1 Nov 2008


By Dee Dee Myers

Despite George W. Bush's improbable path to the presidency—he was, after all, elected not by the people but by the Supreme Court—neither he nor his chief strategist, Karl Rove, felt compelled to moderate their agendas. In fact, Rove went public with his grand ambition early and often: to use Bush's presidency to build a permanent Republican majority, not just in Washington but across the country. Give Rove credit for always thinking big.

Eight years later, however, the verdict is in. And Rove's plan has been a spectacular failure.

George W. Bush is the most unpopular president in modern times. Barely two in ten voters approve of the job he's done, and the other eight wonder how anyone could still find things about his administration to like. In better days, Bush was in high demand, as candidates across the country sought his endorsement, his energetic presence at their events, and his prodigious ability to raise money. How times have changed. According to NBC News, Bush hasn't made a single public campaign appearance with a G.O.P. candidate this cycle. Not one.

When Bush was elected, Republicans controlled both the House and the Senate. And after the events of September 11, their majorities grew. But as voters soured on the war in Iraq, the administration's endless ethical entanglements, and its abominable response to Hurricane Katrina, they gave Democrats back control of both chambers. And this year, Democrats are poised to make even bigger gains: somewhere north of 20 seats in the House and enough seats in the Senate to put them tantalizingly close to a filibuster-proof majority.

And what about the electorate more broadly? To begin with, Republican registration has fallen, and Democratic registration has grown, particularly among new voters, the ones forming impressions of the political parties that can last a lifetime. First-time voters, who are mostly between 18 and 21 years old—as well as those who haven't voted in recent years—prefer Barack Obama to John McCain by huge margins: 69 to 27 percent, according to one recent poll. These same voters prefer a Democratic controlled Congress by 66 to 31 percent.

So even if Barack Obama doesn't win—an unlikely outcome given the dynamics of this race—the Republican party will be in shreds: divided, demoralized, and long, long way from Karl Rove's erstwhile dream of a permanent governing majority.

SOURCE: Vanity Fair


Wananchi wahoji Rais ametumia sheria gani kusamehe wahalifu?
Na Daniel Mjema,Dodoma
BAADHI ya watu nchini wakiwamo, wanasiasa na wabunge wa Bunge la Jamhuri wamepokea kwa hisia tofauti hotuba ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu suala la mafisadi wa fedha zaAkaunti ya Madeni ya nje katika Benki Kuu ya Tanzania ( EPA), huku baadhi wakisema hotuba hiyo imejaa porojo na kuongeza utata zaidi ambao umewakatisha tamaa Watanzania.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge waliunga mkono uamuzi huo wa Rais kuwasamehe wale waliorejesha fedha za EPA ingawa pia wapo wengine waliokataa kutoa maoni yao wakisema bado wanatafakari hotuba hiyo.

Mbunge wa Karatu, Dk Wilbroad Slaa(Chadema) ambaye pia ni Naibu Msemaji wa Kambi ya Upinzani bungeni, aliliambia Mwananchi Jumapili jana kuwa hotuba yake imethibitisha hana muda wa kusoma alama za nyakati na kwamba hata wasaidizi wake hawamsaidii.

Dk Slaa alisema matarajio ya watanzania walio wengi ni kwamba Rais angetaja majina ya watu au makampuni yaliyorejesha Sh69 Bilioni na kutoa ufafanuzi ya fedha zilizorejeshwa ni fedha taslimu au zinajumuisha nyumba na magari ya watuhumiwa ambao serikali ilitangaza kuyataifisha.

“Rais amefanya kosa lile lile alilolifanya alipohutubia Bunge kwa sababu tunataka kufahamu ni akina nani hawa waliorudisha fedha hiyo ni moja lakini pili hizi Bilioni 69 zilizorudishwa ni fedha taslimu au zinajumuisha mali wanazodai wamezitaifisha,”alihoji Dk.Slaa.

Dk Slaa aliongeza kusema; "Angetuambia hizo nyumba na magari ziko wapi na zina thamani gani kwa kweli Rais amezidisha utata zaidi kuliko kutoa majibu…binafsi naiona hotuba ya jana kama porojo za alinacha”.

Mbunge huyo alimtaka Rais Kikwete amwambie ni kifungu gani cha sheria kinachomruhusu kumsamehe mtuhumiwa wa kosa la jinai ambaye hajahukumiwa na mahakama akisema kinachoonekana Rais ana safiri zaidi nje ya nchi na wala hana washauri wazuri wa kumsaidia.

Alisema kama Rais angekuwa na wasaidizi makini asingeiongezea muda kamati ya mwanasheria mkuu wa Serikali Johnson Mwanyika kuendelea kutafuna fedha za walipa kodi kuchunguza makampuni tisa kwa kuwa makampuni hayo yalishatangaza hakuna mtu wanayemdai Tanzania.

Hata hivyo Mbunge wa Nungwi, Ame Pandu Ame (CCM) alikataa kusema lolote kwa sasa akisema hilo ni jambo zito linalohitaji tafakuri ya hali ya juu huku Mbunge wa Same Mashariki,Anna Kilango Malecela(CCM) naye akisema kwa sasa bado anaitafakari hotuba hiyo ya Rais.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini,Zitto Kabwe(CHADEMA),alisema kitendo cha Rais kuwasamehe watuhumiwa wa EPA waliorejesha fedha kimewagawa watanzania kwamba watuhumiwa wakubwa wanatakiwa kurudisha walichokiiba bali wanyonge ndio wanatakiwa kufungwa.

“Watanzania wanachotaka ni kwamba warudishe wasirudishe fedha lazima washitakiwe lakini hiki alichokifanya Rais ni kibaya sana kwamba wezi wakubwa wanatakiwa kurudisha fedha lakini hawa wadogo wanafungwa magerezani…hii ni mbaya sana”alisema Kabwe.

Kabwe alisema msamaha wa Rais una taratibu zake na huwa unamhusu mtu ambaye tayari amehukumiwa na mahakama lakini alichokifanya Rais si sahihi na kusema angalau basi kamati ya Bunge ya mambo ya sheria ingearifiwa ili ijadili na kuridhia kuwasamehe watuhumiwa hao.

“Tusubiri DPP atasema nini lakini tangu mwanzo tulimshauri Rais kwamba wale wa Bilioni 90 wafikishwe mahakamani na wale wa Bilioni 42 uchunguzi wao uendelee na jana(juzi) kwa mara ya kwanza Rais ametofautisha makundi hayo mawili”alisema Kabwe.

Baadhi ya wabunge ambao hawakupenda majina yao yatajwe walipinga hatua ya Rais kuwasamehe waliorejesha fedha hizo wakisema uamuzi huo unakwenda kinyume na misingi ya utawala wa sheria ambao unatambua kuwepo kwa Mahakama katika kushughulikia wahalifu.

"Hata kama wamerejesha fedha hawa ni wezi wamegushi nyaraka wanasamehewaje? kama ni hivyo tuwaachie pia watoto wetu, ndugu zetu na wajomba zetu wanaoozea magerezani kwa kuiba kuku ni jambo la ajabu na limeleta sura mbaya sana kwa jamii,'' alidai Mbunge mmoja.

Mbunge mwingine wa viti maalumu kutoka CCM alisema alitegemea Rais angezingatia maneno ya Spika wa Bunge,Samwel Sitta aliyemtaka Rais kutowaonea huruma watuhumiwa wa EPA kwa kisingizio cha haki za Binadamu kwa sababu hicho ndicho wananchi wanachokitaka.

''Kama utakumbuka alipokuja hapa Bungeni Spika alimweleza waziwazi suala hili na maneno ya Spika ndio ambayo yaliwapa faraja sana wananchi kuliko yale ya Rais ambaye alionekana kama anaogopa kitu fulani kuhusu hawa mafisadi,” alidai Mbunge huyo.

Mbunge wa Mkwajuni, Mzee Ngwali Zubeir(CCM) alisema binafsi haoni tatizo kwa Rais kuwasamehe watuhumiwa hao kwani walipewa muda wa kujirekebisha na kufanya hivyo lakini akasema anaunga mkono kufikishwa mahakamani kwa wale ambao hawajarejesha fedha hizo.

“Nafahamu wapo wananchi ambao hawajafurahishwa na uamuzi huu wa Rais lakini wapo pia wanaona ni uamuzi wa busara nafikiri ni sahihi kuwasamehe wale waliorejesha kwa sababu walipewa muda wa kujisahihisha na wakafanya hivyo”alisema Mbunge huyo.

Masanja James mmoja kati ya wanafunzi wa chuo kikiu cha SAUT Mwanza amesema kuwa katika hotuba ya Rais amejitahidi katika kuzungumzia matatizo mengine kama yale ya mauji ya Albino, na OIC.

Alisema kuwa kulingana na utata wa sula la OIC hoja ni kuanzisha mjadala kama ambavyo rais ameeleza lakini kueleza masikitiko yake kuhusiana na suala la EPA ambalo alisema kuwa Rais bado ameonekana kuwa hatambui anachokijibu kwa wananchi.

''Amezungumza vizuri sana haya masuala mengine, lakini katika suala la EPA hapa hakutoa maelezo ya kuridhisha, kama Rais wa nchi anaweza kueleza kuwa amekuwa akipokea taarifa vipande vipande?

Kubwa ni kwamba, bado Rais hajaeleza wezi hao watashughulikiwa vipi na serikali yake kwa wizi huo, kwa mtazamo wangu ameonesha kuidhinisha wizi kwa waliolipa kurejesha kwa vile hajatwambia hatua ambayo watachukuliwa,” alieleza James.

Alisema kwa kauli ya rais katika hotuba yake wizi wa fedha za umma umeruhusiwa kwa wale wote wataofanikiwa kuiba, isipokuwa kwa wale ambao watashindwa kurejesha wao hatua zitachukuliwa.

James alieleza kuwa hali hiyo itakuza wizi katika sekta mbalimbali serikali kwa vile inaacha somo kuwa kila anayeiba vizuri akirudisha hakuna kuchukulia hatua kama ilivyo kwa wizi wa mabilioni ya EPA.

Mwajabu Bakari alisema kuwa katika hotuba ya Rais Kikwete ameghazabishwa na kuona jinsi serikali isivyo sikiliza kilio cha wananchi kutaka walioiba na kurejesha fedha za EPA wachukuliwe hatua na kusema kuwa jambo hili litalifikisha taifa mahari pabaya.

?Naye Salim Said anaripoti kuwa Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba alisema, amesikitishwa na kusononeshwa sana na hotuba ya Rais Jakaya kwa kuamua kufanya kazi isiyomuhusu.

''Nimesononeshwa, nimesikitishwa na nimekasirishwa sana na hotuba ya Rais, kwa kuwasemehe watu waliofanya jinai kabla ya mahakama kufanya kazi yake. Rais anaweza kusamehe, lakini hadi mahakama ifanye kazi yake. Huu ni ufunjifu wa Sheria za nchi,'' alisema Prof. Lipumba.

Alifafanua kuwa, utawala wa Kikwete ni utawala mbovu uliokosa muelekeo na unaongeza ufisadi ndani ya nchi, kwa kukosa nguvu ya kuwashughulikia mafisadi wa EPA.

''Hatuna utawala kabisa, tumekosa uongozi nchini. Hizi fedha zilituimika katika kumuingiza madarakani na ndio mana leo anakosa nguvu ya kuwashughulikia wezi hao,'' alilalamika Profesa Lipumba.

Profesa Lipumba aliwataka Watanzania kujipanga na kujiandaa kwa ajili ya kuing’oa serikali ya CCM madarakani, katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kabla nchi haijayoyoma.

Naye Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislaam Tanzania, sheikh Ramadhan Sanze alisema, ni mfano mbaya sana kwa mamlaka ya kirais nchini kufagilia sheria kutumikia siasa jambo ambalo ni hatari kwa mamlaka nyengine za chini.

Alisema, inaonekana kuna siri nzito katika suala la wizi wa fedha za EPA kwa kuwa kuchukua fedha kinyume na taratibu ni kosa la jinai lakini rais amelichukulia kama la madai.

''Tatizo si kurudisha fedha, hapa tunataka kukomesha huu mchezo mchafu, kwa sababu kuchukua fedha visivyo ni kosa la jinai. Kwa mpango huu wa rais Kikwete kufagilia Sheria kutumikia siasa, basi watu wataendelea kukwepa sheria kwa mlango wa siasa kila siku,'' alitahadhariasha Sheikh Sanze.

Sheikh Sanze alifafanua kwamba, pamoja na juhudi kubwa anazofanya rais Kikwete katika suala la EPA, bado maslahi ya kisheria na utawala bora yamekiukwa.

''Jambo hili litawafanya Watanzania waanze kuhoji ni jinsi gani nguvu na mamlaka ya rais yananavyoshindwa kufanya kazi ya kuwashughulikia mafisadi. Jambo ambalo linatutia wasiwasi mkubwa juu ya mamlaka na nguvu hiyo,'' alisema Sheikh Sanze.

CHANZO: Mwananchi


This dude is angy because T.I. is calling for people to give tips to Crimestoppers.They call it snitching.So,for this fool,he would rather see his brothers and sistas die rather than help the police to make the street safer!Barack Obama could well win come November 4,but I doubt if his victory as the first Black President of US could help change this crazy mentality horbered by majority of these gangtaz.

31 Oct 2008


HOTUBA YA MWISHO WA MWEZI YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI TAREHE 31 OKTOBA, 2008

Ndugu Wananchi;

Tuanze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia rehema zake tunapata fursa ya kuzungumza mwisho wa mwezi huu Oktoba kwa mujibu wa utaratibu wetu mzuri. Mwisho wa mwezi uliopita sikuweza kuzungumza nanyi kwa sababu ya kuwa New York, Marekani kwa shughuli za kila mwaka za Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Kwanza suala la OIC,
Pili Uchumi wa Dunia,
Tatu mauaji ya wenzetu Albino, 
Nne Madai ya Walimu
Na tano suala la Mfuko wa Madeni ya Nje yaani EPA.

Suala la OIC

Ndugu Wananchi;

Hivi karibuni kumekuwepo na mjadala usiofurahisha kuhusu suala la Jumuiya ya Kiislamu (OIC) kufuatia taarifa iliyotolewa Bungeni na kwenye vyombo vya habari na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Bernard Membe. 

Nasema isiyofurahisha kwa sababu mjadala huo unaelekea kuchukua sura ya malumbano baina ya waumini wa dini zetu kuu na kupandikiza chuki baina ya serikali na wafuasi wa dini hizo. Ni mjadala unaosikitisha sana jambo ambalo napenda kuwasihi Watanzania wenzangu tusiuendeleze na wala tusiuendekeze. Unaweza kulipeleka taifa
letu mahali pabaya.

Napenda kukumbusha kuwa mwaka 1993 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilitakiwa kujiondoa kutoka kwenye jumuiya ya OIC baada ya kujiunga kwa hoja kwamba hilo ni shirika la kimataifa ambalo wanachama wake ni mataifa, hivyo kwa hapa nchini kama kungekuwepo na kujiunga iliyostahili kufanya hivyo ni Serikali ya Muungano. Hayo ndiyo matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo basi Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar ilijiondoa kwenye OIC na kuiachia Serikali ya Muungano kushughulikia jambo hilo na kuamua ipasavyo. 

Tangu wakati huo Zanzibar wamekuwa wanasubiri uamuzi wa Serikali ya Muungano. Kila wakati wenzetu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wamekuwa wanaliuzia suala hilo. Hivi sasa jambo hilo limekuwa mojawapo ya kero kubwa za Muungano zinazoshughulikiwa na Kamati ya pamoja ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi. Kwa mujibu wa muundo wa Serikali ya Muungano kila kero ya Muungano ina Wizara yake inayohusika nayo
kushughulikia. Kwa suala hili ni Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ndiyo inahusika. Wizara imeamua kufanya utafiti wa jambo lenyewe na wakishakamilisha utafiti huo watoe ushauri kwa Serikali zetu mbili kwa uamuzi. 

Ndugu Wananchi;

Nijuavyo mimi, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa haijakamilisha kazi yake ya utafiti na hivyo haijawasilisha Serikalini matokeo ya utafiti wao pamoja na mapendekezo yao kwa ajili ya kutafakariwa na kuamuliwa ipasavyo. Kwa sababu hiyo basi Serikali haijafanya uamuzi wowote kuhusu suala la OIC kwa vile hatujapokea mapendekezo yoyote kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa. Wizara haijamaliza kazi yake. Katika hali hii, nawaomba Watanzania wenzangu tuwe na subira. Tuwaache Wizira ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wafanya kazi yao kwa utulivu ili waishauri Serikali kwa hekima na busara.


Aidha, napenda kuwaomba pia hapo Wizira itakapokamilisha kazi yake (sijui lini) na kuyafikisha mapendekezo yake Serikalini, tuiache Serikali yetu nayo itafakari kwa utulivu ili ifanye uamuzi ya hekima utakaojenga na kulihakikishia taifa letu umoja, amani, utulivu na upendo miongoni mwa raia wa nchi yetu.

Ndugu zangu;

Napenda kuwahakikishia Watanzania wenzangu kuwa siku zote mimi na wenzangu wote Serikalini tunatambua unyeti wa suala la OIC. Aidha, tunatambua dhamana yetu ya kuwa makini katika kufikia uamuzi na kwa uamuzi wenyewe tutakaoufanya kuhusu suala hili. Kamwe hatutafanya uamuzi ambao utavuruga mambo na kuhatarisha amani, umoja na
mshikamano wa nchi yetu, Serikali zetu na watu wake.

Hivyo narudia kuwasihi Watanzania wenzangu tuiache Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ilifanyie kazi kwa ukamilifu suala hili. Tujiepushe na vitendo au kauli ambazo zitawatia watu hofu na kujenga chuki miongoni mwa raia wa nchi yetu wanaopendana na kujenga chuki na kutoaminiana baina ya raia na Serikali yao inayowapenda na kuwathamini.

Madai ya Malimbikizo ya Walimu

Ndugu Watanzania wenzangu;

Jambo la pili ninalotaka kulizungumzia leo, linahusu madai ya malipo ya walimu kuhusu malimbikizo ya mishahara, nauli za likizo na posho za uhamisho na kujikimu. Kama sote tujuavyo Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kiliiarifu Serikali nia yake ya kuitisha mgomo wa walimu wote nchini iwapo madai ya walimu yapatayo shilingi bilioni 16.4 (bilioni 12.2 kwa ajili ya walimu wa shule za msingi na bilioni 4.2
kwa walimu wa shule za sekondari na vyuo vya walimu) yatakuwa hayajalipwa yote ifikapo tarehe 15 Oktoba, 2008. 

Baaada ya kupata taarifa hiyo Serikali iliwasiliana na uongozi wa juu wa CWT kwa nia ya kufanya mazungumzo nao kuhusu madai yao. Bahati nzuri uongozi wa CWT ulikubali, hivyo mazungumzo yakafanyika baina ya Serikali na CWT. Upande wa Serikali uliwakilishwa na wajumbe 12 kutoka Wizara za Utumishi, Fedha na Mipango, TAMISEMI na Elimu na Mafunzo ya Ufundi na upande wa CWT uliwakilishwa na wajumbe saba (7).

Kiongozi kwa upande wa Serikali alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mheshimiwa Hawa Ghasia na upande wa CWT kiongozi alikuwa Ndugu Yahaya Msulwa ambaye ndiye Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu, Tanzania. 

Katika mazungumzo hayo ukiacha suala la madai ya malipo yalikuwepo pia masuala mengine matano yafuatayo:

1. Kupandishwa madaraja (vyeo).

2 CWT kushirikishwa katika uhakiki wa madai ya walimu.

3. Kuundwa kwa Baraza la Majadiliano ya Pamoja katika Sekta ya Elimu (Teachers Joint
Staff Council).

4. Kuandaliwa kwa Taratibu za Uendeshaji wa Utumishi wa Walimu (Teachers Service
Scheme) na

5. Kuwarudisha kwenye Orodha ya Malipo (Payroll) walimu waliofutwa kwenye orodha hiyo.

Baada ya siku 15 za mazungumzo muafaka ukafikiwa juu ya masuala yote sita na makubaliano hayo ya pamoja kutiwa saini na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe kwa niaba ya Serikali na Katibu Mkuu wa CWT,Ndugu Yahaya Msulwa kwa niaba ya Walimu. 

Jambo lililotushanga na kutusikitisha sote ni kauli ya Rais wa CWT, Ndugu Gratian Mkoba tarehe 08 Oktoba, 2008 kwamba mgomo unaendelea. Tena akasisitiza kuwa mgomo huo hauna muda maalum mpaka mwalimu wa mwisho atakapokuwa amelipwa. Nilimuagiza Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuwa, wawatafute viongozi wa CWT kuzungumza nao kuwasihi waache kuendelea na mgomo, lakini juhudi zote hazikuzaa matunda. 
Waling’ang’ania kuendelea na mgomo na ndipo tukaitumia haki yetu kwa mujibu wa Sheria ya Kazi Na. 6 ya mwaka 2004 kuomba Mahakama kuu kitengo cha Kazi iamuru mgomo usiwepo na kuwataka viongozi wa CWT warudi kwenye mazungumzo na Serikali. 

Viongozi wa CWT wanapinga uamuzi huo wa Mahakama Kuu na kutaka waendelee na mgomo. Tupo mahakamani tunasubiri uamuzi wa Mahakama kuhusu rufaa ya CWT.

Ndugu wananchi;

Najua wapo walioushangaa uamuzi wa Serikali wa kwenda mahakamani na wapo pia watu waliotukejeli kwa uamuzi wetu huo. Kwanza kabisa ni haki ya mwajiri kufanya hivyo na mahakama ndicho chombo chenye mamlaka ya kuamua. Lakini, pia, tumefanya hivyo kwa nia njema ya kunusuru janga ambalo mfumo wa elimu ungelikuta nchini kwa mgomo huo ambao ungekuwa wa aina yake. Maana kuendelea kuwepo mpaka mdai wa mwisho atakapolipwa wakati inawezekana baadhi ya wadai wanaweza kuwa na vithibitisho ambavyo vinaweza kukataliwa na mlipaji kwa kutokuwa halali ni sawa na kuwa na mgomo wa kuchukua muda mrefu sana. Unaweza usiwe na ukomo kwani ubishi kuhusu uhalali wa stakabadhi ya mdai unaweza kuchukua muda mrefu. Vinginevyo ichukuliwe kuwa, kila anachodai mwalimu ni sahihi kilipwe na Serikali. Hilo nalo ni gumu kwani upo ushahidi wa kuwepo kwa stakabadhi za kughushi. 

Ndiyo maana sisi katika Serikali tumeyaafiki makubaliano ya kufanya uhakiki wa pamoja utakaoshirikisha CWT na Serikali. Nilipokuwa Tabora hivi karibuni nilielekeza kuwa uhakiki huo ufanywe shule kwa shule na mwalimu kwa mwalimu; usifanywe kwa kukagua mafaili tu katika maofisi ya Maafisa Elimu na Utumishi. Kufanya hivyo kutatupa taarifa iliyo sahihi ya nani anadai nini. Itasaidia kung’oa mzizi wa fitina. Hakutakuwepo na kudaiana kusikokwisha. 

Vilevile, itatusaidia kujua uweli wa walimu waliopo na wako wapi. Kuna minong’ono ya kuwepo walimu hewa ambao pesa zao hutolewa kila mwezi. Pia, wapo walimu waliotangulia mbele ya haki ambao bado wamo kwenye orodha ya utumishi na mishahara yao huendelea kutumwa na hairejeshwi. 

Ndugu Wananchi;

Napenda kuitumia nafasi hii kuwahakikishia walimu na wananchi wote wa Tanzania, kuwa Serikali inawathamini na kuwajali walimu. Serikali ya Awamu ya Nne inaweka kipaumbele cha juu sana kwa maendeleo ya elimu, ndiyo maana bajeti ya elimu ndiyo bajeti kubwa kuliko zote. Inachukua asilimia 19.8 ya bajeti yote ya Serikali. 

Watanzania wote ni mashahidi wa nguvu kubwa tuliyoielekeza katika elimu ya sekondari, elimu ya juu na elimu ya ufundi. Mimi na viongozi wenzangu kuendeleza elimu ni agenda yetu kuu. 

Katika juhudi hizo tunatambua nafasi na umuhimu wa Mwalimu. Hatuwezi kua watu tunaohimiza upanuzi wa elimu lakini tunampuuza mwalimu. La hasha! Mara nilipoingia madarakani, katika mkakati wa kuboresha maslahi ya watumishi, kundi tuliloanza nalo ni walimu na tumeendelea kulipa kipaumbele kila tuliposhughulikia makundi mengine. 

Katika mkakati wa kuboresha maslahi ya watumishi wa umma tulitambua kuwa hatutaweza kufanya hivyo kwa watumishi wote kwa wakati mmoja. Tukaona tukienda kwa makundi tunaweza. Kundi la kwanza tuliloanza nalo ni walimu. Natambua haja ya kuendelea kuboresha maslahi ya watumishi wa umma nchini, ni nia yetu kufanya hivyo. Tumekuwa tunafanya hivyo katika miaka mitatu hii na tutaendelea kufanya hivyo miaka ijayo. 
Pamoja na hayo, mwezi April, 2008, tumewalipa Walimu Shs. 7.2 bilioni, sehemu kubwa ikiwa ni madeni ya nyuma kabla sisi hatujaingia madarakani. Huu ni ushaidi kwamba tunawajali walimu. Mimi nitakuwa mtu wa mwisho kupuuza maslahi ya walimu.


Uchumi wa dunia

Ndugu Wananchi;

Katika hotuba yangu ya Tanga wakati wa sherehe za kuzima Mwenge na maadhimisho ya miaka 9 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere, nilizungumzia hali ya uchumi wa dunia na hasa wa mfumo wa fedha unaozikabili nchi zilizoendelea. 

Nilielezea hofu yangu kuhusu athari ambazo zinaweza kutokea kwa nchi yetu ikiwa uchumi wa dunia utaendelea kuyumba kufuatia misukosuko ya kifedha ya kimataifa. Nilisema kuwa Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani huenda nayo ikakumbwa na madhara yatokanayo na kuyumba huku kwa uchumi wa dunia.

Nilieleza kuwa nchi yetu inaweza kuathirika kwa njia zifuatazo:
1. Kupungua kwa mauzo yetu ya nje kwenye masoko ya nchi za Magharibi kwa sababu ya kupungua kwa uwezo wa watu na nchi hizo kununua bidhaa na huduma. Mazao yetu ya biashara tunayouza nje yanaweza kuathirika kwa ajili hiyo; 

2. Kuna uwezekano wa kupungua kwa mapato yanayotokana na utalii, kutokana na kupungua kwa watalii kutoka mataifa hayo kwa sababu watu wa nchi hizo kuathiriwa na mgogoro wa kifedha unaozikumba nchi zao. Wapo watu wengi ustawi wao wa kifedha na kiuchumi umeshuka kwa sababu ya kuanguka kwa masoko ya hisa na mabenki na kufilisika
kwa makampuni. 

3. Kuna wasiwasi kwamba uwezo wa nchi za Magharibi kutoa misaada kwa nchi yetu utapungua, kutokana na fedha nyingi kutumika katika kuokoa vyombo vya fedha katika nchi zao. Nilitoa mfano kuwa, katika wiki chache zilizopita, nchi za Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Ubelgiji, Iceland na Sweden, zimetangaza kutoa jumla
ya dola za kimarekani trilioni 1.8 kusaidia kuyaokoa baadhi ya mabenki yaliyopata
msukosuko. 

4. Msukosuko huu unaweza kusababisha kupungua kwa mikopo ya kibiashara au kuongezeka kwa gharama za mikopo kutoka nje, na hivyo kupungua kwa uwezo wa mabenki yetu kukopesha.
5. Vilevile kuna wasiwasi wa uwezekano wa kupungua kwa uwekezaji kutoka nje. Huenda uwekezaji hapa nchini kutoka Afrika ya Kusini na Kenya ukapungua kwa kuzingatia kuwa
nchi hizo zina mahusiano zaidi na mtandao wa masoko ya fedha ya kimataifa.

6. Pamoja na hofu ya kupungua kwa uwekezaji kutoka nje, kuna uwezekano mkubwa wa kupungua kwa kiwango na kasi ya uwekezaji wa ndani kutokana na kupungua kwa uwezo wa taasisi zetu za fedha kukopesha. Wakati mwingine ni hofu ya hayo yanayotokea
duniani.

7. Na mwisho msukosuko huu unaweza kusababisha kupungua kwa fedha zinazotumwa na Watanzania walioko nje ya nchi yetu.

Ndugu Wananchi;

Tangu nilipozungumzia suala hili kule Tanga, bado hakujawa na unafuu wowote katika uchumi wa dunia licha ya jitihada kubwa zinazofanywa na mataifa makubwa kurekebisha hali hiyo. Uchumi wa nchi tajiri duniani umeendelea kuyumba kwa maana ya kupungua na kudorora. Hali hiyo imeanza kuleta athari katika biashara ya kimataifa. Mahitaji ya mafuta yameanza kupungua na kusababisha kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia. Hali inaweza kuwa hivyo hivyo hata kwa bidhaa zetu tunazouza nchi za nje.
Kadhalika, tunaendelea kuyasihi mataifa makubwa kiuchumi na nchi tajiri kwa jumla zinazokabilia na matatizo haya yaendelee kuchukua hatua madhubuti na za haraka kurekebisha hali iliyojitokeza katika mfumo wa kifedha wa kimataifa. Aidha, tunasisitiza umuhimu wa kuutazama upya mfumo wa kifedha wa kimataifa unavyofanya kazi kwa nia ya kurekebisha kasoro zilizopo. Naamini kufanya hayo kutatuhakikishia
kwamba msukosuko unaoikumba dunia hivi sasa utapatiwa ufumbuzi na kwamba utaepukika na hautatokea tena siku za usoni. Madhara yake ni makubwa kwa uchumi wa nchi zetu changa na maisha ya watu wetu.

Kwa mantiki hiyo napenda kutumia fursa hii kuungana na viongozi wengine duniani katika kukaribisha wazo la Rais George Bush wa Marekani la kuitisha mkutano maalum wa kimataifa wa kuzungumzia tatizo la kifedha la kimataifa. Ni matumaini yangu kwamba, mkutano huo utatoa ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili. Bahati mbaya Afrika imesahaulika katika mkutano huo. Hii ni dunia yetu sote yanayotokea popote yanatuhusu sote.

Mauaji ya Maalbino

Ndugu zangu, Watanzania wenzangu;

Tarehe 19 Oktoba, 2008 nilipewa heshima ya kupokea maandamano ya kulaani na kupinga mauaji ya wenzetu wa jamii ya Maalbino. Katika maandamano hayo nilielezea kusikitishwa kwangu na matendo hayo ya kikatili na ya aibu kwa nchi yetu. Siku ile nilitoa wito kwa Watanzania wote kushiriki na kushirikiana katika mapambano haya
halali ili kwa umoja wetu tuweze kukomesha mauaji ya ndugu zetu hao.

Leo nataka kuwaelezea azma ya kuwataka Watanzania kote nchini kutoa taarifa kuhusu watu wanaojihusisha na mauaji ya Albino nchini. Kwa maana ya waganga, wauaji, wauzaji na wanunuzi wa viungo vya Albino. Nawataka Watanzania wawataje kwa siri watu hao ili Serikali ifuatilie kwa karibu nyendo zao, kuwabana ipasavyo na kuwachukulia hatua mwafaka. Utaratibu huu ulitusaidia sana katika mapambano dhidi ya majambazi,
naamini utatusaidia hata katika mapambano haya halali na ya haki. Baada ya muda si mrefu tutatoa maelekezo juu ya utaratibu wa kutoa na kukusanya taarifa hizo. 

Nataka kuwahakikishia wananchi kuwa Serikali yenu haitakaa kimya wakati raia wasiokuwa na hatia wanaendelea kuteswa na kuuawa. Albino ni mwanadamu kama alivyo mwanadamu mwingine yeyote. Ana haki ya kuishi na kupata hifadhi ya maisha na mali zake kutoka katika jamii. Kuwaua kwa sababu yoyote ile si haki na ni kosa kubwa. 

Isitoshe kwa sababu wanazouliwa ni aibu kwa mhusika na fedheha kubwa kwa jina zuri la nchi yetu. Kila mmoja wetu anao wajibu wa kuelimisha jamii juu ya madhara ya fikra potofu zinazoenezwa na waganga wa kienyeji wenye tamaa na uchu wa kujipatia utajiri. Utajiri utapatikana kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa na kuwa na nidhamu katika utendaji na matumizi ya mapato yako. Sote tunawajibika kuwafichua
watu hawa ambao ni hatari katika jamii yetu. Naomba ushirikiano wa kila mmoja wetu ili tuikomeshe na kuondoa aibu hii.

Fedha za EPA

Ndugu wananchi;
Jambo la mwisho ninalotaka kuzungumzia leo linahusu urejeshwaji wa fedha za akaunti ya madeni ya nje katika Benki Kuu inayojulikana kwa kifupi kama EPA. Wengi wenu mtakumbuka kuwa, nilipozungumza na Bunge tarehe 21 Agosti, mwaka huu, nilieleza kwa kirefu yaliyotokea, hatua tulizochukuwa na mahali tulipokuwa tumefikia katika kulishughulikia suala hili. Nisingependa kuwachosha kwa kurudia tena yale niliyoyasema. 

Siku ile nilieleza katika hotuba yangu kwamba niliwataka wale wote waliokuwa miongoni mwa yale makampuni 13 yaliyolipwa shilingi 90,359,078,804, waliochukua fedha ambao walikuwa bado hawajarejesha fedha hizo kufanya hivyo ifikapo tarehe 31 Oktoba, 2008. Aidha, niliagiza uchunguzi kwa zile kampuni 9 zilizolipwa shilingi
42,656,107,417 uendelee. Kamati iliomba idhini ya kuwasiliana na vyombo husika vya dola vya mataifa husika ya nje ili kupata ukweli na kukamilisha uchunguzi wao.

Ndugu wananchi;

Nilielezea pia kwamba baada ya tarehe 31 Oktoba, 2008, kwa wale ambao watakuwa hawakuteleza, hatua za kisheria zichukuliwe. Leo ndiyo siku ya mwisho. Napenda kuwajulisha kuwa, taarifa nilizoletewa majira ya mchana leo, ni kuwa kiasi cha shilingi 69,326,437,650 kati ya shilingi 90,359,078,804 zilikuwa zimerejeshwa. Hii ni sawa na asilimia 76.7. 

Kesho tarehe 01 Novemba, 2008 taarifa kamili itatolewa juu ya kiasi halisi ambacho kitakuwa kimerejeshwa. 

Pamoja na kufanya hivyo, nimekwishatoa maelekezo kamili kwa wale ambao hawakutimiza malipo, Kamati ikabidhi majalada yao kwa Mkurugenzi wa Mashtaka mara moja, kwa hatua zipasazo za kisheria. 

Mkurugenzi wa Mashtaka ni idara huru ya Serikali iliyoundwa kwa mujibu wa Katiba ya Nchi. Yeye ndiyo mwenye mamlaka ya kuendesha mashtaka mahakamani baada ya kupokea taarifa za upelelezi kutoka kwa Jeshi la Polisi na Tume ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa. 

Ndugu Watanzania wenzangu;

Kuhusu uchunguzi uliokuwa unaendelea kufanywa kuhusu yale makampuni 9, nasubiri taarifa yao mpya kuhusu maendeleo ya uchunguzi huo. Taarifa niliyopewa wiki mbili zilizopita zinaonyesha kuwa polisi wetu bado hawajapata majibu kutoka kwa wenzao katika nchi walizoomba msaada. Hivyo, nakusudia kuwataka waendelee kufuatilia kwa wenzao ili hatua zipasazo ziweze kuchukuliwa.

Ndugu wananchi;

Kwa mara nyingine tena napenda kuchukua fursa hii kuipongeza Kamati ya Mwanasheria Mkuu kwa kazi nzuri iliyofanya ambayo mbali na kubaini namna ya tuhuma za uhalifu zilivyofanywa, pia ilibaini wahusika na kuwabana kiasi cha kufanikiwa kurejeshwa kwa fedha ambazo vinginevyo zingepotea kabisa. 

Lakini kubwa zaidi, nawashukuru wananchi kwa uvumilivu na uelewa wao wakati wote serikali ilipokuwa inalishughulikia sakata hili la aina yake katika historia ya nchi yetu. Tumefarijika sana kwa uelewa na ushirikiano wenu. Nawaomba tuzidi kushirikiana katika mambo yote yanayohusu mustakabhali wa nchi yetu.

Aidha, utaratibu wa kuzigawa fedha hizo kwa ajili ya shughuli za kilimo na miundombinu zimekamilika.

Madai ya Wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Katika hotuba yangu ya leo, sikuweza kugusia suala la madai ya wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa sababu Serikali inaandaa tamko rasmi litakalowasilishwa Bungeni na Waziri wa Fedha na Mambo ya Uchumi, Mheshimiwa Mustafa Mkullo wiki ijayo. Hivyo nawaomba sote tuvute subira.


Hitimisho

Kabla ya kumaliza napenda kutumia fursa hii kuwashukuru wananchi wote kwa kuendelea kuiunga mkono serikali katika mambo yote ya msingi yanayoihusu nchi yetu. Licha ya mawimbi ya hapa na pale ambayo tunapambana nayo katika safari yetu, tumeendelea kuimarisha umoja na mshikamano wetu ambao ndio nguzo na mhimili wa taifa letu. 

Nawaomba tuendelee kufanya hivyo kwa kutambua kuwa hiyo ndiyo njia pekee ya kujenga nguvu ya pamoja ya kuendeleza taifa letu. Nawasihi tujiepushe na mambo yanayoweza kutugawa na kupandikiza mbegu za chuki miongoni mwetu na badala yake tuimarishe maelewano, mshikamano na umoja wa kitaifa. 


Mungu Ibariki Afrika;
Mungu Ibariki Tanzania.
Asanteni kwa kunisikiliza.

Picha kwa Hisani ya HAKINGOWI

Katika jamii zetu, wazee wana heshima ya pekee kama kisima cha hekima, kielelezo cha uadilifu na taa ya maisha. Wazee wana nafasi ya kipekee ya kujenga jamii; wanawakilisha kile kilicho bora; na kilichokomaa. Wazee ni dawa; lakini, wazee wanakuwa dawa ya matatizo pale tu wanapotenda mambo yanayoshabihiana na sifa za wazee.

Wazee wanapogeuka kuwa viranja wa vitendo vya aibu; wanapovaa migolole ya wavurugaji wa amani na vitendo vinavyoashiria kudharau mamlaka ya utawala wa sheria; wanapofikia ukomo wa matumizi ya busara na hekima na wanapojiingiza katika daraja la wapenda shari, wanaanza kupoteza baadhi ya sifa muhimu zinazokamilisha heshima ya mtu kuitwa mzee.

Jana asubuhi, kwa takribani saa mbili, watu waliojitambulisha kama wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) walihamia kwenye Barabara ya Ali Hassan Mwinyi, eneo la makutano ya barabara hiyo na Umoja wa Mataifa Dar es Salaam na kufanya viroja eti wakishinikiza kulipwa mafao yao.

Kitendo hicho sio tu kwamba kiliwabughudhi watumiaji wa barabara hiyo ambao walishindwa kuingia au kutoka mjini, bali kilisababisha hasara kubwa kutokana na kukwama kwa shughuli za biashara katikati ya jiji la Dar es Salaam.
Kitendo kilichofanywa na watu hao, ambamo pia vijana walikuwamo, ni cha aibu.

Watu hao, walioonekana dhahiri kuwa na jazba kutokana na kile walichodai kutolipwa fedha zao, wameshawahi kufanya vituko vya aina hii kabla ya jana. Lakini kwa kuamua kufunga barabara, huku baadhi ya wanawake wakivua nguo, walionyesha mwisho wa ustaarabu wa mwanadamu katika kudai kile anachodhani ni haki yao.

Hekima na kumbukumbu zilielekea kuwahama wazee hao, walipodai kwamba walikuwa na nia ya kwenda ubalozi wa Uingereza mjini Dar es Salaam 'kuishtaki' Serikali. Tunawashangaa watu wanaoamua kufikisha matatizo yao kwenye balozi za nchi za nje badala ya kutumia vyombo vilivyoanzishwa kushughulikia matatizo ya wananchi.

Lakini tunawashangaa zaidi wazee hao, ambao wengi wao walishuhudia kushushwa kwa bendera ya Mwingereza nchini tarehe 9 Desemba, 1961.
Kisha tunajiuliza: Tangu lini ubalozi wa nchi ya nje ukawa chombo cha rufaa kwa Watanzania?

Hivi anayeamua kulala barabarani, kuwasilisha matatizo kwenye nchi ya nje, kuvua nguo na kubakia na sidiria hadharani na kulumbana na vyombo vya kikatiba vya dola atakuwa na hekima gani ya kuweza kukemea watoto watakaokosa uelewa wa uraia na maadili mema? Je, uchuro wa kukaa uchi ndio urithi ambao wazee wanawakabidhi watoto wao?

Kwa heshima zote ambazo tunazo kwa wazee wa Tanzania na wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, tunadhani wazee waliolala barabarani jana wamepotoka. Tunakubali kwamba wazee na wastaafu wanaoidai Serikali wana haki ya kufanya hivyo. Pengine maandamano ya jana yalifanywa kwa lengo la kuitikisa serikali ambayo tayari nayo ina majibu yake.

Lakini suluhisho la tatizo hili lilishafikiwa na hapakuwa na sababu za mgogoro huu ambao umedumu kwa miaka 30, kuondoka katika ustaarabu wa majadiliano yaliyokubalika. Huu ni wakati mwafaka kukumbushana ukweli kuhusu tatizo la malipo ya baadhi ya wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Serikali kwa muda wote imekuwa ikizingatia makubaliano ya awali, yakiwamo mapendekezo ya kamati ya mwaka 1997.

Historia ndefu ya mgogoro huo pamoja na kufikishana mahakamani kudai mapunjo yaliyotokea kwa kesi namba 95 ya mwaka 2003, iliyowezesha kuwapo kwa hati ya makubaliano ya Septemba 25, 2005 iliyokaziwa hukumu na Jaji Oriyo, inatufanya tuamini kwamba ipo haja ya mambo mengi kuwekwa bayana ili kila Mtanzania na kila mhusika aelewe.

La msingi ambalo tunaliona katika makubaliano hayo ni serikali kukubali kulipa wadai hao 31,831 jumla ya shilingi bilioni 117 kwa misingi ya staili ya kila mmoja kulingana na taarifa zao. Taarifa zilizopo ni kuwa jumla ya shilingi bilioni 114.2 zimelipwa kwa wastaafu hao hadi kufikia Agosti 5 mwaka huu na utaratibu wa malipo unaendelea.

Tunaunga mkono kauli ya serikali kama ilivyosema katika taarifa yake, haiwezi kuendelea kulipa fedha bila kuhakiki. Shinikizo linaloletwa na wazee la kulipwa wote bila kufanyika uhakiki ni sawa na kupoteza dira ya uendeshaji wa hesabu za Serikali. Hili halikubaliki. Fedha za Serikali lazima zitolewe kwa uangalifu.

Nchi haiwezi kuendeshwa kwa kukiuka sheria, lakini pia serikali inayomwaga fedha bila kuhakiki ina tatizo kubwa, kwa maana haifuati sheria ila mkumbo, na hii ni hatari. Kama hati ya makubaliano ilikuwa na fomula ya malipo, inakuwaje sasa wastaafu hao wanashinikiza kulipwa mafao kwa kukokotoa mafao yao kwa fomula yao ambayo haiko mahakamani?

Tunarudia. Kitendo walichofanya wastaafu hao ambao tunawaheshimu kutokana na umri wao ni uchuro usiokubalika, kwani wametumia mbinu za kihuni zinazotofautiana sana na umri wao. Matendo ya wazee yanaangaliwa na wengi, lakini kwa maandamano ya jana na vitendo vyao pale, kunabaki swali nani atawakemea watoto wa Tanzania watakapokuwa wanafanya vitendo kama vya wazee wao?

Je, nani atafidia hasara iliyopatikana kutokana na muda ambao watu walizuiwa kufanya shughuli zao za kiuchumi? Katika fikira za kawaida kama nia ilikuwa kuzuia viongozi ambao ndio watumiaji maarufu wa barabara hiyo wasipite, kwa nini wazee hao wasiwafuate wahusika ofisini kwao ili wengine waendelee na shughuli zao?

Bado tunaamini kuwa mahakama zetu hazijapoteza dira, hivyo ni vyema kwanza wastaafu hao wangeendelea kudai haki zao huko kama walivyofanya kufikia mwafaka wa malipo wa sasa. Haitakuwa ajabu kama kitendo cha wazee kitatekwa na ushabiki wa kisiasa. Wanasiasa wachovu watadandia hoja ya maandamano ya jana ya wazee.

Lakini huu sio wakati wa ushabiki, bali bi wakati wa kusimamia misingi ya maadili na utamaduni wa taifa. Hakuna ushabiki wowote utakaohalalisha vitendo vya wazee ambavyo ndani yake kuna mbegu za kujidhalilisha. Tunawapenda, tunawaheshimu na kuwaenzi wazee wetu. Ndio maana tunasononeka tunapowashuhudia wakifanya mambo ambayo yanamomonyoa maadili ya kitaifa na utamaduni wa Mtanzania.

NASHAWISHIKA KUAMINI KUWA MZAZI WA MWANDISHI WA TAHARIRI HII SI MIONGONI MWA WAZEE HAO WANAODAI HAKI ZAO.KUWAAMBIA BABU NA BABA ZETU "WAACHE UTOTO" SIO LUGHA YA BUSARA.KWA BAHATI NZURI,MWANDISHI WA TAHARIRI HIYO,KAMA ILIVYO KWA WATUMISHI WA EX-EAC, NAE KUNA SIKU ATASTAAFU,NA KWA VILE SUALA LA MAFAO KWA WASTAAFU LIMEKUWA KAMA ZAWADI BADALA YA HAKI (HENCE KULAZIMISHA WASTAAFU KUTUMIA NJIA ZINAZOISHIA KUITWA "UTOTO") HUENDA HUO UTAKUWA WAKATI MZURI KWAKE KUELEWA KWANINI WAZEE WETU WALIFANYA HUO ANAOITA "UTOTO".

Picha kwa hisani ya BONGOPICHA

WAKATI serikali ikishutumiwa na viongozi wa madhehebu ya Kikristo, juu ya Tanzania kutaka kujiunga na Jumuiya ya nchi za Kiislamu (OIC) na kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi nchini, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, amekutana kwa siri na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, kujadili masuala hayo.

Kikao hicho cha faragha cha viongozi hao wawili, kilichukua zaidi ya saa moja katika mazungmzo yao yaliyofanyika jana katika ofisi za Jimbo Kuu la Dar es Salaam, kuanzia saa 10:30 jioni hadi saa 11:30.

Membe alikutana na Pengo jana ikiwa ni siku moja baada ya kardinali huyo kurejea nchi akitokea Vatican ambako alikwenda kwa shughuli za kanisa.

Akizungumza na Tanzania Daima, baada ya kumalizika kwa kikao hicho nyeti, Waziri Membe alikiri kuwa na kikao cha faragha na kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki nchini, lakini hakuwa tayari kusema nini walichojadiliana, kwa madai kuwa, hayapaswi kuwekwa hadharani kwa sasa.

“Unajua Kardinali Pengo ni kiongozi wa kiroho wa ngazi ya juu sana, kila tunapokuwa na masuala mazito ya kitaifa, tunapenda kupata ushauri wake pamoja na viongozi wengine wa kiroho ili kuona wanasemaje,” alisema Waziri Membe.

“Mbali na suala la OIC na Mahakama ya Kadhi, tumezungumza mambo mengi ya kitaifa ambayo mimi sipaswi kueleza zaidi kwa undani, kwani unaweza kumuuliza Baba Kardinali mwenyewe kama atataka kukueleza, lakini ni mambo ambayo yanahusiana na maisha ya Watanzania wote,” alisema Waziri Membe.

Kuhusu mjadala unaoendelea juu ya Tanzania kujiunga na OIC na jinsi hali ilivyo kwa sasa nchini, Waziri Membe alisema ni mambo ya kupita na utulivu utarejea hivi karibuni.

“Hali ya amani na utulivu itarudi hivi karibuni, hakuna shida, serikali ina amini na inawahakikishia wananchi kuwa hakuna vurugu kuhusiana na hilo wala suala lingine lolote.

“Watu watulie, wafanye kazi, serikali itakutana na wadau wote na nasema tena, hakuna tatizo kubwa hapa, tutahakikisha suala hili linaisha kwa amani bila kusababisha vurugu zozote,” aliongeza Membe.

Akizungumzia madai yaliyotolewa na Jumuiya ya Maaskofu wa CCT, kumtaka ajiuzulu hivi karibuni, alisema kuwa hilo hataki kuliongelea kwani amechoka, aachwe apumzike kwanza.

Jitihada za kumtafuta Kardinali Pengo, kuzungumzia juu ya kikao hicho cha siri ziligonga mwamba baada ya kuambiwa kuwa, ameingia kwenye kikao kingine na uongozi wa Kanisa la Mt. Joseph na haijulikani kingeisha saa ngapi.

Mwishoni mwa wiki iliyopita maaskofu wanaounda Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), walielezea kusikitishwa, kushtushwa na kupinga ushawishi unaojengwa na serikali wa kutaka Tanzania iridhie kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na kujiunga na Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu (OIC).

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Askofu Peter Kitula ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, alisema hawatakuwa tayari kukubalia kwa vyovyote vile kuona chama fulani cha siasa kikijaribu kutafuta ridhaa ya wapiga kura kwa gharama ya kutishia umoja wa kitaifa na amani ya nchi.

“Hapa ieleweke kuwa ni hatari na kamwe isiruhusiwe njia hii kutumika ili mradi chama fulani kishike dola hata kama ni kwa gharama ya kuvunjika kwa umoja wa kitaifa na amani ya nchi hii! Jambo hili hatutalikubali kwa vyovyote vile kwa chama chochote kitakachokubali mambo haya mawili aidha wakati wa kampeni za uchaguzi au wakati wowote ule,” lilisema tamko hilo la CCT lililoambatanishwa na majina ya maaskofu 64 wa nchi nzima.

Pasipo kufafafanua huku wakisema kwamba CCT, haifungamani na chama chochote cha siasa, maaskofu hao katika tamko lao walisema, iwapo itafikia hatua ya Tanzania kujiunga na OIC na Mahakama ya Kadhi kuridhiwa, basi wao watalazimika kufikiria upya jinsi ya kukishauri chama hicho tawala kwa kuzingatia kile walichokieleza kuwa ni manufaa ya Watanzania.

“Kipekee wakati huu, kutokana na yanayoendelea kujadiliwa bungeni, tunatoa tahadhari kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake kutoruhusu kabisa kuendelea kwa mjadala huu kama ambavyo tumekuwa tukiomba mara kwa mara kwa nyakati tofauti zilizopita,” linasema tamko hilo.

Pamoja na hilo, maaskofu hao walimtaka Waziri Membe, kujiuzulu wadhifa wake kutokana na hatua yake ya kujenga ushawishi wenye mwelekeo wa kidini wa kuiingiza nchi katika OIC.

Mbali ya hayo, tamko lilisema kuwa hatua ya Tanzania kujiunga OIC inakwenda kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Ibara ya 19 (2) na Sheria ya Vyama vya Siasa nchini.

Askofu Kitula alisema, wanapinga Tanzania kujiunga na OIC kwa maelezo kuwa, katiba ya jumuiya hiyo imejipambanua wazi kuwa na malengo ya kuendelea na kuulinda Uislamu, jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa taifa, lenye watu wa imani nyingine za dini.

Akifafanua askofu huyo alisema, katika Ibara ya 1 (11) ya Katiba ya OIC, kuna kipengele kinachosomeka ‘kusambaza, kuendeleza na kuhifadhi mafundisho ya dini ya Kiislamu….kuendeleza utamaduni wa Kiislamu na kuulinda urithi wake’, maelezo ambayo ni kinyume cha Katiba ya Jamhuri ambayo inahimiza uhiari na uhuru wa mtu binafsi katika masuala yanayohusu kueneza dini au masuala ya imani.

Askofu Kitula ambaye alisoma tamko hilo kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCT, Akofu Donald Mtetemela, aliyesaini tamko hilo, alisema uamuzi wa kujiingiza katika masuala ya namna hiyo ni wa hatari, kwani yanaweza kuleta migogoro kutokana na kuwapo kwa dhana ya udini.

Maaskofu hao walimtaka Waziri Membe kuachana na kauli zake juu ya umuhimu wa kuingia kwenye jumuiya hiyo ya Kiislamu na kuhoji aliyemtuma kufanya hivyo.

CHANZO:Tanzania Daima


*Yataka sheria ziachwe zifuate mkondo wake
*Yasubiri uamuzi kuhusu sakata la ufisadi
*Yaguswa na usanii wa kampuni ya Richmond
*Yaahidi Rais Obama au McCain kuja nchini

Na Hassan Abbas


BALOZI wa Marekani nchini, Bw. Mark Green amekuwa mwanadiplomasia wa kwanza nchini kumshauri Rais Jakaya Kikwete kuhusu nini anachopaswa kukifanya saa chache kabla hajaamua hatima ya waliokwapua mabilioni kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). 

Balozi Green aliyesisitiza kuwa mafisadi si watu wa kuachwa hata kama ni vigogo na kutaka sheria zichukue mkondo wake, ameifafanulia Majira jinsi alivyoguswa baada ya kuona kampuni ya kimarekani ya Richmond ilivyohusika katika utata kwenye sekta ya umeme nchini. 

Balozi Green alisema hayo jana katika mahojiano maalumu na gazeti hili ofisini kwake Dar es Salaam kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu uchaguzi wa Marekani, mtikisiko wa uchumi, hali ya kisiasa nchini na mtazamo wake kuhusu wagombea, maseneta Barack Obama na John McCain. 

EPA na Richmond 

Balozi Green alisema hawezi kujinasibu kuwa Marekani ni Taifa la mfano katika kupambana na rushwa, lakini alisisitiza kuwa katika miaka 232 ya Uhuru wa Taifa hilo, ujenzi wa jamii yenye kuwajibika kwa kufuata utawala wa sheria usiomwogopa mtu ndio msingi. 

"Rais Kikwete anafanya kazi kubwa ya kujenga Taifa. Lakini vita dhidi ya ufisadi inahitaji kutowaacha watu wakatamba. Sheria ichukue mkondo wake hata kama mtu ni mashuhuri kiasi gani. 

"Sisi Marekani tumekuwa na azma ya wazi kuwa kiongozi wa umma akiiba fedha za watu, anachunguzwa na kuchukuliwa hatua. Wamarekani ni wakarimu sana kutoa fedha zao kusaidia watu, lakini ni wakali sana wanapoona inafanyiwa ufisadi. Rais Kikwete akitumia sheria atafanikiwa," alisema Balozi Green na kusisitiza kuwa katika sakata la EPA, waliopoka fedha hizo wanapaswa kuwajibishwa. 

Akifafanua kuhusu hilo, Balozi Green alisema Rais Kikwete alitaja mikakati mizuri alipozungumza bungeni kuhusu namna atakavyowashughulikia mafisadi wa EPA. 

"Rais alitaja mikakati mizuri. Tunasubiri kuona atakavyoitekeleza," alisema. Akizungumza bungeni Agosti 21 mwaka huu, Rais Kikwete aliwapa mafisadi hao hadi Oktoba 30 (jana) wawe wamerejesha fedha hizo, vinginevyo ifikapo Novemba mosi (kesho) wawe wameburutwa kortini. 

Sakata la Richmond, kampuni iliyoshinda zabuni ya kufua umeme wa mamilioni nchini ikijieleza kuwa ilitokea Marekani, ni moja ya matukio yaliyoitikisa Serikali ya Rais Kikwete mwanzoni tu mwa utawala wake. 

Akilizungumzia sakata hilo, Balozi Green alisema Serikali ya Tanzania katika kupambana na rushwa inapaswa kufuata sheria bila kujali mhusika au kampuni husika imetoka nchi gani. 

"Suala la Richmond najua ilikuja ikafanya kazi kupitia kampuni iliyosajiliwa nchini. Lakini bila kujali kampuni hiyo ilitoka wapi, Serikali inapaswa kuchukua sheria haraka inapoona kuna ufisadi," alisema huku akikiri kuwa ukweli kwamba kampuni hiyo ilijieleza kutoka Marekani, ulimsumbua wakati wa sakata hilo, ingawa ubalozi wake hauwajibiki moja kwa moja katika mikataba inayohusu kampuni binafsi. 

Uchaguzi wa Marekani 

Balozi Green alikiri kuwa uchaguzi wa mwaka huu wa nchi hiyo umekuwa na hamasa kubwa hasa kutokana na ushiriki wa Seneta Obama, Mmarekani mwenmye asili ya Afrika wa kwanza kuteuliwa na chama kikuu kuwania urais. 

"Ni kweli kwamba ushiriki wa Seneta Obama umeibua hamasa miongoni mwa Wamarekani wengi, hilo ni suala lisilo na ubishi. Lakini pia hata uteuzi wa Seneta McCain naye umeibua ushawishi katika baadhi ya nchi. 

"Wakati huku Afrika Obama anaonekana kuwa na ushawishi, McCain naye ni kivutio hasa katika nchi za Mashariki ya Mbali ambako kutokana na historia yake ya kushiriki vita ya Vietnamu na kwa miaka mingi aliyokaa kwenye Kamati ya Mambo ya Nje kwenye Bunge la Seneti, alishiriki masuala mengi yanayohusu eneo hilo," alisema Balozi Green ambaye ni mfuasi wa Republican. 

Alisema, akiwatathmini wagombea hao wawili, anaona kuwa wote kwa sera zao, wana uwezo wa kuisaidia Marekani iwapo mmojawapo ataingia Ikulu. 

"Ukiangalia sera zao, hakuna shaka kwamba wote (McCain na Obama) wana mikakati ya dhati kuisaidia Marekani na historia zao zinaonesha wana uwezo mkubwa," aliongeza. 

Akizungumzia somo ambalo nchi za Afrika zinaweza kujifunza kutokana na kampeni zinazoendelea sasa nchini Marekani, Balozi Green alisema kubwa ni umuhimu wa watu kujadiliana masuala ya kitaifa kwa uwazi na mwishowe kila mwananchi akawa na fursa ya kupiga kura na kumchagua kiongozi anayemtaka. 

"Siwezi kusema kuwa Marekani ina demokrasia ya kuigwa, sote bado tunajifunza kutoka kwa kila mmoja. Lakini kama ilivyoonekana, mijadala ya wazi ni kitu muhimu ili kujadili masuala ya kitaifa na mwishowe kuheshimu uhuru wa kupiga kura. Naamini mkiimarisha hili, Afrika na Tanzania zitafanikiwa," aliongeza. 

Msukusuko wa uchumi na Afrika 

Balozi Green alikiri kuwa uchumi wa Marekani umetikisika, lakini akazitoa wasiwasi nchi za Afrika hususani Tanzania, kuwa kiwango cha misaada ya Marekani hakitaathirika kutokana na hali hiyo. 

"Kwa mfano, miradi ambayo tumekubali kuisaidia Tanzania ilishapitishwa na fungu lake lipo, kwa hiyo haitaathirika, sioni sababu ya Watanzania kuwa na wasiwasi," alisisitiza. 

Pia alisema hofu ya miradi mingi iliyoanzishwa chini ya utawala wa chama cha Republican nayo kubatilishwa, iwapo kitaingia madarakani chama cha Democrat haina msingi, kwani wakati wa upitishaji wa miradi hiyo Wamarekani hukubaliana kwa pamoja bila kujali itikadi ya vyama. 

"Kwa bahati nzuri nilikuwa kwenye Baraza la Wawakilishi, ni mmoja wa wawakilishi waliopigania kupitishwa kwa sheria iliyounda shirika la Millenium Challenge Account, linalotoa misaada mbalimbali kwa Afrika ikiwamo Tanzania. 

"Bahati nzuri wakati wa kujadili masuala haya, wabunge walikuwa wamoja bila kujali itikadi. Kwa hiyo hakuna atakayeweza kuzuia miradi hii, iliamuliwa kwa sauti ya Wamarekani wote," alisema.

Obama au McCain kuja Tanzania 

Akizungumzia ushirikiano mzuri baina ya Tanzania na Marekani, Balozi Green aliisifu kazi nzuri iliyofanywa na Rais wa zamani wa Marekani, Bw. Bill Clinton, ambaye ujio wake nchini na kazi za taasisi zake, ziliwafanya Wamarekani wengi kuijua au kuwa na nia ya kuijua Tanzania. 

"Hata ujio wa Bush, watu wanaweza kunipongeza kwa kufanikisha kuja kwake, lakini historia nzuri iliyowekwa na Clinton ndiyo iliyowazindua Wamarekani wengi kisha akaja Bush na baadaye mkutano wa Sullivan, lakini pia wadhifa wa Rais Kikwete kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, vimeifanya Tanzania kujulikana zaidi. 

Akizungumzia uwezekano wa ofisi yake kuhakikisha Rais ajaye wa Marekani anafuata nyayo hizo kwa kufika nchini, Balozi Green alisema: 

"Nitafurahi kuona siku moja Rais ajaye wa Marekani awe Seneta McCain au Seneta Obama anaitembelea Tanzania, kuimarisha uhusiano mzuri uliopo. Niko tayari kushughulikia hilo ili afike hapa. 

"Bahati nzuri Seneta McCain nimeshawahi kukutana naye wakati nikiwa kwenye Baraza la Wawakilishi, Obama hatujaweza kukutana kwa sababu wakati huo nikiwa kwenye siasa, yeye alikuwa bado yuko chini, lakini naamini wote watakuwa tayari kuja kuiona nchi hii nzuri," aliahidi. 

Balozi Green kitaaluma ni mwanasheria aliyepata kujaribu kuwania ugavana wa jimbo la Wisconsin kupitia chama cha Republican mwaka juzi akapoteza.

Chanzo:Majira

30 Oct 2008




IT SHOULD HAVE BEEN  SEN JOHN MCCAIN (R-AZ),AND NOT SEN JOHN MCCAIN (D-AZ) AS SEEN IN THE PHOTO ABOVE, IF YOU HAVENT NOTICED WHT'S WRONG.TRYING TO STEAL OBAMA'S LEAD IN THE POLLS?


Read it HERE

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.