6 Jan 2009

Picha kwa hisani ya Mjengwa.

Habari hiyo ni kwa mujibu wa gazeti la  Sunday Citizen.Pia,mwanablogu BWAYA ameichambua kwa undani habari hiyo ya kusikitisha.Makala za Padre Karugendo ni miongoni mwa maandiko yaliyonishawishi nami njiingize kwenye fani ya uandishi wa makala.Nahisi Kanisa Katoliki limechukua hatua hiyo kutokana na msimamo makini na wa uwazi wa Padre Karugendo kuhusiana na mambo mbalimbali ya Kanisa hilo.Japo mie ni Mkatoliki pia,lakini sipendezwi na namna Kanisa hili lisivyopenda kukosolewa.Nalinganisha tukio hili na lie la Father Nkwera (na wanamaombi) ambaye kimsingi kosa lake kubwa ni kutumia karama kama ile aloyokuwanayo Bwana Yesu ya kuponyesha wagonjwa.Yayumkinika kubashiri kwamba hatma ya Kanisa letu sio ya kuleta matumaini sana kama litaendeleza UKALE na kujifanya halitambua dunia inavyobadilika.

5 Jan 2009


ALIYEKUWA Mkuu wa Majeshi Nchini, Meja Jenerali, Robert Mboma, amesema anaamini kitambi alicho nacho kimesababisha kushindwa katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) za ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini.

Mboma aliyasema hayo juzi wakati akiwashukuru wananchi katika uzinduzi wa kampeni za chama hicho za kinyang'anyiro cha ubunge wa jimbo hilo.Alisisitiza kuwa anaamini kilichochangia kutopata kura nyingi zaidi ni kitambi hicho alichokuwa nacho na kwamba hali hiyo itamkomaza kisiasa.

Mboma ambaye aliwashangaza baadhi ya watu walioshuhudia uzinduzi wa kampeni hizo uliofanywa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi katika kijiji cha Ilembo Mbeya vijijini.Alisema kkuanguka kwake katika jimbo hilo kumetokana na wananchama wa chama hicho kumnyima kura.

Alisema kitendo hicho hakiotamuathiri bali wanamkomaza kisiasa na kwamba endapo kama angeteuliwa kuwa Mbunge wa jimbo hilo angelepeleka maendeleo."Kwa kweli nanawashukuru wananchi mlionipigia kura nilizozipata ingawa hazikuwa ndogo lakini ninasikitika na ninawashukuru ambao hawakunipigia kura na kuniangusha wakati wakijua wazi kuwa mimi ni mzaliwa na hapa na mngenichagua ningewaletea wananchi maendeleo katika jimbo la Mbeya vijijini," alisema.

Aliendelea kusema kuwa sio mbaya hata kama wamemchagua Mchungaji Mwanjali kwa sababu anaimani atawaletea Maendeleo na kurithi yale yote aliyatarajia kuyafanya aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Marehemu Richard Nyaulawa katika kuboresha huduma za jamii hususan maji, umeme na kuboreshea miundombinu...HABARI HII INAENDELEA HAPA.

NILIDHANI WANAJESHI WANASTAHILI KUJIWEKA FIT HATA BAADA YA KUSTAAFU MAJUKUMU YAO.HOW COME MKUU WA MAJESHI AMEJIACHIA KIASI CHA KUWA NA KITAMBI KIKUBWA "KILICHOPELEKEA KUANGUSHWA KWAKE KWENYE KINYANG'ANYIRO HICHO"? BY THE WAY I DONT BUY HIS LAME EXCUSE.NADHANI HAKUFANYA RESEARCH YA KUTOSHA KABLA YA KUJIINGIZA KWENYE COMPETITIVE POLITICS.WATANZANIA WAMEANZA KUTOFAUTISHA KATI YA UMAARUFU WA MTU NA UWEZO WA KUWALETEA MAENDELEO.AND IT'S THE LATTER THAT LED TO MBOMA'S FAILURE TO WIN HIS PARTY'S NOMINATION.

HII DHANA YA KWAMBA ANGEPATA UBUNGE ANGEWEZA KUWALETEA MAENDELEO WANA MBEYA VIJIJINI SIO TU POTOFU BALI PIA MUFILISI.KWANI ILI KULETA MAENDELEO YA WANANCHI WENZIO NI LAZIMA UWE KIONGOZI WAO?ALISHINDWAJE KUWALETEA MAENDELEO ALIPOKUWA KIONGOZI WA KITAIFA (MKUU WA MAJESHI) LAKINI AWEZE ATAPOPATA UBUNGE?NI UKOSEFU WA WASHAURI WAZURI AMBAO WANGEPASWA KUMKUMBUSHA HISTORIA YA MA EX-CDF WENZIE.

Magazeti mbalimbali ya leo huko nyumbani yameongozwa na habari za uzinduzi wa kampeni za CCM katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Mbeya Vijijini unaotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu.Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi ndiye aliyezindua kampeni hizo na kufanya kila ambacho kwa muda mrefu kimekuwa adimu katika duru za siasa za vyama vingi huko nyumbani.Kwa mujibu wa habari hizo,Mwinyi,maarufu kama Mzee Ruksa,alitumia sehemu kubwa ya hotuba yake kuzungumzia maslahi ya wana-Mbeya Vijijini katika uchaguzi huo badala ya kuipigia debe CCM pekee.

"Mwinyi...hakuonyesha unazi kwa CCM wala mgombea wake wakati alipozindua kampeni za chama hicho jana katika kata ya Kijiji cha Ilembo kilicho tarafa ya Isangati wilayani Mbeya Vijijini.Badala yake, Mwinyi alisisitiza amani, mshikamano na maendeleo ya wilaya ya Mbeya Vijijini, akiwataka wananchi wa eneo hilo kuhakikisha wanabakia na mshikamano wakati wanasiasa watakapoondoka jimboni humo baada ya purukushani za uchaguzi...linaandika gazeti la Mwananchi.

Tanzania Daima linamnukuu Mwinyi akisema kwamba "Vyama vya siasa vishindane kwa sera, visitumie lugha za matusi, kejeli, dharau na uongo wakati wa kampeni, uungwana wenu viongozi wa siasa utawapa matumaini wananchi kuchagua chama au mtu wanayemtaka ili kuhakikisha kuwa maendeleo ya nchi yanakua kwa kasi".

Akionyesha kuthamini zaidi maslahi ya wananchi wa Mbeya vijijini kuliko ya kisiasa,Rais huyo mstaafu aliwausia wapiga kura jimboni humo "kumsikiliza kila mgombea kwa makini na baadaye kila mmoja amchague yule anayeona sera za chama chake zinakidhi matumaini ya wananchi wa Mbeya Vijijini, " na kuhakikisha "kwamba wakati wanasiasa wetu wanapoondoka Mbeya Vijijini baada ya kampeni nyinyi mnabaki kuwa kitu kimoja katika umoja wenu," linaeleza Habari Leo.

MIONGONI MWA MAMBO YANAYOKWAZA MAENDELEO NI KUWEKA MBELE MASLAHI YA KISIASA BADALA YA YALE YA WANANCHI.OF COURSE,VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WANAPASWA KUSIMAMIA MASLAHI YA VYAMA VYAO LAKINI NI MUHIMU KWAO KUTAMBUA KUWA JUKUMU KUU LA VYAMA HIVYO NI KUWAHUDUMIA WANANCHI NA NI WANANCHI HAOHAO WANAOWEZESHA KUWEPO HAI KWA CHAMA IN THE FORM OF WANACHAMA.KWA MANTIKI HIYO,WANANCHI,REGARDLESS YA POLITICAL AFFILIATIONS ZAO,WANA NAFASI NA UMUHIMU WA KIPEKEE KWA VYAMA VYA SIASA HASA IKIZINGATIWA PIA KWAMBA WAO NDIO PIA CHIMBUKO LA UONGOZI KATIKA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA.

BAADA YA KUNG'ATUKA KATIKA ACTIVE POLITICS,BABA WA TAIFA ALIJITAHIDI KUCHUKUA NAFASI YA UANASIASA WA KITAIFA BADALA YA KICHAMA AMBAPO MARA KADHAA ALIWEKA MKAZO KATIKA MASUALA YANAYOHUSU TAIFA KWA UPANA BADALA YA YALE YA CHAMA CHAKE CHA CCM PEKEE,LICHA YA KUWA YEYE NDIO ALIKUWA MIONGONI MWA WAASISI WAKUU WA CHAMA HICHO TAWALA.KWA UPANDE MWINGINE,MWINYI NAFASI YA MWINYI BAADA YA KUSTAAFU UENYEKITI WA CCM IMEPEWA ATTENTION NDOGO NA WACHAMBUZI WA SIASA PAMOJA NA MEDIA KWA KUTOFANYA REFERENCE YA NAMNA KIONGOZI HUYO WA ZAMANI ANAVYOJITAHIDI KUFUATA FOOTSTEPS ZA BABA WA TAIFA KATIKA KUTANGULIZA ZAIDI MASLAHI YA WANANCHI NA TAIFA KWA UJUMLA BADALA YA KUENDEKEZA UNAZI WA KISIASA PEKEE.

NI MATUMAINI YA WATANZANIA WOTE WAPENDA MAENDELEO KWAMBA MFANO HUU WA MZEE MWINYI UTAIGWA NA WANASIASA WETU WOTE KAMA KWELI NIA YAO NI KUTUHUDUMIA KUPITIA VYAMA VYAO.LAKINI PIA WANANCHI NAO WANAPASWA KUFUMBUKA MACHO NA KUTAMBUA KWAMBA UNAZI WA KISIASA HAUPASWI KUWA INFRONT OF MASLAHI YAO KAMA WANANCHI,NA KWA MANTIKI HIYO TOFAUTI ZETU ZA KIITIKADI HAZIPASWI KULETA MGAWANYIKO AU KUPELEKEA KUCHAGUA VIONGOZI WABOVU KWA VILE TU WANATOKA KATIKA VYAMA TUNAVYOSHABIKIA.

HONGERA SANA MZEE RUKSA.YOU TRULY HAVE SHOWN THE RIGHT WAY.



4 Jan 2009

Ghana's peaceful presidential election was a rare example of a functioning democracy in Africa and should be a model for the continent, African leaders and voters have said. Skip related content

Much attention in Africa and elsewhere was focused on the Ghanaian vote after a year of political crises, many of them violent, tarnished Africa's democratic credentials.

Opposition candidate John Atta Mills was declared the winner on Saturday after the closely fought election was settled by a run-off.

Kenya's prime minister Raila Odinga said: "John Atta Mills' victory and the conduct of the people of Ghana provides a rare example of democracy at work in Africa."

While the contest raised tensions and some violent incidents were reported, international observers say the vote was mostly peaceful. The conduct of the election contrasted with many other African countries, where democracy was battered in 2008.

More than 1,000 people were killed in post-election violence in Kenya at the start of the year and in Zimbabwe President Robert Mugabe and opposition leader Morgan Tsvangirai have been deadlocked for months over a power-sharing agreement after disputed elections.

SOURCE: ITN

3 Jan 2009

Maelfu ya waandamanaji wanatarajiwa kuandamana baadae leo jijini London kupinga mashambulizi ya Israel dhidi ya Wapalestina.Inakadiriwa takriban watu 20,000 watashiriki maandamano hayo yatakayowajumuisha watu maarufu kama Mbunge wa chama cha Respect,George Galloway na mwanamuziki mkongwe Annie Lennox.Picha ya mwanzo inaonyesha akinamama wa Kiislam walioandamana jana jijini Dar kupinga mashambulizi hayo,na picha za chini zinaonyesha hali ilivyo na uharibifu uliosababishwa na makombora ya Israel huko Gaza.




VYANZO:Sky News,Habari Leo ,The Washington Post na The Guardian.


2 Jan 2009

Soma stori kamili HAPA.

1 Jan 2009

FASHIFASHI LONDON EYE JIJINI LONDON,UINGEREZA

FIREWORKS ST ANDREWS STREET,EDINBURGH,SCOTLAND.

WARSAW,POLAND.

VILNIUS,LITHUANIA.


SALA YA MWAKA MPYA POPE BENEDICT KATIKA MISA YA MKESHA WA MWAKA MPYA HUKO VATICAN CITY,VATICAN.

SHAMRASHAMRA JIJINI VALENCIA,SPAIN.

TAIPEI,TAIWAN.

SOFIA,BULGARIA.

RED SQUARE,MOSCOW

MANILA,PHILIPPINES.

POLISI WAKIDHIBITI WAANDAMANAJI WA KIPALESTINA MKESHA WA MWAKA MPYA HUKO ATHENS,UGIRIKI

GISBORNE,NEW ZEALAND.

CHAMPS ELYSEE,JIJINI PARIS,UFARANSA.

BERLIN,UJERUMANI.

FASHIFASHI JIJINI ATHENS,UGIRIKI.

MALAYSIA.

HONGKONG


SYDNEY,AUSTRALIA.

AUCKLAND,NEW ZEALAND.

31 Dec 2008

HATIMAYE TUMEFIKA MWISHO WA MWAKA 2008.SIJUI MWENZANGU KWAKO MWAKA HUU TUNAOUMALIZA LEO ULIKUWAJE LAKINI BINAFSI 2008 IMENIACHA NA PENGO AMBALO HALITOZIBIKA HADI KIFO CHANGU.TAREHE 29 MEI NILIMPOTEZA MAMA YANGU MZAZI,MAREHEMU ADELINA MAPANGO.KIFO HICHO KILIHITIMISHA SAFARI YAKE NGUMU NA YA MAUMIVU ILIYOANZA MWISHONI MWA MWEZI FEBRUARI AMBAPO ALIANGUKA NA KUPOTEZA FAHAMU.ILINILAZIMU KWENDA TANZANIA MWEZI MACHI NIKIWA NA MATUMAINI KWAMBA HUENDA HALI YAKE INGEBADILIKA LAKINI KWA BAHATI MBAYA HADI ANAFARIKI SIKUPATA BAHATI YA KUONGEA NAE HATA NENO MOJA.MARADHI NA KIFO CHA MAMA VILIPELEKEA KUSHINDWA KWANGU KUHITIMU MASOMO YANGU MWEZI NOVEMBA KUTOKANA NA KUTUMIA TAKRIBAN MIEZI MITANO HUKO NYUMBANI NIKIUGUZA NA KUSHUGHULIKIA TARATIBU ZA MAZISHI NA AROBANI.BWANA ALITOA NA BWANA ALITWAA,LAKINI PENGO ALILOACHA MAMA HALITOZIBIKA MILELE,NA TUKIO HILO NDILO LILILOKUWA KUBWA ZAIDI KWANGU KWA MWAKA HUU TUNAOUMALIZA LEO.

MATUKIO MENGINE NILIYOFANIKIWA KUYAWEKA BLOGUNI AU KUYAFUATILIA KWA KARIBU KUANZIA MWEZI JANUARI NI KAMA IFUATAVYO:
MIONGONI MWA MATUKIO MAKUBWA YA MWEZI JANUARI ILIKUWA NI PAMOJA NA VURUGU ZILIZOJITOKEZA BAADA YA UCHAGUZI MKUU NCHINI KWENYE AMBAPO WAFUASI WA MGOMBEA RAILA ODINGA WALIDAI WAMEPORWA USHINDI NA MWAI KIBAKI.TUKIO JINGINE KUBWA LILIKUWA KIFO CHA WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA PAKISTAN BENAZIR BHUTTO.MAFURIKO NCHINI MSUMBIJI YAUA WATU KADHAA NA KUACHA MAELFU WAKIWA HAWANA MAKAZI.GEORGE W. BUSH ASOMA STATE OF THE UNION ADDRESS KWA MARA YAKE YA MWISHO (HATOKUWA MADARAKANI 2009).PIA SERIKALI ILIYOKUWA CHINI YA WAZIRI MKUU WA ITALIA,ROMANO PRODI,YAVUNJIKA.KADHALIKA,BALOZI WA TANZANIA HUKO AFRIKA KUSINI,EMMANUEL MWAMBULUKUTU APIGWA.SERIKALI YATOA TAMKO KUHUSU ISHU YA EPA.TUKIO JINGINE MUHIMU LILIKUWA KUCHAGULIWA KWA JK KUWA MWENYEKITI WA UMOJA WA AFRIKA (AU).

MWEZI FEBRUARI ULISHUHUDIA UJIO WA RAIS BUSH NCHINI TANZANIA NA KUNG'OKA KWA EDWARD LOWASSA KWENYE UWAZIRI MKUU KUFATIA TUHUMA ZA KAMPUNI YA KITAPELI YA RICHMOND.PIA KATIKA MWEZI HUO KULIKUWA NA KIOJA CHA SPIKA SAMUEL SITTA KUMTAKA NAIBU WAKE ANNE MAKINDA "ASIKURUPUKE" KUENDESHA MJADALA WA ISHU YA RICHMOND HADI HAPO SPIKA ATAPOREJEA KUTOKA SAFARINI UGHAIBUNI.BAADAYE SPIKA ALIAHIRISHA SAFARI HIYO,NA WOTE TUNAJUA KILICHOJIRI BAADA YA MJADALA HUO WA KIHISTORIA.KUJIUZULU KWA LOWASSA KULIMPELEKEA JK KUVUNJA KABINETI YAKE NA KISHA KUMTEUA BW MIZENGO PINDA KUWA WAZIRI MKUU HUKU SURA NYINGI ZA BARAZA LA MAWAZIRI WA ZAMANI ZIKIREJEA.KATI YA WALIOLALAMIKIWA SANA KUTEULIWA KWENYE BARAZA JIPYA NI PAMOJA NA "MZEE WA VIJISENTI" ANDREW CHENGE.PIA KATIKA MWEZI HUO,RAIS MWANAMAPINDUZI WA CUBA,FIDEL CASTRO ALING'ATUKA MADARAKANI.TUKIO JINGINE LILILOVUTA HISIA ZA JAMII YA WATANZANIA MTANDAONI NI KUFUNGIWA KWA JAMBO FORUMS NA WAHUSIKA WAKE WAWILI KUKAMATWA.HATA HIVYO MTANDAO HUO MAHIRI ULIREJEA HEWANI BAADA YA SIKU CHACHE UKIWA NA JINA JIPYA LA JAMII FORUMS.

MWEZI MACHI ULIANZA KWA KUTAWALIWA NA HABARI ZA KINYANG'ANYIRO CHA UCHAGUZI NCHINI MAREKANI AMBAPO MGOMBEA WA CHAMA CHA REPUBLICAN,JOHN MCCAIN,ALI-WIN NOMINATION YA CHAMA CHAKE.PIA SUPER-TUESDAY NDANI YA CHAMA CHA DEMOCRAT ILIZIDISHA MPAMBANO KATI YA HILLARY CLINTON NA BARACK OBAMA.MACHI PIA ILISHUHUDIA KUSAMBARATIKA KWA SERIKALI YA SERBIA.VILEVILE,WAKRISTO SEHEMU MBALIMBALI DUNIANI WALIADHIMISHA KUMBUKUMBU YA KUZALIWA BWANA YESU KRISTO KATIKA SIKUKUU YA PASAKA.WIKI YA MWISHO YA MACHI ILISHUHUDIA REPORTING YA BLOG HII KUTOKA TANZANIA BAADA YA MIE MTUMISHI WAKO KUELEKEA HUKO KUMUUGUZA MZAZI WANGU.

REPORTING LIVE AND DIRECT KUTOKA BONGO,BLOG ILIANZA MWEZI APRILI KWA PICHA KADHAA ZA KUTOKA NYUMBANI.HII ILIKUWA TRANSITION MUHIMU KWA BLOG YENU KWANI NDIO LILIKUWA JARIBIO LA KWANZA LA KUCHANGANYA NEWS ANALYSIS NA PHOTOBLOGGING.NIKIRI KWAMBA BADO NIKO NYUMA SANA IN THE LATTER.BLOG ILIWALETEA PICHA ZINAZOONYESHA HALI HALISI ILIVYO KATIKA HOSPITALI YA MUHIMBILI.PIA KULIKUWA NA MAKALA KUHUSU HUDUMA MBOVU KWENYE HOSPITALI YA REGENCY.KADHALIKA,KULIKUWA NA "BREAKING NEWS YA KIMTINDO" YA MAFURIKO HUKO IFAKARA PAMOJA NA PICHA ZA ADHA YA USAFIRI WILAYANI KILOMBERO.VILEVILE,BLOG ILIJITAHIDI KUUFAHAMISHA UMMA KUHUSU MAPUNGUFU MBALIMBALI KWENYE HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA TAASISI MBALIMBALI ZA HUKO NYUMBANI.MIONGONI MWA HABARI KUBWA ZA MWEZI HUU ILIKUWA NI PAMOJA NA KUJIUZULU KWA MZEE WA VIJISENTI ANDREW CHENGE.

NI VIGUMU KUFANYA EFFECTIVE BLOGGING WAKATI UNAUGUZA MTU MUHIMU KATIKA MAISHA YAKO KAMA MZAZI.KASI YA KU-BLOG NA KU-UPDATE BLOG ILIPUNGUA MWEZI MEI BAADA YA HALI YA MAMA KUZIDI KUDHOOFIKA.KIPINDI HIKI KILINIPA FURSA NZURI YA KUTAMBUA SOME HIDDEN SOCIAL BENEFITS ZA BLOGGING KWANI NILIPATA SALAMU NYINGI ZA SAPOTI KUTOKA KUTOKA KWA WATU NISIOWAFAHAMU LAKINI TULIOJUANA KUPITIA SEHEMU HII AMBAO WALIKUWA WAKINIPA MOYO KATIKA KIPINDI HICHO KIGUMU.PIA MWEZI MEI ULISHUHUDIA SHIRIKA LA NDEGE LA ATC LIKIINGIZA KWA MBWEMBWE DEGE MTUMBA LA AIRBUS A320.WAJUZI WA MAMBO WALIHOJI HATUA HIYO HUKU WAKISISITIZA KWAMBA HUO NI MWENDELEZO WA UFISADI.KADHALIKA,MZEE WA VIJISENTI ANDREW CHENGE ALIZUSHIWA KIFO KABLA YA HABARI HIYO KUKANUSHWA NA FAMILIA YAKE.PIA TAIFA STARS ILIFANYA KWELI KWA KUIBAMIZA THE CRANES 2-0.PIA RAPA MAARUFU 50 CENT ALITUA DAR NA KUFANYA ONYESHO MOJA.ILIFAHAMIKA PIA KWAMBA ALIYEKUWA GAVANA WA BoT DAUDI BALLALI AMEFARIKI HUKO MAREKANI.HABARI HIYO ILIGUBIKWA NA USIRI MKUBWA KIASI CHA BAADHI YA WATU KUHISI NI CHANGA LA MACHO.TAREHE 29 YA MWEZI HUU,SAA 4.30 USIKU (TANZANIAN TIME),MAMA YANGU MPENDWA ALIAGA DUNIA.THIS WAS THE DARKEST DAY OF MY LIFE.
JUNI ILIANZA KWA KUMZIKA MAMA MNAMO TAREHE 2.SINTAISAHAU SIKU HII MAISHANI MWANGU ASILANI.

MATUKIO MENGINE KATIKA MWEZI HUO NI PAMOJA MKUTANO WA LEON SULLIVAN ULIOFANYIKA HUKO ARUSHA HUKU BAADHI YA WAFANYABIASHARA WA NDANI WAKILAUMU KWA KUTELEKEZWA NA WAANDAAJI.TAIFA STARS ILIBORONGA HUKO CAPE VERDE BAADA YA KUTANDIKWA BAO 1-0.PIA MASHABIKI WA SOKA DUNIANI WALIELEKEZA MACHO NA MASIKIO YAO KWENYE KINYANG'ANYIRO CHA MICHUANO YA EURO 2008 AMBAPO HISPANIA ILIIBUKA KIDEDEA.BAJETI YA SERIKALI YASOMWA,MAUMIVU KWA WALALAHOI YAENDELEA.TIMU YA TAIFA YA CAMEROON YATOKA SULUHU NA TAIFA STARS JIJINI DAR HUKU MASTAA KAMA SAMUEL ETOO WAKIWA KIVUTIO.MABONDIA 6 WA TANZANIA WATIWA MBARONI HUKO MAURITIUS KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA UNGA.JENGO MOJA LA GHOROFA LILILOPO JUNCTION YA ZANAKI/KISUTU STR LAPOROMOKA .TAIFA STARS YANYUKWA 2-1 HUKO CAMEROON.OBAMA ASHINDA KUWA MGOMBEA WA CHAMA CHA DEMOCRAT.MAKALA YANGU KWENYE GAZETI LA RAIA MWEMA LA TAREHE 26 IKITABIRI KIFO CHA CCM (KAMA KILIVYOTABIRIWA NA BABA WA TAIFA) YAZUA SONGOMBINGO NA HATIMAYE KUFIKIA UAMUZI WA KUCHUKUA SABBATICAL LEAVE YA UANDISHI WA MAKALA.

MWEZI JULAI UNAANZA KWA PILIKAPILIKA ZA SABA SABA LAKINI UCHUMI MBOVU JAPO VITU KIBWENA KWENYE MABANDA HUKO KILWA ROAD.RAIS WA SHRIKISHO LA NDONDI TANZANIA,ALHAJI SHABAN MWINTANGA ATIWA MBARONI KUHUSIANA NA SAKATA LA MABONDIA WALIKAMATWA NA UNGA HUKO MAURITIUS.MSANII WA BONGOFLEVA T.I.D ATUPWA JELA MWAKA MMOJA.YANGA WAFANYA KITKO CHA KIHISTORIA:WAINGIA MITINI SIKU YA MPAMBANO KATI YAO NA SIMBA.MBUNGE MACHACHARI NA MAKAMU MWENYEKITI WA CHADEMA,CHACHA WANGWE,AFARIKI KWA AJALI YA GARI HUKO DODOMA.MAHAKAMA YA KIMATAIFA (ICC) YATOA WARRANT YA KUKAMATWA KWA RAIS WA SUDAN,OMAR AL-BASHIR,KWA TUHUMA ZA KUHUSIKA NA MAUAJI YA HALAIKI HUKO DARFUR.MHALIFU WA KIVITA,RADOVAN KARADZIC,AKAMATWA KUHUSIANA NA MAUAJI YA HALAIKI HUKO SERBIA.

AGOSTI,MREMBO NASREEM ATWAA TAJI LA MISS TANZANIA 2008.AJALI MBAYA YA BASI YAPOTEZA MAISHA YA WATU 10 NA WENGINE 30 KUJERUHIWA HUKO MBEYA.MWANAMUZIKI SHAGGY ATUA DAR NA KUFANYA ONYESHO.MAANDAMANO NA VURUGU ZATANDA NCHINI VENEZUELA,NA HUKO GEORGIA MAJESHI YA RUSSIA YAENDELEZA UBABE WAKE.HABARI NYINGINE KATIKA MWEZI HUU ILIKUWA NI KUJIUZULU KWA RAIS WA PAKISTAN PERVEZ MUSHARRAF.TUKIO JINGINE KUBWA LILIKUWA NI MICHEZO YA OLIMPIKI HUKO CHINA,NA KWA NYUMBANI WATANZANIA WALITEGESHA MASIKIO YAO HUKO DODOMA WAKATI JK ALIPOHUTUBIA BUNGE.WENGI WALITEGEMEA KUSIKIA HATIMA YA ISHU ZA EPA,RICHMOND NA UFISADI MWINGINE LAKINI HAYO YALIGUSIWA JUU JUU TU.AGOSTI PIA ILISHUHUDIA RAIS WA VISIWA VYA KOMORO,AHMED ABDALLAH MOHAMMED,AKIHUTUBIA BUNGE LA MUUNGANO DODOMA.PM MIZENGO PINDA ASOMA TAARIFA KUHUSU ISHU YA RICHMOND.KAMA KAWAIDA,NI TAARIFA TU HAKUNA ALIYEWAJIBISHWA SO FAR.JK AMTEMBELEA BUSH HUKO WHITE HOUSE NA MWEZI WA TOBA WAANZA.RAIS MWANAWASA WA ZAMBIA AFARIKI DUNIA.

SEPTEMBA YAANZA KWA HABARI ZA VIMBUNGA IKE NA GUSTAV.ASIF ALI ZARDARI,MJANE WA WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA PAKISTAN BENAZIR BHUTTO,ACHAGULIWA KUMRITHI JENERALI MUSHARAF.TETESI ZAZUKA KUHUSU AFYA YA KIONGOZI WA KORA YA KASKAZINI,KIM JUNG IL,IKIDAIWA KWAMBA AMEKUFA LAKINI NCHI HIYO YAKANUSHA HABARI HIZO.JONGWE MUGABE NA MORGAN TSHANGIRAI WAFIKIA MAKUBALIANO YA UONGOZI HUKO ZIMBABWE.MLIPUKO WA BOMU KATIKA HOTELI YA MARRIOT HUKO ISLAMABAD PAKISTAN WAUA NA KUJERUHI WATU KADHAA.KESI YA ZOMBE YAENDELEA KUUNGURUMA HUKO NYUMBANI.JACOB ZUMA NAE ATUA DAR.JAPAN YAPATA WAZIRI MKUU MPYA,TARO ASO,AMBAYE NI MKATOLIKI WA KWANZA KUSHIKA WADHIFA HUO NCHINI HUMO.UCHAGUZI WAFANYIKA NCHINI BELARUS LAKINI WAANGALIZI WA KIMATAIFA WADAI HAUKUWA FREE AND FAIR.PIA SAKATA LA MAZIWA YENYE WALAKINI HUKO CHINA YAPAMBA MOTO KWENYE ANGA ZA HABARI.MSHIRIKI WA TANZANIA KWENYE BIG BROTHER AFRICA 3 ATOLEWA MASHINDANONI,CHA AJABU AREJEA BONGO KAMA SHUJAA NA KUANDALIWA PATI YA PONGEZI!RAIS WA AFRIKA KUSINI,THABO MBEKI AJIUZULU.WAFANYAKAZI WA BENKI YA NMB WAGOMA NA KUSABABISHA USUMBUFU MKUBWA KWA WATEJA.SHEREHE ZA IDD EL FITR ZAKUMBWA NA BALAA BAADA YA VIFO VYA WAOTO 20 MJINI TABORA.USTAADH MMOJA MWENYE MSIMAMO MKALI HUKO SAUDI ARABIA ASOMA FATWA DHIDI YA MICKEY MOUSE KWA MADAI KUWA KIKARAGOSI HICHO NI WAKALA WA SHETANI!

ANGA ZA HABARI ZA KIMATAIFA MWEZI OKTOBA ZILIANZISHWA NA TAARIFA ZA WATEKA MELI (PIRATES) HUKO SOMALIA AMBAPO SAFARI HII WATEKA MELI KUTOKA UKRAINE ILYOKUWA NA VIFARU 33.UCHUMI WA DUNIA WAZIDI KWENDA HARIJOJO NA WASIWASI WAJITOKEZA KUHUSU UWEZEKANO KUFILISIKA KWA NCHI YA ICELAND.NENO ECONOMIC BAILOUT LAWA KAMA SALA KWENYE VYOMBO VYA HABARI VYA KIMAIFA HASA BAADA YA RAIS BUSH KUIDHINISHA BAILOUT YA DOLARI BILIONI 700 KUOKOA UCHUMI WA MAREKANI,NA NCHI KADHAA KUFUATA MKONDO.CHADEMA WASHINDA UCHAGUZI MDOGO WA TARIME ULIOAMBATANA NA KILA AINA YA VITUKO.OBAMA AENDELEA KUTESA KWENYE OPINION POLLS ZA UCHAGUZI MKUU WA MAREKANI.JK AZURU MBEYA,ZIARA YAGUBIKWA NA HABARI ZA MSAFARA WAKE KUTUPIWA MAWE.PIA JK ATAWAZWA KUWA "CHIFU MWANGUPILI" WA WANYAKYUSA.GAZETI LA MWANAHALISI LAFUNGIWA NA SERIKALI KWA MIEZI MITATU.RAIS WA MADAGASCAR AZURU TANZANIA.WALIMU DAR WAMPA KISAGO RAIS WA CHAMA CHAO BAADA YA KUTANGAZA KUAHIRISHWA KWA MGOMO.COLLIN POWELL AM-ENDORSE OBAMA,NA MPANGO WA KUM-ASSASSINATE OBAMA WADHIBITIWA.PIA KATIKA MWEZI HUU,SAKATA LA TANZANIA KUJIUNGA NA OIC NA LILE LA KUANZISHWA KWA MAHAKAMA YA KADHI LILITAWALA SANA HUKU MAASKOFU NA VIONGOZI WA KIISLAM WAKIRUSHIANA MANENO.HATARI LAKINI BADO SALAMA.HUKO DRC MAPAMBANO KATI YA MAJESHI YA SERIKALI NA YA WAASI CHINI YA GEN LAURENT NKUNDA YAZIDI KUPAMBA MOTO.

NOVEMBA YAINGIA NA MSISIMKO WA UCHAGUZI WA MAREKANI,NA KAMA ILIVYOTARAJIWA,OBAMA ASHINDA NA KUWEKA HISTORIA YA KUWA MWEUSI WA KWANZA KUWA RAIS WA NCHI HIYO.MALKIA WA DENMARK AZURU TANZANIA.WASANII WA KAMPUNI YA DOWANS WATANGAZA TENDA YA KUUZA MITAMBO YAO MITUMBA.SERIKALI YAFANYA BAILOUT NYINGINE KWA WAHINDI WA TRL,YALIPA TENA MISHAHARA YA WAFANYAKAZI.WAKATI "JAMES BOND WA SASA" CRAIG DANIEL AKISEMA DUNIA IKO TAYARI KWA "JAMES BOND MWEUSI" (A BLACK BOND),WAJUZI WA MAMBO WADAI KWAMBA HAKUNA UWEZEKANO WA KUWEPO A "BRITISH OBAMA" (PM MWEUSI).MKURUGENZI WA TAKUKURU,EDWARD HOSEA,ADAI KWAMBA WATUHUMIWA WOTE WA EPA WAKIKAMATWA NCHI ITAYUMBA!MAMIA WAFA BAADA YA MASHAMBULIZI YA KIGAIDI HUKO MUMBAI,INDIA.MAMIA WAFA NIGERIA KUFIATIA VURUGU ZA KIDINI NCHINI HUMO.WIMBI LA MIGOMO NA KUFUNGWA KWA VYUO VIKUU LASAMBAA HUKO NYUMBANI.WATUHUMIWA KADHAA WA EPA WAFIKISHWA KORTINI,MRAMBA NA YONA NAO WAFIKISHWA KORTINI,WENGI WAJIULIZA: JUSTICE AT LAST AU CHANGA LA MACHO?

HATIMAYE TUMEINGIA DESEMBA,MWISHO WA MWAKA.MAUAJI DHIDI YA ALBINO YAENDELEA HUKO NYUMBANI NA HAKUNA DALILI YA UFUMBUZI WA TATIZO HILO.VURUGU ZA UGIRIKI ZASAMBAA HADI NCHI NYINGINE ZA ULAYA.BUSH AKUMBWA NA KIMBEMBE HUKO IRAK BAADA YA KUVURUMUSHIWA VIATU NA PAPARAZI MMOJA WAKATI WA PRESS CONFERENCE.UCHAGUZI MKUU NCHINI TURKMENISTAN WAELEZEWA KUWA NI KIINIMACHO NA SIO HURU NA HAKI.KATIBU MKUU WA ZAMANI WA WIZARA YA FEDHA,GRAY MGONJA,NAE APANDISHWA KZIMBANI KWA TUHUMA ZA UFISADI.MEMBE AONYA CCM INAWEZA KUSAMBARATIKA,NAPE NNAUYE AMTUHUMU MAKAMBA KUWA ANAKUMBATIA MAFISADI.HALI YA USALAMA NCHINI SOMALIA YAZIDI KUWA MBAYA KUFUATIA MAPIGANO KATI YA KOO MBALIMBALI NCHINI HUMO.MASTERMIND WA MAUAJI YA KIMBARI NCHI RWANDA,THEONESTE BAGOSORA,AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA.TAKUKURU YAKURUPUKA NA KUDAI HAIMCHUNGUZI MKAPA (SIJUI NANI ALIWAULIZA!).KAPTENI MOUSSA DADIS KAMARA AJITANGAZA RAIS WA GUINEA KATIKA MAPINDUZI YALIYOFUATIA KIFO CHA RAIS LANSANA CONTE.PM PINDA ACHACHAMAA KUHUSU MAGARI YA KIFAHARI SERIKALINI,ILA NI KUANZIA MWAKANI KWANI TAYARI SHEHENA YA MAGARI 700 NA USHEE IMESHAAGIZWA!BEI YA MAFUTA SOKO LA DUNIA YAZIDI KUSHUKA LAKINI BEI YA BIDHAA HIYO HUKO NYUMBANI BADO IKO JUU KABLA YA KUKUMBWA NA UHABA USIOELEZEKA.NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI,AELEZA KWAMBA SERIKALI HAIFAHAMU KWANINI BEI YA MAFUTA IKO JUU LAKINI AKADAI YAKO KIBAO KUKIDHI MAHITAJI.AIAGIZA EWURA IKAE KITAKO NA WAFANYABIASHARA KUHUSIANA NA ISHU HIYO (JAPO AGIZO LA EWURA HIYOHIYO KUWATAKA WAFANYABIASHARA HAO KUPUNGUZA BEI YA MAFUTA LIMEENDELEA KUPUUZWA).ATCL YAENDELEA KUSUASUA JAPO UONGOZI WAKE BADO UNAENDELEA KUPETA.MGOMBEA WA CHADEMA KATIKA UCHAGUZI MDOGO MBEYA VIJIJINI AENGULIWA BAADA YA KUWEKEWA PINGAMIZI NA CCM NA CUF,ADAI AMESHAKATA RUFAA.PIA DESEMBA ILISHUHUDIA TAJIRI WA KIMAREKANI BERNARD MADOFF AKIWALIZA WAWEKEZAJI TAKRIBAN DOLA BILIONI 50 KWENYE PONZI SCHEME.
KWA KIFUPI,HAYO NDIYO MATUKIO YA KUKUMBUKWA NA BLOG HII.NAWASHUKURU NYOTE MNAONITEMBELEA.NAAHIDI KUENDELEA KUWALETEA KILE KITU ROHO ZENU ZINAPENDA.MSISITE KUNIKOSOA,KUNISHAURI NA KUTOA MAONI YENU.BLOGU HII NI YENU NAMI NI MTUMISHI WENU.NAWATAKIA HERI NA BARAKA YA MWAKA 2009.MUNGU AWABARIKI SANA.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.