15 Oct 2008

Maaskofu: Mafisadi wataiangusha CCM
 
2008-10-15 10:43:17 
Na Simon Mhina

Viongozi wa dini nchini wamesema tofauti na wakati wa utawala wa Mwalimu Julius Nyerere ambapo mafisadi walikuwa wanawaogopa viongozi, sasa imekuwa kinyume chake kwani viongozi ndio wanawaogopa. 

Kadhalika, viongozi hao walionya kama mafisadi wataendelea kuwa marafiki wa watawala, ni wazi kuwa wananchi watakiondoa Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani katika chaguzi zijazo. 

Wakizungumza na Nipashe kwa nyakati tofauti kwa lengo la kutoa maoni ya hali ya kisiasa, uchumi na vita dhidi ya rushwa tangu Nyerere afariki dunia miaka tisa iliyopita, viongozi hao walisema kama angekuwepo mafisadi wote nchini wangekuwa rumande. 

Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Alex Malasusa alisema jinsi viongozi wanavyoasi taratibu miiko ya uongozi ya Mwalimu Nyerere, ndivyo CCM inavyozidi kumomonyoka taratibu, lakini kwa kasi ya ajabu mithili ya barafu lililoanikwa juani. 

Alisema Nyerere alikuwa jasiri kukemea maovu, wizi, rushwa na ufisadi, lakini viongozi wa sasa wanahofu kufanya hivyo. 

Alisema hatua ya CCM kukubali kukumbatia mafisadi inakifanya chama hicho kujitengenezea njia ya kujiangamiza siku za usoni. 

Alisema miiko ya uadilifu na ujasiri wa kupamba na uovu huo, aliokuwa nao Nyerere ndio ulioipa CCM umaarufu na kuaminiwa na Watanzania. 

``Kwa hiyo wakienda kinyume imani hiyo itatoweka mara moja, kwa mfano nataka niwaulize hawa wanaochanganya biashara na siasa. 

Hivi Nyerere yeye alikuwa mbumbumbu kiasi kwamba hakujua faida za kuanzisha kampuni. Hivi Nyerere alikuwa hajui utamu wa kujilimbikizia pesa ndani na nje ya nchi?`` alihoji. 

Akitoa maoni yake kuhusu maadhimisho ya kumbukumbu ya Mwalimu yaliyofanyika nchini kote jana, Askofu Mkuu Zakaria Kakobe wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, alisema kinachomtofautisha Mwalimu Nyerere na viongozi wa sasa ni matendo. 

Alisema Nyerere siku zote aliishi sawa sawa na yale aliyokuwa anayahubiri. 

``Nyerere alikuwa sawa kabisa na mwinjilisti anayehubiri injili, mhubiri yeyote lazima matendo yake yawe kielelezo. 

Huwezi kuhubiri kuacha ulevi wakati wewe mwenyewe ni mlevi. Ndio maana unakuta viongozi wetu wanakemea ufisadi kwa mtindo wa rasharasha kwa vile wengi wao wana sehemu katika huo ufisadi,`` alisema. 

Askofu Kakobe alisema hivi sasa ni wazi kwamba tangu Mwalimu afariki, ni vigumu kukemea ufisadi ukiwa ndani ya CCM. 

Alisema njia pekee ya kuifanya CCM iendelee kuwepo sio dola wala propaganda, bali ni viongozi wake kuishi sawa na maisha ya Nyerere, vinginevyo chama hicho kitabomolewa na wananchi. 

``Ndio maana hadi leo Nyerere anaheshimika na thamani yake inaongezeka kila mwaka, ni kwa sababu aliishi sawa sawa na yale anayosema, alipambana na aina zozote za dhuluma na rushwa,`` alisema Kakobe. 

Alipoulizwa mafisadi wataiangusha CCM kwa mtindo upi, Askofu huyo alisema hatua ya CCM kukubali pesa iwe kigezo cha mtu kukubaliwa awe kiongozi, ni njia rahisi watakayoitumia mafisadi kuidondosha. 

``Enzi za Mwalimu pesa hazikuwa kigezo cha kupata uongozi, hivi sasa pesa ndicho kigezo,`` alisema na kuongeza: ``Kwa vile mafisadi wanajua pesa ndicho kigezo cha kupata uongozi, wameshaanza kuchangishana kwa ajili ya 2010. Kibaya zaidi pesa hizo ni hizi hizi walizopora toka kwa masikini.`` 

Alisema kinachoshangaza viongozi wanamuenzi Mwalimu kwa mambo madogo madogo kwa njia za kinafiki, lakini mambo ya msingi wanayaacha. 

Naye Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Methodius Kilaini, alisema hatua ya viongozi kuogopa kuwakamata mafisadi na kuwafungulia mashitaka kwa kigezo kwamba wakishinda kesi watatudai fidia, kinadhihirisha kwamba bado sheria zetu haziko imara. 

Alisema inasikitisha kuona viongozi wanahubiri kumuenzi Mwalimu, ilhali wakubwa wanaokula rushwa na mafisadi wanaachwa wanakula raha. 

``Mwalimu hakumuogopa fisadi wala mla rushwa eti kutokana na utajiri wake, kwa vile wakati huu imekuwa kinyume kwa viongozi wetu ndio maana mafisadi wanatamba,`` alisema. 

Askofu Kilaini alisema wakati rushwa ndogo ndogo zinapungua kutokana na kushughulikiwa kwa haraka na vyombo vya dola, lakini rushwa kubwa zinazowahusisha mafisadi zinazidi kukua kila kukicha, kwa vile hawaguswi. 

Kiongozi huyo alisema kama mbinu alizotumia Mwalimu kupamba na ufisadi zinaonekana zimepitwa na wakati, basi ni vema zikabuni mbinu nyingine na wala sio kukaa kimya. 

``Hivi sasa viongozi wetu hawana ujasiri wa kupamba na rushwa kama wakati wa Mwalimu asingekuwepo fisadi yeyote anayetamba mitaani,`` alisema.

CHANZO:Nipashe


WALIMU wa Mkoa wa Dar es Salaam jana walimshambulia kwa kumrushia mawe, chupa za maji, viti na meza, Rais wa Chama cha Walimu Tanzania nchini (CWT), Gratian Mukoba, kwa madai kuwa amewasaliti kwa kukubali kuahirisha mgomo wao, uliotarajiwa kuanza leo nchi nzima.

Tafrani hiyo ambayo inazidi kuliingiza taifa katika sura mpya ya migomo ya wafanyakazi nchini, ilitokea jana katika Ukumbi wa Diamond Jubilee wakati walimu hao walipokutana kwa ajili ya kufanya maandalizi ya mwisho ya mgomo wao waliodai kuwa usingekuwa na kikomo, wenye lengo la kuishinikiza serikali iwalipe malimbikizo yao, yanayofikia zaidi ya sh bilioni 16.

Kikao hicho kilianza majira ya saa nne asubuhi na kuhudhuriwa na maelfu ya walimu kutoka Mkoa wa Dar es Salaam na wawakilishi wa mikoa ya Shinyanga na Mwanza.

Mwanzoni mwa kikao hicho kilichovunjika kutokana na vurugu hizo, walimu walikuwa watulivu kwenye viti vyao, kusikiliza kauli za viongozi wao, hasa Mukoba aliyekuwa akizungumzia hatima ya mgomo huo.

Ilipofika majira ya saa 6:20 mchana, Mukoba alishika kipaza sauti na kuanza kutoa tamko la chama hicho kwa nchi nzima kwamba mgomo wao ambao ulipangwa kuanza leo, umeahirishwa.

Huku baadhi ya walimu wakianza kunyanyuka kwenye vitu vyao na kutoa kelele za miguno iliyosikika kila kona, Mukoba alisema CWT imelazimika kuahirisha mgomo huo baada ya kushauriana na Mwanasheria wao, Gabriel Mnyele, aliyewataka waahirishe ili wapate nafasi ya kukata rufaa kupinga amri ya Mahakama Kuu, Kitengo cha Kazi, iliyozuia mgomo huo usifanyike leo.

“Kwa tamko hili ninalolisoma hapa mbele yenu, mgomo unaahirishwa kwa nchi nzima, hadi mwanasheria wetu atakapotujibu baadaye kutokana na zuio la mahakama lililotolewa jana (juzi),” alisema Mukoba.

Mara baada ya kutoa kauli, huku akiendelea kusoma maazimio mengine, ghafla umati wa walimu ulisimama kutoka kwenye viti vyao na kuvamia meza kuu, huku baadhi wakiipindua na kusababisha viongozi wa CWT kumwagikiwa maji yaliyokuwa juu za meza yao.

Kama hiyo haitoshi, baadhi ya walimu walianza kurusha chupa za maji na viti kwenye meza kuu, kwa lengo la kuwapiga viongozi wao, hasa Mukoba, aliyeonekana kushambuliwa zaidi.

Tafrani hiyo ilidumu kwa takriban dakika 35 ndani ya ukumbi huo uliokuwa na kelele nyingi za kuzomea, huku maofisa usalama wakilazimika kufanya kazi ya ziada kumwokoa Mukoba na viongozi wenzake, waliotaharuki kutokana na kushambuliwa huko.

Vita ya kurusha makopo, chupa za maji na viti iliposhika kasi, Mukoba na wenzake waliamua kukimbilia kwenye moja ya kona za ukumbi huo kujisalimisha, lakini hali hiyo haikuwasaidia, kwani walizidi kushambuliwa kwa kurushiwa vitu kama vibaka.

Tukio hilo lililoonekana kama filamu, mbali ya kuwapo kwa mashambulizi ya kurusha vitu, pia baadhi ya walimu walitoa lugha chafu kuwatukana viongozi hao na kuwataka wajiuzulu mara moja kwa madai kuwa wamewasaliti.

“Leo hatuwaachii, ama zenu ama zetu, walimu tumeonewa, tumedhalilishwa na kuibiwa vya kutosha na wewe Mukoba funga mdomo wako hapo mbele, tena katisha kusoma hilo tamko lako la kilaghai…sasa leo tutakufunza adabu kwa kukucharaza bakora ili ukome tabia hii ya usaliti.

“Kama ulikuwa unajua unakuja kutusomea hilo tamko la kipuuzi, kwanini usingeenda kwenye vyombo vya habari ukautangazie umma, kuliko kutuita hapa ukumbini kuja kutueleza ujinga kama huu…sasa leo utatujua sisi ni nani,” walisikika baadhi ya walimu wakitoa kauli hiyo.

Wakati vurugu hizo zikiendelea, majira ya saa 7:20 mchana makachero wa Jeshi la Polisi wakiongozwa na Kamanda wa Mkoa wa Ilala, Faustine Shirogile, Kamanda wa Upelelezi Mkoa wa kipolisi Ilala, Mkumbo na makachero zaidi ya 20, wakiwa na gari tatu aina ya Land Rover ‘Defender’, walifika eneo hilo kwa ajili ya kuimarisha ulinzi.

Makachero hao, walifanikiwa kuwatorosha viongozi hao kupitia mlango wa nyuma, huku baadhi ya walimu, nao wakitoka nje, kuangalia mlango uliolengwa kutumika kumtoa Mukoba na wenzake.

Wakiwa wanajipanga kumtorosha Mukoba kupitia mlango wa nyuma na kutaka kumwingiza kwenye gari la Polisi badala ya ‘Shangingi’ alilokuja nalo, walimu walibaini hali hiyo na kuamua kusogea karibu na gari hilo bila kuogopa vitisho vya polisi waliokuwa wakifyatua risasi hewani, kuwatawanya.

Wakati huo walimu wengi walikuwa wameshatoka ndani ya ukumbi kwenda kujipanga kandokando mwa barabara ya kwenda Shule ya Msingi Olympio, kwa lengo la kutaka kuendeleza mashambulizi.

Bila kuogopa risasi, wengine wakiwa na mawe mkononi, walilisogelea gari hilo la Polisi lenye namba za usajili T 220 AMV, huku wakiwakebei polisi kuwa nao wana njaa kama walimu na mishahara yao ni midogo, hivyo hawapaswi kuwazuia.

Ilipofika majira ya saa 7:30, polisi walilazimika kumtoa Mukoba na baadhi ya viongozi wa CWT chini ya ulinzi kwa ajili ya kuwapandisha kwenye gari hilo, lakini walimu nao walivyoona hali hiyo, walirusha mawe na jiwe moja lilimpata Mukoba sehemu ya tumbo na kusababisha aanguke kabla ya kusimama tena na kukimbilia ndani ya ‘Defender’ ya polisi.

Baada ya kuingizwa ndani ya gari hilo, polisi walirusha risasi hewani kabla ya dereva kuliondoa kwa kasi ili kuwatawanya walimu hao ambao walikuwa wakiendelea kulirushia mawe gari hilo.

Baada ya gari hilo kuondoka, hasira za walimu hao ziliishia kwenye kuimba nyimbo za kumsifu Mwalimu Nyerere.

Moja ya nyimbo hizo ni pamoja na ule unaotumika kwenye migomo mingi ya wafanyakazi nchini, ambao wao waliongezea vionjo kwa kusema: “Kama siyo juhudi zako Nyerere; Kikwete, Maghembe, Ghasia wangetoka wapi!”

Pia waliimba wimbo unaodai kuwa CCM ni chama cha mafisadi, huku wakikisifia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kuonyesha alama ya vidole viwili juu, inayotumiwa na chama hicho kusalimiana.

“CHADEMA, CHADEMA, CHADEMA oyeee! Sasa inatulazimu tufanye mapinduzi kama waliyofanya wenzetu wa Tarime kwa kuing’oa serikali ya CCM madarakani kwani inatukandamiza wanyonge na kukumbatia mafisadi,” walisikika wakisema baadhi ya walimu hao.

Hata baada ya Mukoba kuondolewa katika sehemu hiyo na kuliacha gari lake ambalo lilitolewa upepo na walimu hao, bado walimu hao walifunga barabara kuzuia magari yote yaliyokuwa yakipita eneo hilo huku, magari ya kifahari yakipigiwa kelele kuwa ni ya kifisadi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya walimu hao walisema licha ya kuwepo kwa amri ya mahakama kuzuia mgomo huo leo, wataendesha mgomo baridi, kwa kwenda kwenye shule zao, kujiandikisha kwenye vitabu vya mahudhurio, kisha kurejea majumbani mwao.

“Viongozi wa serikali wanajifanya wajanja, sasa sisi ndio walimu, na sisi ndio tunawafundisha watoto mashuleni, tutawafundisha uongo na mzazi mwenye uwezo ni vyema akampeleka mtoto wake shule binafsi,” alisema Mwalimu Lidyia Mhina.

Ilipofika majira ya saa 8:30 mchana, baada ya hali kuwa shwari, walimu walikusanyika nje ya ukumbi huo na Mwalimu Maulid Ng’umbe aliwatangazia walimu hao kuwa kuanzia sasa, CWT haina viongozi.

Juzi, Jaji William Mandia, wa Mahakama Kuu Kitengo cha Kazi, aliamuru CWT kusitisha mgomo mara moja, kwa kuwa unaweza kuharibu mfumo wa elimu, hasa wanafunzi wa kidato cha nne, ambao wapo katika mitihani.

Mgomo huo ulitarajiwa kuanza leo baada ya CWT kutoa notisi ya siku 60 ambayo imemalizika jana. Walimu wote nchini wanaidai serikali zaidi ya sh bilioni 16, zikiwa na fedha za malimbikizo ya mishahara, likizo na kupandishwa madaraja.


Wanakijiji Ichonde wakimbia makazi 

BAADHI ya wanakijiji cha Ichonde wilayani Kilombero, Morogoro, wamedaiwa kukimbia makazi yao kutokana na mateso ya viongozi wa kijiji hicho .Kwa nyakati tofauti wanakijiji hao walizungumza na Tanzania Daima, wakilalamikia mateso na fedheha wanazofanyiwa na viongozi wao wanapolazimishwa kuchangia elimu.

Haji Kawogo, mkazi wa Ichonde, alisema uongozi wa kijiji hutumia mgambo wa vijiji vingine kuwakamata nyakati za usiku, kuwafunga kamba na kuwaweka kwenye moja ya madarasa ya shule ya msingi kijijini hapo.

Alisema, wanakijiji hao hulazimishwa kuchangia elimu huku viongozi hao wakishindwa kuitisha mikutano ya kijiji na kuwasomea mapato na matumizi kama inavyotakiwa.

“Viongozi wetu wanatudhalilisha hasa sisi wanaume maana usiku umelala na familia yako wanakuvamia tena kwa kuwatumia mgambo wa vijiji vingine.

“…Wanatutoa nje ya nyumba zetu usiku, wanatufunga kamba na kutulazimisha kulala sehemu moja ndani ya darasa la shule ya msingi Ichonde,” alisema Kawogo.

Naye Asha Hassan, alisema kukosekana kwa maendeleo ya Kijiji cha Ichonde, kunasababishwa na uongozi mbovu uliopo hivyo aliiomba halmashauri ya wilaya kuingilia kati, ili kunusuru ubabe wa viongozi hao.

“Kijiji cha Ichonde, tunakosa maendeleo kwa sababu ya viongozi wetu, hawatushirikishi katika bajeti ya kijiji wanachojua ni kukusanya michango, lakini hawatuelezi kiasi kilichopatikana wala matumizi yake,” alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kijiji hicho Deogratias Makinda, akana tuhuma hizo na kueleza kwamba hana taarifa za kukamatwa, kufungwa kamba wala kulazwa katika shule ya msingi.

“Mimi sina dola ya kuwakamata wanakijiji, sina taarifa za wao kuteswa ndiyo kwanza nasikia hapa,” alisema mwenyekiti huyo.

Aidha, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ichonde, Salum Sadala, alikiri kwamba wapo wanakijiji wanaokamatwa na kupelekwa katika shule hiyo kwa lengo la kuhamasisha uchangiaji wa maendeleo ya kijiji.



Serikali imeombwa kuwekeza zaidi katika taasisi mbalimbali zinazofanya tafiti za magonjwa pamoja na kuboresha vifaa vya maabara zinavyowasaidia kupata majibu ya utafiti wafanyao. 

Hayo yalisemwa jana Jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Afya ya Ifakara, Dk. Salim Abdulla wakati wa uzinduzi wa taasisi hiyo ambayo zamani ilikuwa ni kituo cha utafiti wa malaria, Ifakara, mkoani Morogoro. 

Dk. Abdulla alisema taasisi hiyo inatafiti magonjwa mbalimbali lakini inakabiliwa na changamoto ikiwamo uhaba wa fedha ambao unakwamisha baadhi ya utafiti ambao unalenga kutokomeza magonjwa kama malaria, kifua kikuu na vifo vya watoto wachanga. 

Alisema ili utafiti uweze kufanikiwa lazima usaidiwe kifedha na kuwezeshwa kuwa na vifaa vya kisasa vya maabara.Alisema taasisi hiyo hivi sasa inatarajia kufanya utafiti kwa magonjwa ya kisukari, kuongezeka uzito na presha, magonjwa aliyosema yanaonekana kuongezeka zaidi na hayapewi kipaumbele huku yakipoteza zaidi maisha ya watu. 

Mwakilishi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Leonard Mboera, alisema serikali itaendelea kuisaidia taasisi hiyo kufanya utafiti wa magonjwa mbalimbali ya binadamu na kuibua mbinu za kupunguza magonjwa na vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga.

CHANZO: Habarileo

Black police officer 'wore traditional African robe to work in protest over dress code'

Last updated at 5:11 PM on 14th October 2008

Paul Bailey

Detective Constable Paul Bailey was found guilty of wearing an African robe, arguing with a senior officer and disputing his appraisal at a tribunal

A black policeman wore a traditional African robe to work after an argument over the force's dress code.

Unhappy with wearing a necktie to work, Detective Constable Paul Bailey, 39, decided to don the traditional robe.

His bizarre protest came after a number of disputes with senior officers over his behaviour and attitude on the force.

After a disgreement over his work appraisal, the detective accused five senior officers at Greater Manchester Police (GMP) of racial discrimination.

A full investigation in his claims was launched by the neighbouring West Yorkshire Police but his complaint was later found to be unsubstantiated.

But senior officers then launched a two-year inquiry into the behaviour of the detective which ended in a tribunal last week.

Following the hearing he was found guilty of wearing the robe, arguing with a senior officer over the force policy on neck ties, disputing his appraisal in an unprofessional way and appearing to look disinterested during briefings.

The panel found the incidents represented a 'continuing course of conduct' and that over a long period of time his 'behaviour was unacceptable'. But the panel ruled he should not face any disciplinary action.   

Mr Bailey, 39, who has been an officer for 18 years and has several commendations for his work, denied the claims.

Last night the Black and Asian Police Association (BAPA) said the investigation had only been launched because the detective had made an unsuccessful complaint of racial discrimination against the force.

African robe

A traditional African robe similar to the one Detective Constable Paul Bailey wore in protest against the force's dress code

Mr Crichlow from BAPA said: 'Paul Bailey has been victimised because he has made a complaint.

'He raised an issue to try to help the force and as a result they try to shoot him down in flames.

'There will have to be a health warning on GMP's equal opportunities policy. It is dead in the water and not worth the paper it is written on.

'If somebody comes to me for advice about what to do about an issue of concern I will have to tell them, you can make a complaint, but I can't guarantee you won't be victimised as a result.

'It means people will be very reluctant to raise issues of concern in the future.'

Assistant Chief Constable Terry Sweeney said: 'The individual made a complaint of racism which was independently investigated by West Yorkshire Police. 

'The force found no evidence of racism, but advised that GMP should consider taking action against the officer for breaches of the police code of conduct.

'We took further independent advice and considered the issues against force policy before deciding the most appropriate action was to proceed to a misconduct tribunal.  

'The panel found that the officer had breached misconduct rules on four occasions but decided that no sanctions should be taken against the individual. 

'Consideration was taken of the length of time between the complaints and the hearing, and the fact that the officer's performance was reported to have improved.'

Mr Bailey has taken legal advice and is taking the force to a employment tribunal on the grounds of racial discrimination.

Mr Sweeney said: 'As we are aware there is an employment tribunal pending, it would be inappropriate for us to comment further.'

Mr Bailey refused to comment.

The Met Police is mired in controversy and infighting after the country's top Asian policeman Tarique Ghaffur, was put on gardening leave and another senior ethnic minority officer, Commander Ali Dizaei, was suspended last month over misconduct allegations.

The Met Commissioner Sir Ian Blair was forced to step down after Mayor of London, Boris Johnson, said he had no confidence in him.

Source: Daily Mail



14 Oct 2008


CLICK THE GRAPH TO ENLARGE


Oscar-winning actor Kevin Spacey has given his inaugural speech as a visiting professor to students at Oxford University.

The Hollywood star delivered his 5pm lecture at St Catherine's College on Monday, a spokeswoman for the University said.

It was the first time Spacey, 48, had spoken in his role as the new Cameron Mackintosh Visiting Professor of Contemporary Theatre at the college.

The one-year post will require him to give lectures, workshops and seminars at the university.

He officially took over the role from Star Trek actor Patrick Stewart when the new academic year started this month.

Previous visiting professors have included composer Stephen Sondheim, playwright Alan Ayckbourn and lyricist Sir Tim Rice.

Spacey won acting Oscars for his roles in American Beauty and The Usual Suspects and has also appeared in hit films such as LA Confidential and Superman Returns.

He is also the artistic director of The Old Vic Theatre Company in London.

He earlier told the BBC he was looking forward to working with the students in his new role, which promotes interest in contemporary theatre.

He added: "If my mother was still alive she would be smiling because she was a great Anglophile. She loved Britain and this would make her quite pleased."

SOURCE: MSN ENTERTAINMENT



 Choo katika behewa la First Class TAZARA

Habari hii imenisikitisha sana kwa vile inanigusa binafsi.Ili nifike nyumbani Ifakara nina choices mbili ambazo zote si nyepesi.Kuna usafiri wa barabara ambao kwa hakika unahitaji moyo hasa kutokana na ubovu wa barabara kuanzia maeneo ya Ruaha/Kilombero.Kana kwamba hiyo haitoshi,wafanyabiashara wa mabasi ya abiria kwenda mikoani ni kama wameisusa barabara ya kwenda kwetu kwani takriban mabasi yote yaendayo huko ni mikweche ya daraja la kwanza.Mabasi kama Moro Best,Islam na Chimpanzee yamechoka kupita kiasi,na yanaendelea kutumika kwa vile tu  imekuwa kawaida yetu Watanzania kuvumilia mateso.Kikwazo kikubwa cha usafiri wa barabara ni msimu wa masika.Kuna eneo sugu kati ya Mang'ula na Kiberege ambapo kupita kunahitaji zaidi ya sala na trekta linalovuta mabasi yanayokwama kwenye matope.

 Kiza katika Stesheni Kuu ya TAZARA Dar es Salaam.Imagine kama stesheni kuu ni hivyo,stesheni ndogo itakuwaje!

Mkombozi wa wengi alikuwa TAZARA japo mara ya mwisho nilipotumia huduma zao (tena daraja la kwanza) nilitamani kulia:madirisha hayafungiki,taa zinawaka kwa kubembelezwa na vyoo ni kama kwenye baa za uswahilini.Ili ushuke kutoka behewani hadi kwenye platform ya stesheni ni muhimu kuwa mwanamazoezi wa short- au long-jump.Sasa ndio hata huduma hiyo ya kichovu nayo imepunguzwa ambapo kutakuwa na safari mbili tu kwa wiki,moja ya express na nyingine ya ordinary.Sishangai TAZARA kuchukua uamuzi huo kwani shirika hilo muhimu liko mahututi intensive care,hali yake ni mbaya na linasubiri kufa kifo cha kizembe siku si nyingi.

 Adha ya usafiri wa barabara kwenda kwetu Ifakara

Najua siko peke yangu ninaesononeshwa na habari hii lakini japo wanasema kilio cha wengi ni harusi ukweli unabaki kwamba Maisha Bora kwa "wana wa pakaya" yanazidi kuwa a distant pipedream.


Wanasema maisha ya jela,popote pale duniani,ni balaa.Lakini maisha ya jela katika nchi masikini kama Tanzania ni zaidi ya balaa.Hebu fikiri,iwapo baadhi ya watu wasio na hatia,na ambao wanalipa kodi kupata huduma stahili,wanateseka kupata HAKI hizo (mifano hai ni kwenye huduma muhimu kama afya,maji,barabara,nk) unatarajia nini kitokee kwa WAHALIFU!Yaani kwa mfano mfupi,kama ndugu wa wanandoa wanawekewa vikwazo kuingia kwenye harusi,what would you expect kwa wazamiaji?

Kuna mantiki zilizojengeka katika jamii kuhusiana na hali flani.Ugonjwa wa ukimwi,mathalan,unahusishwa moja kwa moja na ngono,japo kuna njia nyingine za maambukizi.Kuwa mfungwa nako kunahusishwa moja kwa moja na uhalifu,japo inafahamika wazi kwamba katika baadhi ya sehemu ambapo kuna sheria kwa wenye uwezo na nyingine kwa wasio na uwezo,mtu anaweza kujikuta jela akiwa hana kosa lolote:kasingiziwa kesi,kashindwa kumpata mwanasheria mzuri,nk.Kwahiyo wakati tunahitimisha kwamba wafungwa wote ni wahalifu ni muhimu pia kukumbuka kwamba baadhi yao wapo huko kutokana na haki zao kufinyangwa.Lakini hata kama wote ni wahalifu,hiyo haiondoi umuhimu wa kuwapatia baadhi ya haki za msingi as long as haziwafanyi watamani kuishi jela milele.

Kampuni ya Global Publishers leo imeandaa tamasha la kihistoria huko nyumbani ambapo mwanamuziki mahiri (ambaye kwa sasa anatumikia kifungo cha maisha) Nguza Viking,maarufu kama Babu Seya,na wanae watatumbuiza wafungwa wenzao katika shughuli hiyo itakayofanyika kwenye gereza la Ukonga.Hili ni tukio la kihistoria na Global Publishers wanastahili pongezi nyingi kwa kuja na wazo kama hili.Wakati umefika sasa kuonyesha kwa vitendo kwamba wafungwa ni sehemu ya jamii,hasa ikizingatiwa kwamba status yao ya ufungwa,kwa namna moja au nyingine,ni matokeo ya interaction zao na wanajamii wenzao.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.