Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts
Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts

18 Sept 2016


Majuzi nilikutana na tweet ya rafiki yangu Profesa Kitila Mkumbo ambayo kidogo ilinitatiza. Mwanataaluma huyo ambaye ni pamoja na majukumu yake ya uhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni mshauri wa kitaalamu (consultant) wa taasisi ya Twaweza ambayo majuzi ilichapisha utafiti wake kuhusu masuala mbalimbali yanayoihusu Tanzania.


Tweet ya Profesa Kitila iliyonigusa ni hii hapa chini




Tafsiri ya Kiswahili ni kwamba "tafiti za Twaweza zinawahoji Watanzania, sio tabaka la Watanzania wasomi pekee waliosheheni kwenye mitandao ya kijamii. Katika Tanzania, mitandao ya kijamii hairandani na dunia halisi."



Kutokana na kuguswa kwangu, nilimjibu Profesa Kitila kama ifuatavyo


Nikimaanisha "inasikitisha pale watu wa tabaka halisi la wasomi kama wewe Profesa mnaposhindwa kutambua ni jinsi gani mitandao ya kijamii imebadilisha jinsi tunavyowasiliana."


Na Profesa 'akajitetea' kuwa anaelezea tu 'hali halisi,' na sio kama hathamini mitandao ya kijamii


Niliamua kuahirisha mjadala huo hadi siku nyingine licha ya ukweli kuwa siafikiani na mtazamo wa Profesa Kitila kwamba hali halisi ni kuwa mitandao ya kijamii hairandani na dunia halisi. Sawa, kuna vitu vingi/watu wengi feki katika mitandao ya kijamii, matajiri mtandaoni ilhali masikini wa kutupwa katika maisha yao halisi, furaha mitandaoni lakini majonzi katika maisha halisi, na vitu kama hivyo.

Hata hivyo, miongoni mwa vitu chanya kuhusu mitandao ya jamii ni katika jinsi inavyorahisisha maisha yetu. Na katika hili sio kwa tabaka la wasomi pekee bali takriban kila mtu mwenye uwezo wa kutumia inteneti. 

Na kama kuna kundi ambalo bado linasuasua katika matumizi ya mitandao ya kijamii hukoTanzania basi ni hilo la wasomi. Wakati kwa huku nchi za Magharibi ni suala la kawaida kwa watu wa tabaka la juu kuwasiliana na wenzao wa tabaka hilo au hata wa tabaka la chini kwa meseji, iwe SMS au Whatsapp, kwetu sie 'vigogo' wengi bado wana 'fikra za mwaka 47' kwamba kumtumia mtu meseji ni kama 'mtu amefulia, hana uwezo wa kupiga simu.'

Enewei, lengo la makala hii sio kuelezea kuhusu mjadala huo mfupi kati yangu na Profesa Kitila bali kutoa darasa kuhusu namna ya kurekodi call ya whatsapp na jinsi ya ku-share na ku-save voicenote ya Whatsapp.

Kwanini darasa hili ni muhimu? Kwa sababu Whatsapp imekuwa mkombozi wetu mkubwa katika kukwepa gharama za mawasiliano hususan kwa sie tunaofanya mawasiliano ya kimataifa.

Na kwanini unaweza kuhitaji kurekodi Whatsapp call? Well, labda ni kwa sababu unahitaji kuisikia call hiyo baadaye, lakini pia pengine kuna mtu anakubighudhi na wahitaji kumrekodi kwa minajili ya kumchukulia hatua za kisheria.

KUREKODI WHATSAPP CALL

Katika mazingira ya kawaida, Whatsapp hurekodi calls zote na kuzihifadhi kwenye SD card katika folder liitwalo "Whatsapp calls."
Record WhatsApp Calls
Record WhatsApp Calls




Lakini uwepo wa faili hilo unategemea aina ya simu unayotumia, na iwapo simu yako ina SD card. Na kuna nyakati folder hiyo ipo lakini haina kitu ndani yake.

Kadhalika, inaelezwa kuwa hata kama kuna mafaili yenye calls kwenye folder hiyo, basi calls hizo zina sauti yako tu na sio zote, yaani yako na mtu unayeongea nae.

Kutatua tatizo hilo inabidi kutumia apps zinazorekodi calls. Type 'whatsapp call recorder' na utakutana na orodha ya apps kadhaa. Ushauri wangu ni kwamba jaribu apps mbalimbali kabla hujaamua ipi ni bora zaidi kwa mahitaji yako. 

Mie natumia Samsung Galaxy Note 4 (usipoteze fedha zako ku-upgrade to aidha Note 5 au Note 7 kwani Note bora kabisa ni Note 3 na Note 4, hizo nyingine ni mbwembwe tu. Nitaelezea kuhusu hilo katika makala nyingine) na app ninayotumia kwa kurekodi calls za Whatsapp ni All Call Recorder. 

Kuhusu ku-save au ku-share voice notes za Whatsapp, maelekezo ni rahisi tu. 

1. Highlight voicenote husika kisha click share
2. Share hiyo voice note kwa app inayoweza kuipeleka kwa computer yako. Mie natumia aidha 'Send Anywhere' au 'Pushbullet.'
3. Ukishafikisha kwa computer yako, hatua inayofuatia ni kwenda kwenye website hii www.online-covert.com kisha upload voice yako ambayo itakuwa kwenye mfumo wa faili la sauti wa .opus
4. Ili ku-upload, chagua sehemu iliyoandikwa 'Audio converter.' Kisha kwenye drop-down menu (pameandikwa 'select target format') chagua 'covert to mp3' kisha click 'go.'
5. Utapelekwa kwenye ukurasa mwingine ambapo unatakiwa kwenda palipoandikwa ' upload your audio you want to convert to mp3' kisha bonyeza 'choose your file' itakupeleka mahala ulipohifadhi voice note yako ya Whatsapp kwenye computer yako ikiwa katika mfumo wa faili la sauti wa .opus
6.Upload kisha nenda palipoandikwa 'convert file' katika tovuti hiyo ya www.online-covert.com
7. Ikishamaliza kubadili mfumo wa file la sauti kutoka .opus ya whatsapp voice note kwenda mp3, file husika litakuwa downloaded tayari kwa matumizi yako mengine

Ukitaka ku-save voice note ya Whatsapp, 
1. Highligh voice note husika
2. Chagua share pale juu ya whatsapp
3 Chagua app unayotaka kutumia ku-share
4. Peleka voice note hiyo kwenye app ya ku-save mafaili, zilizo maarufu zaidi ni Google Drive, Dropbox au One Drive. Chaguo ni lako.

Kama una swali au maoni au hata kukosoa basi usisite kunitumia kupitia sehemu ya 'comment.' Endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali za teknolojia na nyinginezo. Karibuni sana 







2 Jun 2016

Hivi kama umeshawahi kutishiwa kifo huko nyuma, kwa maana ya vyombo vya dola kukutaarifu kuwa maisha yako yapo hatarini, utajisikiaje ukipata barua-pepe kama hiyo niliyoiambatanisha hapo chini?

Naam, huko nyuma, nilishawahi kufahamishwa na vyombo vya usalama hapa Uingereza kuwa kuna mpango wa kunidhuru. Nilielezea kwa kirefu kuhusu tukio hilo la kutisha HAPA. Sasa mambo kama haya yakishakutokea maishani, unajifunza kutochukulia vitu kirahisi, kwa lugha nyingine, 'unakuwa unaishi kwa machale.' Sio kama inazuwia kwa asilimia 100 uwezekano wa mtu kudhuru, lakini angalau inapunguza nafasi za mwenye nia ovu.

Sasa leo naingia kwenye barua-pepe zangu nakutana na 'tishio' hili. Mwanzoni nilishtuka kidogo, maana hiyo barua pepe ina dalili nyingi za kuonyesha ni ya kweli. Nikajiambia kuwa kabla ya kukimbili kuripoti polisi, hebu niangalie anwani ya aliyeituma kwangu. Nikagundua kuwa hiyo https://goo.gl/zj173Y ni email address ya mzee mmoja mstaafu huko Marekani. 

Kisha nika-Google "I have been paid to kill you" nikabaini kuwa ni utapeli maarufu mtandaoni japo ukikumbana nao mara ya kwanza waweza kudhani ni wa kweli. Inaelezwa kuwa ukishatumiwa email ya vitisho kama hiyo, mtumaji anakuonya usiwasiliane na vyombo vya dola, na kukutaka uwasiliane nae ndani ya masaa 24. Ukijibu tu basi vitafuata vitisho zaidi, lakini pia utaambiwa uanze kufanya malipo ili kumwezesha huyo 'muuaji amuuwe mtu mwingine badala ya wewe aliyetumwa kukuuwa.' Yaani matapeli hapo wanakujengea picha uwaone kama wasamaria wema wanaookoa maisha yako.

Kwahiyo, ukipokea email kama hii, IPUUZE. USIIJIBU, maana ukiijibu tu utawapa moyo matapeli hao kukutisha zaidi. Puuza na block address ya aliyeituma (not that itasaidia ku-block, kwa sababu hao matapeli wana maelfu ya email feki). La muhimu hapa sio email bali maudhui ambayo ni UTAPELI. Kuwa makini 

Nimeona niwashirikishe wasomaji wapenda ili kesho na keshokutwa, ukikumbana na utapeli huu, usije uka-panic. Ila kwa hakika, ni vigumu kupuuza vitisho vya matapeli hawa laiti wanachotishia kishawahi kukutokea maishani.

Endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali za teknolojia na makala nyinginezo. 

30 May 2016

Mitandao ya jamii imeturahisishia maisha kwa kiasi kikubwa. Sasa tunaishi katika dunia kama kijiji ambapo tukio likotokea sehemu moja ya dunia linafahamika sehemu nyingine muda huohuo bila kutegemea radio, runinga au gazeti pekee. Kadhalika, mitandao ya kijamii imetuwezesha kufahamiana na watu wengi popote walipo duniani bila kukutana ana kwa ana.

Pamoja na mazuri mengi ya mitandao ya kijamii, kuna upande wa pili usiopendeza kuhusu mitandao hiyo ya kijamii. Licha ya kutupatia fursa ya kufahamiana na watu mbalimbali muhimu, mitandao hiyo pia imetoa fursa kwa watu waovu wanaoitumia kwa minajili ya kufanya maovu yao.

Katika makala hii ninaongelea kuhusu tishio kubwa na lililotapakaa kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook, ambapo watu waovu huweka hufungua akaunti feki na kuweka profile feki zinazoambatana na picha za warembo wa kuvutia. Watu hawa wanaweza kuwa aidha wanawake au wanaume lakini hiyo haijalishi kwa sababu lengo lao sio zuri.

Wanachofanya ni rahisi. Wanafungua akaunti feki kwa maana ya jina na taarifa husika, kisha wanaweka picha kadhaa za msichana mrembo. Picha zinazotumika zaidi ni za warembo wa Afrika Kusini. Kama wengi wetu tunavyofahamu, mabinti wengi wa nchi za Kusini mwa Afrika wamejaliwa shepu zenye mvuto. Kwahiyo, tapeli husika anaweka picha kama tano hivi kwa kuanzia, nyingi au zote zikiwa katika pozi za kuvutia kama sio kutamanisha.

Baada ya hapo wanaanza kuomba urafiki (friend requests) kwa kasi ya kimbunga. Kwa makadirio ya chini, mara baada ya kukamilisha profiles zao feki, matapeli hao hutuma friend requests kati ya 100 hadi 300 kwa mkupuo.

Jinsi ya kuwatambua sio ngumu sana. Cha muhimu nikuzingatia kanuni muhimu ya matumizi ya mtandao (Internet) yaani "ukiona ni kizuri kupita maelezo, basi kitlie shaka," wanasema "if it is too good to be true, them may be it is not true." Kanuni hiyo pia ina umuhimu mkubwa katika matumizi ya barua-pepe. Ukipata email kutoka kwa mtu usiyemjua anayedai ana mamilioni ya dola na anataka kuweka kwenye akaunti yako, huyo ni tapeli tu. Hakuna mtu mwenye akili timamu, hata awe tajiri kiasi gani, ambaye yupo tayari kumpatia mtu japo dola 10 tu (achilia mbali hayo mamilioni) mtu asiyemjua.

Kwahiyo, ukipata friend request kutoka kwa binti mrembo kupindukia ilhali hamjuani, basi washa king'ora cha tahadhari. Kitu cha kwanza kabisa ni kuangalia profile husika. Angalia mtu huyo amejiunga lini na Facebook. Pili angalia idadi ya marafiki wapya. Ukikutana na profile inasema "X amekuwa friends na Y na watu 100 au zaidi (kwa mkupuo)" basi uwezekano mkubwa ni kwamba huyo ni tapeli 'anakulia taimingi..'

Kingine ni kuangalia aina ya marafiki zake, Mara nyingi matapeli wa aina hiyo hujifanya wa jinsia ya kike lakini friends wao wengi kabisa kama sio wote ni wanaume. Sio dhambi wala kosa la jinai kwa mwanamke kuwa na marafiki wengi wa kiume kuliko wa kike lakini 'unapaswa kuchezwa na machale.'

Lakini ili kupata uthibitisho zaidi, unaweza ku-save moja ya picha za mtu huyo kwenye computer yako kisha nenda kwenye ukurasa wa kutafuta utambulisho wa picha kwenye Google. 

Ngoja nikuelekeze jinis ya kutumia tovuti hiyo inayoitwa Google Image.

1. Kwanza, ni rahisi zaidi kuitumia Google Image kutafuta utambulisho wa picha kwenye computer kuliko kwenye simu au tablet. Kwahiyo maelezo ninayotoa hapa ni ya kutumia Google Image kwa computer na sio simu au tablet. Andika anwani hii https://images.google.com 


2. Ukishaingia hapo, bonyeza hapo kwenye alama ya kamera kwa ajili ya ku-search kama ilivyo pichani



3. Ukishabonyeza hapo, bonyeza palipoandikwa 'upload an image' kama inavyoonekana pichani,



4. Kisha bonyeza palipoandikwa 'choose file.'



5. Baada ya kubonyeza hapo, nenda sehemu uliyo-save ile picha unayohisi ni feki.



6. Upload picha hiyo



7. Angalia matokeo 

Njia hiyo hapo juu ni muhimu sana sio kwa ajili ya kuangalia kama picha ni feki kwenye Facebook tu bali kwa kuhakiki picha mbalimbali unazokutana nazo mtandaoni.

Hata hivyo, wakati mwingine matokeo ya Google Images search yanaweza yasikupe jibu unalotarajia. Ushauri wangu ni kuzingatia tahadhari nilizotoa awali. Na kumbuka, "if it is too good to be true, may it is not true."

Waweza ku-accept friend request na kusubiri kama huyo 'binti' ataanzisha maongezi nawe. Mara nyingi, akianzisha maongezi, anaweza kukuomba namba ya simu au ya  Whatsapp. Ukimwomba yake atakwambia simu imeharibika aua imeibiwa. Sasa katika mazingira ya kawaida tu, waweza kushawishika kusema "basi nitakununulia simu mpya" au "nitakutumia simu mpya." Hapo utakuwa umeshajigeuza ATM.

Hata hivyo, haina maana kuwa kila binti mrembo atakaye-request friendship kwenye Facebook ni tapeli. Na sio kila friend atakayekuomba msaada kwa Facebook ni tapeli. Kuna watu wanaomba misaada ya dhati. Cha muhimu ni "kuwa na machale."

Ni muhimu kutambua kuwa ushauri niliotoa hapo juu haumaaniishi kwamba 'matapeli wa Facebook' ni mabinti au wanawake pekee. Tunaishi zama za ajabu kabisa ambapo kuna ' vijana wengi tu wa kiume au wanaume wazima wanaowinda akinadada au kinamama wa kuwalea au kuwatapeli.' Kwahiyo ushauri huo ni kwa jinsia zote. 

Kwa akinadada au kinamama , ukikutana na 'handsome boy' mwenye dalili kama hizo hapo juu, basi ni muhimu kuskilizia 'machale' yako. Ndio kuna akina Brad Pitt kibao ambao bado wapo single na wanatafuta marafiki wa kike au wenza, lakini wengine ni matapeli tu.

Endelea kutembelea blogu hii kwa makala mbalimbali kama hii na nyinginezo. Na ususahau ku-share na mwenzio kwa sababu SHARING IS CARING.

19 May 2016


Kuna msemo wa Kiingereza unaoweza kutafsiriwa hivi, "thamani ya fedha ni matumizi." Pesa isiyoweza kutumika haina thamani, inabaki kuwa karatasi tu lenye picha ya kiongozi au alama fulani. Vivyo hivyo, thamani ya elimu/uelewa ni katika kushirikisha watu wengine. Ukiwa na elimu ya kutosha au uelewa mkubwa lakini ikabaki kichwani mwako tu bila kutumiaka basi haina umuhimu. Ni katika mantiki hiyo, sie wengine tumekuwa waumini wakubwa wa filosofia isiyo rasmi ya 'Sharing Is Caring' ambayo mara nyingi huandikwa #SharingIsCaring.

Leo ningependa ku-shea nawe msomaji mbinu muhimu ya ku-post kitu mtandaoni ili kioneknaje au kusomwa na watu wengi. Yaani hapa nazungumzia kuhusu ku-update status yako Facebook iwe ya maneno au picha, au ku-tweet huko Twitter, au ku-post picha yako hujo Instagram.

Tuanze na Facebook. Muda mwafaka wa ku-update status yako ili iweze kusomwa na watu wengi zaidi ni kati ya saa 3 asubuhi hadi saa 1 usiku, lakini muda bora kabisa ni saa 7 mchana hadi saa 9 alasiri.  

Kwa upande wa Twitter, muda mwafaka wa ku-tweet kitu kinachoweza kusomwa na watu wengi zaidi ni saa 6 mchana na kati ya saa 11 jioni na saa 12 jioni.

Kwa Instagram, muda mwafaka ni alfajiri, kwa maana watu wakiamka na kuingia kwenye app hiyo wakutane na picha yako.Lakini mtandao huu ni kimeo na jipu kwa Tanzania. Kwahiyo hata kuelezea kanuni zake ni sawa na kupoteza muda. Mtandao huu umetawaliwa na vitu vichafu na visivyopendeza. Binafsi japo bado ni memba huko lakini siutumii kwa sababu umesheheni kila aina ya maovu.

Maelezo hayo juu ni maalum kwa watu wenye ratiba zao nyingine lakini wanapenda kuwasiliana na jamii kwa kutumia mitandao ya kijamii. Maelezo hayo hayana maana kwa wenzetu ambao wapo mtandaoni kutwa kucha. Yes, kuna wenzetu wapo mtandaoni muda wote.

Kadhalika, maelekezo hayo ni ELEKEZI tu, kwa maana kwamba sio lazima usubiri muda huo mwafaka ndio uposti kitu chako. Muda huo elekezi ni mwafaka kwa minajili ya kuwafikia watu wengi zaidi.

Pichani chini ni infograph kuhusu nilichoeleza hapo juu



Endelea kutembelea blogu hii kwa mada mbalimbali za teknolojia, sambamba na makala zangu za kila wiki katika jarida la Raia Mwema, mada mbalimbali za intelijensia, burudani na michezo, maisha, na kadhalika. Karibuni sana

18 May 2016



Tukubaliane kwamba japo wengi wetu twapenda kutumia mtandao, hususan kutembelea mitandao ya kijamii kama vile Faceboo, Twitter, Instagram, nk bado kuna uelewa mdogo wa mbinu mbalimbali ambazo laiti zikutumika zaweza kuleta ufanisi zaidi katika matumizi ya mtandao au mitandao hiyo ya kijamii.

Siku za nyuma nilikuwa nikiandika makala mbalimbali kuhusu teknolojia lakini kutingwa na majukumu kumesababisha ni we mzembe kidogo. Samahani kwa hile, maana linaathiri ile spirit ya 'Sharing Is Caring.' 

Anyway, long story short, leo nina darasa fupi la jinsi ya kuangalia watu waliotembelea ukurasa (profile) wako wa Facebook. Ni suala la hatua kwa hatua, na nina hakika ukifuata kwa makini utaweza kuona nani ametembelea profile yako. Labda sio muhimu, lakini, hey, kuna watu  wangependa kufahamu vitu kama hivyo.

Samahani, nimejaribu kutafsiri hatua hizo pichani kwa Kiswahili nimechemsha. Natumaini kimnombo kilichotumika sio kigumu, lakini ikitokea mtu hajaelewa vema basi nishtue nitajitahidi kutoa ufafanuzi kwa Kiswahili.


Endelea kutembelea blogu hii kwa mbinu zaidi za mtandaoni pamoja na habari za teknolojia na habari nyinginezo.

Karibuni sana

21 May 2015



Bonyeza HAPA kuangalia specs kamili za simu hii inayotarajiwa kuingia moja kwa moja katika nafasi ya kwanza ya simu bora zilizopo duniani kwa sasa


12 Apr 2015

Wakati mitandao mbalimbali ya kijamii ikiendelea mjadala kuhusu sheria ya kudhibiti uhalifu wa mtandaoni (Cyber Crime Act 2015), ukweli mchungu unabaki kuwa uhalifu huo upo, na unaendelea kuwaathiri watu kila siku.

Jamii inaweza kuendelea kubishana hata kwa miaka 100 kama twahitaji sheria hiyo au la, lakini wahalifu wa mtandaoni wanaendelea kutusumbua kila kukicha. Wakati sheria hiyo haiwezi kumaliza kabisa tatizo la uhalifu wa mtandaoni, angalau kwa kiasi flani itasaidia kumfanya mhalifu atafakari mara mbili kuhusu madhara ya uhalifu wake pindi akikamatwa.

Na kama kuna eneo ambalo wahalifu wa mtandaoni hulipendelea zaidi ni wizi wa nywila, au kwa kimombo PASSWORD. Lakini kinachowafanya wahalifu hao kupendelea wizi wa nywila sio kwa vile wakifanikiwa kuiba watakuwa na 'control' ya akaunti yako bali pia ukweli kwamba watu wengi hufanya makosa wakati wanapofungua akaunti mtandaoni kwa kuchagua nywila dhaifu.

Pengine ushamsikia shushushu mmoja maarufu kabisa duniani aitwaye EDWARD SNOWDEN. Kama hujawahi kumsikia, basi ngoja nikuhabarishe.Huyu jamaa alikuwa anafanya kazi kama mchambuzi katika moja ya taasisi kubwa za ushushushu nchini mMarekani, inayojulikana kakma NSA, yaani National Security Agency. Hawa jamaa kazi yao ni kunasa mawasiliano- iwe ya email, simu au njia nyingine yoyote ile. Sasa Bwana Snowden, kwa kukerwa na ukiukwaji wa haki za binadamu uliokuwa unafanywa na mwajiri wake, akaamua kumwaga siri hadharani.Akawapatia wanahabari, hususan wa gazeti la Guardian la hapa Uingereza, data kibao zilizokuwa zikionyesha jinsi NSA ilivyokuwa ikiwapeleleza Wamarekani na watu wengike kibao duniani.

Sasa, kama ilivyo kawaida kwa taasisi za ushushushu, ukiweka hadharani madhambi yao unakuwa adui yao.Hivyo ilimlazimu Bwana Snowden kutoroka Marekani, na kwa sasa amepata hifadhi ya ukimbizi nchini Russia.

Siku nafasi ikiniruhusu nitaelezea kwa kirefu kuhusu mkasa wa shushushu huyu.Ila kwa leo nitazungumzia ushauri alioutoa hivi karibuni kuhusu nywila imara, itakayowapa kibarua wahalifu wa mtandaoni kuihujumu.

Snowden akiongea katika mahojiano na mtangazaji wa televisheni na mchekeshaji, John Oliver, alieleza kuwa nywila za watu wengi ni dhaifu mno kiasi kwamba inamgharimu mhalifu wa mtandaoni chini ya sekunde moja kuhujumu nywila yenye tarakimu nane.

"Nywila yangu ina tarakimu tano," alieleza Oliver. "Huo sio utani.Kwahiyo hiyo ni mbaya,sawa?" Snowden alikubaliana nae kwamba hiyo ni mbaya sana.

Kwahiyo watu wafanyeje kuhusu nywila zao? Wakati pendekezo la Oliver kuwa na nywila kama 'limpbiscuit4eva' lilionekana halifai,Snowden alikuwa na ushauri mzuri.Sahau kuhusu nywila zinazotumia maneno ya kawaida na badala yake tumia maneno marefu (paraphrases) ambayo ni rahisi kuyakumbuka, kwa mfano 'margaretthatcheris110%SEXY.' Mhalifu wa mtandaoni hawezi kuhisi neno kama hilo na wakati huohuo wewe utabaki na kumbukumbu ya neno hilo refu.


Kwa sie tunaotumia Kiswahili, ushauri wangu ni kujaribu kutumia mchanganyiko wa majina ya ndugu katika familia yenu na namba flani, bila kusahau herufi kubwa japo moja na tarakimu zisizo namba au herufi kama vile £ au % au $.

Unaonaje kama baada ya kusoma makala hii ukibadili nywila yako kuwa imara zaidi na hivyo kukuwezesha kukabiliana na jitihada za wahalifu wa mtandaoni kuihujumu nywila yako?



24 Jan 2015

Whatsapp kwa sasa ni chaguo la wengi linapokuja suala la mawasiliano yasiyohitaji malipo. Awali ilikuwa sio tu haiwezekani kutumia app hiyo katika kompyuta yako bali pia haikuwezekana kuitumia katika 'devices' mbili tofauti kwa namba moja ya simu. Kwa upande mmoja app hiyo haikuwezekana kutumika katika kompyuta, kwa upande mwingine, ili kuitumia katika Tablet yako, ililazimu utumia namba tofauti za simu wakati wa kujisajili, kwani ukitumia namba uliyojisajili kwa simu kwenye Tablet, app hiyo haifanyi kazi tena kwenye simu.

Habari njema ni kwamba sasa waweza kutumia Whatsapp sio tu kwenye Kompyuta bali pia kwenye Tablet yako.

Tuanze na Whatsapp kwenye kompyuta:

1. Kwa kutumia browser ya Chrome, fungua tovuti hii https://web.whatsapp.com/
2. Utakutana na QR code hii


3. Nenda kwenye Whatsapp yako kwenye simu
4. Bonyeza 'menu' (duara ya kijani - kutegemea na aina ya simu yako) kisha nenda 'Whatsapp Web' kama ilivyo pichani chini 


5. Ukibonyeza 'Whatsap Web' itafungua QR Scan kama hapa chini (inabidi simu yako iwe na app hiyo ambayo inapatikana Google Play  )


6. Elekeza QR Scanner hiyo kwenye ukurasa huu https://web.whatsapp.com/
7. Kazi imekwisha. Browser yako sasa itakuwa imeunganishwa na Whatsapp yako ya kwenye simu

Kwenye Tablet.

Hatua zote ni kama hapo juu ila tofauti tu badala ya Kompyuta, utakuwa unatumia Tablet. Kumbuka kuwa kwa sasa browser pekee inayoweza kutumika ni Chrome. Pia waweza kutumia.

Ukikwama, nifahamishe kwa comment katika post hii. Karibuni sana.

ANGALIZO: Maelezo haya ni kwa Android devices ambazo ndo nazitumia. Sijafanya uchunguzi kuhusu iOS devices kama iPad au Mac computers.

Share is caring, ukishasoma na kuelewa, mfahamishe na mwenzako


12 Sept 2014

Viber5 videocalls 730x608 Viber introduces videos calls to its mobile chat apps for Android and iOS
App ya mawasiliano ya meseji, VIBER, inazidi kupata umaarufu, na sasa inakuja na feature mpya na muhimu ambapo mtumiaji anaweza kumwona anayempigia kwa video, yaani sasa Viber inawezesha video calls kati ya wanaowasiliana.

App hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa 'imeifunika' app maarufu ya mawasiliano ya meseji, Skype, ilinunuliwa hivi karibuni na kampuni kubwa ya biashara za mtandaoni (e-commerce) Rakuten ya Japan  kwa dola milioni 900 imetanua mabawa yake kwa kuwezesha video calls kwa simu za Android na iOS.

Viber ilianza jaribio la video calls katika app yake kwenye desktop lakini sasa imhamishia uwezo huo kwenye app ya simu pia.

Kadhalika, toleo jipya la Viber (Viber 5.0) itamwezesha mtumiaji ku-share contacts kwa kutumia QR Code.

Afisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Viber Talmon Marco anasema, "Dhamira yetu haijakamilika...Sasa unaweza kupiga simu kwa video kwa kutumia Viber kwenye PC/Mac yako na kwenye simu katika namna ya kukuridhisha kabisa."

Viber sio app ya kwanza ya meseji kuwezesha video calls. Skype, Line, WeChat, Kakao na lundo la apps nyingine zina feature hiyo pia.

Downloads: Viber kwa Android, iOS, Windows Phones, Blackberry, Nokia, Windows 8 na Viber kwenye desktop yako



10 Sept 2014

Hacked: Hackers revealed nearly 5 million Gmail account details and passwords on the Bitcoin Security site
Takriban passwords milioni tano za akaunti za email za Gmail zimekuwa hacked na kutundikwa kwenye tovuti moja ya hackers wa Russia inayojulikana kama Bitcoin Security. Kufuatia hatua hiyo, kampuni ya Google inayomiliki Gmail imewashauri wenye akaunti za Gmail kubadili passwords zao haraka iwezekanavyo kama hatua ya tahadhari.

Hackers wamesema kwamba asilimia kubwa ya passwords walizo-leak mtandaoni ni za watumiaji wa Gmail nchini Uingereza, Urusi na Hispania, na nyingi ya akaunti hizo 'ziko hai' kwa maana kwamba zinatumika.

Kwa watumiaji wa Gmail watakuwa wanafahamu kwamba mtu akijua password yako ya email anaweza pia ku-access Google Drive na apps kadhaa zinazotumia 'credentials' za ku-log in katika akaunti ya email.

Msemaji wa Google ameeleza kwamba kampuni hiyo inafahamu kuhusu tukio hilo na inawashauri watumiaji wa huduma hiyo kubadili passwords zao.

Kadhalika, Google wanashauri kutumia mbinu inayojulikana kama 'two-steps verification' ambayo kabla ya kuweza ku-access akaunti yako inabidi uingize code uliyotumiwa kwa simu yako.

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka kwa vyanzo mbalimbali mtandaoni




After a wait of more than two years, Apple has finally taken its first foray into the world of wearables with the unveiling of the Apple Watch. 

The rectangular wristwatch was unveiled alongside two new, larger iPhone handsets, and a new mobile payment system called Apple Pay.

The iPhone 6 has a 4.7-inch screen, curved edges and will be available in dark black and gold, while the iPhone 6 Plus has a 5.5-inch screen and 185 per cent more pixels than the 5S.

Scroll down for videos
The watch will be available from early 2015 and prices start at $349.  The straps are interchangeable, and the faces are customisable (pictured). The watch also understands questions in messages, and offers pre-selected answers, and messages can be dictated to the iPhone through the watch
The watch will be available from early 2015 and prices start at $349. The straps are interchangeable, and the faces are customisable (pictured). The watch also understands questions in messages, and offers pre-selected answers, and messages can be dictated to the iPhone through the watch

APPLE WATCH FEATURES 

The watch has a completely new user interface, different from the iPhone, and the 'crown' on the Apple Watch is a dial called the 'digital crown.'
Users can turn the crown to zoom in and out on a map, or scroll a list. The crown can also be pressed to take the user back to the home screen.
Different areas on the watch face can be customised with taps and swipes, and force touches.
The Apple Watch goes on sale early 2015 and prices will start at $349
The Apple Watch goes on sale early 2015 and prices will start at $349
The Glances feature shows info users would like to see, similar to Google Now, and is accessed by swiping the screen up from the bottom.
Music can also be controlled on an iPhone through the Apple Watch.
Built-in is a 'taptic engine' that responds to a subtle vibrations users feel on their wrist for notifications.
It understands questions in messages and then offers pre-selected answers, and messages can be dictated to the iPhone.
Users can also talk to the watch and send a voice reply, or have it transcribed to them.
There is no keyboard on the watch, and messages can only be sent through dictation, or emoji.
Siri also is built into the Apple Watch. 
The Apple Watch, which received a standing ovation at the event, has a rectangular bezel, rectangular sapphire crystal screen, and curved edges and is made of metal.

‘Apple Watch is the most personal device we've ever created.’ said Apple chief executive Tim Cook.

‘It's also a comprehensive health and fitness device [and] is precise, synced to the internet, accurate to within 50 milliseconds.'

The watch has a completely new user interface, different from the iPhone, and the 'crown' on the Apple Watch is a dial called the 'digital crown.'

Users can turn the crown to zoom in and out on a map, or scroll through a list. The crown can also be pressed to take the user back to the home screen.

'It can be worn all day, in any occasion,’ continued Mr Cook.

The watch works 'seamlessly' with the iPhone 5C, 5S as well as the iPhone 6 and 6 Plus, and it lets users dictate messages via a microphone on the device.

Its screen is a touchscreen, but it also senses force, and can tell the difference between 'a tap and a press.' For example, pressing down will recognise as a right click.

All the electronics are packed onto a tiny board, sealed up to protect against water. 
The Apple Watch comes in three finishes - Apple Watch, which comes in silver, the Apple Watch Sport and the Apple Watch Edition, which will be available in 18-karat gold.

The wearable will be available from early 2015 and prices start at $349.

Apple didn't specify what the battery life was like on the Apple Watch, but did say it would need to be charged each night.

The watch's straps are interchangeable, and they come in a range of colours and materials, including plastic and leather.

There are two sizes of the watch, dubbed male and female versions, with matching smaller straps and finishes.

Other features include Glances, which shows information users would like to see, similar to Google Now. 

It is accessed by swiping the screen up from the bottom, and shows calendar invites, weather and traffic for example.
 
The watch also understands questions in messages, and offers pre-selected answers, and messages can be dictated to the iPhone through the watch.

Users can also talk to the watch and send a voice reply, or have it transcribed to them.
There is no keyboard on the watch, and messages can only be sent through dictation, or emoji. 
The devices (pictured right compared to the iPhone 5S left) were unveiled by Phil Schiller, senior vice president of Apple's worldwide marketing, at the Flint Center for the Performing Arts at De Anza College in Cupertino. The iPhone 6 will start at $199 on a two-year contract for 16GB, $299 for 64GB and $399 for 128GB
The devices (pictured right compared to the iPhone 5S left) were unveiled by Phil Schiller, senior vice president of Apple's worldwide marketing, at the Flint Center for the Performing Arts at De Anza College in Cupertino. The iPhone 6 will start at $199 on a two-year contract for 16GB, $299 for 64GB and $399 for 128GB
Apple Pay (pictured being demonstrated by Apple's Eddy Cue) is the firm¿s new payment system compatible with the iPhone 6, iPhone 6 Plus and the Apple Watch. If an iPhone is lost, users can suspend all payments via Find my iPhone . This won¿t cancel the cards because card details themselves are not stored on that device
Apple Pay (pictured being demonstrated by Apple's Eddy Cue) is the firm’s new payment system compatible with the iPhone 6, iPhone 6 Plus and the Apple Watch. If an iPhone is lost, users can suspend all payments via Find my iPhone . This won’t cancel the cards because card details themselves are not stored on that device
Apple also unveiled the Apple Watch. It has a rectangular bezel, rectangular sapphire crystal screen, curved edges and is made of metal. The watch has a completely new user interface, different from the iPhone, and the 'crown' on the Apple Watch is a dial called the 'digital crown', which can be used to control apps
Apple also unveiled the Apple Watch. It has a rectangular bezel, rectangular sapphire crystal screen, curved edges and is made of metal. The watch has a completely new user interface, different from the iPhone, and the 'crown' on the Apple Watch is a dial called the 'digital crown', which can be used to control apps

COMPARISON TABLE: IPHONE 6 AND IPHONE 6 PLUS
HANDSETSCREEN SIZESTORAGEFRONT-FACING CAMERAREAR-FACING CAMERABATTERYHANDSET PRICE
iPhone 64.7"16, 32GB, 64GB and 128GB8MP8MP2915 mAh$199 on a two-year contract, $299 for 64GB and $399 for 128GB (TBA UK)
iPhone 6 Plus5.5"16, 32GB, 64GB and 128GB8MP8MP2915 mAh$299 for 16GB, $399 for 64GB, $499 for 128GB (TBA UK)
Amazon Fire4.7"32GB and 64GB2.1MP13MP2400 mAh$449 US (TBA UK)
Samsung Galaxy Note Edge5.6"32GB and 64GB3.7MP16MP3000mAh$649 US (Å“570 UK)
Samsung Galaxy S55.1"16 and 32GB2MP16MP2800 mAhTBA
iPhone 5S4"16, 32 and 64GB1.2MP8MP1560 mAh$709 US (Å“549 UK)
HTC One4.7"32 and 64GB2.1MP4MP2300 mAh$599 US (Å“396 UK)
HTC One M85"16 and 32GB5MP4MP2600mAh$749 (Å“549)
iPhone 5C4"16 and 32GB1.2MP8MP1510 mAh$599 US (Å“469 UK)
Nokia 10204.5"32GB1.2MP41MP2000 mAh$99.99 (Å“519 UK)
Samsung Galaxy S45"16, 32 and 64GB2MP13MP2600 mAh$880 (Å“355 UK)
Nexus 54.95"16 and 32GB1.3MP8MP2300 mAh$349 (Å“240 UK)
On to apps, the Apple Watch has a photo app that shows favourite photos from the iPhone on the screen.

There's also a Maps app, and users can get turn-by-turn directions on the watch, with different vibrations depending on whether they should turn left or right.

Elsewhere, users can also send their heartbeat, via a sensor, and the receiver feels the vibration that matches their pulse.

WHAT IS APPLE PAY? 

Apple Pay is the firm¿s new payment system compatible with the iPhone 6, iPhone 6 Plus (pictured left and right) and the Apple Watch. The mobile system works by holding phone up to a generic card reader and pressing a finger on the TouchID button. The NFC chip is fitted across the top of the phone
Apple Pay is the firm’s new payment system compatible with the iPhone 6, iPhone 6 Plus (pictured left and right) and the Apple Watch. The mobile system works by holding phone up to a generic card reader and pressing a finger on the TouchID button. The NFC chip is fitted across the top of the phone

Apple Pay is the firm’s new payment system compatible with the iPhone 6, iPhone 6 Plus and the Apple Watch.

The mobile system works by holding phone up to a generic card reader and pressing a finger on the TouchID button.

The NFC chip is fitted across the top of the phone.

All details are encrypted and the system stores payment information securely.

It uses the Passbook app and cards that are already on file with iTunes can be saved to it.
Users can also take a picture of their own credit card and add it to the account. This is verified by the card’s bank before being accepted.

If an iPhone is lost, users can suspend all payments via the Find my iPhone service. This won’t cancel the cards, either, because the card details themselves are not stored on that device.

'Apple doesn't know what you bought, where you bought it, and how much you bought it for,’ said Apple's senior vice president of internet software and services and reports Eddy Cue. 

Starting in US with Amex, MasterCard, and Visa, Apple Pay will also work with banks, and covers 80 per cent of the US, claimed Mr Cue. Apple is said to be 'working hard' to bring it to more countries.

More than 22,000 retailers will work with Apple Pay including Macy's, Bloomingdales, Wallgreens, Duane Reade, Subway and McDonalds. McDonalds is even adding Apple pay to its drive-thru.

Elsewhere, Groupon and Uber will work with Apple Pay.

Third party developers can also make apps for the watch.


Initially, generic notifications will just show up.

But developers can extend that notification with something called WatchKit which gives you notifications of your choice.

The devices were unveiled at the Flint Center for the Performing Arts at De Anza College in Cupertino, the same location where Steve Jobs introduced the original Mac 30 years ago. 
The mobile system works by holding phone up to a card reader (pictured) and pressing a finger on the TouchID button.The NFC chip is fitted across the top of the phone
The mobile system works by holding phone up to a card reader (pictured) and pressing a finger on the TouchID button.The NFC chip is fitted across the top of the phone
Apple Pay uses the Passbook app and cards that are already on file with iTunes can be saved to it (pictured) Users can also take a picture of their own credit card and add it to the account. This is verified by the card¿s bank before being accepted
Apple Pay uses the Passbook app and cards that are already on file with iTunes can be saved to it (pictured) Users can also take a picture of their own credit card and add it to the account. This is verified by the card’s bank before being accepted
Following the announcement, Mr Schiller said the iPhone 5C will now be available for free on a two-year contract, and the iPhone 5S will start at $99. Apple did not reveal which network operators would sell the phones
Following the announcement, Mr Schiller said the iPhone 5C will now be available for free on a two-year contract, and the iPhone 5S will start at $99. Apple did not reveal which network operators would sell the phones

It was a star-studded event, attended by the likes of Gwen Stefani, Stephen Fry, Dr Dre and Rupert Murdoch.

In terms of the new handsets, the iPhone 6 will start at $199 on a two-year contract for 16GB, $299 for 64GB and $399 for 128GB.

While the iPhone 6 Plus starts at $299 for 16GB, $399 for 64GB and $499 for 128GB.
The iPhone 6 is 6.9mm and the iPhone 6 Plus is 7.1mm thick, compared to 7.6mm on the 5S. Both devices have Retina HD displays. 
Its screen (pictured) is a touchscreen, but it also senses force, and can tell the difference between 'a tap and a press.'
Its screen (pictured left) is a touchscreen, but it also senses force, and can tell the difference between 'a tap and a press.' For example, pressing down will recognise as a right click. All the electronics are packed onto a tiny board, sealed up to protect against water. Users can turn the crown to zoom in and out on a map (right)
A series of sensors in the Apple Watch can read a user's heart rate, and it uses the GPS from a connected iPhone to track movement. There are two sizes of watch, but three finishes - including Apple Watch Edition in 18-karat gold, Apple Watch silver (pictured), and Apple Watch Sport
A series of sensors in the Apple Watch can read a user's heart rate, and it uses the GPS from a connected iPhone to track movement. There are two sizes of watch, but three finishes - including Apple Watch Edition in 18-karat gold, Apple Watch silver (pictured), and Apple Watch Sport
The watch works 'seamlessly' with the iPhone 5C, 5S as well as the iPhone 6 and 6 Plus, and lets users dictate messages via a microphone on the watch. It tracks fitness and GPS using built-in sensors
The watch works 'seamlessly' with the iPhone 5C, 5S as well as the iPhone 6 and 6 Plus, and lets users dictate messages via a microphone on the watch. It tracks fitness and GPS using built-in sensors

The devices were unveiled by Apple’s senior vice president of worldwide marketing Phil Schiller. Schiller said: ‘It is truly the most beautiful phone you’ve ever seen. These are a new generation Retina displays, we call them Retina HD. They’re bigger - a lot bigger.' =
Both devices also have a 'broader' angle of view, and there is a new feature being launched with this range of iPhones called 'reachability'.
The layers of the new iPhones are pictured, being demonstrated by Phil Schiller, senior vice president of Apple's worldwide marketing
The layers of the new iPhones are pictured, being demonstrated by Phil Schiller, senior vice president of Apple's worldwide marketing
The iPhone 6 has a 4.7-inch screen, curved edges and will be available in dark black and gold, while the iPhone 6 Plus has a 5.5-inch screen and 185 per cent more pixels than the 5S
The iPhone 6 has a 4.7-inch screen, curved edges and will be available in dark black and gold, while the iPhone 6 Plus has a 5.5-inch screen and 185 per cent more pixels than the 5S

Users will now be able to double-tap the home button and the whole display will slide down, making it easier to reach the top buttons.

Speaking of buttons, Apple has also moved the power button to the side of both devices, so it's easier to reach. 
The iPhone 6 is 6.9mm, the iPhone 6 Plus is 7.1mm thick. This graph compares the thickness of the new devices to the iPhone 5S, which was 7.6mm on the 5S
The iPhone 6 is 6.9mm, the iPhone 6 Plus is 7.1mm thick. This graph compares the thickness of the new devices to the iPhone 5S, which was 7.6mm on the 5S

Inside the devices is the new Apple A8 64-bit chip. It has 2 billion transistors and is 13 per cent smaller than the A7.

The 8MP camera has true-tone flash and its camera iSight sensor will focus pixels, and it also has autofocus that's twice as fast as the last generation.

Both devices will also launch on Apple's next-generation software, iOS 8, which features a new messaging app that lets you quickly send voice notes.
The 8MP camera has true-tone flash. The camera iSight sensor will focus pixels, and it has autofocus that's twice as fast as the last generation. The front-facing camera has also been updated for selfies
The 8MP camera has true-tone flash. The camera iSight sensor will focus pixels, and it has autofocus that's twice as fast as the last generation. The front-facing camera has also been updated for selfies
Both devices have Retina HD displays and they have a new interface, that when held horizontally, produces a two-pane display (pictured). This is similar to the iPad mini
Both devices have Retina HD displays and they have a new interface, that when held horizontally, produces a two-pane display (pictured). This is similar to the iPad mini
This makes the processing unit 20 per cent faster, and 50 per cent faster graphics. 
There is also a host of new sensors, including the M8 'motion coprocessor, which will be useful for fitness apps.

M8 can tell the difference between cycling and running, for example, and it can also calculate distance and elevation.

It does this with a barometer, which uses air pressure to measure relative elevation. 
Both devices will also launch on Apple's next-generation software, iOS 8, which features a new messaging app that lets you quickly send little voice notes (pictured)
Both devices will also launch on Apple's next-generation software, iOS 8, which features a new messaging app that lets you quickly send little voice notes (pictured)
Inside the devices (iPhone 6 pictured left and iPhone 6 Plus pictured right) is the new Apple A8 64-bit chip. It has 2 billion transistors and is 13 per cent smaller than the A7. This makes the processing unit 20 per cent faster, and graphics 50 per cent faster
Inside the devices (iPhone 6 pictured left and iPhone 6 Plus pictured right) is the new Apple A8 64-bit chip. It has 2 billion transistors and is 13 per cent smaller than the A7. This makes the processing unit 20 per cent faster, and graphics 50 per cent faster

APPLE WATCH - HANDS ON - IT'S WORTH THE PRICE! 

The first thing that strikes you when you see the Apple Watch in pictures is that it looks a little chunky.

However, slip it on your wrist, and it’s a revelation - very, very light and unobtrusive.
The curved design really does help hide the body of the watch, and Apple’s very minimalist design almost makes it appear to disappear when you put it on.

While some of the watch faces shown were a little garish, we found that with a relatively plain leather strap and a classic watch face, nobody will give you a second glance while wearing one - until, of course, a notification or email comes in.

Even in the early prototype we were able to try, the quality of manufacturing absolutely shines through. This isn’t a gadget, it’s a piece of jewellery.

The sapphire glass is stunning, and feels great to the touch, while the dial at the side has a really solid feel to it.

The addition of Apple Pay is also a huge selling point for keen shoppers - being able to simply tap your watch to pay is potentially one of the phone’s killer feature.

The fitness functions are all a big step forward, particularly the use of heart rate monitoring - while for every day use, the maps app seems like a winner.

While the messaging functions seem a little gimmicky, they are a nice touch and an indicator that you can write 'real' apps for the Apple Watch.

However, the key to its success - and something Apple didn’t really reveal today, will be battery life.
If Apple can get the watch to last a full day of heavy use, then it’s onto a winner - even with an eye watering $349 price tag. 

IPHONE 6 IN ACTION - IT'S SHOCKINGLY BIG - AND ALL HAIL APPLE PAY

Web browsing is great on the iPhone 6's big screen
Web browsing is great on the iPhone 6's big screen

Apple’s new iPhone 6 plus is big - really big. When you see it lying on a table, it dwarfs even its smaller 4.7inch brother with its 5.5inch screen.

The first time you pick it up, it’s slightly off-putting - but the rounded edges really do make a difference. 

It’s surprisingly light as well, and just about possible to hold comfortably in one hand.

Once you’ve got over the initial shock, and learnt how to use the one handed mode (tap twice on the home button, and everything moves to the bottom of the screen so you can get to it easily), then one thing stands out - the screen.

The quality is superb, with bright, sharp colours, that make even the current screen on the iPhone look lackluster.

After a few minutes, you forget about the vast size, and just start wondering you lived with such a small screen for so long.

However, the one feature that really makes the handset really stand out, and the one that will really change your daily life, is Apple Pay.

We were able to try it out, and it really is as simple as Apple says - simply put your fingerprint on the sensor and tap it against a reader.

With the number of retailers Apple has already signed up, this could be the real killer app of the iPhone 6, and more importantly for Apple, a key reason to upgrade.

It’s a shame Apple couldn’t boost the battery life more, but given the increased screen size and features, its a trade-off most users will be happy to take. 
SOURCE: Mail Online


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.