12 Mar 2021


Rais John Pombe Magufuli amekata roho leo saa kumi na moja nusu Jioni hospitali ya Mzena Dar es Salaam. Makamu wa Rais Samiah Suluh Hassan hajaambiwa. Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa Bwana Diwani Athumani na Daktari wa Rais Professor Mchembe wamekaa na Mwili wa Marehemu mpaka sasa kupanga Makamu wa Rais wanayemtaka Bwana Chamuriho. Tumlinde Samiah, tulinde Katiba. Watanzania Kesho asbh nendeni Mzena kushinikiza Katiba ifuatwe

27 Oct 2020



Network data from the NetBlocks Internet Observatory confirm widespread disruption to social media and online communication platforms via multiple internet providers in Tanzania as of Tuesday 27 October 2020. The incident comes on the eve of Tanzania’s presidential and national assembly elections and the service outages are ongoing at the time of writing.

Real-time metrics show that Twitter, WhatsApp, backend servers for Instagram and some Google services including GMail and Translate are generally or partially unavailable via Tanzania’s leading network operators Vodacom, Airtel, Tigo, Halotel and ZanTel. Meanwhile, data indicate a more generalized disruption of services on state-owned operator TTCL, the Tanzania Telecommunications Corporation. Findings are drawn from an initial set of NetBlocks Web Probe observations from 800 observation points. Twitter Inc. has also subsequently confirmed throttling of its services in Tanzania.

Authorities have not issued a statement on the disruptions as of Tuesday afternoon. A week earlier, the Tanzania Communications Regulatory Authority issued operators with a directive to suspend bulk SMS and telephony services during the election period. However, the directive does not specifically cover internet communications and relevant regulatory frameworks remain unclear.

The incident comes amid heightened concerns over election transparency and follows claims from the opposition over state interference with the accreditation process for electoral observers.

Breaking incident: article will be updated as information is processed


Methodology

This report follows the Election Pathfinder Rapid Response methodology which defines a set of core principles, workflows and benchmarks for network measurement and evaluation during elections and referenda.

Internet performance and service reachability are determined via NetBlocks web probe privacy-preserving analytics. Each measurement consists of latency round trip time, outage type and autonomous system number aggregated in real-time to assess service availability and latency in a given country. Network providers and locations enumerated as vantage point pairs. The root cause of a service outage may be additionally corroborated by means of traffic analysis and manual testing as detailed in the report.

SOURCE: NETBLOCK



Pengine umeshawahi kusikia jina la Profesa Allan Lichtman wa Marekani ambaye ana rekodi ya miaka 30 ya kutabiri kwa usahihi kabisa matokeo ya urais katika nchi hiyo. 



Pengine utabiri uliompatia umaarufu zaidi ni wa mwaka 2016 ambapo takriban kila kura ya maoni ilionyesha kuwa mgombea wa chama cha Democrats, Hillary Clinton, angemshinda mpinzani wake wa chama cha Republican, Donald Trump.

Profesa huyo anatumia vipengele 13 vinavyopatikana kwenye kitabu chake kiitwacho "The Keys To The White House" (funguo za kuingilia Ikulu ya Marekani).

Katika vipengele hivyo 13 ni kauli zenye mrengo wa ushindi kwa mgombea aliyepo madarakani. Kwa muktadha wa Tanzania, vipengele hivi hapa chini vinamhusu Rais John Magufuli wa chama tawala CCM anayechuana vikali na mpinzani wake mkuu, Tundu Lissu wa Chadema.

Endapo majibu ya SI KWELI (FALSE) ni matano au pungufu kwa vipengele hivyo, basi mgombea aliyepo madarakani anatabiriwa kushinda. Lakini endapo majibu ya SI KWELI (FALSE) yatakuwa sita au zaidi, basi mgombea huyo ataanguka kwenye uchaguzi husika.

Naomba nitahadharishe kuwa hii ni mara ya kwanza kwa kanuni hii kutumika kutabiri matokeo ya urais nchini Tanzania. Hata hivyo nimejiridhisha kuwa japo Profesa Lichtman alilenga chaguzi za rais wa Marekani, zaweza pia kutumika kwa muktadha wa Tanzania.

19 May 2020


Nimechapisha makala mbili, moja ya Kiswahili na nyingine ya Kiingereza kuhusu mustakabali wa Rais John Magufuli kutokana na anavyopuuzia janga la korona. Makala ya Kiswahili ni uchambuzi wa kiintelijensia wenye kurasa kadhaa. Ipo HAPA

Pia waweza kuisoma hapa



Makala ya Kiingereza ipo kwenye tovuti ya kimataifa ya African Arguments. BONYEZA HAPA kuisoma

1 May 2020


Kituo cha runinga cha NTV cha nchini Kenya kiliripoti jana jioni kwamba idadi ya vifo vya korona jijini Dar es Salaam pekee kwa jana vilikuwa 50. Kutokana na unyeti wa maradhi haya, yayunkinika kuamini taarifa hiyo kwa sababu sio rahisi kwa chombo cha habari cha kitaifa kama hicho kutoa taarifa nzito kama hiyo bila kujiridhisha. 

Lakini kwa upande mwingine takriban kila anayefuatilia kinachoendelea huko Tanzania anafahamu fika kwamba serikali ya Rais Magufuli sio tu inaficha takwimu kuhusiana na maambukizi na vifo bali pia inafanya mzaha mkubwa dhidi ya jana hilo.

Taarifa nilizopatiwa alfajiri hii zinaeleza kuwa serikali imetoa mwongozo wa siri kuhusu jinsi ya kuwashughulikia wagonjwa wa korona. Kwa mujibu wa mwongozo huo, mgonjwa atakaa hospitalini wak siki tatu tu. Endapo hali ya mgonjwa haitogeuka kuwa mahututi, atarudishwa akaugulie nyumbani. Mtoa taarifa ananiambia kuwa waraka huo ni sehemu ya utekelezaji wa "herd immunity," mkakati hatari ambao kwa lugha nyepesi ni kuruhusu korona iangamize maelfu hadi mamilioni ya Watanzania kwa matarajio kuwa watajenga kinga dhidi ya ugonjwa huo. 

Licha ya uwezo wake mkubwa kiuchumi, Uingereza iliamua mapema tu kuachana na wazo hilo la herd immunity ambapo japo hadi muda huu idadi ya vifo imezidi 20,000 kwa kufuata herd immunity idadi hiyo ingeweza kuwa kubwa zaidi. Kadhalika, herd immunity ni sawa na kuangamiza watu bure kwa nchi kama Tanzania ambayo ina idadi kubwa ya watu wenye magonjwa kama ukimwi, pumu, kisukaribi, shinikizo la damu, nk ambayo yamethibitika "kuwa na ukaribu na korona" ambapo wenye maradhi hayo wamekuwa waathirika wakuu wa janga hilo. 

Endelea kutembelea blogu hii mara wa mara uweze kupata updates mbalimbali hususan kuhusu janga la korona.

Chukua tahadhari, jikinge na uwakinge na wenzio. Na heri ya Mei Mosi.

29 Apr 2020


Shaka imetanda nchini Tanzania kufuatia vifo vya watu 11 mashuhuru ndani ya wiki moja yaliyopita. Muda mfupi kabla ya kuandika chapisho hili, imetangazwa kuwa Mbunge wa Sumve (CCM) Richard Ndassa amefariki.



Kifo hicho ni ni mlolongo wa vifo vya watu maarufu nchini humo ambapo Jumatano iliyopita aliyekuwa Jaji Mkuu, Agustino Ramadhan alifariki.




Kabla ya hapo, Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Ali Haji Pandu alifariki Jumanne siku moja kabla.


Jumapili usiku, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evod Mmanda alifariki,



na siku hiyo hiyo, Mkurugenzi wa zamani wa CTI, Hussein Kamote alifariki pia jijini Dar es Salaam.

Jumanne, Jaji Mstaafu Musa Kwikima alifariki, na siku moja baadaye Afisa mwandamizi wa Idara ya Uhamiaji mkoani Kagera, Pendo Buteghe alifariki.


 Siku hiyo pia ilishuhudia kifo cha wakili maarufu Gaudious Ishengoma.



Watu wengine maarufu waliofariki ni Ben Lowassa - mdogo wake Edward Lowassa, Mbunge wa zamani Abdulkarim Shah na Naibu Meya wa Morogoro Isihaka Sengo.



Kifo cha Ndassa  kinaweza kuhusishwa na tamko la hivi karibuni la Rais John Magufuli kwamba "mvuke unaponya korona," ambapo inaelezwa kuwa chumbani kwa marehemu Ndassa kulikutwa vifaa vya kujifukizia.



Taarifa kutoka kwa wananchi mbalimbali zinaeleza kuwa wamefiwa na ndugu,jamaa na marafiki zao ambao wamezikwa na mamlaka husika lakini hali hiyo haijionyeshi kwenye takwimu za serikali kuhusu idadi vifo.

Leo, baada ya siku kadhaa, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametangaza kuwa



Na haya yote yanajiri huku leo ni siku ya 33 tangu Rais Magufuli alipoondoka Dodoma na kwenda kijijini kwake Chato mnamo Machi 28 mwaka huu.

Awali leo, kiongozi mkuu wa Upinzani Bungeni na mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freemani Mbowe, aliongea masuala kadhaa kuhusiana na janga la korona huku akiitaka serikali kuchukua hatua stahili.




Pia jana, kada maarufu wa CCM, Wakili Albert Msando alijitokeza hadharani kueleza kuwa hali nchini Tanzania ni mbaya kuhusiana na ugonjwa wa korona, kauli iliyotafsiriwa kuwa ni uthibitisho wa hali halisi ilivyo japo serikali imekuwa ikificha ukweli huo.



31 Mar 2020


Huenda kuna watakaosema wakati huu ambapo nchi na dunia ipo kwenye kipindi kigumu kutokana na janga la krona, si muda mwafaka wa kutupiana lawama. Lakini vipi kama lawama hizo zinaweza kusaidia kuleta mabadiliko chanya katika jitihada za kukabiliana na janga hilo?

Kuna mfululizo wa matukio yanayoashiria bayana kuwa Rais Magufuli ana mapungufu ya kiuongozi kila wakati Tanzania yetu inapokumbwa na majanga. Tukio kubwa zaidi ni lile la tetemeko la ardhi Kagera ambapo kwanza alipuuza kutembelea wahanga kwa siku kadhaa, na alipoamua kuwatembelea, akaishia "kuwasemea ovyo" kwa kudai si yeye aliyesababisha tetemeko hilo.


Kwanini tukio hili ni kubwa zaidi? Si tu kwa vile liliathiri watu wengi lakini pia kwa sababu Magufuli anatokea eneo hilo. Kwa lugha nyingine, kama anaweza "kuwafanyia hivyo ndugu zake," kwaninia shindwe kwa "watu baki"?

Matukio mengine ambayo yalipuuzwa na Magufuli ni pamoja na maombolezo ya askari wetu waliouawa huko DRC walikokuwa wakishiriki operesheni za kikosi cha Umoja wa Mataifa cha kulinda amani nchini humo. Licha ya kuwa Amiri Jeshi Mkuu, hakushiriki kuaga miili ya mashujaa wetu hao.


Janga jingine kwa taifa ambalo Magufuli alilipuuza nivifo vya wanafunzi kadhaa wa shule ya St Lucky huko Arusha

Kadhalika, Magufuli alipuuzia janga jingine lililotokea kanda ya Ziwa ambapo mamia walifariki katika ajali ya kivuko cha MV Nyerere


Na akapuuzia pia janga la mlipuko wa lori la mafuta uliopolekea vifo kadhaa

Na kama alivyopuuzia janga la vifo vya mashujaa wetu waliouwa huko DRC, Magufuli hakutokea kwenye kuaga miili ya polisi waliouawa huko MKIRU, licha ya kuwa Amiri Jeshi Mkuu

Katika janga hili la korona, mwenendo wake tangu mwanzo umekuwa ni mwendelezo wa dharau zake kwa majanga yanapolikumba taifa letu. Baada ya Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kutangaza kuwa korona imeingia Tanzania, ilimchukua Magufuli siku 10 hivi kuongea lolote kuhusu janga hilo.

Na alipofungua mdomo wake, akaongea vitu vya ovyo kabisa. Akiwa Kanisani, aliweka kando uanasayansi wake na kudai kuwa "ukimwi unaua, malaria inaua, na ajali pia zinaua," na kusema kuwa "tunatishana sana (kuhusu korona). Haya si maneno ya kuyatarajia kutoka kwa kiongozi mkuu wa nchi ambaye pia ni mfariji mkuu.



Baadaye akahutubia taifa na kuendelea kutoa ujumbe usio na tija.



Baada ya ukimya wa siku kadhaa akaibukia tena huko Dodoma ambapo wakati taifa likiwa kwenye hofu na mashaka ya janga hilo la korona, mkuu huyo wa nchi akaonekana akifanya mzaha kwa kujilaza kwenye mawe.



Na majuzi alionekana akipuuza ushauri wa kitaalamu dhidi ya maambukizi ya korona unaowataka watu kuepuka mikusanyiko.

Na hii ilikuwa baada ya matukio makubwa mawili huko Dodoma yaliyosababisha mkusanyiko - kikao cha baraza la mawaziri na wakuu wa vyombo vya dola, na baadaye kupokea ripoti za TAKUKURU na CAG.
Image

Image

Kwa minajili ya kumbukumbu, mwaka juzi, mwanasiasa nguli wa upinzani Tundu Lissu alihoji kasumba hiyo ya Magufuli kujitenga na majanga ya kitaifa.

Huu sio tu ni mwaka wa tano tangu Magufuli aingie madarakani lakini pia ni mwaka wa uchaguzi mkuu mwingine (kama ataruhusu). Waweza kujiuliza "anapata wapi jeuri hiy ya kupuuzia majanga ya kitaifa miaka yote hii na hata mwaka huu wa uchaguzi?" Jibu ni kwamba anafahamu fika kuwa haitomgharimu chochote. Kwa upande mmoja wapinzani wetu wamekuwa watu wa maneno zaidi kuliko vitendo, ilhali wananchi nao wakiwa bize na ubuyu. Laiti Magufuli angehisi "kuna adhabu inamsubiri" asingefanya dharau hizi. 

Lakini hata kama wapinzani wameshindwa kushikia bango hilo, na wananchi wako bize na ubuyu, ni jukumu letu sie wachache wenye uthubutu wa kukosoa kutochoka kukemea maovu kama haya. Maana sote tukikaa kimyaatadhani tunaafiki kasumba hiyo isiyopendeza.

Nimalizie makala hii kwa ujumbe huu muhimu kuhusu janga la korona.



22 Mar 2020


#Thread: Awali nilipangilia kuwa thread hii iwe maalum kwa ajili ya kueleza jinsi hali ilivyo hapa Uingereza kuhusiana na janga la #Coronavirus kwa matarajio kwamba nanyi huko nyumbani au kwingineko duniani mnaweza kuwa na moja au mawili ya kujifunza. 

Hata hivyo, katika pitapita zangu kabla ya kuandika thread hii nilikutana na makala moja ndefu kuhusu jinsi janga la jorona lilivyoibuka nchini Italia na kwanini nchi hiyo imeathirika vibaya mno, na pia endapo kinachojiri nchini humo ni "template" ya yatayojiri kwingineko. 

Kwahiyo nadhani ni vema nikianza kuongelea kwa kifupi kuhusu makala hiyo, maana ina funzo kwa sie tulioko huku na kwa nyie mliopo huko. 

Kwa kifupi kabisa, moja ya sababu iliyopelekea maambukizi kuwa makubwa na ya kasi nchini Italia ni kusuasua kwa mamlaka kuchukua hatua stahili. 

Kwa mujibu wa makala hiyo, Italia ilikuwa na fursa nzuri ya kujikinga na janga hilo endapo tu kusingekuwepo dhana kwamba "korona ni sawa na mafua tu," (nikamkumbuka MwanaFA na madai yake ya "malaria ni hatari zaidi kuliko korona") na hisia kuwa "korona ni tatizo la China pekee. "

Kilichopaswa kufanywa na mamlaka za taifa hilo ni
(a) "kuyatenga" maeneo yenye maambukizi
(b) kuzuwia movements za watu kitaifa na kuhakikisha sheria kali zinatumika kuhakikisha utekelezaji
(c) mfumo wa mawasiliano usiokanganya kutoka kwa mamlaka husika kwenda kwa wananchi. 

Inaelezwa kuwa katika siku za mwanzo za mlipuko wa janga hilo, Waziri Mkuu wa Italia Conte na viongozi wengine wa ngazi zajuu walijaribu kujenga picha kuwa ugonjwa huo sio tishio kwa nchi hiyo. Walijenga imani feki kuwa mambo ni shwari #tupovizuri

Na hata maambukizi yalipozidi kukua, maelezo yaliyotolewa ni kwamba ongezeko hilo ni matokeo ya "aggressive testing" yaani jitihada kubwa za kupima watu mbalimbali bila hata kujali kama wana dalili za maambukizi. Na kulijitokeza lawama dhidi ya approach hiyo. 

Kama ambavyo sura ngumu Polepole alivyodai majuzi kuwa Tanzania ikifunga mipaka itaathiri sekta ya utalii, awali baadhi ya viongozi wa Italia ikiwa ni pamoja na Waziri Mkuu Conte walikuwa namtazamo kuwa hatua kali dhidi ya korona zingeathiri uchumi wa nchi hiyo. 

Lakini pengine kikubwa zaidi ni kwamba Italia iliangalia kilichokuwa kinatokea China kama "filamu ya sayansi ya kutunga (science fiction movie) ambayo haiwahusi Wataliano."

Kichekesho ni kwamba hali ilipoanza kuwa mbaya nchini Italia, nchi nyingi hasa barani Ulaya na Marekani ziliangalia kinachotokea huko kama "tatizo la Italia tu" kama ambavyo awali Italia ilivyoiangalia korona kuwa ni "tatizo la China tu."

Mtu anayedhaniwa kuwa ndio "msambazaji wa kwanza wa korona" (Patient One) ni mwanaume wa miaka 38 ambaye Februari 18 alikwenda hospitali akiwa na mafua makali lakini hakuna aliyebaini kuwa ni mwathirika wa korona. Na kibaya zaidi, mgonjwa huyo alikataa kulazwa/

Hata hivyo, siku hiyohiyo jamaa huyo alirudi tena hospitalini hapo na kulazwa kwenye wodi ya kawaida (yaani isiyo maalum kwa ajili ya wagonjwa flani). Siku mbili baadaye alizidiwa mno, akapelekwa ICU ambako vipimo vilionyesha ana maambukizi ya korona

Kabla ya kukutwa na korona, mtu huyo alizunguka sehemu mbalimbali ambapo miongoni mwa matukio muhimu ni kuhudhuria pati tatu, alikwenda kucheza futiboli na pia alishirki kwenye jogging na timu ya soka. Yote hayo yalijiri wakati mtu huyo tayari ana maambukizi ya korona

Lakini la kupigia mstari ni kwamba hakuwahi kukutana na mtu yeyote kutoka China wala kutembelea China. 

Maana yake ni kwamba mtu huyo aliambukizwa humohumo Italia, which means kabla yake tayari kulikuwa na mtu/watu wenye maambukizi ya ugonjwa huo. 

Kwa kumalizia kuhusu kilichojiri Italia, moja ya vitu vilivyochangia sana mkanganyiko katika siku za awali ni kitu wanaita "infodemic" yaani kama "pandemic ila inayohusu information."

Kwa hapa Uingereza, hali ni mbaya. Na inatarajiwa kuwa mbaya zaidi. 

Tatizo la hapa ni kama ilivyokuwa Italia, ambapo kulikuwa na kusuasasua kuchukua hatua stahili. Kwa mfano, badala ya "kufunga kila kitu" mapendekezo ya mwanzo yalikuwa kitu kinaitwa "herd immunity."

Herd immunity ni kuacha maambukizi yasambae kisha wingi wa walioambukizwa upelekee kinga ya baadaye dhidi ya wasioambukizwa. 

Matarajio ni kwamba mtu akishaambukizwa virusi vya ugonjwa husika na kupona, anakuwa na kinga ya kuzuwia kuambukizwa tena. 

Lakini wazo hilo la herd immunity lilipingwa vikali hasa baada ya kubainika kuwa lingeweza kupelekea vifo laki mbili unusu au zaidi. 

Kwahiyo serikali ya Waziri Mkuu Boris Johnson ikaja na mkakati wa "watu kujitenga" (social distancing). 

Social distancing inamaanisha hatua kama wafanyakazi kutokwenda makazini na kufanyia kazi kutoka majumbani, sambamba na watu kukwepa kukutana kusiko kwa lazima. 

Kadhalika, mkazo umewekwa kwenye kuongeza kasi ya kupima watu wenye dalili za maambukizi ya korona. 

Sambamba na hilo ni hatua kali dhidi ya mikusanyiko, na kufungashule, sehemu za starehe mabaa, na kupunguza safari za vyombo vya usafiri. Kadhalika, serikali imewekeza vya kutosha kwenye tafiti mbalimbali za kusaka kinga na tiba ya korona. 

Vilevile serikali imechukua jukumu la kulipa asilimia 80 ya mishahara ya waajiriwa ili kuwezesha waajiri kuruhusu wafanyakazi wao wasiende kazini au wafanye kazi kutokea nyumbani. Ikumbukwe pia kuwa hapa watu wasio na kazi hulipwa posho ya kujikimu na ya makazi. 

Inatarajiwa kuwa wiki 12 zijazo zitakuwa ngumu sana kwa nchi hii kwa sababu ndio kipindi ambapo jitihada kubwa zinafanyika kuzuwia maambukizi mapya sambamba na kuzuwia kusambaa kwa maambukizi yaliyopo huku ikitarajiwa kuwa mamilioni ya watu wataweza kujipima wenyewe majumbani. 

Tayari makampuni mbalimbali yamesitisha uzalishaji wa bidhaa zao na kuelekeza nguvu kwenye uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zinazohitajika katika kipindi hiki cha janga la korona hapa Uingereza. Lakini ni ngumu kubaishiri kuwa hatua hizo zinazochukuliwa muda huu zitafanikiwa kukabili janga hilo.

Kwa upande mmoja, ugonjwa huo ni mpya na upya huo unapelekea ugumu wa kuuelewa vizuri. Kwa mfano hakuna uhakika wa kutosha kuwa mtu akipona hatoambukizwa tena. 

Kuhusu huko nyumbani, kwa kweli mie binafsi nina wasiwasi mkubwa. Kwa upande mmoja, licha ya majigambo ya watawala wetu, sie ni masikini wa kutupa. Hatuna uwezo wa lolote bila kutegemea wafadhili. Kibaya ni kwamba wafadhili wetu nao wapo vitani dhidi ya korona. 

Lakini pengine adui mbaya zaidi kwetu ni kasumbailiyoota mizizi ya kufanya kila jambo kuwa ni la kisiasa. Majuzi mmemsikia sura ngumu Polepole akiufananisha ugonjwa wa korona na wapinzani. Na akajigamba kuwa kama wanavyomudu kupambana na wapinzani basi wataimudu korona pia. 

Wakati ambapo taifa linapaswa kuwa kitu kimoja, hawa wahuni wanaleta mzaha wa siasa. Lakini korona hii si ya kuchezewa maana haibagui kati ya huyu wa chama tawala na huyu mpinzani wala kiongozi na raia wa kawaida. 

Pia tuna tatizo la "infodemic."Pandemic ya information. Kwa upande mmoja ni jitihada za akina Bashite kutumia watu kuhadaa kuwa hali ni shwari, kosa ambalo kama umefuatilia vema thread hii linaigharimu Italia na hata Uingereza na Marekani. 

Lakini pengine baya zaidi ni taarifa ninazopokea kila siku kuwa sehemu kadhaa wananchi wamepigwa marufuku "kuongelea korona," ikiwa ni pamoja na watumishi wa sekta ya afya kutishwa kwamba wakiripoti matukio ya korona kwenye hospitali zao wataadhibiwa. 

Mwisho, tuna Bwana @MagufuliJP ambaye hadi leo sijui siku ya ngapi hajaona umuhimu wa kujitokeza hadharani kuongea na Watanzania. Hizi sio dharau tu bali ni kukosa utu. Lakini hali hiyo imeshazoeleka sasa. Kila linapotokea janga anaingia mitini. 

Hata hivyo, tunashukuru tumefanikiwa kupata uongozi mbadala wa Mheshimiwa @zittokabwe ambaye juzi alihutubia taifa kuhusu janga la korona, hotuba bora kabisa yenye taarifa za kutosha na iliyojaa upendo kwa Watanzania. Icheki hapa (youtu.be/Jc7ZD3PDrXc)

Nimalizie kwa kuwasihi nyote mchukue tahadhari dhidi ya janga hili. Pia ni muhimu kukazania sala/dua. Pia tufahamishane taarifa mbalimbali hususan zinazofichwa kwa minajili ya kisiasa au zozote zile zitakazoisaidia jamii kukabiliana na korona.

Be safe. Jumapili njema

UPDATE: Hatimaye Rais Magufuli amehutubia Taifa japo baadhi ya kauli zake zinaweza kuwa kukwaza jitihada za mapambano dhidi ya #coronavirus. Pichani ni baadhi ya kauli hizo





Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.