16 Oct 2009


A black adviser to police on race issues has accused officers of 'horrendous harassment' as he revealed he has been stopped by officers more than 100 times.Ken Hinds, 50, attacked the Metropolitan police for 'racial profiling' as he revealed he had been repeatedly stopped in the past two decades.And he said other people have suffered similarly disproportionate treatment while driving, on the street and at Tube and railway stations

Mr Hinds of Edmonton, north London, sits on the force's Black Independent Advisory Group and is chairman of a monitoring group for stop and search in Haringey.
Earlier this week he won an apology and £22,000 compensation from British Transport Police (BTP) after he was handcuffed as he watched a black youth being arrested at Seven Sisters Tube station in 2004...READ MORE



Picha kwa hisani ya vyanzo mbalimbali mtandaoni.


MBUNGE wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge jana alinguruma ndani ya Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi, alipowataka Watanzania kuacha kutafuta mchawi aliyeua mashirika ya umma, akisema kuwa mengi yalikufa yakiwa mikononi mwao na si mwa wageni.

Chenge, mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, ametoa kauli hiyo wakati wananchi wengi wakilalamikia mikataba mibovu ya uwekezaji na uendeshaji mashirika ya umma kuwa ndiyo iliyochangia baadhi kufa na mengine kuwa katika hali mbaya.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana wakati akichangia Taarifa ya Utekelezaji wa Moboresho ya Shirika la Bima (NIC), Chenge alisema makaburi mengi ya mashirika ya umma yamechimbwa na Watanzania wenyewe.

"Leo (jana) wakati tunamalizia kuadhimisha miaka kumi ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, shirika hili la Bima lilikuwa moja ya malengo yake," alisema Chenge akirejea NIC ambayo ilikua na kutapakaa nchi nzima kabla ya kuanguka kiuchumi kiasi cha kusababisha serikali kuingilia kati na kuitengenezea muundo mpya.

"Lakini shirika hili leo liko hoi; kwa vyovyote vile serikali haiwezi kusimamia shirika hili kwa asilimia 100, lazima likabidhiwe kwa sekta binafsi, lakini Watanzania tumekuwa ni watu wa kupenda kupiga kelele hasa tunapoamua kubinafsisha. Mashirika haya tumeyaua wenyewe wala si wageni."

Chenge alisema: "Watanzania hatupaswi kutafuta mchawi wa mashirika yetu haya. Sisi wenyewe ndiyo tumeyaua na makaburi mengi leo hii yanaonekana."

Alifafanua kwamba, umefika wakati sasa Watanzania wakaachana na dhana ya kulalamika na badala yake wafanye kazi kwa bidii, huku pia akiitaka serikali iondoe dhana ya kuendesha mashirika kijamaa, akitolea mfano uwekaji wa kiwango cha chini cha bei na kutaka bei ya soko ishike hatamu.

Hata hivyo, alionyesha wasiwasi na Kikosi Kazi kinachofanya marekebisho kutokana na kukosa bodi na kuongeza: "Napata shaka kidogo, chombo ambacho kinaandaa taarifa halafu chenyewe pia ndio kijitathmini, nafikiri inapaswa kuundwa bodi."

Akichangia katika kikao hicho cha Kamati ya Fedha na Uchumi, Mbunge wa Tabora Mjini, Juma Kaboyonga aliitaka serikali kuharakisha ununuzi wa nyumba za NIC ambazo thamani yake ni Sh31.7 bilioni.

Mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mchumi alisema serikali haipaswi kucheza na NIC, hivyo ni lazima itafute fedha hizo ili kuliwezesha shirika kwenda kwa kasi zaidi.

Kaboyonga alidai kuwa kumekuwa na hujuma dhidi ya NIC na kuhoji kwamba "kama mashirika binafsi yanaweza, vipi NIC ya serikali ishindwe".

Alisema: "Ipo dhana kwamba mashirika ya serikali hayana wenyewe, lakini mimi nasema yana wenyewe na wenyewe ni wananchi, lazima NIC iangaliwe, iwezeshwe na ipewe mtaji."

Akijibu hoja mbalimbali, Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremia Sumari alisema serikali imepanga kuendeleza huduma nafuu na zenye ubora kutokana na kuamini NIC inaweza kujiendesha kwa faida zaidi.

Sumari alisema uamuzi huo wa serikali kupanga kutoa huduma bora na za gharama nafuu haumaanishi kuwa nchi inarejea kwenye ujamaa, bali ni kuangalia uwezo wa shirika na mahitaji ya Watanzania.

Kuhusu mtaji na mpango wa kununua nyumba za NIC kwa Sh31.7 bilioni, alisema hilo liko katika hatua nzuri na za mwisho na kuongeza: "Lakini hadi sasa nyumba hizi ni za serikali, kuna mahitaji ya nyumba kwa watumishi wetu kama waheshimiwa majaji n.k."

Dk Abdallah Kigoda, ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo, alisema katika majumuisho yake kuwa kuna umuhimu wa serikali kulipatia shirika kiasi hicho cha fedha.

Alisema:" Sioni tatizo kwa serikali kutoa au kukopa Sh31.7 bilioni kuokoa shirika kubwa la umma kama hili, nafikiri kuna umuhimu wa kulipatia kiasi cha fedha kwa sasa."

NIC iko katika kipindi cha mageuzi baada ya kuwepo mvutano kati ya serikali na bunge, hasa tathmini ya mali ambayo awali ilikuwa Sh18 bilioni, lakini Kamati ya Fedha ikaikataa na kutaka ifanyike upya.

Tathmini mpya iliyoonyesha kuwa thamani ya mali za NIC ni Sh31.7 bilioni ilikubaliwa na mwezi Februari, Rais Jakaya Kikwete aliunda Kikosi Kazi kilicho chini ya Balozi Charles Mutalemwa kufanya mageuzi ya shirika hilo.

Hadi Februari wafanyakazi waliokuwa nje ya ajira wakati huo walilipwa malimbikizo ya mishahara yao kwa jumla ya Sh1.90 bilioni.

CHANZO: Mwananchi

MBONA MAMBO!?


NDUGU YANGU Mpayukaji Msemaovyo anasema:

Naitwa Mchumiatumbo mwana wa Tapeli.

Ingawa wakati naandika waraka huu vijana wenzangu wapatao 166 wamo wakimenyeka toka Mwanza hadi Butiama, kama ishara ya kumbukizi ya safari yako adhimu ya ukombozi ukiliungua mkono marehemu azimio la Arusha, mimi sitafanya hivyo.

Nina sababu. Kwanza mimi ni mnafiki wala mjamaa kama wewe. Nina roho nyepesi hasa nionapo vitu kama pesa madaraka na sifa.

Mimi ni mbabaishaji na muongo; au msanii kama washikaji wasemavyo. Ni fisadi through and through. Ninanuka kiasi cha kutostahili hata kukaribia kaburi lako achia mbali nyumba yako, wanao, mkeo, watu wako hata taifa lako. Nisingependa walevi na wazinzi kufagia makaburi ya mitume mwalimu. Hivyo, kwanza nakuwa mkweli kwa nafsi yangu na kwako na umma wako.

Tatu, nitaunga mkono azimio lipi iwapo ninaoona wamenizunguka wakiwaibia watu wako ni wale wale walioliua azimio la Arusha? Nitaadhimisha vipi iwapo miiko ya uongozi na usawa wa binadamu vimetoweka na nafasi yake kuchukuliwa na ufisadi, ujambazi wa mchana, ubabaishaji na uongo?

Nne, mwalimu, sitaki kujidanganya na kukudanganya. Kile ulichopigania kwa sasa hakuna. Ulipigania uhuru na maendeleo. Sasa kuna utumwa na kuporomoka. Ulitekeleza ujamaa na kujitegemea. Sasa tuna uhujumaa na kujimegea. Ulipigania mstakabali wa nchi toka kwa wakoloni wawe wavumbuzi, wamisionari na watawala. Sasa mstakabali huo umo mikononi mwa wawekezaji, na wafadhili wa makuadi wao. Ulipigania ardhi ya Tanzania kabla haijaingia mikononi mwa vijifalme vya kifamilia. Nitakuenzi kwa udhu upi iwapo kila nipitapo Loliondo nakaribishwa kwenye falme za kiarabu utadhani hapa ni uarabuni?

Nitapata wapi mshipa wa kukuenzi wakati nakung’ong’a? Je mwalimu una habari? Yale madini uliyosema vizazi vijavyo vingeyaendeleza na kufaidika nayo yaliuzwa na jamaa yako Tunituni uliyempigia debe usijue jizi.

Tano, mwalimu siwezi kukuenzi wakati nakuchukia na kukudharau. Ningekupenda na kukuheshimu ningeshika urithi wako na kuheshimu wosia wako wa kupendana na kutohujumiana. Nakumbuka wakati ukianga dunia ulikuwa ukiwalilia watanzania wako baada ya kugundua makosa uliyofanya kuwaweka mikononi mwa nunda wala watu. Nami ni mmojawapo.

Je una habari mkoani mwako watu wameishamiminiwa risasi za moto kutokana na kukatiza kwenye ardhi ya mwekezaji na si mtanzania? Una habari mkoani mwako uchafuzi wa mazingira unatishia maisha ya ndugu zako? Hapa kweli nina sababu ya kukuenzi? Je kukuenzi ni matendo au maneno mwalimu?

Ingawa ukiwa kuzimu bado unaliletea sifa taifa langu, sifichi wala kuchelea kukwambia kuwa waliohai wanaliletea aibu na fedheha baada ya kulibinafsisha huku wakibinafsisha hata akili na roho zao. Mwalimu nilikufahamu sana . Ulikaa madarakani kwa kitambo kirefu ukiacha nyuma familia isiyo na ukwasi zaidi ya utu. Uliowawezesha wamefikia hata kuchukua ule mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira uliozawadiwa na rafiki yako Mao Tse Tung.

Mwalimu, vinyamna mwitu na mbwa hawa walitutenda kweli. Walitudanganya kuwa uwekezaji ndiyo sera na njia pekee ya kutukomboa tusijue walikuwa wakimaanisha kinyume. Wengine walituahidi maisha bora kwa wote tusijue wote ni wao washirika zao, watoto zao na wake zao hata nyumba ndogo zao. Tupo msambweni mwalimu wakati huu tunapozidi kuuzana na kuhadaana. Je unaweza kuamini kuwa kwa sasa hakuna tofauti ya polisi na kibaka? Nina ushahidi. Juzi polisi aliuawa kama kibaka na wananchi wenye hasira na kukata tamaa huku polisi tena wakubwa wakiwapiga risasi wafanyabiashara wakidai ni vibaka!

Wakati wa uongozi wako matupinkele au zeruzeru kwa lugha rahisi walikuwa salama. Baada ya kuingia pepo la utajiri usioulizwa ulivyopatikana, maskini hawa wanatolewa kafara na wanganga njaa wa kienyeji. Hivyo ndugu zetu hawa wanauawa hata zaidi ya swala mwalimu na hawana mtetezi zaidi ya vijikesi viwili vitatu vya kuondolea lawama. Tembo kwa sasa wana ulinzi madhubuti zaidi ya ndugu hawa.

Zama zako uliongoza. Uongozi ulikuwa utumishi wa umma na si uchumia tumbo na utumikishaji na uhujumu wa umma. Ikulu ilikuwa mahali patakatifu siyo pa deal. Uongozi ulikuwa uongozi na si uongo kama sasa. Siasa ilikuwa baraka si balaa kama sasa.

Wale watoto wa wachunga mbuzi na maskini wa kunuka uliowatoa kwenye umaskini na kuwasomesha sasa ni matajiri wa kutupwa. Yupo mpumbavu mmoja jizi aliyewahi kuita shilingi bilioni moja vijisenti ukiachia mbali wengine uliowaachia laana kuwa walikuwa wamejilimbikizia chumo la wizi. Na kweli maneno yako hayakuanguka. Kwani wezi wenzao waliwabeba na kuwakweza hatimaye tamaa zao na upofu vikawadondosha.

Mwalimu sitakuenzi,. Siwezi kujidanganya na kuidanganya dunia. Nitakuenzije iwapo kipato changu kinatokana na rushwa, uwekezaji, uuzaji mihadarati, uongo, ahadi hewa, uhujumu na mengine mengi yapinganayo na dhamira ya dira yako mwalimu?

Hivi kweli panya anaweza kumuenzi paka zaidi ya kufaidi ‘uhuru’ baada ya paka kuondoka? Je nune aweza kuishi nje ya kinyesi cha ng’ombe zizini? Si haki nune kuwa mwalimu wa usafi wakati mlo wake na makazi yake ni kwenye uchafu hata anenepe na kunawiri vipi.

Mwalimu naogopa kuja Butiama au kusimama mbele ya kadamnasi ya maadhimisho yako na kukupamba wakati nilisha kuvua nguo. Naogopa. Maana mama Maria hata wanao wananijua. Inawezekana nikakulamba uchogo na kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa kiasi cha kumkera mmojawapo akaamua kunizodoa na nikazidi kudhalilika ingawa niliishadhalilika muda mrefu.

Mwalimu ulikuwa na akili inayochemka. Yangu mimi ni bongolala. Ulikuwa msafi na mwadilifu. Mie ni mchafu sina mfano. Mkeo hakuwa akitumia ofisi yako kuubia umma. Mie wangu nami wote tu wezi. Nikiiba huku yeye anaibia kule. Hata watoto nimewaingiza. Nataka hata ikibidi wawe marais kama siyo mawaziri. Je hapa mwalimu nitakuwa na cha kukuenzi?

Mwalimu ulileta elimu bure kwa wote. Mie nashabikia kuchangia gharama ingawa kimsingi hakuna gharama za kuchangia zaidi ya kutunisha mfuko wa walaji wakubwa. Ulipigania ardhi. Mie natamani niwe rais niiuzie mbali nipate changu nifiche ughaibuni. Mwalimu ulichukia wafanya biashara wezi. Mie hawa ndiyo washitili wangu.

Mwalimu ulisisitiza usawa wa binadamu. Mie naamini binadamu si sawa wala si mfano wa Mungu kama wachungaji wasemavyo. Usawa ni mambo ya kizamani. Kwangu, heshima ya binadamu haitokani na ubinadamu wake bali pochi lake. Hukusikia wahenga wakisema mwalimu kuwa aso kitu si mtu bali kinyama mwitu? Mtu chake bwana. Kwa imani yangu mie si mfano wa Mungu bali mfano wa shetani kutokana na uroho na roho mbaya vyangu. Mungu si mwizi wala muongo wala mbabaishaji kama mimi mwalimu.

14 Oct 2009


Na Fredy Azzah

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa, amesema kashfa za ufisadi zinazowakabili baadhi ya viongozi wake, zimekiumbua chama hicho pamoja na serikali yake.

Akiwahutubia wanafunzi wa matawi ya CCM ya vyuo vikuu vilivyopo jijini Dar es Salaam, wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 10 ya kifo cha Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere jana, alisema ufisadi ambao umewakumba wengi umesababishwa na tabia ya viongozi kulindana na kutosimamia kikamilifu maadili ya uongozi yaliyoainishwa ndani ya katiba ya CCM.

Alisisitiza kuwa tabia hiyo ni kinyume na misingi ambayo Baba wa Taifa, aliwaachia Watanzania....ENDELEA

WAKATI HUOHUO

WASOMI na wanazuoni nchini, wamesema nchi haina dira na kwamba kuna mpasuko mkubwa ambao usiposhughulikiwa mapema, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko.

Wakizungumza juzi katika baraza lililopewa jina la Mbongi, lililoandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Julius Nyerere, walisema mpasuko hiyo ni pamoja na ya udini, ukabila, ukanda, matatizo ya vitambulisho Zanzibar pamoja na hofu ya kuvunjika muungano...ENDELEA

CHANZO: Mwananchi


Police recoup £1.4m from criminals in last two weeks as war on crime profits gathers pace



Oct 12 2009 by Rebekah Oruye, Birmingham Mail



WEST Midlands Police is driving home the message that crime does not pay after confiscating £1.4 million from criminals in the past two weeks.

In addition, nearly £100,000 in cash was seized from a car on the M6 in Birmingham, believed to have been intended for criminal use.

Det Chief Insp Simon Wallis, head of the force’s economic crime team, said: “This money has been taken from those who think crime is an easy way to make money.

“It brings West Midlands Police to a total of £15 million seized from criminals in the last 18 months.

“On many of these occasions through financial investigation and the confiscation process we are able to trace monies and give them back to victims. In cases where money is transferred abroad, it still is able to be retrieved. Crime does not pay. We will investigate those involved in criminality to ensure that they do not enjoy their ill gotten gains.”

Among the success stories for the police is the near £900,000 seized from Walsall conman Mponjoli Malakasuka, who had been stealing and exporting high powered luxury cars.

Malakasuka, aged 36, from the Yew Tree estate, was ordered to pay back the money in one month or face an additional four years in jail. He was originally sentenced to three-and-a-half years in July 2008 for conspiracy to steal.

Malakasuka had used a variety of sophisticated methods to steal prestige vehicles which he then exported out of the UK to Tanzania and Kenya. The cars were stolen both through car key burglaries and a variety of identity fraud and fake hire purchase agreements.

The cars included Mercedes Benz S320 CDi and Porsche Cayenne cars. In all over £300,000-worth of vehicles were stolen.

At the time of his arrest police discovered Malakasuka to be living a life of luxury in his four-bed house. At his address were pictures of luxury houses in Tanzania into which officers believed he had invested his fraudulent cash.

The court accepted the houses in Tanzania were proceeds of his criminality. Financial investigators were also able to show thousands of pounds passing through in excess of 70 bank accounts in the UK and Tanzania including one account which alone had £350,000. Det Sgt Jonathan Jones, who led the investigation for the Economic Crime Team, said: “This has been a great investigation, as not only have we stopped fraud and theft, but we have now recovered the profit that this man made from his criminality.”

In a separate case a money launderer from Birmingham was ordered to pay back more than £450,000 of his criminal profit.

Barrington Fulcott, aged 48, from Kingstanding, was told to pay £450,386 at the hearing in Birmingham Crown Court.

He was given six months to return the cash, or face an extra four years in prison. Fulcott was originally sentenced to 42 months in prison in February 2008 in relation to three counts of money laundering.

He had gathered considerable wealth from his criminal activity which had allowed him to purchase five properties in the West Midlands and begin the development of a large home in St Annes, Jamaica.


13 Oct 2009


WAKATI TUNAADHIMISHA KIFO CHA MWASISI WA TAIFA LA TANZANIA,MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE,TUNAPASWA PIA KUTAFAKARI MAMBO KADHAA AMBAYO KWA KIASI KIKUBWA HAYAKUPATA FURSA YA KUJADILIWA WAKATI WA UHAI WA NYERERE,NA KUYAJADILI BAADA YA KIFO CHAKE INAWEZA KUTOA TAFSIRI POTOFU YA UTOVU WA NIDHAMU.

MENGI YAMEONGELEWA KUHUSU MCHANGO WA NYERERE KATIKA HARAKATI ZA UHURU WA TANGANYIKA,NA NDOTO YAKE YA UMOJA ILIYOZAA TAIFA LA TANZANIA KWA KUUNGANA NA ZANZIBAR,PAMOJA NA MCHANGO WA TANZANIA KATIKA MAPAMBANO YA UHURU KUSINI MWA BARA LA AFRIKA.

BAADHI YA MISINGI ALIYOJENGA NYERERE BADO IPO LICHA YA JITIHADA KUBWA ZA "WANAFUNZI WAKE" KUIBOMOA.WATANZANIA BADO TUNASIFIKA KWA NAMNA TUNAVYOTHAMINI UNDUGU WETU (USHAHIDI UKIWA NENO "NDUGU" KABLA YA MAJINA YETU JAPO WAWAKILISHI WETU BUNGENI WANAITWA WAHESHIMIWA).

KAMA KATUNI YA KIPANYA INAVYOONYESHA HAPO JUU,NYERERE PIA ALITUFANYA TUWE WAPOLE KUPITA KIASI.UPOLE HUO ZAMA ZA CHAMA KIMOJA ULIIMARISHWA NA SHERIA ZILIZOTULAZIMISHA KUAMINI KUWA KIONGOZI YUKO SAHIHI WAKATI WOTE.MADHARA YA IMANI HIYO NI HUJUMA INAYOFANYA NA BAADHI YA WANASIASA KUAHIDI MAMBO WASIYOWEZA KUTEKELEZA LAKINI KWA VILE WATANZANIA NI WAPOLE,NA WANAOAMINI KILA ASEMACHO KIONGOZI,WAMEENDELEA KUTUTAWALA NA SI AJABU WAKAENDELEA KUTUTAWALA ZAIDI.WANAFAHAMU KUWA WANAOWATAWALA HAWANA JEURI YA KUHOJI AHADI ZISIZOTEKELEZEKA ACHIULIA MBALI VITENDO VYA UFISADI VINAVYOFANYWA NA WATEULE WA VIONGOZI HAO.

PAMOJA NA HESHIMA YANGU KUBWA NILIYONAYO KWA BABA WA TAIFA,NALAZIMIKA KUMLAUMU KWA UZAZI NA KULEA TABAKA AMBALO LEO HII TUNALIITA MAFISADI.SIAMINI KABISA KUWA BAADHI YA WANAFUNZI WA MWALIMU WALIKURUPUKA GHAFLA KUWA MATAJIRI KUPINDUKIA HUKUN WAKIKUMBATIA WAGENI NA MARAFIKI ZAO.NAAMINI KUWA WATU HAWA HAWAKUWAHI KUWA WAJAMAA JAPO WALIIMBA NA KUCHEZA UJAMAA MAJUKWAANI WAKIWA NA MWALIMU.

TUMWANGALIE MTU KAMA KINGUNGE NGOMBALE MWIRU.HUYU ALIKUWA SWAHIBA WA MWALIMU NA TULIAMBIWA KUWA DINI YAKE NI UJAMAA.HIVI KWELI KINGUNGE AMEBADILIKA GHAFLA KUWA MTETEZI WA MAFISADI AU ALIKUWA ANAMZUGA TU MWALIMU ZAMA ZA UTAWALA WAKE?

BAADHI YA MADUDU TUNAYOSHUHUDIA LEO YALIANZA ZAMA ZA MWALIMU.KULIKUWA NA KIJITABIA CHA MTU AKIHARIBU HAPA ANAHAMISHIWA PALE,KAMA AMBAVYO AKINA MATTAKA WALIVYOSHINDWA KUIOKOA TRC LAKINI WAKAPELEKWA BIMA.SI KWELI KWAMBA NYERERE HAKUENDEKEZA URAFIKI,MAANA ISINGEKUWA HIVYO BASI ASINGEMPIGIA DEBE MKAPA,RAIS AMBAYE BAADA YA KUTOKA IKULU AMEACHA WATANZANIA WENGI WAKISHANGAA KWA NAMNA ALIVYOTUMIA FURSA HIYO KUJITAJIRISHA (REJEA ISHU YA KIWIRA).

BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA ZA AFRIKA WANAMTUHUMU MWALIMU KUWA WAKATI ANASTAAFU MWAKA 1985 ALIACHA TAIFA LIKIWA KATIKA HALI MBAYA SANA KIUCHUMI.KUNA WANAODAI KWAMBA UAMUZI WA KUNG'ATUKA UNAOPIGIWA MSTARI KAMA MFANO WA KUIGWA ULIKUWA MATOKEO YA KUKWEPA MAJUKUMU.WAPO WANAOKWENDA MBALI ZAIDI NA KUDAI KWAMBA MWALIMU ALIPASWA KUWAOMBA MSAMAHA WATANZANIA KWA KULIFIKISHA TAIFA LILIPOFIKA WAKATI ANASTAAFU.

HATA SIASA YA UJAMAA NAYO IMEZUA MJADALA KWA BAADHI YA WACHAMBUZI WA SIASA.KUNA WANAOONA KUWA NYERERE ALIKUWA MUUMINI PEKEE WA ITIKADI HIYO HUKU AKIWA AMEZUNGUKWA NA KUNDI LENYE BAADHI YA MATAPELI WA KISIASA WALIOKUWA WANAMUUNGA MKONO JAPO NAFSINI MWAO WALIKUWA NA MAWAZO TOFAUTI.NA MFANO UNAOREJEWA MARA NYINGI NI UAMUZI WA KUUA AZIMIO LA ARUSHA MARA BAADA YA MWALIMU KUTOKA MADARAKANI NA KULETA AZIMIO LA ZANZIBAR.

TATIZO JINGINE LA UJAMAA LIKO KWENYE UKWELI KWAMBA ULIKUWA MITHILI YA JARIBIO,AMBALO KWA KIASI KIKUBWA HALIKUFANIKIWA HADI MWALIMU ANAONDOKA MADARAKANI.KUTOKUFANIKIWA HUKO KULICHANGIWA NA NAMNA UJAMAA ULIVYOSAMBAZWA,AMBAPO MATUMIZI YA NGUVU YALIKUWA JAMBO LA KAWAIDA.REJEA NAMNA OPERESHENI VIJIJI VYA UJAMAA ILIVYOWAATHIRI BAADHI YA WATANZANIA KWA KUONDOLEWA MAHALA WALIPOJIJENGA NA KUPAZOWEA NA KUPELEKWA "UGENINI."HOJA HAPA SI KWAMBA WAZO LA UJAMAA LILIKUWA ZURI AU BAYA BALI KAMA LILIKUWA LINATEKELEZEKA HASA IKIZINGATIWA KWAMBA TANZANIA ILIKUWA TEGEMEZI KIUCHUMI TANGU ILIPOPATA UHURU WAKE 1961.

KUDHANI KWAMBA MAFISADI WALIIBUKA GHAFLA NI KUKWEPA KUDADISI CHANZO CHA TATIZO.MAFISADI WENGI NI TABAKA LILILOIBUKA MIAKA YA MWISHO WA HARAKATI ZA UHURU NA BAADA YA KUPATIKANA UHURU.NI KIKUNDI CHA WARASIMU WALIOTUELEKEZA NAMNA YA KUFANYA JAPO WAO WENYEWE HAWAKUFANYA HIVYO.TABAKA HILI LILIKUWA LINASUBIRI MWALIMU AONDOKE MADARAKANI LIANZE "KUFANYA VITU VYAKE",AND SURE THEY DID!

NYERERE ALIZUNGUKWA NA LUNDO LA WANAFIKI.KISICHO NA HAKIKA NI KAMA ALIFAHAMU UNAFIKI WAO NA KUWAVUMILIA AU WALIMZIDI AKILI.YOTE MAWILI HAYAMTOI LAWAMANI KWA VILE PINDI KIONGOZI ANAPOCHAGUA WASAIDIZI WENYE MAPUNGUFU,AIDHA KWA KUTOJUA AU KWA MAKUSUDI,NI LAZIMA ABEBE LAWAMA KWA UTEUZI MBOVU.

UJAMAA,REGARDLESS YA KUWA ITIKADI YA MAJARIBIO,UNGEWEZA KUZAA MATUNDA MEMA IWAPO UNGEGUSA KILA MTANZANIA PASIPO KUJALI NAFASI YAKE KATIKA JAMII.NI DHAHIRI KUWA LAITI HILO LINGETIMIA BASI TUSINGESHUHUDIA AWAMU YA PILI (BAADA YA NYERERE) IKIENDESHA TAIFA KWA MTINDO WA LAISSEZ FAIRE (BORA LIENDE) NA AWAMU YA TATU IKITUAMINISHA UJIO WA ZAMA ZA UWAZI NA UKWELI HUKU WATU WANAUZIANA MGODI WA KIWIRA KWA BEI YA KISHKAJI.YA UFISADI KILA MMOJA WETU ANAFAHAMU HALI ILIVYO.

KWA VILE MIE NI MKRISTO,NA KWA VILE MILA ZETU ZINAKATAZA KUWASEMA VIBAYA MAREHEMU,BASI NAUNGANA NA WATANZANIA WENZANGU KUMTAKIA MWALIMU PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE,APUMZIKE KWA AMANI,AMINA.HATA HIVYO,KAMA SIE WAKATOLIKI TUNAVYOAMINI KUWA ROHO ZA MAREHEMU ZIKO "HAI" TUKIZIKUMBUKA KWA SALA,BILA SHAKA MWALIMU ANAJUTA KUCHAGUA "MARAFIKI" AMBAO BAADA YA KUONDOKA KWAKE WAMEGEUZA TANZANIA KUWA SHMBA LA BIBI,WANACHUMA WATAKAVYO,WANAKWIBA WATAKAVYO,LAKINI KWA VILE ALITUGEYUZA WAPOLE NA WAGUMU KUDAI HAKI ZETU,TUNAENDELEA KUVUMILIA MACHUNGU.

MWISHO,KWA VILE LAWAMA PEKEE HAZIWEZI KUSAIDIA KUTUFIKISHA TUENDAKO,JUST LIKE MAKALA NDEFU ZA KUMBUKUMBU YA MWALIMU ZISIVYOWEZA KUWAKWAMUA WALALAHOI,NI MUHIMU KUITUMIA SIKU HII KUJIULIZA SWALI HILI MUHIMU.JE NYERERE NA WAPIGANIA UHURU WENZAKE WALIPAMBANA NA MKOLONI KWA MINAJILI YA KUMUONDOA MTU MWEUPE NA KUMUWEKA MKOLONI MWEUSI (MAFISADI,et al)?

ANGALAU MKOLONI ALIKUWA NA EXCUSE YA KUTUNYONYA NA KUTUPELEKESHA.HAKUWA MTANZANIA,HAKUWA NA UCHUNGU NA NCHI HII,NA HAKUFIKISHWA ALIPOFIKIA KWA JITIHADA ZA WATANZANIA.LAKINI MAFISADI NI WATANZANIA WENZETU,WANALAZIMIKA KUWA NA UCHUNGU NA NCHI YETU KWA VILE KWA VYOVYOTE VILE BAADHI YA WAATHIRIKA WA UFISADI WAO NI NDUGU ZAO WA MBALI (WA KARIBU WAMESHATENGENEZEWA ULAJI SOMEWHERE).

NJIA BORA YA KUMUENZI MWALIMU NI KUREKEBISHA PALE ALIPOKOSEA (KWA MFANO KUWALEA VIONGOZI WALIOMZUGA KUWA NI WAJAMAA LAKINI WAKAGEUKA MAFISADI MARA BAADA YA KUONDOKA KWAKE) NA KUIANGALIA TANZANIA KAMA NCHI YETU SOTE NA SI YA WATEULE WACHACHE (AMBAO MARA NYINGI HAWATAKI KUSIKIA SAUTI TOFAUTI NA YAO UNLESS IWE NI VIGEREGERE AU MAKOFI YA PONGEZI).TUMUENZI MWALIMU KWA KUKATAA NCHI YETU KUWA SHAMBA LA BIBI HUKU WAWEKEZAJI UCHWARA WAKIJA NA BRIEF CASES TUPU NA KUONDOKA WAKIWA MAMILIONEA.TUKATAE WEZI KAMA WA KAMPUNI YA KAGODA NA MATAPELI KAMA WA RICHMOND,NA UJAMBAZI KAMA WA MEREMETA,TANGOLD,NK KUENDELEA HUKU WAHUSIKA WAKITUPUUZA KWA KUGOMA KUTUELEZA UKWELI.


BONYEZA PICHA KUIKUZA NA KUSOMA STORI



Hivi karibuni niliandika makala flani kuhusu milipuko ya mabomu huko Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kwa kutambua kuwa blogu yangu haina idadi kubwa ya wasomaji (japo nawathamini sana wachache wanaotumia muda wao kuitembelea) niliamua kuisambaza makala hiyo kwa bloga wenzangu wawili ambao “nyumba” zao hupata “wageni” wa kutosha kila siku.

Kwa bahati mbaya, bloga hao waliamua kuiweka makala hiyo kapuni.Siwalaumu,kwa sababu kadhaa. Kwanza, blogu ni mali ya mmiliki, na hilo linampa haki ya kuchagua nini kiwepo kwenye blogu yake na nini kisiwepo.Pili, kila bloga ana mtazamo wake kuhusu mambo mbalimbali yanayotuzunguka, iwe siasa, dini au nyanja nyingine za maisha ya binadamu. Kwa maana hiyo, kama ataletewa makala inayokinzana na mtazamo huo, ana haki ya kuipuuza. Kuna sababu nyingine za kibinafsi lakini sidhani kama zina umuhimu sana.

Makala husika (isome hapa) haikuwa ya matusi, kashfa au utovu wa nidhamu kwa watawala japo ilikuwa ikizungumzia uzembe na kutowajibika kwa baadhi ya viongozi wetu unavyohusika na janga hilo la milipuko ya mabomu.Nilishauri katika makala hiyo kwamba wakati umefika kwa Watanzania kudai haki zao hasa pale zinapopuuzwa makusudi. Kwamba ripoti ya milipuko ya kwanza inaozea katika makabrasha ya Wizara husika, kisha mlipuko mwingine unatokea lakini hakuna anayewajibika, jambo linalohitaji shinikizo la kudai haki na uwajibikaji.

Naamini kwamba laiti makala hiyo ingechapishwa laiti ingekuwa ya kumsifia kiongozi flani au kukumbushia tarehe yake ya kuzaliwa. Au laiti ingekuwa ni tangazo binafsi. Yote hayo ni mazuri kwa vile ni huduma kwa umma. Hata hivyo, harakati tunazohangaika nazo wengine kuboresha future ya nchi yetu ni muhimu pia na hazipaswi kupuuzwa.

Ni rahisi kwangu kuhitimisha kwamba kinachokwanza makala za aina hiyo kuchapishwa ni uoga wa mabloga husika wakihofia kuwaudhi watawala. Japo huo ni uhuru wao kibinadamu, madhara yake kwa jamii ni makubwa kwa vile historia inaonyesha kwamba uoga ni kitalu mwafaka kwa ushamiri wa tawala dhalimu.

Lengo langu si kulaumu bali kushauriana.Kukimbilia kuweka picha za kiongozi akihutubia au akirejea Dar akiwa bukheri wa afya lakini kuchelea kujumuisha maelezo kwamba pia alikumbwa na dhahama ya kiafya ni kutowatendea haki wasomaji wetu. Hapa narejea tukio lililotokea jijini Mwanza hivi karibuni ambapo baadhi ya wenzetu walitonyesha “picha nzuri” za JK lakini “wakabania” maelezo kuhusu mkasa uliomkumba wa kushindwa kuendelea na hotuba yake katika kile kilichoelezwa kuwa “uchovu wa safari.”

Ushirikiano wetu jumuiya iliyojibebesha dhamana ya kuujulisha umma kuhusu mambo mbalimbali usiishie kwenye yanayopendeza machoni pekee bali pia yale yanayoudhi au kukera.

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.