20 Jun 2010

Instead of counting candles,
Or tallying the years,
Contemplate your blessings now,
As your birthday nears.
Consider special people
Who love you, and who care,
And others who’ve enriched your life
Just by being there.
Think about the memories
Passing years can never mar,
Experiences great and small
That have made you who you are.
Another year is a happy gift,
So cut your cake, and say,
"Instead of counting birthdays,
 Count blessings every day!"

18 Jun 2010

ZIARA ya Rais Jakaya Kikwete mkoani Kigoma jana ilipata mushkeli baada ya gari moja kupinduka wakati msafari wake ukitokea Kibondo kuelekea Kigoma Mjini.

Rais Kikwete, ambaye msafara wake umekuwa ukikumbwa na matukio ya hatari katika muda wa wiki tatiu, alikuwa anaenda Kigoma Mjini kuhitimisha ziara yake hiyo ya siku tatu mkoani hapa.

Awali matukio mawili yaliyoukumba msafara wake yaliyuhusu magari ya Ikulu, likiwemo gari alilopanda wakati akiwa ziara ya wiki moja jijini Dar es salaam ambalo lilichomoka tairi muda mfupi baada ya kushuka, lakini ajali ya jana ilihusu gari la CCM mkoani Kigoma.
. Soma habari kamili HAPA.

17 Jun 2010

Desemba 9 mwakani,Tanzania yetu itatimiza miaka 50 tangu ipate uhuru.Pengine tarakimu 50 inapunguza uzito,kwahiyo ni vema kubainisha kuwa umri huo ni sawa na NUSU KARNE (herufi kubwa kuonyesha msisitizo).Wakati umri huo wa mtu mzima ungepaswa kuwa habari njema,hali ni tofauti kwetu.Tulowakabidhi dhamana ya kutuongoza wanakurupuka na mambo ya ajabu ajabu kana kwamba wako ndotoni au wako kwenye mchezo wa kuigiza usio na ujumbe wowote.

Ngoja niende moja kwa moja kwenye pointi.Hivi Mtanzania mwenzangu inakuingia akilini kweli kusikia kauli kwamba jengo la Bunge letu tukufu "litafanyiwa ukarabati wa kufa mtu" unaotarajiwa kugharimu shilingi bilioni 30.9 "ili kuwawezesha waheshimiwa sana waendane na teknolojia ya kisasa wanapokuwa Bungeni"!!!?Kwa mujibu wa Spika Samuel Sitta mchakato wa ukarabati huo umeshakamilika na unatarajiwa kuanza mara moja,ambapo utapokamilika kila kiti cha mbunge kitakuwa na runinga pamoja na mawasilino ya kisasa ya kompyuta.

Ofkozi,ni muhimu kwenda na wakati katika suala zima la teknolojia lakini pamoja na umuhimu huo shilingi bilioni 30 na ushee ni nyingi mno na tunazihitaji kwenye maeneo mengine yaliyo hio bin taaban kama vile miundombinu,huduma za afya,maji,nk.Hivi kweli runinga kwenye kiti cha mbunge ni muhimu kuliko madawati au nyumba za walimu?Je hizo bilioni 30 zingeweza kujenga zahanati ngapi au visima vingapi vya kuwapatia walalahoi huduma ya maji ya uhakika?

Lakini kabla sijatuliza hasira zangu kutokana na kauli hiyo ya Spika Sitta,JK nae amekuja na mpya akidai kwamba katika miaka mitano ijayo kila mwalimu atakuwa na laptop.Namheshimu sana Rais wangu lakini baadhi ya kauli zake zinanitatiza sana.Hivi kipaumbele katika elimu yetu ya kusuasua ni laptop kwa walimu au makazi bora kwa walimu hao sambamba na kuboreshewa maslahi yao na mazingira yao ya kazi?Mwalimu mwenye laptop anafundishaje wanafunzi waliokaa chini ya mti?Na wakati JK anatoa mpya hiyo hajatuambia umeme wa kuziwezesha laptop hizo utakuwa wa nguvu za jua au zitatumia mafuta ya taa kwani sote tunafahamu uhuni wa TANESCO.


Sijui ni uzembe wa watawala wetu kuelewa matatizo yetu na vipaumbele vyetu kama taifa au ni makusudi tu lakini kwa mwenendo huu itatuwia vigumu kutembea vifua mbele hapo mwakani tutaposherehekea nusu karne tangu tupate uhuru. 

Enewei,hebu soma mazingaombwe hayo HAPA na HAPA.

16 Jun 2010

Having lived in Scotland for nearly a decade,I quite understand why a Scottish football legend is not happy with the inclusion of foreign born players in national teams.The Scots are so proud of their identity that some of their sentiments could easily be mistaken for racism.However,although one could finds racists almost throughout the world,Scotland is generally a very welcoming countries to foreigners.

Hendry was quoted in the Daily Record stating categorically that he would rather see Scotland not reach another World Cup final than "play a fraud like Cacau".He was referring to a Brazilian-born German striker,Claudemir Jeronimo Barretto,commonly known as Cacau,who qualified to play for the Germans because their rules allow for naturalisation after two years' residence in the country.

The Scottish legend who captained Hendry, who captained Scotland at France '98, would "rather go down in history with the distinction of being the last man to do that than see his homeland become a haven for uncapped players".

"Every time I went out on the park to play for Scotland I regarded it as going to war for my country", said Hendry and made it clear that the sight of a German team with one Brazilian and three other players who were born in Poland beating Australia was unappealing to him.

I am certainly sure that even after the Swiss victory over Spain with their sole goal coming from a Cape Verde-born Gelson Fernandes,Hendry, with his Scottish Highland upbringing, which represents tradition, heritage and refusal to make nationality an administrative matter,would change his opinion on the the inclusion of foreign born players in national teams.

In my opinion,however,Scots might as well continue to face humiliation in international football should mentality such as Hendry's continue to dominate.I understand the importance of national integrity and identity when it comes to national teams but in football,like in many other sports,winning is everything.It is a result driven business,and when a team wins,identities of those who made such a victory possible is obviously immaterial.

With globalisation bringing people of different background even closer,it is quite hard to pretend that foreign born citizens have a lesser status and role to play in their current nationalities.Why should the issue of national identity be confined to football when we see how many foreign born GPs saving lives in hospitals?If Hendry is comfortable to be served by a foreign born doctor or nurse,why would he feel that a foreign born German player is "a fraud"?

It's important to embrace our diversity and integration by allowing the few who were not born in Scotland to give something to this country they now call home.It would not in any way whatsoever make "a pure Scots" like Hendry less Scottish,just like the goals scored by the likes of Hendrik Larson didn't make Celtic less Scottish.

And HERE is the Daily Record article in question.

15 Jun 2010

Wakati Waingereza wanasubiri Bajeti ya Dharura ya Serikali mpya iliyoingia madarakani hivi karibuni,watawala hapa wameweka bayana kuwa baadhi ya hatua zitakazochukuliwa kurekebisha uchumi zitapelekea machungu kwa wananchi wengi.Hakuna haja ya kudanganyana kwa vile hata wangeficha ukweli huo,muda wa makali hayo ukifika watawala wangeumbuka.Na ni vema pia kuwatayarisha wananchi ili pindi hali itapokwenda mrama wawe katika tahadhari na wamejiandaa vya kutosha.

Lakini kwa watawala wetu,kusema ukweli ni kama kujivunjia heshima.Na si kwa wao tu,bali hata wananchi wanapoamua kuweka bayana hisia zao kuwa nchi yetu inapelekwa pabaya,watawala wanaona kama wanakosewa heshima.Kilichopelekea niandike makala hii ni kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuwa ahadi ambazo hazijatekelezwa katika miaka minne iliyopita zitatekelezwa katika bajeti hii.Sijui ni ushauri mbovu wa washauri wake,sijui ndio kampeni,au sijui ni kuwafanya Watanzania mabwege sana,lakini kwa kila anayefahamu hali ya uchumi wetu na wingi wa ahadi zilizokwishatolewa ni dhahiri kuwa kauli hiyo sio ya kweli.

Kikwete anapaswa kurejea ahadi alizotoa wakati wa kampeni zake mwaka 2005,na alizoendelea kutoa katika miaka minne iliyopita,kisha angejaribu kuangalia nini kimekwaza ahadi hizo.Hebu kwa minajili ya makala hii tuangalie baadhi ya ahadi hizo na kutathmini kama kweli bajeti hii ya kutegemea hisani za wafadhili itaweza kutimiza ahadi hizo.JK alinukuliwa mwezi August 2008 akisema tatizo la umeme lingepatiwa ufumbuzi wa kudumu.Miezi michache baadaye ufumbuzi ukapatikana,si kwa wananchi bali kwa akaunti za matapeli wa Richmond.Je ni kweli kuwa bajeti hii itaweza kutimiza ahadi hiyo ya JK kuhusu tatizo la umeme?Na mbona hatuelezi utatuzi huo utakuwaje?

Twende kwenye suala la rushwa na ufisadi.JK alitamka bayana kuwa watu wasitafsiri vibaya tabasamu lake kwani hatakuwa na huruma kwa fisadi yoyote yule.Akaenda mbele zaidi kutanabaisha kuwa anawafahamu wala rushwa na anawapa muda wa kujirekebisha.Sote tunajua kinachoendelea katika Awamu hii ya Nne chini ya JK.Ufisadi umeota mizizi kupita kiasi huku mafisadi wakiendelea kulindwa,na wanaojiuzulu wanafarijiwa kuwa "kuna siku watarejea serikalini".Hivi ni kweli kuwa bajeti hii itawezesha utekelezaji wa ahadi hiyo ya JK kupambana na mafisadi?Kilichomshinda katika miaka minne iliyopita kitawezekanaje miezi hii michache kabla ya uchaguzi?Na je inahitaji bajeti moja kabla ya uchaguzi kumwezesha kuwadhibiti mafisadi?


Anyway,hebu soma kauli zake katika habari ifuatayo kisha ufanye tafakuri jadidi 



Ahadi za JK kukamilika Bajeti hii
Imeandikwa na Na Maulid Ahmed, Dodoma; Tarehe: 12th June 2010 @ 23:52

Ahadi ambazo hazijatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Nne zitatekelezwa katika Bajeti hii ya mwaka 2010/11, imeelezwa.

Akizungumza jana mjini hapa katika kikao cha kazi na wakuu wa mikoa na wa wilaya pamoja na makatibu tawala wa mikoa yote Tanzania Bara, Rais Jakaya Kikwete aliwataka viongozi hao kusimamia shughuli za Serikali kikamilifu.

Aliwataka kutokwenda likizo katika kipidi hiki cha kuelekea uchaguzi na wasimamie kazi kama wanavyofanya wakati wote.
Rais Kikwete alisema katika kipindi cha miaka mitano tangu Serikali yake iingie madarakani mengi waliyoahidi yametekelezwa.

“Juzi kabla ya Bajeti hata kwenye Baraza la Mawaziri, tulizungumzia ahadi zetu na nyingi tumeshazitekeleza, lakini zilizobaki na majukumu tuliyojipangia kwa miaka yote hii tutatekeleza katika Bajeti hii … tulipoingia mwaka wa kwanza, tulitekeleza ya Awamu ya Mzee Mkapa (Rais mstaafu Benjamin) sasa tunaendelea na kutekeleza yetu,” alisema.

Akizungumzia uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu, alisema “tunakwenda kwenye uchaguzi na michakato imeshaanza, lakini Serikali haiendi likizo, usione uchaguzi nawe ukaenda likizo, fanya shughuli za maendeleo kwa kuzisimamia kama mnavyofanya wakati wote”.

Alisema hataki kuona uchaguzi unaharibikia mikononi mwa viongozi hao na kuwataka kuhakikisha wagombea hawanyimwi haki ya kumwaga sera zao majukwaani, kura zinapigwa kwa amani na kunakuwa na utulivu wakati wote, kuanzia mchakato wa wagombea hadi uchaguzi.

Rais Kikwete aliyehutubia viongozi hao kwa dakika 10, alitaja baadhi ya mafanikio ya Serikali yake, kuwa ni kuendelea na ujenzi wa barabara za lami, watoto kusoma elimu ya msingi na sekondari, upanuzi wa elimu ya juu na huduma bora za afya kupatikana...

CHANZO: Habari Leo

Japo mie si mchambuzi mzuri wa soka lakini naamini utaafikiana nami kuwa Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini zimeendelea "kuboa" wapenzi wa soka.Majuzi tumeshuhudia Waingereza walivyopelekeshwa na vijana wa Obama,huku kipa wao akiingia kwenye vitabu vya historia kama kituko cha mwaka.Kati ya wawakilishi wetu sita wa Bara la Afrika,ni Ghana tu waliotupa raha japo kwa ushindi kiduchu.Wenyeji South Afrika walilazimishwa sare (huku wakionyesha bayana kuwa ni wasindikizaji tu),Nigeria wakatutia machungu zaidi kwa kuonyesha kiwango duni dhidi ya Argentina (ambao nao hawakuonyesha kiwango kilichotarajiwa),Cameroon ndio wakatukata maini kwa kiwango cha chini kabisa cha soka huku Algeria wakifanya kilichotarajiwa (wasindikizaji).Matumaini ya Afrika sasa yamebaki kwa Ivory Coast wanaoingia dimbani mchana huu (kwa mida ya hapa Uingereza).


JapoUjerumani na Uholanzi, vigogo wengine wanaotarajiwa kufanya vizuri kwenye michuano hiyo,wameshaonyesha makali yao huku tukisubiria kuwaona Brazil,Uhispania na Ureno,sare ya Italia kwa Paraguay imeacha maswali kama Wataliano ni tishio kweli kama ilivyotarajiwa,japo wanafahamika kwa tabia yao ya kubadilika kadri michuano inavysonga mbele.

Kwahiyo,kwa kifupi hadi sasa Fainali hizo zinaweza kuelezwa kama "zinaboa" kwa kiasi flani japo ni mapema mno kufikia hitimisho hilo.By the way,hii ni wiki ya kwanza tu na kuna timu kadhaa ambazo hazijaingia dimbani.Yote katika yote,mshindi bayana katika kinyang'anyiro hicho ni VUVUZELA,matarumbeta yanayoendelea kutawala vichwa vya habari kuhusiana na michuano hiyo.

Wakati kuna "kelele" (mithili ya hizo za Vuvuzela) kwamba matarumbeta hayo yanakera huku wengine wakitaka yazuiliwe,Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) na waandaaji wa michuano hiyo wameweka bayana msimamo wao kuwa Vuvuzela ni sehemu muhimu katika michuano hiyo.Ni utamaduni wa wenyeji,na kama tunavyofahamu "ukienda kwa Warumi inabidi uishi kama Warumi".Hata hivyo,tayari hatua kadhaa zimeanza kuchukuliwa dhidi ya kelele za Vuvuzela.Kituo cha runinga cha BBC kinachoonyesha michuano hiyo kwa hapa Uingereza (wakipokezana na ITV ya hapa) kina mpango wa kuwezesha watazamaji kubonyeza kitufe chekundu kwenye runinga zao ili "kuondokana na kelele za Vuvuzela" baada ya kupokea malalamiko 545 kutoka kwa watazamaji wanaodai kuwa matarumbeta hayo "yanawazingua".

Kadhalika,kampuni inayotengeneza Vuvuzela imetangaza aina mpya ya matarumbeta hayo ambayo itakuwa na "kelele pungufu",hatua inayotarajiwa kupunguza malalamiko zaidi.Jana,mchezaji Robin van Persie wa Uholanzi alionekana akilalamika kwa refarii kuwa hakusikia firimbi kuwa ameotea kutokana na kelele za Vuvuzela.Kadhalika,kipa wa timu ya Denmark Thomas Sorensen alieleza kuwa angetumia lugha za alama (sign language) kuwasiliana na wachezaji wenzie kwa vile Vuvuzela "zilikuwa zikimeza sauti yake".Mwanasoka wa Ureno,Christiano ametamka bayana kuwa angependa kuona Vuvuzela zikipigwa stop katika michuano hiyo.


Na kama wasemavyo Waswahili kuwa "kufa kufaana",tayari kuna "wajanja" wameibuka kutengeneza faida kutoka kwa wanaokerwa na kelele za Vuvuzela.Kampuni moja ya Ujerumani inaripoti kuwa imevumbua "teknolojia ya kuchuja kelele za Vuvuzela"ambapo mtazamaji akichomeka kidude kiitwachoSurfpoeten kwenye runinga yake,basi makelele ya Vuvuzela yanakuwa kwishne (angalia picha ifuatayo).
Lakini wakati hayo yakitokea,umaarufu wa Vuvuzela unazidi kupaa kiasi cha baadhi ya watu kuhisi kuwa bila kujali yeyote atakayetwaa ubingwa katika Fainali hizo,mshindi halisi atabaki kuwa Vuvuzela.Inaripotiwa kuwa supamaketi maarufu hapa Uingereza,Sainsbury,imeshauza Vuvuzela 22,000 katika masaa 12 ya mwanzo wa mashindano hayo na mchezaji wa Timu ya Taifa ya Uingereza Jamie Carragher ameshanunua Vuvuzela mbili kwa ajili ya wanawe.Kadhalika,inatarajiwa kuwa msimu ujao wa Ligi Kuu ya hapa utashuhudia Vuvuzela kadhaa kwenye mechi mbalimbali.Wachezesha kamari wa Paddy Power wanaendesha kamari ya kubashiri timu gani itakuwa ya kwanza kuuza matarumbeta hayo kwa mashabiki wake huku Manchester United wakiongoza kwa turufu ya 4/1.

Na katika kuthibitisha kuwa Vuvuzela imejichukulia umaarufu mkubwa,tayari kuna app ya Vuvuzela kwenye simu ya kisasa ya iPhone.Well,kama kuwepo kwa app hiyo hakujakuonyesha umaarufu wa Vuvuzela,idadi ya dowloads yaweza kukushawishi kwani tayari apps 750,000 (yaani robo tatu ya milioni) za Vuvuzela zimeshakuwa downloaded tangu ilipozinduliwa.Inatarajiwa kuwa Vuvuzela app (angalia picha yake hapo chini) itaweza kutumika kwenye iPad na iPod.


Mwisho,kama kuna watu wananufaika vya kutosha na vuguvugu la Kombe la Dunia basi ni Rais wa TFF Leodgar Tenga na wababaishaji wenzake waliojiingiza mkenge kuialika Brazil kisha kuambulia kipigo cha magoli matano na hasara ya bilioni kadhaa.Hata hivyo,licha ya usahaulifu wa kawaida wa Watanzania,michuano hiyo inawasaidia sana akina Tenga kwa vile macho ya mashabiki wengi wa soka wa Tanzania yameelekezwa huko Afrika Kusini na hivyo kusahau kuhusu deni walilobebeshwa na akina Tenga.Ni dhahiri kuwa michano hiyo itapomalizika mwezi ujao,habari ya hasara na deni hilo itakuwa imezikwa na kusahaulika kabisa.

13 Jun 2010


Picha na Habari (bonyeza hapa uisome) kwa Hisani ya MICHUZI

10 Jun 2010

Uandishi wa blogu si jambo rahisi kama inavyodhaniwa na wengi.Na ni jambo gumu zaidi kwa akina sie tunaoelemea zaidi katika kuandisha mambo yanayogusa maslahi ya mafisadi na vibaraka wao.Kwa mfano mara kadhaa nimekuwa nikipata comments zenye matusi ya kila aina kutoka kwa baadhi ya wasomaji.Huwa siyachapishi matusi hayo kwa vile naamini wanaotukana wana mtindio wa mawazo na tafakuri.Hoja hujibiwa kwa hoja na wala si matusi.

Ninafahamu matusi hayo yanatoka wapi,na pia natambua kwanini badala ya hoja zangu kujibiwa kwa hoja zao wanakimbilia kutukana.Ni hivi,ukiona mtu anakusema vibaya au kukutukana wakati hujamkosoea lolote ujue mtu huyo hana zuri upande wake,na maneno mabaya au matusi dhidi yako inakuwa kama njia ya mkato ya kupunguza matatizo yake.Watu wa aina hii wanahitaji ushauri nasaha badala ya kuwatukana.Na kibaya zaidi ni kwamba ukimtukana chizi,basi watu watashindwa kutofautisha kati ya nani mzima au mwenye busara na nani chizi.

Lakini wapenda matusi hawa wananipa faraja moja kubwa.Kwamba hadi kufikia hatua ya kutukana kwa njia ya comment kwenye blogu hii inamaanisha walitumia muda wao kusoma nachoandika.Hiyo ni faraja kubwa kwangu kwani walengwa wangu wakuu ni watu makini na sio vichwa panzi kama hao mabingwa wa matusi.

Ujumbe wangu mfupi kwa wazembe hao wa kufikiri ni huu: kasheshe nilizokumbana nazo huko nyuma kutokana na mtizamo wangu ni mara alfu ya hivyo vijimatusi mnavyotuma kama comments.Kwahiyo endeleeni kupoteza muda wenu kutukana lakini mkae mkifahamu kuwa mnachofanya ni sawa na kutegemea damu kutoka kwenye jiwe.

Anyway,nasikitika kupoteza muda wangu muhimu kuwazungumzia wazushi hawa.Lakini yote katika yote,hivi ni vijimambo tu ambavyo once ukiingia kwenye fani ya kublogu lazima utakumbana navyo.

Bring it on!

9 Jun 2010

WAKATI bajeti ya Serikali inasuasua kutokana na uhaba wa fedha za ndani, familia moja ya Dar es Salaam inayomiliki kampuni inayojihusisha na biashara ya bidhaa za nyumbani imejiingiza katika uwakala wa forodha kwa staili ya aina yake ikiwa ni pamoja na kujikita katika kuwasaidia wafanyabiashara wengine kukwepa kodi; huku wahusika wakijiwekea kinga kwa wanasiasa, Raia Mwema imeelezwa.


Biashara hiyo ya aina yake ya uwakala wa ukwepaji kodi, imeelezwa kuipotezea serikali mabilioni ya shilingi ambazo zilistahili kukusanywa kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali wanaoingiza bidhaa mbalimbali kutoka China na Dubai; huku baadhi ya wanasiasa wenye nguvu serikalini na familia zao wakiwa nyuma ya uhalifu huo.


Vyanzo vya habari ndani ya serikali vimelieleza Raia Mwema kwamba familia hiyo yenye vijana watatu wenye asili ya kiasia ilirithi biashara ya wazazi wao ya kuuza plastic carpets (mazulia ya plastiki), door mats (mikeka ya milangoni), taulo, mapazia na mashuka na baadaye kuamua kuingia katika “uwakala wa ukwepaji kodi”.

Habari za ndani ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) zimeeleza kwamba mamlaka hiyo imekuwa ikifuatilia kwa makini suala hilo pamoja na kuwapo taarifa za uhakika kwamba maofisa waandamizi wa mamlaka hiyo wamekuwa wakishirikiana na wafanyabiashara hao kukwepa kodi.

Mbali ya kuwahusisha watumishi wazito ndani ya TRA, vijana hao wameelezwa kuingizwa katika orodha ya “wachangiaji wakubwa” wa Chama cha Mapinduzi (CCM) pamoja na kuwa karibu na wanasiasa binafsi ndani ya chama hicho tawala.

Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya, hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwa maelezo kwamba hayuko katika nafasi ya kufahamu kila kitu kinachoendelea ndani ya mamlaka hiyo kwa nafasi yake kwa kuwa kila eneo linaongozwa na kamishna wake na “kwa suala hilo anayepaswa kuzungungumzia ni Kamishna wa Forodha.”

Pamoja na kuelezwa kwamba TRA wanazo taarifa za ukwepaji kodi huo na kwamba wamekwisha kuanza uchunguzi, Kitilya alisema: “hilo suala liko chini ya Kamishna wa Forodha na mwenzake Kamishna wa Uchunguzi ambao ndio wanapaswa kulitolea ufafanuzi.”

Raia Mwema ilipomweleza Kitilya kwamba habari za kampuni hiyo kukwepa kodi zimeshawahi kumfikia na ofisi yake kuzitolea maelekezo, alisema, “Ndio kwanza leo unanieleza kuhusu kampuni hiyo, mimi sina taarifa kabisa labda uwatafute Kamishna wa Forodha na wa uchunguzi.”

Hata hivyo, maofisa wa ndani ya TRA wamelieleza Raia Mwema kwamba wafanyabiashara hao vijana wakiongozwa na kaka yao (jina tunalihifadhi kwa sasa), walikuwa wakiagiza bidhaa hizo kutoka nje kupitia bandari ya Tanga kati ya mwaka 2000 hadi 2004 mahali ambako walianza kuwa “mawakala wa ukwepaji kodi”.

“Kutokana na kuzoeleka kwao kwa maofisa wa forodha katika bandari ya Tanga wakati huo, walianza pia kupokea nyaraka za waingizaji wengine wa mizigo tofauti, na kuwasaidia kuivusha kwenye ofisi za Forodha kwa njia za ujanja ujanja.

“Wakati huo hawakuwa na kampuni ya uwakala, walitumia kampuni mbalimbali za kukodi na kutokana na kukua kwa biashara yao na ‘uwakala wao pori’, walijizatiti wakaanzisha mtandao wa kazi kwa kunyoosha au kusafisha njia tangu mizigo inapotoka Tanga hadi kwa wateja Dar es Salaam,” anasema mtoa habari wetu ambaye anafahamu kwa kina mitandao ya ukwepaji kodi.

Imeelezwa kwamba katika ‘kusafisha njia’ walitumia fedha kujitambulisha kwa maofisa forodha na polisi waliokuwa barabarani kudhibiti magendo kwenye vituo muhimu vya udhibiti kama Segera na Kabuku mkoani Tanga; Chalinze na Kibaha mkoani Pwani na kuendelea hadi wakaguzi wengine ndani ya jiji la Dar es Salaam.

“Lakini mwaka 2004 hali ya hewa ya bandari ya Tanga ilibadilika kwa Idara ya Forodha kuziba mianya ya rushwa lakini kwa kuwa vijana hawa walikwisha kuzoea kudanganya katika ulipaji ushuru, ilibidi wahamishie shughuli zao kwingine. Wakaelekeza nguvu zao zote Holili, Kilimanjaro, wakifanya yaleyale waliyokuwa wakiyafanya bandarini Tanga,” anasema mtoa habari wetu.

Imeelezwa kwamba wafanyabiashara hao waliendelea kutoa mizigo Holili kwa muda kati ya mwaka 2004 na 2006 mwishoni walipohamia rasmi bandari ya Dar es Salaam ambako sasa wamekita mizizi.

“Mtandao wao wa Dar es Salaam ni mkubwa wakiwa wameteka mamlaka zote zinazohusika na kodi. Ni mtandao ulioenea kutoka Dar es Salaam hadi nje ya nchi. Zimefunguliwa ofisi Hong Kong na Guanzhou, China na Dubai. Ofisi za nje hutumika kupokea mizigo inayoingia nchini.

“Mwagizaji wa mali yoyote kama nguo, hardware au vifa vya umeme hufanya manunuzi kwenye maeneo hayo na hupewa gharama zote za kufikisha mzigo Dar es Salaam pamoja na ushuru wa forodha na gharama nyinginezo hadi kweye bohari yao iliyopo Dar es Salaam,” kinaeleza chanzo kingine ndani ya serikali.

Imeelezwa kwamba mwagizaji anakabidhi mzigo ofisini China na anakabidhiwa mali yake Dar es Salaam baada ya siku kadhaa kati ya wiki tano hadi sita.

Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini viwango vya gharama zao kwa baadhi ya mali ni kama ifuatavyo:

Kusafirisha na kutoa bandarini vifaa vya ujenzi hutoza Dola za Marekani 350.00 kwa meta moja ya ujazo(1 cbm).
Kusafirisha na kutoa bandarini bidhaa za nguo ni Dola za Marekani 450.00 kwa meta moja ya ujazo (1 cbm).
Kusafirisha na kutoa bandarini bidhaa za umeme kama swichi, circuit breakers na viginevyo ni usd Dola za Marekani 500.00 kwa meta moja ya ujazo (1 cbm).
Mizigo maalumu kama vitenge-mazungumzo hufanyika na bei maalumu hukubaliwa.
“Kinachotisha katika utaratibu huu ni kwamba wakati gharama za usafiri wa meli hupatikana kutegemea uzito na ujazo wa mali, wao wamefika mbali zaidi kwa kukadiria ushuru na kodi za Serikali kwa ujazo (yaani cubic measurements). Kwa kawaida ushuru wa forodha hutozwa kwenye Thamani halisi ya Manunuzi, Bima na Gharama za Usafiri hadi nchini (Cost, Insurane and Freight) na si vinginevyo,” anasema mtumishi mmoja wa TRA mwenye ufahamu wa biashara hiyo akidai kwamba biashara hiyo huwa na ulinzi wa ‘wakubwa’.

Ofisa huyo wa TRA ameendelea kwa kusema, “(wafanyabiashara hao vijana)... hutoza kwa kukadiria na kwa ajili hii wanapata faida kubwa kwa kuwa mfumo mzima umewabeba kuanzia mashirika kama Tiscan ambako nyaraka hupelekwa kuthamishwa (jukumu walilopewa Tiscan kwa mujibu wa mkataba na TRA) hadi bandarini ambako mizigo huruhusiwa kutoka baada ya taratibu zote kukamilika.”

Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kwamba waagizaji wanaopitia mkondo wa vijana hao wamekuwa wakishangaa jinsi mizigo yao inavyoweza kutolewa bandarini bila wao kudaiwa ankara za manunuzi (invoices) wanazokabidhi katika ofisi za China na Dubai.

Wanachoulizwa China na Dubai ni orodha ya mali (packing list) jambo linaloashiria uhalifu wa kutisha kutokana na kudhihirika kwamba ankara za mizigo zinazopelekwa Idara ya Forodha ni za kughushi na hazina uhalisi wowote.

“Kwa kawaida mali au mizigo ya thamani ya manunuzi ya Dola za Marekani 10,000.00 na zaidi (FOB Cost) huwa inauliziwa bei na ubora wake kwenye nchi ilikotoka. Kwa hiyo kwa mteja anayepata huduma kwa hawa watu, nyaraka zake zikifikishwa Tiscan ambayo ni kampuni tanzu ya Cotecna International, wanaulizia kwenye hiyo nchi iliyouza mali hiyo kuja kwetu! Kwa vile hawa watu wamesajili kampuni China na Dubai na nyaraka (invoices) wamezitoa wao, hivyo Tiscan inapata majibu kutoka kwa watu walewale. Mapato ya Serikali yanahujimiwa kuanzia hapa,” anasema ofisa mwingine wa serikali ambaye amewahi kukwama kudhibiti uhalifu huo.

Habari za ndani ya sekta ya forodha zinaeleza kwamba kutokana na mafanikio yao katika kukwepa kodi, wamefikia hatua ya kuhodhi utoaji bandarini wa aina fulani ya bidhaa.

“Sasa ni vigumu sana, na kwa kweli hakuna wakala mwigine anayethubutu kutoa bandarini bidhaa za nguo kwa kuwa nyaraka za kampuni nyingine zifikapo Tiscan au Longroom huwekewa bei za juu ambazo hazilipiki ili kuwakatisha tamaa waagizaji ambao kwa sasa wamechoshwa na huduma za vijana hawa zilizojaa kiburi na dharau.

“Hali hiyo imewafanya waagizaji kukosa pa kwenda bali kwa vijana hao na wakabaki wakisikitika jinsi vyombo vya dola vinavyowekwa mfukoni kwa hasara ya jumla ya Taifa. Waagizaji wanalalamika kwamba hawana tena uhuru kwa kuwa wanalazimika kutumia kampuni moja tu ambayo bei zake hazina majadiliano. Ukienda kubembeleza unaambiwa katafute wakala mwingine ambaye hata hivyo huwezi kumpata kwa kuwa hawa wamehodhi kila kitu,” anaeleza mtoa habari wetu ndani ya sekta ya kodi.

Mfanyabiashara mmoja mzalendo ameliambia Raia Mwema kwamba vijana hao wamewakatisha tamaa wafanyabiashara wengi huku wao wakiwa na uwezo wa kutoa bandarini mizigo siku na wakati wanaotaka wao.

“Wanatoa inapofika fleet ya magari kama 20 kwa wakati mmoja. Wanafanya hivyo baada ya kusafisha njia au kusubiri siku ambayo hakuna ‘wanoko’ kwenye shift fulani huko Forodha. Inawasaidia pia katika mambo ya rushwa kwani fungu moja linatolewa kwa ajili ya makontena mengi zaidi. Hii ina athari kwa sisi waagizaji ambao kontena zetu nne au tano zinaweza kuwa zimefika mapema, lakini ikabidi zisubiri nyingine kwa wiki nne au tano ili nyaraka ziende pamoja na gharama (rushwa) iwe ndogo,” anaeleza mfanyabiashara huyo mwenye ofisi zake maeneo ya Kariakoo.

Mfanyabiashara huyo anaeleza kwamba kwa hali halisi iliyopo kwenye mfumo wa ukusanyaji kodi, ni vugumu kukwepa ushuru kwa kudanganya kiasi (idadi) cha mali kilichomo kwenye kontena (false declaration) au kuweka bei ndogo au ya chini ya ile bei halisi (under invoicing), lakini kwa kampuni hiyo hilo linawezekana kwa kuwa mfumo mzima tangu serikalini, Tiscan na TRA umekuwa nyuma yao kutokana na nguvu kubwa waliyonayo vijana hao.

Imeelezwa kwmaba kwenye kampeni za mwaka 2005 kampuni hiyo ilichangia chama tawala Sh. Milioni 200 na kwamba katika mwaka huu wameahidi kuchangia milioni 500 huku ofisini kwao zikiwa zimejaa picha walizopata kupiga na viongozi wa juu wa chama tawala na Serikali katika hafla za uchangiaji kampeni.

Ili kufahamu kiasi cha mapato ya Serikali yanayopotea angalia hesabu hizi:

Kontena la nguo za kawaida lenye urefu wa futi 20 laweza kuwa na thamani ya Dola za Marekani 60,000.00 hadi Dola za Marekani 80,000.00 kutegemeana na aina, ubora na idadi ya nguo zenyewe. Ushuru wa jumla ni 48% ya thamani halisi (cif value). Kwa hiyo kama thamani ni Dola za Marekani 60,000.00 x 48% = Dola za Marekani 28,000. Kwa thamani ya Dola 1 ya Marekani = Sh.1400, ushuru kwa kontena hili katika shilingi ni 40,320,000.
Kama kontena ni la thamani ya USD 80,000, ushuru ni 80,000.00 x 48% ambazo ni sawa na Dola za Marekani 38,000.00 na kwa Sh ni 53,760,000.

Kwa mujibu wa habari za ndani ya TRA, vijana hao wanakadiria gharama zote kwa meta za ujazo kutoka China hadi Dar es Salaam, na hivyo kontena la futi 20 ambalo lina meta za ujazo 36, ina maana gharama zote ni Dola za Marekani 450 x 36 = Dola za Marekani Dola za Marekani 16,200 ambazo ni sawa na Sh. milioni 22.68.

Ikiwa utaondoa gharama halisi za kusafirisha kontena hadi Dar es Salaam ambazo ni Dola za Marekani 2,500, basi kinachobaki ni Dola za Marekani 16,200 – 2500 = Dola za Marekani 13,700.00 au Sh. 19,180,000.

Uchunguzi wa Raia Mwema umeonyesha kwamba sehemu kubwa ya fedha hutumika katika kulipia ushuru kidogo, rushwa kwa maofisa sehemu mbalimbali husika, gharama za bandari na usafiri wa bandarini kwenda kwenye maghala yao.

“Kwa uzoefu wangu hawa jamaa kontena la nguo la futi 20 hawalipi zaidi ya Sh. milioni 10. Hii ina maana ya kuwa badala ya kulipia gharama halisi ya zaidi ya Sh. milioni 40 wao wanalipa milioni 10 tu. Kwa hiyo, kwa mfano mmoja tu, Serikali hupoteza Sh. milioni 30 kwa kila kontena la nguo la futi 20 linalotoka bandarini. Ikiwa makontena 100 yanaweza kutoka bandarini kwa wiki moja, ina maana serikali hupoteza milioni 30 x 100 = bilioni 3 kwa wiki. Kwa mwaka mmoja hii ni sawa na shilingi bilioni 156,” anaeleza mtaalamu wa kodi ambaye kwa sasa ni mstaafu.

.
CHANZO: Raia Mwema

8 Jun 2010

Rais Kikwete akikabidhi zawadi ya kinyago kwa mchezaji wa Brazil,Kaka,huku mtoto wa Rais,Ridhiwani Kikwete (kulia kwa Rais),akishuhudia na "tabasamu la haja" (Picha kwa hisani ya Ankal Michuzi)

Niite mzandiki,mkosoaji wa kila kitu,au hata mpuuzi.Yote sawa.Lakini haihitaji upeo hata wa mtoto mchanga kutambua kuwa uamuzi wa "kununua" kipigo cha mabao matano kutoka kwa Wabrazili ilhali tumegubikwa na matatizo lukuki ya kiuchumi ni,well,upuuzi.

Nilishabashiri awali kuwa baada ya mechi kati ya Taifa Stars na Wabrazili itakuja mechi kali zaidi kuhusu faida au hasara za mechi hiyo.Na hapa nazungumzia fedha.Kwa mujibu wa tovuti ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC),mechi hiyo ilifanikishwa na mkopo wa benki flani kwa Shirikisho letu la Soka chini ya uongozi wa Leodgar Tenga.Inaelezwa kuwa TFF walitarajia mpambano huo ungeingiza takriban dola milioni tatu ambazo zingerejesha gharama zinazokisiwa kuwa dola milioni mbili unusu (zaidi ya shilingi bilioni tatu)walizotumia "kununua" mechi hiyo.Kwa akili ya Tenga na wenzake,walitarajia uwanja wenye uwezo wa kuchukua watu 60,000 ungefurika na pengine kuzalisha faida kubwa zaidi ya hizo dola milioni tatu zilizokisiwa.Sijui ni kufumbia macho umasikini unaowakabili Watanzania wengi au ni ubishi tu,TFF wakaweka viingilio vya juu na vitakavyoingia kwenye vitabu vya historia ya soka la Tanzania.

Sidhani kama tutafahamisha gharama halisi za mechi hiyo wala kuelezwa hasara kamili.Na si kwamba tutafichwa kwa sababu ya aibu ya waandaaji bali kuna "wajanja" (isomeke MAFISADI) watakaoongeza ukubwa wa hasara hiyo kwa kujirejeshea gharama wasizostahili.Lakini pamoja na usiri huo,tovuti ya BBC imemnukuu Waziri wa Habari na Michezo George Mkuchika akisema kuwa serikali haikuchangia chochote katika "ununuzi" wa mechi hiyo,na akatupa "kigongo" kingine kwa kudai TFF walikopa fedha kutoka benki kumudu gharama hizo.

Lakini kauli ya Mkuchika inakinzana na kauli ya awali iliyotolewa na Tenga,ambapo kwa mujibu wa tovuti ya gazeti la Daily Nation,alinukuliwa akieleza kuwa (nanukuu) "Tuliongea na Rais wetu (Jakaya Kikwete),na ni yeye ndiye aliyewezesha mechi hii kuwezekana".Tenga alisema (nanukuu tena) "(Rais) alivutiwa tangu mwanzo na kuhakikisha kila uwezo wa dola (serikali) unawezesha mechi hiyo".

Sasa sijui nani anasema ukweli kati ya Mkuchika na Tenga.Na pengine swali la muhimu zaidi ni nani atayebeba mzigo wa deni hilo kama si mlipakodi wa Tanzania.Na ni mzigo kweli kwani dalili za wazi za uzembe wa waandaaji wa pambano hilo tunaloaminishwa kuwa litaitangaza Tanzania ni matangazo mengi ya makampuni ya kigeni badala ya vivutio vya taifa letu.Well,unatarajia nini kutoka kwa wazembe walioshindwa hata kuwa na CD  ya uhakika ya wimbo wa taifa letu?

Jasusi ChatBot

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.