Imetumwa na mdau FRANK EYEMBE wa Urban Pulse
7 Jul 2010
Demokrasia katika jamii isiyojali utawala bora ni sawa na kufukia makaratasi ardhini kwa matarajio ya kuota mmea wenye matunda ya noti.Ni mithili ya kualika timu ya Taifa ya Brazil kwa mabilioni ya shilingi kisha mechi husika ituache na bili kubwa pasipo manufaa yoyote.Hebu tafakari.Mwezi Oktoba Watanzania kwa mamilioni yao watapiga kura kumchagua Rais na Wabunge.Japo shughuli hiyo ni ya siku moja tu,maandalizi yake yanagharimu mabilioni ya shilingi.Wenyewe wanasema ndio gharama ya demokrasia.Lakini baada ya uchaguzi,wengi-kama sio wote-wa tutakaowachagua watasahau kabisa kwanini tumewachagua,huku wakiwa bize kutafuta namna ya kufidia gharama walizotumia kuingia madarakani.
Zamani hizo tuliambiwa kuwa demokrasia ni pamoja na uwepo wa vyama vingi vya siasa.Takriban miongo miwili baadaye Watanzania wameshuhudia namna uwepo wa vyamahivyo vingi vya siasa ulivyoshindwa kulikwamua taifa letu kutoka kwenye lindi la umasikini.Sanasana umasikini umekuwa ukizidi kuongezeka huku wanasiasa wetu wakibadili kauli mbiu kila baada ya muhula (kwa mfano kutoka Ari Mpya,Kasi Mpya na Nguvu Mpya kuwa Ari Zaidi,Kasi Zaidi na Nguvu Zaidi).Tumeshuhudia pia mlolongo wa sera,mikakati,mpingo na vitu kama hivyo,from MKUKUTA to MKURABITA to KILIMO KWANZA.Na kwa mawazo mapya hatujambo,shughuli ipo kwenye utekelezaji.
Siku chache zilizopita nilitundika makala kuhusu utata wa kauli za Waziri wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe na zile za Makamu Mwenyekiti wa CCM Pius Msekwa kuhusu suala la uanzishwaji Mahakama ya Kadhi.Wakati Waziri Chikawe aliahidi kuwa mahakama hizo zingeanza kazi mwakani,Msekwa alitamka bayana kuwa suala hilo haliwezekani.Hadi leo hakuna ufafanuzi uliotolewa kuhusu suala hilo ila kilicho bayana ni kuwa CCM imeamua kuachana nalo baada ya kuliingiza kwenye manifesto yake ya Uchaguzi mwaka 2005.Kwa vile sie ni mahiri zaidi wa kuhangaika na mambo kwa mtindo wa zimamoto tunasubiri liwake la kuwaka ndipo tuanze kuhangaika namna ya kudhibiti.Taasisi zenye majukumu ya kuwa proactive (yaani kuazuia majanga kabla hayajatokea) ziko busy zaidi na kuhakikisha CCM inarejea madarakani kwa ushindi wa kishindo badala ya kujishughulisha na jukumu lao la msingi la kulinda na kutetea ustawi wa taifa letu.Kwao,siasa (yaani CCM) ndio nchi na ndio kila kitu.
Majuzi umejitokeza utata mwingine wa kauli kati ya mawaziri wawili waandamizi kuhusu suala la uraia wa nchi mbili (dual citizenship).Na kichekesho ni kwamba tofauti na ule mgongano wa kauli kati ya Chikawe na Msekwa,safari hii mgongano wa kauli za mawaziri hao umejiri ndani ya jengo la Bunge katika kikao kinachoendela cha bajeti ya mwaka 2010/11.Awali,Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha alilieleza Bunge Tukufu kuwa serikali imeamua kuwa huu sio wakati mwafaka kwa suala la uraia wa nchi mbili,na kwamba serikali anaangalia uwezekano wa kuanzisha ukaazi wa kudumu (permanent residency).Waziri Masha alieleza kuwa serikali inaandaa hoja kuhusu suala hilo la permanent recidency kwa minajili ya kuileta bungeni ijadiliwe. "Huu sio wakati mwafaka kuruhusu uraia wa nchi mbili,serikali inaangalia uwezekano wa kuanzisha ukaazi wa kudumu badala ya uraia wa nchi mbili", alisema Masha.
Wakati Masha akisema hivyo,Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Membe alilieleza Bunge hilohilo kuwa serikali imeridhia suala la uraia wa nchi mbili na kwamba Wizara yake iko kwenye mchakato wa kuwasilisha suala hilo kwenye kikao cha Barza la Mawaziri.Pia Membe alieleza kuwa anafanya mawasiliano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ili kupata baraka zao kutokana na suala hilo kuwa la Muungano.Akihitimisha hoja ya bajeti ya wizara hiyo, kwa mwaka wa fedha 2010/2011, Waziri Membe alisema siyo dhambi, Watanzania kutafuta riziki nje ya nchi na ni haki yao kubaki na uraia wa Tanzania.Alisema wakati umefika kwa Watanzania, kupatiwa haki yao ya msingi kwani licha ya kuwa ni manufaa kwao pia ni manufaa kwa nchi kutokana na fursa ya kuongeza pato la taifa.
Kadhalika,inadaiwa kuwa Waziri Membe aliwaeleza Watanzania waliohudhuria mkutano wa Diaspora jijini London hivi karibuni kwamba suala hilo limeshajadiliwa na baraza la mawaziri na linasubiri kuwasilishwa bungeni ili upitishwe au kupingwa na wabunge.Mimi sikuhudhuria Mkutano huo wa Diaspora kwa vile niliamini ungenipotezea muda wangu tu kwa sababu viongozi wetu ni mahiri sana katika kuahidi mambo mazuri kwenye hadhara,na hujifanya wasikivu sana lakini utekelezaji ni zero,sifuri,zilch!
Ni dhahiri kwamba mmoja kati ya mawaziri hawa anadanganya.Wakati sina la kusema kuhusu kauli ya Waziri Masha,kauli za Waziri Membe huko Bungeni na London zinaleta utata unaoweza kuyumkinisha kuwa kuna urongo wa namna flani.Je kauli ipi ni sahihi kati ya hiyo alotoa London kuwa suala hilo limeshajadiliwa na Baraza la Mawaziri na hiyo ya bungeni kuwa suala hilo bado liko wizarani huku likifanyiwa mchakato wa kulipeleka kwenye Baraza la Mawaziri?
Unajua kwanini mmoja wao anadanganya?Sababu ni kadhaa,lakini kwa ufupi,moja,ni kwa vile mdanganyifu huyo anafahamu bayana kuwa wabunge wanaoelezwa suala hilo wapo bize zaidi kufikiri namna watakavyorudi bungeni baada ya uchaguzi (sambamba na kuwazia posho zao nono za vikao vya bunge) kuliko kumkalia kooni waziri aeleze kinagaubaga.Ndio maana mwanzoni mwa makala hii nilibainisha uselessness ya demokrasia yetu.Tunapoteza mabilioni ya shilingi (sambamba na muda wetu kusikiliza porojo za "mkituchagua tufafanya hiki na kile") kuwachagua watu wa kutuwakilisha bungeni lakini wakishafika huko wanakuwa bize zaidi na maslahi yao binafsi.
Pili,anayedanganya kati ya mawaziri hao anafahamu kuwa aliyemteua hatamwajibisha.Kama kuna mtu alimudu kumzuga Rais kwa kuchomekea ishu kadhaa kwenye muswada wa sheria za gharama za uchaguzi na kisha akasalimika,kwanini basi mdanganyifu huyo katika suala hili la uraia mbili awe na hofu?
Tatu,waziri anayedanganya kati ya hao wawili anafahamu udhaifu wa Watanzania katika kudai haki zao za msingi.Kiongozi anaweza kudanganya waziwazi kwenye umati wa watu lakini bado akaishia kupigiwa makofi na vigeregere.Ule wimbo wa "Ndio Mzee" wa Profesa Jay unawakilisha hali halisi ya namna Watanzania wengi wanavyoridhia kuzugwa na wanasiasa wababaishaji.Hebu angalia namna harakati za kuirejesha tena madarakani CCM zinavyopamba moto huko nyumbani.Kwa mgeni,anaweza kudhani labda chama hicho ni kipya na hakihusiki kabisa na kashfa za ufisadi,kubebana,kubomoa uchumi wetu na madudu mengine chungu mbovu yanayoifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi masikini kabisa duniani licha ya raslimali lukuki iliyojaaliwa kuwa nazo.Binafsi naamini kuwa unyonge huo wa Watanzania umechangiwa sana na siasa za chama kimoja ambapo kiongozi alikuwa mithili ya Mungu-mtu,hakosei,lazima ashangiliwe hata akiongea utumbo,sambamba na suala la kujikomba kwa viongozi kwa matarajio ya kujikwamua kwa namna moja au nyingine.
Na kwa vile vyama vya upinzani vimetuthibitishia kuwa uwezo wao katika kuing'oa CCM madrakani ni kama haupo,basi mazingaombwe kama hayo ya Chikawe na Msekwa,na haya ya sasa kati ya Masha na Membe yataendelea kuwepo kwa muda mrefu sana.Unaweza kuhisi kama nimekata tamaa vile kwa namna ninavyoandika.Hapana,ila safari yetu ni ndefu sana,na tatizo sio urefu tu bali ni kiza kilichotanda kwenye njia yetu ambayo imejaa mashimo kadhaa.Ni sawa na kipofu kumsaka paka mweusi kwenye chumba chenye giza ilhali paka huyo hayumo chumbani humo.
6 Jul 2010
Kushoto ni Urban Pulse Director Baraka Baraka,TV Personality Sporah Njau,Landlady Lucy na Young Moogs
Urban Pulse CEO Frank Eyembe na Jackson Mugisha,Mtanzania Pekee Aliyeshiriki Kwenye Mr & Miss East Africa
Wageni na Washindani
Producer wa Muziki Josh Mbajo na Producer wa Filamu Frank Eyembe
Mc Moseh na Urban Pulse
Fyah Sister First Lady wa Urban Pulse
Kundi la Utamaduni Kutoka Zimbabwe
Washindani Wakiwa Katika Mavazi ya Kitamaduni
Urban Pulse Princes Ordain na Young Jos Wakifunika
Baadhi ya Warembo
Mshindi Randa Shelby Kutoka Eritrea
Mshindi Dawggie kutoka Ethiopia
Washindi
Warembo
Urban Pulse CEO Frank Eyembe na Jackson Mugisha,Mtanzania Pekee Aliyeshiriki Kwenye Mr & Miss East Africa
Wageni na Washindani
Producer wa Muziki Josh Mbajo na Producer wa Filamu Frank Eyembe
Mc Moseh na Urban Pulse
Fyah Sister First Lady wa Urban Pulse
Kundi la Utamaduni Kutoka Zimbabwe
Washindani Wakiwa Katika Mavazi ya Kitamaduni
Urban Pulse Princes Ordain na Young Jos Wakifunika
Baadhi ya Warembo
Mshindi Randa Shelby Kutoka Eritrea
Mshindi Dawggie kutoka Ethiopia
Washindi
Warembo
4 Jul 2010
Kwanza naomba samahani kwa kupotea kwa zaidi ya wiki sasa.Afya iliyumba kidogo.Napenda kutumia fursa hii kuwashukuru wote walionitumia meseji za kunitakia afya njema.Bwana Amesikiliza sala na dua zenu.
Jana,katika pitapita zangu mtandaoni nilikutana na habari kwamba Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,Juma Mwapachu,amewashukia wasomi wa vyuo vikuu kwa kuwapotosha wananchi kuhusiana na serikali kujiunga na soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki lililofunguliwa majuzi.
Kwa mujibu wa habari hiyo,Balozi Mwapachu alitoa kauli hiyo kufuatia ya baadhi ya wasomi kudai kuwa soko hilo linaweza kuwaathiri watanzania katika ushindani wa ajira.Akizungumza jana kwenye ufunguzi wa maonyesho ya 34 ya biashara ya kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Balozi Mwapachu alisema wasomi hao ambao wamesomea uchumi, wameshindwa kusema ukweli kuhusiana na kujiunga na soko hilo, na kusababisha wananchi kuingia uoga.
Alisema wasomi walipaswa kuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi kuhusu jumuiya hiyo na faida zake badala ya kuwapotosha wananchi kuhusu suala hilo na kusababisha baadhi ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo kuhofia.
Alisema kabla ya kufungua milango hiyo aliweza kuzunguka katika kila nchi kwa ajili ya kuzungumza na wadau mbalimbali kuhusu suala hilo, lakini wananchi wamekuwa waoga na kusababisha kutoa maoni mbalimbali ya kupotosha.
"Niwashaangaa sana wasomi tena wamesomea uchumi, lakini wamekuwa wa mbele kuwapotosha wananchi kuhusu soko la pamoja la jumuiya ya Afrika Mashariki, hii imesababisha wanachi washindwe kujiamini na kufikiri kuwa wanaweza kukosa ajira,"alisema Mwapachu.
Alisema watanzania wengi wanawaogopa wakenya kwa madai kuwa wanaweza kushindwa kuingia kwenye ushindani wa soko la ajira.
Nadhani kwa mtu mwenye uelewa mkubwa kama Balozi Mwapachu kutoa kauli hizo ni jambo la kusikitisha sana na ni uthibitisho mwingine wa namna maslahi binafsi na ya kisiasa yanavyowekwa mbele ya maslahi ya taifa,sambamba na kupuuza ushauri wa kitaalam.
Yayumkinika kuamini kuwa kwa wadhifa wake kama Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo,ni lazima Mwapachu aipigie debe ili iendelee kuwepo kwani kinyume chake ni kuwa hatakuwa na ajira.Hata hivyo,laiti Mwapachu angeangalia mantiki ya hoja za wasomi (ambazo kwa hakika ziko shared na hata "wasio wasomi") badala ya kuwashambulia kama kundi la kijamii (yaani kujadili hoja badala ya kumjadili mtoa hoja)angeweza kabisa kufahamu kwanini wanaonyesha wasiwasi wao.
Hivi kama kabla ya ujio wa soko la pamoja la Jumuiya hiyo tayari wageni (licha ya hao wanaotoka Kenya na nchi nyingine za Jumuiya) tayari soko la ajira na bidhaa limetawaliwa kwa kiasi kikubwa na wageni,kwanini basi tusihofu kuwa "kuhalalisha" huko kutapelekea hali kuwa mbaya zaidi kwa Watanzania?
Na wakati Mwapachu anatoa porojo zake kuhusu mafanikio ya soko la pamoja,mbona hatuambii yeye na viongozi wenzie wa Kitanzania wameshafanya jitihada zipi kuhamasisha Watanzania kumudu ushindani uliopo na ujao?Siafikiani na mawazo potofu ya Mwapachu kuwa tatizo la Watanzania ni uoga.Na hata kama tatizo lingekuwa ni uoga basi bado hoja ingekuwa iwapo uoga huo ni halali au potofu kwani uoga kama uoga sio dhambi au kosa kama unajengwa kutokana na mantiki.Tatizo la msingi linalowakabili Watanzania kukabiliana na changamoto za mfumuko wa nguvu za nje katika soko la ndani la ajira na bidhaa ni complex sana,na makala hii fupi haiwezi kujadili yote bali itaangalia kwa ufupi.
Kwa upande wa biashara,kuna tatizo sugu la urasimu ambalo kwa kiasi kikubwa linachangiwa na ufisadi.Urasimu kuanzia kwenye utaratibu wa kuandikisha biashara hadi kwenye masuala ya kodi.Sijawahi kufanya biashara lakini nina marafiki kadhaa wanaojaribu kumudu maisha yao kwa kujihusisha na biashara.Kwa kifupi,ajira ya Mtanzania kwa kutegemea biashara ni suala gumu sana.Katika mazingira ya kawaida sio rahisi kwa biashara kudumu kwa angalau miezi kadhaa kama mhusika hatokuwa tayari kutoa chochote kitu kwa wahusika.Yayumkinika kusema kuwa ili biashara halali ishamiri vema ni lazima ikaribishe illegality ya namna flani,yaani uharamu wa biashara ili kuwa halali.
Na wakati Watanzania wengi tu wangependa kujishughulisha na biashara zao kihalali ili wamudu maisha yao,wanakumbana na ushindani kutoka kwa wenzao "wanaobebwa" na vigogo.Hivi mfanyabiashara anayelipa mlolongo wa kodi huku anauza bidhaa za ndani atamudu vipi kupambana na mfanyabiashara anayeagiza vitu kutoka nje (huku vingine vikiwa feki) lakini anavilipia kodi pungufu au halipi kodi kabisa?Ni dhahiri biashara ya huyo "anayebebwa" itashamiri zaidi kuliko ya huyo mnyonge anayejikongoja peke yake.
Lakini pia kuna suala la utamaduni wa kuthamini baidhaa za nje kuliko za ndani.Baadhi ya wachambuzi wanaeleza kuwa miongoni mwa madhara ya utandawazi ni kuibuka kwa mapambano kati ya vitu vya nje dhidi ya vya ndani au vya asili.Hapa simaanishi kuwa kila element ya utandawazi ni mbaya.Sasa kama serikali yetu inaagiza kila kitu kutoka nje kwa ajili ya matumizi yake huku ikiwaacha mafundi seremala wetu "wakidodewa" na samani zao,na hiyo ni kabla ya ufunguzi wa soko hilo,sasa kwanini wasomi wasihofu kuwa soko hilo linaweza kuwa habari mbaya zaidi kwa Watanzania wengi?
Tukija kwenye ajira,hali ndio mbaya zaidi.Wakati Watanzania wamekuwa mahiri zaidi kupeleka watoto wao Kenya na Uganda,wenzetu hao wamekuwa wakileta nguvu kazi yao ya ziada kuchukua nafasi mbalimbali za kazi.Na kama ilivyo kwenye suala la bidhaa,waajiri wetu nao wanaelekea kuwa na ugonjwa uleule wa kuthamini zaidi wageni kuliko wazawa.Mwapachu alipaswa kutueleza ni Watanzania wangapi wana ajira nchini Kenya,Uganda au Rwanda kulinganisha na raia wa nchi hizo waliokamata ajira hapo nyumbani kabla ya ujio wa soko la pamoja.Najua hawezi kusema hilo sio kwa vile hana takwimu (na inawezekana kabisa akawa hana) bali anafahamu kuwa kwa kweka hilo bayana atalazimika kuungana na hofu walionayo wasomi na Watanzania wengine.
Kilichoua Jumuiya ya awali ya Afrika Mashariki ni kuweka siasa mbele ya maslahi ya nchi.sambamba na kupuuza ushauri wa wataalamu.Na akina Mwapachu ambao walikuwa watu wazima muda huo wanataka kurejea makosa hayohayo.Wanajifanya vipofu wa ukweli kwamba ni vigumu kuwa na ushirikiano wa maana palipo na viwango tofauti vya maendeleo kati ya nchi husika.Tunafahamu vema uchumi wa Kenya,Uganda na Rwanda unavyofanya vema zaidi ya uchumi wetu.Sasa kama tunafahamu hilo kwanini basi tusihofu kuwa soko hili jipya linaweza kufanya hali kuwa mbaya zaidi?Au Mwapachu na wenzake wanadhani kuwa ukigusana na tajiri nawe unapata utajiri?They are completely wrong.Mahusiano ya mwenye uwezo wa kiuchumi na mwenye uwezo duni mara nyingi huishia kumnufaisha zaidi mwenye uwezo kwani nguvu ya uchumi inapelekea kuwa na nguvu kwenye maeneo mengine pia.
Akina Mwapachu wanapaswa kufuatilia kwa karibu mambo yanayoyumbisha jumuiya ya Ulaya ambapo nchi kama Uingereza zimeendelea kuwa na msimamo wa kujihusisha kwa kiasi flani tu na sio kwa asilimia 100 kwa vile wanatambua kuwa kuna nchi zenye uchumi duni zinazotarajia ushirikiano huo uwanufaishe wao zaidi at the expense of wale wanaojimudu.
Mwisho,ili Tanzania ijikomboe kutoka uchumi unaomilikiwa kwa zaidi ya asilimia 90 na wageni ni lazima siasa iwekwe kando,ushauri wa kitaalamu uzingatiwe,na kubwa zaidi,maslahi ya taifa yawekwe mbele ya maslahi binafsi.Vinginevyo,soko la pamoja la Afrika Mashariki litaishia kuwa soko la bidhaa na ajira kwa Wakenya,Waganda,Wanyarwanda na Warundi na sie "tukiishia kunufaika" kwa uwepo wa akina Mwapachu kama viongozi wa jumuiya ilhali uchumi wetu ukizidi kuelekea shimoni.
26 Jun 2010
Sijui ni ukosefu wa mawasiliano au uzembe tu,au pengine ni mkakati wa makusudi wa kutoa kauli zinazotofautiana ili baadaye iwe rahisi "kuziruka kimanga",lakini ni dhahiri kuwa mmoja kati ya viongozi hawa anatudanganya.Wakati Waziri wa Sheria na Katiba Mathias Chikawe akirejea ahadi kama ya mwaka 2005 (wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu) kuhusu uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi,Makamu Mwenyekiti wa CCM Pius Msekwa anasema bayana kuwa suala hilo halipo (labda Waislamu wenyewe walishughulikie "kivyao").Hebu soma kwanza hapa chini
Kwa mujibu wa Gazeti la Tanzania Daima: SERIKALI imesema Mahakama ya Kadhi itaanza katika mwaka wa fedha 2010/11 baada ya jopo la wanazuoni wa Kiislamu wanaoziangalia na kuzihuisha sheria za Kiislamu kukamilisha kazi hiyo.
Jambo hilo lilibainishwa jana bungeni na Waziri wa Katiba na Sheria Mathias Chikawe wakati akisoma hotuba ya makadirio ya matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2010/2011 ambapo ameliomba Bunge limuidhinishie kiasi cha sh bilioni 116.8
Alisema kuwa jopo hilo linaziangalia na kuzihuisha sheria za Kiislamu zinazohusiana na ndoa, mirathi na urithi kwa madhumini ya kuziorodhesha ili zitambuliwe chini ya sheria za dini ya Kiislamu (Islamic Law resstatment act).
Aliongeza kuwa jopo hilo lilianza kazi hiyo baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kukutana na Mufti, Sheikh Mkuu, Issa Bin Shaaban Simba, na kukubaliana kuwa waanzishe mchakato wa Mahakama ya Kadhi.
Katika hatua nyingine, Bw. Msekwa amefafanua sababu za ilani ya CCM mwaka huu kutohusisha kipengele cha uanzishwaji wa Mahakam ya Kadhi kama ilivyokuwa mwaka 2005.
Alisema kuwa ahadi hiyo iliyotolewa 2005 tayari utekelezaji wake umekamilika.
Katika ilani hiyo, kifungu namba 108(b) CCM iliahidi kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa mahakama ya kadhi Tanzania bara, ambalo limekamilika kwa kukabidhi wenye dini yenyewe wahusike katika uanzishwaji wa mahakama hiyo, kwa kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siyo ya kidini.
"Serikali inaweza kukubali au kukataa, ndiyo maana ya kulipatia ufumbuzi lakini watu wanalitafsiri vibaya kuwa
serikali kupitia kifungu hicho imekubali kuanzishwa kwa mahakama hiyo wakati sivyo," alisema Bw. Msekwa.
Alibanisha kuwa serikali ilifanyia kazi kupitia Tume ya Kurekebisha sheria ambayo ilishauri kwamba haitakuwa sahihi kwa mahakama ya kadhi kuundwa na serikali kwa kuwa ni suala linalohusu taratibu za dini ya kiislamu.
Aliongeza kuwa baada ya serikali kupata ushauri huo ilifanya uamuzi kwamba haitaunda mahakama ya kadhi lakini kwa kuwa suala hilo linahusu taratibu za dini la kiislamu, waislamu wapo huru kuunda mahakama hiyo ndani ya taratibu za dini yao.
21 Jun 2010
Zaidi ya shilingi bilioni 150 zimefisadiwa kutoka katika Mfuko wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi,na hiyo ni kwa mwaka juzi (2008) pekee. Kiasi hicho kinajumuisha shilingi bilioni 71.2 zilizotengwa katika mwaka wa fedha 2007/8 lakini hazifika mahala zilipokusudiwa.Utafiti unachofuatilia mwenendo wa matumizi ya fedha za umma-PETS (Public Expenditure Tracking Survey)kinaonyesha kuwa takriban shilingi bilioni 47 zinatafunwa kila mwaka kwa udanganyifu wa malipo hewa katika sekta ya elimu.
Ripoti inayoonyesha ufisadi huo,ambayo ni ya kina zaidi kuliko zilizotangulia,ilikabidhiwa kwa serikali tangu mwezi April mwaka jana.
Gazeti la Citizen limepata nakala ya ripoti hiyo ambayo inaonyesha kwa kiasi gani udhibiti hafifu wa mifumo ya fedha za umma unavyochangia kushuka kwa kiwango cha elimu nchini.
Serikali iliamua kuagiza utafiti huo kwa shule za msingi na sekondari Tanzania Bara ili kubaini kama kutanuka kwa miundombinu ya elimu na kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na shule kunaendana na kuongezeka kwa raslimali zinazotengwa.
Kadhalika,ilitaka kufahamu kama raslimali zinafika kwa watoa huduma,hususan shule, na kwa kiwango gani mipango ya utanuzi imetekelezwa pasipo kuathiri kiwango cha ubora wa elimu kwa kuzingatia kipimo cha matokeo ya wanafunzi.
Taasisi zilizoshirikishwa katika kipimo hicho ni pamoja na Wizara za Elimu na Mafunzo,Fedha na Mipango ya Uchumi,Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa),Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto,na Shirika la Taifa la Takwimu (TBS).Kadhalika,wawakilishi wa vikundi vya kiraia na wahisani walihusishwa.
Kwa majibu wa matokeo ya utafiti huo,wakati kwa miaka kadhaa sasa serikali imekuwa ikiongeza bajeti ya elimu kutoka shilingi bilioni 701.1 mwaka 2005/6 hadi kufikia shilingi trilioni 1.43 mwaka 2008/9 na shilingi trilioni 2.045 kwa mwaka 2010/11,raslimali kwa elimu ya msingi zimekuwa zikishuka kutoka asilimia 55.8 zilizotengwa miaka mitano iliyopita hadi asilimia 46.6 mwaka juzi.
Fedha kwa ajili ya ujezi wa madarasa,nyumba za walimu,vyoo na miundombinu mingine pia zimekuwa zikishuka kwa kasi.Wakati wastani wa fedha zilizotengwa zilikuwa wastani wa shilingi bilioni 109 katika awamu ya kwanza ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (PEPD)kutoka mwaka 2002 hadi 2006,kiwango hicho katika mwaka wa fedha 2010/11 kimeshuka hadi kufikia shilingi bilioni 14 tu katika awamu ya pili ya PEPD kuanzia mwaka 2007 hadi 2011.
Na athari ni za hapo kwa hapo na za kina.Kwa mujibu wa takwimu,wakati madarasa 10,771 yalijengwa miaka saba iliyopita,idadi hiyo imepungua hadi kufikia 1,263 katika mwaka 2008.Hiyo ni mbali ya ukweli kwamba uwiano kati ya wanafunzi na uwezo wa darasa ulikuwa 1:78 kwa mwaka huo ni takrban maradufu ya uwiano stahili wa darasa moja kwa wanafunzi 40 (1:40)
Pia Utafiti huo ulibaini kuwa wakati shilingi bilioni 544.2 zilitolewa kwa manispaa kama mtaji na misaada ya kawaida kwa sekta ya elimu katika mwaka wa fedha 2008,kiwango halisi kilichopokelewa kilikuwa shilingi bilioni 473 na kuacha pengo la shilingi bilioni 71.2
Kadhalika,utafiti huo unaonyesha kuwa mamlaka 66 kati ya 131 zilizohusishwa katika utafiti huo zilielekeza shilingi bilioni 28.9 kwenye matumizi mengineyo badala ya minajili ya elimu kama ilivyokusudiwa.
Mwaka 2008,serikali iliwapangia vituo walimu wapya 1271 katika maeneo ya vijijini lakini ni asilimia 35 tu (walimu 444) walioripoti maeneo hayo.Lakini,wakati jiji la Dar es Salaam lilipangiwa walimu 182 tu,mamlaka husika ziliajiri walimu 441.
Habari hii imetafsiriwa kutoka gazeti la The Citizen
20 Jun 2010
“ Ukweli siku zote hujitenga na uongo Haki Elimu ni waongo, wazushi na wanafiki wanapodiriki kuwatangazia umma wa watanzania eti kuna uhaba wa nyumba za walimu zipatazo 22,000 nchini na kwamba Serikali ya Nne kwa kipindi chote cha utawala wake kimemudu kujenga idadi ya nyumba za walimu zipatazo 300 tu haya ni matusi kwetu….kweli akutukanae hakuchagulii tusi…..watu wazima ovyoo” amesema Rais
---------------------------------------------------------------------------------------------------------
RAIS Jakaya Kikwete amesema Serikali ya Awamu ya Nne imetekeleza kwa vitendo ahadi zote za uchaguzi ilizowaahidi wananchi ukiwamo ujenzi wa miradi mikubwa mitatu ya barabara kuu za mkoa wa Rukwa zenye urefu wa kilometa 657.5 kwa kiwango cha lami.
“Tuliyowaahidi wananchi tumeyatekeleza kwa hakika tumefanikiwa vizuri sana katika ujenzi wa barabara, elimu na afya,”
Alisema hayo juzi wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika kiwanja cha michezo cha Nelson Mandela mjini hapa, huku akishangaa wanaobeza safari zake za nje ya nchi.
Alisema watu hao hawamnyimi usingizi hata kidogo na alihoji kama asingekwenda Marekani kuonana na Rais George Bush (mstaafu) nani angefadhili ujenzi wa mradi mkubwa wa barabara ya Tunduma – Laela – Sumbawanga yenye urefu wa kilometa 224.5 kwa kiwango cha lami.
LAKINI NI MAJUZI TU GAZETI LA HABARI LEO LILIMNUKUU RAIS AKISEMA YAFUATAYO
AHADI ambazo hazijatekelezwa na Serikali ya Awamu ya Nne zitatekelezwa katika Bajeti hii ya mwaka 2010/11, imeelezwa.
Akizungumza jana mjini hapa katika kikao cha kazi na wakuu wa mikoa na wa wilaya pamoja na makatibu tawala wa mikoa yote Tanzania Bara, Rais Jakaya Kikwete aliwataka viongozi hao kusimamia shughuli za Serikali kikamilifu.
Aliwataka kutokwenda likizo katika kipidi hiki cha kuelekea uchaguzi na wasimamie kazi kama wanavyofanya wakati wote.
Rais Kikwete alisema katika kipindi cha miaka mitano tangu Serikali yake iingie madarakani mengi waliyoahidi yametekelezwa.
“Juzi kabla ya Bajeti hata kwenye Baraza la Mawaziri, tulizungumzia ahadi zetu na nyingi tumeshazitekeleza, lakini zilizobaki na majukumu tuliyojipangia kwa miaka yote hii tutatekeleza katika Bajeti hii … tulipoingia mwaka wa kwanza, tulitekeleza ya Awamu ya Mzee Mkapa (Rais mstaafu Benjamin) sasa tunaendelea na kutekeleza yetu,” alisema.
SASA KAMA AHADI ZOTE ZIMESHATEKELEZWA,HIZO ZINAZODAIWA KUTEKELEZWA KATIKA BAJETI HII YA 2010/11 NI AHADI ZIPI TENA?
NA SOTE TUNAKUMBUKA THE MOTHER OF ALL PROMISES,ILE YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.HIVI KWELI RAIS KIKWETE ANATAKA KUTUAMBIA KUWA KILA MTANZANIA HIVI SASA ANA MAISHA BORA?
KADHALIKA JK ALITAMKA BAYANA KUWA ANAWAFAHAMU WALA RUSHWA KWA MAJINA NA KUSEMA ANAWAPA MUDA WAJIREKEBISHE VINGINEVYO ANGEWACHUKULIA HATUA.JE RAIS ANAPOTUAMBIA KUWA AHADI ZOTE ZIMESHATEKELEZWA ANAMAANISHA TATIZO LA RUSHWA NALO LIMEKWISHA?AU ANAMAANISHA WALA RUSHWA ALOSEMA ANAWAFAHAMU KWA MAJINA WAMEAMUA KUJIREKEBISHA?
-----------------------------------------------------------------------------------------------
RAIS Jakaya Kikwete amewataka wanaume wasiwe 'mafataki', wawaache watoto wa kike wasome.
Kikwete amesema, wanaume wanapaswa kuwafuata wanawake wakubwa wenzao na si watoto, na kwamba, wanawake wapo wengi.
“Ninachowaomba wanafunzi wa kike washuhulike na masomo, mambo ya mimba yaacheni… kina baba waacheni watoto wa shule kina mama watu wazima wamejaa tele acheni kupiga ufataki” Rais Kikwete ameyasema hayo wakati anajibu swali la mtoto Rehema Abbas wa Dar es Salaam.
HAYA NI MAENDELEO MAPYA BAADA YA KIKWETE HUYUHUYU KUSEMA YAFUATAYO HIVI KARIBUNI
JK: Mimba kwa wanafunzi ni kiherehere chao
Monday, 07 June 2010 07:33
Rais Jakaya Kikwete amesema matukio ya mimba kwa wanafunzi wa kike nchini yanasababishwa na viherehere vya wanafunzi wenyewe.
Aidha, Rais Kikwete amekiri kwamba matukio ya mauaji ya vikongwe pamoja na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), yanalidhalilisha taifa.
Rais Kikwete alitoa kauli hizo katika kijiji cha Kisesa wilayani Magu jana wakati akihutubia wananchi kwenye ufunguzi wa mashindano ya ngoma kwa kabila la Wasukuma; ngoma ambazo zinajulikana kama 'Bulabo'.
" Kila anayepata Ukimwi anaufuata mwenyewe na wengine ni viherehere vyao; kwa mfano watoto wa shule," alisema Rais Kikwete wakati akijibu risala ya Mkurugenzi wa Makumbusho ya Bujola, Fadha Frasince Sandhu, ambaye alisema ujumbe wa mashindano hayo mwaka huu ni vita dhidi ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Kwa mujibu wa Rais Kikwete, suala la zinaa kwa bianadamu, siyo la lazima hivyo binadamu anaweza kujizuia ama kujikinga kwa kutumia kondomu.
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------
20.6.10
Evarist Chahali
CMZ
1 comment
Instead of counting candles,
Or tallying the years,
Contemplate your blessings now,
As your birthday nears.
Consider special people
Who love you, and who care,
And others who’ve enriched your life
Just by being there.
Think about the memories
Passing years can never mar,
Experiences great and small
That have made you who you are.
Another year is a happy gift,
So cut your cake, and say,
"Instead of counting birthdays,
Count blessings every day!"
18 Jun 2010
18.6.10
Evarist Chahali
JAKAYA KIKWETE
1 comment
ZIARA ya Rais Jakaya Kikwete mkoani Kigoma jana ilipata mushkeli baada ya gari moja kupinduka wakati msafari wake ukitokea Kibondo kuelekea Kigoma Mjini.
Rais Kikwete, ambaye msafara wake umekuwa ukikumbwa na matukio ya hatari katika muda wa wiki tatiu, alikuwa anaenda Kigoma Mjini kuhitimisha ziara yake hiyo ya siku tatu mkoani hapa.
Awali matukio mawili yaliyoukumba msafara wake yaliyuhusu magari ya Ikulu, likiwemo gari alilopanda wakati akiwa ziara ya wiki moja jijini Dar es salaam ambalo lilichomoka tairi muda mfupi baada ya kushuka, lakini ajali ya jana ilihusu gari la CCM mkoani Kigoma.
. Soma habari kamili HAPA.17 Jun 2010
Desemba 9 mwakani,Tanzania yetu itatimiza miaka 50 tangu ipate uhuru.Pengine tarakimu 50 inapunguza uzito,kwahiyo ni vema kubainisha kuwa umri huo ni sawa na NUSU KARNE (herufi kubwa kuonyesha msisitizo).Wakati umri huo wa mtu mzima ungepaswa kuwa habari njema,hali ni tofauti kwetu.Tulowakabidhi dhamana ya kutuongoza wanakurupuka na mambo ya ajabu ajabu kana kwamba wako ndotoni au wako kwenye mchezo wa kuigiza usio na ujumbe wowote.
Ngoja niende moja kwa moja kwenye pointi.Hivi Mtanzania mwenzangu inakuingia akilini kweli kusikia kauli kwamba jengo la Bunge letu tukufu "litafanyiwa ukarabati wa kufa mtu" unaotarajiwa kugharimu shilingi bilioni 30.9 "ili kuwawezesha waheshimiwa sana waendane na teknolojia ya kisasa wanapokuwa Bungeni"!!!?Kwa mujibu wa Spika Samuel Sitta mchakato wa ukarabati huo umeshakamilika na unatarajiwa kuanza mara moja,ambapo utapokamilika kila kiti cha mbunge kitakuwa na runinga pamoja na mawasilino ya kisasa ya kompyuta.
Ofkozi,ni muhimu kwenda na wakati katika suala zima la teknolojia lakini pamoja na umuhimu huo shilingi bilioni 30 na ushee ni nyingi mno na tunazihitaji kwenye maeneo mengine yaliyo hio bin taaban kama vile miundombinu,huduma za afya,maji,nk.Hivi kweli runinga kwenye kiti cha mbunge ni muhimu kuliko madawati au nyumba za walimu?Je hizo bilioni 30 zingeweza kujenga zahanati ngapi au visima vingapi vya kuwapatia walalahoi huduma ya maji ya uhakika?
Lakini kabla sijatuliza hasira zangu kutokana na kauli hiyo ya Spika Sitta,JK nae amekuja na mpya akidai kwamba katika miaka mitano ijayo kila mwalimu atakuwa na laptop.Namheshimu sana Rais wangu lakini baadhi ya kauli zake zinanitatiza sana.Hivi kipaumbele katika elimu yetu ya kusuasua ni laptop kwa walimu au makazi bora kwa walimu hao sambamba na kuboreshewa maslahi yao na mazingira yao ya kazi?Mwalimu mwenye laptop anafundishaje wanafunzi waliokaa chini ya mti?Na wakati JK anatoa mpya hiyo hajatuambia umeme wa kuziwezesha laptop hizo utakuwa wa nguvu za jua au zitatumia mafuta ya taa kwani sote tunafahamu uhuni wa TANESCO.
Sijui ni uzembe wa watawala wetu kuelewa matatizo yetu na vipaumbele vyetu kama taifa au ni makusudi tu lakini kwa mwenendo huu itatuwia vigumu kutembea vifua mbele hapo mwakani tutaposherehekea nusu karne tangu tupate uhuru.
Subscribe to:
Comments (Atom)






























