Leo Machi 18, 2019 ni siku ambayo lazima iingie kwenye
vitabu vya kumbukumbu kwa sababu kuu tatu, ambazo zote zinamhusu mwanasiasa
mkongwe Seif Sharif Hamad na Chama cha Wananchi (CUF)
Sababu ya kwanza, leo ni siku ambayo mwanasiasa huyo, maarufu
kwa jina la Maalim Seif, "ametimuliwa" rasmi kutoka chama
alichoshiriki kukiasisi (CUF).
Kibaya zaidi, "kutimuliwa" huko kumekuwa na
baraka kisheria, baada ya Mahakama Kuu kumtambua Profesa Ibrahim Lipumba kuwa
mwenyekiti halali wa chama hicho.
Ikumbukwe tu Lipumba alitangaza kujiuzulu uenyekiti
kwa sababu anazozijua yeye kabla ya kuamua kurejea kwenye wadhifa huo "kwa
mabavu." Kwa bahati mbaya – au pengine makusudi – sheria na kanuni za CUF
zilikuwa zinatoa mwanya kwa Lipumba (au mwanasiasa mwingine yeyote yule)
kufanya "uhuni" kama huo.
Sababu ya pili, ni kwamba leo CUF imekabidhiwa rasmi
kwa Lipumba. Kisheria. Mahakama imetenda haki kwake kwa sababu japo alichofanya
ni uhuni, kisheria uhuni huo ulihalalishwa na CUF yenyewe.
Hili la Lipumba kukabidhiwa chama si jambo dogo. Kuna
mawili hapa. Moja, hii inaweza kuwa fursa nzuri kwa Lipumba kukijenga chama
hicho na hatimaye kukirejesha kwenye nafasi ya kuaminika kama "mbadala wa
CCM."
Lakini la pili, na hili ndilo ninahisi litatokea, ni
mwanzo wa mwisho wa CUF. Sio siri kuwa Lipumba amesaidiwa sana na CCM kuipora
CUF kutoka mikononi mwa Maalim Seif. CCM hawajafanya hayo kwa vile wanampenda
Lipumba.Hapana. Wanamtumia tu kumdhibiti Maalim Seif ambaye licha ya kila hujuma
zilizokuwa zikifanywa na CCM na taasisi zake, ameendelea kuwa mwanasiasa maarufu
zaidi kuliko wote katika siasa za Zanzibar.
Sasa, baada ya Lipumba kutumika "kummaliza Seif ndani
ya CUF," kuna uwezekano wa aina mbili tu. Wa kwanza ni kwa mwanasiasa huyo
msomi kukubali kuendelea kutumika kama kibaraka wa CCM huku CUF ikigeuka kuwa
CCM-B, na wa pili, ni kujaribu kusimama kama chama halisi cha upinzani na
hapohapo "kumwagiwa radhi na CCM" na hatimaye kupelekea kifo cha
chama hicho.
Uwezekano mkubwa zaidi ni huo wa kwanza - ukibaraka.
Kwamba CUF haitokufa. CUF itaendelea kushiriki chaguzi mbalimbali. CUF itajenga
taswira ya chama kamili cha upinzani. Lakini uwepo huo wa CUF hautokuwa kwa
manufaa ya chama hicho au siasa za upinzani bali kwa manufaa ya CCM.
Kuna kila dalili kuwa CCM itaisaidia CUF kujitanua
nchi nzima kwa sababu moja kuu: uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 utakuwa mbovu
kuliko chaguzi zote zilizowahi kutokea Tanzania. Kuna uwezekano mkubwa tu kwa
baadhi ya vyama vikuu vya upinzani kutishia kususia uchaguzi huo. Na hapo ndipo
CUF ya Lipumba itakapotumika kuhalalisha "ushindi wa Magufuli/CCM."
CCM itaisaidia CUF kuweza kusimamisha wagombea takriban
kila jimbo kwa upande wa Tanzania Bara. Lakini pia CCM itaisaidia CUF kuendelea
kuwa chama imara cha upinzani huko Zanzibar, ambako uimara wake utasaidia
kugawa kura dhidi ya CCM na wagombea wake.
Hata hivyo, "laana ya kutumika" itaikumba
CUF baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 na kama isipoishia kusambaratika basi
itabaki "chama jina" kama TLP ya Mrema.
Kuhusu uamuzi wa Maalim Seif kuhamia ACT- Wazalendo,
japo hatua hiyo inaweza kuwashangaza baadhi ya watu, ukweli mchungu baada ya
Mahakama Kuu kuhalalisha "uhuni" wa Lipumba, sambamba na "uhuni"
wake mwingine majuzi ambapo "alijitangaza" kuwa Mwenyekiti kupitia
"uchaguzi mkuu hewa" ambao pia "ulimtimua Maalim Seif" kwa
kuteua mtu mwingine kushika wadhifa wa Katibu Mkuu.
Kwa kuzingatia muda mfupi uliosalia kabbla ya uchaguzi
mkuu wa mwakani, Maalim Seif kuendelea kutafuta haki yake mahakamani kungeweza
kumkuta akiwa bado kwenye korido za mahakama wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu
ujao. Ni vigumu mno kwa chama cha siasa kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi
mkuu huku kikiwa kinakabiliwa na mpasuko katika uongozi wake wa juu.
Kwahiyo, kimkakati, uamuzi huo wa Maalim Seif
unaeleweka, na unaweza kuwa ni mbinu muhimu kwake kuendelea kuwa relevant
kisiasa.
Hata hivyo, kuna uwezekano wa aina mbili kuhusu
mustakabali wa Maalim Seif na wa chama chake kipya cha ACT- Wazalendo.
Uwezekano wa kwanza ni kwa chama hicho kuibuka kuwa
tishio katika siasa za Tanzania. ACT – Wazalendo ni chama kizuri lakini ambacho
hakikui. Kimeendelea kuwa "chama cha mtu mmoja" chini ya uongozi wa
Zitto Kabwe. Kwa muda mwingine, chama hicho kimekuwa cha kiharakati zaidi
kuliko cha kisiasa.
Mapungufu hayo yanaweza kubadilika kwa njia kuu tatu.
Kwanza, Maalim Seif hajawahi kupata fursa nzuri ya kunadi mvuto wake kwenye
majukwaa ya siasa za Tanzania Bara. ACT-Wazalendo wanaweza kuwa Jukwaa muhimu
katika hilo.
Pili, Zitto hajawahi kupata jukwaa mwafaka kunadi mvuto
wake wa kisiasa huko Zanzibar. Kwa kuungana na Maalim Seif, hii inaweza kuwa
ndio fursa mwafaka kwake.
Tatu, ACT-Wazalendo kama chama inaweza kupata fursa
mwafaja kabisa ya kuwa chama cha kitaifa badala ya kuwa "chama cha
Kigoma."
Haya yote yatawezekana tu endapo kutakuwa na
"kujitoa mhanga" kati ya mwenyeji Zitto na mgeni Maalim Seif. Kwa
mara ya kwanza, Zitto atajikuta akiongoza chama ambacho ndani yake kuna
mwanasiasa maarufu zaidi yake. Naam, Maalim Seif ni mkongwe zaidi kisiasa
kuliko Zitto. Endapo Zitto "atajitoa mhanga" (make a sacrifice) na kukubali
"kumezwa" na umaarufu wa Maalim Seif, basi chama hicho kitakuwa na
fursa kubwa ya kupanuka zaidi na hata kuja kuwa chama kikuu cha upinzani katika
pande zote za Muungano.
Lakini endapo kutakuwa na mgongano wa ego kati ya
wanasiasa hao, basi mustakabali wa chama hicho utakuwa mashakani. Lakini
pengine uwezekano wa hili kutokea ni mdogo kutokana na ukweli kwamba suala la
Maalim Seif kujiunga na ACT-Wazalendo sio limetokea tu ghafla. Ni dhahiri kuwa
kulikuwa na majadiliano ya muda mrefu na yayumkinika kuhisi kwamba tofauti kati
ya wanasiasa hao wawili (Maalim Seif na Zitto) zilifanyiwa kazi wakati wa
majadiliano hayo.
Suala jingine ambalo linaweza kuijenga ACT-Wazalendo
"mpya" (ya Zitto na Maalim Seif) au kuibomoa ni mtihani ulioikumba
Chadema mwaka 2015.
Kwa mwelekeo ulivyo ndani ya CCM ambapo Magufuli hafanyi
siri kuwa anataka chama hicho kiwe chini ya uongozi wa watu wake (wengi wao
wakiwa wana-Kanda ya Ziwa wenzake), kuna uwezekano mkubwa wa kuibuka wimbi
kubwa tu la wanasiasa wenye majina watakaotaka kuhamia Upinzani. Na endapo
Zitto na Maalim Seif watakuwa "dream team" ya kuaminika, basi
ACT-Wazalendo inaweza kuwa na mvuto zaidi kwa "wakimbizi kutoka CCM" kuliko
Chadema.
Si ajabu kwa wanasiasa kama Nape Nnauye, Mwigulu
Nchemba, Bernard Membe kujiunga na ACT-Wazalendo endapo chama hicho kitaonekana
kuwa kinaweza kutoa ushindani wa dhati dhidi ya CCM hapo mwakani.
Sasa, wakati kupokea "majina makubwa" kutoka
CCM husaidia kuongeaza umaarufu wa chama, uzoefu umeonyesha kuwa wengi wao
wenye majina hayo makubwa ni wanafiki wanaokwenda upinzani kwa sababu zao
binafsi na sio kwa maslahi ya vyama husika vya upinzani.
Kibaya zaidi, kila ujio wa "wahamiaji" hao
ni fursa mwafaka kwa CCM kupandikiza "mamluki" wake kama ilivyotokea
kwa Chadema ilipompokea Lowassa mwaka 2015.
Je ACT-Wazalendo "mpya" inaweza kutoa
upinzani wa dhati dhidi ya CCM hapo mwakani? Jibu fupi ni "muda ndio utaongea"
(time will tell). Jibu pana zaidi ni kwamba japo uwezekano huo upo lakini
sidhani kama muda unatosha kukitanua chama hicho nchi nzima hususan katika
kipindi hiki ambacho chama pekee cha siasa kinachoruhusiwa kufanya shughuli za
siasa ni CCM tu.
Hata hivyo, endapo mkazo wa ACT-Wazalendo utakuwa katika
sio tu kuongeza idadi ya wanachama bali kujenga kuaminika kwa "Watanzania
wasio na vyama," basi huenda chama hicho kikafanya vizuri kwenye uchaguzi mkuu
huo.
Ni hivi, kundi muhimu kabisa la wapigakura katika
uchaguzi mkuu wowote ule nchini Tanzania ni "Watanzania wasio na
vyama." Kwamba, hakuna chama cha upinzani kinachohitaji kupoteza muda wake
kuwashawishi wafuasi wa CCM wakipigia kura, kama ambavyo CCM haina muda na
wafuasi wa upinzani kuwashawishi waipigie kura. Vilevile, si CCM wala vyama vya
upinzani vinavyohitaji kuwashawishi wanachama/wafuasi wao wapigie kura vyama
vyao. Watu wanaohitaji kushawishiwa ni hao wasio na vyama. Na habari njema ni
kwamba kundi hilo ndilo lwenye idadi kubwa zaidi ya wapiga kura.
Kwa mujibu wa takwimu zisizo rasmi, CCM ina takriban
wanachama milioni 8 ilhali wapinzani wana wanachama takriban milioni 5. Kwa makadirio,
takriban Watanzania milioni 25 walijiandikisha kupiga kura katika uchaguzi mkuu
wa mwaka 2015. Kwahiyo, milioni 8 wa CCM jumlisha milioni 5 wa upinzani jumla
inakuwa milioni 13. Ukichukua milioni 25 kutoa miloni 13 unabakiwa na milioni
12. Kwa makadirio, hawa ni "wapigakura wasio na vyama." Na kimahesabu,
hata nusu tu ya kundi hili likielemea upande mmoja, upande huo unaweza kabisa
kushinda uchaguzi husika. Of course, hapo tunaweka kando hujuma za kawaida za
kuibeba CCM kwenye takriban kila uchaguzi mkuu.
Nimalizie kwa kukumbusha kuwa uchambuzi huu sio exact
science. Umeelemea kwenye uelewa wa kutosha wa mchambuzi kuhusu siasa za
Tanzania.
Kadhalika, uchambuzi huu ni endelevu. Utafanyiwa
marejeo mara kwa mra kila kutakapokuwa na umuhimu wa kufanya hivyo
Kwamba Daudi Albert Bashite ni mhusika mkuu katika utekelezaji wa mpango wa kijahili wa kutemka mfanyabashara maarufu Mohammed Dewji sio suala la siri. Na wala haihitaji uelewa mkubwa wa uchungui wa matukio ya kihalifu kubaini uhusika wa Bashite.
In fact, kabla ya Mo kutekwa, mfanyabiashara mwingine maarufu jijini Dar naye alinusurika kutekwa na vijana wa Bashite. Na majuzi, mfanyabiashara huyo amelazimika kumwaga shehena ya bidhaa baharini baada ya Bashite kutishia kumbambikia kesi kuhusu shehena hiyo.
Ni siri ya wazi kwamba Bashite amekuwa akiwanyanyasa wafanyabishara mbalimbali, akidai mamilioni ya shilingi, huku aktishia kuwabambikizia kesi za madawa ya kulevya iwapo watakataa. Huyo Mo mwenyewe “alishatolewa upepo” mara kadhaa na Bashite.
Kwa upande mwingine, Bashite amefika hapo alipo kwa kubebwa na watawala wetu. Baada ya kumpiga Mzee Warioba kwenye mchakato wa Katiba mpya, Rais wa Awamu ya Nne Jakaya Kikwete akamzawadia Bashite ukuu wa wilaya.
Na katika mazingira ya kushangaza, Rais Magufuli akaona Bashite hastahili kuwa mkuu wa wilaya bali apewe ukuu wa mkoa kabisa. Ninaweza kusema bila kuuma maneno kuwa huu ni mmoja wa maamuzi mabovu kabisa ya Rais Magufuli. Na huenda akatambua hilo huko mbeleni akiendelea kumkumbatia jahili huyo.
Baada ya kupewa ukuu wa mkoa, Bashite akatokea kuwa mtu wa karibu kabisa wa Magufuli. Hata alipovamia studio za Clouds Media Group, Mkuu huyo wa nchi akawamtetea vikali kijana huyo aliyetenda kosa la jinai. Hiyo ikampa Bashite jeuri na kiburi kikubwa.
Mara kadhaa, Magufuli alikuwa akimmwagia sifa Bashite akidai ndio Mkuu wa Mkoa mchapakazi kuliko wote. Mchapakazi kwa kufeli kisha kufojic heti na jina lake? Mchapakazi kwa kudai rushwa kwa wafanyabishara mbalimbali? Mchapakazi kwa yeye na “mlevi mbwa” Kitwanga kumpa yule mbwa Musiba shilingi milioni 7 za kututangaza akina sie kuwa ni watu hatari?
Kumdekeza Bashite na kumpendelea hata pale alipofanya uahlifu ndio kumemfanya haramia huyu kufikia hatua ya kufanikisha mpango wa kumteka Mo Dewji. Bashite ni kiumbe hatari kabisa na janga kubwa kuliko yote katika historia ya Tanzania. Na amin nawaambia, hata alindwe vipi na baba yake, mwisho wa jahili huyu utakuwa mbaya sana.
Na sio kama ninamtetea Magufuli, ila hili la kumteka Mo, ni mpango binafsi wa Bashite alioufanya kwa niaba ya washirika wake kutoka nje ya nchi.
Naamini hadi kufikia muda huu, watu wa Kitengo wameshamfahamisha Magufuli kuwa ‘mwanae’ Bashite ndio aliyemteka Mo, na anajua alipo.
Na hapo ndio tunabaki kujiuliza: je Magufuli atakuwa tayari kuhatarisha urais wake na “kumbeba” tena Bashite? Tayari kuna dalili hizi maana mpaka wakati ninaandika makala hii, Bashite alikuwa hajakamatwa wala kuhojiwa, achilia mbali kutumbuliwa.
Magufuli anaachia fursa adimu ya kujitenga na kijana huyo mhuni ambaye amefanya jithada kubwa kuuharibu utawala wa “baba yake.” Kama kuna mtu mmoja amechangia sana kumfarakanisha Magufuli na Watanzania wengi si mwingine bali Bashite.
Kwa kumchukulia hatua Bashite, Magufuli angeuwa ndege wengi kwa jiwe moja. Kwanza, kumtimua Bashite kungemfanya aonekane kuwa sio tu amekerwa na kutekwa kwa Mo Dewji na bali pia “kujisafisha” yeye mwenyewe dhidi ya tuhuma kuwa huenda waliomteka Mo ni watu wa serikali yake Magufuli.
Lakini pia, kwa kumtumbua Bashite, Magufuli angejiweka kando na mtu ambaye amefanya kila linalowezekana kuchafua jina la “baba yake.” Kama nilivyotanabaisha awali, Bashite amechangia mno kuwafanya Watanzania wengi tu kutoipenda serikali ya Awamu ya Tano.
Pengine kubwa zaidi ya yote ni ukweli kwamba, kwa Magufuli kuchukua hatua dhidi ya Bashite itamsaidia kujenga mahusiano bora na wafanyabiashara wakubwa ambao wamekuwa wahanga wakubwa wa uonevu wa Bashite.
Lakini kubwa zaidi katika hili ni Magufuli kuepusha uwezekano wa wafanyabiashara hao kuungana na maadui wake (Magufuli) hususan ndani ya CCM ambako kuna makundi kadhaa yenye dhamira ya kumfanya awe Rais wa muhula mmoja kama sio kumng’oa kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Ni vigumu kubashiri kwa hakika kuwa hatimaye Magufuli atamwaga Bashite lakini kilicho bayana ni kwamba ana option moja tu: amlinde ahatarishe uraia wake au ambwage ajitengenezee mazingira mazuri ya urais wake. Ifahamike mapema kuwa ikitokea Magufuli kamtumbua Bashite basi Tanzania italipuka kwa mayowe na vigelegele kana kwamba imeshinda Kombe la Dunia.
Mwisho, hatua za Magufuli dhidi ya Bashite ndio ufumbuzi pekee wa sakata la kutekwa kwa Mo. Yaani akikamatwa na kuhojiwa, ataeleza Mo yuko wapi, na hivyo kuwezesha kupatikana kwa mfanya biashara huyo tajiri si Tanzania tu bali pia ni mmoja wa matajiri wakubwa Afrika na duniani kwa ujumla. Ni matumaini yangu kuwa Magufuli atatambua kuwa akiendelea kumlea Bashite basi huenda “akaondoka nae.”
Jana ilitolewa taarifa kwa vyombo vya habari kuwa Rais John Magufuli amemteua "Msalika Robert Makungu kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora." Hata hivyo, kwa makusudi, taarifa haikueleza kabla ya uteuzi huo, Makungu alikuwa na wadhifa gani, japo ilieleza kuwa anakwenda mkoani Tabora kuchukua nafasi ya Dokta Thea Ntara ambaye amestaafu.
"Kilichofichwa" kwenye taarifa hiyo ni ukweli kwamba Makungu alikuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (DDGIS) ambaye aliteuliwa wakati mmoja na Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo, Dokta Modestus Kipilimba, Agosti mwaka jana.
Japo taarifa husika haikutumia neno "kutumbuliwa," lakini haihitaji ufahamu wa mfumo wa utawala wa Idara ya Usalama wa Taifa kumaizi kwamba kutoka u-Naibu Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo nyeti hadi u-Katibu Tawala wa Mkoa ni kushushwa cheo (demotion).
Kwa mujibu wa vyanzo vyangu vya kuaminika ndani ya taasisi hiyo, kilichopelekea hatua hiyo inayoelezwa kuwa ngumu kwa Magufuli ni tofauti kati ya watendaji hao wakuu wa taasisi hiyo, yaani Makungu na aliyekuwa bosi wake, yaani Kipilimba.
Inaelezwa kuwa tofauti kati yao ilikuwa kubwa kiasi cha Kipilimba kutishia kujiuzulu iwapo Magufuli asingechukua hatua dhidi ya Makungu.
Hata hivyo, Makungu alikuwa "mtu wa Magufuli" kwa sababu ni wote wanatoka Kanda ya Ziwa, na ni miongoni mwa "circle ya karibu ya Magufuli" ambayo pamoja na watu wengine, inayojumuisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Katibu Mkuu wa Hazina Dotto James, na aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga.
Kwahiyo wakati ingetarajiwa Magufuli "angemkumbatia poti wake Makungu" lakini kwa mujibu wa vyanzo vyangu, umuhimu wa Kipilimba kwa Magufuli ni mkubwa zaidi.
Tukio hilo ambalo halikuvuta hisia za wengi hasa kwa vile lilitokea muda mfupi baada ya kupatikana taarifa za kifo cha mlimbwende maarufu Agnes Masogange aliyefariki jijini Dar jana.
Japo wadhifa wa "Naibu Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa" (DDGIS) sio wa muda mrefu tangu uanzishwe (Makungu alikuwa mtu wa pili kushika wadhifa huo baada ya Jack Zoka kuwa wa kwanza), kitendo tu cha Mkurugenzi katika taasisi hiyo kutolewa na kupelekwa mkoani ni cha kushangaza na kinaingia moja kwa moja kwenye kumbukumbu za kihistoria.
Hata hivyo, kabla ya Makungu "kutumbuliwa" tayari kuna Mkurugenzi mwingine ambaye aliondolewa kwenye wadhifa wake kama nilivyoripoti kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter
#Tanzania Intelligence agency's Director of External Operations removed from her post. Sources indicate her pro-reform stance didn't sit well with anti-reform elements within the highly secretive organisation
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana wakati huo, kuondoka kwa mwanamama huyo kulichangiwa na mtazamo wake wa kutaka mabadiliko ndani ya taasisi hiyo ambao ulikinzana na wahafidhina wasiotaka mabadiliko yoyote kwa taasisi hiyo.
Wakati hayo yanatokea, Zoka, aliyekuwa Balozi wa Tanzania huko Canada nae alitolewa katika wadhifa huo hivi karibuni. Nilieleza kwa kirefu kuhusu tukio hilo katika makala HII
Kama ambavyo Zoka aliandamwa na lawama kwamba alikuwa akiongoza mkakati wa kuhujumu vyama vya upinzani, Makungu pia ametoka katika nafasi hiyo akikabiliwa na lawama kama hizo.
Kwa upande wangu binafsi kama afisa wa zamani katika taasisi hiyo, wakati fulani nililazimika kumwandikia barua Makungu kutokana na taarifa flani zilzonikera. Na katika barua hiyo nilimkumbusha kuwa cheo ni dhamana, na hakina mwamana.
Huyu Robert nilimtumia barua Mei mwaka jana baada ya kusikia taarifa flani zilizonikera. Nikamweleza kuwa haya madaraka hayana mwamana. Ni vitu vya kupita. Sikujua kama karma was waiting to screw him. He's learning the hard way.
Tatizo kwa wenzetu wengi wanaposhika madaraka ni ile hali ya kujisahau wakidhani watafia wakiwa kwenye madaraka. Hupuuzia ukweli kuwa ipo siku watatoka katika nafasi zinazowapa jeuri na kujikuta "mtaani." Maisha hayatabiriki, leo unalala ukiwa DDGIS kesho unaamka ukiwa RAS.
Kuhusu iwapo hatua hiyo ya Magufuli kuwa na atahri zozote, kwa sasa ni mapema mno kubashiri. Baadhi ya maafisa waliopo kazini na wastaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa walidokeza kwamba taarifa hiyo ya kuondolewa kwa Makungu imewashtua wengi
#Tanzania spoken to couple of current & ex-TISS guys and they all are shocked. It's exceedingly unprecedented for a DDGIS to be demoted to RAS.
Even more confusing is fact Makungu was a Magufuli main chap in TISS, with some regarding him as de-facto DGIS and Kipilimba a proxy pic.twitter.com/HTXMHnth9f
Kwa upande mwingine, wakati yote haya yanatokea, haijafahamika hali ikoje kwa "Idara ya Usalama wa Taifa nje ya Idara ya Usalama wa Taifa," yaani kile kikosi kilicho chini ya Daudi Alabert Bashite.
Kwamba Kipilimba ameweza kumn'goa "poti wa Magufuli" Makungu, basi huenda pia akawezesha kung'oka kwa Bashite, mtu anayeutia doa utawala wa Magufuli kwa kila hali.
Ni muhimu pia kujumuisha tweet ya mtu mmoja ambaye hujitambulisha kama Gavana wa zamani wa Benki Kuu, Daudi Balali.
Baada ya mvutano wa kimadaraka ndani ya Usalama wa Taifa, baadaye idara imegawanyika pande mbili na kudhoofu. Magufuli alielezwa wazi kwamba achague kijana wake (Msalika) aondoke na aadhibiwe au DG Kipilimba ajiuzulu. Kipilimba anaungwa mkono na jeshi na wakongwe idarani.
Nianze
makala hii kwa kuwashukuru ndugu nyote mlionitumia salamu za upendo,kunipa pole/kunipa
moyo baada ya jina langu kutajwa miongoni mwa watu 9 wanaodaiwa kuwa hatari kwa
usalama wa Tanzania.
Orodha
hiyo ilitajwa na mtu mmoja anayejiita Cyprian Musiba japo taarifa nilizonazo ni
kwamba jina hilo lina walakini kama lilivyo jina la rafiki yake – na miongoni
mwa watu waliofanikisha press conference yake – Daudi Albert Bashite. Waingereza
wanasema "birds of a feather flock
together."
Kichekesho
ni kwamba mara ya kwanza kumfahamu mtu huyo ni wakati flani aliponitumia ujumbe
kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akinifahamisha kuwa wana gazeti lao
linaitwa 'Tanzanite' na kuniomba niwe nawatumia makala. Nilipuuza ombi hilo kwa
sababu kutoka level ya kuandikia gazeti kubwa kama Raia Mwema kwenda kuandikia
kijigazeti kipya kama hicho cha Tanzanite ingekuwa kujishushia heshima yangu.
Kwa
upande mmoja,tuhuma za huyo mtu hazijanishangaza kwa sababu kadhaa. Kwanza,
tunafahamu fika ugumu wa maisha huko nyumbani, na sio suala la ajabu kuona
baadhi ya watu wakiuza utu wao ili mradi tu "njia ya kwenda msalani isiote
nyasi."
Lakini
pili, kuna jitihada kubwa za kuigeuza Tanzania kuwa kama wilaya ya Kanda ya
Ziwa. Huyo mtoa tuhuma ana asili ya maeneo hayo, na kuna hali inayozidi kuota mizizi
kwa baadhi ya wahuni wanaotoka eneo moja na Magufuli kujiona wana hatimiliki ya
Tanzania yetu.
Jingine
ambalo lilinifanya nipuuze hizo tuhuma za huyo bwege ni ukweli kwamba safari
yangu kimaisha hadi hapa nilipo imepshapitia vilima na mabonde. Nimeshaeleza
mara kadhaa kuhusu janga lililonisibu Februari 2, 2013 ambapo chombo kimoja cha
usalama hapa kilinifahamisha kuwa kuna tishio dhidi ya uhai wangu, tishio from
Tanzania. Na kwa zaidi ya mwaka mzima tangu wakati huo, nikawa ninaishi maisha
ya kutambua kuwa muda wowote ule naweza kudhurika. Licha ya ugumu mkubwa, hali
hiyo ilinipa uzoefu wa kuishi na vitisho.
Lakini
pia, hiyo hatua tu ya huyo mzembe kunituhumu naona kama tusi flani kwangu. Mie
sio wa kutuhumiwa na mtu asiyejulikana kama yeye. Ilipaswa labda awe kigogo
flani wa Usalama wa Taifa, ndo ningeweza kuchukulia suala hilo seriously.
Wanasema "usiongee na mbwa bali ongea na mwenye mbwa."
Hata
hivyo, japo sikushangazwa na tukio hilo la kihuni, nilikerwa na vitu vikuu
vitatu. Kwanza, wakati nina uhakika wa asilimia 100 kuwa huyo bwege ametumwa tu,
nilikerwa mno na uongo wa mchana kweupe uliokuwemo kwenye tuhuma zake. Uongo
huo ni pamoja na kudai kuwa FBI ni shirika la ujasusi la Marekani. Hivi hao
wapuuzi waliomtuma hawakufanya research japo kidogo ya kuwaelewesha kuwa
shirika la ujasusi la Marekani ni CIA na sio FBI?
Halafu
huyo bwege akachapia tena kwa kudai kuwa chama cha Kansela Angela Markel ni CDP
ilhali chama chake ni CDU. Halafu sijui ni mie tu na "macho yangu ya
kishushushu" niliyeona huyo jamaa akiongea kwa kuhema kana kwamba
anakimbizwa, huku amejawa na uoga mkubwa. Hizi njaa zitakuwa watu mwaka huu.
Seriously!
Kingine
kilichonikera ni jinsi huyo bwege alivyopewa umuhimu mkubwa asiostahili. Hivi
kwa mfano hiyo video ya press conference yake ingepuuzwa, nani angejua kuwa
kuwa mwendawazimu flani kuitisha press conference kutuhumu watu kadhaa wenye
heshima zao katika jamii? Kuna nyakati ukimya una nguvu zaidi ya kupigiana
kelele na mtu. So far, huyo mhuni amefanikiwa kufikisha ujumbe wake kwa watu
wengi mno kutokana na sie wenyewe – including tuliotuhumiwa -kumsaidia
kusambaza ujumbe wake muflis. Anyway, by muda huu hizo 15 minutes of fame
zimeshaisha muda wake.
Lakini
pia nilikerwa na ukweli kwamba uhuni wa aina hii ukiachwa tu bila kuchuliwa
hatua unaweza kusababisha madhara makubwa huko mbele. Maana tumeshaona jinsi Bashite
alivyoweza kuvamia studio za Clouds kisha Rais Magufuli bila aibu akamtetea
hadharani na kumsifia kuwa ni mchapakazi. Kwa kifupi, huko ni kusherehesha
uhuni.
Sasa
huyu bwege si mara ya kwanza kuibuka na press conference za kiendawazimu.Last
time aliitisha press conference na kutishia kumfungulia mashtaka shujaa Tundu
Lissu. Katika tukio hilo nilikerwa zaidi na ukweli kwamba kuna viumbe wenye
roho mbaya kama wachawi, ambao hawajatosheka na mateso aliyepitia Lissu baada
ya karibio la kutaka kumuuwa. Mie nimesoma"War Studies" na miongoni
mwa kanuni za vita ni kwamba pindi adui yako akiwa chini basi unatarajiwa kutomdhuru.
Kwahiyo hata kama Lissu ni adui yao, basi angalau wangesubiri apone kwanza
kabla ya kuanza kumwandama namna hiyo
Kwa
taarifa nilizonazo, press conference ya huyo bwege inamhusisha Bashite ambaye
bila shaka ana baraka za baba yake, lakini pia watu wa Kitengo nao wamehusika.
Ni vigumu kujua "kitengo kipi" maana kwa sasa ni kama tuna "Idara
mbili" – hiyo tunayoifahamu na hiyo "kampuni binafsi ya ulinzi wa
JPM/Bashite."
So who is this man Cyprian Musiba? Surely someone was behind his press conference: Is it @MagufuliJP? Bashite or TISS?
I'll have answers soon
| Je mtu huyu Cyprian Musiba ni nani? Kwa hakika ametumwa: Je ametumwa na Magufuli? DAB au Kitengo?
Lakini
kubwa zaidi, na hasa ndio lengo la makala hii ni kuwafahamisha Watanzania
wenzangu kwamba tafsiri halisi ya tuhuma zilizotolewa kwenye hiyo press
conference ni kuwafanya ninyi Watanzania hamna akili ya kuweza kubaini nani
hasa ni tishio kwa usalama wa taifa lenu.
Twende
hatua kwa hatua japo kwa umbali mfupi tu.Hivi katika ya hao watu tisa ni yupi
alishiriki kupanga na kutekeleza shambulio la kinyama dhidi ya Lissu? Kibaya
zaidi, Lissu nae yumo katika orodha hiyo.
Je
ni yui kati ya hao tisa alitoa ruhusa kwa askari kumpiga risasi na kumuuwa
binti asiye na hatia Akwilina? Je ni nani kati yetu aliyehusika na mauaji wa
Katibu wa Chadema Kata ya Hananasifu marehemu Daniel na Diwani wa Kata ya Namwawala
Marehemu Luena? Maana kwa matukio haya matatu tu, na pengine la nne ni la
Lissu, inatosha kuonyesha kuwa kuna pattern ya mauaji dhidi ya raia wasio na
hatia. Na kwa vile hakuna jitihada zozote za vyombo vya dola kuwasaka wahusika
na kuwatia nguvuni, yayumkinika kuhisi ushiriki wa serikali ya Magufuli katika
matukio yote hayo.
Sasa
yule bwege kuwaona ninyi Watanzania hamnazo, kwamba "anamudu kuwalisha matango
pori" kwa kudai kuwa huyo na huyu ndiyo tishio kwa usalama wa nchi yetu,
ilhali kila mwenye akili timamu anafahamu bayana kuwa tishio kubwa zaidi kwa
sasa linatoka kwa WATU WASIOJULIKANA.
Je
sie tisa tuliotajwa ndo tumegeuka kuwa "watu wasiojulikana" ambao
sote wenye akili timamu twatambua ndio tishio kwa usalama wa Tanzania?
Ni
rahisi kulitazama suala hilo kama ni uhuni wa huyo mbwa dhidi yetu lakini
kiukweli mbwa huyo kawanyea Watanzania wote wenye akili timamu. Kawafanya hamna
uwezo wa kutofautisha pumba na mchele. Huyu mtu ni adui yenu zaidi ya adui wa
sie aliotutuhumu.
Sasa
je hasira yako dhidi ya mtu huyu na waliomtuma unaionyeshaje? Mie ushauri wangu
ni mwepesi tu: kama una uwezo wa kuwasomea dua mbaya, itakuwa vema. Kama una
utaalamu wa masuala ya asili, basi ni vema pia. Hata ukitukana kimoyomoyo ni
vema pia. Lakini ukipata wasaa wa "kumpa a uso" popote pale – iwe mtandaoni
au mtaani – tafadhali fanya hivyo.
Naamini
kabisa kati ya sie tisa tuliotajwa na huyo bwege, tuna watu walio tayari
kutafuta haki kwa ajili yetu.Na haki si lazima ipatikane mahakamani. Na
mahakama zenyewe hizi zinazoendeshwa kwa rimoti na Magufuli hadi kumfunga Sugu
wala hazina maana. Ombi langu kwenu ni kila aina ya laana dhidi ya mtu huyo, si
kwa sababu labda ana umuhimu flani bali ukweli huo niliyotanabaisha hapo juu
kuwa amewaona ninyi Watanzania kama hamnazo hadi kufikia hatua ya kutuzushia
sie tusio na hatia tuhuma hizo za kuhatarisha usalama ilhali sote tunafahamu
vema akina nani wanaohatarisha usalama wa Tanzania yetu.
Kama
ukinitumia picha wakati unamfanyia kisomo huyo mbwa basi itakuwa vema sana haha
Jana
Januari 9, 2018, wiki moja na siku mbili baada ya kuanza kwa mwaka huu mpya, duru
za siasa za Tanzania zilitikiswa na habari kuhusu kiongozi maarufu wa Chadema,
Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kukutana na Rais John Magufuli kwa “mazungumzo”,
Ikulu jijini Dar es Salaam.
Baada
ya “mazungumzo” hayo Lowassa alimmwagia pongezi Magufuli kwa kile alichokiita “kazi
nzuri anayoifanya” na kutaja mafanikio katika sera ya elimu bila malipo, ujenzi
wa mradi wa uzalishaji wa umeme katika maporomoko ya mto Rufiji (Stiegler’s
Gorge), na ujenzi wa viwanda na ujenzi wa reli ya “standard gauge”.
“Nimepata faraja sana kuja hapa Ikulu kuonana
na Mheshimiwa Rais, tumezungumza nae na nimempongeza kwa kazi nzuri
anayoifanya, lazima tukiri anafanya kazi nzuri na anahitaji kutiwa moyo,” alinukuliwa
Lowassa aliyejiunga na Chadema miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka
2015 baada ya ndoto zake kuwania urais kwa tiketi ya CCM “kuota mbawa.”
Mwanasiasa
huyo ambaye baada ya kujiunga na Chadema alipitishwa kuwa mgombea urais kwa
tiketi ya muungano wa vyama vinne vya upinzani – Chadema, CUF, NCCR Mageuzi na
NLD – uliofahamika kama UKAWA, aliendelea kusema kuwa “Moja kubwa ambalo ni la msingi sana ni la kujenga ajira, katika kuanza
ujenzi wa reli ya kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro hapo anajenga ajira, na
kwenye nchi yoyote inayoendelea suala muhimu ni kujenga ajira, Stiegler’s Gorge
ni kujenga ajira na mingine ya aina hiyo, lazima kuwepo na kipaumbele cha
kusema kwamba tunajenga ajira. Jingine ni la elimu, ni muhimu sana, hauwezi
kuacha elimu katika mambo yako unayofanya, hili nalo lazima lisemwe vya
kutosha, kwa kweli nakushukuru Mheshimiwa Rais, you made my day.”
Rais
Magufuli kwa upande wake alimpongeza Lowassa kwa kile alichokiita “kutambua
kazi kubwa inayofanywa na Serikali” na kumtaja Lowassa kama mmoja wa viongozi
ambaye kwa wakati wake alitoa mchango wake katika nchi.
Magufuli
alimmwagia sifa Lowassa akidai kuwa “ni mwanasiasa mzuri kwani hata wakati wa
kampeni za uchaguzi mkuu uliopita ambao naye aligombea kiti cha Urais, hakuwahi
kumtukana.”
“Mheshimiwa Lowassa ameniomba mara nyingi
nikutane nae, na leo nimekutana nae, tumezungumza mambo mengi, ameniambia ya
kwake na mimi nimemwambia ya kwangu. Kwa ujumla Mheshimiwa Lowassa ni
mwanasiasa mzuri na tuendelee kuwaenzi wazee hawa ambao kwa nyakati fulani
walifanya mambo mazuri, na mimi napenda kumpongeza Mhe. Lowassa ambaye kama
alivyosema hapa kuwa tumefanya mambo mazuri mengi,” alisema Rais Magufuli
“Ametaja miradi mbalimbali tunayotekeleza,
ametaja mradi wa Stiegler’s Gorge utakaogharimu zaidi ya Shilingi Trilioni 7,
amezungumzia juu ya elimu bure, amezungumzia juu ya maji ambayo kwa bahati
nzuri yeye alikuwa Waziri wa Maji na anafahamu sasa tumefikia wapi, amezungumza
juu ya umeme tulivyosambaza katika vijiji mbalimbali, elimu bure, huduma za
hospitali na mengine” aliongeza Rais Magufuli.
Kwanza,
ni muhimu kutambua kuwa kama Mtanzania yeyote yule, Lowassa alikuwa na kila
haki ya kukutana na Rais wake. Kadhalika, kama mmoja wa viongozi wakuu wa
upinzani, isingepaswa kuwa jambo la kushangaza kwa viongozi hao wawili
kukutana.
Hata
hivyo, Lowassa sio tu amekutana na Magufuli, bali pia ammemwamgia sifa. Je ni
dhambi kwa kiongozi wa chama cha upinzani kumwagia sifa Rais aliyepo
madarakani? Jibu lingepaswa kuwa “si dhambi,” laiti uhusiano kati ya Rais
Magufuli, serikali yake na taasisi zake (kama vile jeshi la polisi, Tume ya Taifa
ya Uchaguzi, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa), watendaji wa serikali (hasa
mawaziri na manaibu wao, na wakuu wa mikoa na wilaya), pamoja na chama cha Magufuli
yaani CCM, na chama anachotoka Lowassa, yaani Chadema, na Upinzani kwa ujumla,
ungekuwa mzuri.
Lakini
ukweli ni kwamba japo tangu kuruhusiwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992,
uhusiano kati ya CCM, serikali zake na taasisi zake, na vyama vya upinzani
umekuwa “wa kusuasua,” hali katika miaka miwili tu ya utawala wa Magufuli
imekuwa mbaya zaidi hususan kutokana na ukweli kwamba hakuna jitihada za
kuficha chuki iliyopo dhidi ya Upinzani.
Kama
kiongozi wa ngazi za juu kabisa wa Chadema, na pengine mwanasiasa anayeheshimiwa
zaidi ya kiongozi mwingine yoyote ndani ya chama hicho, ni wazi Lowassa
anafahamu vema msimamo na mtazamo wa chama chake kuhusu Magufuli na utendaji
kazi wake, na serikali yake, na chama chake.
Pengine
kwa kuweka picha sawia, inaelezwa kwamba hadi wakati huu, zaidi ya wana-Chadema
400 ikiwa ni pamoja na viongozi na wanachama, aidha wapo jela au wana kesi
zinazoendelea mahakamani ambazo takriban zote ni matokeo ya chuki za kisiasa
zinazofanywa na Magufuli, serikali yake na chama chake.
Kadhalika,
katika utawala wa Magufuli, vyama vya upinzani ikiwemo Chadema ambayo Lowassa
ni kiongozi wake wa kitaifa vimepigwa marufuku kufanya shughuli zao za kisiasa
ikiwa ni pamoja na mikutano na maandamano. Hayo yanatokea wakati CCM ikiwa huru
kufanya mikutano na maandamano itakavyo, mara nyingi ikitumia raslimali za
umma.
Sambamba
na jitihada za Magufuli kubana fursa ya siasa (political space), utawala wa
kiongozi huyo umekuwa mstari wa mbele kuvibana vyombo vya habari na kudhibiti
uhuru na haki ya wananchi kutoa mawazo yao kama Katiba inavyowaruhusu.
Lakini
jingine ambalo Chadema ni mhanga mkubwa, kada maarufu wa chama hicho Ben
Saanane “alipotea” Novemba mwaka jana na hadi leo hajapatikana.
Na
ni wakati ninaandika makala hii nimebaini kuwa Lowassa hajawahi kuongelea suala
la kada huyo (naomba nikosolewe kama nimekosea).
Kubwa
zaidi linaloweza kuhalalisha hasira za Chadema kwa utawala wa Magufuli ni tukio
la hivi karibuni ambapo Mbunge wake maarufu, ambaye pia alikuwa mpinzani
maarufu dhidi ya Magufuli, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, kunusurika
kuuawa baada ya shambulio la risasi kadhaa huko Dodoma. Kwa sasa Lissu yupo
nchini Ubelgiji kwa matibabu, lakini japo Lowassa alimtembelea alipokuwa
hospitalini Nairobi, Magufuli hakuwahi kutia mguu kumjulia hali mwanasiasa huyo
ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa upinzani bungeni na Rais wa Tanganyika Law
Society (TLS).
Kwahiyo
japo pongezi za Lowassa kwa Magufuli zinaweza kuwa na uzito, mapungufu ya
utawala wa rais huyo wa awamu ya tano, hususan kuhusiana na chuki na uonevu
dhidi ya vyama vya upinzani, hususan Chadema, yalipaswa “kumzuwia” kada huyo wa
zamani wa CCM kumwaga pongezi hizo.
Kibaya
zaidi, imebainika kuwa Lowassa alishawahi kumwomba Mkuu wa Mkoa wa Arusha,
Mrisho Gambo amsaidie kukutana na Magufuli. Hata hivyo, Gambo alipotamka hilo
hadharani, Lowassa “aliruka kimanga.”
#OMG! So this was actually true. Uzuri wa hii drama ya leo kuhusu Lowassa inathibitisha kuwa sie tuliojivua ushabiki wa Chadema (baada ya ujio wake huko) tulikuwa sahihi. I hope waliotutukana watapata ujasiri wa kutuomba msamaha pic.twitter.com/pctNKaXnaU
Hata
hivyo, jana Magufuli alitamka bayana kuwa Lowassa aliomba mara kadhaa kukutana
naye. Kwahiyo, alichosema Gambo kilikuwa kweli, na Lowassa hakuwa mkweli
alipokana kuwa hajaomba kukutana na Magufuli.
Tukio
hilo la Lowassa kukutana na Magufuli na kumwagia pongezi limepokelewa kwa hisia
tofauti. Wakati kuna kundi dogo la wana-Chadema waliopongeza hatua hiyo, kwa
mfano “kada” mmoja wa chama hicho Yericko Nyerere, wengi ikiwa ni pamoja na
baadhi ya viongozi wamepingana waziwazi na Lowassa.
Wakati
Yericko aliandika haya
Mbunge
maarufu wa Chadema, Godbless Lema alikuwa wa kwanza kueleza bayana kutoafikiana
na pongezi za Lowassa kwa Magufuli.
Mh Lowassa,umeikosea Tanzania kwa kauli baada ya kutoka Ikulu,mema yapi umeyaona katika Serikali hii?Wkt Mbunge Lissu bado anauguza majeraha ya risasi,maiti zinaokotwa,Uchumi unaanguka,Benki zinafungwa ,demokrasia imekufa Bungeni /Nje ya Bunge na Sioi mkwe wako bado yuko Magereza
Baadaye, Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema,
Freeman Mbowe, naye alieleza kuwa kauli za Lowassa ni zake binafsi na sio
msimamo wa chama hicho.
"Alichokisema Lowassa leo alipotembelea Ikulu ya Tanzania ni msimamo wake binafsi na wala sio msimamo wa CHADEMA" ~ Freeman Mbowe leo, ameyasema hayo akihojiwa na DW- Idhaa ya Kiswahili jioni hii. pic.twitter.com/WUjOo9qocL
Kadhalika, Mbowe alionekana kumkumbusha Lowassa kuhusu matukio mbalimbali yasiyopendeza katika utawala wa Magufuli
"Kumekuwepo na matukio ya watu kuuawa na kupotea, demokrasia na haki za binadamu zinaminywa, uchumi unazidi kudidimia. Katika mazingira hayo, tunashindwa kuelewa unapata wapi ujasiri wa kuisifu serikali ya Rais Magufuli."- M/Kiti CHADEMA, Freeman Mbowe (Mb) pic.twitter.com/AVXmnNMqg0
Lakini
pengine aliyeeleza kwa kirefu kuhusu suala hilo ni Lissu, ambaye akiwa
hospitalini huko Ubelgiji, alitoa waraka huu hapa chini.
Waheshimiwa
habari za Tanzania na poleni kwa yote.
Naomba
na mimi niseme kwa uchache kuhusu suala hili. Samahani kama 'uchache' wangu
utakuwa mrefu kidogo.
Baada
ya Mwenyekiti kuzungumzia jambo hili, inaelekea kuwa wazi kwamba Mheshimiwa
Lowassa hakumshirikisha Mwenyekiti kabla ya kukubali au kuamua kwenda Ikulu
kukutana na Rais Magufuli.
Na
juzi tu wakubwa wetu hawa wawili walikuwa pamoja hospitalini kumsalimia Mzee
Ngombale Mwiru.
Je,
inawezekana Mheshimiwa Lowassa hakuwa anajua tayari kwamba ana appointment
Ikulu?
Kama
alikuwa anajua, kutokumshirikisha Mwenyekiti wake kuna tafsiri gani hasa?
Katika
mazingira ya sasa ya Tanzania ya Magufuli, uamuzi wowote wa kufanya nae
mazungumzo, hata kwa nia njema yoyote ile, bila kushauriana au kuwashirikisha
viongozi wa juu wa chama, ni uamuzi usio sahihi na mgumu kukubalika.
Vile
vile, kauli za aina ambayo tumeisikia leo kutoka kwa Mheshimiwa
Lowassa, zina athari kubwa kisiasa.
Sio
tu zinachanganya wanachama na wafuasi wetu, lakini pia zinawapa mtaji wa
kisiasa maadui zetu.
Kuanzia
sasa tutegemee sana kuwasikia maCCM yakishangilia 'busara' za Mheshimiwa
Lowassa.
Masuala
ya ukiukwaji haki za binadamu, uvunjwaji wa Katiba na mengine mengi sasa
yatajibiwa kwa namna moja: Lowassa amemkubali Magufuli nyie wengine mnapiga
kelele za nini.
Huu
ni mtaji wa bure kwa Magufuli. Ukweli, ambao umesemwa sana humu, ni kwamba
amefeli karibu katika kila jambo.
Hata
hiyo reli anayosifiwa nayo na Lowassa bado ni ndoto tu: nani ajuaye itajengwa
kwa hela za nani???
Za
Wachina kama tulivyoambiwa mwanzoni; au za Waturuki kama tulivyoambiwa baadae;
au za Afrika Kusini kama alivyosema mwenyewe anaenda kumwomba Zuma???
Kama
chama hatujawahi kukataa mazungumzo na Rais au kiongozi mwingine yeyote wa
serikali.
Na
hatukatai kuzungumza na Magufuli kuhusu matatizo mengi na makubwa yanayoikabili
nchi yetu.
Lakini
ni muhimu na lazima viongozi wakuu wa chama washirikishane na washauriane kabla
ya mazungumzo hayo.
Na
baada ya mazungumzo, ni lazima viongozi wakubaliane juu ya kauli za kutoa
hadharani kwa umma ili wote tuwe kwenye ukurasa mmoja.
Katika
mazingira ya sasa, ambako viongozi na wanachama wetu wanashambuliwa hadharani
kwa mapanga na hata kwa risasi, kumsifia Rais ni kumuunga mkono yeye na matendo
yake.
Katika
mazingira ya kesi nyingi za kutunga dhidi yetu, 'kazi nzuri' inayofanywa na
Magufuli ina maana gani hasa, kama sio kuhalalisha ukandamizaji tunaofanyiwa.
Katika
mazingira ambapo hata jumuiya ya kimataifa imeanza kuhoji mwenendo wa Rais
Magufuli, kutoa kauli kwamba 'anafanya kazi nzuri' ni 'kumtupia taulo' la
propaganda litakalomfichia madhambi mengi aliyowafanyia Watanzania katika miaka
hii miwili.
Kwa
vyovyote vile, kitendo cha Mheshimiwa Lowassa sio cha kunyamaziwa au
kuhalalishwa kwa hoja nyepesi nyepesi.
TUNDU
LISSU(MB).
Top of Form
Kadhalika,
kada maarufu wa kike wa chama hicho, Hilda Newton nae alieleza masikitiko yake
kutokana na kauli za Lowassa.
Bila kumung'unya maneno leo Mh @edwardlowassatz kanikwaza mpaka nahisi kupasuka
Yani kabisa umefunga safar unaenda kuongea na adui tena mwenye roho ya Ukatili alaf unamsifia??
Nmeumia sana mpaka machozi yamenitoka, Lowassa katukosea sana yani nchi ipo kwenye mkwamo wa kisiasa yeye anaenda kumsifia adui!!..@tundulissutz kashambuliwa kwa risasi, Serikali ipo kimya hakuna cha uchunguzi wala nin yeye kapata wapi ujasir wa kumsifia adui ??
Kama
alivyotahadharisha Lissu, ni wazi kwamba CCM watakuwa wamepewa “silaha” mpya
katika “kumpamba” Magufuli na “kuwapenda” wapinzani, kwamba “hata Lowassa wenu
anamkubali Magufuli.” Na ni rahisi kwa CCM kuonekana wana mantiki katika hoja
hiyo, kwa kudai “kama mtu muhimu kabisa kwenye chama chenu (yaani Lowassa)
ambaye ndiye aliyekuwa mpinzani mkuu wa Magufuli kwenye uchaguzi mkuu uliopita,
anamkubali mkuu huyo wa nchi, ninyi ni akina nani kumpinga?”
And guess what, Lowassa amewapatia CCM narrative muhimu sana: "hata @edwardlowassatz wenu anamkubali @MagufuliJP" and unless you missed your meds, you can't disagree with them.
Wakati
ni wazi kwamba uamuzi wa Lowassa kukutana na Magufuli, na kumwagia pongezi,
umezua “sintofahamu” huko Chadema, kuna masuala kadhaa ya muhimu yanayopaswa
kuangaliwa kwa makini kwa ajili ya mustakabali wa chama hicho.
Kwanza,
ni muhimu kwa viongozi na wanachama wa Chadema kutambua nafasi ya Lowassa katika
chama hicho. Wakati baadhi ya wachambuzi wa siasa – mie nikiwa mmoja wao –
wanaamini kuwa ujio wa Lowassa katika chama hicho ulikuwa na hasara zaidi
kuliko faida, jitihada zilizofanywa na chama hicho kumpigania mwanasiasa huyo
zimemjengea hadhi ambayo haipo kwa mwanasiasa mwingine yoyote ndani na nje ya
chama hicho.
Ikumbukwe
kuwa hadi wakati jina lake lilipokatwa na vikao vya CCM katika mchakato wa
kusaka mgombea wa urais kwa tiketi ya chama hicho tawala, Lowassa alikuwa ndiye
mwanasiasa maarufu kuliko wote Tanzania. Yayumkinika kusema alikuwa mtu wa pili
kwa umaarufu baada ya marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere. Licha ya
kulazimika kujiuzulu Uwaziri Mkuu mwaka 2008 kutokana na kashfa ya Richmond,
Lowassa aliendelea kuwa mwanasiasa maarufu na mwenye nguvu kuliko yeyote yule
ndani ya CCM, hata zaidi ya Rais na mwenyekiti wa taifa wa chama hicho wakati
huo, Jakaya Kikwete.
Na
japo kukatwa kwa jina la Lowassa huko CCM kulimpunguzia kidogo umaarufu wake
kwa siasa za Tanzania – ilikuwa kama miujiza kuona CCM ilikuwa na ujasiri wa
kukata jina la mwanasiasa huyo- alihamia Chadema akiwa na sapoti ya kutosha
kiasi japo si kubwa kama ilivyotarajiwa.
Japo
kuna “tuliopishana nae mlangoni” – kwa maana yeye alipoingia, sie tukatoka –
ujio wake ulipelekea kuwa mwanasiasa maarufu zaidi ya wote wa Upinzani. Na ndio
maana haikuwa vigumu kwake kupitishwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA.
Nimeeleza
kuwa baadhi yetu “tulipishana nae mlangoni” kwa sababu mie binafsi nilikuwa
naiunga mkono Chadema, si kama mwanachama bali ukweli kwamba kwa muda mrefu
nimekuwa nikijihusisha na harakati za mapambano dhidi ya ufisadi, na chama hicho
kilijitokeza kuwa championi wa mapambano hayo. Kwahiyo, “naturally” nilijikuita
nikikiunga mkono.
Hata
hivyo, ujio wa Lowassa katika chama hicho ulinikimbiza. Sababu kuu ni binafsi
zaidi, na nisingependa kuongelea hapa, lakini sababu nyingine ni kile
nilichotafsiri kama usaliti wa Chadema. Ikumbukwe kuwa tangu mwaka 2006, chama
hicho “kilimkalia kooni” Lowassa kumtuhumu kuwa ni fisadi, na ndicho
kilichofanya jitihada kubwa zilizopelekea mwanasiasa huyo kujiuzulu Uwaziri
Mkuu mwaka 2008.
Mmoja wa watu walionipa kiu ya uandishi asema "Lowassa anawaadhibu Mbowe,Lissu,nk kwa kumwita fisadi for 9 yrs." Mtu huyo ni Johnson Mbwambo
Sasa
bila hata kutumia jitihada kidogo tu za busara, chama kilichomwandama Lowassa
kuwa ni fisadi, kwa miaka 9 mfululizo, yaani 2006 hadi 2015, kilionekana kituko
kwa baadhi yetu tuliokuwa tukikiamini, kwa sababu, pamoja na mengine,
isingewezekana kutumia miezi mitatu (Julai 2015 Lowassa alipojiunga na chama
hicho hadi Oktoba wakati wa uchaguzi mkuu) kumsafisha vya kutosha.
Na
gharama ya ujio wa Lowassa ilikuwa kubwa. Moja kubwa zaidi ilikuwa lazima kwa
Chadema “kuitosa” turufu yake muhimu, ajenda ya vita dhidi ya ufisadi.
Ililazimika kufanya hivyo kwa sababu kuzungumzia ufisadi ilhali chama hicho
kimemkumbatia mwanasiasa kiliyemwita “baba wa ufisadi” kwa miaka 9 mfululizo
ingeonekana kioja.
Kadhalika,
kwa kumpokea Lowassa, Chadema ilikuwa haina jinsi ya kukwepa tuhuma kutoka CCM
kuwa chama hicho upinzani ni cha kifisadi kwa sababu ya kumkumbatia mwanasiasa
ambaye kilikuwa kikimuita fisadi. Jitihada za Chadema kujibu mashambulizi kuwa “kama
Lowassa ni fisadi mbona hajachukuliwa hatua,” zilikuwa hazina mashiko.
Lakini
jingine lililoipa jeuri CCM ni ukweli kwamba kwa chama hicho, Lowassa alikuwa
ni “makapi” sambamba na wanasiasa wengine waliomfuata huko Chadema. Hiyo
ilikipa chama hicho tawala “jeuri” ya namna flani. Na waliitumia vema kwenye kampeni,
kwamba “hawa jamaa si lolote si chochote. Yani wameshindwa hata kutafuta
mgombea wao wenyewe mpaka wakasubiri makapi kutoka kwetu ndo wakapata mgombea
urais.” Na pamoja na maneno hayo kuwa machungu, ndo ukweli ulivyokuwa.
Chadema
na UKAWA kwa ujumla walikuwa na takriban mwaka mzima wa kujipanga; kuafikiana
kuhusu mgombea urais kwa tiketi ya umoja huo, na kumnadi, huku wakitumia “advantage”
ya “vita vya wenyewe kwa wenyewe” kati ya zaidi ya makada 40 waliokuwa
wakichuana kuteuliwa na CCM.
Badala
yake, kumbe tayari kulikuwa na makubaliano ya siri kati ya uongozi wa baadhi ya
viongozi wa juu wa Chadema kwamba wasubiri kutangaza mgombea wao hadi baada ya
mchakato wa CCM kupata mgombea wake, ka maana ya “kumhifadhia nafasi Lowassa
endapo jina lake litakatwa huko CCM.”
Kabla
ya kwenda mbali na makala hii ningependa nishauri Chadema irejee suala hilo la
Lowassa kuandaliwa nafasi ya kuwania urais japo wakati huo alikuwa CCM. Hatua
stahili zinapaswa kuchuliwa dhidi ya wote waliohusika na mpango huo.
Na
ujio wa Lowassa ulipelekea Chadema kumpelekea mmoja wa magwiji wa siasa za
upinzani, Dokta Willbrord Slaa. Umahiri wa Dokta Slaa haukuwa tu katika
kuchukia ufisadi kwa dhati bali umahiri wake mkubwa katika kujenga hoja kisomi.
Kadhalika, alikuwa akiaminiwa na watu mbalimbali muhimu ndani ya serikali,
kiasi kwamba baadhi yao walihatarisha ajira zao kwa kumpatia mwanasiasa huyo
nyaraka muhimu zilizoiwezesha Chadema kuwa na ushahidi mbalimbali katika vita
yake dhidi ya ufisadi.
Na
kuonyesha kuwa alikuwa na msimamo imara, Dokta Slaa aliamua kujiweka kando katika
uongozi kupinga Lowassa kupewa ugombea urais wa UKAWA. Lakini jambo la
kusikitisha mno, kiongozi huyo aliyekifanyia mengi chama hicho alidhalilishwa
na kutukanwa kupita kiasi.
Na
“akina sie” tulishindwa kustahimili ujio wa Lowassa, na kwa vile kwa baadhi
yetu ilikuwa muhimu kumzuwia asiingie Ikulu, na hivyo kulazimika kumpigia
kampeni mpinzani wake yaani Magufuli, tulitukanwa kila aina ya matusi. Sijui
watu hawa waliojitoa ufahamu wataweka wapi sura zao pindi Lowassa “akirejea
nyumbani” CCM.
Wakati
anajiweka kando na uongozi wa Chadema, Dokta Slaa alikitahadharisha chama hicho
kuwa ili kuleta mabadiliko ya kweli (badala ya hayo “ya kisanii” aliyokuwa
akiyanadi Lowassa) chama hicho kinahitaji mkakati makini utakaoongozwa na watu
makini. Na kwa hakika, tangu wakati huo, Chadema imekuwa kama kundi la
wanaharakati wa kudandia hoja kuliko chama cha siasa chenye ajenda ya
kueleweka. Uamuzi wa kuitelekeza ajenda ya vita dhidi ya ufisadi ulipelekea chama
hicho kutokuwa na ajenda moja ya maana, huku CCM “wakipora” kiurahisi ajenda ya
vita dhidi ya ufisadi.
Je
mustakabali wa Chadema ukoje? Japo sio rahisi sana kubashiri kwa uhakika kuhusu
hatma ya chama hicho, binafsi – kwa kutumia uzoefu wangu na uelewa wa kutosha
wa siasa za Tanzania, sambamba na kuwa na fursa ya kufahamu “yanayojiri nyuma
ya pazia” la siasa za nchi yetu – ninadhani kuwa kuna uwezekano mkubwa tu kwa
Lowassa kurudi CCM kama sio kuachana kabisa na siasa.
Kwanini
Lowassa anaweza kurudi CCM? Kuna sababu kuu mbili. Moja ni dalili za wazi kuwa
ndoto zake za urais kupitia chama hicho ni kama zimeyeyuka. Umaarufu wake
umegubikwa na kuibuka na kuimarika kwa umaarufu wa Lissu. Ni dhahiri kwamba
ikipigwa kura ya maoni kuwa nani kati ya Lowassa na Lissu awe mgombea urais kwa
tiketi ya Chadema mwaka 2020, Lissu ataibuka mshindi. Na Lowassa anafahamu kuwa
hakuna njia ya mkato kwa yeye “kulazimisha” awe mgombea katika uchaguzi mkuu
huo ujao, licha ya ukweli kwamba alishatangaza kuwa atagombea.
Sababu
nyingine ni binafsi zaidi. Lowassa ni mmoja wa matajiri wakubwa nchini
Tanzania. Kama utajiri huo ulipatikana kihalali au kifisadi, si lengo la makala
hii kujiingiza katika mjadala huo. Lililo wazi ni ukweli kwamba licha ya kuwa
mwanasiasa, yeye pia ni mfanyabiashara. Na kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika,
serikali ya Magufuli imefanikiwa kutumia nyenzo yake muhimu dhidi ya wapinzani
ambao pia ni wafanyabiashara, KODI.
Inaelezwa
pia kwamba mali mbalimbali za mwanasiasa huyo zipo hatarini kutokana na uwepo
wake huko Upinzani. Inadaiwa kuwa hata jengo la Tanesco Ubungo ambalo serikali
imetangaza kulivunja, linamilikiwa na Lowassa, na tishio la kulivunja lilikuwa
kama kufikisha ujumbe kwake.
Katika
hili, Lowassa hatoonekana mtu wa ajabu akiamua kurudi CCM ili asibughudhiwe
kuhusu biashara na mali zake. Ni nani kati yetu anayeweza kujitoa mhanga kwa
ajili tu ya imani yake ya siasa? Si kama hawapo ila ni adimu mnooo! Na kibaya
zaidi, hata akiamua kung’ang’ania huko Chadema, hatma yake na ya chama hicho haieleweki
kwa sababu hadi muda huu – na hii ni licha ya zuwio la Magufuli dhidi ya vyama
vya upinzani kufanya shughuli zao za siasa – chama hicho kikuu cha upinzani “kipo
kipo” tu. Hakina ajenda moja ya kueleweka zaidi ya kudandia kila tukio
linalojiri.
Iwapo
Lowassa ataamua kubaki Chadema, hiyo itakuwa fursa mwafaka kwa chama hicho
kumpumzisha. Naamini kuwa wana-Chadema wakiweka kando ushabiki wa kisiasa,
wanafahamu fika kuwa mwanasiasa huyo hana nguvu, uwezo wala mvuto wa
kukabiliana na siasa hatari zinazoendelea muda huu huko nyumbani.
"Aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya UKAWA katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, atangaza kurejea CCM. Asema anaridhishwa na uchapakazi wa Rais Magufuli"#FutureTweet#MarkThisTweet [Future Tweet ni tweet ya kufikirika japo yaweza kuwa kweli] pic.twitter.com/DiiKxtbwj3
Kwa upande mwingine, tukio la Lowassa kukutana na Magufuli Ikulu linaweza pia kuhusishwa na tamko la hivi karibuni la Katibu Mkuu wa CUF, Seif Sharif Hamad, ambaye kama Lowassa, alimmwagia sifa Magufuli.
Je kuna disconnect kati ya baadhi ya viongozi wakuu wa upinzani na wengi wa wafuasi wa vyama hivyo? pic.twitter.com/IkA9566Oop
Nimefanya uchambuzi kuhusu kauli za wanasiasa hao wawili hapa, lakini ninachoweza kugusia hapa ni haja ya kutambua kuwa wanasiasa hao bado wanatunzwa na serikali kutokana na nyadhifa walizowahi kushika huko nyuma. Haihitaji uelewa mkubwa kuhusu "siasa za kibabe" kuhisi kwamba huenda "malezi" wanayopewa na serikali yametumika kama "chambo" cha kuwavuta karibu na Magufuli. Kuhusu matatizo yanayoikabili Chadema muda huu,ukweli ni kwamba ni zaidi ya uwepo wa Lowassa ndani ya
chama hicho. Japo huu ni ukweli mchungu usioruhusiwa kabisa kusikika ndani ya
chama hicho, licha ya kazi nzuri ya kuifikisha Chadema ilipo leo, mwenyekiti wa
taifa Mbowe anapaswa kutoa fursa kwa wana-Chadema wengine kusukuma gurudumu la
chama hicho. Na hatua hiyo wala haihusiani na mchango wake mkubwa wa kumleta
Lowassa ndani ya chama hicho na “kumpa” ugombea urais wa UKAWA.
Kirefu
cha Chadema ni Chama cha DEMOKRASIA na Maendeleo. Sasa ni demokrasia gani hiyo
ambayo inaruhusu mwenyekiti mmoja kuwa madarakani milele? What if “uenyekiti wa
milele” ni miongoni mwa vikwazo kwa maendeleo ya chama hicho?
Lakini
hata kama “muda wa Mbowe kutoka madarakani haujafika,” busara tu inapaswa
kumfahamisha kiongozi huyo kuwa ni vema kuzingatia busara za akina Nyerere
waliojing’atua wakiwa bado wanahitajika. Sipendi kubashiri hili, lakini laiti
Mbowe asipohamasisha mageuzi kwenye medani ya uongozi wa chama hicho, haitokuwa
jambo la ajabu akiishia kung’olewa kwa nguvu.
Na
kwa bahati mbaya kwake, hili “songombingo” alilolianzisha Lowassa jana linaweza
kuwa kama mnyororo mrefu ambao mahala flani yupo Mbowe. Ndiye aliyemkaribisha
Lowassa.
Moja
ya mapungufu makubwa mno yanayoitafuna Chadema muda huu ni pamoja na kulipuuza
kundi muhimu linalokisaidia mno chama hicho, lundo la vijana wanaoshinda na
kukesha katika mitandao ya kijamii wakijaribu kukinadi chama hicho angalau kwa
kuikemea serikali ya Magufuli au CCM kwa ujumla.
Laiti
chama hicho kingekuwa na ajenda ya kueleweka, basi jeshi hili la vijana
lingekuwa nyenzo muhimu mno. Ni rahisi kuwalaumu vijana hawa kuwa “kazi yao
kubwa ni kudandia hoja tu,” lakini ukweli ni kwamba chama chao hakiwapatii
ajenda ya/za kueleweka. Kibaya zaidi, hata pale wanapojaribu kutengeneza ajenda
wao wenyewe – kwa mfano jitihada za kumsaka Ben Saanane – hawapati sapoti ya
kutosha kutoka uongozi wa juu wa chama hicho.
Ni
hivi, wengi wa hawa vijana wanahatarisha maisha yao kwa kuwa tu “upande usiotakiwa”
na serikali ya Magufuli. Hawategemei malipo yoyote zaidi ya kuamini kuwa siku
moja wanaweza kukiingiza chama chao madarakani. Hakuna jitihada za makusudi za
uongozi wa juu wa chama hicho kuwa karibu na kundi hili muhimu.
Ukiwa
UVCCM una uhakika wa angalau “kuhongwa na Bashite” au kualikwa kwenye “mnuso”
sehemu flani. Lakini ukiwa kijana wa upinzani, “zawadi” kubwa yaweza kuwa
kusumbuliwa na vyombo vya dola na kuishi maisha ya wasiwasi. Kwahiyo vijana wa
upinzani wana kila sababu ya kuichukia siasa, kwa sababu inahatarisha maisha
yao, lakini mapenzi yao katika imani ya chama inawalazimisha kung’ang’ania
hivyo hivyo.
Niionye
Chadema kuwa katika zama hizi za “ununuzi wa binadamu kama zama za utumwa,”
chama hicho kisishangae pindi wengi wa vijana hawa watakapoamua kubwaga
manyanga na kukubali “kununuliwa.” Kwanini waendelee kuhatarisha maisha yao
ilhali uongozi wa juu wa chama hicho hauna muda nao?
Akina
Hilda Newton, Ben Malisa, Bob Wangwe, Ndehani Mwenda, Noel Shao, Gift Nanyaro
ni miongoni mwa vijana wanaofanya kazi kubwa kwa ajili ya Chadema, bila ya
matarajio ya malipo au fadhila flani, zaidi ya kuhatarisha maisha yao. Kama
ilivyo kawaida ya mwanadamu yeyote yule, inaweza kufika mahala mtu akarudi
nyuma na kujiuliza, “is it worth it?” Na japo sitarajii kuona makada hao vijana
wakiamua kuipa kisogo Chadema, lakini sintoshangaa baadhi yao wakiamua kuipa
kisogo siasa, hasa kama tasnia hiyo itaendelea kuwa “yenye manufaa kwa genge
flani tu.”
Nihitimishe
makala hii kwa kukuhamasisha msomaji kujipatia nakala yako ya kitabu changu kipya
cha kielektroniki kinachochambua kwa kina miaka miwili ya utawala wa Magufuli.
Baadhi
ya niliyaoyazungumzia kwenye makala hii yamezungumwa kwa kirefu katika kitabu
hicho ambacho hakielemei upande wowote. Kitabu hicho kwa sasa kinasubiri
uzinduzi rasmi utakaokiwezesha kununulika kwa “mobile money” kama m-pesa,
tigopesa,nk. Nitawataarifu. Ila kwa wasiohitaji kusubiri, waweza kukinunua HAPA