Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts
Showing posts with label TEKNOLOJIA. Show all posts

3 Sept 2014










Chanzo: CNET


Mnyanyasaji wa mtandaoni, Peter Nunn (pichani) anakabiliwa na uwezekano wa kifungo jela baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kumtumia mbunge Stella Creasy  wa jimbo la Walthamstow kwa tiketi ya Chama cha Labour, hapa Uingereza, tweets za kutishia kumbaka.

Mnyanyasaji huyo alitumia mtandao wa kijamii wa Twitter kumwandama mbunge huyo aliyemwita mchawi katika tweets zake.

Nunn alijitetea kwamba hakuzungumzia suala la kumbaka mbunge huyo bali ujumbe  wake ulikuwa utani tu.

Kadhalika alikanusha kuendesha kampeni ya chuki dhidi ya mwanasiasa huyo wa kike, ambaye alikuwa akimsapoti mwanaharakati wa masuala ya wanawake  (feminist), Caroline Criado-Perez, katika kampeni ya  kudai noti ya Paundi 10 ya Uingereza iwe na picha ya mwanamke mwingine zaidi ya Malkia Elizabeth wa Pili ilivyo sasa.

Mnyanyasaji huyo ambaye ni dereva kutoka mji wa Bristol jana alipatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kudhalilisha na kutisha kwa kutumia mtandao wa wazi wa kielektroniki kati ya Juni 28 na Agosti 5 mwaka jana.

Jaji wa mahakama ya wilaya Elizabeth Roscoe alisema, "yeye (Nunn) anasema hadhani mbunge huyo na mwenzie walikwazwa na ujumbe wake. Hapana, siwezi kuamini maelezo hayo hata kidogo."

"Nina uhakika timilifu kabisa kuwa tweets zake zilikuwa na malengo mabaya."

Nunn alionekana kutahayari wakati hukumu hiyo dhidi yake inasomwa.katika mahakama ya City of London.

Baada ya hukumu hiyo, mbunge huyo ambaye hakuwepo mahakamani ali-tweet "sasa kesi ya mnyanyasaji Twitter imekwisha, ujumbe upo wazi: tishio ni tishio, iwe kwenye karatasi, picha au uso kwa uso."

Mnyanyasaji huyo alizana kampeni yake ya za kubughudhi Julai 29 mwaka jana, siku 5 baada ya Benki Kuu ya Uingereza kutangaza kuwa Jane Austen, mwandishi wa riwaya wa Kiingereza wa karne ya 18 atakuwa  sura mpya katika noti za Paundi 10.

Nunn aliposti tweets luluki dhidi ya kwa mwanasiasa huyo wa kike, ikiwa ni pamoja na video 6. Katika tweet yake moja, alieleza kuwa njia mwafaka ya kumbaka mbunge huyo ni kwa kumzamisha majini kwanza.

Baadaye ali-tweet "kama huwezi kutishia kumbaka mtu maarufu (celebrity), kuna haja gani ya kuwa nao?"

Nunn atahukumiwa tarehe 29 mwezi huu na waendesha mashtaka wameeleza kuwa wataomba kibali cha kumzuwia kuwasiliana na Mbunge huyo mwanamke.

CHANZO : Daily Express 

Miongoni mwa vyanzo vya 'matatizo' katika matumizi ya mitandao ya kijamii ni uelewa mdogo wa wengi wanaoitumia mitandao hiyo. Ni vigumu kubainisha sababu moja inayochangia uelewa huo mdogo lakini yayumkinika kuhisi kwamba baadhi ya wenzetu hawapendi kujishughulisha kusaka maarifa/ uelewa.

Lakini pengine kikwazo kikubwa zaidi katika kupata uelewa, si tu kwa matumizi ya mitandao pekee bali kila kitu, ni 'kiburi' cha aidha kutotaka kuuliza pale mhusika haelewi au kufinya anaelewa ilhali haelewi, au kibaya zaidi, kuwavunja moyo wale wanaojitahidi kueneza uelewa wa masuala mbalimbali (mara nyingi huitwa 'wajuaji' kana kwamba kujua kitu na kuki-share ni kosa la jinai).

Tuliopitia JKT twafahamu 'kanuni ya kwanza unapowasili kambini,' yaani kufahamu mahali pa kujisaidia (kichekesho ni kwamba mara nyingi kambi za porini - na nyingi ya kambi za JKT enzi hizo zilikuwa maporini- hazina vyoo, na vikiwepo ni kwa matumizi ya maafande tu. Makuruta hupaswa kutengeneza vyoo katika muda wao binafsi).

Kadhalika, japo ni jambo linalopuuzwa na wengi, ni muhimu kwa kila mtumiaji wa mtandao wa kijamii, na kwa hakika mtandao wowote ule, kujibidiisha kufahamu japo kanuni na taratibu za msingi za mtandao husika, hususan haki na wajibu wake na wa mwenye mtandao. Uelewa huu si tu ni muhimu kwa kurahisisha 'maisha yetu mtandaoni' bali pia waweza kumsaidia mtumiaji kuepuka matatizo ya kisheria pindi akikiuka taratibu na kanuni hizo.

Kwa mtandaoni, kila mtandao, uwe wa kijamii au 'wa kawaida,' una kanuni na taratibu zake. Moja ya taratibu muhimu ni pamoja na haki za mtumiaji na wajibu wake. Miongoni mwa haki hizo ni pamoja na 'taarifa za mtumiaji' wa mtandao husika. Ndio maana ikitokea mtandao ukaweka hadharani anwani ya mtumiaji pasi ridhaa yake, unaweza kufunguliwa mashtaka kwa kukiuka haki za mtumiaji.

Kadhalika, mtandao ukiruhusu (makusudi au kwa bahati mbaya) mtu asiye na mamlaka kisheria kuweka taarifa 'nyeti' za mtu mtandaoni pasi ridhaa ya mhusika, unaweza kujiingiza katika matatizo makubwa ya kisheria

Sasa nimeona huko katika mtandao wa Twitter 'harakati' zinazofanyika kuhusu haja ya kufungwa kwa akaunti ya Twitter ya ndugu yetu, marehemu Betty Ndejembi, aliyefariki hivi karibuni.

Na pengine harakati hizo zinaisaidia jamii kuonyesha umuhimu wa HARAKATI japo kuna baadhi ya wenzetu wanaotafsiri uana-harakati kama kosa la jinai.Binafsi nadhani tatizo la watu wa aina hii ni kuzowea mno kufanyiwa mambo na serikali, taasisi au watu wengine (kwa mfano wanasiasa) kiasi kwamba wanapoona mtu binafsi anachukua msimamo katika suala flani wanamtafsiri ndivyo sivyo. Harkati chanya ni kitu kizuri kwa jamii kwani zaondoa haja ya utegemezi kwa taasisi kama serikali na kuwezesha 'nguvu ya umma.'

Harakati hizo za kutaka akaunti ya marehemu ifungwe zimehusisha ombi kwa mwanasiasa mmoja maarufu ashughulikie suala hilo. Binafsi sina tatizo na waliotoa ombi hilo bali laiti wangejihangaisha japo ku-Google 'how to request Twitter to close a deceased account' (jinsi ya kuiomba Twitter ifunge akaunti ya mtu aliyefariki) wasingehitaji kutuma ombil hilo kwa mwanasiasa huyo. Naomba ieleweke kuwa si dhambi kuomba msaada kwa mtu yeyote yule, let alone mwanasiasa. Lakini kuna masuala ambayo yapo ndani ya uwezo wetu ila tatizo ni uelewa mdogo au kutokuwa na uelewa.

Taratibu za kuiomba Twitter ifunge akaunti ya mtu aliyefariki ziko hivi (tafsiri ya Kiswahili ni yangu):

"Kuwasiliana na Twitter kuhusu mtumiaji aliyefariki...

Kinapotokea kifo cha mtumiaji wa Twitter, twaweza kushirikiana na mtu mwenye mamlaka ya kushughulikia mali (estates) za marehemu au mwanafamilia aliyethibitishwa wa marehemu kuwezesha kufunga akaunti ya marehemu.

Ili kutuwezesha kushughulikia kufunga akaunti (ya marehemu), tafadhali tupatie taarifa zifuatazo:

1. Jina (username) la marehemu katika akaunti yake ya Twitter, yaani katika ishu ya marehemu Betty itakuwa @BettyNdejembi au twitter.com/BettyNdejembi 
2. Nakala ya cheti cha kifo cha marehemu. 
3. Nakala ya kitambulisho kilichotolewa na serikali (kwa mfano leseni ya udereva au hata hati ya kusafiria)
4. Tamko (statement) lililosainiwa linalojumisha vitu vifuatavyo-Jina la kwanza na la mwisho la anayetuma ombil la kufungwa kwa akaunti ya marehemu-Barua pepe ya mwombaji-Mawasiliano (simu, anwani,nk)-Uhusiano wa mwamobaji na marehemu au mali za marehemu (estate)-Dhima ya ombi kwa Twitter (kwa mfano ; ninaomba Twitter ifunge akaunti ya marehemu')-Maelezo mafupi ya kuthibitisha kuwa akaunti husika ni ya marehemu, iwapo jina lililopo kwenye akaunti hiyo halifanani la lililopo kwenye hati ya kifo cha marehemu)-Kiungo (link) cha tanzia (obirtuary) au nakala ya tanzia kutoka gazetini (sio lazima-optional) 
5 Tafadhali tutumie nyaraka hizo kwa faksi au barua-pepe kwa anwani ifuatayo: 
Twitter, Incc/o Trust & Safety1355 Market St., Suite 900San Fransisco, CA 94103Fax: 1-415-865-5405 
Zingatia: Hii ni namba ya Marekani, kwahiyo hakikisha ina namba sahihi ya kipiga simu za kimataifa (international dialing code) iwapo unatuma kutoka nje ya Marekani. 
Tunafanya mawasiliano yetu yote kwa kutumia barua-pepe, iwapo tutahitaji taarifa nyingine, tutawasiliana nawe kwa anwani ya barua-pepe uliyotupatia. Iwapo una swali lolote, waweza kuwasiliana nasi kwa [email protected]

Sasa, kwa kuangalia tu utaratibu huu, hutoshindwa kutambua kuwa hili ni suala la kifamilia zaidi kuliko lenye kuhitaji mwanasiasa ashughulikie, unless mwanasiasa husika ni mwanafamilia ya marehemu.

Kuna kitu twaweza kujifunza hapa. Kwa wenzetu huku nchi za Magharibi, kufanya maandalizi ya 'nini kifanyike baada ya kifo changu' ni jambo la kawaida. Licha ya huduma kama bima ya kifo, kuna taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na huduma za maandalizi baada ya kifo kama vile kushughulikia maiti yako utapofariki ikiwa ni pamoja na mahali utapozikwa, usimamizi wa mirathi, nk.

Lakini pia kuna huduma mbalimbali za bure mtandaoni kuhusu hatma yetu mtandaoni baada ya vifo vyetu. Kimsingi, mada ya 'kifo na mtandao' (Death and the Internet) ina maingizo 242,000,000 katika tovuti ya kutafutia taarifa (search engine) ya Google

Ninatambua kuwa kwa mujibu wa mila na desturi mbalimbali za Kiafrika, kuchukua hatua hizi za maandalizi ya baada ya kifo kwaweza kutafsiriwa kama 'uchuro,' licha ya ukweli kwamba siku moja kila mmoja wetu atakuwa marehemu kwani kifo haikiepukiki.

Nimalizie kwa kutanabaisha kuwa lengo la makala hii sio kudhihaki harakati za wanaotaka akaunti ya marehemu Betty ifungwe (hasa nikiwa natambua uwepo wa 'uhuni usiopendeza hata chembe' wa baadhi ya watu wanaojifanya ku-tweet kana kwamba ni marehemu mwenyewe ana-tweet "kudai atendewe haki" japo tweet husika haikutoka katika akaunti ya marehemu) bali ni kuelimisha kuhusu utaratibu wa kuomba akaunti ya Twitter ya mtu aliyefariki ifungwe, suala ambalo kwa wenye uelewa  ni la kifamilia zaidi kuliko kuhitaji 'msaada' kutoka kwa wanasiasa. 

Ushauri wangu kwa wanaotaka kuona akaunti hiyo ikifungwa ni kuwasiliana na familia ya marehemu na kuwafahamisha utaratibu husika (iwapo hawafahamu). Ikumbukwe kuwa akaunti ya marehemu, iwe Twitter au katika mtandao wowote ule, ni mali ya marehemu, kama ilivyo akaunti yake ya benki, hati yake ya kusafiria, hati ya kiwanja, au mali yake yoyote ile. Ili, kwa mfano kuweza kufunga akaunti yake benki, ni lazima ipatikane ridhaa ya wenye mamlaka na marehemu, kwa mfano maelekezo katika wosia wake au maamuzi ya famili yake. Kadhalika, ili akaunti yake ya Twitter iweze kufungwa, ni lazima kupata ridhaa ya marehemu kupitia wosia wake au uamuzi wa wanafamilia yake.

Mungu amlaze marehemu Betty mahala pema peponi, Amen.


28 Aug 2014

Kabla ya kukuletea 'darasa' hili ni vema nikakufahamisha kitu kimoja: 'tabia' iliyozoeleka miongoni mwa Wamarekani wengi kudhani kuwa 'dunia' inaishia kwenye mipaka ya nchi hiyo tu. Kuna idadi kubwa tu ya Wamarekani wasio na habari na 'dunia nje ya Marekani,' na pengine ndo maana si ajabu kukutana na 'Kombe la Dunia' la mchezo flani nchi humo linalohusisha timu za Marekani pekee...kwa vile kwa mtizamo wa wengi, Marekani ndio dunia.

Twende kwenye mada husika. Pengine kutokana na mtizamo huo fyongo, baadhi ya watengenezaji apps za simu 'hujisahau' na kudhani wamiliki pekee wa simu wapo Marekani hivyo apps zao zikiwekwa Google Play, kwa mfano, zinaweza kutumika nchini humo tu. Na hii ni moja ya sababu za kukutana na ujumbe "This app is not available in your country."

Lakini next time ukikutana na ujumbe huo usipaniki, kwani darasa lifuatalo linakueleza kiufasaha jinsi unavyoweza 'kuizunguka amri hiyo,' na kufanikiwa ku-download app yoyote ile katika simu yako, alimradi iwe 'compatible.'

Fuatilia video ifuatayo, lakini kama utakwama mahali flani basi usisite kuwasiliana nami kwa ufafanuzi zaidi.



Kwa habari zaidi za teknolojia, endelea kutembelea blogu hii, na rahisisha zoezi hilo kwa kubonyeza menu ya TEKNOLOJIA hapo juu. Karibuni sana.

24 Aug 2014

Smart mannequins that ¿talk¿ to shoppers through their smartphones will go live today in branches of House of Fraser, Hawes & Curtis and the Bentalls department store

Tafsiri: 1. Duka la nguo linaingiza mtandaoni taarifa kuhusu bidhaa husika.

2. Mteja anapaswa ku-download app iitwayo Icneme katika simu yake ili kuwezesha connection ya Bluetooth.

3. Mteja akipita futi 150 karibu ya duka husika, anapata ujumbe katika simu yake, na sasa anaweza kupata taarifa kamili ya nguo husika ilivyovaliwa na mdoli (mannequin) wa maonyesho ya nguo dukani.

4. App iliyomo kwenye simu ya mteja itamwonyesha malili ilipo nguo husika ndani ya duka husika. Pia itampa kiungo (link) ya tovuti ya duka hilo kumwezesha kuinunua nguo hiyo katika muda wowote ule, iwe mchana au usiku.


21 Aug 2014

Naomba kukiri hadharani kwamba katika mitandao yote ya jamii, Twitter ndio namba wani kwangu. Mtandao huo sio tu umeniwezesha kufahamiana na watu muhimu kabisa, bali pia ni moja ya vyanzo vyangu vikuu vya habari na uelewa. Nitaanda makala maalum ya kukufahamisha msomaji jinsi ninavyoitumia Twitter kwa ufanisi, na jinsi inavyoweza kukidhi mahitaji yangu.

Baadhi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii wamekuwa wakiilaumu kwa mapungufu wanayokutana nayo. Kwa mfano, nimesikia kwa watu kadhaa wakiilaumu Instagram kwamba imegeuka uwanja wa matusi. Jamani, tatizo sio Instagram, Twitter, Facebook au mtandao mwingine wowote ule wa kijamii bali tatizo ni mtumiaji. Kama ilivyo mtaani, ukikaa kijiweni utaambulia ya kijiweni. Ukitumia muda wako mwingi maktaba, utaweza kupata vya kupatikana maktaba. Uki-hang out na walevi, well, twajua ni utapata. Ukipendelea kuwa na watu wa Neno la Mungu, utapata Neno la Mungu. Ukijiweka karibu na wasomi, utafaidika na uelewa (knowledge). Ukifuatilia vyombo vya habari, utahabarika. 

Msanii maarufu wa muziki na filamu nchini Marekani, Tyrese Gibson, anatoa ushauri huu 

Employees hanging out with employees is just going to further your career as an employee. You start hanging out with bosses, you eventually become one. (Mwajiriwa anayetumia muda mwingi na waajiriwa wenzie wa kawaida, atadumisha ajira yake kama mwajiriwa wa kawaida tu.Ukianza 'kujichanganya na mabosi, basi nawe waweza kuishia kuwa bosi)
Naam, watu unaojihusisha nao wanachangia kukufanya kuwa mtu wa aina flani. Na kanuni hiyo ina-apply pia kwenye mitandao ya jamii. Uki-follow watu wenye kuendekeza matusi au majungu, utaishia kukutana na matusi au majungu. 

Basi hapa chini ninakupatia orodha ya maprofesa waliobobea katika fani zao ambao wapo Twitter, na waweza kuwa-follow au  kuwaingiza katika LIST yako (nitaandaa makala ya jinsi ya kutumia 


Uongozi (Leadership)
Bill GeorgeHarvard Business School, @Bill_George

Adam GrantWharton School of Finance, @AdamMGrant
Monique ValcourEDHEC, @MoniqueValcour
Karl MooreMcGill University, @ProfKJMoore
Gianpiero PetriglieriINSEAD, @GPetriglieri
Stew FriedmanWharton School of Finance, @StewFriedman
Sir Cary Cooper, Lancaster University, @ProfCaryCooper
CV HarquailHowe School of Business, @CVHarquail
Bret SimmonsUniversity of Nevada-Reno, @DrBret
Mark EspositoHarvard University, @Exp_Mark
Ian McCarthyBeedie School of Business, @Toffeemen68
Gautum MukundaHarvard Business School, @GMukunda
Thomas RouletUniversity of Bath, @ThomRoulet
Terri GriffithSanta Clara University, @TerriGriffith
Patrick J. MurphyDePaul University, @ProfPJM

Ubunifu (Innovation)

Richard FloridaRotman School of Management, @Richard_Florida
Clayton ChristensenHarvard Business School, @ClayChristensen
Calestous JumaHarvard University, @Calestous
Alf RehnÃ…bo Akademi University, @AlfRehn
Marcel BogersUniversity of Southern Denmark, @Bogers
Cyndi BurnettBuffalo State College, @CyndiBurnett
Diego RodriguezStanford University @Metacool
Bob SuttonStanford University, @Work_Matters
Karim R. LakhaniHarvard Business School @KLakhani
Tim KastelleUniversity of Queensland, @TimKastelle
Tor GronsundUniversity of Olso, @Tor
Frank PillerRWTH Aachen University, @MassCustom
Tina SeligStanford University, @TSeelig
Bill FischerIMD Business School, @Bill_Fischer
Gary HamelLondon Business School, @ProfHamel

Mikakati (Strategy)

Michael PorterHarvard Business School, @MichaelEPorter
Estelle MetayerMcGill University, @Competia
Ioannis Ioannou, London Business School, @iioannoulbs
Rita McGrathColumbia Business School @RGMcGrath
Teppo FelinUniversity of Oxford, @TeppoFelin
Roger Martin, Rotman School of Management, @RogerLMartin
Peter G. KleinUniversity of Missouri-Columbia, @PeterGKlein
Mislek Piskorski Harvard Business School, @MPiskorski
Kevin BoudreauLondon Business School, @KevinJBoudreau
Sheen S. LevineColumbia University, @SSLevine
Freek VermeulenLondon Business School, @Freek_Vermeulen
Marion Debruyne, Vlerick Business School, @MarionDebruyne
Robin TeiglandStockholm School of Economics, @RobinTeigland
Dan Elfenbein, Washington University, @OrgStratProf
Sydney FinkelsteinTuck School of Management, @SydFinkelstein

Watajwa wa heshima (Honorable Mentions)

Terry Linhart, Bethel College,@ TerryLinhart
Teresa AmabileHarvard Business School @TeresaAmabile
Terri ScanduraUniversity of Miami, @TerriScandura
Michael RobertoBryant University, @MichaelARoberto
Nadia KazimHigher Colleges of Technology @Nadiakazim

Wasomi hawa mahiri duniani ni visima vya uelewa (knowledge). Na kama sote tunavyoelewa, ili uweze kuchota maji kutoka katika kisima shurti uende kisimani.

Basi endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali, ikiwa ni pamoja na hizi za teknolojia. Bonyeza TEKNOLOJIA hapo kwenye menu juu upelekwe moja kwa moja kwenye habari hizo.


15 Aug 2014

Hebu pata picha: unaingia kwenye email yako unakutana na ujumbe kwamba usubiri kwa muda kwa vile 'internet imejaa.' Kama lengo lilikuwa kusoma tu emails zako, yaweza kuwa sio big deal. Lakini kama uliingia kwenye e-mail ili utume CV kwa mwajiri, au utume assignment yako kwa mwalimu/mhadhiri, basi kwa hakika hali hiyo itakuwa na athari kwako.

Taarifa zinaonyesha kwamba kupotea hewani kwa mitandao kunaweza kuwa jambo la kawaida huko mbeleni kufuatia Internet kuanza kuishiwa nafasi.Jumanne wiki hii, makampuni mbalimbali yaliingia hasara kubwa kufuatia kupotea mawasiliano ya internet kutokana na ufinyu wa nafasi.

Mtandao maaarufu wa kuuza na kununua bidhaa, eBay, ulikuwa miongoni mwa wahanga wa tukio hilo la Jumanne, ambapo ulipotea hewani kwa takriban siku nzima na kukwamisha shughuli lukuki zinazofanyika katika mtandao huo wa biashara.

Maelfu kwa maelfu ya wateja walishindwa kuingia kwenye akaunti zao za eBay huku malalamiko mengi yakiwasilishwa na wateja kutaka warerejeshewe fedha walizonunulia bidhaa.

Inaelezwa kuwa chanzo cha tatizo hilo kilikuwa kinachofahamika kama Border Gateway Protocal (BGP). Makampuni yanayotumia internet na mitandao mignine mikubwa hutumia 'barabara' (route map) hiyo yenye mamia kwa maelfu ya 'njia' kupelekeana taarifa kupitia mtandaoni. Video ifuatayo yaelezea kwa undani zaidi:



Katika mazingira ya kawaida, mtu anapotembelea tovuti anategemea mashine zioitwazo 'router' kukumbuka njia salama katika mtandao mpana wa Internet. Hata hivyo 'routers' za zamani zinapata wakati mgumu kumudu teknolojia mpya- kwa mfano simu za kisasa (smartphones) na Tablets ambazo sio tu zina watumiaji wengi bali pia huongeza muda ambao mtumiaji huwa mtandaoni. Hali hiyo imepelekea 'foleni' kubwa mtandaoni na kusabababisha baadhi ya routers kukabiliwa na changamoto ya kumbukumbu (memory) na uwezo wa kuzifanyia kazi data.

Mfano sahihi wa kilichotokea ni pale ubongo wa binadamu unapozidiwa na uwezo wa kukumbuka vitu njiani baada ya safari ndefu.

Ili kukabiliana na tatizo hilo, routers zinabidi kuboreshwa zaidi katika uwezo wa kumbukumbu na kufanyia kazi data.

Wataalamu wanadai kwamba tatizo hilo litazidi kujitokeza huko mbeleni hasa kwa kuzingatia kuongezeka kwa mauzo ya simu za kisasa na Tablets.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka gazeti la Daily Mail la hapa Uingereza

Endelea kupata habari za teknolojia kwa kutembelea blogu hii, na kwa urahisi zaidi, bonyeza hapo juu kwenye menu palipoandikwa TEKNOLOJIA


11 Aug 2014

Tuwe wakweli, japo matumizi ya emoji yanaweza kufanya ulichoandika kionekane sio serious lakini kwa hakika emoji zinasaidia kuonyesha mood yako. Sasa sote twafahamu kuwa emoji hutumika zaidi kwenye simu, hasa za kisasa. Je wafanyaje ukitaka kuzitumia mtandaoni, kwenye Twitter au kwingineko?

Tembelea tovuti hii na utakuta lundo la emoji. Ukishaiona unayotaka, i-copy kisha i-paste kwenye sentensi yako...there you go!

Endelea kutembelea blogu hii kwa habari mbalimbali ikiwa ni pamoja na za teknolojia. Bonyeza TEKNOLOJIA hapo kwenye main menu utakutana na mengi ya muhimu katika eneo hilo. Karibuni sana

9 Aug 2014

Kwanza ninaomba kukiri kuwa habari nyingi katika blogu hii kuhusu apps zinahusu jukwaa (platform) la Android. Hata hivyo, ninaahidi kuandika pia kuhusu apps za jukwaa la iOS (Apple) kadri nitakavyokutana nazo. Tatizo kubwa linalonikwaza kuhusu apps za iOS ni ukweli kwamba mie nimekuwa mtumiaji wa Android kitambo sasa. Nilianza na HTC Desire kwa miaka miwili, kisha nikaja kwenye Samsung Galaxy S2 kwa miaka miwili tena, na sasa nipo na Samsung Galaxy S5 ambayo nina contract ya miaka miwili kutoka mwezi Machi mwaka huu. Vilevile ninatumia tablet ya Samsung Galaxy Tab2 10.1 kitambo sasa, na Tablet ninayofikira kuwa nayo huko mbeleni ni Samsung Galaxy Tab S 10.5 au nyingineyo ya Android.

Loe ninawaletea app moja inayoweza kukurahisishia kutuma SMS kutoka kwa kompyuta au tablet yako kwenda kwa simu yoyote ile.Sote twafahamu kuna nyakati twajikuta hatuna simu, na katika amzingira ya kawaida, huwezi kutuma SMS bila simu. Tatizo hilo lina ufumbuzi kwa kutumia apps mbalimbali, lakini ninayoipenda na kuitumia zaidi ni MIGHTY TEXT.

Cha kufanya ni kui-download kwenye simu yako, kisha kama una Tablet, download huko pia. Ili uweze kuitumia kwenye kompyuta yako, unapaswa kui-install kama extension ya browser ya Chrome au browser nyingine kama Safari, Firefox na Internet Explorer, kisha nenda kwenye app ya mtandaoni ya Might Text kwa ajili ya kuruhusu akaunti yako ya Google iiwezeshe app hiyo kutuma na kupokea SMS.

Iwapo utakumbana na tatizo lolote basi usisite kuwasiliana nami ili nikusaidie kupata ufumbuzi.

Endelea kutembelea blogu hii kupata habari mbalimbali ikiwa ni pamoja na kama hii ya teknolojia, ambayo unaweza kuifikia kirahisi kwa kubonyeza TEKNOLOJIA kwenye menyu ya Blogu hii



2 Aug 2014

Kiuhalisia, kuna aina lukuki za watumiaji wa mitandao ya kijamii. Lakini katika kuweka mambo sawia, isingipendeza kuwa na 'makundi makuu' kama makabila vile kisha ukijitanabaisha upo 'kabila' lipi miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii?

Kimsingi, mitandao ya kijamii ni nyenzo ya kukuunganisha na watu-aidha kusikia au kutaka kusikika. Na kwa maana hiyo, ni muhimu kwa mtumiaji kujitambua mapema, na kujiweka katika kundi analodhani linamfaa au lina manufaa zaidi kwake.

Kwahiyo,katika uchambuzi huu, kuna makundi 10 ya msingi ya watumiaji mbalimbali wa mitandao hiyo ya kijamii. Ni matarajio ya makala hii kwamba utapomaliza kuisoma,utabaini upo kundi gani, au ungependa kuwa katika kundi gani. Enjoy!

068ecf0a8e7ac52b676ef4afe6a5a811

Kundi la kwanza ni MSIKILIZAJI: Huyu anapendelea sana mitandao ya kijamii lakini mara nyingi yupo kinya, hataki kuonekana wala kusikika. Kama jina lilivyo, yeye ni msikilizaji tu.Anaweza kuipenda post yako kwenye Facebook lakini akakaa kimya.

Kundi jingine ni MWANAHARAKATI: Huyu ni mtu anayetambua nguvu ya mitandao ya kijamii katika kufikisha ujumbe,na anafanya kila awezalo kuitumia ipasavyo ili kufikisha sauti yake iskike na hatimaye kuleta tofauti inayokusudiwa. (Binafsi nadhani ninaangukia katika kundi hili)

Kundi la tatu ni MCHAFUZI WA HALI YA HEWA: Huyu ni mtu anayedhani kwamba mabandiko yake mtandaoni ni ya kiwango cha hali ya juu, kiasi cha kuamini kuwa kila mtu anastahili kutumiwa kwenye inbox yake (tena pasi kujali ridhaa ya mtumiwa). Nadhani ushakutana na DM au meseji Facebook yenye ujumbe 'angalia picha hii...' na ukilogwa kubonyeza link husika waweza kujutia nafsi yako.

Kundi la nne ni MWENYE MAHABA NA ISHU FLANI: Ushakutana na mtu anapenda mpira kupita kiasi, na ukifuatilia mabandiko yake kwenye mitandao ya kijamii utadhani ni chombo cha habari. Mtu wa aina hii anaendeshwa na mahaba ya akipendacho-iwe siasa, burudani, uchumi au ishu nyingine yoyote ile, na anatumia muda kuifuatilia ishu hiyo na ku-share na jamii. Kimsingi watu wa aina hii wanaweza kuufanya mtandao wa kijamii kuwa mahala pa kujifunza kama sio kuburudisha. (Nahisi pia ninaangukia kundi hili kwa mada nizipendazo, yaani siasa, teknolojia, habari na intelijensia)

Kundi la tano ni KIPEPEO WA JAMII Huyu ni yeye na picha. Atakjuonyesha kila sehemu aliyotembelea, kila shughuli aliyofanya, na kila hachoki ku-tag watu kwenye picha hizo. Pengine ni mtu wa watu lakini pengine ni msumbufu tu anayetaka kuonyesha maisha yake kwa njia ya picha. Kipepeo wa jamii anaweza kutengeneza idadi kubwa ya marafiki kwa sababu mara nyingi huwa kama analazimisha kila mtu awe rafiki yake kwa njia ya picha.

Kundi la sita ni WASUMBUFU MTANDAONI: Huyu ni mtu anayeweza kuvuka mpaka kati ya kupishana hoja kistaarabu hadi kufikia kashfa,matusi na udhalilishaji. Mara nyingi mtu wa aina hii hung'ang'ania ishu zisizo za msingi lakini zenye madhara kwa hadhi au heshima ya mlengwa katika jamii. Njia pekee ya kukabiliana na mtu wa aina hii ni kum-block, kwa sababu jaribio lolote la kumuelimisha-hata liwe la kistaarabu kiasi gani-litaishia kuzua mabalaa zaidi.

Kundi la saba ni MWALIMU: Huyu ni kama yuole wa kundi la nne hapo juu (mwenye mahaba na ishu flani) lakini yeye hana ishu maalumu bali anapenda ku-share uelewa (knowledge). Mara nyingi anakuwa na uelewa wa kutosha lakini haridhika kukaa na uelewa huo peke yake na badala yake anashirikisha wengine.Mtu wa aina hii anaweza kuwa muhimu sana katika mtandao wa kijamii kwani anatoa elimu bure (nami najihisi kama nipo kundi hilo,japo siwezi kujihukumu).

Kundi la nane ni ALIYEANZA KITAMBO: Mara nyingi utamgundua mtu huyu katika katika mtandao mpya (angalau kwake), ambapo kwa vile alikuwepo tangu zama za Facebook haijawa maarufu kama sasa basi anataka kila mtandao wa kijamii anaojiunga nao 'ufuate kanuni' za Facebook ya zamani. Watu wa aina hii hupatikana zaidi Twitter ambapo hufanya kiola wawezalo kuigeuza Twitter kuwa Facebook. Huyu anaweza kukukera kirahisi kwa sababu anataka kulazimisha matamanio yake yawe ya watu wote.

Kundi la tisa ni la MWENYE KITABU CHEUSI: Kama hufahamu, kitabu cheusi ni kama diary yenye kumbukumbu mbalimbali za kila siku pamoja na namba za simu au anwani za watu mbalimbali. Mara nyingi mtu wa aina hii yupo kwenye mtandao wa kijamii kwa ajili ya mawasiliano na wengine. Si ajabu kuona mtu wa aina hii akiwa na 'marafiki' au 'wafuasi' kibao kwa sababu yupo kwenye mtandao wa kijamii kwa ajili hiyo.

Kundi la kumi na la mwisho ni MTU WA FAMILIA:Huyu anaweza kuwa mtu asiye na uzoefu sana na teknolojia lakini mara baada ya kufahamu jinsi ya kuitumia basi anataka kuhakikisha anakuwa karibu na 'familia' yake. Mara nyingi mtu wa aina hii yupo katika mtandao wa kijamii kwa minajili ya kifamilia zaidi, na ninaposema familia inajumuisha pia watu wa karibu na mhusika.

Kama nilivyobainisha awali, mitandao ya kijamii ina aina lukuki za watumiaji japo hizi 10 zinaweka pamoja watu hao katika makundi hayo makuu. Je hadi kufikia hapa unadhani upo katika kundi gani?

CHANZO: Makala hii imetafsiriwa kutoka tovuti ya DAILYGENIUS

Endelea kutembelea blogu hii ili kupata makala na habari mbalimbali, na iwapo ni mpenzi wa teknolojia kama mie basi usikose kubonyeza hapo juu ya blogu palipoandika TEKNOLOJIA ili kupata kila kilicho bora katika anga hizo. 



31 Jul 2014

'Malkia wa selfies' Kim Kardashian. 
Kwa mujibu wa kamusi ya Kiingereza ya Oxford, neno selfie maana yake ni picha ambayo mtu amejipiga mwenyewe, hususan kwa kutumia simu za kisasa (smartphones) au 'kamera ya mtandao' (webcam)kwa minajili ya kuiposti kwenye mitandao ya kijamii (social media).
Moja ya selfie maarufu kabisa iliyopigwa katika tuzo za Oscar mapema mwaka huu
Kwa kifupi, selfie ni kwa ajili ya 'maonyesho,' na hakuna anayetaka kupiga selfie isiyopendeza, ya kumpatika 'likes' za kutosha. Sasa kwa vile selfies ni kwa ajili ya 'maonyesho,' ni wazi hakuna anayetaka kupizo vizuri, akajipiga picha, lakini matokeo yake picha husika ikawa kama ya kuchora- kwa maana ya ubora hafifu.

Makala hii fupi inakupa orodha ya apps za kupiga picha za selfies za kiwango bora kabisa. Orodha hii ni kwa ajili ya simu za Android pekee (orodha ya apps za selfie kwa iOS itawajia baadaye). Enjoy!

INSTAGRAM

instagram android

Instagram ni kama 'baba lao' linapokuja sula la selfie. App hii ina nyenzo kadhaa za kuhariri na kunoresha selfie yako. Na kikubwa zaidi, Instagram ndio kama 'makao makuu' ya selfies, kwa maana ya kuwa ni app maalum kwa ajili ya picha za aina hiyo.


frontback android

Uzuri wa app hii ni uwezo wake mkubwa wa kupiga picha ya 'mhusika na mazingira yake.' Yaani selfie yako sio tu itakuonyesha wewe mhusika bali pia hata mazingira yanayokuzunguka, ambapo inatumia kamera zote mbili za simu: ya mbele na ya nyuma- kwa wakati mmoja.


retrica android

Kuna msemo wa kiswahili usemao 'ya kale ni dhahabu,' na hapo ndipo ulipo unora wa app hii.Retrica yakuwezesha kupiga picha inayoonekana kama ya 'mwaka 47,' yaani mwonekano wa kizamani. Lakini umahiri zaidi wa app hii upo katika kuifanyia uhariri picha yako. Wakati mara nyingi apps za picha hukuwezesha kuhariri picha mara baada ya kupiga picha halisi, kwa Retrica zoezi hilo linafanyika 'laivu' kwa maana kwamba unaweza kuihariri picha yako kabla hujaisevu au kuiposti mtandaoni. Japo hii ni faida, yaweza pia kuwa hasara kwa maana pindi ukishapiga selfie yako, huwezi kuihariri kwa ufanisi.


line android

Hii ni moja ya apps maarufu kabisa kwa picha kwa simu za Android. Umahiri wa Line Camera unachangiwa na ukweli kwamba unaweza ku-download nyenzo lukuki na za aina tofauti (za bure au za kununua) pindi unapohitaji ladha ya ziada ya zinazopatikana kwenye app yenyewe.

candy camera

Kama jina lenyewe 'candy' linavyoashiria 'utamu,', ndivyo ulivyo ubora wa app hii ambayo inatumia zaidi mwelekeo wa vidole vyako kwenye picha/screen yaani 'gestures' kwa kimombo.Waweza 'kuisukuma' (swipe) picha yako kulia au kushoto kufanya uchaguzi sahihi wa taswira unayotaka, au kusukuma juu au chini kwa ajili ya kupata nyenzo mbalimbali za kuhariri picha yako. Kadhalika, Candy Camera inakuwezesha kuhariri selfie yako 'laivu' lakini tofauti na Retrica, yenyewe yakuwezesha kuhariri selfie yako hata baada ya 'kuifotoa' au kuisevu.


smart selfie android 

Tofauti na apps nyingine za selfie, Smart Selfie inatumia kamera ya nyuma ya simu yako. Kwahiyo badala ya kuchukua selfie wakati kamera ya mbele inakuangalia, katika app hii yakulazimu kuigeuza simu yako na kuchukua selfie kwa kutumia kamera ya nyuma. App hii ni nzuri zaidi kama unataka kuchukua selfie ya watu wengine, kwa maana unawafotoa kama ambavyo unapiga 'picha ya kawaida' kisha unachagua iwapo unataka simu iwe 'imesimama' (potrait)au 'imelala' (landscape), kisha unaishika vizuri simu yako, na app hiyo itakupa maelekezo kwa sauti ili kupata selfie mwafaka, kwa mfano kukueleza 'sogea karibu' au 'sogea kulia.'

Ofkoz, kuna apps nyingine lukuki ambazo ni maalum kwa ajili ya selfies lakini hizi 6 zinaelezwa kuwa ni bora kabisa. Kazi kweny wapenda selfies.

Usikose kutembelea blogu hii kwa ajili ya habari mbalimbali za teknolojia na nyinginezo. Waweza kupata kirahisi habari za Teknolojia kwa kubonyeza section ya TEKNOLOJIA hapo juu ya blogu.


30 Jul 2014

signalapp
Mie ni miongoni mwa waumini wakubwa wa filosofia ya 'ishu binafsi shurti zibaki kuwa za binafsi' (private things should always remain private). Na ninaposema 'ishu binafsi' ninamaanisha pia masuala nyeti yasiyopaswa kusikizwa na yeyote yule asiyehusika nayo. Siwezi kufafanua zaidi ila naamini kwamba kuna nyakati tunakuwa na masuala yanayopaswa kufahamika kwa wahusika tu.

Sasa iwapo unatumia iPhone,kuna app moja inaweza kuwa na manufaa makubwa kwako pindi ukijikuta katika mazingira ambapo unataka kuwasiliana na mtu pasi maongezi hayo 'kunaswa' na watu wengine. Labda kama hadi hapa hujanielewa vizuri, ni vema ukafahamu kuwa taarifa za hivi karibuni kutoka kampuni ya simu za mkononi ya Vodafone inaonyesha kuwa Tanzania ni moja ya nchi inayoshika nafasi za juu duniani kwa mashushushu wake kunasa mawasiliano binafsi ya simu za wananchi.

App husika inaitwa SIGNAL, na inapatikana bure kwenye App Store.

Kwa kutumia teknolojia inayoruhusu wahusika tu wa ujumbe husika kuupata ukiwa kamilifu (encryption), app hiyo ya Signal inayafanya maongezi katika iPhone kuwa ya faragha kiasi kwamba mtu asiyehusika hawezi kuyanasa.

Jinsi ya kui-set up App hiyo ni rahisi kabisa, na unahitaji kuingiza namba yako ya simu tu na kuithibitisha kwa kuingiza tarakimu 6 (6-digit code), ambazo zitatumwa kwako kwa SMS au simu, na utakuwa tayari kuitumia app hiyo. Namba za simu ulizohifadhi katika simu yako zitahamia kwenye app hiyo mara moja, lakini zitakazoonekana ni zile tu ambazo mtumiaji naye anatumia app hiyo. Ukimpigia simu mtu asiyetumia app hiyo,atatumiwa ujumbe wa ku-install app hiyo kwenye simu yake.

Unapopiga simu kwa kutumia app hiyo kwa mtu ambaye simu yake nayo ina app hiyo, faragha ya mawasiliano yenu inahakikiwa kwa kutumia maneno yanayoonekana katika screen ya simu ya anayepiga na anayepigiwa.Kisha mnafananisha maneno hayo kuhakikisha kuwa yanalingana, na yakilingana basi mawasiliano yenu yanakuwa ya siri. Yasipolingana basi inamaanisha kuna mtu anaingilia (anasikiliza) maongezi yenu.

Wakati kwa sasa app hiyo inaweza tu kuyafanya maongezi ya simu kuwa ya siri, kampuni iliyotengeneza app hiyo imeeleza kuwa ipo mbino kuwezesha hata mawasiliano ya SMS nayo kuwa ya siri.

29 Jul 2014

An armed pro-Russia militant stands guard at the MH17 crash site.
Katika jitihada za kubaini chanzo-nani na kitu gani-cha kudunguliwa ndege ya Shirika la Ndege la Malaysia MH17,kundi la waandishi wa habari wa kijamii (citizen journalism) wakitumia mtandao wa intanet na hisia zao tu wamekuwa wakikusanya habari pengine zaidi ya mashushushu wa Kimarekani.

Jumanne iliyopita, maafisa usalama wa Marekani walikiri kwamba japo ni kweli kwamba Russia imekuwa ikiwasaidia waasi wanaoiunga mkono, huko Ukraine, kwa miezi kadhaa, hakuna uthibitisho wowote kuonyesha kuwa kifaru cha kurusha makombora ya kutoka ardhini kwenda angani (surface -to-air missile) aina ya Buk SA-11, ambacho Marekani inadai ndio kilitungua ndege hiyo, kilikuwa cha Russia. Hata hivyo, waasi hao wa Ukraine walijigamba awali kuwa wana makombora ya aina hiyo.

Msemaji wa serikali ya Marekani alikiri kwamba kuna uhaba mkubwa wa maelezo kuhusu silaha iliyotumika kudungua ndege hiyo, na kuthibitisha kuwa ni vigumu kuja na ushahidi mpya wa kuthibitisha uhusika wa Russia katika tukio hilo.

Lakini kundi la waandishi wa habari wa kijamii likiongozwa na Ellliot Higgins, anayefahamika zaidi kwa jina lake la mtandaoni kama "Brown Moses," ameonyesha ushahidi mwingi kuhusiana na tukio hilo. Kwa msaada wa wafuasi wake (followers) katika mtandao wa kijamii wa Twitter, ameweza kuonyesha sehemu kilipokuwa kifaru cha kurusha makombora (launcher) ya Buk wakati kinasafirishwa katika eneo la Snizhne, lililopo chini ya milki ya waasi wanaoungwa mkono na Russia, kulingana na video inayosambaa kwenye mtandao wa video wa Yout Tube

Siku iliyofuata, Aric Toler, mfuasi wa muda mrefu wa Higgins, alionyesha eneo sahihi la kifaru cha kurushia makombora ya Buk katika mji uliopo Mashariki kwa Ukraine wa Torez, akitumia taarifa alizozikusanya kwa vyanzo vya wazi (open source information) na video nyingine za YouTube zilizorekodiwa eneo hilo.

Toler na Higgins waliweza kuthibitisha kuwa picha hiyo ilipigwa saa 5.40 asubuhi, kwa kutumia nyenzo ya mtandaoni iitwayo Suncalc, ambayo inawezesha kukokotoa nafasi (position) ya jua kwa kuzingatia muda na sehemu husika. Hiyo iliwawezesha kuthibitisha kuwa kifaru hicho kilikuwa eneo ilipodunguliwa ndege ya MH17.

Uchambuzi mwingine wa kutumia watu wengi (crowdsourced analysis) ambao Higgins aliukusanya Jumanne iliyopita unatoa ushahidi mkubwa kuhusu video iliyotolewa hadharani na serikali ya Ukraine ikionyesha kifaru husika kikihamishwa kutoka eneo linaloshikiliwa na waasi kuelekea Russia. Katika video husika, mtambo wa kurushia makombora (launcher) hauonekani 

Serikali ya Russia ilikanusha usahihi wa video hiyo, ikidai kwamba ilirekodiwa katika mji wa Krasnoarmeisk, ambao upo chini ya himaya ya majeshi ya Ukraine. Hata hivyo, shukrani kwa uchambuzi wa habari kwa kutumia vyanzo vya wazi, ilikuja kufahamika kuwa mji huo wala sio uliotajwa bali mwingine ulio chini ya himaya  ya waasi wanaoungwa mkono na Ruassia wa Luhansk, kilomita 30 kutoka mpaka wa Russia na Ukraine.

"Russia imeongopa," aliandika Higgins katika tovuti yake ya Bellingcat, anayoitumia kuhamasisha kazi za waandishi wengine wa wa kijamii wanaoandika habari za uchunguzi na kufundiha kuhusu nyenzo mbalimbali kwa ajili ya kazi hiyo. 

Matokeo ya uchunguzi huo hayathibitishi kwa hakika uhusika wa Russia katika kuidungua ndege hiyo ya Malaysia, kama anavyokiri Higgins mwenyewe, lakini yanathibitisha kuwa waasi wanaoungwa mkono na Russia wanamiliki kifaru cha kurushia makombora ya Buk,.na kilikuwa karibu na eneo ilipodunguliwa ndege hiyo.

Kwa Higgins, kazi yao ni sawa na ushushushu lakini kwa kutumia njia rahisi,na unaweza kuwasaidia wachunguzi wa ajali hiyo. Baada ya yeye na mwenzie Toler kuonyesha eneo na muda picha ya kifaru hicho lipopigwa, waandishi wa habari walikwenda huko na kukutana na mashuhuda waliothibitisha maelezo ya Higgins na mwenzake.

Uchunguzi wa aina hii ni mfano mzuri wa anachotaka kufanya Higgins kupitia tovuti yake ya Bellingcat: kujenga jamii ya waandishi wa kijamii mtandaoni wanaojuhusisha na uchunguzi ambao waweza kuibua ukweli mbalimbali. Higgins amekuwa akifanya hivyo kwa miaka kadhaa, akibandika mtandaoni video mbalimbali kutoka Syria ili kbainisha zipi ni za kweli au la.

Yeye alikuwa mmoja wa waangalizi huru wa mwanzo kuthibitisha kuwa utawala wa Rais Bashir al-Assad wa Syria ulitumia silaha za sumu katika kitongoji cha Ghouta Agosti mwaka jana,a aliibua biashara ya kuingiza silaha nchini humo, akiwa nyumbani kwake, Leicester, Uingereza.  Sasa anataka kuwaunga mkono watu wengine wanaofanya kazi kama yake na kuwafundisha jinsi ya kupata ujuzi husika.

"Ni muhimu kufahamu kuwa uchunguzi huu ulifanywa na na watu wa aina mbalimbali, na hiyo inaonyesha umuhimu wa kufanya nyenzo na mbinu za kukusanya habari kwa vyanzo vya wazi kuwa za wazi kwa yeyeote yule."

Chanzo: Imetafsiriwa kutoka mtandao wa WAtoday.com.au



27 Jul 2014

Pengine umeamua kufuta SMS baada ya kuona SMS Inbox yako inajaa au pengine umefuta SMS kwa bahati mbaya. Katika mazingira ya kawaida, ukisahfuta SMS ndio 'imetoka hiyo.' Lakini kimsingi waweza kuzirejesha kwenye inbox japo kitu cha muhimu kabisa na muda. Uwezekano wa SMS ulizozifuta kurejea inbox kunategemea sana uharaka: kadri unavopokea SMS mpya au updates za apps zako ndivyo fursa ya kuzirejesha inavyozidi kuwa ndogo.

Kuna nyenzo kadhaa za PC au Mac za kuweza kukuongoza katika zoezi la kurejesha SMS zako kwenye simu yako.Nyingi ya nyenzo hizo ni za bure, na hata zinazohitaji malipo,zinakupa fursa ya majaribio kabla ya kununua (free trial). Aina gani ya nyenzo uitumie,yategemea mapendezeo yako,lakini zote zafanya kazi moja ku-scan memory ya simu yako,kutambua na kuokoa SMS zilizofutwa. Zitakuongoza katika hatua nne muhimu za zoezi hili: kuunganisha, ku-scan, ku-review na kuziokoa (recover).

Baadhi ya zana za PC au Mac zinazoweza kukusaidia ni pamoja na Coolmuster Android SMS+Contacts Recovery, Wondershare Dr Fone for Android (hii inahitaji simu yako iwe rooted) na Android Data Recovery

Hatua zifuatazo zinaweza kuwa tofauti kutegemea na zana ya PC/Mac utakayoamua kutumia hapa imetumika Wondershare Dr Fone kwa minajili ya maelezo kwa picha).

1. Download moja ya nyenzo nilizotaja hapo juu kwenye PC/Mac yako,kisha iwashe (launch)
2. Unganisha simu yako na PC/Mac kwa kutumia waya wa USB

drfone android sc01
3. Wezesha 'USB Debugging' katika simu yako kwa kwenda kwenye 'Developer Options' katika 'Setting.' Vinginevyo, waweza kwenda kwenye 'About Phone' kisha 'Build Number,' piga eneo hilo na kidole chako mfululizo (tap repeatedly) na hatimaye utapelekwa kwenye 'Developer Options.' Kutoka hapo,nenda kwenye 'USB Debugging' (au Android Debugging kutegemea aina ya simu yako) kisha tiki kiboksi husika.
drfone android sc02
4. Fuata maelekezo kama yanavyoonyeshwa katika zana unayotumia kwenye PC/Mac yako
drfone android sc05
5. Ukishamaliza, sasa utaweza kuona data zilizopo kwenye memory ya simu yako, na SMS ulizofuta kwa bahati mbaya au makusudi-kutegemea kama hakuna SMS mpya au updates za apps,maana kitu chochote kipya kwenye memory kitaondoa uwezekano wa kuokoa SMS ulizofuta.
drfone android sc09

6. Tafuta folder ya SMS,chagua SMS unayotaka/unazotaka kuzirejesha inbox,na aidha tumia option ya 'Recover' kwenye PC/Mac yako au 'save' kwenye kompyuta yako.

Natumaini makala hii itakuwa na msaada na manufaa kwako. Usikose kufuatilia makali nyinginezo za teknolojia katika blogu hii.Bonyeza TEKNOLOJIA hapo juu na utapelekwa moja kwa moja katika makala hizo.



Je wafahamu kwamba unaweza ku-print document kutoka katika simu yako ya Android kwenda kwenye printer? Makala hii inakuelekeza jinsi ya kufanya hivyo.

Baadhi ya simu za kisasa zaidi kwa mfano Samsung Galaxy S5 tayari zina app hiyo, na hakuna haja ya ku-download upya.

androidpit cloud print one

Hatua ya kwanza ni ku-download Google Cloud Print  kisha 'add new printer'

androidpit cloud print two

Baada ya kuchagua 'add new printer' utapalekwa kwenye ukurasa wa Google wa Cloud Print, au kwenye akaunti yako ya Google iwapo hujasaini.

androidpit cloud print three

Japo ukurasa wa Cloud Print haupo bayana sana kimatumizi, zoezi la ku-'set up' si gumu. Fata maelekezo kutoka kwa printer yako,iwe ni offline model au Cloud ready model.
androidpit cloud print four

Sasa nenda kwenye faili unalotaka ku-print kutoka katika simu yako, na utaona chaguo la kulichapisha.

Iwapo unahitaji ku-print SMS,njia nyepesi ni kutumia app iitwayo SMS Backup& Restore. App hii ina-backup SMSzako kwenye simu yako,email au huduma za 'cloud' kama vile Dropbox na Google Drive. Ukisha-backup,nenda mahala ulipohifadhi SMS hizo,kisha chagua 'print'

androidpit cloud print five

CHANZO: Andoidpit
Natumaini makala hii itakuwa na msaada na manufaa kwako pindi utapohitaji kuchapisha dokumenti au SMS zako. Usikose makala nyingine za teknolojia katika blogu hii,ambazo utazipata kirahisi kwa kubonyeza hapo juu kwenye blogu palipoandikwa TEKNOLOJIA


23 Jul 2014

Nimekutana nayo hii katika Facebook


Tafsiri ya alichoandika Chiume, rafiki yangu mmoja huko Twitter na Facebook, ni hii:

"Utasalmu amri kwa intaneti. Duka hili katika kitongoji cha Sinza, Dar,linatumia picha yetu ya harusi. ambalo ni jambo la kufurahisha/kupendeza lakini ingekuwa vema kama tungelipwa! Kuna mwanasheria yeyote mzuri (wa kufuatilia ishu hii?) Lol! Asanteni aliyeleta picha na 'aliyetutonya' kuhusu ishu hii, ambayo 'tumekanusha' kwa kudai ni kushabihiana tu."




Mtandao wa kijamii wa Twitter unazidisha ushindani miongoni mwa apps za ku-chat, hususan Whatsapp, kwa kuboresha huduma yake ya ujumbe wa moja kwa moja (Direct Message) au DM kama inavyojulikaza.

DM ni tweets zinazotumwa faragha kati ya watu wawili 'wanaofuatana' (follow each other), au kwa ujumbe wa moja kwa moja kwa watu maarufu wenye akaunti zilizohakikiwa (verified) ambazo zinawawezesha kupokea ujumbe wa aina hiyo hata kwa watu wasiowa-follow.

"Katika wiki chache zijazo, tutatambulisha update itakayorahisisha kufuta DM kiurahisi mtandaoni na katika simu au tablet," wameeleza Twitter,na kuongeza, "pia tutatambulisha update kwa iPhone na Android itakayomwezesha mtumiaji kuona historia nzima ya DMs.

DM zinawakwaza watumaiji kutokana na limit ya tarakimu 140 na mapungufu katika ku-sync kati ya mtandao na simu au tablet.

Mafanikio ya Whatsapp yalijidhihirisha mwezi Februari mwaka huu baada ya app hiyo kununuliwa na Facebook kwa dola bilioni 19, na sasa app hiyo inatumiwa na watu zaidi ya milioni 500.


ENDELEA KUTEMBELEA BLOGU HII KUFUATILIA MAENDELEO YA HABARI HII NA NYINGINEZO KWA KUBONYEZA KIPENGELE CHA 'TEKNOLOJIA' HAPO JUU

20 Jul 2014

twitter etiquette
I love Twitter for a lot of reasons. There’s a lot to like and a lot of really awesome people using it effectively. But then there are those people who don’t use it so well – or at least those who have annoying Twitter behaviors. While this post isn’t a full rant, it’s a mini rant – about how to properly say thank you on Twitter.
Here’s the thing, when someone takes the time and effort to share your content on Twitter, you should take the time to thank them for it.
Yes, it’s that simple.
Now, there are various ways you can go about thanking them. And these will vary depending on how you use Twitter but you should still be thanking people.
But, first, let’s look at what is NOT a good thank you on Twitter. Retweeting someone’s Twitter post that shared your content is NOT a thank you. It is selfish and self-aggrandizing.
All this does is acknowledge that you saw they shared it, but that you’d rather more people see that they shared it. It doesn’t thank them for their time. It promotes you. It doesn’t thank them for reading your post. It promotes you.
So. STOP. Doing. This. (If you currently do.)
Instead, here is how you should thank people on Twitter.

Say Thank You

I know, crazy concept! But actually saying thank you is the best way to say thank you. Reply to their original tweet (so they know what you’re thanking them for) and actually say “thank you”. Or “thanks”. Or “I appreciate it”. Or something else with gratitude.
thank you on twitter
You can even wish them a lovely day, nice weekend, or other greeting. You can ask them a question or start a conversation with them.
twitter etiquette

Favorite the Tweet

If you get a lot of shares and notifications or maybe you just don’t have enough time to thank everyone, you can at least throw up a “favorite” on the tweet to let the person know you saw it and appreciate it.
When possible though, or when someone writes up a comment or summary of your content in their tweet, take the extra time to thank them.

Tweet their Content

One of the most rewarding ways to thank someone (and, yes, it will take more time) is to share their content as reciprocation for them sharing yours. Take a look at their Twitter feed, find a post or link that is of relevance to you and your audience and retweet it to your followers.
SOURCE: Jenn's Trends


14 Jun 2011

Window on the world: Gone are the small aircraft windows in the 'vitalising zone' which provides a panoramic view for passengers

Pichani juu ni muundo wa ndege za kizazi kijacho ambazo badala ya vijidirisha vidogo tulivyovizowea,ndege hizo zitakuwa transparent.Hiyo inamaanisha abiria wataweza kuona ndege inavyopasua anga...na hapo ndio shughuli kwa waoga wa vina.

Hata hivyo,kama wewe ni miongoni mwa waoga hao,basi usihofu sana kwani inatarajiwa kuwa ndege za aina hiyo zitaanza kazi miaka 40 ijayo.

CHANZO (NA KWA HABARI KAMILI): Daily Mail

19 Apr 2010

Ni dhahiri unapokutana na kitangulizi 'http://...' unafikiri kuwa kinachofuata ni anuani ya tovuti flani.Lakini je 'http://' (kifupisho cha Hypertext Transfer Protocal)bado ina umuhimu katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuitambua anuani ya tovuti hata bila kitangulizi hicho? . 
Wanateknolojia wa Google Chrome hawadhani kama kitangulizi hicho bado ni muhimu na wameamua kukificha katika toleo jipya la browser hiyo.

Hata hivyo,ufumbuzi huo sio rahisi kama inavyoonekana kwani unaweza kuficha kitangulizi hicho unapoandika anuani ya tovuti lakini bado kipo.Pia inatarajiwa kuwa maendeleo hayo yanaweza kuzua mkanganyiko kwa baadhi ya watumiaji wa intaneti.

Makala hii imetafsiriwa (katika tafsiri isiyo rasmi) kutoka mtandao wa Mashable

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.