawazungumzi jambo bila vielelezo ndio maana wanajiamini kwa kila wanachokisema hadharani.

Dk Slaa alitupia lawama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwamba amekuwa akisisitiza ifutwe kwa sababu inashindwa kufanya kazi yake, ikiwamo kufanya uchunguzi kwa watu wanaotuhumiwa kupata utajiri katika mazingira yenye utata.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Ridhiwani alikanusha kuwa kijana bilionea kama Dk Slaa anavyomtuhumu.Alisema anamiliki shamba mkoani Pwani, lenye ukubwa wa ekari 1.5, gari ndogo na akaunti kwenye benki ya CRDB, NBC na Stanbic, ambazo hakutaja kiasi cha fedha.

Dk Slaa alipinga vikali kauli hiyo na kwamba, alimaliza shule miaka michache iliyopita, lakini sasa ni bilionea na utajiri huo aliupata kwenye mazingira ya utata.

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, alisema atatoa uthibitisho mahakamani kuhusu mali alizozitaja kuwa zinamilikiwa na Ridhiwani.“Siwezi kumuomba radhi mtu, nina uhakika wa kuwa kijana yule anamiliki mali ambazo hajazipata kwa njia halali, itakuwa vizuri ikiwa atanipeleka mahakamani, kwani huko ndiko nitakakoonyesha uthibitisho wangu,” alisema Mchungaji Mtikila.

Jumamosi iliyopita, Mtikila alikaririwa na vyombo vya habari akisema, Ridhiwani ni bilionea anayemiliki nyumba za ghorofa, malori, kampuni za ujenzi wa barabara na ardhi.
CHANZO: Mwananchi

Uzuri wa sakata hili upo katika pembe nyingi.Kwanza,Ridhiwani ni mwanasheria kitaaluma,kwahiyo yayumkinika kuamini kuwa tishio lake (la kuwapeleka Dkt Slaa na Mtikila mahakamani iwapo watashindwa kuthibitisha tuhuma dhidi yake) lilikuwa sio danganya toto.Pili,Ridhiwani ni mtoto wa Rais Kikwete,na kwa vile tuhuma hizo zinamhusisha pia baba yake (kwa maana ya kutumia fursa ya urais kumnufaisha mwanaye) inatarajiwa kuwa suala hapa sio kujisafisha yeye tu bali pia baba yake.

Lakini kwa upande wa pili ni wasifu wa Dkt Slaa,na pengine Mtikila.Wengi tunafahamu kuwa Mtikila na mahakama ni kama mtu na nyumbani kwake.Japokuwa siku za karibuni amekuwa na msimamo unaoyumba lakini bado anatambulika kuwa anapoamua kupigania haki basi atakwenda umbali wowote ule pasipo kuchelea madhara ya kufanya hivyo.

Kwa Dokta Slaa,wengi tunamfahamu kama mmoja wa wanasiasa adimu kabisa ambao ni nadra kutoma matamshi pasipo kuyafanyia utafiti wa kutosha na kuwa na uthibitisho.Yayumkinika kuamini kuwa Dkt Slaa alikuwa akifahamu vema kuwa kwa vile Ridhiwani ni mwanasheria,na pia asingependa kuona jina lake na la baba yake yanahusishwa na ufisadi hadharani,ni lazima angetishia kwenda mahakamani kama sio kwenda kabisa huko mahakamani kufungua kesi ya madai.Kwa mantiki hiyo,na kwa kurejea historia ya Dkt Slaa,inawezekana kuamini kuwa alikuwa na uhakika na alichosema,sambamba na kuwa na ushahidi mzito kuhusu madai hayo.

Enewei,siku saba si nyingi.Leo ni siku ya pili,tumebakiwa na siku tano.Tusubiri kusikia kauli kutoka kwa Ridhiwani Jumatatu ijayo ambapo siku saba alizotoa zitakuwa zimekwisha muda wake.

Ngoma inogire!

15 Sept 2008

Some political analysts argue that ruling parties in Africa never lose elections,and if they do,which is rarely,it is likely not because they failed to deliver to the people who put the parties in power but rather either due to their internal conflicts or laxity.One could easily blame majority of opposition parties in Africa for their failures in organizing themselves in quest to remove ruling parties from power.But the fact is,in most African countries,the idea of an opposition party coming into power spells inexplicable uncertainty to the rulers,largely due to their "sins" during their terms of leadership.

In Tanzania,opposition parties have consistently cried foul during elections accusing the ruling party,CCM,of sabotaging them by either inciting conflicts in the parties or "bribing" their leaders to defect.CCM has also been accused of reluctance to reform the electoral system,which the opposition parties,see as unfair and biased.

I strongly believe that our nation's interest should come first,mainly because political parties may come and go but the nation should always remain intact,peacefully and flourishing.Had every Tanzanian looked beyond partisan politics,it is fair to conclude that those who criticize the ruling party for its perceived failure to deals with mafisadi (economic saboteurs),for instance,would not be considered as giving ammunitions to opposition parties but instead they would be given enormous support.

A while ago,I came across this story which in my view would stir trouble in Tanzania's opposition politics.
Mtikila atamka mazito kifo cha Wangwe

Na Waandishi Wetu 

WAKATI mazingira ya kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime marehemu Chacha Wangwe yakiendelea kuwa tete, Mwenyekiti wa Democratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila, ameibuka na kile alichodai, taarifa za mpango kamili hadi mauaji ya mwanasiasa huyo. 

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mchungaji Mtikila alidai mipango ya kumuua marehemu Wangwe ilianza kusukwa mkoani Dodoma na baadaye vikao vya kukamilisha mkakati huo, vilifanyika jijini Dar es Salaam wilayani Kinondoni. 

Aliongeza kuwa wahusika baada ya kukamilisha mpango huo na jinsi utakavyotekelezwa, walikwenda nchini Kenya kukodi watu wawili ambao alidai walilipwa sh. milioni 120 kama ujira wa 'kazi' hiyo. 

Mchungaji Mtikila alidai kuwa wauaji hao, ndio walioshirikiana na Bw.Deus Mallya ambaye anadaiwa wakati huo alikuwa amejenga uhusiano mzuri na marehemu Wangwe. 

Alidai siku ya tukio, marehemu Wangwe hakutaka kusafiri lakini alishinikizwa zaidi ya mara tatu na Bw. Mallya ambaye hadi sasa anashitakiwa kwa kosa la kusababisha ajali na kuendesha gari bila leseni.

"Baada ya kushinikizwa sana, marehemu Wangwe alikubali kuanza safari ambapo Bw. Mallya aliwasiliana na washirika wake ambao muda huo walikuwa eneo la tukio wakiwasubiri," alidai Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa; 

"Wakati huo ilikuwa bado mapema hivyo walimshauri apoteze muda japo wa nusu saa, ndipo alipozusha hitilafu ndani ya gari na kurudi gereji na baada ya muda huo kupita ndipo walianza safari kuelekea jijini Dar es Salaam." 

Huku akidai kuwa ana ushahidi wa tukio hilo na yupo tayari kutoa ushirikiano kwa Rais Jakaya Kikwete, Mchungaji Mtikila alizidi kueleza kuwa Bw. Mallya aliendelea kuwasiliana na washirika wake hadi walipofika eneo Pandambili, wilayani Kongwa na kusimamisha gari. 

"Baada ya kusimamisha gari, washirika wa Mallya walipanda na kumpulizia dawa ya usingizi usoni mara nne na hapo hapo alipoteza fahamu," alieleza Mchungaji Mtikila na kuongeza kuwa baada ya hapo ndipo alipigwa kwa kitu cha ncha kali kisogoni. 

"Kwa kuwa Mungu alimpenda sana hakukata roho, aliendelea kuhema ndipo alipopigwa na nyundo na kummalizia kabisa," alidai. Aliongeza kuwa baada ya kutimiza hilo waliweka jiwe kwenye kiongeza mwendo gari likaondoka kwa kasi na lilipindua ili kuonesha kuwa marehemu alikufa kwa ajali lakini muda huo Mallya alikuwa hayuko kwenye gari," 

Alidai kuwa kabla ya kupindua gari hilo, walimfunga marehemu mkanda na kumwibia sh. milioni tisa alizokuwa nazo pamoja na kompyuta yake ndogo 'Lap top' ambayo ilikuwa na nyaraka zake za siri. 

Alidai kuwa baada ya kufanikisha mauaji hayo, Bw. Mallya alitoa 'line' yake ya simu ambayo alikuwa akiitumia kuwasiliana na washirika wake na kuitupa. Alidai kuwa hadi anakamatwa simu yake haikuwa na 'line' yoyote. 

Kwa mujibu wa Mchungaji Mtikila mauaji hayo yalifanyika kati ya 1.30 hadi saa 2.00 usiku, muda mfupi baada ya kumaliza kuwasiliana na familia yake saa 1.27. 

Huku akijata majina ya watu wanaodaiwa kuhusika kwenye mpango huo, alieleza kuwa kipindi cha mchakato wa mpango wa kumuua, Bw. Wangwe, walikuwa wakisafiri kwenda nchini Kenya kusuka mpango huo. 

Mchungaji Mtikila alielekeza lawama zake kwa askari wote waliohusika na uchunguzi wa mauaji hayo kwa akidai kuwa hawakusema ukweli hivyo nao wanastahili kuunganishwa kwenye kesi hiyo. 

Kutokana na mazingira ya kifo cha marehemu Wangwe kugubikwa na maswali mengi, Mchungaji Mtikila amemuomba Rais Kikwete kuunda tume ya kuchunguza mazingira ya kifo chake kama alivyofanya kwa wafanyabiashara wa madini wa Mahenge, Morogoro ambao wanadaiwa kuuawa na Polisi. 

Alidai kwa wadhifa aliokuwa nao marehemu Wangwe katika jamii akiwa Mbunge wa Tarime, Rais ana nafasi ya kuunda tume. "Naupongeza uamuzi wake wa kuunda tume ya kuchunguza vifo vya wafanyabiashara lakini na kwa hili aunde tume na mimi nitakuwa tayari kutoa ushirikiano,"alisisitiza. 

Aliongeza kuwa kama Rais hatafanya hivyo, yeye ataleta wataalam wake kutoka nje kufanya uchunguzi kwani ameishafanya mazungumzo na ubalozi wa nchi moja ambao hakuutaja. 

Mchungaji Mtikila alidai kuwa atakwenda jimboni Tarime wakati huu wa kampeni ili kuwaeleza wananchi ukweli kuhusu kifo cha marehemu Wangwe. Alisema amesimamisha mgombea kupitia chama chake, Bw. Benson Makanya, ili apate jukwaa la kueleza ukweli kuhusiana na kifo hicho. 

Marehemu Wangwe alikufa kwa ajali ya gari iliyotokea eneo la Pandambili mkoani Dodoma Julai 28 mwaka huu lakini tangu kifo chake, yameibuka maswali mengi huku baadhi ya watu wakidai kuwa aliuawa. 

Hata hivyo uchunguzi uliofanywa na madaktari wawili kwa nyakati tofauti ulionesha kuwa hakupigwa risasi bali kifo chake kilisababishwa na ajali ya gari.

According to one local paper,the suspects are Freeman Mbowe,Dr Wilbroad Slaa and Tindu Lissu.This is how I look at the picture:If the accused trio decide to ignore Mtikila,it goes without saying that the public would buy the story,and it could bring their political careers to an abrupt end.Going to the court might be the only option left on their table,but Mtikila has a long history of winning charges brought against him in various courts.It should be all smiles in the ruling party's quarters as a Swahili saying goes "adui yako mwombee mabaya" (wish evil things to your enemy)

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.